Simulizi: Msichana Ndotoni Mwangu

Simulizi: Msichana Ndotoni Mwangu

SEHEMU YA 49


Genevieve aliendelea kugonga mlango kwa muda bila baba yake kuitikia, naye pia akaanza kulia akimwita bibi Magdalena aje ili waungane kusaidia kumfanya Phillip afungue mlango. Kwa muda wa nusu saa nzima bado walisimama nje ya mlango wakimsihi Phillip afungue lakini hakufanya hivyo zaidi sauti ilisikika kutoka ndani ya chumba ikiwaeleza wazi kwamba alitaka kufanya uamuzi mgumu hivyo alihitaji nafasi.
“Phillip lakini ni vyema ukatambua kwamba maisha baada ya kifo cha mkeo ni lazima yaendelee.”
“Najua hilo tangu mwanzo lakini inauma, ni bora nikaungana nao.”
“Usimkufuru Mungu na huyu mtoto?”
“Mtoto? Ah! Atapata wasamaria wema wengine wa kumtunza.”
“Baba! Baba!” Genevieve aliita na kwikwi ya kulia ikamkaba, hakuongea tena kitu akatoka mbio eneo hilo na kukimbilia ndani ya chumba kisha naye kujifungia.
Ukawa ni mtihani kwa bibi Magdalena hakufahamu nini afanye kwani kila kitu kilionekana kwenda kombo, kwa muda aliendelea kusimama eneo hilo akitafakari nini cha kufanya hatimaye wazo likamjia ndani ya kichwa chake kwamba ni lazima Phillip akubali kushuka kwani hali ya Genevieve ilikuwa mbaya kutokana na sentensi aliyokuwa ameitamka muda mfupi uliopita.
“Genevieve ameumizwa na kauli yako, hivyo amekimbia kuelekea chumbani, kwa ujumla ameumia.”
“Unasema?”
“Hivyo ndivyo, tafadhali nakusihi utoke na kumwendea ili kumbembeleza.”
Ukimya wa ajabu ukatokea na sekunde tatu tu mlango wa chumba ukaonekana ukifunguliwa na Phillip kutokeza huku jasho jingi likitiririka mwilini mwake, hakusema kitu zaidi ya kukimbia kuelekea upande ambako ndiko chumba cha Genevieve kilikuwepo. Akausukuma mlango na kuingia ndani ya chumba na kilichosikika muda mfupi tu ndani ya chumba hicho ni kilio, wote wawili walikuwa wakilia.
***
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam ndimo Mariya, Merina na Mwanasheria wao walipokuwa wamefikia hapo ndipo pangekuwa nyumbani kwao kwa muda wote ambao wangekuwa Afrika, nchini Tanzania kusaka ukweli wa maisha ya baba yao Victor Federov kwa gharama yoyote ile.
“Tutapumzika leo na kesho tutaanza mchakato, lazima kwanza tuitishe mkutano na waandishi wa habari lakini kabla ya hayo tunahitaji kukutana na mtu mmoja ambaye tutamfanya rafiki huyo ndiye atatusaidia.”
“Mh! Naona kama ni zoezi gumu kidogo,” Mariya.
“La hasha! Ni kitu rahisi nitampata mtu hapa hapa hotelini,” mwanasheria aliwaambia.
“Haya ngoja tuone lakini pia uwe makini kwani hapa tupo ugenini,” Mariya alishauri.
“Usiwe na shaka Mariya kila kitu kitakwenda sawia.”
Baada ya mazungumzo hayo kukamilika pamoja na kwamba alikuwa ni mgeni kabisa, Morgan alitoka ndani ya hoteli hiyo kuangalia mazingira akitafuta ni namna gani angepata msaada ambao ungemsaidia kufanya kazi yake kwa urahisi, kwa kutumia lifti akashuka mpaka mapokezi hapo akawasabahi watu aliowakuta na ghafla kabla hajapiga hatua kutoka nje ya hoteli hiyo macho yake yakagongana na mtu aliyekuwa ameketi pembeni kabisa mwa hoteli hiyo mkononi akiwa na gazeti lililosomeka Uwazi, akapata hamu ya kusogea karibu yake ili aongee naye mambo kadhaa kwake hiyo akaiona kama bahati.
“Habari?” alisabahi kwa lugha ya Kiingereza.
“Nzuri tu,”
“Ah! Naitwa Morgan natokea Urusi.”
“Oh! Karibu mimi naitwa Erick Evarist naishi hapa hapa Tanzania,” Erick alijitambulisha.
“Naweza kuungana na wewe hapa?”
“Bila shaka karibu.”
“Napenda kukufahamu zaidi.”
“Ni mwandishi wa habari nafanya kazi zangu kwenye Kampuni ya Global Publishers.”
“Oh! My God!” Morgan alipaza sauti na kuwafanya watu wote waliokuwa eneo hilo kuacha shughuli zao wakabaki kumshangaa. Erick naye akashindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kinatokea eneo hilo.
Kabla hajaendelea kusema chochote, Morgan akamwomba Erick wasogee pembeni ili waweze kuongea zaidi.
“Hakuna shida,” Erick aliongea akimfuata mwanaume huyo na wote wakaketi kwenye viti vilivyokuwa hapo na mazungumzo maalum yakaanza, Morgan akimweleza wazi kwamba alifurahi kukutana naye na kazi iliyokuwa imemleta nchini Tanzania ni kutaka amsaidie kwa kila kitu na kama angehitaji kiasi chochote cha fedha angekuwa tayari kumpatia lakini tu amsaidie.
Hakuficha kitu akaweka kila kitu wazi kwamba walikuja nchini hapo kutafuta ukweli wa mwanaume aliyeitwa Phillip na mkewe Genevieve na hawakuwa na msaada wowote.
“Niko tayari kukusaidia.”
“Kivipi?”
“Nitakusaidia ufanye kitu kinachoitwa Press Conference, utakutana na waandishi wa habari ambao nitaongea nao kuwaeleza shida yako halafu utatakiwa kufanya kikao cha pamoja kisha kupiga picha ili kuandika habari hizo kwenye magazeti yetu, watu wakisoma naamini utapata ufumbuzi wa tatizo lako.”
“Inaweza ikachukua muda gani kuanzia sasa?”
“Kazi hiyo nitaifanya leo na kesho nitakupa majibu,”
“Tutakutana wapi?”
“Nitakuja hapa hapa hotelini lakini ni vyema ukanipatia namba yako ya simu ili iwe rahisi kuwasiliana na wewe.”
“Ahsante rafiki, wewe kwangu ni kama malaika, chukua hii,” aliongea Morgan akichomoa kadi yake yenye namba za simu na kumkabidhi Erick ambaye aliipokea, wakaagana wakiahidiana kukutana tena kesho yake.
Baada tu ya Erick kuondoka eneo hilo, Morgan alipandisha lifti haraka kwenda chumbani kwa akina Marina kuwaeleza kila kitu. Mariya na Marina walifurahi sana kupewa habari hizo njema.
“Mungu yupo pamoja nasi, naona mwanzo umekuwa mzuri,” Mariya aliwaambia.
“Tena tutakapofanikisha jambo hili itabidi tukamtolee shukurani ya pekee,” Marina aliunga mkono.
Wakiwa pale hotelini, waliona saa zinachelewa ili kuifikia siku iliyofuata ambayo mwanasheria wao angekutana na Erick na kumpa utaratibu wa mkutano wao na waandishi wa habari ambao ungemaliza kazi iliyowaleta Tanzania.
Kama walivyokuwa wamepanga kesho ikawadia, Morgan akiwa tayari kumsubiri Erick afike ili waendelee na mazungumzo yao na kuona walikuwa wamefanikiwa kwa kiasi gani kuhusu shughuli iliyokuwa mbele yao.
Ilipotimu saa tatu kamili asuhubi, Erick aliwasilia hotelini hapo na mazungumzo yakafanyika na mwisho ukaonekana kuwa mzuri akimweleza wazi kwamba alishafanikiwa kukutana na baadhi ya waandishi na kuwaeleza habari hiyo na walipanga kukutana siku iliyofuata pale hotelini.
Morgan akashukuru na kupeana ahadi ya kukutana na Erick siku iliyofuata kisha wakaagana.
Muda huo huo alifanya utaratibu wa kupata kibali cha kufanya mkutano ndani ya hoteli hiyo, ambapo alipewa chumba kikubwa kilichotumika kwa shughuli hiyo.
***
Hali ya Phillip ilikuwa imebadilika kabisa utanashati wote aliokuwa nao kipindi akiwa na mke wake ukawa umepotea, mahudhurio ya kazi nayo yalionekana kusuasua kitendo kilichofanya mpaka mabosi wake waaanze kuingiwa na wasiwasi.
Nyumbani nako hali ilikuwa tofauti kwani muda mwingi aliutumia kulala na alipochoka alitoka bila kuaga na kuingia mtaani kunywa pombe ili kupoteza msongo wa mawazo.
Phillip akawa ni mtu wa kukitamani kifo kuliko kitu kingine, haikuishia hapo akaanza tabia ya kutoka nyumbani na kwenda makaburini na alipofika huko alitafuta kaburi la mkewe Lina na kulala juu yake.
Ni hali hiyo ndiyo iliyozidi kuichanganya zaidi familia yake nao pia wakaingiwa na wasiwasi na kuamini kwamba si muda mrefu Phillip angekuwa mwendawazimu, ndugu na jamaa wakakaa kikao kuangalia ni jinsi gani wanaweza kumsaidia na walipomuuliza, jibu lilikuwa moja tu.
“Nataka kufa, basi.”

MAISHA yalikuwa yamebadilika kabisa kwa Phillip ni kama vile dunia yake ilikuwa imegeuka na kuwa nje ndani, akapoteza kabisa mwelekeo wa maisha yake na kusahau kwamba alikuwa ana jukumu la kumlea mtoto mdogo Genevieve ambaye bado alihitaji ushauri wa wazazi wake japo tayari mmoja alishaaga dunia.
Ushauri na ushawishi mkubwa wa ndugu, jamaa na marafiki haukusaidia kitu na hata walipoamua kutumia ofisi yake kumshauri bado hakubadilika ndiyo kwanza alizidisha ulevi na kutembea barabarani kutwa nzima akiongea na kutukana watu bila sababu.

Phillip akawa ameharibikiwa kabisa, ofisi ikaamua kumwachisha kazi kwa nguvu lakini wakiahidi kumsaidia kama tu msaada wowote ungehitajika, nyumbani nako hali kwa mtoto ikawa mbaya hata shule akawa haendi tena kwa sababu hapakuwa na ada ili aweze kuendelea na masomo, hakika maisha yakawa magumu kupindukia.
Lakini bado watu mbalimbali waliomfahamu Phillip hawakumwacha peke yake waliendelea kumshauri na kumpa moyo kwamba maisha yaliendelea na kamwe yasingesimama. Phillip akapokea ushauri wao ambao uliingia sikio la kulia na kutokea sikio la kushoto kwani hakuweza kubadilika, zaidi sana vituko viliongezeka nao pia wakaanza kuchoka na kumwacha afanye alivyopenda.

***
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam chumba maalum kilikuwa kimeandaliwa tayari kwa mkutano mfupi ambao ungefanyika siku hiyo. Mariya na Merina ambao ndiyo waongeaji wakubwa, pembeni yao akiwepo mwanasheria aliyesimamia mambo yote zikiwemo mali za baba yao Victor Fedorov ambaye mpaka wakati huo hakufahamika kama alikuwa amekufa au la!
Waandishi walikuwa ni wengi mno mikononi mwao wakiwa na kalamu zao na kamera ili kuchukua habari ambayo ingepelekwa katika vyombo vyote vya habari yaani magazeti, redio na televisheni.

Mkutano ukawa umeanza, Mariya na Merina wakijitambulisha kwamba walikuwa akina nani na walitokea wapi na nini lilikuwa lengo lililowaleta nchini Tanzania, waliongea katika lugha ya Kirusi na Morgan akaitohoa katika lugha ya Kiingereza na baadaye Erick Evarist akatafsiri katika lugha ya Kiswahili.
Wakisisitiza kwamba walihitaji kufahamu mahali ambako Phillip na mkewe Genevieve wangepatikana na kwa gharama yoyote ile wangekuwa tayari kutimiza hilo lakini tu wapate ushirikiano.

Hivyo ndivyo mambo yalivyoendelea ndani ya hoteli hiyo kwenye chumba maalum, kwa muda wa saa nzima watoto hao waliendelea kuongea na waandishi wa habari wakiwaomba na kuwasihi kusaidia kuandika habari hizo ili hatimaye mtu anayetafutwa aweze kupatikana kwa urahisi.
“Wanamtafuta nani?”
“Wanasema wanatafuta familia ya Phillip na mkewe Genevieve.”
“Mh!”

“Kwa nini?”
“Hata sisi hatujui ila wanasema kwamba Genevieve ndiye mama yao mzazi.”
“Hawa watoto mbona siyo Watanzania?”
“Unalosema ni kweli lakini hatuwezi kujua, sisi tufanye tu kazi yetu,” yalikuwa ni maongezi kati ya waandishi wa habari waliokuwepo kwenye mkutano huo wakijiuliza maswali mengi juu ya mkutano huo na watu waliouitisha.

Baada ya habari kukamilika Mariya na Merina wakawashukuru waandishi huku wakiwashika mkono na kuwapatia bahasha ambayo ndani yake haikufahamika ilikuwa na nini na kuwatakia kila la kheri katika utendaji wa kazi zao na kuwaeleza wazi kwamba ili waweze kuwapata watu waliowahitaji, waliwategemea sana wao.
Waandishi nao wakashukuru wakiahidi kufanya kila kilichowezekana habari hiyo ichapishwe katika magazeti na ikiwezekana kutangazwa katika vyombo vyote vya habari zikiwemo redio na televisheni.

Baada ya waandishi kuondoka, wakarejea ndani ya vyumba vyao hamu yao kubwa ikabaki kusubiri nini magazeti yangeandika, ambapo macho na masikio yao yote yakaelekezwa huko.
“Nafikiria kila kitu kitakwenda sawa, tusubiri kesho tuone,” Morgan aliongea.
“Hata mimi nahisi hivyo ngoja tuone,” waliendelea kuongea wakijipa matumaini kwamba kila kitu kingekwenda sawa.
Saa zikazidi kusonga mbele hatimaye kiza kikaingia, hapo wakaamua kula chakula cha usiku na kuingia kwenye vitanda vyao wakiwa na hamu ya kujua kesho yake kitatokea nini.

***
Asubuhi ya siku iliyofuata Morgan alikuwa wa kwanza kutoka ndani ya chumba na bila kufanya kitu chochote akashuka kwa lifti mpaka mapokezi hapo akasabahi watu aliowakuta kisha kutoka nje ya hoteli kuelekea barabarani akitafuta mahali ambako angekutana na wauza magazeti na kununua ili kusoma kama habari yao ingekuwa imeandikwa siku hiyo.
Ni kweli kabisa alichokuwa amekifikiria kichwani mwake hakikuwa uongo, mtu wa kwanza tu aliyekutana naye akiwa na magazeti mkononi akamwita na kuchukua moja ya magazeti aliyokuwa nayo, macho yake yakakutana na picha ya Mariya na Merina mbele yao kukiwa na vipaza sauti vingi, hakuelewa lugha ya Kiswahili lakini aliweza kuisoma picha.

Akamwomba tena muuza magazeti ampatie magazeti mengine zaidi, nayo habari iliyosomeka ukurasa wa kwanza tu wa magazeti hayo ilikuwa ileile ya kwao, furaha ikamjaa moyoni mwake akajiona mshindi kati ya washindi na akalazimika kununua magazeti zaidi ya sita akalipa na kurejea ndani ya hoteli huku jasho likimtoka.
Haraka akapandisha lifti na moja kwa moja akauendea mlango ambao ndani yake walilala Mariya na Merina akagonga kwa nguvu na kusubiri mlango ufunguliwe na akiwa hapo akashuhudia Mariya akichungulia baada ya kufungua mlango.

“Magazeti haya hapa,” aliongea akinyoosha mkono kumpatia Mariya magazeti yote aliyokuwa nayo.
Kwa macho yake yote mawili akashuhudia kurasa za mbele za magazeti hayo zikiwa na picha yao kubwa akacheka na kutabasamu na bila kusema neno akarejea ndani ya chumba chao huku akimwita Merina.
“Merina! Merina, amka uone mwenyewe magazeti karibu yote yameandika habari yetu, kazi imekuwa rahisi sana kuliko tulivyotarajia…,” aliongea Mariya bila kuweka kituo.

Furaha ilikuwa imetawala ndani ya chumba wakiamini kwamba muda si mrefu kila kitu kingekwenda sawa kama walivyofikiria, kwa pamoja wakakumbatiana na kupigana mabusu lakini ghafla wakiwa katika furaha yao hiyo taswira ya baba yao Victor Fedorov mwanaume aliyewapenda kupindukia ikawajia, ni kweli walikuwa na furaha ya kuufahamu ukweli mwingine uliokuwa umejificha lakini pia Fedorov alikuwa ndiye mzazi wao halisi pamoja na mambo yote mabaya aliyoyatenda bado walimpenda.
“Sijui atakuwa wapi? Amepatwa na kitu gani? Inauma sana,” aliongea Merina huku akilia.

***
Asubuhi ya siku iliyofuata baada tu ya Merina na Mariya kufanya mkutano jana yake na waandishi wa habari, Phillip alikuwa katika mitaa ya Posta akikatisha huku na kule bila kuelewa anakwenda wapi.
Ghafla mbele yake akaiona meza ya magazeti na kuamua kutupa macho juu yake ili angalau asome kilichokuwa kimeandikwa siku hiyo, akasogea karibu kabisa na muuza magazeti kisha kumsabahi.
“Habari za leo?”
“Nzuri tu kaka karibu.”

“Ahsante, naweza kupitishapitisha macho kidogo?”
“Bila shaka lakini usiguse kama hutalinunua.”
Akaitika kwa ishara ya kutingisha kichwa kisha akasogea karibu na meza hiyo na kutupa macho juu ya magazeti, ni habari ya kwanza tu katika gazeti la Uwazi ikamshtua.
“Mh!”

“Mbona umeguna kaka?”
“Hii habari, inanihusu mimi kabisa na hao ni watoto wangu lakini walikufa.”
“Wewe mzee chizi nini utakuwa hamnazo watoto wako? Wewe? Hebu ondoka hapa haraka kabla sijakuitia mgambo wa jiji.”
“Dorice na Dorica,” alitamka kwa sauti ya juu.
Nimekuambia ondoka haraka,” aliongea muuza magazeti huyo akimvuta Phillip kumwondoa eneo hilo.

“Usinifanyie hivyo ndugu yangu nakuambia ukweli tafadhali nipe gazeti nione vizuri.”
“Wazee wengine bwana sijui wachawi au wanatumwa kuwangia biashara za watu! Asubuhi hii, kama unataka gazeti si ununue lakini siyo ujipendekeze kwa watoto wa watu.”
“Usinivu…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake tayari akashuhudia vibao mfululizo vikipita mashavuni mwake.

je nini kiliendelea
 
SEHEMU YA 50


ILIPOISHIA


“Usinifanyie hivyo ndugu yangu nakuambia ukweli tafadhali nipe gazeti nione vizuri.”
“Wazee wengine bwana sijui wachawi au wanatumwa kuwangia biashara za watu! Asubuhi hii, kama unataka gazeti si ununue lakini siyo ujipendekeze kwa watoto wa watu.”
“Usinivu…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake tayari akashuhudia vibao mfululizo vikipita mashavuni mwake

SASA ENDELEA

VIBAO mfululizo vilikuwa vimetua kwenye mashavu ya Phillip na kumpeleka chini akajikuta ameketi kitako bila kutarajia huku akilia na kujaribu kumweleza kijana yule ukweli kwamba habari iliyoandikwa ilimhusu yeye na watoto wake ambao hakika kwa wakati huo walikuwa ni marehemu.
Ni kilio cha Phillip ndicho kilichokusanya watu eneo la tukio, wengi wakijaribu kudadisi ni kitu gani kilikuwa kimetokea asubuhi hiyo. Kijana wa magazeti akaanza kusimulia tukio zima, muda wote huo Phillip akiendelea kulia.

Bahati nzuri asubuhi hiyo watu wengi walikuwa wakielekea makazini kwao, ni mfanyakazi mmoja aliyefanya kazi na Phillip alipita eneo hilo naye akitaka kuangalia nini lilikuwa tatizo. Akiwa hapo akatupa macho yake katikati ya umati wa watu akamwona mwanaume akiwa chini tena akilia.
“Mh!” akaguna akisogea karibu ili kuhakikisha kitu alichokiona.
“Phillip!” alitamka kwa sauti ya juu na kufanya watu wote kumwangalia yeye.

“Namjua huyu ni shemeji yangu pia ni mfanyakazi mwenzangu, jamani amefanya nini tena? Halafu ana tatizo la akili kidogo toka amefiwa na mkewe amekuwa hivyo, hebu njoo,” msichana huyo aliongea.
“Blandina sitaondoka hapa mpaka nipate gazeti.”
“Gazeti?”
“Ndiyo.”

“Lina nini?”
“Nimesoma kwa macho yangu habari kwamba Dorice na Dorica wako hapa Tanzania tena wananitafuta mimi na mama yao.”
“Phillip!”
“Hutaamini lakini huo ndiyo ukweli, wewe nunua usome kisha utanipatia na mimi.”

Msichana huyo bila ubishi akafungua mkoba wake na kutoa noti ya shilingi mia tano kisha kununua gazeti la Nipashe haraka akatupa macho yake ukurasa wa mbele, yeye pia akashuhudia picha kubwa iliyoonyesha wasichana wawili na chini yake kulionekana habari iliyowahusu lakini pia ikimtaja Phillip kwa majina yote matatu na Genevieve ambaye kwa historia aliyokuwa ameipata alikuwa ni mke wa Phillip aliyefariki dunia miaka kadhaa iliyopita.
“Naota au?”

“Huoti unachokiona hapo ni kweli tupu, tafadhali nisaidie nahitaji kujua wako wapi niwafuate nikaongee nao niujue ukweli,” aliongea Phillip akinyanyuka kutoka chini.
Watu wote waliokuwa eneo la tukio pamoja na kijana aliyekuwa akiuza magazeti wakaonekana kupigwa na butwaa kwani kwa wengi Phillip alionekana kichaa.
“Twende,” aliongea msichana huyo akimshika Phillip mkono, wakatembea mpaka kwenye mgahawa mmoja hapo wakaketi na kwa umakini wa hali ya juu wakaanza kusoma habari hiyo mwanzo mpaka mwisho na kuelewa sehemu ambayo watoto hao walikuwa wamefikia.

“Nisaidie ndugu yangu nahitaji kuonana nao leo hii.”
“Hakuna shida ila watakubali? Unayo kumbukumbu gani itakayokufanya wakuamini kwamba wewe ni baba yao?”
“Ninazo nyingi tu mojawapo ni picha zao za utotoni ziko nyumbani naweza kwenda kuzichukua.”
“Basi twende tukajaribu,” msichana huyo akaamua kushirikiana na Phillip ili kumsaidia.

Wakatembea mpaka kando kidogo na hapo akaita teksi ambayo iliwapeleka moja kwa moja nyumbani kwa Phillip ambako aliingia ndani na bila kusema kitu chochote akaingia chumbani kwake na kutoka na bahasha mkononi huku akikimbia akitoka tena nje na kuielekea teksi iliyokuwa ikimsubiri, akaingia ndani na dereva akaondoka kwa kasi ya ajabu moja kwa moja kuelekea katika hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam ambako wangejitambulisha na kuomba kuonana na Mariya na Merina.
Njia nzima Phillip alikuwa akilia, hakuamini mambo yaliyokuwa yanamtokea maishani mwake na mara kadhaa akamwomba msichana aliyekuwa naye ajaribu kumfinya pengine angeamka kutoka usingizini.

“Phillip shemeji yangu huoti hata kidogo yote yanayotokea ni kweli tupu, tatizo ni moja tu iweje watoto waliokuwa wamekufa na kuzikwa wawe hai? Hapo mimi nashindwa kabisa kuelewa na je, watakubali na kuamini kwamba wewe ndiye baba yao?”
Swali hilo lilipenya moja kwa moja masikioni mwa Phillip na kwenda ndani kabisa ya kichwa chake, akaiona picha yote jinsi walivyohangaika mpaka kufikia kununua mbegu za mwanaume mwingine ambaye aliitwa Victor Fedorov, alipofika hapo machozi yakambubujika.

Gari likaendeshwa na hatimaye nusu saa tu baadaye lilishawasili nje ya hoteli hiyo maarufu na wakalipa kisha kushuka kutembea kuelekea mapokezi ambako wangejitambulisha na kuomba kusaidiwa shida yao.
Kwao zoezi halikuwa gumu walifanya kama walivyopanga na kufanikiwa kuonana na watoto hao wawili. Mapokezi simu ikapigwa moja kwa moja kwenye chumba alicholala Morgan na simu hiyo ikapokelewa.

“Naongea kutoka mapokezi hapa kuna wageni wenu wawili.”
“Wawili? Wa jinsia gani?”
“Mwanamke na mwanaume.”
“Mh! Sawa waeleze tutakuwa hapo baada ya dakika tano kuanzia sasa hivi.” Morgan alijibu na kukata simu na bila kuchelewa akatoka chumbani kwake kwenda kwa akina Marina hapo akawapa taarifa na kuwataka wajiandae kukutana na wageni waliokuwa wamefika pale kuwatafuta.

“Pengine ndiyo hao tunaowatafuta.”
“Umejuaje hebu tukawaone kwanza.”
Haraka wakajiandaa na walipokuwa tayari wakatembea kuelekea sehemu kulikokuwa na mlango wenye lifti wote watatu wakashuka kuelekea chini wakitamani kuonana na watu hao.
“Je, tutawaamini vipi kama kweli ndiyo wenyewe?” Morgan aliuliza.

“Kabla ya yote tutahitaji kuwasikiliza kwanza wao na kama kuna kitu chochote kinachoonyesha kwamba wao ndiyo haswa walengwa wa safari yetu.”
“Hilo nakubaliana na wewe,”Merina alidakia na tayari walishafika chini mlango wa lifti ukaonekana kufunguka na kutoka nje.

Huku vichwani mwao wakijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu wakatokeza mapokezi na macho yao kukutana na watu wawili, mwanamke na mwanaume, ambao hawakuwafahamu kabisa lakini ghafla kabla hawajapiga hatua nyingine kwenda mbele zaidi wakashtushwa na sauti kubwa ndani ya chumba.
“Dorice! Dorica! Si mliku…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake akaanguka chini kama mzigo.

ULIKUWA ni mshtuko mkubwa Phillip alipoanguka chini watu wote ndani ya chumba walianza kukimbizana huku na kule kutafuta msaada, Blandina aliyekuwa ameongozana na Phillip yeye pia alikuwa akilia huku akimwita Phillip.
“Tafadhali usife, huu ndiyo wakati wa kuufahamu ukweli, amka nakuomba.”
Lakini bado Phillip aliendelea kulala chini akiwa hajitambui.

Haraka daktari aliyefanya kazi ndani ya hoteli kwa dharura akaitwa na mara moja akaanza kumpatia Phillip huduma ya kwanza ili kumnusuru na umauti ambao ulikuwa unamnyemelea.
Kwa takribani nusu saa nzima daktari aliendelea kumpatia huduma ya kwanza Phillip mwisho naye akaanza kukata tamaa akieleza wazi kwamba ni vyema mtu huyo akapelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi.

“Hospitali?”
”Ndiyo kwa jinsi hali ninavyoiona ni bora iwe hivyo.”
“Mh!” Blandina akaguna lakini ghafla wakiwa katika kujadili wakashuhudia Phillip akifungua macho yake na kuangaza huku na kule ndani ya hoteli.
Haraka kama vile alikuwa akiota akakurupuka kutoka chini na kusimama akionekana kutafuta kitu ambacho hakikuonekana kwa wengi.
“Bahasha yangu! Nataka bahasha yangu nilikuwa nayo muda si mrefu.”

“Hii hapa,” Blandina aliongea akinyoosha mkono kukabidhi bahasha kwa Phillip.
“Nasema ukweli watoto hao hapo ni wa kwangu lakini sikuwahi kuwapa majina hayo ya Mariya na Merina waliitwa Dorica na Dorice!”
“Lakini hawa ni Mariya na Merina si majina hayo unayosema wewe!”
“Hakika ninawaeleza ni watoto wangu ushahidi wangu upo, ni picha nakumbuka vizuri sura zao na mama yao pia,” Phillip aliongea mfululizo.
Morgan ambaye ndiye alikuwa mwanasheria aliyeongozana na akina Merina na Mariya akasogea karibu na Phillip ili kupata ushahidi wa picha kama Phillip mwenyewe alivyosema.

“Naweza kuona picha hizo?” aliuliza.
“Hizi hapa,” Phillip aliongea akifungua mfuko wa khaki na kuchomoa picha zilizokuwa ndani yake akazikabidhi kwa Morgan ambaye alianza kupitisha macho juu yake.
“Mh!” akaguna, picha zilizokuwa mikononi mwake zilikuwa za watoto wawili waliokuwa wamesimama mbele yake yaani Merina na Mariya akashuhudia picha nyingine za watoto hao wakiwa na mama yao mzazi ambaye ndiye aliitwa Genevieve, yeye pia akapigwa na butwaa.

Mariya na Merina nao pia wakasogea karibu na Morgan ili kushuhudia kilichokuwa kikiendelea, macho yao yakatua moja kwa moja katika picha zao na mwanamke mmoja akiwa pembeni yao, huyo ndiye alikuwa mama yao.
“Anafanana na sisi kabisa kwa kila kitu,” waliongea kwa sauti.
“Ni kweli yawezekana huyo ndiye tunayemtafuta.”
“Je, yuko wapi mwanamke huyu?”

“Genevieve alikufa!”
“Unasema?”
“Amini ninachowaambia, huo ndiyo ukweli wangu kama mnaweza kusadiki maneno yangu basi sadikini,” Phillip aliongea huku kwikwi ya kulia ikimkaba.
Maswali yakawa mengi bila majibu, ni kweli walimtafuta mwanaume aliyeitwa Phillip na mkewe Genevieve lakini kilichozidi kuwashangaza zaidi ni kwamba iweje mwanaume huyo aseme kwamba walikufa na kuzikwa miaka mingi iliyopita ili hali wao walikuwa hai?

Baada ya mvutano mrefu wakaomba chumba maalum ili waweze kuongea vizuri kuupata ukweli waliokuwa wakiutafuta Morgan akiwa ndiye kiongozi wa kikao, huko waliongea mengi Phillip akijaribu kueleza ukweli na ni kwa nini aliamini watoto hao walikufa. Akasimulia ajali ya gari kulipuliwa kwa bomu na watoto wote kufahamika walikufa.
Ilikuwa ni historia chungu lakini ilibidi Merina na Mariya waikubali, wakataka kuonyeshwa makaburi ili wakashuhudie kwa macho yao, jambo ambalo halikuwa na tatizo. Historia nyingine iliyokuwa imewaumiza watoto hao ni taarifa kwamba mama yao alikufa muda mrefu lakini pia alizikwa pembeni mwa makaburi yao.

“Hatuna muda wa kupoteza tunachohitaji sisi ni kuona hayo makaburi tena kama inawezekana sasa hivi,” Morgan aliongea.
“Hakuna shida tunaweza kwenda,” Phillip aliongea kwa majonzi.
Safari kuelekea makaburini ikaanza na kwa sababu walitumia usafiri wa kukodi haikuchukua muda wakawasili katika makaburi ambako walisemekana kuzikwa, wakashuka wakiwa na hamu ya kufahamu historia ya kifo. Kwa sababu makaburi yao hayakuwa mbali sana haikuchukua muda kuyafikia ambapo wakashuhudia picha zikiwa katika fremu kwa pamoja wakaangua kilio.

“Ni kwa nini haya yote? Mbona sisi tuko hai? Kuna nini kilitokea? Lazima ipo siri ambayo hatuwezi kuifahamu, na huyu ndiye mama yetu?” wakauliza.
“Mnachokiona wanangu ndicho kilichotokea, sikuwahi kufahamu kwamba hamkufa, mimi pia nahisi ni mchezo ulichezwa naomba mnisamehe.”
“Ukweli ni historia inayosikitisha sana lakini hatuna budi kuikubali pamoja na kuugundua ukweli huu wewe utabaki kuwa ba..ba..ye…tu!” waliongea watoto hao huku wakilia.

Mioyo yao ilikuwa imeumia kupita kiasi kwa historia waliyokuwa wameipata lakini upande mwingine walionekana kufurahia kujua ukweli kwani walioufahamu kama ndiyo ukweli haukuwa sawa, Federov alikuwa ndiye baba yao halisi na mama yao alikuwa Genevieve lakini Phillip alihusishwa zaidi kwani ndiye aliyewalea wakiwa watoto wadogo baada ya kununua mbegu za kiume kutoka kwa Fedorov.
“Tunakupenda sana,” waliongea wakitembea kuondoka eneo la makaburini kurejea hotelini ndani ya vichwa vyao wakiwaza na kuwazua mambo mengi bila kupata majibu, walihitaji kupata historia zaidi ili waamini kwa asilimia zote.

“Lakini tunahitaji kupata historia ya ndani zaidi ili kukufahamu vizuri.”
“Hakuna shida niko tayari kueleza kila kitu ambacho mtahitaji.”
Wakati wakiongea hayo walishafika eneo la maegesho la hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam, wakashuka na kuingia ndani ili kuendelea na maongezi zaidi wakiwa tayari kumsikiliza Phillip.

Walitaka kusikia kama Phillip angekuwa tayari kusema ukweli wake wote alioufahamu ili nao waoanishe na maelezo ambayo waliyasoma kutoka kwenye nyaraka za baba yao.
“Historia nitakayosema inaumiza kupita maelezo lakini naomba muipokee kwa mikono miwili na kuichunguza hapo ndipo mtaugundua ukweli wote.”
“Mh! Tuko tayari kukusikiliza.”

“Mimi na mama yenu ambaye ni marehemu yaani Genevieve tulifunga ndoa miaka mingi iliyopita na maisha yetu yalikuwa ya raha mustarehe, jambo moja tu lilikosekana kwa bahati mbaya mimi sikuwa na mbegu za uzazi za kuweza kuzalisha mwanamke hivyo tukatafuta daktari ambaye tulimpata kama sikosei aliitwa Dk. Koher huyu alitusaidia sana na tukafanikiwa kupata mbegu za kununua kwa mwanaume mmoja aliyekuwa maskini akiishi mtaani, huyo aliitwa Victor Fedorov.

Ukafanyika utaalam wa kitabibu na ninyi mkazaliwa, furaha ndani ya nyumba ikaongezeka huku tukiwalea vyema na kuwatunza mpaka mlipofikisha umri wa miaka mitano ndipo tukaamua kuwapeleka shule lakini siku moja asubuhi nikapata ujumbe kwamba gari iliyokuwa imewabeba ilitegeshwa bomu hivyo lingelipuka na watoto wote kufa.

Nilijitahidi sana kunusuru maisha yenu lakini nilishachelewa, gari likalipuka na watoto wote ndani ya basi kuaminika kufa, tulilia na kuomboleza baadaye tukafanya mazishi ndiyo yale makaburi niliyowapeleka yakiwa na picha zenu juu. Akili yangu inavurugika zaidi iweje leo muwe hai tena katika nchi nyingine kabisa…,” aliongea Phillip muda wote huo akibubujikwa na machozi.
“Usilie tafadhali nyamaza.”
“Inanichanganya akili iweje muwe hai wakati mlishakufa tukawazika? Hapana hii ni ndoto pengine nitaamka na kukuta kila kitu kiko sawa, hebu nifinye.”

Je, nini kitaendelea? Historia aliyoitoa Phillip mbele ya watoto wake baada ya kutoka makaburini wataiamini?
 
SEHEMU YA 51


ILIPOISHIA

Ukafanyika utaalam wa kitabibu na ninyi mkazaliwa, furaha ndani ya nyumba ikaongezeka huku tukiwalea vyema na kuwatunza mpaka mlipofikisha umri wa miaka mitano ndipo tukaamua kuwapeleka shule lakini siku moja asubuhi nikapata ujumbe kwamba gari iliyokuwa imewabeba ilitegeshwa bomu hivyo lingelipuka na watoto wote kufa.

Nilijitahidi sana kunusuru maisha yenu lakini nilishachelewa, gari likalipuka na watoto wote ndani ya basi kuaminika kufa, tulilia na kuomboleza baadaye tukafanya mazishi ndiyo yale makaburi niliyowapeleka yakiwa na picha zenu juu. Akili yangu inavurugika zaidi iweje leo muwe hai tena katika nchi nyingine kabisa…,” aliongea Phillip muda wote huo akibubujikwa na machozi.
“Usilie tafadhali nyamaza.”
“Inanichanganya akili iweje muwe hai wakati mlishakufa tukawazika? Hapana hii ni ndoto pengine nitaamka na kukuta kila kitu kiko sawa, hebu nifinye.”

Je, nini kitaendelea? Historia aliyoitoa Phillip mbele ya watoto wake baada ya kutoka makaburini wataiamini?
SONGA NAYO

Ukafanyika utaalam wa kitabibu na ninyi mkazaliwa, furaha ndani ya nyumba ikaongezeka huku tukiwalea vyema na kuwatunza mpaka mlipofikisha umri wa miaka mitano ndipo tukaamua kuwapeleka shule lakini siku moja asubuhi nikapata ujumbe kwamba gari iliyokuwa imewabeba ilitegeshwa bomu hivyo lingelipuka na watoto wote kufa.

Nilijitahidi sana kunusuru maisha yenu lakini nilishachelewa, gari likalipuka na watoto wote ndani ya basi kuaminika kufa, tulilia na kuomboleza baadaye tukafanya mazishi ndiyo yale makaburi niliyowapeleka yakiwa na picha zenu juu. Akili yangu inavurugika zaidi iweje leo muwe hai tena katika nchi nyingine kabisa…,” aliongea Phillip muda wote huo akibubujikwa na machozi.
“Usilie tafadhali nyamaza.”
“Inanichanganya akili iweje muwe hai wakati mlishakufa tukawazika? Hapana hii ni ndoto pengine nitaamka na kukuta kila kitu kiko sawa, hebu nifinye.”

Je, nini kitaendelea? Historia aliyoitoa Phillip mbele ya watoto wake baada ya kutoka makaburini wataiamini?
PHILLIP hakuwa katika ndoto kama alivyokuwa akifikiria kwani mambo yote yaliyokuwa yakimtokea yalikuwa ya kweli japo historia iliumiza mioyo ya wengi.
Vilio na machozi kwa Merina na Mariya havikukauka, walilia na kuomboleza kwa mambo mengi lakini kubwa zaidi ni lile la kuelezwa kwamba walikufa miaka mingi iliyopita kwa ajali ya bomu ambalo lilitegwa kwenye gari lao la shule na kuzikwa sehemu ambayo waliishuhudia kwa macho yao.

“Ni nini kilitokea? Kuna nini baba alifanya? Huu lazima utakuwa ni mchezo,” Merina na Mariya walisema kwa lugha ya Kirusi.”
Muafaka ukawa umefikiwa kwamba Phillip apewe muda wa kutafuta nyaraka zote muhimu za kumtambulisha kwamba yeye ndiye haswa alikuwa baba aliyewalea watoto hao. Akapata cheti cha ndoa na nyaraka nyingine kadhaa, pia baadhi ya ndugu nao wakasimama kusema ukweli mbele ya mwanasheria Morgan aliyepewa jukumu la kuongoza mambo yote yaliyotakiwa.

Siku ya kwanza ikapita, ikaja siku ya pili na hatimaye wiki ikakatika wakiwa bado katika uchunguzi mzito. Vielelezo vingi vilipatikana na baadhi ya watu wakatoa ushahidi wao kuhusu Phillip.
Jinsi watu wengi walivyotegemea ndivyo ilivyokuwa kwani baada ya uchunguzi wa kina, ukweli ulibainika. Phillip akaonekana kuwa mwenye haki pamoja na kwamba hakuwa baba wa kuwazaa watoto Mariya na Merina.
“Nini kinaendelea kwa sasa?” Morgan aliuliza siku moja.

“Nadhani mtu pekee wa kumtafuta kwa sasa ni Eric Evarist ili atusaidie tena tupate nafasi ya kuzungumza na waandishi wa habari.
Jambo hilo likafanyika mara moja, mwandishi huyo akatafutwa na kupewa taarifa kamili. Siku mbili baadaye, kilifanyika kikao kingine ndani ya hoteli ileile waliyofikia.
Waandishi wa habari wakafurika ndani ya chumba maalum tayari kwa kuchukua taarifa muhimu, macho na masikio vikawa makini kabisa kuhakikisha hawakosei kitu chochote.

Hata waandishi wenyewe baada ya kusikia historia iliyokuwa imetolewa na mashahidi wa pande zote mbili, walishtushwa sana. Kilichowatatiza ni kwamba, iweje watu waliozikwa siku nyingi wawe hai tena?
“Ndugu zangu ninayo mambo matatu tu muhimu ya kuongea nanyi asubuhi ya leo lakini nianze kwa kuwaomba radhi kuchukua muda wenu mwingi kuja hapa kwetu,” aliongea Morgan na alipomaliza akapokelewa kwa shangwe, nderemo na makofi mengi ndani ya chumba.

Mariya na Merina ndiyo walioanza kufungua mkutano huo, wakati wakiongea, Morgan ambaye ndiye alikuwa mwanasheria wao, alikuwa akitafsiri kwa lugha ya Kiingereza ambayo waliamini kabisa itaeleweka kwa watu wote. Walipomaliza, Phillip naye alikaribishwa kuongea na waandishi, akaeleza kila kitu bila kificho. Machoni mwa watu alionekana kama mwongo aliyetaka kujipatia fedha kutoka kwa watoto hao matajiri lakini Morgan alikanusha vikali uvumi huo, akasimama kumtetea Phillip kwa kipindi chote.
“Hadanganyi, ni kweli ndiye baba halisi wa watoto hawa.”

“Mh!”
“Huo ndiyo ukweli?”
“Lakini anasema wake walishakufa miaka mingi iliyopita kwa ajali, pengine wanafanana tu.”
“Uchunguzi wa kina umefanyika na tumegundua kila kitu, kwa hilo naomba tukubaliane na tuungane na huyu ndugu yetu hapa,” Morgan alisema kwa kujiamini.

Wakiwa hapo, waliongea mambo yote lakini jambo moja likabaki kuwa siri ya familia kwamba watoto hao walikuwa si mali ya Phillip kwani hakuwa na uwezo wa kumpa ujauzito mwanamke. Jambo hilo liliendelea kubaki siri ya familia ili kulinda heshima yake.
Kwa muda wote huo, Phillip aliendelea kumwagika machoz. Si kwamba alikuwa akiliakwa majonzi bali furaha ya kukubaliwa na watoto wake wawili ambao kwa wakati huo walishabadili majina na kuitwa Merina na Mariya (Dorice na Dorica) ndiyo kitu kilichomliza.
Wote kwa pamoja wakasimama na kukumbatiana, watoto pia walikuwa wakilia kwa furaha kwani walimpata mtu waliyekuwa wakimtafuta pamoja na kwamba Genevieve ambaye ndiye mama yao alishakufa.

Kazi yote ikawa imeachwa mikononi mwa vyombo vya habari kutangaza ukweli kwa Watanzania kwamba mwanaume ambaye ndiye hasa alikuwa akitafutwa, alikuwa amepatikana na Mariya na Merina wakishirikiana na mwanasheria wao walikuwa wakiwashukuru watu wote waliofanikisha kupatikana kwa Phillip. Mariya na Merina walikuwa na hamu kubwa ya kuwafahamu ndugu wengine wa Phillip, ikabidi wasubiri vyombo vya habari vifanye kazi yao.

Baada ya waandishi kuondoka, Phillip aliwaongoza Mariya, Merina na Morgan kuelekea nyumbani kwake ambako angekutana na familia yake, yaani mtoto wake Genevieve na bibi Magdalena ili kufahamiana zaidi, jambo ambalo lilichukua muda wa nusu saa hivi. Baada ya kufika nyumbani kwa Phillip, mapokezi yakafanyika kisha wakaungana na familia kufahamiana zaidi.
Waliongea mengi huku furaha ikitawala, mara kadhaa Phillip alionesha mapenzi ya dhati kwa watoto wake kwa kuwapiga mabusu mfululizo kama ishara ya mapenzi ya dhati kwao. Baada ya kumaliza utambulisho huo, waliaga na kuondoka wakimtaka Phillip kufika hotelini asubuhi ya siku iliyofuata ili wazungumze zaidi.
***
Magazeti yote ya siku iliyofuatia yaliandika habari ya kupatikana kwa Phillip, mwanaume aliyekuwa akisakwa kwa udi na uvumba ambaye haswa ndiye alikuwa baba wa Merina na Mariya watoto wa Kirusi waliokuja nchini kuufahamu ukweli wa maisha yao.
Vichwa vingi vya habari vilisomeka tofauti, wapo walioandika: “Baba wa watoto ajitokeza.” Mengine yakataka vipimo vya vinasaba (DNA) vifanyike ili kujua ukweli wa historia. “Watoto walioaminika kufa miaka mingi iliyopita wafufuka,” liliandika gazeti lingine. Kila gazeti liliandika lilivyotaka ilimradi kufanya biashara. Lakini wote hao hawakuufahamu upande wa pili wa shilingi kwamba nyuma yake kulikuwa na historia nyingine, tena ya kusikitisha ambayo ilikuwa ndani ya mioyo ya watoto wenyewe na Phillip.

WATANZANIA wengi wakabaki midomo wazi baada ya kusoma habari hizo kwenye vyombo vya habari mbalimbali. Wengi wakijiuliza kuna kitu gani kilitokea mpaka dunia ikaamini kwamba watoto hao waliokuwa wakiuza magazeti kwa wakati huo walikuwa wamekufa kumbe walikuwa hai. Maswali hayo yote hayakuwa na majibu na yakaendelea kuwa kitendawili kwa wengi.
Wakati dunia ikishangaa kwa upande wa Mariya, Merina na Phillip, kwao ilikuwa furaha kubwa, wakifurahia kuonana wakiwa hai, masikitiko makubwa yalitokea tu pale walipomkumbuka mama yao yaani Genevieve lakini wakajipa moyo na kuamini kwamba hiyo ndiyo dunia waliyoishi ndani yake, furaha kidogo na uchungu mwingi.

Si watoto tu waliowaza siku iliyofuata hata Phillip naye hakupata hata lepe la usingizi, akifikiria kesho yake ingekuwaje, lakini alikabidhi kila kitu mikononi mwa Mungu ili yeye ndiye awe jaji wa kila jambo ambalo lingekwenda kutokea, lakini zaidi alitaka watoto hao wafahamu kwamba pamoja na kuwa hakuwa baba yao wa kuwazaa lakini aliwapenda kwa dhati kupita maelezo na shahidi pekee alikuwa ni Mungu na mama yao Genevieve ambaye kwa wakati huo alikuwa ni marehemu.

Akaamka na kujiandaa na baada ya maandalizi hayo akatoka sebuleni na kuisabahi familia yake, hapo akaaga na kuondoka kuelekea hotelini akiahidi kurejea muda mfupi baadaye na kuwapa taarifa ni kitu gani kilizungumzwa. Njia nzima aliwaza na kuwazua bila kupata majibu, hatimaye nusu saa tu baadaye akawasili kwenye hoteli waliyokuwa wamefikia watoto wake, hapo akaingia moja kwa moja mapokezi na kuomba mawasiliano nao.

“Niko hapa kuonana na watu watatu, Mariya, Merina na Morgan,” aliongea.
“Sawa, karibu sana kaka taarifa zako ninazo kitambo sana.”
“Ahsante,” alijibu Phillip akijivuta kuelekea kwenye kiti kilichokuwa maeneo hayo na kuketi kusubiri na haikuchukua muda akawaona watoto hao wakitokeza na kutembea kumwelekea huku wakionyesha uso wa tabasamu wakamsabahi na kumkaribisha kwenye chumba maalum ambacho kiliandaliwa.

Wakaingia ndani na kuanza mazungumzo ambayo hakika Phillip mwenyewe hakuwa tayari kuyaamini mara zote alibubujikwa na machozi mfululizo. Morgan aliyekuwa pembeni akiwa ndiye mkalimani akitafsiri jambo moja baada ya jingine na mwisho muafaka ukawa umefikiwa.
“Kwa muda wa wiki nzima tumesubiri kuona kama kungejitokeza mtu mwingine na kudai kwamba sisi ni watoto wake lakini historia yako uliyotueleza inaendana kabisa na vielelezo vyetu.

“Awali tulikuwa navyo hivyo tumelazimika kukuamini kwa asilimia zote ingawa ukweli wote uko wazi, hakika pamoja na mambo yote yaliyotokea maishani mwetu, wewe bado utabaki kuwa baba yetu.” “Tutakupenda mpaka mwisho na hivi tunavyoongea na wewe tayari tumeishaanza kufanya utaratibu maalum wa kuondoka na wewe, si wewe tu bali pia familia yako yote ili tukaishi wote kama ndugu.”
“Ahsante, ahsanteni kwa kunijali wanangu hakika mnanipenda lakini kuna jambo moja linalosumbua ubongo wangu…,” aliongea Phillip lakini hakuweza kumalizia sentensi yake kwikwi ya kulia ikamkaba.

“Ni kwa nini unalia?”
“Mh! Unajua…”
“Hebu nyamaza ueleze linalokusibu.”
“Nalia furaha lakini pia swali moja linazunguka kichwani mwangu ni kwamba itakuwaje tukifika huko wakati ukweli wote mmeufahamu kwamba mimi si baba yenu?”
“Wewe ndiye baba yetu hakika tunayo kila sababu ya kusimamia hilo hata ikiwezekana kwa mtutu wa bunduki.”
“Mnasema kweli?”

“Kweli kabisa!”
“Na je vipi kuhusu Victor Fedorov ambaye ndiye mhusika wa kila kitu?””Tutakwenda kujua hukohuko kwani yapata kipindi kirefu sasa tangu ametoweka katika mazingira ya kutatanisha na hivi tunavyoongea nawe tumeliachia kazi jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kujua ni wapi alipo na kama yuko hai au la!” Mariya aliongea akimpigapiga Phillip mgongoni.

Hatimaye muafaka ukafikiwa kwamba kwa kuwa Mariya , Merina na Morgan walikuwa wametoa muda wa wiki nzima kusubiri kuona kama kungetokea jambo lolote lakini halikuwepo, uamuzi pekee walioufikia ni kuondoka na Phillip na familia yake yote. Hivyo utaratibu ukaanza mara moja wakitakiwa kuwakilisha vielelezo vyao vyote muhimu ili kupata vibali vya kuondoka nchini.
Hilo ndilo likawa jambo kubwa mbele yao, kwa Phillip yote hayo yakionekana kuwa ndoto akiamini kwamba ipo siku angeamka kutoka katika usingizi mzito aliokuwa amelala na kuona kila kitu kikiwa tofauti. Siku zikazidi kusonga mbele Morgan akishughulikia vibali vyote muhimu, hatimaye baada ya muda mrefu akafanikiwa kuvipata na furaha ikaendelea kutawala kati yao.

“Nashukuru Mungu kila kitu kimekwenda sawa, kilichobaki mbele yetu ni safari tu nadhani ni bora tukafanya maandalizi haya haraka ili turejee nyumbani kuendelea na shughuli nyingine kubwa, zaidi ni ile tuliyoiacha ikiendelea kuhusu Victor Fedorov, ni lazima tufahamu nini kiliendelea baada ya sisi kuondoka, alipatikana akiwa hai au alifikwa na umauti?” aliongea Morgan akionyesha msisitizo na kuwafanya watu wote waliokuwepo hapo wakimsikiliza kumwaga machozi, kwani bado watoto Mariya na Merina walimhitaji baba yao kupita maelezo ili naye ashuhudie kilichokuwa kimetokea na kumkubali Phillip na familia yake yote kama mmoja wa familia yao.

Kila kitu kikaenda kama walivyotarajia, Phillip akapewa nafsi ya kuaga ndugu, jamaa na rafiki zake akitakiwa kuwataarifu juu ya safari ambayo ilikuwa mbele yake naye akafanya hivyo bila kusita huku furaha ikiendelea kutawala katika moyo wake, kwa walio wengi walionekana kumpongeza na kufurahia tukio hilo lakini baadhi pia wakionekana kuumizwa kwa kumkosa kwani pamoja na matatizo yote aliyokuwa nayo alikuwa ni mtu wa watu.

Siku mbili baadaye safari ilishawadia wote kwa pamoja wakiwa ndani ya gari la kukodi liliwachukua na moja kwa moja kuwapeleka uwanja wa ndege ambako wangefanya utaratibu na kuondoka kuelekea nchini Urusi kwenda kufaidi maisha.

KWA Phillip, Genevieve na bibi Magdalena jambo lililokuwa likitokea mbele yao lilionekana kama ndoto na muda si mrefu wangezinduka kutoka katika uzingizi mzito. Lakini ukweli ulikuwa umebaki pale pale kwamba walikuwa safarini kuelekea nchini Urusi wakiambatana na wenyeji wao watatu yaani Merina, Mariya na Morgan ambaye alisimama kama mwanasheria wao.

Ndege waliyokuwa wamepanda iliondoka uwanja wa ndege wa Dar es Salaam saa tisa na ilitarajiwa kutua nchini Gairo kwa mapumziko kidogo, hatimaye Moscow ilitakiwa kutua muda wa saa mbili asubuhi na hapo ndipo ingekuwa mwisho wa safari yao.
Kama walivyokuwa wametarajia waliwasili saa mbili kamili za asubuhi, ndege ilipokanyaga tu ardhi ya nchi hiyo Mariya na Merina wakawa wa kwanza kushuka huku wakiwakaribisha Phillip na familia yake, muda wote huo furaha ilikuwa ikitawala kati yao walishasahau machungu yote na kilichokuwa mbele yao ni kuyafaidi maisha.

“Karibuni sana nyumbani,” Morgan aliongea kwa lugha ya Kiingereza.
“Tunashukuru sana,” Phillip alijibu akiachia tabasamu laini usoni mwake.
Wakati Phillip akifurahia kuingia nchini urusi, kichwani mwa Mariya na Merina pamoja na kuwa na furaha walifikiria jambo moja tu, baba yao alikuwa wapi hivyo walipanga baada ya kufika tu kwenda kufuatilia taarifa za uchunguzi wa polisi ili kujua nini kilitokea baada ya wao kuikabidhi kazi ya kumsaka baba yao mikononi mwao.

Wakaondoka ndani ya uwanja wa ndege moja kwa moja kuelekea nyumbani, huko wakapokelewa na wenyeji wao kisha wakawakaribisha Phillip na familia aliyoambatana nayo.
Wakahakikisha kila kitu kinakwenda sawa na wageni walikuwa wamepata mahitaji yote muhimu wao wakaaga na kutoka kuelekea makao makuu ya polisi kufuatilia majibu ya uchunguzi, wakiongozana na Morgan.

Gari likaendeshwa kwa kasi na baada ya nusu saa tu baadaye walishawasili kituoni hapo.
Kwa umaarufu wao walikaribishwa moja kwa moja ndani na kuonana na mkuu wa polisi wakafanya mkutano mfupi wakitaka kujua nini kiliendelea na ripoti ya polisi haikufichwa ilielezwa wazi kwamba tangu kupotea kwa Victor Fedorov yapata miezi sita, walikuwa wamefanya kila walichoweza na juhudi zote zilionekana kufikia ukingoni, wakapitiliza mbele zaidi na kusema kwamba huenda alikufa na kufunikwa na barafu nzito hivyo kumpoteza kabisa.

Baada ya taarifa hiyo huzuni kubwa ikawafunika wao pia wakahisi kukata tamaa ya kumwona tena baba yao akiwa hai, lakini wakatamani kuona hata maiti yake tu waizike kwa heshima zote lakini hilo nalo lilikuwa limeshindikana, wakabaki njia panda wakisubiri muujiza. Huku wakionyesha masikitiko makubwa wakamshukuru mkuu wa polisi, wakamuaga na kurejea nyumbani.
Mioyo yao iliuma kupita kiasi, mara kadhaa kumbukumbu za baba yao ziliwajia ndani ya vichwa vyao wakikumbuka wema, ucheshi na upendo mwingi aliowaonyesha na sasa alikuwa ametoweka kama upepo mbele ya macho yao.

Ni mawazo hayo ndiyo yaliyosababisha watoto hao kububujikwa na machozi, hakika walikuwa wamepoteza mtu muhimu sana katika maisha yao na asingekuwepo wala kutokea mwingine ambaye angeweza kukidhi shida zao ni kweli alikuwa mkosaji lakini bado aliendelea kubaki kuwa ndiye baba halisi na kibaya zaidi na cha kuumiza, mama yao waliyefunga safari mpaka Afrika, nchini Tanzania kumfuata naye alishakufa miaka mingi iliyopita.

Baada ya gari kufunga breki ndani ya jengo lao, haraka bila kuongea kitu watoto hao wakashuka mbio huku wakikimbia na kuingia ndani ambako nako walipita mbio sebuleni na kuingia chumbani kwao, jambo hilo liliwashangaza wengi na hata Phillip aliyewashuhudia alipojaribu kufuatilia hakupata jibu la kueleweka zaidi sana alisikia sauti ya vilio ikiambatana na kwikwi.

“Morgan kimetokea nini huko mlikokwenda?”
“Hali ni mbaya mpaka sasa hakuna taarifa yoyote muhimu juu ya Victor Fedorov na uchunguzi wa polisi umefikia kikomo jambo moja tu naweza kusema huenda alikufa na kufunikwa na barafu nzito, basi”
“Mungu wangu!” Philllip aliongea kwa sauti ya juu.
“Huo ndiyo ukweli japo unauma hatuna budi kuukubali,” Morgan aliongea naye machozi yalionekana kububujika kwenye mashavu yake.

“Inauma,” Phillip alijibu.
Morgan na Phillip waliendelea kubaki sebuleni kwa muda mrefu wakiongea mambo mengi kama kubadilishana mawazo hatimaye ushauri ukatoka kwamba Mariya na Merina waitwe ili waweze kuongea nao mambo fulani.

“Hata mimi naunga mkono jambo hilo ni lazima tuwape maneno ya faraja, walikubali tukio hilo na kusubiri kama pengine atakuwa hakufa basi ipo siku atajitokeza na kuugana nao,” Phillip aliongea na sekunde tatu tu baadaye Mariya na Merina walishafika sebuleni na kuungana nao, hapo wakafanya mkutano mfupi wa majonzi wakijaribu kuwaeleza wazi kwamba hapakuwa na sababu ya kuhuzunika kwani kila jambo linalotokea katika maisha ya mwanadamu waamini kwamba lilikuwa na sababu.

Wakionyesha majonzi makubwa, wakakubaliana na kilichotokea, zaidi sana Morgan aliwataka kufahamu haki zote za baba yao na yeye angekuwa nao bega kwa bega kuhakikisha hakuna kinachopotea.
Maneno hayo yakawa yamerejesha furaha kwa watoto hao, wakageuka upande aliokuwa ameketi Phillip na kwa pamoja wakatamka maneno haya;

“Umekuja kuchukua nafasi ya baba yetu, hakika wewe ndiye, kuanzia leo utachukua majukumu yote na kuifanya familia kuwa yenye furaha siku zote, tafadhali tunakuomba ukubali na kwa pamoja tunasema tunakupenda,” aliongea Merina kisha walisimama na kutembea kumwelekea Phillip.

Walipomkaribia wakapiga magoti na kuanza kulia huku wakimweleza kwamba walimpenda sana.
“Ninawepanda pia wanangu Mungu alikuwa nayo sababu niwashukuru pia nanyi kwa kunikubali kunipokea na kunilea, Mungu awabariki sana,” Phillip aliwaambia Merina na Mariya.
Kwa pamoja wakakumbatiana na kuanza kulia, yalikuwa ni machozi ya furaha pamoja na kwamba walikuwa katika masikitiko makubwa ya kupotelewa na baba yao kipenzi.

Baada ya muungano huo wote kwa pamoja walidhamiria kushikamana kama ndugu wakiapa kutimiza wajibu na kulinda heshima ya baba yao ambaye alikuwa ndiye muasisi wa utajiri wote waliokuwa nao.
“Jambo la muhimu hivi sasa pamoja na yote tuliyoongea ni muhimu tukatangaza habari za kifo cha Victor Fedorov kwenye vyombo vya habari kwa muda usiopungua mwezi mmoja tuone nini matokeo yake,” Phillip alitoa wazo na wote wakalipokea kwa mikono miwili.

Je, nini kitaendelea baada ya kutangaza kifo kwa mtu ambaye hakujulikana alikufa au yu hai?
 
SEHEMU YA 52


ILIPOISHI

Baada ya muungano huo wote kwa pamoja walidhamiria kushikamana kama ndugu wakiapa kutimiza wajibu na kulinda heshima ya baba yao ambaye alikuwa ndiye muasisi wa utajiri wote waliokuwa nao.
“Jambo la muhimu hivi sasa pamoja na yote tuliyoongea ni muhimu tukatangaza habari za kifo cha Victor Fedorov kwenye vyombo vya habari kwa muda usiopungua mwezi mmoja tuone nini matokeo yake,” Phillip alitoa wazo na wote wakalipokea kwa mikono miwili.

Je, nini kitaendelea baada ya kutangaza kifo kwa mtu ambaye hakujulikana alikufa au yu hai?

SONGA NAYO

Ilionekana kuwa safari nyingine ngumu lakini ilikuwa ni lazima waizoee na kuikubali ili maisha yaendelee kwani hivyo ndivyo dunia ilivyokuwa. Kwa pamoja wakakubaliana na kusimama, tegemeo lao kubwa kwa wakati huo akiwa ni Phillip, ndiye alikuwa baba wa familia kipindi chote wakisubiri kuona nini kingetokea baada ya kutangaza kwenye vyombo vya habari.
“Tutakupenda mpaka mwisho na jambo pekee kwa hivi sasa ni vyema Genevieve akaanza shule haraka iwezekanavyo ili naye apate elimu kama sisi,” Mariya aliongea siku moja wakiwa sebuleni.
“Ni kweli kabisa ni lazima aanze shule mara moja, kesho nitakwenda kuongea na mwalimu wa shule tuliyosoma.”
“Ada je?”
“Tutalipa hakuna shida huyu ni mdogo wetu ni lazima tutimize wajibu kwake.”
“Ahsanteni wanangu Mungu awabariki sana,” Phillip aliongea huku akibubujikwa na machozi.
Furaha ilikuwa imeizunguka nyumba ya Victor Fedorov, kazi zote zikiwa chini ya usimamizi wa Phillip kama baba na Morgan ambaye alikuwa ndiye haswa mwanasheria wa miradi yote iliyomilikiwa na tajiri huyo.
Siku nazo zikazidi kusonga mbele mambo yote yakiwa sawa kama walivyopanga, Genevieve akiwa tayari ameshaanza shule, Phillip, Mariya na Merina wakihakikisha miradi yote inakwenda sawa.
Mwezi wa kwanza ukapita bado wakiwa katika kusubiri, taarifa mbalimbali zikiendelea kutolewa na vyombo vya habari wakati mwingine hata televisheni kubwa nchini humo, lakini bado hakukuwa na majibu yoyote hatimaye nao wakaanza kukubaliana na madai ya polisi ya uchunguzi wao walioufanya kwa kina na kuamini kwamba huenda mzee huyo alikufa na kufunikwa na barafu nzito.
“Pengine inawezekana kweli baba alikufa kitambo kama uchunguzi unavyosema.”
“Hapana hebu tusubiri pengine anataka kutupima kama tumekua.”
“Mariya hakyanani amini tu kwamba baba amefariki.”
“Sijakataa, inawezekana ikawa hivyo ninachokiona mimi hebu tusubiri zaidi.”
“Sawa,” Mariya aliitikia.
Kwa muda wa miezi minne mfululizo bado waliendelea kusubiri huku wakiendelea na shughuli zao kama kawaida na ilipotimia mwezi wa tano wakaanza kuchoka na kukata tamaa kwani walikuwa wamefuatilia kwa karibu sana kila kitu kuchunguza kwa umakini wa hali ya juu na jibu walilokuwa wamelipata halikutofautiana na polisi. Huzuni na majonzi vikatawala upya wakikumbuka mema yote aliyowatendea baba yao enzi za uhai wake.
Hatimaye ikatimu miezi sita wakiwa katika kusubiri mwisho wakafikia uamuzi wa kuutangazia umma kwamba Victor Fedorov aliaminika kufa katika mchezo wa kuteleza kwenye barafu.
“Ni lazima sasa tutangaze kwamba Victor Fedorov alikufa.”
“Tunaungana na wewe.”
“Je, kama ikitokea siku moja akarudi?”
“Hiyo itakuwa habari nyingine lakini sidhani kama jambo hili litatokea.”
“Mh!”
“Huo ndiyo ukweli, hakuna haja ya kuguna wala kujiuliza mara mbilimbili.”
“Morgan kesho asubuhi mchakato huo uanze, sisi kama watoto wa marehemu tupate wasaa japo wa dakika kumi tu katika televisheni ya taifa kuuelezea umma juu ya jambo hilo.”
“Nakubaliana nanyi na kazi hiyo kesho asubuhi itafanyika.”
Saa zikazidi kusonga mbele hatimaye kesho waliyoisubiri kwa hamu kubwa ikawadia na Morgan akafanya taratibu zote na kurejesha majibu kwa Mariya na Merina kwamba alishafanikiwa kuongea na televisheni hiyo kubwa. Maandalizi maalum yakafanyika hatimaye wakaiweka habari hiyo kweupe ikiliacha taifa la Urusi katika mshangao mkubwa na maumivu kutokana na ushirikiano wa mzee huyo kwa jamii iliyomzunguka, umaarufu wa Victor Fedorov ulikuwa mkubwa hivyo kitendo cha kutangazwa kwamba aliaminika kufa kiliwaumiza wengi.
Majonzi, vilio na kuomboleza vikatawala nyumbani kwake, watu mbalimbali maarufu wakiongozwa na rais wa nchi hiyo walifika kutoa pole na rambirambi, wengi wao wakitaka kujua historia kamili ya tukio. Sehemu maalum ilitengwa na kuweka picha kubwa ya Fedorov huku chini yake kukiwa na maneno “Герой ушел” yakimaanisha “Shujaa ameondoka”.
Kutokana na umaarufu wa tajiri huyo nchini Urusi, serikali ikatoa wiki nzima ya maombolezo ishara tosha kwamba alikuwa kipenzi cha watu wengi, hakuwepo mtu hata mmoja aliyefahamu upande wake wa pili kwamba alikuwa ni mtu hatari kupindukia.
Ikiwa ni siku tatu tu tangu kufanyika kwa maombolezo ya Fedorov, kama familia waliamua kwenda kutembelea eneo ambalo ndilo haswa lililoaminika kuchukua maisha ya baba yao kipenzi ambapo mashada mengi yakawekwa eneo hilo pamoja na picha yake kama kumbukumbu pekee katika maisha yao na zoezi hilo lilipokamilika wakarejea nyumbani kuendelea na maombolezo.
Siku ya nne asubuhi jambo la ajabu likatokea na kufanya watu wengi kupigwa na butwaa, ni taarifa kwamba mwili wa mtu asiyefahamika ulikuwa umeonekana ndani ya shimo kubwa lililokuwa Mashariki ya Urusi na mtu mmoja aliyekuwa akifanya mchezo wa kuteleza katika barafu ndiye aliyegundua hilo na kuamua kutoa taarifa polisi ambao walifika mara moja eneo hilo.Gari maalum likatolewa likiwa na polisi ndani yake na likaenda moja kwa moja mpaka eneo husika ili kushuhudia tukio hilo, na ni kweli kabisa wao pia macho yao yaliona kama walivyokuwa wameelezwa.
Haraka taratibu za kuutoa mwili zikafanyika na kuufikisha katika hospitali kuu nchini humo kwa utambuzi, watu wengi walifika na kuangalia kama wangeweza kumfahamu.
***
Akiwa mafichoni aliweza kufuatilia mambo yote ya tajiri huyo mkubwa lengo lake likiwa ni kutaka kulipa kisasi kwa ubaya aliomtendea, hakuwepo mtu hata mmoja aliyefahamu kwamba Ditrov alikuwa hai sehemu fulani kama ilivyoaminika kwa wengi alishakufa muda mrefu.
“Nitakaa hapa huku nikifuatilia nijue jinsi ya kumpata huyu mpumbavu na kulipa kisasi, safari hii atanijua mimi ni nani,” aliwaza Ditrov siku moja lakini ghafla akazipata habari kwamba Victor alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na alikuwa akitafutwa bila mafanikio na kama familia walishaamua kuliweka jambo hilo wazi kwamba alikufa.
“Mh! Atakufaje kabla sijakutana naye? Lakini acha afe ili mimi niendelee kula maisha na sasa nitarejea nyumbani,” alijisemea Ditrov. Akafanya maandalizi ya safari kurejea nyumbani nchini Urusi, huko ndiko alikofahamu ukweli kwamba hakika mwanaume huyo alikuwa amekufa na mwili wake ulikuwa umeokotwa kwenye shimo wakati wa mchezo wa kuteleza katika barafu na watoto wake walithibitisha jambo hilo.
“Maisha sasa mswano pamoja na ubaya wake Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina!” alimaliza Ditrov huku machozi yakimlengalenga.
***
“Mimi naona tukafanye ukaguzi wa mwili huo,” Morgan aliongea ikiwa ni siku ya nne tu.
Bila ubishi wakaondoka nyumbani kuelekea hospitali kila mmoja akiwaza jambo kichwani mwake, bila kupoteza muda moja kwa moja mpaka chumba cha kuhifadhia maiti hapo wakajitambulisha na kuomba kuutambua mwili wa mwanaume aliyeonekana akiwa amekufa.
“Mh!” Merina ndiye aliyekuwa wa kwanza kukagua.
“Kwa nini umeguna?”
“Hapana siye baba, mbona amevimba kiasi hiki? Halafu amekuwa mweusi kupindukia.”
“Hebu?” Mariya akadakia naye bila kukawia akatupa macho yake kuangalia na ghafla wakashuhudia kilio kikali ndani ya chumba.
“Huyu ndiye!” ndilo neno pekee aliloweza kutamka Mariya na kufuatiwa na kwikwi kali.
“Unasema?” Phillip akauliza.
“Hakika nawaambieni aliyelala hapo ni baba yetu!”
Morgan akasogea karibu na kuangalia kwa umakini ni kweli alikuwa Victor Fedorov, mwili wake ukiwa katika hali mbaya kutokana na kukaa katika barafu kwa muda mrefu.
“Hii ni maiti ya Fedorov!”
“Mna uhakika?”
“Ulio kamilifu, hatujakosea hata kidogo, tungependa kupewa kibali cha kuuzika kwa heshima zote,” ndivyo alivyotamka huku akiukagua vyema mwili huo.

Taratibu maalum zikafanyika wakitafuta vibali husika ili kupata ruhusa ya kuuzika mwili huo kwa heshima zote na hatimaye uchunguzi ulipokamilika na kuridhika wakakabidhiwa mwili wa Fedorov ili wauzike.

Jambo hilo liliamsha vilio upya watu wakalia na kuomboleza, wengi wakionekana kuzimia kwa tukio hilo lakini hatimaye mwili wa Fedorov ukashushwa kaburini kwa heshima zote, watu mbalimbali wakahudhuria msiba huo. Lilikuwa ni tukio la kuhuzunisha sana pengine kuliko yote yaliyowahi kutokea kwa wakati huo. Tajiri mkubwa, Victor Fedorov akawa amezikwa.
Kama familia, baada ya maziko wakatoa muda wa mwezi mzima kuomboleza wakisimamisha shughuli zote kwa ajili ya maombolezo.
Mwezi mmoja ulipomalizika wakiwa katika majonzi walianza tena kazi zao na Phillip akateuliwa kushika wadhifa wa Victor Fedorov, akipewa majukumu yote kama baba wa familia hiyo mpya.
Furaha, upendo na amani vikitawala ndani na nje ya familia huku akipewa heshima zote kwa kila kitu. Maisha kwa Phillip yakanyanyuka tena baada ya kuwa ameshaumizwa moyo mara kadhaa lakini akaonekana kusahau na kufurahia maisha mapya akifuta maumivu yote aliyowahi kuyapata maishani mwake.
“Мы любим не только вас, но и Женевьевы и его жены Магдалены. Для нас вы являетесь частью нашей крови ...”
(Tunakupenda si wewe tu bali pia Genevieve na bibi Magdalena. Kwetu sisi ninyi ni sehemu ya damu yetu...) waliongea Mariya na Merina kwa lugha ya Kirusi na wote kwa pamoja wakanyanyuka na kumsogelea Phillip wakammwagia mabusu mfululizo huku wakimkumbatia, ishara tosha kwamba walikuwa wamemkubali na kumpokea kama baba yao katika maisha yote yaliyobaki baada ya Victor Fedorov kufariki.
“Морган! Женевьева! Г-жа Магдалена пожалуйста, приезжают сюда, чтобы быть счастливыми вместе.” (Morgan! Genevieve! Bibi Magdalena tafadhali njooni huku tufurahi pamoja.) Mariya alipaza sauti yake kuwaita watu hao ambao walikuja mbio na wote kwa pamoja wakakamilisha furaha kwa kukumbatiana wakiachia vicheko.
MWISHOOOOOOO!!!!!
 
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi @Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad @Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO @multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden
bwii ONTARIO Kobe The Vein @Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya SITAKI ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo @shedede kamtu33 SteveMollel Ngushi DONALD stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 Ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom