Simulizi ya Kifaransa: Ubora "THE HIGHEST GOOD"

Simulizi ya Kifaransa: Ubora "THE HIGHEST GOOD"

Iam back_Euphoria

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2024
Posts
356
Reaction score
1,071
Ndugu zangu habari za kuwapotea? Naam ni mimi Euphoria mwandishi wa Solo king, mniwie radhi kwa kupotea na kuwa kimya kwa muda mrefu zaidi, kipindi kile nilikuwa nikiumwa, nilikuwa nalala kitanani muda wote, na kuna mambo mengine yalitokea ukijumlisha na matukio ya oct 29, nisiongee sana maana nitaharibu

Ila nilipoteza access ya kuingia JF na kule fasihinet

Nimewaletea simulizi nyingine iitwayo UBORA "THE HIGHEST GOOD" kwa sababu simulizi ya awali nilipoteza research zake hivyo sidhani kama itaendelea hivyo muisamehe

Kuliko kukaa kimya na kuipotezea nimewaletea hii👇

TekTok-20260305-015837_719x1017.png


THE HIGHEST GOOD

BY EUPHORIA

CHAPTER 1: Nafasi ya kuishi tena


Anga la bluu lilikuwa limetulia likipendezeshwa na nyota nyingi angani pamoja na mwezi umulikao usiku huo, hali ya hewa ilikuwa tulivu, upepo mwanana ukipuliza maeneo yote ya mji

Usiku huo wa saa nne alionekana mwanaume kijana akitembea hali ya kuwa katika mawazo, muda wote alikuwa akiangalia chini tu, alikuwa amevalia nguo shirt la mikono mirefu rangi damu ya mzee, suruali nyeusi ya kitambaa iliyopauka na viatu vyeusi vilivyoonekana kutumika kwa muda mrefu sana

Haikueleweka mtu huyo alikuwa akiwaza nini kichwani mwake nyakati hiyo ya usiku

Upande wa mbele yake umbali wa kama kilomita mbili kulionekana gari ambalo lilikuwa likija upande wake kwa kasi sana, na bila shaka ilionekana dereva wa gari hilo alikuwa amelewa chakari kutokana na uendeshaji wake wa gari

Mwanaume yule aliyekuwa katika mawazo alionekana kutosikia kabisa wala kuona kutokana na kuzama katika kina cha mawazo na kwa bahati mbaya aligongwa na gari lile na kurushwa na kuanguka na alidhurika vibaya sana, damu nyingi zikimtoka na kumwagikia ardhini

Dereva wa gari kutokana na kuogopa kwa kosa alilolifanya hakusimama wala! bali aliendelea kuendesha gari kuondoka eneo hilo haraka kukimbia dhambi aliyoifanya usiku huo, kibaya zaidi eneo hilo hakukuwa na watu.

Mwanaume yule alikuwa ametulia tuli akiugulia maumivu ardhini kichwa kikiangalia angani na mara muda huohuo mvua ikaanza kunyesha ilikuwa ni mvua ya kawaida sio kubwa sana wala ndogo sana.

"Je huu ndio mwisho wangu? Hivi ndivyo ilivyopangwa nife? Huu ndio mwisho wangu? Mmh?" aliongea akilini mwake mwanaume huyo bila kujua maswali hayo yanamlenga nani au labda pengine alikuwa akijiuliza mwenyewe?

Maskini kijana wa watu alikufa kiholela sana, pengine asingekuwa katika hali ile ya mawazo angeweza kusalimika lakini uzembe siku zote ni uzembe tu, na uzembe huo wa kutokuwa makini ulimgharimu maisha yake na haikuwezekana kurudisha muda nyuma kurekebisha uzembe wake sababu muda siku zote haurudi nyuma kamwe bali unasonga mbele.

Ni jambo la kuhuzunisha sana kwa mtu kufa lakini huo ndio uhalisia wenyewe kwamba kifo ni lazima. Kibaya zaidi kijana huyo alikuwa ndio kwanza amepata ajira baada ya juhudi nyingi na kusota kote kwa lengo la kuishi maisha bora. Lakini unajua nini? Ulimwengu siku zote ni katili sana.

"Sina demu, sina mtoto ndoto yangu ya kuwa baba ndio inakufa hivihivi? Vipi kuhusu ahadi zangu kwa mama na dogo? Kwanini inakuwa hivi? KWANINI?" aliendelea kuongea akilini mwake huku machozi yakimtoka bila sauti

Mvua iliendelea kunyesha juu ya mwili wake uliokuwa umelala barabarani kana kwamba mbingu zenyewe zilikuwa zikilia pamoja naye kimya kimya. Maji yalichanganyika na damu yake, yakasafisha damu yake ardhini taratibu, yakafuta alama za maisha yake kama vile hakuwahi kuwepo.

Dakika zikageuka kuwa saa.

Asubuhi ilipowadia, watu wachache waliokuwa wakielekea makazini walikusanyika kwa mshangao. Simu zikatolewa, picha zikapigwa, vichwa vikatikiswa kwa huzuni, kisha kila mmoja akaendelea na shughuli zake. Hakuna aliyemjua. Hakuna aliyejua jina lake wala sura yake. Alikuwa tu ni “mwili wa kijana asiyejulikana.”

Lakini kwa upande mwingine , katika chumba kidogo cha kupanga kilichojaa unyevunyevu, simu ya mama yake iliita bila kupokelewa. Alikuwa ameamka mapema kuandaa chai, moyo wake ukiwa na furaha kwa sababu jana tu mwanawe alimwambia:

“Mama, nimepata kazi… sasa mambo yatabadilika.”

Alikuwa ameahidi kumpeleka hospitalini kwa matibabu ya muda mrefu aliyokuwa akiahirisha kwa kukosa pesa. Alikuwa ameahidi kumlipia mdogo wake ada ya shule. Alikuwa ameahidi kujenga nyumba ndogo kijijini. Lakini ahadi zake zote zilibaki kuwa historia yaani maneno tupu.

Baadaye, polisi walipogundua kitambulisho mfukoni mwake, simu ile ile ya mama yake ikaita tena safari hii kutoka namba isiyojulikana.

Habari zilipofika, kikombe cha chai kilimdondoka mikononi mwake na kuvunjika sakafuni. Alianguka chini na kufa kwa mshtuko wa moyo familia ile maskini iilivunjika ndani ya siku moja kws uzembe wa mtu mwingine. Kwa uzembe wa dereva aliyekimbia majukumu yake! Ni ulimwengu katili ulioje

*****

"Niko wapi hapa ni wapi" ilikuwa ni sauti ya mwanaume ikiuliza

Mwanaume huyo alikuwa mahali ambapo kulikuwa na nuru nyeupeee asionekane mtu mwingine zaidi ya yeye mwenyewe

"Usiogope mahali hapa ni salama" ilisikika sauti yenye kujirudia rudia kama mwangwi

"Wewe ni nani na mbona sikuoni?" aliuliza tena yule mwanaume

"Mimi? Unauliza kwamba mimi ni nani?"

"Ndio, wewe ni nani?" aliuliza tena

"Sawa nitakujibu kwa uchache wewe mwanadamu, kwakuwa ninyi ni viumbe wenye shauku na kutaka kujua msiyoyafahamu"

"Mimi ndiye, mimi ni MIMI. Mimi ni fahamu ya nafsi yangu. Mimi ni mtu mkuu, mwenye nguvu, niliyeiteka roho yako kabla haijatoweka. Huna haja ya kujua jina langu; unachohitaji kujua ni kwamba nataka kukupa nafasi ya kuishi tena kwa huruma tu lakini kwa masharti kadhaa.”"

"Wewe ni Mungu?"

"Mungu? Hahaha hapana mimi si Mungu, kuhusu mimi ni kiumbe gani hutakiwi kujua"

"Sawa sitakiwi kujua lakini unamaanisha nini kusema kwamba unanipa nafasi ya kuishi kwa mashati kadhaa?"

"Ndivyo nilivyomaanisha kipi kingine unadhani nimemaanisha?"

"Kwanini unanisaidia?"

"Nishasema ni kwasababu ya huruma, lakini juu yako kukubali au kukataa"

"Siwezi kukubali bila kusikia masharti"

"Hahaha usiwe na wasiwasi ninakueleza nilikuwa nikisubiri useme hivyo, sharti la kwanza utafanikisha misheni ambazo nitakuwa nakupatia, of coz zawadi ipo ukifaulu nadhabu pia ukifeli, pili utaishi katika ulimwengu tofauti na huo uliotoka, utakuwa na uhusika mwingine na mwisho kabisa uwe mtiifu"

"Hayo tu?"

"Naam ni hayo tu"

"Unamaanisha nini kuwa mtiifu mi naona unamaanisha itaonekana sitakuwa huru"

"Ni juu yako kuchagua"

"vipi nikikataa?" ,

"Jibu ni rahisi tu ukikataa utakufa roho yako itayeyuka na kupotea"

"Okay nimekuelewa, sharti la kuishi kwingine naweza kukubaliana lakini unamaanisha nini kusema misheni"

"Usijali nitakupa muongozo ambao utajibu majibu hayo mawili ila fanya uamuzi kwanza je unakubali hii nafasi ama unaikataa?"

"Fursa adimu haiji mara mbili na nilikotoka hakunaga kitu cha bure hivyo naweza kukuamini na jibu langu ni Naam" alijibu yule mwanaume na palepale mwanga mkali mweupe ukaongezeka kisha kikatokea duara fulani hivi la bluu kama mpira ueleao na kumsogelea taratibu mwanaume yule

"Usiogope, huo ndio mwongozo wangu na huyo ni msaidizi wangu mruhusu kuungana nawe" ilisikika sauti ya mwangwi na yule mwanaume alitii na kutulia tuli kisha kile kile kimpira kikaungana na roho yake na kuwa umoja(oneness)

*****

Katika ulimwengu ambao ulionekana wa kale sana yaani ulimwengu ambayo teknolojia ilikuwa ni ndogo mno tena mnoo alionekana kijana mtanashati mwenye asili ya ki-asia akiwa amelala ardhini, alikuwa ni mtanashati kweli, alikuwa na mwili wenye afya kama mwanariadha, alikuwa na nywele nyeupe kichwani, yani ieleweke naposema nyeupe, licha ya kuonekana nyeupe alionekana kijana zaidi, alikuwa amevaa mavazi ya kizamani sana, na mavazi yake yalikuwa yamechakaa kwelikweli, alikuwa na umri wa miaka ya ishirini ya mwanzoni

`Kwahiyo huu ndio ulimwengu mwingine nitakaoishi? " alijiuliza

" Naam ndio mdio huu ndio utakaokuwa ukiishi" ilisikika sauti nyingine kutoka katika nafsi yake na kushanga

"Unashangaa nini? Mimi ndiyo muongozo wake ninaitwa" yule mwenye manufaa"

"Jina lako ni yule mwenye manufaa?"

"Naam hilo ndilo jina langu"

"Vipi kuhusu mimi jina langu ni nani?"

"Emiichi, wewe unaitwa Emiichi Shohei" Ilijibu ile sauti kutoka nafsini mwake

"Ooh okay kwakuwa naitwa Emiichi shohei, Basi nawei nikuite Kosei, unaonaje issitoshe kukuita" yule mwenye manufaa" ni kupoteza sauti tu au unasemaje? AliongeaShohei huku akinyanyuka na kukaa kitako ardhini

"Hahaha! sio baya hata hivyo"

"Haya Kosei hapa tupo wapi? na misheni yangu hapa ni ipi na imekuwaje nipo hapa?

"inakubidi nikujibu kwa kirefu Bwana Shohei, kwanza kabisa hapa tupo kwenye himaya la dhehebu fulani au tunaita" sect"" aliongea Kosei na kumfanya Shohei kuangalia huku na huko kwenye eneo walilopo

"Dhehebu hili sio baya lakini, ingawa limekaa kizamani bado pia ni zuri, hewa pia ni Safi kabisa!" aliongea Shohei

"Ni kweli kabisa sasa muanzilishi wa hili dhehebu kiongozi aitwaye Paso Pasio aliwahi kuanguka katika maporomoko marefu na kunusurika hivyo akaunda dhehebu hili na kulipatia jina" mfupa wa chuma" aliendelea kosei na kumfanya Shohei acheke kidogo

"Lengo la kuunda dhehebu hili ni kuwa wenye miili na roho za xhuma ili waje kuisaidia jamii na kufanya yale ya kheri na amani, kiongozi paso pasio alifanya kazi kwa bidii sana kwa zaidi ya miaka kumi na hatimae kufanikisha kuligeuza dhehebu leo ya tisa"

"Levo ya tisa? Ni ukubwa na hadhi gani iliyonayo?" Shohei aliuliza

"Level ya tisa ndio level ya chini kabisa kuliko zote, unapaswa kuelewa zipo leo tisa za hadhi kwa kila dhehebu huku levo ya kwanza ndiyo ya juu zaidi yenye ufalme na heshima iliyoenea" Kosei alimjibu

"Sawa endelea"

"Basi baadae kiongoziPaso Pasii alifungwa jela kwa kufanya kwenye madanguro!"

"Hahaha usinichekeshe bhana, kwamba amefungwa jela kwa kosa la kustarehe kwenye madanguro? Mbona haingii akilini"

"Huu ulimwengu sio kama ule uliotoka kama ilivyokuwa kwenu huko kuwa na sheria zenu huku nako kuna sheria zao, kiongozi wa dhehebu ni kama padre hivyo kufanya uzinzi ni kosa kisheria kwa mujibu wa ulimwengu huu"

"Asee inasikitisha sana, inaonekana huu ulimwengu umekaa kitemi zaidi kuliko ule niliotoka"

**********

CHAPTER 2: Misheni ya kwanza


"Baadae Paso Pasio aliuawa kwa kujaribu kutoka gerezani na wewe Emiichi Shohei namaanishi mmiliki halali wa huo mwili kabla yako alikuwa ni mwanafunzi wa shujaa huyo anayesikitisha" aliendelea kuelezea

"Kwa kifupi Emiichi Shohei halisi, Emiichi wa ulimwengu huu hatuna naye tena, siku tatu baada ya kifo cha mwalimu wake alifariki kwa kudondokewa na ubao mzito usiku wa manena akitaka kwenda chooni, kwahiyo roho yako imeingizwa katika mwili huo na aliyekupa nafasi ya kuishi tena"

"Mpaka hapo umenijibu maswali mawili niliyouliza bado moja la misheni yangu ni ipi?"

"Ooh misheni yako kuu ni kuwa kiongozi wa dhehebu hili na kulifikisha katika kilele cha utukufu unaostahili na unatakiwa utimize misheni hii ndani miaka hamsini ukifeli katika muda huo roho yako itayeyuka na kupotea ni sawa na kusema utakufa"

"Swali langu ni utukufu gani unaostahili hili dhehebu?"

"Swali zuri, utukufu unaostahili dhehebu hili ni kulifanya liwe dhehebu lenye nguvu kuliko madhehebu yote katika ulimwengu huu ikiwa na idadi ya wanafunzi zaidi ya laki moja na katika hilo kutatokea misheni ndogo ndogo na kubwa kubwa"

"Ooh ni hayo tu?" aliuliza Shohei

"Ndio, kwanza unanielewa ninaposema dhehebu?"

"Ndio ndio naelewa unachomaanisha si dini bali dhehebu la kuwafunza watu mbinu za siri na mapigano na kisha kulitumikia kwa jinsi ya sheria zake ni kama wafanyavyo mashaolin"

"Naam inaonekana unafahamu mambo mengi"

"Sana tu"

Mara baada ya mazungumzo hayo marefu kidogo kati ya shohei na kosei basi Shohei alinyanyuka na kusimama na kuanza kutalii eneo lote la himaya hiyo na alikuja kugundua kwamba ni eneo kubwa sana sawa na mita laki tatu za mraba na lilizungukwa na milima mirefu na mabonde kama ngao

Ifahamike kwamba lugha katika mazungumzo ilikuwa ni tofauti kabisa ilikuwa ni lugha ya kale zaidi isijulikane ni lugha gani na Shohei alikuwa akielewa vizuri automatically hata yeye alijishangaa ila hakulitilia maanani jambo hilo

Basi Shohei alitafuta maji akaoga na kubadili nguo safi alizozipata baada ya kuhangaika kuzitafuta kisha kwenda kusimama kwenye eneo la kuingia ndani ya dhehebu hilo yaani langoni kisha kuvuta hewa safi na kuangalia angani

"Sasa kwa kuwa nimekuja katika ulimwengu huu, nitaishi tofauti kama mfalme. Nitakamilisha misheni zote na pia nitawashinda magwiji wote wa ulimwengu huu kwa maarifa yangu yote, ingawa sina uelewa mkubwa na jinsi gani naweza kukamilisha misheni kuu ila ninao muda wa kutosha wa kufikiria na kutafuta njia." aliongea Shohei kisha kunyanyua mikono yake juu kama vile anapokea kitu kutoka angani kisha kusema kwa sauti ya hali ya juu

" Mbinu adimu za uvunaji nishati mbalimbali , maandiko ya siri njooni kwangu!” alinena lakini hakuna kilichotokea zaidi ya upepo kupuliza kisha baada ya kama dakika tatu ukasikika mlio wa ajabu

Ghafla mbele ya macho yako alikuwa akiona mfano kama wa Tv ya hologram, ni kama "touch screen" iliyokuwa na maelezo kuhusu yeye jina lake, umri wake hadhi yake kwa wakati huo na mengi ya maelezo kuhusu dhehebu hilo la mfupa wa chuma

"Oya kosei ni nini hiki naona? Mi nilikuwa nanena to kupoteza sauti" aliuliza

"Huyo unayemuona ni mimi nikijidhihirisha hivyo na hayo maelezo ni kuhusu wewe na dhehebu lako kama unavyoona" aliongea kosei

"Kwamba wwwe ni kama mfumo au robot si ndio?"

"Unaweza sema hivyo ila hapana mimi ni zaidi ya unavyonifikiria utanijua zaidi mbele kwa mbele"

"Maelezo hapo yanaaema natakiwa kutafuta wanafunzi mia moja kukamilisha wanafunzi wanaohitajika kwa dhehebu la hadhi levo ya tisa, na ni misheni nayopaswa kuianza sasahivi nikikaidi napewa adhabu ya kupunguziwa muda kutoka miaka hamsini ya kukamilisha misheni kuu kwenda arobaini seriously!"

"Huu ni unyanyasaji sasa!" aliishia kulalama ila kibishi aliamua tu kuanza mchakato wa kufanikisha misheni ya kutafuta wanafunzi akizingatia lile sharti la utiifu

"Umesahau au unajisahaulisha? hujaja hapa kustarehe kijana, umekuja hapa kutimiza makusudi fulani hivyo changamka kijana muda ni wa thamani sana"

"Nadhani nimesahau kitu unatakiwa kulifanya dhehebu liwe na nguvu kuliko madhehebu yote katika bara hili liitwalo Ardhi ya nyota"

"Nini!? Unasema? Bara zima?"

"Naam" alijibu kosei

"Miaka 50 na unataka nilifanye dhehebu kuwa nguvu namba moja barani? Ni sawa nakuniambia nitumie nusu ya uhai wangu kuhangaikia misheni ya kikuda, laiti ningejua hiki ndicho nachokwenda kufanya nisingekubaliana hata na yale masharti ila kwakuwa nimeyavulia maji nguo sina budi kuyaoga"

"Ding!" ulisikika mlio kwenye nafsi yake na palepale upanga ukatokelezea hewani kimaajabu na kuanguka ukijichomeka ardhini na kumfanya Shohei kushangaa kitendo hiko

"Huo ni upanga wa maafa na kwakuwa unaanza misheni yako ya kwanza siraha hiyo itakufaa sana katika kujilinda unaweza kuuhifashi kwenye stoo iliyoko kwenye mfumo, natumai utautumia vizuri" aliongea kosei na kumuelekeza jinsi ya kutumia mfumo na alifanikiwa kuuhifadhi kwani upanga ule ulipotea kabisa hewani

"Ngoja niucheki huu mfumo kwanza nujue na kupata taarifa" alijisemea na kuanza kubofyabofya kama vile anatumia smartphone

Basi baada ya kuchezeshachezesha vidole hewani kwa dakika kadhaa kuna alivyo elewa na kuna asivyoelewa

"Kuna niliyoelewa hapa ila levo ya ujenzi wa dhehebu na thamani ya mchango wa dhehebu ndio nini hii?"

"Iko hivi dhehebu lako lina sehemu nyingi za kufanyia ujenzi hivyo Kadiri kiwango(level) kinavyokuwa cha juu, ndivyo kazi nyingi zaidi za dhehebu zinavyoweza kufunguliwa."

"Na hapa inaonyesha ni level namba moja je ni kwa namna gani naweza kupandisha levo ya ujenzi?"

"Jibu ni kwa kusajili wanafunzi zaidi"

"Vipi kuhusu thamani ya mchango wa dhehebu"

"Kupitia thamani za mchango unaweza kununua vifaa na vitu vingine kwa lugha nyepesi utanunua kutoka kwangu tutakuwa tunafanya biashara"

"Oh kumbe pia kuna vya kununua kwenye mfumo. Je nikwa namna gani naweza kukuza thamani?"

"Jibu ni lile sajili wanafunzi zaidi"

"Hahaha nishaelewa sasa, iwe ujenzi wa dhehebu, thamani ya mchango wa dhehebu na kufanya dhehebu liwe imara njia ni ileile tu nayo ni kusajili wanafunzi zaidi haya sasa kazi ianze" aliongea Shohei akiwa na dhamira kuu akichukulia ni kazi rahisi sana

Muda mchache mbele alikuwa amekaa nje kwenye benchi na meza ya mbao huku pembeni yake kukiwa na ubao umeandikwa USAJILI WA WANAFUNZI KATIKA DHEHEBU LA MFUPA WA VHUMA kwa lugha ya kale

"Kwa utanashati nilionao nina hakika ndani ya siku tatu nitakuwa nimeshakamilisha idadi mia ya wanafunzi" alijiambia

"Kweli?" kosei alimuuliza

"Tulia ujionee nina uzoefu na hili"




BAADA YA MWEZI MMOJA NA SIKU KADHAA


"Hakuna mtu? Kosei hivi unaweza kuamini kwa mwezi na masiku kadhaa nakosa hata mtu mmoja? Kama sio mikosi ni nini? " aliongea Shohei huku akila viazi vitamu vya kuchemsha akisukumizia na maji

"Pengine huna bahati"

"Sasa tofauti ya mikosi na kutokuwa na bahati ni ipi? Mi naona unanikejeli tu sina hata hamu ya kula" aliongea huku kinishi akila viazi vyake alikuwa amechoka kwelikweli

"Kwa mwezi na masiku nateseka kwa kula viazi na maji na kuketi kwenye mbao kwa masaa nengi nikiumiza makalio yangu halafu hakuna hata mmoja?" Shohei aliongea kwa kukata tamaa na kuinua kichwa juu kuangalia anga la jioni lililopambwa na mawingu pamoja na mwanga wa dhahabu wa jua kuzama

" Hey mkaka nataka kujiunga na dhehebu la mfupa wa chuma" ilisikika sauti nyororo ile ya kumtoa nyoka pangoni

Shohei kusikia sauti hiyo alishusha kichwa kuangalia ni nani

"Hakika ni mrembo! Mimi kama kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma ninakukaribisha kwa moyo wa dhati kabisa" haikueleweka nguvu alizipata wapi ilihali alikuwa amechoka ile mbaya

"Wewe ndio kiongozi? Basi nimeghairi kujiunga na dhehebu lako"

"Aah tafadhari usiondoke dhehebu langu lina uwezo mkubwa sana, ninaweza kuonekana kijana lakini nitaweza kuleta maendeleo katika dhehebu, kwasasa hivi ni mtu wa kawaida ila ukijiunga utakuwa mtu wa maana mbeleni, mimi nimekuwa kiongozi wa dhehebu hili kws umri mdogo kutokana na juhudi hivyo naimani utafika mahali ukijiunga na dhehebu langu" Shohei alianza kumshawishi kwa maneno ya uongo na kweli na kama dakika hivi alifanikiwa kumshawishi na akajiunga kisha binti yule mrembo akaanza kutalii eneo hilo

"Hatimae nimeweza kumshawishi na maneno hakika mimi ni mtaalamu kwenye sanaa ya kucheza na maneno(art of talking)" alijigamba

"Hongera kwa sasa dhehebu lako lina jumla ya wanachama wawili pia na thamani ya mchango ni moja"

"Unaweza kufanya biashara nami kwa kununua bidhaa katika mfumo" aliendelea kosei

"Kosei" Shohei aliita

"Naam"

"Tangu lini umekuwa tapeli? Unataka kunifilisi eeh yaani nimepata thamani moja na unataka kunipora?

" Tuliza wenge kijana hiyo thamani moja inatosha kabisa kununua bidhaa yenye manufaa nishakwambia mimi ni yule mwenye manufaa"

" Emu nionyeshe bidhaa zilizoko sokoni kwasasa" aliongea Shohei na skrini ya hologram ikajitokeza mbele yake ikiwa na bidhaa nyingi

"Asee mpaka mbinu mbali mbali za uvunaji nishati na mbinu za mapigano wow!, eti kosei kwa thamani moja ni bidhaa gani inayopatikana ikanifaa?" aliuliza maana bidhaa zilikuwa ghali kidogo

"Ngoja tuone" alijibu kosei na kumtafutia

"Naam ni hii Talisman" alimuonyesha kwenye skrini na kuendelea inaitwa Talisman ya uzoefu"

"Itaninufaisha kivipi mimi hiyo Talisman ya uzoefu?"

"Itakusaidia katika hatua za mwanzo za uvunaji nishati ukiipiga makofi kwa mikono yako miwili kwa pamoja kama unaikandamiza itakuvusha levo kadhaa bila juhudi yoyote"

"Sio mbaya nitanunua" aliingea Shohei na kufata maelekezo ya kununua na kuitumia kama alivyoambiwa kwani mara baada ya kuipiga makofi ilibadilika na kuwa moshi mweupe na kumvaa mwilini

Shohei alihisi mwili wake ukiingiwa na nguvu kama umeme hivi na baada ya hilo kuisha na moshi kupotea alijihisi wa tofauti sana mwili mwepesi kuliko mwanzo"

"Hongera Bwana Emiichi shohei kwa kufikia levo ya tano ya ufunguzi wa meridian katika kuvuna nishati"

"Asee nahisi nishati nyingi zikiingia mwilini mwangu" aliongea Shohei kwa bashasha

"Acha kufikiria mbali kijana, levo zote kumi na mbili za ufunguzi wa meridian ni sawa na introduction katika hili bara la ardhi ya nyota kwenye Uwanja wa nishati , levo halisi za uvunaji wa nishata katika ulimwengu wa Martial arts kuanzia chini kwenda juu ziko kama ifuatavyo, baada ya kufungua meridian mpaka levo ya kumi na mbili unaingia kwenye levo ya Mwanafunzi wa mapigano kisha Bwana wa mapigano kisha Bwana mkuu wa mapigano , kisha Mfalme wa mapigano kisha mfalme mkuu wa mapigano kisha mtakatifu wa mapigano kisha Mungu wa mapigano ambayo ndiyo ya juu na katika kila levo kuvuka utapitia stage tisa"




********

CHAPTER 3: kipigo kwa wanafunzi


"Vipi kuhusu hii Talisman ya ufunguzi wa muhuri?" aliuliza kwa shauku

"Hiyo ni kwaajili ya kufungua nguvu za ule upanga wa maafa"

"Damn we kweli ni tapeli, haiwezekani upanga nilioupata bure nao unahitaji kufunguliwa?"

"Ofa ina kikomo kijana pambana hakuna vya bure bure"

******

Ilikuwa ni sehemu yenye mandhari ya kuvutia na asilia zaidi, kukiwa na miti na mimea mingi hali iliyoleta ukijani mwingi

"Kijana! Unaonekana kuwa na kipaji cha asili; wewe ni gwiji wa sanaa za mapigano wa kipekee kati ya mamillion, unaonaje ukijiunga na dhehebu langu la mfupa wa chuma kisha utakuwa hauna ukomo katika uwezo.” aliongea Shohei huku akionekana amemkaja mtu usoni na kiatu chake, alikuwa akimshawishi kimabavu

"Tafadhali Sir unaweza kuondoa mguu wako kwanza?" aliongea kijana huku akijiambia mawazoni gwiji ilihali umenipiga hivi unanikejeli sio?

"Aah uniwie radhi nilikuona ukimsumbua mwanafunzi wangu hivyo nikashindwa kujizuia"

"Nilikuwa tu naongea nae..." kabla hajamaliza alinyanyuliwa juu na kusimama

"Oh kumbe ni hivyo, nisamehe sana inuka sasa!" kisha akamsogelea karibu kabisa na uso wa huyo kijana akiwa na tabasamu la kishetani kisha kumnong'oneza

"Fikiria kwa makini kuhusu kujiunga na dhehebu langu" kwa jinsi alivyonong'ona ni kama vile ilikuwa ni amri na sio ombi

"Vipi kama nitakataa kujiunga!,Tayari nishajiunga na dhehebu la maji ya chemchem" aliongea yule kijana na kumfanya shohei ashushe pumzi nyingi

"Inaonekana huna hatma ya kujiunga na dhehebu langu" aliongea shohei kisha akageuza shingo upande mwingine na kuuliza

"Yaoyao huyu jamaa si alikuwa akikusumbua?"

"Eeh ndio, alikuwa akijaribu kunishika mkono wangu" alijibu Yaoyao kwa sauti tamu na alikuwa ni mwanafunzi wa kwanza kabisa, yule binti aliyemjia, Naam jina lake aliitwa Yaoyao, alikuwa ni kachina karembo

Alikuwa ni binti mrembo kweli tena mrembo kuliko neno lenyewe, alikuwa amevalia mavazi meupe ya kikale na kitamaduni zaidi mkono akishika upanga wake uliochomekwa kwenye ala yake Shohei mara baada ya kusikia jibu lile alimgeukia yule kijana na sura kama ya fisi aliyeona kitoweo

"Umejiletea maafa yako kwa mkono wako mwenyewe" alimaka na kuanza kumshushia kipigo cha mbwa koko kwa mara nyingine

"Lakini sikufanya hivyo.....nilijaribu lakini...jaribio langu likashindwa.....lilikuwa...ni jaribio....tu" alikuwa akiongea kujitetea kijana wa watu huku akishushiwa kipigo

"Yaoyao hawezi kunidanganya namuamini, leo lazima nikushikishe adabu, nyie wahuni ndio mnaotuharibia dada zetu" ilionekana ni kana kwamba kipigo hiko alichompa ni kutolea tu hasira zake za kukataliwa kujiunga na dhehebu lake alikuwa akipooza hasira kutokana na msoto wa kuhangaika kutafuta wanafunzi wapya, aliyekuwa akishushiwa kipigo alikuwa ni kijana mdogo miaka kama kumi na sita hivi!

Aaah....aah....aaaah mkono wanguuu!! "alipiga yowe dogo wa watu."

Baada ya Shohei kuridhika na kipigo alichompa alimuacha kisha akamwambia Yaoyao waendelee na safari yao

"Yaoyao si nimefsanya vizuri eeh?" aliongea shohei na Yaoyao binti mrembo hakumjibu lolote

Huko waendako ilikuwa baada ya shohei kupewa taarifa na koseo ya kwamba kuna usajili unafanyika siku hiyo katika moja ya mji, na kama anataka kufanikisha misheni haraka ni kheri afike mapema, hivyo kukataliwa kwake na yule kijana muhuni hakuona haikumuuma sana

Wakiwa wanatembea kila mmoja akiwa kimya kwa kama nusu saa ghafla walitokea watu tano vijana kabisa wakiruka juu ya miti kama nyani na kutua mbele yao wasijulikane wametokea wapi na walionekana kuwa wanafunzi wa dhehebu fulani kutokana na sare za nguo zao

Mara akaongezeka mtu wa sita akitembea kwa tabu mno

"Kaka mkubwa huyu ndiye aliyenipiga" aliongea kijana yule wa sita akibubujikwa na machozi huku akimnyooshea kidole Shohei

Shohei na Yaoyao walikuwa katika sintofahamu kwa sekunde kadhaa kisha yaoyao akaongea kwa sauti ya kunong'ona

"Kiongozi huyu ni nani?" aliuliza

"Ni yule muhuni aliyekuwa akikusumbua nadhani, kidoho nimsahau" aliongea kwa kunong'ona pia na ilikuwa kweli kwani sura ya yule kijana ilikuwa imevimba na kutoka manundu kadhaa kwenye komwe na kungumu kumtambua

"Wewe mpuuzi unathubutu vipi kumpiga mwanafunzi wa thehebu la maji ya chemchem? Kwanza wewe ni nani? " aliongea mmoja aliyeonekana kuwaongoza

"Emiichi Shohei, kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma" alimjibu

Yule jamaa baada ys kusikia vile aliwageukia wenzie na kuuliza "Hilo si ni dhehebu ambalo kiongozi wa awali alikamatwa na serikali kwa kustarehe kwenye madanguro? Kisha kuuawa baada ya kujaribu kutoroka gerezani?"

"Naam ndio ndio kaka mkubwa nasikia pia dhehebu lilianguka na kufeli kabisa, nashangaa kusikia yeye ni kiongozi wa dhehebu hilo" mmoja kati yao alijibu

"Madanguro? (kisha kusafisha koo na kuendelea) yaani mmetuziba njia ili udhalilishe dhehebu langu?" Shohei aliongea kwa kupanic mara baada ya yaoyao kusikia "madanguro" alikuwa akihofia pengine kwa sifa hiyo mbaya anaweza kuhama dhehebu

"Kiongozi wa dhehebu la hovyo mchanga usiye na uzoefu, unapata wapi udhubutu wa kumpiga mwanafunzi wetu mpya?" alifoka mmoja kati yao na wote kujiandaa kumshikisha adabu

"Yaoyao kaa pembeni, nataka niwashikishe adabu hawa wapuuzi"

"Sawa ila kabla hujafa ukumbuke pia kunirithisha nafasi yako ya uongozi" aliongea Yaoyao aliyekuwa pembeni akiwaachia uwanja vijana hao

Shohei kusikia kauli hiyo aliishia kunying'onyea na kusikitika, alijiambia yaani ana mwanafunzi mmoja tu na ni siku hiyo hiyo amebahatika kumsajil lakini keshaanza kutamani nafasi yake?

Alimpotezea, kisha kushusha pumzi ndefu na kuchaneli meridian zilizofunguka na ghafla mwili wake ulianza kupitia mabadiliko yasiyo ya kawaida kwani katika mkono wake ilionekana miduara mitatu rangi kama ya chungwa kwenye mikono yote miwili eneo la "wrist" kama vile amevaa bangili

Wale vijana kuona vile waliishia kucheka na kumdharau,

*Yaani miduara mitatu mkononi? Hahaha upo kati levo ya tatu katika ufunguzi wa meridian, wewe ni sawa na kunguni tu usiyejua nafasi yako" kiongozi wao alimdhiklhaki

"Hahaha kiongozi yeyote wa dhehebu angalau anatakiwa awe katika levo ya mwanafunzi wa mapigano hata kama dhehebu ni la hadhi ya chini levo tisa" aliongea mwingine

"Na yeye ndio kwanza yupo kwenye levo ya tatu ya ufunguzi wa meridian! Na bado anapata uthubutu wa kutaka kupigana nasi! Hahaha ni kichekesho kilioje!" alidakia mwingine

"Sikia ewe Emiichi Shohei, kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma, ukipiga magoti na kuniomba nikuhurumie pengine naweza kukusameha na kusahau makosa yako" aliongea kiongozi wa wale vijana kibabe kisha naye akachannel nguvu zake za kufungua meridian zake na miduara kama bangili mikinoni mwake jumla ikiwa minne ilionekana, rangi ya bluu bahari na wenzake wakafuatia na wote walikuwa levo sawa

Upande wa Yaoyao pembeni alikuwa ametulia tuli akiangalia na kujiambia kwahyo wale wanafunzi wote wapo katika levo ya nne ya ufunguzi wa meridian?

"Piga magoti...." kabla hata hajamaliza kauli yake alishtukia mtu yuko mbele yake na kukung'utwa ngumo ya uso na kurushwa nyuma kidogo

"Unatania au sio? Yaani mimi nipige magoti?" wenzake yule kiongozi walikuwa katika bumbuwazi wasielewe imekuwaje mtu yule aliye dhaifu kuliko wao akawa na nguvu vile na kushambulia pasipo wao kushtuka mapema

"Inawezekana vipi mtu kama wewe aliye katika levo ya tatu ya ufunguzi kuwa na nguvu hivi?" aliuliza kiongozi wa wale vijana baada ya kunyanyuka

"Kwasababu mimi ni kiongozi wa dhehebu" Shohei alimjibu kisha kufumba na kufumbua alikuwa uso kwa uso na yule kiongozi tena na kumtandika teke la tumbo lililomrusha kwa mara nyingine tena

"Ding!" Shohei alisikia mlio kisha sauti ya kosei ikamwambia ""Umepewa misheni, unatakiwa kudili na hao wanafunzi uwashikishe adabu kwa kukudhihaki ili kutunza heshima yako kama kiongozi"

Ifahamke sauti ya Kosei inasikika kwa Shohei pekee na anawasiliana naye kwa namna mbili kwa kuongea kwa sauti na kupitia mawazo/fikra na hapo kosei alinena kupitia fikra

"Usiwaze sana hii misheni ni rahisi kwangu na nimeipenda hivyo nitaikamilisha na matokeo yakuridhisha" Shohei alimjibu kwa fikra pia

Wale wanafunzi wengine kuona vile waliamua kushambulia kwa pamoja na Shohei alipoona hivyo ghafla aliongeza nguvu na kufikia levo ya tano ya ufunguzi ambao ndio ukomo wake wa nguvu ulipofikia

"Levo ya tano ya ufunguzi?" wote walihamaki na kusita kushambulia

"Inaonekana huyu mtu alificha nguvu zake halisi" alidakia kiongozi akinyanyuka kwa mara nyingine safari hii akitokwa na damu puani

Shohei hakutaka kupoteza muda kusikiliza ngojera zao aliona wanamcheleweshea muda hivyo dakika mbili na sekunde kadhaa pekee zilitosha kuwakung'uta na kuwashikisha adabu kisawasawa na walikuwa chini hoi wakiugulia maumivu

"Sikutegemea kama utakuwa unaja kupigana" Ksei aliongea kwa fikra baada ya Shohei kumalizana na wale vijana wasio na adabu

"Unanichukuliaje kwani? Unaniona mzembe sio? Katika maisha yangu ya nyuma nilikuwa nikijifunza mbinu mbalimbali za kujilinda na kupambana japo kwa njia ngumu kutokana na kukosa walimu, naweza nisiwe mtaalamu ila kukinukisha kwa kiasi flani naweza"

"Oh hongera kwa hilo na kwa kukamilisha misheni hii ndogo umepata thamani tano za mchango wa dhehebu kama pongezi kwa kukamilisha misheni" aliongea Kosei na skrini ya mfumo au tuite system ilionekana mbele yake na kuona balance la thamani na kutabasamu kisha skrini ikapotea (Hapa pia ifahamike skrini haionekani kwa yeyote zaidi ya Shohei)

"kwaherini nyote, natumai tukutane tena siku za usoni, Yaoyao tuondoke" aliongea Shohei kisha kuongoza njia

Walipofika mbele kidogo Yaoyao alivunja ukimya na kunena "Tungewaua tu kuepuka usumbufu wa baadae"

Shohei kusikia vile kijasho kilimtoka na kumuangalia Yaoyao kwa sekunde kadhaa na kumwambia

"Kwanini tuwe wakatili hivyo?"

"Ardhi ya nyota ni kama msitu na unatakiwa ufahamu na kufata sheria za msituni hakuna kuonyesha huruma kwa adui" Yaoyao alimjibu kikauzu

"Kama umeshindwa kufahamu hilo basi huna vigezo vya kuwa kiongozi wa dhehebu" aliendelea na kumuacha Shohei katika tafakari

"Yupo sahihi huyo binti, haupo tena kwenye dunia uliyozaliwa uko katika ulimwengu mwingine sasa na huu ulimwengu unaheshimu uwezo wa kupambana pamoja na sheria za msituni huku watu hawatakiwi kuwaonyeshea huruma adui zao" Kosei aliongea fikra akionekana kumuunga mkono binti Yaoyao

"Hata hivyo licha ya kwamba ni ukweli muelimishe binti huyo kutunza heshima na utu wako, na hii ni misheni ndogo uliopatiwa" aliendelea kuongea


**********
 

Attachments

  • TekTok-20260228-004611_609x1079.png
    TekTok-20260228-004611_609x1079.png
    1 MB · Views: 6
CHAPTER 4: Mji ung'aao

"Nini? Misheni gani hii sasa yaani nimuelimishe Yaoyao? Kwa lipi la kumuelimisha? " alilalama

"Ingawa dhehebu la mfupa wa chuma ni la hadhi ndogo na wanachama mpo wawili lakini wewe ni kiongozi hivyo unatakiwa kuonyesha mamlaka ili apate kutambua nani ni boss" Kosei alimjibu kifikra na Shohei kuona kweli mwamba ana mantiki

Shohei alimuangalia Yaoyao kwa sekunde kadhaa kisha akampa mgongo na kuangalia angani kisha kusema

"Yaoyao, upo sahihi ni kweli hatutakiwi kuonyesha wema kwa adui lakini unatakiwa kufahamu hili pia. Sisi ni wanadhehebu tunaotafuta ukweli na haki, ni jambo la kudhalilisha kuonea walio dhaifu, wale ni wanafunzi wasio na tishio lolote kwangu, kuwauoa ni kuchafua mikono yangu, hadhi na sifa za Dhehebu letu" kwa pozi alilotumia alionekana ni kama mzee mwenye hekima na busara zake kwa hotuba hiyo fupi na maneno yale yalionekana kumuingia Yaoyao kwani hakuwa na usemi

"Haha! Shohei unaonekana ni mzoefu kwenye kutoa hotuba" aliongea kosei kifikra

"Nilishakwambia mimi ni mtaalamu kwenye Sanaa ya kucheza na maneno"

"Sawasawa na kwasababu hiyo umefanikiwa kupata thamani moja ya mchango wa dhehebu kwa kukamilisha misheni ndogo ya kumuelimisha"

"Sawa kiongozi, kuwaua wale kunguni ni kukuchafulia sifa na utukufu nitakusaidia" aliongea Yaoyao huku akichomoa upanga kwenye ala yake

"hey, umenielewa vibaya!" aliongea na kumfanya kosei acheke

"Inaonekana kweli wewe ni mtaalamu kwenye sanaa ya kucheza na maneno" Kosei alimtania kifikra

"Unanikejeli sio?" aliongea Shohei na kumpotezea Kosei

"Yaoyao unapaswa kuwa mstaarabu kama msichana wa kawaida sio kuwaza kuua na kupigana tu" Aliongea kirafiki bila kujua kwamba amechochea moto uliokuwa ukitaka kuzimika kwa maneno hayo

Kwani Ile anamalizia kauli yake tu anastukia kawekewa upanga shingoni

"Kwanini jinsia ya kike haturuhusiwi kufanya hivyo? Wewe ni kiongozi wa dhehebu sawa nitatii nia yako ya kutotaka kuwaua wale wajinga ila usidharau jinsia ya kike" aliongea kikauzu akimaanisha kwanini wasiruhusiwe kupigana na kuua? Vipi ikitokea wamevamia na adui? Kwamba wabaki tu kuduwaa? Hivyo ni wazi Shohei alimuudhi

Shohei alipoona usiriaz wa mwanamke huyo aliishia kujiambia inaonekana binti amepitia mengi sana yenye taabu

Muda mchache mbeleni walikuwa wakiendelea na safari yao wakitembea kuelekea mjini kupitia msitu mdogo, Shohei alionekana kuwa bize akiscroll skrini ya mfumo akiangalia bidhaa zilizoko kama silaha, mbinu za mapigano n.k

Upande ws Yaoyao alimuona kiongozi wake kama chizi fulani hivi kwa kuona akichezesha mikono yake hewani kisha kumpotezea

"Mbona vyote ni gharama, hakuna hata bidhaa yenye kugharimu point moja asee" alijiambia huku akiendelea kuscroll tu

"Ewaah, nimepata" alifurahi baada ya kupata bidhaa yenye kugharimu thamani moja na Kwa maelezo ya mfumo kilikuwa ni kidonge cha kuponyesha "Healing pill" na kimetengeneza kupitia mimea yenye nishati za mbingu na ardhi

"Aah yaani kitu cha kwanza kununua ni dawa? Hapana sinunui nitanunua nikikaribia kufa au nikiumwa" alijiambia

Wakati wakiendelea kutembea ghafla walisimama na Yaoyao alijiandaa kukumbana na hatari yoyote baada ya kuhisi uwepo wa kiumbe karibu na wao

"Natumai sio Zimwi maana kwa level niliyopo sidhani kama nitakuwa salama" alijiwazia Shohei

"Aah huu msitu unaonekana ni mchafu na hovyo kabisa tuchukue uelekeo nwingine" aliongea Shohei huku akilazimisha tabasamu , ukweli msitu ulikuwa safi tu ni vile alikuwa akitafuta kisingizuo cha kukimbia asionekane muoga

"Sio zimwi ni binaadam" aliongea Yaoyao kana kwamba alikuwa katika mawqzo yake baada ya kusogelea kichaka alichohisi uwepo wa kiumbe na ni kweli alionekana kijana akiwa amejeruhika vibaya sana akiwa amekaa chini akijiegemeza kwenye mti mpana pumzi zake zilikuwa zikielekea kukata

Shohei alimsogelea kijana yule na kuweka mkono kuangalia kama anapumua na aligundua alikuwa akitoa pumzi hafifu sana na muda wowote anakwenda kufa, akamchunguza mwili na alionekana ana mikwaruzo ya kucha zenye makali kama upanga na sumu na kujiuliza ni mnyama gani huyo wa kumjeruhi hivyo?

"Inatosha, tunapaswa kuondoka giza linaingia, tukikutana na mnyama mkali usiku usiku tutaishia kama yeye hivyo tuondoke" Aliongea Yaoyao bila huruma kiasi cha Shohei kumshangaa na kujiambia mbona ni katili hivi huyu binti?

"Kwahiyo hatumsaidii?" Shohei alimuuliza

"Unataka kumsaidia? Amejeruhika vibaya mno na kupoteza damu nyingi utamsaidiaje? Halafu sio kama wewe ni daktari"

"Ninaweza nisiwe daktari lakini..." aliongea huku akifanya ishara ya mkono hewani kama anapokea kitu na ghafla kidonge cha kijani kikatokezea hewani kimaajabu kana kwamba kilikuwa kimejificha hewani na kukidaka ilionekana ni ile "Healing pill"

"Naam umefanya uamuzi mzuri sana kununua, unakaribishwa muda wowote kufanya biashara nami" aliongea Kosea kwa njia ya fikra

"Ebu nyamanza we tapeli kwanza sikutegemea kama nitanunua mapema hivi" Shohei alimsogelea kijana yule na kumlisha kidonge kile

"Ana majeraha ya ndani pia hio dawa haita...." Yaoyao aliishia njiani baada ya kushuhudia maajabu ya kidonge kile kwani mara baada ya kijana kumezeshwa ilimchukua sekunde kadhaa kijana kupona kana kwamba hakujeruhiwa kabisa

"Inawezekanaje hii!" alishangaa binti huyo

"Ilionekana nilikuwa nakuchukulia poa sana ndugu kosei haha nadhani unastahili kuitwa yule mwenye manufaa!" alimwambia kwa njia ya fikra huku akicheka kama shetani aliyeiba kitu chenye thamani sana

"Najua unachowaz..."

"Hahahaha nakwenda kuwa tajiri hahaha!" Shohei alimkatisha na kucheka kwa sauti mpaka Yaoyao kujiuliza kiongozi wake amepatwa na ukichaa gani mpaka kucheka hivyo

"Kwenye huu ulimwengu wa Martial arts na uvunaji nishati watu wengi huumia sana, nitatumia thamani nitakazopata kununua vidonge na kuviuza kwa gharama ya juu sana na nitakuwa tajiri na nitaboresha dhehebu langu na kuwa la kuvutia ili kuvuta wanafunzi wengi zaidi hahaha! Ni fursa adimu ilioje! aliendelea kujiwazia tu kisha kufungua skrini ya mfumo na kutaka kununua vidonge vichavhe lakini alinyong'onyea baada ya kuona kwamba kidonge ununuzi wake una ukomo, kwamba ni kidonge kimoja kila mwezi

"Tatizo lako unatukana mamba ukiwa katikati ya mto" Kosei alimwambia

"Potezea hata hivyo nimefanya wema" aliongea Shohei akijifariji na kumtafuta kijana yule na kukuta hayupo na kumuuliza Yaoyao kwamba ameenda wapi

"Ameondoka bila nenio lolote" alijibiwa

"Bila hata asante? Ni punda aliyoje asiye na shukrani!" alilaani na kujutia hasara aliyoipata ya thamani kumsaidia mtu asiye na shukrani

"Kiongozi nashauri uwe mwenye roho mbaya na ngumu sana, hutopata chochote kwa usamaria wema kwenye hii ardhi ya nyota" Yaoyao alishauri

Shohei alimpotezea huyo binti na maneno yakealikuwa amepanga baada ya kumsaidia amshawishi ajiunge na dhehebu lake akitumia usamaria wake wema kama kete kuu

Alijiambia katika maisha yake ya kabla yaliambatana na mikosi mingi pengine ni kwasababu ya kuwa mwema sana, kule alikotoka(duniani) watu walikuwa wakimdhalilisha na kumpiga, hukimbia mara baada ya kupata msaada kutoka kwake

Aliendelea kujiambia kuwa alikotoka kulikuwa na sheria, lakini huku hakuna., Kule alikotoka kulikuwa na vizuizi vingi zaidi, lakini huku aliko sasa hakuna vizuizi. Na sasa kwa kuwa yuko hapo, ni muda sasa wa kufuata sheria za ulimwengu huu, sheria za msituni..!

Aliyakumbuka maneno aliyowahi kuyasikia hapo kabla yakisema hivi "Je unataka kuwa huru dhidi ya watu wanaokusumbua? Je unataka kuwa na mamlaka ya juu na mali zisizo na kikomo? Je unataka kuwa na wake na masuria wengi kadiri utakavyo? Je unataka kuabudiwa na wengine? Basi unachotakiwa kufanya ni kuwa mwenye nguvu yaani mwenye nguvu kupindukia! Kwa sababu kuwa na nguvu ni fursa ya wewe kupata unachokitaka.
Utawezaje kupata unachokitaka ikiwa wewe ni dhaifu?"

" Nakupongeza kwa kuelewa na kuchagua kufata sheria za msituni, umepata thamani kumi za mchango wa dhehebu kwa kufanikisha misheni ya siri" aliongea kosei kifikra na ilionekana kila anachowaza Shohei anajua

"Misheni ya siri?"

"Ndio misheni zako zimegawanyika katika maeneo matatu, misheni kuu, misheni za dharula na misheni za siri, sina haja ya kuelezea kuhusu misheni kuu na misheni za dharula kwakuwa unafahamu, kuhusu misheni za siri ni sawa nakusema ni kama bahati nasibu kwamba utazitimiza kwa bahati bila mimi kukutaarifu! " alieleza

"Asee kwahiyo kuna hadi kubeti" alijiamba huku akicheka kama mazuuri vile

"Ooh pia kuna misheni za hatari ila ni mpaka ukifikia levo maalumu utaanza rasmi kutimiza misheni za hatari, kuhusu tuzo(rewards) itategemea na utendaji kazi wako"

"Sio mbaya hata hivyo nimepata jumla ya thamani 15 za mchango ngoja angalau ninunu..." kabla hajamaliza alishtukia ala ya upanga ikimpiga kichwani kwenye utosi

"Ouch!"

"Tumefika kiongozi" aliongea Yaoyao, ilionekana Shohei alikuwa bize sana kiasi cha kutokutanbua kama wamefika

"Yaoyao mara nyingine usinipige usoni utaniharibia sura yangu ya kitanashati" aliongea na kuangaza macho mbele

"Wow! Kuta ni ndefu" aliongea Shohei kwa mshangao maana mbele ya macho yake zilikuwa ni kuta ndefu kama mnala na katika geti la kuingilia juu kulikuwa na ubao umeandikwa kwa lugha ya kale ikimaanisha "Mji Ung'aao"

Kama nilivyosema hapo huo ni ulimwengu wa kale hivyo majengo pia yalikuwa yakikale zaidi na kitamaduni zaidi

"Nami siku moja nitalifanya dhehebu la mfupa wa chuma kuwa kuu kuliko hata hizi kuta" aliongea kwa sauti ya kawaida lakini ilisikika na karibia kila mtu aliyekuwa getini kutaka kuingia ndani ya mji huo

"Ina maana huyu kijana ni mwanafunzi wa dhehebu la mfupa wa chuma na yupo hapa mjini?" aliongea mtu na Shohei alimsikia

"Unakosea mimi sio mwanafunzi bali ni kiongozi wa pili wa dhehebu la mfupa wa chuma" Shohei alimrekebisha

Watu walioko hapo baada ya kumsikia hivyo walianza kuangua kicheko wakimdhihaki na kumkejeli

"Wewe? Kiongozi wa dhehebu? Hahaha"

"Hivi lile dhehebu bado lipo nilidhani limekwenda na maji"

*********'

CHAPTER 5: Yeri Su


Ilionekana dhehebu la mfupa wa chuma lilikuwa na sifa mbaya kiasi cha kufahamika na watu wengi sana katika ulimwengu huo, maana kama tu watu baada ya kusikia jina la dhehebu watu walianza kukejeli, walikejeli kwelikweli

"Anapata hadi uthubutu wa kuja mjini na kutaka kusajili wanachama wapya hana aibu huyu! "

"Eti! Sitashangaa akifuata nyayo za kiongozi wake wa awali" kejeli ziliendelea kama kawaida

Upande wa Shohei kwa uvumilivu mkubwa alikuwa akiyameza maneno yao bila kuwajibu, sura yake ilionekana kusinyaa na kujiambia Asee! walimwengu wengine hawakawii kutafuta sababu za kutaka kubamizwa, maana kuna maneno mengine yalimchoma kwelikweli kama kisu

Yaoyao alimshika bega na kumwambia "wapotezee tu hao japo kuna ukweli fulani"

Shohei alidhani labda atafarijiwa aliposhikwa begani lakini aliishia kuyafuta hayo mawazo kichwani na kujiambia ni mkosi ulioje kupata mwanafunzi asiye na chembe ya huruma!

"Usijali sana kuhusu mimi, nimepitia mengi pia ya walimwengu hivyo maneno yao hayanibabaishi, ebu tuingie ndani ya mji kwa kile kilichotuleta" aliongea Shohei

Lilikuwa ni giza la saa moja usiku na baada ya wawili hao kuingia ndani ya mji huo, walikutana na majengo yaliyoundwa kitamaduni na kizamani, yalikuwa yakivutia kutokana na namna yalivyoundwa majengo hayo, na asilimia kubwa ya malighafi zilizotumika katika ujenzi ni mbao kwa wingi, miti ya bamboi na matofali kwa uchache, pia kulikuwa kuna taa nyingi zikilizokuwa zimefungwa kila kona kama kwamba kuna sherehe inafanyika, na kutokana na chanzo cha tasa hizo kuwa ni moto mji ulikuwa uking'aa mwangaza rangi ya njano, hakika ulivutia sana mji huo! na ulistahili kuitwa mji ung'aao

"Kiongozi" Yaoyao aliita

"Naam" aliitikia

"Hivi unawezaje kuacha yapite baada ya kuaibishwa na watu vile?"

"Ni uamuzi wangu kufanya hivyo isitoshe ni raia wa kawaida wenye stress zao tu" aliongea Shohei huku akijiwazia na kusema we binti huwezi kuelewa ngoja ukue wewe bado mdogo si kila kosa ni la kuadhibu mengine unapotezea tu kuokoa muda na nguvu

"eniwei tunapaswa kutafuta mahali pa kupumzika usiku huu na kula kesho asubuhi tunaanza shughuli" aliendelea kuongea Shohei

Kutokana na kuwa na pesa kiasi fulani kwenye kifungashio za urithi kutoka kwa kiongozi wa awali basi alitafuta mahali pakula na kutulia usiku huo na kufanikiwa kisha usiku nao ukaenda hadi kukakucha kukiwa ni siku nyingine tena

Katika eneo fulani ndani ya mji huo kulikuwa na meza na viti kadhaa na watu mbalimbali kuwepo wameketi huku vibao vilivyokuwa pembeni yao vikitangaza usajili wa wanafunzi wapya kwenye madhehebu yao

"Dikoni nina hakika safari hii tutavuna vijana wenye vipaji asilia" aliongea mzee mmoja akimwambia mwenzake wakionekana wameketi kwenye meza

"Nyie! sisi sote ni madhehebu hadhi levo ya nane hivyo hamtovuna peke yenu kutokana na ushindani uliopo" aliongea mzee mwingine wa dhehebu jingine

"Sisi kama dhehebu la upanga utambaao huu mwaka lazima tutapata vijana wengi wenye vipaji vikubwa"

Wazee wale walikuwa wakijibishana kama watoto wadogo kwamba siku hiyo watavuna vipaji asilia na meza zao zilikuwa zimeachana umbali kama wa mita nne hivi

Wakati wazee hao viongozi wa madhehebu wakiendelea kujibizana alionekana mwanaume mwenye nywele nyeupe akiwa amebeba mwamvuli mkubwa akisogelea eneo walilopo huku pembeni yake akiwa binti mrembo amebeba kiti na baada ya kuwafikia, sasa kwenye ule uwazi wa mita nne Shohei alichomeka mwamvuli ule mkubwa katikati kisha kuchukua kiti alichobeba binti Yaoyao na kukiweka chini ya kivuli kisha kuketi huku Yaoyao akisimama pembeni yake kwa nyuma kidogo upande wa kushoto na kuchomeka ubao wa tangazo la usajili upande wake wa kulia na kukunja nne

Wakati anafanya yote hayo wazee walikuwa wakimwagalia tu mwanaume huyo pasipo kutoa nene mpaka pale alipomaliza ndipo mmoja akaanza kuongea

"Kijana huo sio ustaarabu kufanya biashara karibu na wengine, unataka kutuibia wateja? Kwanza wewe ni nani?" aliongea mzee aitwaye Dikoni

"Ni dhehebu la mfupa wa chuma hilo, aibu ya umoja wa madhehebu mia moja kwenye ardhi ya nyota na bila shaka wapo hapa kwa uandikishaji wa wanachama wapya" alimjibu mwenzake baada ya kusoma kibao alichochomeka Shohei

"Oh kumbe ni lile dhehebu la hovyo?" aliongea mzee Dikoni kisha kumuangalia Shohei kwa macho makali na kufoka

"Unapata wapi uthubutu wa kuweka kibanda chako karibu na dhehebu letu la Ngurumo ya Simba? Hili eneo ni kwaajili ya uandikishaji wa dhehebu letu,. tafuta eneo jingine "

"Mzee huna haja ya kuwa na roho mbaya hivyo isitoshe sio kama umekodi hili eneo, uandikishaji unaanza mda si mrefu hivyo sisi kama wanachama wa umoja wa madhehebu mia tunapaswa kushirikiana"

"Kushirikiana? Kama isingekuwa kwa kiongozi wa awali kufanya udhalilishaji muda huu ningekuacha, ni kichefuchefu kwa dhehebu lako kufanya uandikishaji karibu nasi" aliongea mzee wa dhehebu la upanga utambaao

"Vyovyote vile sijali halafu mimi sio yule kiongozi hivyo siondoki mahali hapa, nipo hapa kulikuza dhehebu langu na nyinyi viwalaza hamwezi kunizuia" alimjibu Shohei na kauli yake ilitosha kwa wale wazee kukunja ndita kutokana na hasira. hata hivyo Shohei alikuwa sahihi wale wazee walikuwa na viwalaza

"Kijana usiye na adabu wewe! Kwani kuna tatizo kuwa na kiwalaza? Wanafunzi sikieni amri yangu muondoeni huyu punguani hapa mkatupie mbali nasi" mzee wa dhehebu la upanga utambaao aliwaamuru wanafunzi wake wachache aliokuja nao na walianza kumsogelea

"Sio mbaya, nitatumia hii fursa kutangaza dhehebu langu" Shohei alijiwazia kisha kuinuka, alipanga kupigana nao na kuwashinda na kwa hilo basi wanafunzi wapya wangevutiwa na dhehebu lake

Kwanza kabisa ndugu wasomaji niwaelezee kuhusu neno dhehebu kwa undani kidogo, naposema dhehebu namaanisha "Sect" kwa kiingereza. Ni mfumo wa kijamii na kiroho unaowakusanya watu wenye lengo moja kukuza nguvu zao, kulinda mafundisho yao na kupigania heshima yao katika ulimwengu wa Martial arts, chukulia mfano kama wa mashaolin temples

Katika Ardhi ya Nyota, dhehebu si tu kikundi cha watu wanaokaa pamoja, Dhehebu ni taasisi, ni familia, ni jeshi, ni shule, ni himaya ndogo ndani ya himaya kubwa.

Na kila dhehebu lina mafundisho yake, mafundisho ya siri ya uvunaji nishati, mbinu za kuimarisha mwili, mbinu za silaha, na hata mbinu za kiroho. Mafundisho haya ndiyo yanayomtofautisha mwanachama wa dhehebu moja na jingine. Pia Madini adimu, dawa za kuongeza nguvu, vitabu vya siri, silaha za kipekee. Bila rasilimali kama hizi, hata dhehebu lenye jina kubwa linakuwa halina maana

Na kiongozi ndiye mhimili wa dhehebu. Nguvu yake na utaalamu wake huamua hadhi ya dhehebu. Akiwa dhaifu, dhehebu hudharauliwa. Akiwa mwamba, dhehebu hutetemesha ulimwengu.

Mbali na kiongozi kuna ngazi zingine kama vile wazee wa dhehebu, wanajihusisha zaidi katika kutoa ushauri kwa kiongozi na kulinda dhehebu wakati wa maafa makubwa, na wanafunzi ndio damu mpya. hujiunga kwa matumaini ya kupata nguvu, umaarufu, ulinzi, au hata utajiri n.k nadhani naeleweka ndugu wasomaji

Si madhehebu yote yana heshima. Kuna madhehebu ya hadhi ya juu, ya kifalme, yenye historia ya mamia ya miaka. Kuna yza hadhi ya kati yanayopambana kupanda ngazi na kutambulika ulimwenguni, Na kuna za hadhi ya chini yanayodharauliwa, na wakati mwingine kusahaulika na dhehebu la Mfupa wa Chuma lilikuwa kwenye kundi la mwisho.

Sasa katika Ardhi ya nyota kila mwaka kunakuwa na uandikishaji wa wanafunzi wapya. Vipaji vipya ni kama mbegu. Ukipanda vizuri, baada ya miaka kadhaa unavuna mashujaa watakaoilinda bendera yako na Shohei ndicho alichokuwa akifanya yaani kulikuza dhehebu lake kwa kusajili wanafunzi wenye vipaji kwa kuvizia pembeni ya uandikishaji wa madhehebu mengine yenye sifa, japo aliona ni mbinu ya kijinga hakujali wala nini alijiambia potelea pote maana siku zote kwenye vita kitu chenye maana ni ushindi bila kujali umetumia mbinu au hila gani

"Yeri Su kutoka Familia ya Su amewasili!" ilisikika sauti ikinena wakati ambao Shohei na wanafunzi wa dhehebu la upanga utambaao kutaka kulianzisha

"Yeri Su? amewasili? Mpotezeeni huyo punguani twendeni kule" aliongea mzee ghafla kuwafanya wanafunzi wake kusitisha dhamira yao

"Tunapaswa kumvutia upande wetu kabla hajawahiwa kuhusu huyo punguani tutadili nae baadae"

Aliongea yule mzee huku akibeba fomu za uandikishaji akikimbilia eneo la upande mwingine ambako jina la Yeri Su lilisikika, wazee wa madhehebu mengine pia walikimbilia eneo lile na kumuacha Shohei akisimama huku sura yake ikibadilika na kuwa kama ya mbuzi

"Eti kosei Yeri Su ndio nani?" Shohei alimuuliza mwenzake kwa njia ya fikra

"Kutokana na taarifa nilizonazo kwenye hii Ardhi ya nyota, Yeri Su ni uzao wa familia ya Su kwenye huu mji ung'aao na ni familia yenye hadhi kubwa mjini, inasemekana kwamba mwamba akiwa na miaka kumi na moja pekee alibahatika kuamsha nguvu za kiroho za hali ya juu"

"Nguvu za kiroho za hali ya juu? Unamaanisha nini"

"Katika Ardhi ya nyota kasi ya uvunaji nishati hutegemea na nguvu za kiroho za mtu pia"

"Oh kumbe, endelea kunijuza ni nguvu kiasi gani za kiroho anazo"

"Kama ilivyo kwa uvunaji nishati za mbingu na ardhi kuwa na levo vilevile nguvu za kiroho zina levo zake, levo ya kwanza ni kivuli ambapo mtu anakuwa hajaamsha bado nguvu, levo ya pili inaitwa "mwanzo" bapo katika levo hii mtu ndio anaanza harakati za kuamsha nguvu zake kisha levo ya tatu huitwa mwangaza hafifu ambapo katika levo hii nguvu za kiroho zinakuwa zimeamka sawa kipimo cha theluthi

Levo ya nne huitwa mwangaza mkuu ambapo katika hatua hii nguvu zinaamka kwa kipimo sawa na robo na katika levo hii mtu anahesabika kuwa mwenye kipaji cha hali ya juu miongoni mwa wenye vipaji, levo ya tano huitwa utakatifu au umalaika na katika levo hii nguvu zinaamka kipimo cha nusu na kwenye levo hii mtu huanza kufanya maajabu bila kuvuna nishati za mbingu na ardhi, anakuwa na ulinzi mkali sana wa kiroho, hii levo ni sawa na manabii wanaosemekana kuwahi kuwepo hapo zamani za kale kwenye ulimwengu wako ulikotoka sijui kuita moto mbinguni sijui kutenganisha bahari nadhani kitu kama hicho

Halafu levo ya mwisho kabisa huitwa Uungu na hii levo nguvu za kiroho za mtu zinaamka katika ukamilifu wake na nguvu za kiroho zinakuwa hazina kikomo, ni kama nishati za kiroho zote ulimwenguni na yeye ni kitu kimoja"

**********
 
  • Thanks
Reactions: Sax
Hii ni account mbadala ya jf baada ya kupotea acces, hata kule fasihinet nilipoteza access pia na ni juzi hapa ndio nimepata access
 
Screenshot_20260304-190539.png


Karibuni fasihinet kusoma free kabisa sababu Jf ya sasa ni tofauti na mwanza tangu ilipofungiwa kisha kufunguliwa baada ya miezi 3 imekuwa ikisumbua kupost maana kuna nyakati website haifunguki

Vipande kuanzia 6 hadi kumi👇

Screenshot_20260304-190003.png


Once again mniwie radhi waungwana, binadamu kuna nyakati tunafeli. Na huku pia nitakuwa napost kwa wale wasio na access na fasihinet japo itakuwa tabu kidogo kutokana na website kuzingua
 
CHAPTER 6: Historia tukufu

"Ni levo ipi huyu Yeri Su amefanikiwa kufikia?" Shohei aliuliza


"Ni katika levo ya mwangaza mkuu, ni mwenye talanta kwelikweli, kwenye ulimwengu wako wazungu wanaita "Heaven defying talent" siku za mbeleni akiweka juhudi katika mafunzo ni suala la muda mfupi kupanda levo za juu"


"Oh kumbe huyu Yeri Su ni hazina!" aliongea Shohei


"Kwenye mji huu mdogo Yeri Su ni zaidi ya hazina na watu kama hawa hugombaniwa sana na madhehebu" Kosei alikazia


"Inasikitisha sana mimi kama kiongozi wa dhehebu kutokuwa na nguvu za kiroho"


"Acha kujifananisha na watu, vipi huna mpango wa kumvuta ajiunge na dhehebu lako?"


"Huyu ni "one-in-a-century talent" siwezi acha fursa inipite kirahisi hivi lazima nimlaghai ajiunge nasi" aliongea Shohei akitoa tabasamu lisilokuwa tabasamu


"Yeri Su, ungana na dhehebu letu la mwewe wa dhahabu, ukijiunga utafanikiwa katika mengi kwenye sanaa mbalimbali za mapigano na uvunaji nishati" aliongea kiongozi mmoja wa dhehebu


"Hilo tu? Yeri Su! achana na huyo umgana nasi na tutakupatia cheo katika baraza la wazee" aliongea mwingine mwanaume wa makamo mwenye upara


"Yeri Su! Ukiungana na dhehebu la nyangumi nitahakikisha tunakupatia mbinu zote za mafunzo hata zile za siri" aliongea mwingine


"Yeri Su! Vipi kuhusu dhehebu langu? Ukijiunga wanafunzi wote wakubwa kwa wadogo watakuwa chini ya amri yako"


Viongozi wa madhehebu walikuwa wakijitahidi kuweka ofa kubwa kubwa ili kumvutia upande wao, Yeri Su hivi, Yeri Su vile ilimradi ni ofa kubwa kubwa lakini Kijana huyo aitwaye Yeri Su aliishia kuwapa tabasamu tu bila kuwajibu, alikuwa ni mvulana wa miaka kumi na saba, kijana mtanashati kwelikweli kuliko hata Shohei, tena kumfananisha na mtu kama Shohei ni kumdhalilisha kabisa


Shohei alikuwa amesimama tu mahali pale akiangalia upande wa Yeri Su ambaye alikuwa akija upande wake


"Yaoyao hivi kuna mahali nimemuona huyu kijana?" Shohei alimuuliza mwanafunzi wake wa kike baada ya kuhisi kama amekutana naye mahali


"Ni yule tuliyemuokoa kule maporini na kuondoka bila hata shukrani" Yaoyao alimjibu


"Ni kweli ni yeye" Shohei alikubaliana naye


Wakati Yeri Su akimkaribia Shohei alikuja mzee mmoja mbele yake, mwenye makadirio ya umri wa miaka sitini ya mwanzoni, alikuwa amevalia joho kubwa la kale sana rangi ya kijani kibichi, haikueleweka hata joho alilovaa ni la tamaduni gani lakini lilitosha kumpa hadhi ya mtu mzito mwenye mamlaka fulani hivi


"Yeri Su, vipi unavutiwa kuungana na dhehebu la mlima mrefu?" aliuliza mzee yule


"Mlima mrefu! Dhehebu la mlima mrefu! Nimesikia vibaya au?" mmoja wa watu aliongea


"Umesikia vyema ni moja la dhehebu yenye hadhi levo ya tano!"


"Asee tushamkosa mwamba" watu waliendelea kunong'ona tu


Shohei baada ya kusikia mzee ni kutoka dhehebu la hadhi ya levo tano aliishia kunyong'onyea na kujiambia huu ni mkosi mwingine, mwanzoni alipanga kumshawishi baada ya kuona wengine hawawezi kumshawishi ila ujio wa mzee huyo umekuwa sumu kwenye kukamilisha mpango wake, palepale aliishia kukaa kwenye kiti chake kivivu


"Ni mwenye kipaji sana hivyo ni jambo zuri kwake kuungana na dhehebu la levo hiyo" aliongea Yaoyao kwa sauti ya chini na kuzidi kumvunja moyo Shohei kwa maneno yake


Shohei alijiambia huyu binti hajui maana ya hasara, kumkosa Yeri Su kwake ilikuwa ni hasara kubwa tena alikumbuka kidonge chake alichomsaidia na kuishia kuumia ndani kwa ndani


Upande wa Yeri Su wala hakumjibu yule mzee zaidi ya kutabasamu na kumpita na kwenda kusimama mbele ya Shohei aliyekaa kwenye kiti chake kivivu


"Samahani, je wewe ni kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma?" aliuliza Yeri Su


"Naam ndimi! Mimi ndiye kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma, naitwa Emiichi Shohei" alimjibu na kukaa vizuri kama vile boss akikunja nne


"Inakuwaje Yeri Su akamfuata kiongozi wa lile dhehebu la kishenzi?" aliuliza mmoja na kuibua minong'ono mingine lakini Yeri Su na Shohei wala hawakuwajali


Yeri Su palepale aliinamsha kichwa chini kuinama akiashiria kuomba radhi


"Dikoni ninaota au? Yaani genius ndani ya mji huu anamuinamia yule mpumbavu na kuomba msamaha?" aliongea mzee mmoja


"Nilikuwa nina haraka sana ya kurudi nyumbani hivyo sikupata nafasi ya kutoa shukrani, nisamehe kwa kutokuwa na adabu" aliongea Yeri Su


"Oh Yeri Su usiseme hivyo nilifanya kile ambacho binadamu anapaswa kufanya nilikuwa nimeshasahau mpaka ulipokumbushia sasa" aliongea Shohei huku akinyanyuka kwenye kiti na kumuinua Yeri Su asiendelee kuinama


Upande wa Yaoyao aliishia kujiambia huyu kiongozi wake kweli anajua kuigiza nadhani hata Kosei aliwaza vivyo hivyo


"Asante kwa msaada wako, je unaweza kunielezea kuhusu dhehebu lako? " alishukuru kisha akauliza


Ding! Ulisikika mlio akilini mwake ambao aliufahamu vyema na palepale sauti ya kosei ilisikika kwenye fikra zake


"Umepatiwa misheni ya dharula! Unapaswa kumuelezea Yeri Su historia tukufu ya dhehebu la mfupa wa chuma"


"Seriously? Historia naijulia wapi wakati nimefika huku ulimwenguni jana tu, usiniambie unataka nimwambie historia ya kiongozi wa awali kulala kwenye madanguro au unaijua historia tukufu? Nielezee nimwambie"


"Siijui mie hiyo historia tukufu, mimi nishafikisha yangu ni juu yako kuikamilisha misheni si ulisema wewe ni mtaalamu wa kuongea? Tumia maneno yako ya utaalamu "


"Damn! Hivi yule kiumbe kwanini nilimkubalia kichwa kichwa masharti ya kikuda hivi? " Shohei alianza kujutia kwa kiasi fulani


"Kijana Yeri Su! Dhehebu la mfupa wa chuma haina historia yoyote tukufu" walipayuka wale wazee watatu wenye viwalaza mmoja wa dhehebu la upanga utambaao na wawili kutoka Dhehebu la ngurumo ya Simba


"Mchango mkubwa zaidi wa Dhehebu la Mfupa wa Chuma ni kwamba kiongozi wa awali wa dhehebu hilo alisaidia kukomesha bidhaa na machapisho ya kingono tu, hakuna lingine la maana" aliendelea mmoja wao


"Kweli kabisa kujiunga na hilo dhehebu ni kujidhalilisha wewe mwenyewe na kipaji chako, dhehebu hilo ni takataka" wenzake walikazia


"Mmemaliza kuongea?" aliwauliza Shohei huku akiwaangalia macho makali yenye kuashiria kutaka kuwadunda kisha kuwapotezea


"Usisikilize hao wazee sababu hakuna wajualo kuhusu dhehebu ambalo si lao, ukweli ni kwamba dhehebu langu lina historia ndefu tukufu"


"Elezea kwa undani zaidi" Yeri Su aliomba maelezo


"Ushawahi kusikia bahari ya kaskazini?" Shohei alimuuliza


"Ndiyo kaskazini mwa Ardhi ya nyota kuna bahari kikubwa isiyojulikana mwisho wake" alijibu Yeri Su na kumfanya Shohei atabasamu, ukweli aliuliza vile kujua kama kuna bahari kaskazini mwa Ardhi ya nyota ili atunge uongo wake


"Sasa basi mwisho wa bahari hiyo kuna nchi iitwayo Adlai, kuna milima miwili mitakatifu, mmoja una mioto ya asili kama mimea ya matunda n.k na mwingine ni mlima wa mifupa ya chuma" alinyamanza kusafisha koo kisha kuendelea


"Dhehebu la mfupawa chuma asili yake ni ule mlima wa mifupa ya chuma, muanzilishi wa dhehebu hili aliitwa Kosei Hemei na alikuwa ni kiumbe mwenye mifupa ya chuma aishiye katika mlima ule"


"Kijana, usiniingize kwenye uongo wako tafadhali" aliongea Kosei kifikra


"Tulia, we si umekataa kunipa historia tukufu? Angalia namna navyokwenda kuikamilisha hii misheni kwa kutulia" alimjibu kifikra


"Huyu jamaa anaongea pumba gani?" aliongea kiongozi mmoja wa dhehebu fulani


"Kijana nakushauri usimsikilize huyu mtu, ni wazi anaongea pumba" hatimae yule mzee mwenye Joho rangi ya kijani aliongea


"Bahari ya kaskazini inaonekana kuwa ya hatari mno hata wavuna nishati wenye uwezo wa juu hawathubutu kabisa kuingia, pia hakuna rekodi zozote zinazoonyesha kwamba kuna nchii iitwayo Adlai mwisho wa bahari hiyo achilia mbali mlima wa mifupa ya chuma" aliendelea yule mzee


"Mzee inaonekana hujui lolote kuhusu Bara la Ardhi ya nyota"


*Sijui lolote? Haya niambie ni nani huyo Kosei Hemei unayemuongelea na ni nani master wake?"alimuuliza


"Mwanzilishi wa kwanza wa dhehebu la mfupa wa chuma alipata nguvu zake kupitia asili, asili ilimchagua na kumpa nguvu alikuwa na mwili wa chuma kigumu sana na master wake aliitwa Martin kitinde aliyemuongoza" alimjibu huku jina Martin kitinde likiwa ni jina lake halisi la ulimwengu alikotoka yaani duniani


"Ujinga! Ni ujinga mtupu unaongea, binadamu asili ya miili yao ni damu na nyama iweje huyo Kosei awe na mwili wa chuma?" Yule mzee aliuliza swali jingine


"Mzee inaonekana pia hujui kuhusu mageuzi ya viumbe na sina mpango wa kukuelezea jilo ni kupoteza muda na sauti" aliongea huku akijiambia ukijua sana vitu vingi kuna faida yake kwenye kudanganya watu


"Unadhani mimi ni mjinga kiasi hicho? Kijana huna adabu kwa wazee, unathubutu kutudanganya? Hakuna mtu ataamini upuuzi wako"


"Sikujua kama dhehebu la mfupa wa chuma lina historia ndefu hivyo, ni historia tukufu iliyoje!" aliongea Yeri Su na kumfanya mzee na wazee wengine kuchoka kabisa, inamaana anakubali kudanganyika kirahisi hivyo?


"Lakini unachoongelea ni kimebaki historia, kuna uspesho gani kwenye dhehebu lako? Nini faida zake nikijiunga?" aliuliza Yeri Su


"Oh ninachojua mimini kwamba hakuna kidumucho milele, haijalishi dhehebu lina nguvu kubwa kiasi gani ipo siku litaanguka, na ndio kilichotokea kwenye dhehebu langu, limeanguka na kuwa hivi lilivyo sasa


Hata hivyo dhehebu langu lina historia ya kale yenye heshima, ingawa siku za utukufu wake zimekwisha ila bado dhehebu lina msingi imara nadhani kidonge nilichokumezesha ni ushahidi tosha" alimjibu kwa kirefu


Yeri Su alitafakari na kujiambia kidonge chenye uwezo wa kumponyesha mtu majeraha ndani ya sekunde kadhaa ni hazina adimu sana na bado akaamua kukitoa kuokoa maisha yangu, pengine anachoongea ni kweli


"Ninakwenda kulikuza dhehebu langu na kulipaisha viwango vya juu hivyo nahitaji vipaji kama wewe kwenye kunisaidi kstika hili" aliongea kisha kukohoa kidogo na kuendelea


"Ni ngumu kwangu kukupatia vile walivyoku-ofa ila kama utataka kufikia levo ya mtawala katika uvunaji nishati kujiunga na dhehebu langu ni chaguo sahihi"


"Levo ya utawala? Unapata wapi uthubutu wa kujigamba hivyo? " Mzee Dikoni alifoka huku mate yakiruka kutoka mdomoni kana kwamba amesikia tusi kubwa



**********
 
CHAPTER 7: Staili tisa


Levo ya utawala yaani mtawala wa mapigano katika Ardhi ya nyota ni levo ya juu sana, na wavuna nishati waliofika katika levo hiyo wanachukuliwa kama miungu wanaosujudiwa na wengi


Sasa Shohei kutamka kirahisi tu kwamba anaweza kumfikisha kijana Yeri Su katika levo hiyo ilikuwa ni kama tusi masikioni mwao, yaani kwa dhehebu lenye hadhi ya chini kabisa ambalo kiongozi wake yuko katika hatua ya ufunguzi wa meridian, anathubutu kujigamba hivyo? Kwao walimuona ni chizi mmoja hivi kuwahi kutokea katika ulimwengu huo


"Sawa, nitajiunga na dhehebu lako la mfupa wa chuma" aliongea Yeri Su huku akitabasamu, uso wake uking'aa kama mwangaza wa jua!


Yule mzee na wengine walioko eneo hilo kidogo watapike damu baada ya kusikia kauli ya Yeri Su ila wangefanyaje sasa? Isitoshe mwanafunzi kujiunga dhehebu lolote ni kwa hiari yake mwenyewe hivyo wasingelazimisha


Shohei alifurahi kusikia hivyo na kujiambia Ewaah umefanya uamuzi mzuri, hakika hutojutia uamuzi wako!


Na palepale alinyoosha mkono kuelekea kwa Yaoyao kama anaomba kitu na binti huyo alielewa kwani ni yeye ndiye aliyebeba fomu za usajili na mengine muhimu hivyo alimpatia fomu moja na Shohei alimpatia Yeri Su fomu hiyo na kumtaka ajaze


Bila hiyana kijana huyo alisogea kwenye meza ya karibu kisha kupewa kalamu ya unyoya wa mwewe kisha kujaza na kusaini fomu hiyo kwa alama ya kidole kwa kuweka kidole gumba kwenye wino kisha kukandamiza sehemu ya sahini na usajili kukamilika


"Kijana niseme tu wewe ni mtu wa aina yake! Nakupongeza kwa kufanikisha misheni ya dharula na umepata mchango wa thamani tano, jumla ya wanachama ni tatu na balansi la thamani ni 20" aliongea kosei kifikra


"Una mustakabali mzuri sana kwa sababu ya nguvu yako ya kiroho iliyo bora, lakini unaharibu hatima yako kwa kujiunga na dhehebu hilo la takataka?" aliongea yule mzee mwenye joho la kijani akimwambia Yeri Su, alionekana kutoridhika na uamuzi wa kijana huyo


"Ingawa kwa sasa dhehebu langu halina maana ila hiyo hali haitadumu kwa muda mrefu, Yeri Su! Una neno langu, ndani ya miaka mitatu tutalipiku dhehebu la mlima mrefu achana na huyo mzee" aliongea Shohei akimuhakikishia hilo kwa sura ya usiriaz


"Unaongea ujinga gani? Kulipiku dhehebu langu la mlima mrefu?" aliongea yule mzee huku akibadilika na kusambaza msisimko fulani wa kuogopesha


"Hivi unadhani unaweza kutumia maneno tu kuontesha dhehebu lako lina nguvu?" aliendelea kuongea huku taratibu hali ya hewa ikianza kubadilika kutokana na msisimko aliokuwa akitoa na ghafla kiganja cha mkono wake wa kulia ukaanza kutoa mvuke mwekundu, ilionekana wazi kwamba amedhamiria kumshikisha adabu kijana huyo anaejaribu kumdhalilisha


"Nadhani inabidi nikuonyeshe ni ukubwa kiasi gani uliopo kati yangu mimi na wewe pamoja na dhehebu lako" aliongea mzee yule na kufanya watu walioko hapo kupanic kwa kile kinachokwenda kutokea





Hakuna yeyote aliyekuwa na uthubutu wa kuingilia kabisa ukizingatia madhehebu yote yalikuwa ni ya hadhi ya chni levo ya tisa na nane, sasa ni nani atakayethubutu kuingilia suala hilo ambalo kiongozi wa dhehebu la hadhi ya tano ameliamulia?


"Tafadhali usithubutu kufanya unachodhamiria kufanya dhidi ya kiongozi wetu" aliongea Yeri Su kama mwanafunzi rasmi akitambua Shohei kuwa kiongozi wake, akiwa na uso usio na utani hata kidogo


Yule mzee baada ya kusikia kauli ile kutoka kwa kijana huyo alimwangalia kwa sekunde kadhaa na kufikiria kwa sekunde kisha kusitisha kile alichokuwa akitaka kufanya, haikueleweka ni kutokana na Yeri Su kutoka katika familia yenye hadhi kubwa mjini ama kuna kingine


"Sawa, nitakaa pembeni na kushuhudia mtakavyolikuza dhehebu lenu" aliongea mzee yule kisha kugeuka na kupiga hatua kuondoka hapo


"Mzee Shuma tafadhali subiri kidogo usiondoke" ilisikika sauti na kumfanya mzee huyo kugeuka na kuangalia sauti iliko toka


Alikuwa ni mwanaume wa makamo mwenye nywele ndefu na mustachi, alikuwa amevalia Joho kubwa rangi ya dhahabu lenye michoro ya rangi nyeupe, alikuwa akitoa ile hadhi ya heshima na utajiri kutokana na alivyovaa


"Ni mzee Su! Baba mzazi wa Yeri Su!" alisikika mmoja wao akinong'ona


"Mzee Shuma, mwanangu bado ni mchanga asiye na uzoefu, mimi kama baba yake nitakubali mualiko wako wa kujiunga na dhehebu lako kwa niaba yake" aliongea mzee Su baada ya kumkaribia mzee Shuma mwenye Joho la kijani


"Baba! Tayari nimeshajiunga na dhehebu la mfupa wa chuma!" aliongea Yeri Su kwa sauti


"Nyamanza!" alimkaripia


"Hili suala litaathiri maisha yako ya baadae na familia yetu kwa ujumla, si juu yako kuamua" aliendelea kufoka


"Baba si ni wewe uliyenifunza kuwa muwazi na mkweli? Sasa kwakuwa nimeshajiunga na dhehebu la mfupa wa chuma, sijiondoi!" alimjibu baba yake


"Yeri Raka Su! Mtoto usiye na adabu, unathubutu vipi kwenda kinyume na baba yako kwa dhehebu duni lisilo na maana? Kama hutojiondoa sasahivi wewe sio mwanangu tena na usirudi nyumbani!" alifoka kwelikweli mzee wa watu kiasi cha kuanza kukohoa mfululizo, ilionekana afya yake haikuwa nzuri


Pembeni ya mzee Raka Su alikuwa kijakazi wa familia yao, na kijakazi huyo wa kiume alimsaidia Bwana wake kusugua mgongo kumtuliza


"Bwana mdogo tafadhali msikilize baba yako, usimkasirishe afya yake si nzuri, tafadhali jiondoe" kijakazi yule alimsihi


"Utiifu kwa wazazi ndio msingi wa maadili yote; huku ni kukosa utiifu kumpinga baba yako" alikazia mzee Shuma na kumfanya Yeri Su ajihisi hatia


"Mzee Raka Su, dhehebu langu sio batili kama unavyodhani, na kwakuwa ameshajiunga nakuahidi mwanao atafika mahali" aliongea Shohei akimshika bega Yeri Su


Mzee Raka Su, baada ya kusikia vile alimwangalia Shohei na kujiwazia eti atafika mahali? Wewe mpuuzi usiye na thamani yeyote bila shaka mwanangu amejiunga na dhehebu lako kutokana na maneno yako ya ulaghai


"Wewe ndiye kiongozi wa dhehebu bwana Emiichi Shohei?" aliuliza mzee Raka Su


"Naam ndimi" Shohei alimjibu kwa kujiamini


"Inaonekana bado ni kijana mdogo sana na kwa muonekano wako sidhani kama umemzidi mwanangu zaidi ya miaka mitano lakini hata hivyo umri sio tstizo


Kiongozi shohei, ili kuweza kuwafunda wanafunzi wako na kuwa imara inatakiwa uwe na ueleww mkubwa kuhusu sanaa za mapigano na mbinu za uvunaji nishati.
Kwakuwa unajiamini sana utakuwa na uelewa mkubwa si ndio?" Mzee Raka Su aliuliza


"Sitaka kuonekana najigamba sana ili tukija kwenye suala la uelewa wa sanaa za mapigano na uvunaji nishati nina uelewa kuwazidi wote hata mkiungana" aliongea Shohei


Upande wa Yaoyao aliishia kujiambia huyu kiongozi wake awamu hii amevuka mipaka kwenye kujigamba na kuona ngoja aendelee kutazama kuona atafikia wapi


"Ooh kweli? Kama ni hivyo unaonaje ukanitoa tongotongo?
Kwenye himaya ya huu mji ung'aao kuna mbinu ya sanaa ya upanga iliyorithishwa kiazi hadi kizazi kwa miaka zaidi ya miaka mia, inaitwa Staili tisa za upanga wa ghadhabu


Zipo staili tisa ila nane tu ndizo zilizofanikiwa kurithiwa na wataalam wa masuala ya mapigano, kwa zaiddi ya miaka mia moja maelfu ya wataalamu walihangaika ku-master style ya tisa bila mafanikio" aliongea huku akichomoa kitabu kidogo kwenye mfuko wa Joho lake chenye maelezo ya hiyo mbinu


"Ukiweza kuzimaster hata staili tano tu nitakuamini na kukuachia mwanangu ila ukifeli itakupasa umuondoe" aliendelea


Shohei kusikia vile alijiambia huyu mzee anajaribu kumuaibisha na kutaka kumuonyesha mwanae kwamba dhehebu lake ni dhaifu hivyo aliishia kutoa tabasamu fulani hivu na kukubali


"Sawa haina shida" aliongea Shohei kisha palepale skrini ya hologram ilijitokeza mbele ya macho yake bila yeyote kuona zaidi ya yeye peke yake na kuanza kuscroll huku na kule


Shohei jana yake usiku alikuwa akipitia duka lililopo kwenye mfumo huo na kuangalia mbinu kadhaa na kusoma maelezo na kupata uelewa na mojawapo ya mbinu aliyobahatika kuiona iliitwa Talisman ya maono na muda muda huo alikuwa akifanya muamala kuinunua, na ilimgharimu thamani kumi za mchango wa dhehebu


Ni talisman iliyomuwezesha mtumiaji kuweza kupata maono na uelewa wa mbinu za sanaa na uvunaji nishati pamoja na kuisoma miondoko ya adui kwa muda wa dakika sitini yaani lisaa limoja


Na mara baada ya kununua tu karatasi fulani ilijitokeza hewani ambayo yeye pekee aliiona kisha kuipiga makofi kwa mikono yake miwili kwa pamoja na ulitokea moshi ambao ulimuingia machoni na kufanya mboni za macho yake kubadili rangi kadhaa kisha kurudi katika hali yake ya kawaida


Baada ya kitendo hiko alichukua kitabu chenye maelezo ya mbinu hiyo ya staili tisa za upanga wa ghadhabu na kupitia haraka haraka, zilikuwa ni kurasa chache tu hivyo ilimchukua dakika moja tu kupitia zote kwa umakini kisha kumrudishia kitabu mzee yule


"Yaoyao tafadhali niazime upanga wako kwa dakika kadhaa" aliongea Shohei na Yaoyao bila hiyana alichomoa upanga kwenye ala yake na kumkabidhi na watu kusogea mbali naye kumpa nafasi kubwa


Palepale alinyoosha upanga juu hewani na kufyeka kurudi chini kama vile anakata keki huku akichannel meridian zilizofunguka kisha kuingiza nishati za mbingu na ardhi kwenye upanga ule na kufanya upanga ule kutoa mlio wa kishindo kama bomu kulipika


Sababu ya mlio ule ni baada ya nguvu ya nishati ya upanga ule kama vile upepo mkali wenye nguvu kutoka na kupigiza ardhini


"Inawezekanaje hii! Yaani ameweza kuimaster staili ya kwanza? Na imemchukua sekunde kadhaa tu?" aliongea mzee Shamu mwenye uelewa wa hiyo mbinu, kwa kutoamini


"Imenichukua siku tano kuweza kuimaster staili ya kwanza lakini imemchukua muda mfupi hivi?" hata mzee Raka Su naye alikuwa akishangaa


Shohei hakujali mshangao wa wale wazee na kwa ustadi wa hali ya juu na miondoko ya ajabu kama vile anacheza mziki aliweza kumaster staili nane zote kwa dakika moja na sekunde kadhaa pekee hali iliyowaacha midomo wazi wazee hao na wale wa madhehebu mengine


"Pengine aliwahi kujifunza mbinu hiyo hapo kabla vinginevyo ni vigumu kuamini imemchukua dakika moja kuzimaster staili nane" aliongea mzee Raka Su akijifariji huku akikumbuka kwamba ilimchukua miezi sita kufikia kuimaster staili ya nane


Baada ya staili zile nane Shohei alisimama kwa kutulia akinyoosha upanga ncha ikielekea ardhini huku mkono wingine akiuweka nyuma akiyafumba macho yake na kutulia tuli, kwa jinsi alivyopozi alionekana ni kama master fulani mwenye uzoefu


"Kiongozi Shohei, je ulijifunza hapo kabla a mbinu hii?" aliuliza mzee Shamu lakini hakujibiwa


Ghafla upanga ule ulianza kutoa mng'ao fulani, haukuwa mkali wala haukuwa hafifu lakini wenye kuonekana vyema


Mzee yule baada ya kuona tukio hilo alipatwa na mshangao na kujiambia kutokana na msisimko anaotoa Shohei na kwa jinsi upanga unavyong'aa aliweza kugundua bila shaka hiyo ni staili ya tisa ya upanga wa ghadhabu kulingana na maelezo ya kitabu cha mbinu hiyo





**********
 
CHAPTER 8: Naomba muongozo


"Hii si ni staili ya tisa?" alinong'ona mzee mmoja


"Naam hujakosea, ndiyo yenyewe hiyo kwa mujibu wa maelezo ya kitabu chake" alijibiwa na mwingine


"kwa miaka zaidi ya mia hakuna mtu aliyeweza kuimaster staili ya tisa ila huyu kijana nadhani tulimchukulia poa"


Watu walianza kunong'ona tena kama kawaida yao huku upande wa Yeri Su na Yaoyao wakimuangalia kiongozi wao kwa namna ya kumkubali kwa uwezo wake huku wakijiambia wamefanya uamuzi sahihi kujiunga na dhehebu lake


"Kaeni kimya! Yupo katika hali ya kupokea ufunuo, ni fursa adimu sana hii hivyo kimya tafadhalini" aliongea mzee Shuma kwa sauti kubwa na ghafla kukawa kimya


Baada ya kama dakika mbili kupita alifungua macho yake akionekana kupata ufunuo tayari, uso wake ulikuwa ni wenye umakini mno!


Alimwangalia mzee Shuma na kumwambia
"Inaonekana una uzoefu pia ni mwenye nguvu, hivyo nitaomba unisaidie katika kufanya majaribio ya ufunuo nilioupata kwasababu nahisi ni wewe pekee hapa ndiye mwenye kuweza kufanya hivyo" aliongea huku akimnyooshea upanga na bila kusubiri jibu alifyeka upanga hewani kama anachora alama X mara saba huku akinena


"Ghadhabu takatifu, mikato saba!" alipayuka na mawimbi saba ya upepo yenye ukali ukatao yalielekea upande alipo mzee yule Shuma


Mzee yule alionekana kutokushtuka na aliyakaribisha kwa kuyapangua kwa ustadi wa hali ya juu japo kwa tabu kidogo kutokana na nishati ya mikato ile kuwa kubwa


Mzee yule mara baada ya kupangua mashambulizi yale alimwangalia Shohei kwa macho yake ya kuchunguza


"Levo ya ufunguzi? Ukali wote ule na yupo hatua ya tano ya ufunguzi wa meridian?" aliwaza, alikuwa haamini macho yake


Mawimbi yale ya nishati yalikuwa na ukali kiasi cha kuacha alama ardhini,.
Watu walioko eneo hilo walikuwa katika nyuso za kushangaa na kumkubali Shohei kwa wakati mmoja kutokana na utaalamu aliouonyesha huku wale wazee watatu wakihisi aibu kutokana na kumdharau kwao kabla


"Mzee Shuma, ni kweli shambulizi alilotuma ni staili ya tisa?" aliuliza mzee Raka Su


"Japo nimefanikiwa kulipangua ila nahisi ni yenyewe hii, pengine ina makali kuliko navyodhani" alimjibu mzee huyo


"Kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma bwana Emiichi Shohei, kwa utaalamu wako ulioonyesha kwa kumaster mbinu ngumu kwa dakika nne pekee basi unastahili heshima zangu kijana"


"Haha unanisifia bure tu"


"Je unaweza kuniambia umewezaje kuimster staili ya tisa ilihali kwa wengine imekuwa ngumu sana?" aliuliza kupata ufafanuzi


"Sawa mzee kwakuwa umeomba sio vizuri nikikukatalia, iko hivi, katika staili zote tisa, staili nane ni kama njia ya kukupeleka kwenye ufunuo, chukulia mfano wa kupanda mlima ili kufika kileleni na sababu ya wengi kushindwa kumaster staili ya tisa ni kutokuelewa kwamba staili ya tisa ni hatua ya kupokea ufunuo na si mbinu, pale unapofanikiwa kumaster levo zote nane unaunganisha dots na kupata uelewa na kuona kile kilichojificha, na ufunuo utakaoupata hiyo ndio staili ya tisa, nadhani umenielewa" aliongea Shohei kwa kifupi


Ndugu msomaji kupata ufunua kwa lugha nyingine ni kilele cha uelewa, kutambua siri iliyojificha n.k


Mzee Shuma baada ya kupewa maelezo hayo mafupi alionekana kuelewa na kujiambia kumbe ndio iko hivyo


"Shukrani kwa maelezo kiongozi Shohei, basi mimi mzee nina ombi kwako kijana kwasababu inaonekana una uelewa mkubwa wa sanaa za mapigano na uvunaji nishati"


"Nakusikiliza mzee, niambie" alikubali bila kusita


"Kwa miaka sasa nimekuwa nikivuna nishati kwa mbinu fulani na nimekwama katika levo ya pili kwenye hatua fulani na imekuwa vigumu kuivuka, natumai utanipatia muongozo" aliongea yule mzee huku akiinamisha kichwa kuonyesha heshima na unyenyekevu


Watu walioko katika eneo hilo mara baada ya kuona na kumsikia mzee yule waliishia kushangaa na kujiambia wameona na kusikia vibaya ama ni macho yao yanawadanganya? Yaani mzee wa dhehebu la hadhi ya tano ananyenyekea nakuomba muongozo kwa kiongozi wa dhehebu hadhi ya tisa?


"Kama upo tayari kunielezea hiyo mbinu yako ya uvunaji nishati niko tayari kujaribu" aliongea Shohei na mzee Shuma kusikia vile alimsogelea karibu kisha kumuomba sikio amnong'oneze


Shohei bila hiyana alitega sikio lake na kumsikiliza mzee kwa umakini wa hali ya juu na kisha kwa Talisman ya maono aliweza kugundua tatizo lilipo kisha kumuelezea mzee yule kwa njia ileile ya kunong'ona masikioni


"Kumbe!" mzee alichanua macho kwa furaha


"Kiongozi unaonekana kuwa na uelewa mkubwa, mara baada ya kusikiliza muongozo wako nimepata uelewa mpya, hakika unastahili sifa" aliendelea huku akitabasamu


"Ukifuata muongozo niliokupatia ninakuhakikishia ndani ya miezi mitano utakuwa umevuka hatua zote na kuingia katika levo nyingine" aliongea Shohei huku akitoa tabasamu la ujivuni


"Shukrani sana kiongozi Shohei, basi niruhusu niondoke nina mambo mengi ya kushughulikia kwenye dhehebu langu, tukijaaliwa kukutana tena nitaomba muongozo na ushauri kwa mara nyingine tena au unasemaje? "


"Unakaribishwa wakati wowote" alimjibu Shohei na mzee huyo aliondoka baada ya kuaga


Yaani ghafla tu Shohei na yule mzee waligeuka kuwa marafiki kitendo kilichowashangaza wengi walioko hapo


"Kiomgozi Shohei je unaweza kunipa muongozo na ushauri kwenye shida yangu?" aliongea kiongozi mmoja wa dhehebu la mwewe wa dhahabu


"Mimi pia, nitakulipa" alidakia mwingine


"Kama umeweza kumshauri mtu kama Mzee Shuma mwenye heshima na anayesemekana kuwa katika levo ya pili ya uvunaji nishati bila shaka tatizo langu dogo utalitatua"


Ghafla hali ya hewa ilibadilika kutoka kuwa uandikishaji wa wanafunzi wapya na kuwa uombaji muongozo na ushauri


"Kosei zimebaki dakika ngapi za Talisman ya maono kuendelea kufanya kazi?" alouliza kifikra


"Umebakiwa na dakika hamsini na sita" alijibiwa na palepale alitoa tabasamu la kifisi na kujiambia muda huu unatosha kuwachuna kabisa hao wazee


"Shekeli hamsini kwa kila swali, je mko tayari?" aliongea Shohei akigeuka kuwa tapeli, katika Ardhi hiyo pesa zilikuwa zikipimwa kwa shekeli na madini mengine kama dhahabu, silver, yakuti, almasi n.k


"Nitalipa!"


"Mimi pia!"


Watu walikuwa tayari kulipa, hawakujali sana kama ni utapeli sababu kwenye ulimwengu huo kuvuna nishati na kupanda levo ndio kila kitu


Muda mchache mbele watu walionekana kupanga mstari kila mmoja akisubiri zamu yakle kupata muongozo na ushauri kulingana na tatizo lake, Yeri Su akiwa anapokea pesa huku Yaoyao akihakikisha wanapanga mstari na hakuna fujo inatokea huku Shohei akitoa muongozo


"Kwa hii Talisman ya maono natengeneza pesa na kujifunza mbinu zao kwa wakati mmoja, ni faida kubwa ilioje!" alijiambia Shohei akilini mwake


"Mwingine!" aliongea Shohei baada ya kumaliza kumpa mtu muongozo na kuita anayefuata


Basi akaja mtu mwingine na bila shaka alikuwa ni baba Yake Yeri Su, mzee Raka Su


"Kiongozi Shohei mimi pia nina shida yangu hivyo natumai utanipatia muongozo" aliongea


"Oh sawa, kwa wewe utalipia shekeli mia mbili" alijibu na kumfanya nzee wa watu akunje ndita


"Unatania? Yaani wengine walipie shekeli hamsini lakini mimi nilipie mia mbili? Nimemkabidhi mwanangu kwenye dhehebu lako na bado unataka kunichuna hivyo?, hata kama unaniona tajiri nifanyie haki basi" aliongea mzee Raka Su akitaka kupaaliwa na mate


"Oh kumbe wewe ni baba yake Yeri su! Basi nitakupa punguzo la asilimia tisini na tisa" aliongea kwa sauti akihakikisha sauti yake inasikikika vyema na wengi


Alionekana kufanya makusudi akiwa na lengo lake kichwani kisha aliendelea


"Ofa hii ni kwa kila mzazi ambaye mtoto wake atajiunga na dhehebu la mfupa wa chuma"


Ifahamike pia kwamba katika uandikishaji wa wanachama wazazi huja pia kuwakabidhi watoto wao wanaoanza kujiunga na dhehebu isitoshe umri wa kuanza kujiunga ni miaka kumi na sita na kuendelea, ni kuwakabidhi wanao pia waanze kujitegemea wenyewe!


Miongoni mwao waliokuwa wakitaka muongozo na ushairi walikuwa ni wazazi wa kawaida wakiwemo wenye mafunzo ya nishati levo ya chini sanaa na wasio na mafunzo ila wenye mafunzo mengine yasiyo ya nishati, ikiwemo utaalamu katika tiba n.k wengine wakiwa hawana mafunzo yaani raia wa kawaida


Sasa kusikia kwamba kuna punguzo la asilimia tisini na tisa hawakutaka kupitwa na Fursa, kingine pia walijionea uwezo wa kiongozi huyo kijana


"Kiongozi Shohei binti yangu wa kike atajiunga na dhehebu lako, nakuhakikishia hilo" aliongea mzazi mmoja


"Kiongozi Shohei mwanangu wa kiume anataka kujiunga na dhehebu lako la mfupa wa chuma" aliongea mwingine


"Kiongozi Shohei mwanangu yupo katika orodha ya vijana wenye vipaji ndani ya mji" aliongea mwingine pia


Wazazi wengi walianza kuichangamkia fursa na Shohei aliishia kutabasamu baada ya kuona lengo lake limetimia


"Yaoyao, Yeri Su hatimae usajili wa wanafunzi wapya unaanza rasmi" aliongea Shohei


Muda mchache mbele Shohei akiwa ameshamaliza kutoa muongozo na ushauri kupitia talisman ya maono alionekana kuwa bize kwelikweli kusajili wanafunzi wapya akisaidiana na Yeri Su pamoja na Yaoyao


Alijiambia kwa staili hii kupata wanafunzi laki moja ni suala la muda tu huku akijichekea moyoni akiendelea kusajili


Ding! mlio huo ulisikika kichwani mwake kisha sauti ya Kosei ikamwambia


"Hongera umeweza kufanikisha kusajili wanafunzi wapya na kutimiza idadi ya wanachama inayohitajika, na huruhusiwi kusajili zaidi"


"Nini? Unaongea upuuzi gani we kosei? Kwamba sitakiwi kusajili wanafunzi zaidi ya mia?"


"Ndio, kwasababu misheni uliyopewa ni kutimiza idadi mia moja na ukikaidi utapewa adhabu ya kutoweza kupanda levo kwa miaka kumi na kupunguziwa muda kukamilisha misheni kuu" alielezea kosei


"Hata hivyo idadi ya wanafunzi ya wenye vipaji inaridhisha, umeweza kupata wanafunzi kumi walio katika uamko wa kiroho mwangaza hafifu, arobaini wakiwa na uamko wa mwanzo, kisha idadi iliyobakia ni vivuli na kwa hilo umepata thamani ya mchango wa dhehebu 110" aliongea kosei huku akimuonyesha kupitia skrini ya hologram


Kupitia hologram aliweza kuona kwenye profile yake balansi la thamani ya mchango likiwa 120/120, ujenzi wa dhehebu ikiwa levo ya kwanza, idadi ya wanachama ikiwa ni 100/100 na pia aliona kuna maelezo mengine yameongezeka


"Hadi balansi la thamani limefikia kikomo? Asee kosei mbona unanichanganya" alilalama


"Na vipi kuhusu hayo maelezo yaliyoongezeka? Mafanikio ya dhehebu ndo nini? Na Misheni za dhehebu ndio nini?"


"Oh itabidi kukuelezea kwa kirefu zaidi ili unielewe zaidi hivyo nisikilize kwa umakini"




**********
 
CHAPTER 9: Jukwaa la malalamiko


Kwa mujibu wa Kosei akimuelezea Shohei ni kwamba sababu ya kuwa na ukomo wa idadi mia moja licha ya kwamba misheni kuu ilimtaka atimize idadi ya wanafunzi zaidi ya laki moja ni kwasababu ya hadhi ya dhehebu lake kuwa la china mno, yaani levo ya tisa, na kama atataka kuvunja ukomo basi atatakiwa kufanya misheni za dhehebu


Misheni za dhehebu ni jukumu la wanafunzi na yeye kulitimiza, japo yeye sio lazima kufanya hizo misheni za dhehebu


Na endapo misheni za dhehebu kufanikiwa ndipo inapokuja ishu ya mafanikio ya dhehebu, na dhehebu likiwa lina mafanikio mengi linaweza kupanda hadhi na ikifikia idadi mia moja ya mafanikio ya dhehebu ndipo ule ukomo wa kusajili wanafunzi unapoongezeka


Na kuhusu ukomo wa thamani ya mchango utaongezeka pale idadi ya usajili wanafunzi imeongezeka


"Anha kumbe iko hivyo, lakini mbona tabu hivi? Majukumu yanaongezeka kadri mda unavyozidi kusonga" aliongea Shohei kifikra kuonyesha kuelewa lakini na kulalama pia


"Kaza tu kijana, ulikuwa una nafasi ya kukataa lakini uliishia kukubali hivyo inakubidi uende na biti " aliongea Kosei kifikra


"Huu ni uonevu kwakweli" alimjibu


Wakati Shohei akiwa bize kuzungumza na Kosei kifikra ghafla mbele yake alikuja mtu mrefu wa kama futi sita na nukta kadhaa huku akiwa na mwili uliotuna kama baunsa


Alikuwa amevalia kitamaduni ila sio kwa mtindo wa joho, sijui ni mtindo gani hata! ila tu rangi ya nguo zake ilikuwa ni bluu bahari, alikuwa na nywele za afro licha ya kuonekana mweupe wa ngozi


"Kwahiyo kumbe wewe ndio Emiichi Shohei" aliongea lilre jitu


"Unathubutu kuwapiga wanafunzi wangu wa dhehebu la maji ya chemchem na hujalipia gharama yake bado, nawezaje kuliacha hili lipite kwa mfano?" aliendelea kuongea lile jitu


"Jamani ni kinju winu! Ni moja ya wazee wa baraza katika dhehebu la maji ya chemchem!" aliongea mzee mmoja kwa kupanic na kumfanya Shohei kutamani kucheka baada ya kusikia jina hilo alijiambia huu ulimwengu watu wana majina ya ajabu ajabu sana


"Mwaka jana kuna mwanafunzi wa dhehebu moja la hadhi levo ya nane alimpiga mwanafunzi wa dhehebu hilo, matokeo yake kiongozi wa hilo dhehebu la hadhi ya nane ilimlazimu kumuadhibu mwanafunzi wake na kumfukuza kwenye dhehebu kisha kulipa fidia ya shekeli nyingi kwa dhehebu la maji ya chemchem" aliendelea kuongea yule aliyepayuka akiwaambia wengine, alikuwa ni yule mzee mwenye kiwalaza kiongozi wa dhehebu la upanga utambaao


"Yeri Su dhehebu la maji ya chemchem si ni la hadhi levo ya tisa? Iweje madhehebu levo ya nane kuwaogopa?" aliuliza Shohei


"Ni kwasababu baraza la wazee wa dhehebu hilo ni wanafunzi waliotoka katika dhehebu hadhi levo ya tano na kwa pamoja wakaanzisha dhehebu lao, ndio sababu wanaogopwa" Yeri Su alimjibu kwa kifupi akionekana kujua mambo licha ya umri wake kuwa mdogo


"Kwakuwa sasa ushafahamu ni nani niliye mbele yako, unapaswa kupiga magoti na kuomba radhi kisha uache mali zako(shekeli) na uharibu mzizi wa nguvu zako za nishati kisha upotee mbele ya macho yangu" liliongea lile jitu


"Wale wanafunzi wako walitaka kujaribu kumnyanyasa kingono mwanafunzi wangu wa kike, nilichofanya ni kuwapa adhabu ndogo, mpaka hapo nimewaonyeshea huruma kubwa kuhusu mimi kufanya unavyoniambia sahau kabisa isitoshe sina kosa" aliongea Shohei na ilikuwa ni kweli, yule jamaa aliyemshikisha adabu alijaribu kumtongoza na kumshika mwanafunzi wake wa kike binti Yaoyao mbele yake na yeye kama kiongozi ulikuwa ni udhalilishaji hivyo alikuwa sahihi kumshushia kipondo


"Sijali walichofanya, nachojua ni kwamba umewaumiza wanafunzi wa dhehebu langu hivyo unapaswa kulipa gharama vinginevyo unajitafutia kifo" aliongea kibabe na palepale alianza kusambaza msisimko, na kufumba na kufumbua mikononi mwake zilionekana bangili kumi na mbili za ukungu rangi ya bluu bahari


"Kama uwezo unao tunaweza kusuluhisha kwenye jukwaa la malalamiko" aliendelea lile jitu bwana Kinju winu


"Kiongozi, huyu mtu anaonekana yupo katika hatua ya kumi na mbili ya ufunguzi wa meridian pia kwenye jukwaa la malalamiko ni pambano la kufa na kupona" Yeri Su alimwambia Shohei


"Kama ni hivyo sina pingamizi nakubali tulisuluhishe" aliongea Shohei akimjibu yule jitu Kinju winu bila woga


Ding! Ulisikika mlio kisha sauti ya kosei kunena katika fikra "Kijana umepatiwa misheni ya kwanza ya dhehebu, wewe kama kiongozi unapaswa kufanikisha kusuluhisha tatizo" alimtaarifu


"Mbona mapema hivyo? Ila hata hivyo usiwaze nitahakikisha nalisuluhisha vizuri na kukamilisha misheni ya dhehebu" alimjibu


Muda mchache mbele watu wengi walikusanyika mahali pamoja wakizunguka eneo na katikati kulikuwa na jukwaa la wastani la mapambano dhidi ya wapiganaji


Naam lilikuwa jukwaa la malalamiko, jukwaa hilo halikuwa kwaajili ya mapambano au masindano ya heshima wala kwaajili ya kuvutia watu ndani ya Mji huo


Lilikuwa ni kama mahakama ya mwisho, ni pale ambapo madhehebu mawili yanashindwa kufikia makubaliano, pale ambapo heshima imekanyagwa na damu inataka kulipwa kwa damu na hakuna mtu wa kuingilia awe mfalme au yoyote yule na ukifa kila mtu anaufyata kama hakuna kilichotokea


Na kupewa jina jla ukwaa la malalamiko ni Kwa sababu ya makelele ya maumivu yanayosikika kwa wapambanaji wakishushiwa kipigo Katika jukwaa hilo hata kupoteza uhai.


"Je kiongozi wetu wa dhehebu yupo katika levo ya uanafunzi katika uvunaji nishati?" yeri Su alimuuliza Yaoyao


"Hapana yupo katika hatua ya tano ya ufunguzi wa meridian" Yaoyao alimjibu na kumfanya Yeri Su kushangaa


"Hajaacha wosia kweli kuhusu dhehebu?" aliuliza tena huku akijiambia inaonekana kiongozi wake anakwenda kupigika pengine kupoteza uhai


Upande wa jukwaa walionekana Shohei na Kinjuro wakiwa wamesimama wakiangaliana, umbali walioachana ulikuwa ni wa mita sita hivi


"We punguani, ungefanya kama nilivyokuambia ungesalimika ila naona hupendi kuishi" aliongea Kinju


"Mimi na wewe nani ni punguani? Badala ya kulisuluhisha unaleta ngojera, Hiyo ni sababu tosha wewe ndiye punguani hapa"


Lile jitu Kinju lilikasirishwa na kauli ile na ghafla misuli ya mwili wake ilianza kutuna na kukaza kwelikweli, bila kupoteza muda kwa spidi alichomoka pale alipo akisindikiza ngumi nzito iliyolenga kumpiga usoni na licha ya kuwa ni jitu likubwa lakini alikuwa mwepesi mno


Upande wa Shohei alibaki kusimama vilevile wima na imara bila kupepesa macho akionekana kulikaribisha shambulizi hilo


Bam!


Ulisikika mlio wa ngumi nzito ikigongana na kitu fulani kama ngao na alionekana Shohei akiwa amesimama vilevile bila kusogea hata inchi moja, hakujisumbua hata kulipangua lakini ngumi ile ilionekana kuishia sentimeta kadhaa karibu na uso wake, ni kama vile ngumi hiyo imezuiwa na kitu kisichoonekana


Lile jitu liitwalo Kinju winu liliishia kushangaa na kujiuliza imekuwaje hii? Amemuacha mbali kwenye hatua ya ufunguzi meridian sasa iweje shambulizi lake lisifanye kazi kibaya zaidi hakuelewa kwanini ngumi yake imeishia hewani bila kumgusa lakini akahisi kwamba amapiga kitu kama ukuta mgumu


Hakutaka kuonekana dhaifu mbele ya watu hivyo alirusha ngumi nyingine lakini hali ilikuwa ni ileile.


"Bam! Bam! Bam! Bam!" alirusha ngumi mfululizo lakini wapi, hakuna ngumi iliweza kumkaribia Shohei zaidi ya kupiga makelele ya mgongano wa ngao


"Inakuwaje mtu wa levo ya chini kama wewe kuweza kukabiliana na mashambulizi yangu? Ni mbinu gani unatumia?" aliuliza lile jitu akiwa haelewi nini kinaendelea hapo


Upande wa Yeri Su aliuliza baada ya kushuhudia pambano hilo


"Ni mbinu gani kiongozi wetu anatumia? Sijawahi kuiona wala kuisikia hapo kabla, au itakuwa ni miongoni mwa mbinu alizorithi kutoka dhehebu la chuma?" alimuuliza Yaoyao


"Ingawa hata sijui ni mbinu gani anatumia lakini nina uhakika kuna uwezekano mkubwa hajatumia uwezo wake wa nishati" aliongea Yaoyao


"Unaweza kumuona ni mzembe mzembe ila ana siri nyingi ambazo hakuna anayezijua" aliendelea Yaoyao akikumbuka lile tukio la kule msituni kwa kidonge kutokezea hewani ghafla tu, kwake lilimshangaza sana ni vile tu hakutaka kuonyesha


Upande wa Shohei alikuwa ametulia tuli alipoulizwa ni mbinu gani anatumia aliishia kutabasamu


"Tangu lini ukaona mpiganaji anatoa siri kwa adui yake? Ebu usinichekeshe basi unachopaswa kufanya ni kuangalia namna ya kutatua tatizo na sio kuulizauliza maswali" alimjibu


"Hata kama hutoniambia mbinu yako, kama mashambulizi yangu machache yameshindwa nitaongezea mengine zaidi" aliongea huku akianza kurusha ngumi nyingi kwa mara nyingine tena, safari hii akitumia nguvu zake zote za mwili na nishati


Ulikuwa ni mwendo wa bam! bam! bam! Kwa dakika mbili kiasi kwamba watu walianza kuboreka na makelele hayo


"Ni mbinu ya kinga ya kushangaza ilioje!" aliongea Kinju huku akihema kana kwamba ametoka kukimbia maili kadhaa


"Ongeza bidii, kama umeshindwa kugusa hata nguo yangu unadhani wana watakuchukuliaje?, unadhani madhehebu mengine yataendelea kukuogopa baada ya kujidhalilisha hivi?" aliongea Shohei huku akitoa uchafu masikioni kwa kidole cha shahada


Kinju winu baada ya kuambiwa hivyo alikasirika, sio kwa sababu maneno ya Shohei yalikuwa na mantiki bali ni kwasababu ya kuona anadharauliwa hasa kwa jinsi alivyopozi akiongea


"Vijana wa siku hizi hamna adabu, pumbavu! nitahakikisha nakuua kifo cha maumivu" alifoka kwa hasira kisha palepale aliweka mkao fulani akiikandamiza miguu yake ardhini ardhini kupata balansi na kuvuta mkono mmoja kana kwamba analega kitu kisha alianza kukusanya nishati na kuzisafirisha kwenda kwenye ngumi hiyo ya mkono wa kulia


Upande wa Yeri Su baada ya kushuhudia mabadiliko ya Kinju alimwangalia kiongozi wake


"Kiongozi kuwa makini, hiyo ni mbinu hatari katika dhehebu la maji ya chemchem yenye kuweza kumjeruhi hata aliyeko katika levo ya uanafunzi katika uvunaji nishati" aliongea na Shohei kumgeukia


"Oh kumbe ni hatari hivyo?" aliongea


"Unathubutu kuangalia pembeni katikati ya pambano? Kufa mwanaharamu wewe!" alifoka


"Ngumi ya mwamba wa chemchem" alipayuka na kuachia ngumi huku wimbi la nishati kubwa rangi ya buluu likimuendea Shohei kwa kasi ya ajabu


Boom!


Ulisikika mlipuko wa kuumiza masikio lakini zaidi ni kwamba shambulizi lile halikuweza kumdhuru Shohei zaidi ya kugongana na kitu kama ngao isiyoonekana na nishati ile kulipuka


Yeri Su na wengine walioko hapo waliishia kuachama midomo yao wazi kana kwamba wamemuona jini, walijiuliza ni mbinu ya aina gani kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma anatumia






**********
 
CHAPTER 10: Upanga wa ghadhabu, hukumu takatifu!


Kwa Shohei hata yeye pia alishangazwa ila tu hakutaka kuonyesha asionekane mshamba, alifanya hivyo kujipa utukufu


"Asee kosei, kama nilivyotegemea mbinu zako ni za kushangaza mno!" aliongea Shohei kifikra


"Haha! Nilishakwambia na ninakuambia tena. Mimi ni yule mwenye manufaa"


"Ni kweli, thamani zangu 40 hazijaenda bure, nikimalizana naye nitahitaji maelezo ya hii mbinu" alimwambia kisha kumtazama Kinju winu


"Vipi, bado una mbinu nyingine za kunionyesha? Au umechoka?"


"Nimechoka?" alimaka Kinju akihema, ilionekana mbinu hiyo aliyotumia ilimchukua nguvu nyingi sana


"Nadhani kinju amechoka kweli" aliongea mmoja wa waliokuwa wakishuhudia pambano


"Inaonekana! Ingawa mbinu kama hizo zina athari ila zinanyonya sana nguvu" mwingine alikubaliana naye


"Kwahiyo anakwenda kushindwa pambano ama?" aliongea mwingine


Ukweli Kinju winu alionyesha kuchoka ila alikataa kukubaliana na ukweli, alivuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha kuchomoa upanga mnene aliokuwa ameubeba mgongoni, ndio alibeba upanga mgongoni mwake ni kwamba sikuelezea hapo kabla


"Unadhani kwa muda mchache kama huu kwenye pambano utanichosha?" aliongea akikaa mkao wa kupambana, akiushika upanga wake imara


Ulikuwa ni upanga aina ya "Saber" uliopinda kidogo na mnene ukiwa na makali upande mmoja.


"Huu ni upanga uliotengenezwa na master Fushi, ni mtaalamu na bingwa wa kuunda silaha za kivita kwenye hii Ardhi ya nyota, nimegharamika pakubwa mno kufanikiwa kuupata na ni mara yangu ya kwanza kuuonyesha hadharani hivyo unapaswa kuhisi heshima nayokuonyesha kwa kwenda kukuua kwa makali ya upanga huu" aliongea kinju winu na kumfanya Shohei ajiulize master fushi ndio nani? Aah potelea pote simjui kwanza na sihitaji kumjua


Shohei aliuangalia ule upanga kwa makini na kuuchunguza vizuri na aliishia kujichekea moyoni, alijiuliza Kwahiyo huo ni upanga uliotengenezwa na mtaalamu master Fushi?


Ule upanga sehemu yenye makali ulionekana kuwa na mipasuko na kuishia kusema "Huo ndio upanga uliotengenezwa na mtaalamu? Bro umetapeliwa si bora tu ungenunua ungekula hiyo hela kuliko kumpatia tapeli, kwanza unajua maana ya utaalamu?" alijiambia kimoyomoyo


"Nadhani napaswa kuweka uwiano sawa kwenye pambano" aliongea na kuonekana kuchezesha vidole hewani na ghafla upanga ulitokelezea hewani kimaajabu na kuanguka lakini kabla haujagusa sakafu ya jukwaa lileShohei aliudaka


Ulikuwa ni ule upanga wa maafa aliopatiwa na kosei akiwa katika hatua ya kuanza harakati za kukamilisha misheni kuu


Ulikuwa ni upanga mfano wa katana ila huu haukuwa umepinda, ulionyooka kama mstari mnyoofu, ulikuwa pia na makali pande zote mbili, urefu wake ulikuwa ni wa inchi thelathini


Kinju winu mara baada ya kuona tukio hilo hakutaka kupoteza muda kwani Palepale aliunganisha nishati kwenye upanga na kufyeka mara mbili hewani na wimbi la nishati yenye makali lilimsogelea Shohei kwa kasi


Naye Shohei hakutaka kuzubaa kwani sekunde ambayo kinju anafyeka upanga hewani naye pia alifyeka mara mbili na nishati za mawimbi kugoganga na mlio wa boom! Ulisikika nishati zikisambaratika baada ya kugongwa na kusababisha upepo mkubwa kuvuma eneo hilo


Wote kwa pamoja mara baada ya mashambulizi yao kufeli walichomoka kama mshale kila mmoja akimuelekea mwenzake kwa spidi


"Teng!!" mlio wa vyuma vya mapanga kugongana ulisikika na kutokana na nguvu iliyotumika basi cheche nazo pia ziliruka hewani huku kwa wakati mmoja wakitazamana na sura za kazi, sura zisizo na utani!


"Teng! teng! teng! teng!" mpambano uligeuka kutoka kuwa wa ngumi na kuwa wa mapanga huku cheche za moto zikiruka hewani, lilikuwa pambano lakuvutia macho kwa watazamaji


Ingawa Shohei alikuwa si mtaalamu kwenye sanaa ya kucheza na upanga ila kwa msaada wa mbinu ya staili tisa za upanga wa ghadhabu aliweza kupangua mashambulizi kwa ustadi wa hali ya juu huku pia faida ikiwa upande wake kutokana na mshindani wake kupoteza nguvu nyingi za nishati mwanzoni mwa pambano


"Makali ya upanga wa chemchem ya uzima!" alipayuka bwana Kinju na Shohei kujiambia anapaswa kumaliza pambano mapema kabla hajachoka na palepale aliachia shambulizi la ufunuo alioupata katika staili tisa za upanga wa ghadhabu





"Upanga wa ghadhabu, hukumu takatifu!" aliongea Shohei na kufyeka upanga hewani kwa mtindo wa vertically na nishati rangi ya njano kwa kasi ya kimondo kuvaana na ile nishati ya buluu bahari


Mara baada ya nishati hizo mbili kukutana, nishati ya chemchem ilisambaratishwa kutokana na shambulio la nishati la Shohei kuwa na kasi pamoja na nguvu kubwa


"Chwaa!" ulisikika mlio wa kukata ukiambata na ukelele wa maumivu


"Utaniwia radhi, hii ni mara yangu ya kwanza kutumia mbinu hii na kushindwa kuidhibiti" aliongea Shohei akimwambia kinju ambaye wakati huo alikuwa amepiga magoti sakafuni huku damu zikiwa zinamvuja kwa wingi





Mkono wake wa kulia alioshikilia upanga ulikuwa umekatwa wote na kuangukia sakafuni mwa jukwaa hilo, alikuwa aking'ata meno yake kwa nguvu akiugulia maumivu





Shambulizi la Shohei lilikuwa ni ufunuo alioupata katika kuzismaster staili tisa za upanga wa ghadhabu, kuhusu funuo ngapi amepata hilo mimi sijui


"Au nimeenda mbali? Lakini alitaka kuniua, kukata mkono wake ni adhabu tosha" alijiuliza mwenyewe akilini mwake na kujijibu


Hakutaka kuendelea kubaki hapo jukwaani kwani alishuka kisha kuwakaribia Yeri Su na Yaoyao kisha kuwaambia


"Nadhani hatuna sababu ya kuendelea kubakk hapa mjini isitoshe usajili umekamilika hivyo turudi kwenye dhehebu letu" aliongea


Watu wengi walikuwa wakimuangalia Shohei kwa macho ya kustaajabu


"Kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma ameweza kumshinda kinju mwenye cheo katika baraza la wazee ndani ya dhehebu la maji ya chemchem" walikuwa wakiliongelea pambano


"Sio kumshinda tu, amemkata na mkono, na cha kushangaza zaidi ni kwamba yupo katika levo ya tano ya hatua za ufunguzi wa meridian"


"Hata hivyo sidhani kama dhehebu la maji ya chemchem litaacha hili lipite wakifahamu"


"Ni kweli, hapa nawaza kama ataweza kudili na hilo dhehebu la maji ya chemchem"


Waliendelea kuongea wao kwa wao huku wakimpisha Shohei njia na hatimae Shohei aliweza kutoka mbali na kadamnasi ile yeye na wanafunzi wake wawili

"Kiongozi ni mbinu gani uliyokuwa ukitumia kuweza kuhimili yale mashambulizi" aliuliza Yeri Su akimaanisha wakati ambao Shohei akiwa akipokea mashambulizi bila madhara akisimama tu na hata Yaoyao alionyesha kutaka maelezo pia


"Oh kuhusu hilo, ngoja nifikirie namna nzuri ya kuwajibu" aliongea Shohei kisha kumuuliza kosei kifikra


"Kosei unaweza nipa maelezo ya kina, kwanini mbinu ile ya ngao ya chuma, licha ya kwamba adui yangu kunizidi hatua saba za ufunguzi kwenye kuvuna nishati za mbingu na ardhi lakini bado akashindwa kuvunja"


"Oh sawa, iko hivi, ile ni mbinu kama mbinu ila si mbinu ya kuvuna nishati"


"Unamaanisha nini kusema hivyo?"


"Unapaswa kufahamu kwamba mbinu za kimapigano, mbinu za siri zenye kutumia nguvu za kiroho na nyinginezo na uvunaji nishati wa mbingu na ardhi ni vitu viwili tofauti


Ni vitu viwili tofauti vinavyojitegemea na vilevile vinaweza kufanya kazi kwa pamoja, kwanza labda nikuulize unajua kwanini levo za uvunaji nishati zinaitwa uanafunzi wa mapigano, bwana wa mapigano na kuendelea lakini si uaafunzi wa nishati, bwana wa nishati n.k"


"Najuaje mimi sasa na ufahamu wangu mdogo kwenye baya masuala"


"Ni kwa sababu wapiganaji wanavuna nishati ili kuweza kuzitumia katika mbinu za mapigano, wanazivuna nishati na kuziunganisha kwenye mbinu mbalimbali za mapigano na nguvu za kiroho ili kuleta ufanisi na athari kubwa mara mbili yake au zaidi"


"Oh kwahiyo unamaanisha kwamba kuna mbinu za mapigano zina nguvu na kitendo cha kuziunganisha na nishati za mbingu na ardhi zinakuwa na athari kwa hata yule aliyekuzidi levo?"


"Naam ndivyo navyomaanisha"


"Kwahiyo nilipotumia Talisman ya ngao ya chuma kisha kuunganisha na nishati za mbingu na ardhi ndio kumeipa mbinu nguvu maradufu" aliongea Shohei kifikra, ilionekana kabla ya kuanza pambano kisirisiri alitumia Talisman ya ngao ya chuma kisha kuunganisha na nguvu za nishati ya mbingu na ardhi


"Ooh sawa, vipi kuhusu hizi mbinu za Talisman unaweza nielezea zinafanyaje kazi"


"Chukulia kama mbadala wa kidonge kitakachokupa nguvu kwa muda maalum, talisman yenyewe ni nishati, imetengenezwa kwa muunganiko wa nguvu za kiroho na nishati za mbingu na ardhi na pale unapotumia talisman husika basi hugeuka kuwa nishati itakayokusaidia kwa muda, mfano mdogo ni hiyo talisman ya ngao ya chuma


Mara ulipoiamsha nguvu ya nishati ile itokayo kwenye talisman, iligeuka kuwa ngao ya nishati isiyoonekana, ngao ngumu kama chuma na ndio maana mashambulizi ya yule kinju hayakuweza kukugusa" alielezewa na Kumfanya kuelewa


Shohei alitumia maelezo yale kuwaelezea kwa kifupi wanafunzi wake kuwaondolea shauku huku akiwaambia Talisman hiyo ilikuwa sehemu ya urithi wa nguvu kwenye dhehebu kutoka kwa muanzilishi ili kuepuka maswali


Baadae kidogo Shohei akiwa pamoja na Yeri Su na Yaoyao walikuwa nje ya geti la mji huo


"Yeri Su ukishaanza mafunzo rasmi itakuwa ngumu kwako kukutana na wazazi wako, hivyo nenda nyumbani utumie siku kumi kuwa pamoja na familia yako kisha baada ya siku kumi uwasili makao makuu"


"Kiongozi, baba yangu tayari anafata muongozo na ushauri wako katika kuvuna nishati na huwaga hapendi usumbufu akiwa anavuna nishati hivyo kurudi nyumbani kutakuwa hakuna maana"


"Oh kama ni hivyo unaweza kurudi pamoja nami kwenye dhehebu"


"Pia kiongozi nina ombi kwako tafadhali" aliongea Yeri Su


"Nakusikiliza"


"Ni kwamba kuna mtu ningependa kuja naye kwenye dhehebu" aliongea na kumfanya Shohei atoe tabasamu la uzoefu kisha kumuuliza


"Si ni msichana eeh?"


"Aah... Ndio ni mchumba wangu kutoka katika moja ya familia" aliongea huku akitabasamu kwa kushtukiwa


"Kwahiyo hio ni sababu ya kukataa madhehebu yote na kuungana na dhehebu langu si ndio?" alimuuliza


"Ukweli nilishaamua kitambo kujiunga na dhehebu lako kabla hata ya kufika kwenye usajili isitoshe kwa dhehebu lenye hadhi na heshima kama mlima mrefu wasingeniruhusu kuleta mtu wa nje ambaye si mwanachama" aliongea


"Sawa nimekuelewa, dhehebu letu linakosa wafanya kazi hivyo mlete atatusaidia sana kwenye kupika na mengineyo lakini....." aliongea kisha kunyamanza na kuweka sura ya kutia huruma kana kwamba ameonewa









**********
SEE YA TOMORROW KWA MUENDELEZO
 
CHAPTER 11: kiongozi asiye na aibu


"Una miaka kumi na saba tu na tayari uko kwenye mapenzi? Mbona mapema sana hivyo? Hivi umefikiria kuhusu hisia zangu? Mimi ni mkubwa zaidi yako kwa mbali na bado niko single, hivi kwanini unashindwa kunionea huruma kiongozi wako? Unataka niishi kwa wivu" alilalama kwa hisia na kutia huruma kiasi kwamba ungemuona ungecheka sana, ni kama vile alikuwa akijuana na Yeri Su kwa muda mrefu


"Hata hivyo kamlete hapa ili tuondoke naye, pia ukusanye na vitu vyako muhimu nitakusubiri na Yaoyao" aliongea


Bila kupoteza muda Yeri Su aliondoka mahali hapo kurudi ndani ya mji, Yaoyao aliishia kutingisha kichwa kwa masikitiko kwa kiongozi wake kukosa aibu


"Hey binti, mbona unakuwa kauzu muda wote hivyo? Mtoto wa kike kununa muda wote haipendezi tabasamu hata kidogo basi" aliongea Shohei kichokozi baada ya Yeri Su kuondoka kws maana mwingi binti huyo alikuwa kimya


"Sijanuna, ni mawazo yako tuyanakusumbua" alimjibu


"Hivi kiongozi unamiaka mingapi?" alimuuliza


"Oh wataka kujua umri wangu? Kwakuwa mwanafunzi wangu umeniuliza, sio vibaya nikakujibu. Nina miaka ishirini na mitatu" aliongea Shohei akitabasamu akitaja umri wake halisi


"Kweli? Una uhakika ni umri wenyewe huo? Una miaka ishirini na tatu lakini una tabia kama za mtoto wa miaka mitano, Kiongozi usiye na aibu..!"


"Binti maneno yako yanavunja moyo ujue, hata kama umri wangu ni mdogo kuweza kuwa kiongozi lakini angalau unapaswa kunipa heshima"


"Heshima nitakupa pale unapostahili kupewa, sijui hata imekuwaje ukawa kiongozi, pengine ni kwa sababu huna aibu na kulaghai watu kwa maneno yako ya uongo na kweli"


Shohei aliishia kujiambia akilini mwake "Unadhani napenda sana kuwa kiongozi? Ni vile tu hujui navyohangaika kutimiza majukumu ya dhehebu, kwanza unajua maumivu ya kukaa kwenye benchi gumu zaidi ya mwezi wewe?" aliona ni kheri kumpotezea tu kuliko kujielezea


Dakika kadhaa mbele Yeri Su alionekana akirudi huku akiwa na uso wenye huzuni nyingi, alikuwa akitia huruma


"Hakutaka kuwa kikwazo kwenye mustakabali wa maisha yangu, hivyo ametoweka kwao akiniachia barua" aliongea kwa huzuni alipowakaribia, alikuwa amebeba kifungashio chenye vitu vyake muhimu huku mkononi akiwa amehika barua


"Oh inaonekana ni yale mambo ya familia tajiri na familia maskini si ndio?" aliongea Shohei kwa kuotea na alikuwa sahihi


"Kama mchumba wako ni kutoka katika familia duni, yeye kuondoka kimyakimya ni uamuzi sahihi aliofanya kwaajili ya manufaa kwa kila mmoja" aliendelea na maneno yake yalionekana kuwa ya baridi kwani Yeri Su alimwangalia kiongozi huyo kwa macho fulani hivi kana kwamba anataka kumkaba koo


"Kiongozi hata wewe unadhani si chaguo sahihi kwangu?" Yeri Su alimuuliza


"Hapana, ni watu wa familia yenu ndivyo wanavyofikiri hivyo, mimi naona ni kinyume chake"


"Isitoshe upendo wa kweli haungalii hadhi bali ni nia ya dhati na moyo uliopenda kweli, hayo mambo ya sijui hadhi ni kutaka kuwakosesha watu mema ya ulimwengu na utamu wa tunda" aliendelea akionekana kuwa na uzoefu na hayo mambo


"Endapo nikifanikiwa na kuwa mwenye nguvu, haijalishi kama yupo kwenye miisho ya huu ulimwengu nitamtafuta mpaka nimpate, kisha nimwambie ni mimi Yeri Raka Su ambaye watu walidhani hatuendani na sasa nipo hapa kuwadhibitishia kwamba walikosea" aliongea akiwa na dhamira kuu ingawa hakuelewa nini maana ya "utamu wa tunda"


"Naam hayo ndiyo maneno sasa nami Emiichi Shohei nitakuvunjavunja kisha kukujenga upya na kuwa mwenye nguvu" alimtia moyo kiasi cha Yeri Su kuanza kububujikwa na machozi


Masaa kadhaa mbele watatu hao walionekana kuwa mbele ya lango la kuingilia dhehebu la mfupa wa chuma, Ingawa dhehebu lilikuwa kubwa ila lilikuwa limechakaa sana kana kwamba liliwahi pigwa na bomu hapo kabla kama sio kudondokewa na kimondo


"Msiwaze sana kuhusu muonekano wa dhehebu, kwakuwa leo tumepata wingi wa hela hivyo marekebisho yatafanyika"


Wakati Shohei anaongea hivyo, pale mlangoni kulikuwa na katoto kadogo kakijoa eneo hilo huku kakicheka kama mazuri vile na kitendo kile kilimfanya Shohei akunje ndita


"Yeri Su ebu niachie! nataka kukashikisha adabu haka katoto, kanapata wapi uthubutu wa kukojoa mbele ya mlango wa dhehebu la mfupa wa chuma?" aliongea kwa jazba akitaka kukifata kile kitoto lakini alizuiwa na Yeri Su


"Kiongozi punguza jazba, ni mtoto tu asiye na uelewa na anachokifanya"


"Ni mtoto asiye na uelewa? Ebu ona jinsi anavyocheka"


Kale katoto kalipomaliza kukojoa kaligeuka na baada ya kuona watu watatu nyuma yake kalianza kukimbia kuondoka eneo hilo


"Unakimbilia wapi? Njoo hapaa nikufunze adabu wewe!" aliendelea kumaka akitaka kukizuia lakini Yeri Su hakumuaxhia mkono wake na kale katoto kalifanikiea kukimbia


Shohei alitulia na kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha kuongea


"Naanzaje kwanza kujibishana na katoto ka miaka mitatu kwa mfano? Huku ni kujishushia heshima kama kiongozi wenu, ebu tuingie ndani kwanza" aliongea kama sio yeye aliyekuwa akimfokea kale katoto


"Kujishushia heshima? Kwahiyo mpaka hapo unajiona bado una heshima sio?" Kosei alimuuliza kifikra pengine alikubaliana na maneno ya Yaoyao hapo kabla kwamba kiongozi huyo hana aibu


"Tulia we tapeli, mimi kama kiongozi bado nina heshima isitoshe nilichokuwa nataka kufanya ni kulilinda dhehebu dhidi ya mkojo wa kale katoto"


Aliongea kifikra huku akipiga hatua kuingia ndani na alipokaribia kizingiti cha lango lile ghafla ubao mkubwa ulimuangukia na kumgonga kichwani karibu na komwe kisha kuanguka chini


Sekunde si nyingi nundu lilianza kuonekana karibu na komwe lake


"Aarrgghh! Yeri Su ebu niachie bhana nataka kuuvunjavunja huu ubao" alimaka huku akitaka kuuvunja kweli ule ubao kwa hasira alizo nazo lakini alizuiwa na Yeri Su ambaye alionekana kusoma mawazo yake na kumuwahi


"Kiongozi huo ni ubao unaotambulisha dhehebu letu, tafadhari punguza jazba"


Muda mbele kidogo Shohei alionekana ameketi kwenye kiti cha mbao huku kichwani alizungushia kitambaa kwa mtindo wa kuvaa kilemba akificha nundu alilopata muda mchache pamoja na nywele zake


Mbele yake walisimama Yeri Su na Yaoyao wakijizuia kwa uwezo wao wasicheke mbele yake


"Misheni ya sasa ya dhehebu ni kuliboresha ipasavyo sehemu zilizoharibika, kama madirisha, milango na mengineyo ya muhimu,n Yeri Su na Yaoyao nitawaacha msimamie hili suala, hakikisheni mnalifanya kwa umakini na kukamilisha" aliongea Shohei huku akimkabidhi Yeri Su hela zote zile za urithi na kiasi fulani za zile alizofanikiwa kupata siku hiyo


"Lishughulikieni hilo, mimi kichwa kinaniuma hivyo nahitaji kupumzika" aliongea huku akisimama kuelekea kilipo chumba cha kiongozi wa dhehebu


******


Baada ya siku kadhaa kupita Shohei alionekana kutoka kwenye chumba chake na kukagua mazingira ya dhehebu hilo, alionekana kutoka kuamka usingizini


Kulikuwa na mafundi ambao walikuwa wakiendelea na kazi zao za ujenzi kuboresha dhehebu hilo


"Kama kawaida naona ujenzi unaendelea vizuri, inaonekana wanafunzi wangu ni wa kutegemewa kwenye baadhi ya mambo" alijiwazia


"Kwa hali hii ninapata muda wa kuwa huru wa kujiimarisha kwenye kuvuna nishati, kosei si ulisema kasi ya uvunaji nishati hutegemeana na mwamko wa nguvu za kiroho wa mhusika?" aliuliza kwa sauti ya kawaida isiyosikika na watu


"Naam ndivyo nilivyosema"


"Vipi kuhusu hiki kidonge hakina madhara kweli? Kwa maelezo yako unasema kitanisaidia katika kuamsha nguvu za kiroho?" aliongea huku mkononi mwake kikionekana kidonge rangi you kijivu


"Niamini kijana siwezi kukuuzia kitu chenye kukuletea madhara, kidonge hicho kweli kitakusaidia kuamsha mwamko kwa hatua moja"


"Sawa, lakini ndio kinigharimu thamani kumi za mchango? Kidonge cha kuponyesha kilinigharimu thamani moja tu, iweje gharama ipande mara tisa?"


"Utofauti wa matumizi na ubora pia, halafu acha ubahili si bado umekuwa na thamani nyingi tu?"


"Thamani nyingi? Unatania au? Yaani themanini zilizobaki unaita nyingi?"


"Usichukulie poa thamani za mchango wa dhehebu, thamani moja ni sawa na jiwe la madini lenye uzito wa gramu ishirini, mfano tuchukulie jiwe hilo ni rubi. Je kwa gharama ya huko ulikotoka ni kiasi gani?"


"Gramu 20?" aliuliza kwa mshangao kisha kutafakari akipiga mahesabu


"Unataka kuniambia thamani moja ya mchango wa dhehebu ni sawa na sh millioni ishirini na tano na ushee kwa thamani ya nchi yangu"


"Ingawa thamani ya nchi yako siijui ila kama mahesabu yako hivyo basi uko sahihi"


"Kudadeki! Nilijua we ni tapeli kama matapeli wengine, kumbe ni zaidi ya tapeli? Ebu tusiliongelee hili maana roho itazidi kuniuama" aliongea kwa uchungu


"Ngoja kwanza niupe mwili wangu msingi mzuri kwanza" alijiambia kisha kumeza kidonge
Mara baada ya kumeza kidonge kile hazikupita hata sekunde kumi alianza kuhisi mabadiliko ya mwili wake, alikuwa akipitia hisia za ajabu ambazo hakuwahi kuzihisi hapo kabla


Alijihisi mwepesi mno kuliko mwanzo na hata milango yake ya fahamu kuimarika


"Hongera Shohei kwa kupitia mwamko wa nguvu za kiroho, ulikuwa kivuli ila kwa sasa upo katika levo ya mwanzo" aliongea kosei akimpongeza


"Na kwasababu ya mwamko wako wa kiroho, kwa msaada wa nguvu za kiroho kumekuvusha mpaka hatua ya kumi ya ufunguzi wa meridian"


"Hahaha kama nguvu za kiroho zina faida hivi bila shaka nikipiga hatua nyingine ya uamko wa nguvu kutakuwa na faida zaidi" aliongea kichangamfu


"Eti kosei ukiachana na mimi kutumia njia za mkato je hakuna namna nyingine ya kupanda levo?" aliuliza


"Ipo"


"Ipi hiyo?"


"Kuna namna ipi nyingine tofauti na kutumia muongozo wa mbinu mbalimbali za uvunaji nishati za mbingu na ardhi?"


"Oh ni kweli na kuna haja ya kupata muongozo wa kuvuna nishati kwaajili yangu na wanafunzi kwa ujumla"


"Usiwaze sana, nina mbinu nyingi sana ni suala la wewe tu kuamua kununua"


"Nina machungi bado ya kutapeliwa na wewe, tafadhali usitake kuniongezea machungu wakati bado sijapoa!" aliongea


"Ngoja kwanza nione ni athari kiasi gani za nilizonazo baada ya kufikia hatua ya kumi ya ufunguzi" aliendelea kisha palepale alizichaneli nguvu katika mwili wake na kupiga ngumi ukuta uliokuwa karibu yake


"Boof!" kutokana na nguvu zake za nishati kuongezeka ukuta ulibomoka na ukelele ule kuwashtua mafundi na Yeri Su aliyekuwa akisimamia ujenzi


Yeri Su alikuwa ameshika daftari dogo na mara baada ya ukuta kubomolewa alianza kuandika andika kisha baada ya kumaliza alimuangalia kiongozi wake


"Kiongozi, huo ukuta uliobomoa itahitajika angalau shekeli mia mbili kuurekebisha" aliongea, kumbe alikuwa akipiga hesabu na kuongezea bajeti ya ujenzi


Shohei mara baada ya kusikia vile alirudi kwenye chumba chake na baada ya dakika kama mbili alitoka na hela zote zilizobakia na kumkabidhi Yeri Su





********
 
CHAPTER 12: Himaya ya mlima mweusi


"Ninakukabidhi hela hizi zote kwaajili ya ujenzi endapo bajeti itaongezeka utatumia, hivyo sitotaka usumbufu kwa muda nahitaji kuwa peke yangu" aliongea Shohei akimaanisha anajitenga kwaajili ya kuvuna nishati

"Pia itabidi kasi ya ujenzi iongezeke kabla ya wanafunzi wenzako kuwasili, muda wa siku kumi niliowapa unaksribia kuisha" aliendelea kuongea

"Usiwaze kiongozi siku tatu tu zitatosha kukamilisha kila kitu" aliongea Yeri Su


BAADA YA SIKU TATU


Kukiwa asubuhi na mapema, mwangaza wa jua la asubuhi liking'arisha anga na ulimwengu wote wa Ardhi ya nyota, alionekana Shohei ndani ya chumba kipana kilichopangiliwa vizuri kwa ustadi wa hali ya juu na kitamaduni zaidi

Alikuwa amekaa mkao wa kufanya tahajudi, akiwa amefumba macho huku mwangaza wa jua kupitia dirishani ukimulika uso wake na kufanya nywele zake nyeupe kung'aa kama wingu jeupe ling'aavyo angani

Alifumbua macho yake akishusha pumzi nyingi kuonyesha kuchoka kwa kukaa staili hiyo kwa muda mrefu, alisimama kisha kivivu alianza harakati za kuusafisha mwili wake, alipiga mswaki kwa kutumia kijiti kinene cha mti fulani hivi wa mkwaju, kisha baada ya kuoga alivaa nguo za siku hiyo

Lilikuwa ni joho flani hivi la kale rangi ya zambarau lenye michoro kama ya chata fulani rangi nyeupe, kiunoni akifunga mshipi rangi ya kijivu na kuonekana kama mtu mwenye hadhi kubwa, kifupi alipendeza

Baada ya kutoka nje aliweza kushuhudia mabadiliko ya mazingira la dhehebu kiasi cha kutolitambua kirahisi kama ni dhehebu lake, ilionekana alijifungia ndani kwa siku tatu

Alishangaa na kuvutiwa na uzuri wa mazingira ya dhehebu lake akiangalia huku na huko moyoni akijiambia wow!

“Wow…” alinong’ona kwa sauti ya chini iliyojaa mshangao.

Kulikuwa na bustani ya kuvutia sana. Njia za mawe zilipangwa kwa ustadi mkubwa zikielekea katika majengo mbalimbali ya dhehebu hilo. Kila upande kulikuwa na miti mirefu iliyosimama kwa fahari, majani yake yakipeperushwa taratibu na upepo wa asubuhi uliobeba harufu nzuri ya maua

Mabanda na majumba ya dhehebu yalikuwa yameboreshwa kwa ustadi wa kale uliodhihirisha hadhi na historia ya dhehebu hilo.

"Kiongozi je umeridhishwa na maboresho ya dhehebu?" aliuliza Yeri Su isieleweke amefikaje hapo na kumtoa Shohei kwenye mshangao

"Nimeridhishwa, tena sana! Nilidhani labda nimeingia kwenye himaya ya watu" aliongea Shohei akikubali huku akitoa ishara ya kidole gumba kukazia manena yake

"Ni jambo zuri kama umeridhishwa na ujenzi, pia nataka niripori kiasi cha hela zilizobaki" aliongea kwa tabasamu

Dakika kadhaa mbele Shohei alionekana kukaa chini kwenye ngazi na sura kama ya kuomboleza

"Yeri Su usiniambie hizi ndio pesa zilizobaki" aliongea huku magotini zikionekana pesa za sarafu kiasi kidogo mno

"Shekeli elfu kadhaa sio kiasi kikubwa kama unavyofikiri, bado pia maboresho ya uwanja wa mafunzo na sekta ya upishi kwenye dhehebu itahitajika Shekeli elfu sitini" aliongea Yeri Su

"Shekeli laki mbili unaita elfu kadhaa? Na bado unahitaji shekeli elfu sitini!? Nilidhani Kosei pekee ndiye tapeli nayemjua ona sasa kuna tapeli mwingine anayenifilisha mapema" alilaumu moyoni

Wakati Shohei akiwa analaumu moyoni ghafla baadhi ya wanafunzi walianza kuwasili wakiwa na mizigo yao

"Whoa! Dhehebu linapendeza na kuvutia mno!" alisikika akiongea mmoja wa wanafunzi

Shohei alijiambia linashindwaje kupendeza na kuvutia baada ya maelfu ya shekeli kutumika kuboresha? Nipo ukingoni kufilisika ujue?

"Mbona mpo wachache hivyo wengine wako wapi?" aliuliza Shohei

"Kiongozi wengine wanaishi mbali nadhani watachelewa kuwasili" alijibiwa na mwanafunzi mmoja wapo

Mara kwa mbali alionekana mwanafunzi akitembea kwa tabu na mara alipofika karibu na kizingiti can lango la kuingilia na kujikwaa lakini kabla hajaanguka kufumba na kufumbua Shohei alikuwa amemdaka pembeni yake pia akiwa Yeri Su

"Kiongozi si alikuwa katika hatua ya tano ya ufunguzi, iweje akawa na spidi kunizidi?" alijisemea Yeri Su ilionekana yeye pia kutaka kumuwahi asianguke lakini Kwasababu kiongozi wake alikuwa na spidi kumzildi, alichelewa

"Nini kimekukuta?" Shohei aliuliza

"Kiongozi, tulikuwa tunasafiri kuja hapa tukiwa kundi la wanafunzi zaidi ya arobaini, lakini katikati ya safari tukavamiwa na kutekwa" aliongea kivivu huku mkononi akiwa ameshika karatasi lenye ujumbe

Shohei alimkabidhi kijana yule kwa Yeri Su kisha kusoma ujumbe uliokuwa kwenye karatasi lile na aliishia kukunja ndita

Ujumbe Ulikuwa ukisema hivi "Kusanya hela za kutosha na vitu vyenye thamani kisha uje navyo kwenye himaya ya mlima mweusi kwaajili ya mabadilishano na wanafunzi wako, ukikaidi subiri maiti nyingi zikitupwa nje ya lango la dhehebu lako

"Wanapata wapi uthubutu wa kuteka wanafunzi wangu, inaonekana wamechoka kuishi" aliongea kwa sauti yenye bezi akitupa karatasi hewani

"Yeri Su nitakutaka uwaangalie wanafunzi wenzako, ninaenda kwenye himaya ya mlima mweusi kuwarudisha wanafunzi wangu" aliongea na bila kusubiri jibu alipiga hatua kuondoka

"Kiongozi usikurupuke, himaya ya mlima mweusi ni himaya ya wahalifu, kuna wahalifu zaidi ya mia mbili" alipanic Yeri Su

"Pia wewe kama kiongozi wetu upo katika hatua ya ufunguzi, ingawa sijui ni hatua ipi umefikia, ni wazi unaenda kuvamia msafara wa mamba, watakuua, angalau nami nije nawe" aliongea Yeri Su

"Kwenye msafara wa mamba kenge lazima niwemo, bakini na mshughulike na mambo ya dhehebu hakuna mtu kuambatana nami" aliongea kibabe

"Lakini...."

"Ni amri sio ombi" alimkatisha

********

Zaidi ya nusu saa mbele Shohei alionekana kufika mahali, mbele yake kulikuwa na mabonde na mlima mmoja mpana na mrefu mweusi, naam ilikuwa ndiyo himaya ya mlima mweusi

Ingawa alikuwa mgeni katika ulimwengu huu na kutofahamu maeneo mengi lakini kwa msaada wa Kosei aliweza kufika

Alianza kupanda mabonde kwa zaidi ya dakika kumi na kwa mbele aliweza kuona watu wawili wamesimama ni kama vile walikuwa wakilinda, mikononi walibeba upanga

"Oi angalia kule, kuna mtu anathubutu kutalii kwenye mabonde ya himaya ya mlima mweusi" aliongea wa kwanza

"Anaonekana kuwa dhaifu mno, pengine ni mwanafunzi wa dhehebu fulani" aliendelea wa kwanza kisha kumkaribia Shohei

"Kijana kabidhi vitu vyako vyenye thamani na pesa, au wataka nikugae?" aliongea akitoa tabasamu ovu akimnyooshea upanga

"Ni kwamba ukiniacha nikukague matokeo yake utabakia vipande ila ukivitoa mwenyewe pengine utabakia kipande" aliongea akimaanisha kwamba akikaidi atatumia nguvu na kumuua ila akitii atasalimika

"Boss wako yuko wapi?" Shohei alimuuliza akimuangalia kwa macho yaliyojaa usiriaz

"Boss wangu? Unaongea upuuzi ga.." kabla hata ya kumaliza sentensi yake alikatwa koo, lilikuwa ni shambulizi la kushtukiza

"chwaa!" ilikuwa ni sauti ya damu kuruka na koo kuchanika, kilikuwa ni kitendo cha sekunde

Shohei mkononi mwake kwenye vidole alikuwa ameloa damu, ilionekana alitumia mkono wake kufanya shambulizi na kwa faida ya kucha zake pamoja na spidi ya shambulizi aliweza kufanikisha hilo

Yule mtu aliishia kushika koo yake na kuanguka chini akikata roho kama kuku aliyetoka kuchinjwa

Upande wa yule mtu wa pili mara baada ya kushuhudia kitendo kile alipatwa na hofu, kiasi kwamba alianza kutetemeka kana kwamba ameona zimwi

Shohei alimwangalia kwa macho makali kisha kuongea

"Narudia tena, Boss wenu yuko wapi?" aliongea akiwa ameshamkaribia yule mtu uso kwa uso kwa spidi ya hatari

Kwanza angeletaje ubishi kwa mfano? Kama mwenzake ameweza kuuliwa ndani ya sekunde chache yeye je itakuwa sekunde ngapi? Isitoshe hawakuwa na mafunzo yoyote ya uvunaji nishati zaidi ya kuwa wahalifu wa kawaida

"Yu..Yuko nyuma ya mlima mweusi" aliongea kwa hofu huku akihisi kutaka kujikojolea kutokana na msisimko ambao Shohei aliokuwa akimsambazia

"Nenda kamwambie hivii, kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma yuko hapa kuwachukua mateka wake" aliongea

Dakika kadhaa mbele nyuma ya mlima mweusi kulionekana majengo kadhaa ya mbao na mapango kisha kuna sehemu kubwaa yenye uwanja na mbele ya uwanja huo kulikuwa na kijukwaa kidogo ambapo pia kulikuwa na kiti fulani cha enzi

Kwenye kiti hiko alionekana mwanaume mwenye nywele nyingii zilizokosa matunzo, mwili uliojengeka vyema kimazoezi akiwa ameketi kwenye kiti hicho kisha nyuma yake upande wa kulia na kushoto wa kiti walikuwa wamesimama watu wapatao nane

Yule mtu alionekana kuwa ndio boss wa himaya hiyo ndogo akiwa amevalia mavazi mazito na magumu yaliyotengenezwa kwa ngozi ya mnyama

Kwenye uwanja huo katikati alionekana Shohei akiwa amesimama akizungukwa na kundi kubwa la wahalifu

"Hii himaya ya hawa wahalifu imezungukwa na milima mikubwa pande tatu, na sehemu pekee ya kuingia kwenye himaya hiyo kuna ulinzi mkali, haishangazi kwa serikali na baadhi ya madhehebu kushindwa kudili nalo na matokeo yake kupata hasara tu" alijisemea moyoni kutokana na maelezo aliyopatiwa na kosei kwamba serikali ya ardhi ya nyota ilijaribu kudili na hao wahalifu lakini walishindwa

"Hao watu nane walioko nyuma ya kiongozi wao ni wataalamu na wenye uzoefu wote wanaonekana kuwa hstua ya kumi ya ufunguzi au zaidi" kosei alimwambia kwa njia ya fikra

"Na kiongozi wao anaonekana kuwa ni katika levo ya uanafunzi wa mapigano katika uvunaji nishati" aliongea Shohei

"Upo sahihi yupo katika levo hiyo" kosei alimuunga mkono

"Tunahisi heshima kwa uwepo wako kiongozi, huwa inaleta baraka kwenye himaya yangu kwa viongozi wa madhehebu wanapofika" aliongea kwa sauti nzito mkuu wa himaya hiyo

Shohei aliishia kujiambia kama yupo katika levo ya uanafunzi wa uvunaji nishati za mbingu na ardhi si uwezo wake utakuwa ni sawa na watu kumi walioko katika hatua ya kumi na mbili ya ufunguzi wa meridian? Alijilaumu kwa kuja mwenyewe hata hivyo kwakuwa alishaaindikiza chakula mdomoni hakuwa na budi kukitafuna kisha kukimeza bila kujali ladha kama ni mbaya au nzuri

"Huwa sipendi kupoteza pumzi na sauti hivyo nitakwenda kwenye pointi, nimekuja kuwachukua wanafunzi wangu" aliongea shohei

"Nami pia sipendi kuzungukazunguka. Shekeli mia moja kwa kila mwanafunzi" aliongea mkuu wa himaya hiyo

"Wapo idadi si chini arobaini hivyo ni shekeli elfu tano kwa wote" aliendelea

"Inaonekana hunielewi bado, sipo hapa kununua mateka, eniwei unaonaje shekeli moja? Unawaachia wanafunzi wangu na kuwaomba radhi kisha nakulipa shekeli moja kama ada ya malezi" aliongea Shohei kibabe





**********
TUKUTANE TOMORROW AGAIN KWA MUENDELEZO
 
CHAPTER 13: Chui wa milia


"Kiongozi wa dhehebu la mfupa wa chuma nadhani unanichukulia kama fala mwenzio sio?" aliongea na kunyanyua mkono wa kulia kisha kugusanisha kidole gumba na cha shahada kisha ku-snap na kutoa sauti


Kwenye moja ya pango la himaya hiyo ulisikika mburuzo na sauti ya mtu kulalama maumivu na palepale kwenye lango la pango alionekana mtu mwenye sura mbovu kama nyanya iliyooza


Alikuwa ameshika mguu wa mtu huku akimburuza bila huruma, mtu aliyekuwa akiburuzwa alikuwa kijana mdogo mwenye umri wa miaka kumi na sita aliyefungwa kamba mwilini asifurukute


"Kiongozi...kiongozi... nisaidie, niokoe jamani!" alikuwa akilia sana kiasi cha kutia huruma


Yule kijana alitupwa karibu na mkuu wa himaya hiyo kisha yule mkuu alisimama na kumuinua kichwa kwa kushika nywele zake


"Kiongozi Shohei nitamuua mwanafunzi wako mmoja halafu tuone kama utaendelea kuleta kiburi" aliongea


"Tafadhali usiniue, nipo tayari kuwa mmoja wa wafuasi wako, nipo tayari kuwa mtumwa wako, tafadhali usiniue!" alilia akiomba kuonewa huruma


"Huyu kijana bila shaka woga umemzidia, ona mpaka ana jikojolea na kuinajisi madhabahu ya mkuu wetu" aliongea mmoja wa wahalifu waliomzunguka shohei


Shohei aliishia kujiambia ni mwanafunzi wa aina gani amemsajili? Hana uaminifu kabisa, hata kama ni muoga ndio kulisaliti dhehebu na kutaka kuwa miongoni mwa maadui? Hata hivyo alielewa alikuwa bado kijana mdogo mwenye ndoto nyingi za kutaka kutimiza ndio maana hakutaka kufa mapema


"Kiongozi Shohei, kwa mwanafunzi muoga kama huyu na msaliti sidhani kama utahoji nikimuua?" aliongea na palepale bila kupoteza muda alizungusha shingo ya kijana yule, na kupoteza maisha papohapo


Shohei moyo ulimdunda paah! akiwa na uso usioelezeka, na palepale mlio wa ding! ulisikika akilini mwake kisha kosei kwa njia ya kifikra alimtaarifu


"Umepoteza mwanafunzi mmoja na kwasababu hiyo umepatiwa misheni ya dharula, waue wote walioko hapo asibaki hai hata mmoja, ili roho ya mwanafunzi huyo ipate amani huko iliko"


"Hehehe! Inaonekana huyu mwanaharamu amekasirika" aliongea kibaraka yule aliyehusika kumburuza kijana aliyesimama karibu na jukwaa alipo mkuu wake mara baada ya kumuona Shohei yupo kimya kana kwamba alikuwa kwenye maombolezo ya kimya kimya


"Unapaswa kushukuru we mwanaharamu, mkuu wetu amekusaidia kushugulika na mwanafunzi wako msaliti" aliendelea kuongea na ile anamaliza sentensi yake tu alishtukia kutobolewa kifuani upande wa moyo kiasi cha upanga kutokelezea mbele


Na nyuma yake alionekana Shohei ambaye alitimiza azma hiyo, haikueleweka upanga ameutoa saa ngapi


"Kibaraka wako alikuwa anapiga domo hovyo, hakuwa na adabu hivyo na imani pia hutonioji kwa kukusaidia kumshughulikia sio?" aliongea Shohei


"Umethubutu kumuua ndugu yangu? Unapaswa kulipia kwa uhai wako!" alimaka mmoja wa wahalifu kwa hasira na kumsogelea Shohei kwa spidi akilenga kumpiga ngumi ya utosi akidhamiria kupasua kichwa chake kwa nguvu za nishati ya mbingu na ardhi


Hata hivyo Shohei alionekana kuwa makini mno kwani alikwepa ngumi ile na kwa wakati huohuo akichannel nguvu za nishati kwenda mguuni mwake na kumsindilia teke lililomrudisha nyuma mita kadhaa, licha ya kuvaa joho, kurusha teke haikuwa tabu kutokana joho kuwa pana


"Acheni kupigana!" ilisikika sauti ya mamlaka na msisimko wa nguvu kusambaa eneo llote kiasi kwamba Shohei alihisi ubaridi kwenye uti wake wa mgongo


“Hakika ustadi wako wa sanaa za mapigano ni wa kipekee sana, nakubali kwa kumuua kibaraka wangu na mimi huwa sipendi kukuza jambo dogo kuwa kubwa. Umebakiwa na wanafunzi arobaini na sita walio mikononi mwangu


Kabidhi shekeli elfu arobaini na sita kwa wote kisha kila mmoja ashike njia yake” aliongea mkuu yule


Shohei alijiambia inaonekana huyu mkuu ana shida sana na pesa, kwani alikuwa tayari kupoteza kibaraka wake kwa ajili ya pesa Hata hivyo haikumshangaza sana


"Nimeshasema na narudia tena kusema, Shekeli moja kama ada ya malezi hakuna maridhiano"


"We mshenzi..!" alikunja ndita huku akijizuia hasira


"Mkuu niachie mimi hii kazi, nitamuua kisha tunamsachi tu nguo zake na kama tukikosa bila shaka ndani ya dhehebu lake kutakuwa na za kutosha" aliongea yule mtu aliyedhamiria kumpasua kichwa mwanzo


"kuwa makini, inaonekana huyu kijana ana kasi kubwa" mkuu yule alimruhusu


"Usiwaze sana mkuu wangu hawezi kunizidi kasi" alimjibu mkuu wake


"Usimuonyeshee huruma, mpatie kifo chenye maumivu kulipiza kisasi kwa wenzetu waliotangulizwa kwa mkono wake!" aliongea mmoja wa wahalifu akionekana kuwa chawa na asiye na mafunzo ya kinishati


"Mvunje mifupa huyo ya kila mwili aone ya maumivu!" aliongea chawa mwingine


Upande wa Shohei hakujisumbua hata kuwasikiliza zaidi ya kutulia tuli akitazamana na yule mtu, alijiambia kwa muonekano wake wa kibaunsa bila shaka atakuwa ni aina ya wale wanaotumia uzito wa miili kushambulia hivyo kudili naye ni suala la kufumba na kufumbua tu


Lile baunsa alikuwa akitumia mafunzo ya nishati, alikaa mkao wa kuwa tayari kwa pambano kisha alichannel nishati za mbingu na ardhi katika mishipa yake kuongeza kasi ya msukumo wa damu na kwa uwepesi wa hali ya juu kama unyoya wa kuku alimsogelea Shohei akimtandika ngumi ya kifua iliyomrusha mita kadhaa na kujibamiza mgongo kwenye moja ya nguzo za mbao eneo hilo na kuanguka chini


"Sh*t anaspidi kali" aliongea huku akitema damu mdomoni kisha kwa msaada wa upanga alioushika alijinyanyua na kusimama wima


Alionekana kumchukulia poa sana mshindani wake na palepale alikumbuka sheria ya kwanza kwenye pambano aliyowahi kujifunza kwa njia ngumu.


Kwamba usimdharau adui yako hata kama anaonekana mdhaifu mbele yako, kwani hata chui wa milia awindapo hadharau kitoweo chake hata kama ni sungura mdogo


Alijiambia anapaswa kuwa kama Chui wa milia na palepale alikaa mkao wa utayari wa kupambana awamu hio akiwa na sura ya kazi kwelikweli kuliko mwanzo


Kufumba na kufumbua Shohei kwa spidi ya hali ya juu baada ya kuamsha nguvu zake za nishati alimsogelea


"Shwaah! Shwiih! Swiiih! Shwuush!" ilikuwa ni milio ya upanga kukata hewa, kwani mshindani wake alionekana kuwa na spidi kubwa kumzidi bado hivyo alikwepa mashambulizi ya Shohei bila tabu


"Una spidi ndogo sana, ngoja nikuonyeshe maana halisi ya kuwa na spidi kali" aliongea mtu yule na palepale alianza kumzunguka Shohei kws kasi ya ajabu na kuonekana kana kwamba anazungukwa na kimbunga


"Inaonekana ameimarika karltika mbinu ya hatua saba za kimbunga kuliko mwanzo" aliongea mkuu wa himaya akiangalia pambano kwa namna ya kuridhika


"Ni kweli hata mimi pia kwa spidi yake ya sasa inanipa wakati mgumu kidogo kuendana naye" alimuunga mkono mmoja wa kibaraka wake aliyesimama nyuma yake upande wa kushoto


"Haijalishi huyo kiongozi ana utaalamu gani ila mbele ya spidi kubwa ni bure tu!" aliendelea


Upande wa Shohei aliyekuwa akizungukwa kwa spidi aliishia tu kutabasamu na kuushika upanga ule wa maafa imara kisha kwa spidi alifanya shambulizi kama anajaribu kuchoma upepo


Na palepale kichwa cha yule nmtu kilitenganishwa na shingo yake huku damu nyingi zikiruka kwa kasi kama bomba lililofunguliwa maji


"Spidi yako ni kubwa sana kiasi kwamba unashindwa hata kuicontrol, kwani hujui kukata kona? Kulikuwa na ulazima wa kulivamia psnga langu? ona sasa ulivyokufa kizembe!" aliongea bila hatia yoyote


Ukweli alichofanya ni kuegesha tu upanga usawa wa shingo kwenye mzunguko wa yule mtu na kutokana na kazi asingeweza kuepuka kulivamia panga lake, ni kama alikuwa akiwaonyeshea udhaifu wa hiyo mbinu yao


Yule mtu aliyepoteza uhai alikuwa ni miongoni mwa wale watu nane waliosimama nyuma ya mkuu wao, hivyo idadi kupungua na kubaki saba


Hivyo baada ya kuona mwenzao ameuawa kirahisi hivyo walikasirika na kumuona Shohei kuwa tishio na wote kwa pamoja waliamua kumshambulia wakimzunguka pande zote


Shohei alionekana kushtukia hilo mapema na palepale alisafirisha nguvu za nishati kwenda miguuni mwake na kuruka juu urefu wa kama mita thelathini na ushee na wakati akiwa hewani aliachia mashambulizi ya mawimbi yenye makali kama upanga hivyo hawakuwa na jinsi zaidi ya kujikinga na mashambulizi hayo na kurudi nyuma


"Kwahiyo mmeona mnishambulie kwa pamoja baada ya kuona kila mmoja haniwezi?, inaonekana sina jinsi zaidi ya kutumia ile mvinu" aliongea Shohei baada ya kutua ardhini


Kisha palepale baada ya kuchezesha mkono hewani ilitokea karatasi nyeupe yenye michoro na maneno ya ajabu, ilikuwa ni ile talasimu ya ufunguzi wa muhuri kwa upanga huo wa maafa


Na bila kupoteza muda aliipigisha ile talasimu kwenye upanga wake na ile talasimu kugeuka moshi na moshi ule kuuvamia upanga huo


Kilikuwa ni kitendo cha sekunde tano kwa kutoa talasimu kwenye mfumo na kuigusanisha na upaga ule, kisha sekunde tatu zingine upanga ule ulianza kutoa mwanga mkali kiasi cha kufunika eneo lote wasipate kuona vizuri


"Inaonekana alikuwa amebeba siraha ya kimiujiza" alijiwazia mkuu wa himaya hiyo huku akikinga macho yake kwa mkono kutokana na mwanga kuwa mkali


Sekunde ambayo mwanga ule mkali unapotea mkuu huyo alishtukia ncha ya upanga ule kuwa karibu na uso wake


Kilichomshangaza ni umbali uliopo kati Shohei na yeye, umbali wa mita arobaini, kilichomvchangaza zaidi ni msisimko uliokuwa ukitoa, na ule ni msisimko ulimfanya kutetemeka bila kupenda, kupumua nako kulikuwa ni kwa tabu sana kutokana na mkandamizo wa hewa


Hisia alizokuwa akizipata ni kana kwamba upanga huo una uhai ndani yake, na upanga kuwa ni kiumbe cha kutisha


Mara aligundua kitu kingine tena kilichozidi kumuogopesha zaidi, ni kuwa watu wake wote walikuwa wamekufa miili yao ikiwa chini imetenganishwa kwa kukatwa viuno. Damu nyingi zilikuwa zimetapakaa ardhini


"Kwahiyo hii ndio nguvu iliyojificha ya huu upaga wa maafa? Lakini urefu wa mita arobaini ni mrefu kishenzi" alijiongelesha, ilioneka upanga ule uliongezeka urefu na makali






**********
 
Screenshot_20260312-150401.png


Welcome to Faaihinet. Jamiiforum kufungua sometime inakataa

Unasoma free
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom