Nilikupenda sana Emmanuel lakini katu hukuthamini penzi langu,ulipoumwa nilikubembeleza kwa maneno matamu uone jinsi gani nakujali na kukutakia uzima,ulipokasirishwa kazini bado nlikutia moyo,maumivu yako pia niliyabeba ili kukupnguzia uzito lakini wewe hukuthamini penzi langu katu..mapenzi yako kwangu yalishuka kila siku hupigi simu hadi nipige,tunaishi Dsm hii wote lakini inapita hata miezi 3-4 hatuonani hadi nibembeleze sana,kila nilichokuomba ulidai huna ilihali ulkuwa navyo.
Miaka yako 32 ilinifanya mwanzoni nkuone nmepata kuwa utawaza familia kumbe umri so tabia...machozi yangu hukuyajali wala kunithamini,nilikupenda sana emmanuel mwezi uliopita nilikutamkia tuachane nikajua ni gia ya kukubadilisha ndo kwanza ukasema nenda ili uendelee na wanawake wengine..(wanaume wapendeni wanawake wanaoonyesha kuwapenda kwa moyo kwani mtakuja kujuta baadaye)hyu niliyempenda hakunithamini ipo siku atanikumbuka..
Pole sana lkn kwa upande mwingne mshukuru MUNGU angekuoa afu ikawa ivo ungeumia zaid move on sis utapata atakae kupenda kwa dhati,pliz usivunjwe moyo na wasiojua kupendwa...