Binti wa zamani
Platinum Member
- Nov 19, 2011
- 11,763
- 27,149
Wakati najifungua mtoto wangu wa kwanza kuna daktari nafikiri alikua bado ni mwanafunzi Muhimbili alinishika mkono kwa zaidi ya lisaa limoja wodini akinituliza, na kunitia moyo.
Yule daktari alikaa pembeni ya kitanda changu akawa ananiambia itakua fine, itakua fine, kwa sababu niliingiwa hofu (anxiety) nikawa nalia nasema “naogopa”.
Hakunifokea wala kuniongelesha kwa ukali na alielewa situation yangu (nilienda hospitali kliniki yangu ya mwisho kumbe tayari nimeshaingia kwenye labour bila kujijua, nikabaki hospitali kujifungua bila kutarajia).
Sitasahau alivyonicomfort na kubaki na mimi wodini mpaka mume na mama yangu walivyofika. Na aliendelea kubaki wodini mpaka nilivyojifungua masaa mawili baadaye.
Ule moyo wake ulinigusa sana, huwa namkumbuka mara kwa mara na kumuombea mema. Sikuwahi kukutana naye tena baada ya kujifungua na sijui yuko wapi. Natumai popote alipo anazidi kubarikiwa sana.
Nani alikutendea wema kwenye kipindi chako cha uhitaji hautakuja kumsahau?
Yule daktari alikaa pembeni ya kitanda changu akawa ananiambia itakua fine, itakua fine, kwa sababu niliingiwa hofu (anxiety) nikawa nalia nasema “naogopa”.
Hakunifokea wala kuniongelesha kwa ukali na alielewa situation yangu (nilienda hospitali kliniki yangu ya mwisho kumbe tayari nimeshaingia kwenye labour bila kujijua, nikabaki hospitali kujifungua bila kutarajia).
Sitasahau alivyonicomfort na kubaki na mimi wodini mpaka mume na mama yangu walivyofika. Na aliendelea kubaki wodini mpaka nilivyojifungua masaa mawili baadaye.
Ule moyo wake ulinigusa sana, huwa namkumbuka mara kwa mara na kumuombea mema. Sikuwahi kukutana naye tena baada ya kujifungua na sijui yuko wapi. Natumai popote alipo anazidi kubarikiwa sana.
Nani alikutendea wema kwenye kipindi chako cha uhitaji hautakuja kumsahau?