Kweli Wabunge Mnyika,Tundu lissu na Halima Mdee ni Hazina ya Kutunza kwa ajili ya Mustakbali wa Taifa Hili.Ukisikia watu wa Kazi ndio wale
Jioni hii nilikuwa nafatilia kipindi cha Bunge hasa Kipengee cha Kupitia Budget ya Wizara ya Nchi ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano) iliyowasilishwa na Waziri Samia Suluhu baadae kujibu hoja kisha kupitiwa Kifungu kwa Kifungu!Kila waheshimiwa Mnyika na Lissu wakijenga hoja zao baada ya Kutoa Shilingai,Sita Anapotokea Akisimama kutete serikali Anaonekana kupwaya kwa kutoa Majibu ya Kuwaridhisha watoa Shilingi!Hadi hatua ya Mwenyekiti kuamua kura na ndipo hoja ya Shilingi inaposhindwa na Kura za Ndiyo na Hapana zile Makelele nafikiri Itikadi zinachangia ndio kushinda.Sita alikuwa anashindwa kufafanua jambo kwenye suala moja la Ukaguzi ktk Masuala ya Mazingira hadi Mh.Mnyika Akamlipua kwa kusema analidanganya Taifa!Afu Mnyika Akadadavua swala lenyewe!
Nae Mh.Ndugai Hayupo vizuri ktk ufafanuzu wa kikanuni za Bunge! alikuwa anababaika na Kutoa maelekezo kijujuu tu!Kazi Ipo kama hawa ndio Reserve ya Uongozi wa Serikali na Bunge basi Kazi tunayo!Manake jioni hii wote ni Wasaidizi wa Spika na wa PM!
Kazi ipo!Bora sisi wakulima tuliozoea yate!Mvua Kiduchu na Jua Kibao
Kama kawaida ya thread za makada, imekaa kishabiki na kusujudia watu bila kuangalia ukweli. Hatujaambiwa huko kupwaya na kwa namna gani, majibu yake, muonekano wake au ni kitu gani?