Chilojnr
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 302
- 1,306
Mawasiliano namba: 0718069269
Sehemu ya 01
Watu walishika vichwa vyao, vinywa wazi kuonyesha mshtuko walioupata, kila mmoja alikuwa haamini alichokuwa akikiona mbele ya macho yake. Ajali mbaya ya gari ilitokea Mwenge katika makutano ya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi na Sam Nujoma.
Gari ndogo aina ya Subaru iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aliyekuwa na asili ya Kiarabu ilirushwa juu, zilisikika sauti za watu wawili wakilia ndani ya gari hilo lililokuwa limeendeshwa kwa kasi ambalo liligongana uso kwa uso na lori la mchanga.
Ilikuwa ni ajali mbaya hata kwa kuiangalia kwa macho tu, gari hilo ambalo ilionyesha uzembe mkubwa wa dereva ama kugoma kwa breki lilipokuwa juu sauti za watu hao zilikuwa zikisikika lakini baada ya kutua chini, hapakuwa na sauti yoyote ile.
Watu waliogopa, wanawake wasiokuwa na mioyo migumu wakafumba macho yao na wengine kuondoka mahali hapo. Waliogopa, picha iliyokuwa imeonekana mbele yao ilitisha na kusisimua mno.
Wanaume kadhaa wakaanza kukimbia kulifuata gari lile ambalo baada ya kutua chini, lilibingirika kwa umbali fulani na kukaa mataili yakiwa juu. Walipofika hapo, kitu cha kwanza kukiona kilikuwa ni damu zilizokuwa zikitiririka barabarani katika vipande vya vioo vilivyokuwa vimevunjika.
“Jamani kuna mtu amepona humu?” lilikuwa swali la kwanza aliloliuliza jamaa ambaye alifika hapo huku akionekana kuwa na hofu kama wenzake.
Hapakuwa na mtu aliyemjibu, lilikuwa swali ambalo hakutakiwa kujibiwa kwa haraka mpaka pale ambapo watu wangewaona watu waliopata ajali hiyo ambao bado walikuwa ndani ya gari hiyo.
Watu wakavunja vioo vya dirishani na kuchungulia ndani. Waliwaona watu wawili, mmoja alikuwa mwanaume wa Kiarabu aliyenyoa kwa mbwembwe kabisa, alikuwa kimya, mdomo wake, pua vilipasuka kwa kiasi kikubwa, ni kama taya lilianza kuachia huku kichwani mwake akiwa amechomwa na kioo ambacho kiliingia ndani kabisa. Alikuwa amefariki dunia hapohapo.
Upande wake mwingine kulikuwa na msichana aliyekuwa kimya kabisa. Huyu hakuwa na majeraha makubwa zaidi ya damu ambayo ilikuwa ikimtoka puani tu, aliyafumba macho yake kama mtu ambaye alikuwa amekwishakata roho ndani ya gari hilo.
“Mungu wangu!” alisema jamaa mmoja alipomwangalia msichana huyo.
Haraka sana watu hawakutaka kupoteza muda, wakaanza kuwatoa watu hao ndani ya gari hilo. Maiti ya mwanaume huyo ikatolewa na kuwekwa barabarani na kisha msichana huyo kufuata.
Watu walijazana mahali hapo, walihitaji kushuhudia hao waliopata ajali kwenye gari hilo, walihitaji kujua walikuwa kwenye hali gani kwani kwa jinsi ajali ilivyotokea, kila mmoja alikuwa na uhakika hapakuwa na mtu aliyenusurika.
“Wazima hao?” aliuliza mwanaume mwingine huku akiwaangalia watu hao.
“Mwanaume amekufa ila sijajua kuhusu huyu msichana! Mh! Lakini mzuri kishenzi!” alijibu jamaa mwingine.
Alichokisema kilikuwa kweli kabisa. Msichana aliyekuwa akionekana mbele yao alikuwa mrembo mno, alivutia, alichanganyikana rangi, inawezekana kabisa mmoja kati ya wazazi wake alikuwa Mwarabu na mwingine Mswahili kama wengine.
Moja ya magari yaliyokuwa yakipita mahali hapo likasimishwa, haraka sana watu hao wakaingizwa humo na safari ya kuelekea katika Hospitali ya Lugalo kuanza mara moja.
Ndani ya gari hilo mbali na watu waliopata ajali na dereva kulikuwa na wanaume watatu ambao walikuwa wakiizungumzia ajali hiyo lakini kubwa zaidi walikuwa wakimzungumzia msichana yule ambaye sura yake ‘iliita’, alikuwa na umbo matata huku kifua chake kikiwa cha saa sita kabisa.
“Mh!” jamaa mmoja, wenzake walijua kwa nini aliguna, wote wakatabasamu, walitamani kucheka lakini hawakufanya hivyo kutokana na kile kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Baada ya dakika kadhaa wakafika katika hospitali hiyo, machela ikaletwa, watu hao wakateremshwa na kuingizwa ndani. Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwapima, mwanaume wa Kiarabu ambaye ndiye alikuwa dereva ilithibitishwa kufariki lakini msichana aliyekuwa pembeni yake alikuwa mzima japokuwa mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa mbali sana.
Akapelekwa katika chumba cha upasuaji ambacho kwa nje juu ya mlango kiliandikwa Theatre na kuanza kupata matibabu, madaktari walikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha msichana huyo anapata nafuu, muonekano wake ulionekana kuwaridhisha kidogo kwa sababu hakuwa na majeraha makubwa ila wasiwasi wao mkubwa ulikuwa ndani ya mwili wake.
“Miguu yake?” aliuliza daktari mmoja, haraka sana akashikwa miguu.
“Ipo safi!” alijibu daktari mwingine.
“Na mikono?”
Ilikuwa ni kazi ya kumwangalia kwa kumgusa kabla ya kumuingiza kwenye mashine ya MRI (Magnetic Resonance Imaging) na kuangalia sehemu zingine za mwili.
Kwa kila sehemu ambayo walimgusa alionekana kuwa safi, yaani hakuwa na mvunjiko wowote ule kitu kilichomfanya kila mmoja kuona alikuwa na bahati sana.
Walimtibu kwa saa moja katika sehemu ambazo walikuwa na hofu nazo na baada ya hapo walihitaji kujua zaidi kuhusu ndani ya mwili wake kama alikuwa na tatizo lolote lile.
Akachukuliwa, mlango ukafunguliwa na kupelekwa katika chumba kingine kilichokuwa na mashine ya MRI kwa lengo la kumwangalia kwa ndani zaidi ili wajue ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mwilini mwake. Akaingizwa kwenye mashine hiyo na kupigwa picha.
Kilichotoka, madaktari wote hawakuamini macho yao, msichana huyo mrembo alivunjika mgongo wake mara mbili, yaani pingili za uti wa mgongo zilivunjika juu na chini.
“Ni hatari!” alisema daktari mmoja kwa sauti ndogo.
Wanaume wale waliokuwa wamempeleka hospitalini pale walikuwa nje ya chumba kile wakisubiri, waliambiwa na madaktari kwamba hawakutakiwa kuondoka mpaka pale ambapo wangepewa majibu ya kile kilichokuwa kikiendelea, hivyo wakasubiri.
Mikononi mwao walikuwa na simu za watu hao, walitaka kuwasiliana na ndugu zao lakini kwanza wakasita, hawakutaka kufanya haraka mpaka pale ambapo wangepewa majibu ya kilichokuwa kikiendelea.
Baada ya saa moja na nusu daktari mmoja akawafuata watu hao na kuongea nao kirafiki, hakutaka kuwaficha, aliwaambia wazi kwamba yule mwanaume alifariki dunia hata kabla ya kupelekwa ndani ya hospitali ile kwa ajili ya matibabu.
“Hilo tulilijua! Na yule msichana?” aliuliza jamaa mmoja.
“Yupo mahututi! Hali yake ni mbaya sana!”
“Mbaya sana?”
“Ndiyo!”
Wakatamani kuwapigia simu watu wao wa karibu kwa lengo la kuwapa taarifa lakini simu zote zilifungwa, yaani ilikuwa ni lazima uingize namba ya siri na ndipo ufungue, hivyo wakashindwa kufanya hivyo.
Walichokifanya ni kumkabidhi daktari simu hizo na wao kuondoka mahali hapo kwani kama ni wema, waliufanya pasipo kuangalia ni nani.
Dokta alikaa na simu hizo kwa dakika kadhaa tu, marafiki na ndugu wa watu hao wakaanza kupiga simu ndipo dokta akapokea na kuwapa taarifa juu ya kilichotokea.
“Hospitali gani?” lilikuwa swali lililoulizwa na kila mtu aliyepiga simu.
“Lugalo!” alijibu daktari.
Je, nini kitaendelea?
Hii itakuwa inatoka kila Jumatano na Jumapili. Itakuwa inapishana na ile ya Ulimwengu Ndotoni Mwangu inayotoka kila Jumanne na Ijumaa.
Sehemu ya 01
Watu walishika vichwa vyao, vinywa wazi kuonyesha mshtuko walioupata, kila mmoja alikuwa haamini alichokuwa akikiona mbele ya macho yake. Ajali mbaya ya gari ilitokea Mwenge katika makutano ya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi na Sam Nujoma.
Gari ndogo aina ya Subaru iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aliyekuwa na asili ya Kiarabu ilirushwa juu, zilisikika sauti za watu wawili wakilia ndani ya gari hilo lililokuwa limeendeshwa kwa kasi ambalo liligongana uso kwa uso na lori la mchanga.
Ilikuwa ni ajali mbaya hata kwa kuiangalia kwa macho tu, gari hilo ambalo ilionyesha uzembe mkubwa wa dereva ama kugoma kwa breki lilipokuwa juu sauti za watu hao zilikuwa zikisikika lakini baada ya kutua chini, hapakuwa na sauti yoyote ile.
Watu waliogopa, wanawake wasiokuwa na mioyo migumu wakafumba macho yao na wengine kuondoka mahali hapo. Waliogopa, picha iliyokuwa imeonekana mbele yao ilitisha na kusisimua mno.
Wanaume kadhaa wakaanza kukimbia kulifuata gari lile ambalo baada ya kutua chini, lilibingirika kwa umbali fulani na kukaa mataili yakiwa juu. Walipofika hapo, kitu cha kwanza kukiona kilikuwa ni damu zilizokuwa zikitiririka barabarani katika vipande vya vioo vilivyokuwa vimevunjika.
“Jamani kuna mtu amepona humu?” lilikuwa swali la kwanza aliloliuliza jamaa ambaye alifika hapo huku akionekana kuwa na hofu kama wenzake.
Hapakuwa na mtu aliyemjibu, lilikuwa swali ambalo hakutakiwa kujibiwa kwa haraka mpaka pale ambapo watu wangewaona watu waliopata ajali hiyo ambao bado walikuwa ndani ya gari hiyo.
Watu wakavunja vioo vya dirishani na kuchungulia ndani. Waliwaona watu wawili, mmoja alikuwa mwanaume wa Kiarabu aliyenyoa kwa mbwembwe kabisa, alikuwa kimya, mdomo wake, pua vilipasuka kwa kiasi kikubwa, ni kama taya lilianza kuachia huku kichwani mwake akiwa amechomwa na kioo ambacho kiliingia ndani kabisa. Alikuwa amefariki dunia hapohapo.
Upande wake mwingine kulikuwa na msichana aliyekuwa kimya kabisa. Huyu hakuwa na majeraha makubwa zaidi ya damu ambayo ilikuwa ikimtoka puani tu, aliyafumba macho yake kama mtu ambaye alikuwa amekwishakata roho ndani ya gari hilo.
“Mungu wangu!” alisema jamaa mmoja alipomwangalia msichana huyo.
Haraka sana watu hawakutaka kupoteza muda, wakaanza kuwatoa watu hao ndani ya gari hilo. Maiti ya mwanaume huyo ikatolewa na kuwekwa barabarani na kisha msichana huyo kufuata.
Watu walijazana mahali hapo, walihitaji kushuhudia hao waliopata ajali kwenye gari hilo, walihitaji kujua walikuwa kwenye hali gani kwani kwa jinsi ajali ilivyotokea, kila mmoja alikuwa na uhakika hapakuwa na mtu aliyenusurika.
“Wazima hao?” aliuliza mwanaume mwingine huku akiwaangalia watu hao.
“Mwanaume amekufa ila sijajua kuhusu huyu msichana! Mh! Lakini mzuri kishenzi!” alijibu jamaa mwingine.
Alichokisema kilikuwa kweli kabisa. Msichana aliyekuwa akionekana mbele yao alikuwa mrembo mno, alivutia, alichanganyikana rangi, inawezekana kabisa mmoja kati ya wazazi wake alikuwa Mwarabu na mwingine Mswahili kama wengine.
Moja ya magari yaliyokuwa yakipita mahali hapo likasimishwa, haraka sana watu hao wakaingizwa humo na safari ya kuelekea katika Hospitali ya Lugalo kuanza mara moja.
Ndani ya gari hilo mbali na watu waliopata ajali na dereva kulikuwa na wanaume watatu ambao walikuwa wakiizungumzia ajali hiyo lakini kubwa zaidi walikuwa wakimzungumzia msichana yule ambaye sura yake ‘iliita’, alikuwa na umbo matata huku kifua chake kikiwa cha saa sita kabisa.
“Mh!” jamaa mmoja, wenzake walijua kwa nini aliguna, wote wakatabasamu, walitamani kucheka lakini hawakufanya hivyo kutokana na kile kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Baada ya dakika kadhaa wakafika katika hospitali hiyo, machela ikaletwa, watu hao wakateremshwa na kuingizwa ndani. Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwapima, mwanaume wa Kiarabu ambaye ndiye alikuwa dereva ilithibitishwa kufariki lakini msichana aliyekuwa pembeni yake alikuwa mzima japokuwa mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa mbali sana.
Akapelekwa katika chumba cha upasuaji ambacho kwa nje juu ya mlango kiliandikwa Theatre na kuanza kupata matibabu, madaktari walikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha msichana huyo anapata nafuu, muonekano wake ulionekana kuwaridhisha kidogo kwa sababu hakuwa na majeraha makubwa ila wasiwasi wao mkubwa ulikuwa ndani ya mwili wake.
“Miguu yake?” aliuliza daktari mmoja, haraka sana akashikwa miguu.
“Ipo safi!” alijibu daktari mwingine.
“Na mikono?”
Ilikuwa ni kazi ya kumwangalia kwa kumgusa kabla ya kumuingiza kwenye mashine ya MRI (Magnetic Resonance Imaging) na kuangalia sehemu zingine za mwili.
Kwa kila sehemu ambayo walimgusa alionekana kuwa safi, yaani hakuwa na mvunjiko wowote ule kitu kilichomfanya kila mmoja kuona alikuwa na bahati sana.
Walimtibu kwa saa moja katika sehemu ambazo walikuwa na hofu nazo na baada ya hapo walihitaji kujua zaidi kuhusu ndani ya mwili wake kama alikuwa na tatizo lolote lile.
Akachukuliwa, mlango ukafunguliwa na kupelekwa katika chumba kingine kilichokuwa na mashine ya MRI kwa lengo la kumwangalia kwa ndani zaidi ili wajue ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mwilini mwake. Akaingizwa kwenye mashine hiyo na kupigwa picha.
Kilichotoka, madaktari wote hawakuamini macho yao, msichana huyo mrembo alivunjika mgongo wake mara mbili, yaani pingili za uti wa mgongo zilivunjika juu na chini.
“Ni hatari!” alisema daktari mmoja kwa sauti ndogo.
Wanaume wale waliokuwa wamempeleka hospitalini pale walikuwa nje ya chumba kile wakisubiri, waliambiwa na madaktari kwamba hawakutakiwa kuondoka mpaka pale ambapo wangepewa majibu ya kile kilichokuwa kikiendelea, hivyo wakasubiri.
Mikononi mwao walikuwa na simu za watu hao, walitaka kuwasiliana na ndugu zao lakini kwanza wakasita, hawakutaka kufanya haraka mpaka pale ambapo wangepewa majibu ya kilichokuwa kikiendelea.
Baada ya saa moja na nusu daktari mmoja akawafuata watu hao na kuongea nao kirafiki, hakutaka kuwaficha, aliwaambia wazi kwamba yule mwanaume alifariki dunia hata kabla ya kupelekwa ndani ya hospitali ile kwa ajili ya matibabu.
“Hilo tulilijua! Na yule msichana?” aliuliza jamaa mmoja.
“Yupo mahututi! Hali yake ni mbaya sana!”
“Mbaya sana?”
“Ndiyo!”
Wakatamani kuwapigia simu watu wao wa karibu kwa lengo la kuwapa taarifa lakini simu zote zilifungwa, yaani ilikuwa ni lazima uingize namba ya siri na ndipo ufungue, hivyo wakashindwa kufanya hivyo.
Walichokifanya ni kumkabidhi daktari simu hizo na wao kuondoka mahali hapo kwani kama ni wema, waliufanya pasipo kuangalia ni nani.
Dokta alikaa na simu hizo kwa dakika kadhaa tu, marafiki na ndugu wa watu hao wakaanza kupiga simu ndipo dokta akapokea na kuwapa taarifa juu ya kilichotokea.
“Hospitali gani?” lilikuwa swali lililoulizwa na kila mtu aliyepiga simu.
“Lugalo!” alijibu daktari.
Je, nini kitaendelea?
Hii itakuwa inatoka kila Jumatano na Jumapili. Itakuwa inapishana na ile ya Ulimwengu Ndotoni Mwangu inayotoka kila Jumanne na Ijumaa.