Single Mother: Usimruhusu aliyekuharibia future yako kuja kukuvunjia ndoa yako mpya

Makau Js

Member
May 25, 2017
93
233
SingleMother-Usimruhusu mwanaume aliyekuharibia future yako kwa kukupa uja uzito na kukukimbia na kumruhusu kuja kukuvunjia ndoa yako mpya, kuwa makini na mwenye nidhamu pamoja na heshima na adabu.

Baadhi ya wanaume hutamani wanawake wenye watoto kwa tamaa za kimwili na sio kwa dhamira ya kutengeneza ndoa ,inatakiwa uwe na chujio la kupima maneno ya wanaume walaghai na dhamira zao .

Hakikisha unaitawala smart phone na usiruhusu smart phone ikutawale ,jifunze kupevuka kiakili kwa kuacha kuwasiliana ovyo na wanaume wengine ambao hawana tija katika maisha yako.

Ukutanapo na baba watoto wako futa dhana/hisia ya mapenzi na tengeneza dhamira na fikra kwa mchumba wako mpya au mume wako wa ndoa ambaye si baba wa mtoto wako ya kuwa ,unayekutana nae/wasiliana naye ni baba watoto wako na mzazi mwenzio na sio mpenzi wako hata kama umezaa nae ili kujenga daraja la uaminifu kwake .

Kizazi chetu cha sasa ni kizazi kibovu ambacho kinahitaji mtoto kulelewa na wazazi wote wawili .Mtegemee Mwenyezi-Mungu kwa kila jambo naye atakupigania katika kila jambo kama alivyosema Katika kitabu cha Isaya [54:4-6 ]Usiogope maana hutaaibishwa tena usifadhaike maana hutadharauliwa tena.Utaisahau aibu ya ujana wako,wala hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.Muumba wako atakuwa mume wako.

Darasa:Usimtegemee mwanadamu kwa lolote lile bali ,mtumaini Mwenyezi-Mungu akupe mume mwema,na fanya toba kwa kukubali kosa la kwanza, kisha Mwenyezi Mungu atafuta kosa lako ka kukupa hitaji la moyo wako.

Tambua kuna benki na hazina ya wanaume bora, wanaosali na kumuomba Mwenyezi -Mungu awapatie wake bora wenye hekima na busara ,jifunze kusali na kuomba ili sala za mke mwema zikutane na sala za mume mwema katika anga na mbingu na Agano takatifu litimie la ndoa bora.

Hauwezi kuwa mke mbaya harafu Mwenyezi Mungu akupe mume mwema ,ukiwa mwanamke mbaya utapata mwanaume aina yako ukiwa bora Mwenyezi Mungu atakupa mume bora.Tumia akili yako kufuata mafundisho;tumia masikio yako kusikiliza maarifa [HASHTAG]#SingleMother[/HASHTAG].

41504e14d7dd702cce59d8abd7994f9a.jpg
 
SingleMother-Usimruhusu mwanaume aliyekuharibia future yako kwa kukupa uja uzito na kukukimbia na kumruhusu kuja kukuvunjia ndoa yako mpya, kuwa makini na mwenye nidhamu pamoja na heshima na adabu.

Baadhi ya wanaume hutamani wanawake wenye watoto kwa tamaa za kimwili na sio kwa dhamira ya kutengeneza ndoa ,inatakiwa uwe na chujio la kupima maneno ya wanaume walaghai na dhamira zao .

Hakikisha unaitawala smart phone na usiruhusu smart phone ikutawale ,jifunze kupevuka kiakili kwa kuacha kuwasiliana ovyo na wanaume wengine ambao hawana tija katika maisha yako.

Ukutanapo na baba watoto wako futa dhana/hisia ya mapenzi na tengeneza dhamira na fikra kwa mchumba wako mpya au mume wako wa ndoa ambaye si baba wa mtoto wako ya kuwa ,unayekutana nae/wasiliana naye ni baba watoto wako na mzazi mwenzio na sio mpenzi wako hata kama umezaa nae ili kujenga daraja la uaminifu kwake .

Kizazi chetu cha sasa ni kizazi kibovu ambacho kinahitaji mtoto kulelewa na wazazi wote wawili .Mtegemee Mwenyezi-Mungu kwa kila jambo naye atakupigania katika kila jambo kama alivyosema Katika kitabu cha Isaya [54:4-6 ]Usiogope maana hutaaibishwa tena usifadhaike maana hutadharauliwa tena.Utaisahau aibu ya ujana wako,wala hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.Muumba wako atakuwa mume wako.

Darasa:Usimtegemee mwanadamu kwa lolote lile bali ,mtumaini Mwenyezi-Mungu akupe mume mwema,na fanya toba kwa kukubali kosa la kwanza, kisha Mwenyezi Mungu atafuta kosa lako ka kukupa hitaji la moyo wako.

Tambua kuna benki na hazina ya wanaume bora, wanaosali na kumuomba Mwenyezi -Mungu awapatie wake bora wenye hekima na busara ,jifunze kusali na kuomba ili sala za mke mwema zikutane na sala za mume mwema katika anga na mbingu na Agano takatifu litimie la ndoa bora.

Hauwezi kuwa mke mbaya harafu Mwenyezi Mungu akupe mume mwema ,ukiwa mwanamke mbaya utapata mwanaume aina yako ukiwa bora Mwenyezi Mungu atakupa mume bora.Tumia akili yako kufuata mafundisho;tumia masikio yako kusikiliza maarifa [HASHTAG]#SingleMother[/HASHTAG].

41504e14d7dd702cce59d8abd7994f9a.jpg
kuna mahali unawatia moyo na kuna mahala unawalaumu sasa umeshawachanganya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom