Siyo Siri CHADEMA Imepata Jeraha

Nyie watu nyie..mikutano ya chadema tu ndio inakuwa imejaa watu/wafuasi halali?CCM na wengine wanaleta mamluki,wengie wanaletwa na mabasi kutoka sehemu nyigine ili kujaza mikutano, hivi hamjishangai nyie mikutano yenu tu ndio inakuwa wafuasi halali?
 

Unaweza kuweka takwimu sahihi hapa juu ya tangu Zitto awepo huko Kigoma CHADEMA katika majimbo yote ina Wabunge wangapi? pia kuna Madiwani wangapi wa CHADEMA katika wilaya zote huko Kigoma, tambua kuwa Zitto huko Kigoma ameiporomosha sana CHADEMA na hakuwepo kwa ajili ya kuijenga CHADEMA bali alichokuwa akikifanya ni kujijenga yeye binafsi na ndio maana hata katika uchaguzi mkuu uliopita 2010 hakujihusisha kumpigia kampeni Dr. Slaa.
 
Kwa vyovyote vile chadema wamepoteza kura nyingi sana maana watu wengi wanaojiunga ACT wanatoka chadema.

Huko ni kujidanganya kuwa waliojiunga wengi wanatoka cdm peke yake,wengi wametoka ccm na wataendelea kutoka ccm
 
CHADEMA wanafanya kazi kwa kuongozwa na hisia sana. Kwa nchi zilizoendelea hata kama mwanasiasa amethibitika anakihujumu chama, ila as long as ana impact ndani na nje ya chama, sometimes its normal to work with the devil!
 
Mimi pamoja na familia yangu pamoja na marafiki wangu watano tumechoma kadi za uachama wa chadema pamoja na nguo zao, chama gani cha ukabila na ukoo namna ile.
kutoka watu 12 ndani ya chadema ni pengo, huoni kwamba ni hasara?


Majibu hayo hapo juu. Hapo ni Iringa week end hii
 
Mimi pamoja na familia yangu pamoja na marafiki wangu watano tumechoma kadi za uachama wa chadema pamoja na nguo zao, chama gani cha ukabila na ukoo namna ile.
kutoka watu 12 ndani ya chadema ni pengo, huoni kwamba ni hasara?

Hongera kwa kukihama CDM,kila la kheri huko uendako.Ngoja tusubiri CDM kikipasuka kwa kuhamwa na watu type yako.Watu 12 ni wachache kidogo,nakushauri uchukue kijiji kizima hapo ulipo ili CDM kife mapema zaidi.
 
Ati wanajidai wako makini!
Hawajui siasa ni kuvumiliana kwa lengo kubwa zaidi, CCM pamoja na madudu ya Lowassa inaishia kutoa natamko tu lakini hawawezi kumtimua.
Hiyo ndo siasa.
Siyo siri, wamejeruhiwa.
 

Jaribu kufikiri kidogo. Naiamini taasisi hiyo na ninaamini hawakuwa na namna bali kutimua tu watu wa aina ile. Hata wanaowaacha wenza wao huwa wanafahamu madhara lakini wanakuwa hawana namna bali kuacha. Na kwa umakini wa CHADEMA pamoja na unachokiona kuwa ni jeraha mambo yataenda tu maana waliona kabla kabla ya kumpiga chura teke. Mpaka ACT iwe kama CHADEMA nitakuwa nimesha kufa.
 

Ushahidi mkuu japo orodha ya majina au mfumo uliotumika kuwalipa??!!!
 
Watnzania SI wajinga kiasi hicho, kama kweli Zzk Ana madhara kwa cdm tutaona out come ya ukawa baada ya uchaguzi mkuu!
 
Mtoto wa kiume akimbaka mama yake na mama kama ana akili timamu lazima amlaani....hawezi kumsamehe eti kisa ni mwanae....Ayatollah Zitto amelaaniwa na chadema kwa hiyo chama kimeona njia nzuri ni kumlaani tu bila kujali umaarufu wake.

Kwa kifupi zitto hana tena huo umaarufu kwa watanzania zaidi ya hayo maigizo anayoyafanya kwa watanzania. Chadema walikuwa sahihi waliposema zitto ni mhaini ndani ya chama.

Huwezi kuanzisha chama ndani ya chama ukabaki salama huwezi! Chadema walituambia zitto ndo muasisi wa chama cha ACT tukabeza, leo imeonekana wazi baada ya kufukuzwa ghafla akajiunga na ACT. cha ajabu zaidi alikuwa akisubiriwa yeye ili wazindue chama chao.

Ukiwa unatuhumiwa kwamba, unatembea na mwanamke X ghafla mkaachana na mke wako wa ndoa na siku hiyohiyo ukaenda kulala kwa yule mwanamke X na wiki moja mkafunga na ndoa; hahahaha huitaji elimu ya kindagateni kuelewa jambo hili.

Mwisho, zitto ni mnafiki mkubwa hana lolote mpuuzeni si mwanamageuzi kama anavyojipambanua eti ni mzalendo hana hata hizo chembechembe mpuuzeni.
 
Mwenye data kamili juu ya nini usaliti wa ZZK ndani ya CDM amwage HAPA hadharani,CHADEMA WAKUBALI WAMEUMIA KUODOKA WA ZITO.
 
Mwenye data kamili juu ya nini usaliti wa ZZK ndani ya CDM amwage HAPA hadharani,CHADEMA WAKUBALI WAMEUMIA KUODOKA WA ZITO.

Usitegemee kitu kama hicho. Zaidi wana kale ka toilet paper ka waraka. Mtunzi akiwa Kubenea na TeamMbowe hata Slaa alipohojiwa aliukana na kuuruka kwa kusema hajui umetoka wapi...

Ni woga tu wa mbowe kuogopa ushindani ndani ya chama. Wanahubiri demokrasia mdomoni lakini hawatendi.
 

Mkuu jaribu kutulia wakati unaandika!
 
CHADEMA wanafanya kazi kwa kuongozwa na hisia sana. Kwa nchi zilizoendelea hata kama mwanasiasa amethibitika anakihujumu chama, ila as long as ana impact ndani na nje ya chama, sometimes its normal to work with the devil!

...wee unajua maana ya PATIENT ZERO ? mkeo anatoka nje ya ndoa na anaandaa mipango ya kukuua ili arithi mali zako, uta compromise hapo ? basi we hamnazo...!!
 
Last edited by a moderator:

Unazungumzia jeraha, ATC ilianzishwa na wana C.C.M ili kuiua Chadema, isingekuwa intelijisia nzuri ya Chadema tungekuwa tunaongea mengine hapa
 
Mwiba ukikuchoma usiogope kuutoa kwa sababu utaacha jeraha. Jeraha lina Tina na dawa ya mwiba ni kuung'oa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…