Siyo kwa Kiasi Hicho? 60% hawako huru kumkosoa Rais lakini 83% wanaweza kuwakosoa Wenyeviti wa Mtaa au Kijiji

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138
Wananchi 6 kati ya 10 wanasema hawako huru kukosoa kauli zinazotolewa na Rais.

Idadi kubwa ya wananchi (60%) wanasema hawako huru kukosoa kauli zinazotolewa na Rais
wakati asilimia 54 wanasema hivyo kuhusu kauli zinazotolewa na Makamu wa Rais na asilimia
51 Waziri Mkuu.

Wananchi wanajisikia huru zaidi kuwakosoa viongozi katika ngazi za chini za serikali au viongozi
wenye mamlaka ndogo. Wananchi nane kati ya kumi wanasema wanajisikia huru kuwakosoa
mwenyeviti wa vijiji/mitaa (83%), viongozi wa vyama vya upinzani (77%), madiwani (76%).

Inavyoonekana, wananchi wanajisikia huru zaidi kuwakosoa wabunge wao kuliko wakuu wa
mikoa na wakuu wa wilaya. Hii inaweza kuwa ni kwa sababu wananchi wanawachagua wabunge
kama wawakilishi wao na hivyo wanaona kuwa mbunge ana jukumu la kusikiliza mahitaji na
vipaumbele vyao na kuvifanyia kazi ipasavyo. Vinginevyo, inawezekana wananchi wanaona kuwa
wakuu wa mikoa na wilaya wanaonekana wapo karibu na Rais.

6.PNG


Idadi kubwa ya wananchi wanasema ‘wanaamini kabisa’ taarifa zinazotolewa na Rais (70%) au
Waziri Mkuu (64%). Wananchi wengi wanaamini ‘kwa kiasi fulani tu’ taarifa zinazotolewa na
viongozi wengine huku taarifa zinazotolewa na wabunge wa vyama vya upinzani, wanachama na
wafuasi wake zikichukuliwa kwa tahadhari.

Idadi kubwa ya wananchi wanasema ‘wanaamini kabisa’ taarifa zinazotolewa na Rais (70%) au
Waziri Mkuu (64%). Wananchi wengi wanaamini ‘kwa kiasi fulani tu’ taarifa zinazotolewa na
viongozi wengine huku taarifa zinazotolewa na wabunge wa vyama vya upinzani, wanachama na
wafuasi wake zikichukuliwa kwa tahadhari.

7.PNG


Source: Twaweza
 
Taarifa ya nani unaiamini zaidi? Majibu ya wananchi
1f447.png
: ‬

‪- Rais (70%)‬
‪- Waziri Mkuu (64%).‬
‪- Mwenyekiti wa kijiji (30%)‬
‪- Wabunge (chama tawala) (26%)‬
‪- Wabunge wa upinzani (12%)‬
‪- Viongozi wa Serikali kwa ujumla (22%).‬

‪Chanzo - [HASHTAG]#TWAWEZA[/HASHTAG]

Maoni yangu ni kwamba jumla ya idadi ya waliotoa maoni ni 100%
Vipengere vya maoni viko sita .... ukijumlisha maoni yao kwa % ndo unapata 100. Iweje sasa hizo nikizijumlisha zinazidi 100?

Hii hesabu ya asilimia imekaaje?
 
Utafiti huu umehoji watu wangapi? Umri gani? Wanaishi wapi? Uiano wa jinsia ukoje? Njia za ukusanyaji taarifa zilijuwaje? Nikijibiwa nitarudi kutoa maoni yangu!
 
Hata wao Twaweza wanadiriki kutoa matokeo ya utafiti unaoikosoa serikali? Hawajipendi?
 
Katika utafiti uliofanywa na Taasisi ya kitafiti ya Twaweza imebainisha kuwa asilimia 70 ya Watanzania wanaamini kabisa kila kile ambacho Rais Magufuli anakisema wakati asilimia 12 wanaamini kabisa kila kile ambacho wapinzani wanakisema.

Katika tafiti hii, asilimia 24 wanaamini kwa kiasi kile ambacho Rais Magufuli anakisema wakati asilimia 62 inawaamini kwa kiasi viongozi wa upinzani. Ni asilimia 3 tu ndio haiamini kile ambacho Rais anakisema.

Twaweza wameenda mbele zaidi na kusema utafiti wao umegundua wananchi wanawaamini wanachama/wafuasi wa upinzani kwa asilimia 9 tu.

Utafiti huu unazidi kudhihirisha kuwa wapinzani wana safari ndefu sana ili waaminike kwa wananchi wengi.

Ikumbukwe kuwa nguzo kuu ya ushindi kwa wanasiasa ni kuaminika kwa wananchi wengi.

Hali imekuwa mbaya zaidi kwa wapinzani baada ya kutumia miaka zaidi ya nane wakituaminisha kuwa Lowassa ni fisadi Papa na hafai hata kupewa fomu ya kugombea Urais halafu baada ya CCM kulikata jina la Lowassa, wapinzani wakamchukua na kumfanya mgombea wao bila hata kufuata mchakato waliojiwekea kikatiba na kikanuni.

twaweza.jpg
 
Kama kuna mtu humu alihojiwa na twaweza ajitokeze.sababu huwezi kukusanya takwimu bila kuuliza raia mmoja mmoja
 
Back
Top Bottom