Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 49
Genevieve aliendelea kugonga mlango kwa muda bila baba yake kuitikia, naye pia akaanza kulia akimwita bibi Magdalena aje ili waungane kusaidia kumfanya Phillip afungue mlango. Kwa muda wa nusu saa nzima bado walisimama nje ya mlango wakimsihi Phillip afungue lakini hakufanya hivyo zaidi sauti ilisikika kutoka ndani ya chumba ikiwaeleza wazi kwamba alitaka kufanya uamuzi mgumu hivyo alihitaji nafasi.
“Phillip lakini ni vyema ukatambua kwamba maisha baada ya kifo cha mkeo ni lazima yaendelee.”
“Najua hilo tangu mwanzo lakini inauma, ni bora nikaungana nao.”
“Usimkufuru Mungu na huyu mtoto?”
“Mtoto? Ah! Atapata wasamaria wema wengine wa kumtunza.”
“Baba! Baba!” Genevieve aliita na kwikwi ya kulia ikamkaba, hakuongea tena kitu akatoka mbio eneo hilo na kukimbilia ndani ya chumba kisha naye kujifungia.
Ukawa ni mtihani kwa bibi Magdalena hakufahamu nini afanye kwani kila kitu kilionekana kwenda kombo, kwa muda aliendelea kusimama eneo hilo akitafakari nini cha kufanya hatimaye wazo likamjia ndani ya kichwa chake kwamba ni lazima Phillip akubali kushuka kwani hali ya Genevieve ilikuwa mbaya kutokana na sentensi aliyokuwa ameitamka muda mfupi uliopita.
“Genevieve ameumizwa na kauli yako, hivyo amekimbia kuelekea chumbani, kwa ujumla ameumia.”
“Unasema?”
“Hivyo ndivyo, tafadhali nakusihi utoke na kumwendea ili kumbembeleza.”
Ukimya wa ajabu ukatokea na sekunde tatu tu mlango wa chumba ukaonekana ukifunguliwa na Phillip kutokeza huku jasho jingi likitiririka mwilini mwake, hakusema kitu zaidi ya kukimbia kuelekea upande ambako ndiko chumba cha Genevieve kilikuwepo. Akausukuma mlango na kuingia ndani ya chumba na kilichosikika muda mfupi tu ndani ya chumba hicho ni kilio, wote wawili walikuwa wakilia.
***
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam ndimo Mariya, Merina na Mwanasheria wao walipokuwa wamefikia hapo ndipo pangekuwa nyumbani kwao kwa muda wote ambao wangekuwa Afrika, nchini Tanzania kusaka ukweli wa maisha ya baba yao Victor Federov kwa gharama yoyote ile.
“Tutapumzika leo na kesho tutaanza mchakato, lazima kwanza tuitishe mkutano na waandishi wa habari lakini kabla ya hayo tunahitaji kukutana na mtu mmoja ambaye tutamfanya rafiki huyo ndiye atatusaidia.”
“Mh! Naona kama ni zoezi gumu kidogo,” Mariya.
“La hasha! Ni kitu rahisi nitampata mtu hapa hapa hotelini,” mwanasheria aliwaambia.
“Haya ngoja tuone lakini pia uwe makini kwani hapa tupo ugenini,” Mariya alishauri.
“Usiwe na shaka Mariya kila kitu kitakwenda sawia.”
Baada ya mazungumzo hayo kukamilika pamoja na kwamba alikuwa ni mgeni kabisa, Morgan alitoka ndani ya hoteli hiyo kuangalia mazingira akitafuta ni namna gani angepata msaada ambao ungemsaidia kufanya kazi yake kwa urahisi, kwa kutumia lifti akashuka mpaka mapokezi hapo akawasabahi watu aliowakuta na ghafla kabla hajapiga hatua kutoka nje ya hoteli hiyo macho yake yakagongana na mtu aliyekuwa ameketi pembeni kabisa mwa hoteli hiyo mkononi akiwa na gazeti lililosomeka Uwazi, akapata hamu ya kusogea karibu yake ili aongee naye mambo kadhaa kwake hiyo akaiona kama bahati.
“Habari?” alisabahi kwa lugha ya Kiingereza.
“Nzuri tu,”
“Ah! Naitwa Morgan natokea Urusi.”
“Oh! Karibu mimi naitwa Erick Evarist naishi hapa hapa Tanzania,” Erick alijitambulisha.
“Naweza kuungana na wewe hapa?”
“Bila shaka karibu.”
“Napenda kukufahamu zaidi.”
“Ni mwandishi wa habari nafanya kazi zangu kwenye Kampuni ya Global Publishers.”
“Oh! My God!” Morgan alipaza sauti na kuwafanya watu wote waliokuwa eneo hilo kuacha shughuli zao wakabaki kumshangaa. Erick naye akashindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kinatokea eneo hilo.
Kabla hajaendelea kusema chochote, Morgan akamwomba Erick wasogee pembeni ili waweze kuongea zaidi.
“Hakuna shida,” Erick aliongea akimfuata mwanaume huyo na wote wakaketi kwenye viti vilivyokuwa hapo na mazungumzo maalum yakaanza, Morgan akimweleza wazi kwamba alifurahi kukutana naye na kazi iliyokuwa imemleta nchini Tanzania ni kutaka amsaidie kwa kila kitu na kama angehitaji kiasi chochote cha fedha angekuwa tayari kumpatia lakini tu amsaidie.
Hakuficha kitu akaweka kila kitu wazi kwamba walikuja nchini hapo kutafuta ukweli wa mwanaume aliyeitwa Phillip na mkewe Genevieve na hawakuwa na msaada wowote.
“Niko tayari kukusaidia.”
“Kivipi?”
“Nitakusaidia ufanye kitu kinachoitwa Press Conference, utakutana na waandishi wa habari ambao nitaongea nao kuwaeleza shida yako halafu utatakiwa kufanya kikao cha pamoja kisha kupiga picha ili kuandika habari hizo kwenye magazeti yetu, watu wakisoma naamini utapata ufumbuzi wa tatizo lako.”
“Inaweza ikachukua muda gani kuanzia sasa?”
“Kazi hiyo nitaifanya leo na kesho nitakupa majibu,”
“Tutakutana wapi?”
“Nitakuja hapa hapa hotelini lakini ni vyema ukanipatia namba yako ya simu ili iwe rahisi kuwasiliana na wewe.”
“Ahsante rafiki, wewe kwangu ni kama malaika, chukua hii,” aliongea Morgan akichomoa kadi yake yenye namba za simu na kumkabidhi Erick ambaye aliipokea, wakaagana wakiahidiana kukutana tena kesho yake.
Baada tu ya Erick kuondoka eneo hilo, Morgan alipandisha lifti haraka kwenda chumbani kwa akina Marina kuwaeleza kila kitu. Mariya na Marina walifurahi sana kupewa habari hizo njema.
“Mungu yupo pamoja nasi, naona mwanzo umekuwa mzuri,” Mariya aliwaambia.
“Tena tutakapofanikisha jambo hili itabidi tukamtolee shukurani ya pekee,” Marina aliunga mkono.
Wakiwa pale hotelini, waliona saa zinachelewa ili kuifikia siku iliyofuata ambayo mwanasheria wao angekutana na Erick na kumpa utaratibu wa mkutano wao na waandishi wa habari ambao ungemaliza kazi iliyowaleta Tanzania.
Kama walivyokuwa wamepanga kesho ikawadia, Morgan akiwa tayari kumsubiri Erick afike ili waendelee na mazungumzo yao na kuona walikuwa wamefanikiwa kwa kiasi gani kuhusu shughuli iliyokuwa mbele yao.
Ilipotimu saa tatu kamili asuhubi, Erick aliwasilia hotelini hapo na mazungumzo yakafanyika na mwisho ukaonekana kuwa mzuri akimweleza wazi kwamba alishafanikiwa kukutana na baadhi ya waandishi na kuwaeleza habari hiyo na walipanga kukutana siku iliyofuata pale hotelini.
Morgan akashukuru na kupeana ahadi ya kukutana na Erick siku iliyofuata kisha wakaagana.
Muda huo huo alifanya utaratibu wa kupata kibali cha kufanya mkutano ndani ya hoteli hiyo, ambapo alipewa chumba kikubwa kilichotumika kwa shughuli hiyo.
***
Hali ya Phillip ilikuwa imebadilika kabisa utanashati wote aliokuwa nao kipindi akiwa na mke wake ukawa umepotea, mahudhurio ya kazi nayo yalionekana kusuasua kitendo kilichofanya mpaka mabosi wake waaanze kuingiwa na wasiwasi.
Nyumbani nako hali ilikuwa tofauti kwani muda mwingi aliutumia kulala na alipochoka alitoka bila kuaga na kuingia mtaani kunywa pombe ili kupoteza msongo wa mawazo.
Phillip akawa ni mtu wa kukitamani kifo kuliko kitu kingine, haikuishia hapo akaanza tabia ya kutoka nyumbani na kwenda makaburini na alipofika huko alitafuta kaburi la mkewe Lina na kulala juu yake.
Ni hali hiyo ndiyo iliyozidi kuichanganya zaidi familia yake nao pia wakaingiwa na wasiwasi na kuamini kwamba si muda mrefu Phillip angekuwa mwendawazimu, ndugu na jamaa wakakaa kikao kuangalia ni jinsi gani wanaweza kumsaidia na walipomuuliza, jibu lilikuwa moja tu.
“Nataka kufa, basi.”
MAISHA yalikuwa yamebadilika kabisa kwa Phillip ni kama vile dunia yake ilikuwa imegeuka na kuwa nje ndani, akapoteza kabisa mwelekeo wa maisha yake na kusahau kwamba alikuwa ana jukumu la kumlea mtoto mdogo Genevieve ambaye bado alihitaji ushauri wa wazazi wake japo tayari mmoja alishaaga dunia.
Ushauri na ushawishi mkubwa wa ndugu, jamaa na marafiki haukusaidia kitu na hata walipoamua kutumia ofisi yake kumshauri bado hakubadilika ndiyo kwanza alizidisha ulevi na kutembea barabarani kutwa nzima akiongea na kutukana watu bila sababu.
Phillip akawa ameharibikiwa kabisa, ofisi ikaamua kumwachisha kazi kwa nguvu lakini wakiahidi kumsaidia kama tu msaada wowote ungehitajika, nyumbani nako hali kwa mtoto ikawa mbaya hata shule akawa haendi tena kwa sababu hapakuwa na ada ili aweze kuendelea na masomo, hakika maisha yakawa magumu kupindukia.
Lakini bado watu mbalimbali waliomfahamu Phillip hawakumwacha peke yake waliendelea kumshauri na kumpa moyo kwamba maisha yaliendelea na kamwe yasingesimama. Phillip akapokea ushauri wao ambao uliingia sikio la kulia na kutokea sikio la kushoto kwani hakuweza kubadilika, zaidi sana vituko viliongezeka nao pia wakaanza kuchoka na kumwacha afanye alivyopenda.
***
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam chumba maalum kilikuwa kimeandaliwa tayari kwa mkutano mfupi ambao ungefanyika siku hiyo. Mariya na Merina ambao ndiyo waongeaji wakubwa, pembeni yao akiwepo mwanasheria aliyesimamia mambo yote zikiwemo mali za baba yao Victor Fedorov ambaye mpaka wakati huo hakufahamika kama alikuwa amekufa au la!
Waandishi walikuwa ni wengi mno mikononi mwao wakiwa na kalamu zao na kamera ili kuchukua habari ambayo ingepelekwa katika vyombo vyote vya habari yaani magazeti, redio na televisheni.
Mkutano ukawa umeanza, Mariya na Merina wakijitambulisha kwamba walikuwa akina nani na walitokea wapi na nini lilikuwa lengo lililowaleta nchini Tanzania, waliongea katika lugha ya Kirusi na Morgan akaitohoa katika lugha ya Kiingereza na baadaye Erick Evarist akatafsiri katika lugha ya Kiswahili.
Wakisisitiza kwamba walihitaji kufahamu mahali ambako Phillip na mkewe Genevieve wangepatikana na kwa gharama yoyote ile wangekuwa tayari kutimiza hilo lakini tu wapate ushirikiano.
Hivyo ndivyo mambo yalivyoendelea ndani ya hoteli hiyo kwenye chumba maalum, kwa muda wa saa nzima watoto hao waliendelea kuongea na waandishi wa habari wakiwaomba na kuwasihi kusaidia kuandika habari hizo ili hatimaye mtu anayetafutwa aweze kupatikana kwa urahisi.
“Wanamtafuta nani?”
“Wanasema wanatafuta familia ya Phillip na mkewe Genevieve.”
“Mh!”
“Kwa nini?”
“Hata sisi hatujui ila wanasema kwamba Genevieve ndiye mama yao mzazi.”
“Hawa watoto mbona siyo Watanzania?”
“Unalosema ni kweli lakini hatuwezi kujua, sisi tufanye tu kazi yetu,” yalikuwa ni maongezi kati ya waandishi wa habari waliokuwepo kwenye mkutano huo wakijiuliza maswali mengi juu ya mkutano huo na watu waliouitisha.
Baada ya habari kukamilika Mariya na Merina wakawashukuru waandishi huku wakiwashika mkono na kuwapatia bahasha ambayo ndani yake haikufahamika ilikuwa na nini na kuwatakia kila la kheri katika utendaji wa kazi zao na kuwaeleza wazi kwamba ili waweze kuwapata watu waliowahitaji, waliwategemea sana wao.
Waandishi nao wakashukuru wakiahidi kufanya kila kilichowezekana habari hiyo ichapishwe katika magazeti na ikiwezekana kutangazwa katika vyombo vyote vya habari zikiwemo redio na televisheni.
Baada ya waandishi kuondoka, wakarejea ndani ya vyumba vyao hamu yao kubwa ikabaki kusubiri nini magazeti yangeandika, ambapo macho na masikio yao yote yakaelekezwa huko.
“Nafikiria kila kitu kitakwenda sawa, tusubiri kesho tuone,” Morgan aliongea.
“Hata mimi nahisi hivyo ngoja tuone,” waliendelea kuongea wakijipa matumaini kwamba kila kitu kingekwenda sawa.
Saa zikazidi kusonga mbele hatimaye kiza kikaingia, hapo wakaamua kula chakula cha usiku na kuingia kwenye vitanda vyao wakiwa na hamu ya kujua kesho yake kitatokea nini.
***
Asubuhi ya siku iliyofuata Morgan alikuwa wa kwanza kutoka ndani ya chumba na bila kufanya kitu chochote akashuka kwa lifti mpaka mapokezi hapo akasabahi watu aliowakuta kisha kutoka nje ya hoteli kuelekea barabarani akitafuta mahali ambako angekutana na wauza magazeti na kununua ili kusoma kama habari yao ingekuwa imeandikwa siku hiyo.
Ni kweli kabisa alichokuwa amekifikiria kichwani mwake hakikuwa uongo, mtu wa kwanza tu aliyekutana naye akiwa na magazeti mkononi akamwita na kuchukua moja ya magazeti aliyokuwa nayo, macho yake yakakutana na picha ya Mariya na Merina mbele yao kukiwa na vipaza sauti vingi, hakuelewa lugha ya Kiswahili lakini aliweza kuisoma picha.
Akamwomba tena muuza magazeti ampatie magazeti mengine zaidi, nayo habari iliyosomeka ukurasa wa kwanza tu wa magazeti hayo ilikuwa ileile ya kwao, furaha ikamjaa moyoni mwake akajiona mshindi kati ya washindi na akalazimika kununua magazeti zaidi ya sita akalipa na kurejea ndani ya hoteli huku jasho likimtoka.
Haraka akapandisha lifti na moja kwa moja akauendea mlango ambao ndani yake walilala Mariya na Merina akagonga kwa nguvu na kusubiri mlango ufunguliwe na akiwa hapo akashuhudia Mariya akichungulia baada ya kufungua mlango.
“Magazeti haya hapa,” aliongea akinyoosha mkono kumpatia Mariya magazeti yote aliyokuwa nayo.
Kwa macho yake yote mawili akashuhudia kurasa za mbele za magazeti hayo zikiwa na picha yao kubwa akacheka na kutabasamu na bila kusema neno akarejea ndani ya chumba chao huku akimwita Merina.
“Merina! Merina, amka uone mwenyewe magazeti karibu yote yameandika habari yetu, kazi imekuwa rahisi sana kuliko tulivyotarajia…,” aliongea Mariya bila kuweka kituo.
Furaha ilikuwa imetawala ndani ya chumba wakiamini kwamba muda si mrefu kila kitu kingekwenda sawa kama walivyofikiria, kwa pamoja wakakumbatiana na kupigana mabusu lakini ghafla wakiwa katika furaha yao hiyo taswira ya baba yao Victor Fedorov mwanaume aliyewapenda kupindukia ikawajia, ni kweli walikuwa na furaha ya kuufahamu ukweli mwingine uliokuwa umejificha lakini pia Fedorov alikuwa ndiye mzazi wao halisi pamoja na mambo yote mabaya aliyoyatenda bado walimpenda.
“Sijui atakuwa wapi? Amepatwa na kitu gani? Inauma sana,” aliongea Merina huku akilia.
***
Asubuhi ya siku iliyofuata baada tu ya Merina na Mariya kufanya mkutano jana yake na waandishi wa habari, Phillip alikuwa katika mitaa ya Posta akikatisha huku na kule bila kuelewa anakwenda wapi.
Ghafla mbele yake akaiona meza ya magazeti na kuamua kutupa macho juu yake ili angalau asome kilichokuwa kimeandikwa siku hiyo, akasogea karibu kabisa na muuza magazeti kisha kumsabahi.
“Habari za leo?”
“Nzuri tu kaka karibu.”
“Ahsante, naweza kupitishapitisha macho kidogo?”
“Bila shaka lakini usiguse kama hutalinunua.”
Akaitika kwa ishara ya kutingisha kichwa kisha akasogea karibu na meza hiyo na kutupa macho juu ya magazeti, ni habari ya kwanza tu katika gazeti la Uwazi ikamshtua.
“Mh!”
“Mbona umeguna kaka?”
“Hii habari, inanihusu mimi kabisa na hao ni watoto wangu lakini walikufa.”
“Wewe mzee chizi nini utakuwa hamnazo watoto wako? Wewe? Hebu ondoka hapa haraka kabla sijakuitia mgambo wa jiji.”
“Dorice na Dorica,” alitamka kwa sauti ya juu.
Nimekuambia ondoka haraka,” aliongea muuza magazeti huyo akimvuta Phillip kumwondoa eneo hilo.
“Usinifanyie hivyo ndugu yangu nakuambia ukweli tafadhali nipe gazeti nione vizuri.”
“Wazee wengine bwana sijui wachawi au wanatumwa kuwangia biashara za watu! Asubuhi hii, kama unataka gazeti si ununue lakini siyo ujipendekeze kwa watoto wa watu.”
“Usinivu…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake tayari akashuhudia vibao mfululizo vikipita mashavuni mwake.
je nini kiliendelea
Genevieve aliendelea kugonga mlango kwa muda bila baba yake kuitikia, naye pia akaanza kulia akimwita bibi Magdalena aje ili waungane kusaidia kumfanya Phillip afungue mlango. Kwa muda wa nusu saa nzima bado walisimama nje ya mlango wakimsihi Phillip afungue lakini hakufanya hivyo zaidi sauti ilisikika kutoka ndani ya chumba ikiwaeleza wazi kwamba alitaka kufanya uamuzi mgumu hivyo alihitaji nafasi.
“Phillip lakini ni vyema ukatambua kwamba maisha baada ya kifo cha mkeo ni lazima yaendelee.”
“Najua hilo tangu mwanzo lakini inauma, ni bora nikaungana nao.”
“Usimkufuru Mungu na huyu mtoto?”
“Mtoto? Ah! Atapata wasamaria wema wengine wa kumtunza.”
“Baba! Baba!” Genevieve aliita na kwikwi ya kulia ikamkaba, hakuongea tena kitu akatoka mbio eneo hilo na kukimbilia ndani ya chumba kisha naye kujifungia.
Ukawa ni mtihani kwa bibi Magdalena hakufahamu nini afanye kwani kila kitu kilionekana kwenda kombo, kwa muda aliendelea kusimama eneo hilo akitafakari nini cha kufanya hatimaye wazo likamjia ndani ya kichwa chake kwamba ni lazima Phillip akubali kushuka kwani hali ya Genevieve ilikuwa mbaya kutokana na sentensi aliyokuwa ameitamka muda mfupi uliopita.
“Genevieve ameumizwa na kauli yako, hivyo amekimbia kuelekea chumbani, kwa ujumla ameumia.”
“Unasema?”
“Hivyo ndivyo, tafadhali nakusihi utoke na kumwendea ili kumbembeleza.”
Ukimya wa ajabu ukatokea na sekunde tatu tu mlango wa chumba ukaonekana ukifunguliwa na Phillip kutokeza huku jasho jingi likitiririka mwilini mwake, hakusema kitu zaidi ya kukimbia kuelekea upande ambako ndiko chumba cha Genevieve kilikuwepo. Akausukuma mlango na kuingia ndani ya chumba na kilichosikika muda mfupi tu ndani ya chumba hicho ni kilio, wote wawili walikuwa wakilia.
***
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam ndimo Mariya, Merina na Mwanasheria wao walipokuwa wamefikia hapo ndipo pangekuwa nyumbani kwao kwa muda wote ambao wangekuwa Afrika, nchini Tanzania kusaka ukweli wa maisha ya baba yao Victor Federov kwa gharama yoyote ile.
“Tutapumzika leo na kesho tutaanza mchakato, lazima kwanza tuitishe mkutano na waandishi wa habari lakini kabla ya hayo tunahitaji kukutana na mtu mmoja ambaye tutamfanya rafiki huyo ndiye atatusaidia.”
“Mh! Naona kama ni zoezi gumu kidogo,” Mariya.
“La hasha! Ni kitu rahisi nitampata mtu hapa hapa hotelini,” mwanasheria aliwaambia.
“Haya ngoja tuone lakini pia uwe makini kwani hapa tupo ugenini,” Mariya alishauri.
“Usiwe na shaka Mariya kila kitu kitakwenda sawia.”
Baada ya mazungumzo hayo kukamilika pamoja na kwamba alikuwa ni mgeni kabisa, Morgan alitoka ndani ya hoteli hiyo kuangalia mazingira akitafuta ni namna gani angepata msaada ambao ungemsaidia kufanya kazi yake kwa urahisi, kwa kutumia lifti akashuka mpaka mapokezi hapo akawasabahi watu aliowakuta na ghafla kabla hajapiga hatua kutoka nje ya hoteli hiyo macho yake yakagongana na mtu aliyekuwa ameketi pembeni kabisa mwa hoteli hiyo mkononi akiwa na gazeti lililosomeka Uwazi, akapata hamu ya kusogea karibu yake ili aongee naye mambo kadhaa kwake hiyo akaiona kama bahati.
“Habari?” alisabahi kwa lugha ya Kiingereza.
“Nzuri tu,”
“Ah! Naitwa Morgan natokea Urusi.”
“Oh! Karibu mimi naitwa Erick Evarist naishi hapa hapa Tanzania,” Erick alijitambulisha.
“Naweza kuungana na wewe hapa?”
“Bila shaka karibu.”
“Napenda kukufahamu zaidi.”
“Ni mwandishi wa habari nafanya kazi zangu kwenye Kampuni ya Global Publishers.”
“Oh! My God!” Morgan alipaza sauti na kuwafanya watu wote waliokuwa eneo hilo kuacha shughuli zao wakabaki kumshangaa. Erick naye akashindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kinatokea eneo hilo.
Kabla hajaendelea kusema chochote, Morgan akamwomba Erick wasogee pembeni ili waweze kuongea zaidi.
“Hakuna shida,” Erick aliongea akimfuata mwanaume huyo na wote wakaketi kwenye viti vilivyokuwa hapo na mazungumzo maalum yakaanza, Morgan akimweleza wazi kwamba alifurahi kukutana naye na kazi iliyokuwa imemleta nchini Tanzania ni kutaka amsaidie kwa kila kitu na kama angehitaji kiasi chochote cha fedha angekuwa tayari kumpatia lakini tu amsaidie.
Hakuficha kitu akaweka kila kitu wazi kwamba walikuja nchini hapo kutafuta ukweli wa mwanaume aliyeitwa Phillip na mkewe Genevieve na hawakuwa na msaada wowote.
“Niko tayari kukusaidia.”
“Kivipi?”
“Nitakusaidia ufanye kitu kinachoitwa Press Conference, utakutana na waandishi wa habari ambao nitaongea nao kuwaeleza shida yako halafu utatakiwa kufanya kikao cha pamoja kisha kupiga picha ili kuandika habari hizo kwenye magazeti yetu, watu wakisoma naamini utapata ufumbuzi wa tatizo lako.”
“Inaweza ikachukua muda gani kuanzia sasa?”
“Kazi hiyo nitaifanya leo na kesho nitakupa majibu,”
“Tutakutana wapi?”
“Nitakuja hapa hapa hotelini lakini ni vyema ukanipatia namba yako ya simu ili iwe rahisi kuwasiliana na wewe.”
“Ahsante rafiki, wewe kwangu ni kama malaika, chukua hii,” aliongea Morgan akichomoa kadi yake yenye namba za simu na kumkabidhi Erick ambaye aliipokea, wakaagana wakiahidiana kukutana tena kesho yake.
Baada tu ya Erick kuondoka eneo hilo, Morgan alipandisha lifti haraka kwenda chumbani kwa akina Marina kuwaeleza kila kitu. Mariya na Marina walifurahi sana kupewa habari hizo njema.
“Mungu yupo pamoja nasi, naona mwanzo umekuwa mzuri,” Mariya aliwaambia.
“Tena tutakapofanikisha jambo hili itabidi tukamtolee shukurani ya pekee,” Marina aliunga mkono.
Wakiwa pale hotelini, waliona saa zinachelewa ili kuifikia siku iliyofuata ambayo mwanasheria wao angekutana na Erick na kumpa utaratibu wa mkutano wao na waandishi wa habari ambao ungemaliza kazi iliyowaleta Tanzania.
Kama walivyokuwa wamepanga kesho ikawadia, Morgan akiwa tayari kumsubiri Erick afike ili waendelee na mazungumzo yao na kuona walikuwa wamefanikiwa kwa kiasi gani kuhusu shughuli iliyokuwa mbele yao.
Ilipotimu saa tatu kamili asuhubi, Erick aliwasilia hotelini hapo na mazungumzo yakafanyika na mwisho ukaonekana kuwa mzuri akimweleza wazi kwamba alishafanikiwa kukutana na baadhi ya waandishi na kuwaeleza habari hiyo na walipanga kukutana siku iliyofuata pale hotelini.
Morgan akashukuru na kupeana ahadi ya kukutana na Erick siku iliyofuata kisha wakaagana.
Muda huo huo alifanya utaratibu wa kupata kibali cha kufanya mkutano ndani ya hoteli hiyo, ambapo alipewa chumba kikubwa kilichotumika kwa shughuli hiyo.
***
Hali ya Phillip ilikuwa imebadilika kabisa utanashati wote aliokuwa nao kipindi akiwa na mke wake ukawa umepotea, mahudhurio ya kazi nayo yalionekana kusuasua kitendo kilichofanya mpaka mabosi wake waaanze kuingiwa na wasiwasi.
Nyumbani nako hali ilikuwa tofauti kwani muda mwingi aliutumia kulala na alipochoka alitoka bila kuaga na kuingia mtaani kunywa pombe ili kupoteza msongo wa mawazo.
Phillip akawa ni mtu wa kukitamani kifo kuliko kitu kingine, haikuishia hapo akaanza tabia ya kutoka nyumbani na kwenda makaburini na alipofika huko alitafuta kaburi la mkewe Lina na kulala juu yake.
Ni hali hiyo ndiyo iliyozidi kuichanganya zaidi familia yake nao pia wakaingiwa na wasiwasi na kuamini kwamba si muda mrefu Phillip angekuwa mwendawazimu, ndugu na jamaa wakakaa kikao kuangalia ni jinsi gani wanaweza kumsaidia na walipomuuliza, jibu lilikuwa moja tu.
“Nataka kufa, basi.”
MAISHA yalikuwa yamebadilika kabisa kwa Phillip ni kama vile dunia yake ilikuwa imegeuka na kuwa nje ndani, akapoteza kabisa mwelekeo wa maisha yake na kusahau kwamba alikuwa ana jukumu la kumlea mtoto mdogo Genevieve ambaye bado alihitaji ushauri wa wazazi wake japo tayari mmoja alishaaga dunia.
Ushauri na ushawishi mkubwa wa ndugu, jamaa na marafiki haukusaidia kitu na hata walipoamua kutumia ofisi yake kumshauri bado hakubadilika ndiyo kwanza alizidisha ulevi na kutembea barabarani kutwa nzima akiongea na kutukana watu bila sababu.
Phillip akawa ameharibikiwa kabisa, ofisi ikaamua kumwachisha kazi kwa nguvu lakini wakiahidi kumsaidia kama tu msaada wowote ungehitajika, nyumbani nako hali kwa mtoto ikawa mbaya hata shule akawa haendi tena kwa sababu hapakuwa na ada ili aweze kuendelea na masomo, hakika maisha yakawa magumu kupindukia.
Lakini bado watu mbalimbali waliomfahamu Phillip hawakumwacha peke yake waliendelea kumshauri na kumpa moyo kwamba maisha yaliendelea na kamwe yasingesimama. Phillip akapokea ushauri wao ambao uliingia sikio la kulia na kutokea sikio la kushoto kwani hakuweza kubadilika, zaidi sana vituko viliongezeka nao pia wakaanza kuchoka na kumwacha afanye alivyopenda.
***
Ndani ya hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam chumba maalum kilikuwa kimeandaliwa tayari kwa mkutano mfupi ambao ungefanyika siku hiyo. Mariya na Merina ambao ndiyo waongeaji wakubwa, pembeni yao akiwepo mwanasheria aliyesimamia mambo yote zikiwemo mali za baba yao Victor Fedorov ambaye mpaka wakati huo hakufahamika kama alikuwa amekufa au la!
Waandishi walikuwa ni wengi mno mikononi mwao wakiwa na kalamu zao na kamera ili kuchukua habari ambayo ingepelekwa katika vyombo vyote vya habari yaani magazeti, redio na televisheni.
Mkutano ukawa umeanza, Mariya na Merina wakijitambulisha kwamba walikuwa akina nani na walitokea wapi na nini lilikuwa lengo lililowaleta nchini Tanzania, waliongea katika lugha ya Kirusi na Morgan akaitohoa katika lugha ya Kiingereza na baadaye Erick Evarist akatafsiri katika lugha ya Kiswahili.
Wakisisitiza kwamba walihitaji kufahamu mahali ambako Phillip na mkewe Genevieve wangepatikana na kwa gharama yoyote ile wangekuwa tayari kutimiza hilo lakini tu wapate ushirikiano.
Hivyo ndivyo mambo yalivyoendelea ndani ya hoteli hiyo kwenye chumba maalum, kwa muda wa saa nzima watoto hao waliendelea kuongea na waandishi wa habari wakiwaomba na kuwasihi kusaidia kuandika habari hizo ili hatimaye mtu anayetafutwa aweze kupatikana kwa urahisi.
“Wanamtafuta nani?”
“Wanasema wanatafuta familia ya Phillip na mkewe Genevieve.”
“Mh!”
“Kwa nini?”
“Hata sisi hatujui ila wanasema kwamba Genevieve ndiye mama yao mzazi.”
“Hawa watoto mbona siyo Watanzania?”
“Unalosema ni kweli lakini hatuwezi kujua, sisi tufanye tu kazi yetu,” yalikuwa ni maongezi kati ya waandishi wa habari waliokuwepo kwenye mkutano huo wakijiuliza maswali mengi juu ya mkutano huo na watu waliouitisha.
Baada ya habari kukamilika Mariya na Merina wakawashukuru waandishi huku wakiwashika mkono na kuwapatia bahasha ambayo ndani yake haikufahamika ilikuwa na nini na kuwatakia kila la kheri katika utendaji wa kazi zao na kuwaeleza wazi kwamba ili waweze kuwapata watu waliowahitaji, waliwategemea sana wao.
Waandishi nao wakashukuru wakiahidi kufanya kila kilichowezekana habari hiyo ichapishwe katika magazeti na ikiwezekana kutangazwa katika vyombo vyote vya habari zikiwemo redio na televisheni.
Baada ya waandishi kuondoka, wakarejea ndani ya vyumba vyao hamu yao kubwa ikabaki kusubiri nini magazeti yangeandika, ambapo macho na masikio yao yote yakaelekezwa huko.
“Nafikiria kila kitu kitakwenda sawa, tusubiri kesho tuone,” Morgan aliongea.
“Hata mimi nahisi hivyo ngoja tuone,” waliendelea kuongea wakijipa matumaini kwamba kila kitu kingekwenda sawa.
Saa zikazidi kusonga mbele hatimaye kiza kikaingia, hapo wakaamua kula chakula cha usiku na kuingia kwenye vitanda vyao wakiwa na hamu ya kujua kesho yake kitatokea nini.
***
Asubuhi ya siku iliyofuata Morgan alikuwa wa kwanza kutoka ndani ya chumba na bila kufanya kitu chochote akashuka kwa lifti mpaka mapokezi hapo akasabahi watu aliowakuta kisha kutoka nje ya hoteli kuelekea barabarani akitafuta mahali ambako angekutana na wauza magazeti na kununua ili kusoma kama habari yao ingekuwa imeandikwa siku hiyo.
Ni kweli kabisa alichokuwa amekifikiria kichwani mwake hakikuwa uongo, mtu wa kwanza tu aliyekutana naye akiwa na magazeti mkononi akamwita na kuchukua moja ya magazeti aliyokuwa nayo, macho yake yakakutana na picha ya Mariya na Merina mbele yao kukiwa na vipaza sauti vingi, hakuelewa lugha ya Kiswahili lakini aliweza kuisoma picha.
Akamwomba tena muuza magazeti ampatie magazeti mengine zaidi, nayo habari iliyosomeka ukurasa wa kwanza tu wa magazeti hayo ilikuwa ileile ya kwao, furaha ikamjaa moyoni mwake akajiona mshindi kati ya washindi na akalazimika kununua magazeti zaidi ya sita akalipa na kurejea ndani ya hoteli huku jasho likimtoka.
Haraka akapandisha lifti na moja kwa moja akauendea mlango ambao ndani yake walilala Mariya na Merina akagonga kwa nguvu na kusubiri mlango ufunguliwe na akiwa hapo akashuhudia Mariya akichungulia baada ya kufungua mlango.
“Magazeti haya hapa,” aliongea akinyoosha mkono kumpatia Mariya magazeti yote aliyokuwa nayo.
Kwa macho yake yote mawili akashuhudia kurasa za mbele za magazeti hayo zikiwa na picha yao kubwa akacheka na kutabasamu na bila kusema neno akarejea ndani ya chumba chao huku akimwita Merina.
“Merina! Merina, amka uone mwenyewe magazeti karibu yote yameandika habari yetu, kazi imekuwa rahisi sana kuliko tulivyotarajia…,” aliongea Mariya bila kuweka kituo.
Furaha ilikuwa imetawala ndani ya chumba wakiamini kwamba muda si mrefu kila kitu kingekwenda sawa kama walivyofikiria, kwa pamoja wakakumbatiana na kupigana mabusu lakini ghafla wakiwa katika furaha yao hiyo taswira ya baba yao Victor Fedorov mwanaume aliyewapenda kupindukia ikawajia, ni kweli walikuwa na furaha ya kuufahamu ukweli mwingine uliokuwa umejificha lakini pia Fedorov alikuwa ndiye mzazi wao halisi pamoja na mambo yote mabaya aliyoyatenda bado walimpenda.
“Sijui atakuwa wapi? Amepatwa na kitu gani? Inauma sana,” aliongea Merina huku akilia.
***
Asubuhi ya siku iliyofuata baada tu ya Merina na Mariya kufanya mkutano jana yake na waandishi wa habari, Phillip alikuwa katika mitaa ya Posta akikatisha huku na kule bila kuelewa anakwenda wapi.
Ghafla mbele yake akaiona meza ya magazeti na kuamua kutupa macho juu yake ili angalau asome kilichokuwa kimeandikwa siku hiyo, akasogea karibu kabisa na muuza magazeti kisha kumsabahi.
“Habari za leo?”
“Nzuri tu kaka karibu.”
“Ahsante, naweza kupitishapitisha macho kidogo?”
“Bila shaka lakini usiguse kama hutalinunua.”
Akaitika kwa ishara ya kutingisha kichwa kisha akasogea karibu na meza hiyo na kutupa macho juu ya magazeti, ni habari ya kwanza tu katika gazeti la Uwazi ikamshtua.
“Mh!”
“Mbona umeguna kaka?”
“Hii habari, inanihusu mimi kabisa na hao ni watoto wangu lakini walikufa.”
“Wewe mzee chizi nini utakuwa hamnazo watoto wako? Wewe? Hebu ondoka hapa haraka kabla sijakuitia mgambo wa jiji.”
“Dorice na Dorica,” alitamka kwa sauti ya juu.
Nimekuambia ondoka haraka,” aliongea muuza magazeti huyo akimvuta Phillip kumwondoa eneo hilo.
“Usinifanyie hivyo ndugu yangu nakuambia ukweli tafadhali nipe gazeti nione vizuri.”
“Wazee wengine bwana sijui wachawi au wanatumwa kuwangia biashara za watu! Asubuhi hii, kama unataka gazeti si ununue lakini siyo ujipendekeze kwa watoto wa watu.”
“Usinivu…,” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake tayari akashuhudia vibao mfululizo vikipita mashavuni mwake.
je nini kiliendelea