Simulizi ( safari ya kijiji)

Simulizi ( safari ya kijiji)

luswaguty

Member
Joined
Oct 13, 2017
Posts
86
Reaction score
29
SIMULIZI
Mtunzi:Issa,M.M
Jina la simulizi:SAFARI YA KIJIJIN
......Ilikua ni saa 12:30 za asubuhi wakat nimejilaza kitandani Mguu mmoja nimeubwaga kule na mwengine kule utazani nimekufa maji nilijigeuza huku na kule ghafla nilijishika mkono wa kushoto nikagundua kua jana nilipolala nilisahau kuvua saa yangu ya mkononi niliitupia macho nikagundua tayar bado robo saa kutimilia sa moja kamili "dah! Kumbe bado robo saa" nilijisemea huku nikijienua kwa uvivu lakin kabla ya kusimama wima nilishtushwa na mlio wa sim yangu ilikua inaita "dah!!! Nani tena asubuhi yote hii ata mapambazuko bado...watu wengine bwana wanasumbua"nilijisemea kimoyo moyo huku nikiifata sim kiuvivu utazan nimelazimishwa
.....niliitupia macho ile sim nikagundua aliepiga ni mpenzi wangu Uwoya ambae tunasoma chuo kimoja cha Mwalim nyerere lakin yeye alikua ni mwaka wa pili na mimi mwaka wa kwanza"Dah!! kumbe ni Uwoya" nilijisemea na kuipokea
"Ooh baby Abdul nahitaji uje hom kijijin tuonane" Uwoya alisema kwa sauti nyororo ambayo ilinipa hisia za kimwili nikajikuta najibwaga tena kitandani kwa jinsi sauti ilivyokua na mionzi mikali
"Dah!!! Mpenzi wangu unanipa kazi sasa mimi nitakujua vipi kwenu sijaja ata siku moja afu kijijini mbali...aa aa njoo wewe jamani mjini"nilisema kwa unyonge na kwa sauti ya kimahaba kumbembelea mtoto uwoya lakin mh!!! Aligoma kinielewa
"Abdul mimi nitachukua mda kuja mjini sina plane ya kuja mjini siku hizi please nakuomba uje...mimi siku ngapi nakuja mjini kukufata wewe leo nataka uje wewe hom lakin unasema hukujui au huataki kuja" Uwoya alisema kwa huzuni fulani na kunifanya nikubali kwenda japo kua sikujui vema na kikubwa zaid mtoto Uwoya alishapoteza vyake vingi sana kwa ajili yangu
" Sawa uwoya usjali nitakuja" nikasema kwa unyonge
"Sawa wakati ukipanda gari mwambie konda akushushe sehemu inaitwa stone pub lakin kabla ya kufika nipigie simu ili nikusubiri sawa Abdul" Alisema Uwoya nami nikajikuta nakubali
"Sawa ntafanya hivyo" akakata simu
....kijana nikafanya usafi chap chap manukato fresh nikapiga pamba za ukweli japo kua nipoenda ni kijijini nilitaka Uwoya ajue kua mimi ni kijana wa mjini na zaid nikutaka kumfanya mtoto Uwoya azidi kunifurahia so kijana kikavaa kiukweli nikavaa kitown nikatoka ruti kuelekea njia kuu lakin Dah!!! Kwa bahati sehemu ile ya kusubiri gari palikua na watu wengi sana walikua wanasubir gari ambayo ndo hio ninayoisubir mimi ghafla ata mda haujaenda sana niliskia sauti za watu "gari inakuja hio" mh mtu mzima nikakaa sawa nikaweka rasket yangu vema mgongoni......INAENDELEA
 
SAFARI YA KIJIJINI
SEHEMU YA PILI....
Mtunzi:Issa M.M
.....niliweka rasket yangu vema mgogoni nikawa tayari sasa kusubiri gari na kila mmoja alikua yupo tayar kupambana na mwenzake ili apate kuwahi kuingia ndani ya gari......Mh gari kabla ya kutia nanga watu waliikimbilia na mimi nikiwa mmoja wao konda alipofungua mlango tu papatu likaanza konda alitupwa kule "oyaa dogo kaza alaah!!!" Mmoja wa makaka waliokua wanaleta vurugu kutaka kuingia ndani aliniambia na mimi kweli nilikaza kiume nikamshika ukosi mtu mmoja aliekua mbele yangu ili kujiskumia kwa mbele lakin wakati naishika ile shati"oyaa wacha shati yangu dogo" yule kaka niliekamata shati yake alisema kwa hasira lakin mwanaume nikakomaa sikuacha mpaka nikaingia ndani ya gari jasho linanitiririka "mama mama sogea upande wa pili apo" konda alisema na
Watu walizidi kujazana kwenye gari joto mtindo mmoja gari ilikaa kama daika saba bado haijaondoka"oyaa ondoa gari bwana gari limejaa ondoa bwana"watu walianza kulalama walipoona gari bado inazidi kukawia
"Oya dereva usizingue ondoa gari" mmoja wa abiria alisema nikataka kujua ni mtu wa aina gani maana sauti ilikua mzito nikamtupia macho Daah!kumbe ni jitu la miraba saba ata sauti yake ilikua ya kutisha hapo ndipo gari ikaanza kuondoka
Baada ya kama nusu saa hivi gari kuondoka ndani mlikua shuari kila mmoja alikua bize na lake............
"Bmkubwa samahani nataka nilale ila konda akisema Town pub niambie"nilimwambia mdada mmoja aliekua tumekaa siti moja na alioneka mzur kiasi kwamba watu kazaa walikua wanamtupia macho kwa jinsi alivyokua ata mimi nilimezea mate lakini ata hivyo mawazo yangu tayar yalikua yameshanasa kwa mtoto Uwoya ambae ndo ninae mfata kijijini na hafla usingizi ukanichukua..........
"WE KAKA WE KAKAA!!! amka tayari tushafika down pub" yule dada aliniamsha
"Eeee unasema!!!" Nilishtuka hafla na swali ambalo sikutarajia kuliuliza
"Tayari tumefika down pub"alisema tena yule dada kwa msisitizo
"Olaaa!!! Wakushuka ashuke bwana" konda alisema kwa ukali
"Nikajienua kwa haraka mpaka mlangoni
"Lete nauli dogo"konda alisema na mimi nikatia mkono mfukoni kutaka kutoa pesa naona lakin mtihani ulioje sikuona kitu nikatia mkono mfuko mwengine pia sikuona kitu
"Olaa dogo lete helaa mbona unachelewesha mda"konda alisema kwa ukali
"Subir konda kidogo!"nilisema kwa unyonge na mtihani zaidi ata sim haikuwemo
"Dah!!! Ata simu yangu haimo"nilijikuta najisemea baada ya kuona ata simu yangu haikuwemo ndani ya mfuko nilipoitia nikazidi kukodoa macho na hapo watu kazaa wakaanza kunitupia macho nikazidi kujisachi nilikua kama niliepumbaa
"OLAA DOGO!!! Ntakuzingua mimi lete nauli kama ushaibiwa sio mpango wangu mimi nipe changu upotee" konda alizidi kunikaripia na mimi sikua na lakufanya nikabaki nimetoa macho tu
"Konda shika hela yako na kata kabisa ya uyo kaka" ghafka niliskia sauti ikisema kutoka nje ya gari kumbe alikua ni yule mdada nilie kaa nae siti moja
"Ndo unamlipia sio"konda aliuliza
"Ndio namlipia uyo kaka"yule dada lisema
"Mimi au?" Nikauliza kwa pupa na mshangao
"Ndio nakulipia wewe" yule dada alisema na mimi nikashuka kwenye gari
"Dada panda gari tuondoke" kaonda alisema kumwambia yule dada
"Mimi mbona nishafika" yule dada alisema na hapo lile gari likaondoka nilibaki namshangaa yule dada kumbe na yeye alikua anashuka sehemu nilioshuka Mimi ilikua ni barabarani lakin hapakua na ngumba na ilikua mida ya jioni
"Kaka unaenda wapi" yule dada aliniuliza
"Ah!!! Dada angu kuna mtu aliniambia nishuke hapa lakini kabla ya kushuka alitaka nimpigie simu lakini nilijisahau kwenye gari na simu pesa zote zimeibiwa ntafaya nini mimi jaman na hii sehemu ndo mara yangu ya kwanza kufika hapa"nilimpa mkasa yule dada kwanini nilifika pale dah!!! Machozi yalikua yananilengalenga
"Kaka usjali ntakusaidia" alisema yule dada
"Utanisaidia vipi dada angu" nilimtupia swali ghafla yule dada
"Nifuate"alisema yule dada
"Dada angu nikufuate tuende wapi na mimi nimeambia nifikie hapa"nilisema kwa huzuni na kwa mshangao
"Mh kaka angu nishakwambia nifuate"alizidi kunisisitiza yule dada nimfuate dah!!! Maswali kazaa yalikuja akilin mwangu nimfuate au la.........INAENDELEA
 
nasubiri nione mwisho ndio nianze kusoma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom