Sitta afunguka kuhusu Bandari

Hatupaswi kumwamini mwongo hata akiongea ukweli. sitta tulikupenda sana. Ila ulivyotufanya hatutaki kukiamini tena
 
Ningeomba Magufuli kwa ujasiri wake asiishie kutumbua wakurugenzi na makamishna huko bandarini lakni pia awatumbue mawaziri waliokua na dhamana hiyo km tunaona uozo huo na ikiwa tulikua na mawaziri waliotujibia hoja za bandari bungeni basi wanasabb ya kuhusikaaaaaa!!
 
Rais anayo madaraka ya kuvunja Bodi na kuteua nyingine kwa utashi wake! Ameivunja hiyo Bodi kwasababu anazozifahamu mwenyewe na washauri wake! Mbona hakumlalamikia JK aliyeteua wateule wake hadi dakika za mwisho!
 
mtajuana wenyewe
Mzee Sitta ni mwongo. Alinufaika na aliowateua ktk ufalme wa bandari: (1)Gari mpya la ofisi yake kama waziri V 8. (2) Ajitokeze hadharani awaambie watanzania namna pesa ya fidia ya waliohamishwa kupisha upanuzi wa airport ilivyopatikana na ilivyolipwa kwa victims. Note: Conflict of interest. Huyu ni JIPU KUBWA. Akae kimya tutamwaga uchafu wake wote huko bandarini.
 
Eeeh tumbuaneni vizuri
 
Mzee Six vipi akidi haijatimia tu au tusubiri na wale walioenda hijja,kapumzike mzee kalale mzee umekunywa uji wa wapi.?
 
Mzee sita ni miongoni mwa wazee wa hovyo kabisa,ambao hata nikizeeka sitaki kuwa kama yeye,kila nikikumbuka namna alivyosimamia kunyongwa kwa maoni yetu yaliyokusanywa na iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba,hakika najikuta kumchukia Mzee sita kuliko hata Makinda!MZEE SITTA HOVYO KABISA!
 
Kwanza ni muhimu tufahamu kwamba hujuma pale bandari zimekuwepo mpaka baada ya uchaguzi ambapo viongozi hao walikuwepo. Kiufupi pale palikuwa na mtandao ninaimani hata yeye mwenyewe ni jibu, kwa nini hakuibua ufisdi huo mkubwa. Uchunguzi ufanyike vizuri na kama kuna mawaziri walihusika wapelekwe mbele ya sharia.
 
Ana hoja nzito. Kwa ukweli kukurupuka kuna adha na kiwango fulani cha kusigina haki.

Jinsi ya kuwarudishia angalau haki na utu wao walioathirika ni vigumu.

Ni sawa na kuvua nguo wakati wa kuoga mtoni halafu kichaa akakimbia na nguo zako.
Kuwa mjumbe wa bodi sio haki. Ni dhamana tu. Inaweza kuondolewa muda wowote hata kama unafanya vizuri namna gani.
 
Mimi najiuliza wewe ni waziri mwenye dhamana, umeunda management body kwa ajili ya kukusaidia kubaini mapungufu, hiyo ni mwezi january, alafu hao watu wasikae kikao mda wote huo mpaka october...!!! alafu hapo hapo, mtu unasema kwamba ndio wenyewe waliibua mapungufu ambayo ndio alipewa waziri Majaliwa! Hivi hawa watu walikuwa wanafanya vipi kazi huku hawajakutana kwenye kikao hata kimoja tangu walipoteuliwa mpaka mwaka unaisha!!!!!!
Yani inashangaza, kikao kimoja between january na october, huku hakuna mapungufu yoyote yaliyoshughulikiwa, alafu unasema wameonewa!?

...kama report ya mapungufu aliyokuwa nayo Majaliwa ilikuwa yao hao wajumbe, kwanini Majaliwa aone kuna haja ya kuwaondoa!!!!!?
 
Alipigisha kura wafu bunge la katiba, kwa nini nimuamini sasa? Mzee, nenda urambo kapumzike, acha nchi mlioibomoa ijengwe!
 
Labda angedokeza hao wstakaoleta vikwazo.
 
Wamekutana mara moja tokea wameteuliwa, wamefanya ubadilifu wa kiwango gani?

... ...tukiweka ushabiki pembeni, kwani hao watu waliondolewa kwasababu wenyewe kama wao walifanya ubadhilifu, au waliondolewa kwasababu walinyamazia ubadhilifu wa wazi ambao haukuitaji kungoja mpaka mwaka uishe ndio waufanyie kazi
...mimi sioni kama hawa wajumbe wanatofauti yoyote na sitta ambaye ndiye alikuwa waziri mwenye dhamana lakini akaondoka bila kuyafanyia kazi hayo madudu ya TPA... Kwahiyo, wakwende zao tu
 
.....six tulia ushaanikwa huko! Acha RAIS NA WAZIRI MKUU WAFANYE KAZI BANA...../
HIZI ZAMA ZINGINE BANA!
STAY COOL AND WATCH ""MEN AT WORK""
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…