Siri nyingi za mafanikio hujificha kwenye vitu vidogovidogo kama hivi

Peter Agostino

Senior Member
Sep 23, 2016
105
226
Mafanikio katika jambo lolote lile maishani mwanadamu analolenga kufanya hutokea nje ya uwanja wake wa faraja, kwa kimombo wanasema, “outside of your comfort zone”,. Unataka kuwahi kazini, shuleni au kwenye biashara zako kwa lengo la kuzidisha mafanikio, ufanisi au kipato zaidi, ni lazima ukubaliane na kuachia shuka, kukatisha usingizi wako mtamu wa alfajiri na kupambana na umande wa asubuhiasubuhi kwenye nyasi katika uchochoro unaotoka nyumbani kwako kabla hujafika stendi kupanda basi.

Unataka mwili wako kuwa imara(fiti), ni lazima kwanza uvuje jasho jingi kwa mazoezi nk. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa katika biashara au sekta nyingine zozote zile za kimaisha. Mafanikio yanamtaka mtu kuchukua hatua ambazo mara nyingi haziwezi kumpendeza hata kidogo, na hali hiyo ya kutokupendezwa ndiyo tunayopigana nayo kila siku ndani ya fikra zetu, na ili tufanikiwe basi ni lazima tushinde vita hiyo ya kifikra kabla hatujaanza kusaka njia kuu za mafanikio katika maisha.

Binadamu mara nyingi tumekuwa tukisaka siri za mafanikio katika mambo mbalimbali tunayoyafanya kama vile, jinsi ya kufanikiwa kibiashara, jinsi ya kupata pesa, kufanikiwa katika masomo, au katika maeneo mengine yeyote yale kwenye maisha. Ukweli ni kwamba majibu ya swali hilo wala siyo magumu hata kidogo kwani siri kuu za mafanikio hujidhihirisha zenyewe katika mifano ya vitu, watu na hata mambo mbalimbali yanayotokea kwenye mazingira yetu ya kawaida kabisa.


Mifano hiyo katika maisha ya kawaida ndiyo leo nataka nikutajie katika makala hii, hivyo karibu sana tujifunze pamoja, hakikisha unaisoma makala hii mpaka mwisho kupata manufaa yote yaliyokusudiwa. Tafadhali bonyeza kiungo kifuatacho kuisoma makala hiyo yote katika blogu ya jifunzeujasiriamali.
SIRI NYINGI ZA MAFANIKIO HUJIFICHA KWENYE VITU VIDOGOVIDOGO KAMA HIVI...
 
Kuna vitu ni vigumu kupata majibu sahihi yanavyovihusu hivyo vitu, mfano mafanikio
 
Hakuna jibu sahihi kwenye mafanikio ndio au hapana yote ni majibu ya mafanikio kupata si ujanja wala kufanya juhudi kubwa na kukosa pia sio ujinga wala uzembe
Nimekusoma vyema!
Ila jiulize mafanikio ni nini?
 
"Success Has No Formulae"
Mafanikio Hayana Njia Nyoofu, fulani anaweza fanikiwa kutokana na formular zake..Ila hakuna guarantee zitafanya kazi sababu ni nyakati mbili tofauti, na ni watu tofayti..labda hata ndoto ni tofauti..Katika Mafanikio kila mtu atakwambia yale yale..Kujituma, Kutokata Tamaa, Kuwa Na Malengo, Kujiamini, nk...Na Hizo Sio Siri...... Hakuna Formulae
....Ahsante Pia Kwa Mada
Uko sawa - kama ilivyo kwamba kila chombo cha kielektroniki kilivyo na serial number - ndivyo kila mwanadamu alivyo na SIRI YA MAFANIKIO YAKE.
 
Mafanikio katika jambo lolote lile maishani mwanadamu analolenga kufanya hutokea nje ya uwanja wake wa faraja, kwa kimombo wanasema, “outside of your comfort zone”,. Unataka kuwahi kazini, shuleni au kwenye biashara zako kwa lengo la kuzidisha mafanikio, ufanisi au kipato zaidi, ni lazima ukubaliane na kuachia shuka, kukatisha usingizi wako mtamu wa alfajiri na kupambana na umande wa asubuhiasubuhi kwenye nyasi katika uchochoro unaotoka nyumbani kwako kabla hujafika stendi kupanda basi.

Unataka mwili wako kuwa imara(fiti), ni lazima kwanza uvuje jasho jingi kwa mazoezi nk. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa katika biashara au sekta nyingine zozote zile za kimaisha. Mafanikio yanamtaka mtu kuchukua hatua ambazo mara nyingi haziwezi kumpendeza hata kidogo, na hali hiyo ya kutokupendezwa ndiyo tunayopigana nayo kila siku ndani ya fikra zetu, na ili tufanikiwe basi ni lazima tushinde vita hiyo ya kifikra kabla hatujaanza kusaka njia kuu za mafanikio katika maisha.

Binadamu mara nyingi tumekuwa tukisaka siri za mafanikio katika mambo mbalimbali tunayoyafanya kama vile, jinsi ya kufanikiwa kibiashara, jinsi ya kupata pesa, kufanikiwa katika masomo, au katika maeneo mengine yeyote yale kwenye maisha. Ukweli ni kwamba majibu ya swali hilo wala siyo magumu hata kidogo kwani siri kuu za mafanikio hujidhihirisha zenyewe katika mifano ya vitu, watu na hata mambo mbalimbali yanayotokea kwenye mazingira yetu ya kawaida kabisa.


Mifano hiyo katika maisha ya kawaida ndiyo leo nataka nikutajie katika makala hii, hivyo karibu sana tujifunze pamoja, hakikisha unaisoma makala hii mpaka mwisho kupata manufaa yote yaliyokusudiwa. Tafadhali bonyeza kiungo kifuatacho kuisoma makala hiyo yote katika blogu ya jifunzeujasiriamali.
SIRI NYINGI ZA MAFANIKIO HUJIFICHA KWENYE VITU VIDOGOVIDOGO KAMA HIVI...
Ni ngumu sana kudefine maana ya mafanikio....mafanikio yako kwangu yaweza kuwa ni failure na failure yangu kwako inaweza kuwa ni mafanikio...
 
Nimepitia kule kwenye Blog yako mkuu " nachoweza kusema ni Kwamba kila siku asubuhi sinto thubutu kauacha kupita na kuingiza vitu vipya ...

Topic zilizopo kule ni Tija sana kwa free thinkers...ASANTE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom