Siogei tena vile visabuni vya gesti

Siogei tena vile visabuni vya gesti

adden

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
7,033
Reaction score
15,699
Morning all,
Niende kwenye mada moja moja.
Juzi nilikuwa na miadi na shori flani tukutane gest mitaa ya kati.
Mi nilitangulia kufika pale nikimsubiri huku nikipata konyagi nachanganya na valuu.
Mwisho nilipowasiliana nae ilikuwa ndo anakaribia kufika.
Nikaamua kulipia room na kuzama humo nikimsubiri shori.
Ebwanaee manzi si akayeyusha na nishakula hasara ya chumba..
Nikaona isiwe shida acha hata nioge ili nirudishe hata ela za chenji ya gest.
Nikazama bafuni nikakuta kile kisabuni cheupe ebwana kwa hasira nilikiogea hadi kikaisha na nyetoo juu.
Nimemaliza mida ya saa 2 usiku huyo nikajimuvuzisha hom na hasira zangu..
yaani nimefika sijaingia hata ndani nikaulizwa "ENHEE ULIKUWA GEST GANI LEO??!!"
nikabaki nimetumbua macho nikawekwa kofi moja matata sana akili ikarudi nikamjibu nilikuwa kaoshi.
Yaani hadi nimeondoka hom ugomvi haujaisha.
Kinachoniuma nimezinguliwa na shori na hom nimeharibu yaani nipo sieleweki.
Kuanzia leo nakuwa naenda na sabuni yangu gesti
 
Nawewe ungempa kibao cha nguvu alafu una muuliza umejuaje harufu ya sabuni ya gest?

Lakini nadhani uitengeneze nafsi yako kwanza ili umuone mkeo ndie bora zaidi ya mtu mwingine.

Kutamani kupo mkuu lakini vita ambayo tumeumbiwa wanaume ni kuyadhibiti matamanio yetu,sio kwamba tujizuie tusitamani hapana.wanaume tunatamani sana tu.lakini ishu ni kuyazuia matamanio na uchafu kama wa kuzini n.k

Nakutakia maisha mema
 
Back
Top Bottom