Singita Hotel-most expensive

Singita Hotel-most expensive

Amavubi it seems ulipata taarifa nyingi zaidi ya harakati zilizokupeleka...hahahahaaa

Watz wanapigana majungu pale balaa,,,kama alivyosema Ngongo labour turnover iko juu sana
yaaah na taarifa nyingine ni kwamba kutokana na umbali ngono imekithiri sana miongoni mwa wafanyakazi na wengine hujilengesha (sikujipatiamo)kwa wageni, besides wabongo wanalazimihsa TIP sana mahotelini
 
Nilimaanisha Mkuu wa KAYA huwa anakwenda Lodge kukutana na Jones....Madhara yake ni kwamba waendeshaji (South Africans) hutumia hizo visits kama fimbo ya kuwakandamiza zaidi wazawa.
watakua wanatahmini faida na mgawo
 
Amavubi hebu tuambie tume huru ndio ipi? kwanini Mwakiembe alisema wafanyakazi wa wizara yake wapande ndege daraja la kawaida, nchi hiii inaliwa na wenye meno na inajengwa na wenye moyo ambao hata kwa mkono unaeza wahesabu
mkuu kuna vyeo vingine inabidi ujipe hakuna atakayekupa, mimi nasikiaga tu Tume huru hapa nikajipachika kwamba nilijituma mwenyewe nikiwa HURU bila TORs ili niweze kufungua yaliyofungwa
 
Hapo kwenye red upo sawa kiongozi.

Kwa upande mmoja hii lodge imepunguza umaskini kwa mwana familia wetu mmoja, maana mwisho wa mwezi si haba. Ila post zote nyeti wamewekwa wageni....masilahi ya taifa walakini mtupu.

Mara nyingi Jones akiwepo wanakutana na best yake pal
e....nani asiyependa kuwa best friend wa Mkuu wa KAYA??

Hapo kwenye red nipo sawa mkuu, kama umewahi fika maeneo hayo, ukiwa unatokea Mugumu unakaribia Nata majengo ya hotel unayaona kwa mbali mkono wa kushoto au kama unatokea Nata kwenda Fort Ikoma kama kilometre 2 hivi kutoka Nata kuna camp za staffs na ofisi zao kutoka pale ukienda mbele kidogo mkono wa kushoto kuna njia inakwenda kule hotelini. Maeneo haya mpaka unafika Fort Ikoma unaendelea mpaka Lubanda yana wana wanyama karibu wote wanaokula Nyasi sina uhakika na chui na simba maana wengi wanapatikana ukikaribia Seronera ila bado huku unakuwa hujaianza kabisa mbuga ya serengeti kwa undani kwa kuwa geti la kuingilia Serengeti ambako ndio unalipa sasa kuingia lipo mbali kabisa na hii hotel na kote huku unapopita kama Fort Ikoma na Lubanda kuna makazi ya watu wanaishi though kuna wanyama. Alichofanya yeye ni kila mwaka anatoa kama 2 million kila kata ili wasishiriki katika uwindaji wanyama (lengo hapo utaona kama kulinda hifadhi lakini ukiangalia kwa undani wanyama wasiwe disturbed mwisho wa siku anaendelea kupiga biashara na ukikutwa unawinda maeneo hayo ni issue)

Hapo bolded kweli mkuu nadhani ndio alichukua idea na yeye akaji-engage kwenye Bilila Kempisky ambayo yenyewe sasa ndio ipo kabisa ndani ya mbuga kabisa ambayo inasemekana mkulu ana hisa

Ni kweli pia faida anayo make ni kubwa kuliko hata hiyo anayolipa kwenye hizo kata maana wao halmashauri nasikia walitaja 2 million kila kata walitegemea jamaa atakataa lakini mwisho wa siku jamaa likakubali. Jamaa amecheza na saikolojia ya watz maana ukimkamata mmoja basi atakupa mbinu za kuwalipa watz mishahara. All in all watz wanaoishi jirani na maeneo hayo waliofanikiwa kupata ajira hapo wengi wameridhika na wapo happy hata kama wanalipwa kidogo na wengine wanaendekeza majungu kwa wenzao

Maslai ya taifa kweli kuna walakini maana hapo booking directly from USA hatuendi kama tunavyoingia hotel zetu zingine hizi tunazoita nyota ngapi sijui, kwenye mapato hapo inakuwa ni issue akipenda lakini ni za kawaida, Manufaa hapo ni kuitangaza serengeti national park tu mie ndio naona tulichonufaika
 
View attachment 73956
hAPA NI KWA rOOM; Kioo kimoja unasimamisha nyumba, ni vigumu sana ili wanyama wasivunje, IMAGINE!!!

Kwa mmatumbi mimi sintoweza kusinzia! WEWE SEMA KIOO KIGUMU.....nikiona ngiri kwenye kioo lazima nidumbukie chini ya kitanda!!!!

Good and lovely hotel; japo sio kwa sisi (kulingana na gharama zake)...Kwa wenye uwezo ni value for money kwa kweli
 
it looks very nice from far but NOT from the analytical point of view
Hapo kwenye red nipo sawa mkuu, kama umewahi fika maeneo hayo, ukiwa unatokea Mugumu unakaribia Nata majengo ya hotel unayaona kwa mbali mkono wa kushoto au kama unatokea Nata kwenda Fort Ikoma kama kilometre 2 hivi kutoka Nata kuna camp za staffs na ofisi zao kutoka pale ukienda mbele kidogo mkono wa kushoto kuna njia inakwenda kule hotelini. Maeneo haya mpaka unafika Fort Ikoma unaendelea mpaka Lubanda yana wana wanyama karibu wote wanaokula Nyasi sina uhakika na chui na simba maana wengi wanapatikana ukikaribia Seronera ila bado huku unakuwa hujaianza kabisa mbuga ya serengeti kwa undani kwa kuwa geti la kuingilia Serengeti ambako ndio unalipa sasa kuingia lipo mbali kabisa na hii hotel na kote huku unapopita kama Fort Ikoma na Lubanda kuna makazi ya watu wanaishi though kuna wanyama. Alichofanya yeye ni kila mwaka anatoa kama 2 million kila kata ili wasishiriki katika uwindaji wanyama (lengo hapo utaona kama kulinda hifadhi lakini ukiangalia kwa undani wanyama wasiwe disturbed mwisho wa siku anaendelea kupiga biashara na ukikutwa unawinda maeneo hayo ni issue)

Hapo bolded kweli mkuu nadhani ndio alichukua idea na yeye akaji-engage kwenye Bilila Kempisky ambayo yenyewe sasa ndio ipo kabisa ndani ya mbuga kabisa ambayo inasemekana mkulu ana hisa
 
Nimeipenda Hotel kusema kweli
Kwa hiyo nidundulize shilingi ngapi ile niweze kukaa hata siku mbili?:sleepy:
shosti hapo bila m 5 usinyanyue kwato zako kwa hizo siku mbili, naamanisha m1 ya usafiri na m4 za malazi, manywaji makulaji na tour
 
Kwa mmatumbi mimi sintoweza kusinzia! WEWE SEMA KIOO KIGUMU.....nikiona ngiri kwenye kioo lazima nidumbukie chini ya kitanda!!!!

Good and lovely hotel; japo sio kwa sisi (kulingana na gharama zake)...Kwa wenye uwezo ni value for money kwa kweli
haikujengewa wanayama hiyo, JIPE MOYO MTU WA MUNGU, Dont allow yoursel to be weak unless the weakness is against you..............penye nia pana njia, kama mimi nilifika sembuse wewe great thinker?
 
images.jpg
waziri ndani ya Singita, huyu ndiye Jones?
 
images (1).jpg
madege hayo unatua mojakwa moja, yanaondoka na wanyama, angalieni tovuti yao msije sema photoshop
 
Mkuu Amavubi ni kweli ngono miongoni mwa wafanyakazi wote bila kujali wazawa na wageni iko juu sana,uwiyano kati ya wafanyakazi wa kiume na wanawake ni sababu tosha pia vyakula vya wafanyakazi na umbali ni factors zinazochangia zoezi la ngono kwenda juu ya viwango vilivyokubaliwa na shirika la afya dunia [WHO].

yaaah na taarifa nyingine ni kwamba kutokana na umbali ngono imekithiri sana miongoni mwa wafanyakazi na wengine hujilengesha (sikujipatiamo)kwa wageni, besides wabongo wanalazimihsa TIP sana mahotelini
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Amavubi ni kweli ngono miongoni mwa wafanyakazi wote bila kujali wazawa na wageni iko juu sana,uwiyano kati ya wafanyakazi wa kiume na wanawake ni sababu tosha pia vyakula vya wafanyakazi na umbali ni factors zinazochangia zoezi la ngono kwenda juu ya viwango vilivyokubaliwa na shirika la afya dunia [WHO].
idadavuzi wa kina huu, nipe hivyo viwango mkuu vya WHO
 
Duh Amavubi ni kweli uvivu na udokozi umechangia kuwaangusha sana wazawa lakini si wote sifa za udokozi zipo hata kwa wafanyakazi wageni.Tofauti ya mishahara baina ya wafanyakazi wa kigeni na wazawa inachangia kiasi fulani wafanyakazi wazawa kuwa wadokozi.Ajira kwa wageni haizingatii utaalamu na uzoefu wa kazi utashangaa anaajriwa mgeni asiyekuwa na ujuzi wowote zaidi ya lugha na analipwa mshahara mkubwa mara 20 kuliko mzawa.

inasemekana wazawa wana changamoto nyingi ikiwemo uvivu wa kupindukia na majungu
 
Last edited by a moderator:
hii imetamalaki maeneo mengi sana hapa nchini.................na wote tnasihia kwenye viganja (zamani kwenye kalamu) tu, sijui nani atamfunga paka kengele
Duh Amavubi ni kweli uvivu na udokozi umechangia kuwaangusha sana wazawa lakini si wote sifa za udokozi zipo hata kwa wafanyakazi wageni.Tofauti ya mishahara baina ya wafanyakazi wa kigeni na wazawa inachangia kiasi fulani wafanyakazi wazawa kuwa wadokozi.Ajira kwa wageni haizingatii utaalamu na uzoefu wa kazi utashangaa anaajriwa mgeni asiyekuwa na ujuzi wowote zaidi ya lugha na analipwa mshahara mkubwa mara 20 kuliko mzawa.
 
starehe garama...natamani next time nijilipue niende hapo jamani...ila dah.
 
Back
Top Bottom