Tanzania Foods and Drugs Administration(TFDA) ni shirika lililoundwa kisheria ili liweze kuwalinda wananchi dhidi ya madhara yanyoweza kuwapata kwa kutumia dawa na vyakula visivyo faa.Hata hivyo shirika hili linalo ongozwa na mama Ndomondo limeshindwa kazi hiyo kabisa.Si mchukii Mama Ndomondo lakini ninachotaka mimi ni ufanisi,ambao sioni kabisa katika shirika hili.
Katika tukio la hivi karibuni ambalo kwangu mimi ni kichekesho,mwananchi mmoja aligundua uwepo wa Metakelfin fake na aka-blow the whistle.Ninachojiuliza ni kwamba hivi TFDA imeachia wanachi ambao hata utaalam hawana, kazi ya ku-dentify madawa fake nchini?Na imekuaje TFDA iachie dawa hiyo ivuke mpaka wa Tanzania na hata kuuzwa kwenye maduka ya dawa.Hivi si kazi ya TFDA kuhakikisha kwamba dawa fake haziingizwi nchini mwetu kabisa?Katika uzembe huu,tunajua ni watanzania wangapi wameathirika kwa kunywa dawa hii,na ni wangapi wamekufa?Katika mazingira ya namna hii,inaonyesha wazi kwamba kuna dawa nyingi fake ziko kwenye shelves za maduka ya dawa,na watanzania maskini wengi wanaendelea kuathirika na kufa bila kuwa na chombo dhabiti cha kuwatetea!Hali hii ya kutisha itaachiwa iendelee hadi lini.
Tumeshawahi kupigia kelele uwepo wa dawa fake kujaa kwenye maduka yetu lakini hakuna mtu anayesikiliza.Sio siri tena kwamba ukifika dukani,kama unaumwa malaria unaulizwa dawa ipi inakutibu.Ni aibu sana.Hivi mwananchi wa kawaida, asiyekuwa hata na chembe ya ufahamu juu ya madawa katika hali hii ataishi vipi?Kila mtu anajua yaliyotokea baada ya kuondoa Chloroquine kama tiba ya Malaria, ni aibu tupu.Hivi tunaelekea wapi.Mara SP,mara Quinine,mara Aluu,tunatangatanga tu.Kwa kweli mazingira yaliyopo kwenye mfumo mzima wa madawa ni wa kifisadi na kitapeli.Mazingira ambayo wenye nguvu kifedha wameachwa wafanye wanalotaka,wachezee afya za walala hoi wafe kama panzi,huku wao wakiendekea kujitajirisha.Ni mchezo mchafu sana.
TFDA hasa ina kazi gani?Hapana, kwa kweli sioni.
Sasa kwa vile,TFDA imeamua tulinde afya zetu,basi ni vema wakapokea tips hizi ili wazifanyie kazi.
*Mwaka 2002 Deutch Welle waliongelea uwepo wa Cyproflaxin inayotengenezwa Ujerumani ambayo ni fake,na ambayo ni vigumu kuitofautisha na Cyproflaxin halisi,na ambayo inasambazwa duniani kote.
*Mwaka wa jana mimi binafsi nilifungua capsule ya Chloramphenicol na kugundua kwamba unga uliokuwepo haukuwa mchungu kabisa, jambo linalo ashiria kwamba unga ule haukuwa wa active ingridient halisi ya Chloramphenicol.
*Brands za Panadol zilizoko madukani sasa hivi nyingi zinamomonyoka kama bonge la udongo na ukiweka kwenye maji ndio kabisaaa, zinasambaratika mara moja, jambo linaloashiria kwamba si panadol halisi ila lipo tatizo!
*Kwa ujumla matatizo ya madawa ni makubwa,na kama TFDA haikufanya kazi yake inavyotakiwa,we are sitting on a time bomb.
Katika tukio la hivi karibuni ambalo kwangu mimi ni kichekesho,mwananchi mmoja aligundua uwepo wa Metakelfin fake na aka-blow the whistle.Ninachojiuliza ni kwamba hivi TFDA imeachia wanachi ambao hata utaalam hawana, kazi ya ku-dentify madawa fake nchini?Na imekuaje TFDA iachie dawa hiyo ivuke mpaka wa Tanzania na hata kuuzwa kwenye maduka ya dawa.Hivi si kazi ya TFDA kuhakikisha kwamba dawa fake haziingizwi nchini mwetu kabisa?Katika uzembe huu,tunajua ni watanzania wangapi wameathirika kwa kunywa dawa hii,na ni wangapi wamekufa?Katika mazingira ya namna hii,inaonyesha wazi kwamba kuna dawa nyingi fake ziko kwenye shelves za maduka ya dawa,na watanzania maskini wengi wanaendelea kuathirika na kufa bila kuwa na chombo dhabiti cha kuwatetea!Hali hii ya kutisha itaachiwa iendelee hadi lini.
Tumeshawahi kupigia kelele uwepo wa dawa fake kujaa kwenye maduka yetu lakini hakuna mtu anayesikiliza.Sio siri tena kwamba ukifika dukani,kama unaumwa malaria unaulizwa dawa ipi inakutibu.Ni aibu sana.Hivi mwananchi wa kawaida, asiyekuwa hata na chembe ya ufahamu juu ya madawa katika hali hii ataishi vipi?Kila mtu anajua yaliyotokea baada ya kuondoa Chloroquine kama tiba ya Malaria, ni aibu tupu.Hivi tunaelekea wapi.Mara SP,mara Quinine,mara Aluu,tunatangatanga tu.Kwa kweli mazingira yaliyopo kwenye mfumo mzima wa madawa ni wa kifisadi na kitapeli.Mazingira ambayo wenye nguvu kifedha wameachwa wafanye wanalotaka,wachezee afya za walala hoi wafe kama panzi,huku wao wakiendekea kujitajirisha.Ni mchezo mchafu sana.
TFDA hasa ina kazi gani?Hapana, kwa kweli sioni.
Sasa kwa vile,TFDA imeamua tulinde afya zetu,basi ni vema wakapokea tips hizi ili wazifanyie kazi.
*Mwaka 2002 Deutch Welle waliongelea uwepo wa Cyproflaxin inayotengenezwa Ujerumani ambayo ni fake,na ambayo ni vigumu kuitofautisha na Cyproflaxin halisi,na ambayo inasambazwa duniani kote.
*Mwaka wa jana mimi binafsi nilifungua capsule ya Chloramphenicol na kugundua kwamba unga uliokuwepo haukuwa mchungu kabisa, jambo linalo ashiria kwamba unga ule haukuwa wa active ingridient halisi ya Chloramphenicol.
*Brands za Panadol zilizoko madukani sasa hivi nyingi zinamomonyoka kama bonge la udongo na ukiweka kwenye maji ndio kabisaaa, zinasambaratika mara moja, jambo linaloashiria kwamba si panadol halisi ila lipo tatizo!
*Kwa ujumla matatizo ya madawa ni makubwa,na kama TFDA haikufanya kazi yake inavyotakiwa,we are sitting on a time bomb.