Simulizi: Msichana Ndotoni Mwangu

Simulizi: Msichana Ndotoni Mwangu

SEHEMU YA 29


SURA yake ilikuwa imebadilika kabisa, macho yakabadilika na kuwa ya rangi nyekundu, mwili wake ukaanza kutetemeka kama mtu aliyekuwa na homa kali, Victor Fedorov akauona utajiri wote aliokuwa nao haukuwa na maana kwake kama tu angewakosa watoto wake ambao kwa hakika alikuwa ametumia kiasi kikubwa cha fedha ili kuwapata na sasa walikuwa katika hatari nyingine ya kifo kama tu asingetimiza jambo alilotakiwa kulifanya ndani ya saa chache alizopewa.

Kwa muda wa dakika tano aliendelea kutafakari na hakuelewa ni kwa nini mtekaji huyo alifanya tendo hilo, akavuta kumbukumbu zake nyuma akijaribu kufikiria watu wote aliowahi kuwakosea na kuwadhulumu lakini hakuna alichokumbuka.
Mara kadhaa taswira ya Ditrov ilimjia lakini akatupilia mbali mawazo juu ya mtu huyo na kuamini kwamba tayari alishakufa.

“Nilimuua ili kuficha siri sikuwa na tatizo jingine kabla!” alisema akitembea kukielekea kiti kilichokuwa mbele yake. Huku jasho jingi likimtiririka, akakisogelea kiti na kuketi, moyoni mwake akiwa na hofu juu ya watoto wake.

“Nitatoa kiasi chochote cha fedha atakachohitaji mtu huyo ili mradi tu niwapate watoto wangu!” aliwaza akijifuta machozi.
Alipotupa macho yake kwenye saa yake ya mkononi hofu ikazidi kumwingia, mbele yake kulikuwa na saa kumi tu zilizobaki katika saa ishirini na nne alizopewa na muuaji.

Haraka akanyanyuka kitini na kusogelea tena simu akapiga namba zilezile alizobonyeza mwanzo kisha kuiweka simu sikioni, alikuwa hapo kuzungumza na mtu huyo ataje kiasi hicho cha fedha na sehemu ambapo angezikuta na yeye kupata watoto wake wakiwa salama.
***
Ilikuwa ni familia yenye furaha kupita kawaida, kila mtu aliyewaona aliona wivu, hakika walivutia, walikuwa na kila sababu ya kuitwa mke na mume. Lakini pamoja na mambo yote hayo kutawala maishani mwao, jambo moja tu lilikuwa likiwasumbua ni wapi wangepata mtoto.

Kwa mwanamke halikuwa tatizo sana, kazi kubwa ilikuwa kwa mwanaume ambaye alitumia muda mwingi kufikiria namna gani angeitwa baba kama ilivyowahi kutokea miaka mingi kabla.
“Darling” (mpenzi), Phillip aliita siku moja asubuhi.
“Yes baby!” (Ndiyo mpenzi)

“Ni miaka minne sasa tupo kwenye ndoa lakini mimi sina uwezo wa kuzaa nataka tuliongelee jambo hili ili tufikie muafaka juu ya nini cha kufanya, napenda niitwe baba hata kama mtoto huyo atakuwa si wa kwangu,” alisema Phillip.
“Unamaanisha nini Phillip?”
“Sina nia mbaya, ila nataka nikupe nafasi ya wewe kuzaa kwa sababu huna tatizo lolote.”
“Mh!” Lina akaguna.

“Ni ukweli mke wangu nakupenda sana lakini nitakupenda zaidi utakapofanikiwa kuniletea mtoto.”
“Phillip mbona sikuelewi, mtoto atoke wapi? Ni kweli mimi sina tatizo lakini nitampata wapi mtoto ili hali wewe ndiye mume wangu na tayari una tatizo?”

“Tafuta mwanaume yeyote ambaye atakuwa tayari kuzaa na wewe Lina halafu mimi nitalea mtoto huyo!” alisema Phillip akilengwalengwa na machozi.
Ilikuwa ni kauli ngumu sana kuitamka mdomoni hasa kwa mwanaume aliyempenda mke wake kupita maelezo, lakini haikukwepeka kwa sababu walihitaji mtoto ndani ya nyumba ambaye angekuwa mrithi wa mali zote walizokuwa nazo.

Lina akamwangalia Phillip kwa muda, hakuwa tayari kuamini kauli aliyoisikia mdomoni mwa Phillip, kwani katika muda wote walioishi pamoja ndani ya nyumba Phillip alionyesha kumpenda na mara kadhaa akimwomba kuwa mwaminifu katika mapenzi yao.
“Phillip!” Lina aliita.

“Yes honey” (ndiyo mpenzi) aliitikia Phillip huku macho yake yakimwangalia Lina kwa huruma.
“Unamaanisha unachosema?”
“Hakika, wala sina utani juu ya hilo.”

“Ni kwa nini umefikia hapo, hivi kweli unanipenda?”
“Nakupenda kupita maelezo wewe mwenyewe unafahamu.”
“Sasa?”
“Nataka kuitwa baba.”

“Phillip hutaumia kugundua kwamba mkeo unayempenda kwa dhati amekutana na mwanaume mwingine kisha kupata ujauzito?”
“Nimekaa na kufikiria kwa muda mrefu si kwamba sitaumia, ninachohitaji ni wewe kufanya kila unachoweza upate ujauzito halafu mimi nitautunza mpaka utakapojifungua mke wangu.”
“Phillip kumbe hunipendi,” alisema Lina akibubujikwa na machozi.

Phillip akanyanyuka kitini na kusogea karibu kabisa na kiti alichoketi Lina kisha kumkumbatia wote kwa pamoja wakaanza kulia.
“Uamuzi wangu si mbaya, ninachohitaji wewe uwe na furaha mke wangu matatizo yangu mimi yasikufanye ukakosa kuitwa mama maishani mwako,” aliongea huku akimpigapiga Lina mgongoni.

“Phillip hivi utajisikiaje kuona mimi ni mjamzito halafu si wa kwako?”
“Kwa sababu nimetoa idhini mimi mwenyewe sitaumia, ninachotaka ni wewe uitwe mama na mimi baba basi.”
“Ni ngumu Phillip, mimi siwezi kulisaliti penzi letu acha tubaki hivihivi bila mtoto naamini Mungu alikuwa na makusudi juu ya hilo.”

“Unasema?” aliuliza Phillip akinyanyuka kitini, alikuwa hatanii bali alimaanisha alichokuwa akikisema. Haja ya moyo wake ilikuwa ni kuitwa baba bila kujali ni wapi mtoto huyo angepatikana.
“Phillip.” Lina akaita huku akijaribu kumfuata.
“Lina nataka mtoto!”

“Phillip haiwezekani mimi siko tayari kusaliti penzi letu.”
“Unanipenda?” Phillip aliuliza kwa kujiamini.
“Nakupenda sana mume wangu.”
“Basi nataka mtoto!” aliongea Phillip huku akitembea kuondoka eneo hilo.

“Mungu wangu! Ni papa?”alijiuliza huku akinyanyua taa yake ndogo na kumulika eneo hilo huku akitetemeka kwa hofu.
Akayatoa macho yake yote kuangalia mbele lakini kwa sababu ya mwanga mdogo uliokuwepo hakuweza kuona vyema. Woga ukazidi kumwingia na wazo pekee lililomjia kichwani kwa wakati ule lilikuwa ni kugeuza mtumbwi wake haraka na kurejea alikotoka, jambo ambalo hakuwa na uhakika nalo kama lingesaidia kuokoa maisha yake.

Akiwa hapo alishuhudia mtumbwi wake ukiyumbishwa huku na kule, akajua tayari amejiingiza kwenye hatari.
“Leo ninakufa huku nikijiona,” alisema Oleg Malenko huku machozi yakimbubujika kwa wingi mashavuni. Hofu kuu ilikuwa imemkumba na hakuna alichokuwa anakisubiri zaidi ya kifo, tena cha kuliwa na papa.

Aliifanya kazi ya uvuvi kwa kipindi kirefu lakini hata siku moja hakuwahi kukutana na dhahama kama ile. Zaidi alifanya kusimuliwa na wavuvi wenzake kwamba watu wengi hufa baharini, hasa wavuvi baada ya mitubwi yao kuvamiwa na kupinduliwa na samaki wakubwa.

Kwa Oleg Malenko siku hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kushuhudia tukio hilo, akaamini kabisa kwamba kifo kilikuwa kimemkaribia. Taswira za mke na watoto wake zikawa zinapita kwa kasi kichwani mwake kama filamu ya kusisimua, machozi ya uchungu yakawa yanamtoka.

Akiwa katika mawazo hayo, haraka alipata wazo la kupiga kasia kwa nguvu na kugeuza mtubwi wake kwa kasi kurejea upande aliokuwa mara ya kwanza lakini tayari alishachelewa, akahisi mtumbwi ukivutwa kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu.
“Nakufaa! Nakufaa!” alisema kwa lugha ya Kirusi akiomba msaada.

***
Muda mfupi baada ya kuzamishwa baharini akiwa amefungwa jiwe kubwa mwilini mwake ili asipate nafasi ya kujiokoa kwa lengo la kupoteza ushahidi, Ditrov alirejewa na fahamu baada ya kupigwa na baridi kali. Alijaribu kufurukuta kwa kupiga mbizi ili kujiokoa lakini hakufanikiwa.

Alipotumia nguvu za ziada alizokuwa nazo mwilini mwake, bado aliendelea kutapatapa na sasa akawa anavutwa kuelekea chini ya bahari na lile jiwe kubwa alilokuwa amefunganishwa mwilini. Akiwa katikati ya hali ya kupoteza fahamu na uzima, alikumbuka picha ya tukio zima lililotokea ofisini kwa bosi wake, Victor Fedorov hadi wakati ule. Alikumbuka jinsi alivyofyatuliwa risasi bila huruma ambazo zilipenya kwenye mwili wake na kumsababishia maumivu makali.

Akiwa katika hali hiyo kwa takribani dakika kumi nzima, aliendelea kujivuta huku na kule ndani ya maji ili kujiokoa lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu kwake. Akawa anazidi kuzama! Ditrov alizidiwa nguvu na maji, akaanza kukata tamaa lakini upande mwingine wa akili yake alikuwa na matumaini makubwa ya kusalimika na kifo.
“Ma…ji!” alitamka kwa tabu akiwa bado anatapatapa, moyoni akasikia sauti ikimwambia kuwa hapaswi kukata tama kwani kufanya hivyo kungemaanisha kifo chake.

“Sitaki ku…fa!” akatamka tena kwa tabu.
Hali yake ilizidi kuwa mbaya, uwezekano wa kutoka baharini akiwa salama ukazidi kupungua kutokana na maumivu aliyokuwa anayahisi baada ya risasi kuupenya mwili wake na kusababisha atokwe na damu nyingi. Pamoja na kuwa jabali, Ditrov hakuwa na uhakika kama angesalimika lakini bado hakukata tamaa.

Ghafla akiwa katika hali ya kukata tama, alikumbuka kitu. Wakati anaingia ofisini kwa Victor Fedorov, ndani ya mfuko mmoja katika suruali yake alikuwa na kisu kidogo cha kukunja, akaamini huenda kingemsaidia kuokoa uhai wake.
Kwa nguvu zake zote alijitahidi kuingiza mkono mfukoni lakini hakufanikiwa, akajaribu tena upande mwingine wa suruali yake na kukumbana na maumivu makali.

Licha ya maumivu hayo alijaribu tena kuusogeza mkono wake zaidi mpaka akaufikia mfuko wa suruali, kwa taabu kubwa akafanikiwa kugusa kitu kigumu na kuamini kwamba kilikuwa chenyewe.
Akiwa katika hali ya kutapatapa akafanikiwa kuupenyeza mkono mfukoni na kuchomoa kisu, kwa taabu kubwa akakishika vyema na kujaribu kuikata kamba ili ajinusuru na umauti uliokuwa ukiinyemelea roho yake.

Hakuwa tayari kukutana na kifo. Ni kweli alifahamu wazi kwamba kila binadamu angeonja mauti lakini hakuwa tayari kufa kikatili kiasi hicho.
“Nitajaribu mpaka mwisho, ikishindikana basi,”aliwaza akilini mwake.
Kwa nguvu kidogo alizokuwa nazo alikishika vyema kisu kidogo alichokuwa nacho mkononi, licha ya maumivu makali aliyokuwa nayo upande wake wa kulia, aliikamata vyema kamba aliyokuwa amefungwa shingoni na kuanza kuikata.

“Krii!Krii!Krii!” aliendelea kusugua kisu katika kamba ili ikatike na kumwacha huru. Kwa takribani dakika tano nzima aliendelea kung’ang’ana na kisu lakini zoezi hilo lilionekana kumshinda. Akaanza kuhisi fahamu zikipotea na nguvu kidogo alizobakiwa nazo zikamwishia. Licha ya hayo yote, bado hakuchoka, alitaka kuendelea kujaribu.

***
“Ngrii!Ngrii!Ngri” Ulikuwa ni mlio wa simu ndani ya nyumba ya Victor Fedorov. Aliinuka taratibu huku akitetemeka na kuisogelea simu hiyo ili aipokee akiwa haelewi ni nani alikuwa akipiga.
“Ndiyo,” akajibu huku akitetemeka.
“Muda unazidi kuyoyoma! Ninachohitaji kutoka kwako ni kiasi cha dola milioni 290 ili niweze kuwaachia watoto wako. Ningependa fedha hizo nizipate ndani ya Msitu wa Beloomut, kusini mwa Jiji la Moscow kwa usalama zaidi.

“Msitu wa Beloomut?” aliuliza lakini kabla hajapata jibu kutoka upande wa pili wa simu, alisikia sauti za watoto wake wakimwita.
“Daaaady!” (Babaaaa!) kilio kikali kilifuatia nyuma yake, Fedorov akazidi kuchanganyikiwa akili.

Je, nini kitaendelea? Victor Fedorov atakuwa tayari kutoa kiasi hicho cha fedha ili kuwakomboa watoto wake? Ni kwa nini muuaji ametaka fedha hizo zipelekwe kwenye Msitu wa Beloomut?
ITAENDELEA,
 
SEHEMU YA 30


HALI yake ilikuwa mbaya hakuwa na uwezo wa kutoka baharini akiwa salama, risasi zilizoupenya mwili wake zilifanya amwage damu nyingi. Pamoja na kuwa jabali, Ditrov hakuwa na uhakika kama angesalimika.
Ghafla akiwa katika hali ya kukata tamaa akakumbuka kitu wakati anaingia ofisini kwa Victor Fedorov, mfuko mmoja katika suruali yake alikuwa na kisu kidogo cha kukunja akaamini huenda kisu hicho kingemsaidia kwa asilimia zote.

Kwa nguvu zake zote akajitahidi kuingiza mkono mfukoni lakini hakufanikiwa akajaribu tena upande mwingine wa suruali yake na kukumbana na maumivu makali lakini pamoja na maumivu hayo akajaribu kuusogeza mkono wake zaidi mpaka kuufikia mfuko wa suruali. Kwa taabu kubwa akafanikiwa kukuta kitu kigumu na kuamini kwamba kilikuwa chenyewe.

Akiwa katika hali ya kutapatapa akafanikiwa kuupenyeza mkono mfukoni na kukichomoa kisu kwa taabu kubwa, akakishika vyema na kujaribu kuikata kamba ili ajinusuru na umauti uliokuwa ukiinyemelea roho yake.
Hakuwa tayari kukutana na kifo, ni kweli alifahamu wazi kwamba kila binadamu angeonja mauti lakini hakuwa tayari kufa kwa ukatili kiasi hicho, hivyo alitaka kujiokoa.

Upande mwingine wa hadithi hii tunamwona Victor Fedorov na sharti alilopewa la kuzipeleka fedha hizo kwenye msitu wa Beloomut. Je, atafanikiwa kuzifikisha na kuwapata watoto wake? SONGA NAYO…

“Tafuta mwanaume yeyote ambaye atakuwa tayari kuzaa na wewe Lina halafu mimi nitalea mtoto huyo,” maneno hayo yalijirudia kichwani mwa Lina.
Hali ya hewa ikabadilika ghafla furaha yote iliyokuwepo ndani ya nyumba ikapotea, Phillip akiwaza jambo moja tu mtoto, hata Lina alipojaribu kumpa ushauri bado hakusikiliza.

“Phillip mimi siko tayari,” alisema Lina.
“Unamaanisha nini?”
“Siko tayari kusaliti penzi letu sababu kubwa ikiwa ni mtoto.”
“Mimi ndiyo mumeo nimeshasema tafadhali fanyia kazi maneno yangu.”

“Hapana, kwa hilo nimekataa.”
“Lina unanipenda kweli?”
“Asilimia mia moja.”
“Basi fanya ninachotaka.”

Lina hakujibu kitu akainamisha kichwa chake chini huku kwikwi ya kulia ikimkaba, hakuwa tayari kukubaliana na maneno ya mumewe, kwake yeye mapenzi yangekuwepo tu hata bila kupata mtoto. Ni kweli yeye binafsi alikuwa mzima, tatizo lilikuwa kwa mume wake lakini tangu mwanzo alishakubaliana nalo.
Akiwa katika mawazo hayo akamshuhudia Phillip akitoka sebuleni na kuelekea chumbani huko hakuchukua muda mrefu sana akamwona tena akitoka mkononi akiwa na funguo za gari.

“Phillip!” Lina aliita lakini hakuitikiwa badala yake akashuhudia macho makali ya Phillip yakimwangalia, yalionyesha dalili zote kwamba alikuwa na hasira kali. Akamshuhudia akifungua mlango na kutoka nje bila kusema neno lolote.
Uchungu wa ajabu ukaugubika moyo wa Lina, hakuwahi kushuhudia katika kipindi chote cha miaka minne alichoishi na Phillip kama mke na mume kwamba siku moja ingegeuka na kuwa shubiri.

Machozi ya uchungu yakamtiririka mashavuni mwake.
“Mtoto! Mtoto analeta matatizo katika penzi letu,” alisema Lina akinyanyuka kitini kuelekea nje huko nako akamshuhudia Phillip akiwasha gari na kutokomea kwenda sehemu ambayo haikujulikana.

***
Msitu wa Beloomut ulikuwa ni wa hatari sana, kila mtu nchini Urusi aliuogopa, wengi wakaupachika jina la msitu wa ajabu kwa matukio mbalimbali ya kutisha yaliyowahi kutokea ndani yake.
Iliaminika kwamba mpaka wakati huo zaidi ya Warusi elfu moja walishakufa baada ya kuingia ndani ya msitu huo na wengi wao miili yao haikuonekana kabisa. Ni matukio hayo ya kutisha ndiyo yaliyosababisha serikali ya nchi hiyo kuingilia kati na kuutangaza msitu huo kwamba ulikuwa tishio na watu kupewa onyo kwamba asitokee mtu yeyote kwenda eneo hilo.

“Msitu wa Beloomut?” lilikuwa ni swali likipita kichwani mwa Victor Fedorov, pamoja na kuwa mwanaume wa shoka, jina hilo lilimtia wasiwasi, akavuta kumbukumbu zake mara kadhaa juu ya matukio mabaya yaliyowahi kutokea katika msitu huo, akaangua kilio.

Kwa Victor Fedorov kiasi cha fedha alichotakiwa kukipeleka kwenye msitu huo hakikuwa tatizo, utajiri wake ulitisha lakini kitu kimoja tu kilimsumbua akilini mwake, ni majanga mengi juu ya msitu huo, hakuwa tayari kwenda kufa lakini aliwahitaji sana watoto wake na ili awapate ni lazima apeleke fedha hizo sehemu aliyoelekezwa.

“Niko tayari kutoa kiasi hicho cha fedha lakini je, nitanusurika? Watoto wangu watakuwa hai?” bado aliendelea kujiuliza kichwani mwake. Pamoja na maswali yote hayo bado taswira za Merina na Mariya ziliendelea kuzunguka ndani ya akili yake, hakuwa tayari kuwapoteza, hao ndiyo ndugu pekee aliokuwa nao.

“Nitafanya kila ninachoweza kuwakomboa watoto wangu hata ikitokea mimi mwenyewe nikafa lakini wao wapone,” aliwaza.
Akili yake ikaonekana kusimama, kwa mara ya kwanza akamkumbuka Ditrov, kwa wakati huo alionekana kuwa ni mtu muhimu sana kwake, aliamini kabisa kwamba mtu huyo angekuwepo maishani mwake kila kitu kingekwenda kama alivyotaka kwani fedha zilikuwa kila kitu katika maisha yake.

“Sitaki kujutia kifo cha Ditrov, nitapambana kiume,” alisema kwa sauti ya kunong’ona.
Akiwa na hofu, taratibu alianza kutembea kuelekea chumbani ambako alifungua mlango na kuingia ndani akanyoosha moja kwa moja mpaka kwenye moja ya makabati makubwa na kufungua. Pamoja na utajiri wote aliokuwa nao, Victor Fedorov aliweka kiasi kikubwa cha fedha ndani ya nyumba ili kukwepa usumbufu wa kwenda benki mara kwa mara.

Huku machozi yakimbubujika, akanyoosha mkono na kuvuta moja ya mifuko iliyoonekana ndani ya kabati hilo na kuutoa nje, fedha nyingi zikaonekana na bila kupoteza muda akaanza kuchukua bunda moja moja na kuyahesabu.
“Nitafanya kila kinachowezekana kuwapata watoto wangu hata akitaka nusu ya utajiri wangu nitampa lakini …” hakumalizia sentensi hiyo mara mlio wa simu ndani ya nyumba yake ukasikika.

***
Kwa muda wa saa nne mfululizo Lina aliendelea kumsubiri Phillip lakini hakuonekana, hata alipopiga simu yake ya mkononi haikupatikana. Lina akachanganyikiwa, hakuelewa ni wapi alikuwa na kitu gani kilimpata kwani hali aliyoondoka nayo nyumbani siku hiyo haikuwa ya kawaida.
“Mungu nisaidie arejee nyumbani akiwa mzima, nitaendelea kusubiri kama saa moja mbele asipotokea nitakwenda kutoa taarifa polisi, pengine amejinyo…” alisema Lina na sentensi yake kukatizwa na honi ya gari nje ya lango la nyumba yao iliposikika.

Haraka akasimama kitini ili achungulie nje, akamshuhudia mlinzi akilisogelea lango lakini badala ya kufungua akachungulia, hofu ikazidi kumwingia.
“Ngoja niende mwenyewe,” alijisemea Lina akitembea kutoka nje kuelekea langoni na bila kusema chochote akauliza swali moja tu kwa mlinzi huyo.

“Ni Phillip?”
“Hapana ni mgeni tu.””Mgeni? Hebu nimwone,” alisema naye pia akachungulia.
Ilikuwa ni sura ngeni kabisa kati yao, alipoliangalia gari pia hakulifahamu, taratibu akasogea na kumsabahi kijana aliyesimama nje ya gari.

“Ndiyo kaka nikusaidie?”
“Samahani sijui hapa ndiyo kwa Phillip?”
“Ndiyo!”alijibu Lina akionekana mwenye wasiwasi mwingi.
“Amenituma barua hii hapa,” alisema kijana huyo akinyoosha mkono kumwelekea Lina ili amkabidhi bahasha ndogo iliyokuwa mikononi mwake.
HUKU akitetemeka aliunyoosha mkono na kupokea barua hiyo macho yake yote yakimwangalia kijana aliyemkabidhi, alitaka kumsoma vyema na kumwelewa alitoka wapi na alitumwa na nani.
“Ahsante kaka sijui naweza kukuuliza jambo?”
“Uliza tu dada yangu.”

“Naweza kufahamu barua hii imetoka wapi na kwa nani?”
“Mh, kwa kweli sifahamu mimi nimetumwa tu kuileta hapa.”
“Uliambiwa umpe nani?”
“Mke wake Phillip?”

Tayari mashavu ya Lina yalishajaa machozi, kichwani mwake alielewa kabisa kwamba barua hiyo ilitoka kwa Phillip hivyo alitaka kuthibitisha jambo hilo.
Baada ya maongezi hayo kijana huyo aliingia ndani ya gari lake na kuliwasha kisha kuondoka.
Taratibu huku mapigo ya moyo yakimwenda mbio, Lina alijikaza na kutembea kuingia ndani lakini hakufika mbali sana akaketi chini. Haraka akaanza kuchana bahasha ili asome barua iliyokuwa ndani.

Mke wangu mpendwa,Kwanza kabisa amini kwamba ninakupenda kwa dhati Mungu ni shahidi juu ya hili, nimeamua kuondoka hapo nyumbani kutokana na hasira iliyokuwa ndani yangu. Lengo langu kwako si baya ni zuri, sihitaji kitu kingine kutoka kwako zaidi ya mtoto, napenda unizalie mtoto mmoja tu nami niitwe baba. Jambo nililokueleza mwanzo sikukosea, nilitamka nikiwa na akili zangu timamu. Lina naamini unanipenda ndiyo maana ukaamua kunipokea mimi na matatizo yangu yote. Tafadhali fanya kila unachoweza ili lengo letu litimie.

Najua itakuwia vigumu kuamini maneno yangu lakini kipande hiki cha barua ni ushahidi tosha kwamba siwezi kukuruka hata kitokee nini, nakupenda mke wangu.
Ni kweli inauma sana lakini hakuna jinsi fanya unavyoweza tafuta mwanaume ambaye wewe mwenyewe utamridhia na uhakikishe unapata ujauzito wake, mimi binafsi sihitaji kumfahamu hata kidogo ninachohitaji ni wewe kupata ujauzito basi.

Najua kichwani mwako utakuwa na maswali mengi ambayo hayatapata majibu lakini huo ndiyo uamuzi wangu, Lina uvumilivu umefikia mwisho. Tafadhali mke wangu niamini niko tayari tena kwa moyo mkunjufu, nahitaji mtoto.
Kama utakuwa tayari kukubaliana na jambo hili na mimi mumeo, basi nipigie simu na kunijulisha nami nitakuwa tayari kurejea nyumbani tuendelee kuishi kama awali.

Sisi wewe tu unayelia machozi hata mimi mwenyewe nakiri kutoka ndani ya moyo wangu huku nilipo sina raha hata kidogo akili yangu yote ikiwa kwako mke wangu mpenzi.
Tafadhali chukua hatua fanya maamuzi sahihi kisha utanijulisha.
Nakupenda.
Ilimaliza barua hiyo.

Kwikwi ya kulia ikamkaba Lina, hakuwa tayari kuamini maneno yaliyokuwa ndani ya barua hiyo, taswira ya Phillip ikamjia kichwani mwake mfululizo, siku zote aliamini kwamba Phillip alikuwa ni mwanaume wa maisha yake lakini sasa kulikuwa na dalili zote kwamba penzi lao lilikuwa likielekea mwisho.
“Nampenda sana Phillip lakini kwa hili sipo tayari,” alisema Lina huku akijifuta machozi, haraka akanyanyuka na kukimbilia ndani.

Ulikuwa ni mtihani mwingine tena katika maisha yake. Hakuwahi kusikia wala kuona mwanaume aliyeweza kumtoa mkewe kwa mwanaume mwingine ili wafanye tendo la ndoa lengo hasa likiwa ni kupata ujauzito.
“Mh! Phillip hivi amepatwa na nini? Kwangu mimi mtoto si kitu, ninachojali ni mapenzi ya dhati, kwa nini asikubaliane na mimi? Mungu wangu tafadhali okoa jahazi hili lisizame, mimi siko tayari kufanya hivi anavyotaka.” Aliongea Lina machozi yakimbubujika.

Hatimaye usiku ukaingia bila kumwona Phillip akirejea nyumbani hapo ndipo akaamini kwamba mwanaume huyo alikuwa akimaanisha alichokisema.
“Nitamsubiri mpaka asubuhi niangalie kama kweli hatarudi basi nitajua cha kufanya.”
Usiku mzima hakupata hata lepe la usingizi, muda wote akimfikiria Phillip na mtihani aliokuwa amempa. Upande mwingine wa akili yake ulimwambia kwamba huenda mtu huyo alikuwa akimpima imani lakini upande mwingine ulimweleza wazi kwamba Phillip hakutania. Hatimaye mapambazuko yakawadia, Phillip akiwa bado hajarejea nyumbani, akayaamini maneno yake.

Siku nzima Lina alishinda ndani, aliamua kupiga simu kazini kwake na kuwaeleza kwamba siku hiyo asingeweza kudhuhuria kwani alikuwa mgonjwa hivyo alihitaji kupumzika ili kuangalia afya yake. Aliamua kuuficha ukweli kwa kudanganya hivyo ili tu asipate bughudha, huku akiwa na mawazo mengi kichwani mwake Lina bila kula kitu chohote alirejea kitandani kwake na kulala usingizi.

Saa zikazidi kusonga, hatimaye mchana ukaingia, akiwa hapo akapata wazo la kuamua kumpigia mmoja wa marafiki zake ofisini ili aongee naye na kumuuliza kama alishamuona Phillip ofisini siku hiyo. Akaisogelea simu kisha kubonyeza namba kadhaa na kuiweka sikioni.

“Habari?” alisikika akisalimia mtu upande wa pili wa simu ambaye hakuonekana akatulia kidogo na kisha kujibu.
“Oh! Leo naumwa rafiki siko sawa, nauliza jambo moja tu vipi leo umemwona shemejio?” akatulia tena.
“Yupo, basi nilitaka tu kujua kama amekuja maana anaweza kusema amekwenda kazini kumbe kapita kona,” alidanganya kisha wakaagana na simu kukatwa.

“Yaani Phillip! Phillip ananitenda hivi? Ameshindwa kurejea nyumbani lakini ameweza kwenda kazini? Lazima atakuwa na mwanamke sehemu fulani.
Amepata wapi nguo za kuvaa? Kwa inavyoonekana Phillip hatanii anamaanisha anachokisema…lakini mimi siwezi kufanya anavyotaka…mh! Naona penzi letu limefikia mwisho,” aliwaza Lina. Lakini ghafla akarejesha akili yake nyuma na kukumbuka mmoja wa marafiki zake katika ofisi yake alivyokuwa akimsifia Phillip, alionekana kumpenda kama si kumtamani.

“Inawezekana Magreth amenigeuka? Mara kadhaa amekuwa akimsifia sana Phillip, pengine ndiko huko alikokwenda? Hapana nitafanya uchunguzi kwanza.”
Wiki nzima ikakatika bila Phillip kurejea nyumbani, hali hiyo ikazidi kumtia Lina kizungumkuti, ni hapo ndipo alipoamua kumpigia simu Phillip na kumweleza kwamba anamwomba arejee nyumbani ili wafanye mazumgumzo.
“Tafadhali mume wangu naomba urudi nyumbani tuzungumze,” alisema Lina huku akilia.
“Je, umekubaliana na mimi?” aliuliza Phillip.

Kwa muda alikaa kimya akijaribu kutafakari ni jibu gani angempa mume wake ili akubali na kurejea nyumbani, hakuwa na jinsi alimhitaji mno. Huyo ndiye alikuwa mwanaume wa maisha yake, hakika alimpenda Phillip kwa dhati.
“Ni…ko…taya…ri,” alitamka Lina huku akilia.
–naongeza kwajili ya kukosa siku mbili
BAADA tu ya kufanikiwa kuikata kamba na kutumia nguvu kidogo alizokuwa nazo huku damu nyingi zikimwagika sehemu ya bega la kushoto, alijaribu kupiga mbizi, lengo lake likiwa ni kujiokoa, kichwani mwake hakuwa na matumaini yoyote pamoja na kwamba alishapitia mambo mengi ya Kimafia lakini hilo kwake lilionekana kuwa gumu.

Kadiri alivyoendelea kupiga mbizi ndivyo fahamu nazo zilivyozidi kupotea taratibu, nguvu zikaonekana kumwishia, akazama mara ya kwanza na kuibuka juu akijaribu kupunga mikono hewani kuona kama angepata msaada wowote lakini haikuwa hivyo, akazama mara ya pili na kuibuka huku akimeza maji mengi akaanza kukata tamaa ya kuiona dunia akiwa hai.

Ni wimbi hilo ndilo lililotingisha mtumbwi wa Oleg Malenko na kumfanya kuamini kwamba sasa kifo chake kilikuwa kimekaribia kwa kuliwa na samaki mkubwa, kichwani mwake hakuelewa kabisa kwamba alikuwa ni mtu aliyekuwa akitapatapa baharini ili kujiokoa.

“Hapana nitahakikisha najiokoa, sipo tayari kuliwa na samaki hapa baharini,” alisema akiweka vizuri mtumbwi wake lakini ghafla alipotupa macho yake vizuri eneo hilo huku mapigo yake ya moyo yakimwenda mbio, alishuhudia mikono ya mtu ikichomoza kutoka ndani ya maji.

“Mh! Mbona naona mikono?” alijiuliza akimulika eneo hilo kwa taa yake ndogo aliyokuwa akiitumia katika shughuli zake za uvuvi. Macho yake hayakukosea ni kweli alikuwa ni mtu ambaye hakuelewa alikuwa mzima au mfu, kwa macho alionekana tayari alishakufa.
“Inawezekana amekufa lakini nitajuaje? Ni lazima nimguse kwa kasia ili nione pengine anaweza kuwa amezimia tu,” aliwaza.

Ghafla akiwa katika mawazo hayo alishuhudia mtu huyo akizama na kuibuka juu akitapatapa kama mtu aliyekuwa akikata roho kisha kutulia kimya, mwili wake ukaelea juu ya maji. Haraka bila kuchelewa, Oleg, kwa kutumia kasia alilokuwa nalo mkononi mwake, akalikamata vyema na kusogea karibu kabisa na mwili wa mtu huyo ambaye kwa kumwangalia mara moja alionekana kuwa amekufa.

Akiwa na hofu, akamgusa mtu huyo kwa kutumia kasia.
“Uko hai kweli wewe? Masikini wamekuua?” alijiuliza Oleg kwa Kirusi akizidi kumgeuza mtu huyo ambaye bado alionekana kutulia.

***
“Tafadhali mume wangu naomba urudi nyumbani njoo tuzungumze,” alisema Lina huku akilia.
“Je, umekubaliana na mimi?” aliuliza Phillip.
Kwa muda alikaa kimya akijaribu kutafakari ni jibu gani angempa mume wake ili akubali na kurejea nyumbani, hakuwa na jinsi alimhitaji mno, huyo ndiye alikuwa mwanaume wa maisha yake hakika alimpenda Phillip kwa dhati.
“Ni…ko…taya…ri,” alitamka Lina huku akilia.

Akiwa hapo ghafla akasikia simu upande wa pili ikikatwa bila kupewa jibu lolote.
“Amekata simu?” alijiuliza huku akijifuta machozi.
Ulikuwa ni mtihani mgumu kweli kwa Lina lakini alitakiwa kuufanya na kufaulu kama tu alimhitaji Phillip maishani mwake, huku akilia akarejea moja kwa moja na kuketi kwenye kiti, tayari ilishatimu saa kumi na mbili za jioni na mawazo yake yote yakiwa kwa Phillip ambaye mpaka wakati huo hakuelewa kama angerejea nyumbani au la kwani hakuwa ametoa jibu lolote.

“Piii! Piii! Piii!” ilikuwa ni honi nje ya lango la nyumba yao.
“Naomba Mungu awe yeye, niongee naye na kumbembeleza ili anielewe mimi siko tayari kufanya tendo la ndoa nje ya ndoa yetu,” alijisemea Lina.
Mawazo yake hayakukosea ni kweli alikuwa ni Phillip, Lina akanyanyuka kitini na kuusogelea mlango kisha kuufungua akimkaribisha ndani.

“Karibu mume wangu.”
“Mwaa!” lilikuwa ni busu lililotua moja kwa moja usoni mwa Lina kutoka kwa Phillip. Akiwa haamini alichokishuhudia kwa macho yake machozi ya uchungu yakamtoka Lina.
“Tafadhali usilie mke wangu yote haya yanatokea kwa sababu moja tu, mtoto!”
“Phillip, maisha bila mtoto hayaendi?”

“Yatakwenda lakini mtoto ni lazima Lina, sikia nimekuja kwa suala moja tu,” alisema Phillip safari hii akionekana mpole.
“Ndiyo.”
“Lina ninakupa mwezi mmoja tu nipate matokeo ya mjadala wetu vinginevyo utanikosa kabisa katika maisha yako,” alisema Phillip akionyesha umakini wa hali ya juu.
“Phillip hapana, bado nakupenda, nakuhitaji mume wangu.”

“Basi kama hivyo ndivyo fanya ninachotaka.”
“Nitafanya unachokitaka mume wangu lakini na nani?”
“Hilo suala nakuachia wewe mimi nimetoa ruhusa fanya unachoweza Lina wewe ni mwanamke tumia akili zako.”

“Mh!” Lina aliguna tayari Phillip alishanyanyuka kwenye kiti na kumwacha hapo peke yake akatembea kuuelekea mlango wa chumba chao, akaufungua na kuingia ndani. Lina akamwaga machozi, ni kweli alikuwa amefanikiwa kumrejesha Phillip nyumbani lakini hakuwa tayari kukabiliana na mtihani uliokuwa mbele yake kwani alishatumia akili zake zote kumshawishi kuondokana na mawazo hayo lakini ilionekana kushindikana, haja ya Phillip ilikuwa ni mtoto basi.

***
“Nitamuokoa hata kama atakuwa amekufa nitamzika kwa heshima zote, hastahili kuachwa kama mzoga!” alisema Oleg.
Moyo wake uliingia huruma na aliumia zaidi alipomwangalia mtu huyo akielea majini mwili wake ukiwa mtupu bila nguo.
“Ni kwa nini watu wanafanya ukatili wa aina hii? Alikosa nini huyu mpaka kustahili adhabu hii? Mungu nisaidie!” alisema mfululizo, muda wote huo akiendelea kumtingisha mtu huyo kwa kutumia kasia.

Dakika tano nzima aliendelea kumtingisha bila mtu huyo kujigeuza wala kujitingisha hapo ndipo akaamini kwamba tayari alishakufa hivyo kufikia uamuzi wa kumtoa ndani ya maji ili ampeleke ufukweni na huko angetafuta sehemu na kumzika kwa heshima zote.
Huku akitetemeka na jasho jingi kumtoka, Oleg Malenko alijitahidi kwa nguvu zake zote kumtoa mtu huyo ndani ya maji na kumpandisha juu ya mtumbwi wake tayari kwa kurejea nchi kavu. Aliamini akifika huko ndiyo angefahamu ukweli wote kama alikuwa hai au amekufa.

“Kama atakuwa amekufa basi itakuwa ni bahati mbaya, nitamzika,” aliwaza huku akimgusa mtu huyo shingoni mwake. Baada tu ya kumpandisha ndani ya mtumbwi, bila kuchelewa akaugeuza haraka na kuanza kupiga kasia kurejea nchi kavu. Haikumchukua muda, akawa tayari amewasili ufukweni, akaegesha vizuri mtumbwi wake na kushuka, mikononi mwake akiwa amembeba mtu huyo.

Alipohakikisha kwamba tayari ameshayaacha maji kwa umbali mrefu, kwa haraka alimshusha chini na kumlaza, akainama na kuanza kusikiliza mapigo ya moyo. Kwa takribani dakika tatu nzima alikuwa akisikiliza lakini hakusikia kitu, kichwani mwake akaamini kabisa kwamba mtu huyo hakuwa hai.

“Nitachimba shimo pale haraka haraka na kumfukia hapo,” aliongea kwa kunong’ona. Akaangaza macho yake huku na kule kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote eneo lile lakini hakufanikiwa kuona kitu.
“Huu ndiyo muda, nikichelewa tu watu wakaniona watajua mimi ndiye nimemuua kumbe nasaidia tu,” akiwa katika mawazo hayo ghafla alisikia mtu akikohoa mfululizo.
“Khoo!Khoo!Khoooo!” Oleg Malenko alishtuka na kugeuka kuangalia, lakini hakuona mtu, alipogeuka tena upande mwingine sauti ya kikohozi ikasikika, safari hii kwa nguvu.

Haraka akatupa macho yake kumwangalia mwanaume aliyekuwa amelala chini, huyo ndiye aliyekuwa akikohoa mfululizo. Bila kuchelewa akasogea karibu ili asikie vizuri, hakukosea alikuwa ni yeye.
“Mh! Amekohoa? Hajafa huyu, ngoja nimpe huduma ya kwanza niangalie itakuwajea,” alisema huku akimgeuza mtu huyo na kumlaza kifudifudi. Akapiga magoti juu ya mgongo wake na kumkandamiza ili kumsaidia kutoa maji yaliyokuwa tumboni mwake.

Hakukosea, alichokuwa akikifanya kilikuwa ni sawa kabisa. Kwa takribani dakika tatu nzima aliendelea kumkandamiza mgongoni, maji mengi yakawa yanamtoka hadi alipohakikisha maji aliyoyameza mtu huyo yamekwisha. Akamgeuza na kumlaza kiubavu huku akijaribu kuongea naye.
“Wewe ni nani? Umetoka wapi? Imekuwaje ukawa hapa?” aliuliza mfululizo lakini hakupata jibu kutoka kwa mtu huyo ambaye alilala kimya ardhini akitetemeka.

“Tafadhali niambie nini kimekupata?” aliendelea kuuliza huku akimchunguza vyema mtu huyo.
“Di…t…ro…” aliongea kwa shida lakini kabla hajamaliza sentensi yake, Oleg Malenko akashuhudia mtu huyo akirusha mikono na miguu kisha kutulia kimya.
“Mh! Hizi damu zinatoka wapi?” alijiuliza huku akimfunua upande huo. Macho yake yakakutana na jeraha kubwa.
“Hili ni jeraha la risasi ambalo limesababisha kuvuja kwa damu nyingi kiasi hiki, lazima nifanye kitu kuokoa maisha ya mtu huyu,” alisema huku akijaribu kumnyanyua sehemu aliyokuwa amelala.
Wazo pekee likamjia kichwani mwake kwamba ni lazima mtu huyo apate matibabu haraka hospitalini lakini hakujua atampeleka hospitali gani.

Hiyo ilikuwa ni kwa sababu ya machafuko makubwa yaliyoikumba nchi ya Urusi. Aliendelea kujiuliza ni hospitali gani angempeleka mtu huyo na kupokelewa bila maelezo ya kutosha! Akahisi hiyo ingekuwa hatari nyingine kwake. Alihisi anaweza kuingia kwenye kesi ambayo asingeweza kujinasua kama mtu huyo angekuwa amekufa.

“Hapana, sitampeleka hospitali. Nitampeleka nyumbani kwangu, naamini hajafa. Huko nitampa matibabu mpaka apone kabisa, hapo atakuwa tayari kunieleza ukweli wa nini kilichompata,” alisema Oleg Malenko. Tayari mapambazuko yalishaanza kuchomoza.
***
Mapenzi yote yaliyokuwa katikati yao yalionekana kupotea, furaha ndani ya nyumba ikageuka na kuwa shubiri. Phillip akisisitiza jambo moja tu, mtoto! Kwa muda wa wiki nzima, Lina aliendelea kumbembeleza na kumsihi Phillip aachane na jambo lililokuwepo kichwani mwake na badala yake wale na kufurahia maisha.
“Lina, hakika hujaweza kunishauri juu ya hili. Fanya ninachotaka halafu tutaelewana,” alisema Phillip huku akigeuka upande mwingine wa kitanda, akavuta shuka na kujifunika gubigubi. Hata Lina alipojaribu kumuita, bado hakujibu wala kugeuka. Kwa mara nyingine tena moyo wa Lina ukauma kupita kawaida, akanyanyuka kitandani, akafungua mlango wa chumba na kutoka nje huku akilia.


Wakati akitembea kuelekea sebuleni ghafla wazo likamjia kichwani mwake. Akalikumbuka jina Daniel, kijana mtanashati kweli kweli ambaye kwa muda mrefu alikuwa akimfuatilia Lina akimtaka kimapenzi. Mara zote aliambulia majibu ya karaha na pengine yaliyouchoma moyo wake kama mkuki wa moto.


“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa! Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ilhali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip. Naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina, akakisogelea kiti na kuketi juu yake kwa muda. Aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya nyumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.


“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel, najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atakayewe…” alisema lakini kabla hajamaliza sentensi yake, kwikwi ya kulia ikamkaba tena.JE NINI KILIENDELEA
 
SEHEMU YA 31


“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa! Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ilhali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip. Naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina, akakisogelea kiti na kuketi juu yake kwa muda. Aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya nyumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.


“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel, najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atakayewe…” alisema lakini kabla hajamaliza sentensi yake, kwikwi ya kulia ikamkaba tena.

SONGA NAYO
“Daniel! Sijui atakuwa wapi kwa sasa? Na sijui kama bado atakuwa hajaoa? Je, nitaanzia wapi kumweleza kwamba nampenda ili hali nilishamuumiza moyo? Lakini nitajaribu, sipendi kumpoteza Phillip, naamini huyu ndiye mwanaume wa maisha yangu yote,” alisema Lina akakisogelea kiti na kuketi juu yake, kwa muda aliendelea kutafakari juu ya tatizo lililokuwa ndani ya nyumba yake, alitakiwa afanye kitu fulani ili kuinusuru ndoa yake. Tayari mashavu yake yalishalowa kwa machozi.


“Kesho asubuhi nitamtafuta Daniel najua atashangaa lakini sina jinsi, huyu pekee ndiye atawe…” aliwaza lakini kabla hajamaliza sentensi yake kwikwi ya kulia ikamkaba tena.


Hakika hakuelewa maisha yake yangekuwa vipi kama tu asingeweza kukubaliana na Phillip, mumewe, ambaye mpaka wakati huo hawakuwa na maelewano mazuri ndani ya nyumba. Aliendelea kubaki eneo hilo bila kurejea chumbani hapo, kazi ikawa moja tu kulia mpaka usingizi ulipomchukua ambapo alizinduliwa na sauti ya mlango ukifunguliwa na aliponyanyua uso kuangalia alimwona Phillip akitembea kumsogelea.

Bila kusema kitu alimshuhudia akimwinamia na kumbusu kisha kumpigapiga mgongoni.
“Lina!”
“Yes darling!” alijibu huku machozi yakimbubujika, akili yake ikarejea kwenye mazungumzo yote yaliyofanyika jana yake.


“Naamini umeshapata jibu la tatizo linalotusumbua.”
Bila kujibu chochote akiwa hapo akanyanyua uso wake na kumwangalia Phillip machoni.
“Unalia nini?” lilikuwa ni swali kutoka kwa Phillip baada ya kumwangalia vyema Lina usoni aligundua macho yake yalikuwa yamevimba kupita kawaida.


“Hakika huo ndio msimamo wangu mke wangu, ni kweli inauma lakini sina jinsi.”
“Yupo mtu ambaye nimemfikiria jana usiku, huyu nadhani anaweza kunisaidia.”
“Ni vyema ukafanya hivyo mara moja lakini tu awe ni mtu unayemwamini sana na nisingependa afahamu siri iliyoko kati yetu, cha muhimu ni wewe kujiweka sawa ili kupata ujauzito basi mambo mengine tutajua mbele ya safari. Sawa mke wangu?”


“Sa…wa,” alijibu lina huku akilia.
Bila kusema kitu Phillip akanyanyuka kitini kisha kumnyanyua Lina wote wawili wakaingia chumbani ili kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini, lakini mambo hayakuwa hivyo.

Baada tu ya kuingia ndani huku wote wawili wakiwa kimya Phillip alimnyanyua Lina na kumrushia kitandani naye akifuata kwa nyuma bila kuchelewa, akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine kisha akabaki mtupu kama alivyozaliwa.


“Lina nakupenda,” ilikuwa ni sauti ya Phillip ikipita masikioni mwa Lina.
“Una..se…ma..kwe..li?” aliuliza lina kwa sauti ya kutetemeka.

“Asilimia mia moja mke wangu mambo yote haya yanatokea si kwa sababu mimi nakuchukia hapana…” alisema Phillip akilivuta shuka na wote wawili wakajifunika gubigubi.


Kilichofuata baada ya hapo hakiandikiki kwani ilikuwa ni kama vile watu wakiimba mapambio na wengine kuitikia, mara chache sana sauti ya Lina ilisikika lakini ilimezwa na mabusu mfululizo yaliyotoka kinywani mwa Phillip. Saa mbili baadaye wote wawili walikuwa hoi bin taaban jasho jingi likiwatiririka.
“Nimeamua kufanya hivi kwa sababu nataka uamini kwamba ninakupenda kwa dhati na si kitu kingine, sawa?” Phillip alisema.

“Ahsante!” alijibu Lina akimwangalia Phillip kwa jicho la huruma.
“Hebu nieleze ni nani huyo unayemfikiria?” Phillip aliuliza kwa upole.
“Yupo kijana mmoja anaitwa Daniel huyu tulisoma naye huko nyuma na alinipenda sana.”
“Je, unamwamini?”

“Asilimia zote labda itokee tu kwamba ameoa kwa sasa?”
“Hata kama ameoa tunachohitaji sisi ni yeye kukupa mamba, basi, mambo mengine yote atuachie sisi wenyewe.”

“Nipe muda nimtafute kisha nitakujulisha.”
“Ahsante mke wangu sasa naamini kweli unanipenda.”
“Nakupenda pia Phillip, yote haya nafanya ili kulinda penzi letu, sipendi kukupoteza, wewe ni wangu mpaka mwisho.”
“Najua jambo hilo ila kitu kimoja tu nikuombe.”
“Ni nini hicho?”
“Nihakikishie kwamba baada tu ya kufahamu kwamba umepata mimba hutarejea tena kwa Daniel.”
“Siwezi kufanya hivyo Phillip unanifahamu vyema, jambo hili linatokea kwa sababu wewe ndiye umetaka.”
“Basi nakuamini fanya kila unachoweza umpate kisha utanijulisha kila hatua, sawa?”
“Nitafanya hivyo,” alisema Lina na wote wawili wakanyanyuka na kuingia bafuni kuoga ili wajiandae tayari kuelekea kazini.

Dakika tano baadaye tayari wote wawili walishakuwa tayari wakatoka mpaka nje ambako walisalimiana na mlinzi kisha wakaingia ndani ya gari, Phillip akiketi kwenye usukani, safari kuelekea ofisini ikaanza, njiani wakiongea mambo mengi kuhusu maisha na mapenzi yao na furaha ilionekana kurejea tena katika mapenzi yao.

Kutokana na msongamano wa magari siku hiyo walilazimika kutumia saa moja mpaka kufika ofisini kwao, wakafika na kuegesha gari lao kisha kushuka. Phillip akazunguka mpaka sehemu alipokuwa amesimama Lina na kumshika mkono, kwa pamoja wakatembea kuingia ndani ya ofisi. Yalikuwa ni mazoea ya Phillip kumsindikiza Lina mpaka anahakikisha ameingia ndani ya ofisi yake ndipo yeye atoke na kuelekea ofisini kwake.

Taratibu huku wakionyesha nyuso za tabasamu walitembea mpaka kuufikia mlango wa ofisi ya Lina, akafungua ili aingie ndani lakini kabla hajafanya hivyo akavutwa kwa nyuma.
“Darling!” ilikuwa ni sauti ya Phillip.
“Yes.” (Ndiyo.)
“Nimesahau kitu.”
“Kitu gani?”
Bila kusema kitu chochote akamsogelea Lina na kuanza kumbusu mfululizo bila kujali watu waliokuwa wakipita eneo hilo.
“Ahsante…” alisema Lina akitabasamu.
“Tafadhali kumbuka kumtafuta Daniel” alisema Phillip kwa sauti ya kunong’ona.
***
“Vrooom!Vrooom!” ilikuwa ni sauti ya kitu kikiburuzwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Kwa sababu hakutaka jambo hilo ligundulike na mtu mwingine, aliamua kuuficha ukweli huo kwa kumburuza mtu huyo na kwenda kumweka pembezoni mwa mitumbwi mibovu amwache hapo na yeye atembee kurejea mpaka sehemu ambako aliamini angepata usafiri na amchukue tayari kwa kumpelekea nyumbani kwake ambako angefanya kila kilichowezekana kuokoa uhai wa mtu huyo.

“Nikipata tu usafiri na kuongea na dereva anisaidie kumfikisha mtu huyu nyumbani itakuwa safi, nitamlipa kiasi atakachotaka lakini afiche siri hii,” aliwaza Oleg Malenko.

Haraka bila kupoteza muda alipohakikisha kwamba amemweka mtu huyo sehemu salama, alitoka haraka na kuangaza macho yake huku na kule na alipohakikisha kwamba hapakuwa na mtu, akaanza kutembea kuondoka eneo hilo.

“Nitamsaidia mpaka mwisho bila kuchoka kwa kumwangalia, anaonekana ni mtu mwema, naomba Mungu asije kuwa mtu mbaya,” alijisemea akizidi kusonga mbele.

Dakika tano tu tayari alishatokeza barabarani, akaongoza moja kwa moja mpaka mahali ambako teksi zilisimama hapo kungoja wateja, akaisogelea moja na kuanza kuongea na dereva, kwa dakika tatu nzima walifanya mazungumzo na kuonekana kukubaliana, haraka akazunguka upande wa pili na kupanda kisha gari hilo kuondoka eneo hilo.

“Nitakuonyesha sehemu ya kusimama kisha kuomba msaada wako ili tumchukue haraka kumpandisha ndani ya gari.”
“Hakuna shida,” alijibu dereva huyo kwa lugha ya Kirusi.
Haikuchukua muda tayari wakawasili eneo la tukio, Oleg Malenko akawa mtu wa kwanza kushuka ndani ya gari na kuanza kumwongoza mwenzake lakini kabla hawajamfikia, macho yake yalishuhudia jambo ambalo halikuwa la kawaida.
“Mh!” aliguna.
“Tafadhali kumbuka kumtafuta Daniel,” aliongea Phillip kwa sauti ya kunong’ona.
Ni maneno hayo yaliyofanya kumbukumbu za Lina kurejea upya kichwani mwake, moyo wake ukaenda mapigo ya haraka haraka kama vile mtu aliyekuwa akikimbia mbio ndefu.

“Mungu nisaidie kufanya jambo hili.” Alinong’ona akizama ndani ya ofisi yake. Taratibu akakisogelea kiti kikubwa kilichokuwa nyuma ya meza kubwa na kuketi huku jasho likimtiririka.
“Sina namna ni lazima nimtafute Daniel tu ili kulinda penzi langu kwa Phillip.” Aliwaza.
Kwa muda wa dakika tano nzima alikaa kimya akijaribu kutafakari nini cha kufanya lakini bado hakupata jibu na upande mmoja wa akili yake ulimwambia kwamba kama asingethubutu kufanya jambo hilo hakika angemkosa Phillip maisha yake yote.

Akiwa hapo huku machozi yakimbubujika, Lina akavuta moja ya droo iliyokuwa karibu na meza aliyoketi, akaanza kuchambua karatasi moja baada ya nyingine akitafuta mahali ambako aliamini angeweza kupata maelezo ya namna ya kumpata Daniel.
Alipitia karatasi moja baada ya nyingine na kwa bahati nzuri akafanikiwa kupata moja ya barua ambazo Daniel aliwahi kumwandikia miaka mingi.

“Nimeipata.” Aliongea akiichomoa karatasi hiyo na kuishika vyema mikononi mwake ili asome.
Taswira ya Daniel ikamjia kichwani mwake, akamwona jinsi alivyokuwa ni kweli alistahili kuitwa mwanaume wa shoka kwani alikuwa na kila sababu ya kupewa tunu hiyo, alikuwa ni kijana mrefu, rangi yake ya ngozi pia ilivutia na midomo yake ilikuwa minene na zaidi ya yote, Daniel alikuwa na kifua kipana kilichofanya kila mwanamke aliyemwona amtamani kimapenzi. Hakika alisisimua.
“Anazo sifa zote lakini mimi …” Lina aliongea, hata kabla hajamalizia sentensi yake mlango wa ofisi yake ukagongwa.

***
“Mh!” Oleg Malengo aliguna akijaribu kuangaza macho yake huku na kule kama vile alikuwa akiangalia kitu fulani.
“Kuna nini?” Dereva wa teksi naye akauliza akionesha wasiwasi mwingi.
Bila kujibu swali alilokuwa ameulizwa alitembea haraka kusonga mbele hakika alionekana kama mtu aliyekuwa akisaka kitu ambacho hakikuonekana.

“Kimetokea nini? Mbona alikuwa hapa?” Alijiuliza.
Kwa ujasiri mkubwa akasogea mpaka mahali alipokuwa amemwacha mwanaume aliyemwokoa ndani ya maji lakini hakumwona, alichokuwa amekishuhudia kwa macho yake yote mawili ni alama za mburuzo ulioonekana ardhini.
“Ameondoka.” Aliongea.
“Nani?”

“Yule niliyekueleza kwamba nahitaji unisaidie?”
“Lakini si ulisema ana hali mbaya?”
“Ni kweli nashangaa pengine amepata nguvu.”
“Sidhani hebu kumbuka vizuri ni hapa kweli ulipomwacha?”
“Hakika ni hapa alama zake zi hizi hapa.”

“Mh.” Dereva teksi naye akaguna hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea.
Kabla ya Oleg Malenko kwenda kutafuta usafiri alipokuwa akimweka mwanaume huyo vyema eneo aliloamini kuwa ni salama na kuondoka kuelekea barabarani kwa ajili ya kutafuta usafiri jambo la ajabu lilitokea, upepo mkali ukiambatana na ubaridi mkali ulipiga eneo la ufukweni na upepo huo ndiyo uliosababisha mwanaume aliyekuwa katika hali ya kutojitambua aanze kutapatapa kutafuta msaada, hatimaye kujikuta amejiburuza na kuelekea nyuma ya mitubwi mibovu iliyokuwa karibu yake.

“Kama kweli una uhakika basi atakuwepo hapa hapa hebu tufuatilie alama za miburuzo kuangalia ilipoishia.” Aliongea dereva teksi huyo na moja kwa moja wakaanza kuufuatilia miburuzo hiyo.
“Umepita hapa.” Aliongea Oleg Malenko.
Akili ya dereva teksi ilikuwa imefanya kazi sawasawa, ni kweli kabisa alikuwa hawajakosea wazo lake la kufuata miburuzo iliyokuwa ikionekana ardhini lilisaidia na hatua chache tu kutoka mahali waliposimama waliona miguu ya mtu.
“Hii ni miguu ya mtu.”

“Ni kweli, hebu tuone,” Oleg Malenko aliongea.
Haraka haraka bila kuchelewa wakazunguka na kuanza kumwangalia mtu huyo usoni, alikuwa ni yule yule aliyekuwa amemwacha muda mfupi uliopita, akamgeuza na kumlaza chali mdomoni alionekana kutokwa na mapovu mengi.
“Mh! Yuko hai kweli huyo?” Dereva teksi aliuliza.
“Sijui hata mimi nashangaa, nilipomwacha muda mfupi hakuwa hivi alikuwa amepoteza tu fahamu.”

“Sasa amefikaje hapa na ni kitu gani kimempata mpaka kufikia hatua hii?”
“Sina jibu ila nisaidie tu tumwondoe hapa.”
“Kwenda wapi, anaonekana tayari ameshakufa huyu.”
Oleg Malenko akainamna na kumshika mwanaume huyo sehemu ya shingo yake kuangalia kama moyo yake yalikuwa yakipiga au la!
“Bado hajafa nasikia mapigo yake yakipiga lakini kwa mbali.”

“Ushauri wangu ni bora umwache afe tu hapa kwani hakuna mtu atakayegundua.”
“Tafadhali nisaidie hata kama atakufa, basi afie ndani ya nyumba yangu wakati nikijaribu kumsaidia.” Aliongea Oleg Malenko kwa sauti ya upole.
“Sawa nitakusaidia wewe tenga tu fedha yangu.” Aliongea dereva huyo kwa lugha ya Kirusi.

Wote kwa pamoja wakainamna na kumnyanyua mwanaume aliyekuwa amelala chini na kuanza kutembea kuelekea sehemu walipokuwa wameegesha gari hapo wakamlaza tena chini na dereva kufungua mlango kisha wakamwinua na kumweka kwenye kiti cha nyuma, wote wakaingia ndani ya gari na safari kuelekea nyumbani kwa Oleg Malenko ikaanza, njia nzima alikuwa akimfikiria mgonjwa aliyekuwa naye, alitaka apone ili amsimulie ni kitu gani kilichompata.

“Naomba Mungu amsaidie asife, apone.” Aliwaza kichwani mwake gari likizidi kuchanja mbuga.
Baada ya mwendo wa nusu saa walishawasili nyumbani kwa Oleg Malenko, yeye akawa mtu wa kwanza kufungua mlango na kushuka bila kusema kitu akamwomba tena dereva wa gari aliyekuja naye amsaidie kumshusha mgonjwa, haraka wakafanya hivyo na kumwingiza mgonjwa ndani ya nyumba.
“Ahsante sana rafiki.” Aliongea Oleg Malenko akimkabidhi dereva huyo kiasi cha fedha kama malipo yake na kumshukuru.

***
“Ngo!Ngo!Ngo!” Sauti ya mlango ikasikika na kumshtua Lina kutoka katika mawazo aliyokuwa nayo. Haraka bila kuchelewa hata kabla hajaitika akaifungua droo na kuitumbukiza barua hiyo haraka alipohakikisha kwamba alikuwa sawa akamkaribisha mtu aliyekuwa mlangoni.
“Ndiyo karibu.” Aliongea kwa sauti ya upole.

Mlango ukafunguliwa na mwanaume mmoja akaonekana akiingia.
“Oh! Karibu sana bosi.” Aliongea Lina akionyesha tabasamu usoni mwake.
“Natumaini hujambo, nimekuja kwa jambo moja tu hapa.”
“Ndiyo bosi.”
“Ah! Mwezi ujao kutakuwa na safari ya kwenda Ujerumani na itatuhusisha mimi na wewe ni vyema ukawa na ufahamu na jambo hilo.”

Badala ya kujibu Lina akainamisha kichwa chake chini, si kwamba hakuifurahia safari hiyo, la hasha! Kichwa chake kilijaa mawazo mengi juu ya ndoa yake na kitu pekee alichokuwa akikihitaji ni kulinda penzi lake kwa Phillip basi.
“Lina!” Sauti ikasikika.
“Bee”

“Kuna nini kinaendelea kichwani mwako? Hauko sawa kabisa.”
“Hapana bosi niko sawa niko tayari kwa safari hakuna shida.” Alijibu Lina kwa sauti ya chini.
Wakaagana, kisha bosi akafungua mlango na kutoka nje akimwacha Lina ndani ya ofisi peke yake.

Huku akitetemeka taratibu akanyoosha tena mkono wake na kufungua droo ambayo ndani yake ilikuwepo barua iliyokuwa na maelezo yote jinsi ya kumpata Danniel akaichukua na kuanza kubonyeza.
“Ngrii! Ngrii! Ngriii,”Simu ilikuwa ikiita upande wa pili.JE NINI KILENDELEA
 
SEHEMU YA 32


NDANI ya chumba wanaongea mengi juu ya maisha na jinsi walivyokuwa wamepotezana kwa muda mrefu. Daniel anasisitiza kwamba bado anampenda Lina pamoja na mambo yote yaliyotokea maishani mwao. Muda wote huo Lina alikuwa akibubujikwa na machozi, mara kadhaa taswira ya mume wake Phillip ilimjia kichwani mwake na sauti ikamsisitiza juu ya kuhakikisha anafanya tendo la ndoa ili hatimaye apate ujauzito.

Ni mambo hayo ndiyo yaliyomfanya Lina azidi kulia, kitu ambacho kilimshangaza sana Daniel. Alitumia muda mwingi kumbembeleza Lina ili anyamaze lakini ilionekana kuwa ngumu.

Kwa muda wa saa zima walikuwa chumbani, kazi ikiwa moja tu ya kumbembeleza Lina ili anyamaze ndiyo waendelee na mambo mengine. Hata alipopewa chakula alikataa bila kusema sababu, hatimaye Daniel uvumilivu nao unamshinda. Uchu wa kufanya tendo la ndoa na Lina unamkamata, anaona huo ndiyo muda muafaka kwake.

Taratibu bila kusema kitu chochote baada ya kuwa ameshambembeleza kwa muda mrefu, anasogea karibu na Lina kisha anamnyanyua na kumlaza kitandani huku akimpiga mabusu mfululizo.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…

HALI ya Ditrov ilikuwa ikiendelea vyema, akipata kila aina ya msaada kutoka kwa Oleg Malenko. Jeraha lake lilishapata nafuu kubwa na mwili wake ulionekana kurejea katika hali yake ya kawaida. Pamoja na yote hayo bado hakuwa tayari kueleza ukweli kwamba alitokea wapi na ni kitu gani kilisababisha akatoswa baharini.

“Nashukuru Mungu unaendelea vizuri, nadhani sasa tunaweza kuongea kidogo kuhusu wewe,” Oleg Malenko alisema.
“Sipo tayari kueleza chochote, kikubwa ninachokuomba ndugu yangu unitunzie siri ya mimi kuwepo hapa katika nyumba yako. Muda si mrefu nitaondoka ili kukuepushia matatizo.”

“Matatizo yapi?”
“Ni historia ndefu sana kuhusu mkasa ulionipata. Ninachokushukuru sana ni kuokoa maisha yangu.”
“Hakuna shida,” alisema Oleg lakini tayari kichwani mwake alishaweka viulizo ni kwa nini mtu aliyekuwa ndani ya nyumba yake hakutaka kueleza ukweli wa nini kilichompata na zaidi ya yote alitaka jambo hilo lifanywe siri.

Hivyo ndivyo maisha yalivyokwenda, Ditrov akawa ni mtu wa ndani muda wote akihitaji kubaki peke yake, jambo ambalo lilizidi kuitia shaka familia ya Oleg Malenko. Wiki ya kwanza ikakatika, hali yake ikazidi kuwa imara na wiki ya pili ilipofika katikati akaamua kuvunja ukimya. Alimwita Oleg Malenko ili waongee.

“Hivi sasa wewe ni kama ndugu yangu kwani umeokoa maisha yangu. Nakushukuru sana lakini naomba msaada mmoja tu kutoka kwako.”
“Sema tu ndugu yangu nitakusaidia.”
“Nahitaji fedha kidogo kwa ajili ya nauli.”

“Kwenda wapi?”
“Nataka kurejea nyumbani,” alidanganya.
“Hakuna shida, nipo tayari kukusaidia. Sijui unahitaji lini?”
“Ikiwezekana kesho asubuhi ili niondoke hapa,” alisema Ditrov akionesha shaka machoni mwake.

***
“Nakupenda mpenzi wangu, ni muda mrefu nimengoja jambo hili litokee hatimaye leo hii limewadia. Nieleze ni kitu gani kimesababisha unitafute Lina, huu kwangu ni muujiza,” alisema Daniel akizidi kumwagia Lina mabusu mfululizo.
“Mh!” Aliguna huku kwikwi ya kulia ikizidi kumkaba.
“Lina,” Daniel aliita.

“Tafadhali toa ushirikiano, kwa nini unalia?”
“Hakuna kitu, nipo sawa.”
“Si kweli! Kama upo sawa hayo machozi ni ya nini sasa?”
“Una…ju…a nini?”

Daniel akatulia kidogo ili asikilize ni kitu gani Lina alitaka kumweleza.
“Nimefurahi kukutana na wewe Daniel, ni muda mrefu umepita eeh?” Aliuliza Lina akimpigapiga Daniel mgongoni. Mawazo na akili zake zote hazikuwa ndani ya chumba hicho, mara kadhaa taswira ya mumewe Phillip ilimjia kichwani mwake na hiyo ndiyo iliyomfanya abubujikwe na machozi muda wote.

***
Nje ya hoteli, Phillip bado aliendelea kubaki hapo akimsubiri mkewe Lina, mapigo yake ya moyo yalikwenda mbio hakuelewa ni kitu gani kingekuwa kimetokea ndani ya chumba kwani tangu mwanzo Lina alishaonesha dalili kwamba hakupenda kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine isipokuwa yeye tu.

“Atakuwa amefanikiwa, ni muda mrefu tangu aingie huko,” aliwaza Phillip.
Akaendelea kujiambia mwenyewe kwamba kusingekuwa na tatizo lolote, akatupa macho yake kwenye saa yake ya mkononi na kugundua kuwa tayari ilishatimu saa tatu na nusu za usiku. Mpaka wakati huo hakuwa na taarifa yoyote ya Lina.

“Akichelewa zaidi nitampigia simu,” aliwaza Phillip akitoka ndani ya gari na kutembeatembea kulizunguka gari lake. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda kasi kwani hakufikiria kwamba Lina angechukua muda mrefu kiasi kile.

***
Ndani ya chumba, Daniel aliendelea kuongea mambo mengi juu ya maisha yake baada ya kuachana na Lina. Aliweka wazi zaidi na kumweleza kwamba tayari alishaoa na alikuwa na mtoto mmoja lakini akajiapiza kutoka ndani ya moyo wake kwamba alilazimika kuoa kwani umri ulikuwa ukienda. Akamwambia hakuwahi kumpenda mwanamke mwingine kama ilivyotokea kwa Lina.
“Daniel unasema kweli?”

“Huo ndiyo ukweli wangu, hutaniamini lakini…”
“Usiseme hivyo bwana.”
“Lina ukweli nilikupenda na nitaendelea kukupenda maisha yangu yote, hapa nilipo nahisi nipo ndotoni pengine nitaaamka muda si mrefu.”

“Daniel uko na mimi wala si ndoto.”
“Umefikiria nini mpaka kuamua kunitafuta Lina?”
“Maisha yamesababisha hivyo, wahenga walisema milima haikutani lakini binadamu tunakutana, ndiyo kama hivi.”
“Ahsante kwa kunikumbuka na kuniingiza tena ndani ya moyo wako.”

Ukimya wa ajabu ukatokea kati yao, ghafla Daniel akaanza kumpapasa Lina sehemu mbalimbali za mwili wake huku akimpa maneno matamu yaliyoambatana na mabusu.
“Leo sitarudi nyumbani, nitalala hapa na wewe. Nataka nikuoneshe ni jinsi gani ninavyokupenda Lina. Nataka ujue kwamba mimi ndiye Daniel wa ukweli, niambie unataka nifanye nini?” alisema Daniel huku akizidi kumpapasa mwilini.

Tayari hamu ya mapenzi ilishawaingia, kila mmoja alikuwa akihemka, si Daniel wala Lina wote walikuwa taabani.
“I lov..e yo…u ba…by...”(Nakupenda mpenzi) ilikuwa ni sauti nzito ya Daniel ambayo ilipenya na kwenda moja kwa moja kwenye sikio la Lina aliyekuwa amelala kimya bila kusema kitu chochote. Bila kupata kibali chochote kutoka kwa Lina, Daniel akaanza kumvua viatu na kuvitupa chini, taratibu akapanda juu na kuanza kumfungua vishikizo vya blauzi aliyokuwa amevaa.

“Leo ndiyo leo nataka kuweka historia ya mapenzi kwako,” alisema Daniel. Tayari macho yake yalishabadilika rangi na kuwa mekundu.
“Daniel!” Lina aliita.
“Yes baby.”
“Twende taratibu, usiwe na haraka.”

“Nashindwa kuvumilia, nilikusubiri kwa muda mrefu.”
“Hapana,” alisema Lina akijaribu kuitoa mikono ya Daniel kifuani kwake.
“Basi naomba nitoe tu hii halafu...” alisema Daniel tayari alishamaliza vishikizo vyote vya blauzi.

“Oh! My God!”(Oh! Mungu wangu!) alisema kimoyomoyo, hakuwa tayari kuamini alichokishuhudia juu ya kifua cha Lina. Chuchu ndogo zilizosimama vizuri zilizidi kumpagawisha Daniel, akawa anapumua kwa kasi kubwa.


“Mbona anazidi kuchelewa? Au kapatwa na tatizo kubwa? Nahisi hayupo sawa, kwa nini harejei?” Phillip alijiuliza maswali mengi ambayo hayakuwa na majibu. Alikuwa akizungukazunguka pale nje kama mtu aliyepoteza kitu. Mara kwa mara alikuwa akiingia ndani ya gari na kushuka, akiwa haelewi nini anachokitafuta. Akili yake ilikuwa haitulii kabisa.

Wivu na hofu vilikuwa vikimshambulia kwa wakati mmoja. Kuna wakati alihisi huenda Lina amenogewa na penzi alilopewa na mwanaume aliyeenda kukutana naye kiasi cha kujisahau. Akili nyingine ilimtuma kuwa huenda ameamua kuondoka na huyo mwanaume ingawa alishindwa kuelewa wamepitia wapi kwani muda wote yeye alikuwa pale nje.
Hofu nayo haikumuacha, alihisi huenda amekumbana na kitu kibaya ambacho kimemdhuru na ndiyo maana hatoki mapema kama walivyokubaliana.

Mambo yote yalikuwa yakipita akilini mwake kama mkanda wa sinema. Japokuwa ni yeye ndiye aliyetoa wazo lile, kwa upande mwingine alijikuta akijutia uamuzi wake lakini kwa kuwa alikuwa na shida ya mtoto, ilibidi avumilie.

Phillip aliendelea kujizungusha huku na kule huku akiangalia saa yake karibu kila baada ya dakika moja. Aliona muda unaenda taratibu sana, akatamani angekuwa na nguvu za ziada za kuweza kuona kilichokuwa kinaendelea kwa Lina.
“Zikipita dakika kumi kama bado hajatoka, itabidi niende mapokezi kuuliza, ikishindikana nitaenda mpaka kwenye chumba alichoingia,” alisema Phillip huku kichwa chake kikichemka kwa mawazo.

Muda ulizidi kuyoyoma bila Lina kutoka, hali iliyozidi kumuweka Phillip kwenye wakati mgumu. Aliendelea kuhesabu sekunde, dakika na saa hatimaye uvumilivu ukamshinda. Kijasho chembamba kilikuwa kikimtiririka, akafunga mlango wa gari na kuanza kupiga hatua za taratibu kuelekea mapokezi huku akiendelea kujiuliza maswali mengi ambayo yote yalikosa majibu.
***
Baada ya kupata nafuu kwa msaada mkubwa wa Oleg Malenko, Ditrov alijiandaa kuondoka huku mawazo mengi yakipita ndani ya kichwa chake. Mazingira yaliyomfanya akaokolewa na Oleg Malenko yalimfanya atambue kuwa Mungu yupo kwani alishakata tamaa ya kuendelea kuishi. Alikuwa akijiuliza mara kwa mara kwamba alimkosea nini bosi wake, Victor Federov mpaka kufikia hatua ya kumpiga risasi na kwenda kumtosa baharini, tena akiwa amefungwa na jiwe kubwa shingoni.

Kila alipokuwa anakumbuka jinsi alivyonusurika kufa, mwili wote ulikuwa ukimsisimka. Baada ya kuagana na mwenyeji wake pamoja na familia yake, Ditrov alianza safari ya kuondoka ndani ya nyumba ya Oleg Malenko, akiwa haelewi anaelekea wapi. Alitembea taratibu mpaka alipotoka nje, akageuka nyuma na kuwapungia mkono Oleg Malenko na familia yake kwa ishara ya kuwaaga.

Wakamsindikiza kwa macho mpaka alipopotea kwenye upeo wa macho yao. Alikuwa anatembea huku kichwa chake amekiinamisha chini akiwa hataki mtu yeyote amtambue. Alikuwa akikwepa macho ya watu kwani aliamini wengi wao walikuwa wanamfahamu.
“Mimi ni mwanaume bwana! Kama Mungu amenisimamia nimenusurika na mauti, hawezi kushindwa kuniongoza mahali pa kwenda wakati najiandaa kulipa kisasi.

Nitatafuta sehemu yoyote ambapo nitajihifadhi wakati nafikiria jinsi ya kurudi kulipa kisasi, lazima nimfunze adabu Victor Federov. Tena kazi itakuwa rahisi kwani anaamini nimeshakufa, hajui kuwa Mungu ambaye nilishaacha hata kumuabudu miaka mingi iliyopita amenipigania na naendelea kupumua,” alisema Ditrov wakati akizidi kuchanja mbuga kuelekea mahali asikokujua.

Kumbukumbu za kuhuzunisha ziliendelea kuzunguka ndani ya kichwa chake, akajikuta akishindwa kuyazuia machozi kumtoka, hasa alipokumbuka maisha aliyokuwa anaishi kabla ya kutokewa na balaa lile na kuponea chupuchupu kufa.
Taswira ya maisha aliyokuwa anaishi, japokuwa yalikuwa yanategemea kufanya shughuli haramu mara chache, ilikuwa ikipita akilini mwake na kumfanya ashindwe kukubaliana na hali halisi.

Maisha mazuri aliyoishi, tena ya kifahari yalimfanya asiamini kuwa wakati ule alikuwa akitangatanga mahali asipopajua na kuishi kama mkimbizi. Maisha ya kujificha kama digidigi hakuyazoea lakini sasa ndiyo alitakiwa ayaishi wakati anajiandaa kulipa kisasi akikwepa kugundulika kabla hajatimiza alichokipanga.

Alitembea kwa muda mrefu mpaka akaanza kuhisi uchovu. Ukizingatia kuwa afya yake ilikuwa bado haijatengamaa, nguvu zilimwisha kirahisi. Akaamua kutafuta mahali pa kupumzika huku akiendelea kujiuliza kichwani mwake ni wapi angekwenda na kupata fedha za kumsaidia kukimu shida zake mbele ya safari. Alipiga moyo konde na kuamini kuwa hakuna linaloshindikana chini ya jua.

“Najua nitapata shida sana lakini haya yote yatapita. Nitaanzia chini kabisa lakini naamini ipo siku nitapata fedha ambazo zitanifanya nirudi tena kwenye daraja la maisha ya kifahari kama ilivyokuwa mwanzo, nikila na kunywa hadi kusaza,” alijisemea Ditrov wakati akiinuka na kuendelea na safari yake baada ya kupumzika kwa muda.
Kichwani mwake hakuwa na ramani ya mahali anapokwenda lakini aliamini atafika tu mahali palipotulia ambapo ndipo yatakapokuwa makazi yake ya muda wakati akijiandaa kulipa kisasi.

***
“Lina,” Daniel aliita.
“Abee,” aliitikia kwa sauti ya chini.
“Kweli unanipenda?”
“Ndiyo!”

“Kama kweli unanipenda tafadhali niache niwe huru juu ya mwili wako. Naomba unipe nafasi ya mimi kufanya ninachotaka, usinishike mikono na kunizuia, niache nifurahie mapenzi yako,” alisema Daniel kwa sauti ya kubembeleza kuonesha kuwa hamu yake ilikuwa imefika juu kabisa.
Lina hakuwa mwepesi wa kukubali Daniel afanye kila alichokitaka kwenye mwili wake. Mara kwa mara alikuwa akiushika mkono wake na kumzuia kumpapasa maungoni mwake, jambo ambalo lilizidi kumpa Daniel wakati mgumu.

“Yaani shida ya mtoto ndiyo inifanye nifanye jambo nisilolitaka, roho inaniuma sana,” alijisemea kimoyomoyo Lina huku dhamira yake ikigoma kabisa kumruhusu Daniel afaidi penzi lake. Daniel hakukata tamaa, aliendelea kumbembeleza Lina kwa maneno matamu huku akitumia ujanja kuupapasa mwili wake.

Cha ajabu, kwa muda wote huo Lina alikuwa akibubujikwa na machozi kama yupo msibani, jambo lililomfanaya Daniel abaki njia panda. Alijiuliza kwa nini Lina analia kiasi kile wakati ni yeye ndiye aliyempigia simu na wakakubaliana kukutana pale.
“Lina mpenzi wangu, naomba nipe haki yangu tafadhali, nionee huruma mwenzio nateseka,” Daniel alisema kwa sauti iliyokuwa inatetemeka baada ya kuzidiwa na haja ya mwili wake kulifurahia penzi la Lina.

Alipoona hamjibu kitu bali anaendelea kulia, aliinuka kidogo na kujaribu kuivua sketi fupi aliyokuwa ameivaa Lina. Lina alishtuka na kuanza kumzuia, wakawa wanavutana pale kitandani.
“Usitumie nguvu Daniel, niache nitavua mwenyewe,” alijitetea Lina lakini Daniel hakutaka kumuelewa. Akaikamata vizuri na kuivua kwa nguvu, Lina akabakia na nguo ya ndani pekee.

“Duu! Leo sijui itakuwaje, si mchezo,” Daniel alijisemea kimoyomoyo wakati akimuangalia Lina aliyekuwa amebakiwa na ‘kufuli’ nyeupe iliyozidi kupandisha mashetani ya Daniel.
“Nipe nafasi mpenzi wangu, mwenyewe utafurahi,” alisema Daniel huku akipeleka mikono yake kujaribu kulitoa kufuli la Lina.
“Subiri Daniel, nitakupa nafasi lakini usiwe na papara, subiri kidogo,” alijitetea Lina huku akibana miguu yake na kumzuia Daniel.

“Hakuna shida, nitasubiri hata ukisema mpaka usiku wa manane. Nakuhakikishia kuwa shughuli nitakayokupa leo, mwenyewe utanitafuta tena.”

Lina alifumba macho na kumruhusu Daniel apitishe mikono yake kiunoni, akawa anampapasa kimahaba huku akimpiga mabusu mwili mzima. Alipoona Lina amejisahau, alishika pindo za kufuli lake na kuanza kuliteremsha kwa kushtukiza. Lina aliwahi kumzuia, lakini likiwa tayari limeshashuka mpaka karibu na magoti. Daniel aliendelea kusumbuana naye, hatimaye akafanikiwa na wote wakabaki kama walivyoletwa duniani.
Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 33


Lina alifumba macho na kumruhusu Daniel apitishe mikono yake kiunoni, akawa anampapasa kimahaba huku akimpiga mabusu mwili mzima. Alipoona Lina amejisahau, alishika pindo za kufuli lake na kuanza kuliteremsha kwa kushtukiza. Lina aliwahi kumzuia, lakini likiwa tayari limeshashuka mpaka karibu na magoti. Daniel aliendelea kusumbuana naye, hatimaye akafanikiwa na wote wakabaki kama walivyoletwa duniani.
Je, nini kitaendelea?

SONGA NAYO

Uwiii!” Daniel alisema kimoyomoyo, macho yake hayakuwa tayari kuamini kile alichokuwa akikishuhudia mbele ya macho yake, uzuri wa Lina haukuwa na maelezo, akili ya Daniel ikazidi kuchanganyika zaidi aliposhusha macho yake na kuangalia mapaja ya Lina.
“Mungu wangu! Ninaota au?” alijiuliza.

“Huoti Daniel unachokiona ndicho.”
“Lina!”
“Yes.”
“Hakika wewe ni mwanamke mrembo,” aliongea Daniel na tayari mikono yake ilikuwa ikipita huku na kule juu ya mapaja ya Lina huku akihemuka, akimeza mate mfululizo.
Akamnyanyua Lina na kumlaza kifudifudi mikono yake yote miwili ikiendelea kucheza juu ya mwili wake laini.

“Hakika wewe ni mwanamke mtamu.”
“Whaaat?” (Nini?)
“Naaminisha wewe ni mzuri sana.”
“Kama wewe Danny.”

“Sidhani,” alisema akishusha mdomo wake na kuanza kumng’ata ng’ata Lina jambo hilo likazidi kuwasha moto zaidi kwa Lina.
“Mh! Mh! Baby, taratibu usiwe na shaka leo ni siku yako.”
“Nahisi kuchelewa Lina tafadhali nipe.”
“Ah! tucheze kwanza kidogo muda ukifika nitakupa.”
“Shiiii! Mh! Uwiii! Yalaaa!” alilalama Daniel.

Kwa muda wa saa mbili mfululizo waliendelea kucheza juu ya kitanda huku kila mmoja akionekana kukolezwa na mwenzake, mara kadhaa Daniel alimgeuza Lina akijaribu kumlaza chali lakini Lina alikataa akimweleza wazi kwamba muda muafaka ulikuwa bado haujafika.
Kwa kuwaangalia wote wawili walikuwa hoi kwa mapenzi kila mmoja akiguna na kuongea maneno yake huku wakiendelea kushikana hapa na pale.

“Lina inatosha tafadhali ni…pe,” aliongea Daniel lakini hakumaliza sentensi yake tayari mdomo wake ukafunikwa na kiganja cha Lina.
“Shiii! Hebu jikaze bwa....” aliongea Lina lakini naye alionekana kuwa hoi kupita kawaida.
Kwa sauti ya upole huku akionyesha tabasamu akamwomba Daniel naye alale ili aweze kumfanyia alichotaka kufanya, bila hiyana taratibu mwanaume akashuka kitandani na kulala akimpa Lina nafasi ya kufanya alichokusudia
“Mh!Mh!Mhhhhh” ilikuwa ni miguno kutoka kwa Daniel.

“Vipi?” Lina aliuliza.
“Imetosha, naomba unipe ki…do..go,” aliongea.
“Niachie nafasi kidogo nikupe raha Daniel ambayo nina hakika hutaisahau maishani mwako.”
Ulimi wa Lina ulikuwa ukipita ndani ya sikio la Daniel.

Ni tukio hilo ndilo lililofamfanya Daniel akajikunja kitandani kama jogoo, raha aliyokuwa ameisikia ilikuwa haielezeki hata kidogo, ni kweli alishakutana na wanawake wengi maishani mwake lakini kwa Lina ilionekana kuwa kiboko.
“Lina niko tayari kuachana na mke wangu nikuoe wewe, unasemaje?”
“Danny! Hebu acha utani unamaanisha unachokisema?”

“Niko tayari hakika sitanii.”
“Unaweza kumwacha sasa hivi tena kwa kumpigia simu?”
“Haijalishi.”
Daniel alikuwa amechanganyikiwa kabisa, akili zake ziligeuka na alikuwa tayari kufanya kila kitu ambacho Lina angemwambia ili mradi tu aendelee kupata raha aliyokuwa anaipata siku hiyo, kichwani mwake akisahau kabisa kwamba alikuwa ni baba wa watoto wawili waliomtegemea kwa kila kitu duniani.

***
Akiwa ndani ya gari lake usingizini, ubaridi mkali wa kiyoyozi ndiyo uliomshitua na kumfanya afungue macho na kuangaza huku na kule ndani ya gari na kugundua kwamba alikuwa peke yake bado, haraka akanyoosha mkono wake na kuwasha redio ndani ya gari na sauti ikasikika ikitangaza kwamba muda huo ndiyo ilikuwa ikitimu saa sita kamili usiku.

“Mungu wangu mpaka saa hizi? Amepatwa na kitu gani huyu mwanamke?”
aliongea Phillip akishuka ndani ya gari.
Akiwa hapo akaangaza huku na kule bila kuona kitu chochote, taratibu akazima gari na kuchomoa funguo kisha kufunga mlango.

“Lina amenisaliti hawezi kukaa ndani ya hoteli kwa muda mrefu kiasi hicho mkataba wangu mimi na yeye ni kuhakikisha anakutana na mwanaume huyo na kufanya naye tendo la ndoa baada ya hapo basi atoke na tuondoke, kwa nini amechukua muda mrefu kiasi hiki? Inawezekana amepewa mambo mazuri mpaka amenisahau?” aliongea Phillip akionyesha hasira nyingi.

Hofu ilishaugubika moyo wake, akiwa haelewi ni kitu gani angekwenda kushuhudia huko, Phillip alianza kutembea kichwani mwake akijiuliza maswali mengi na mara kadhaa akianza kujilaumu kwa kitendo chake cha kumshawishi mkewe kwenda kukutana na mwanaume mwingine ili tu wafanye tendo la ndoa na kupata ujauzito ambao angeulea na kuutunza mpaka mtoto atakapozaliwa. Moyo wake ukauma.
“Hivi kweli anaweza kuwa ameondoka na kuniacha mimi nikiwa hapa? Lina, sidhani lakini akili za mwanamke anazijua mwenyewe pengine ameamua kufanya kweli ili kunikomoa kwani hakuwa tayari kufanya jambo hilo, mimi ndiye nimemlazimisha.”

Lawama nyingi akazielekeza kwake na kujiona ni mwanaume mjinga kiasi gani kwa kitendo cha kuruhusu mkewe kwenda kufanya ngono na mwanaume mwingine, hakika alifahamu wazi kwamba kama dunia ingefahamu jambo hilo basi ingekuwa ni aibu mpaka siku anaingia kaburini.

Huku akiwa na wasiwasi mwingi moyoni mwake taratibu akaanza kutembea, lengo lake likiwa kuelekea eneo la mapokezi ambako angeingia na kuuliza.
“Najua nitakutana na maswali mengi sana hasa ukizingatia kwamba ni usiku
mkubwa lakini nitajibu moja baada ya jingine nikijifanya mimi ni dereva wake niliyekuwa nikimsubiri hapo nje,” aliendelea kuwaza akitembea taratibu.

Kwa fedha kidogo alizokuwa nazo, akiwa haelewi kabisa nini ingekuwa hatima ya safari yake hiyo, Ditrov alijipa moyo na kujiapiza kwamba ni lazima angefanya kila kinachowezekana kusukuma maisha yake kwenda mbele lakini zaidi ya yote akili yake ilifikiria juu ya kulipa kisasi kwa Victor Fedorov. Alijiapiza kuwa hata kama ingechukua miaka mingapi ni lazima jambo hilo litokee, hakufahamu lingetokea vipi lakini aliamini hivyo.

Hasira ya maisha mapya ilikuwa imemkaa Ditrov kupita maelezo, alitaka kurejea kwenye hali yake ya awali na kuwa Ditrov yuleyule wa zamani, bila mtu yeyote kufahamu kwamba hakufa. Alipanga kujichimbia mahali na kuishi kwa siri kubwa akitafuta mbinu za kulipa kisasi kwa mtu aliyeamini kwamba alikuwa ni adui yake.

“Yupo mtu mmoja tu nchini Urusi anayeweza kufanya kazi ninayotaka afanye. Nikitulia kidogo nitamfuta,” aliwaza siku moja akiwa ndani ya chumba chake kidogo kilichokuwa nje kabisa ya mji.

Kwa muda wa wiki mbili mfululizo aliendelea kutafakari juu ya nani angeweza kufanya zoezi ambalo alilihitaji, hatimaye kumbukumbu zake zikamrejesha moja kwa moja kwa kijana mmoja aliyeishi nchini Urusi ambaye aliamini kabisa kwamba angeweza kufanya kile alichokitaka.

Baada ya kuchunguza kwa muda mrefu, alimkumbuka kijana mmoja katili ambaye aliamini kabisa angeweza kufanya kazi ngumu iliyokuwa mbele yake. Mara kadhaa alikumbuka matukio ya kutisha ambayo aliwahi kufanya kipindi cha nyuma.
“Nitampa kazi hii lakini sitaki afanye mauaji yoyote, kama ni kisasi nitalipa mimi mwenyewe,” aliwaza Ditrov.

Kazi yake ikabaki kuwa moja tu, kutafuta simu ambayo angeitumia kuwasiliana na kijana huyo ili ampe kazi hiyo mara moja.
“Kesho nitahakikisha napata simu kwa ajili ya mawasiliano,” alisema Ditrov akijaribu kuzungusha akili yake huku na kule. Akiwa hapo akaingiza mkono katika moja ya mfuko wake wa suruali akijaribu kukagua kama angepata akiba yoyote ambayo ingeweza kumsaidia kupiga simu.

“Yes, hii itatosha kwa kazi hiyo,” alisema huku akitoka ndani. Nyumba aliyokuwa anaishi ilikuwa ndogo na iliyochakaa kupita kawaida. Hapakuwa na jirani yeyote maeneo hayo na ilivyoonekana, nyumba ile ilikuwa imetelekezwa kwa muda mrefu. Hapo ndipo Ditrov alipoweka makazi yake, akiishi peke yake.

Licha ya mvua kubwa iliyokuwa inanyesha, Ditrov aliamua kutoka ili kwenda kutafuta mahali ambapo angepata simu na kupiga nchini Urusi ili aweze kuongea na mtu ambaye aliamini angemsaidia shida yake. Taratibu akatoka na kuanza kutembea, kichwani mwake akiwaza mambo mengi huku akitupa lawama nyingi kwa Victor Fedorov kwamba bila yeye maisha yake yasingekuwa kama yalivyo. Alipofikiria hivyo, moyo wake ukazidi kumuuma.

“Mimi ni mwanaume, naamini nitashinda hata kama gharama yake itakuwa kubwa kiasi gani, lazima nishinde tu,” alisema huku akitokomea kwenda mbele.
Kwa muda wa saa nzima Ditrov alitembea bila kukutana na mtu yeyote zaidi ya magari machache yaliyoonekana kupita eneo hilo kwa kasi huku baadhi ya watu waliokuwa ndani yake wakimshangaa.

“Mh! Kwa nini watu wananishangaa kiasi hiki, inawezekana eneo hili ni hatari?” alijiuliza huku akisonga mbele. Hatimaye nusu saa baadaye alifanikiwa kufika katika mji mdogo ambao hata hakuufahamu jina lake. Akaona maduka kadhaa, huku akiwa na wasiwasi mkubwa akatembea na kusogea katika moja ya maduka yaliyokuwepo eneo hilo. Bado watu walionekana kumshangaa kwani alionekana kuwa mgeni kwa kila kitu.

“Habari yako?” alimsabahi muuza duka.
“Salama nikusaidie nini?”
“Naweza kupata wapi huduma ya simu hapa?”
“Hata hapa unaweza kuipata,” alijibu mzee aliyekuwepo dukani hapo na bila kusema kitu chochote Ditrov akainamisha kichwa chini kama mtu aliyekuwa anakumbuka kitu fulani, alipoinuka aliomba kalamu na karatasi kisha akaanza kuandika namba kwenye kipande cha karatasi.

”Hii hapa.”
Mzee mwenye duka akanyoosha mkono na kuipokea karatasi hiyo kisha bila kuchelewa akabonyeza namba alizopewa. Haikupita hata sekunde mbili, simu ikasikika ikiita upande wa pili.
“Ngrii!Ngrii!Ngrii!” Haraka akakabidhi mkono wa simu kwa mteja wake.
“Mimi ni Ditrov, sikufa kama watu wengi nchini Urusi wanavyofahamu, nilinusurika na nina kazi moja nzito ambayo nitataka uifanye kwa uaminifu mkubwa. Nakupa muda wa siku tatu tu iwe imekamilika, umenielewa?” Aliongea Ditrov kwa ukali, kitendo kilichofanya watu wote waliokuwepo eneo hilo kupigwa na butwaa.

“Mungu wangu kumbe hukufa? Nini kilitokea mpaka ukawa hai? Dunia nzima inafahamu kwamba wewe na washirika wako wote mlishakufa?” Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza.
“Ni historia ndefu kidogo lakini kwa ufupi nipo hai.”
“Nisikilize vizuri, tena kwa makini usije ukafanya kosa kabisa.”
“Nipo tayari.”

“Nahitaji kupata fedha ndani ya siku tatu, hakikisha unafanikiwa vinginevyo hata wewe maisha yako yatakuwa hatarini,” alisema Ditrov kwa msisitizo.
“Bosi nitazipata wapi? Tafadhali nipe maelekezo ya kufanikisha zoezi hilo.”
“Wewe ni Mafia nz umeshafanya michezo mingi hatari, hilo kwako halitakushinda. Kumbuka nimekuwa bosi wako kwa muda mrefu hivyo nafahamu wazi siri zote na naamini unajua nini cha kufanya.”

“Mh!”
“Kumbuka nahitaji fedha hizo ndani ya siku tatu, nitakupigia simu baada ya siku mbili kujua umefikia wapi, sawa?” alisema Ditrov na alipomaliza alimkabidhi mkono wa simu muuza duka, akatajiwa gharama ya huduma ile na kulipa.

Je, ni nani huyo? Ataweza kufanya kazi aliyoagizwa na bosi wake na kupata fedha zinazohitajika?
 
SEHEMU YA 34


“Nitahakikisha napata ninachokitaka,” aliongea Ditrov akitokomea kuingia mashambani.
Ditrov alikuwa amedhamiria na alitaka kutimiza alichokitamka kutoka mdomoni mwake pamoja na kwamba alifahamu wazi kwamba pengine zoezi hilo lingeweza kutoa hata uhai wa mtu lakini kwake jambo hilo lilionekana kuwa dogo.

Taratibu huku akionekana mwenye wasiwasi mwingi alianza kutembea na kutokomea kuingia zaidi mashambani ambako ndiko hasa kulikuwa na makazi yake, kichwani mwake akimfikiria Victor Fedorov na unyama aliomfanyia, hakika aliapa kumchukia mtu huyo maisha yake yote na aliuahidi moyo wake kufanya kila kilichowezekana mpaka afanikiwe kulipa kisasi hata kama ingechukua miaka mingapi lakini aliamini jambo hilo lingetokea.

Kichwani mwake alidhamiria kabisa kulipa kisasi, lakini bila fedha? Jambo hilo lisingewezakana, alitaka kuwa na fedha hata kama kidogo tu ambazo zingempatia gari, simu na hata wafuasi wachache ambao angewatumia kumwinda mbaya wake huyo kila sehemu mpaka mwisho na hatimaye kumpata.

“Nikifanikiwa nitatoka huku mashambani na kutafuta makazi mazuri kisha kuanza mchakato wa nini cha kufanya,” aliwaza.
Siku ya kwanza ikapita akiwa bado yuko mashambani na chakula chake kikubwa kikawa ni matunda tu na maji kidogo yaliyopatikana eneo hilo.

Hali yake iliendelea kutengemaa kadiri siku zilivyokwenda mbele, mara kadhaa akiikumbuka familia ya Oleg Malenko na kuishukuru kwa msaada wote iliyompatia.
Akauahidi moyo wake siku moja kurudi kulipa fadhila kwa mema aliyotendewa na familia hiyo.

“Ipo siku nitarudi naomba niwakute hai, najua watanidadisi sana lakini nitarudi na kuwapa shukrani zangu, wameokoa maisha yangu wale, sijui isingekuwa Oleg ingekuwaje kwani nilishakata tamaa nikiamini kwamba sasa ninakufa maji na maiti yangu kuliwa na samaki wakubwa baharini, hivyo hakuna mtu ambaye angefahamu nini kilitokea katika maisha yangu,” aliwaza.

Siku ya pili asubuhi Ditrov alitoka tena kuelekea mji mdogo kwa lengo moja tu la kupiga simu kwa mtu aliyekuwa amempa kazi, alitaka kufahamu aliendeleaje na kumkumbusha kwamba ilikuwa imebaki siku moja tu mbele ili kukamilisha mpango mzima na kumtaka asifanye mchezo na suala hilo vinginevyo angekiona cha moto.

Muda wote akitembea hakudiriki hata mara moja kuinua uso wake na kama alifanya hivyo ni mara moja tu na kuendelea na safari yake, hatimaye akafika kwenye mji mdogo sehemu ileile aliyowahi kupiga simu kwa mara ya kwanza na kutoa namba kisha kuomba msaada wa kupigiwa simu.

Sekunde tatu tu baadaye alikuwa katika simu akiongea na mtu upande wa pili huku akionyesha msisitizo na kwa sababu aliongea kwa lugha ya Kirusi hakuwepo mtu eneo hilo aliyeweza kuelewa ni kitu gani aliongea, wengi walimtazama kwa macho na kugundua kwamba alikuwa na tatizo fulani kwani macho yake yalionekana mekundu muda wote alipokuwa akiongea na simu.
“Sikia kwa makini nitakuwepo tena hapa muda kama huu kukupigia ili nikupe maelezo jinsi ya kunipata mara utakapofanikiwa kuchukua huo mzigo, sawa?” aliongea na kuuliza.

“Sitaki uue lakini kama itatokea nitakupa ruhusa ya kujeruhi tu na si vinginevyo, nadhani unanielewa vyema sina mchezo na kazi yangu hasa pale ninapotaka kitu ni lazima nikipate…”aliongea Ditrov huku akitetemeka, alionekana kama mtu aliyekuwa na homa kali.

Haraka akarudisha mkono wa simu huku akiuliza kiasi cha fedha anachodaiwa, bila kuchelewa akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi hicho akalipa na taratibu akaanza kuondoka eneo hilo.
“Mh!” Mtu aliyempa huduma ya simu dukani aliguna, alionekana kumshangaa Ditrov kupita kawaida, kwanza kwa jinsi alivyokuwa na sura yake ilitisha.

Mwili wake mkubwa uliojazia vyema ni jambo lililosababisha kuingiwa na wasiwasi na kuamini kabisa kwamba mtu huyo hakuwa wa kawaida alikuwa na kitu alichokuwa akikitafuta.

“Inawezekana akawa ni jambazi huyu,” aliongea macho yake yakimwangalia Ditrov kwa makini.
“Nimesikia akisema kesho atarejea tena hapa dukani kwa ajili ya kupiga simu nitamwangalia tena na kama nitakuwa sijamwelewa vyema nitatoa taarifa polisi haraka ili waje kumkamata na kwenda kumhoji zaidi.”

***
Ndani ya chumba kila mtu alikuwa hoi kupita maelezo, kila mmoja akionekana kumhitaji mwenzake kwa hali na mali.
Mara kadhaa Daniel alipojaribu kupeleka mkono wake kwa lengo la kushika chuchu za Lina ili azitumbukize mdomoni mwake, jambo hilo lilionekana kuwa gumu kwani Lina alimsukuma pembeni akimtaka kusubiri kwanza.

“Lakini kuna tatizo gani mpenzi wangu mimi nakuhitaji sana.”
“Najua lakini mimi siko tayari bado kidogo.””Unataka nikufanyie nini ili unipe nafasi Lina?”
“Mh! Haya inatosha njoo basi.”

Daniel akasogea karibu zaidi na Lina alipotupa macho yake kumwangalia usoni aligundua jambo fulani, macho yake yalikuwa mekundu kupita maelezo na mwili wake ulionekana kutetemeka.”
“Daniel,” aliita.
“Yes, Lina.”

“Nipe kidogo halafu tupumzike, hali yangu kwa jinsi ilivyo hainiruhusu kuendelea zaidi ya hapa naweza kufa kama si kuzimia.”
“Na wewe una haraka kama nini sijui!”
“Nakuambia ukweli usiponipa naweza kufa muda si mrefu, nipe kidogo,” alibembeleza Daniel akionyesha umakini wa hali ya juu.
Maneno hayo yakapenya moja kwa moja masikioni mwa Lina na kumfanya amwonee huruma Daniel kupita kawaida, kwa sauti ya upole akamnong’oneza Daniel sikioni mwake na kumweleza kwamba sasa alikuwa amekubali kufanya kitu alichokitaka.

“Ahsante Lina, nataka uamini kitu kimoja tu.”
“Kipi hicho?” aliuliza Lina kwa sauti ya mahaba.
“Nakupenda sana mpaka sasa siamini kama umenikubali lakini nitaamini zaidi pale tu utakaporuhusu tukafanya tendo la ndoa.”
Lina alikuwa kimya kitandani bila kujibu chochote huku machozi yakimbubujika, taswira ya mumewe Phillip ilionekana mbele yake ikimhimiza juu ya kukubali kufanya tendo hilo na Daniel.

Ni hali hiyo ndiyo ilimfanya Daniel aamini kwamba sasa Lina alikuwa tayari kwa kila kitu bila kujiuliza mara mbili akamsogeza Lina karibu yake kisha kumlaza vizuri kitandani tayari kwa kazi moja tu kutimiza shughuli moja ya kumpa Lina raha ambayo kamwe hataisahau maishani mwake.
“Lala vizuri basi mpenzi wangu tuanze...” aliongea Daniel kwa sauti ya kukatikakatika.

KWAKE fedha hazikuwa na maana kuliko maisha ya watoto wake, Mariya na Merina ambao walikuwa kwenye hatari kubwa. Akiwa na hofu nyingi baada ya kumaliza kuweka kiasi cha fedha alichotakiwa kwenye begi, Victor Federov alilikamata sawasawa na kuanza kutembea kutoka nje ya chumba kuelekea sebuleni. Alipofika alipitiliza mpaka nje na kuingia ndani ya gari kisha kuliwasha, akiwa tayari kwa safari ya kuelekea Msitu wa Beloomut ambako alitakiwa kupeleka fedha hizo kama masharti ya kukabidhiwa watoto wake wakiwa hai.

“No way out, I have to do this for my daughters,” (Hakuna jinsi, ni lazima nifanye hivi kwa ajili ya wanangu) Aliongea Victor Fedorov akiwa ndani ya gari lake.

Lakini kabla hajaingia ndani yake alikumbuka kitu kimoja muhimu sana kwa wakati huo, bastola ambayo aliamini kabisa ingeweza kumsaidia kama tu angekutana na hatari yoyote katika safari yake, akalitupa begi la fedha ndani ya gari na yeye kutoka mbio kuelekea ndani ambako haikumchukua hata dakika tatu tayari akawa amesharejea na kuingia ndani ya gari tayari kwa safari ndefu.

Moyoni mwake alikuwa na machungu makubwa, muda mwingi machozi yalikuwa yakimbumbujika. Hakuona tena thamani ya tajiri wake.
“This is the worst day in my entire life” (Hii ni siku mbaya zaidi katika maisha yangu yote) alizidi kuwaza Fedorov.

“Piiii! Piiii! Piii!” Ilikuwa ni honi ya gari akipiga kuomba msaada wa kufunguliwa lango na mlinzi ili atoke. Kwa kasi ya ajabu akaliendesha gari mpaka langoni na kabla hajatoka alisimama na kuongea jambo fulani na mlinzi wake kisha akapandisha kioo na kuondoka.

Njia nzima aliliendesha gari akiwa ni mwingi wa mawazo kwanza maisha ya watoto wake na pili uhai wake yeye mwenyewe hakufahamu kabisa mtu aliyekwenda kukutana naye alikuwa vipi na ni kwanini alisisitiza fedha hizo zipelekwe katika msitu wa Beloomut ambao kwa hakika historia yake haikuwa njema.

“Acha niende cha muhimu ni kupata watoto wangu kama ni hizi fedha nitapata tu nyingine…”Aliwaza akizidi kukanyaga mafuta na gari kusonga mbele.

Mbele yake yalikuwa zilikuwa zimebaki saa saba tu ambazo zingefanya kutimia kwa saa ishirini na nne ambazo alikuwa amepewa na mtekaji wa watoto wake hivyo kuchelewa kwake kungesababisha maradha makubwa na hata kusababisha kupoteza maisha ya Merina na Mariya.

Akiwa katika mwendo wa kasi akatupa macho yake kwenye saa yake ya mkono na kugundua kwamba alitakiwa kufanya kila alichoweza kuhakikisha saa hizo zinamkuta akiwa tayari ndani ya msitu wa Beloomut ili kunusuru maisha ya watoto wake. Akaongeza mwendo wa kasi zaidi na kufanya kila aliyekutana naye barabarani kushangaa na pengine kudhani kwamba alikuwa ni mwizi wa gari aliyekuwa ameiba sehemu fulani.

Kwa Victor Federov mwendo ulionekana kuwa mrefu kila alipotupa macho yake kwenye saa yake aligundua muda ulikuwa ukizidi kusonga kama vile kulikuwa na mtu akihimiza kikimbiza saa mawazo mengi yakazidi kuufunika moyo wake akajikuta ameanza kukata tamaa juu ya kuwapata watoto wake wakiwa hai.

“Oh my God, do something for my daughters, they are the only kids I have” (Oh..Mungu wangu, tenda jambo flani kwa wanangu, ni watoto pekee nilionao) alijikuta akitamka maneno hayo kwa nguvu japo hajawahi kukanyaga kanisani wala msikitini katika historia ya maisha yake.

“Kama sitawakuta wakiwa hai hata mimi sitaona sababu ya kuendelea kuishi nitajipiga risasi ili nife.” Aliwaza machozi yakzidui kuuchakaza uso wake.

***
Hasira kali zilikuwa zimempanda kupita maelezo akisahau kabisa kwamba chanzo cha mambo yote hayo ilikuwa ni yeye kumruhusu mkewe kwenda kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine ili tu ashike ujauzito ambao angeulea na kuutunza mpaka mtoto atakapozaliwa.

Phillip alitoka ndani ya gari lake na kufunga mlango nyuma yake bila kujiuliza mara mbili kwamba kitendo alichotaka kwenda kufanya ndani ya hoteli hiyo kilikuwa cha aibu kuwa alitembea moja kwa moja na kuingia mapokezi.
“Habari yako dada?” Aliuliza kwa sauti ya juu.
“Salama tu nikusaidie?”

“Ah! Mh! Ah!”
“Kaka nakusikiliza nimekuuliza nikusaidie?”
“Ndio.”
“Sijui naweza kufahamu jambo fulani hapa?”

“Unaweza na hiyo ndiyo kazi yangu sema tu.”
“Nauliza…nauliza…”Aliongea akirudiarudia.
“Mh!” Msichana wa mapokezi aliguna yeye pia hakumwelewa Phillip alihitaji nini na kibaya zaidi tayari usiku ulikuwa umeshaingia.

“Taratibu bila kusema kitu chochote huku macho yake yote yakimwangalia kwa makini alinyanyua simu na kupiga namba kadhaa hapo kisha kusikiliza.
“Hallow…ndio…tafadhali naomba ulinzi hapa mapokezi… kuna mtu ameingia hapa hata simuelewi…sijui anataka nini…nimeongea naye simuelewi kabisa…inavyoonena kama vile amechanganyikiwa kidogo…tafadhali njoo mara moja… nina hofu kubwa sana…” Aliongea kwa sauti ya chini lakini bado Phillip aliendelea kusimama eneo hilo bila kusema kitu chochote alionekana kama mtu aliyepigwa na butwaa.

Hazikupita hata sekunde tatu tayari watu wawili walioonekana kuwa walinzi waliingia mikononi mwao wakiwa wameshika bunduki. Kwa haraka wakatembea mpaka sehemu ambako alisimama Phillip na kumsabahi.
“Sijui unahitaji nini ndugu yetu hapa?”
“Mh!”
“Tafadhali ongea vinginevyo tutavunja miguu yako sasa hivi.”

“Kwa kosa gani sasa?”
“Hii si sehemu ya kusimama tu kibaya zaidi ni usiku sasa, unahitaji nini tukusaidie?” Mlinzi mmoja aliongea huku akifoka tayari alishaiweka vyema bunduki kulenga miguu ya Phillip.
“Tafadhali msinidhuru niko hapa kuhitaji msaada mmoja tu.”
“Ndio tunaotaka kukusaidia.”

“Nauliza….nauliza dada mmoja anaitwa…Lina.”
“Lina?”
“Ndio.”
“Hebu niangalie kwenye kitabu cha wageni wangu leo.” Haraka dada wa mapokezi akavuta daftari kubwa na kuanza kufunua ukurasa mmoja baada ya mwingine akiangalia jina hilo.”

“Hatuna jina la mtu huyo leo labda kama ana jina jingine.”
“Hapana anaitwa Lina ndilo jina lake.”
Phillip akabaki mdomo wazi hakuwa na namna nyingine ya kueleza kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo chumbani lilikuwa ni siri kubwa bila kutarajia machozi yakaanza kumbubujika.
“Mungu baba, niondolee kikombe hiki kinazidi kuwa cha moto zaidi” aliwaza Phillip akiwa amejiinamia.

Je, nini kitaendelea? Phillip atakuwa tayari kueleza ukweli ili apate msaada wa kumpata Lina? Nini hatima ya Victor Fedorov na watoto wake kwenye msitu wa Beloomut?
 
SEHEMU YA 35


ILIPOISHIA

“Hatuna jina la mtu huyo leo labda kama ana jina jingine.”
“Hapana anaitwa Lina ndilo jina lake.”
Phillip akabaki mdomo wazi hakuwa na namna nyingine ya kueleza kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo chumbani lilikuwa ni siri kubwa bila kutarajia machozi yakaanza kumbubujika.
“Mungu baba, niondolee kikombe hiki kinazidi kuwa cha moto zaidi” aliwaza Phillip akiwa amejiinamia.

Je, nini kitaendelea? Phillip atakuwa tayari kueleza ukweli ili apate msaada wa kumpata Lina? Nini hatima ya Victor Fedorov na watoto wake kwenye msitu wa Beloomut? SASA ENDELEA

Huku akionekana mwenye wasiwasi mwingi machoni mwake, aliendesha gari mara kadhaa akigeuza shingo yake huku na kule kuangalia usalama kwani alifahamu wazi kwamba sifa za msitu huo nchini Urusi zilitisha kupita maelezo, njia nzima aliendesha gari bila kukutana na mtu yeyote na kwa ilivyoonekana hapakuwepo kiumbe hai kilichoishi ndani ya msitu huo.

Moyoni mwake hakuwa na uhakika kama angeweza kutoka ndani ya msitu huo akiwa salama lakini zaidi ya yote ni watoto wake Mariya na Merina hao ndiyo walikuwa kila kitu na alitaka afanye kila alichoweza kuhakikisha anawapata wakiwa hai.
“Ikitokea nikifa halitakuwa tatizo sana lakini watoto wangu wapone, najua wataweza kuendesha maisha kwa utajiri nilionao, ninashukuru kwamba nimeandika kila kitu kwa wakili wangu…”aliongea.

Victor Fedorov alifanikiwa kuingia ndani ya msitu na kuegesha gari lake sehemu moja iliyoonekana kuwa wazi, hapo akajiweka sawa akiangalia usalama wake, taratibu bila kujiuliza mara mbili akalikamata vyema begi lililokuwa na fedha ndani yake kisha akaichomeka bastola yake kiunoni na kushuka garini.
Akatupa macho yake huku na kule bila kuona kitu chochote, akiwa katika hali hiyo milio ya risasi ikasikika.

“Puuu! Puuu! Puuu!”
“Mungu wangu… hiyo ni milio ya risasi…isijekuwa…” aliongea akijaribu kuzungusha macho yake huku na kule na katika kuangalia vyema macho yake yakakutana na kitu cha ajabu mbele yake, mtu aliyevalia nguo nyeusi na uso wake ukiwa umefunikwa na kuacha sehemu ya macho tu.

Mtu huyo alisimama pembeni kidogo mahali Victor Fedorov alipokuwa ameegesha gari.
“Haaa! Haaa! Haaa” mtu huyo alicheka kwa sauti ya kebehi.
Akitetemeka, akatembea akisogea kuelekea mahali aliposimama mwanaume huyo lakini kabla hajamfikia karibu sauti nyingine ikasikika.
“Victor Fedorov?” mwanaume huyo aliuliza.

“Ndiyo.”
“Vyema umefika muda muafaka kabisa.”
“Watoto wangu wako wapi?”
“Usiwe na haraka watoto wapo lakini nataka kufahamu jambo moja; je umefika hapa na nani?”
“Peke yangu kabisa hakuna mtu…”

“Una uhakika?”
“Asilimia mia moja.”
“Kumbuka kama unaye mtu mwingine kwenye gari lako jambo hilo litamaanisha hatari kubwa pengine kupoteza watoto wote.”
“Ninachokizungumza ni ukweli mtupu, tafadhali chukua fedha hizi hapa kisha unipatie watoto wangu,” aliongea Victor Fedorov machozi yakimbubujika.

Pamoja na ukatili wake wote hapo alikuwa amefunga breki, hakuwa na namna nyingine yoyote ya kufanya zaidi ya kukubali kila alichokuwa ameelezwa ili mradi tu awapate watoto wake Mariya na Merina.
“Daddyyyyy.” (baba.) Sauti hiyo ilipenya moja kwa moja masikioni mwa Victor Fedorov.
Haraka akageuza shingo yake huku na kule kuangalia ni wapi sauti hiyo ilitokea lakini hakufanikiwa kuona kitu chochote, alirudisha macho yake kumwangalia mwanaume aliyekuwa mbele yake.

“Najua wazi huwezi kukosa silaha ni vyema ukaiweka chini haraka.”
Bila kusema kitu chochote akaichomoa bastola yake na kuitupa chini huku akiendelea kumsihi mwanaume huyo kumweleza ni wapi walipokuwa watoto wake.
“Weka pia begi hilo hapo chini na urudi nyuma mita tano!” aliamuru mwanaume huyo.

Taratibu, Victor Fedorov alitii kila alichoelezwa, akaliweka begi chini na kuanza kurudi kinyumenyume, macho yake yote yakimwangalia mwanaume huyo ambaye hakuonekana sura kwani kichwa chake kilifunikwa na kitu kama soksi iliyoacha nafasi ndogo sehemu ya macho tu.

Wasiwasi mwingi ukamfunika na kumfanya ashindwe kuelewa ni kitu gani kingetokea mbele yake baada ya muda mfupi kwani kama ni silaha tayari alishaikabidhi kwa adui aliyekuwa mbele yake.
“Mh!”aliguna huku akiendelea kurudi nyuma akahisi vitu vyepesi vikipenya kutoka ndani ya suruali yake kuelekea chini.

***
Baada ya mhudumu wa mapokezi kusoma kitabu cha wageni kwa muda akitafuta jina la Lina bila mafanikio, aliinua macho yake na kumwangalia Phillip ambaye naye alionekana kulengwalengwa na machozi akimweleza wazi kwamba jina hilo halikuwepo ndani ya kitabu chake labda kama mgeni wake huyo alikuwa na jina jingine alilolitumia.
“Hapana jina lake ni hilo hilo la Lina.”

“Kaka halipo tafadhali niamini na uondoke,” aliongea dada wa mapokezi akitoa ishara kwa walinzi waliokuwepo eneo hilo.
Akiwa katika hali ya kupigwa na butwaa upande mmoja wa akili yake ulimwambia aondoke na kurejea nyumbani huko angeendelea kumsubiri mkewe mpaka atakaporejea lakini upande mwingine wa akili yake ulimwambia atoke nje ya hoteli hiyo na kuingia ndani ya gari lake akae hapo kusubiri mpaka mwisho.

“Mzee nadhani umepata maelezo yanayotosha kabisa kukufanya uelewe, tafadhali tunaomba nafasi hapa.”
Bila kujibu chochote Phillip akainua macho yake na kuwaangalia watu hao, moyo wake ulijaa siri nzito kupindukia lakini hakuwa na uwezo wa kumshirikisha mtu mwingine kwani jambo lililokuwa likifanyika ndani ya hoteli hiyo usiku huo lilikuwa ni siri kubwa.

Machozi yakambubujika, taratibu akaanza kutembea kuelekea nje, moyoni mwake akijilaumu kwa kumtoa mkewe sadaka kwa mwanaume mwingine, akilini mwake akiamini kabisa kwamba Lina alikuwa ameamua kumkimbia.
“Najutia maamuzi yangu haya isingekuwa mimi yote haya yasingetokea, Lina atakuwa ameamua kunitenda kama kisasi,” aliongea Phillip akiukaribia mlango ili atoke nje

“Hapana! Hapana Mariya usife mwanangu bado nakuhitaji amka uungane na mwenzako Merina yule palee,” aliongea mfululizo akizidi kumtingisha Mariya aliyekuwa amelala chini kimya bila kufungua macho wala kujitingisha.
Hali ilionekana kuwa mbaya, Victor Fedorov alizidi kumtingisha mwanaye ili aamke lakini haikuwa hivyo, Mariya alikuwa amelala ardhini kimya kabisa, akatupa macho yake huku na kule kama vile mtu aliyekuwa akitafuta kitu fulani vile, giza nalo lilianza kutanda katika msitu huo.
“Ni lazima niondoke hapa haraka sana kabla giza halijaingia zaidi,” aliwaza akimnyanyua mtoto wake Mariya na kuanza kukimbia kuelekea kwenye gari lake.
Haraka akamketisha na alipohakikisha kila kitu kilikuwa sawa akaingia ndani ya gari na kukaa kwenye usukani huku akiwa na hofu, akawasha na kukanyaga mafuta, lengo likiwa kuondoka eneo hilo.
Akiwa ndani ya gari baada ya kutoka nje ya msitu huo alisimamisha gari na kuanza kumwita tena Mariya ambaye bado alikuwa ametulia kimya.
“Mariya! Mariya! Nini kimekupata mwanangu?” aliuliza.
“Daddy!” Merina aliita huku akitetemeka, yeye pia afya yake haikuwa nzuri, walidhoofika sana, miili yao ilikuwa michafu kupindukia hata nywele zao zilionekana kujisokota.
“Yes, tafadhali nieleze ni kitu gani kimempata nduguyo?” aliuliza hamu yake kubwa ikiwa ni kufahamu tatizo lililotokea huko nyuma kabla hawajafika eneo hilo.
Merina hakujibu kitu chochote, zaidi aliishia kuangua kilio kilichozidi kumtia wasiwasi baba yao akashindwa kuendelea na safari na kuliegesha gari pembeni kwanza ili azungumze na Merina ambaye alionyesha nafuu kidogo kuliko mwenzake Mariya.
“Baba tafadhali endesha gari ukichelewa kidogo tu hata mimi nitakuwa kama Mari…”aliongea Merina na kabla hajamalizia sentensi yake naye pia akatulia kimya kitini.
Victor Fedorov akazidi kuchanganyikiwa zaidi akashindwa afanye kitu gani kwani kila kitu kilichokuwa kikimtokea katika maisha yake kwa wakati huo kilionekana kuwa kama ndoto, alishatoa fedha nyingi ili kuokoa maisha ya watoto wake lakini ni hao sasa waliokuwa katika hali ya kufa kwani wote walionekana kupoteza fahamu, moyo ukamuuma sana akajutia uamuzi wake wa kuwateka watoto hao kutoka nchini Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia yoyote.
“Ubinafsi umeniponza pengine Mungu ananipa pigo hili ili nitubu kwa dhambi niliyoifanya ya kuwateka watoto hawa, lakini si ni uzao wangu huu? Hapana, nasema hapana siko tayari nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu wote kuhakikisha maisha yao yanarejea tena naamini watakuwa hawajafa bali wamezimia tu…” aliwaza huku akizidi kukanyaga mafuta.
Akili yake yote ilishahama na kwenda moja kwa moja kuokoa maisha ya watoto wake, alitaka afike nyumbani haraka na kutafuta daktari ambaye angeweza kufanya kila atakachoweza kuokoa maisha ya watoto hao pacha, hata kama safari hii ingegharimu utajiri wake wote aliokuwa nao, Victor Fedorov alikuwa tayari.
Kwa muda wa saa tatu bado alikuwa barabarani, mara kadhaa akisimama na kuwaangalia watoto wake ili kujua hali zao, bado zilikuwa zilezile hawakuzungumza chochote zaidi ya kutulia kimya vitini.
Saa sita baadaye huku akimwagika jasho mwili mzima tayari alishawasili nje ya lango la nyumba yake, akapiga honi na mara moja lango likaonekana likifunguliwa na gari kuzama ndani, bila kusema kitu chochote na mlinzi wake akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho, akasimama na kushuka haraka garini kisha akafungua milango ya nyuma.
“Mlinzi!”aliita kwa sauti ya juu na mara moja akakimbia na kusimama mbele ya gari lake.
“Tafadhali nisaidie kubeba mtoto mmoja haraka kwenda ndani,” aliamuru tayari mikononi mwake alishambeba Mariya.
Mlinzi hakuchelewa, alimbeba Merina wakaanza kukimbia kuelekea ndani.
***
Huku machozi yakimbubujika, moyoni mwake akiumia, Phillip alianza kutembea kuuelekea mlango wa mapokezi ili atoke nje na kuondoka eneo hilo kama alivyoamriwa.
Walinzi wawili wenye silaha walikuwepo nyuma yake kumsindikiza, wao pia walionyesha kuchukizwa sana na kitendo alichokuwa amekifanya Phillip eneo lao la kazi hivyo hawakuwa na utani walitaka kulinda vyema kibarua chao.
“Tembea haraka bwana tena tunakusihi uondoke eneo hili haraka sana kabla hatujakuchakaza…umesikia bwana mdogo…tembea…” aliongea askari mmoja akimsukuma kwenda mbele. Machozi yakambubujika kwa mara nyingine tena hakuwa tayari kuondoka hotelini hapo na kumwacha mkewe Lina ambaye aliamini kabisa kwamba bado alikuwepo ndani.
Wakati mlinzi wa mwisho anatoka na kufunga mlango nyuma yake sauti kali ikasikika ndani ya hoteli hiyo mwanamke akilia kuomba msaada na kishindo cha mtu akikimbia kuelekea eneo la mapokezi kikasikika.
“Uwiii! Nisaidieni! Tafadhali niokoeni jamani! Anani…”
“Mh!” wote wakaguna.
“Sauti kama ya Lina! Ni sauti ya mk…” aliongea Phillip mfululizo na kushindwa kumalizia sentensi yake, wote wakaonekana wakikimbia mbio kurejea ndani ya hoteli.

Je, nini kitatokea? Sauti iliyosikika ndani ya hoteli Phillip ameitambua kwamba ni ya mkewe Lina, ni kitu gani kimempata huko?
 
SEHEMU YA 36


”Daktari, ni lazima nipate daktari ambaye atakuja hapa kuwaangalia nitamlipa kiasi chochote kile cha fedha ilimradi tu aokoe maisha ya watoto wangu,” aliongea kwa majonzi, na taratibu akanyanyuka na kuisogelea simu lakini kabla hajaifikia alimsikia mlinzi akiguna.

Bila kujiuliza mara mbili akatoka mbio kuelekea eneo hilo, alichokishuhudia hapo kilimtoa machozi; Mariya na Merina walilala chini huku mapovu mengi yakitoka midomoni mwao pia walionekana kutupa mikono na miguu kama vile walikuwa wakikata roho. Victor Federov akalia kama mtoto mdogo.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…

“Bosi hebu njoo uone mbona wanatoka mapovu!”
“Mapovu?” aliuliza akikimbia kurejea eneo hilo. Ni kweli Mariya na Merina walikuwa wakitiririkwa na mapovu kutoka midomoni mwao.

“Mungu wangu ni kitu gani hiki? watoto wangu wamepewa…”
“Wamepewa nini bosi wangu?”
“Wamepewa sumu hawa haya mapovu ni ya nini? Watoto wangu wanakufa wakati nikiwa tayari nimeshapoteza fedha nyingi, tafadhali msiniache, naomba msiniache nitabaki na nani katika dunia hii? Fedha na mali si kitu kama sina ndugu wala mtoto yeyote? Mungu nisaidie,” aliongea mfululizo.

Akiwa hapo, Victor Fedorov akionyesha kukata tamaa kabisa, mawazo yake yote yakampeleka kwa jambazi aliyemwona ndani ya msitu wa Beloomut akamshuhudia akikimbia na begi lililojaa fedha nyingi ndani yake na kutokomea.

“Kama ni fedha nilimpatia, kwa nini ameua watoto wangu? Kwa nini amewatesa viumbe wasio na hatia? Utajiri wangu umekwenda, na watoto pia wananiacha, nimekosea nini kwa Mungu? Pengine jambo hili linatokea kwangu kama adhabu kwa makosa niliyoyafanya huko nyuma? Hapana! Nashindwa kuelewa…” aliongea mfululizo akiwa pembeni mwa watoto wake ambao mpaka wakati huo walishatulia kimya, mapovu hayakutoka tena midomoni mwao na miguu na mikono yao ilikuwa imetulia kimya.

“Yametimia!” hivyo ndivyo alivyosema Victor Fedorov na kuangua kilio kikali ndani ya nyumba, mlinzi akasogea karibu yake na kumbembeleza.
“Haiko haja ya kuishi! Bora nife niuungane na familia yangu? Watoto wangu wa kwanza walikufa kifo kibaya wakati wakicheza mchezo wa kuteleza katika barafu na hawa nao …”
Kwikwi ya kulia ikamkaba ni kweli taswira za watoto wake wawili pamoja na mkewe waliokuwa wamekufa miaka mingi kabla, ilimjia kichwani mwake akajiona ni mtu mwenye mkosi duniani hata thamani ya utajiri aliokuwa nao hakuiona, akatamani kuungana na familia yake.

“Nitakufa! Si muda mrefu kuanzia sasa nitaungana na familia yangu…Mungu wangu…kwa nini yote haya…kwa nini mimi? Nimekosa nini?” alizidi kujilaumu.
Akionyesha kukata tamaa kabisa, akasogeza mkono wake wa kulia na kuupeleka moja kwa moja upande wa shingo ya Mariya ili kupima mapigo yake ya moyo ambapo yalionekana kutulia akageuka tena upande wa pili na kugusa mapigo ya Merina nayo yalionekana kuwa kimya kabisa.

Bila kusema tena neno lolote akatembea na kwenda kuketi juu ya kiti huku jasho jingi likimtoka na mwili wake ukitetemeka.
“Bosi mimi naona tuwapeleke hospitali huko tutapata mtaalamu ambaye atasema neno.”

“Lipi zaidi?”
“Mimi nashauri tufanye hivyo pengine wamezimia tu.”
“Nina hakika wamekufa, watoto wangu, wameniacha lakini naamini kabisa nyuma ya mchezo huu yupo mtu fulani sijui ni nani ila yupo, mbona nimetimiza masharti yote? Nimetoa fedha nyingi sana kuwakomboa lakini amenilipa ubaya?” aliongea muda wote huo akiwa ameketi akionyesha kukata tamaa juu ya maisha yake na mbele yake alifikiria kitu kimoja tu; kifo basi.
***
Baada tu ya kutoka ndani ya lango kuu la hoteli ya Lamada, Lina akiwa amejifunika shuka alikimbia na kuvuka upande wa pili wa barabara, watu wachache waliokuwepo eneo hilo wakimshangaa, lakini hakujali alidhamiria kuondoka hapo na kutokomea, huku akilia akasogelea moja ya teksi.

“Wewe ni mtu au mzimu?” aliuliza dereva teksi aliyekuwa ndani ya gari, haraka akaufungua mlango na kutoka nje tayari kukimbia kwani mara kadhaa historia katika eneo hilo ilionyesha kwamba mizimu ilikuja hapo kutoka makaburi ya jirani hivyo kutokea kwa mtu huyo tena akiwa katika shuka nyeupe kulimwogopesha.
“Kaka usikimbie tafadhali naomba msaada wako mimi ni mwanadamu wa kawaida.”

“Mh! Hapana usinidanganye tena ona unaongea sauti ya mwanamke, kwa jina la Yesu toka mbele ya macho yangu!”
“Mimi si mzi…” aliongea Lina lakini kijana huyo hakuwa tayari kumsikiliza bado aliendelea kurudi kinyumenyume akijiandaa kukimbia ili kuondoka eneo hilo.

“Ona! Mimi ni mwanadamu!” aliongea akijaribu kufunua shuka alilojifunika.
“Mungu wangu! Nakufa jamani, jini hili tena yuko…” alipaza sauti na kufanya teksi nyingine zote zilizokuwa jirani madereva wake wawashe magari yao na kuondoka eneo hilo kwa kasi.

Kwa uwezo wake wote alijaribu kujitetea kuwafanya watu waliokuwepo eneo hilo wamwone kwamba alikuwa ni mwanamke wa kawaida lakini ilionekana kushindikana, teksi zote zikaondoka eneo hilo na kubaki moja tu ambayo dereva wake aliondoka na kuacha gari peke yake eneo hilo.

“Nitafanya nini sasa?” alijiuliza huku akilia, alitaka kufanya kila kilichowezekana kuondoka eneo hilo kurejea nyumbani kwake, ndani ya moyo wake kulijaa hasira kali juu ya Phillip, hakika hakumpenda tena na aliapa kumchukia maisha yake yote yaliyobaki.

“Phillip amenidhalilisha kupita maelezo, sipo tayari tena kuendelea kuwa naye! Yaani hivi? Mimi kabisa? Mh! Siyo Lina nadhani ni mzimu wake?” alijiuliza akizidi kusonga mbele, kichwani mwake hakuwa na picha ni wapi alikuwa akielekea lakini alitaka tu kuondoka eneo hilo.

“Naamini nitapata tu njia ya kuondoka hapa kabla hakujapambazuka,” aliwaza.
***
“Ngrii! Ngrii!Ngriii!” Ulikuwa ni mlio wa simu, mlinzi wa Victor Fedorov baada ya kuona kwamba bosi wake alikuwa amekata tamaa aliamua kutumia uwezo aliokuwa nao, akasogea karibu na simu na kubonyeza namba kadhaa kitengo cha hatari akiomba gari la wagonjwa.

“Naweza kupata gari la wagonjwa haraka sana?”
Upande wa pili ulijibu.
“Ni nyumbani kwa Victor Fedorov nadhani ni mtu anayefahamika sana hapa kwetu, tafadhali fanyeni haraka kuna wagonjwa hapa…” aliongea kwa msisitizo.
“Hakuna haja tayari wamesha…” aliongea Victor Fedorov huku akilia.

“Hapana bosi sisi si madaktari ngoja tuwapeleke hospitali pengine huko tunaweza kupata ufumbuzi wa tatizo.”
“Kweli?”
“Ni kweli kabisa.”
“Mariya! Merina kweli mmeondoka na kuniacha wanangu? Maisha bila ninyi si kitu, nilijaribu kwa nguvu na uwezo wangu wote kuwapata lakini sasa mmeondoka wana…”

Wakiwa hapo haikuchukua hata muda wa dakika tano tayari king’ora kikasikika nje ya lango la kuingilia ndani ya nyumba ya Fedorov, mlinzi akakimbia haraka kwenda kufungua geti, moja kwa moja gari likazama ndani na watu wawili wakiwa wamevalia nguo za rangi ya bluu wakashuka.

“Yuko wapi huyo mgonjwa?”
“Siyo mgonjwa ni wagonjwa wako wawili?”
“Wawili?”
“Ndiyo.”
“Wako wapi?”
“Huku! Twendeni huku nikawaonyeshe,” mlinzi aliongea akitangulia mbele huku akikimbia.

Wote watatu wakazama ndani ambako mlinzi aliwaonyesha wagonjwa na kumtambulisha Victor Fedorov kwamba ndiye baba wa watoto hao na bila kusema kitu watu hao wakainama na kuanza kuwachunguza watoto hao wakishika sehemu mbalimbali za miili yao kuwaangalia na mwisho kabisa wakachukua kipimo maalum cha kusikiliza mapigo yao ya moyo.

Muda wote huo wakihangaika, Victor Fedorov alikuwa pembeni yao naye pia akionyesha wasiwasi mwingi.
“Wako hai?” aliuliza.

“Mh! Mh!” waliguna kwa pamoja huku wakinyanyua macho yao kumwangalia Fedorov, naye akayasoma vyema na kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.

“Tafadhali nielezeni ukweli msinifiche jambo kuna kitu hapa.”
“Mzee! Matumaini haya…” hawakumalizia sentensi yao wakamshuhudia Victor Fedorov akishuka chini na moja kwa moja akawainamia watoto wake na kuanza kuwabusu mfululizo huku akilia.

Lina aliendelea kutembea barabarani huku akilia akili yake haikuonekana kufanya kazi kwani kila kitu alichokifikiria kuwa msaada kwake kilionekana kukwamwa kabisa.

“Ni lazima niondoke hapa kabla hakujapambazuka.” Aliongea akizidi kusonga mbele.

Huku akijilaumu moyoni mwake kwa mambo yote yaliyomtokea, aliamini bila kukutana na Phillip na kumpenda kisha kufunga ndoa naye hayo yote yasingempata, akazitupa lawama zote kwa mwanaume huyo na kumchukia kabisa.

Jambo moja liliendelea kupita kichwani mwake ni kwamba, mara tu akifanikiwa kufika nyumbani ni kuchukua kila kilichokuwa cha kwake kisha kumwachia Phillip nyumba na yeye kwenda kutafuta sehemu nyingine ambako angeishi maisha yake.
“Nitaondoka, nitamwachia Phillip nyumba, kwa kitendo hiki siko tayari kumsamehe amenidhalilisha sana,” bado Lina aliendelea kujilaumu.
***
Phillip aliyekuwa ndani ya hoteli pamoja na walinzi wawili waliushuhudia mchezo mzima jinsi ulivyokuwa ukiendelea lakini hakuthubutu kufungua mdomo wake kueleza jambo lolote.
Kufanya kwake hivyo ingekuwa ni kujipalia makaa ya moto kwani mwanamke aliyetoka mbio ndani ya chumba akiwa na shuka tu mwilini mwake ni mkewe na kibaya zaidi mwanaume alikuwa akimfuata kwa nyuma huku akimwita ili arejee wamalizie shughuli iliyokuwa mbele yao, ilikuwa ni fedheha ya kutosha kwake.
“Sijui anakwenda wapi? Masikini mke wangu… nisamehe halikuwa kusudio langu kutenda haya,” aliwaza huku akikimbia kuelekea lango kuu la kutokea hotelini ili ashuhudie ni wapi Lina alikuwa akielekea.
Kabla hajatoka nje ya lango akalikumbuka gari lake, akaamua kurejea ili alichukue na kuondoka nalo kumfuatilia Lina, jambo hilo lilifanyika kwa haraka, alipolifikia bila kusema kitu akaingia ndani ya gart hilo na kuliwasha haraka akakanyaga mafuta na likatii amri ba kutoka nje ya hoteli hiyo.
Aliwashuhudia walinzi wawili aliokuwanao wakiwa na mtu mwingine wa tatu na alipotupa macho yake kumwangalia mtu yule alimtambua kuwa ni mwanaume aliyekuwa na Lina ndani ya hoteli, alikuwa akiangua kilio huku akiongea maneno ambayo Phillip hakuyasikia vyema.
“Nitamtafuta Lina mpaka nimpate nimwombe msamaha mke wangu najua ananipenda na atanisamehe,” aliongea akikunja usukuni na kutokeza barabarani.
Moyo wake ulijawa hofu na kujitupia lawama nyingine lakini alijipa moyo baada ya kuamini kwamba jambo lililokuwa limetokea siku hiyo lilikuwa ni kati ya makubaliano yake na mkewe Lina.
Hakuwa na ufahamu kabisa wa kile kilichotokea ndani ya chumba cha hoteli ile mpaka mfarakano ukatokea, hakufahamu kabisa kwamba Lina hakuwa tayari kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine, kwake yeye aliamini kwamba kufanya hivyo kungeidhalilisha ndoa yake kama si kuisaliti.
Phillip akaliendesha gari taratibu huku akitupa macho yake huku na kule kuangalia kama angeweza kumwona Lina eneo hilo lakini hakufanikiwa.
Baada ya mwendo mrefu alitupa macho upande wa pili wa barabara na kufanikiwa kulishuhudia kundi kubwa la watu walioonekana kubishana kitu fulani, wazo la kuwafuata watu wale kujaribu kuwauliza likamwingia kichwani mwake.
Philip akaliendesha gari na kuelekea upande wa pili wa barabara na kupaki pembeni kisha kulizima kabisa, akashukua ndani na kuwasogelea watu wale waliokuwa wamekusanyika kila mmoja akiongea lake.
“Habari za saa hizi jamani?” Aliuliza kwa sauti ya kiume.
“Salama!”
“Naomba kuuliza.”
“Uliza tu tunakusikiliza.”
“Sijui mmefanikiwa kumwona mwanamke mmoja akipita hapa?”
“Mwanamke?”
“Ndiyo”
“Mh! Yule si mwanamke ni mzimu.”
“Mzimu?”
“Ndiyo, tena umevaa shuka nyeupe, umekimbilia kuleeee,” alisema mtu mmoja huku akinyosha kidole kuelekeza upande alipoelekea Lina.
“Wapi?”
“Wee kaka huo mzimu unaoulizia umekwenda kule.”
Maumivu makali yakauchomoa moyo wake, yalikuwa kama vile mshale wa moto, Phillip akaonekana kama mtu aliyenyeshewa na mvua, bila kujibu chochote taratibu akaingia tena ndani ya gari lake na kuanza kuondoka eneo lile bila kuuliza tena swali kwa mtu yeyote.
Watu waliokuwepo katika kundi lili wakazidi kumshangaa.
***
“Mzee hakuna haja ya kulia nashauri tuwapeleke watoto hospitalini.”
“Kufanya nini wakati wameshakufa?” Victor Fedorov aliuliza huku machozi yakimbubujika.
“Hakuna aliyesema wamekufa hawa ila…”
“Ila nini? Mbona mnazidi kunichanganya ninyi?”
“Bosi tufuate ushauri wa watalaam,” mlinzi wa Victor aliongea akimpigapiga bosi wake sehemu za mabegani.
“Sawa lakini matumaini hayapo, watoto wangu wameniacha mkiwa, Mariya na Merina wameondok…” Victor Fedorov aliangua kilio huku kwikwi ikimkaba.
Kwa Victor Fedorov tajiri ambaye alivuma kupita maelezo ilionekana kama ndoto, hakuwa tayari kuamini kwamba alibaki peke yake duniani huku akiwa ametoa karibu nusu ya utajiri wake wote kuwakomboa watoto wake Mariya na Merina lakini sasa nao walikuwa wamemwacha mkiwa katika dunia ambayo hakika hakufahamu nini ingekuwa hatima yake.
Utajiri wake wote aliokuwa nao sasa ulikuwa hauna maana tena.
“Ngoja twende hospitali nitajua kila kitu huko,” aliwaza kichwani mwake huku akishuhudia watoto wake wakibebwa mmoja baada ya mwingine na kuingizwa ndani ya gari la wagonjwa.
“Mzee kwa sababu nafasi yetu ni finyu tungeomba uendeshe gari lako ukitufuata kwa nyuma”
“Hakuna shida”
Victor Fedorov akafanya hivyo lakini akamwomba mlinzi wake waongozane wote kwani hakuwa katika hali nzuri. Baada ya kuhakikisha kwamba kila kitu kilikuwa sawa nyumbani hapo wakafunga milango na wote kutoka.
Gari la wagonjwa lilikuwa mbele yao huku likipiga king’ora cha kuashiria hatari na wao wakiwa nyuma huku Fedorov akionekana kuzama katika lindi la mawazo.
Victor Fedorov aliendesha gari sambamba kabisa na gari la wagonjwa hakutaka kuliacha hata hatua moja, hamu yake kubwa ilikuwa ni kufika hospitalini na kuona watoto wake wakifanyiwa uchunguzi maalum ambao aliamini ungerejesha majibu yakatayomfanya arejee tena katika dunia, kwani tayari alishajihesabu kwamba alikuwa ni marehemu mtarajiwa kama tu angeelezwa kwamba watoto wake Mariya na Merina hawakuwa na maisha tena.
“Hapana! Sitaki wafe, nataka waishi, Mungu naomba unisaidie jambo hili, nawapenda mno watoto wangu kama kweli watakuwa wamefariki basi na mimi nitakufa, hakika watazikwa siku moja na mimi,” aliongea kwa sauti iliyomshtua mlinzi wake ambaye muda wote huo naye alikjuwa akiwafikiria watoto hao.
“Hawatakufa,” mlinzi alijibu akimwangalia Fedorov.
“Vruuu! Vruuu!” Sauti ilisikika


JE NINI KILIENDELEA
 
SEHEMU YA 37


Victor Fedorov akafanya hivyo lakini akamwomba mlinzi wake waongozane wote kwani hakuwa katika hali nzuri. Baada ya kuhakikisha kwamba kila kitu kilikuwa sawa nyumbani hapo wakafunga milango na wote kutoka.
Gari la wagonjwa lilikuwa mbele yao huku likipiga king’ora cha kuashiria hatari na wao wakiwa nyuma huku Fedorov akionekana kuzama katika lindi la mawazo.
Victor Fedorov aliendesha gari sambamba kabisa na gari la wagonjwa hakutaka kuliacha hata hatua moja, hamu yake kubwa ilikuwa ni kufika hospitalini na kuona watoto wake wakifanyiwa uchunguzi maalum ambao aliamini ungerejesha majibu yakatayomfanya arejee tena katika dunia, kwani tayari alishajihesabu kwamba alikuwa ni marehemu mtarajiwa kama tu angeelezwa kwamba watoto wake Mariya na Merina hawakuwa na maisha tena.
“Hapana! Sitaki wafe, nataka waishi, Mungu naomba unisaidie jambo hili, nawapenda mno watoto wangu kama kweli watakuwa wamefariki basi na mimi nitakufa, hakika watazikwa siku moja na mimi,” aliongea kwa sauti iliyomshtua mlinzi wake ambaye muda wote huo naye alikjuwa akiwafikiria watoto hao.
“Hawatakufa,” mlinzi alijibu akimwangalia Fedorov.
“Vruuu! Vruuu!” Sauti ilisikika

SONGA NAYO

“Vruuu! Vruuu!” sauti ilisikika.
Kelele za matairi ya gari yakisugua barabara zilisikika, dereva wa gari alikuwa akijitahidi kadiri ya uwezo wake kukanyaga breki ili kunusuru maisha ya mtu aliyekuwa akikatiza barabarani asubuhi hiyo.
“Mungu wangu! ” Victor Fedorov aliongea macho yake yote yakimwangalia mtu huyo, hasira ya ajabu ilikuwa imemshika lakini alipokumbuka kwamba alitakiwa kuondoka eneo hilo haraka kuliwahi gari la wagonjwa lililobeba watoto wake hakuongea neno jingine zaidi, akaliwasha gari na kuondoka eneo hilo haraka.

“Pole sana bosi,” mlinzi aliongea.
“Ni balaa hilo limeshapita zake.”
“Dah! Sijui alikuwa haoni?”
“Siyo kuona tu hata king’ora hakukisikia?”
“Msamehe, pengine mawazo ya maisha yamemchanganya.”

“Ni kweli kabisa nimeshamsamehe, ndiyo maana sikufanya chochote zaidi ya kumwangalia tu,” aliongea Fedorov akikanyaga mafuta kulifuata gari lililobeba watoto wake ambalo halikuwa umbali mrefu sana na gari lake.

Kwa mwendo wa dakika kumi nzima aliendelea kulifuata gari la wagonjwa kwa nyuma, hofu yake ikizidi kuongezeka juu ya hali ya watoto wake, na mawazo mengi yaliufunika mtima wake. Ni mlinzi ndiye aliyekuwa pembeni yake kumfariji na kumweleza kwamba kila kitu kingekwenda sawa na hakusita kumweleza wazi kwamba watoto hao hawakufa bali walikuwa katika hali ya kuzimia na muda si mrefu baada tu ya kuonana na madaktari wangepata nafuu na wote kurejea nyumbani.“Ahsante ndugu yangu, sipendi kushuhudia vifo vya watoto wangu kwani hao ndiyo ndugu pekee niliobakiza duniani, kama ikitokea wakaniacha basi na mimi sitaweza tena kuendelea kuishi dunia ya peke yangu, nitawafuata.”

Maneno hayo yalipita moja kwa moja masikioni mwa mlinzi na akili yake ikauona utajiri wa Victor Fedorov mikononi mwake kwani kama ingetokea watoto wale wakawa wamefariki dunia na Victor Fedorov kujiua kama alivyokuwa akisema basi utajiri wote ungekuwa wake, aliliamini jambo hilo kwa asilimia mia moja.
“Akijiua kweli basi nitakuwa mrithi wake, kwani hana ndugu huyu na kama mwenyewe alivyokiri kwa kinywa chake, utajiri huo utakuwa mikononi mwangu, ” aliongea.

Ni sauti ya Fedorov iliyomshtua na kumtoa katika dimbwi hilo la mawazo.
“Je,uko wapi mbona umenyamaza ghafla, umepatwa na nini?”
“Ah! Bosi unajua ninakuonea huruma sana…lakini zaidi afya ya watoto…”
“Watakufa?” alidakia tena Fedorov.

“Mh! Kwa kweli sijui chochote mpaka sasa ngoja tufike hospitali kwanza,” aliongea mlinzi huyo akimwangalia bosi wake kwa jicho la tamaa ya utajiri.
“Ongea neno wewe sasa si mlinzi tu bali ndugu yangu.”
“Unasema?”
“Wewe ni ndugu yangu bwana,” kauli hiyo ikazidi kumchanganya zaidi ubongo wake.

“Mh! Au amenigudua? Kwa nini ameniambia kitu ninachokifikiria?” alijiuliza kimoyomoyo na haikuchukua muda mrefu sana, tayari wakawa wameshafika hospitalini ambapo haraka wote wawili baada ya kuegesha gari sehemu ya maegesho wakashuka na kuanza kukimbilia eneo la mapokezi ambako gari la wagonjwa lilionekana.
“Wakikaribia eneo hilo wakashuhudia machela mbili zikisukumwa kutoka ndani na kusogezwa karibu kabisa na mlango wa gari kisha kufunguliwa na watoto wawili wakatolewa na kuweka juu yake.

“Tafadhali fanyeni haraka sana tujitahidi kuokoa maisha ya wagonjwa hawa,” ilikuwa ni sauti ya daktari aliyekuwepo ndani ya gari la wagonjwa.
Wakati zoezi hilo likiendelea Victor Fedorov alishafika eneo hilo na kushuhudia machela zikisukumwa kwa kasi ya ajabu kuingizwa ndani ambako naye alizifuata kwa nyuma akiwa na mlinzi wake.

“Na ninyi mnakwenda wapi huku?” ilikuwa ni sauti ya mwanaume aliyesimama eneo hilo akionekana kuwa mlinzi.
“Watoto wangu, hawa ni watoto wangu.”
“Watoto wako?”
“Ndiyo,” alijibu akikimbia kuelekea mbele.

“Na wewe ni nani?”
“Huyo hapo ni bosi wangu mimi ni mlinzi wake.”
“Wewe unaweza kubaki hapa acha mhusika afuate nyuma, sawa?” aliuliza akimzuia mlinzi aliyekuwa ameongozana na Fedorov.
Akashuhudia Fedorov na wauguzi waliokuwa wakisukuma machela wakitokomea na kumwacha hapo peke yake akiwa hajui nini cha kufanya.

***
“Lina! Lina! Linaaaa!” ilikuwa ni sauti ya Phillip akiita jina la mke wake.
Ni sauti hiyo ndiyo iliyopenya moja kwa kwa moja masikioni mwa Lina na kumfanya ageuke kuangalia ilitokea wapi, taratibu huku akibubujikwa na machozi akageuza shingo yake na kuangalia nyuma pamoja na kwamba kulikuwa na giza lakini aliweza kuona taa za gari zikija nyuma yake kwa kasi kubwa, akasimama. ”Tafadhali simama, simama tuongee mke wangu.”

“Mh! Sauti ya Phillip hiyo,” aliongea.
Akiwa hapo akashuhudia gari likisimama mbele yake na mwanaume akachomoka ndani yake akikimbia kumfuata.
“Nisamehe mke wangu ishara ya magoti kwako ni kuonyesha kwamba nimekukosea,” aliongea Phillip akipiga magoti mbele ya Lina.
Machozi yakambubujika Lina, hasira ilikuwa imemkaba zaidi alipomshuhudia mwanaume aliyempenda kupita kiasi akiwa mbele yake kumwomba msamaha na ni huyu ndiye aliyekuwa amesababisha kutokea kwa sakata lote hilo ndani ya hoteli ya Lamada.
“Umenidhalilisha Phillip.”

“Nisamehe ndiyo maana niko chini ya miguu yako.”
“Phillip! Phillip nyanyuka uondoke sita…” aliongea Lina akijitoa mikononi mwa Phillip ambaye muda wote huo bado alikuwa chini amepiga magoti.
Kwa nguvu zake zote Lina alijaribu kujitoa kwa Phillip lakini haikuwezekana, wote wawili wakajikuta wakigalagala chini.
Phillip bado aliendelea kumwomba Lina msamaha akimsihi akubaliane na ombi lake pia akubali kuingia ndani ya gari waondoke kwenda nyumbani, huko wangemaliza tofauti zao zote.

“Sitaki! Sitaki nasema sitaki mbona hutaki kunielewa, kwa kitendo hiki kilichotokea leo siko tayari kukusamehe.”
“Nisamehe mke wangu mimi mwenyewe ninaumia moyo.”
“Phillip uumie wewe? Nakuambia umenidhalilisha na si mimi tu hata Daniel, sidhani kama atakuwa tayari kunisamehe kwa ninavyomfahamu, huko aliko anapanga jinsi ya kulipa kisasi kwangu, masikini wa Mungu haikuwa dhamira yangu kufanya yaliyotokea ni wewe ndiye umeni…” aliongea Lina na kushindwa kumalizia sentensi yake kwani kwikwi ya kulia ikamkaba zaidi.

Phillip akautumia udhaifu huo wa Lina na kumbeba juujuu kama mtoto kisha kumwingiza ndani ya gari yeye pia kukimbilia upande wa pili na kuingia kisha kuliwasha na kuondoka eneo hilo kwa kasi ya ajabu, watu wote waliokuwepo eneo hilo wakishangaa kwa kitendo hicho.
***
“Kazi uliyonituma mzee nimemaliza na mzigo ni huu hapa,” ilisikika sauti ndani ya chumba kidogo ndani yake, mwanga hafifu wa taa ulionekana na mzee mfupi akiwa ameketi pembezoni kabisa mwa chumba hicho akaonekana.

“Haraka wapelekeni chumba cha wagonjwa mahututi,” ilikuwa ni sauti ya mwanaume aliyekuwa kwenye korido ambaye kwa kumwangalia tu ilitosha kugundua kwamba ni daktari.

Bila kusema kitu chochote, machela zote mbili zikaanza kusukumwa kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi huku Victor Fedorov naye akifuata kwa nyuma. Akili yake haikuonekana kufanya kazi kwa mateso aliyokuwa akiyashuhudia mbele yake, aliiona dunia haina maana kwake.

“Nisaidie jamani watoto wangu wasife, hawa ndiyo ndugu pekee niliobakiza duniani, bila hawa hata utajiri wote nilionao mimi si kitu, niko tayari kutoa kiasi chochote cha fedha lakini ilimradi watoto wangu waokolewe…” alisema mfululizo.
Hakuwepo mtu hata mmoja aliyeweza kuongea kwa wakati huo, si wauguzi wala madaktari, wote walikuwa na hofu kubwa juu ya maisha ya watoto hao. Hatimaye dakika tatu tu baadaye machela mbili ziliwasili nje ya wodi kubwa, Victor Fedorov akashuhudia maneno ICU juu ya mlango wa wodi hiyo.

”Oh! My God!”(Oh! Mungu wangu!) alisema.
“Shaka ondoa mzee, wanaingia kwenye chumba cha usalama, kila kitu kitakuwa sawa,” alisema muuguzi mmoja huku akimwangalia Fedorov kwa macho ya huruma.
“Watapona kweli?”
“Mh! Watapona.”

“Mbona umeonesha kusita dada?”
“Tuombe Mungu kwani mpaka sasa hatufahamu vyema tatizo linalowasumbua.”
Wakiwa hapo, mlango ukafunguliwa na machela zote mbili zikaingizwa ndani na kumwacha Fedorov peke yake nje akiwa haelewi nini cha kufanya, akawa analia huku akizungusha macho yake huku na kule. Pembeni kabisa ya wodi aliuona msingi, pamoja na kwamba juu yake paliandikwa kuwa si ruhusa kukaa yeye alinyoosha moja kwa moja na kwenda kuketi juu yake.

“Nitakaa hapahapa nikisubiri matokeo, siwezi kwenda mbali, moyo wangu umegubikwa na hofu kupindukia… masikini Mariya na Merina! Nimejitahidi kuokoa maisha yenu wanangu lakini naona Mungu hakupanga jambo hili, hakupanga muendelee kubaki na mimi baba yenu! Bora ningewaacha tu Tanzania pengine yote haya yasingetokea… lakini hapana ninyi ni sehemu ya damu yangu, isingekuwa rahisi kufanya hivyo,” Fedorov alikuwa akijisemea huku picha ya jinsi alivyotoa mbegu zake za kiume na kuziuza kwa familia ya Phillip na Genevieve ikijirudia kichwani mwake. Alikumbuka pia fedha nyingi alizotoa kwa ajili ya malipo kwa Ditrov ya kuwateka watoto hao kutoka mikononi mwa Phillip na kuwaleta nchini Urusi, hakutaka kuamini kuwa sasa walikuwa katika hali mbaya kiasi kile.

Akiwa katika dimbwi hilo la mawazo, ghafla akasikia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi ukifunguliwa na wauguzi wawili wakatoka mbio wakikimbia. Alipojaribu kuwafuata ili aongee nao na kufahamu hali za watoto wake, walimzuia na kumweleza kwamba walikuwa na haraka sana hivyo aendelee kusubiri eneo hilo mpaka watakaporejea.
“Hatuwezi kukusikiliza, kuna jambo muhimu sana linatakiwa kufanyika sasa hivi.”
“Nataka kujua hali za wanangu… nisaidieni jamani… akili yangu haifanyi kazi vizuri,” alisema mfululizo lakini tayari wauguzi hao walishaondoka na kumwacha hapo.

Haikuchukua hata dakika tano, kwa mbali akawashuhudia tena wauguzi wale wakirejea, lakini safari hii wakisukuma vitu viwili kama mitungi mikubwa. Akili yake ikafanya kazi haraka na kugundua kwamba ilikuwa ni mitungi yenye hewa safi ya Oksijeni.
“Hii si mitungi ya gesi kweli?”alijiuliza huku akikodoa macho kuangalia.
Hakukosea, ilikuwa ni mitungi ya hewa ya oksijeni ikisukumwa kuingizwa ndani ya wodi ya wagonjwa mahututi, Fedorov akalia kwa uchungu.

“Hali imekuwa mbaya mpaka wanawekewa hii?” aliuliza huku machozi yakibubujika mashavuni mwake. Kwa hali aliyoiona alizidi kukata tamaa ya kuwaona tena watoto wake wakiwa hai kwani mara kadhaa wagonjwa wengi waliowekewa hewa hivyo hawakuishi muda mrefu.
“Ni kweli lakini yakupasa uwe mvumilivu, utaelezwa kila kitu kinachoendelea baadaye…” walisema wauguzi wale na kusukuma mitungi hiyo kuingia ndani ya wodi.

Fedorov akalisikia jasho jembamba likitiririka mwilini mwake taratibu huku akiwa hajui nini cha kufanya, akajikongoja na kusogea pembeni huku moyoni mwake akiwaza jambo moja tu, kubaki hapo mpaka mwisho.
“Sitaondoka, nitakaa hapa kusubiri,” alisema.
***
“Puuuh!”
Ulikuwa ni mlio wa kitu kikirushwa juu ya meza.
Mzee mfupi mwenye mwili uliojazia kisawasawa, huku akitabasamu alinyanyuka kwenye kiti na kusogea karibu na meza ambayo juu yake ilikuwa na mzigo.
“Umeifanya vyema kazi hii,” alisema huku akipadisha suruali yake vizuri.
“Bila shaka mzee, hakuna tatizo juu ya hilo?”

“Una uhakika na maelezo yako kijana?” Sauti nzito ya mzee huyo ikasikika tena, safari hii akimzunguka kijana huyo kila upande na kukagua mifuko yote ya suruali yake akimtaka kusalimisha silaha yoyote aliyokuwa nayo juu ya meza.
Bila kusema kitu chochote, kijana yule, huku akionesha kujiamini aliweka silaha zote mezani na alipomaliza aliachia kicheko.
“Kwa nini unacheka?” aliuliza.
“Bosi, inavyoonekana huniamini hata kidogo.”

“Uaminifu wangu umesafiri mbali sana na sidhani kama utarejea leo kwa mchezo mbaya niliofanyiwa huko nyuma, sipo tayari kumwamini mtu yeyote tena maishani mwangu, labda roho yangu tu. Teh!Teh! Teh!” alimaliza mzee huyo kwa kicheko cha kejeli.
“Hata mimi kijana wako?”
“Nilichosema ndiyo hicho,”alisema huku akiendelea kuzungukazunguka ndani ya chumba hicho.

“Sawa nimekuelewa bosi wangu, ni vyema ukanipatia mgao wangu na mimi niondoke kuendelea na masuala mengine.”
“Naweza kuuliza tena?”
“Bila shaka?”
“Hukuua wala kujeruhi?”
“La hasha!”

“Watoto wote wawili wapo salama?” aliuliza mzee huyo akikodoa macho kumwangalia kijana aliyesimama mbele yake.
“Mh!”
“Unaguna nini?”
“Nauliza tena wako salama?”
“Baada ya kupata mzigo huu niliwarusha kutoka ndani ya gari langu mpaka chini, mmoja baada ya mwingine na mimi kuondoka eneo hilo haraka bila kuangalia nyuma... lakini pia…” kigugumizi cha ghafla kikamshika kijana huyo na kushindwa kumalizia sentensi yake.

“Lakini nini? Umewaua?”aliuliza mzee huyo, safari hii kwa ukali.
“Hawajafa ila hali zao ni mba…ya sijui kama wataiona ke…sho?”
“Kwa nini?”
“Niliwa…” alisema kijana huyo huku akitetemeka.

“Unasema?” lilikuwa ni swali kutoka kwa mzee aliyekuwepo ndani ya chumba, bila huruma akaikamata vyema bastola iliyokuwa juu ya meza, akainyoosha na kulielekea paji la uso wa kijana aliyesimama mbele yake.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 38


KWA muda wa saa tatu mfululizo bado aliendelea kusimama nje ya chumba cha wagonjwa mahututi, macho yake yote yakielekezwa kwenye mlango huo ili kuona mtu ambaye angetoka na yeye kuweza kumuuliza nini kiliendelea kwa watoto wake Mariya na Merina.
Victor Fedorov alikuwa ni mwanaume wa shoka lakini sasa alianza kuonyesha udhaifu wake kwani mpaka wakati huo tayari alishakata tamaa, moyo wake ulimuuma kupita kiasi, akasikiliza sauti ndani yake ikimlaumu kwa kitendo chake cha kuwateka watoto hao kutoka Tanzania na kuwaleta nchini Urusi na sasa walikuwa wakifa bila hatia.

Saa nne ilipogonga akaushuhudia mlango wa chumba hicho ukifunguliwa na kushuhudia machela ikisukumwa kutoka ndani ya wodi kwenda nje, juu yake ikionekana kulazwa mtu aliyefunikwa na shuka la kijani kuanzia kichwani mpaka miguuni, hofu kwamba tayari kulikuwa na tatizo ikaugubika moyo wake.
“Mh!” aliguna akikimbia kuisogelea.
“Unakwenda wapi?” sauti ya muuguzi ilisikika ikimuuliza.

“Nataka nione hapo,” aliongea akinyoosha kidole chake cha shahada kuelekea ilipokuwa machela.
“Kaka samahani sana sheria yetu ya kazi hairuhusu kufanya hivyo,” muuguzi huyo alijibu na tayari walishaanza kusukuma tena machela kuondoka eneo hilo, Victor Fedorov naye akifuata nyuma huku akilia.
“Dada tafadhali niruhusu nimwone huyo aliyelala hapo nataka nijue tu pengine ni mwanangu.”
“Mwanao?”
“Ndiyo!”

“Lakini hatuna ruhusa ya kufanya hivyo, kaka yangu, utanifanya nifukuzwe kazi.”
“Nionee huruma.”
“Hapana,” alijibu muuguzi huyo na kwa kasi ya ajabu akaisukuma machela kuondoka eneo hilo kuelekea chumba cha kuhifadhia maiti, Victor Fedorov akaangua kilio na kushuhudia machela hiyo ikizama ndani.
Akaamini kwamba hakika mmoja wa watoto wake tayari alikuwa ameaga dunia.

***
“Nataka kuondoka na nitakuachia kila kitu ndani ya nyumba hii.”
“Uende wapi mke wangu wewe ndiye wangu wa maisha.”
“Nimeshachoka huwezi kunidhalilisha kiasi hicho halafu ukadai kwamba unanipenda.”
“Chukua maneno yangu na uyafanyie kazi, wewe mwenyewe unafahamu ni jinsi gani ninavyokupenda.”
“Mh! Unaniona mimi mjinga? Hivi unafikiri mimi mtoto, unanichapa halafu unanibembeleza kwa pipi?” aliuliza Lina akizidi kukusanya nguo zake na kuzitupia ndani ya sanduku.

“Haiko haja ya wewe kuondoka, hapa ni kwako acha mimi niondoke.”
Tayari Lina alishanyanyua sanduku akatembea na kuusogelea mlango wa chumba chao na kuufungua ili atoke nje.
“Hapana mpenzi, tafadhali nisemehe hamu ya kuitwa baba ndiyo ilinifikisha hapo.”
“Basi mtafute mwanamke mwingine ambaye atakubali kufanya unayotaka.”

Ukimya wa ajabu ukatokea kati yao Phillip aliyekuwa amepiga magoti chini akakimbia na kulikamata sanduku la Lina huku akimsihi asifanye maamuzi kama hayo, lakini zoezi hilo lilionekana kushindikana na kujikuta akiambulia teke kutoka kwa mwanamke huyo.
Hasira ya Lina ilionekana wazi, si kwamba kweli hakumpenda Phillip bali alimpenda kwa dhati lakini hakuwa tayari kukutana kimwili na mwanaume mwingine ili kupata ujauzito hivyo kitendo cha Phillip kulazimisha jambo hilo ndicho kilisababisha machafuko hayo kutokea ndani ya nyumba yao.

“Umenidhalilisha sana ni wapi nitaficha uso wangu pale nitakapokutana na Daniel? Hivi huoni umenijengea uadui mkubwa sana? Kwa hilo siko tayari kukusamehe Phillip, mimi naondoka tutaonana tena kama si hapa duniani basi akhera,” aliongea Lina kwa sauti ya upole huku akifungua mlango wa sebuleni na kutoka nje.
“Nakupenda mke wangu, ni shetani aliingilia kati penzi letu na kunipa akili isiyofaa.”
“Eti shetani, usimsingizie bure huyo shetani ni wewe mwenyewe.”
“Basi nakubali mke wangu nisamehe, tafadhali rudisha penzi lako kwangu tuanze upya, tukipanga ni namna gani tufanye ili tupate angalau mtoto mmoja.”

“Phillip sahau jambo hilo halipo tena,” aliongea Lina akiingia ndani ya gari tayari kuondoka eneo hilo.
“Hatanii, nikimwacha akaondoka nitamkosa nami sipo tayari,” aliongea Phillip na haraka akili ikamjia kichwani mwake, ili kumzuia Lina ni lazima aende na kulala mbele ya lango la kutokea.
Haraka akatoka mbio na kwenda kujitupa katikati ya lango kuu la nyumba hiyo na kutulia kimya.

Wakati yote hayo yakitokea Lina akiwa ndani ya gari lake akaliwasha na kuanza kurudi nyuma kwa kasi ya ajabu bila kuangalia. Kilichofuatia ni sauti ya mayowe iliyopigwa na mlinzi wa nyumba yao.
“Mungu wangu utauaaa! Utauaaa!” ni sauti hiyo ndiyo iliyomfanya Lina afunge breki za gari kwa nguvu na kushuka kuangalia ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
“Phillip unafanya nini? Unataka nikugonge halafu nipate kesi?”

“ Bora iwe hivyo kuliko kuondoka.”
“Sikia wewe ni mtu mzima sasa tafadhali ondoka ili mimi nipite.”
“Sitaondoka hapa mpaka utakaponipa msamaha wako.”
“Unasema?”

“Lina umesikia nini, nasema sina haja ya kurudia.”
“Unacheza na mimi, wewe hufahamu kwamba siku zote ulikuwa ukiishi na mwanamke Mafia? Leo utanifahamu mimi ni nani? Naapa nitaondoka kwa nguvu wala sitanii...sasa kaa hapo ushuhudie ninavyoondoka. Pumbavu mkubwa wewe.”
***
“Kwa nini?”
“Niliwa…” alisema kijana huyo huku akitetemeka.
“Unasema?” lilikuwa ni swali kutoka kwa mzee aliyekuwepo ndani ya chumba, bila huruma akaikamata vyema bastola iliyokuwa juu ya meza, akainyosha na kulielekea paji la uso wa kijana aliyesimama mbele yake. Kwa alivyomfahamu mzee huyo hakika alikuwa hatanii alimaanisha alichokifanya, hofu ikaugubika moyo wake, akiwa haelewi nini cha kufanya akasikia kitu kama mkojo kikipenya kutoka ndani ya suruali yake.

“Nisemehe mzee wangu.”
“Nataka kufahamu ni kitu gani kiliendelea kwa watoto.”
“Hawajafa, nina hakika watakuwa hai japo hali zao sielewi zinaendeleaje?”
“Uliwapa nini?”
“Mh!” kijana aliguna.
“Husemi? Sasa nitakuonyesha mimi ni nani.”

“Hapana! Nipe muda nitakueleza.”
Mzee aliyekuwa ameiweka bastola kwenye paji la kijana aliyesimama mbele yake, taratibu huku akitabasamu akaishusha bastola hiyo chini.
“Fyuuuu!” kijana alishusha pumzi.
“Ninakupa dakika mbili tu kuanzia sasa uwe tayari kueleza kilichowapata watoto vinginevyo leo utani…” aliongea mzee huyo akiiweka vyema bastola yake.

Dakika mbili zikakatika bila kijana huyo kufungua mdomo kusema neno lolote, jambo hilo ndilo lililomtia hasira mzee aliyekuwa amesimama ndani ya chumba hicho kidogo, akasogea karibu kabisa na kuiweka tena bastola juu ya paji la kijana huyo na haikuchukua hata sekunde mbili mlio wa bastola ukasika.
“Paa! Paaa!” kicheko kikafuatia nyuma yake.

“Unacheza na mimi wewe, hivi hufahamu kwamba siku zote ulikuwa ukiishi na mwanamke Mafia? Leo utanifahamu mimi ni nani? Naapa nitaondoka kwa nguvu zangu, wala sitanii! Kaa hapohapo ushuhudie ninavyoondoka. Pumbavu mkubwa wewe,” alisema Lina huku akitembea kwa kasi kulielekea gari na kuingia ndani yake.
“Bora unikanyage nife lakini sipo tayari kukuacha uondoke, nakupenda sana Lina, mambo yote haya yaliyotokea ni Shetani tu.

“Eti Shetani? Shetani ni wewe mwenyewe, hebu ondoka mimi nipite.”
Phillip aliendelea kulala chini huku akilia, hakuwa tayari kushuhudia mwanamke aliyempenda akiondoka mbele ya macho yake. Ghafla akiwa hapo, taswira ya Genevieve mkewe ikamjia, watoto wake wawili, Dorice na Dorica nao pia wakapita kichwani mwake kama sinema kali, machozi yakazidi kumbubujika.

“Bora nife niwafuate …” alisema Phillip, safari hii kwa sauti.
“Bosi kuna kitu gani kimetokea? Mbona mnanichanganya?” mlinzi aliuliza.
“Haya mambo hayakuhusu, ni vyema ukaachana nayo na wewe kuendelea na shughuli zako.”
“Lakini mimi ni mmoja wa watu wa familia hii?”

“Ondoka kafanye kazi, husikii?” aliuliza Phillip safari hii kwa ukali.
Taratibu bila kusema kitu, alianza kutembea kuondoka eneo hilo na kusogea pembeni ambako aliendelea kutupa macho yake na kumwona Phillip akiwa bado hajabadilisha uamuzi wake wa kuendelea kulala eneo lilelile.
“Akifanya mchezo huyu mwanamke atamkanyaga kweli, kwa inavyoonekana wana ugomvi mkubwa sana hawa, lakini ni wa nini?

Mbona walitoka wote? Lakini mwanamke amerudi akiwa amejifunika shuka mwilini mwake? Mh! Hakyanani vile, kuna kitu kikubwa hapa kimetokea…” mlinzi aliendelea kuwaza kichwani mwake, yeye pia alishaanza kuhofia kibarua chake, alifahamu wazi kuwa kama kweli Lina aongeondoka, basi ajira yake ingekuwa matatani.
Akalishuhudia gari likija kwa kasi ya ajabu kuelekea eneo hilo, alipoangalia vizuri kuona kama bosi wake Phillip alikuwa ameondoka, alishangaa kumuona akiwa bado amelala eneo lilelile bila kusogea.
***
Machela iliyokuwa ikisukumwa na kuingizwa chumba cha maiti ilimtia hofu sana Victor Fedorov, kichwani mwake hakuwa na picha kamili ya nini kingefuata baada ya hapo, mawazo mengi yakaufunika ubongo wake.
“Sijui itakuwa nini? Lakini ngoja nirudi kule wodini, najua nitapata jibu kamili,” alisema mzee huyo na kuanza kutoka mbio kuondoka eneo hilo.

Kwa dakika tatu nzima, aliendelea kukimbia hatimaye akakifikia chumba cha wagonjwa mahututi, akaweka kambi hapo kusubiri mtu ambaye angetoka eneo hilo na kumweleza ukweli juu ya afya za watoto wake na nini kilitokea.
Kwa takribani dakika tano nzima, aliendelea kuketi eneo hilo, ghafla macho yake yakaushuhudia mlango wa chumba hicho ukifunguliwa na mtu aliyevalia koti jeupe akatokeza nje.
“Ni daktari,”alisema.
Mwanaume huyo akatembea kuelekea eneo alilokuwa ameketi Victor Fedorov na kumsabahi kisha kuanza kumuuliza maswali machache.

“Kama sijakosea nadhani wewe ndiye baba wa watoto wale wawili?’
“Eh! Ndiyo kabisa.”
“Naweza kufahamu umekuja na nani?”
“Mimi?”
“Ndiyo mzee.”
“Mh! Mh! Kwani kuna kitu gani daktari?”

“Ni vyema nikafahamu, umekuja hapa na nani?”
Swali hilo likaingia moja kwa moja masikioni mwa Fedorov na kwenda kugonga sehemu fulani ya ubongo wake. Akiwa hapo akanyanyua macho na kumwangalia daktari ambaye bado aliendelea kusimama pembeni akimwangalia.
“Daktari?” aliita.
“Ndiyo mzee.”

“Nieleze ukweli, nini kimetokea ndani ya chumba hicho kwani muda mfupi uliopita nikiwa hapa nimeshuhudia machela ikipitishwa hapa kuelekea chumba cha kuhifadhia maiti na juu yake kwa nilivyoona kuna mtu…”
“Si kazi yako hiyo mzee, hebu nijibu swali langu.”
Victor Fedorov hakujibu tena kitu, akainamisha kichwa chake chini, hakuwa tayari kusikia kwamba mmoja kati ya watoto wake alikuwa ameaga dunia.
“Tafadhali naomba kufahamu kuna ujumbe muhimu nataka kuutoa kwenu.”

“Ninaye mlinzi wangu kule mapokezi.”
“Tunaweza kuongozana?”
“Hakuna shida,” alijibu Fedorov akitetemeka.
Bila kuongea tena kitu chochote na daktari huyo, taratibu akaanza kutembea akimfuata nyuma. Hofu yake ikazidi kuongezeka kwani kitendo cha kuulizwa kwamba alikuja na nani hospitalini hapo kilizidi kumtia hofu, mambo mengi yakazunguka kichwani mwake bila kujua cha kufanya.

“Nitapokea majibu yoyote nitakayopewa lakini si ya vifo vya watoto wangu.”
Akiwa katika mawazo hayo ni sauti ya daktari ndiyo iliyomshtua, alikuwa akimuuliza yu wapi mtu aliyeambatana naye.
“He! Kumbe tumefika mapokezi?”aliuliza.
“Mzee akili yako iko wapi?” Daktari alimuuliza huku akimpigapiga mgongoni.
“Yule paleee!”alinyoosha kidole chake cha shahada kuelekeza eneo alilokuwa ameketi kijana mmoja, haraka wote wawili wakatembea na kufika eneo hilo.

“Habari yako?”
“Nzuri tu.”
“Nadhani wewe ni mmoja kati ya watu waliokuja na mzee huyu hapa kwetu.”
“Ndiyo, ni bosi wangu huyu.”

“Ni vyema tukaongozana wote mpaka ofisini kwangu, ningependa kuongea na ninyi kuhusu watoto waliofikishwa hapa asubuhi hii.”
“Nini kimetokea? Hali zao zikoje? Wame…” Victor Fedorov aliuliza maswali mfululizo na alipotupa macho yake kumwangalia daktari aliyesimama mbele yake, aligundua kitu fulani katika macho yake.
***
“Piiii!Piiiii!Piiiii!” ilikuwa ni honi ya gari ikipiga kuomba kupishwa eneo hilo lakini mtu aliyeonekana kulala chini bado hakushtuka wala kujitingisha.
“Mungu wangu! Mama yangu weee! Ayaaaa! Tayari ameua...” ilikuwa ni sauti ya mlinzi wa Lina akiwa pembezoni kabisa mwa kibanda kidogo karibu kabisa na lango la kutokea.
“Nakufaaaaa!” Ndiyo sauti pekee iliyosikika.
 
SEHEMU YA 39


ILIPOISHIA

“Piiii!Piiiii!Piiiii!” ilikuwa ni honi ya gari ikipiga kuomba kupishwa eneo hilo lakini mtu aliyeonekana kulala chini bado hakushtuka wala kujitingisha.
“Mungu wangu! Mama yangu weee! Ayaaaa! Tayari ameua...” ilikuwa ni sauti ya mlinzi wa Lina akiwa pembezoni kabisa mwa kibanda kidogo karibu kabisa na lango la kutokea.
“Nakufaaaaa!” Ndiyo sauti pekee iliyosikika.

SASA ENDELEA

UNAUA! Unaua! Mama yangu weee! Dah!”
Ni sauti hiyo ndiyo iliyopenya moja kwa moja masikioni mwa Lina akiwa ndani ya gari lake huku akionekana kuwa mwenye hasira nyingi, hakuwa na habari kabisa kwamba wakati anamweleza Phillip kuhusu kuondoka eneo hilo hakufanya hivyo, aliendelea kubaki palepale.
“Whaat?”(Nini?) alijiuliza baada ya kugeuka na kumwona mlinzi wake akishika mikono kichwani huku akikimbia kuelekea langoni.

Akiwa ndani ya gari huku akiwa haelewi nini cha kufanya, alimshuhudia mlinzi akiruka kutoka kwenye kibanda chake na kuruka kuelekea mbele ya gari lake.
Bila kujiuliza akashuka haraka na kuugana na mlinzi wake, akamshuhudia Phillip akiwa chini ya gari. Alipomwangalia vizuri aligundua alikuwa akilia.
“Niue! Nasema niue siko tayari kukuruhusu uondoke hapa na kuniacha peke yangu.”

Maneno yale yakapenya tena moja kwa moja masikioni mwa Lina, naye akaangua kilio kama mtoto mdogo, akainama na kupiga magoti huku akimbembeleza Phillip atoke chini ya uvungu wa gari ili waongee.
“Unasema kweli?”
“Hakika nakuambia.”
“Huwezi kunidanganya?”
“Mimi? Nakupenda sana Phillip,” aliongea Lina akimshika Phillip mkono kumsaidia kutoka chini ya uvungu wa gari.

Kwa takribani dakika tano nzima Phillip aliendelea kulala chini ya gari hata Lina alipombembeleza bado hakuwa tayari kuamini maneno yake, alichukulia kama yalikuwa ni gia ya kumtoa yeye ili apate nafasi ya kuondoka na kumwacha salama bila majeraha.
Baada ya Lina kuona ameshindwa kumtoa Phillip, aliamua kumtumia mlinzi ambaye alikuwepo eneo hilo akatumia ushawishi wake wote ili kumtoa Phillip lakini naye hakufanikiwa.
“Lina!” Phillip aliita.
“Ukitaka nitoke hapa nipatie funguo za gari.”

“Hicho tu?”
“Ukifanya hivyo naweza kutoka.”
“Basi chukua huu hapa,” Lina alijibu akinyoosha mkono uliokuwa na funguo kumwelekea Phillip ambaye aliunyakua kwa nguvu kama vile mwewe anyakuavyo kifaranga cha kuku akiwa haamini kinachotokea, akachomoza na kuketi kitako pembeni kidogo tu mwa Lina.
“Nisamehe mke wangu.”
“Nimekusamehe toka zamani sana twende ndani,” aliongea Lina akimshika Phillip mkono na kumnyanyua kutoka chini na wote wakaongozana kwenda chumbani kwao.

Walipoingia tu, Lina hakuwa na mazungumzo mengine zaidi akamkamata Phillip kwa nguvu zake zote na kuanza kumvua nguo moja baada ya nyingine huku akimmiminia mabusu motomoto na alipomaliza akazikamata pia nguo zake na kuzitupa pembeni wote wawili wakabaki kama walivyozaliwa na kazi ikawa ni moja tu.
Ndani ya chumba ni sauti pekee ya miguno na mihemo ya mahaba iliyosikika kila mmoja akionyesha ufundi wake kwa mwenzake, mara kadhaa Phillip akiendelea kumwomba mkewe msamaha kwa mambo yote yaliyotokea na kumweleza wazi kwamba alimpenda kwa dhati.

“Je, ulifanikiwa kufanya tendo la ndoa na yule mwanaume?”
“Mh!” Lina aliguna.
“Nieleze mpenzi wangu ili nitoe dukuduku lililoko ndani ya moyo wangu.”
“Kwa nini unauliza hivyo? Na kama je ilitokea nikafanya hivyo utaniacha?”
Lilikuwa ni swali gumu kutoka kwa Lina kwenda kwa Phillip ambaye alikuwa kimya juu ya kitanda mikono yake ikiendelea kuupapasa mwili wa Lina.

Kwa muda wa saa nne mfululizo bado walikuwa juu ya kitanda wakibadilisha staili kutoka moja kwenda nyingine ili mradi kila mmoja wao alikuwa akisikia raha.
“Mpenzi hebu tupumzike kidogo mwili hauna nguvu kabisa.”
“Unasema?” Phillip aliuliza.

“Nimecho…kaaa,” aliongea Lina akitetemeka.
“Bado nataka leo nikuonyesha ufundi wangu wote, nadhani utaamini maneno yangu kwamba ninakupenda.”
“Ashhhhh! Ashhhhh! Hapa…na,” Lina alizidi kulalama kitandani.
Kwa jinsi zoezi lilivyokuwa kwa Lina ilionekana ni pata shika nguo kuchanika, Phillip hakuwa tayari kumwachia Lina kwani alipania kumuonesha ufundi wake wote.

***
Victor Fedorov alisimama ndani ya chumba cha daktari akitetemeka mwili mzima, hakuelewa mpaka wakati huo ni ujumbe gani ambao daktari alikuwa akienda kuutoa kwao, hofu ya kwamba mmoja kati ya watoto wake alikuwa ameaga dunia hakuwa tayari kuupokea.
“Daktari hebu nenda moja kwa moja kwenye ujumbe wako.”
“Tafadhali naomba mketi kwanza.”
“Haipo haja, tueleze tu tukiwa wima.”

“Mh! Unajua ninyi sasa ni watu wazima yawapasa kukubali na kuelewa nini kinaendelea mpaka sasa,” Daktari aliongea na kutulia kidogo kisha kuendelea.
“Kikubwa kilichonifanya niwaite ndani ya chumba hiki ni juu ya hali za watoto wenu ambao mpaka saa wako chumba cha wagonjwa mahututi wakipatiwa matibabu lakini…”
“Fyuuuuu!” Victor Fedorov alishusha pumzi.

“Kutokana na hali zao kuwa mbaya na sisi kama madaktari tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu wote kuokoa maisha yao lakini hali inaonekana kuwa tete hivyo basi, ni vyema nikawashauri kuwahamisha kwenda katika hospitali kubwa zaidi pengine huko mnaweza kufanikiwa.”
“Daktari kwani wanawasumbuliwa na kitu gani?”
“Kwa inavyoonekana kama siyo njaa basi watakuwa wamepewa sumu.”
“Sumu?”

“Inavyoonekana.”
“Mungu wangu walitenda ubaya gani watoto hawa mpaka kustahili adhabu hiyo?” Mlinzi wa Victor Fedorov aliuliza.
“Nadhani sasa si wakati wa kuuliza hayo ni vyema mkafanya utaratibu na kuwahamisha haraka iwezekanavyo,” alimaliza daktari huyo huku macho yake yakimwangalia Victor Fedorov ambaye muda wote alinyamaza kimya akionekana mwenye mawazo mengi kichwani.

***
Central Clinical Hospital ndiyo ilikuwa hospitali iliyokuwa na sifa kila kona ya nchi ya Urusi na ilisifika zaidi kwa watendaji wake wa kazi, kuanzia madaktari, wauguzi na watu wengine wote waliofanya kazi ndani ya hospitali hiyo. Huko ndiko daktari aliyekuwa akiwahudumia watoto wa Victor Fedorov alishauri wapelekwe kwani aliamini kwamba kufika katika hospitali hiyo kungeweza kunusuru maisha ya watoto hao.
“Huko mtapata kila kilicho kizuri, madaktari, wauguzi na hata huduma ili mradi tu uwe na fedha.”

“Ahsante,” alijibu Victor Fedorov akimfuata daktari kwa nyuma mawazo yake yote yakahama kutoka eneo hilo na kwenda moja kwa moja kwa watoto wake, hao ndiyo walikuwa ni kila kitu kwake.
Maandalizi yakafanyika haraka, gari maalumu la wagonjwa likaandaliwa na watoto wakatolewa chumba cha wagonjwa mahututi huku mashine ya hewa ya oksijeni ikiwa imefungwa kwa kila mmoja wao, hakika kwa kuwaangalia iliumiza sana, walilala kimya kitandani bila kujitambua.
Victor Fedorov akashindwa kuvumilia, akamwaga machozi mfululizo.

“Haraka wapelekeni chumba cha daktari,” muuguzi aliyekuwa ameongozana na watoto wa tajiri Victor Fedorov kutoka katika hospitali ya awali kwenda Central Clinical Hospital alisema baada tu ya machela mbili zilizowabeba watoto wake kuteremshwa kutoka garini.
Kwa jinsi hali ilivyokuwa, watoto hao walihitajika kuingia moja kwa moja kwenye chumba cha daktari bila kusubiri utaratibu mwingine. Haikuchukua hata sekunde tano wakawa tayari wamewasili ndani ya chumba cha daktari.


“Nini tatizo?”
“Wagonjwa sana.”
“Naweza kufahamu nini kinawasumbua?”
Ukimya wa ajabu ukatokea, hakuna mtu aliyeweza kueleza kilichokuwa kikiwasumbua watoto hao wawili.
“Mzazi wao yupo wapi?” daktari aliuliza.
“Mimi hapa,” alijibu Fedorov kwa sauti kubwa.
“Sogea karibu.”


Huku akionesha uso uliojawa na mashaka, Fedorov alisogea karibu kabisa na daktari.
“Ndiyo, hali hii imeanza lini?”
“Ni muda wa wiki sasa daktari lakini leo hali imebadilika zaidi.”
Daktari aliyekuwepo ndani ya chumba kile alianza kumpima mtoto mmoja baada ya mwingine, mara kadhaa alitingisha kichwa chake na zoezi hilo lilipokamilika akawa anaandika maelezo fulani ndani ya mafaili ya wagonjwa. Alipomaliza alimwita muuguzi akimtaka awapeleke watoto hao kwenye wodi ya wagonjwa mahututi, zoezi hilo likafanyika mara moja.


“Daktari, watoto wangu watapona?” Fedorov aliuliza huku macho yake yote yakimwangalia daktari huyo.
“Mh!”
“Tafadhali nijibu.”
“Ah! Unajua? Lakini watapona.”
“Umeonesha hofu sana, nini kinaendelea?” Fedorov aliuliza safari hii kwa sauti ya upole. Akili yake haikufanya kazi vizuri, alihisi kama anakaribia kuwa mwendawazimu.
“Usijali, wapo katika mikono salama, watapona tu hawa,” daktari alijaribu kumpa moyo Fedorov ambaye kwa kumwangalia tu ungeweza kugundua ni kwa kiasi gani yupo kwenye mateso na maumivu makali.

Machela mbili zilisukumwa moja kwa moja mpaka chumba cha wagonjwa mahututi, daktari akawa anafuata kwa nyuma.
“Watoeni juu ya mechela na kuwalaza kwenye vitanda,” ilikuwa ni sauti ya daktari akiwapa maelekezo manesi.
Haraka zoezi hilo likafanyika, watoto wote wawili wakalazwa juu ya vitanda vyao na daktari akaanza kufanya uchunguzi kwa kila mmoja akitafuta tatizo.


Kwa muda wa takribani saa tatu na nusu, bado alikuwa akiendelea kuchunguza afya za watoto hao, vipimo kadhaa vikachukuliwa na kupelekwa maabara.
Nje ya wodi, Fedorov aliendelea kusimama, hamu yake kubwa ikiwa ni kupata taarifa kutoka ndani ya wodi, jasho jembamba lilikuwa likitiririka mwilini mwake.
“Mh! Mungu wasaidie wanangu, naamini hapa ndipo mahali ambapo watarejewa na fahamu zao na maisha yao kuendelea tena hata kama itanigharimu kia…” alisema lakini kabla hajamalizia sentensi yake, macho yake yalishuhudia mlango wa wodi ya wagonjwa mahututi ukifunguliwa, yule daktari aliyewapokea wale watoto akatokeza.


Kwa mbali akanyoosha mkono wake kwa ishara na kumwita Fedorov.
“Niambie daktari, umegundua tatizo gani?”
“Mh, baada ya kufanya uchunguzi wa kina tumegundua tatizo.
“Ahsante, ahsante sana daktari na Mungu akubariki. Je, mmegundua nini tatizo?”
“Uchunguzi tuliofanya umebaini kuwa watoto wako walipigwa na kitu kizito kichwani au walianguka kutoka umbali mrefu kwani kuna baadhi ya mishipa imepasuka na kufanya damu kuvilia kwa ndani. Hilo ndiyo hasa tatizo kubwa linalowasumbua.”


Sentensi hiyo ilipenya moja kwa moja masikioni mwa Fedorov, kumbukumbu ya namna watoto wake walivyorushwa kutoka garini na kudondoka chini kama mizigo ikamjia kichwani mwake kama sinema.
“Mzee! Mzee tafadhali ongea na mimi.”
“Mh! Inawezekana kabisa daktari lakini hilo si la muhimu sana kwangu, ninachotaka ni kuokoa maisha ya wanangu, basi.”
“Hivi ninavyoongea na wewe tayari wanaandaliwa ili kuingizwa chumba cha upasuaji tukajaribu kutoa hiyo damu iliyovilia.”


“Daktari watapona?” lilikuwa ni swali jingine kutoka kwa Fedorov, tayari daktari alishaanza kuondoka eneo hilo kurejea ndani ya chumba cha upasuaji.
“Tuombe Mungu lakini pia tutahitaji utie saini sehemu fulani ya fomu zetu ili kukubaliana na suala la wanao kufanyiwa upasuaji.”
“Nipo tayari daktari,” alijibu Fedorov huku mapigo yake ya moyo yakibadilika kwa kasi.


***
Mapumziko ndani ya chumba yalifanyika kwa dakika tano tu baada ya Lina kulia na kumbembeleza sana Phillip akidai kuwa amechoka. Baada ya dakika tano kuisha kazi ilianza upya. Phillip alitaka kuonesha kwamba alikuwa ni mwanaume wa kuotea mbali, hakika hakutaka kumpa Lina nafasi hata kidogo, jambo lililozidi kummaliza nguvu.
“Mpenzi kwa leo inatosha, tafadhali nisikilize mimi ni wako tutafanya…”
“Mwaaa!Mwaaa!” Phillip alimmwagia Lina mabusu mfululizo.

Shughuli ilikuwa pevu kwani wawili hao walicheza ‘rigwaride’ kwa saa tano, Lina akionekana kuwa taabani. Hata sauti nayo ilishakatika kwa kulalama. “Nakupenda Lina ndiyo maana nafanya yote haya.”
“Mi…mi…pi..a” alijibu Lina.
“Nataka kuona nini mwisho wake.”
“Uta..niu.a…utani..ua.”

“Nataka kukupa raha ambayo nina hakika hukuwahi kuipata, leo ndiyo leo…” Phillip alizidi kujitapa huku akimpa Lina mambo, aliendelea kufanya hivyo mpaka saa saba zilipokatika, akakubali kushuka na kumwacha Lina huru baada ya kuridhika kabisa. Lina alilala kimya kitandani, macho na miguno ndiyo vitu pekee vilivyomfanya Phillip aamini kuwa bado alikuwa hai.
“Ahhhhh!” Phillip alishusha pumzi ndefu, akasogea pembeni mwa Lina na kuketi kitako huku akimwangalia kwa jicho la husuda.


“Nakupenda sana Phillip.”
“Nakupenda pia Lina.”
“Ahsante kwa mapenzi matamu, kweli leo nimekuaminia.”
“Ha!Ha!Haaa!” Phillip alicheka huku akijifuta jasho kwa taulo lililokuwa pembeni.
“Kweli sikutanii, hapa nilipo nipo hoi bin taaban sijiwezi kabisa.”
“Ahsante mke wangu.”


“Phillip,” Lina aliita kwa sauti ya upole.
“Yes baby,” Phillip akajibu.
“Ninalo wazo kichwani mwangu.”
“Unataka kuniacha tena?”

JE NINI KILIENDELEA ???
 
SEHEMU YA 40


ILIPOISHIA

“Nakupenda sana Phillip.”
“Nakupenda pia Lina.”
“Ahsante kwa mapenzi matamu, kweli leo nimekuaminia.”
“Ha!Ha!Haaa!” Phillip alicheka huku akijifuta jasho kwa taulo lililokuwa pembeni.
“Kweli sikutanii, hapa nilipo nipo hoi bin taaban sijiwezi kabisa.”
“Ahsante mke wangu.”


“Phillip,” Lina aliita kwa sauti ya upole.
“Yes baby,” Phillip akajibu.
“Ninalo wazo kichwani mwangu.”
“Unataka kuniacha tena?” ENDELEA

NDANI ya chumba cha upasuaji kulikuwa na hekaheka, madaktari wasiopungua watano wakiambatana na wauguzi waliingia na walionekana kuwa na hamu kubwa ya kutaka kuokoa maisha ya watoto wawili pacha waliolala kitandani bila kujitambua pamoja na kwamba walikuwa wagonjwa, uzuri wao ulionekana wazi. Si madaktari wala wauguzi waliokuwa na tumaini juu ya watoto hao, lakini walitaka kujaribu.
“Watoto waandaliwe kwa ajili ya upasuaji.”

“Tayari daktari.”
“Basi hakikisheni kabla ya yote mashine za hewa ya oksijeni zifungwe ili kuwapatia hewa safi haraka sana,” ilikuwa ni sauti ya daktari mmoja aliyekuwa karibu na kitanda cha mtoto mmoja.
“Sawa daktari tunafanya hivyo.”
“Wengine wagawanyike waende kwenye mashine nyingine haraka.”
“Hakuna shida.”

Haikuchukua hata sekunde mbili tayari watoto hao midomoni mwao zilishafungwa mashine hizo ili kuwasaidia kupata hewa safi.
Mambo yote hayo yalifanyika chini ya uangalizi maalum wa madaktari wao ambao ndiyo walioshika usukani wa kuendesha kila kitu ndani ya wodi na baada ya kuhakikisha kwamba maandalizi yalitosha nao pia walijiweka sawa kwa kazi.
Vifaa vyote muhimu vilisogezwa karibu, hakika kwa kuviangalia vifaa hivyo, kwa mtu mwenye akili timamu lazima ungeingia woga.
“Ni vyema tukaanza kazi sasa, ni lazima tufanye kila kinachowezekana kuokoa maisha ya watoto hawa, ni wazuri mno kufa…sawa jamani?”

“Hakuna shida daktari lakini pia bila kumshirikisha Mungu hakuna kitakachokwenda sawa,” aliongea muuguzi mmoja aliyekuwa pembeni, naye pia alionekana kuwaonea huruma watoto hao.
Zoezi likaanza, visu na mikasi ikipita huku na kule ni jambo hilo pekee ndilo lililoonyesha kwamba watu ndani ya chumba hicho walikuwa bize kupindukia. Saa ya kwanza ikapita hatimaye ya tatu bado madaktari wakihangaikia kutoa damu iliyokuwa imevujia ndani ya ubongo wa watoto hao.

***
Nje ya wodi mambo kwa Victor Fedorov yalikuwa magumu, muda wote alikuwa akizungukazunguka huku na kule bila kutulia sehemu moja, alitaka kufahamu ni kitu gani kiliendelea ndani ya chumba, hivyo muda wote macho yake hayakubanduka kwenye mlango wa chumba cha upasuaji.
Kwa saa tano aliendelea kubaki hapo, mwisho akaanza kukata tamaa kwani hakuwepo muuguzi wala daktari aliyetoka wodini.
“Kinaendelea nini humo?” aliuliza na sauti hiyo ikapenya moja kwa moja masikioni mwa mlinzi wake, huyo ndiye aliyekuwa hapo kumfariji.

“Bosi tuwe wavumilivu nahisi kazi ni kubwa.”
“Mh! Hapana moyo wangu unahisi hatari.”
“Kama ipi?”
“Sidhani kama watoto wangu watapona tena, hakika hawataamka.”
“Hapana lakini wewe siyo Mungu, hebu tumwachie yeye kila kitu anaweza,” mlinzi wake alizidi kumtia moyo na kumfariji wakati wote.

“Uwii! Mamaaa! Wananguuuu jamani…” Fedorov aliangua kilio, uvumilivu ulionekana kumshinda kabisa.
Saa saba baadaye bado hawakuona mtu, hofu ikawafunika mioyoni mwao nao pia wakashindwa kuelewa ni kitu kilikuwa kimetokea ndani ya chumba kwani isingekuwa rahisi mpaka wakati huo asitokee mtu yeyote.
“Pengine wamepitia mlango mwingine,” aliongea Fedorov.
“Hapana mlango ni huu mmoja na kama kuna tatizo ni lazima watupe taarifa sisi wahusika.”
“Pengine wanaogopa au hawajui wataanzia wapi.”

“Bosi si rahisi, ni lazima watueleze tena bila kificho.”
“Basi tusubiri tuone,” aliongea Fedorov, tayari alishanyamaza kulia kwani maneno aliyopewa na kushauriwa na mlinzi wake yalionekana kuingia kichwani mwake.
Wakiwa katika hali ya kupigwa butwaa, wakashuhudia mlango wa chumba cha upasuaji ukifunguliwa na machela ikitolewa na nyingine ikifuata kwa nyuma, Victor Fedorov akaamini kwamba hao walikuwa ni watoto wake.

“Hao hapo,” alisema kwa sauti huku akisogea karibu kuhakikisha kama alichokuwa akikiona kilikuwa sawa au ni ndoto za mchana.
Akionekana mwenye mawazo mengi na wasiwasi, akatembea kwa unyonge na kusogea karibu lakini muuguzi aliyesukuma machela hiyo alionyesha wazi kupingana na kitendo cha Fedorov kusogea karibu huku akimweleza wazi kwamba awe mvumilivu na muda si mrefu atapewa ruhusa ya kuwaona watoto wake.
“Wanaendeleaje?” aliuliza tena.

“Majibu yote kaka utayapata kwa madaktari.”
“Wako wapi sasa?”
“Subiri kidogo utawaona,” aliongea muuguzi akizidi kusonga mbele.
Ni kweli alichokuwa ameelezwa na muuguzi, alipogeuza shingo yake kuangalia nyuma alishuhudia jopo kubwa la madaktari na wauguzi wakitoka, alipowaangalia vyema aligundua simanzi lililokuwa mioyoni mwao, naye bila kusita alisimama na kuwasubiri wafike karibu na mahali alipokuwa ili awaulize.

“Daktari, hebu nielezeni juu ya hali za watoto wangu.”
“Mh! Tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuondoa damu iliyokuwa imeganda ndani ya kichwa na kazi imekuwa ngumu sana ndiyo maana tumechukua muda wa saa saba, tunatumaini zoezi letu litafanikiwa kwa asilimia kubwa.”
“Watapona?” aliuliza Fedorov.
“Kazi yetu sisi ilikuwa ni kuondoa tatizo ambalo tumefanikiwa, mengine tumwachie Mungu…ah! Sijui unaweza kuja ofisi mara moja?” daktari alisema.

“Bila shaka,” alijibu Fedorov akiungana na madaktari kuelekea ofisini kwa ajili ya kupata maelezo zaidi.
Taratibu wakatembea na kuufikia mlango ambao ndiyo ulikuwa chumba cha daktari, akakaribishwa na kuingia huko na akaonyeshwa kiti ili aketi kwa mazungumzo zaidi.
“Kwanza pole sana mzee wetu.””Ahsanteni poleni na ninyi.”

“Ah! Sisi ni kazi yetu kuhakikisha tunafanya kila kinachowezekana kuokoa maisha ya wagonjwa,” daktari mmoja alijibu akimwangalia Fedorov ambaye aliketi pembeni, macho yake yakionesha wasiwasi mkubwa.
“Hawa mbele yako ni madaktari waliohusika na upasuaji wa watoto wako.”
“Ndiyo.”

“Kazi tumemaliza tunachosubiri sasa ni kuona kama tutakuwa tumefanikiwa.”
“Nahitaji kufahamu kama tu wataamka,” Fedorov aliuliza.
“Kuamka wataamka lakini ni baada ya saa ishirini na nne kuanzia sasa, yakupasa uwe mvulivu,” aliongea daktari mwingine.
“Saa ishirini na nne?” aliuliza kwa sauti

“SAA ishirini na nne?” Aliuliza kwa sauti.
Muda wa saa ishirini na nne ulionekana kama miaka mitatu au minne kwa Fedorov, asingeweza kuvumilia kukaa mbali na watoto wake ambao kwake ndiyo walikuwa ndugu pekee duniani.
“Daktari tafadhali naomba kwa ruhusa yako niwaone japo kidogo.”
“Mh! Kwa sheria za kidaktari haturuhusu mtu kufanya hivyo, yakupasa uwe mvumilivu mpaka baada ya saa hizo.”

“Lakini sitaweza, natamani kuwaona watoto wangu,”aliongea tena huku akibubujikwa machozi.
“Dk. Nyoshi mpatie ruhusa awaone japo kidogo tu pengine ataridhika.”
“Lakini daktari wewe mwenyewe unafahamu utaratibu wetu.”
“Najua ila nimemwonea sana huruma mzee huyu.”
“Sawa,”alijibu daktari huyo akinyanyuka kwenye kiti.

Taratibu mlango ukafunguliwa na daktari akaanza kumwongoza Fedorov kuelekea chumba cha wagonjwa mahututi.
“Daktari naweza kukuuliza tena?”
“Uliza tu hakuna shaka.”
“Nataka kujua kama watoto wangu watapona.”
“Kama nilivyokueleza mwanzo, kazi yetu sisi kama madaktari tumeifanya vizuri hiyo sehemu nyingine tumemwachia Mungu atende.”
“Fyuuu!” Fedorov akashusha pumzi kwa nguvu.

Wakaufikia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi, mapigo ya moyo wa Fedorov yakaenda mbio mithili ya mtu aliyekimbia mita ndefu, walipomaliza kufanya taratibu zote wakaingia ndani.
Baada tu ya kuingia, macho ya Fedorov yakapiga moja kwa moja juu ya vitanda viwili vikiwa vimezungukwa na mashine ya hewa ya oksijeni, machozi yakambubujika.
“Mungu wangu!”Ndiyo sauti pekee iliyosikika.

“Kuna nini?” Daktari akauliza.
“Mariya! Merina,” alitamka majina ya watoto wake akisogea taratibu kuelekea kwenye vitanda hivyo huku macho yake yakishuhudia vichwa vya watoto hao vikiwa vimefungwa bandeji na kuachwa sehemu ndogo sana upande wa macho.
“Daktari mbona kama wamevimba vichwa?”
“Ni kweli kabisa lakini vitarejea katika hali yake ya kawaida kadiri muda unavyozidi kusonga.”
“Mh!” Fedorov akaguna kuonyesha kuumizwa na hali hiyo.

Kwa takribani dakika tano waliendelea kubaki ndani ya chumba hicho, Fedorov akizunguka kitanda kimoja na kurudi kingine na mara kadhaa akitamka;
“Mungu, wasaidie watoto wangu napenda kuona wanapona…sitaki wafe nataka waishi…naomba unisaidie…”aliongea kwa sauti ya chini.

***
“Phillip,” Lina aliita kwa sauti ya upole.
“Yes baby,” Phillip akajibu.
“Ninalo wazo kichwani mwangu.”
Phillip akageuka na kuketi vizuri macho yake yote yakimwangalia mwanamke aliyekuwa amelala kitandani, hofu ikaonekana kuufunika moyo wake akitaka kufahamu ni kitu gani hasa Lina alitaka kumweleza.
“Unataka kuniacha?” Akauliza.

“Haa!Haaa!Haaa!” Lina akacheka.
“Ninakuomba usije ukanieleza kitu cha kuumiza mtima wangu.”
“Phillip hivi unadhani ni rahisi hivyo?”
“Nini?”
“Kukuacha, nikuhakikishe siwezi si kwa sababu ya penzi ulilonipa leo la hasha lakini toka ndani ya moyo wangu ninakupenda na siko tayari kukukosa katika maisha yangu.”

“Mh! Nieleze basi,” aliongea Phillip, tayari macho yake yalishabadilika na kuwa mekundu.
Lina akajivuta kutoka kitandani na kuketi karibu, akamuangalia na kuachia kuachia tabasamu.
“Kwanza naomba nikutoe wasiwasi mume wangu, ukweli ninachokueleza hapa ndiyo ukichukue na kukifanya kuwa ukweli, sikuwahi na wala sikufanya mapenzi na Daniel si kwamba sikuweza ila nakuheshimu sana…”
“Ukweli?”

“Hakika.”
“Tukiwa katika harakati hizo nilikurupuka kutoka juu ya kitanda na kukimbia ndiyo maana nilitoka na shuka tu.”
“Mwaa! Nakupenda Lina.”
“Natumai nitakuwa nimekutoa wasiwasi juu ya hilo.”
“Ni kweli kabisa lakini umeniambia unalo wazo.”
“Mh! Unajua…nitapenda uuangane na mimi katika hilo.”

“Lina niondoe jakamoyo nililonalo.”
“Nataka tukubaliane ili tushirikiane kulifanya pamoja.”
“Nimeshakueleza niko tayari kwa lolote,”aliongea Phillip kwa kujiamini.
“Phillip nimefikiria sana juu ya mtoto, wazo pekee nililonalo nimeona tutafute mtoto wa kuasili.”
“Mh!”

“Kwa sababu ya tatizo ulilonalo ili mimi na wewe tuendelee kuishi na kupendana mpaka mwisho wa uhai wetu ni bora tuasili mtoto mmoja tu.”
“Unamaanisha unachokisema.”
“Hakika nimefikia hapo ili kulinda penzi letu.”
“Lina!” Phillip aliita.
“Na iwe hivyo.”

“Jinsia gani?” Phillip aliuliza.
“Chagua wewe.”
“Hapana.”
“Mimi binafsi napenda mtoto wa kike sijui wewe?”
“Hata mimi,” Lina alijibu na kumpiga Phillip mabusu mfululizo.

Takribani sekunde tano, Phillip alibaki kimya akizungusha akili yake, hakuwa tayari kukubaliana na maneno aliyoyasikia kutoka kwa mkewe Lina.
“Lina nimeamini kwamba kweli unanipenda, ahsante mke wangu ninaungana na wewe asilimia zote na ninakuahidi kulitunza penzi letu hadi mwisho Mungu akiwa mlinzi wetu, sipendi na wala sitaki kukuudhi tena...” alimaliza Phillip akiachia mabusu mfululizo.
Ghafla kama mshale uliofyatuliwa, akamkamata Lina na kumlaza tena kitandani na wote kujifunika shuka gubigubi, kilichofuata baada ya hapo kilikuwa hakielezeki wala hakiandikiki gazetini.

Zoezi hilo lilipokamilika Phillip akamshukuru Lina akimweleza wazi kwamba angeshirikiana naye bega kwa bega kukamilisha mkakati wao wa kupata mtoto wa kumuasili.
“Kesho tutaanza taratibu zote, nataka ndani ya mwezi huu tupate mtoto wetu ambaye tutamlea vyema nasi tuingie katika ulimwengu wa kuitwa baba na mama.”
“Ahsante mke wangu, ahsante kwa kunipenda.”
“Nakupenda pia.”

Je, nini kitaendelea? Watoto Mariya na Merina watapona? Phillip na Lina je, watafanikiwa kupata mtoto wa kuasili?
 
SEHEMU YA 41


Ghafla, kama mshale uliofyatuliwa, Phillip anamkamata Lina na kumnyanyua juu, anamlaza tena kitandani na wote wanajifunika shuka gubigubi, kinachofuata baada ya hapo hakielezeki.
Wanakubaliana kuwa siku inayofuata wafanye taratibu zote na kuzikamilisha ili wampate mtoto wa kuasili. Walikuwa na hamu kubwa ya kuitwa baba na mama.

Baada ya kufikia muafaka wa kuasili mtoto ambaye wangemlea vyema na kumtunza katika maadili ya Kitanzania.
Wanaendelea kucheza kitandani mpaka usingizi unawapitia.
Upande wa pili, watoto wa tajiri mkubwa nchini Urusi, Victor Fedorov wapo hospitali na bado hali zao ni tete.
Wanakaa kwa zaidi ya saa sabini na mbili bila kuzinduka. Hali hiyo inamtia shaka baba yao, Fedorov na haamini kama wanaweza kutoka ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi wakiwa hai.
Je,nini kitaendelea? SONGA NAYO…

“HA! ” Ilisikika sauti ya mtu akiguna ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi ambako watoto wawili mapacha, Mariya na Merina walikuwa wamelazwa.
“Kuna nini tena?” mwingine aliuliza.
“Ameamka huyu! Ameamka.”
“Mungu wangu! Kweli jamani.”

Jopo lote la madaktari pamoja na wauguzi waliokuwa ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi walisogea karibu na kitanda.
“Chafya!”
“Mh! Kweli, hakyanani vile pacha mmoja ameamka na kupiga chafya.”
“Kweli Mungu mkubwa,” alisema mmoja wa madaktari.
“Kwa jinsi hali inavyoendelea, hata huyu mwingine ataamka muda si mrefu.”
“Ona! Amefumbua na macho.”

“Kweli,” daktari mwingine alijibu na wote wakatabasamu.
Dalili iliyokuwa imeoneshwa na pacha mmoja ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi, ilimfurahisha kila mtu. Hofu iliyokuwa imeanza kutanda katika mioyo yao ikaondoka na matumaini mapya yakafufuka.
Hakuwepo hata mtu mmoja aliyetaka historia mbaya juu ya upasuaji huo wa watoto iandikwe.


“Hebu tuendelee kusubiri, tukiangalia nini kitaendelea kwa huyu pacha mwingine, naye ataamka muda si mrefu.”
Maongezi yaliendelea ndani ya chumba hicho kila mmoja akisema lake juu ya upasuaji huo. Saa ya kwanza ikapita, matumaini ya pacha mwingine kuzinduka yakawa yanazidi kuongezeka, waliamini kwamba muda si mrefu naye angeamka.

“Daktari ni vyema tukatoa taarifa kwa mzazi wake juu ya nini kinaendelea humu ndani,” alisema muuguzi mmoja.
“Hakuna shida anaweza kupata kibali cha kuingia na kujionea mwenyewe.”
Muuguzi mwingine akatembea na kufungua mlango wa kutokea ndani ya chumba hicho, akatokeza nje na kwa ishara akamwita mzee aliyekuwa ameketi chini pembeni ya mlango wa kutokea ndani ya chumba hicho kwa ishara.
“Samahani kidogo tunakuomba,” sauti ya muuguzi ilipenya katika masikio ya mzee yule ambaye alikua ametawaliwa na uso wa huruma.

“Mh! Nini tena watoto wangu wameamka?” alihoji huku akinyanyuka.
“Tafadhali tunakuomba mara moja.”
Taratibu bila kusema kitu tena mzee yule akatembea na kuufikia mlango kisha kuuliza tena swali kama alilouliza mwanzo.
“Muuguzi nini kimetokea?”
“Hakuna matatizo kuna habari njema kwako.”

“Oh! Habari njema? Watoto wameamka?” Aliuliza.
“Mh! Ni mmoja lakini mwingine bado.”
“Hapana, kwa nini iwe hivyo?”
“Utapata maelezo yote ndani ya chumba hiki, tafadhali ingia ndani na ufuate taratibu zetu,” muuguzi alisema na kuanza kumwongoza Fedorov kwenye chumba maalum.

Mbele kidogo Fedorov akapewa maelezo kisha kuvishwa nguo maalum ambazo ilizivaa na kuingia ndani ya chumba hicho.
Baada ya zoezi hilo kukamilika alianza kumfuata muuguzi ambaye alimwongoza moja kwa moja mpaka kwenye wodi ambayo alishuhudia umati wa wauguzi na madaktari ukiwa pembeni ya vitanda kila mmoja akionesha furaha.
“Pole sana mzee wetu,”
“Mh!” badala ya kujibu Fedorov aliguna tu na taratibu akasogea katika moja ya vitanda ambavyo juu yake ndipo walipolala watoto wake Mariya na Merina.

“Mmoja wa pacha amepata fahamu zake japo bado hajaweza kusema kitu.”
“Yupi?”
“Huyo hapo.”
“Mariya!” Fedorov akamwita kwa sauti na kusogea karibu zaidi akiwa hapo akashuhudia mtoto huyo akifumbua macho kwa tabu kisha kuyafumba, machozi ya furaha yakamtoka akainama na kumbusu kwenye paji lake la uso huku akiongea.


“Nakupenda sana mwanangu nataka wote mtoke turejee nyumbani kuendelea na maisha, sipendi mniache, wewe umeamka lakini Merina bado…ahsante Mungu kwa kujibu sala zangu, sijui ningekuwa mgeni wa nani katika dunia hii, ahsanteni pia madaktari kwa kazi nzuri.”

“Usijali kikubwa tunachoomba ni huyu mwenzake naye aamke,”
“Tii! Tiii!” mlio ndani ya chumba ukasikika na kuwafanya watu wote wageuke kuangalia upande ulipotokea mlio huo.
Ilikuwa ni mashine ya hewa ya oksijeni iliyokuwa imefungwa kwa mtoto Merina ikionekana kusimama.
“Mungu wangu mashine inataka kusimama...”

***
“Ahsante mke wangu, ahsante kwa kunipenda.”
“Ahsante nawe pia.”
Safari ya kuelekea ofisini ikaanza furaha ya Phillip ikionekana wazi na mara kadhaa alikuwa akimgeukia Lina na kumweleza wazi kwamba alimpenda kupita maelezo.
Nusu saa tu baadaye waliingia ofisini na kila mmoja kuingia mzigoni lakini vichwa vyao vilionekana kufikiria juu ya kesho yake, kwani walitaka kumaliza mambo hayo haraka sana.

“Rafiki leo unaonekana una furaha sana, hebu niambie unafurahia kitu gani?” Rafiki mmoja wa Lina aliuliza.
“Maisha, hakuna kitu kingine, pia nimempata mume anayenipenda kwa dhati.”
“Mh! Mshukuru Mungu wako, mimi natamani kupata mume kama wako.”
“Wee huko unakoelekea siko, usije ukaja…” aliongea Lina lakini kabla ya kumalizia sentensi yake rafiki yake akaingilia kati.

“Ahaa! Rafiki siwezi bwana, Phillip ni shemeji yangu na atabaki kuwa hivyo maisha.”
“Unanitia mashaka, unamsifia mno…haa!Haaa,” Lina aliongea na kuachia tabasamu lililoambatana na kicheko.
Aliyekuwa ndani ya ofisi ya Lina alikuwa ni rafiki yake wa siku nyingi waliyesoma naye chuo Kikuu na hatimaye walijikuta pamoja tena katika ofisi moja lakini kila mmoja akiwa kwenye kitengo chake.
Walipendana na kuheshimiana kwa kila kitu na huyo ndiye aliyekuwa msiri wake mkubwa, halikuwepo jambo lililoendelea kati yake na Phillip na rafiki huyo asilifahamu.

“Mimi natoka nilikuja kukusalimu tu kwani ni muda sijakutia machoni.”
“Ahsante,” alijibu Lina kwa kutabasamu.
Saa zikazidi kusogea na hatimaye muda wa kutoka ukawadia, Lina akakusanya kila kilichokuwa chake, kabla ya kutoka ndani ya ofisi akanyanyua simu yake na kubonyeza namba kadhaa, baada ya muda akaonekana akizungumza na mtu upande wa pili.

“Darling muda wa kuondoka umefika, nakuja kukupitia hapo sasa hivi, twende nyumbani tukampumzike,” alisema na kukata simu kisha akaanza kutembea kutoka ndani ya ofisi yake.
Baada ya sekunde tatu tu alishafika nje ya mlango wa ofisi ya mumewe, akaugonga mlango.
“Karibu,” sauti iliskika wakati alipokamata kitasa cha mlango na kufungua mlango, macho yake yakatua kwa Phillip aliyekuwa ameketi ofisini kwake akionesha tabasamu.

“Twende nyumbani tukampumzike kesho tunatakiwa kuwahi mapema sana kituo cha Msimbazi kukamilisha kazi.., sawa?” alisema Lina akionesha kumsisitiza Phillip ambaye hakuwa na hiyana, akakusanya vitu vyake kisha akanyanyuka na kutoka nje kuelekea nyumbani.
Kwao usiku ulionekana kwenda taratibu mno, saa zikisonga pole pole lakini hatimaye asubuhi ikafika na wote wakajiandaa kwa safari, Phillip akiwa ndiye dereva.

Saa moja na nusu walifika katika kituo cha Msimbazi na kuelekea kwenye ofisi ya sista mkuu aliyewapokea na kuwakaribisha ndani ya ofisi ambako walikuta taratibu zote zimeshaandaliwa na mwanasheria aliyekuwa akiwasubiri.
Baada tu ya utambulisho mfupi sista mkuu akawaomba waanze utaratibu ili kwenda na wakati, wakapewa fomu maalum Phillip na mkewe wakaisoma vyema na kuielewa kisha wakatakiwa kuijaza kwa ufasaha.
Kwa takribani dakika kumi nzima walifanya zoezi hilo na walipolikamilisha wakairejesha tena kwa sista mkuu ambaye akawauliza kama wameyakubali masharti yote yaliyoandikwa ndani ya fomu hiyo.

“Tunakubaliana na yote yaliyoandikwa humo na tuko tayari kumtunza na kumlea mtoto tutakayemchukua hapa kwa nguvu na juhudi zetu zote, tunahakikisha atapata maisha anayostahili.”
“Basi ni wakati wa ninyi kula kiapo mbele ya mwanasheria wetu.”
“Sawa sista,” walijibu kwa pamoja na baada ya muda wakala kiapo na zoezi hilo lilipokamilika sista mkuu akauliza walihitaji mtoto wa jinsia gani na umri wake.

“Kuanzia miezi mitatu na awe wa jinsia ya kike.”
Sista hakuongeza tena neno lingine, akawataka wamfuate, akawaongoza mpaka kwenye chumba kimoja kilichokuwa karibu kabisa na ofisi yake.
Akawakaribisha na kuwaingiza ndani ambako kulikuwa na watoto wadogo wakiwa wamelala kwenye vitanda na wafanyakazi wachache wakiwa hapo kuwaangalia.

Hapo walitakiwa kuchagua mtoto mmoja tu ambaye ndiye wangemchukua na kwenda kumtunza mpaka mwisho wa uhai wake, wakafumbua macho yao yote kuwaangalia watoto hao ambao kwa kweli walikuwa wazuri mno.
“Mnachagua mmoja tu,” sista mkuu aliongea akitabasamu.
“Mh! Watoto wote wazuri sijui tuchukue yupi kati yao,” Lina alimuuliza Phillip.

“Huyu hapa anafanana na sisi,” alisema Lina.
“Sawa…sista huyu ndiye tuliyemchagua,”
aliongeza Phillip akimnyanyua mtoto mzuri aliyekuwa amelala kitandani, alikuwa ni mdogo lakini uzuri wake ulionekana wazi

MAMBO hayakuwa kama walivyotarajia kwamba baada ya saa kadhaa mtoto huyo angeamka na kuungana na mwenzake, saa ya kwanza ikapita na sasa ilikuwa ikielekea ya pili, Victor Fedorov uvumilivu ukaanza kumshinda akajikuta akimwaga machozi kama mtoto mdogo, kazi ya wauguzi ndani ya chumba ikawa ni kumtuliza wakimtaka awe mvumilivu.
“Lakini ni muda mrefu sana mbona mwenzake amesharejewa na fahamu?” aliuliza akisogea karibu kabisa na kitanda cha pacha ambaye hakuonyesha dalili yoyote ya kuamka.
“Ataamka, kuwa mvumilivu.”

“Mbona kama ni upasuaji umefanyika kwa saa sawa iweje yule aamke na huyu bado?” bado aliendelea kuuliza maswali mfululizo.
“Tafadhali tunaomba sasa mzee utupishe tuendelee na matibabu yetu tutakuwa tukikujulisha kila kitu kadiri muda unavyokwenda tunaomba uende nje,” aliongea daktari mmoja, muuguzi aliyekuwa karibu na Fedorov akamshika mkono na kumwongoza kutoka nje naye pia akijaribu kuongea maneno ya kumpa faraja.

Mzee huyo akatoka akilia, mawazo na akili zake zote zilikuwa juu ya mtoto wake huyo ambaye hakuonyesha matumaini, akatembea hatua ya kwanza na ya pili kisha akageuka nyuma kuangalia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi.
“Sitakwenda popote nitakaa hapahapa mpaka mwisho nataka kujua nini kinaendelea,” aliongea Fedorov akiketi chini, akiwa hapo haikupita hata sekunde tatu mlinzi wake naye akaungana naye, pia akijaribu kumfariji mzee huyo lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu.

“Naumia, moyo wangu una wasiwasi mkubwa sana juu ya mtoto wangu…sijui kama ataamka…lakini kama kuna kitu kibaya kwa nini wanifiche? Nataka wanieleze ukweli ili nijiandae kwa tatizo linalokuja,” aliongea akibubujikwa machozi.
“Hapana bosi hawezi kufa, Mungu mkubwa anatenda.”
“Najua hilo lakini kwa sasa nimekata…….”
“Hutakiwi kukata tamaa unachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuamini kwamba naye pia ataamka, mimi ninaamini kwamba yuko katika mikono ya madaktari bingwa atapona tu.”
“Mh! Labda hebu tuone,”aliongea Fedorov akijifuta machozi.

***
“Mnachagua mmoja tu,” sista mkuu aliongea akitabasamu.
“Mh! Watoto wote wazuri sijui tuchukue yupi kati yao,” Lina alimuuliza Phillip.
“Huyu hapa anafanana na sisi.”
“Sawa…sista huyu ndiye tuliyemchagua.”

Mabusu mfululizo yakatua kwenye paji la mtoto waliyemchukua, alikuwa ni mtoto wa jinsi ya kike, pamoja na kuwa mtoto mdogo uzuri wake ulionekana wazi, rangi ya ngozi yake ilifanana kabisa na ya Phillip, furaha ya ajabu ikatawala, hakuwepo hata mtu mmoja kati yao aliyeamini kwamba sasa wangekuwa wakiitwa baba na mama wa mtoto waliyemuasili kutoka katika Kituo cha Msimbazi.
“Tutamlea na kumtunza mpaka mwisho wa uhai wetu tukimpatia kila aina ya mahitaji,” Phillip aliongea akimwangalia sista mkuu.
“Ombi letu kwenu ninyi ni hili hapa,” sista aliongea.
“Ndiyo sista tunakusiliza.”

“Tutakuwa tukihitaji kumtembelea mtoto huyu kila baada ya mwezi mmoja kujua na kufahamu anaendeleaje, hiyo ni moja ya sheria zetu mpaka atakapofikisha umri wa miaka kumi na nane ambapo tutakuwa huru kumwacha aendelee na maisha yake kwani atakuwa ni mtu mzima.”
“Hilo halina shaka sista na kama inawezekana tunaweza tu kuongozana mpaka nyumbani.”
“Nitawapa mtu ambaye mtaongozana naye mpaka huko kwa ajili ya kupafahamu na kama kutatokea mabadiliko yoyote yawe ya kuhama nyumba au kwenda nje ya nchi ni vyema mkatujulisha mapema, sawa?” sista mkuu aliuliza.

“Tumesikia,” Phillip na Lina walijibu kwa pamoja na kuanza kutoka nje ya chumba kuelekea ofisini kwa sista mkuu ambako wangekamilisha taratibu zote kisha kuondoka na mtoto waliyekuwa naye.
Taratibu maalum zikafanyika ikiwa ni pamoja na kupigwa picha na kutia saini kwenye makubaliano yote yaliyofanyika ofisini kisha wakakabidhiwa mtoto na sista mmoja ambaye wangeongozana naye mpaka mahali wanapoishi. Wakatoka na kumshukuru sista kisha kutembea kuelekea sehemu waliyokuwa wameegesha gari, Phillip ndiye alikuwa dereva na Lina aliketi kiti cha nyuma akiwa amempakata mtoto.

Gari liliendeshwa na kwa muda wa saa moja tu walifika nyumbani kwa Phillip na Lina wakamkaribisha sista waliyeongozana naye wakimweleza wazi kwamba hapo ndipo palikuwa nyumbani kwao ambako mtoto waliyekuwa wamemwasili angeishi maisha yake yote akitunzwa na kulelewa vyema.
“Karibu sana sista hapa ndipo nyumbani kwetu ambako mtoto huyu atalelewa na kuishi, akitunzwa kwa hali na mali.”
“Mh! Ahsanteni sana nafurahi kupafahamu tutakuwa tukija kila mwezi kumtembelea ili kujua maendeleo yake.”
“Karibuni sana.”

Dakika kumi na tano baadaye sista aliyeongozana na Phillip na Lina aliaga na kuondoka akiahidi kurejea tena baada ya mwezi mmoja kujua hali ya mtoto huyo. Wakamsindikiza kisha akaondoka.
Kwa siku nzima walishinda ndani ya nyumba wakipanga mipango yote na jinsi ya kumlea na kumtunza mtoto huyo. Lina akatoa wazo kwamba ni vyema wangemtafuta mfanyakazi wa ndani ambaye angekuwa tayari kumlea mtoto huyo na wao wangemlipa mshahara ambao angeutaka.

“Ni lazima atafutwe mtu wa kumlea mtoto huyu kwa upendo wote,” Lina aliongea.
“Kabisa, lakini nashauri awe mtu mzima kidogo.”
“Jinsi ya kumpata sasa ndiyo tatizo, sijui tuanzie wapi?”
“Hebu subiri kidogo,” Phillip aliongea akinyanyuka kitini kuelekea chumbani.

je nini kiliendelea
 
SEHEMU YA 42


ILIPOISHIA

Dakika kumi na tano baadaye sista aliyeongozana na Phillip na Lina aliaga na kuondoka akiahidi kurejea tena baada ya mwezi mmoja kujua hali ya mtoto huyo. Wakamsindikiza kisha akaondoka.
Kwa siku nzima walishinda ndani ya nyumba wakipanga mipango yote na jinsi ya kumlea na kumtunza mtoto huyo. Lina akatoa wazo kwamba ni vyema wangemtafuta mfanyakazi wa ndani ambaye angekuwa tayari kumlea mtoto huyo na wao wangemlipa mshahara ambao angeutaka.

“Ni lazima atafutwe mtu wa kumlea mtoto huyu kwa upendo wote,” Lina aliongea.
“Kabisa, lakini nashauri awe mtu mzima kidogo.”
“Jinsi ya kumpata sasa ndiyo tatizo, sijui tuanzie wapi?”
“Hebu subiri kidogo,” Phillip aliongea akinyanyuka kitini kuelekea chumbani.

SONGA NAYO

PHILLIP alitembea moja kwa moja na kuelekea mlango wa chumba chao akaingia na haikumchukua hata sekunde tatu tayari akawa amerejea akamsogelea Lina aliyekuwa ameketi bado sebuleni akimsubiri.
“Soma hapa,” shika hiki kipande cha gazeti halafu nitakuonyesha kitu.
Lina bila kusema kitu akionyesha kushangazwa na mumewe akanyoosha mkono wake na kupokea kipande hicho kisha kutulia akisikiliza maelekezo.

“Ndani ya kipande hicho kuna tangazo la kampuni inayowatafutia watu wafanyakazi wa majumbani.”
“Mh! Wewe ulikitoa wapi na ulijuaje kama tunaweza kutafuta mfanyakazi siku moja?” Lina aliuliza akiachia tabasamu.
“Si unajua tena sisi watu wenye upako huwa tunaona vitu mapema sana kabla…,” aliongea Phillip akimwangalia Lina na kuachia tabasamu.
Lina akakodoa macho yake na kuanza kusoma kipande hicho cha gazeti, ghafla akakutana na tangazo hilo akalisoma kwa umakini wa hali ya juu mpaka mwisho na kukutana na namba za simu kwa ajili ya mawasiliano kama tu mtu angehitaji mfanyakazi.

“Mh! Hili liko safi tena wako wa aina mbili kike na kiume sijui yupi mume wangu?” Aliuliza Lina.
“Wewe acha utani wako mwanaume wa nini hapa ndani ataweza kulea kweli?”
“Anaweza kwani si sheria na masharti tu.”
“Hapana tutafute wa kike,” aliongea Phillip akijilaza kwenye sofa.

Lina akanyoosha mkono wake na kuchukua simu yake ya mkononi kisha kuanza kubonyeza namba kadhaa na kuweka simu sikioni, haikumchukua hata sekunde mbili tayari upande wa pili ukasikika.
“Ndiyo naitwa Lina napiga simu kutoka hapa hapa Dar es Salaam, nimesoma tangazo lenu na nahitaji kupata mfanyakazi wa ndani ambaye umri wake ni mkubwa kidogo atakayeweza kulea vyema mtoto mdogo,” alimaliza Lina.
“Hakuna shida dada yupo anapatikana sijui unamhitaji kwa lini?”

“Hata leo ikiwezekana.”
“Basi ni vyema ukatueleza wewe unapatikana wapi nasi tutakuja moja kwa moja nyumbani kwako na watu wawili kisha wewe utamchagua mmoja,”
“Sawa.”
Zoezi hili likawa limekamilika Lina akatoa maelekezo ya jinsi ya kufika nyumbani kwao na watu hao wakakubaliana naye na kumweleza wazi kwamba baada tu ya nusu saa wangefika nyumbani hapo.

“Unajua nini mke wangu?”
“Mh!”
“Ubongo wangu unazunguka kuhusu majibu ambayo tutawapa watu wakitaka kufahamu juu ya huyu mtoto wetu tuliyemwasili?”
“Mume wangu siku zote huwa watu hawakosi cha kusema wataongea na kujiuliza maswali mengi sana juu ya mtoto wetu lakini mwisho watanyamaza, hili litabaki kuwa jambo la familia na si vinginevyo.”

“Mwaa! Mwaa! Mwanamke una akili sana wewe,” Phillip aliachia mabusu mfululizo kwenda kwa Lina ambaye naye aliyapokea kwa bashasha huku akinyanyuka na kutembea kwa madaha kuelekea sebuleni kumwangalia mtoto mchanga aliyekuwa amelala.
“Bado amelala huyu,” sauti ya Lina ilisikika kutoka chumbani.
“Basi njoo tuendelee kuongea hapa tukisubiri wageni.”
“Sawa nakuja lakini mume wangu jambo moja hatujalifanya bado.”

“Lipi hilo?” Phillip aliuliza kwa kutahamaki.
“Hatujampa jina mtoto wetu.”
“Hebu anza wewe kutoa la kwako,” Phillip alimwambia Lina.
“Wewe kama baba wa familia unatakiwa useme na mimi nitafuata.”

“Kutoka ndani ya moyo wangu mimi napenda sana mtoto huyu aitwe Genevieve.”
“Saaaafi!” Lina aliongea kwa sauti.
Hiyo pekee ilitosha kabisa kuonyesha kwamba jina hilo lilikuwa limepita moja kwa moja bila kipingamizi kwa pamoja wakanyanyuka na kukimbilia chumbani alikolazwa mtoto.

***
“Nashauri huyu mtoto afanyiwe CT-Scan kuangalia tena upya mfumo mzima wa kichwa chake huenda kuna tatizo ambalo halikuonekana wakati wa upasuaji wa mwanzo,” aliongea daktari mmoja ndani ya chumba baada ya kuona kwamba hali ilikuwa si nzuri kwani saa nyingi zilishapita na tumaini la kurejewa na fahamu kwa mtoto mwingine halikuwepo.
“Huo ni uamuzi mzuri.”
Haraka akapandishwa katika machela na kuanza kusukumwa kuelekea kwenye chumba ambacho kipimo hicho kingefanyika na kutoa picha kamili ya tatizo ambalo lingeonekana.

Mchakato mzima ukafanyika haraka picha ikachukuliwa na majibu hayakuchukua muda mrefu sana yakarejeshwa tena kwa madaktari ambao waliisoma vyema ripoti hiyo.
“Mungu wangu!”
“Nini tena?”
“Mh! Haya majibu nakosea au nasoma sawa?”
“Ni sawa kabisa daktari hivyo ndivyo yalivyo.”

“Kwa hiyo?”
“Hatuna jinsi ni lazima tufanye tena upasuaji ili kumsaidia huyu mtoto vinginevyo atakufa.”
“Kwani kilitokea nini mpaka kuacha bonge hili la damu?”
“Huu si wakati wa kulaumiana ni wakati wa kuokoa maisha ya mtoto huyu jamani mimi nashauri maandalizi yafanyike haraka sana na kazi ianze mara moja.”
“Mzazi wake je?”

“Ni lazima apewe taarifa na akubali jambo hili vinginevyo atampoteza mtoto wake.”
“Sawa aitwe na kuelezwa kila kitu.”
Muuguzi mmoja akatoka mbio na kumwita Fedorov akimtaka aingie ndani ya chumba ili kuongea na madaktari dakika moja tu baadaye watu wawili wakaingia ndani alikuwa ni muuguzi na Fedorov bila kupoteza muda daktari mmoja akamweleza wazi kwamba ililazimu mtoto wake arejeshwe tena chumba cha upasuaji haraka ili kuokoa maisha yake kwani picha iliyochukuliwa ilionyesha wazi kwamba kulikuwepo tatizo na kama tu wangezidi kumchelewesha basi asingeamka milele.

“Mungu wa…ngu…sa…fari hii..hatapo…” Fedorov aliongea kwa sauti ya kukatikatika huku machozi yakumbubujika, macho yake yakashuhudia machela ikisukumwa haraka kutoka nje ya wodi hiyo kuelekea chumba cha upasuaji.

MTOTO aliyeingia katika maisha ya Phillip na Lina na kupewa jina la Genevieve alikuwa ameleta furaha kubwa sana katika ndoa hiyo, kwani walimpenda kupita kawaida wakihakikisha wanampatia kila kilichohitajika katika maisha yake.
“Genevieve, hatimaye jina hili limerudi tena katika maisha yangu,” alitamka Phillip kwa sauti ya juu.
“Naam, hilo ndilo litakuwa jina lake.”

“Ahsante Lina hii itakuwa kumbukumbu kwa mpenzi mke wangu ambaye aliondoka duniani nikiwa bado nampenda, mtoto huyu ameziba kabisa pengo lake.”
“Ninafurahi pamoja na wewe mume wangu, siku zote haja ya moyo wangu ni kukuona unayo furaha kama hii,” Lina aliongea akitabasamu.
“Nitampenda mtoto huyu mpaka kufa.”
“Naungana na wewe lakini ninalo swali moja kwako Phillip.”

“Endelea.”
“Nataka kujua kama utanipenda kwa dhati kama ilivyokuwa mwanzo.”
“Lina! Hakika nakuhakishia kutoka moyoni mwangu kwamba ninakupenda mno.”
“Ahsante kwa penzi lako Phillip, hebu twende chumbani mara moja,” aliongea Lina huku akimwangalia mumewe na kuachia tabasamu. Ni Lina aliyekuwa wa kwanza kusimama na kumsogelea mumewe kisha kumshika mkono na kumnyanyua kutoka kitini wote wakaanza kutembea kuelekea chumbani.

Kilichoendelea ndani ya chumba hakika kilikuwa hakielezeki wala kuandikika gazetini, kwani miguno na mihemo ya kila aina iliendelea kwa muda wa saa nne mfululizo, kilichowashtua hapo ilikuwa ni sauti ya honi ya gari nje ya lango lao, kwa sababu walifahamu kwamba mlinzi alikuwepo kwa kazi hiyo wao waliendelea na shughuli zao.
“Lina sasa inatosha bwana.”

“Hapana, mimi bado sijachoka.”
“Wewe mtoto ataa…” aliongea Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake wakasikia sauti ya mlango ukigongwa.
“Bosi! Bosi kuna wageni hapa,” sauti ya mlinzi ilisikika.
“Nenda wewe mimi mpaka nikaoge.”

“Sawa hakuna shida mke wangu,” Phillip aliongea huku akisogelea bukta yake iliyokuwa pembeni kisha akaiweka mwilini na taratibu akafungua mlango na kutembea kuelekea sebuleni ambako alifungua mlango na kukutana na sura ngeni za watu watatu na mtu wa nne akiwa mlinzi.
“Karibuni,” aliongea.
“Ahsante sana, nadhani hatujakosea, hapa ndiyo nyumbani kwa Phillip.”
“Ni kweli kabisa karibuni sana.”

“Oke, sisi ni wale watu mliotupigia simu muda mchache uliopita mkihitaji mfanyakazi tuko hapa.”
Wakaingia ndani na mlinzi kurejea sehemu yake ya kazi, haikuchukua hata sekunde tatu Lina naye akaungana nao sebuleni, mazumgumzo maalum yakaanza na hatimaye wakatakiwa kuchagua mtu mmoja kati ya wawili waliokuwepo hapo.
“Sisi tunamchagua huyu hapa,” waliongea karibu kwa pamoja.

“Hakuna shida hata sisi tulipendekeza huyuhuyu.”
“Karibu sana mama sijui unaitwa nani?”
“Naitwa Magdalena Simon, mwenyeji wa Rukwa na nimezaliwa miaka arobaini na saba iliyopita.”
“Mh !” Phillip na Lina wakaguna, mwanamke huyo alikuwa ni mtu mzima si kwa mtoto mdogo tu bali hata kwao.
“Mama utaweza kazi ya kulea mtoto kweli? Na je wewe katika maisha yako ulibahatika kupata mtoto?” Lina aliuliza akikodoa macho kumwangalia mwanamke huyo.

“Mh! Mh! Hapana !” mwanamke huyo alijibu na walipomwangalia vyema usoni mwake waligundua alikuwa akibubujikwa machozi.
“Basi mama sisi tunakupokea kwa mikono miwili ukae nasi na ulee mtoto wetu umpe mapenzi yote.”
“Ahsante.”

Makubaliano yakafanyika wakatakiwa kulipa kiasi cha fedha ambacho ndicho mwanamke huyo alitolewa kwao na wakamshukuru mtu aliyemleta mfanyakazi huyo huku akiwaeleza wazi kwamba angekuwa karibu nao kwa kila kitu kuhakikisha hapatokei tatizo lolote. Wakaaga na kuondoka.

Wakampokea bibi Magdalena na kumwonyesha mambo yote yaliyomstahili ndani ya nyumba hiyo ikiwa ni pamoja na chumba ambacho angekitumia muda wote ambao angeishi hapo. Baada ya zoezi hilo wakamtaka aingie jikoni kuandaa chakula cha jioni hiyo ikiwa ni kama jaribio la kwanza kisha wao wakarejea chumbani.
***
Upasuaji wa pili ulikuwa umefanyika kwa ufanisi wa hali ya juu na madaktari wakihakikisha halijirudii tena tatizo kama lililotokea mwanzo wakiomba Mungu mtoto huyo mzuri anyanyuke na kuendelea na maisha.
“Tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa, sasa atolewe humu na kurudishwa chumba cha wagonjwa mahututi.”

“Sawa daktari,” wauguzi waliitikia, na bila kuchelewa machela ikaanza kusukumwa kutoka nje ya chumba ambako walimkuta Fedorov akiwa amesimama.
“Oh! My God !” aliongea mzee huyo kwa sauti ya juu baada ya kuona bandeji iliyotapakaa damu ikiwa imefungwa kuzunguka kichwa cha mtoto wake.
Machela ikapitishwa na wauguzi ambao hawakuongea kitu chochote zaidi ya neno moja tu.

“Pole sana mzee.”
“Ataamka baada ya saa ngapi?”
“Saa kumi na mbili kuanzia sasa.”
“Mh!” Fedorov aliguna hakika kwa kumwangalia tu mzee huyo ungegundua tu kwamba tayari alishachoka moyoni na tumaini lote lilishapotea katika maisha yake, mpaka kufikia hapo kwa umri aliokuwa nao hakuwahi kukutana na changamoto kubwa kama hiyo.

Machela ikasukumwa na kuingizwa chumba cha wagonjwa mahututi pembeni tu ya pacha mwenzake ambaye kwa wakati huo tayari alishaanza kufungua macho na kuuliza maswali kadhaa japo kwa taabu akitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea.
Victor Fedorov akatakiwa kusubiri nje ya chumba hicho kwa muda mwingine wa saa kumi na mbili.je nini kitaendelea? tukutane
 
SEHEMU YA 43


ILIPOISHIA

“Saa kumi na mbili kuanza sasa.”
“Mh!” Fedorov aliguna hakika kwa kumwangalia tu mzee huyo ungegundua kwamba tayari alishachoka moyo na tumaini lote lilishapotea katika maisha yake mpaka kufikia hapo kwa umri aliokuwa nao hakuwahi kukutana na changamoto kubwa kama hiyo.

Machela ikasukumwa na kuingizwa chumba cha wagonjwa mahututi pembeni tu ya pacha mwenzake ambaye yeye kwa wakati huo tayari alishaanza kufungua macho na kuuliza maswali kadhaa japo kwa taabu akitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea.
Victor Fedorov akatakiwa kusubiri nje ya chumba hicho kwa muda mwingine wa saa kumi na mbili.
Je, nini kinaendelea hapa? Mtoto atapona na kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya tatizo kuondolewa? SONGA NAYO…

“Paa! Paa! Paaa!” Ulikuwa ni mlio wa bastola ndani ya chumba kidogo chenye mwanga hafifu na mzee mfupi aliyejazia misuli akiwa amesimama mbele ya kijana mmoja akionekana mwenye hasira kali.
“Usiniu…naomba uni…”
“Unasema?”
“Tafadhali mzee wangu kama ni huo mgawo wangu basi mimi nakuachia zote lakini wewe pia ufikirie maisha yangu.”

“Ha! Haaaa!” Sauti ya kicheko kikali ikasikika tena mzee aliyesimama mbele ya kijana huyo huku akiwa amenyoosha bastola akashuka mkono wake na kuanza kutembea kumfuata mahali alipokuwa.
“Simama,” alitamka kwa sauti ya ukali.
“Mh!”
“Ina manaa hujaelewa, nasema simama upesi.”

Kijana yule bila kusema tena kitu akaanza kujivuta kutoka sakafuni na aliposimama tu wima vitu kama maji maji vilionekana kuchuruzika kutoka ndani ya suruali yake kwenda chini.
“Hee! Umejikojolea?”
“Nisamehe mzee wangu si kusudio langu ni bahati mbaya.”
“Unaumwa?”
“Hapana ni woga tu.”

“Lakini wewe ni mtoto wa kiume unatakiwa kuwa shupavu.”
“Mh!” Kijana huyo alibaki akiguna tu huku akiwa amekodoa macho yote kumwangalia mzee huyo.
Kwa ishara akaongozwa ili kusogelea meza ambayo juu yake ilikuwa na begi.
“Fungua,” mzee huyo aliamuru.

Taratibu kijana akalisogelea begi na kuanza kulifungua huku akionyesha hofu nyingi machoni mwake. Kwa sekunde tatu tu tayari alishamaliza kulifungua na idadi kubwa ya noti ikaonekana ndani yake.
“Tayari mzee,” aliongea kwa sauti ya upole.
“Sawa kabisa, sasa nisikilize vyema tena kwa umakini mkubwa,”
“Ndiyo mzee.”

“Kwa kuwa umeonyesha kufanya kazi vyema na mimi tena kwa ujasiri wa hali ya juu nikiamini kabisa kwamba hakukuwa na madhara yoyote yaliyotokea juu ya watoto, basi nakupa mgawo huu, uende ukaanze maisha na kumbuka mtu aliyesimama mbele yako si mtu mzuri hata kidogo, upande wake wa pili unatisha sitasita kutoa uhai wako pale utakapokuwa umenisaliti au kufanya jambo tofauti na kiapo chetu, mambo yote yaliyotokea ndani ya chumba hiki ilikuwa ni kukupima imani, nilitaka kujua jinsi unavyoweza kuhimili vishindo.”
“Ndiyo mzee.”

“Una hakika watoto wako salama? Nisingependa kusikia watoto wamekufa kwani hawana hatia hata kidogo, mwenye hatia ni baba yao ambaye nitashughulika naye mwenyewe.”
“Mh! Mzee sina uhakika ila watakuwa wazima.”
“Haya kamata hii halafu utokomee nisikuone mbele ya macho yangu,”aliongea mzee huyo akimkabidhi kijana maburungutu ya noti yasiyopungua kumi. Akazungusha macho yake huku na kule ndani ya chumba hicho na kufanikiwa kuona mfuko mmoja mchafumchafu, huo ndiyo aliutumia kuweka fedha zake zote alizokabidhiwa muda mfupi uliopita akamshukuru mzee huyo na kuanza kutembea kuelekea nje.

“Kumbuka hutakiwi kusema kitu chochote juu ya maisha yangu, sawa?”
“Sawa mzee hakuna shida.”
“Tumia fedha hizo kuendeleza maisha yako, hivi sasa wewe ni mtu mzima.”
“Ahsante mzee wangu nami pia nakutakia maisha mema, utakapokuwa na shida usisite kunitafuta...,” aliongea kijana huyo akitokomea.

Hivyo ndivyo Ditrov alivyoagana na kijana huyo kisha kwa kujiamini kabisa akatembea kulisogelea begi lililokuwa juu ya meza akalinyanyua na kumwaga fedha zote juu ya meza.
“Yap! Federov alikuwa hajui anacheza na mtu wa aina gani, hajui kwamba sisi tulishatangulia zamani, sasa asubiri kisasi changu ni lazima nitamtenda ubaya…,” aliongea Ditrov kwa kujiamini.

***
Upasuaji ndani ya chumba ulifanyika kwa umakini mkubwa na hatimaye wakafanikiwa kulitoa bonge la damu lililokuwa limengandamiza ubongo wa mtoto Merina, wakarudisha kila kitu katika sehemu yake na wakamtoa kumpeleka chumba cha wagonjwa mahututi huku akiwa amefungiwa mashine ya hewa ya oksijeni ili kumsaidia kuvuta hewa safi.
Muda wote huo Fedorov bado alikuwa nje ya mlango wa chumba hicho akizunguka huku na kule.

“Ametoka!” alitamka baada tu ya kuona machela ikisukumwa kutoka ndani ya chumba cha upasuaji kutolewa nje.
“Mzee tumefanikiwa kuondoa damu iliyoonekana na tunaamini sasa mtoto ataendelea vizuri lakini yahitaji saa kumi na mbili tena kupata fahamu zake,” aliongea daktari na machela ikasukumwa moja kwa moja chumba cha wagonjwa mahututi Fedovor akitakiwa kusubiri mpaka muda huo ufike na angepewa taarifa zote.

Nje ya chumba hakutulia kabisa, alitaka kufahamu kila kitu kilichoendelea ndani ya wodi mara kadhaa akitupa macho kwenye saa yake ya mkononi kuangalia wakati hatimaye mpaka wakati huo saa kumi na mbili zilishapita hivyo mbele yake alikuwa na saa mbili tu muda alioelezwa na madaktari ufike na mtoto wake Merina kurejewa na fahamu. Macho yake yaliendelea kushuhudia wauguzi na madaktari wakitoka na kuingia kama vile walipeana zamu ndani ya chumba huku naye hofu ikimgubika likiwa limebaki saa moja tu mbele yake.

***
“Baba! Baba!” Aliita kwa sauti iliyosikika ndani ya chumba.
“Mh!” muuguzi ndani ya wodi aliguna kuonyesha mshangao wa ajabu kwani kitendo alichokishuhudia hakikuwa cha kawaida mtoto Mariya alikuwa amenyanyuka na kuketi kitako kitandani.
“Amemwita baba yake,” waliongea wakisogea karibu na kitanda alichokuwa mtoto huyo.”
“Unajisikiaje?” walimuuliza.

“Merina! Merina”
“Unaitwa nani?”
“Namtaka baba yangu…Merina uko wapi?” aliongea mtoto huyo huku akinyanyua mikono yake na kushika kichwa chake akakutana na bendeji kubwa, hiyo ndiyo ilimfanya azidi kulia.
“Baaaaba!” akapaza sauti.

“Namtaka baba yangu…Merina uko wapi?” aliongea mtoto huyo huku akinyanyua mikono yake na kushika kichwa chake akakutana na bendeji kubwa, hiyo ndiyo iliyomfanya azidi kulia zaidi.
“Baaaaba!” akapaza sauti.
“Hebu mwiteni baba yake aje hapa haraka, hatakiwi kuongea muda mrefu kutokana na hali yake,” daktari aliongea kwa msisitizo na muuguzi akaonekana akitoka nje huku akikimbia.

“Mzee tafadhali tunakuomba ndani ya chumba.”
“Mh! Tatizo jingine tena,” aliongea tajiri Federov akinyanyuka kutoka chini alipokuwa ameketi, taratibu akatembea na kuingia ndani ya chumba ambako aliongozwa moja kwa moja mpaka mahali watoto wake pacha walipokuwa wamelala juu ya vitanda.
Kwa macho yake akamshuhudia Mariya akiwa ameketi juu ya kitanda na alipotokeza tu mtoto huyo akaita tena kwa sauti ya juu.
“Babaaa!”

“Mwanangu, umeamka?”
“Sogea karibu yangu baba.”
Fedorov akasogea kisha akainamisha kichwa chake karibu kabisa na mwanaye, hapo akaachia mabusu mfululizo huku naye akilia.
“Nini kimetokea baba? Kwa nini niko hapa? Merina, je, yuko wapi?”
“Mh!” Watu wote ndani ya chumba waliguna. Hakukuwa na jibu kamili la kumpa Mariya kwamba pacha mwenzake alikuwa mgonjwa taabani muda mfupi uliopita.

“Nataka kumwona Merina,” Mariya alizidi kusisitiza huku akizungusha kichwa chake huku na kule ndani ya chumba kama vile alikuwa akitafuta kitu fulani.
Kwa nusu saa nzima walikuwa wamejaribu kumnyamazisha Mariya lakini ilionekana kushindikana, ni hapo ndipo daktari aliposhauri mtoto huyo aelezwe ukweli kwani kutokana na afya yake hakutakiwa kupata msongo wa mawazo ili kunusuru matatizo mengine yasitokee kwenye upasuaji wake wa kichwa.
“Merina,” Fedorov aliita.

“Mh!”
“Merina yule pale, yeye bado hajaamka.”
“Hajaamka? Kwa nini kalala mpaka sasa?”
“La hasha si usingizi wa kawaida bali anaumwa.”
“Anaumwa nini?” Aliuliza huku akizungusha mikono yake kushika sehemu ya kichwa.
“Mwanangu hata wewe ni mgonjwa na hapa tulipo tupo hospitalini kwa muda sasa.”

“Ina maana tunaumwa wote?”
“Huo ndiyo ukweli.”
“Basi nataka niende kumwona, si mmesema ndiye yule pale,” aliongea Mariya akielekeza kidole upande aliokuwa ameonyeshwa.
Daktari aliyekuwa ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi akatakiwa kutoa ushauri kwani ili mtoto huyo anyamaze, ilikuwa ni lazima asogezwe mpaka karibu na kitanda cha pacha wake.
“Kwa sababu kitanda kina magudurumu kisogezwe taratibu kwa uangalifu mkubwa mpaka pale ili akamwone mwenzake, nadhani baada ya jambo hilo ataacha kulia.”

Ushauri uliotolewa na daktari ukafuatwa, taratibu kitanda kikaanza kusukumwa kuelekea eneo ambako kulikuwa na kitanda kingine ambacho juu yake alilala Merina akiwa hajitambui kabisa.
“Huyu hapa Merina.”
“Maskini wa Mungu kilitokea nini baba?”
“Mlipata ajali mbaya, hiyo ndiyo iliyosababisha ninyi nyote kuwa hapa mkiwa mmeumia vibaya.”

“Ajali! Baba!” Aliongea Mariya lakini kabla hajaenda mbali zaidi tukio zima la jinsi walivyotekwa na mwanaume wasiyemfahamu kisha kuwafungia mahali ambako walipata mateso wakiwa hawana chakula wala maji liliingia kichwani mwa Mariya kama sinema.
“Baba na yule aliyetufunga vitambaa na kutupakiza ndani ya gari kisha kuturusha kama…” kwikwi ya kulia ikamkaba, alikumbuka kila kitu kilichotokea siku nyingi nyuma.
“Nyamaza kulia mwanangu hayo yote yalishapita cha muhimu ni afya zenu.”

“Lakini baba mbona mimi nimeamka na Merina bado, kwa nini?”
“Huyu alipatwa na tatizo ambalo ilibidi afanyiwe tena upasuaji kwa mara ya pili lakini ataamka muda si mrefu.”
“Napenda iwe hivyo, sipendi kumkosa nampenda mno,” aliongea Mariya akionyesha msisitizo.
Baada ya mazungumzo hayo walimsihi arejeshwe sehemu alikokuwa lakini alionekana kugoma akisisitiza kubaki eneo hilohilo mpaka mwenzake aamke ili aongee naye.

“Nitakaa hapahapa mpaka aamke, nataka kuongea naye, najua anasikia ila kujibu tu ndiyo tatizo…Merina! Merina tafadhali amka mimi Mariya nakuita… nakupenda sana, pia baba yuko hapa naye anataka kuona umeamka ili uongee nasi tunakumi…,” aliongea mtoto huyo kwa uchungu jambo lililowafanya wauguzi na madaktari waliokuwepo ndani ya chumba nao walengwe na machozi.
Wakiwa katika mawazo hayo ghafla jambo lisilokuwa la kawaida likatokea.
“Mh! Mh!” Ilikuwa ni sauti ya mguno kutoka kwa Merina, tayari zilishatimia saa kumi na mbili tangu atoke chumba cha upasuaji, watu watu wote wakaonekana kupigwa butwaa.
JE NINI KILIENDELEA?
 
SEHEMU YA 44


ILIPOISHIA


“Nitakaa hapahapa mpaka aamke, nataka kuongea naye, najua anasikia ila kujibu tu ndiyo tatizo…Merina! Merina tafadhali amka mimi Mariya nakuita… nakupenda sana, pia baba yuko hapa naye anataka kuona umeamka ili uongee nasi tunakumi…,” aliongea mtoto huyo kwa uchungu jambo lililowafanya wauguzi na madaktari waliokuwepo ndani ya chumba nao walengwe na machozi.
Wakiwa katika mawazo hayo ghafla jambo lisilokuwa la kawaida likatokea.
“Mh! Mh!” Ilikuwa ni sauti ya mguno kutoka kwa Merina, tayari zilishatimia saa kumi na mbili tangu atoke chumba cha upasuaji, watu wote wakaonekana kupigwa butwaa.

SASA ENDELEA

MIAKA mitatu baadaye furaha ikiendelea kutawala ndani ya familia ya Phillip na mkewe Lina, mtoto Genevieve akiendelea kukua vyema mara kadhaa wawakilishi kutoka kituo cha Msimbazi cha kulelea watoto walikwenda nyumbani kwa Phillip kufuatilia maisha aliyoishi mtoto huyo, walionyesha furaha na kumshukuru Mungu kwani alipata mapenzi yote ya baba na mama.
“Hakika Genevieve amekuwa binti mkubwa sasa.”

“Sisi pia tunamshukuru Mungu kwa afya na baraka anazompa mtoto huyu.”
“Amina,” aliongea Sista Maryjoyce.
“Lakini pia anasoma shule nzuri sana mtoto wetu.”
“Ah! Inaitwaje?”

“Inaitwa FEZA huko ndiko tumeona inafaa na tunashukuru hata walimu pia wanatupa ushirikiano mzuri sana.”
“Hakika mtoto huyu alikuwa anasubiri ujio wenu katika kituo chetu, hebu mwone nadhani anajua jinsi mnavyompenda.”
“Hata sisi tunaona hivyo, tunaomba tu tuendelee kumwona akikua vyema.”
“Hizo ni baraka za kila mzazi mwenye watoto.”

Waliongea mengi huku wakiburudika kwa vinywaji, masista hawakusita kutoa sifa zao kwa familia ya Phillip wakimwombea kwa Mungu azidi kuwa na moyo huo mpaka mwisho. Baada ya mazungumzo hayo kwa sababu saa zilikuwa zimesonga sana wakaomba ruhusa ya kuondoka kurejea kwenye makazi yao, wakakubaliwa na kuondoka.
Genevieve hakuwa mbali na mahali walipokuwa wameketi hivyo alipoona tu watu wakinyanyuka vitini alifahamu wazi kwamba walikuwa wakiondoka kitendo ambacho hakukipenda hivyo kuangua kilio.
“Usilie mtoto mzuri tunakupenda tutakuja tena kukutembelea siku nyingine, sawa?” Sista MaryJoyce aliongea akimbembeleza Genevieve.

***
Mapenzi yote ya Phillip yakatoka kwa Lina na kuhamia kwa Genevieve, alitumia muda mwingi kukaa na mtoto huyo kuliko ilivyokuwa kwa mkewe jambo ambalo lilianza kuleta matatizo kwani Lina pia akitaka apate nafasi kwa mumewe.
“Mume nami pia nahitaji mapenzi yako unanishangaza sana kutwa kucha wewe na mtoto tu… huna tena muda wa kuwa nami,” Lina aliongea siku moja wakiwa wameketi bustanini nje ya nyumba yao.

“Lina yaani unasikia wivu hata kwa mtoto wetu? Mke wangu jamani si hivyo kumbuka ni mtoto huyu huyu aliyekuwa akitugombanisha mimi na wewe, tafadhali mpatie naye nafasi mbona mimi silalamiki pale unapomchukua na kutoka naye?”
“Ah! Unajua nini?”
“Mh!”
“Naona kama umenisahau sana, maana kila ukitoka na kurudi mkononi umebeba zawadi zake tu mimi ah!”

“Haa!Haa!Haaa! Lina huo ni wivu tu mke wangu achana nao hebu tushirikiane kumlea mtoto wetu bwana, Mungu ametubariki ametupa mtoto mzuri kweli kweli huyu akikua atakuwa tishio, nitashikia watu bastola.”
“Mh! Haya ngoja tuone itakuwaje, mwaa!mwaa!” Lina aliongea akisogea karibu na Phillip kisha kumwachia mabusu kwenye paji lake la uso.
“Ahsante! Mwaaa, hebu twende ndani kwanza mara moja” Phillip naye akajibu kwa busu huku akimtaka Lina waingie ndani.
“Kufanya nini?”

“Nasema hivi twende ndani.”
“Mtoto je?”
“Atabaki na Magdalena hana shida.”
“Na wewe,” Lina aliyemfahamu Phillip kupita maelezo aliongea kwani mara kadhaa alipomtaka kwenda ndani basi lazima kulikuwa na jambo.
“Hivi wewe umenielewa nakuhitaji ndani haraka sana,” Phillip aliongea akionyesha msisitizo na tayari alishaanza kupiga hatua kuondoka eneo hilo.

Lina bila ubishi naye akaanza kufuata nyuma akiwa na mtoto alipoingia tu sebuleni akamkabidhi mtoto kwa Magdalena kisha naye kufuata nyayo kuingia chumbani.
“Funga mlango kwa funguo,” alitamka Phillip.
“Unataka kunipiga?”
“La hasha mwanamke huwa hapigwi kwa ngumi na mateka, anapigwa kwa kipande cha khanga lakini wewe sitakupiga hivyo nita…” Phillip aliongea huku akimvuta Lina na kumtupia juu ya kitanda.

***
Miezi mitatu baadaye tayari afya za watoto wawili pacha Mariya na Merina zilikuwa zikindelea vizuri hatimaye wakawa wameruhusiwa kurejea nyumbani wakitakiwa kuhudhuria kliniki zao kila baada ya mwezi mmoja ili kuwaangalia kwa ukaribu.
“Ahsanteni madaktari na Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya watoto wangu, sijui ningekuwa mgeni wa nani hapa duniani bila ya kuwa na watoto, utajiri wangu wote usingekuwa na maana, hakika ninawapenda sana wanangu,” aliongea Fedorov akichomoa burungutu la fedha na kuwapa madaktari pamoja na wauguzi kama ahsante kwa jinsi walivyojitoa kwake.

“Ah! Mzee hakuna haja sisi ndiyo kazi yetu bwana.”
“Najua ndiyo kazi yenu lakini hii si rushwa nawapa soda tu jamani ndugu zangu, tafadhali pokeeni vinginevyo nitajisikia vibaya sana.”
Mabishano yakawa yametokea kwa muda wa dakika tano nzima, wakipiga hatua hiyo ya Federov kutoa fedha mfukoni mwake na kuwapatia lakini aliposihi na kubembeleza sana hatimaye walizipokea na kumshukuru.

Utaratibu maalum ukafanyika na watoto wakachukuliwa kupelekwa nyumbani ambako furaha iliendelea, akawapokea tena na kuwakaribisha wao pia walikuwa na furaha lakini zaidi ya yote walitaka kufahamu ni kitu gani kilisababisha mpaka wakawa katika hali ile.
“Wanangu ni historia ndefu sana sioni kama kuna haja ya kuwasimulia…nadhani mtaumia na nisingependa jambo hilo litokee tena, kwa ushauri wa madaktari hamtakiwi kupata kitu kitakachowafanya mfikirie sana.”
“Basi baba hakuna shida lakini tunalo ombi moja kwako.”

“Ombi gani tena?”
“Tunataka kuendelea na shule ikiwezekana hata kesho.”
“Hakuna shida mpumzike kwa muda wa wiki moja hivi halafu wiki inayofuata mtaanza tena shule.”
“Ahsante baba tunakupenda sana,” waliongea Mariya na Merina kisha kunyanyuka vitini na kumsogelea baba yao, wakamkumbatia na kuanza kububujikwa machozi.

MIAKA kumi na tano baadaye.
Maisha nyumbani kwa tajiri Victor Fedorov yaliendelea, Mariya na Merina walisahau kabisa mambo yote yaliyotokea maishani mwao.
Kilichotawala katika familia hiyo kilikuwa ni upendo, furaha na amani. Fedorov alihakikisha anafanya kila kitu kuwapa furaha watoto wake.
Akiwa ameketi na Mariya na Merina, aliwaeleza kwamba maisha hayakuwa rahisi kama walivyofikiria hivyo kuwataka wasome kwa bidii ili nao wapate kitu ambacho kitaongoza maisha yao.

“Nataka msome tena kwa bidii nami nitawaunga mkono kwa kila jambo, sawa wanangu?”
“Ndiyo baba nasi hatutakuangusha.”
Watoto hao kwa sababu walimpenda sana baba yao walijitahidi kufanya kila kilichokuwa kizuri ili wasimtie aibu, kwani walipata kila kitu walichohitaji.
Hakika walijivunia kuwa na baba kama Fedorov bila kufahamu kwamba nyuma yake hakuwa mtu mzuri, alikuwa mtu hatari aliyeogopwa na kila mtu.

“Nitahakikisha watoto hawa hawagundui jambo lolote linalohusu maisha yao na yangu,” aliongea Fedorov akisogelea kabati kubwa lililokuwa ndani ya chumba na kulifungua, taratibu akionekana mwenye wasiwasi mwingi akachomoa kitu kama faili na kuketi kitako juu ya kitanda.
Kwa umakini wa hali ya juu akaanza kusoma karatasi moja baada ya nyingine. Lilikuwa ni faili lenye siri kubwa ambayo aliamini kabisa kwamba hakuwepo mtu yeyote aliyefahamu siri hiyo.
“Maskini wa Mungu,” aliongea akigeuza shingo yake huku na kule na alipohakikisha kwamba hapakuwa na mtu aliyemwona akasogea tena mpaka kabatini na kulirejesha faili na kufunga mlango.

“Nitahakikisha hakuna mtu hata mmoja atakayefahamu umafia nilioucheza, itabaki kuwa siri yangu tu.”
Maneno aliyokuwa ameapa Fedorov yalimaanisha alichokisema lakini yeye kama mwanadamu hakufahamu kabisa kwamba maisha yake yalikuwa mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Alikuwa amefanikiwa kuficha siri kwa kuua watu wote waliofahamu umafia alioutenda.
Ndani ya faili alilolihifadhi kabatini, kuliandikwa kila kitu jinsi alivyofanikiwa kuteka watoto wawili yaani Mariya na Merina kutoka Tanzania na kuwafikisha nchini Urusi huku akihakikisha wanafutwa kumbukumbu zote na kuwafanya wamtambue yeye kama baba yao, jambo ambalo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa lakini pia mauaji ya Ditrov na wenzake ili kuficha mpango mzima wa utekaji nyara.

Pia kulikuwa na wosia mzito juu ya mali na fedha zote alizokuwa nazo akiagiza kama litatokea lolote basi huo ndiyo urithi kwa watoto wake hao. Alipohakikisha kila kitu kimekwenda sawa, akapanda kitandani na kujilaza.
***
Kilichokuwa kinasikika ndani ya chumba kwa wakati huo ni kelele za kitanda tu, kwa zaidi ya saa tatu mfululizo Phillip na mkewe Lina walikuwa wakiwajibika ipasavyo.
“Leo ndiyo leo asemaye kesho ni mwongo, Lina ukweli nakupenda kutoka ndani ya moyo wangu na furaha hiyo imeongezeka zaidi baada ya mtoto wetu Genevieve kuingia ndani ya familia yetu…mwaaa”.

“Ahsante Phillip nami pia ninakupenda kuliko maelezo ndiyo maana sikuwaza kukusaliti hata mara moja, ingawa nilikuwa na uwezo huo.”
“Mh! Usiseme hivyo mke wangu ni shetani tu, nilitamani kuitwa baba.”
“Nami nililifahamu jambo hilo mapema ndiyo maana nikapata wazo la kuasili mtoto na kweli umekubali na sasa tunaye Genevieve.”
“Nitampenda mtoto huyu mpaka mwisho, sipo tayari kuona akiteseka wakati nikiwa hai, sasa ni wakati wa mimi na wewe kufanya kazi kwa bidii ili mtoto aishi maisha ya kifalme baadaye au?”

“Umesema kweli mu…” Lina alishindwa kumalizi sentensi yake, kigugumizi kikaonekana kumkamata.
Waliendelea kubaki ndani ya chumba kwa muda mwingine wa saa mbili na kutimiza saa tano kamili.
“Mume wangu sasa inatosha ni vyema tukatoka kwenda kumwangalia mtoto wetu ametumisi sana jamani.”
“Umesema kweli kabisa lakini ni lazima nasi tupate nafasi kama hii.”
“Ahsante nimeamini kwamba kweli unanipenda.”

“Saaana!” Phillip aliongea akinyanyuka kitandani kuelekea bafuni kuoga.
Hayo ndiyo yakawa maisha yao wakifurahia mtoto aliyeingia ndani ya familia yao, wote wakiamini kwamba ameleta upya furaha katika nyumba yao, kila mmoja akiahidi kumpenda na kumtunza kwa hali na mali lakini mapenzi ya Phillip yalionekana wazi kwa sababu mtoto huyo alipewa jina la marehemu mke wake.
“Hatimaye Genevieve amerudi tena katika maisha yangu…,” aliwaza kichwani mwake akitoka ndani ya chumba kuelekea sebuleni.
“Phillip nimekumbuka jambo moja.”

“Lipi tena hilo?”
“Kesho ni siku ya kutembelea makaburi ya ndugu zetu kuangalia na kuyaweka safi, sijui unakumbuka?”
“Mh! Ahsante sana kwa kunikumbusha, ndiyo maana Mungu amenipa mwanamke kama wewe, hakika unajali.”
Ilikuwa ni kama desturi kwa Phillip kutembelea makaburi ya mke na watoto wake kufanya ibada kisha kufanya usafi ikiwa ni ishara mojawapo ya kuwaenzi.

***
Tayari Mariya na Merina walishatimiza umri wa miaka kumi na nane na walihitimu elimu yao ya chuo kikuu, walitamani sana kufanya kazi lakini msimamo wa baba yao ulihitaji waendelee kusoma zaidi ili waje kuongoza makampuni aliyokuwa nayo, hivyo walitakiwa kupumzika kidogo kisha kuendelea na masomo ya juu zaidi.
“Nataka muendelee kusoma zaidi ninyi ndiyo warithi wangu, mtapumzika kidogo halafu mtaendelea na masomo sijui mnataka kwenda nchi gani kwa mapumziko?”

“Mh! Baba tunataka tukae hapahapa na wewe, hatuwezi kwenda mbali na upeo wa macho yako.”
“Basi sawa na ni zawadi gani mnapenda?”
“Mh! Gari aina ya Ferrari.”

“Wow! Wazo hilo ndilo lilikuwa akilini mwangu, nilitaka kuwafanya miongoni mwa mastaa mjulikane ulimwengu mzima kama mimi ninavyojulikana.”
“Ahsante baba kwa mapenzi unayotuonyesha, hakika unatupenda.

JE NINI KILIENDELEA
 
SEHEMU YA 45


ILIPOISHIA

Tayari Mariya na Merina walishatimiza umri wa miaka kumi na nane na walihitimu elimu yao ya chuo kikuu, walitamani sana kufanya kazi lakini msimamo wa baba yao ulihitaji waendelee kusoma zaidi ili waje kuongoza makampuni aliyokuwa nayo, hivyo walitakiwa kupumzika kidogo kisha kuendelea na masomo ya juu zaidi.
“Nataka muendelee kusoma zaidi ninyi ndiyo warithi wangu, mtapumzika kidogo halafu mtaendelea na masomo sijui mnataka kwenda nchi gani kwa mapumziko?”

“Mh! Baba tunataka tukae hapahapa na wewe, hatuwezi kwenda mbali na upeo wa macho yako.”
“Basi sawa na ni zawadi gani mnapenda?”
“Mh! Gari aina ya Ferrari.”

“Wow! Wazo hilo ndilo lilikuwa akilini mwangu, nilitaka kuwafanya miongoni mwa mastaa mjulikane ulimwengu mzima kama mimi ninavyojulikana.”
“Ahsante baba kwa mapenzi unayotuonyesha, hakika unatupenda.

ENDELEA

TAYARI ilikuwa imeshatimia miaka kumi huku mtoto Geneveive akikua vyema na akiendelea na masomo yake katika shule ya Feza, mapenzi mema aliyopewa na wazazi wake wawili yalimfanya ajisikie mwenye furaha sana.
Phillip na Lina walimtunza na kumfanyia kila lililo jema wakihakikisha hapungukiwi na kitu chochote maishani mwake.
“Phillip ni vyema sasa tukamweleza mtoto huyu siri ambayo tumeiweka ndani ya mioyo yetu kwa muda mrefu.”
“Lina!” Phillip alimwita mkewe kwa mshangao.

“Ni lazima siku moja aje kuufahamu ukweli mume wangu.”
“Najua hilo lakini si sasa, bado umri wake ni mdogo, anahitaji kukua zaidi.”
“Mh! Haya kumbuka lakini sisi ni binadamu lolote linaweza kutokea.”
“Lina tafadhali achana na fikra potofu,” aliongea Phillip huku akimwita Genevieve asogee karibu yake.
Alihakikisha mtoto huyo anapata mapenzi ya dhati kutoka kwake na mkewe, hakuwa tayari kuona mtoto huyo akiumia wala kuumizwa na mtu mwingine.

“Nakupenda sana mwanangu.”
“Ahsante baba yangu nakupenda pia.”
“Genevieve mimi pia ninakupenda,” aliongea Lina akiachia tabasamu mdomoni mwake.
Hayo ndiyo yakawa maisha yao ndani ya nyumba, kuonesha mapenzi ya dhati kwa vitendo na maneno kwa Genevieve huku wakiitunza siri ya kwamba hawakuwa wazazi wake wa kumzaa bali walimuasili kutoka katika kituo cha watoto Yatima cha Msimbazi.

Waliendelea kubaki sebuleni kwa mazungumzo wakiongea na kufurahi pamoja, mara kadhaa wakimsisitiza mtoto Genevieve umuhimu wa shule, wakimtaka asome kwa bidii kwani elimu ndiyo ulikuwa urithi wake mkubwa katika maisha yake ya baadaye.
“Chakula tayari karibuni mezani,” ilikuwa ni sauti ya mfanyakazi wa ndani, Magdalena akiwakaribisha mezani kwa ajili ya chakula, wakamshukuru na kusogea mezani.

Saa mbili baadaye walishapumzika vya kutosha na mmoja baada ya mwingine wakaaga na kuingia ndani ya vyumba vyao kupumzika kwa ajili ya siku iliyofuata, Lina na Phillip nao wakiingia ndani ya chumba chao.
“Mke wangu kusema ukweli ninakupenda sana.”
“Mimi pia nakupenda Phillip sikuwahi kumpenda mwanaume mwingine maishani mwangu kama ilivyokuwa kwako.”
“Ahsante kwa kunipenda lakini ninataka kukueleza kitu kimoja.”

“Kitu gani?”
“Ninapokuwa na wewe hivi huwa sichoki kufanya tendo la ndoa na wewe, nakuhitaji kila wakati mke wangu…mh! Unajua nini?...hebu sogea hapa…” aliongea Phillip kwa sauti ya kutetemeka huku akimvuta Lina upande aliokuwa ameketi yeye.
“Mh! Mh! Bwa…na” aliongea Lina kwa sauti ya chini chini huku akisogea kumfuata mumewe.

***
Mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwa watoto wake alihakikisha wanayafaidi maisha yote mazuri, akiwapa kila kitu muhimu maishani, hivyo, baada ya maongezi yao kukamilika na watoto kuhitaji zawadi ya gari kama ambavyo baba yao alivyowauliza aliahidi kuwatafuta gari hilo ndani ya saa ishirini na nne tu.

Saa sita zikakatika watoto Mariya na Merina wakimsubiri baba yao kwa hamu kubwa, ghafla wakasikia sauti ya honi nje ya lango la kuingia ndani ya nyumba yao, haraka wakanyanyuka kwenye viti kuelekea langoni ambako mlinzi alishafungua kuruhusu gari kuingia.
“Gosh!” walijikuta wakitamka maneno hayo.
Mbele ya macho yao yalishuhudia gari aina ya Ferrari ambalo walilihitaji ndani yake kukiwa na mwanaume mmoja aliyejazia misuli, akaliendesha na kuliingia ndani kisha kuliegesha sehemu maalum na kushuka.

“Naitwa Ford niko hapa kwa maelezo ya bosi Fedorov,” aliongea mwanaume huyo.
Mariya na Merina hawakujibu kitu chochote macho yao yalikuwa bize yakishangaa huku na kule kuangalia gari hilo, wakiongea wenyewe katika mioyo yao na kujijibu.
“Hallow” aliita mwanaume huyo.

“Subiri kwanza kaka tutaongea baadaye.
Kwa muda wa nusu saa nzima waliendelea kulishangaa gari lililokuwa ndani ya ngome yao, wakijiuliza maswali mbalimbali na waliporidhika walimsogelea mwanaume aliyekuwa pembeni na kuongea naye akajitambulisha tena kwa mara ya pili kwao.
“Ahaa! Karibu sana.

“Mimi naitwa Mariya na huyu anaitwa Merina ni watoto wa Victor Fedorov.”
“Vizuri nimetumwa na bosi wangu kuja hapa nyumbani si kuleta tu gari hili bali pia mimi ndiye nitakuwa dereva wenu kwa muda.”
“Oh! Ahsante baba yuko wapi?”
“Atakuja muda si mrefu mimi nimetangulia.

Wakiwa katika maongezi hayo haikuchukua hata dakika tano, honi nyingine ikasikika nje ya lango la kuingilia ndani ya nyumba, mlinzi akaongekana akifungua lango na gari ya Fedorov kuingia ndani huku akipiga honi nyingi kuashiria furaha, akaliendesha gari mpaka sehemu ya maegesho akaliegesha na kushuka na watoto wake wote wawili wakamkimbilia na kumkumbatia huku wakimbusu kwa wingi katika mashavu yake.

“I love you daddy,”(tunakupenda baba) walitamka maneno hayo wakimwangalia baba yao kwa macho ya upole.
“I love you too,”(Nawapenda pia) Fedorov alijibu huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.
“Baba kwa nini unalia?”
“Mh! Hapana”

“Tafadhali tueleze nini kimekupata huko ulikotoka?”
“Hakuna kitu wanangu ila…”
“Bosi! Bosi! Nini kimetokea nini huko utokako?”
Victor Fedorov hakuwa na jibu la kutoa kwa wakati huo akasogea taratibu na kuketi pembeni ya msingi uliokuwepo hapo kwikwi za kulia zikamkamata.

“TAFADHALI tueleze nini tatizo?”
“Mh!”
“Baba kwa nini unatuweka roho juu?”
“Naomba nitamke wazi leo…” kwikwi ya kulia ikamkamata tena Fedorov na kuangua kilio kama mtoto mdogo.
Kwa takribani dakika tano nzima waliendelea kubaki eneo hilo wakiwa wameshikwa na butwaa wakiwa hawaelewi ni kitu gani kilikuwa kimetokea huko alikokuwa kabla ya kufika nyumbani.

Walipohakikisha ametulia hawakuchoka kuendelea kumuuliza tena.
“Mnajua nini?”
“Eh!”
“Ninawapenda sana wanangu historia yenu inanikumbusha maisha ya nyuma ambayo yanaumiza kupita maelezo.”
“Baba lakini ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya. Unamkumbuka mama yetu?”
“Mh!”

“Unakumbuka nini?”
“Jinsi nilivyowalea mpaka kufikia hapa nikiwa sina msaada wowote.”
“Lakini baba hata sisi tunakupenda kupita maelezo.”
“Najua wanangu nami nawapenda pia.”
“Ahsante kwa zawadi nzuri ya gari.”

“Ni wajibu wangu kufanya hivyo kwenu kama wanangu na huyu hapa mbele yetu ndiye atakuwa dereva wenu mpaka mtakapokuwa mmefuzu vyema udereva, atawapeleka kokote mtakapotaka na kuhakikisha anawapa ulinzi wa kutosha.”
“Ahsante baba,” walijibu Mariya na Merina wakitabasamu.
“Leo nitaomba tujumuike wote kwa chakula cha jioni ili kukamilisha furaha yetu wanangu na kesho ninafikiria kufanya matembezi kidogo kwenye mchezo wa kuteleza kwenye barafu.”
“Babaaa!”

“Ni kweli kabisa kwa sasa ni msimu mzuri wa kwenda huko nitaondoka na nitarejea baada ya wiki tatu.”
“Twende wote.”
“Hapana acha mimi niende kwanza nikirudi mara nyingine nitawachukua wote.”
“Sawa baba tutashukuru.”
Wakaingia ndani na kujiandaa kwa ajili ya kutoka kwenda kula chakula cha jioni kama familia wakifurahia maisha na mapenzi makubwa waliyoyapata kutoka kwa baba yao. Kwa muda wa saa nzima walikuwa chumbani wakijiandaa na waliporidhika walitoka.
“Wow!” sauti ya Fedorov ilisikika baada tu ya kuwaona watoto wake wakitoka chumbani.

“Heheee!” walicheka.
“Mmempendeza sana wanangu hakika ninyi ni mabinti wazuri sana.”
“Ahsante baba.”
Wakatembea kwa mwendo wa madaha na kulielekea gari lao aina ya Ferarri na kuingia ndani ambapo Fedorov naye akaingia kwenye gari lake, yeye ndiye akawa mtu wa kwanza kutoka ndani, gari walilopanda watoto wake likifuata kwa nyuma.
Kwa mwendo wa nusu saa hivi walikuwa barabarani hatimaye wakafika kwenye mgahawa maarufu wa Kalinin. Fedorov akawa wa kwanza kushuka ndani ya gari na kubaki kusubiri watoto pamoja na dereva washuke ili waingie wote kwa pamoja.

Akionekana wenye furaha, akawakumbatia watoto wake na kuanza kutembea kuingia ndani ya mgahawa, wote wakionekana wenye furaha kupita maelezo. Kwa umaarufu na utajiri aliokuwa nao mzee huyo nchini Urusi alipewa heshima kubwa sana, alipokelewa kwa furaha na wafanyakazi karibu wote katika mgahawa huo na akaongozwa kupelekwa sehemu maalum kabisa akikaribishwa mara nyingi.
“Leo nimekuja na watoto wangu, huyu hapa anaitwa Mariya na huyu ni Merina, huyu mwingine ni dereva wao anaitwa Ford,” aliongea Fedorov kwa kujiamini kabisa.

“Karibuni sana ndugu zetu.”
Menu yenye orodha ya chakula na vinywaji ikawekwa mezani na mhudumu akiwataka wachague kitu ambacho wangependa kula na kunywa siku hiyo na wakionekana wenye furaha, kila mmoja aliagiza alichotamani kula.
Wakala na kunywa wakifurahi pamoja na baada ya hapo walilipa na kuondoka na kuingia maduka mbalimbali kununua vitu walivyohitaji na kurejea nyumbani.

“Usiku mwema wanangu!”
“Kwako pia baba!”
Wakaingia ndani ya vyumba vyao na kulala na siku iliyofuata Fedorov ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuamka ili ajiandae kwa safari ambayo ingemchukua muda wa wiki mbili mfululizo akiwaacha watoto wake peke yao nyumbani, akatoka chumbani akiwa tayari na mizigo yake kisha kugonga mlango wa chumba cha watoto wake huku akiwaita majina akiwaaga na akiwatakia kila lililo jema na kutoa maelekezo ya mahali ambako wangechukua fedha za matumizi kwa muda wote ambao hangekuwepo.

Kwa pamoja wakamrukia baba yao na kumkumbatia wakimtakia safari njema na kumtaka awahi kurejea nyumbani kwani kwa muda ambao hatakuwepo watakuwa wapweke sana.
“Nitarejea muda si mrefu, mwaa ninawapenda sana,” aliongea lakini watoto wake walipomwangalia vyema usoni mwake waligundua alikuwa akibubujikwa na machozi na walipomuuliza ni kwa nini alipatwa na hali hiyo Fedorov hakujibu kitu zaidi ya kuanza kutembea kuelekea nje ya nyumba yake akiwa na begi kubwa mgongoni mwake.

***
“Phillip! Phillip!” Lina aliita mfululizo
“Naam!”
“Ah! Najisikia vibaya.”
“Kidogo tu mke wangu sita…”
“Mh! Siyo hivyo mwenzio najisikia kizunguzungu.”

“Kizunguzungu?” aliuliza kwa mshangao.
“Ndiyo, nipe…”
“Lina acha basi utani wako unanicha…”
“Hapana Phillip naumwa mbona naona giza!”
“Eh!”

“Nipe maji ya kunywa fanya haraka kabla sija…” aliongea Lina lakini kabla hajamalizia sentensi yake ukimya wa ajabu ukatokea na Phillip alipojaribu kumwita na kumtingisha hakupata ushirikiano wowote zaidi ya yote alimshuhudia Lina akilegea kama mlenda.
“Mungu wangu! Kimetokea nini?” alijiuliza akimlaza Lina vyema kitandani na yeye kushuka kitandani.
Phillip akalisogelea taulo lililokuwa pembeni na kujifunga kiunoni, jasho jingi likimtiririka.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 46


ILIPOISHIA


“Nipe maji ya kunywa fanya haraka kabla sija…” aliongea Lina lakini kabla hajamalizia sentensi yake ukimya wa ajabu ukatokea na Phillip alipojaribu kumwita na kumtingisha hakupata ushirikiano wowote zaidi ya yote alimshuhudia Lina akilegea kama mlenda.
“Mungu wangu! Kimetokea nini?” alijiuliza akimlaza Lina vyema kitandani na yeye kushuka kitandani.
Phillip akalisogelea taulo lililokuwa pembeni na kujifunga kiunoni, jasho jingi likimtiririka.

SASA ENDELEA

Nipe maji ya kunywa fanya haraka kabla sija…,” aliongea Lina lakini kabla hajamalizia sentensi yake ukimya wa ajabu ukatokea na Phillip alipojaribu kumwita na kumtingisha hakupata ushirikiano wowote, zaidi ya yote alimshuhudia Lina akilegea kama mlenda.
“Mungu wangu! Kimetokea nini?” alijiuliza akimlaza Lina vyema kitandani na yeye kushuka haraka kitandani, haraka akachukua taulo lililokuwa pembeni na kufunga kiunoni jasho jingi likimtiririka. Kitu kilichokuwa kikitokea mbele yake kilionekana kuwa ni ndoto kama siyo muujiza, akakizunguka chumba huku na kule akifikiria cha kufanya.

“Lina! Lina mke wangu kimetokea nini?” aliita Phillip lakini hakupata jibu lolote kutoka kwa mkewe aliyekuwa kitandani akiwa ametulia kimya.
“Hapa ni hospitali tu, hakuna kingine cha kufanya,” aliongea Phillip.
Akiwa amechanganyikiwa alivaa shati kisha kumvalisha Lina, akausogelea mlango na kuufungua huku akiita jina la Bibi Magdalena ili aje kumsaidia.

“Njoo haraka! Tafadhali njoo upesi,” alisisitiza Phillip.
Haraka bila kuchelewa, Bibi Magdalena aliingia chumbani kwa Phillip na kumkuta Lina akiwa amelala kimya kitandani huku mumewe akizunguka huku na kule.
“Nini kimetokea bosi wangu?”
“Lina amenyamaza ghafla,” Phillip alimjibu Bibi Magdalena.
“Umempiga?”

“Huu si muda muafaka wa kuuliza hivyo tusaidieni nimpeleke hospitali,” Phillip alimwambia Bibi Magdalena.
“Sawa bosi.”
Haraka Phillip akamnyanyua Lina, Bibi Magdalena akitangulia mbele kufungua mlango, walipofika kwenye gari lililofunguliwa mlango, walimuingiza Lina na kumlaza siti ya nyuma kisha Phillip akazunguka upande wa pili na kuingia.
Kabla hajaondoka, alimuaga Bibi Magdalena na kumwambia akifika hospitali atamfahamisha kilichomsibu mkewe.

“Haya kila la kheri,” alijibu Bibi Magdalena akitembea kurejea ndani, furaha yote iliyokuwepo muda mchache uliopita ilikuwa imetoweka.
“Sijui kapatwa na nini?” alijiuliza bibi huyo akiingia ndani.
Kwa muda wa saa tatu na nusu Phillip bado alikuwa hajarejea, wasiwasi ukaugubika moyo wa Bibi Magdalana akitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea huko alikokuwa Phillip na mkewe Lina ambaye alikuwa mgonjwa taaban.

Saa zilipozidi kusonga mtoto Geneveve alianza kumsumbua Bibi Magdalena akitaka kujua wazazi wake walikuwa wapi.
Bila kujibu kitu chochote yeye mwenyewe akiwa na wasiwasi mwingi moyoni mwake alimtuliza mtoto Theresia na kumtaka atulie kwani wazazi wake wangerejea muda si mrefu, akatoka nje na kuelekea kwa mlinzi na kumweleza wazi wasiwasi aliokuwa nao.
“Hebu tusubiri kidogo pengine wako njiani.”
“Mh! Ni muda sana mtoto naye ananisumbua sijui wamepatwa na kitu gani, eh haya ni matatizo mengine tena!” aliongea bibi huyo akionyesha kulengwalengwa na machozi.

Ghafla wakiwa katika maongezi hayo, honi ikasikika nje ya lango la kuingilia ndani ya nyumba yao.
“Si hao!” aliongea mlinzi akilisogelea lango na kufungua, hakuwa amekosea gari la bosi wake lilikuwa limesimama nje ya lango hilo.
Taratibu bila kusema kitu akionekana mwenye mawazo mengi kichwani mwake, Phillip akaendesha gari mpaka sehemu ya maegesho. Alipoangalia kwenye kibaraza cha nyumba yake, akamshuhudia mtoto wake Genevieve akikimbia kumfuata.

“Dady why are you crying?”(Baba kwa nini unalia?)
“It’s too painful,”(Inauma sana)
“What?”(Nini?)
Kwikwi ya kulia ikamkaba Phillip, akajikuta akilia mbele ya mtoto wake kitu kilichozidi kumchanganya zaidi Genevieve, naye bila kutegemea akaanza kuangulia kilio.

***
Fedorov alitembea hatua mbili na kugeuka nyuma kuwaangalia watoto wake, hakuonekana kuwa na furaha kama ilivyokuwa siku zote aliposafiri kwenda mbali.
Alipolifikia gari lake, akafungua sehemu ya kuweka mizigo akaweka begi na vifaa alivyokuwa navyo ndani kisha akawaita tena watoto wake;
“Mariya, Merina.”

“Bee,” waliitika wakikimbia kumfuata na walipomfikia karibu waligundua baba yao alikuwa tofauti kabisa.
“Lakini unaonekana hauko sawa?” Merina aliuliza.
“Unajua nini?”
“Mh!”
“Ninasikia sauti ndani ya moyo wake ikiniambia kwamba nisiwaache.”
“Basi twende wote baba!”

“Hapana nataka mbaki nyumbani nami niende kwenye mchezo huo nitarejea tu niombeeni wanangu,” aliongea Fedorov huku akiwakumbatia watoto wake.
“Lakini umesema moyo wako hautaki kwenda huko?”
“Hivyo ndivyo ninavyosikia ila acheni niende.”
“Mh!” Mariya aliguna yeye pia alihisi kitu fulani ndani ya moyo wake lakini akajaribu kupingana na hisia hizo ili kumfanya baba yake arejee katika hali yake ya kawaida.

“Nawapenda sana wanangu mbaki salama, nitarejea baada ya wiki mbili, mnapenda niwaletee nini nikirudi?”
“Mh! Mh!”
“Semeni basi!” aliongea Fedorov akifungua mlango ili aingie garini.
“Tuletee zawadi ya saa.”
“Hilo tu?”
“Mh!” Waliitikia kwa kuguna huku wakitingisha vichwa vyao kuonyesha ishara ya kukubali.

Fedorov akaingia ndani ya gari na kuliwasha kisha taratibu huku akiwaangalia watoto wake akaliendesha gari hadi langoni ambako mlinzi alifungua kisha akatoka ndani.
“See you then,”(Tutaonana) ndiyo maneno pekee aliyoongea akitokomea.
Wiki ya kwanza ikakatika hatimaye ikaja ya pili Mariya na Merina wakiwa tayari kumsubiri baba yao bila matarajio, walipojaribu kufanya mawasiliano naye kwa njia ya simu ya upepo bado Fedorov hakupatikana wakaanza kuingiwa na wasiwasi kwani halikuwa jambo la kawaida na kibaya zaidi safari hiyo aliondoka peke yake bila ya mlinzi.
“Hivi unafikiri baba atakuwa wapi mpaka sasa?”

“Kwa kweli sijui ila tusubiri tuone pengine yuko njiani.”
“Mh! Nahisi hatari fulani ndani ya moyo wangu…,” aliongea Merina kwa sauti ya upole.
Hatimaye wakiwa katika kusubiri wiki ya tatu ikaanza kuyoyoma bila baba yao kutokea, wakaingiwa na hofu na kuamua kutoa taarifa za kupotea kwa baba yao katika vituo mbalimbali vya televisheni na redio lakini hata baada ya matangazo kutolewa mzee huyo hakuonekana.

MWEZI mmoja ulikuwa umekatika tayari watoto Mariya na Merina wakiwa katika kusubiri, mioyo yao ikiwa na huzuni kubwa kupita maelezo, ni mlinzi wa nyumbani kwao na dereva aliyewaendesha ndiyo waliotoa faraja kwa watoto hao wakiwapa moyo kwamba ipo siku Fedorov angerejea na huko alikokuwa hakukuwa na tatizo lolote kwani kama lingekuwepo mpaka wakati huo wangeshapewa taarifa.
“Msiwe na hofu atarejea tu, huyu mtu ni mfanyabishara pengine ameshatoka huko na kuelekea nchi nyingine.”
“Lakini bila kusema kitu chochote?” Merina alihoji.

“Inawezekana anajua hakuna kitu kibaya.”
“Hapana mimi ninawaeleza wazi kabisa ipo sauti ndani ya moyo wangu inanieleza jambo fulani la hatari, lazima kuna tatizo,” Mariya aliongea akibubujikwa na machozi.
“Usilie nyamaza baba atarejea tu tena si muda mrefu.”
“Mimi nashauri tutoe taarifa polisi.”

”Juu ya nini?”
“Upoteaji wa baba yetu, mimi ninawaambia lazima atakuwa kwenye matatizo makubwa sana kama siyo kifo.”
“Mh!” Wote wakaguna kwa mshangao.
Baada ya maongezi hayo kwisha kila mmoja akionekana kuwa na msongo wa mawazo kichwani mwake, Mariya na Merina walinyanyuka na kuingia ndani ya chumba ambamo kwa takribani nusu saa nzima waliendelea kubaki huku wakiwaacha mlinzi na dereva waliokuwa wameketi bustanini wakiendelea kujiuliza maswali na ghafla wakiwa hapo wakawashuhudia tena watoto hao wakirejea.

“Dereva tafadhali tupeleke.”
“Wapi?”
“Kituo cha polisi.”
“Lakini tumepatana tuvute subira kidogo pengine yuko njiani anarejea.”
“Hapana tumeamua twende tu polisi.”
“Mh! Haya twendeni niwapeleke.”

“Naweza kuongozana nanyi?” mlinzi aliuliza.
“Hapana wewe baki tu hapa nyumbani tutarejea muda si mrefu.”
“Sawa.”
Wakatoka wakiongozana na dereva mpaka kwenye maegesho ya gari kisha wote wakafungua milango na kuingia ndani, Mariya na Merina wakiwa wameketi kiti cha nyuma na mara kadhaa wakiongea jambo fulani kwa kunong’ona.

Gari likaendeshwa mpaka sehemu kulikokuwa na kituo cha polisi, hapo wakashuka na kuingia moja kwa moja ndani wakimtaka dereva aendelee kusubiri eneo lilelile.
Wote wawili wakatembea na kuingia ndani ya kituo na kupokelewa na askari waliokuwa eneo hilo, kwa sababu ya umaarufu wao moja kwa moja wakaongozwa kuingia kwenye chumba maalum ambako walimkuta polisi akiwa ameketi akawakaribisha na kuwataka waeleze shida yao.
“Ahsante sana,” aliongea Merina ambaye kwa kumwangalia tu machoni mwake ungegundua alikuwa akilia.
“Kuna tatizo gani?” Polisi aliuliza.

“Ni mwezi sasa umepita hatujui baba yetu yuko wapi?”
“Tajiri Fedorov?”
“Hujakosea,” Mariya alijibu.
“Mh!” Polisi naye akaguna kuonyesha mshtuko, kwani historia ya mzee huyo ilifahamika nchini kote na kwa umafia wake aliogopwa na kila mtu.
“Tunahitaji kutoa taarifa hii kwenu ili msako ufanyike haraka sana na kufahamu ni wapi alipo baba yetu, juu ya malipo hakuna shida ilimradi tu apatikane.”

“Hata akiwa amekufa?”
“Tunahitaji maiti yake.”
“Basi hakuna shida tutafungua faili ambalo tutaandika malalamiko yenu kisha tutaanza msako na mnachotakiwa kufanya ni ninyi kutangaza kwenye vyombo vya habari vyote.”
“Hakuna shida tutaifanya kazi hiyo, tunachotaka sisi ni kumpata baba yetu basi!” walijibu watoto hao kwa kujiamini.

Baada ya kuhakikisha kwamba taarifa hiyo ilikuwa imefika jeshi la polisi, waliaga na kutoka nje wakitembea kuelekea lilipokuwa gari lao, wakapanda na dereva bila kusema kitu chochote akaliendesha moja kwa moja kuelekea nyumbani.
Jambo moja lilitawala vichwa vyao: ni wapi baba yao alikuwa na kama alikuwa amekufa maisha yao yangekuwaje baada ya hapo?
“Merina tunatakiwa tuanze kutangaza mara moja kwenye vyombo vya habari bila kuchelewa.”
“Kazi hii tutampatia huyu dereva azunguke kwenye vyombo vyote vya habari hata kama watahitaji fedha lakini watoe tangazo hili.”
“Hakuna shida.”

Nusu saa tu baadaye gari lilishafika nyumbani kwa tajiri Fedorov, lango likafunguliwa na dereva kuingiza gari ndani wakashuka na kumsabahi mlinzi wao na hawakusema tena kitu chochote wakatokomea na kuingia ndani.
Watoto hao waliendelea kubaki ndani ya chumba kwa zaidi ya saa tatu wakiongea mambo mbalimbali, hata mlango wa chumba chao ulipogongwa wakitakiwa kwenda kula waliendelea kugoma wakitoa agizo kwamba watu wengine waendelee nao wangejumuika baadaye.
Hata walipoitwa tena baada ya saa sita waliendelea kubaki chumbani na safari hii hawakusikika wakijibu kitu chochote zaidi ya ukimya tu.
“Mh! Wanafanya nini hawa?”

“Sijui hata wakiitwa hawaitiki.”
“Wasije kuwa wamechukua maamuzi mabaya.”
“Haiwezekani hebu tuchungulie dirishani.”
Mlinzi na dereva wakazunguka nyuma ya nyumba na kuelekea sehemu dirisha la chumba cha watoto hao lilipokuwa na walipojaribu kutupa macho yao ndani yalikutana na pazia zito likiwa limefunikwa kwenye dirisha hilo.
***
“Genevieve?” Phillip aliita kwa sauti ya upole.
“Bee baba!”
“Si kwamba napenda kulia mwanangu lakini…” kwikwi ya kulia ikamkaba tena Phillip akaangua kilio mbele ya mtoto wake.
“Tafadhali nyamaza na utueleze tatizo, nini kimetokea huko?” Magdalena aliyekuwa mfanyakazi wa ndani nyumbani kwa Phillip aliongea.


“Hali ya Lina ni mbaya sijui kama…” aliongea Phillip na kabla hajamalizia sentensi yake mlio wa simu ikiita ukasikika, taratibu akaingiza mkono wake mfukoni na kuichomoa haraka kisha akatupa macho kwenye kioo cha simu ili asome jina.
“Hospitali!” Alitamka Phillip kwa sauti ya juu.

Je, nini kinaendelea hapo? Simu iliyoingia ina ujumbe gani kwa Phillip? Fedorov, je, yuko wapi?
 
SEHEMU YA 47

ILIPOISHIA


“Hali ya Lina ni mbaya sijui kama…” aliongea Phillip na kabla hajamalizia sentensi yake mlio wa simu ikiita ukasikika, taratibu akaingiza mkono wake mfukoni na kuichomoa haraka kisha akatupa macho kwenye kioo cha simu ili asome jina.
“Hospitali!” Alitamka Phillip kwa sauti ya juu.

Je, nini kinaendelea hapo? Simu iliyoingia ina ujumbe gani kwa Phillip? Fedorov, je, yuko wapi?
SONGA NAYO

MSAKO nchini Urusi ulikuwa mkali kweli kweli polisi wakifanya kazi usiku na mchana kumsaka tajiri mkubwa nchini humo, Victor `Fedorov ambaye alitoweka katika mazingira ya kutatanisha, makundi kwa makundi yalikuwa yakigawanyika ambapo watu wengine walielekea sehemu ambako tajiri huyo alikwenda kwenye mchezo wa kuteleza katika barafu.

“Mkuu tumefika mpaka hapa lakini hakuna mtu wala hakuna taarifa yoyote ile inayoonyesha kwamba kuna uhai wa mtu na kwa mujibu wa mazingira hatukushudia kitu chochote kinachoonyesha uwepo wa mwanadamu,” ilikuwa ni sauti ya polisi mmoja katika kundi la polisi wasiopungua kumi waliotumwa kwenda kufanya uchunguzi eneo ambalo ndilo hasa Fedorov aliaga kwenda huko.
“Kitu gani kingine kimefanyika?”

“Tumejaribu kwa uwezo wetu wote kuangalia pengine hata nyayo na nguo ili kuridhika na upelelezi wetu lakini hatujafanikiwa kuona kitu.”
“Basi ni vyema mkarejea na kufanya mkakati mwingine.”
“Sawa mkuu.”
Simu ya upepo ikakatika na polisi wakajiandaa na kupanda ndani ya helikopta kisha kurejea jijini kwa mkakati mwingine.

***
Ndani ya chumba Mariya na Merina walikuwa wakipanga mkakati wa jinsi ya kumpata baba yao ambaye mpaka wakati huo hawakufahamu ni wapi alipokuwa na kama alikuwa mzima au la! Machozi na vilio vilitawala kila mmoja akionekana kumfariji mwenzake.
“Baba atakuwa amekufa.”
“Hapana usiseme hivyo.”

“Nahisi hivyo si kawaida yake hata simu tu?”
“Mh! Unasema kweli kwa jinsi anavyotupenda haiwezekani hata kidogo.”
“Ngoja tuone uchunguzi wa polisi utasema nini?”
“Hapana Merina ni muda mrefu sana…yapata miezi mitatu sasa lazina kuna tatizo mimi ninakuambia...”

Mariya aliyekuwa ameketi kimya kitandani bila kujibu kitu machozi yakaonekana yakimbubujika, kichwani mwake hakupata picha kama kweli baba yao mpendwa angekuwa amekufa maisha bila yeye yangekuwaje? Ilikuwa ni picha ya kuumiza sana hakumfahamu mtu mwingine zaidi ya mlinzi na dereva waliyekuwa naye wakati huo.
“Kama ikitokea mzee asionekane nini kitatokea katika maisha yetu?”
“Kwa kweli sijui na hatukuwahi kumfahamu ndugu mwingine yeyote na kama sijakosea baba alitueleza kwamba mama yetu alifariki miaka mingi sana hivyo yeye ndiye alikuwa kila kitu.”

“Sawa kabisa, kitu alichokuwa amekiongea Mariya kilikuwa ni ukweli, hawakufahamu ni kitu gani kingeendelea kwao, maisha yangekuwaje na ndugu wengine wangewafahamu vipi kwani Fedorov hakutaka kuwaeleza ukweli.
“Lakini lazima kuna sehemu baba atakuwa ameandika kitu fulani hivi kweli hana ndugu?”
“Wewe hivi unamjua vizuri baba?”
“Namjua hebu…,” aliongea Merina akinyanyuka kitandani na kuanza kutembea kuelekea mlangoni akitoa ishara ya kumwita Mariya.
“Twende huku.”

“Wapi?”
“Wewe twende tu utaona ninachotaka kwenda kufanya.”
Baada tu ya kutoka ndani ya chumba chao wote wawili wakapiga hatua tatu kusonga mbele ambako macho yao yalikutana na mlango wa kioo hicho ndicho kilikuwa chumba cha baba yao.
“Tuingie huku chumbani.”
“Kufanya nini wakati ni chumba cha baba?”

‘Wewe nifuate mimi acha ubishi wako.”Haraka bila kujiuliza mara mbili wakaufungua mlango na kuzama ndani Mariya akionyesha hofu kubwa.
Kwa saa tatu mfululizo waliendelea kubaki ndani ya chumba cha mzee wao wakifanya upekuzi kila kona kusoma na kutafuta mahali ambako wangegundua kuwepo kwa nyaraka zozote za siri ambazo zingewazesha kupata angalau ndugu mmoja upande wa baba au mama yao. Lakini bado hawakufanikiwa mwisho nao wakaanza kukata tamaa kabisa lakini ghafla wakiwa hapo wakakumbuka kwamba walifanya upekuzi kila mahali na walikuwa wamesahau sehemu moja tu ndani ya chumba hicho kabati kubwa lililokuwa pembeni kabisa mwa chumba.

“Bado hili kabati hapa.”
“Ehhe kweli tulisahau.”
Wote wakakimbia kulielekea kabati hilo na kufungua mlango mmoja baada ya mwingine kupekua ndani wakitoa nyaraka moja baada ya nyingine na kuzisoma lakini bado hawakuona sehemu yoyote ambayo iliandikwa kuonyesha kama Federov alikuwa nani na alitokea wapi akiwa na ndugu wangapi.

“Mh! Mimi mwenzako nimechoka.”
“Basi pumzika mimi niendelee lazima tupate kitu humu ndani ya hili kabati vinginevyo sitatoka hapa,” aliongea Merina akiangusha vitu kutoka ndani ya kabati bila kujali.
“Mh!” Merina aliguna.

“Nini?”
“Hili kabrasha ni la nini?”
“Hebu? Tena la rangi nyekundu?”
“Fungua ndani tuone,” Mariya aliongea na taratibu akasogea karibu kushuhudia ni kitu gani kingeonekana ndani yake.

Walikuwa wawili tu ndani ya chumba lakini kila mmoja alionekana kuwa na hofu, walitaka kufahamu ni kitu gani kilikuwa ndani ya kabrasha hilo na kibaya zaidi lilikuwa la rangi nyekundu na juu yake maneno “Nyaraka muhimu” yalisomeka.
“Mh! Kwa nini maneno hayo?”
“Hata mimi sijui ila ngoja tufungue tuone.”
“Mimi naogopa sana.”
“Acha woga tunachotaka kufahamu sisi ni ndugu wa baba au upande wa mama yetu ambaye hatukuwahi kumfahamu.”
“Haya fungua,” Mariya alizidi kusisitiza.
Wakatembea na kuketi juu ya kitanda hapo wakiwa tayari kufungua kabrasha hilo na kwa ujasiri wa hali ya juu walilifungua na kuliacha wazi, kitu cha kwanza walichokishuhudia kilikuwa ni vyeti vilivyofungwa vizuri na vilivyoonyesha majina yao.
“Majina yetu haya.”
“Mh!” pacha mmoja aliguna na kuonyesha mshangao.
Wakaendelea mbele zaidi kufunua katarasi nyingine, hapo walikutana na wosia mzito wa Victor Federov ukieleza kwamba yeye alikuwa nani na alitokea wapi, alizaliwa miaka mingapi iliyopita, haukuishia hapo ukaendelea mbele zaidi akitaja mali zote alizokuwa nazo na kiasi chote cha fedha alizokuwa nazo katika benki mbalimbali nchini Urusi, majengo makubwamakubwa na miradi mbalimbali na alitaka vitu hivyo vyote chini ya mwanasheria aliyekuwepo ndani ya wosia huo kama siku ikitokea akafa basi utajiri wote huo uende kwa watoto wake.
Maneno yale yalichoma mioyo ya watoto hao, machozi mfululizo yakawabubujika wakilia na kuomboleza kwani mpaka wakati huo pamoja na kwamba walishatoa taarifa katika vyombo vya habari na taarifa nyingine kuzipeleka kwenye vyombo vya habari wakimtafuta baba yao kwa udi na uvumba, alikuwa bado hajapatikana.
“Nahisi hatari fulani.”
“Mimi pia naungana na wewe.”
“Ni kwa nini baba aliamua kuandika kitu kama hiki? Je, alifahamu kwamba atakufa muda si mrefu? Na huyu mwanasheria ni nani?” walijiuliza maswali mfululizo.
Huzuni ilikuwa imewagubika lakini pamoja na yote hayo bado hawakutaka kuacha kusoma nyaraka zote zilizokuwa ndani ya kabrasha hilo wakitaka kufahamu zaidi siri zilizokuwa ndani.
“Historia kamili ya watoto Mariya na Merina ilipoanzia mpaka hapa walipo leo, jinsi walivyopatikana na nani hasa alikuwa ni mama yao mzazi” maneno hayo yalisomeka kwenye moja ya karatasi ndani ya kabrasha.
“Mh!” wakaguna.
Wakaendelea mbele zaidi na kukutana na jina Genevieve huyo ndiye alikuwa mama yao wa kuwazaa lakini mwanamke huyo aliolewa na mwanaume aliyeitwa Phillip na waliishi nchini Tanzania.
Maswali mengi yaliendelea kuzunguka ndani ya vichwa vyao wakitaka kufahamu ukweli wa historia yao lakini kwa wakati huo hakuwepo mtu ambaye angewaeleza ukweli, mtu pekee waliyemtengemea alikuwa ni Victor Fedorov.
“Baba anajua ukweli wote na sasa hayupo, hebu tuendelee mbele zaidi tutajua tu,” aliongea Merina akionyesha msisitizo.
Kadiri walivyozidi kusonga mbele ndivyo mambo mengi makubwa yalivyoibuka na kuzidi kuwaacha midomo wazi bila kupata ufafanuzi wowote.
“Mama yetu aliitwa Genevieve?”
“Historia inaonyesha tulipatikana kwa kupandikizwa katika chupa?”
Bado watoto hao waliendelea kujiuliza maswali mengi kichwani mwao huku huzuni ikigubika ndani ya mioyo yao, hakika walikuwa wamesoma kitu ambacho mpaka wanafikisha umri wa miaka kumi na nane hawakufahamu ukweli wa jambo lolote zaidi sana Fedorov ndiye alikuwa kila kitu.
“Ni lazima tuzungumze na huyu mwanasheria pengine anaweza kutusaidia zaidi.”
“Umeongea jambo la maana sana.”
“Lakini kabla ya yote tusubiri kwanza tuone taarifa za polisi zitasemaje kuhusu baba yetu.”
Hivyo ndivyo walivyokubaliana na waliamua kusubiri kwa muda mpaka miezi sita baadaye lakini bado Fedorov alikuwa hajapatikana nao pia wakaamini kabisa kwamba huenda baba yao alikufa katika mchezo wa barafu na maiti yake kufukiwa na theluji.
Wakiwa wenye majonzi mioyoni mwao, walipanga kukutana na mwanasheria ambaye alikuwa kwenye nyaraka za Fedorov ili kuongea na kufahamu ukweli wa mambo yote.
Waliamini huyo angeweza kuwasaidia kwa mambo yote muhimu na kufahamu zaidi utajiri wa baba yao, ni kweli wakafanikiwa kuonana naye na kuongea naye akawaambia alikuwa ameshtushwa na habari za kupotea kwa Fedorov lakini akawaahidi kwamba angefuatilia kwa karibu majibu ya polisi na angekuwa nao bega kwa bega.
“Tunakushukuru kwa kila kitu lakini jambo moja tunaomba kutoka kwako.”
“Hakuna shida.”
“Pamoja na kwamba hivi sasa sisi ni watu wazima lakini tunahitaji uendelee kuwa mshauri na msimamizi wa mali za baba yetu.”
“Niko tayari,” mwanasheria huyo aliongea kwa kujiamini.
Wote kwa pamoja wakasimama na kumshika mkono huku wakimtaka kuwa karibu yao na kushirikiana naye kwa kila jambo, wakamshukuru na kuondoka kurejea nyumbani.
“Wiki ijayo lazima tufunge safari kuelekea Tanzania tukamwone huyo anayedaiwa kuwa mama yetu,” Mariya aliongea na Merina akamuunga mkono.
Maandalizi maalum yakafanyika na utaratibu ulipokamilika Mariya na Merina wakasafiri kuja Afrika ya Mashariki nchini Tanzania, hamu yote ikiwa ni kuwafahamu watu wawili Phillip na mkewe Genevieve, pamoja na kugundua ukweli wote wa jinsi walivyopatikana, walitamani kuwaona watu hao wakiamini kabisa kwamba walikuwa ni watu muhimu mno katika maisha yao.
***
“Haraka mpelekeni chumba cha wagonjwa mahututi na afungiwe mashine ya hewa ya oksijeni imsadie kupumua,” ilikuwa ni sauti ya daktari mmoja ndani ya wodi aliyekuwa akimhudumia Lina.
“Kimetokea nini?”
“Hali yake imebadilika ghafla, kwa inavyoonekana ana tatizo kubwa ndani ya kichwa chake ambalo linamsumbua.”
“Mungu wangu na mume wake ameondoka sasa hivi kwenda nyumbani,” muuguzi aliongea.
“Kama ana simu apigiwe haraka sana arudi hapa mara moja,” daktari alizidi kusisitiza.
Muuguzi akachukua faili lililokuwa na kumbukumbu za Lina, hapo akakutana na namba ya mumewe Phillip, haraka bila kuchelewa akakimbia mpaka mapokezi ambako aliomba msaada wa kupigiwa namba hiyo.
Haikuchukua hata dakika mbili tayari namba hiyo ikawa imeita.
“Hallow, ndiyo hapa ni hospitali tunahitaji urejee haraka sana, hali ya mke wako ni mbaya na hivi sasa ninavyoongea na wewe tunajiandaa kumpeleka chumba cha wagonjwa mahututi…,” aliongea muuguzi huyo na simu ikakatika.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 48


ILIPOISHIA

“Haraka mpelekeni chumba cha wagonjwa mahututi na afungiwe mashine ya hewa ya oksijeni imsaidie kupumua,” ilikuwa ni sauti ya daktari mmoja ndani ya wodi aliyekuwa akimhudumia Lina.
“Kimetokea nini?”
“Hali yake imebadilika ghafla kwa inavyoonekana ana tatizo kubwa ndani ya kichwa chake ambalo linamsumbua.”
“Mungu wangu na mume wake ameondoka sasa hivi kwenda nyumbani,” muuguzi aliongea.
“Kama ana simu apigiwe haraka sana arudi hapa mara moja,” daktari alizidi kusisitiza.
Muuguzi akachukua faili lililokuwa na kumbukumbu za Lina hapo akakutana na namba ya mumewe Phillip, haraka bila kuchelewa akakimbia mpaka mapokezi ambako aliomba msaada wa kupigiwa namba hiyo.
Haikuchukua hata dakika mbili tayari namba hiyo ikawa imeita.
“Hallow, ndiyo hapa ni hospitali tunahitaji urejee haraka sana hali ya mke wako ni mbaya na hivi sasa ninavyoongea na wewe tunajiandaa kumpeleka chumba cha wagonjwa mahututi…,” aliongea muuguzi huyo na simu ikakatika.
“Wiki ijayo safari kuelekea Tanzania ni lazima, tukamwone huyo anayedaiwa kuwa mama yetu,” Mariya aliongea na Merina akamuunga mkono.
Maandalizi maalum yakafanyika na utaratibu ulipokamilika Mariya na Merina wakasafiri kuja Afrika ya Mashariki nchini Tanzania, hamu yote ikiwa ni kuwafahamu watu wawili, Phillip na mkewe Genevieve pamoja na kugungua ukweli wote wa jinsi walivyopatikana, walitamani kuwaona watu hao wakiamini kabisa kwamba walikuwa ni muhimu mno katika maisha yao.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...

Taarifa walizokuwa wamezisoma Mariya na Merina kwenye kabrasha la siri la baba yao, hakika lilikuwa limewatia simanzi kubwa ndani ya mioyo yao, pamoja na kwamba waliufahamu ukweli wote lakini watoto hao walihitaji kumwona mama yao na mtu mwingine aliyekuwa ametajwa ndani ya nyaraka hizo aliyejulikana kama Phillip, walitamani kufika nchini Tanzania kwa gharama yoyote ile ilimradi tu wakutane na watu hao.


Maandalizi yakafanyika haraka chini ya Mwanasheria wao wa familia ambaye ndiye alisimamia kila kitu na safari nzima ya watoto hao akihakikisha kwa fedha zilizokuwepo wangeweza kusafiri salama na kurejea salama bila matatizo yoyote yale.
“Mariya lakini huyu ndiye baba yetu mzazi,”
“Ni kweli kabisa hilo sina shaka nalo tatizo moja tu linakuja ni kwa nini baba hakuwa mkweli kwetu?”


“Pengine alifahamu tukipata habari hizo tutaumia kwani kwa maelezo yaliyotolewa ni kwamba baba aliuza mbegu zake za kiume kwa familia ya Phillip ambazo zilipandikizwa kwa mwanamke aliyeitwa Genevieve huyo ndiye mama yetu lakini pia Phillip ni mtu muhimu kwetu ni kama baba ni lazima twende haraka, nakumbuka kuna wakati baba aliwahi kutueleza kwamba mama yetu alikufa, hivi inawezekana kweli?”
“Inawezekana hawezi kusema uongo kama huo,”


“Twende mambo mengine yote tutayajua huko huko?”
“Tutafanya nini ili kuwafahamu watu hao?” Mariya alimuuliza Merina.
“Tutatumia vyombo vya habari kutangaza na ikiwezekana kuzungumza kabisa na vyombo hivyo,” Merina alijibu.
“Kivipi?”Mariya alihoji.


“Fedha ni kila kitu kwetu,” Merina aliongea kwa kujiamini.
Hivyo ndivyo walivyomaliza mazungumzo yao na kuanza kujitayarisha kwenda Afrika wakiwa hawaelewi kabisa ni wapi baba yao alipokuwa na alipatwa na kitu gani lakini walilazimika kufanya hivyo kwa sababu ya nyaraka za siri walizozisoma. Mioyo yao iliuma mara kadhaa walipomkumbuka baba yao, ucheshi,utani na mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwao hakika kwa wakati huo vilikuwa vimekosekana.


“Mimi naona ni bora tukaondoka na huyu mwanasheria wetu ili akasaidie mchakato huu.”
“Mh! Wazo zuri sana hebu tumpigie simu naye afanye maandalizi ili kesho jioni tuweze kuondoka.”

Wakafanya kama walivyokubaliana simu ikapigwa na mwanasheria kupewa taarifa kwamba safari iliyokuwepo mbele yao ililazimu kuongozana nao kwa gharama yoyote.
Hivyo ndivyo walivyofanya siku iliyofuata safari ikaanza, hamu yao kubwa ikiwa ni kuwafahamu watu hao wawili, Phillip na Genevieve, walitamani kuongea nao ili kufahamu ukweli juu ya nini kilichotokea.


Safari yao ilisadikiwa kuchukua saa nane mpaka kufika nchini Tanzania ambako wangefanya utaratibu maalum wa kuwapata walengwa ambao walikuwa ni Phillip na Genevieve.
***
Simu iliyokuwa imeingia kwa Phillip ikimtaarifu kwamba alitakiwa kufika hospitalini mara moja ilikuwa imemchanganya kupita maelezo, akiwa hapo alihisi hatari na kuiona taa nyekundu ikiwaka ndani ya kichwa chake.


“Lina! Lina atakuwa amezidiwa,” hivyo ndivyo alivyoongea huku akitweta na bila kuchelewa aliwaaga bibi Magdalena na mtoto wake Genevieve waliokuwa pembeni yake akiwaambia wazi kwamba alitakiwa kurejea hospitalini haraka sana.
“Twende wote baba,” Genevieve aliongea.
“Hapa…,” alijibu Phillip lakini kabla hajamalizia sentensi yake bibi Magdalena aliingilia.
“Ni lazima tuongozane nasi tufahamu nini kimetokea huko, hatuko tayari kubaki hapa nyumbani, sawa?”
“Mh! Unajua.”


“Phillip hakuna haja ya mabishano hapo Genevieve hebu twende…,” bibi Magdalena aliongea akimvuta Genevieve kuelekea kwenye gari.
Wote wakaingia ndani na Phillip akiwa ndiye dereva alionekana kuwa mtu mwenye msongo mwingi wa mawazo lakini hayo ndiyo yalikuwa maisha hakuwa na mtu mwingine wa kumsaidia tatizo lililokuwa mbele yake, kwa kasi ya ajabu akaliendesha gari hatimaye akafanikiwa kufika hospitali ndani ya dakika kumi na tano tu.


Haraka akaegesha gari sehemu maalum na kushuka mbio bila kusema chochote kuelekea chumba ambacho ndicho hasa Lina alilazwa, Genevieve na Magdalena wakimfuata kwa nyuma nao pia wakionekana wenye wasiwasi mwingi.


Dakika tano tu baadaye alifanikiwa kufika kwenye wodi hiyo lakini alishangazwa na ukimya uliokuwepo eneo hilo, bila kuuliza wala kusubiri akausukuma mlango na kuzama ndani, kitanda kilikuwa kitupu.
“Nini kimetokea?” alijiuliza na ghafla akiwa katika kujiuliza muuguzi aliingia ndani ya wodi hiyo.
“Dada! Dada!” aliita mfululizo.
“Ndiyo kaka yangu nakusikiliza.”
“Nauliza mgonjwa aliyekuwa amelazwa hapa muda mchache tu, anaitwa Lina.”


“Lina?”
“Ndiyo.”
“Mh!” badala ya kujibu muuguzi aliguna.
“Kwa nini unaguna dada?” aliuliza Phillip akimwangalia muuguzi machoni na kugundua kitu tofauti.
“Ah! Hebu subiri kidogo.”
“Dada mbona sikuelewi tafadhali nieleze nini kimetokea hapa?” Phillip aliuliza akionyesha msisitizo.


“Kaka hali ya mgonjwa imebadilika ghafla kwa ujumla ni mbaya…,” aliongea muuguzi huyo lakini hakumaliza sentensi yake mlango ukafunguliwa kwa nguvu.
“Monica!” ilikuwa ni sauti ya kiume ikiita ndani ya wodi.
“Bee!” aliitika muuguzi huyo.
“Unagonja nini tunasubiri hilo faili haraka?”


“Sawa daktari lakini kuna huyu kaka hapa anauliza kuhusu mgonjwa Lina.”
“Hebu nifuateni nyuma haraka,” daktari huyo aliongea na wote wakaanza kutoka mbio kumfuata kwa nyuma.
Hawakupiga hata hatua kumi mbele ya mlango uliokuwa umeandikwa ICU walishuhudia machela ikitolewa kwa mwendo wa kasi kupelekwa sehemu ambayo hawakuielewa, Phillip alikuwa wa kwanza kutupa macho juu yake na kumwonga Lina akiwa amelala kimya mdomoni mwake akiwa amefungwa mashine ya oksijeni.
“Mke wangu!” aliongea kwa sauti ya juu.


“Hali yake ni mbaya tunajaribu kuokoa maisha yake imetulazimu kumpeleka chumba cha upasuaji haraka sana…” aliongea daktari huku machela ikisukumwa kuingizwa ndani ya chumba cha upasuaji, Phillip, Genevieve pamoja na Magdalena wakitakiwa kubaki hapo kusubiri.

Baada ya Lina kuingizwa chumba cha wagonjwa mahututi, uchunguzi maalum uliendelea na Phillip ndiye aliyetakiwa kutoa historia ya mkewe kwani kwa wakati huo hakuwa akijitambua. Akawa tayari kueleza kila kitu kilichomtokea mkewe ikiwepo ajali ya moto aliyoipata baada ya gari lake kuwaka moto.
Katika kufanya uchunguzi kuwa rahisi, jopo la madaktari likaanza kazi, na ni hapo ndipo walipogundua kwamba jeraha la moto alilolipata Lina lilileta madhara makubwa sana kwa ndani, madhara ambayo hayakufahamika mapema hivyo walitaka kujaribu kumsaidia kwa kumfanyia upasuaji ili kuondoa tatizo lililoonekana ndani ya kichwa.
Wakiwa katika hali ya kusubiri kuona kama angerejewa na fahamu zake ili kukamilisha vyema uchunguzi wao, hali ya Lina ilibadilika ghafla, ni hapo ndipo walipolazimika kumkimbiza chumba cha upasuaji ili kuokoa maisha yake.
“Hali yake ni mbaya tunajaribu kuokoa maisha yake imetulazimu kumpeleka chumba cha upasuaji haraka sana…,” aliongea daktari huku machela ikisukumwa kuingizwa ndani ya chumba cha upasuaji, Phillip, Genevieve pamoja na Magdalena wakitakiwa kubaki hapo kusubiri. Hayo yalikuwa maneno pekee aliyotamka daktari na kuingia ndani ya chumba.
Walibaki nje ya chumba wakionyesha hofu kubwa, Phillip yeye alishindwa kujizuia akajikuta akitokwa na machozi.
“Baba usilie mama atapona tu,” Genevieve aliongea akimpigapiga baba yake.
“Najua atapona lakini…” kwikwi ya kulia ikamkamata Phillip binafsi ndani ya moyo wake kwani aliufahamu ukweli kwamba Lina alikuwa katika hali ya kufa kwani ripoti ya uchunguzi iliyokuwa imefanyika ilionyesha wazi kwamba alikuwa na tatizo kubwa ndani ya kichwa chake na tayari lilikuwa limechelewa kupata ufumbuzi.
Kwa muda wa saa nne mfululizo waliendelea kusubiri, hamu yao kubwa ikiwa ni kufahamu ni kitu gani kiliendelea ndani ya chumba cha upasuaji, macho na masikio yao yote yalielekea kwenye mlango wa chumba kuangalia na kusikiliza.
“Mbona wamechukua muda mrefu sana,” aliuliza Phillip.
“Inawezekana bado wanafanya upasuaji.”
“Mh!”
“Hebu tuvute subira kidogo tuangalie,” Magdalena aliongea akijaribu kumpa Phillip moyo wa matumaini.Waliendelea kusubiri saa nyingine mbili na kufanya idadi ya saa kutimia sita lakini bado hawakuona muuguzi wala daktari akitoka ndani ya chumba hicho, wakaanza kukata tamaa na mioyo yao kuhisi kuna jambo la hatari lilikuwa limetokea na taa nyekundu iliyoashiria hatari ikawa kichwani mwa Phillip.
“Lazima kuna tatizo siyo rahisi,” aliongea Phillip akitembea kusogelea mlango wa chumba cha upasuaji, akapiga hatua tatu mbele lakini kabla hajanyanyua hatua ya nne mlango wa chumba hicho ukaonekana ukifunguliwa na mwanaume aliyevalia koti jeupe akatokeza, Phillip alipomwangalia alimgundua kwamba alikuwa ni daktari hivyo wakajikuta wakigonganisha macho na daktari akainama chini.
Taratibu akionekana mwenye huzuni akamsogelea Phillip kisha akamsabahi na kumtaka kuongozana naye mpaka ofisini kwa maongezi zaidi.
Ndani ya ofisi tu baada ya kuingia daktari hakutaka kupoteza muda zaidi alimtaka Phillip aketi kwenye kiti naye akaketi, ni hapo ndipo alipomweleza ukweli ambao alitakiwa kuufahamu.
“Pole sana ndugu yetu, sisi kama madaktari pamoja na wauguzi tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu wote kuokoa maisha ya mke wako lakini imeshindi…”
“Lina wangu amefariki?” Phillip alitamka kwa sauti akinyanyuka kitini.
“Wewe ni mwanaume hebu jikaze kidogo kwani hayo ndiyo maisha yetu.”
“Daktari! Daktari unamaanisha unachosema?”
“Ni kweli tupu mkeo amefariki dunia akiwa juu ya kitanda cha upasuaji muda mfupi tu baada ya kupasua kichwa chake.”
“Uwiii!Uwiiii!” Phillip alipiga mayowe akiwa hataki kuamini maneno aliyoyasikia kutoka kwa daktari kwamba mkewe mpendwa alikuwa ameaga dunia.
“Huo ndiyo ukweli wote, tunasikitika sana lakini pia tunakupa pole.”
Phillip hakujibu kitu tena akanyanyuka kwenye kiti akaufungua mlango na kutoka mbio kuelekea chumba cha upasuaji huku akilia kwa sauti ambayo ndiyo iliyowashtua Genevieve na Magdalana waliokuwa wameketi nje ya wodi wakimsubiri.
“Lina hayupo nasi tena, ameondoka ametuacha” aliongea Phillip huku akilia.
“Lina amefariki?”
“Huo ndiyo ukweli hatutamwona tena,” wakiwa hapo wakashuhudia mlango ukifunguliwa na machela iliyoonekana kubeba mtu juu yake akiwa amefunikwa kwa shuka la rangi ya kijani kuanzia kichwani hadi miguu ikapitishwa mbele yao.
“Mke wangu! Huyu ni mke wangu nataka nimwone, Lina wangu kweli umeniacha kama alivyoniacha Genevieve?” Phillip alilia kwa uchungu akitamka maneno ya kuumiza moyo. Wakiwa hapo huku wote wakilia wakashuhudia machela ikisukumwa na kupelekwa chumba cha maiti.
Huku wakiwa na uchungu mioyoni mwao wakaondoka kurejea nyumbani ili kufanya taratibu nyingine, taarifa mbalimbali zikatolewa juu ya tukio hilo, simu nyingi zilipigwa na watu wengi walifika nyumbani kwa Phillip kumpa pole na kuomboleza, wengi wao wakiwa wafanyakazi waliofanya kazi na Lina ofisi moja.
Siku tatu zikatolewa kwa maombolezo, watu wakilia wengi wakisikitikia kifo kilichomkuta Lina. Familia za Phillip na Lina zikajumuika pamoja hatimaye mazishi yakafanyika Phillip akitaka mkewe huyo azikwe pembeni tu mwa kaburi la mkewe wa kwanza na watoto wake. Jambo hilo likafanikiwa na Lina akazikwa akiwaacha watu wengi katika majonzi, kwa Phillip ikionekana kuwa kama ndoto lakini huo ndiyo ulikuwa ukweli.
Ni wiki moja tu baada ya Phillip kumzika mkewe mambo yalianza kubadilika, mara kadhaa akionekana kama mtu aliyekuwa na tatizo la akili na alipoulizwa hakuwa na jibu la kutoa zaidi ya kububujikwa na machozi, kazini nako mambo hayakwenda sawa hivyo wakalazimika kumpa likizo ya muda akae nyumbani pengine akili yake ingetulia.
Ni kama vile uamuzi huo walikuwa wameukosea, kwani Phillip badala ya kubadilika hali ndiyo ikazidi kuwa mbaya, akawa mlevi kupindukia na kuongea peke yake, jambo lililozidi kuishangaza familia yake.
“Baba kwa nini umekuwa hivyo?” Genevieve aliuliza. Alikuwa ni mtoto mdogo lakini alikuwa na upeo wa kufahamu mazuri na mabaya.
“Dunia hainitendei haki, ilichukua mke na watoto wangu wawili na sasa imegeuka na kumchukua Lina… ni bora na mimi niwafuate na kuungana nao, bora nife…nasem…” aliongea huku kwikwi ya kulia ikimkaba, haraka akanyanyuka kutoka kitini na kukimbia kuelekea chumbani.
“Baba!Baba!” mtoto Genevieve alikimbia kumfuata baba yake lakini tayari alishachelewa aliposhika mlango ili ausukume kuingia ndani ulionekana kufungwa.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom