Iam back_Euphoria
JF-Expert Member
- Sep 17, 2024
- 365
- 1,072
- Thread starter
- #21
THE HIGHEST GOOD
BY EUPHORIA
CHAPTER 14: Chui wa milia
"Kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma nadhani unanichukulia kama fala mwenzio sio?" aliongea na kunyanyua mkono wa kulia kisha kugusanisha kidole gumba na cha shahada kisha ku-snap na kutoa sauti
Kwenye moja ya pango la himaya hiyo ulisikika mburuzo na sauti ya mtu kulalama maumivu na palepale kwenye lango la pango alionekana mtu mwenye sura mbovu kama nyanya iliyooza
Alikuwa ameshika mguu wa mtu huku akimburuza bila huruma, mtu aliyekuwa akiburuzwa alikuwa kijana mdogo mwenye umri wa miaka kumi na sita aliyefungwa kamba mwilini asifurukute
"Kiongozi...kiongozi... nisaidie, niokoe jamani!" alikuwa akilia sana kiasi cha kutia huruma
Yule kijana alitupwa karibu na mkuu wa himaya hiyo kisha yule mkuu alisimama na kumuinua kichwa kwa kushika nywele zake
"Kiongozi Shohei nitamuua mwanafunzi wako mmoja halafu tuone kama utaendelea kuleta kiburi" aliongea
"Tafadhali usiniue, nipo tayari kuwa mmoja wa wafuasi wako, nipo tayari kuwa mtumwa wako, tafadhali usiniue!" alilia akiomba kuonewa huruma
"Huyu kijana bila shaka woga umemzidia, ona mpaka ana jikojolea na kuinajisi madhabahu ya mkuu wetu" aliongea mmoja wa wahalifu waliomzunguka shohei
Shohei aliishia kujiambia ni mwanafunzi wa aina gani amemsajili? Hana uaminifu kabisa, hata kama ni muoga ndio kulisaliti dhehebu na kutaka kuwa miongoni mwa maadui? Hata hivyo alielewa alikuwa bado kijana mdogo mwenye ndoto nyingi za kutaka kutimiza ndio maana hakutaka kufa mapema
"Kiongozi Shohei, kwa mwanafunzi muoga kama huyu na msaliti sidhani kama utahoji nikimuua?" aliongea na palepale bila kupoteza muda alizungusha shingo ya kijana yule, na kupoteza maisha papohapo
Shohei moyo ulimdunda paah! akiwa na uso usioelezeka, na palepale mlio wa ding! ulisikika akilini mwake kisha kosei kwa njia ya kifikra alimtaarifu
"Umepoteza mwanafunzi mmoja na kwasababu hiyo umepatiwa misheni ya dharula, waue wote walioko hapo asibaki hai hata mmoja, ili roho ya mwanafunzi huyo ipate amani huko iliko"
"Hehehe! Inaonekana huyu mwanaharamu amekasirika" aliongea kibaraka yule aliyehusika kumburuza kijana aliyesimama karibu na jukwaa alipo mkuu wake mara baada ya kumuona Shohei yupo kimya kana kwamba alikuwa kwenye maombolezo ya kimya kimya
"Unapaswa kushukuru we mwanaharamu, mkuu wetu amekusaidia kushugulika na mwanafunzi wako msaliti" aliendelea kuongea na ile anamaliza sentensi yake tu alishtukia kutobolewa kifuani upande wa moyo kiasi cha upanga kutokelezea mbele
Na nyuma yake alionekana Shohei ambaye alitimiza azma hiyo, haikueleweka upanga ameutoa saa ngapi
"Kibaraka wako alikuwa anapiga domo hovyo, hakuwa na adabu hivyo na imani pia hutonioji kwa kukusaidia kumshughulikia sio?" aliongea Shohei
"Umethubutu kumuua ndugu yangu? Unapaswa kulipia kwa uhai wako!" alimaka mmoja wa wahalifu kwa hasira na kumsogelea Shohei kwa spidi akilenga kumpiga ngumi ya utosi akidhamiria kupasua kichwa chake kwa nguvu za nishati ya mbingu na ardhi
Hata hivyo Shohei alionekana kuwa makini mno kwani alikwepa ngumi ile na kwa wakati huohuo akichannel nguvu za nishati kwenda mguuni mwake na kumsindilia teke lililomrudisha nyuma mita kadhaa, licha ya kuvaa joho, kurusha teke haikuwa tabu kutokana joho kuwa pana
"Acheni kupigana!" ilisikika sauti ya mamlaka na msisimko wa nguvu kusambaa eneo llote kiasi kwamba Shohei alihisi ubaridi kwenye uti wake wa mgongo
“Hakika ustadi wako wa sanaa za mapigano ni wa kipekee sana, nakubali kwa kumuua kibaraka wangu na mimi huwa sipendi kukuza jambo dogo kuwa kubwa. Umebakiwa na wanafunzi arobaini na sita walio mikononi mwangu
Kabidhi shekeli elfu arobaini na sita kwa wote kisha kila mmoja ashike njia yake” aliongea mkuu yule
Shohei alijiambia inaonekana huyu mkuu ana shida sana na pesa, kwani alikuwa tayari kupoteza kibaraka wake kwa ajili ya pesa Hata hivyo haikumshangaza sana
"Nimeshasema na narudia tena kusema, Shekeli moja kama ada ya malezi hakuna maridhiano"
"We mshenzi..!" alikunja ndita huku akijizuia hasira
"Mkuu niachie mimi hii kazi, nitamuua kisha tunamsachi tu nguo zake na kama tukikosa bila shaka ndani ya dhehebu lake kutakuwa na za kutosha" aliongea yule mtu aliyedhamiria kumpasua kichwa mwanzo
"kuwa makini, inaonekana huyu kijana ana kasi kubwa" mkuu yule alimruhusu
"Usiwaze sana mkuu wangu hawezi kunizidi kasi" alimjibu mkuu wake
"Usimuonyeshee huruma, mpatie kifo chenye maumivu kulipiza kisasi kwa wenzetu waliotangulizwa kwa mkono wake!" aliongea mmoja wa wahalifu akionekana kuwa chawa na asiye na mafunzo ya kinishati
"Mvunje mifupa huyo ya kila mwili aone ya maumivu!" aliongea chawa mwingine
Upande wa Shohei hakujisumbua hata kuwasikiliza zaidi ya kutulia tuli akitazamana na yule mtu, alijiambia kwa muonekano wake wa kibaunsa bila shaka atakuwa ni aina ya wale wanaotumia uzito wa miili kushambulia hivyo kudili naye ni suala la kufumba na kufumbua tu
Lile baunsa alikuwa akitumia mafunzo ya nishati, alikaa mkao wa kuwa tayari kwa pambano kisha alichannel nishati za mbingu na ardhi katika mishipa yake kuongeza kasi ya msukumo wa damu na kwa uwepesi wa hali ya juu kama unyoya wa kuku alimsogelea Shohei akimtandika ngumi ya kifua iliyomrusha mita kadhaa na kujibamiza mgongo kwenye moja ya nguzo za mbao eneo hilo na kuanguka chini
"Sh*t anaspidi kali" aliongea huku akitema damu mdomoni kisha kwa msaada wa upanga alioushika alijinyanyua na kusimama wima
Alionekana kumchukulia poa sana mshindani wake na palepale alikumbuka sheria ya kwanza kwenye pambano aliyowahi kujifunza kwa njia ngumu.
Kwamba usimdharau adui yako hata kama anaonekana mdhaifu mbele yako, kwani hata chui wa milia awindapo hadharau kitoweo chake hata kama ni sungura mdogo
Alijiambia anapaswa kuwa kama Chui wa milia na palepale alikaa mkao wa utayari wa kupambana awamu hio akiwa na sura ya kazi kwelikweli kuliko mwanzo
Kufumba na kufumbua Shohei kwa spidi ya hali ya juu baada ya kuamsha nguvu zake za nishati alimsogelea
"Shwaah! Shwiih! Swiiih! Shwuush!" ilikuwa ni milio ya upanga kukata hewa, kwani mshindani wake alionekana kuwa na spidi kubwa kumzidi bado hivyo alikwepa mashambulizi ya Shohei bila tabu
"Una spidi ndogo sana, ngoja nikuonyeshe maana halisi ya kuwa na spidi kali" aliongea mtu yule na palepale alianza kumzunguka Shohei kws kasi ya ajabu na kuonekana kana kwamba anazungukwa na kimbunga
"Inaonekana ameimarika karltika mbinu ya hatua saba za kimbunga kuliko mwanzo" aliongea mkuu wa himaya akiangalia pambano kwa namna ya kuridhika
"Ni kweli hata mimi pia kwa spidi yake ya sasa inanipa wakati mgumu kidogo kuendana naye" alimuunga mkono mmoja wa kibaraka wake aliyesimama nyuma yake upande wa kushoto
"Haijalishi huyo kiongozi ana utaalamu gani ila mbele ya spidi kubwa ni bure tu!" aliendelea
Upande wa Shohei aliyekuwa akizungukwa kwa spidi aliishia tu kutabasamu na kuushika upanga ule wa maafa imara kisha kwa spidi alifanya shambulizi kama anajaribu kuchoma upepo
Na palepale kichwa cha yule nmtu kilitenganishwa na shingo yake huku damu nyingi zikiruka kwa kasi kama bomba lililofunguliwa maji
"Spidi yako ni kubwa sana kiasi kwamba unashindwa hata kuicontrol, kwani hujui kukata kona? Kulikuwa na ulazima wa kulivamia psnga langu? ona sasa ulivyokufa kizembe!" aliongea bila hatia yoyote
Ukweli alichofanya ni kuegesha tu upanga usawa wa shingo kwenye mzunguko wa yule mtu na kutokana na kazi asingeweza kuepuka kulivamia panga lake, ni kama alikuwa akiwaonyeshea udhaifu wa hiyo mbinu yao
Yule mtu aliyepoteza uhai alikuwa ni miongoni mwa wale watu nane waliosimama nyuma ya mkuu wao, hivyo idadi kupungua na kubaki saba
Hivyo baada ya kuona mwenzao ameuawa kirahisi hivyo walikasirika na kumuona Shohei kuwa tishio na wote kwa pamoja waliamua kumshambulia wakimzunguka pande zote
Shohei alionekana kushtukia hilo mapema na palepale alisafirisha nguvu za nishati kwenda miguuni mwake na kuruka juu urefu wa kama mita thelathini na ushee na wakati akiwa hewani aliachia mashambulizi ya mawimbi yenye makali kama upanga hivyo hawakuwa na jinsi zaidi ya kujikinga na mashambulizi hayo na kurudi nyuma
"Kwahiyo mmeona mnishambulie kwa pamoja baada ya kuona kila mmoja haniwezi?, inaonekana sina jinsi zaidi ya kutumia ile mvinu" aliongea Shohei baada ya kutua ardhini
Kisha palepale baada ya kuchezesha mkono hewani ilitokea karatasi nyeupe yenye michoro na maneno ya ajabu, ilikuwa ni ile talasimu ya ufunguzi wa muhuri kwa upanga huo wa maafa
Na bila kupoteza muda aliipigisha ile talasimu kwenye upanga wake na ile talasimu kugeuka moshi na moshi ule kuuvamia upanga huo
Kilikuwa ni kitendo cha sekunde tano kwa kutoa talasimu kwenye mfumo na kuigusanisha na upaga ule, kisha sekunde tatu zingine upanga ule ulianza kutoa mwanga mkali kiasi cha kufunika eneo lote wasipate kuona vizuri
"Inaonekana alikuwa amebeba siraha ya kimiujiza" alijiwazia mkuu wa himaya hiyo huku akikinga macho yake kwa mkono kutokana na mwanga kuwa mkali
Sekunde ambayo mwanga ule mkali unapotea mkuu huyo alishtukia ncha ya upanga ule kuwa karibu na uso wake
Kilichomshangaza ni umbali uliopo kati Shohei na yeye, umbali wa mita arobaini, kilichomvchangaza zaidi ni msisimko uliokuwa ukitoa, na ule ni msisimko ulimfanya kutetemeka bila kupenda, kupumua nako kulikuwa ni kwa tabu sana kutokana na mkandamizo wa hewa
Hisia alizokuwa akizipata ni kana kwamba upanga huo una uhai ndani yake, na upanga kuwa ni kiumbe cha kutisha
Mara aligundua kitu kingine tena kilichozidi kumuogopesha zaidi, ni kuwa watu wake wote walikuwa wamekufa miili yao ikiwa chini imetenganishwa kwa kukatwa viuno. Damu nyingi zilikuwa zimetapakaa ardhini
"Kwahiyo hii ndio nguvu iliyojificha ya huu upaga wa maafa? Lakini urefu wa mita arobaini ni mrefu kishenzi" alijiongelesha, ilioneka upanga ule uliongezeka urefu na makali
**********
BY EUPHORIA
CHAPTER 14: Chui wa milia
"Kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma nadhani unanichukulia kama fala mwenzio sio?" aliongea na kunyanyua mkono wa kulia kisha kugusanisha kidole gumba na cha shahada kisha ku-snap na kutoa sauti
Kwenye moja ya pango la himaya hiyo ulisikika mburuzo na sauti ya mtu kulalama maumivu na palepale kwenye lango la pango alionekana mtu mwenye sura mbovu kama nyanya iliyooza
Alikuwa ameshika mguu wa mtu huku akimburuza bila huruma, mtu aliyekuwa akiburuzwa alikuwa kijana mdogo mwenye umri wa miaka kumi na sita aliyefungwa kamba mwilini asifurukute
"Kiongozi...kiongozi... nisaidie, niokoe jamani!" alikuwa akilia sana kiasi cha kutia huruma
Yule kijana alitupwa karibu na mkuu wa himaya hiyo kisha yule mkuu alisimama na kumuinua kichwa kwa kushika nywele zake
"Kiongozi Shohei nitamuua mwanafunzi wako mmoja halafu tuone kama utaendelea kuleta kiburi" aliongea
"Tafadhali usiniue, nipo tayari kuwa mmoja wa wafuasi wako, nipo tayari kuwa mtumwa wako, tafadhali usiniue!" alilia akiomba kuonewa huruma
"Huyu kijana bila shaka woga umemzidia, ona mpaka ana jikojolea na kuinajisi madhabahu ya mkuu wetu" aliongea mmoja wa wahalifu waliomzunguka shohei
Shohei aliishia kujiambia ni mwanafunzi wa aina gani amemsajili? Hana uaminifu kabisa, hata kama ni muoga ndio kulisaliti dhehebu na kutaka kuwa miongoni mwa maadui? Hata hivyo alielewa alikuwa bado kijana mdogo mwenye ndoto nyingi za kutaka kutimiza ndio maana hakutaka kufa mapema
"Kiongozi Shohei, kwa mwanafunzi muoga kama huyu na msaliti sidhani kama utahoji nikimuua?" aliongea na palepale bila kupoteza muda alizungusha shingo ya kijana yule, na kupoteza maisha papohapo
Shohei moyo ulimdunda paah! akiwa na uso usioelezeka, na palepale mlio wa ding! ulisikika akilini mwake kisha kosei kwa njia ya kifikra alimtaarifu
"Umepoteza mwanafunzi mmoja na kwasababu hiyo umepatiwa misheni ya dharula, waue wote walioko hapo asibaki hai hata mmoja, ili roho ya mwanafunzi huyo ipate amani huko iliko"
"Hehehe! Inaonekana huyu mwanaharamu amekasirika" aliongea kibaraka yule aliyehusika kumburuza kijana aliyesimama karibu na jukwaa alipo mkuu wake mara baada ya kumuona Shohei yupo kimya kana kwamba alikuwa kwenye maombolezo ya kimya kimya
"Unapaswa kushukuru we mwanaharamu, mkuu wetu amekusaidia kushugulika na mwanafunzi wako msaliti" aliendelea kuongea na ile anamaliza sentensi yake tu alishtukia kutobolewa kifuani upande wa moyo kiasi cha upanga kutokelezea mbele
Na nyuma yake alionekana Shohei ambaye alitimiza azma hiyo, haikueleweka upanga ameutoa saa ngapi
"Kibaraka wako alikuwa anapiga domo hovyo, hakuwa na adabu hivyo na imani pia hutonioji kwa kukusaidia kumshughulikia sio?" aliongea Shohei
"Umethubutu kumuua ndugu yangu? Unapaswa kulipia kwa uhai wako!" alimaka mmoja wa wahalifu kwa hasira na kumsogelea Shohei kwa spidi akilenga kumpiga ngumi ya utosi akidhamiria kupasua kichwa chake kwa nguvu za nishati ya mbingu na ardhi
Hata hivyo Shohei alionekana kuwa makini mno kwani alikwepa ngumi ile na kwa wakati huohuo akichannel nguvu za nishati kwenda mguuni mwake na kumsindilia teke lililomrudisha nyuma mita kadhaa, licha ya kuvaa joho, kurusha teke haikuwa tabu kutokana joho kuwa pana
"Acheni kupigana!" ilisikika sauti ya mamlaka na msisimko wa nguvu kusambaa eneo llote kiasi kwamba Shohei alihisi ubaridi kwenye uti wake wa mgongo
“Hakika ustadi wako wa sanaa za mapigano ni wa kipekee sana, nakubali kwa kumuua kibaraka wangu na mimi huwa sipendi kukuza jambo dogo kuwa kubwa. Umebakiwa na wanafunzi arobaini na sita walio mikononi mwangu
Kabidhi shekeli elfu arobaini na sita kwa wote kisha kila mmoja ashike njia yake” aliongea mkuu yule
Shohei alijiambia inaonekana huyu mkuu ana shida sana na pesa, kwani alikuwa tayari kupoteza kibaraka wake kwa ajili ya pesa Hata hivyo haikumshangaza sana
"Nimeshasema na narudia tena kusema, Shekeli moja kama ada ya malezi hakuna maridhiano"
"We mshenzi..!" alikunja ndita huku akijizuia hasira
"Mkuu niachie mimi hii kazi, nitamuua kisha tunamsachi tu nguo zake na kama tukikosa bila shaka ndani ya dhehebu lake kutakuwa na za kutosha" aliongea yule mtu aliyedhamiria kumpasua kichwa mwanzo
"kuwa makini, inaonekana huyu kijana ana kasi kubwa" mkuu yule alimruhusu
"Usiwaze sana mkuu wangu hawezi kunizidi kasi" alimjibu mkuu wake
"Usimuonyeshee huruma, mpatie kifo chenye maumivu kulipiza kisasi kwa wenzetu waliotangulizwa kwa mkono wake!" aliongea mmoja wa wahalifu akionekana kuwa chawa na asiye na mafunzo ya kinishati
"Mvunje mifupa huyo ya kila mwili aone ya maumivu!" aliongea chawa mwingine
Upande wa Shohei hakujisumbua hata kuwasikiliza zaidi ya kutulia tuli akitazamana na yule mtu, alijiambia kwa muonekano wake wa kibaunsa bila shaka atakuwa ni aina ya wale wanaotumia uzito wa miili kushambulia hivyo kudili naye ni suala la kufumba na kufumbua tu
Lile baunsa alikuwa akitumia mafunzo ya nishati, alikaa mkao wa kuwa tayari kwa pambano kisha alichannel nishati za mbingu na ardhi katika mishipa yake kuongeza kasi ya msukumo wa damu na kwa uwepesi wa hali ya juu kama unyoya wa kuku alimsogelea Shohei akimtandika ngumi ya kifua iliyomrusha mita kadhaa na kujibamiza mgongo kwenye moja ya nguzo za mbao eneo hilo na kuanguka chini
"Sh*t anaspidi kali" aliongea huku akitema damu mdomoni kisha kwa msaada wa upanga alioushika alijinyanyua na kusimama wima
Alionekana kumchukulia poa sana mshindani wake na palepale alikumbuka sheria ya kwanza kwenye pambano aliyowahi kujifunza kwa njia ngumu.
Kwamba usimdharau adui yako hata kama anaonekana mdhaifu mbele yako, kwani hata chui wa milia awindapo hadharau kitoweo chake hata kama ni sungura mdogo
Alijiambia anapaswa kuwa kama Chui wa milia na palepale alikaa mkao wa utayari wa kupambana awamu hio akiwa na sura ya kazi kwelikweli kuliko mwanzo
Kufumba na kufumbua Shohei kwa spidi ya hali ya juu baada ya kuamsha nguvu zake za nishati alimsogelea
"Shwaah! Shwiih! Swiiih! Shwuush!" ilikuwa ni milio ya upanga kukata hewa, kwani mshindani wake alionekana kuwa na spidi kubwa kumzidi bado hivyo alikwepa mashambulizi ya Shohei bila tabu
"Una spidi ndogo sana, ngoja nikuonyeshe maana halisi ya kuwa na spidi kali" aliongea mtu yule na palepale alianza kumzunguka Shohei kws kasi ya ajabu na kuonekana kana kwamba anazungukwa na kimbunga
"Inaonekana ameimarika karltika mbinu ya hatua saba za kimbunga kuliko mwanzo" aliongea mkuu wa himaya akiangalia pambano kwa namna ya kuridhika
"Ni kweli hata mimi pia kwa spidi yake ya sasa inanipa wakati mgumu kidogo kuendana naye" alimuunga mkono mmoja wa kibaraka wake aliyesimama nyuma yake upande wa kushoto
"Haijalishi huyo kiongozi ana utaalamu gani ila mbele ya spidi kubwa ni bure tu!" aliendelea
Upande wa Shohei aliyekuwa akizungukwa kwa spidi aliishia tu kutabasamu na kuushika upanga ule wa maafa imara kisha kwa spidi alifanya shambulizi kama anajaribu kuchoma upepo
Na palepale kichwa cha yule nmtu kilitenganishwa na shingo yake huku damu nyingi zikiruka kwa kasi kama bomba lililofunguliwa maji
"Spidi yako ni kubwa sana kiasi kwamba unashindwa hata kuicontrol, kwani hujui kukata kona? Kulikuwa na ulazima wa kulivamia psnga langu? ona sasa ulivyokufa kizembe!" aliongea bila hatia yoyote
Ukweli alichofanya ni kuegesha tu upanga usawa wa shingo kwenye mzunguko wa yule mtu na kutokana na kazi asingeweza kuepuka kulivamia panga lake, ni kama alikuwa akiwaonyeshea udhaifu wa hiyo mbinu yao
Yule mtu aliyepoteza uhai alikuwa ni miongoni mwa wale watu nane waliosimama nyuma ya mkuu wao, hivyo idadi kupungua na kubaki saba
Hivyo baada ya kuona mwenzao ameuawa kirahisi hivyo walikasirika na kumuona Shohei kuwa tishio na wote kwa pamoja waliamua kumshambulia wakimzunguka pande zote
Shohei alionekana kushtukia hilo mapema na palepale alisafirisha nguvu za nishati kwenda miguuni mwake na kuruka juu urefu wa kama mita thelathini na ushee na wakati akiwa hewani aliachia mashambulizi ya mawimbi yenye makali kama upanga hivyo hawakuwa na jinsi zaidi ya kujikinga na mashambulizi hayo na kurudi nyuma
"Kwahiyo mmeona mnishambulie kwa pamoja baada ya kuona kila mmoja haniwezi?, inaonekana sina jinsi zaidi ya kutumia ile mvinu" aliongea Shohei baada ya kutua ardhini
Kisha palepale baada ya kuchezesha mkono hewani ilitokea karatasi nyeupe yenye michoro na maneno ya ajabu, ilikuwa ni ile talasimu ya ufunguzi wa muhuri kwa upanga huo wa maafa
Na bila kupoteza muda aliipigisha ile talasimu kwenye upanga wake na ile talasimu kugeuka moshi na moshi ule kuuvamia upanga huo
Kilikuwa ni kitendo cha sekunde tano kwa kutoa talasimu kwenye mfumo na kuigusanisha na upaga ule, kisha sekunde tatu zingine upanga ule ulianza kutoa mwanga mkali kiasi cha kufunika eneo lote wasipate kuona vizuri
"Inaonekana alikuwa amebeba siraha ya kimiujiza" alijiwazia mkuu wa himaya hiyo huku akikinga macho yake kwa mkono kutokana na mwanga kuwa mkali
Sekunde ambayo mwanga ule mkali unapotea mkuu huyo alishtukia ncha ya upanga ule kuwa karibu na uso wake
Kilichomshangaza ni umbali uliopo kati Shohei na yeye, umbali wa mita arobaini, kilichomvchangaza zaidi ni msisimko uliokuwa ukitoa, na ule ni msisimko ulimfanya kutetemeka bila kupenda, kupumua nako kulikuwa ni kwa tabu sana kutokana na mkandamizo wa hewa
Hisia alizokuwa akizipata ni kana kwamba upanga huo una uhai ndani yake, na upanga kuwa ni kiumbe cha kutisha
Mara aligundua kitu kingine tena kilichozidi kumuogopesha zaidi, ni kuwa watu wake wote walikuwa wamekufa miili yao ikiwa chini imetenganishwa kwa kukatwa viuno. Damu nyingi zilikuwa zimetapakaa ardhini
"Kwahiyo hii ndio nguvu iliyojificha ya huu upaga wa maafa? Lakini urefu wa mita arobaini ni mrefu kishenzi" alijiongelesha, ilioneka upanga ule uliongezeka urefu na makali
**********