Kwa sababu gani umeshangaa Singida kutokuwa supplier wa kuku?
Siijui Singida vizuri lakini ukiongelea ufugaji wa mifugo kama ng'ombe,mbuzi na kuku hasa ufugaji wa kisasa lazima hali ya hewa ya eneo itahusika, jamii pia inayozunguka kama soko.
Singida,Dodoma ni pakavu sana,sjui ubora wa maji yao ukoje[hasa kwa upande wa kuku],trend ya joto pia yaweza kuwa ni sababu ambazo hazivutii sana uwekezaji mkubwa.
Mashamba ya mifugo utayakuta huku kusini na kaskazini kule sababu hali ya hewa inaruhusu.
Note: Watu wa Dar wanafuga sababu soko ni kubwa huko japo wanapambana na hali ya hewa.
Karibu Green City,Mbeya uje ufuge😎