Simulizi: Nilipanga nyumba moja na majini

Simulizi: Nilipanga nyumba moja na majini

gemplatnumz

Senior Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
133
Reaction score
371
SIMULIZI: THE HOUSE OF DEVIL
(Nyumba ya
kishetani)

Sehemu ya 01

MWANDISHI: METECK DERTHOD

MSIMULIAJI: HUMULI SAMAKI

TYPE: TRUE STORY (Simulizi ya kweli)

UTANGULIZI:

Kama kuna watu hawayajui haya
nitakayoyaongea basi nawataka kuanzia sasa
wajue kwamba, hapa Dar kuna mambo makubwa
sana ambayo ukisimuliwa unaweza kusema si ya
kweli, lakini wale wanaoyapata hayo mambo
wanajua na wewe usiombe yakukute hata siku
moja," ndivyo alivyoanza kusimulia Bw. Humuli
Samaki (43), mkazi wa Buguruni (kwa sasa)
ambaye alipata mkasa mzito akidai alipanga
nyumba moja na majini Magomeni, Dar es
Salaam.

SASA ENDELEA MWENYEWE

"Si zamani sana mkasa huu uliponitokea, ilikuwa
mwaka 2009 tu, kwa hiyo naweza kusema ni
juzijuzi tu. Kwa sasa naishi hapa Buguruni, baada
ya kuhama kutoka Magomeni ambako nilipata
mkasa mzito na wa kuogopesha. Nilipanga
nyumba moja na majini."

Mwaka huo (2009), awali nilikuwa nikiishi
Mwanyamala Mwinjuma, jirani kabisa na Makao
Makuu ya Bendi ya TOT, hata Kapteni John
Komba nilizoeana naye kwa kuonanaonana naye
pale CCM-Mwinjuma, ingawa jina langu najua
hakuwa akilifahamu.

Ile nyumba niliyokuwa nikiishi pale
Mwananyamala iliingia kwenye mgogoro wa
kifamilia na kufikishana mahakamani kwa ajili ya
kugawana mirathi. Hukumu ilipotoka ikaamriwa
iuzwe kisha ndugu wagawane fedha.
Kwa maana hiyo, mimi na wapangaji wenzangu
watano, tulipewa notisi ya kuhama baada ya
mteja kupatikana. Huyu mteja anaitwa Masawe
anafanya kazi Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) lakini sijui ofisi za wapi.
Ilibidi mimi niangalie mwelekeo mwingine,
niliamua nibadili upepo, nikaishi Magomeni. Kwa
wakati huo nilikuwa sina familia. Sina mke wala
mtoto hata wa kusingiziwa, kwa hiyo nilikuwa
naishi peke yangu. Ni mwaka jana ndiyo nimeoa
mke wangu huyu, anaitwa Hadija Mashada.
Rafiki yangu mmoja anayeitwa Mohamed Kombe
alinipa namba ya dalali kwani yeye anaishi
Magomeni hata sasa. Nilimpigia simu dalali wake,
anayeitwa Yusuf Mwamba, akaniita Magomeni
pale kwenye nyumba wanayosema aliwahi kuishi
Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Nilikwenda mpaka pale, nilimkuta amesimama nje
ya nyumba hiyo, tukasalimiana, akaniuliza nataka
nyumba yenye sifa gani, nikamweleza.

Niliwajibu mimi mwenyewe sijui, lakini sikumaindi
sana. Akaja mama mmoja aliyesema anaishi
nyumba ya pili, akasalimia na kuniuliza maswali.

"Hamjambo wanangu?"

Tuliitikia wote, akauliza nani anahamia pale kati
ya sisi wote, tulikuwa watano mbali na dereva.

"Ni mimi."

"Ooo, mzima baba?"

"Mimi mzima mama."

"Unaitwa nani?"

"Humuli Samaki."

"Unahamia peke yako au uko na mke na watoto?"

"Peke yangu mama."

"Humuli Samaki ni mwenyeji wa wapi?"

"Usukumani."

"Haya, naamini uliaga wakati unaondoka
nyumbani."

"Hilo lilikuwa la kwanza mama."

"Haya, kila la kheri."

Tuliendelea na kazi ya kuingiza vyombo ndani
hadi tukamaliza. Wale wenye gari wakaondoka,
nikabaki mimi peke yangu.
Nilijiwekea malengo kwamba, nihakikishe naweka
sawa kila kitu ili kesho yake nisiwe na kazi hiyo
zaidi ya kwenda kazini. Niliifanya kazi kwa muda
wa saa tatu, mpaka kwenye saa saba na nusu
usiku nikamaliza.

Nilibadili nguo, nikavaa taulo na kwenda kuoga.
Nilikuta bafu limetoka kutumika kama dakika
kumi nyuma, sikushangaa kwani si kuna
wapangaji wengine ambao tulitakuwa tunatumia
bafu moja.
Usiku kabla ya kuzima taa, nilizima taa,
nikapanda kitandani. Kabla sijapata usingizi,
niliwasikia wenzangu wakicheka sana na kuongea
huku wameweka muziki. Lakini ule muziki
haukuwa wa kiarabu, kizungu wala kiswahili.
Hata maongezo yao, mimi nilisikia sauti tu lakini
kusema walikuwa wanatumia lugha gani si rahisi.
Kuna wakati kama walikuwa wakiongea kihindi,
pia niliwasikia kama wanaongea kiarabu, nikajua
ni watu wa namna hiyo.
Lakini sikulala mpaka nikampigia simu dalali
kumuuliza kama wale wapangaji wenzangu ni
weupe au waswahili kama mimi, akasema hata
yeye hajui kwani hakuwahi kuwaona hata siku
moja..

.! ITAENDELEA
 
SIMULIZI: THE HOUSE OF THE DEVIL (Nyumba
ya kishetani)

SEHEMU YA 02

MSIMULIAJI: HUMULI SAMAKI
MWANDISHI: METECK DERTHOD

Endelea...

Lakini sikulala mpaka nikampigia simu dalali
kumuuliza kama wale wapangaji wenzangu ni
weupe au waswahili kama mimi, akasema hata
yeye hajui kwani hakuwahi kuwaona hata siku
moja.

Basi, nililala. Asubuhi niliamka nikiwa nimechoka
sana. Wakati nakwenda bafuni kuoga niligundua
ni mimi peke yangu ndiye niliyekuwa nimetangulia
kuamka, kwani bafuni hakukuwa na maji
yaliyomwagika kwa muda huo.

Baada ya kuoga nilirudi chumbani kwangu
kujiandaa kwenda kazini. Wakati najiandaa,
nilisikia mlango ukifunguliwa, nikajua ni wenzangu
wanakwenda kuoga au chooni kama ilivyo
kawaida kwa wanadamu wakiamka asubuhi.

Niliamua kutumia nafasi hiyo kuwatambua.
Nilivizia pale niliposikia mlio wa maji bafuni na
mimi nikatoka kwenda kupiga mswaki kwa marau
ya pili. Sehemu niliyosimama, mtu akitoka bafuni
kwenda ndani ilikuwa lazima nimuone kwani
ilikuwa kiasi cha kugeuka tu.
Lakini cha kushangaza, nilikuwa sisikii maji
kumwagika, nikageuka na kuona mlango wa
bafuni upo wazi. Mbali na mlango kuwa wazi, pia
chini nikaona alama za kandambili nne zikiwa
zimekanyaga, nikajua wametoka.

"Lakini wamepitaje hapa?" nilijiuliza.
Nilirudi ndani, mlangoni kwao nilikuta kandambili
pea mbili zikiwa bado na majimaji kwa mbali,
jambo hili lilinifanya nijiulize sana.

Nilijipa ujasiri na kuamua kuchungulia ndani ya
chumba hicho kwa kutumia nafasi ya katikati ya
mlango ambapo niliweza kuona hadi kitanda
lakini sikumwona mtu mwingine.
Niliingia kwangu, nikaweka mswaki, nikavaa vizuri
na kuondoka zangu. Nilitegemea wenzangu
nimewaacha ndani, kwani nilipofika mlangoni
nilikuta umefunguliwa na upo wazi. Nilirudi ndani
hadi kwenye mlango wao.

"Wa ndugu," niliita kwa sauti.

"Jamani wa ndugu."

Ukimya ndiyo ulinifanya nibaini walishaondoka.
Kwani kulikuwa kimya sana na kandambili
zilikuwa pembeni ya mlango si pale pa kwanza.
Nilifunga mlango mkubwa nikaondoka, mbele
nilimwona yule mama aliyekuja usiku kuniuliza
maswali. Alikuwa amesimama nje ya nyumba
yake, aliponiona akashutuka na kuita majina
mawili ya watu. Wakatoka watoto wake wawili, ni
mabinti wenye miaka kama kumi na nane na
ishirini na mbili hivi.

"Hujambo kijana?" yule mama alinisalimia kwa
furaha.

"Sijambo mama, shikamoo."

"Marhaba." Kisha akawaambia kitu wale watoto
wake nao wakanikazia macho.

"Mama umewaona majirani zangu hapa?"

"Majirani zako akina nani?"

"Wapangaji wenzangu."

"Kijana, kua uyaone ya dunia. We si umeshakua,
utayaona ya dunia."

Kauli hiyo iliniogopesha sana, nikashtuka na
kumuuliza mama.

"Mama una maana gani?"

"Sisi hatutaki umbeya kijana."

"We si umeambiwa utayaona kwa hiyo subiri tu,"

alidakia binti yake mkubwa.

Miguu ilitetemeka, mwili uliisha nguvu, nikajikuta
nataka kukaa, lakini sikuweza. Nilichoamua ni
kuondoka huku nampigia simu yule dalali.

"Vipi hujambo bwana?"

"Mimi sijambo."

"Za makazi mapya."

"Si nzuri bwana."

"Kwa nini tena?"

"Sielewielewi."
"Kivipi?"

"Kuna mambo kama si ya kawaida."
"Yapi hayo?"

ITAENDELEA...
NATAKA KULIKE KWA SANA PIA
COMMENT YAKO NI MUHIMU
 
SIMULIZI: THE HOUSE OF THE DEVIL (Nyumba
ya kishetani)

MSIMULIAJI: HUMULI SAMAKI

MWANDISHI: METECK DERTHOD

Sehemu ya 03

Endelea...

"Wale wapangaji wenzangu siwaelewi kabisa."

"Kivipi?"

"Ah! Watu gani mimi mgeni nimehamia
washindwe kutoka kunisalimia ili angalau
tufahamiane?"

Dalali alicheka sana kisha akasema:
"Wale ndivyo walivyo bwana, si unajua tena
malezi, mwingine kalelewa vile, mwingine hivi. Ila
ulichokisema ni kweli, haiwezekani nyumba
mnayoishi mpate mgeni halafu msitambuane,
sasa mkikutana njiani je?"

"Si ndiyo hapo sasa," nilisema nikijifanya lawama
zangu ni kwa ajili ya hilo tu, lakini kumbe
nilikuwa na zaidi ya hapo.

Kazini siku hiyo nilishinda sina amani, sina raha,
mwili ulikuwa kama umetoka kufanya kazi nzito
ambayo sijawahi kuifanya kwa siku nyingi,
wenyeji wa Pwani wanaita mavune.
Kwa upande mwingine nilitamani sana jioni ifike
ili nikaone siku hiyo kitatokea kitu gani kipya
kwenye nyumba ile. Jioni ilifika, nikaondoka
kazini, sikutaka kupitia popote, dukuduku langu
lilikuwa kwenda nyumbani tu.
Nilichukua kama saa moja kutoka kazini hadi
kufika nyumbani. Nje nilikuta mfuko wa rambo
mweusi, ndani yake ulionekana kuwa na kitu
kwani ulikuwa umetuna sana. Niliinama
kuipekenyua ili nijue ndani kulikuwa na nini,
nilishangaa kuona ni vipande vya nyama za
kuchoma tena vilikuwa vya moto
.
"Kha! Atakuwa nani ameweka?" nilijiuliza
mwenyewe, nikauacha palepale, mimi nikapanda
ngazi za kuingia ndani. Mlango ulikuwa wazi hali
iliyoashiria kwamba, wenzangu walisharudi.
Nilisukuma mlango, nikaingia. Nilikutana na
harufu ya pafyumu, nikahisi walikuwa wakijiandaa
kutoka.

"Jamani za leo?" nilisalimia kwa sauti ya juu
licha ya kwamba, mlango wao ulikuwa
umefungwa, hakuna aliyeniitikia, hilo sikulijali
sana kwani niliamini kwa kuwa walikuwa ndani,
isingekuwa rahisi wasikie salamu yangu.
Niliingia sebuleni kwangu, kisha nikaenda
chumbani, kuna kitu kilinishangaza, nikasimama
kwa mshtuko. Nilikuta sehemu nilipoweka kiberiti
asubuhi siyo, nilikiacha juu ya meza, nikakikuta
juu ya kitanda.

Niliacha kioo na kitana juu ya
kitanda, lakini nikavikuta kwenye stuli, niliguna!

Nilikishika kioo na kukiangalia kwa umakini kama
kina mabadiliko yoyote, lakini sikuona, nikashika
kitana. Nilipokigaua sana pia sikuona kitu cha
tofauti, nikaamua kuchania, nikahisi kuguswa na
kitu kama nywele ndefu kama za mtu aliyefuga.
Nilikiweka kitana juu usawa wa dirishani, nikaona
nywelenywele nene, nyeusi, mwili wote
ukasisimka.
Ninavyojua mimi, mwanamke mwenye nywele
nyingi akichania kitana, ndiyo huacha nywele,
sasa mimi nilikuwa na nywele fupi sana
zisingeweza kuacha nywele ndefu kwenye kitana.

"Mh! Hapa kuna kinachoendelea," nilisema
moyoni huku nikikaa. Nilishtuka zaidi kuona soksi
zikiwa kwenye msumari nyuma ya mlango wakati
niliacha chini.

"Huyu ni nani?" niliuliza kwa sauti ya ukali.
Ghafla nikasikia kicheko kutoka chumbani kwa
wale wenzangu. Nilikaa kwenye kochi, nikaanza
kuangalia sehemu mbalimbali za mle ndani
ambazo niliamini naweza kuona mabadiliko
mengine mbali na yale ambayo nilishayaona,
lakini sikubahatika.

Nilitoka, nikaenda sebuleni ambako nako nilianza
kuangalia kila kona ya sebule.

Nilishangaa kuona
glasi ya maji ya kunywa ambayo niliitumia
asubuhi kisha nikaacha maji yamejaa, ikiwa haina
hata tone la maji mbaya zaidi, iliwekwa juu ya
kabati ambapo mimi niliiweka kwenye meza ya
katikati ya sebule.

"Mh! Hii kali sasa," nilijikuta nikisema kwa sauti,

mara nikasikia kicheko tena kutokea upande wa
pili kule kwa wenzangu. Sasa nikaanza kama
kuhisi kitu kuhusu watu hao. Ni kwa nini kila
nilipoongea kwa sauti ndipo na wao waliangua
kicheko?

Niliamua kujaribu tena, nikasema kwa sauti:

"Nitakuja kuua mtu, kweli tena." Nikasikia
kicheko tena, safari hii kilidumu kwa muda.
Moyoni nikasema naanza kufanyia kazi uhusiano
wa maneno yangu na vicheko vya wale majirani.
Nilitoka kurudi chumbani, wakati napita kwenye
korido, nilisimama jirani na mlango wao.
Walikuwa wakiongea, lakini niliposimama mimi,
kukawa kimya ghafla kama hakuna watu.
Nilipozama chumbani, nyuma wakaanza kuongea
tena. Sikufunga mlango ili niweze kusikia
wanachokiongea, lakini jamani kwa kusema ule
ukweli wa Mungu, sikujua walikuwa wakitumia
lugha gani katika kuwasiliana hata pale
nilipojitahidi kutega masikio kwa umakini wa hali
ya juu sana.
Kuna wakati utadhani wanatumia sana neno
dotikom, lakini ukisema usikilize zaidi unasikia
wakisema sana kotoko au kiburate, wakati
mwingine sauti ya kike ilisema kaunto, ya kiume
ikarudia hivyohivyo, kaunto.
Nia yangu kubwa ilikuwa kuwaona kwa sura na
kufahamu kama ni ngozi nyeusi au nyeupe. Hilo
peke yake lingenipa mwanga ni watu wa aina
gani naishi nao pale ndani ya nyumba.
Nilisikia mlango wa chumbani kwao ukifunguliwa
na mimi nikatoka haraka sana, cha ajabu sikuona
mtu akitoka lakini mlangoni kulikuwa na
kandambili pea moja tu wakati zilikuwa pea mbili.
Hilo lilimaanisha kwamba, mmoja wao alitoka
kwenda chooni, nilichofanya ni kuamua
kusimama katikati ya mlango wangu ili huyo
aliyekwenda chooni akirudi nimuone. Ni kweli
mmoja wao alikwenda chooni kwani nilisikia mlio
wa maji.

NilijiTahidi kusimama mlangoni kwangu
kumsubiria. Kwa ramani ya nyumba ile ilivyo,
asingeweza kutoka chooni bila mimi kumwona
hata kama angekuwa anataka kutoka kwenda nje
au uani.
Mlio wa maji ulikosa kusikika, nikawa natumbulia
macho kule huku moyoni nikisema:

"Leo ndiyo
leo, asemaye kesho mwongo, hata afanyaje,
hawezi kunichenga hapa hata kidogo," nilisema
moyoni, ingawa wakati huo mapigo ya moyo
yalikuwa yakinienda kwa kasi.
Nilipoanza kuhisi muda unakwenda na hakuna
mtu aliyetoka, nikampa dakika tatu kwamba
lazima atakuwa anavaa ndiyo maana
anachelewa: "Labda alikuwa anajisaidia haja
kubwa, maana wengine huwa wanavua nguo
zote, lakini mimi nipo, siendi kokote," nilisema
moyoni nikiwa bado nimesimama mlangoni
kwangu.
Baada ya muda, nikasikia watu wakiongea
chumbani kwao, nikashtuka, nilijikuta nikisema:
"Haa!"
Haraka sana nilitupa macho mlangoni kuangalia
kandambili, nikazikuta pea mbili, nikashangaa:
"Ina maana amenipita hapahapa au?
Haiwezekani, asingeweza kunipita hata kama
ingekuwaje?" niliwaza. Nilitoka kuelekea chooni,
nikakuta mlango uko wazi, nikachungulia ndani,
hakukuwa na mtu, nikanyoosha mikoni, nikarudi
ndani.
Nilifikia kwenye kochi sebuleni, nikahema kwa
nguvu kwani niliamini nimo ndani ya miujiza
mikubwa ya ndani ya nyumba ile.
"Hivi ni kwa nini dalali alinidanganya hivi?"
nilijiuliza mwenyewe nikiamini kwamba, dalali
aliyenipangisha nyumba ile alijua mchezo mzima
ila alitaka kupata fedha tu ndiyo maana
alinipangisha bila kunipa tahadhari....!

ITAENDELEA...
 
THE HOUSE OF THE DEVIL (Nyumba
ya kishetani)

MSIMULIAJI: HUMULI SAMAKI

MWANDISHI: METECK DERTHOD

Sehemu ya 04

Endelea...

Nilitoka sebuleni, nikaenda chumbani, kitandani
nikakuta toilet paper' ikiwa imekatwa sehemu.
Mimi niliicha pembeni ya dirisha, lakini ikaonesha
kuna mtu aliichukua na kunyofoa kidogo kisha
badala ya kuirudishia palepale, yeye aliiacha
kitandani.

Mbali na toilet paper' pia kuna kikopo chenye
vijiti vyenye pamba za masikio kilikuwa kwenye
stuli jirani na kitanda, lakini kwa muda huo
kilikuwa kimeanguka chini halafu vijiti vimebaki
kama vitatu tu kwa maana kwamba, aliyeingia
kuchukua toilet paper' ndiye huyohuyo aliyechota
vijiti vya pamba.
Nilianza kuhisi kuwa sikuwa kwenye nyumba
salama, lakini kwa uthibitisho upi? Moyoni
nikasema nitajua tu, mimi ndiyo mimi.
Nilikaa ndani kwangu hadi usiku ulipoingia,
nikasema nibadili nguo kwa kuvaa bukta na
singilendi halafu nitoke kwenda kula gengeni
kwani siku hiyo sikuwa najisikia kupika chochote.
Ni mara nyingi nilipenda kula gengeni.

Nilitoka, nikasimama mlangoni ili nifunge mlango
wa chumbani, nilipoangalia chini, upande wa
wenzangu nilikuta nje ya mlango wao pana vijiti
vya pamba za masikioni vikiwa vimetumika,

nikiwa katika mshango, mbele nikaona tishu ikiwa
imefutiwa majimaji yenye rangi nyekundu kama
damu.
Nilitembea kwa wasiwasi, nikatoka nje, sikufunga
mlango kwa funguo, lakini niliubamiza tu, funguo
nilikuwa nazo, nikaenda gengeni kula.

Pale kwenye genge ambapo si mbali sana na
nyumbani, alikuja yule mama aliyeniuliza mimi ni
mtu wa wapi, nilimsalimia, lakini kabla hajaitikia
alishtuka kuniona.

"Upo kijana wangu?"Nipo mama, nimetoka kazini nimekuja kupata
kidogo."

"Pole sana, uoe sasa."

"Huo ndiyo mpango wangu mama."

"Ee, uoe halafu mimi nitakupa vyumba viwili pale
kwangu, nakuahidi."

"Nashukuru sana mama. Naanza kujipanga."

"Sawa, vipi wenzako lakini?"

Nilisita kumjibu, nikabaki namwangalia tu, naye
alibaini kwamba nimepata mshtuko na swali lake.

"Vipi wapangaji wenzako, naamini utakuwa
hujaonana nao?"

"Ni kweli mama, tena hebu nakuomba kidogo,"
nilisema nikienda pembeni kidogo ili na yeye
anifuate tukaongee.

"Niambie," alianza kusema.
Nilimuuliza kama kuna anachokijua chochote kile
kuhusu wale wapangaji wenzangu. Alianza kwa
kusema:

"Kusema ule ukweli sina kwa undani, ila napenda
kukwambia kwamba, unaishi na watu ambao
unahitajika moyo wa ziada ili uweze kuendelea
kuishi nao.

"Pale mbali na wewe, pameshakaa wapangaji
wengine saba, tena wote kama wewe, hawajaoa.
Lakini kinachoshangaza ni kwamba, wanaondoka
baada ya wiki mbili, mmoja aliondoka baada ya
siku tatu tu."

"Kwa hiyo hakuna hata mmoja aliyewahi
kukwambia ameona nini kule ndani?
"
"Hakuna."

"Lo! Mimi mama mambo ninayoyaona yanatisha."

"Kama mambo yapi, nisimulie kidogo."
Nilipotaka kuanza kumsimulia huyu mwanamke,
ghafla alitokea msichana mmoja, mweupe, mrefu
kiasi, amejazia sehemu mbalimbali za mwili,
akaguna na kusema:

"Kaka Humuli mambo vipi, za siku?"

Nilipata kigugumizi kikubwa kumjibu mambo poa
kwani sikumjua na sikuwa nakumbuka chochote
kuhusu yeye, sura yake ilikataa kichwani
mwangu.

"Wewe ni nani kwani?" nilimuuliza.
Akaachia tabasamu kwa mbali, uzuri wake
ukaongezeka.

"Ha! Humuli, hunikumbuki mimi, kweli?"
"Sikukumbuki hata kidogo."
"Sasa we binti, kama wewe ndiyo unamkumbuka
si umkumbushe mlionana wapi?" yule mwanamke
alisema kwa sauti ya mshangao.
Lakini yule msichana mrembo alimwangalia yule
mwanamke kwa macho yaliyojaa hasira

"Mama uhusiki."

"Najua, lakini unapoteza muda kwa
kuzungushazungusha wakati kumbe wewe
unamkumbuka, yeye umeshajua hakukumbuki na
amekwambia tayari."

Nilishangaa kumwona yule msichana akibetua
kichwa kama aliyekuwa akiweka vizuri nywele
zake, ghafla yule mwanamke niliyekuwa naye
akajishika kichwa na kulalamika kinamuuma
sana.

"Jamani kichwa! Kichwa jamani, daa!"
"Vipi mama, imekuwaje kwani?" nilimuuliza.

"Kichwa Humuli, kinavuta ghafla! Uwiii."
Nilianza kuogopa, nilihisi naangukiwa na msala
maana akifa pale na watu waliona nikienda naye

pembeni si nitahojiwa mimi?

"Kwani mama una kawaida ya
kuumwa kichwa?"

nilimuuliza nikimsogelea ambapo yeye sasa
alikuwa ameinama.

"Sina, ndiyo nashangaa hapa."

Niliona hakuna dawa nyingine zaidi ya kumpeleka
kwake ili nikaungane na familia yake kumpeleka
hospitali. Lakini kabla ya kufanya hivyo niliinua
macho ili nimwambie yule dada anisaidie na
kama anataka kunikumbusha, hayo yangefanyika
baadaye.
Ile naanaza kusema anti huku nikiwa nimeinua
macho, nilishangaa kutomwona yule msichana
pale.

"Khaa!" nilijikuta nikisema hivyo.

"Mama twende nyumbani ili tukupeleke hospitali
na watoto wako."

"Ha! Mbona kimeachia," alisema akionekana
kushangaa na kuniangalia, alikuwa amepanua
kinywa.

"Kweli?"

"Eee, niko mzima kabisa."

"Au?" nilitaka kusema neno lakini zikulimaliza,
nikahisi ulimi unakuwa mzito si kwa kushikwa bali
kwa matakwa yangu.

"Humuli."
"Naam."

"Ni kweli yule binti humjui?"
"Simjui mama."
"Kuna mawili hapo, humjui au humkumbuki."
"Vyote mama, simkumbuki na pia simjui."
"Lakini wewe si alikutaja kwa jina?"
"Mwenyewe nilishangaa sana."
"Basi Humuli nimeshaelewa, kwaheri, nimeelawa
ni kwa nini nimeugua kichwa na yule ni nani, pole
sana wewe kijana," alisema yule mwanamke
huku akiondoka zake kuelekea kwake.
Nilimtazama, lakini baadaye nilirudi kwenye
kibanda cha chipsi.
"Mzee nakuona na miss jini," muuza chipsi
mmoja alisema.
"Yupi, yule mwanamke?"
"Hapana, yule msichana."
"Mi simjui, kwani anaishi wapi?
Maana kasema
ananijua, ameniita na jina."

"Khaa! Kumbe wewe kama sisi. Huyu dada
anaishi mitaa hiihii, lakini hakuna hata mmoja
anayejua nyumba anayoishi!

"Kuna jamaa mmoja anaitwa Maleke, Maleke
aliwahi kumfuatilia kwa nyuma lakini alishindwa
kujua aliingia nyumba gani!"

"Mh! Au jini?" niliuliza kwa mshtuko mkubwa.

"Ndivyo watu wanavyosema, sasa alipokuja
kusimama na wewe, tukawa tunabishana,
wengine wanasema ni miss jini, wengine siye,
lakini alipokuwa anaondoka tukagundua ni miss
jini."

Basi, tuliishia hapo, nikachukua chipsi zangu na
kwenda nazo nyumbani, niliamua kwenda kulia
kule.
Nilifika, nikasukuma mlango mkubwa nikazama
ndani kwangu. Lakini wakati napita kwenye
usawa wa chumba cha wale wenzangu nikasikia
vicheko, tena vicheko kwelikweli.
Sikuwajali, nikaingia sebuleni kwangu, nikafunga
mlango kwa ndani, nikaweka chipsi juu ya meza,
nikaenda pembeni ya chumba ambako kuna ndoo
ya maji ili nichote ya kunawa. Wakati naanza
kula nilihisi na kugundua kitu. Niligundua
mabakimabaki ya chipsi na kuku juu ya meza
yangu wakati ukweli ni kwamba, tangu nimehamia
pale sikuwahi kula chipsi wala kuku
.
"Humu ndani kuna mtu anaingia kufanya mambo
yake, lini mimi nimekula chipsi na kuku humu
ndani?" nilijiuliza, nikasikia kicheko kutoka kwa
wenzangu.

"Haa! Haaa! Ha! Haaaa haah"

ITAENDELEA...
 
SIMULIZI: THE HOUSE OF THE DEVIL (Nyumba
ya kishetani)
MSIMULIAJI: HUMULI SAMAKI
MWANDISHI: METECK DERTHOD
Sehemu ya 05
Endelea...!
"Humu ndani kuna mtu anaingia kufanya mambo
yake, lini mimi nimekula chipsi na kuku humu
ndani?" nilijiuliza, nikasikia kicheko kutoka kwa
wenzangu.
"Haa! Haaa! Ha! Haaaah."
Niliinua macho kuangalia juu kwenye silingbodi'
kama vile niliyekuwa nimeona kitu, akili yangu
ikawaza kitu cha dakika chache nyuma, nacho ni
hiki:
"Humuli."
"Naam."
"Ni kweli yule binti humjui?"
"Simjui mama."
"Kuna mawili hapo, humjui au humkumbuki."
"Vyote mama, simkumbuki na pia simjui."
"Lakini wewe si alikutaja kwa jina?"
"Mwenyewe nilishangaa sana."
"Basi Humuli nimeshaelewa, kwaheri, nimeelawa
ni kwa nini nimeugua kichwa na yule ni nani, pole
sana wewe kijana."
Je, ni kwanini Humuli aliyarejea mazungumzo
yake na yule mwanamke aliyeumwa kichwa
ghafla? Nilianza kuamini kwamba, kuna uhusiano
mkubwa kati ya yule msichana na wale
wapangaji wa pale ndani nilipo, inawezekana
alinijua jina kwa sababu naishi nao na wana
uwezo wa kujua jina la mtu kulingana na
mazingira yao.
Pia niliwaza kwamba, kuna uwezekano mkubwa
yule msichana alitokea baada ya maono yao
kuniona mimi na yule mama wa jirani tukitaka
kuwazungumzia wao kama wapangaji wenye
maajabu hivyo hawakupenda iwe hivyo ndiyo
maana msichana akaibuka na kusababisha
mvurugano.
"Itakuwa kweli, ndiyo maana yule mama naye
alisema ameshajua ni kwa nini aliugua kichwa
ghafla, alijua yule msichana ni nani na kwa nini
yeye kasikia maumivu ya ghafla vile."
"Lakini pia kuna wale wauza chipsi, nao
niliwakumbuka hasa yule mmoja aliyesema yule
msichana wanamjua, anaishi mtaani, lakini
hawajawahi kubaini anaishi nyumba gani na kwa
mzee nani wala anajishughulisha na nini," hayo
yote niliyawaza mimi.
Nilisimama, nikachukua sabuni ya kuogea
ambayo haijafunguliwa, nikaipiga chini kwenye
kapeti kwa hasira huku nikisonya, nikasema kwa
sauti ya chini:
"Humu ndani naishi na majini."
Kule chumbani nikasikia wakicheka.
"Si unaona, nimes mimi, lazima naishi nao
humu ndani, da! Najuta sana," nilisema. Kicheko
kikasikika tena, safari hii kilikuwa cha juu zaidi
kuliko kile cha awali.
Moyo ulijaa mawazo, akili ilihisi uchungu wa
maisha, niliwaza fedha nilizozilipa kwa ajili ya
kupanga mle ndani, nikamkumbuka dalili,
niligundua alichofanya ni kunitapeli na hakuna
lingine wala hakuwa msaada kwangu.
"Mimi ni mwanaume, kama niliweza kupata fedha
za kupanga hapa, sishindwi kupata nyingine za
kupanga sehemu nyingine tena mbali na hapa,"
nilisema kwa moyoni.
***
Usiku nikiwa nimelala, nilichelewa sana kupata
usingizi, ghafla nikaona taswira za watu ukutani,
wawili tena wakiwa wamesimama, ni mwanamke
na mwanaume. Niliogopa sana, nikainua kichwa
polepole kuwaangalia kwa umakini, japo kulikuwa
na giza, lakini niliweza kuona vizuri lakini si kwa
uwazi mkubwa kama ambavyo taa ingekuwa
inawaka.
Ni kweli walikuwa watu wawili kama nilivyoona,
tena weupe nikimaanisha si watu weusi.
Walikuwa wakionesha vitendo vya kucheka huku
wakijinyonganyonga.
Kuna wakati walitembea mpaka jirani na kitanda
changu kisha wakageuza na kurudi pale ukutani.
Nilipeleka mkono hadi kwenye swichi ya kitanda
(bed switch), nikawasha, cha ajabu sikumwona
mtu wala dalili pale ukutani.
Niliamka nikiwa nahema kwa kasi mpaka
nikajishika kifuani, nikafungua mlango na kutoka
nje ili nijifanye nakwenda chooni lengo langu
lilikuwa kupata picha kwa wenzangu kukoje
maana niliwashuku wao na wale walioonekana
chumbani kwangu.
Kwa wenzangu niliwasikia wakikoroma kwa
zamu. Nikajiuliza ina maana si wao waliokuja
chumbani kwangu? Niliona ni utani wa hali ya
juu.
Niliamua kurudi chumbani na kukatisha safari ya
kwenda chooni, nikafunga mlango wangu kwa
funguo na kupanda kitandani, nilizima taa ili
nione kama yale mauzauza yatatokea tena.
Ukimya ulitawala kwa muda bila kujitokeza
chochote, nikaanza kupitiwa na usingizi kwa
kusinziasinzia, ghafla ukutani nikawaona tena
wale watu wawili.
Safari hii walikuja hadi kitandani, wakakaa,
wakasimama, wakaenda kwenye kabati,
wakafungua, wakatoa mashuka na kujifunika,
wakayarudisha, wakaenda nyuma ya mlango,
wakatungua mashati yangu mawili, wakagawana
na kuyavaa kisha wakayavua, mmoja mwanaume
akaenda sehemu yenye redio, akapeleka mkono,
nikajua anataka kuiwasha, lakini hakufanya hivyo.
Nilichoamua kukifanya akilini ni kuwasha taa kwa
ghafla na kuwavamia na nilipanga kumvamia
mwanamke nikiamini ndiye aliyekuja kule kwenye
chipsi. Polepole nilipeleka mkono hadi kwenye
swichi, nikawasha taa kwa ghafla huku macho
yangu yakiwa kwao, lakini sikumwona hata
mmoja! Kwangu haikuwa mapambano bali
nilichukulia kama changamoto za maisha.
Asubuhi, niliamka nikiwa nimechoka sana, lakini
kabla sijatoka kitandani nilisikia nje ya mlango
kukiwa na hali ya watu kutembeatembea tena
kwa kasi, niliinua shingo ili nione kama nitasikia
zaidi, lakini kukawa kimya.
Niliamka, nikatoka, nilikwenda sebuleni kwanza
kuangalia kama kuko salama.
Nilishangaa kukuta mezani kuna mfuko wa rambo
uliojaa chipsi kuku kama nilivyonunua mimi, lakini
zangu nilikula, sasa zile sikujua zilitoka wapi.
Niliubeba ule mfuko nikatoka nao, nilifungua
mlango mkubwa wa nje nikautupia pembeni
kidogo, niliporudi, nikaenda chooni, mlango
ulikuwa umefungwa kwa ndani kwani hata
niliposhika kitasa na kukivuta kilikuwa kigumu.
Hii iliashiria kwamba kuna mtu, kwa hiyo moyoni
nilisema nisimame palepale nje ya mlango hadi
atoke. Nilisimama eneo ambalo akitoka tu, uso
kwa uso na mimi.
"Tuone leo, wao si wajanja, leo nimemnasa
mmoja wao," nilisema moyoni. Dalili zote
zilionesha kwamba mle chooni mlikuwa na mtu
kwani niliweza kusikia hata kuhema kwake, mara
mlio wa maji, mara alikohoa, tena kwenye
kukohoa nikabaini mtu mwenyewe alikuwa ni
mwanamke ndiye aliyekuwa mle.
"We kohoa mpaka utapike, lakini mimi nipo hapa
mpaka utoke," nilisema moyoni. Nilikaa sana,
ikafika mahali nikachoka, lakini moyoni nikasema
siondoki hata iweje, lakini nilishtuka kitu,
niligundua muda mrefu sijazisikia zile dalili kama
maji au kuhema, nikafunguka akili. "Mh! Siyo
kwamba ametoka?"
Ile namalizia kusema ametoka?' nikasikia kicheko
kutoka kwenye chumba chao. Vicheko vikubwa
sana cha kike na kiume.
Nilirudi chumbani mwili ukinisisimka, hapo ndipo
niliamini mia kwa mia kwamba, nilikuwa nadili na
watu wasiokuwa wa kawaida.
Niliingia chumbani, nikampigia simu dalali.
"Haloo," niliita.
"Haloo. Halooo," nilirudia lakini sikupokelewa.
Nikiwa nimeachana na simu, mara iliita yenyewe,
alikuwa ni dalali nikapokea.
"Haloo," niliita.
"Haloo," niliitikiwa lakini sauti haikuwa ya dalali.
"Mzima bwana?" nilisalimia.
"Tuone leo, wao si wajanja, leo nimemnasa
mmoja wao."
Ha! Nilishtuka sana, nilisikia sauti yangu
mwenyewe ikisema hivyo. Ikaendelea.
"We kohoa mpaka utapike, lakini mimi nipo hapa
mpaka utoke."
Nilikata simu, nilikuwa nahema sana, mapigo ya
moyo yalikuwa yakienda kwa kasi ya ajabu huku
nikishindwa kuona sawasawa.
"Hii ni hatari sasa," nilisema.
ITAENDELEA..!
 
SIMULIZI: THE HOUSE OF THE DEVIL (Nyumba
ya kishetani)

MSIMULIAJI: HUMULI SAMAKI

MWANDISHI: METECK DERTHOD

Sehemu ya 06

Endelea...

"We kohoa mpaka utapike, lakini mimi nipo hapa
mpaka utoke."
Nilikata simu, nilikuwa nahema sana, mapigo ya
moyo yalikuwa yakienda kwa kasi ya ajabu huku
nikishindwa kuona sawasawa.
"Hii ni hatari sasa," nilisema.
Usiku wa siku hiyo sikulala kusema kweli kwani
kila nilipofikiria maisha yale sikuona sababu ya
kuendelea kuishi pale. Moyoni nilisema kwamba,
ni afadhali ningeishi na watu ambao ni
majambazi kuliko hawa, nafuu ningepanga
nyumba moja na makahaba kuliko kupanga
nyumba moja na majini.
Nilichoamua, asubuhi nikifika kibaruani tu niombe
ruksa kisha nianze kumsaka yule dalali na pia
nitafute dalali mwingine ambaye atanitafutia
vyumba kwingine na si maeneo yale tena kwani
niliyaona yana nuksi.
Asubuhi kulikucha salama kabisa, tena usiku wa
siku hiyo sikuona mauzauza wala dalili zake.
Nilikwenda kuoga bila kukagua mazingira, moyoni
nilisema liwalo na liwe kwa maana kwamba,
wawepo wasiwepo sawa tu.
Bafuni niligundua wameshaoga kwani kulikuwa
na majimaji ya muda mfupi uliopita. Nilipomaliza
kuoga, nilijiandaa na kutoka. Nje nilikutana na
mtu ana mkokoteni, akanisalimia.
"Za asubuhi bwana mkubwa?"
"Salama, karibu sana."
"Asante, kuna watu fulani wanaishi humu nina
shida nao."
Aliposema hivyo nilishtuka sana, niliamini yeye ni
mmoja wa wale ila amejigeuza kwa kujifanya ana
shughuli za mkokoteni.
"Unawajua kwa sura?" nilimuuliza huku nikiwa na
wasiwasi maana alinikazia macho.
"Siwajui."
"Sasa una shida nao kivipi watu usiowajua kwa
sura?"
Ni kwamba, kuna binti mmoja huwa wanamtuma
niwaletee maji, nikifika hapa huyo binti anabeba
madumu kupeleka ndani, sasa jana nilikutana na
huyo binti nikamuuliza kuhusu malipo yangu ya
mwezi sasa, akasema nije nifuatilie mwenyewe."
Nilishangaa sana kusikia hivyo. Nijuavyo mimi
mle ndani mna watu wawili, mwanamke na
mwanaume, sasa kama kuna binti hilo lilikuwa
jipya kwangu, labda lakini.
"Huyo binti naye anaishi humu au?" nilimuuliza.
"Sidhani, inaonekana kama huwa wanamtuma
tu."
"Kwa nini huamini kama anaishi humuhumu
ndani? Hafanani na wao wenyewe?" hili swali
niliuliza likiwa na mtego mkubwa sana, nilitaka
nijue uhalisia wake.
"Siwezi kusema hafanani wakati wao siwajui kwa
sura."
Hapo ndipo nilipopataka, nilidhani atasema
hafanani nao, ningejua ni walewale.
"Oke, nadhani wameondoka kwenda kazini."
"Ah! Sasa mimi fedha zangu nitazipataje jamani?"
"Subiri wakirudi jioni."
"Wewe utakuwepo?"
Nililishangaa swali hilo, hakuwa akinidai mimi
lakini anataka niwepo?
"Unataka niwepo?"
"Ee."
"Kwa nini?"
"Naamini utanisaidia kuzipata fedha zangu."
"Uliwahi kuja wakagoma kukupa?"
"Siyo hivyo, ila kila nikija, nikigonga mlango huwa
hawafungui."
"Basi nitakuwepo."
"Asante kaka. Nije saa ngapi?"
"Saa moja nitakuwa nimerudi."
Aligeuza mkokoteni na kuondoka zake huku
akisema:
"Muda huo nitakuwa nimefika kaka."
Niliondoka kwenda kazini kuomba ruksa. Lakini
wakati naondoka, mfanyakazi mwenzangu mmoja
aliniuliza nakwenda wapi, nikaamua kumsimulia
kwa ufupi kisa changu.
"Kha! Sasa hapo tatizo liko wapi, mbona dawa
ipo rahisi sana."
"Rahisi! Ni ipi hiyo?"
"Sikia, twende pembeni nikakusimulie," aliniambia
yule mfanyakazi mwenzangu huku akiangalia
kulia na kushoto kama mabosi watatokea.
Tulikwenda kusimama pembeni, akaanza
kuniambia:
"Sikiliza, kama unaishi nyumba ya namna hiyo,
unachotakiwa kufanya, kila siku asubuhi na jioni
au usiku unapuliza bangi ndani ya nyumba, kama
ni majini, mapepo sijui nini, utaona mambo poa
kabisa."
Sikuamini maneno hayo, nikamuuliza mara
mbilimbili kama ni kweli.
"Khaa! Nina mjomba'ngu aliwahi kuishi kwenye
nyumba ya hivyo, akaenda sehemu akaelekezwa
dawa ni hiyo, akaitumia, mpaka sasa anaishi kwa
raha hakuna cha majini wala mapepo," alisema.
Nilimsikiliza nikianza kuamini kwa mbali, lakini
nilifika mahali nikamuuliza hiyo bangi mimi
nitavuta au nitaiwasha ili itoe moshi yenyewe?
"Ukishaiwasha, utaiweka mezani au popote ndani
kwako, lakini angalia isizimike ili moshi wake
usambae chumba kizima au sebule nzima."
"Hilo linawezekana," nilimwambia nikimtumbulia
macho.
Kwa sababu nilikuwa nimeshaaga, ilibidi niondoke
tu na kurudi baadaye. Nilikwenda mtaani,
nilitafuta bangi nikapata maeneo ya Kariakoo,
nikaitia mfukoni.
Nilizurura sana siku hiyo, saa tisa kamili nilikuwa
njiani narudi kazini. Nilipiga hesabu za kufika
kazini na kuondoka, maana muda wa kazi ni saa
tisa na nusu.
Wakati napita pale Kituo cha Polisi Msimbazi,
fujo zikazuka, kuna machinga wawili walikuwa
wanapigana kwa sababu ya kugombea sehemu
ya kufanyia biashara, katika ugomvi huo mimi
nilibaini mmoja wao ndiyo mwenye kosa.
Nikampa laivu kuwa yeye ndiye mwenye tatizo,
alikuja juu, akachukua boksi lenye viatu na
kunirushia, likanipata kwenye bega la kulia,
sikukubali, nikaokota jiwe na kumrushia,
likampata mkononi.
Polisi walifika haraka sana, wakanikamata mimi,
yeye na yule machinga niliyeona anaonewa,
tukapelekwa Msimbazi polisi.
Tulipofika pale, afande aliyetukamata alituamuru
kuvua viatu, mikanda, simu kuweka pembeni.
Halafu mmoja alianza
kutusachi mifukoni. Wakati tendo hilo linaanza
kwa wenzangu, ndipo nikakumbuka mimi mfukoni
nina vipisi viwili vya bangi.
Nilitaka kutoka mbio kituoni hapo, lakini sehemu
tuliyokaa, ningesema nitoke, nisingefika nje au
hata kama ningefika ningekamatwa au kupigwa
risasi kama mhalifu, nilitetemeka, mwili uliisha
nguvu.
Ilipofika zamu yangu kusachiwa, askari
mwenyewe alishangaa kuniona nachezesha
miguu kama niliyebanwa na haja ndogo,
akaniuliza:
"We vipi, unaumwa?"
Nikamjibu naumwa afande.
"Unaumwa nini?"
"Sijui, nadhani homa."
Hakunijibu, alianza kwa kutumbukiza mkono
kwenye mfuko usiokuwa na kitu, akahamia wa
nyuma ambao una waleti, akapeleka wa kulia
kwangu ambao ndiyo wenye bangi, aliposhika,
akakunja sura, alipotoa akashtuka sana na
kusema:
"Haa! Hii bangi siyo?" ITAENDELEA..!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom