Skendo ya Sukari Yaendelea Kugawa Wabunge

Skendo ya Sukari Yaendelea Kugawa Wabunge

Shondola

Member
Joined
Apr 2, 2014
Posts
95
Reaction score
58
Unapozungumzi Kikao cha Bunge kinachotazamiwa kuanza mapema wiki ijayo si rahisi sana kusahau kuzungumzia skendo ya SUKARI ambayo kwa sasa imekuwa ikiitafuna Nchi.

Tumetoka kwenye Skendo kubwa ya Account ya Tegeta Escrow majuzi na sasa Skendo ya Sukari limekuwa ni janga kwa Taifa hasa kutokana na swala hili kuhusisha viongozi wakubwa waandamizi wa Taifa hili.

Taifa hili linajua kuwa ni vigumu sana kuzungumzia swala la Sukari ukaacha kumtaja mtu kama Pinda na mfanyabiashara maarufu kutoka Zanzibar Bwana Turkey.

Skendo hii ya Sukari sasa imechukua sura mpya hasa baada ya Ofisi ya Bunge kumpiga Stop Mhe. ASUMPTA MSHAMA (Mb) kuwasilisha hoja yake binafsi kuhusiana na Skendo hiyo.

Mhe. Asumpta Mshama aliiomba ofisi ya Bunge kama kanuni zinavyomtaka ili aweze kutoa hoja binafsi kuhusiana na skendo hiyo ya sukari lakini bila hata ya kupewa majibu ya kuridhisha Mbunge huyu alipigwa stop.

Wabunge walio wengi wamesema wanajua na wanaelewa ni kwa nini Asumpta kapewa zuio kimsingi ni ili kumlinda Waziri Mkuu ambaye ndiye muhusika mkuu katika Skendo hii. Wabunge wameapa kwamba hata kama Asumpta akipigwa Stop hili swala ni lazma lizungumziwe.

"Wao wanadhani kumnyamazisha Asumpta ndiyo suluhu?? Hatuwezi acha Nchi inatafunwa namna hii halafu tuendelee kukaa kimya tulianza na Escrow na hili la Sukari nalo lazma lichukue mkondo wake." Alisikika akizungumza kwa hasira Mhe. Kigwangala..

Wabunge vile vile wameonekana kusikitishwa sana na jitihada anazozifanya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu Ndgu William Vangimembe Lukuvi za kutoa kiasi kikubwa cha HONGO kwa baadhi ya wabunge ili kuhakikisha swala hili linazimwa na linafia mbali. Katika hili Lukuvi anasaidiana sana na mfanyabiashara kutoka Zanzibar bwana Turky.

"Sikiliza mwandishi sisi tulio malofa tunajua na tumeshaona jitihada za Lukuvi za kugawa pesa tena pesa zenyewe zinagawiwa kwa staili anazamwa nani apewe nini.... Hela tutapokea angalau tukajiandae vyema majimboni ila nakuhakikishia huu moto ushakama bati hauzimiki tena huko Bungeni lazma tutatoana roho.. Huu unafiki wa mtu kujifanya masikini kumbe anatuzunguka na ana mihela kibao hatuutaki tena tumechoka bwana" aliongea huku akisisitiza Mhe. KESSY.......

Hata hivyo tulitamani vile vile kupata maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya PAC juu ya Skendo hii. Na mwenyekiti wake alilikugusia kwa juu tu "kamati yangu ilikwenda mpaka kwenye kiwanda cha sukari tumezungumza kwa kina na wahusika na bodi ya sukari vile vile na tumepata tunachohitaji..... Yatosha kusema hata wagawe Mabilioni hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe jingine....."

Mpambe mmoja wa Waziri Mkuu Pinda ambaye ndiye anayesemekana kuwa mbeba mikoba na mshika fedha za Uraisi alipotakiwa kuzungumzia hili sakata hasa kutokana na Mkubwa wake kuhusishwa na Skendo hii moja kwa moja hakuonekana kukubali wala kukataa alisema sentensi fupi sana ambayo bado tunaifanyia tafakuri alisema hivi "Wao wanamwona Pinda tu wakaulize na ziara zinazofanywa na Chama fedha zinatoka wapi...." Hapa tuliachwa njia panda na kutufanya tuendelee kutafiti maneno haya ya bwana mkubwa huyu..... Kwa kuwa sentensi yake ina maana zaidi ya Moja. Kwanza yeye anakubaliana na hilo la Sukari dhidi ya Mkubwa wake lakini pili anataka kuaminisha watu kuwa si Pinda peke yake ila kuna vigogo wengine.


Macho na Masikio ya watanzania sasa yanaanza kuelekea Dodoma kuanzia tarehe 27.............
 
Mwaka huu tutasikia mengi mpaka tufike kwenye uchaguzi!Let me have my popcorn ready for more drama coming ahead!
 
ndo maana kumbe sukari imepanda bei hadi 2500,kumbe na huko wameiba sukari pia?
 
Zitto mwizi sana utakuja kusikia kuwa yeye ndiye mhusika mkuu halafu atakimbilia kwa mengi wapakazie wengine.
 
Ccm itabaki vipande mwaka huu. Issue ya sukari,bomba la gesi na bandari ni moto wa petrol. Tena hiki ndicho kipindi kizuri cha kuwachanganya ccm huku kukiwa na joto la uchaguzi mkuu.
 
Mud slinging. . . . . .Ping pong. . . . . .tit for tat. . . . Bora tukose wote! !!!
 
Zitto mwizi sana utakuja kusikia kuwa yeye ndiye mhusika mkuu halafu atakimbilia kwa mengi wapakazie wengine.

makubwa! Leo hii amekuwa mwizi? Kilichokuwa kinawafanya mseme ni mzalendo na kiongozi bora ajaye wa tz enzi za migogoro CHADEMA ni kitu gani,kama sio ushen*zi wenu na unafiki wenu lumumba B7,ukiwemo wewe,Lizaboni,Fazafoxy,Thatha,mjepo,Ritz,msalani nk.
 
Zitto mwizi sana utakuja kusikia kuwa yeye ndiye mhusika mkuu halafu atakimbilia kwa mengi wapakazie wengine.

wee njaaa itakuuwa uko tayari kuwatetea wezi na mafisadi kwa kitu chochote.....shame on you
 
Zitto mwizi sana utakuja kusikia kuwa yeye ndiye mhusika mkuu halafu atakimbilia kwa mengi wapakazie wengine.
Hivi bado manaweweseka kwa bosi wenu muongo kupigwa chini? mbona chama chenu kimeridhia wezi wote watoswe? wewe uko chama gani?
 
CCM mbona ina miradi mingi, viwanja vya mpira maeneo ya kulaza magari, majengo ya kupangisha, ruzuku kutoka serikalini karibu 1 bilion sasa inahusishwaje tena na skandali za kutumia fedha haramu za sukari kwa ajili ya viongozi wake kufanya ziara?
 
Zitto mwizi sana utakuja kusikia kuwa yeye ndiye mhusika mkuu halafu atakimbilia kwa mengi wapakazie wengine.

Hivi likipigwa baragumu na kuita watu wenye akili timamu wajitokeze wewe unaweza kuwa na courage ya kujitokeza? Binafsi unaamini uko sawa kweli? Nenda kamuone mshauri nasaha akusaidie.
 
Back
Top Bottom