Sirat fundisho la uongo kutoka upagani

Sirat fundisho la uongo kutoka upagani

hamis77

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
18,250
Reaction score
26,639
UISLAMU NDANI YA UPAGANI WA SIRAT (DARAJA LA JEHANAMU)

Moja ya mafundisho yanayopatikana ndani ya Uislamu ni fundisho la Sirat daraja linalowekwa juu ya Jahannamu ambalo wanadamu wote watalivuka siku ya hukumu. Wengine watapita salama, wengine kwa shida, na wengine wataanguka motoni.

Lakini Sirat si fundisho pekee linalohusiana na hatua ya mpito baada ya kifo. Ndani ya Uislamu pia kuna dhana ya adhabu za kaburi mateso au neema anayopata mtu kabla ya siku ya hukumu.

Leo hii tutachunguza mfanano kati ya

Toharani (Purgatory) ya Kanisa Katoliki
Sirat katika Uislamu
Adhabu za kaburi
Ritual za Freemasonry
Mafundisho ya Misri ya kale


Swali kuu, Je, dhana hizi ni za kipekee au zina muundo mmoja wa kihistoria?

Toharani (Purgatory) katika Ukatoliki
Kwa mujibu wa mafundisho ya Kanisa Katoliki, mtu akifa haendi moja kwa moja mbinguni, bali anaweza kwenda Toharani kwa ajili ya kutakaswa.

I.A. Sadler anaandika katika Mystery, Babylon the Great (Vol. 1, uk. 53)

Purgatory ni mahali ambapo roho huteseka kwa muda baada ya kifo kwa sababu ya dhambi, na inaweza kusaidiwa kwa maombi ya waliobaki duniani.

Muundo wake ni
➡️ Kifo
➡️ Mateso ya muda
➡️ Kutakaswa
➡️ Kisha kuingia mbinguni

Adhabu za Kaburi katika Uislamu
Ndani ya hadithi za Kiislamu,
inaelezwa kuwa mtu anapokufa, ataulizwa maswali kaburini na anaweza kupata neema au adhabu mpaka siku ya hukumu.
Katika hadithi zilizomo ndani ya
Sahih al-Bukhari na Sahih Muslim,

inaelezwa kwamba

Maiti ataulizwa kuhusu Mola wake, dini yake na Mtume wake.
Kaburi linaweza kubanwa.
Wengine wataadhibiwa kwa sababu ya matendo yao.


Hapa tunaona dhana ya

➡️ Mateso baada ya kifo
➡️ Kabla ya hukumu ya mwisho
➡️ Hali ya mpito

Hii inafanana kimuundo na Toharani sehemu ya muda kabla ya hukumu kamili.

Sirat – Daraja la Jahannamu

Qur’an 19:71 inasema

“Wala hapana yeyote katika nyinyi ila ni mwenye kuifikia (Jahannamu).”

Katika hadithi ndani ya Sahih al-Bukhari, iliyopokelewa na Abu Sa'id al-Khudri, daraja linaelezwa kuwa

La kuteleza
Lina miiba na ndoano
Wengine watavuka haraka
Wengine watapata majeraha
Wengine wataanguka motoni


Hapa tena tuna

➡️ Kupitia juu ya moto
➡️ Hatari ya kuanguka
➡️ Mtihani
➡️ Kuingia Peponi

Freemasonry na Mtihani wa Moto
Katika maandiko ya I.A. Sadler (Vol. 1, uk. 14)

Mtu akishindwa kuvuka ufa wa hekalu huanguka katika shimo la moto.

Huu ni mtihani wa kiibada unaohusisha

➡️ Kuvuka ufa
➡️ Moto
➡️ Hatari ya kuanguka
➡️ Kupata hadhi ya juu baada ya kufaulu

Misri ya Kale – Kupitia Kisiwa cha Moto

Katika The Egyptian Book of the Dead, roho inasema


“Niruhusu nipite katika kisiwa cha moto… nimetakaswa… nimejitakasa…”

Muundo ni ule ule
➡️ Moto
➡️ Hukumu
➡️ Utakaso
➡️ Kuingia
7️⃣ Muundo wa Pamoja

Tukiziangalia kwa pamoja
Adhabu za kaburi
Sirat
Toharani
Ritual za Freemason
Mafundisho ya Misri ya kale


Zinaonesha mfumo wa hatua tatu
Kifo
Sehemu ya mpito yenye mateso au mtihani
Kutakaswa au kuangamia
Kuingia katika hali ya utukufu au kuendelea katika adhabu


Hoja inayojengwa hapa ni kwamba dhana ya “moto wa mpito” au “mateso kabla ya hukumu kamili” imekuwepo katika mifumo mingi kabla ya Uislamu.

Na mwanzilishi wa huu UONGO,UPOTOSHAJI,UMIZIMU NI SHETANI MWENYEWE akianzia pale Edeni

Genesis 2:17, Mungu alisema:

“...hakika utakufa.”

Lakini katika Book of Genesis 3:4, nyoka alisema

“Hakika hamtakufa.”

baada ya mwanadamu kuanza kufa , Shetani akabadili msemo kuwa watu hawafi Bali Kuna sehemu wanakwenda ,na huu UONGO ndio unaitwa UMIZIMU,

Tunauona kwenye Hadi muhamad anakuja kuuingiza kwenye UISLAMU kwa kusema kuwa roho huendelea kuishi mahali fulani.

Ndipo zikazaliwa dhana za
Adhabu za kaburi
Toharani
Daraja la moto
Maeneo ya utakaso


MAFUNDISHO HAYA NI KAULI ILE ILE YA SHETANI YA PALE EDENI ALIPOSEMA HAKIKA HAMTAKUFA

Kwa kulinganisha Sirat, adhabu za kaburi, Toharani, ritual za Freemasonry na mafundisho ya Misri ya kale, tunaona mfanano wa muundo huu 👇

Moto → Mtihani → Utakaso → Kuingia au Kuangamia

Swali linalobaki ni hili, Je Muhammad kuchukua FUNDISHO LA UONGO KUTOKA KWA WAKATOLIKI ilikuwa ni bahati mbaya ?

TAFAKARI
images - 2026-02-14T190640.702.jpeg
 
Watu wa dini hadi tutachanganyikiwa sasa maana wenyewe kwa wenyewe tunapigana spana halafu kuna wale wanasema hakuna Mungu basi mtu ukikutana na post mbili mfano huu unabaki tepetepe umeloa jasho.

All in all bado game ni ngumu,mshindi ni yule atakaeilinda imani yake (kama ya kweli au siyo kweli kwa mujibu wetu to each other) mpaka mwisho.
 
Watu wa dini hadi tutachanganyikiwa sasa maana wenyewe kwa wenyewe tunapigana spana halafu kuna wale wanasema hakuna Mungu basi mtu ukikutana na post mbili mfano huu unabaki tepetepe umeloa jasho.

All in all bado game ni ngumu,mshindi ni yule atakaeilinda imani yake (kama ya kweli au siyo kweli kwa mujibu wetu to each other) mpaka mwisho.
Katika zama hizi inatakiwa tuweke uongo wote hadharani

Watu wamedanganywa sana
 
Kobaz ni matatizo matupu, roho ya mtu ikifa imekufa tu wala hapana mahali huenda, hutulia kaburini hata wakati wa hukumu utakapowadia.
 
Nilichokiona ni kuwa kila mahali kuna moto na huu haujalishi ulikuwa mwema au mmbaya 😭😭
 
Back
Top Bottom