Singida: Nilitegemea kuona Viwanda vya Ufugaji kuku

Jitihida ni hii hapa. Nimeweka juhudi hapa jukwaani.
Kwa sababu gani umeshangaa Singida kutokuwa supplier wa kuku?

Siijui Singida vizuri lakini ukiongelea ufugaji wa mifugo kama ng'ombe,mbuzi na kuku hasa ufugaji wa kisasa lazima hali ya hewa ya eneo itahusika, jamii pia inayozunguka kama soko.

Singida,Dodoma ni pakavu sana,sjui ubora wa maji yao ukoje[hasa kwa upande wa kuku],trend ya joto pia yaweza kuwa ni sababu ambazo hazivutii sana uwekezaji mkubwa.

Mashamba ya mifugo utayakuta huku kusini na kaskazini kule sababu hali ya hewa inaruhusu.

Note: Watu wa Dar wanafuga sababu soko ni kubwa huko japo wanapambana na hali ya hewa.

Karibu Green City,Mbeya uje ufuge😎
 
Rejea Historia ya nchi Tanzania. Ndio ujiulize Singida na uzalishaji wa Kuku wapi na wapi?

Kwa msaada: Singida ndio Mkoa pekee ulio na neema ya Ufugaji Kuku wazuri, watamu na wenye ubora wa hali ya juu tangu enzi na enzi. Tumeitupa mbali kimawazo na kimaendeleo hasa Uwekezaji wa Viwanda vya Kuku (Tuenzi huu utamaduni biashara kama vile Dodoma wanavyoenzi Zabibu).

Asante.
 
Habari Tanzania !

Jamani imekuwaje leo hii Singida wanashindwa kuwa suppliers wa Kuku wa Kienyeji na Kisasa nchi nzima?

Hivi nyie mnaotokea Singida mnajisikiaje yaani ?

Karibuni
Kwa sababu gani?
 
Habari Tanzania !

Jamani imekuwaje leo hii Singida wanashindwa kuwa suppliers wa Kuku wa Kienyeji na Kisasa nchi nzima?

Hivi nyie mnaotokea Singida mnajisikiaje yaani ?

Karibuni
Mkuu nchi inapitia magumu utekaji na mauaji wewe unabakia tu kuwaza msos nyama ya kuku. Siyo poa asee.
 
Njoo wewe ufungue tajiri, supply ni ya kutosha ushindwe wewe tu.

Sio lazima uwe mkazi wa singida ili kufungua kiwanda singida
 
Njoo wewe ufungue tajiri, supply ni ya kutosha ushindwe wewe tu.

Sio lazima uwe mkazi wa singida ili kufungua kiwanda singida
Mie yangu ni mawazo na hoja chokozi mpendwa.

Lengo langu ni kutoa mwanga wa viongozi kuwaza nje ya box hasa kwa mikoa yenye faida kwa Taifa.
 
Mkuu acha kuwaza kulakula tu mikuku. Kuna mambo mengi tu ya maana kujadili kuliko nyama ya kuku. Tendea haki jukwaa hili.

Sau'waah?
Chakula, Vinywaji na Mavazi havipitwi na muda. Nyie si mnaangaika na mambo ya kupita, ila nilivyovitaja hata ipite miaka mingapi jibu hitaji lake liko palepale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…