Simulizi: Sihusiki

Simulizi: Sihusiki

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
7,147
Reaction score
14,708
Alipoamua siku hiyo kuwa karibu na msichana anayehudumu katika klabu ya Tanga Raha, Jackson Malima ambaye pia alipachikwa jina la ‘Baba Mchungaji’ na wafanyakazi wenzake, hakujua kwamba hatua hiyo ilikuwa chanzo cha mlolongo wa matatizo lukuki; ndoa yake kutetereka, cheo cha ukurugenzi alichopaswa kupewa kuchukuliwa na mtu mwingine, na baya zaidi ni kujikuta akituhumiwa kwa mauaji ambayo hayajui…

Kutoka kwa mtunzi wa 'Gereza la Kifo'
Simu: 0758 143457


sihusik-ii.jpg


JACKSON Malima, alitoka bafuni na kuangalia saa yake iliyomwonesha kwamba inaelekea saa mbili usiku. Akiwa bado amejifunga taulo, aliamua kuangalia taarifa ya habari kabla ya kutoka kama alivyokuwa amepanga.

Kwa takribani siku sita alizokuwa Tanga, alikuwa hajaangalia taarifa ya habari ya usiku kama ilivyo kawaida yake anapokuwa nyumbani kwake Dar es Salaam kutokana na kubanwa na ratiba.

Alipokuwa akitoka kwenye semina jioni, alilazimika ama kuandaa kile atakachowasilisha kesho kwenye semina au kwenda kutafuta chakula cha usiku alikotumia muda huo kubadilishana mawazo na wenzake.

Alishagundua kwamba pale kwenye klabu alipokuwa akienda kupata chakula cha usiku, mbali na kukosa utulivu hata kama angeomba wahusika waweke taarifa ya habari wasingemwelewa kwani kilichokuwa kinapendelewa zaidi na wengi ni mpira wa miguu au muziki.

Aliwasha seti ya runinga katika chumba chake alimofikia katika nyumba ya kulala wageni ya Twiga Executive Lodge na kuketi kitandani.

Taarifa ya habari ilimkaliza chumbani humo hadi saa tatu kasorobo alipozima runinga. Alivaa suruali ya michezo, tisheti ya rangi ya maziwa na raba kisha akatoka baada ya kuhakikisha kwamba hajasahau kuchukua fedha kidogo kwa ajili ya matumizi ya usiku huo.

“Binti, natoka kidogo,” alisema akikabidhi funguo za chumba chake kilichokuwa kimepewa jina la Kigoma kwa binti aliyekuwa mapokezi. Akaondoka.

Nyumba ya kulala wageni aliyofikia, kama zilivyo nyingine nyingi mjini Tanga, ilikuwa haiandai chakula cha mchana wala usiku zaidi ya kifungua kinywa asubuhi. Wateja walikuwa wakielekezwa kwenda kutafuta chakula katika hoteli, klabu au migahawa ya karibu.

Chakula cha mchana, Jackson na wanasemina wenzake walikuwa wakikipata katika Hoteli ya Kitalii ya Mkonge walikokuwa wakifanyia semina yao ya wiki moja ambayo sasa ilikuwa inaelekea ukingoni, huku yeye na wenzake wakilazimika kujitafutia chakula cha usiku. Jackson alikuwa ameamua kukaa katika nyumba hiyo ya wageni kutokana na kuwa eneo tulivu huku wenzake wanne aliotoka nao ofisi moja wakiamua kukaa katika nyumba za wageni zilizoko katikati ya jiji la Tanga.

Hao wenzake walikuwa wanywaji wa pombe na wapenda wanawake lakini yeye alikuwa akijitahidi sana kujitenga na mambo hayo, hali iliyofanya apachikwe na baadhi ya wafanyakazi wenziye jina la Baba Mchungaji.

Hata hivyo, baada ya semina mara nyingi alikuwa anakutana na wenzake hao pamoja na wanasemina kutoka taasisi zingine zilizokuwa zinashiriki kwenye semina hiyo usiku katika klabu ya Tanga Raha ambayo haikuwa mbali sana na alikokuwa amefikia.

Klabu hiyo ilikuwa inachangamka sana, hasa nyakati za usiku kutokana na kuandaa vyakula vya aina mbalimbali pamoja na vinywaji. Lakini kitu kilichokuwa kinavutia wateja wengi hususani wanaume ni uwepo wa wasichana warembo, wengi wakiwa ni wale waliojaaliwa kuwa na maumbo halisi ya Kiafrika.

Wasichana vimbaumbau pia walikuwepo wachache lakini wengi walikuwa ni wale ambao utadhani meneja wa klabu hiyo alikuwa akipita nchi nzima akisaka mabinti warefu, wenye sura za kuvutia na makalio makubwa.

Ilikuwa wastani wa takribani dakika nane kutembea kwa miguu kutoka nyumba ya wageni alimofikia Jackson hadi Tanga Raha Club kama bango lake lilivyokuwa linasomeka.

Wakati Jackson anafika kwenye klabu hiyo usiku huo, nje kulikuwa na magari mengi kiasi kwamba yeyote aliyekuwa akija kwa gari muda huo alilazimika kwenda mbali kidogo kuegesha gari lake. Ndani pia palikuwa tayari pamejaa watu kiasi kwamba upatikanaji wa viti ulianza kuwa wa shida.

Jackson alisimama pembeni karibu na mlango mkubwa akiangaza mahala ambapo anaweza kuona kiti aende kukaa. Kwa kawaida mwanga wa ndani ya klabu hiyo ambayo mchana ukipita unaweza kudhani ni godauni au gereji, ulikuwa si mkubwa sana. Wakati mwingine mpaka umkaribie mtu ndipo unamtambua.

Aliangaza huku na kule akitafuta pia kuwaona wanasemina au wafanyakazi wenzake katika Tume ya Teknolojia na Mawasiliano (TTM) ili kuungana nao lakini hakuona yeyote, labda kutokana na mwanga hafifu wa mahala pale. Alikuwa hana hakika pia kama mfanyakazi mwenziye na rafiki yake wa karibu, Andrew Mambo, alikuwa ameshawasili. Alisogea pembeni na kupiga simu yake lakini hakupokea.

Mara aliona wanasemina wawili wakiongozana na walipofika pale alipokuwa amesimama karibu na mlango, wakamsalimia. Wakasema wanahamia kwingine. Alipoangalia mahala walipotokea, akaona watu wengine wakiwahi viti walivyoviacha. Ilikuwa ni sehemu ambayo wapenzi wa mpira wakikaa wanaona vizuri kutokana na skrini kubwa iliyokuwa mahala hapo.

Wakati bado anaangaza macho huku na kule, msichana mmoja, mhudumu wa klabu hiyo, alimfuata na kumshika mkono.

“Habari kaka… Twende nikuoneshe mahala pa kukaa.”

Jackson aliandamana naye, hiyo ikiwa ni mara ya tatu au zaidi kuhudumiwa naye na sasa bila shaka kila mmoja wao alikuwa ameshamkariri sura mwenzake. Ni msichana ambaye kwa mtazamo wake alikuwa mrembo kupita wote katika klabu hiyo. Hata siku ya kwanza alipomwita amhudumie, binti huyo maji ya kunde ‘alimtikisa’ vilivyo Jackson lakini akaheshimu maadili aliyojiwekea.

Ukiwa ni mwaka wa 15 tangu afunge ndoa, Jackson alikuwa hajawahi kwenda nje ya ndoa yake. Mbali ya kumwogopa Mwenyezi Mungu anayewakataza viumbe wake kuzini katika vitabu vyake vyote, Biblia na Kurani, Jackson alikuwa hafikirii kwamba kuna siku atamsaliti mkewe mpenzi, Salome Bakunda. Ni mwanamke aliyempenda na kumridhisha kwa kila hali na hivyo hakuona sababu ya kuchepuka kama alivyokuwa akiona kwa wenzake akiwemo rafiki yake, Andrew.

Isitoshe, yeye alikuwa mshauri mkubwa wa wafanyakazi wenzake, hususani vijana waliokuwa wakianza kazi katika ofisi yao kuhusu kuzingatia maadili bora ya kazi, kujiheshimu, kuacha zinaa na kufanya yanayompendeza Mwenyezi Mungu.

“Kaka, inaonekana wewe hunywi lakini nadhani leo utanipa offer ya bia moja tu, yaani nina kiu sana kaka yangu… Nakuomba,” alisema yule binti baada ya kumpeleka kwenye meza moja iliyokuwa kwenye kona, upande wa kulia wa klabu hiyo kutoka lango kuu la kuingilia. Katika meza hiyo kulikuwa na viti vingine viwili vitupu lakini kule eneo la kuingilia alikokuwa amesimama awali alikuwa hawezi kupaona.

“Bia moja tu mdogo wangu, haya, nitakununulia...”

“Asante sana kaka… Enhe, nikuletee nini?”

“Nitapata kuku nusu wa kienyeji wa kuchoma na ndizi mzuzu mbili za kuchoma pamoja na mbogamboga?”

“Bila shaka kaka,” alijibu yule msichana akiachia tabasamu pana lililoanza kumgusa Jackson. Alitoa Sh 20,000 na kumuuliza kama kiasi hicho cha fedha kinatosha chakula alichoagiza na bia aliyoomba. Alijibu kwa bashasha kwamba kinatosha sana.

“Je, nikitaka soda pia ili niwe navutia muda wakati nasubiri kuku wangu, pesa inatosha?”

“Bado inatosha na chenji inarudi.”

“Basi niletee soda ya moto,” alisema kisha msichana yule ambaye muda wote alikuwa amesimama, akageuka na kuondoka.

Sasa Jackson, Mwanasheria Mkuu wa Tume ya Teknolojia na Mawasiliano (TTM), alipata wasaa mzuri wa kumtazama kwa nyuma na kung’amua kwamba uumbaji wa Mwenyezi Mungu Mtukufu ulikuwa umekamilika vilivyo kwa kiumbe wake huyo.

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia riwaya hii ya kusisimua...
 
SIHUSIKI - 2

Aliendelea kumsindikiza kwa macho hadi alipopotelea katika eneo la jiko na hivyo akabaki anajiuliza inakuwaje msichana mrembo kiasi kile alikuwa akifanya kazi ile ambayo yeye aliiona dhalili. Kwa mtazamo wake aliona kwamba msichana huyo alipaswa awe ametulia kwa mumewe au akifanya kazi yenye staha zaidi.

“Hivi wazazi wa hawa wasichana walio humu klabu wanaweza kuwa akina nani hasa? Wamewasomesha kiasi gani watoto wao? Je, wameridhia kuona mabinti zao warembo kama huyu wanafanya kazi hii ya kibaamedi?” Alijiuliza lakini akajijibu pia kwamba kimsingi kazi ni kazi tu na katika mgawanyo wa maisha lazima pia kuwe na mgawanyo wa kazi na kwamba kimsingi hakuna kazi dhalili.

Aliuonya pia moyo wake uache kudharau kazi za wengine huku akijiuliza hali ingekuwaje kama kusingekuwa na wahudumu kama huyo binti na wenzake katika klabu hiyo? Pamoja na kukiri kwamba hakuna kazi bora kuliko nyingine bado, hakutaka siku moja watoto wake wawili, wote wa kike, Hellen na mdogo wake Hilda, wafanye kazi ya baa.

Wakati bado akiwaza kuhusu binti huyo na wenzake kwenye klabu hiyo, alimwona akirejea na kisha akaweka chupa ya soda mezani. Akamfungulia soda, akamkaribisha kunywa.

“Naitwa Eggy… Agnes kama utanihitaji… Nitaleta chakula ulichoagiza kikiwa tayari punde, karibu kaka na asante sana.”

“Nilidhani unakuja na wewe kunywea bia yako hapa?” Alijikuta akiuliza neno ambalo wala hakulitegemea na haikuwa kawaida yake.

“Sasa hivi meneja haturuhusu kukaa. Nitakuja tu baadaye kaka, asante sana kwa bia,” alisema Eggy na kumpa chenji iliyobaki, kisha akaondoka. Kama kawaida, Jackson alijikuta tena akiwa na kibarua cha kumsindikiza kwa macho kutokana na kuvutiwa na umbo lake hadi msichana huyo alipoitwa kwenye meza nyingine kwa ajili ya kutoa huduma.

Dakika chache baadaye, Jackson alimwona Mhandisi Mkuu wa TTM, Bruno Mapunda, akipita karibu yake akiwa na mkoba kama vile anatafuta mtu au mahala pa kukaa. Ilionekana kwamba hajafika hotelini alikokuwa amefikia tangu kumalizika kwa semina jioni.

Bruno alimkaribia kabisa lakini akageuka na kwenda uelekeo mwingine bila kumwona au alimwona bila kumtambua. Jackson akashukuru kwa sababu hakutaka kukaa naye kama ilivyokuwa imetokea jana yake ambapo Bruno alilazimisha kwenda kukaa naye. Wawili hao hawakuwa na uhusiano mzuri kazini na hasa kutokana na kila mara Jackson kusikia Bruno akimsema vibaya na kukejeli kila alichokuwa akikifanya.

Baada ya dakika takribani 25 za kusubiri huku muda mwingi akisoma mitandao ya kijamii hususani Facebook na WhatsApp, Jackson alishituliwa na Eggy aliyekuwa akiweka sahani ya nyama ya kuku wa kuchoma kwenye meza aliyokuwa ameketi.

“Nikuletee maji ya kunawa au utakwenda pale kunawa?”

“Nitakwenda mwenyewe. Usiwe na wasiwasi,” alijibu Jackson akinyanyuka kwenda kunawa huku Eggy akibaki akilinda chakula kile.

“Uliomba bia, lakini vipi kuhusu chakula, wewe tayari?” Alihoji Jackson wakati aliporejea na kuketi.

“Sijala na nitashukuru sana kama utanipa offer nyingine ya chakula kaka’ngu,” alijibu Eggy.

“Utapenda kula nini?”

“Mchemsho wa kuku.”

“Basi agiza,” alisema huku akimpa yule msichana noti ya shilingi 10,000 na kumuuliza kama kiasi kile kilikuwa kinatosha. Eggy alijibu kwa kichwa kuashiria kwamba kiasi kile kilikuwa kinatosha.

Wakati akiendelea kula, Eggy alikuja pale mezani kwake akiwa na bakuli la mchemsho wa kuku na kuketi kisha akaanza kula.

“Wakati ule ulisema huwezi kukaa kwa sababu meneja anawazuia imekuwaje sasa umekaa?”

“Meneja mwenyewe yuko kule anakula. Ngoja nile haraka haraka kabla hajaniona.”

“Kwani nyinyi wahudumu mnakula saa ngapi?”

“Tunakula baada ya kazi, mara nyingi kwenye saa sita usiku… Unadhani tunakula basi, tunalambalamba tu kwani mara nyingi chakula hakitoshi. Usipokula kama hivi ndio unajikuta wakati mwingine unalalia mchuzi wa makongoro na kipande cha ndizi.”

“Wewe unaishi wapi?”

“Nimepanga chumba hapo mtaani, mimi na mwenzangu ambaye tunafanya kazi naye hapa.”

“Ni mwenyeji wa wapi?”

“Mimi ni mwenyeji wa hapa hapa Tanga, Mdigo. Asili yetu ni kule Chongoleani, si mbali sana kutoka hapa mjini.”

“Wazazi wako wapo?”

“Hapana, wazazi wangu walikufa nikiwa mdogo na sehemu kubwa nimelelewa na bibi yangu.”

“Pole sana,” alisema Jackson na sasa maswali yake kuhusu kinachoweza kuwa kimemsibu msichana huyo mrembo kuhusu maendeleo yake kielimu yakianza kupata majibu. Alimwomba Mungu ampe maisha marefu ili asomeshe watoto wake, mkubwa wakati huo akiwa darasa la nne na mdogo darasa la kwanza, hadi kiwango cha chuo kikuu.

“Una mchumba Eggy?”

“Hapana, niliwahi kuishi na bwana mmoja lakini nikaona hana mwelekeo. Nikaamua kuachana naye.”

“Ukisema alikuwa hana mwelekeo unamaanisha nini?”

“Alikuwa amesoma lakini mvivu, hafikirii maisha na anataka tuendelee kuishi kwao. Nikaona ananipotezea muda wangu bure.”

“Ulizaa naye mtoto?”

“Hapana, lakini ninaye mtoto ambaye nilizaa na bwana mwingine kabla ya kukutana na huyo jamaa.”

“Vipi mtu akianzisha kitu kama mgahawa Dar es Salaam, kisha akakuchukua ukafanye kazi huko unaweza kuja?”

“Kwa nini nisije kama maslahi ni mazuri kuliko hapa? Isitoshe nimeshachoka na maisha ya Tanga.”

“Ninao mpango wa kufungua mgahawa Dar. Nikifikia hatua hiyo nitakutafuta ingawa sijui mke wangu atafikiria nini kuhusu msichana mrembo kama wewe, lakini ananiamini. Hana mashaka na mimi.”

“Mimi niko tayari hata kesho… Naona bosi keshamaliza kula. Ngoja nimalizie kuku wangu haraka haraka niondoke.”

“Ratiba yako ya leo baada ya kazi ikoje?”

“Hapa tunamaliza kazi kati ya saa tano na nusu na saa sita usiku... Wewe umefikia wapi?”

“Mimi niko hapo Twiga Executive Lodge.”

“Nitakuja baada ya kazi. Uko chumba gani?”

“Chumba kimoja kinaitwa Kigoma.”

“Aha, Kigoma mwisho wa reli! Basi nitakuja… baadaye nitakuletea namba yangu ya simu au unaweza kuinakili harakaharaka?”

“Nitajie.” Agnes alimtajia namba zake za simu kisha Jackson alipozinakili, akambipu na msichana huyo akahifadhi za kwake pia.

Alinyanyuka na kuondoka bila kumalizia chakula chake sawasawa baada ya kumwona bosi wao aliyekuwa amesimama katikati mwa ukumbi wa klabu hiyo akiangaza huku na kule. Jackson aliendelea kula chakula chake taratibu huku akianza kujilaumu kwa kufanya jambo ambalo siyo sahihi sana, la kuwa karibu na msichana yule hadi kupeana ahadi ya kukutana baadaye.

Endelea kufuatilia riwaya hii ya kusisimua...
 
SIHUSIKI - 3

“Hivi nimekuwaje leo, au ndio nimeshalishwa limbwata la Tanga?” Alijiuliza. Akapanga kwamba baadaye atarekebisha kile alichopotoka kwa maana ya kumzuia msichana huyo kwenda chumbani kwake.

Wakati anamaliza kula, mchezo wa mpira wa miguu uliokuwa unasubiriwa usiku huo wa vilabu mahasimu nchini Hispania, Real Madrid na Barcelona ulikuwa ndio unaanza huku skrini kubwa sita ndani ya klabu hiyo zikiuonesha. Yeye alikuwa jirani na skrini moja wapo na hivyo hakuwa na sababu ya kugeuka au kuhama kama alivyoona kwa baadhi ya wapenzi wengine wa mpira.

Toka jana usiku walipokuwa kwenye klabu hiyo na Andrew pamoja na Bruno aliyelazimisha kwenda kukaa nao, walipanga kwamba wangekuja kutazamia hapo mchezo huo na siyo vyumbani.

Kilichokuwa kinampa jeuri zaidi kuchelewa kwenda kulala hata kama angelikaa hadi klabu hiyo kufungwa ni asubuhi yake, siku ya Ijumaa ambayo ilikuwa siku ya mwisho ya semina yao, kutokuwa mmoja wa wawasilishaji wa mada.

Semina hiyo ambayo ilikuwa imeandaliwa na ofisi yao kwa ajili ya taasisi na wadau kadhaa wanaofanya kazi kwa karibu na TTM yakiwemo makampuni ya simu, ilihusu mambo mbalimbali ya maendeleo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Duniani (TEHAMA) na jinsi nchi inavyoweza kunufaika zaidi na teknolojia hiyo.

Yeye kama mwanasheria wa Tume, alikuwa na kazi kubwa ya kuelezea sheria za nchi na za kimataifa zinazohusu suala zima la matumizi ya TEHAMA. Pia alikuwa akitoa elimu, kuhusu sheria ya makosa ya mitandaoni na ya vyombo vya habari, hususani vya kielektroniki.

Wakati akiendelea kutazama mpira huku kelele ukumbini zikiwa zimeongezeka kutokana na ubishi au kutambiana baina ya wapenzi wa vilabu hivyo, alikuwa pia akimwangaza Eggy. Alipomwona alimwita kwa ishara na alipofika akamwagiza amletee juisi ya embe.

Kabla Eggy hajaondoka kwenye meza yake kumfuatia juisi, Bruno alikuwa anafika na kumzuia Eggy kuondoka.

“Usiondoke kwanza mrembo,” alisema Bruno akiketi katika kiti kilichokuwa wazi na kisha akamsalimia Jackson kwa bashasha.

“Karibu mkuu,” Jackson alimkaribisha sasa akihisi kwamba pengine Bruno alikuwa ameamua kuweka mbali hali ya uhasama baina yao, hususani katika kipindi hicho ambacho baada ya semina hiyo kulikuwa na tukio kubwa ambalo Jackson alihisi litazidi kuwafanya wahasimiane zaidi. Tukio la Mkurugenzi wa TTM kustaafu huku waliotazamiwa kukaimu nafasi yake wakiwa ni mmoja kati yao.

“Nimefurahi kugundua uko hapa Malima,” alisema Bruno kisha akamgeukia Eggy aliyekuwa amesimama akisubiri maelekezo.

“Mrembo, nifuatie bia yangu kwenye meza ile pale. Niletee na ule mkoba wangu,” Bruno alimwelekeza kwa kidole na Eggy akaiona meza moja iliyokuwa katikati ya ukumbi ambayo alibaki mwanaume mmoja akiendelea kunywa.

“Haya mheshimiwa,” alijibu Eggy na kuondoka.

Bruno, mmoja wa watu waliompokea Jackson kazini takribani miaka tisa iliyopita, aliketi na kumweleza Jackson kwamba angetamani kuona siku moja wanashirikiana katika kunywa pombe pamoja.

“Hivi starehe yako kubwa ni ipi Malima… Ina maana hujawahi kunywa pombe maishani mwako?”

“Sijawahi kunywa na wala sitarajii kunywa,” alijibu Jackson. Bado alikuwa akitafakari mabadiliko ya Bruno katika siku mbili hizo akikumbuka hali ya uhasama baina yao iliyokuwa imeongezeka kabla ya kuondoka Dar es Salaam kwa ajili ya semina hiyo.

Jackson alikuwa amesikia maneno mengi mabaya yakisemwa na Bruno juu yake baada ya kuwepo kwa uvumi kwamba Mkurugenzi wa TTM aliyekuwa anastaafu, Ibrahim Matakwali, alikuwa anafikiria kumpendekeza yeye Jackson kwenye Bodi ya Tume kukaimu nafasi yake ya ukurugenzi.

Sasa aliona hana sababu ya moyo wake kuendelea kusinyaa dhidi ya Bruno ambaye inaonekana alikuwa ameamua kukunjua moyo wake kwake.

Akiwa amevaa tisheti nyekundu kama wahudumu wenzake na suruali ya aina ya Jeans iliyombana na hivyo kuonyesha maumbile yake kwa uwazi, Eggy alileta bia aliyokuwa akinywa Bruno pale mezani na mkoba wake, kisha akaondoka kufuata juisi ambayo Bruno sasa alisema atailipia yeye.

“Hivi kesho hatuwezi kumaliza semina mapema tukaondoka na basi za jioni kurudi Dar?” Alianzisha mazungumzo Bruno akionesha kuchangamka.

“Kuwahi au kutowahi kumaliza itaanzia kwako endapo wasilisho lako halitakuwa na wachangiaji wengi na mawasilisho mengine mawili ya mwisho. Lakini kwa mtazamo wangu sioni sababu ya kuondoka kesho kurejea Dar kwa sababu wakati mwingine safari za usiku usiku si nzuri sana. Mimi nimeshaamua nitaondoka Jumamosi asubuhi.”

Eggy alileta juisi na kuiweka mezani, Bruno akamgeukia.“Mrembo, ninamjua huyu ndugu yangu ni mpenzi wa vitu vitamu, utamletea juisi nyingine, chenji utakunywa bia,” alisema Bruno akitoa noti ya shilingi elfu kumi.

“Asante sana mkuu. Hii moja inatosha,” alisema Jackson lakini Bruno akakataa, akamlazimisha Eggy kwamba akiona juisi aliyomletea Bruno inapungua amletee nyingine mara moja.

“Sawa mheshimiwa,” alijibu Eggy.

“Mkuu, soda au hizi juisi si kama bia ambazo ukikojoa inaisha mwilini. Hii ilikuwa inatosha kabisa,” alisema Jackson wakati Eggy akiondoka.

“Unadhani kwamba hadi mpira unaisha utakuwa hujaenda kujisaidia? Jana nilikuona ukienda msalani mara mbili wakati mimi ninayekunywa pombe nimeenda mara moja tu,” alisema Bruno.

Baada ya muda Eggy alirejea na bia akajiunga nao na kuendelea kunywa. Wakati wakiendelea kutazama mpira, kila mara Bruno alikuwa akimhimiza Jackson anywe juisi ili aletewe nyingine ambayo alikuwa keshailipia huku pia akifanya hivyo kwa Eggy.

Jackson alianza kuhisi kuwa Bruno keshachanganyikiwa kwa Eggy aliyekuwa akinyanyuka mara kwa mara kwenda kuhudumia wateja na kurejea. Hata hivyo, kutokana na kukosekana kwa Andrew ambaye alihisi usiku huo alikuwa kaenda sehemu nyingine, Jackson sasa alijipangia kuondoka wakati wa mapumziko na kwenda kumalizia mtanange huo wa mpira chumbani kwake.

Kipenga cha mapumziko kilipopulizwa huku timu zote zikiwa hazijafungana, Jackson alinyanyuka kwenda kujisaidia na kumjulisha Bruno kwamba akirejea hatokaa sana.

“Mimi ninataka huyu bwana aendelee kukaa, hebu mfuatie juisi nyingine ya embe,” Bruno alimwagiza Eggy akimpa pesa na kumtaka aongeze bia nyingine mbili kwa ajili yao wawili.

Jackson alirejea kutoka msalani na kumwona Eggy akimhudumia mteja aliyekuwa jirani yao ambaye pia alionekana kumtaka msichana huyo.

Akashangaa kuona vinywaji vimeongezeka mezani huku yeye akiona ulikuwa muda mwafaka wa kuondoka ikiwezekana bila hata kumuaga Eggy.

Jackson aliamini kwamba Bruno aliyekuwa akiongea sana na kuwa tayari kumnunulia yeyote pale mezani chochote, ilikuwa ni moja ya mbinu za kumvutia kwake binti huyo mwenye haiba na umbo la kuvutia. Yeye alifurahia hilo.

“Mbona umeongeza juisi hata kabla hii haijaisha mkuu? Mimi naondoka hivyo,” aliuliza Jackson baada ya kuketi.

“Unawahi wapi na kesho huna wasilisho. Tuangalie mpira kidogo.”

“Hapana, ngoja nimalizie hii juisi niondoke. Hiyo siwezi kuinywa,” alisema na kushauri kwamba juisi ya boksi iliyoletwa ataichukua Eggy na kuinywa au kuigawa kwa sababu ilikuwa haijafunguliwa.

Wakati anapeleka mkono kuchukua juisi yake ili anywe mafunda mawili matatu kisha aondoke, kijana mmoja mlevi aliyekuwa akicheza pembeni mwa meza yao aliiangukia ile meza na kusababisha vinywaji vyote kumwagika.

Endelea kufuatilia riwaya hii ya kusisimua...
 
SIHUSIKI - 4

ILIPOISHIA...

“Unawahi wapi na kesho huna wasilisho. Tuangalie mpira kidogo.”

“Hapana, ngoja nimalizie hii juisi niondoke. Hiyo siwezi kuinywa,” alisema na kushauri kwamba juisi ya boksi iliyoletwa ataichukua Eggy na kuinywa au kuigawa kwa sababu ilikuwa haijafunguliwa.

Wakati anapeleka mkono kuchukua juisi yake ili anywe mafunda mawili matatu kisha aondoke, kijana mmoja mlevi aliyekuwa akicheza pembeni mwa meza yao aliiangukia ile meza na kusababisha vinywaji vyote kumwagika.

ENDELEA...

Bruno alikuja juu na kumkwida shati yule kijana aliyekuwa akijitahidi kunyanyuka akimlazimisha kununua vinywaji vyao.

“Bahati mbaya father,” alisema kijana yule kwa sauti ya kilevilevi huku Bruno aliyekuwa na hasira akiendelea kumkwida na kumtaka Eggy ambaye alikuja haraka pale mezani amwite meneja wa baa.

“Huyo kijana ni mlevi tunamfahamu hapa. Pengine hapo keshalewa gongo huko mitaani ndipo akaja hapa. Ninamjua hana uwezo wa kununua hivi vinywaji lakini akiwa hajalewa ni mkarimu sana,” alisema Eggy akimsihi Bruno amwache kwa sababu atamuua bure. Jackson pia alimsihi amwache.

“Mkuu mimi nakuacha. Lakini ngoja niwanunulie bia mimi,” alisema Jackson huku akisimama.

“Hapana acha tu… Mimi bado kidogo. Hii ndiyo sebule yetu hapa Tanga,” alisema Bruno na kumsihi sana Jackson aendelee kukaa. Lakini alikataa akisema ataenda kumalizia dakika zilizobaki za mpira akiwa chumbani kwake

“Usiku mwema mkuu.”

“Hata hivyo, umejitahidi. Mpaka sasa bado uko hapa?” Alisema Bruno akiangalia saa yake. Ilikuwa inaelekea saa tano na robo usiku.

“Mpira ndio umenichelewesha… Haya kesho.”

“Sawa,” alijibu Bruno.

“Kaka naomba nikusindikize,” alisema Eggy akisimama.

“Binti, wewe bado uko kazini. Kaa na mkuu hapa utamsindikiza yeye.”

“Sasa hivi kazi zimepungua sana, hakuna wateja wapya wengi.”

“Ulikuwa unasemaje?”

“Ah, twende nikusindikize,” alisema Eggy akimshika mkono Jackson na kisha kuongozana naye.

Jackson alishangaa kumwona Andrew Mambo, Meneja Rasilimali Watu wa Tume akiwa pia ukumbini humo, mtu ambaye ndiye alitaka awe naye tangu alipowasili na siyo Bruno. Alikuwa ameketi na msichana mwingine, mmoja wa wahudumu wa klabu hiyo.

“Vipi Andrew sikujua uko hapa. Kwa nini leo umejitenga nami… Lakini nimeshaona sababu!”

“Ah! Nipo na nilikuona wakati unaingia. Bruno alipokuja dakika mbili hivi baada ya wewe kuingia akakuulizia nikamwambia sijui ulipo ingawa nilikuona ulipokwenda kukaa na ilikuwa nikufuate. Nikaona anakutafuta lakini hakukuona, akarudi tena hapa na kukaa. Amekaa hapa akinikera mara nikaona anaamka na kisha nikaona anahamia kwako baada ya kukuona. Nadhani mambo yamekwenda vyema kuona mahasimu mnakaa tena meza moja. Nikaamua kuwaacha. Bruno kwa kweli simpendi na alipotoka hapa nikashukuru. Hata jana alinikera sana alipolazimisha kuja kukaa na sisi.”

“Naona ameamua kubadilika. Nadhani hatuna sababu ya kumtenga kama anataka ushirikiano.”

“Bruno abadilike! Labda pombe tu au anaigiza…”

“Aisee tutaonana kesho,” aliaga Jackson na kuondoka huku Eggy aliyekuwa amesimama pembeni wakati akizungumza na Andrew akijiunga naye tena kutoka nje ya ukumbi huo. Baada ya kupiga hatua kadhaa, Jackson alimgeukia Eggy na kumwambia inaonekana jamaa waliyemwacha pale mezani kwa maana ya Bruno anamtaka. Akasema yeye hana kinyongo na kwamba anamshauri kwa moyo mmoja akaungane naye.

“Ah yule bwana hana nyimbo.”

“Kwa nini unasema hana nyimbo?”

“Anapenda sana wanawake huyo mzee. Hapa anatongoza kila msichana. Mimi sipendi watu wa aina hiyo. Napenda watu wastaarabu kama wewe. Na nikipata bwana wa kunioa wa aina yako hata pombe nitaacha.”

“Kwani unamfahamu huyo bwana?”

“Nimeanza tu kumwona siku mbili tatu hizi lakini hii si mara yake ya kwanza kuja hapa klabu. Mwezi uliopita alikuwepo hapa pia.”

Jackson alijua Eggy anasema kweli kwani kipindi hicho Bruno alikuwa Tanga akishiriki semina nyingine.

“Unataka kusema hujawahi kuondoka naye?”

“Wala simtaki.”

“Acha masihara. Humtaki kwa lipi?”

“Basi tu… Yaani kila mara alikuwa ananikonyeza niondoke naye lakini nimemnong’oneza kwamba nina mtu tayari lakini yeye anang’ang’ana tu. Nimekusindikiza makusudi ili aone picha.”

“Ah! Nakushauri uondoke naye tu wala hamna shida kabisa… Ehe! Ulikuwa unasemaje?”

“Kwani wewe una mtu mwingine?”

“Hapana. Nakwenda tu kulala ila nimechoka sana.”

“Mimi nakutaka wewe na kama umechoka nitakuchangamsha… Ninaomba uniachie shilingi elfu mbili tu kwa ajili ya bodaboda nitakapokuwa ninakuja chumbani kwako.”

“Kama nilivyosema nimechoka sana na hivyo huna sababu ya kuja. Halafu hapo Twiga kama ukiamua kuja, bodaboda ya nini? Mbona mimi ninakuja hapa kwa mguu na kurejea kwa mguu?”

“We’ mwanamume. Unaijua hii mitaa usiku? Vijana wa kihuni wanaweza kunibaka.”

“Sikiliza binti, kwa hayo mazingira magumu unayosema huna sababu kabisa ya kuja. Kwa heri,” alisema na kuanza kupiga hatua.

“Haya kaka.”

Kabla hajafika mbali, yule mlevi aliyeangukia meza alimsimamisha. Inaonekana alikuwa akimfuata kwa nyuma. Jackson alishituka kidogo akihisi amekuja kwa shari, labda ni mpenzi wa Eggy na hivyo anataka kumfanyia fujo.

“Braza nilikuwa nakufuata wewe. Nimekuokoa maisha miye. Nipe pesa ya bia tu,” alisema yule kijana.

Jackson hakumwelewa, sasa akahisi huyo mlevi anataka kumtapeli, akaendelea na safari yake lakini yeye alizidi kumfuata akimsemesha.

“Mimi pale sikuanguka braza, nilijiangusha tu kwa sababu niliona mtu anaweka kitu kwenye kinywaji chako. Wewe si ulikuwa unakunywa juisi halafu ukaondoka kidogo?”

Jackson aliona anamsumbua bure. Akashika mfukoni na kumpa noti ya shilingi elfu moja.

“Haya kaka, lakini ungejua nimekuokoa, ungenipa hata laki,” alisema yule kijana akikimbia kisogo chake kwani alishageuka kuondoka.

Jackson aliingia chumbani huku roho yake ikimuuma sana kwa kitendo chake cha kuwa karibu na yule msichana hadi kumkaribisha kwake. Alishukuru kwamba alimudu kumnyima pesa ya bodaboda na kumshauri asiende chumbani kwake.

“Bila shaka amenielewa kwamba simhitaji,” alijisemea huku akijaribu kuvaa viatu vya mkewe. Kwamba atajisikiaje siku akisikia kuna mtu anatembea na mkewe?

“Bila shaka nitajisikia vibaya sana. Vivyo hivyo na yeye ataumia sana akisikia mimi mumewe kipenzi ninatumia nafasi hii ya kuwa mbali naye kulala na mwanamke mwingine. Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe na shetani huyu aliyekuwa ananishawishi kuwa karibu na huyo msichana. Mwondoe kwangu, ashindwe na alegee,” alizidi kujisemea.

Aliwasha runinga kuendelea kuangalia mpira. Zilikuwa zimesalia dakika 15 na bado timu zilikuwa hazijafungana. Alivua nguo na kuvaa ya kulalia, akakaa kidogo kumwomba Mwenyezi Mungu kwa kumhifadhi mchana huo, kisha akajitupa kitandani akiendelea kuangalia mpira.

Endelea kufuatilia...

CC Litro the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J
 
SIHUSIKI - 5

sihusiki JamiiForums 2.jpg


ILIKUWA haijapita muda mrefu tangu usingizi umchukue wakati simu yake ilipoita. Alishtuka na kuangalia anayepiga simu muda ule alikuwa nani. Alipoangalia kwenye skrini ya simu akaona namba ngeni.

“Halo,” aliita.

“Halo, kaka mimi Eggy niko hapa nje hotelini kwako, mlinzi keshanifungulia. Umesema uko chumbani gani?”

“Eggy, mbona umekuja. Si nilikwambia huna sababu ya kuja? Nikakwambia nimechoka?”

“Ina maana umechukua msichana mwingine, siyo? Kumbe wewe na yule mzee malaya sana eh!”

“Hapana Eggy, niko peke yangu lakini sikujua kama utakuja baada ya kukwambia vile. Naomba urudi tu na samahani sana kwa usumbufu.”

“Muda huu nirudi wapi?”

“Ngoja basi nikuletee pesa uchukue bodaboda.”

“Mimi ndio nilishamuaga mwenzangu tunayeishi naye na sasa hivi watakuwa wamefunga nyumba, siwezi kufunguliwa. Unadhani nitalala wapi?”

“Duh! Sasa itakuwaje?”

“Kaka, si umesema huna mtu, sasa kwa nini unanifanyia hivi?”

“Basi mwambie huyo mlinzi akulete Kigoma,” alisema Jackson.

Mwanaume huyo aliketi kitandani akijilaumu ni kwa nini alikuwa amefanya kilichosababisha msichana huyo kuja kwake. Hata hivyo, aliapa kwamba pamoja na kumkaribisha chumbani kwake, katu asingemgusa.

Alisikia hodi ikigongwa na mlinzi na alipokwenda kufungua akamkuta mlinzi huyo akiwa na Eggy. Jackson alilazimika kumkaribisha msichana huyo ambaye alikuwa ameshikilia mkoba wake na bia mkononi.

“Karibu. Duh! Umekuja na bia huku?”

“Kanilazimisha yule mzee, rafiki yako,” alisema Eggy akiweka ile bia juu ya meza ndogo pale chumbani.

“Kwa hiyo ulikuwa unakuja barabarani unakunywa, siyo?”

“Hapana, kwa nini unaniuliza hivyo?”

“Si ninaona umeshaifungua.”

“Yule mshenzi ndiye kanipa hii bia, alikuwa ameshaifungua anywe yeye kisha akaamua kuniachia.”

“Sasa unachukuaje kinywaji kilichofunguliwa na mtu mwingine?”

“Haina shida… Hata kama alishatia mdomo wake sijali. Leo nina hamu sana na bia hasa ukizingatia kwamba karibu wiki nilikuwa naumwa na hivyo kujitenga na kinywaji. Tena mimi nikimaliza hii bia nitakuwa nimefika ninakopataka na nitakufurahisha zaidi leo, amini usiamini.”

Yule binti, alianza kunywa bia yake akiwa ameketi kwenye kochi pembeni mwa kitanda huku Jackson akitafuta maneno ya kumwambia ili wasifanye chochote.

Huku bado akiwaza atafanya nini kumkwepa Agnes ndani ya chumba kimoja walimokuwa, Jackson alimwona akimaliza kunywa bia yake na kunyanyuka. Akavua blauzi na suruali yake ya kubana na kuzitundika nyuma ya mlango na kuanza kuvuta hatua kuelekea bafuni kuoga akiwa kabaki na nguo ya ndani pekee.

Maumbile ya msichana huyo yalimsisimua vilivyo Jackson, akaanza kufikiria kubadili uamuzi wake lakini alipokumbuka kwamba alishaapa kutosaliti ndoa yake jambo ambalo pia ni kumuudhi mola wake akajiapiza tena kwamba asingefanya lolote. Alitakiwa amshinde shetani kadiri inavyowezekana.

Baada ya muda Eggy alirejea, akazima taa yenye mwanga mkali na kuasha yenye mwanga hafifu, hatua iliyoonesha kwamba alikuwa mwenyeji katika chumba au nyumba hiyo ya kulala wageni, kisha akajilaza pembeni mwake. Jackson akaamua kutoka kitandani na kwenda kulala kwenye kochi moja lililokuwa kwenye chumba hicho.

“Vipi kaka, mbona sikuelewi?”

“Licha ya uchovu, lakini nimegundua kwamba nimesahau kuchukua kinga, kwa hiyo wewe lala tu. Mambo mengine tutajiandaa kesho.”

Eggy, huku sasa akiwa hana nguo yoyote mwilini na Jackson akijitahidi kukwepa kumtazama, alikwenda kwenye pochi yake aliyokuwa ameiacha kwenye meza na kutoa kinga, kisha akamtupia Jackson pale kwenye kochi alipokuwa amejilaza.

“Sikiliza Eggy, natamani kushiriki na wewe haya mambo ukiwa huna ulevi. Nashauri tulale halafu mambo mengine tufanya asubuhi pombe zikishakutoka, sawa?” Alisema Jackson.

Msichana huyo hakujibu, akamfuata pale kwenye kochi na kuanza kumshika shika akimtaka waende kitandani kulala lakini Jackson alimsihi amwache.

“Binti, ninakuomba kwa hisani yako. Wewe lala.”

“Haiwezekani. Nimekuja hapa kwa ajili yako… Kwani una tatizo lolote kaka? Sikuelewi!”

“Ndio, kwa sasa nina tatizo na ndio maana ninakwambia mambo yote kesho.”

“Hapana baby. Wala sikuelewi. Njoo tulale, unataka kunifanyia mambo gani wewe?” Aliuliza huku akiendelea kupeleka mikono yake kwenye sehemu hatarishi za Jackson ambaye muda huo alikuwa kavaa kaptula nyepesi ambayo alikuwa akiitumia kwa kulalia.

Taratibu, hali ya Jackson ilianza kubadilika, uvumilivu ulianza kumshinda. “Haya tangulia kitandani nakuja,” alisema akipapasa pale kwenye kochi kutafuta kinga. Wakati akipambana na hisia na sasa akihema kwa nguvu kuonesha kwamba moyo ulikuwa unafanya kazi ya kupeleka damu nyingi kwenye baadhi ya viungo vyake vya uzazi, ghafla alimsikia yule binti akigumia kwa maumivu. “Ah mbona tumbo linanisokota hivi?”

“Tumbo linakusokota?” Akauliza Jackson.

“Sana, limenianza tu ghafla nilipomaliza kunywa hiyo bia. Lakini litapoa tu. Nadhani nimekula kitu kibaya.”

“Kitu gani?”

“Wala sijui… Hebu kwanza nijisikilizie,” alisema Eggy.

Jackson alishukuru Mungu na kurejea kwenye kochi lakini baada ya ukimya wa kama dakika tatu hivi, yule msichana alimwita akimwambia tumbo halipoi na badala yake anajisikia tumbo linazidi kumkata sana na kwamba ameanza kusikia kizunguzungu na kichefu chefu.

“Nasikia hata nguvu zinaniishia.”

“Binti, umekula kitu kibaya?”

“Sijui… Nasikia hali inazidi kuwa mbaya,” alizidi kulalamika, hali iliyomfanya Jackson kunyanyuka. Msichana yule ambaye alikuwa mtupu pale kwenye kitanda kipana alikuwa akigaragara huku akiwa ameshikilia tumbo. Jasho pia lilianza kumyoka.

“Vipi, nikupeleke hospitali?”

“Hapana, nadhani hali hii itatulia tu. Ni kawaida nikila kitu kibaya kufikwa na hali hii. Niwashie feni,” alisema.

Jackson aliwasha kiyoyozi kisha akamwona yule msichana akinyanyuka kwenda chooni ambako alimsikia akitapika. Alipotoka chooni alijitupa kitandani na Jackson alipomuuliza anajisikiaje akamwambia baada ya kutapika anajisikia afueni kidogo lakini tumbo bado linamkata na mwili unaishiwa nguvu.

“Jilaze, hali itatulia. Hebu jaribu kunywa maji,” alisema Jackson na kufungua chupa ndogo ya maji na kumpa. Alirudi kwenye kochi na kujilaza na sasa alikuwa anahisi usingizi mzito. Baada ya utulivu wa takribani dakika sita, Jackson alishikwa na usingizi mzito pale kwenye kochi.

Alishituka usingizini na kuhisi kama kuna kitu kilikuwa kinakoroma mule chumbani. Alisimama haraka na kuelekea kitandani na kumkuta binti yule akikoroma. Alipojaribu kumsemesha akagundua kwamba Eggy alikuwa amepoteza fahamu huku povu likimtoka mdomoni.

Endelea kufuatilia...
 
SIHUSIKI - 6

Alikuwa keshatapika pale kitandani na sasa alikuwa kalalia matapishi yake bila kujitambua. Hali ile ilimtisha sana huku akimwonea huruma msichana yule mrembo. Akatamani kwenda kuwaamsha wahusika wa nyumba hiyo ya kulala wageni ili kumwahisha hospitali kuokoa maisha yake.

“Mbona amefikia hali hii bila kuniamsha?” Alijiuliza.

Kwa vile mkojo ulikuwa umembana kutokana na kunywa soda na juisi, Jackson aliingia bafuni kujisaidia huku akipanga kwamba ilikuwa ni lazima achukue hatua za haraka za kumwahisha Eggy hospitali. Hali ile ilikuwa si ya kawaida.

“Atakuwa kala nini huyu binti?” Alijiuliza tena bila kupata majibu.

Alitoka bafuni akipanga kumvalisha nguo haraka haraka, kumfuta matapishi na kisha kuomba msaada wa kumpeleka hospitali. Lakini aliporejea pale kitandani, hali ile ya kukoroma ilikuwa imekatika. Alimkuta akiwa sasa ametulia tuli huku akiwa kaachama kiasi. Hali ile ilizidi kumtisha na moyo kumwenda mbio. Alipomgusa maeneo ya moyo, aligundua kwamba, ingawa mwili wake ulikuwa wa moto, hakukuwa na mapigo yoyote anayoyasikia. Aliweka pia kidole kwenye pua yake lakini hakusikia upepo wa kupumua.

Wasiwasi na uwoga ulizidi kumfunika asiamini kwamba mrembo yule ambaye alikuwa akitoa huduma pale Tanga Raha Club saa chache zilizopita, akiwa mzima na buheri wa afya, anaweza akawa kapoteza maisha.

“Haiwezekani,” alijisemea akianza kumtikisa ili kumwamsha kwani alihisi atakuwa amezirai tu, lakini hakushituka.

Kwa vile aliwahi kupata mafunzo ya huduma ya kwanza ikiwa ni pamoja na kuamsha moyo au kumzindua mtu aliyezirai (Cardiopulmonary Resuscitation - CPR), aliona afanye jaribio hilo. Bado aliamini kwamba binti yule alikuwa amezirai tu.

Alimlaza chali, akaweka kiganja cha mkono wake wa kushoto kwenye kifua chake. Akaweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto na kubana vidole. Akaanza kukandamiza kwenye kifua chake ili kushitua mapigo ya moyo. Alimwacha kidogo, akapanua pua na kupuliza ili kufungua njia ya hewa na kurudia tena kumkandamiza kama mwanzo lakini msichana yule hakushituka.

Hali hiyo ilizidi kumtisha kwani ilikuwa inamthibitishia kwamba roho ya binti huyo ilikuwa tayari imeachana na mwili wake. Alirejea kuketi kwenye lile kochi huku kijasho chembamba kikitanda usoni mwake. Aliwaza na kujiuliza afanye nini na hali ile? Je, kulikuwa na haja ya kuwaamsha wahusika wa nyumba hiyo ya kulala wageni? Atawaambia nini? Alijiuliza. Aliangalia saa yake. Ilikuwa inaelekea saa tisa usiku.

Aliona kwamba pengine jambo la msingi la kufanya kwa wakati ule ni kuwapigia simu polisi. Alichukua simu yake akijiuliza kama anakumbuka namba ya simu ya dharura ya polisi. Alijitahidi kukumbuka bila mafanikio. Akajilaumu sana kwa sababu aliamini huo ni uzembe mkubwa kwani kila mtu alitakiwa kuwa na namba hiyo pamoja na ya kikosi cha zimamoto.

Alisimama ili kwenda kuulizia namba ya polisi kwa wenyeji na pia kuwaeleza kadhia iliyompata.

Kabla hajatoka nje akapata wazo la kumpigia simu Andrew Mambo kumweleza tukio lililompata na kama anaweza kuwa na namba ya polisi ya dharura. Aliona lilikuwa ni wazo zuri zaidi kumshirikisha kadhia hiyo ili pia kama ana ushauri mzuri wa ziada ampe.

Aliamini Andrew, tofauti na Bruno ambaye pia alipata wazo la kumshirikisha lakini akalifuta, alikuwa mtu mkarimu na muungwana. Hakuwa na ugomvi naye na alikuwa na ushauri mzuri. Hata wafanyakazi wengi walikuwa wakimpenda Andrew kama walivyokuwa wakimpenda yeye. Simu ya Andrew ilipoita akashukuru kwamba ilikuwa hewani.

“Malima, kuna nini. Nilidhani kumekucha lakini naangalia saa naona bado ni usiku mzito,” alihoji Andrew baada ya kupokea simu sauti yake ikionesha wazi kwamba alikuwa katika usingizi mzito.

“Aisee kuna jambo la ajabu na hatari limenitokea. Una mtu hapo chumbani?”

“Hapana niko peke yangu.”

“Nilidhani umeondoka na yule msichana niliyekuacha naye.”

“Hapana, niko peke yangu.” Kwa majibu yake, Jackson alianza kumsimulia kisa na mkasa na kisha akamwomba namba za simu za polisi za dharura kama anazo.

Andrew alishitushwa sana na masimulizi ya Jackson na usingizi ukampaa. Kimsingi naye alishangaa alipomwona akiandamana na msichana wakati anatoka kwa sababu wameshakuwa naye katika safari nyingi na hata tabia zake ofisini anamjua Jackson kama mwanamume asiyejihusisha kabisa na mahusiano nje ya ndoa yake.

Yeye binafsi alikuwa akitamani aishi kama Jackson lakini alikuwa anashindwa. Hata siku hiyo alikuwa amepania kuondoka na msichana aliyekuwa naye lakini mwishoni baada ya kunywa bia zake kadhaa akadai kwamba alikuwa anahisi kuingia katika siku zake, jambo lililomkasirisha sana Andrew.

“Sikiliza Malima. Mimi nashauri hili jambo usiwashirikishe polisi wasije wakakung’ang’ania kwa kukutuhumu kwa chochote. Mpaka watakapokuja kukuachia baada ya kujua ukweli wa mambo utakuwa umeshateseka.”

Jackson alibaki kimya kwa sekunde kadhaa akitafakari ushauri ule kisha akamuuliza: “Sasa unashauri nifanyeje?”

“Wewe ondoka hapo kimya kimya kisha uje huku.”

“Hapa kuna mlinzi. Nitaondokaje usiku kama huu na anajua nina msichana chumbani? Bila shaka atapatwa na wasiwasi.”

“Basi fanya jambo moja, subiri kidogo ikifika alfajiri, ondoka na kila kitu chako na mlinzi mwambie kuna binti humo kalala, ataamka kwa wakati wake.”

“Mh! Siyo kwamba nitajichongea kwa sababu jina langu wanalo hapa kwenye kitabu cha wageni.”

“Fanya kitu kimoja. Kama unaweza kuongea na mhusika. Mpe hata pesa afute jina lako kwenye hicho kitabu. Ikiwezekana anyofoe kabisa karatasi zenye jina lako.”

“Mh! Hilo ni gumu, si rahisi kumshawishi akanielewa haraka haraka. Suala la mtu kufia kwenye gesti yao halafu akubali kufuta majina yangu, si rahisi.”

“Basi jaribu kuiba hicho kitabu kama utaweza.”

“Hilo nalo gumu… Lakini ngoja nijaribu.”

“Hebu jaribu hilo na tafadhali usimwambia mtu yeyote. Ibaki siri yangu na yako. Na hakikisha Bruno hafahamu hili.”

“Kwa nini umemtaja Bruno?”

“Ninamjua, si mtu mzuri, hasa kwako. Ninajua jinsi alivyohamanika kusikia kwamba huenda wewe ndiye utakaimu ukurugenzi. Ninajua anavyohangaika kuhakikisha anachukua nafasi hiyo. Hata wewe unajua hilo na unajua kwamba kwa hulka yake Bruno ni mtu mshari sana.”

“Asante sana Andrew. Nitafanyia kazi ushauri wako.”

Jackson, akiwa amevaa nguo ya kulalia, alitoka taratibu kwa kunyata hadi ofisi ya mapokezi. Mhudumu wa zamu alikuwa kalala kwenye ofisi hiyo. Kulikuwa na kochi, kiti na kitanda. Alichungulia na kugundua kwamba kitabu cha wageni kilikuwa kwenye kaunta na yule binti, mhudumu wa zamu, alikuwa amelala fofofo.

Alitaka kuchukua kitabu chote na kuondoka nacho lakini akahisi hilo linaweza kumshtua yule msichana akiamka na kuona kitabu hakipo.

Kwa kutumia mwanga hafifu wa nje uliokuwa unaingia mahala pale, alikifungua taratibu kitabu hicho cha wageni na kunyofoa karatasi alizoamini zilikuwa na jina lake. Wakati anakunja hizo karatasi mkononi, alisikia yule msichana wa kaunta anauliza.

“Nani… nani, mwizi?”

Mambo yanazidi kunoga, endelea kufuatilia...
 
Hongera. Ila nahisi umeikatakata kupata hivyo vipande. Sehemu ya sita halisi inaishia pale jamaa anapokamatwa na mkewe kumkana sababu ya ufedhuli pasi na kumsikiliza.
 
Hongera. Ila nahisi umeikatakata kupata hivyo vipande. Sehemu ya sita halisi inaishia pale jamaa anapokamatwa na mkewe kumkana sababu ya ufedhuli pasi na kumsikiliza.
Labda, lakini pia inategemea na muono wako...
 
SIHUSIKI - 7

ILIPOISHIA...

Kwa kutumia mwanga hafifu wa nje uliokuwa unaingia mahala pale, alikifungua taratibu kitabu hicho cha wageni na kunyofoa karatasi alizoamini zilikuwa na jina lake. Wakati anakunja hizo karatasi mkononi, alisikia yule msichana wa kaunta anauliza.

“Nani… nani, mwizi?”

ENDELEA...

“Hapana ni mimi.”

“Nani, na unafanya nini hapa?” Alihoji yule msichana na kuwasha taa iliyojaza mwanga katika eneo hilo.

Huku akikunja zile karatasi na kuzishika kiganjani mwake haraka haraka, Jackson alimtuliza na kumjulisha kwamba alikuwa anataka kumwamsha ili amuuzie maji kwa sababu anasikia kiu lakini akawa anasita na kwamba alikuwa ameshaamua kuondoka na kujaribu kulala na kiu yake.

“Kama unaweza kunisaidia nitashukuru. Nisamehe kwa usumbufu,” alisema Jackson akihakikisha yule msichana hagundui alichokuwa amefumbata kwenye mkono wake wa kulia.

Yule msichana alinyanyuka kwenda kumchukulia maji kwenye friji na yeye haraka haraka akasokomeza zile karatasi kwenye mifuko ya nguo yake ya kulalia.

“Nadhani unakumbuka nilibakiza chenji yangu kwako. Kama sivyo nitakulipa asubuhi.”

“Yes, nakumbuka kuna chenji yako kaka.”

“Haya usiku mwema na samahani sana kwa usumbufu.”

“Hamna taabu kaka. Haya ndio majukumu yetu,” alisema na kurudi kulala, kisha akazima taa.

Jackson aliporudi chumbani kwake, alimpigia simu tena Andrew na kumweleza hatua aliyofikia.

“Basi wewe, subiri. Ikifika kwenye saa kumi na moja kasorobo hivi alfajiri wewe aga. Njoo hapa chumbani kwangu. Tutaondokea hapa kwenda kwenye semina. Bado kama saa mbili tu hivi.”

“Asante sana kwa ushauri wako.”

“Lakini nimekumbuka lingine. Usiache simu ya huyo marehemu. Ichukue kwa sababu ukiiacha polisi wataanzia hapo kusaka watu aliowasiliana nao na bila shaka wewe ndiye mtu wa mwisho kuwasiliana naye. Na kuanzia sasa jitahidi kila unachogusa uwe umevaa kitambaa ili usiendelee kuacha alama zako za vidole.”

“Aisee nimefanya vyema kukupigia simu. Hilo sikuwa ninalifikiria pamoja na mimi kuwa mwanasheria, yaani nimeshachanganyikiwa,” alisema.

Baada ya kukata simu, Jackson alijikuta na kibarua kizito cha kukaa chumbani mule na maiti hadi muda utakaofaa yeye kuondoka. Mawazo mengi yalizidi kumwandama hasa kama mpango wake wa kukimbia maiti ile utagundulika. Kuna wakati alikuwa anaona kama wazo la Andrew linaweza kumtia matatani zaidi kuliko kuwajulisha polisi lakini akajiuliza kama tayari alikuwa ameondoa ushahidi kwamba alilala kwenye nyumba hiyo, nini kitamhusisha na kifo kile?

Kingine kilichokuwa kinamtisha kuwajulisha polisi ni endapo watamkamata kwa kufanya uchunguzi na kisha suala hilo likawafikia waandishi wa habari na hatimaye mkewe. Itakuwa ni aibu na fedheha kubwa sana kwake kwamba alichukua changudoa na kumfia chumbani!

Aliona ni vyema aendelee kufanyia kazi ushauri wa Andrew. Alivaa kitambaa akachukua simu ya yule binti, akaizima na kuiweka kwenye sanduku lake dogo la safari, kisha akakagua mkoba wa yule binti ambapo hakuona cha maana kinachoweza kuwapa polisi ushahidi dhidi yake.

Alianza kupanga nguo zake kwenye begi na kuchukua kila kilicho chake akihakikisha haachi zile karatasi alizonyofoa kwenye kitabu cha wageni. Kisha akavaa nguo alizodhamiria kuvaa siku hiyo, akamfunika yule binti shuka kiasi cha kuonekana kama aliyelala tu. Akaketi kwenye kochi kusubiri alfajiri ifike, aondoke.

* * *

Saa 11 kasorobo, Jackson alikuwa anashuka kwenye boda boda na kugonga hodi kwenye nyumba ya kulala wageni ya Tanga Kunani aliyofikia Andrew. Alimkuta nje akimsubiri baada ya kumpigia simu, akachukua begi lake na kuongozana naye hadi chumbani kwake.

“Aisee pole sana.”

“Yaani sijui ni mkosi gani huu ambao umenikuta. Yule binti alikuwa mzima kabisa tulipokuwa naye pale baa. Yaani nashangaa sana.”

“Binadamu huwa tunatembea na magonjwa. Nadhani alikuwa anaumwa.”

“Yaani nilisita sana kuondoka naye kama nilivyokueleza kwenye simu. Na nilijilaumu sana kumpa namba yangu ya simu. Na hata alipokuja nilijaribu kumtaka arudi lakini akasema hawezi kurudi muda ule… Yaani nashangaa sana ndugu yangu.”

“Mimi huwa ninachukua sana wanawake kama hawa hasa ninapokuwa safarini, nadhani hata wewe unajua lakini sijawahi kutokewa na kitu kama hiki. Hata usiku huu nilitaka kuondoka na yule binti uliyenikuta ninaongea naye pale lakini ndio akanitapeli kwamba mambo yamemharibikia. Hili lako limenifundisha mengi.”

“Siku ya leo kwa kweli sitaisahau maishani mwangu.”

“Usijali. Matatizo tumeumbiwa wanaume. Tuombe Mungu kwamba hili suala lipite salama na nina matumaini kwamba litapita, lakini chonde chonde usimwambie mtu mwingine,” alisema Andrew.

“Unategemea nimwambie mtu mwingine? Haiwezekani Andrew,” alisema Jackson.

Anita Msuya alimaliza kufanya usafi vyumba vyote kasoro kimoja cha Kigoma ambacho mteja aliyekuwemo aliaga kukirudisha lakini akasema kuna mgeni wake bado amelala na kwamba akiamka ataondoka.

Kwa kuwa ilikuwa inaelekea saa nne asubuhi na chumba hicho kilitakiwa kutayarishwa kwa ajili ya mgeni mwingine, aliona ni wakati mwafaka wa kumgongea mtu huyo ili akitayarishe na kama kuna mpango wa kuendelea kukitumia pia ajue.

Akiwa na vifaa vya usafi, ndoo na brashi ya kudekia, Anita alisimama mbele ya chumba hicho akitazamana na maandishi yaliyoandikwa mlangoni, Kigoma, na kuanza kugonga.

Aligonga mara nne bila kuitikiwa, akahisi kwamba huenda mtu aliyekuwemo ndani aliondoka kimya kimya bila kuaga wakati yeye akifanya usafi katika vyumba vingine. Hilo lilikuwa jambo la kawaida kutokea.

Alijaribu kufungua mlango ukafunguka. Alipopepesa macho akagundua kwamba mgeni wa mteja wake ambaye alikuwa anajua kwa asilimia 100 ni mwanamke mwenzake alikuwa bado kalala. Mtu huyo, pale kitandani alikuwa amejifunika gubigubi.

Kama mteja aliyekuwa kwenye chumba hicho wakati anaondoka alfajiri asingesema kwamba anarudisha chumba, Anita angemwacha na kurudi zake lakini ilitakiwa amwamshe.

“Dada, dada,” Anita alijaribu kumwita akahisi alikuwa na usingizi mzito. Alizingatia muda aliokuja ambao kimsingi ilikuwa imeshaingia siku nyingine, yaani siku hiyo na akahisi pia kilichomleta humo kilimfanya achelewe kulala na ndio maana mwanaume aliyekuwa naye akamwacha akiwa kalala. Alisogea kitandani na kumshika bega kisha kumtikisa.

“Dada, dada… kumekucha, dada amka,” alijaribu kumwamsha lakini bado mtu yule hakuamka.

Aliongeza nguvu ya kumtikisa lakini hakuamka. Akapata wasiwasi na kumfunua uso. Alishituka sana alivyoutafakari uso aliokuwa akiuangalia. Kuna kitu kilimwambia kuna tatizo, akalazimika kutoka nje haraka kumfuata mhudumu mwenzake wa kiume.

Mhudumu huyo, Ramadhani Wakati, alikuwa akifanya usafi nje pamoja na kumwagilia maua yaliyokuwa yakizunguka nyumba hiyo ya wageni. Kijana huyo aliyekuwa akija asubuhi na kuondoka jioni huku pia akiwa na undugu na mmiliki wa nyumba hiyo ya wageni alikuwa pia akifanya kazi kama mlinzi wa mchana.

Anita alimjulisha kwamba ana mashaka na hali ya mtu aliyelala chumba cha Kigoma. Ramadhani, aliongozana na Anita hadi chumba cha Kigoma na alipomchunguza msichana yule kwa sekunde kadhaa ikiwa ni pamoja na kuweka kidole kwenye pua yake na kisha kusikiliza mapigo ya moyo akamgeukia Anita.

“Huyu si mzima. Kafa. Tumpigie simu uncle,” alisema akimaanisha wamwite mmiliki wa nyumba hiyo ya kulala wageni.

Endelea kufuatilia...
 
SIHUSIKI - 8

“Unasema kweli Rama?”

“Naona hivyo. Kafariki huyu,” alisisitiza.

Dakika chache baadaye, mmiliki wa nyumba hiyo ya kulala wageni, Muhidin Mbwana, alifika na gari lake dogo. Naye alipomchunguza msichana yule aliyesuka rasta pale kitandani, akagundua kwamba hakuwa hai.

Mara moja akataka kujua jina la mtu aliyekuwa amepanga chumba hicho na taarifa zake zote kama zinavyonakiliwa kwenye kitabu cha wageni ili awasiliane na polisi. Anita alipoleta kitabu cha wageni, waligundua kwamba karatasi za mbele zilizokuwa na jina na taarifa za mteja huyo zilikuwa zimenyofolewa. Anita akakumbuka namna mteja huyo alivyomshitua usingizini usiku wa manane akidai alitaka maji na yeye kulazimika kumhudumia.

“Unajua niliposhituka nilihisi kama kuna mtu anachana karatasi lakini nikadhani nilikuwa naota. Kumbe ndio alikuwa akinyofoa hizi karatasi,” alisema na kusimulia kilichotokea.

“Huyu mtu ni criminal. Kamuua binti wa watu halafu kaondoka,” alisema mmiliki wa gesti hiyo, Mbwana.

Alipiga simu polisi walioahidi kufika baada ya muda mfupi. Dakika chache baadaye askari watatu walifika, wawili wakiwa wamevaa nguo za kiraia na mmoja sare za polisi na kuanza uchunguzi wao.

Askari hao walimhoji Anita na kisha wakataka pia kumhoji mlinzi aliyekuwepo kwani Anita alisema mlinzi huyo ndiye alimpokea marehemu alipokuja usiku na alisikia wakiongea mawili matatu nje.

“Binti, huyo mteja aliyekuwa chumba mnachokiita Kigoma ukimwona utamtambua?” Askari aliyejitambulisha kwa jina la Sajini Omar alimuuliza Anita wakati wakimsubiri mlinzi kuja baada ya kupigiwa simu.

“Ingawa nilianza zamu juzi lakini nina hakika nikimwona namfahamu. Ni baba mmoja anaonekana mstaarabu sana,” alisema.

“Unaweza kukumbuka kitabuni aliandika anatokea wapi na kazi yake ni ipi?” Akauliza tena huyo askari.

“Sikumbuki kazi yake lakini anatokea Dar es Salaam. Jana alikuwa ananiambia kwamba angeliondoka Jumamosi lakini alfajiri akaniambia ataondoka leo kurudi Dar es Salaam na ndio maana akarejesha chumba.”

“Je, unaweza kufahamu hapa Tanga amekuja kufanya nini?”

“Sifahamu kwa kweli,” alijibu Anita. Kabla hawajaendelea kumhoji zaidi, mlinzi aliyekuwa zamu usiku huo, Abdallah Shariff, alifika kwa usafiri bodaboda. Mlinzi huyo alieleza kwamba msichana huyo alipofika kwenye saa sita karibu na nusu usiku alitaka kwenda moja kwa moja chumba cha Kigoma lakini yeye akamzuia.

“Mimi nilimzuia nikamtaka kama ana simu ampigie kwanza mwenyeji wake kwa sababu hakuniambia kuna mgeni wake angelikuja. Alipompigia nikamwambia aweke loud speaker ili nami nisikie. Nilimsikia mwenyeji wake akimshauri arudi anakotoka lakini msichana akalazimisha kulala na ndipo akamwambia aniombe nimpeleke chumbani kwake. Nikampeleka.”

“Huyu msichana ulishawahi kumwona?” Alihoji askari mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Koplo Burhani.

“Namfahamu, ni baamedi wa pale Tanga Raha Club.”

“Una uhakika?” Aliuliza tena yule askari.

“Nina uhakika asilimia mia moja na hapa alishakuja siyo mara moja wala mbili na wanaume. Vyumba vyote humu ukimtajia; Musoma, Arusha, Lindi, Geita na vinginevyo anavijua,” alisema.

“Huyo bwana aliyekuwa Kigoma, ukimwona utamfahamu?” Alizidi kuhoji Koplo Burhani.

“Hata gizani ninaweza kumfahamu.”

“Unaweza kujua hapa Tanga alikuja kufanya nini?”

“Alikuja kwenye semina Mkonge Hotel. Kwa sababu siku ya kwanza mimi ndiye nilimtafutia usafiri wa kwenda Mkonge.”

“Alfajiri alipoondoka alikuaga?”

“Ndiyo.”

“Alisema anakwenda wapi?”

“Nilipomwona na begi nikamuuliza vipi, semina imeisha?”

“Akasema imeisha.”

“Alisema anaondoka muda ule kurejea Dar es Salaam?”

“Hapana, alisema tu semina imeisha.” Baada ya maelezo hayo, askari wakaona kuna haja ya kwenda Mkonge Hotel kunusa labda wanaweza kujua lolote kama kuna semina imeisha.

“Inawezekana semina ikawa inaisha leo na huyo jamaa amepanga kuondoka leo,” alisema askari Burhani kumweleza mwenziye ambaye alikubaliana naye. Waliona hata kama kuna semina itakuwa imeisha jana yake, wanaweza wakapata majina ya wahusika na kuanza kufuatilia jina moja baada ya lingine.

Baadaye waliuliza kama kuna mwenye namba ya meneja au mmiliki wa Tanga Raha Club. Hakuna aliyekuwa nayo. Mbwana, mmiliki wa gesti hiyo, alisema anaweza kuipata. Alimpigia simu mtu mmoja ambaye alimpa namba mbili za mmiliki na meneja wa klabu hiyo.

Mara moja askari wale walimpigia meneja na kumweleza kwamba kuna binti kafia Twiga Executive Lodge anayeaminika kuwa mmoja wa wahudumu katika klabu hiyo maarufu. Mara moja wakamtaka aje pale kumtambua marehemu. Meneja huyo alifika baada ya dakika tano na alipomwangalia yule binti kitandani alimtambua.

“Ndio, huyu ni Agnes Makata. Ni mhudumu wetu na jana alikuwa kazini.”

“Alipokuwa kazini alikuwa anaumwa?” Alihoji Sajini Omar.

“Hapana, alikuwa mzima. Lakini kiasi cha siku nne hivi alikuwa akisumbuliwa na malaria. Tangu majuzi ni mzima na anakuja kazini kama kawaida.”

“Unamjua mtu aliyeondoka naye baada ya kazi usiku wa kuamkia leo?”

“Hapana. Baadhi ya wasichana tulio nao klabu wako palepale ghetto lakini Agnes na mwenzake anaitwa Mariamu wamepanga chumba mtaani,” alijibu Meneja yule, Hashim Thomas maarufu kama Makilikili.

“Tutamhitaji huyo Mariamu baadaye,” alisema Sajini Omar na kuongeza: “Sasa nyinyi wawili; wewe mtu wa mapokezi na wewe mlinzi tutaondoka nanyi kwenda Mkonge Hotel kama tunaweza kumwona huyu mtuhumiwa au kujua chochote. Lakini kwanza ngoja tushughulikie mwili wa marehemu ukahifadhiwe hospitalini Bombo.”

Askari wale waliokuja na gari ya polisi aina ya Land Rover, walimwita dereva na kisha wakashirikiana kubeba maiti ile hadi kwenye gari lao. Kisha wakatoa maagizo kwamba chumba kile kisiguswe hadi wataalamu wa alama za vidole watakapokuja.

“Tunapeleka maiti kwenye chumba cha kuhifadhia maiti hospitalini, tutarudi kwa ajili ya kuwachukua nyinyi mkaandike maelezo na kisha tutakwenda Mkonge Hotel,” alitoa maagizo Sajini Omar kuwaambia Anita na Abdallah.

“Samahani afande, huyu bwana inawezekana ameondoka kurudi Dar es Salaam. Tutaenda Mkonge kufanya nini?” Alihoji Abdallah.

Sajini Omar akamgeukia: “Lakini hukusema kwa asilimia mia moja kama semina anayoshiriki imeisha, na huyu mwenzio, anasema huyo bwana aliwahi kumwambia atakuwepo hapa hadi kesho Jumamosi. Kama hakuna semina iliyomalizika leo, tutajaribu kupita semina zote zinazoendelea pale na wahusika watatueleza pia kama kuna semina iliisha jana ili tupate majina ya wahusika na uchunguzi wetu uanzie hapo, sawa?”

“Sawa afande.”

* * *

“Tumepata taarifa sasa hivi kwamba chakula tayari. Kwa hiyo tutaendelea baada ya chakula kwa ajili ya mjadala wa mada iliyoko mbele yenu. Sasa hivi ni saa saba na nusu. Naomba saa nane na nusu tuwe hapa,” alisema mwasilishaji wa mada ya mwisho katika semina hiyo akiangalia saa yake. Akaongeza:

“Nadhani saa moja itatutosha kwa mjadala na kufunga semina saa tisa na nusu. Nimesikia basi la mwisho kwenda Dar linaondoka saa 11 na nusu kwa hiyo watakaokuwa tayari kusafiri muda huo ruksa.”

Wanasemina walifunga vifaa vyao na kusimama kuondoka. Hatua ile ya watu kuondoka ndiyo iliyomshtua Jackson aliyekuwa anasinzia. Tangu aingie kwenye semina hiyo iliyokuwa inaanza saa tatu kamili, mawazo yake yalikuwa mbali sana. Alikuwepo pale kimwili lakini si kifikra.

Endelea kufuatilia...
 
SIHUSIKI - 9

Alikuwa anaendelea kujiuliza sababu hasa za kifo cha yule msichana na alitamani kubaki Tanga ili kujua madaktari wangesema nini kuhusu chanzo cha kifo chake lakini ni jambo ambalo lilikuwa haliwezekani yeye kulifuatilia.

Aliendelea kujilaumu kwa nini alijiingiza katika masuala ya wanawake, jambo ambalo huwa analipiga vita na kuwa mshauri wa vijana wengi huku akihimiza watu kushika ibada na wakati mwingine kuwasomea baadhi ya vifungu vya Biblia hadi kupachikwa jina la Baba Mchungaji.

Hakuwa amesikia tangazo la chakula lakini hali ile ya watu kuamka ghafla alijua ni wakati wa chakula. Wakati ananyanyuka akiwa wa mwisho kutoka kwenye chumba cha semina, Bruno alimsubiri na alipomfikia alimgeukia.

“Malima, vipi? Naona hauko nasi kwenye semina. Kuna shida yoyote?”

“Hamna shida yoyote mkuu isipokuwa uchovu tu.”

“Au umeserebuka sana na yule binti. Kumbe Baba Mchungaji umo ma’nake jana ulinizidi ujanja.”

“Wala si kwa sababu hiyo. Kwanza sikuwa naye.”

“Usinidanganye Malima, alikuja chumbani kwako kwa sababu wanafunga klabu yao mimi nipo pale na aliniaga.”

“Alikuaga kwamba anakuja kwangu?”

“Ndio, aliniambia ninakwenda kwa rafiki yako, yaani kwako. Wala hakuficha.”

“Wala sikumwona… Samahani, napitia maliwatoni kidogo,” alisema Jackson na kuachana na Bruno. Licha ya kwamba alikuwa anasikia haja ndogo, lakini hakutaka kuendelea kuzungumzia suala la msichana huyo na Bruno.

Alipotoka maliwatoni alirudi tena chumba cha semina baada ya kugundua amesahau miwani yake. Baada ya kuichukua akatoka nje kuelekea kwenye eneo la chakula. Kulikuwa na semina nne zilizokuwa zinaendeshwa kwa wiki hiyo katika hoteli hiyo na watu wote walikuwa wakitoka kwa pamoja kwenda kwenye eneo la chakula.

Kule kwenye ukumbi wa chakula kulikuwa na bufee mbili na meza za wahusika wa kila semina ziliwekwa majina ya semina husika na bufee watakayotumia. Wakati anakaribia kuingia kwenye eneo la chakula kuna watu wanne walikuwa mbele yake, msichana na wanaume watatu.

Alipoangalia vizuri akagundua kwamba msichana yule, japo alikuwa amemtega kisogo ni yule mhudumu wa Twiga Executive Lodge na mmoja wa wale wanaume ni yule kijana mlinzi. Aligeuka mara moja na kurudi nyuma. Alirudi tena chooni haraka huku moyo ukimwenda mbio. Alihisi kwamba wale wanaume wawili waliovaa kiraia wanaweza kuwa askari polisi na pengine walitaka kutumia mwanya huo wa chakula kumnasa mpangaji aliyekuwa chumba cha Kigoma.

“Labda nimewafananisha,” alijisemea na kwa vile eneo la chakula lilikuwa ufukweni aliamua kutoka nje na kupitia njia nyingine kama anaweza kuwaangalia vizuri zaidi katika mazingira ambayo hawawezi kumwona. Alipotoka nje akaona Land Rover ya Polisi na mule ndani kukiwa na askari wawili waliokuwa wamevaa sare.

“Naona kumekucha. Lazima niondoke sasa hivi katika hili eneo,” alijisemea na kurudi kwenye chumba cha semina hotelini hapo. Hakuwa na haja tena ya kwenda kuhakikisha sura za watu wale. Pale kwenye semina alimkuta mhudumu aliyekuwa akilinda mizigo na vifaa vya wanasemina.

“Dada, nadhani unanifahamu vyema eh?”

“Wewe tena, ninakufahamu mkuu.”

“Sasa ninajisikia vibaya na hata chakula nimeacha. Nimerudia njiani. Ngoja nikapumzike hotelini.”

“Na kweli nilipokuja kuleta taarifa ya chai na hata ya chakula nilikuona umelela ukiwa umeegemea meza.”

“Kweli ninaumwa. Nimerudia mkoba wangu. Naondoka.”

“Sawa kaka, chukua tu.”

Jackson alichukua mkoba wake na kuondoka. Pale nje ya hoteli alichukua teksi na kuelekea hotelini alikofikia Andrew. Alipofika, alisimama nje ya hoteli na kumpigia simu Andrew na kumweleza kilichotokea.

“Aisee unasema kweli, kwa sababu hata sisi tunashangaa hapa tulipokuwa kwenye foleni ya chakula, tuliona watu wanapita wakimwangalia kila mtu usoni. Na hivi ninavyoongea wamehamia kwenye mstari wa bufee nyingine,” alisema Andrew.

“Sasa mimi naona niondoke sasa hivi kwenda stendi nirejee Dar es Salaam. Sasa hawa watu watanipa funguo kweli nichukue mzigo wangu?”

“Kuna huyo mhudumu wa mapokezi nina namba yake ngoja nijaribu kumpigia, uko hapo mapokezi?”

“Hapana, ngoja niende.”

“Basi nitapiga simu hapo baada ya dakika mbili.”

“Sawa.”

“Nimemwambia katibu mkuu ukweli kwamba tunadhani kwamba Bwana Malima ana uwezo mkubwa wa kuongoza Tume kuliko mtu mwingine,” Profesa Aboubakar Mwinchumu, Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Teknolojia na Mawasiliano, alimwambia makamu wake, Josiah Mafumu.

Profesa Mwinchumu ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia, alikuwa akiteta na makamu wake akiwa ofisini kwake.

“Tuseme katibu mkuu alikuwa anataka nini, Profesa?” Alihoji Mafumu.

“Alitaka tu kujua mpango tulio nao kuhusu mrithi wa Bw. Matakwali lakini ninajua hizi zote ni kampeni za Bruno. Kwa hiyo Bruno anahaha kuhakikisha anachukua hii nafasi wakati hafai.”

“Ni kweli, halali usingizi. Anajaribu kuweka mazingira kwamba anayepaswa kuongoza Tume ni muhimu awe mhandisi kama yeye. Hizi ni dhana za ovyo kwa sababu tunataka mtu wa kuongoza na siyo mtu wa kwenda field. Katibu mkuu ameelewa kweli?”

“Nadhani ameelewa. Na nimemtaka amwambie waziri kwamba endapo Mheshimiwa Rais atataka jina la atakayempitisha rasmi kuchukua nafasi ya Bw. Matakwali basi ni Malima. Lakini yeye ameshauri huyo tutakayempendekeza ni bora akaimu kwanza tuone uwezo wake. Nina hakika Tume itakuwa imepata mtu sahihi na atakayeleta mafanikio makubwa ndani ya uongozi wake,” alisema Profesa Mwinchumu.

“Ninajua Malima ni mtu makini sana na ndio maana hata Matakwali anampendekeza yeye na siyo Mapunda.”

“Ni kweli, Mapunda ni mzoefu kwenye Tume lakini mbambaishaji sana. Matakwali anakiri kwamba alichelewa sana kugundua vipaji vya uongozi kwa Malima na anasema kama unaona mabadiliko yoyote chanya kwa sasa kwenye Tume basi ni ushauri wa Malima. Isitoshe ni mtu mwadilifu sana, mchapakazi na anayeendana sawia na falsafa ya uadilifu ya Rais wetu. Kwa hiyo tutakapokutana na wajumbe wote wa bodi itabidi tuweke hadharani CV za hawa watu wawili.”

“Lakini Mapunda anafanya kampeni za kufa mtu. Isije ikawa wajumbe wote keshawakamata kwa sababu hata mimi juzi kanirushia laki moja na nusu akanitumia na ujumbe kwamba hicho ni kianzio. Labda ni wewe tu anayekuogopa pengine na mkurugenzi anayestaafu, Matakwali, kwa sababu ameshajua hayuko upande wake. Tutafanyaje hapo?”

“Hiyo pesa yake umeila?”

“Nitaila lakini simpendekezi abadani.”

“Hata mimi alinipigia simu na kuniambia eti kama kulionekana mapungufu huko nyuma niwe na uhakika atayasawazisha kwa kutumia uzoefu wake. Akasema maneno mengi ya kujaribu kuonesha kwamba Jackson bado haijui Tume sawasawa. Mimi nikamwambia maneno machache tu kwamba kiongozi anawekwa na Mungu na sisi ndiye atatuongoza kumpata mtu safi. Nikamwambia mtu huyo anaweza kuwa yeye au mwingine. Nilitaka kumwambia maneno ya Mwalimu Nyerere kwamba uongozi ni mzigo na kwamba mtu safi kabisa haukimbilii lakini nikaona nisimkatishe tamaa.”

“Sasa wajumbe wengi wakimpendekeza itakuwaje na kama unavyoona hata katibu mkuu amefikia kukuhoji mtazamo wako?”

“Watu wenye kura ya turufu pale ni sisi; mimi, wewe na Matakwali. Hana ujanja. Kupita kwake ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano.”

Endelea kufuatilia...
 
SIHUSIKI - 10

“Sawa mwenyekiti lakini wiki iliyopita nilikuwa ninaongea na Andrew Mambo, yule Meneja Rasilimali Watu, unajua yule nilimwacha Form One, ananiambia Mapunda amefikia hata hatua ya kwenda kwa waganga. Anasema Jumapili moja hivi karibuni walinzi walimwona na mtu anayeaminika kuwa ni mganga wa jadi usiku wa manane pale ofisi za Tume wakiwanga.”

“Duh! Bado katika karne hii huyu bwana anategemea matunguri?”

“Andrew unajua tunaongea naye sana. Ananiambia hata huko Tanga waliko kwenye semina Mapunda ana kazi moja tu ya kuhangaika kuhakikisha anakaimu yeye ukurugenzi. Yaani ni balaa.”

“Mwalimu Nyerere alisema kweli. Kwamba ukiona mtu anatafuta madaraka, tena kwa kuhonga honga pesa, mtu huyo ni wa kuogopa kama ukoma.”

* * *

Alikuwa mezani akimsaidia mwanawe, Hellen kufanya kazi za shule alizopewa kufanyia nyumbani. Msichana wa kazi alikuwa anaandaa meza kwa ajili ya chakula cha usiku.

Mkewe, Salome, ambaye ni ofisa uraghibishi katika asasi ya kiraia ya Mwanamke Lulu, inayopigania haki za mwanamke dhidi ya mfumo dume, alikuwa ametoka jikoni na kuketi sebuleni kujiandaa kuangalia taarifa ya habari.

Kama mwanaharakati na mwanasheria, mwanamke huyo alikuwa mpenzi sana wa kusikiliza taarifa za habari, kusoma magazeti na hata kuchangia maoni mbalimbali kwenye vyombo vya habari linapokuja suala la kutetea haki za wanawake.

Alikuwa na mwaka mmoja sasa tangu alipofanikiwa kuapishwa kama wakili wa Mahakama Kuu baada ya kufaulu mafunzo husika lakini alikuwa hajaanza kufanya kazi za uwakili kutokana na kubanwa na shughuli za uanaharakati katika asasi yao isiyo ya kiserikali ambayo ilikuwa inapata misaada mingi kutoka kwa wahisani.

Salome alikutana na Jackson Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wakati akiwa mwaka wa kwanza na Jackson akiwa mwaka wa mwisho. Walifunga ndoa siku chache baada ya Salome kuhitimu masomo hata kabla Jackson hajapata kazi.

Wakati muhtasari wa taarifa ya habari ya saa mbili ulipoanza katika kituo cha televisheni cha taifa, Jackson hakuwa anazingatia kinachoendelea ingawa alikuwa anasikia. Lakini aliposikia mtangazaji akisema kwamba miongoni mwa habari walizonazo Jumamosi hiyo usiku ni pamoja na ya baamedi kuuliwa kwa sumu na mpenzi wake wakiwa gesti mjini Tanga na kisha mwanaume huyo kutoweka, kulimfanya aondoke mezani ili kusikiliza taarifa ya habari.

“Hellen, endelea mama, ngoja kwanza nisikilize taarifa ya habari,” alisema akinyanyuka kwenda kukaa kwenye kochi. Moyo ulimdunda na mapigo ya moyo yakabadilika, jasho jembamba likaanza kumtoka na akatamani kuongeza kasi ya feni lililokuwa linazunguka juu ya kichwa chake pale sebuleni.

“Vipi, mbona hivyo, kuna shida yoyote?” Alihoji mkewe ambaye aligundua kwamba kuna kitu hakikuwa sawa kwa mumewe.

“Moyo umeshituka tu... Sasa nataka niache kunywa soda na vyakula vya wanga. Naona karibu nikumbwe na shinikizo la damu,” alilazimika kuongopa.

Waliendelea kufuatilia habari na hata mwanawe alipomfuata pale kwenye kochi kumuuliza swali, alimtaka asubiri kwanza taarifa ya habari iishe.

“Ngoja taarifa ya habari iishe. Hata hivyo utaendelea na mama yako, mimi ninajisikia vibaya,” alimjibu mwanawe.

Baadaye ikafika habari aliyokuwa anaisubiri Jackson na ingawa mapigo ya moyo yaliongezeka tena lakini akajitahidi kuisikiliza kwa makini. Kwa vile ilikuwa ni habari iliyohusisha masuala ya ukatili wa kijinsia, mwanaume kumuua mpenzi wake, Salome naye alikaa mkao wa kuisikiliza kwa makini huku akitamani kuchukua kalamu na karatasi. Akaamua kuirekodi kwa simu yake.

Mtangazaji alirudia ule muhtasari kisha akamwachia ripota wao kutoka Tanga kuendelea na habari ile. Mwandishi alimkariri Mkuu wa Jeshi la Polisi la mkoa wa Tanga, Naibu Kamishina wa Jeshi la Polisi Joel Kambi, akitaarifu kutokea kwa mauaji katika nyumba ya kulala wageni ya Twiga Executive Lodge iliyoko maeneo ya Sabasaba. Alisema msichana ambaye ni mhudumu wa baa alikutwa amekufa huku mwanaume aliyekuwa naye katika nyumba hiyo ya kulala wageni akitoweka na kunyofoa taarifa zake kwenye kitabu cha wageni.

Huku picha ya marehemu ikioneshwa kwenye skrini na kumfanya Salome aseme kwamba marehemu alikuwa mrembo na umri mdogo, mkuu huyo wa polisi alisema uchunguzi wa awali wa madaktari ulionesha kwamba marehemu alikuwa amenyweshwa sumu aina ya aconite.

Akasema kwamba sumu hiyo pia ilionekana kwenye chupa ya bia iliyokutwa chumbani humo. Mwandishi pia alimhoji daktari mmoja akaeleza kwamba kutegemea na wingi wa dozi sumu ya aconite inaweza kuua hapo hapo au baada ya saa kadhaa.

“Hii ni sumu ambayo hutumiwa zaidi na wafugaji wa mbwa. Mbwa wanapopata ugonjwa kama wa kichaa cha mbwa, ni sumu nzuri ya kuwaua lakini mwanadamu akitiliwa kwenye kinywaji humuua pia,” alisema daktari katika taarifa hiyo.

Mmiliki wa Twiga Executive Lodge naye alihojiwa akieleza kilichotokea na jinsi mtuhumiwa alivyofanikiwa kutoroka huku akinyofoa taarifa zake kwenye kitabu cha wageni pamoja na kuondoka na simu ya marehemu ili kupoteza ushahidi.

“Taarifa zilizopo ni kwamba mtuhumiwa ni mkazi wa Dar es Salaam aliyekuwa akishiriki kwenye semina hapa Tanga,” alisema mtu huyo.

Kwa upande wake, Meneja wa Tanga Raha Club alimwelezea marehemu kama mtu mcheshi na mchapa kazi hodari na kwamba siku ya tukio alikuwa buheri wa afya.

“Baa kadhaa za jirani zilishajaribu kumwiba Agnes kutoka kwetu lakini anakataa. Ni msichana tuliyekuwa tunamtegemea sana kwa kweli. Niseme tu ukweli kama wangeondoka wasichana watano nikabaki na Agnes wala nisingejali,” alisema Meneja huyo.

Meneja huyo aliendelea kumsifu Agnes Makata akisema ni msichana aliyesaidia sana kuwaunganisha wasichana wenzake katika klabu yake.

“Kama ni shuleni tunasema alikuwa ndiye dada mkuu. Mpaka leo kazi zimeshindwa kufanyika hapa klabuni tangu wenzake waliposikia kwamba Agnes hatunaye tena duniani na hasa tuhuma kwamba kauliwa na mtu aliyeondoka kwenda kupitisha naye usiku huo,” alisema Meneja huyo na kuanza kulia hadi mwandishi wa habari alipoanza kumbembeleza anyamaze.

Hata hivyo, Meneja huyo alipoulizwa baada ya kutulia kama anamjua mpenzi wa marehemu, alisema aliwahi kuwa na mchumba dereva teksi lakini waliachana. Lakini akasema alipowahoji wafanyakazi wenzake wakaonesha kwamba siku ya tukio aliondoka na mtu ambaye alionekana mgeni kwenye klabu yake.

Akasema kwamba siku hiyo inasemekana alionekana na wanaume wawili muda mrefu waliokuwa wameketi meza moja ambao inadhaniwa kwamba si wenyeji wa Tanga na kwamba aliondoka na mmoja wao.

Pia msichana aliyekuwa amepanga naye chumba kimoja, Mariamu Hafidh, alihojiwa akasema maneno ambayo hayakutofautiana sana na ya bosi wake, Meneja Makilikili.

“Tulipomaliza kazi Eggy aliniaga kwamba amepata buzi anakwenda kulichuna. Mimi nilisepa zangu lakini huyo mwanaume hakuwahi hata kunitajia jina lake,” alisema na kuongeza kwamba anaamini hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza kwa Agnes kuondoka na mwanaume huyo.

Alipoulizwa kama akimwona mwanaume huyo anaweza kumfahamu alijibu pengine anaweza kumtambua kwa sababu alimwona Agnes akiwa naye hadi walipokuwa wanakaribia kufunga huduma.

Itaendelea...
 
Alipoamua siku hiyo kuwa karibu na msichana anayehudumu katika klabu ya Tanga Raha, Jackson Malima ambaye pia alipachikwa jina la ‘Baba Mchungaji’ na wafanyakazi wenzake, hakujua kwamba hatua hiyo ilikuwa chanzo cha mlolongo wa matatizo lukuki; ndoa yake kutetereka, cheo cha ukurugenzi alichopaswa kupewa kuchukuliwa na mtu mwingine, na baya zaidi ni kujikuta akituhumiwa kwa mauaji ambayo hayajui…

Kutoka kwa mtunzi wa 'Gereza la Kifo'
Simu: 0758 143457


View attachment 1459809

JACKSON Malima, alitoka bafuni na kuangalia saa yake iliyomwonesha kwamba inaelekea saa mbili usiku. Akiwa bado amejifunga taulo, aliamua kuangalia taarifa ya habari kabla ya kutoka kama alivyokuwa amepanga.

Kwa takribani siku sita alizokuwa Tanga, alikuwa hajaangalia taarifa ya habari ya usiku kama ilivyo kawaida yake anapokuwa nyumbani kwake Dar es Salaam kutokana na kubanwa na ratiba.

Alipokuwa akitoka kwenye semina jioni, alilazimika ama kuandaa kile atakachowasilisha kesho kwenye semina au kwenda kutafuta chakula cha usiku alikotumia muda huo kubadilishana mawazo na wenzake.

Alishagundua kwamba pale kwenye klabu alipokuwa akienda kupata chakula cha usiku, mbali na kukosa utulivu hata kama angeomba wahusika waweke taarifa ya habari wasingemwelewa kwani kilichokuwa kinapendelewa zaidi na wengi ni mpira wa miguu au muziki.

Aliwasha seti ya runinga katika chumba chake alimofikia katika nyumba ya kulala wageni ya Twiga Executive Lodge na kuketi kitandani.

Taarifa ya habari ilimkaliza chumbani humo hadi saa tatu kasorobo alipozima runinga. Alivaa suruali ya michezo, tisheti ya rangi ya maziwa na raba kisha akatoka baada ya kuhakikisha kwamba hajasahau kuchukua fedha kidogo kwa ajili ya matumizi ya usiku huo.

“Binti, natoka kidogo,” alisema akikabidhi funguo za chumba chake kilichokuwa kimepewa jina la Kigoma kwa binti aliyekuwa mapokezi. Akaondoka.

Nyumba ya kulala wageni aliyofikia, kama zilivyo nyingine nyingi mjini Tanga, ilikuwa haiandai chakula cha mchana wala usiku zaidi ya kifungua kinywa asubuhi. Wateja walikuwa wakielekezwa kwenda kutafuta chakula katika hoteli, klabu au migahawa ya karibu.

Chakula cha mchana, Jackson na wanasemina wenzake walikuwa wakikipata katika Hoteli ya Kitalii ya Mkonge walikokuwa wakifanyia semina yao ya wiki moja ambayo sasa ilikuwa inaelekea ukingoni, huku yeye na wenzake wakilazimika kujitafutia chakula cha usiku. Jackson alikuwa ameamua kukaa katika nyumba hiyo ya wageni kutokana na kuwa eneo tulivu huku wenzake wanne aliotoka nao ofisi moja wakiamua kukaa katika nyumba za wageni zilizoko katikati ya jiji la Tanga.

Hao wenzake walikuwa wanywaji wa pombe na wapenda wanawake lakini yeye alikuwa akijitahidi sana kujitenga na mambo hayo, hali iliyofanya apachikwe na baadhi ya wafanyakazi wenziye jina la Baba Mchungaji.

Hata hivyo, baada ya semina mara nyingi alikuwa anakutana na wenzake hao pamoja na wanasemina kutoka taasisi zingine zilizokuwa zinashiriki kwenye semina hiyo usiku katika klabu ya Tanga Raha ambayo haikuwa mbali sana na alikokuwa amefikia.

Klabu hiyo ilikuwa inachangamka sana, hasa nyakati za usiku kutokana na kuandaa vyakula vya aina mbalimbali pamoja na vinywaji. Lakini kitu kilichokuwa kinavutia wateja wengi hususani wanaume ni uwepo wa wasichana warembo, wengi wakiwa ni wale waliojaaliwa kuwa na maumbo halisi ya Kiafrika.

Wasichana vimbaumbau pia walikuwepo wachache lakini wengi walikuwa ni wale ambao utadhani meneja wa klabu hiyo alikuwa akipita nchi nzima akisaka mabinti warefu, wenye sura za kuvutia na makalio makubwa.

Ilikuwa wastani wa takribani dakika nane kutembea kwa miguu kutoka nyumba ya wageni alimofikia Jackson hadi Tanga Raha Club kama bango lake lilivyokuwa linasomeka.

Wakati Jackson anafika kwenye klabu hiyo usiku huo, nje kulikuwa na magari mengi kiasi kwamba yeyote aliyekuwa akija kwa gari muda huo alilazimika kwenda mbali kidogo kuegesha gari lake. Ndani pia palikuwa tayari pamejaa watu kiasi kwamba upatikanaji wa viti ulianza kuwa wa shida.

Jackson alisimama pembeni karibu na mlango mkubwa akiangaza mahala ambapo anaweza kuona kiti aende kukaa. Kwa kawaida mwanga wa ndani ya klabu hiyo ambayo mchana ukipita unaweza kudhani ni godauni au gereji, ulikuwa si mkubwa sana. Wakati mwingine mpaka umkaribie mtu ndipo unamtambua.

Aliangaza huku na kule akitafuta pia kuwaona wanasemina au wafanyakazi wenzake katika Tume ya Teknolojia na Mawasiliano (TTM) ili kuungana nao lakini hakuona yeyote, labda kutokana na mwanga hafifu wa mahala pale. Alikuwa hana hakika pia kama mfanyakazi mwenziye na rafiki yake wa karibu, Andrew Mambo, alikuwa ameshawasili. Alisogea pembeni na kupiga simu yake lakini hakupokea.

Mara aliona wanasemina wawili wakiongozana na walipofika pale alipokuwa amesimama karibu na mlango, wakamsalimia. Wakasema wanahamia kwingine. Alipoangalia mahala walipotokea, akaona watu wengine wakiwahi viti walivyoviacha. Ilikuwa ni sehemu ambayo wapenzi wa mpira wakikaa wanaona vizuri kutokana na skrini kubwa iliyokuwa mahala hapo.

Wakati bado anaangaza macho huku na kule, msichana mmoja, mhudumu wa klabu hiyo, alimfuata na kumshika mkono.

“Habari kaka… Twende nikuoneshe mahala pa kukaa.”

Jackson aliandamana naye, hiyo ikiwa ni mara ya tatu au zaidi kuhudumiwa naye na sasa bila shaka kila mmoja wao alikuwa ameshamkariri sura mwenzake. Ni msichana ambaye kwa mtazamo wake alikuwa mrembo kupita wote katika klabu hiyo. Hata siku ya kwanza alipomwita amhudumie, binti huyo maji ya kunde ‘alimtikisa’ vilivyo Jackson lakini akaheshimu maadili aliyojiwekea.

Ukiwa ni mwaka wa 15 tangu afunge ndoa, Jackson alikuwa hajawahi kwenda nje ya ndoa yake. Mbali ya kumwogopa Mwenyezi Mungu anayewakataza viumbe wake kuzini katika vitabu vyake vyote, Biblia na Kurani, Jackson alikuwa hafikirii kwamba kuna siku atamsaliti mkewe mpenzi, Salome Bakunda. Ni mwanamke aliyempenda na kumridhisha kwa kila hali na hivyo hakuona sababu ya kuchepuka kama alivyokuwa akiona kwa wenzake akiwemo rafiki yake, Andrew.

Isitoshe, yeye alikuwa mshauri mkubwa wa wafanyakazi wenzake, hususani vijana waliokuwa wakianza kazi katika ofisi yao kuhusu kuzingatia maadili bora ya kazi, kujiheshimu, kuacha zinaa na kufanya yanayompendeza Mwenyezi Mungu.

“Kaka, inaonekana wewe hunywi lakini nadhani leo utanipa offer ya bia moja tu, yaani nina kiu sana kaka yangu… Nakuomba,” alisema yule binti baada ya kumpeleka kwenye meza moja iliyokuwa kwenye kona, upande wa kulia wa klabu hiyo kutoka lango kuu la kuingilia. Katika meza hiyo kulikuwa na viti vingine viwili vitupu lakini kule eneo la kuingilia alikokuwa amesimama awali alikuwa hawezi kupaona.

“Bia moja tu mdogo wangu, haya, nitakununulia...”

“Asante sana kaka… Enhe, nikuletee nini?”

“Nitapata kuku nusu wa kienyeji wa kuchoma na ndizi mzuzu mbili za kuchoma pamoja na mbogamboga?”

“Bila shaka kaka,” alijibu yule msichana akiachia tabasamu pana lililoanza kumgusa Jackson. Alitoa Sh 20,000 na kumuuliza kama kiasi hicho cha fedha kinatosha chakula alichoagiza na bia aliyoomba. Alijibu kwa bashasha kwamba kinatosha sana.

“Je, nikitaka soda pia ili niwe navutia muda wakati nasubiri kuku wangu, pesa inatosha?”

“Bado inatosha na chenji inarudi.”

“Basi niletee soda ya moto,” alisema kisha msichana yule ambaye muda wote alikuwa amesimama, akageuka na kuondoka.

Sasa Jackson, Mwanasheria Mkuu wa Tume ya Teknolojia na Mawasiliano (TTM), alipata wasaa mzuri wa kumtazama kwa nyuma na kung’amua kwamba uumbaji wa Mwenyezi Mungu Mtukufu ulikuwa umekamilika vilivyo kwa kiumbe wake huyo.

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia riwaya hii ya kusisimua...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J
Bushop a.k.a baba mchungaji welcome again
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom