Siri kubwa CCM!!!

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2009
Posts
6,157
Reaction score
4,454
Nimekuwa nafuatilia masuala ya CCM ni kwanini viongozi wake wengi wanakumbwa na tuhuma za ufisadi??? Nimeingia kwenye website yao nimesoma masharti ya uanachama ndani ya CCM ni pamoja na kuwa "mbu". Moja ya masharti ya uanachama CCM inasomeka hivi:

Kuwa mtu anayependa kushirikiana na wenzake. Kuwa mbu ambaye siku zote yuko mstari wa mbele katika utekelezaji wa mambo yote ya umma, kulingana na miongozo ya CCM.

Kwa uelewa wangu mtu mwenye tabia za mbu ni mnyonyaji na hafai katika jamii hivyo, huenda wanachama wake wanatimiza hili sharti.

Aleast sasa sitoweza kumlaumu Lowasa, Rostam wala Kalamagi ila CCM yenyewe ibadilishe masharti yake.

Source:Chama Cha Mapinduzi - CCM
 
Hapo kwenye MBU wangeongezea kuwa KUPE!

Unarukia mada bila hata kutafakari nini konaweza kukuta kisheria, hivi huoni kwamba mtoa mada amekitukana chama kwa kutoa maneno ya kichochezi? hata chama kikiwa hovyo vipi hakiwezi kikawa na sharti kama hilo.
 

Kama wewe siyo mwana CCM Unatafuta nini kwenye website ya CCM? Hauna hoja
 
Yaani niwe mbu?? Haiwezekani
 
Unarukia mada bila hata kutafakari nini konaweza kukuta kisheria, hivi huoni kwamba mtoa mada amekitukana chama kwa kutoa maneno ya kichochezi? hata chama kikiwa hovyo vipi hakiwezi kikawa na sharti kama hilo.

acha kuzusha amekitukana chama wapi? yeye si amenukuu moja ya sharti ya uanachama wa CCM? kama ni mfurukutwa basi umekubuhu
 
Kama wewe siyo mwana CCM Unatafuta nini kwenye website ya CCM? Hauna hoja

Nadhani wewe ndio hauna hoja.
Kwenye website yao kuna sehemu wametamka USIFUNGUE WEBSITE HII KAMA WEWE SIO CCM?
 
Unarukia mada bila hata kutafakari nini konaweza kukuta kisheria, hivi huoni kwamba mtoa mada amekitukana chama kwa kutoa maneno ya kichochezi? hata chama kikiwa hovyo vipi hakiwezi kikawa na sharti kama hilo.

MwanaCCM mimi nadhani tujadiri ukweli je hilo sharti halipo? Kwasababu nia yangu siyo mbaya ni kujua tu kwanini viongozi wa CCM wengi wanaandamwa na tuhuma za ufisadi, nikiwa nahangaika kujua sera za chama na malengo yake nikakutana na hilo sharti sasa unategemea hapa sijaupata ukweli?
 
........
Kuwa mtu anayependa kushirikiana na wenzake. Kuwa mbu ambaye siku zote yuko mstari wa mbele katika utekelezaji wa mambo yote ya umma, kulingana na miongozo ya CCM.

Aisee hii kali sana yaani katika kutumia lugha ya picha wameona mbu ndo anafaa. Si bora wangetumia nyuki au mchwa ambao n wadudu hufanya kazi kwa bidii na ushirikiano mkubwa.

Mbu yuko mstari wa mbele kuleta magonjwa. Nadhani watairekebisha siku si nyingi

Mtikilia yeye anasema alama za jembe na nyundo za CCM kazi yake ni

  • Nyundo inakugonga kichwani mpaka unakufa

  • Jembe - kazi yake ni kufukia na kuzika.

Bora wabadilishe nazo hizo waweke picha ya trekta na .....
 

Asante lakini moyoni kwako hakuna jema, nyie ndo wale hata ukitendewa mema miamoja lakini kwa bahati mbaya ukatendewa baya moja tuu unasahau yooote
 
Asante lakini moyoni kwako hakuna jema, nyie ndo wale hata ukitendewa mema miamoja lakini kwa bahati mbaya ukatendewa baya moja tuu unasahau yooote

Du! mkuu bado unawakumbatia ccm tuu?
Umepitwa na wakati jamaa yangu.
 

Mkuu nimeingia humo kwenye iyo website, ni kweli mbu imeandikwa but ukisoma vizuri utaona kuwa ni typing error. Ingekuwa wana maanisha hivyo, neno mbu lingetumika hata kwenye sentensi ya mwazo ya paragraph. CCM siwapendi kabisaaa but atleast haki yao nawapa pale wanapostaili.

(Kuwa mtu anayependa kushirikiana na wenzake. Kuwa mbu ambaye siku zote yuko mstari wa mbele katika utekelezaji wa mambo yote ya umma, kulingana na miongozo ya CCM.)
 
Unarukia mada bila hata kutafakari nini konaweza kukuta kisheria, hivi huoni kwamba mtoa mada amekitukana chama kwa kutoa maneno ya kichochezi? hata chama kikiwa hovyo vipi hakiwezi kikawa na sharti kama hilo.

sipendi kuita mawazo ya watu wengine CRAP, ila kama ningeweza ningeiita hii CRAP....ila siwezi.
 

Angalia ndugu yangu huenda hawakumaanisha unavyotaka kumaanisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…