Sipati picha siku ya hukumu itakuaje

Sipati picha siku ya hukumu itakuaje

Nebuchadinezzer

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2018
Posts
1,403
Reaction score
2,549
Hebu fikiria siku ambayo halaiki ya watu imekodoa macho kuangalia matendo yako yote yaliyo ya wazi na yale ya siri.

Hebu piga picha yule rafiki yako uliyemchukulia mke wake anakuona unazini na mke wake.

Hebu piga picha mzazi mwenzako anakuona vile unamtoa kafara mtoto wenu kisa utajirike.

Hebu piga picha tunakuona ukiwa unaroga majirani zako na wakati kanisani au msikitini hukosi.

Hebu piga picha tunaona ukiwapanga majambazi wakavamie kwa mjomba, binamu au baba yako.

Hebu piga picha wewe mchungaji au shehe unaonekana ukizini gesti na mhumini wako.

Hebu piga picha wewe unayetoa kafara raia wasio na hatia ili ushinde uchaguzi wa jimbo lako.

Hebu piga picha ulivyomuaga mmeo kuwa unaenda sokoni au kwa rafiki yako kumbe unaenda gheto la mchepuko wako.

Hebu piga picha siku hiyo kale katabia kako ka kudanganya wana JF. kanaonekana wazi.

Hebu piga picha siku ambayo yule Adam na Hawa uliyemsikia na kumsoma unamuona kwa macho.

Hebu piga picha pale unapogundua kwa mara ya kwanza watoto ulionao sio wako.

Hebu piga picha wafanya kazi wenzako kwa mara ya kwanza wanajua kua ulipata cheo chako baada ya kutanua mabaja.

Hebu piga picha siku ambayo kwa mara ya kwanza JF members tunajua jina lako halisi.

Mimi nimejaribu kupiga picha na kisimu changu sipati picha kamili.

Unaambiwa kila jambo unalolitenda litaletwa hadharani haijalishi la wazi au la siri.

Unaambiwa mimea, mawe , mchanga, vitanda oxgen na kila kitu kinachoonekana na kisichoonekana huwa vinarekodi matukio ya wanadamu.

ASANTENI
 
Ohooo hukumu tenaaaa? Usharefusha usiku nakat kitanda chenyewe kinakungun inatakiwa nikifka nimechoka nazima mpk asubuh?
 
Kwa hiyo wanaokufa sasa hivi hawahukumiwi kumbe? Mbona wanapelekwa motoni wengine mbinguni?
Wanapewa adhabu kabla ya hukumu?

Story za kujifariji hizi
 
Kwa hiyo wanaokufa sasa hivi hawahukumiwi kumbe? Mbona wanapelekwa motoni wengine mbinguni?
Wanapewa adhabu kabla ya hukumu?
Wanaenda Mbinguni?

Mbna mimi huwa naona wanafukiwa aridhini..au ni mimi peked yangu huwa naona hivyo?
 
Hebu fikiria siku ambayo halaiki ya watu imekodoa macho kuangalia matendo yako yote yaliyo ya wazi na yale ya siri.

Hebu piga picha yule rafiki yako uliyemchukulia mke wake anakuona unazini na mke wake.

Hebu piga picha mzazi mwenzako anakuona vile unamtoa kafara mtoto wenu kisa utajirike.

Hebu piga picha tunakuona ukiwa unaroga majirani zako na wakati kanisani au msikitini hukosi.

Hebu piga picha tunaona ukiwapanga majambazi wakavamie kwa mjomba, binamu au baba yako.

Hebu piga picha wewe mchungaji au shehe unaonekana ukizini gesti na mhumini wako.

Hebu piga picha wewe unayetoa kafara raia wasio na hatia ili ushinde uchaguzi wa jimbo lako.

Hebu piga picha ulivyomuaga mmeo kuwa unaenda sokoni au kwa rafiki yako kumbe unaenda gheto la mchepuko wako.

Hebu piga picha siku hiyo kale katabia kako ka kudanganya wana JF. kanaonekana wazi.

Hebu piga picha siku ambayo yule Adam na Hawa uliyemsikia na kumsoma unamuona kwa macho.

Hebu piga picha pale unapogundua kwa mara ya kwanza watoto ulionao sio wako.

Hebu piga picha wafanya kazi wenzako kwa mara ya kwanza wanajua kua ulipata cheo chako baada ya kutanua mabaja.

Hebu piga picha siku ambayo kwa mara ya kwanza JF members tunajua jina lako halisi.

Mimi nimejaribu kupiga picha na kisimu changu sipati picha kamili.

Unaambiwa kila jambo unalolitenda litaletwa hadharani haijalishi la wazi au la siri.

Unaambiwa mimea, mawe , mchanga, vitanda oxgen na kila kitu kinachoonekana na kisichoonekana huwa vinarekodi matukio ya wanadamu.

ASANTENI
Hakuna siku ya mwisho, we kama huitumii dunia kisa eti utaingia sijui peponi unapoteza muda wako. Waliotuletea dini ndo wanaogoza kwa zambi za kuuana na kutuletea virusi vya magonjwa, ndo wanaoongoza kwa roho mbaya jiulize mbona hawafikirii hayo ya peponi/motoni?
 
Back
Top Bottom