Fimbo ya Musa
Member
- Jul 21, 2012
- 94
- 13
Habari zenu wana janv! Mimi kero yangu ni hii: unakuta uko na rafiki yako au hata wife anaongea na simu then from no where anakupa simu eti uongee na huyo mtu anayeongea naye kwenye simu BILA KUKWAMBIA NI NANI! Mimi huwa inanifedhehesha sana kwa kweli kwani saa ingine unakuta ni mama mkwe! Ambapo ilitakiwa akwambie kabla ili ujiandae kuongea naye. Halafu saa ingine unakuwa hauko kwenye MOOD ya kuongea na simu,lakini unashangaa ghafla unapewa simu eti uongee na mtu ambaye hata hujaambiwa ni nani! Nasema hivi wenye tabia hii acheeeeeeeeeeen hizo!