SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 422
- 1,314
Simulizi: ๐๐๐๐๐๐
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Sehemu ya...........01
๐๐๐๐๐๐
Wingu kubwa jeusi, radi na miungurumo ya hapa na pale ilikuwa imeshika kasi na kufunika mlima mkubwa maarufu kama mliwa wa Zaron. Karibu na kilele cha mlima huo kulikuwa na pango moja kubwa lenye upana na umbali mrefu kuingia ndani mithiri ya zile barabara za chini za treni. Moshi mwingi ulionekana ukifuka kutokea ndani ya pango hilo la kutisha. Ndani kabisa ya pango hilo mzee mmoja aliyevalia mavazi meupe, kofia ya kifalme iliyotengenezwa kwa dhahabu ilikuwa imekipamba kichwa chake chenye mvi, mkononi mwake alikuwa na mkongojo wenye rangi nyeupe pia alionekana akiwa amesimama kwa unyenyekevu mkubwa mbele ya sanamu kubwa lenye muundo wa kichwa cha mnyama wa ajabu mwenye pembe tatu ndefu. Mdomo wa sanamu hilo ndipo ulipokuwa ukitoka ule moshi ulioonekana nje na kusambaa karibu maeneo yote ya mlima wa Zaron.
"Mtihani ulionipa ni mkubwa sana Mungu wangu, kwa nini umeruhusu nipitie haya yote, umeninyang'anya ufalme wangu, ukaruhusu watu wangu waangamizwe na maadui zetu, bado haitoshi ukanitenga mbali na ndugu zangu, nilikuja hapa na kulia mbele zako ukaniahidi ukasema vita ya leo hii ni lazima nitashinda na kurudisha ufalme wangu uliopotea, lakini tazamana kilichotokea mambo ni tofauti kabisa, kwa nini umeruhusu nipitie haya Mungu wa Zaron" Yule mzee mwenye mavazi meupe alikuwa akiongea kwa uchungu wakati huo akiwa amepiga magoti mbele ya lile sanamu kubwa na kuinua mikono yake juu.
Kimya kilitawala kwa muda na mara sauti kubwa nzito na ya kutisha iliyoambatana na mungurumo pamoja na ongezeko kubwa la moshi kutoka kwenye mdomo wa lile sanamu ilisikika ikisema.
"Mfalme Luther, yote unayoyapitia imetokana na uzembe wa kushindwa kuwaongoza watu wako. Makosa yamekuwa ni mengi mno Luther, hebu tazama ni siku chache zimepita ulikuja hapa na kulia mbele zangu nikakuahidi kama hakutakuwa kosa jingine basi utashinda vita yako na kuurejesha ufalme wako mikononi mwako leo lakini unajua nini kimetokea? Umekosa tena Luther"
"Hapana, nimejitahidi sana kulinda heshima na ahadi zangu kwako sijafanya kosa lolo...."
"NYAMAZAAAAAAA!!" Sauti ya kile kiumbe kisichoonekana kutoka kwenye ile sanamu ya kichwa cha mnyama ilisikika ikifoka kiasi cha kusababisha radi na miungurumo mikali kuongezeka na kutetemesha mlima wote wa Zaron.
Binti mmoja aliyekuwa amevalia mavazi ya vita akiwa na mlinzi wake nje pango hilo alionekana kuogopeshwa sana na hali hiyo.
"Baba" alisema yule binti huku akionekana mwenye hofu sana akataka kuingia ndani ya lile pango lakini yule mlinzi alisimama mbele yake kumzuia.
"Lilitha usifanye hivyo, hii ni hali ya kawaida sana huwa inatokea kila wakati baba yako anapokuja kuongea na Mungu wa Zaron usiogope atatoka salama" Alisema yule mlinzi
"Unataka kumaanisha nini? Unafikiri ni mara yangu ya kwanza kuja hapa?" binti Lilitha aliongea kwa kufoka macho yake yakabadilika rangi na kuwa ya bluu, hii ilikuwa ni ishara tosha kuwa watu hawa hawakuwa viumbe wa kawaida.
"Nisamehe Lilitha lakini kumbuka mfalme Luther alisema nisikuruhusu uingie hata iwaje" Yule mlinzi aliendelea kushikilia msimamo wake na hapo Lilitha alikuwa mpole na macho yake yakabadilika na kurudi katika hali ya kawaida.



Hali iliendelea kuwa ni tete ndani ya pango kulipokuwa kukiendelea mazungumzo kati ya Mfalme Luther na Mungu wa Zaron.
"Nimesema NYAMAZAAAAAAA... Watu wako bado wanaendelea kufanya makosa kila siku, kuna mtu wako mmoja hayupo hapa kaenda ulimwengu mwingine anaua viumbe wasio na hatia kinyume kabisa na kanuni na taratibu zetu"
Maneno haya kutoka kwa Mungu wa Zaron yalimfanya mfalme Luther abaki kinywa wazi, zilikuwa ni taarifa zilizomshtua na wala hakutegemea kabisa kusikia kitu kama hicho.
"Kuna mtu wangu yupo ulimwenguni mwingine kivipi!?" Mfalme Luther alijiuliza mwenyewe huku mdomo wake ukiwa wazi, haikuwa rahisi kuamini.
"Hakikisha unamdhibiti huyo mtu wako mapema kabla hajaleta maafa katika ulimwengu wa watu wengine, mambo yanaweza kuwa mazito sana zaidi ya unavyofikiri Luther, haya inuka hapo na uondoke ONDOKAAAAAA" ilifoka ile sauti, kwa mara nyingine tena radi na muungurumo mkali ukatokea.
Kwa mara nyingine tena binti wa mfalme Lilitha alijikuta uvumilivu unamshinda, akaanza kupiga hatua kuingia ndani ya lile pango lakini yule mlinzi alifika haraka na kusimama mbele yake.
" Lilitha tafadhali jaribu kuwa muelewa" alisema yule mlinzi lakini Lilitha hakutaka kupoteza muda alirudisha mkono wake nyuma na kuupeleka mbele kwa nguvu hata kabla hajamgusa yule mlinzi alirushwa umbali mrefu na kwenda kujigonga kwenye ukuta wa lile pango akaanguka chini huku akiwa amejeruhiwa kwenye baadhi ya maneno ya mwili wake, damu yenye rangi ya bluu ikawa inamtoka.
Lilitha aliendelea kwenda mbele lakini ajabu yule mlinzi aliinuka kama radi na kuruka umbali mrefu akatua mbele ya Lilitha. Lilitha alipo jaribu kumsukuma tena kama awali yule mlinzi alimkwepa na kumzunguuka nyuma kwa kasi kama umeme. Wakati huo kila mmoja macho yake yalikuwa yamebadilika na kuwa na mwanga wa bluu sio mlinzi wala sio Lilitha wote walikuwa katika hali hiyo.
"Mnafanya ujinga gani hapo acheniii" Mara sauti kali kutoka ndani ya lile pango ilisikika wote wakageuka kutazama, alikuwa ni Mfalme Luther.
"Baba" Lilitha aliita huku akikimbia na kusimama mbele ya baba yake, alionekana mwenywe shauku ya kujua ni nini kimetokea. Sura yenye huzuni na muonekano wa baba yake vilitosha kumthibitishia kuwa mambo hayakuwa shwari kabisa.
"Binti yangu" Mfalme Luther aliita kwa sauti iliyojaa simanzi.
"Ndio baba, nini kimetokea? Mungu wa Zaron kasemaje?"
"Kuna kosa kubwa tumefanya mwanangu, kosa kubwa sana"
"Kosa gani tena baba? Mbona tulihakikisha kila kitu kinakuwa sawa?"
"Kuna mtu wetu kaondoka ameenda ulimwengu mwingine, anaua watu wasio na hatia. Mungu wa Zaron kakasirika sana kaagiza tumrudishe haraka kama si hivyo basi mambo yatazidi kuwa magumu kwetu na mwisho taifa langu litaangamizwa lote"
Kauli hiyo ilionekana kumshangaza sana Lilitha, taratibu aligeuka nyuma na kumtazama mlinzi wake, wakatazamana kwa sekunde kadhaa mwisho yule mlinzi akainamisha macho yake chini.
"Kuna nini?" Aliuliza Mfalme Luther baada ya kuona kuna kitu hakipo sawa kati ya binti yake Lilitha na mlinzi.
"Baba" Lilitha aliita
"Ndiyo mwanangu"
"Mlinzi aliniambia kuwa kaka Damon hayupo alitoroka tangu usiku wa juzi tulipokuwa tunajiandaa na vita mpaka sasa hajaonekana"
Alisema Lilitha taarifa iliyomfanya Mfalme Luther atoe macho kwa mshangao.
"Eti nini? Kaka yako Damon ametoroka kivipi yani! Si tulimfunga na kuweka ulinzi wa kutosha kivipi tena unasema ametoroka"
"Ilikuwa ni usiku sana, tulishangaa nguvu zake zimerudi ghafula akakata minyororo yote na kisha kuwashambulia walinzi wetu wote baada ya hapo alitoweka" Yule mlinzi alieleza.
Maelezo hayo yalimfanya Mfalme Luther apige hatua na kusimama mbele ya yule mlinzi.
"Kwa nini hamkuniambia? " Mfalme Luther aliuliza kwa hasira huku kidevu chake chenye mvi nyingi kikicheza cheza kwa hasira.
"Mfalme wangu, ulikuwa ukijiandaa na vita ya muhimu sana kwa taifa lako hivyo tuliona tusikusumbue, tulimtuma Raffat afuatilie nina imani atarudi hapa na majibu, tutamrudisha Damon nakuahidi hivyo mtukufu Mfalme" Mlinzi alieleza huku akitetemeka kwa hofu.
Mfalme aliondoka bila kusema chochote, akapiga hatua na kwenda kupanda moja kati ya farasi waliokuwa wamefungwa chini ya mti.
"Mleteni Raffat kwangu mara moja" Alisema Mfalme Luther na hapo akavuta kamba za farasi na kuondoka kwa kasi.



Nusu saa baadae ndani ya hema moja kati ya mengi yaliyokuwa yamejengwa chini na mlima wa Zaron, Mfalme Luther alionekana ameketi katika kiti chake cha kifalme huku akiwa amezunguukwa na walinzi na pembeni yake alikaa binti yake mrembo na mpendwa Lilitha. Mbele yake alikuwepo mwaume mmoja aliyevaa vazi la kivita kiunoni akiwa na upanga mrefu kwenye ara yake. Huyu aliitwa Raffat kiongozi wa ulinzi wa mipaka ya ufalme wa taifa la Mfalme Luther. Raffat alikuwa akitoa taarifa mara baada ya kupewa kazi ya kumfuatilia Damon kaka yake Lilitha ambaye ni mtoto wa kiume wa mfalme Luther.
"Mfalme kama unavyojua Damon aliathirika sana kiakili mara baada ya kuupoteza ufalme wetu na watu wengi kuuwawa kipindi kile hivyo alikuwa ni mtu asiyetulia na aliwaza kisasi mda wote, kama utakumbuka katika vita ile walimuua mpenzi wake Zuzuya hivyo Damon hawezi kutulia anataka kulipa kisasi licha ya kumfungia na kumzuia asitumie nguvu zake lakini Damon amepambana amerudisha nguvu zake na kutoroka" alieleza Raffat
"Acha kueleza mambo ninayoyajua sema Raffat yuko wapi kwa sasa"
Alisema Mfalme Luther baada ya kumsikiliza Raffat kwa muda mrefu.
"Sawa Mfalme, kama utakumbuka watu waliotuvamia na kuua ndugu zetu kipindi kile mpaka sasa hawajulikani ni wa wapi ila walikuwa wamevaa vizibao vya rangi ya KIJANI, Damon amekuwa akihangaika kuzunguuka kila kona ya ulimwengu kuwatafuta kwa bahati mbaya amefika hadi Duniani. Kama tunavyojua akili ya Damon haiko sawa kabisa, kuna nchi moja iko afrika inaitwa Tanzania hivi sasa ipo katika zoezi muhimu la kuhesabu watu wanaita Sensa, watu wanaofanya zoezi hilo wanavaa reflector'/ vizibao vya kijani sawa kabisa na walivyovaa wale watu waliokuja kutuvamia. Tarehe 22 ilikuwa ni siku ya ufunguzi wa Sensa watu wengi sana wanaoitwa Makarani walivaa hivyo vizibao karibu nchi nzima kama ufunguzi wa tukio hilo la muhimu kwa nchi yao. kwa bahati mbaya siku hiyo Damon ndio alikuwa anapita akawaona. Akaweka makazi yake hapo Tanzania akiamini amewapata wabaya wake, Tarehe 23 Damon alianza kuwawinda mmoja baada ya mwingine, kila atakae muona amevaa kile kizibao Damon anamuwinda mwisho anamuua kikatiri na kumnywa damu yake. Mpaka sasa tunavyoongea Damon ameua MAKARANI watatu nchini Tanzania, anafanya kazi hii taratibu sana na kama unavyojua WANADAMU wahawezi kunyamaza kimya watataka kupambana nae na hapo mambo yanaweza kuwa magumu zaidi" Raffat alimaliza kueleza.
Mfalme Luther alisimama kwenye kiti chake mara tu baada ya maelezo hayo.
"Hectoooor" Mfalme Luther aliita na hapo akaingia jamaa mmoja wa miraba minne ambaye yeye alionekana kuwa tofauti kabisa na wengine, macho yake yalikuwa ya bluu wakati wote.
"Nipo hapa Mfalme"
"Kusanya jeshi lako haraka, nenda Dunia hakikisha unamkamata Damon na kumrudisha huku haraka" Alisema Luther lakini mara Lilitha akasimama na kupaza sauti.
"Hapana baba"
Watu wote wakageuka na kumtazama Lilitha
"Baba hatuna haja ya kutuma majeshi kwenda Dunia, tutazua taharuki kubwa na huenda wenzetu wakashindwa kutuelewe, tunaweza kuongeza tatizo ndani ya tatizo na pengine hata kudhuru WANADAMU na viumbe wengine wasio na hatia, kumbuka akili ya kaka Damon haiko sawa na siku hizi za karibu Damon ameonekana kuwa na nguvu ya ziada na hatujuo inatoka wapi, baba nitume mimi niende Duniani nakuahidi nitamrudisha kaka Damon ndani ya siku chache tu, yule ni kaka yangu hawezi kunidhuru" Lilitha aliongea kwa kujiamini sana.
Huu ulikuwa ni mtihani mkubwa kwa Mfalme Luther, alimpenda sana binti yake hata siku moja alikuwa hataki kuruhusu Lilitha akae mbali naye, zipo sababu zinazomfanya Mfalme Luther kumpenda sana Lilitha sababu zinazobeba siri nzito sana katika taifa lake.



DUNIANI-AFRICA-TANZANIA
MTWARA- MASASI.
Tukio lingine la kushangaza linatokea nchini Tanzania, ukiacha yale matukio ya kufurahisha ya Makarani kuibiwa vishikwambi wengine kujinyonga na wengine kukataa kufanya kazi sasa kulikuwa na matukio mengine ya kutisha ambayo yalishika macho na masikio ya watu wengi. Ilikuwa ni mfuatano wa mtukio ya kutisha ya kuuwawa kwa MAKARANI wa sensa nchini Tanzania. Mpaka sasa kulikuwa na vifo viwili vya kutisha na vyote vinafanana. Leo tena katika hali ile ile na mazingira yale yale KARANI mwingine wa Sensa mkoani Mtwara - Masasi anakutwa ameuwawa kikatiri na mwili wake kutupwa pembezoni kwa barabara.
Hofu,simanzi na sintofahamu inatanda nchini Tanzania. Kila mmoja anakosa majibu ni nini hasa chanzo cha mauaji hayo ya kutisha. Hata serikali yenyewe inajikuta katika mazingira magumu, kabla haijamaliza kupeleleza kifo hiki mara kifo cha KARANI mwingine kinatokea. Hali inakuwa ya kutisha tena ya kutisha sana. Taratibu Makarani wengine wanaanza kuingiwa na hofu ya kufanya kazi yao jambo linalopelekea zoezi muhimu la serikali yaani Sensa ya watu na makazi kuwa gumu.
Je nini kitatokea?
FUATILIA SIMULIZI HII YENYE KISA CHA KUSISIMUA NA LOVE STORY NZURI NDANI YAKE...
Mtunzi: Saul David
Simu: 0756862047....
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
Sehemu ya...........01
๐๐๐๐๐๐
Wingu kubwa jeusi, radi na miungurumo ya hapa na pale ilikuwa imeshika kasi na kufunika mlima mkubwa maarufu kama mliwa wa Zaron. Karibu na kilele cha mlima huo kulikuwa na pango moja kubwa lenye upana na umbali mrefu kuingia ndani mithiri ya zile barabara za chini za treni. Moshi mwingi ulionekana ukifuka kutokea ndani ya pango hilo la kutisha. Ndani kabisa ya pango hilo mzee mmoja aliyevalia mavazi meupe, kofia ya kifalme iliyotengenezwa kwa dhahabu ilikuwa imekipamba kichwa chake chenye mvi, mkononi mwake alikuwa na mkongojo wenye rangi nyeupe pia alionekana akiwa amesimama kwa unyenyekevu mkubwa mbele ya sanamu kubwa lenye muundo wa kichwa cha mnyama wa ajabu mwenye pembe tatu ndefu. Mdomo wa sanamu hilo ndipo ulipokuwa ukitoka ule moshi ulioonekana nje na kusambaa karibu maeneo yote ya mlima wa Zaron.
"Mtihani ulionipa ni mkubwa sana Mungu wangu, kwa nini umeruhusu nipitie haya yote, umeninyang'anya ufalme wangu, ukaruhusu watu wangu waangamizwe na maadui zetu, bado haitoshi ukanitenga mbali na ndugu zangu, nilikuja hapa na kulia mbele zako ukaniahidi ukasema vita ya leo hii ni lazima nitashinda na kurudisha ufalme wangu uliopotea, lakini tazamana kilichotokea mambo ni tofauti kabisa, kwa nini umeruhusu nipitie haya Mungu wa Zaron" Yule mzee mwenye mavazi meupe alikuwa akiongea kwa uchungu wakati huo akiwa amepiga magoti mbele ya lile sanamu kubwa na kuinua mikono yake juu.
Kimya kilitawala kwa muda na mara sauti kubwa nzito na ya kutisha iliyoambatana na mungurumo pamoja na ongezeko kubwa la moshi kutoka kwenye mdomo wa lile sanamu ilisikika ikisema.
"Mfalme Luther, yote unayoyapitia imetokana na uzembe wa kushindwa kuwaongoza watu wako. Makosa yamekuwa ni mengi mno Luther, hebu tazama ni siku chache zimepita ulikuja hapa na kulia mbele zangu nikakuahidi kama hakutakuwa kosa jingine basi utashinda vita yako na kuurejesha ufalme wako mikononi mwako leo lakini unajua nini kimetokea? Umekosa tena Luther"
"Hapana, nimejitahidi sana kulinda heshima na ahadi zangu kwako sijafanya kosa lolo...."
"NYAMAZAAAAAAA!!" Sauti ya kile kiumbe kisichoonekana kutoka kwenye ile sanamu ya kichwa cha mnyama ilisikika ikifoka kiasi cha kusababisha radi na miungurumo mikali kuongezeka na kutetemesha mlima wote wa Zaron.
Binti mmoja aliyekuwa amevalia mavazi ya vita akiwa na mlinzi wake nje pango hilo alionekana kuogopeshwa sana na hali hiyo.
"Baba" alisema yule binti huku akionekana mwenye hofu sana akataka kuingia ndani ya lile pango lakini yule mlinzi alisimama mbele yake kumzuia.
"Lilitha usifanye hivyo, hii ni hali ya kawaida sana huwa inatokea kila wakati baba yako anapokuja kuongea na Mungu wa Zaron usiogope atatoka salama" Alisema yule mlinzi
"Unataka kumaanisha nini? Unafikiri ni mara yangu ya kwanza kuja hapa?" binti Lilitha aliongea kwa kufoka macho yake yakabadilika rangi na kuwa ya bluu, hii ilikuwa ni ishara tosha kuwa watu hawa hawakuwa viumbe wa kawaida.
"Nisamehe Lilitha lakini kumbuka mfalme Luther alisema nisikuruhusu uingie hata iwaje" Yule mlinzi aliendelea kushikilia msimamo wake na hapo Lilitha alikuwa mpole na macho yake yakabadilika na kurudi katika hali ya kawaida.



Hali iliendelea kuwa ni tete ndani ya pango kulipokuwa kukiendelea mazungumzo kati ya Mfalme Luther na Mungu wa Zaron.
"Nimesema NYAMAZAAAAAAA... Watu wako bado wanaendelea kufanya makosa kila siku, kuna mtu wako mmoja hayupo hapa kaenda ulimwengu mwingine anaua viumbe wasio na hatia kinyume kabisa na kanuni na taratibu zetu"
Maneno haya kutoka kwa Mungu wa Zaron yalimfanya mfalme Luther abaki kinywa wazi, zilikuwa ni taarifa zilizomshtua na wala hakutegemea kabisa kusikia kitu kama hicho.
"Kuna mtu wangu yupo ulimwenguni mwingine kivipi!?" Mfalme Luther alijiuliza mwenyewe huku mdomo wake ukiwa wazi, haikuwa rahisi kuamini.
"Hakikisha unamdhibiti huyo mtu wako mapema kabla hajaleta maafa katika ulimwengu wa watu wengine, mambo yanaweza kuwa mazito sana zaidi ya unavyofikiri Luther, haya inuka hapo na uondoke ONDOKAAAAAA" ilifoka ile sauti, kwa mara nyingine tena radi na muungurumo mkali ukatokea.
Kwa mara nyingine tena binti wa mfalme Lilitha alijikuta uvumilivu unamshinda, akaanza kupiga hatua kuingia ndani ya lile pango lakini yule mlinzi alifika haraka na kusimama mbele yake.
" Lilitha tafadhali jaribu kuwa muelewa" alisema yule mlinzi lakini Lilitha hakutaka kupoteza muda alirudisha mkono wake nyuma na kuupeleka mbele kwa nguvu hata kabla hajamgusa yule mlinzi alirushwa umbali mrefu na kwenda kujigonga kwenye ukuta wa lile pango akaanguka chini huku akiwa amejeruhiwa kwenye baadhi ya maneno ya mwili wake, damu yenye rangi ya bluu ikawa inamtoka.
Lilitha aliendelea kwenda mbele lakini ajabu yule mlinzi aliinuka kama radi na kuruka umbali mrefu akatua mbele ya Lilitha. Lilitha alipo jaribu kumsukuma tena kama awali yule mlinzi alimkwepa na kumzunguuka nyuma kwa kasi kama umeme. Wakati huo kila mmoja macho yake yalikuwa yamebadilika na kuwa na mwanga wa bluu sio mlinzi wala sio Lilitha wote walikuwa katika hali hiyo.
"Mnafanya ujinga gani hapo acheniii" Mara sauti kali kutoka ndani ya lile pango ilisikika wote wakageuka kutazama, alikuwa ni Mfalme Luther.
"Baba" Lilitha aliita huku akikimbia na kusimama mbele ya baba yake, alionekana mwenywe shauku ya kujua ni nini kimetokea. Sura yenye huzuni na muonekano wa baba yake vilitosha kumthibitishia kuwa mambo hayakuwa shwari kabisa.
"Binti yangu" Mfalme Luther aliita kwa sauti iliyojaa simanzi.
"Ndio baba, nini kimetokea? Mungu wa Zaron kasemaje?"
"Kuna kosa kubwa tumefanya mwanangu, kosa kubwa sana"
"Kosa gani tena baba? Mbona tulihakikisha kila kitu kinakuwa sawa?"
"Kuna mtu wetu kaondoka ameenda ulimwengu mwingine, anaua watu wasio na hatia. Mungu wa Zaron kakasirika sana kaagiza tumrudishe haraka kama si hivyo basi mambo yatazidi kuwa magumu kwetu na mwisho taifa langu litaangamizwa lote"
Kauli hiyo ilionekana kumshangaza sana Lilitha, taratibu aligeuka nyuma na kumtazama mlinzi wake, wakatazamana kwa sekunde kadhaa mwisho yule mlinzi akainamisha macho yake chini.
"Kuna nini?" Aliuliza Mfalme Luther baada ya kuona kuna kitu hakipo sawa kati ya binti yake Lilitha na mlinzi.
"Baba" Lilitha aliita
"Ndiyo mwanangu"
"Mlinzi aliniambia kuwa kaka Damon hayupo alitoroka tangu usiku wa juzi tulipokuwa tunajiandaa na vita mpaka sasa hajaonekana"
Alisema Lilitha taarifa iliyomfanya Mfalme Luther atoe macho kwa mshangao.
"Eti nini? Kaka yako Damon ametoroka kivipi yani! Si tulimfunga na kuweka ulinzi wa kutosha kivipi tena unasema ametoroka"
"Ilikuwa ni usiku sana, tulishangaa nguvu zake zimerudi ghafula akakata minyororo yote na kisha kuwashambulia walinzi wetu wote baada ya hapo alitoweka" Yule mlinzi alieleza.
Maelezo hayo yalimfanya Mfalme Luther apige hatua na kusimama mbele ya yule mlinzi.
"Kwa nini hamkuniambia? " Mfalme Luther aliuliza kwa hasira huku kidevu chake chenye mvi nyingi kikicheza cheza kwa hasira.
"Mfalme wangu, ulikuwa ukijiandaa na vita ya muhimu sana kwa taifa lako hivyo tuliona tusikusumbue, tulimtuma Raffat afuatilie nina imani atarudi hapa na majibu, tutamrudisha Damon nakuahidi hivyo mtukufu Mfalme" Mlinzi alieleza huku akitetemeka kwa hofu.
Mfalme aliondoka bila kusema chochote, akapiga hatua na kwenda kupanda moja kati ya farasi waliokuwa wamefungwa chini ya mti.
"Mleteni Raffat kwangu mara moja" Alisema Mfalme Luther na hapo akavuta kamba za farasi na kuondoka kwa kasi.



Nusu saa baadae ndani ya hema moja kati ya mengi yaliyokuwa yamejengwa chini na mlima wa Zaron, Mfalme Luther alionekana ameketi katika kiti chake cha kifalme huku akiwa amezunguukwa na walinzi na pembeni yake alikaa binti yake mrembo na mpendwa Lilitha. Mbele yake alikuwepo mwaume mmoja aliyevaa vazi la kivita kiunoni akiwa na upanga mrefu kwenye ara yake. Huyu aliitwa Raffat kiongozi wa ulinzi wa mipaka ya ufalme wa taifa la Mfalme Luther. Raffat alikuwa akitoa taarifa mara baada ya kupewa kazi ya kumfuatilia Damon kaka yake Lilitha ambaye ni mtoto wa kiume wa mfalme Luther.
"Mfalme kama unavyojua Damon aliathirika sana kiakili mara baada ya kuupoteza ufalme wetu na watu wengi kuuwawa kipindi kile hivyo alikuwa ni mtu asiyetulia na aliwaza kisasi mda wote, kama utakumbuka katika vita ile walimuua mpenzi wake Zuzuya hivyo Damon hawezi kutulia anataka kulipa kisasi licha ya kumfungia na kumzuia asitumie nguvu zake lakini Damon amepambana amerudisha nguvu zake na kutoroka" alieleza Raffat
"Acha kueleza mambo ninayoyajua sema Raffat yuko wapi kwa sasa"
Alisema Mfalme Luther baada ya kumsikiliza Raffat kwa muda mrefu.
"Sawa Mfalme, kama utakumbuka watu waliotuvamia na kuua ndugu zetu kipindi kile mpaka sasa hawajulikani ni wa wapi ila walikuwa wamevaa vizibao vya rangi ya KIJANI, Damon amekuwa akihangaika kuzunguuka kila kona ya ulimwengu kuwatafuta kwa bahati mbaya amefika hadi Duniani. Kama tunavyojua akili ya Damon haiko sawa kabisa, kuna nchi moja iko afrika inaitwa Tanzania hivi sasa ipo katika zoezi muhimu la kuhesabu watu wanaita Sensa, watu wanaofanya zoezi hilo wanavaa reflector'/ vizibao vya kijani sawa kabisa na walivyovaa wale watu waliokuja kutuvamia. Tarehe 22 ilikuwa ni siku ya ufunguzi wa Sensa watu wengi sana wanaoitwa Makarani walivaa hivyo vizibao karibu nchi nzima kama ufunguzi wa tukio hilo la muhimu kwa nchi yao. kwa bahati mbaya siku hiyo Damon ndio alikuwa anapita akawaona. Akaweka makazi yake hapo Tanzania akiamini amewapata wabaya wake, Tarehe 23 Damon alianza kuwawinda mmoja baada ya mwingine, kila atakae muona amevaa kile kizibao Damon anamuwinda mwisho anamuua kikatiri na kumnywa damu yake. Mpaka sasa tunavyoongea Damon ameua MAKARANI watatu nchini Tanzania, anafanya kazi hii taratibu sana na kama unavyojua WANADAMU wahawezi kunyamaza kimya watataka kupambana nae na hapo mambo yanaweza kuwa magumu zaidi" Raffat alimaliza kueleza.
Mfalme Luther alisimama kwenye kiti chake mara tu baada ya maelezo hayo.
"Hectoooor" Mfalme Luther aliita na hapo akaingia jamaa mmoja wa miraba minne ambaye yeye alionekana kuwa tofauti kabisa na wengine, macho yake yalikuwa ya bluu wakati wote.
"Nipo hapa Mfalme"
"Kusanya jeshi lako haraka, nenda Dunia hakikisha unamkamata Damon na kumrudisha huku haraka" Alisema Luther lakini mara Lilitha akasimama na kupaza sauti.
"Hapana baba"
Watu wote wakageuka na kumtazama Lilitha
"Baba hatuna haja ya kutuma majeshi kwenda Dunia, tutazua taharuki kubwa na huenda wenzetu wakashindwa kutuelewe, tunaweza kuongeza tatizo ndani ya tatizo na pengine hata kudhuru WANADAMU na viumbe wengine wasio na hatia, kumbuka akili ya kaka Damon haiko sawa na siku hizi za karibu Damon ameonekana kuwa na nguvu ya ziada na hatujuo inatoka wapi, baba nitume mimi niende Duniani nakuahidi nitamrudisha kaka Damon ndani ya siku chache tu, yule ni kaka yangu hawezi kunidhuru" Lilitha aliongea kwa kujiamini sana.
Huu ulikuwa ni mtihani mkubwa kwa Mfalme Luther, alimpenda sana binti yake hata siku moja alikuwa hataki kuruhusu Lilitha akae mbali naye, zipo sababu zinazomfanya Mfalme Luther kumpenda sana Lilitha sababu zinazobeba siri nzito sana katika taifa lake.



DUNIANI-AFRICA-TANZANIA
MTWARA- MASASI.
Tukio lingine la kushangaza linatokea nchini Tanzania, ukiacha yale matukio ya kufurahisha ya Makarani kuibiwa vishikwambi wengine kujinyonga na wengine kukataa kufanya kazi sasa kulikuwa na matukio mengine ya kutisha ambayo yalishika macho na masikio ya watu wengi. Ilikuwa ni mfuatano wa mtukio ya kutisha ya kuuwawa kwa MAKARANI wa sensa nchini Tanzania. Mpaka sasa kulikuwa na vifo viwili vya kutisha na vyote vinafanana. Leo tena katika hali ile ile na mazingira yale yale KARANI mwingine wa Sensa mkoani Mtwara - Masasi anakutwa ameuwawa kikatiri na mwili wake kutupwa pembezoni kwa barabara.
Hofu,simanzi na sintofahamu inatanda nchini Tanzania. Kila mmoja anakosa majibu ni nini hasa chanzo cha mauaji hayo ya kutisha. Hata serikali yenyewe inajikuta katika mazingira magumu, kabla haijamaliza kupeleleza kifo hiki mara kifo cha KARANI mwingine kinatokea. Hali inakuwa ya kutisha tena ya kutisha sana. Taratibu Makarani wengine wanaanza kuingiwa na hofu ya kufanya kazi yao jambo linalopelekea zoezi muhimu la serikali yaani Sensa ya watu na makazi kuwa gumu.
Je nini kitatokea?
FUATILIA SIMULIZI HII YENYE KISA CHA KUSISIMUA NA LOVE STORY NZURI NDANI YAKE...
Mtunzi: Saul David
Simu: 0756862047....
