Ili swali nimejaribu kuuliza wee, nimechoka sijapata jibu lake yaani wataalamu wameshindwa kabisa kunidadavulia. Asante mkuu umeliweka wazi ngoja waje wataalam wa JF labda tunaweza pata jibu.
Nimeitoa Mahali kupitia Group moja la WhatsApp nadhani huyu kijana amejaribu kuelezea vizuri,kuhusu hivyo vitu vya Sanitizer Mkuu.Na mimi nilikuwa na utata lakini nilimuelewa vizuri kabisa.
HAND SANITIZER
Watu mnajiuliza kuna nini ndani ya Hand Sanitizer na baadhi yenu mkilalamika uwepo wa feki mtaani,Sasa Hii ifuatayo ni elimu kidogo kuhusu Hand Sanitizer na kwanini tunasisitizwa tunawe mikono yetu kila muda.
Lugha za kisayansi kidogo ila ukinunua soma uone Components zake ujue ipi ni bora na ipi sio bora,na kwanini huwezi kunywa hand sanitizer.*
Hand sanitizer zipo za makundi mawili ambayo ni Alcohol-based(Yenye Pombe) and Alcohol free hand(Isiyo na pombe) sanitizer.Ila kwa sasa muhimu kwetu na ambayo ina ufanisi mkubwa ni Alcohol- Based Hand sanitizer.
Sasa Hand sanitizer huwa na components zifuatazo
Alcohol 60-95%
Ambapo alcohol inayotumiwa sana ni Ethanol(CH3CH2OH) na nyinginezo zinazofaa kama ulisoma form four Organic chemistry utakuwa unakumbuka,na hiyo ethanol au Alcohol yoyote ambayo ina faa kuwepo basi ukinunua kwenye chupa inayoonyesha vilivyopo ndani Alcohol yoyote inaishia na herufi za mwisho 'ol' na itakuonyesha na asilimia zake na huwa inakuwepo kwa kiwango kikubwa(Asilimia).
Components zingine ambazo zinaweza kuwepo zikiambata ndani ni kama vile.. Water,Glycerin,Hydrogen peroxide, Isopropyl myristate,Propylene glycol, Tocopheryl acetate,Carbomer,Fragrance(Harufu) ndiyo maana huwa unaona zinanukia vizuri.
UFANISI WA HAND SANITIZER
Ufanisi wake inategemea na jinsi gani au ni kwa namna gani inatumika.Kwa mfano kiwango gani kinatumika,muda wa kutumia,kiasi cha matumizi au unachotumia,Wadudu gani au uchafu uliopo kwenye mikono ya mtu ambapo hivyo vyote vinategemea na mchanganyiko uliopo kwenye Hand sanitizer.
Kwa ushauri tu Alcohol-Based sanitizer ndiyo bora zaidi.
Hata hivyo kutokana na utofauti wa ufanisi wa hizo Hand Sanitizer inaweza
kudhibiti kusambaa kwa magonjwa ya kuambukiza kwenye mazingira ambayo unawaji wa mikono ni hafifu .Nadhani hapa kwenye group pia nanyi ni mashahidi kwa sisi Watanzania kunawa mikono ni shidaa.
Twende kwenye kama Hand-Sanitizer inaua vijidudu na virusi vilivyopo kwenye mikono na kwanini basi huruhusiwi
kunywa??
Madhara ya kunywa hiyo hand-sanitizer ni kwamba ukinywa unaweza kusababisha kuharibiwa kwa viungo vya ndani ya mwili kama vile INI na Figo,Matatizo ya kuona,Kupoteza kumbukumbu,Sumu za Pombe ambapo zinaweza kupelekea KIFO.Hii ni kwa sababu pombe iliyopo kwenye Hand-Sanitizer haijawekwa tayari kwa ajili ya kunywaa kama zile zingine zinazonywewa.
Ikumbukwe pia kama huna Hand-Sanitizer Nawa tu mikono vizuri na Sabuni yako na Maji tiririka basi hapo utaua vijidudu vyote vilivyopo mikononi.
TUENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI,CORONA IPO NA NI HATARI,JILINDE WEWE NA WENZAKO PIA,FUATA MAELEKEZO YOTE YA WATAALAMU ACHA MZAHA.NA TUENDELEE KULIOMBEA TAIFA LETU KWA MUNGU.