MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,586
Eti ujumbe wa wanawake wenye kuiba waume za watu, Eti aache, eti kahangaika nae mwaka jana wooote huyo Bwana kama anakupenda kweli hajamwacha mkewe unadhani mwaka huu utafanikiwa? Eti wengine bado waenda roga ili waolewe wao, jamani ndumba za mwaka jana umezivaa kiunonimpaka zimeota kutu bado wavaa nyingine eh. Mie huyu Bi Hindu leo kanchekesha hadi nalia machozi. Na hapa katuasa sote wake kwa waume; mwanaume mwache mke wa mtu ulokuwa naye na mwanamke amwache mume wa mwenzie na mwenzie apumzike na kuifurahia ndoa yake ah.................... nimechoka mie. Ila nimejiuliza kwani wote wanaotembea na waume za watu lengo lao ni kupindua wenzao au ndo mambo ya kuutilize to hii MBA resource (Married But Available) ambayo siku hizi sio scarce tena?