0713417189
Senior Member
- May 12, 2021
- 108
- 196
- Thread starter
- #21
Duh! Vumilia kidogo.Mmh mimi haya mambo ya watoto kuteseka tena jaman ntashindwa japo ni hadithi
Duh! Vumilia kidogo.Mmh mimi haya mambo ya watoto kuteseka tena jaman ntashindwa japo ni hadithi
Asante ila tunalisongeshaDaah pole mwaya
Duh! Vumilia kidogo.
Noma saana
Nashushaaaa......njoo basi na huku tuendelee mkuu
nakungojaNashushaaaa......
shukranNTAGAMBI.......16
Mtunzi; Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304.( WHATSAP )
0622 738 310.
Tanga.
SEHEMU YA KUMI NA
SITA.
( 16 )
ILIPOISHIA...
Ntagambi nae hali ilizidi kuwa mbaya, tumbo likawa litatowa ngurumo kama za radi, akawa anamuangalia tu mtoto akilia. Nguvu za kumbeba hakuwa nazo tena.
"Uzito wa kudra za mateso umenipiga dafrau, kama tamviri. Nimeyumbishwa, sina wa kunisitiri, nayaona maisha kama laana. Naishia kusema laiti ningelikufa mapema." aliongea kwa uchungu mkubwa sana Ntagambi. Huku akiwa analia.....
ENDELEA NAYO.....
Ntagambi alikuwa pale akipapatika. Alipapatika kama mfamaji. Iwapo angekufa, wangesema alikufa kutokana na wingi wa mipapatiko. Mipapatiko iliyomlemaza na kumsomba kama mafuriko na baadae kumrejesha akiwa ameelea.
Kwa takdiri, hakuisaliti dunia. Aliamua tu kujikaza. Kifo nacho kiliona kweli alikuwa kapania kuishi. Kama kivuli cha mwizi wa kuku aliyefumaniwa, hichooooo, kilitikomea. Chidumu alikuwa si wa maji si wa uji. Mboga zile zilikuwa zimemkalia. Kwake yeye, alionekana kama kobe chini ya mgongo wa ndovu. Alizidi kulemewa. Povu mdomoni lilimtoka. Macho yalimtoka Pima. Pima kama nanigwanzula aliyebanwa na mlango. Hali ya sintofahamu ilimkumba Ntagambi.
Asijue afanye nini wakati ule. Akili ilisimama kuwaza. Ni kweli siku ya nyani kufa, miti yote huteleza. Mambo yalikuwa si mambo tena. Mambo yalikuwa yameanza kugeuka kama msimu. Aliona njia bora ni kulia. Kulia ili kuiyeyusha barafu iliyokuwa imegandamana kwenye kifua, na ubongoni mwake. Asiweze kuwaza!.
"Hii ndio zawadi nayostahili kupewa mimi kweli? wapendwa wangu wanaondoka, wakiwa katika mikono yangu. Nifanye nini? Dunia inanionea sana! amka Chidumu wangu. Uone ishara ya upendo katika paji langu la uso. Sioni kama tunaupenyo wa kuwa hai tena." alilamika Ntagambi huku akiwa anamtikisa kwa nguvu Chidumu, aone kama ataamka.
Ntagambi alijitahidi kuunyoosha mkono wake. Akashika chombo kilichokuwa na kile chakula akamwaga. Chakula hicho kilianza kuyeyuka chenyewe kikielekea ardhini. Hiyo ndio ikawa salama yao. Chidumu alishtuka na kuacha kutapika.
"Yuko wapi mwanangu? msogeze anione mamaye. Moyo wa uvumilivu umenifika mwisho. Nataabika hapa mimi kwanini? nakufa! nakufa! nakufa angali nikiwa bado binti mbichi kiasi hiki. Mwili si wangu tena huu. Nimetapika sana, mpaka mbavu zaniuma. Nalia sababu ya mwangu. Nalia sababu ya nchi yangu. Ila nakufa mwenyewe sababu ya maumivu yangu" ilikuwa ni sauti ya Chidumu akilalama kwa maumivu. Huku akimuomba Ntagambi ampe mwanaye.
Maneno hayo, yenye maumivu yalipenya mpaka kifuani kwa Ntagambi, na kuacha jeraha. Alimpakata Chidumu na kuanza kumbembelea, "Hakika sitakubali uondoke mapema kiasi hiki. Kumbuka bila wewe sina maisha mwenzio. Tulipotoka mpaka kufika hapa ni historia ndefu na ya kuumiza. Kile chakula ndio kimetuumiza, ulivyoona kivuli ungenijulisha tungemwaga. Nakupenda sana mpenzi" ni sauti ya kufariji kutoka kwa Ntagambi.
"Kifua changu nacho kimenisaliti. Mbona maziwa hayatoki jamani! mwanangu, utakula nini, tazama ulivyodhoofu. Huna tabasamu.Nisamehe mimi, kwa kukuzaa kisha uje kuteseka" alizungumza Chidumu, akijaribu kuzikamua chuchu zake, angalau mwanaye apate maziwa hata kidogo.
Ghafla kimya kilitawala, kwa dakika kadhaa katika kajumba hako ka miti. Waliwaza mengi, wakakumbuka mara kadhaa jinsi walivyonusurika na kifo. Kila mtu machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike, yakalowanisha mashavu yao na kudondoka kwenye nyasi zilizokuwa hapo chini.
Mtoto alilala, Chidumu akamlaza pembeni huku yeye akipiga magoti chini. Na kuikusanya mikono kwa pamoja, kama mtu ambaye yupo mbele ya madhabau. Akayainua macho yake na kutazama juu angani, huku akiwa anazungumza.
"Enyi mababu zetu wa ardhi ya Omulenga. Mnauona moyo wangu ulivyopondwa na magumu ya Dunia hii? hiki ndicho kilio changu cha mwisho kwenu. Hata huu moyo wangu umekauka sababu ya huzuni! Enyi mababu zangu. Iangalieni roho yangu iliyopondeka, inayolia na kuhuzunika ndani ya kijumba hiki cha miti. Mnihurumie mimi, ninaeteseka na kutoa machozi. Njoeni hima mnisaidie" hakuweza kuendelea kuzungumza, aliangua kilio kizito Chidumu. Akiwa amemuegemea kifuani Ntagambi.
Ntagambi alifanikiwa kumtuliza Chidumu. Akamfuta machozi, na kumwambia yote yatakwisha, na kubaki kama simulizi ya miaka mingi iliyopita. Isomwe na vizazi vijavyo vya ardhi ya Omulenga.
"Kumbuka kwamba wewe ndiwe chaguo la moyo wangu. Wewe ndiye ua la moyo wangu. Kumbuka kwamba, wewe ndiwe baba wa wa mtoto wangu. Naomba hilo uliafiki mwaaah" alizungumza Chidumu, akiwa amemkumbatia Ntagambi na kumbusu shavuni.
"Ewe baba wa mtoto wangu. Ewe kiyeyushi cha barafu ya moyo wangu. maji ya kitala changu. Ewe rutuba ya penzi langu. Nikumbatie. Sogea unipe busu, Nipapase." Mahaba yalinoga, ilikuwa ni sauti nyororo toka kwa Chidumu.
"Wewe ni maisha yangu, na siwezi ishi bila wewe. Maisha yangu bila wewe, kama kinywa bila meno. Nakupenda saana kipenzi changu," alizungumza Ntagambi. Wakacheka kwa pamoja huku wakiwa wanazigusanisha ndimi zao.
"Niweke karibu na uso wako. Niwe kama kitabu kizuri cha kupendeza. Nifunikie na penzi lako ninukie vizuri kama Ua la rahani. Hakika wewe ni dunia yangu. Wewe ni kila kitu kwangu. Wewe ndiwe uhai wangu, pumzi ya kuendesha uhai wangu. Moyo wako uwe kama kikumbatio cha uhai wangu" alizungumza Chidumu kwa mahaba mazito huku akijilaza chali na Ntagambi kumlalia kwa juu.
"Kushoto kumi, kulia ishirini. Tuzunguke haraka.Ni mwendo wa kutambaa. Kichwa chini, mshale juu. Macho mbele, nyuma na pembeni. Kichwa usawa wa nyasi kama nyoka." alitoa amri kwa kufoka. Kiongozi wa msafara wa askari.
"Yeyote atakayekatiza mbele, mwili wake ufyatuliwe mishale Kama mia" alitoa tena amri muongoza msafara.
"Omuleeeeeeee...!" kiongozi alitoa kauli mbiu, wakaitikia,
"Ngaaaaaaaaaaa...!"
"Omuleeeeeeee...!!"
"Ngaaaaaaaaaaa.." waliitikia kwa pamoja, kisha wakaendelea na safari.
Ntagambi na Chidumu wakiwa wamezama katika penzi zito, hapo ndani. Ghafla bin vuu walistushwa na mishale ya sumu, ikiwa imetuwa kwenye kijumba chao.
ITAENDELEA.........
Pamoja saaana.shukran
Noma saanaDuu Hatari tupu
Pamoja saanaSafi sana story nzuri...
hivi kesho sindo leo wajameni"Kesho panapo majaaliwa tunaendelea na simulizi ya NTAGAMBI."
"Si punde naachia."hivi kesho sindo leo wajameni