Sina hamu na NMB Benki na makato yao

Sina hamu na NMB Benki na makato yao

nusuhela

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2014
Posts
6,274
Reaction score
7,774
Baada ya kurudi Mbeya nyumbani, kuna mradi wa familia niliuona kuwa potential hasa kwa mazingira ya vijijini. Mradi huu unaingiza faida ya sh 10000 kwa siku. Ni mradi ambao hakika ukisimamiwa vizuri, unaweza leta mabadiliko.

Nikapiga mahesabu ya tangu kuwa na huu mradi familia ina akiba ya sh ngapi? Nikakuta ni zero. Yaani wanautumia huu mradi kama sehemu ya kutatulia shida zao huku mradi huu ukiwa hauna back up.

Hakika iliniuma nilipoona zaidi ya miaka 5 ya mradi huu bado fimilia haina hata balance.
Nikaamua niweke mikakati ya kuweka akiba kwaajili ya back up ili hata mashine zikisumbua, tusianze kuhangaika. Basi bwana kuna ka account kangu ka nmb nilikua nako na kapo active, nikaona sio mbaya nikiwa naweka huko hela wakati nafanya mpango wa kufungua account maalum kwaajili ya huu mradi. Nikaweka kama sh 80,000 hivi. Kwakua nina NMB MKONONI app, nikataka kuangalia salio. Eeeebwana eehh!! Nilichokikuta huko nilipagawa. Badala ya sh kukuta 80,000, nikakuta kuna 70,880. Ikabidi nichoke. Nikaona acha niombe statement ili nijiridhishe. Kunitumia statement kwenye email yangu wakakata sh 1,000 ikabaki sh 69,880. Nikasema hapa usinitanie, kesho lazima nikatoe balance hii. Basi leo ilipofika asubuhi na mapema nikaenda ATM ya pale Mbalizi tawi la NMB USONGWE. Kila nikijaribu kutoa sh 60,00, naambiwa huduma haijakamilika. Ikabidi niingie ndani ili nitolee dirishani. Kilichonikuta ndicho kilichofanya niandike hapa. Nikachukua fomu ya kutolea ha na nikaijaza vizuri ili niweze kutoa japo sh 68,000. Kwenda dirishani nikaambiwa siwezi kutoa kiwango hicho kwakua salio halitoshi. Nikashtuka. Nikamwambia teller kuwa mbona acc yangu ina sh 69,880? Akanijibu kwa ukali kuwa "bro kutoa hapa ni sh 6,500 kwahiyo inatakiwa utoa sh 60,000" nikahamaki huku nikijisonya kwanini nilidumbukiza hela bank.

Nikiwa na uchungu wa hela yote ninayoipa NMB pasipo wao kutoa jasho, nikajaza fomu ya kutoa sh 60,000

Hakika ni bora kuchimbia hela chini kuliko kuweka hela NMB
 
Mbona umelia lia saana halafu sijaona point yako mkuu,kwani hujui kuwa kutoa pesa dirishani panakuwa na makato makubwa??
 
Kuna haja ya kurudi kwenye vibubu tu maana haya mabenki jumlisha na tozo za chifu Hangaya tunawafanyia wao tu.
 
Zipp benki zina makato nafuu kiasi kwamba hata huwezi hisi maumivu ya makato.
 
ungeweka crdb ungelia kabisa ha ha ha ha kule wangekukwangua kabisa nazani wameweka makato tuchangie ujenzi wa makao yao makuu ya pale upanga
 
Baada ya kurudi Mbeya nyumbani, kuna mradi wa familia niliuona kuwa potential hasa kwa mazingira ya vijijini. Mradi huu unaingiza faida ya sh 10000 kwa siku. Ni mradi ambao hakika ukisimamiwa vizuri, unaweza leta mabadiliko.

Nikapiga mahesabu ya tangu kuwa na huu mradi familia ina akiba ya sh ngapi? Nikakuta ni zero. Yaani wanautumia huu mradi kama sehemu ya kutatulia shida zao huku mradi huu ukiwa hauna back up.

Hakika iliniuma nilipoona zaidi ya miaka 5 ya mradi huu bado fimilia haina hata balance.
Nikaamua niweke mikakati ya kuweka akiba kwaajili ya back up ili hata mashine zikisumbua, tusianze kuhangaika. Basi bwana kuna ka account kangu ka nmb nilikua nako na kapo active, nikaona sio mbaya nikiwa naweka huko hela wakati nafanya mpango wa kufungua account maalum kwaajili ya huu mradi. Nikaweka kama sh 80,000 hivi. Kwakua nina NMB MKONONI app, nikataka kuangalia salio. Eeeebwana eehh!! Nilichokikuta huko nilipagawa. Badala ya sh kukuta 80,000, nikakuta kuna 70,880. Ikabidi nichoke. Nikaona acha niombe statement ili nijiridhishe. Kunitumia statement kwenye email yangu wakakata sh 1,000 ikabaki sh 69,880. Nikasema hapa usinitanie, kesho lazima nikatoe balance hii. Basi leo ilipofika asubuhi na mapema nikaenda ATM ya pale Mbalizi tawi la NMB USONGWE. Kila nikijaribu kutoa sh 60,00, naambiwa huduma haijakamilika. Ikabidi niingie ndani ili nitolee dirishani. Kilichonikuta ndicho kilichofanya niandike hapa. Nikachukua fomu ya kutolea ha na nikaijaza vizuri ili niweze kutoa japo sh 68,000. Kwenda dirishani nikaambiwa siwezi kutoa kiwango hicho kwakua salio halitoshi. Nikashtuka. Nikamwambia teller kuwa mbona acc yangu ina sh 69,880? Akanijibu kwa ukali kuwa "bro kutoa hapa ni sh 6,500 kwahiyo inatakiwa utoa sh 60,000" nikahamaki huku nikijisonya kwanini nilidumbukiza hela bank.

Nikiwa na uchungu wa hela yote ninayoipa NMB pasipo wao kutoa jasho, nikajaza fomu ya kutoa sh 60,000

Hakika ni bora kuchimbia hela chini kuliko kuweka hela NMB
Mabenki yana makato ya hatari mimi week mbili zilizopita CRDB wamenilima kama laki yani mpaka sasa sijaelewa wameilima vipi, sema nimekosa muda wa kufuatilia ila nimeamua siweki pesa tena kwenye hiyo account labda kwa bahati mbaya.
 
Tulikuwa na tabia ya kuangalia salio kwa mtindo wa kutoa hela kwenye NMB ili itoke au kama huna salio ijibu insuficient balance. Sasa siku hizi hata hilo jibu la INSUFICIENT BALANCE utakatwa mara tu hela itakapoingia.
 
Bank za bongo ni balaa...ungekuwa unataka kutoa 10m ndio ungefurahi
 
Mbona umelia lia saana halafu sijaona point yako mkuu,kwani hujui kuwa kutoa pesa dirishani panakuwa na makato makubwa??
Huwezi kuona kwakua hujataka kuona
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Back
Top Bottom