Sioni mantiki ya ziara ya Mh.Samwel Sitta

Sioni mantiki ya ziara ya Mh.Samwel Sitta

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Mh.Samwel John Sitta ni Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Kimamlaka ni kiranja wa Bunge hilo kuhakikisha kuwa Wajumbe wanajadili Rasimu na kuipitisha. Ni kuwaongoza Wajumbe kufikia lengo lao la kuipitisha Rasimu tayari kupigiwa kura na wananchi kuwa Katiba mpya.

Kikanuni na kimamlaka,Mh.Sitta hana nafasi ya kuingiza maoni au mapendekezo yake katika Rasimu iliyopo. Wajibu huo ni wa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba ambao watatenda kazi zao kulingana na Sheria na Kanuni zinazowaongoza ambazo Mh.Sitta anazisimamia.

Leo imeripotiwa kuwa Mh.Sitta amefanya ziara na kufanya mazungumzo ya faragha na Mwadhama Polycap Kardinali Pengo na Sheikh Issa Shaaban Bin Simba.Hawa ni viongozi wa juu wa kidini nchini kwa wakatoliki na waislamu. Nasema,sioni mantiki ya ziara hii.Nina sababu zangu.

Kwanza,kama ni kupokea maoni yao,iliyokuwa Tume ya Jaji Warioba ilikutana nao na kupata maoni yao.Na hakuna aliyebadilisha msimamo wake.Maoni yao yamo kwenye Rasimu iliyopo Bungeni. Kwahiyo,kuwatembelea tena hakuna mshiko.Pili,wao si viiongozi pekee wa kidini nchini.Kuwatembelea wao tu ni kuwatenga wengine na kuibua maneno yasiyo na maana.

Tatu, kuwatembelea viongozi hao na kufanya nao mazungumzo faraghani muda huu wa kujadili Rasimu,ni kuwachora kama wanaoweza kufuatwa,kushawishiwa na kutumiwa kupitisha ajenda mbalimbali za Mh.Sitta au yeyote awaye. Hakukuwa na haja ya ziara kama hii muda kama huu.

Naamini kuwa ziara hii,kama inahusiana na masuala ya Katiba mpya,haina mantiki na haikufaa kuwepo.
 
Mbona rahisi kaka, anatumia fursa vizuri. Ni hivi, Kwenda kuongea na watu kama hao ktk kipindi hiki ambapo yeye anagonga vichwa vya magazeti ni fursa ya yeye kujenga mahusiano mazuri na hao watu hao kuelekea magogoni. Mbona rahisi tu. Zaidi hapo, hakuna jambo la maana. Ili uende magogoni lazima ukae nao vizuri.
 
Mbona rahisi kaka, anatumia fursa vizuri. Ni hivi, Kwenda kuongea na watu kama hao ktk kipindi hiki ambapo yeye anagonga vichwa vya magazeti ni fursa ya yeye kujenga mahusiano mazuri na hao watu hao kuelekea magogoni. Mbona rahisi tu. Zaidi hapo, hakuna jambo la maana. Ili uende magogoni lazima ukae nao vizuri.

Yawezekana kaka
 
Nakubaliana na ukweli kwamba Ziara hii ni usanii usio na tija katika mchakato wa kupata katika mpya. Ziara hii ni ya kinafiki na imempata haswaa mnafiki kiongozi. Ni kama vile upele kupata mkunaji.
 
Hakuna kingine zaidi ya kutapatapa,wawakilishi wa viongozi wa dini amewaacha huko Dodoma anashinda nao mjengoni.bila shaka wanatoa updates za kinachoendelea kwa wanaowawakilisha.
Sitta kufunga safari tena kwenda kuwaona watu ambao tayari walishatoa maoni yao kwenye tume, kwa kisingizio eti chakuwapa briefings kwa yanayojiri mjengoni,naona ni ila za CCM kutaka msaada wa viongozi hao baada yakuona jahazi linazama hasa kuhusiana na muundo wa kuwa na serikali tatu.
Sasa tutashuhudia ila njama na kila aina ya uozo katka kutekeleza adhma yao yakulazimisha muundo wa serikali mbili,just imagine hata tovuti ya tume imefungwa kimizengwe,serikali ya wapi inayoendesha mambo kiuni namna hii.
 
Kwani kuwa m/kiti wa bunge la katiba unakuwa huruhusiwi kufanya mambo mengine ebu twambieni nyie hiyo ni kanuni ya ngapi maake hata kusali mtamzuia naamini mnatumika m----------- basi tafuteni vitu vya msingi ili muonekane hizo Pesa mlizolipwa mumezifanyia Kazi!!!
 
Jamani hivi Watanzania mmerogwa na nani? Hivi bado mna imani ya dhati kutoka mioyoni yenu kwamba huyo Sitta wenu ana tofauti na mi-CCM mingine?! Si ndiyo huyu Sitta aliyepindisha kanuni na kumfanya Kikwete kufungua bunge la katiba baada ya Judge Warioba kuwakilisha rasimu ya pili ya katiba? Si ni huyu huyu Sitta aliyeleta mapendekezo ya kubadilisha kanuni za Bunge la katiba hata kabla kanuni hizo hazijaanza kutumika?! Hivi kwanini Watanzania mnakuwa na akili kama za samaki? Mnasikitisha sana kama sio kuhurumiwa! INSANITY IS TO REPEAT THE SAME THING EXPECTING DIFFERENT RESULTS. If Tanzanians are still expecting something different from Sitta, then they are insane!
 
Asante Sita kwa kuthibitisha kuwa CCM inatambua Roman Catholic na Waislam wa BAKWATA pekee....wale waliokuja kulalamika Wapentekoste naanza kuona walikuwa na hoja ya msingi......
 
Hapa Sitta Mtamuonea tu bure

JK.jpg
 
Asante Sita kwa kuthibitisha kuwa CCM inatambua Roman Catholic na Waislam wa BAKWATA pekee....wale waliokuja kulalamika Wapentekoste naanza kuona walikuwa na hoja ya msingi......

Hapa kuna jambo hapa...............si bure
 
Back
Top Bottom