Sisi wake zetu hawatongozwi??

Sisi wake zetu hawatongozwi??

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2009
Posts
6,157
Reaction score
4,454
Nilishaambiwa au kusikia mara kadhaa kwamba Mwanamke kashtaki kwa Mmewe kwamba kuna Mwanamme anamfuatilia/anamtongoza, matukio haya yapo ya aina kadhaa:-

1. Mwanamke kulalamika kwa Mmewe kwamba katongozwa na mtu anayemfahamu huyu mwanamke kaolewa na kaolewa na nani.

2. Mwanamke kulalamika kwa Mmewe kwamba katongozwa na Mwanamme asiyefahamu kwamba huyu Mwanamke kaolewa.

Kwa sisi ambao wake zetu hawajawahi kutuambia kama huwa wanatongozwa tubaki na picha gani?

1.Wake zetu hawatongozwi?
2.Wanatongozwa wanakataa lakini Wanapuuzia kutuambia?
3.Wanatongozwa wanakubali na kuifanya iwe siri?

Najaribu kuwaza tu kwasababu mimi mke wangu hajawahi kuniambia kwamba ametongozwa na mtu yeyote.
 
Kwa mila na desturi zetu, kabla ya mwanamke hajaolewa na au mara tu anapovunja ungo hupewa mafunzo maalumu
yanayojulikana kama unyago, msondo, nk. Katika mafunzo haya mwanamke anafundishwa namna ya kuishi na mume,
kumtunza mume na watoto, nakadhalika. Mwanamke hatarajiwi kuwa sababu ya fadhaa, wasiwasi, au hasira ya mumewe, hivyo hatarajiwi kumwelezea mumewe juu ya yeyote anayemtongoza au mahusiano yake ya siku za nyuma. Kikubwa anachotarajiwa ni kuwa mwaminifu kumkataa yeyote anayemtongoza na kutokujiweka katika mazingira ya kutongozwa kwani mwaname hutongoza anapoona kuna mwanya/dalili za kufanikiwa kama akijaribu. Mwanamke ambaye kila kukicha anamueleza mumewe kuwa fulani kamtongoza basi hajafuzu mafunzo ya unyago, atamfanya mumewe kuwa na wasiwasi wakati wote na kushindwa kufanya kazi, pia atamgombanisha na marafiki, jamaa na ndugu zake. Mwanamke ukijiweka katika mazingira ya kutongozwa, mfano kujichekeshachekesha, kuombaomba ofa, kukubali mialiko isiyo ya kazi wala biashara, kupenda sana kusifiwa kuhusu sura na umbile lake,kupenda sana kuwaelezea watu kuhusu madhaifu ya mumewe, na kugawa ovyo namba yake ya simu ni baadhi tu mazingira yanayotoa mwanya wa kutongozwa.
Wanaume tunajua kuwa kuna mwanamke ambaye hata kama unamtamani kiasi gani lakini kila ukimwangalia usoni huoni uwezekano/nafasi ya kukubaliwa, hivyo hujikuta ukiahirisha kila mara wazo la kumtongoza.
 
Hivi kutongoza ni issue? Issue ni kukubali ukijijua kabisa wewe ni mke wa mtu. Kuna wanaume wanatongoza kwa burudani tu asikie dada atasemaje.
 
Kwa mila na desturi zetu, kabla ya mwanamke hajaolewa na au mara tu anapovunja ungo hupewa mafunzo maalumu
yanayojulikana kama unyago, msondo, nk. Katika mafunzo haya mwanamke anafundishwa namna ya kuishi na mume,
kumtunza mume na watoto, nakadhalika. Mwanamke hatarajiwi kuwa sababu ya fadhaa, wasiwasi, au hasira ya mumewe, hivyo hatarajiwi kumwelezea mumewe juu ya yeyote anayemtongoza au mahusiano yake ya siku za nyuma. Kikubwa anachotarajiwa ni kuwa mwaminifu kumkataa yeyote anayemtongoza na kutokujiweka katika mazingira ya kutongozwa kwani mwaname hutongoza anapoona kuna mwanya/dalili za kufanikiwa kama akijaribu. Mwanamke ambaye kila kukicha anamueleza mumewe kuwa fulani kamtongoza basi hajafuzu mafunzo ya unyago, atamfanya mumewe kuwa na wasiwasi wakati wote na kushindwa kufanya kazi, pia atamgombanisha na marafiki, jamaa na ndugu zake. Mwanamke ukijiweka katika mazingira ya kutongozwa, mfano kujichekeshachekesha, kuombaomba ofa, kukubali mialiko isiyo ya kazi wala biashara, kupenda sana kusifiwa kuhusu sura na umbile lake,kupenda sana kuwaelezea watu kuhusu madhaifu ya mumewe, na kugawa ovyo namba yake ya simu ni baadhi tu mazingira yanayotoa mwanya wa kutongozwa.
Wanaume tunajua kuwa kuna mwanamke ambaye hata kama unamtamani kiasi gani lakini kila ukimwangalia usoni huoni uwezekano/nafasi ya kukubaliwa, hivyo hujikuta ukiahirisha kila mara wazo la kumtongoza.
Umemaliza kila kitu
 
Kwa mila na desturi zetu, kabla ya mwanamke hajaolewa na au mara tu anapovunja ungo hupewa mafunzo maalumu
yanayojulikana kama unyago, msondo, nk. Katika mafunzo haya mwanamke anafundishwa namna ya kuishi na mume,
kumtunza mume na watoto, nakadhalika. Mwanamke hatarajiwi kuwa sababu ya fadhaa, wasiwasi, au hasira ya mumewe, hivyo hatarajiwi kumwelezea mumewe juu ya yeyote anayemtongoza au mahusiano yake ya siku za nyuma. Kikubwa anachotarajiwa ni kuwa mwaminifu kumkataa yeyote anayemtongoza na kutokujiweka katika mazingira ya kutongozwa kwani mwaname hutongoza anapoona kuna mwanya/dalili za kufanikiwa kama akijaribu. Mwanamke ambaye kila kukicha anamueleza mumewe kuwa fulani kamtongoza basi hajafuzu mafunzo ya unyago, atamfanya mumewe kuwa na wasiwasi wakati wote na kushindwa kufanya kazi, pia atamgombanisha na marafiki, jamaa na ndugu zake. Mwanamke ukijiweka katika mazingira ya kutongozwa, mfano kujichekeshachekesha, kuombaomba ofa, kukubali mialiko isiyo ya kazi wala biashara, kupenda sana kusifiwa kuhusu sura na umbile lake,kupenda sana kuwaelezea watu kuhusu madhaifu ya mumewe, na kugawa ovyo namba yake ya simu ni baadhi tu mazingira yanayotoa mwanya wa kutongozwa.
Wanaume tunajua kuwa kuna mwanamke ambaye hata kama unamtamani kiasi gani lakini kila ukimwangalia usoni huoni uwezekano/nafasi ya kukubaliwa, hivyo hujikuta ukiahirisha kila mara wazo la kumtongoza.

Kwa hiyo huwenda wake zetu pia wanatongozwa lakini hawatuambii tu
 
ha haaa, kuna kakangu aliwahi sema kuwa siku mkewe akija kumwambia kuwa fulani kamtongoza ndo siku atakayompa kibano, maana atajua kabisa kuwa huyo kamwambia sababu hamtaki, anayemtaka hatamwambia......

Ukweli mimi sioni sababu ya kumwambia mume fulani kanitongoza, ili iweje?
 
Hivi kutongoza ni issue? Issue ni kukubali ukijijua kabisa wewe ni mke wa mtu. Kuna wanaume wanatongoza kwa burudani tu asikie dada atasemaje.

Kutongoza ni kitu serious bana!!! achana na ile hali ya kumtania mwanamke
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom