RODRIGUEZ NORIEGA DUERTET
Member
- Mar 26, 2018
- 72
- 59
Habarini wana jamvi,
Kuna kitu sijaelewa kuhusu mifuko ya jamii na suala zima la kuunganisha mifuko ya jamii, kwa update nilizoona kuna mfumo uko indicated by picture ukionyesha SSRA(Regulatory Authority),ndo mfuko mama ukiwa na watoto wawili PSSF(Public Sector) na NSSF(Private Sector), PSSF na NSSF na wana watoto watatu kila mmoja ikiwa na maana PSSSF watoto wake ni PPF/LAPF/GEPF na NSSF watoto wake ni PPF/LAPF/GEPF.
Kuhusu mchanganu wa stucture yake haina shida sana, ila nimejaribu kuchimba sheria zipi zinaaply wakati mtu ukiwa unataka kupata mafao yako baada ya kuacha, kusimamishwa au kufukuzwa bado sijapata clear information ila nna case study mbili.
1.Dada yangu alikuwa anafanya kazi NMB alikuwa akitumia mfuko wa NSSF, baadae akaona maslahi ni madogo hivyo akaamua kuachana na kazi na kutafuta njia mpya ya kutafuta riziki yake,alifuatilia mafao yako NSSF akaambiwa mpaka afikishe umri wa miaka 55.Akaendelea kufuatilia maslahi yake kiasi cha kwenda kwa mkuu wa mkoa Mh. Makonda lakini at the end majibu yakawa ni yaleyale.
2.Rafiki yangu alikuwa akifanya kazi katika kampuni changa ya simu hapa Tanzania alikuwa LAPF, kutokana na msongo wa maisha na kutokuelewana na mabosi zake akaamua kubwaga manyanga lakini last month alifuatilia mafao yake kiasi cha Tsh. 5,000,000 na kufanikiwa kupata ela zake bila tatizo lolote.
Kwa kutumia hizo casy study hizo mbili nimeshindwa kuelewa je ile sheria ya kuchukua mafao ni mpaka miaka 55 imeshasainiwa na Mh. Rais wa wanyonge au bado? Pia napenda kujua kwanini treatment kwenye mifuko zinakuwa tofauti? Wengine kama NSSF/PSPF wanakwambia mpaka ufikishe miaka 55, wengine wanatoa?
Kwa ambaye anafahamu ili suala kiundani naomba ufafanuzi ili niweze kujua au mwenye document zinazoonyesha sheria na taratibu za kuchukua mafao za sasa naomba atume hapa japo nipate uhakika kuhusu ili suala.
MWISHO.
Hivi Watanzania tumelogwa na nani? Wabunge wetu ni wasomi kweli au zuga? Unapomwambia mtu kuchukua mafao yake ni mpaka akifikishe miaka 55, je sisi tuliofanya kazi mwaka mmoja na mikataba yetu kukatishwa na kwenye mifuko yetu ya jamii tuna 1.5 milioni, Je milion 1.5 ya mwaka wa 2018 itakuwa na uwiano gani na 1.5 ya mwaka 2045 wakati nitapofikisha umri wa miaka 55.
Mpaka mwaka 2045 milioni 1.5 itakuwa ni ela ya kuendea sokoni kutafuta vitu vya kupika au kuendea kunywa bia mbili na kongoro, kwanini wasinipe wakati ambao inaweza kununua Bodaboda au kufungua genge la nyanya na vitunguu.
Akili zetu huwa tunaziweka wapi wakati tunatunga sheria za nchi hii
Kuna kitu sijaelewa kuhusu mifuko ya jamii na suala zima la kuunganisha mifuko ya jamii, kwa update nilizoona kuna mfumo uko indicated by picture ukionyesha SSRA(Regulatory Authority),ndo mfuko mama ukiwa na watoto wawili PSSF(Public Sector) na NSSF(Private Sector), PSSF na NSSF na wana watoto watatu kila mmoja ikiwa na maana PSSSF watoto wake ni PPF/LAPF/GEPF na NSSF watoto wake ni PPF/LAPF/GEPF.
Kuhusu mchanganu wa stucture yake haina shida sana, ila nimejaribu kuchimba sheria zipi zinaaply wakati mtu ukiwa unataka kupata mafao yako baada ya kuacha, kusimamishwa au kufukuzwa bado sijapata clear information ila nna case study mbili.
1.Dada yangu alikuwa anafanya kazi NMB alikuwa akitumia mfuko wa NSSF, baadae akaona maslahi ni madogo hivyo akaamua kuachana na kazi na kutafuta njia mpya ya kutafuta riziki yake,alifuatilia mafao yako NSSF akaambiwa mpaka afikishe umri wa miaka 55.Akaendelea kufuatilia maslahi yake kiasi cha kwenda kwa mkuu wa mkoa Mh. Makonda lakini at the end majibu yakawa ni yaleyale.
2.Rafiki yangu alikuwa akifanya kazi katika kampuni changa ya simu hapa Tanzania alikuwa LAPF, kutokana na msongo wa maisha na kutokuelewana na mabosi zake akaamua kubwaga manyanga lakini last month alifuatilia mafao yake kiasi cha Tsh. 5,000,000 na kufanikiwa kupata ela zake bila tatizo lolote.
Kwa kutumia hizo casy study hizo mbili nimeshindwa kuelewa je ile sheria ya kuchukua mafao ni mpaka miaka 55 imeshasainiwa na Mh. Rais wa wanyonge au bado? Pia napenda kujua kwanini treatment kwenye mifuko zinakuwa tofauti? Wengine kama NSSF/PSPF wanakwambia mpaka ufikishe miaka 55, wengine wanatoa?
Kwa ambaye anafahamu ili suala kiundani naomba ufafanuzi ili niweze kujua au mwenye document zinazoonyesha sheria na taratibu za kuchukua mafao za sasa naomba atume hapa japo nipate uhakika kuhusu ili suala.
MWISHO.
Hivi Watanzania tumelogwa na nani? Wabunge wetu ni wasomi kweli au zuga? Unapomwambia mtu kuchukua mafao yake ni mpaka akifikishe miaka 55, je sisi tuliofanya kazi mwaka mmoja na mikataba yetu kukatishwa na kwenye mifuko yetu ya jamii tuna 1.5 milioni, Je milion 1.5 ya mwaka wa 2018 itakuwa na uwiano gani na 1.5 ya mwaka 2045 wakati nitapofikisha umri wa miaka 55.
Mpaka mwaka 2045 milioni 1.5 itakuwa ni ela ya kuendea sokoni kutafuta vitu vya kupika au kuendea kunywa bia mbili na kongoro, kwanini wasinipe wakati ambao inaweza kununua Bodaboda au kufungua genge la nyanya na vitunguu.
Akili zetu huwa tunaziweka wapi wakati tunatunga sheria za nchi hii