P h a r a o h
JF-Expert Member
- Mar 25, 2024
- 993
- 1,882
Wakati wengi wanamkumbuka Isaac Newton kwa kuweka misingi ya physics ya kisasa na kubalilisha jinsi tunavyoelewa ulimwengu kwa ugunduzi wa gravity na laws of motion, watu wachache wanajua kuwa pia alijishughulisha sana na tafsiri za maandiko ya Biblia, hasa kitabu cha unabii cha Daniel na Ufunuo wa Yohane.
Sir Isaac Newton ameandika vitu vingi zaidi kuhusu biblia na imani kuliko maandiko yake kuhusu hesabu na physics yakijumlishwa. hivyo alikua curious sana kwenye mambo ya dini.
Katika maandishi yake ya binafsi (ambayo hayakuchapishwa wakati wa uhai wake), Newton alijaribu kuchambua namba na alama za kinabii zilizomo kwenye Biblia. Akitumia mahesabu hayo, alifikia wazo kwamba mwaka 2060 unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wa mfumo wa dunia wa sasa.
Hata hivyo Newton hakusema dunia italipuka au kuangamia kabisa mwaka huo. Alimaanisha kuwa ukawa mwaka ambao utaratibu wa dunia utabadilika sana, na kua mwanzo wa kipindi kipya cha kihistoria au kiroho.
Muhimu zaidi, Newton aliandika wazi kuwa 2060 ni mwaka wa mapema zaidi unaowezekana. Lengo lake lilikuwa pia kupinga watu waliokuwa wanatabiri tarehe za mwisho wa dunia, kwa kuonyesha kuwa kwa tafsiri yake tukio hilo haliwezi kuwa mapema hivyo.
Kwa hiyo, hata mmoja wa wanasayansi wakubwa kabisa katika historia alikua na curious kujaribu kuelewa siri za wakati wa mwisho, akichanganya sayansi, historia, na tafsiri za maandiko ya dini.
Sir Isaac Newton ameandika vitu vingi zaidi kuhusu biblia na imani kuliko maandiko yake kuhusu hesabu na physics yakijumlishwa. hivyo alikua curious sana kwenye mambo ya dini.
Katika maandishi yake ya binafsi (ambayo hayakuchapishwa wakati wa uhai wake), Newton alijaribu kuchambua namba na alama za kinabii zilizomo kwenye Biblia. Akitumia mahesabu hayo, alifikia wazo kwamba mwaka 2060 unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wa mfumo wa dunia wa sasa.
Hata hivyo Newton hakusema dunia italipuka au kuangamia kabisa mwaka huo. Alimaanisha kuwa ukawa mwaka ambao utaratibu wa dunia utabadilika sana, na kua mwanzo wa kipindi kipya cha kihistoria au kiroho.
Muhimu zaidi, Newton aliandika wazi kuwa 2060 ni mwaka wa mapema zaidi unaowezekana. Lengo lake lilikuwa pia kupinga watu waliokuwa wanatabiri tarehe za mwisho wa dunia, kwa kuonyesha kuwa kwa tafsiri yake tukio hilo haliwezi kuwa mapema hivyo.
Kwa hiyo, hata mmoja wa wanasayansi wakubwa kabisa katika historia alikua na curious kujaribu kuelewa siri za wakati wa mwisho, akichanganya sayansi, historia, na tafsiri za maandiko ya dini.