Simulizi: Ntagambi (1 _ 12)

NTAGAMBI.......15
Mtunzi; Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304.( WHATSAP )
0622 738 310.
0713 417 189.
Tanga.


SEHEMU YA KUMI NA
TANO.
( 15 )


ILIPOISHIA...
"Wahhhhhh.! Wahhhhh" mtoto alilia tena kwa sauti ya maumivu. Lakini awamu hii tumbo lilikuwa likivimba, pamoja na miguu. "Uchungu wa mwana aujuaye mzazi" Chidumu alishindwa kuvumilia, nae akaanza kulia. Ntagambi akawa na jukumu la kuwabembeleza wote wawili.

ENDELEA NAYO......
"Kuna majani kama yale, mama aliwahi nipaka. Nikiwa nimeugua ugonjwa wa ajabu usioeleweka" kumbukumbu hiyo ilimuijia ghafla Ntagambi, akakimbia na kuyachuma majani hayo. Akampaka mwanaye kwa utulivu. Dakika thelathini tu zilitosha kumrejesha mwanaye katika hali ya kawaida.

Kwa mara nyingine tena, Chidumu anatabasamu. "Hii misukosuko itakwisha lini?" Chidumu aliuliza. "Haya ni mapito tusikate tamaa!" alijibu Ntagambi. "Lakini kwa yale tuliyoshuhudia usiku, hapa pia si mahali salama!" alieleza Chidumu. "Ni kweli, usemalo. Nipo hapa naumiza kichwa ni wapi tuelekee. Tupo katika nyakati ngumu, uvumilivu ndio silaha pekee itakayotukomboa" alizidi kusisitiza Ntagambi.,

Upepo mkali ulikuwa ukivuma. Vumbi nalo lilizidi kutimka na kuzunguka kwa kasi ya ajabu huku likiikusanya kila aina ya taka. Tufani! Miti iliinama na kuinuka. Shwiii shwaaa zikisikika kule na huko. Ndege angani wenye rangi za kutamanisha na kuliwaza kwa pumbazo la kibakunja, hawakuachwa nyuma. Waliruka huku wakiziachia mbawa zao kwa madoido. Ni dhahiri walikuwa wakiikaribisha siku ya kipekee. Siku ambayo iliaminika vuli zingeungana na kuleta mvua kubwa ya masika....

Hiyo ndiyo hali ya hewa iliyokuwepo porini hapo. Ilikuwa ni siku ambayo Ntagambi aliamini ilishiba matumaini, na uzao upya wa maisha ya familia yake.

Himaya ya ardhi ya Omulenga.
Huzuni ilitanda, vilio visivyo na mwisho vikalipamba anga hilo. Malkia alikuwa katika mateso mapya. Kila alipokuwa anamkumbuka mwanaye, alilia sana, na kupoteza fahamu.

"Yuko wapi mwanangu jamani? damu yangu! kipenzi changu!. Ukute anateseka huko alipo! moyo wangu unaumia. Nateseka mimi, masikini ya Mungu. Sijui mwanangu kauawa au laa" alilamika Malkia. Machozi yakiwa yanambubujika bila simile.

Mfalme Bunini nae alikuwa hoi. Usiku na mchana askari walizunguka, kumsaka Chidumu. Walitamani ni bora wakaupata hata mwili wake akiwa mfu. Kuliko kuendelea kumtafuta pasi mafanikio.

"Natoa siku tatu za mwisho. Binti yangu apatikane!" alifoka kwa hasira mfalme. "Na yule kijana, tuliyemtoa gerezani akamtafute binti yangu. Kisha hajaonekana mpaka leo, mleteni hapa akiwa mfu!" alimalizia kuzungumza mfalme.

Ni wakati mgumu tena kwa askari. Njia na wao, wao na njia. Awamu hii walidhamiria kweli, kwamba liwalo na liwe. Walitumia farasi, wakiibeba mishale ya sumu. Mbwa wa kunusa harusu walitangulizwa mbele.

"Kwa taarifa tulizopata, alikimbilia katika pori hili!" alizungumza mkuu wa msafara huo.

"Huyu mbona tutampata tu!" alidakia askari wa pili.

"Twendeni tukakague pale, unaona mbwa wamekatali papo huku wakibweka" alizungumza askari wa tatu. Walipofika hapo wakakuta ni kama kijumba kimejengwa. Naam! ni kile kijumba cha awali alichokijenga Ntagambi, kisha akaondoka.

"Inavyoonekana huyu mtu aliishi hapa. Kasikia tunakuja kakimbia, najua hayupo mbali na hapa, tusonge mbele" ilikuwa ni sauti ya mkuu wa msafara akitoa amri.
Waliendelea na safari. Mishale ikiwa tayari kufyatuliwa kwa adui yeyote yule, ambaye angelikatiza mbele yao. Hii ya sasa ilikuwa ni kufa na kupona. Walijiapiza ni lazima Ntagambi apatikane, na binti mfalme pia.

"Twendeeee, twendeni, tupambane mpaka mwisho. Twendeeeni, tusichoke nasema twendeeee. Twendeeeni. Tuipiganie ardhi ya Omulenga, twendeni." askari walikuwa wakiimba njiani. Wakatamani angepatikana mtu kama marehemu mzee Moris mwenye uwezo wa kupiga ngoma kumi, ingependeza sana. Nyimbo hizo ziliwaongezea morali ya kuzidi kusonga mbele bila ya kuchoka. Yalibaki masaa kadhaa waweze kuikanyaga ardhi ya pori jipya lenye mandhari ya kipekee kabisa.

"Kwa hapa tuongeze umakini zaidi. Huyu mtu hayuko mbali!" alizungumza mkuu wa msafara. Wakapeana majukumu, wakajigawa katika makundi matatu. Kisha wakatawanyika kila kundi na upande wake. Anga lilikuwa limetulia tuli. Likawapa wepesi wakupanga mipango yao. Waliuchagua mwendo wa kunyata, ili adui yao asipate kushtuka na kujipanga zaidi yao.
Askari walianza kufyatua mishale ovyo. Wakawa wanafunga mitego katikati ya miti. Wakatengeneza na mabomu ya kienyeji ya kurusha. Lakini katika pori hilo. Walikuwa wakisikia kama watu wanalia, wengine wanaimba na kushangilia. Wakatafuta zinapotokea sauti hizo, lakini hawakufanikiwa.

"Mnasikia hizo kelele! zinatokea wapi?" alinong'ona kwa sauti ya chini kabisa askari mmoja. Wakiwa bado wanatafakari hilo. Awamu hii wakasikia kama mtu anachapwa fimbo na kulia kwa sauti ya juu. "Mniacheee!! mniacheee" sauti hiyo ilisikika hivyo.

"Mishale juu, tembea chini. Tumbo kwa nyasi, kidevu kwa ardhi. Tambaa kwa utayari, kaza mkono. Elekeza mshale kila Kona, haya tusonge" alitoa amri kiongozi wa msafara. Ikaanza kufyatuliwa mishale ya sumu. Sauti hizo za watu wasioonekana ziliwachanga Sana.

"Kipenzi changu! hapa si mahali salama kwetu" alizungumza Ntagambi.

"Ngoja tukae hizi siku mbili, kisha tuone tunaelekea wapi!" alijibu Chidumu.

"Huoni kama itakuwa hatari kwetu?" alihoji Ntagambi.

"Kikubwa tuwe makini sana!" alijibu Chidumu.

"Basi haina neno, andaa chakula, tuweze kula mapema!" alizungumza Ntagambi.

Chidumu aliamka na kwenda nje kuandaa chakula. Wakati huo Ntagambi aliutumia kunoa panga lake. Mapigo ya moyo yalimuenda mbio, akahisi hali ya usalama si shwari. Akaamua kujipanga mapema kwaajili ya usalama wa familia yake pendwa.

Chidumu aliingia ndani kuchukua kibakuli. Aliporudi anakuta kivuli cha mtu kimesisima lilipo jiko. Alipotokeza tu kivuli kile kilikimbia. Alishtuka ila akajua labda hajaona vizuri. Basi akaendelea na upishi. Alipika mboga za majani za porini na ugali kidogo. Walianza kula huku walikumbushana siku ya kwanza kuonana. Wakacheka sana huku wakigonga mikono yao kwa pamoja.

Walivyomaliza kula, zikapita dakika thelathini. Matumbo yaliwavuruga, si Chidumu wala Ntagambi. Walianza kutapika ovyo.

"Hiki chakula umeweka nini?" aliuliza Ntagambi, akiwa ameuweka mkono wake kinywani kuyakabili matapishi.

"Sijaweka kitu chochote!" alijibu Chidumu. Nguvu zilikuwa zimemuishia sababu ya kutapika. Maumivu makali ya tumbo yaliwakabili. Ntagambi akawa anajikaza huku anaumia. Chidumu alipoa akajikunja akiwa amelishika tumbo lake.

"Mwanangu nakuacha peke yako! naondoka mwanangu! tumbo, tumboooo, mama ayiiiiii. Aaah! nitunzie mwanangu, naumiaaaa, nipeleke kwa mama kabla sijafa" alilamika Chidumu akiwa analia, maumivu yalikuwa makali, akashindwa kuvumilia akapoteza fahamu.

Mtoto nae alianza kulia, Ntagambi mkono mmoja akilishika tumbo lake lililojawa na maumivu. Mkono mwingine akimpepea mkewe. Mwanamke kazimia, atamnyonyesha vipi mtoto apate kunyamza. Ulikuwa ni mtihani kwa Ntagambi.

Ntagambi nae hali ilizidi kuwa mbaya, tumbo likawa litatowa ngurumo kama za radi, akawa anamuangalia tu mtoto akilia. Nguvu za kumbeba hakuwa nazo tena.

"Uzito wa kudra za mateso umenipiga dafrau, kama tamviri. Nimeyumbishwa, sina wa kunisitiri, nayaona maisha kama laana. Naishia kusema laiti ningelikufa mapema." aliongea kwa uchungu mkubwa sana Ntagambi. Huku akiwa analia.....

********* ITAENDELEA ********














received_153933766528024.jpg
 
NTAGAMBI.......16
Mtunzi; Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304.( WHATSAP )
0622 738 310.
Tanga.


SEHEMU YA KUMI NA
SITA.
( 16 )


ILIPOISHIA...
Ntagambi nae hali ilizidi kuwa mbaya, tumbo likawa litatowa ngurumo kama za radi, akawa anamuangalia tu mtoto akilia. Nguvu za kumbeba hakuwa nazo tena.
"Uzito wa kudra za mateso umenipiga dafrau, kama tamviri. Nimeyumbishwa, sina wa kunisitiri, nayaona maisha kama laana. Naishia kusema laiti ningelikufa mapema." aliongea kwa uchungu mkubwa sana Ntagambi. Huku akiwa analia.....

ENDELEA NAYO.....

Ntagambi alikuwa pale akipapatika. Alipapatika kama mfamaji. Iwapo angekufa, wangesema alikufa kutokana na wingi wa mipapatiko. Mipapatiko iliyomlemaza na kumsomba kama mafuriko na baadae kumrejesha akiwa ameelea.

Kwa takdiri, hakuisaliti dunia. Aliamua tu kujikaza. Kifo nacho kiliona kweli alikuwa kapania kuishi. Kama kivuli cha mwizi wa kuku aliyefumaniwa, hichooooo, kilitikomea. Chidumu alikuwa si wa maji si wa uji. Mboga zile zilikuwa zimemkalia. Kwake yeye, alionekana kama kobe chini ya mgongo wa ndovu. Alizidi kulemewa. Povu mdomoni lilimtoka. Macho yalimtoka Pima. Pima kama nanigwanzula aliyebanwa na mlango. Hali ya sintofahamu ilimkumba Ntagambi.

Asijue afanye nini wakati ule. Akili ilisimama kuwaza. Ni kweli siku ya nyani kufa, miti yote huteleza. Mambo yalikuwa si mambo tena. Mambo yalikuwa yameanza kugeuka kama msimu. Aliona njia bora ni kulia. Kulia ili kuiyeyusha barafu iliyokuwa imegandamana kwenye kifua, na ubongoni mwake. Asiweze kuwaza!.

"Hii ndio zawadi nayostahili kupewa mimi kweli? wapendwa wangu wanaondoka, wakiwa katika mikono yangu. Nifanye nini? Dunia inanionea sana! amka Chidumu wangu. Uone ishara ya upendo katika paji langu la uso. Sioni kama tunaupenyo wa kuwa hai tena." alilamika Ntagambi huku akiwa anamtikisa kwa nguvu Chidumu, aone kama ataamka.

Ntagambi alijitahidi kuunyoosha mkono wake. Akashika chombo kilichokuwa na kile chakula akamwaga. Chakula hicho kilianza kuyeyuka chenyewe kikielekea ardhini. Hiyo ndio ikawa salama yao. Chidumu alishtuka na kuacha kutapika.

"Yuko wapi mwanangu? msogeze anione mamaye. Moyo wa uvumilivu umenifika mwisho. Nataabika hapa mimi kwanini? nakufa! nakufa! nakufa angali nikiwa bado binti mbichi kiasi hiki. Mwili si wangu tena huu. Nimetapika sana, mpaka mbavu zaniuma. Nalia sababu ya mwangu. Nalia sababu ya nchi yangu. Ila nakufa mwenyewe sababu ya maumivu yangu" ilikuwa ni sauti ya Chidumu akilalama kwa maumivu. Huku akimuomba Ntagambi ampe mwanaye.

Maneno hayo, yenye maumivu yalipenya mpaka kifuani kwa Ntagambi, na kuacha jeraha. Alimpakata Chidumu na kuanza kumbembelea, "Hakika sitakubali uondoke mapema kiasi hiki. Kumbuka bila wewe sina maisha mwenzio. Tulipotoka mpaka kufika hapa ni historia ndefu na ya kuumiza. Kile chakula ndio kimetuumiza, ulivyoona kivuli ungenijulisha tungemwaga. Nakupenda sana mpenzi" ni sauti ya kufariji kutoka kwa Ntagambi.

"Kifua changu nacho kimenisaliti. Mbona maziwa hayatoki jamani! mwanangu, utakula nini, tazama ulivyodhoofu. Huna tabasamu.Nisamehe mimi, kwa kukuzaa kisha uje kuteseka" alizungumza Chidumu, akijaribu kuzikamua chuchu zake, angalau mwanaye apate maziwa hata kidogo.

Ghafla kimya kilitawala, kwa dakika kadhaa katika kajumba hako ka miti. Waliwaza mengi, wakakumbuka mara kadhaa jinsi walivyonusurika na kifo. Kila mtu machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike, yakalowanisha mashavu yao na kudondoka kwenye nyasi zilizokuwa hapo chini.

Mtoto alilala, Chidumu akamlaza pembeni huku yeye akipiga magoti chini. Na kuikusanya mikono kwa pamoja, kama mtu ambaye yupo mbele ya madhabau. Akayainua macho yake na kutazama juu angani, huku akiwa anazungumza.

"Enyi mababu zetu wa ardhi ya Omulenga. Mnauona moyo wangu ulivyopondwa na magumu ya Dunia hii? hiki ndicho kilio changu cha mwisho kwenu. Hata huu moyo wangu umekauka sababu ya huzuni! Enyi mababu zangu. Iangalieni roho yangu iliyopondeka, inayolia na kuhuzunika ndani ya kijumba hiki cha miti. Mnihurumie mimi, ninaeteseka na kutoa machozi. Njoeni hima mnisaidie" hakuweza kuendelea kuzungumza, aliangua kilio kizito Chidumu. Akiwa amemuegemea kifuani Ntagambi.

Ntagambi alifanikiwa kumtuliza Chidumu. Akamfuta machozi, na kumwambia yote yatakwisha, na kubaki kama simulizi ya miaka mingi iliyopita. Isomwe na vizazi vijavyo vya ardhi ya Omulenga.

"Kumbuka kwamba wewe ndiwe chaguo la moyo wangu. Wewe ndiye ua la moyo wangu. Kumbuka kwamba, wewe ndiwe baba wa wa mtoto wangu. Naomba hilo uliafiki mwaaah" alizungumza Chidumu, akiwa amemkumbatia Ntagambi na kumbusu shavuni.

"Ewe baba wa mtoto wangu. Ewe kiyeyushi cha barafu ya moyo wangu. maji ya kitala changu. Ewe rutuba ya penzi langu. Nikumbatie. Sogea unipe busu, Nipapase." Mahaba yalinoga, ilikuwa ni sauti nyororo toka kwa Chidumu.

"Wewe ni maisha yangu, na siwezi ishi bila wewe. Maisha yangu bila wewe, kama kinywa bila meno. Nakupenda saana kipenzi changu," alizungumza Ntagambi. Wakacheka kwa pamoja huku wakiwa wanazigusanisha ndimi zao.

"Niweke karibu na uso wako. Niwe kama kitabu kizuri cha kupendeza. Nifunikie na penzi lako ninukie vizuri kama Ua la rahani. Hakika wewe ni dunia yangu. Wewe ni kila kitu kwangu. Wewe ndiwe uhai wangu, pumzi ya kuendesha uhai wangu. Moyo wako uwe kama kikumbatio cha uhai wangu" alizungumza Chidumu kwa mahaba mazito huku akijilaza chali na Ntagambi kumlalia kwa juu.

"Kushoto kumi, kulia ishirini. Tuzunguke haraka.Ni mwendo wa kutambaa. Kichwa chini, mshale juu. Macho mbele, nyuma na pembeni. Kichwa usawa wa nyasi kama nyoka." alitoa amri kwa kufoka. Kiongozi wa msafara wa askari.

"Yeyote atakayekatiza mbele, mwili wake ufyatuliwe mishale Kama mia" alitoa tena amri muongoza msafara.

"Omuleeeeeeee...!" kiongozi alitoa kauli mbiu, wakaitikia,
"Ngaaaaaaaaaaa...!"

"Omuleeeeeeee...!!"

"Ngaaaaaaaaaaa.." waliitikia kwa pamoja, kisha wakaendelea na safari.

Ntagambi na Chidumu wakiwa wamezama katika penzi zito, hapo ndani. Ghafla bin vuu walistushwa na mishale ya sumu, ikiwa imetuwa kwenye kijumba chao.

ITAENDELEA.........
 
NTAGAMBI.......16
Mtunzi; Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304.( WHATSAP )
0622 738 310.
Tanga.


SEHEMU YA KUMI NA
SITA.
( 16 )


ILIPOISHIA...
Ntagambi nae hali ilizidi kuwa mbaya, tumbo likawa litatowa ngurumo kama za radi, akawa anamuangalia tu mtoto akilia. Nguvu za kumbeba hakuwa nazo tena.
"Uzito wa kudra za mateso umenipiga dafrau, kama tamviri. Nimeyumbishwa, sina wa kunisitiri, nayaona maisha kama laana. Naishia kusema laiti ningelikufa mapema." aliongea kwa uchungu mkubwa sana Ntagambi. Huku akiwa analia.....

ENDELEA NAYO.....

Ntagambi alikuwa pale akipapatika. Alipapatika kama mfamaji. Iwapo angekufa, wangesema alikufa kutokana na wingi wa mipapatiko. Mipapatiko iliyomlemaza na kumsomba kama mafuriko na baadae kumrejesha akiwa ameelea.

Kwa takdiri, hakuisaliti dunia. Aliamua tu kujikaza. Kifo nacho kiliona kweli alikuwa kapania kuishi. Kama kivuli cha mwizi wa kuku aliyefumaniwa, hichooooo, kilitikomea. Chidumu alikuwa si wa maji si wa uji. Mboga zile zilikuwa zimemkalia. Kwake yeye, alionekana kama kobe chini ya mgongo wa ndovu. Alizidi kulemewa. Povu mdomoni lilimtoka. Macho yalimtoka Pima. Pima kama nanigwanzula aliyebanwa na mlango. Hali ya sintofahamu ilimkumba Ntagambi.

Asijue afanye nini wakati ule. Akili ilisimama kuwaza. Ni kweli siku ya nyani kufa, miti yote huteleza. Mambo yalikuwa si mambo tena. Mambo yalikuwa yameanza kugeuka kama msimu. Aliona njia bora ni kulia. Kulia ili kuiyeyusha barafu iliyokuwa imegandamana kwenye kifua, na ubongoni mwake. Asiweze kuwaza!.

"Hii ndio zawadi nayostahili kupewa mimi kweli? wapendwa wangu wanaondoka, wakiwa katika mikono yangu. Nifanye nini? Dunia inanionea sana! amka Chidumu wangu. Uone ishara ya upendo katika paji langu la uso. Sioni kama tunaupenyo wa kuwa hai tena." alilamika Ntagambi huku akiwa anamtikisa kwa nguvu Chidumu, aone kama ataamka.

Ntagambi alijitahidi kuunyoosha mkono wake. Akashika chombo kilichokuwa na kile chakula akamwaga. Chakula hicho kilianza kuyeyuka chenyewe kikielekea ardhini. Hiyo ndio ikawa salama yao. Chidumu alishtuka na kuacha kutapika.

"Yuko wapi mwanangu? msogeze anione mamaye. Moyo wa uvumilivu umenifika mwisho. Nataabika hapa mimi kwanini? nakufa! nakufa! nakufa angali nikiwa bado binti mbichi kiasi hiki. Mwili si wangu tena huu. Nimetapika sana, mpaka mbavu zaniuma. Nalia sababu ya mwangu. Nalia sababu ya nchi yangu. Ila nakufa mwenyewe sababu ya maumivu yangu" ilikuwa ni sauti ya Chidumu akilalama kwa maumivu. Huku akimuomba Ntagambi ampe mwanaye.

Maneno hayo, yenye maumivu yalipenya mpaka kifuani kwa Ntagambi, na kuacha jeraha. Alimpakata Chidumu na kuanza kumbembelea, "Hakika sitakubali uondoke mapema kiasi hiki. Kumbuka bila wewe sina maisha mwenzio. Tulipotoka mpaka kufika hapa ni historia ndefu na ya kuumiza. Kile chakula ndio kimetuumiza, ulivyoona kivuli ungenijulisha tungemwaga. Nakupenda sana mpenzi" ni sauti ya kufariji kutoka kwa Ntagambi.

"Kifua changu nacho kimenisaliti. Mbona maziwa hayatoki jamani! mwanangu, utakula nini, tazama ulivyodhoofu. Huna tabasamu.Nisamehe mimi, kwa kukuzaa kisha uje kuteseka" alizungumza Chidumu, akijaribu kuzikamua chuchu zake, angalau mwanaye apate maziwa hata kidogo.

Ghafla kimya kilitawala, kwa dakika kadhaa katika kajumba hako ka miti. Waliwaza mengi, wakakumbuka mara kadhaa jinsi walivyonusurika na kifo. Kila mtu machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike, yakalowanisha mashavu yao na kudondoka kwenye nyasi zilizokuwa hapo chini.

Mtoto alilala, Chidumu akamlaza pembeni huku yeye akipiga magoti chini. Na kuikusanya mikono kwa pamoja, kama mtu ambaye yupo mbele ya madhabau. Akayainua macho yake na kutazama juu angani, huku akiwa anazungumza.

"Enyi mababu zetu wa ardhi ya Omulenga. Mnauona moyo wangu ulivyopondwa na magumu ya Dunia hii? hiki ndicho kilio changu cha mwisho kwenu. Hata huu moyo wangu umekauka sababu ya huzuni! Enyi mababu zangu. Iangalieni roho yangu iliyopondeka, inayolia na kuhuzunika ndani ya kijumba hiki cha miti. Mnihurumie mimi, ninaeteseka na kutoa machozi. Njoeni hima mnisaidie" hakuweza kuendelea kuzungumza, aliangua kilio kizito Chidumu. Akiwa amemuegemea kifuani Ntagambi.

Ntagambi alifanikiwa kumtuliza Chidumu. Akamfuta machozi, na kumwambia yote yatakwisha, na kubaki kama simulizi ya miaka mingi iliyopita. Isomwe na vizazi vijavyo vya ardhi ya Omulenga.

"Kumbuka kwamba wewe ndiwe chaguo la moyo wangu. Wewe ndiye ua la moyo wangu. Kumbuka kwamba, wewe ndiwe baba wa wa mtoto wangu. Naomba hilo uliafiki mwaaah" alizungumza Chidumu, akiwa amemkumbatia Ntagambi na kumbusu shavuni.

"Ewe baba wa mtoto wangu. Ewe kiyeyushi cha barafu ya moyo wangu. maji ya kitala changu. Ewe rutuba ya penzi langu. Nikumbatie. Sogea unipe busu, Nipapase." Mahaba yalinoga, ilikuwa ni sauti nyororo toka kwa Chidumu.

"Wewe ni maisha yangu, na siwezi ishi bila wewe. Maisha yangu bila wewe, kama kinywa bila meno. Nakupenda saana kipenzi changu," alizungumza Ntagambi. Wakacheka kwa pamoja huku wakiwa wanazigusanisha ndimi zao.

"Niweke karibu na uso wako. Niwe kama kitabu kizuri cha kupendeza. Nifunikie na penzi lako ninukie vizuri kama Ua la rahani. Hakika wewe ni dunia yangu. Wewe ni kila kitu kwangu. Wewe ndiwe uhai wangu, pumzi ya kuendesha uhai wangu. Moyo wako uwe kama kikumbatio cha uhai wangu" alizungumza Chidumu kwa mahaba mazito huku akijilaza chali na Ntagambi kumlalia kwa juu.

"Kushoto kumi, kulia ishirini. Tuzunguke haraka.Ni mwendo wa kutambaa. Kichwa chini, mshale juu. Macho mbele, nyuma na pembeni. Kichwa usawa wa nyasi kama nyoka." alitoa amri kwa kufoka. Kiongozi wa msafara wa askari.

"Yeyote atakayekatiza mbele, mwili wake ufyatuliwe mishale Kama mia" alitoa tena amri muongoza msafara.

"Omuleeeeeeee...!" kiongozi alitoa kauli mbiu, wakaitikia,
"Ngaaaaaaaaaaa...!"

"Omuleeeeeeee...!!"

"Ngaaaaaaaaaaa.." waliitikia kwa pamoja, kisha wakaendelea na safari.

Ntagambi na Chidumu wakiwa wamezama katika penzi zito, hapo ndani. Ghafla bin vuu walistushwa na mishale ya sumu, ikiwa imetuwa kwenye kijumba chao.

ITAENDELEA.........
shukran
 
NTAGAMBI.......17
Mtunzi; Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304.( WHATSAP )
0622 738 310.
Tanga.


SEHEMU YA KUMI NA
SABA.
( 17 )


ILIPOISHIA...
Ntagambi na Chidumu wakiwa wamezama katika penzi zito, hapo ndani. Ghafla bin vuu walistushwa na mishale ya sumu, ikiwa imetuwa kwenye kijumba chao.

ENDELEA NAYO....
Mfalme Bunini, alikuwa wa kitandani. Upweke na mawazo yalikaribisha maradhi mengi katika mwili wake. Alizivuta pumzi kwa shida. Baadhi ya wananchi wa ardhi hiyo walilazimishwa kumuombea mfalme.

Jua liliitandika ardhi ya Omulenga. Mazao yakakauka, mifugo ikafa sababu ya uhaba wa marisho na maji. Ilikuwa ni vuta n'kuvute, vibaka wakatawala kila kona kutafuta ridhiki. Watoto wakadhoofika, wakinamama wakalia kwa kuwazika wapendwa wao sababu ya baa la njaa. Hakika ilikuwa ni patashika nguo kuchanika, katika himaya ya mfalme Bunini.

"Tusogee mbele kwa mwendo wa taratibu. Kila mmoja awe makini." ilikuwa ni sauti ya kiongozi wa msafara kwa askari.
"Tutawanyike tukipeana nafasi. Tuangalie kila pembe, huwezijua adui atatokea kona gani!" alizungumza askari wa kwanza.

"Kwa haya mazingira yanavyoonekana, huyu mpuuzi hayupo mbali!" alidakia askari wa pili.
"Huyu tunamshika, jiandaeni kwaajili ya kufyatua mishale huku tukisogea mbele!" alisisitiza kiongozi wa msafara.

Miti na matawi yaliyolizunguka eneo hilo yalionekana yakiyumba huku na kule. Askari wakajawa na taharuki, palionekana kama kuna mtu kajificha mahali pale. Wakalizunguka eneo hilo, baadhi ya askari wakawa wanatoa maneno ya vitisho,

"Jitokeze mwenyewe, kabla hatujaanza kukushambulia" hakuna mtu aliyejibu kutoka katika miti hiyo. Kiongozi wa msafara akapaza sauti iliyojawa na vitisho vya kila aina ndani yake,

"Nahesabu moja mpaka tatu, uwe umetoka humo! sasa ngoja tukuonyeshe kazi" baada ya kauli hiyo, askari walianza kufyatua mishale ya sumu isiyo na idadi.

Na hapo ndipo balaa lilipoanzia, katikati ya miti hiyo alitokeza mnyama mkubwa akiwa na madoa meusi yenye weupe kwa mbali. Alikuwa na uzito wa kilogramu elfu moja na miambili. Pembe mbili ndefu, meno yalijipanga ovyo kama Simba. Mnyama huyo ana sifa ya kulala masaa kumi na tano. Na analala akiwa amesimama, hapendi kelele. Nyama za viumbe hai Kama binadamu ndio chakula chake. Naam! waliingia katika vita mpya ambayo hawakuitaraji.

Ni bora ukachomwa na panga, kuliko pembe la mnyama huyo. Naam! ndivyo ilivyokuwa, askari walikuwa wakichomwa na pembe katikati ya tumbo, kisha kuinuliwa juu na kutupwa chini kwa kishindo. Hakuna aliyethubutu kuamka, zaidi ya damu kuchuruzika na kutapakaa chini ya nyasi hizo.

"Fyatueni mishaleeee" alipaza sauti askari mmoja. Baada ya kuona askari wanavyotobolewa matumbo yao. Walijuta, wakatamani kukimbia lakini, kwa kasi ya mnyama huyo wasingeweza kujinusuru kwa kutumia mbio.

Kiongozi wa msafara, alikuwa amejificha pembezoni mwa mti mkubwa. Akauvuta mshale wake vyema, akauelekeza nao ukatii amri na kwenda kutua katikati ya mdomo wa mnyama huyu.
"Nghruuuuuuuuuh...Nghruuuuuuh.." alitoa muungurumo wa ajabu mnyama huyo, kisha akadondoka chini, damu zikawa zinamtoka mdomoni, hakuweza kuamka tena. Askari walizivuta pumzi kwa fujo na kuzitoa nje taratibu. Mapigo ya moyo yakiwa yanawenda mbio na kuvifanya vifua vyao vipande na kushuka.

Hawakuamini kama mnyama huyo amekufa, basi wakaanza kumfyatulia mishale kadhaa akiwa pale chini. Wakawa wamemmaliza kabisa. Wakatafuta miti iliyokauka wakaipanga juu yake kisha wakamteketeza kwa moto. Wakavuta na wale askari waliouawa wakajumuisha katika moto huo. Ili wao waendelee na safari ya kumsaka binti mfalme pamoja na Ntagambi, waweze kuwafikisha mbele ya Mfalme.

"Tuweke silaha tayari, kila mtu mshale na panga lake liwe juu. Tusonge mbele" ilikuwa ni amri ya kishujaa na kijasiri kutoka kwa askari kiongozi.

Homa ilizidi kupanda, katika kile kijumba cha Ntagambi. Mapigano yote aliyasikia, lakini sehemu ya kutorokea ilikuwa ni lazima aonekane tu. Akaamua kutulia tuli ndani ya kale kajumba kake. Lakini Chidumu aliona penzi lao linaenda kufika kikomo. Akawa analia akiwa amemkumbatia mwanaye.

"Nilikwambia mapema, tuondoke hapa, kwanini hukunisikia?" alifoka Chidumu, akiwa anataka atoke mwenyewe na akimbie. Ntagambi alimzuia huku akimwambia,

"Mama, huu sio wakati wa kunilaumu. Tuko hatarini, na askari wa mfalme wale, wapo mbele yetu!" Ntagambi alizungumza kwa upole saana, akimsihi Chidumu.

"Acha nitoke, kama ni kunishika wanishike tu. Kuliko kufika hapa wakanifyatulia mishale wakatuuwa wote, nampenda mwanangu. Ni kumbukumbu ya zawadi bora kutoka kwako, sikotayari kuipoteza" alizungumza Chidumu, akiwa analia. Huku amesimama na kutaka kutoka ndani ya kajumba hako ka miti. Ntagambi naye alisimama, akauweka chini upanga wake nakuanza kutumia nguvu, kumzuia Chidumu asitoke.

Wakati wakiendelea na malumbano hayo mishale kumi, ilituwa tena kwenye kijumba chao. Awamu hii Ntagambi alizidi kuchanganyikiwa. Akaushika upanga wake, japo alikuwa na asilimia chache za kupona. Chidumu alimuelewa Ntagambi, hivyo nae akauchukua upanga pamoja na mshale, wakawa tayari kutazama upande wa kutokea.

Ntagambi kuchungulia nje, akamuona askari mmoja katangulia mbele akiwa na farasi. "Sasa inama tupite kwa kutambaa tukajifiche nyuma ya huo mwamba hapo nje" alinong'ona Ntagambi kwa sauti ya chini. Chidumu akafanya alivyoelekezwa.

Yule askari alishtuka, baada ya kuona kile kijumba, akadai kwa mbali kaona watu wawili wakitoka. Hivyo akawaambia askari wengine waongeze kasi.

"Mtoto akilia tu, basi tumekwisha!" alijisemea kimoyomoyo Chidumu. Lakini mtoto nae siku hiyo hakulia hata kidogo. Kana kwamba nae alikuwa ni miongoni mwa wapiganaji waliohitaji ukimya na vitendo tu dhidi ya maneno. Askari mwenye farasi alikuwa tayari amefika kwenye kijumba, akaona vyombo kwa ndani akawaambia wenzake wawahi. Ile anazunguka kwa nyuma alikutana na panga la shingo huku akizibwa mdomo. Alikuwa ni mwadada Chidumu katika umahiri wake wa kutumia panga. Wakamvuta farasi yule. Ntagambi akatangulia, Chidumu akafata huku mtoto akipakatwa kwa mbele. Farasi akatimua mbio.

"Waleeee wako wote wawili!" askari mmoja alipiga kelele, aliwaona Chidumu na Ntagambi wakiyoyoma na farasi. Naam! Mambo yalinoga, farasi kama zote zilimfukuzia Ntagambi, mapanga yakiwa juu. Ntagambi alipogeuka nyuma, anakuta askari wamemkaribia, alikata tamaa akasema liwalo na liwe.

Chidumu alikuwa akimpigapiga Ntagambi mgongoni huku akimwambia, "Wako nyuma hapa wamefika, wanatukamataaaaaa.!!" sauti hiyo kutoka kwa Chidumu ilikuwa ikimuumiza sana Ntagambi, na alipogeuka nyuma, kweli anaona askari wamemkaribia.

Akili ya Chidumu ilifanya kazi mara mbili. Akaushika upanga wake, shingo yake ikaangalia nyuma. Kila askari aliyewasogelea alijuta yeye pamoja na farasi wake. Chidumu alikuwa anawatembezea panga mpaka farasi anapoteza mwelekeo. Askari waliogopa kufyatua mishale baada ya kuona Ntagambi akiwa na Chidumu. Mfalme anautaka mwili wa bintiye akiwa hai, Lakini Ntagambi akipelekwa mfu ni furaha kwa mfalme.

Ntagambi alifika mbele, akakutana na mto mkubwa. Akawaza na kuwauza. Akisema asimame atashikwa, akaamua apite. Ile farasi anaruka kuingia katika mto huo, mtoto aliteleza kutoka kwa mamaye aliyekuwa bize na upanga. Akatumbukia mtoni.


"ITAENDELEA."


received_153933766528024.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom