Sina hamu ya kuwa na mpenzi kabisa

Sina hamu ya kuwa na mpenzi kabisa

Robbykan

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2015
Posts
509
Reaction score
470
Wakuu habarini za mida hii,

Poleni kwa majukumu ya kila siku ya kukabiliana na changamoto za maisha. Nina hoja nataka mnipe ushauri ndugu zangu.

Nimejikuta nakosa hamu kabisa ya kuwa na msichana. Hii hali imenitokea karibia mwezi unaisha. Ninaye mpenzi ila saivi namchukia sana na nataka niachane naye. Yaani nimetokea kumchukia sana sijui kwanini hadi najishangaa mwenyewe sina msichana mwingine pembeni ila nimejikuta tuu na hii hali.

Yaani akili yangu inanituma niishi peke yangu bila mwanamke. Nimekuwa navumilia tuu kujikaza ili huyu mpenzi wangu asijue lolote ila kiukweli sina hamu kabisa na mahusiano na mwanamke. Ifahamike kuwa sina tatizo na wanawake ila hii hali imenitawala kwenye ubongo wangu yaani hadi sijielewi.

Naombeni ushauri wenu hasa wataalam wa saikolojia kwanini nakuwa hivi.
 
angalia kuna jini mahaba kakuingia ndiyo maana unamchukia mpenzi wako, nenda kanisani kaombewe litoke hilo jini mahaba
Nitajuaje kama kuna jini mahaba limeniingia?
 
Utakuwa na stress,ndo maana unakuwa hivyo.
Daaaaah Mbona nipo kawaida tuu.. Cyo tofaut na kipindi cha nyuma.. Yaani Sina mawazo kiivo Sana yaani ni Hali tuu imezuka ghafla
 
Kushuhudia kuwaona wapenzi wanasalitiana, wanagombana na kila thread unayoisoma ya wanandoa na wapenzi wamegombana na kuibiwa mke wa mtu na stori za michepuko inatosha kabisa kuwachukia wanawake. Umeingia uwoga tu na hofu ya kuwahukumu wanawake wote sio wakuwaamini.
 
Wakuu habarini za mida hii,

Poleni kwa majukumu ya kila siku ya kukabiliana na changamoto za maisha. Nina hoja nataka mnipe ushauri ndugu zangu.

Nimejikuta nakosa hamu kabisa ya kuwa na msichana. Hii hali imenitokea karibia mwezi unaisha. Ninaye mpenzi ila saivi namchukia sana na nataka niachane naye. Yaani nimetokea kumchukia sana sijui kwanini hadi najishangaa mwenyewe sina msichana mwingine pembeni ila nimejikuta tuu na hii hali.

Yaani akili yangu inanituma niishi peke yangu bila mwanamke. Nimekuwa navumilia tuu kujikaza ili huyu mpenzi wangu asijue lolote ila kiukweli sina hamu kabisa na mahusiano na mwanamke. Ifahamike kuwa sina tatizo na wanawake ila hii hali imenitawala kwenye ubongo wangu yaani hadi sijielewi.

Naombeni ushauri wenu hasa wataalam wa saikolojia kwanini nakuwa hivi.
Umemchukia tangu lini kama ni baada ya jpm kuzuia wizi basi ujue ulikuwa na mapenzi ya hela,maana sasa helaa imeadimika huwez kumtoa out mpenzio unasingizia kumchukia,jishughulishe ktk haki mambo yataenda
 
Kutokuwa na mpenzi kabisa sio jambo zuri maana huwezi zuia hizi hisia. Bora uchague usijechaguliwa.
 
Acha strees mkuu jiamini usikae mwenyewe home jichanganye na.marafik wema.. usiwe bze sana na kazi pata muda WA kula bata kdogo.. kula chakula ushibe na kunywa maji ya ktosha.. usichelewe kulala usiku.. simpo sana utakuwa vzur kama umezaliwa jana...
 
Wakuu habarini za mida hii,

Poleni kwa majukumu ya kila siku ya kukabiliana na changamoto za maisha. Nina hoja nataka mnipe ushauri ndugu zangu.

Nimejikuta nakosa hamu kabisa ya kuwa na msichana. Hii hali imenitokea karibia mwezi unaisha. Ninaye mpenzi ila saivi namchukia sana na nataka niachane naye. Yaani nimetokea kumchukia sana sijui kwanini hadi najishangaa mwenyewe sina msichana mwingine pembeni ila nimejikuta tuu na hii hali.

Yaani akili yangu inanituma niishi peke yangu bila mwanamke. Nimekuwa navumilia tuu kujikaza ili huyu mpenzi wangu asijue lolote ila kiukweli sina hamu kabisa na mahusiano na mwanamke. Ifahamike kuwa sina tatizo na wanawake ila hii hali imenitawala kwenye ubongo wangu yaani hadi sijielewi.

Naombeni ushauri wenu hasa wataalam wa saikolojia kwanini nakuwa hivi.
pole, huwa inatokea, usijali, muda huponya magonjwa yote
 
Back
Top Bottom