Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 09
KWA hakika nilichanganyikiwa macho yangu yaliganda kwa muda ndani ya gari nikimwangalia Tyra kwa macho ya matamanio kisha nikayarudisha tena kwa Monalisa ambaye taratibu alikuwa akitembea kuja upande wetu.
Mwili ulinitetemeka lakini nilijitahidi sana kuficha hali hiyo. Sikutaka kuonekana dhaifu lakini lazima nikiri kwamba wanawake hao wawili waliuchanganya sana moyo wangu.
“Phillip get in the car, please!” (Phillip ingia kwenye gari tafadhali!)Tyra aliniambia kwa sauti yenye ukali kidogo.
Kwa mara ya kwanza nilimshuhudia Tyra akizungumza kwa sauti ya ukali. Nilitulia kwa muda nikitafakari cha kufanya, kabla sijapata majibu tayari Monalisa naye alikuwa anaongea.
“Come with me, please, baby!” (Tafadhali njoo huku, mpenzi.)
Kwa kweli nilichanganyikiwa nikapoteza mwelekeo, nikashindwa kuelewa kitu cha kufanya. Sekunde chache baadaye Monalisa alikuwa ameshafika nilipokuwa nimesimama, akanipigapiga begani kisha akaanza kuzungumza tena:
“Phillip why can’t you here my voice, please. Let’s go!” (Philip mbona husikii sauti yangu tafadhali. Twen’zetu!)
“Excuse me, Monalisa. I am going somewhere with Tyra, I had an appointment with her.” (Samahani Monalisa. Ninakwenda sehemu fulani na Tyra, nilikuwa na ahadi naye.)
Hata hivyo, moyoni nilijua kabisa kwamba nilimjibu kwa kumridhisha maana sikuwa na ahadi naye. Isitoshe hakuna yeyote kati yao niliyekuwa na uhusiano naye wa kimapenzi, hivyo nilikuwa na uhuru wa kufanya chochote bila ruhusa ya yeyote.
“Where to?” (Wapi huko?)
“Bagamoyo.”
“Who is this girl?” (Huyu msichana ni nani?)
“She is just my friend.” (Ni rafiki yangu tu.)
“If it is so, can’t you postpone it as I have very important talks with you?” (Kama ndiyo hivyo, huwezi kuahirisha maana nina mazungumzo muhimu nawe?”
Nilishangazwa na jinsi Monalisa anavyojiamini, isingekuwa rahisi kwa mwanamke mwingine kujiamini na kuongea na mwanaume maneno yale mbele ya mwenzake ambaye hajajua uhusiano wao.
Sikuwa mwepesi kujibu swali lake, nilichokifanya ni kusoma kupitia macho ya Tyra. Nilichokifanya ni kuinama kidogo kisha kuchungulia kwenye kioo cha gari nikakutana na macho ya Tyra yakizungumza; alikuwa analia.
Moyo wangu ukaenda mbio, Tyra hakujua kitu kimoja machozi yake yalimfanya azidi kuonekana mrembo zaidi. Nikahisi huruma moyoni mwangu. Ni kweli kwamba Tyra alitaka kutoka na mimi, tena ni yeye aliyenipigia simu kuniomba, nami kwa moyo mkunjufu nikamkubalia.
Kwa vile hakuna yeyote kati yao niliyekuwa na uhusiano naye wa kimapenzi ilikuwa rahisi sana kufanya uamuzi. Kitu pekee nilichotakiwa kukifanya ni kuondoka na Tyra kama nilivyokuwa nimekubaliana naye mwanzoni.
Nikainua kichwa changu kisha nikayatuliza macho yangu juu ya uso wa Monalisa. Midomo yangu ikaanza kucheza, nilikuwa natafakari maneno ya kumwambia ili aridhike.
“Excuse me, Monalisa. I cannot go out with you today as I already have an appointment with Tyra. I am sorry for inconveniencing you, but I believe you will understand me.” (Samahani Monalisa. Siwezi kutoka na wewe leo kwa sababu tayari nilikuwa na ahadi na Tyra. Samahani kama nitakuwa nimekuudhi, lakini naamini umenielewa.)
Baada ya hapo sikuongea neno jingine lolote zaidi ya kufungua mlango na kuketi upande wa abiria, nikageuza shingo yangu kumwangalia Tyra, alikuwa akijifuta machozi kwa kitambaa cheupe.
“Excuse me, Tyra. I did not like this to happen. Let’s go,” (Samahani sana Tyra, sikupenda haya yatokee, washa gari twende), nilimwambia Tyra nikiwa nimeyatuliza macho yangu usoni mwake.
Kitu cha ajabu, hakusema neno lolote zaidi ya kuwasha gari kisha akageuza na kuliondoa kwa kasi. Monalisa akabaki anatusindikiza kwa macho hadi tulipotokomea. Nilikuwa kimya kwenye gari, nikitafakari mambo yaliyotokea.
Kwa kweli sikuwa na la kuzungumza na Trya ambaye alionekana kuvimba kwa hasira. Kimsingi hakuwa na sababu ya kukasirika maana ni kweli kwamba hakuwa na uhusiano na mimi. Ukimya wangu ulimfanya naye awe kimya!
Mpaka tunafika Mwenge, hakuna aliyezungumza na mwenzake, gari likakata kushoto kuifuata barabara ya Bagamoyo na kwenda kwa kasi ile ile. Kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni kabisa siku hiyo, hivyo alikuwa na uwezo wa kuendesha kwa kasi aliyoipenda.
Nilijitahidi kukaa kimya, lakini tulipofika Mapinga, nilishindwa kuvumilia. Nikaamua kufungua kinywa changu na kuanzisha mazungumzo.
“Mbona umenyamaza muda wote? Bado una hasira Tyra?” Niliongea kwa sauti ya taratibu kabisa.
“Tutaongea Bagamoyo!”
“Ok!”
Ni kama Tyra alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mimi maana tukio la Monalisa lilimchanganya sana kichwa chake. Ni kweli hakufungua tena kinywa chake kuongea na mimi hadi tulipoingia Bagamoyo katika Hoteli ya Paradise, tukashuka na kwenda kukaa kwenye moja ya meza zilizokuwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi.
Punde mhudumu alifika kutusikiliza, tukaagiza vinywaji na vyakula. Muda mfupi baadaye alituletea vinywaji kisha akatuambia kwamba vyakula vilikuwa vikitayarishwa jikoni na vingeletwa mezani baada ya dakika thelathini na tano.
Tukaanza kunywa pamoja lakini usoni Tyra alionekana kama anatunga sheria. Uso wake ulionesha kuwa ana mambo mengi sana yanayomchanganya.
“Ndiyo umefanya nini Phillip?”
“Kwa nini? Kivipi?”
“Hujui ulichokifanya?”
“Niambie basi!”
“Sikutegemea kama uliniita ili uniumize. Kwa nini unanitesa kiasi hicho?”
“Unajua mpaka sasa hivi sijakuelewa Tyra, bila shaka unazungumza kuhusu Monalisa.”
“Ndiyo huyo huyo Monalisa wako ambaye nilikwambia mchana kwamba chuo kizima kinajua uhusiano wenu ukakataa, sasa nimeshuhudia kwa macho yangu.”
“Tyra kwani sitakiwi kuwa na marafiki?”
“Simaanishi hivyo lakini kwa nini unautesa moyo wangu kwa kiwango hicho?”
“Inabidi uwe muwazi zaidi ya hapo!”
“BABY I LOVE YOU SO MUCH I HAVE ALWAYS SHOWED YOU VARIOUS SIGNS AND DONE MANY THINGS TO SHOW YOU MY LOVE. DO YOU WANT TO TELL ME THAT YOU DO NOT SEE THEM? WHY DO YOU WANT TO TORTURE ME IN THIS WAY? PLEASE, I ASK YOU TO OPEN YOUR HEART FOR ME. I LOVE YOU PHILLIP!” (Mpenzi nakupenda sana, kila mara nimekuwa nikikuonesha ishara kadhaa za mapenzi yangu kwako. Unataka kuniambia huzioni? Kwa nini unataka kunitesa kiasi hiki? Tafadhali naomba uufungue moyo wako unikaribishe. Nakupenda Phillip!) Tyra alitamka maneno haya akionesha hisia kali za mapenzi.
Nilisisimka mwili, aliongea maneno mazito ambayo yalinichoma. Kwa hakika nilimwonea huruma, nikatamani kuwa naye lakini tatizo lilikuwa ni Zamaradi. Kwa mbali nilianza kuhisi harufu ya manukato ya Zamaradi wangu. Woga uliongezeka baada ya kugundua kwamba tulikuwa tumekaa ufukweni mwa bahari, eneo ambalo ndani yake ndiyo makazi ya Zamaradi.
HAKIKA Tyra alikuwa akinieleza maneno mazito sana, siwezi kumlaumu maana zilikuwa ni hisia kutoka ndani ya moyo wake. Alikuwa na haki ya msingi ya kueleza kila alichojisikia moyoni mwake.
Nilitegemea kusikia maneno hayo, maana siku zote niligundua kwamba Tyra alikuwa akinipenda sana. Si yeye peke yake bali wanawake wengi kila wanaponitazama walivutiwa na mimi. Haikuwa kosa lake bali moyo wake.
Ni kweli hata mimi nilimpenda sana, hilo napenda nikiri mbele yenu, lakini nisingeweza kuwa na mwanamke mwingine tofauti na Zamaradi. Natamani sana jambo hilo litokee lakini niliogopa kutokana na maneno ya Zamaradi aliyokuwa akijiapiza mara kwa mara anaponitokea usiku.
Ukimya wangu ukamfanya Tyra apate wasiwasi, alitamani kusikia sauti yangu nikisema chochote kuhusu ombi lake. Akayatuliza macho yake usoni mwangu, nami pia. Hata hivyo, sikuwa na jibu la kumpa.
“Phillip!” Tyra aliita kwa sauti ya taratibu sana.
“Nakusikia.”
“Nasubiri jibu lako.”
“Samahani, hatuwezi kubaki kuwa marafiki?”
“Hapana, acha utani wako bwana. Kumbuka hizi ni hisia za ndani ya moyo wangu. Naomba usizidhihaki, nipokee tafadhali. Nakupenda!”
“Najua lakini kwa nionavyo mimi, tunapendeza tukibaki hivi tulivyo kuliko kuanza uhusiano mwingine mpya!”
“Hapana sikia kilio changu, mimi nakupenda.”
“Najua hata mimi nakupenda tena nakupenda zaidi ya unavyonipenda, lakini kwa sababu ya mapenzi hayo ndiyo maana sitaki tuanzishe kitu kingine tofauti.”
“Mbona sikuelewi?”
“Hautanielewa kirahisi lakini unachotakiwa kufahamu ni kwamba ni hatari sana mimi kuwa na uhusiano na wewe. Tafadhali naomba uelewe.”
“Mbona sikuelewi? Unanichanganya kabisa!”
Kufikia hapo nikazidi kuchanganyikiwa maana Tyra alikuwa king’ang’anizi kweli kweli. Akanisogelea nilipokuwa nimekaa kisha akanikalia, hapo woga ukanizidi, nikamwona kabisa Zamaradi akija mbele yangu, kitu ambacho sikutaka kabisa kitokee.
Kwa mara nyingine nikaanza kumchukia tena Zamaradi, ni kweli alikuwa mwanamke mzuri lakini alininyima uhuru wa kufanya mambo yangu. Mbaya zaidi hatokei katika hali ya kawaida, ananinyanyasa na kuninyima uhuru.
Lakini sikutaka matatizo na Zamaradi, hivyo nikamsukuma Tyra aliyeanguka pembeni. Akaanza kulia kwa uchungu huku akilaumu kitendo nilichomfanyia.
“Kwa nini unanifanyia hivi, kwa sababu nimekupenda?”
“Hapana napenda sana maisha yako, utapata matatizo, usitake kuwa na mimi. Tafadhali niondoe kichwani mwako, nifanye kama rafiki tu,” nikamwambia kwa uchungu moyoni.
Maneno hayo ni kama hayakumwingia kabisa Tyra ambaye aliinuka pale chini na kunifuata kisha kunikumbatia kwa nguvu akiuleta mdomo wake kinywani mwangu, nilijua kilichotaka kutokea, sikuwa tayari.
Nikamsukuma kwa nguvu, akaanguka pembeni. Nikatumia nafasi hiyo kukimbia. Nilipofanya hivyo alinikimbiza kwa nyuma huku akiita jina langu lakini sikugeuka. Hakuweza kunikimbiza umbali mrefu nikafanikiwa kutoka nje ya geti la Hoteli ya Paradise kisha nikasimamisha pikipiki iliyonipeleka hadi kituo cha mabasi.
Hapo nikapanda basi linaloelekea Mwenge, Dar es Salaam. Moyoni nilikuwa na maumivu makali. Sikutaka kumuumiza kiasi kile Tyra lakini sikuwa na jinsi ya kufanya. Ilikuwa ni lazima niondoke maana maisha yake na yangu yalikuwa muhimu sana.
Nilimfahamu vyema Zamaradi, siku zote huwa na hasira sana juu yangu, nilijua kama ningeendelea kuwa na Tyra katika hali ile, lazima angemdhuru. Lakini pia nilisubiri adhabu yangu usiku ambapo nilitegemea lazima angenijia.
Nikiwa kituoni nilifanikiwa kupanda basi lililonifikisha mpaka Mwenge ambapo nilipanda daladala inayoelekea chuo. Niliposhuka katika kituo cha Utawala, macho yangu yaligongana na Monalisa aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Cresta. Akapiga honi kisha akafinya mkono kuashiria kuniita.
“Nakuja!” nilisema nikivuka upande wa pili.
“Ingia kwenye gari tafadhali,” alisema Monalisa kwa mtindo wa kuamrisha.
Nami nikaingia. Hakusema neno lolote zaidi ya kuwasha gari kisha akakata kulia akiifuata barabara ya chuo kuelekea kwenye geti la kwenda Ubungo.
“Vipi usharudi Bagamoyo?” aliuliza Monalisa akinitizama usoni.
“Ndiyo!” Nikamjibu kwa kifupi.
“Ok! Naona uliamua kuniacha sababu ya Tyra, lakini ni vile tu hujajua ni kiasi gani nakupenda. Ungenipa nafasi hiyo ningekuonyesha mapenzi motomoto.”
Hakujua ni kiasi gani maneno yake yalinichoma maana nilimkimbia Tyra huko Bagamoyo kutokana na mambo kama aliyoniambia. Nilimshangaa lakini pia nilimwonea huruma.
“Hatuwezi kubadilisha stori?”
“Tunaweza, naona unachukia sana tukizungumza kuhusu huyo mwanamke wako.”
“Halafu tunaelekea wapi?”
“Hapa Mlimani City, hutaki kukaa na mimi japo tupate maji ya matunda?”
“Ok!”
Monalisa akaendelea kuendesha gari hadi Mlimani City ambapo tulitafuta sehemu tukakaa na kuanza kula na kunywa. Tuliongea mambo mengi sana, kitu kilichonifurahisha zaidi ni kwamba Monalisa alinielewa maana hakuzungumza tena mambo ya mapenzi.
Tukaendelea kunywa kwa furaha hadi usiku sana. Monalisa akaniambia tuondoke, mimi nilikuwa nimeshika boksi lenye juisi na Monalisa alikuwa na boksi lenye mvinyo mweupe. Tulipoingia kwenye gari nikaanza kuhisi kuchangamka ghafla, ni hali ambayo sikuielewa, maana ilifikia mahali Monalisa alikuwa akinibusu nami nikamrudishia. Baada ya hapo sikukumbuka kitu chochote.
***
Utulivu ule ulinishitusha kidogo, lakini joto la mwanamke akiwa pembani yangu lilinizidishia woga, nilipofungua macho yangu na kujiangalia vizuri nikagundua kwamba nilikuwa mtupu na Monalisa.
Haikunichukua muda mrefu kugundua kwamba nilikuwa nimefanya mapenzi na Monalisa tena pembeni mwa barabara, ndani ya gari. Nikashituka sana.
“Umenifanya nini Monalisa?”
“Usiogope kwani hujui tulichokifanya? Naomba unisamehe lakini sikuwa na njia nyingine yoyote ya kukufanya uelewe kwamba nakupenda.”
“Utapata matatizo, nakuonea huruma sana, hatupaswi kufanya hivi.”
“I DON’T CARE PROVIDED I LOVE YOU, I’M READY FOR ANY EVENTUALITY!” (Sijali, maadam nakupenda nipo tayari kwa lolote.) Monalisa aliniambia akionesha kujiamini sana.
Nilimuonea huruma, maana hakujua kama kuna Zamaradi, mwanamke wa ndotoni mwangu ambaye ni hatari sana.
KWA hakika nilichanganyikiwa macho yangu yaliganda kwa muda ndani ya gari nikimwangalia Tyra kwa macho ya matamanio kisha nikayarudisha tena kwa Monalisa ambaye taratibu alikuwa akitembea kuja upande wetu.
Mwili ulinitetemeka lakini nilijitahidi sana kuficha hali hiyo. Sikutaka kuonekana dhaifu lakini lazima nikiri kwamba wanawake hao wawili waliuchanganya sana moyo wangu.
“Phillip get in the car, please!” (Phillip ingia kwenye gari tafadhali!)Tyra aliniambia kwa sauti yenye ukali kidogo.
Kwa mara ya kwanza nilimshuhudia Tyra akizungumza kwa sauti ya ukali. Nilitulia kwa muda nikitafakari cha kufanya, kabla sijapata majibu tayari Monalisa naye alikuwa anaongea.
“Come with me, please, baby!” (Tafadhali njoo huku, mpenzi.)
Kwa kweli nilichanganyikiwa nikapoteza mwelekeo, nikashindwa kuelewa kitu cha kufanya. Sekunde chache baadaye Monalisa alikuwa ameshafika nilipokuwa nimesimama, akanipigapiga begani kisha akaanza kuzungumza tena:
“Phillip why can’t you here my voice, please. Let’s go!” (Philip mbona husikii sauti yangu tafadhali. Twen’zetu!)
“Excuse me, Monalisa. I am going somewhere with Tyra, I had an appointment with her.” (Samahani Monalisa. Ninakwenda sehemu fulani na Tyra, nilikuwa na ahadi naye.)
Hata hivyo, moyoni nilijua kabisa kwamba nilimjibu kwa kumridhisha maana sikuwa na ahadi naye. Isitoshe hakuna yeyote kati yao niliyekuwa na uhusiano naye wa kimapenzi, hivyo nilikuwa na uhuru wa kufanya chochote bila ruhusa ya yeyote.
“Where to?” (Wapi huko?)
“Bagamoyo.”
“Who is this girl?” (Huyu msichana ni nani?)
“She is just my friend.” (Ni rafiki yangu tu.)
“If it is so, can’t you postpone it as I have very important talks with you?” (Kama ndiyo hivyo, huwezi kuahirisha maana nina mazungumzo muhimu nawe?”
Nilishangazwa na jinsi Monalisa anavyojiamini, isingekuwa rahisi kwa mwanamke mwingine kujiamini na kuongea na mwanaume maneno yale mbele ya mwenzake ambaye hajajua uhusiano wao.
Sikuwa mwepesi kujibu swali lake, nilichokifanya ni kusoma kupitia macho ya Tyra. Nilichokifanya ni kuinama kidogo kisha kuchungulia kwenye kioo cha gari nikakutana na macho ya Tyra yakizungumza; alikuwa analia.
Moyo wangu ukaenda mbio, Tyra hakujua kitu kimoja machozi yake yalimfanya azidi kuonekana mrembo zaidi. Nikahisi huruma moyoni mwangu. Ni kweli kwamba Tyra alitaka kutoka na mimi, tena ni yeye aliyenipigia simu kuniomba, nami kwa moyo mkunjufu nikamkubalia.
Kwa vile hakuna yeyote kati yao niliyekuwa na uhusiano naye wa kimapenzi ilikuwa rahisi sana kufanya uamuzi. Kitu pekee nilichotakiwa kukifanya ni kuondoka na Tyra kama nilivyokuwa nimekubaliana naye mwanzoni.
Nikainua kichwa changu kisha nikayatuliza macho yangu juu ya uso wa Monalisa. Midomo yangu ikaanza kucheza, nilikuwa natafakari maneno ya kumwambia ili aridhike.
“Excuse me, Monalisa. I cannot go out with you today as I already have an appointment with Tyra. I am sorry for inconveniencing you, but I believe you will understand me.” (Samahani Monalisa. Siwezi kutoka na wewe leo kwa sababu tayari nilikuwa na ahadi na Tyra. Samahani kama nitakuwa nimekuudhi, lakini naamini umenielewa.)
Baada ya hapo sikuongea neno jingine lolote zaidi ya kufungua mlango na kuketi upande wa abiria, nikageuza shingo yangu kumwangalia Tyra, alikuwa akijifuta machozi kwa kitambaa cheupe.
“Excuse me, Tyra. I did not like this to happen. Let’s go,” (Samahani sana Tyra, sikupenda haya yatokee, washa gari twende), nilimwambia Tyra nikiwa nimeyatuliza macho yangu usoni mwake.
Kitu cha ajabu, hakusema neno lolote zaidi ya kuwasha gari kisha akageuza na kuliondoa kwa kasi. Monalisa akabaki anatusindikiza kwa macho hadi tulipotokomea. Nilikuwa kimya kwenye gari, nikitafakari mambo yaliyotokea.
Kwa kweli sikuwa na la kuzungumza na Trya ambaye alionekana kuvimba kwa hasira. Kimsingi hakuwa na sababu ya kukasirika maana ni kweli kwamba hakuwa na uhusiano na mimi. Ukimya wangu ulimfanya naye awe kimya!
Mpaka tunafika Mwenge, hakuna aliyezungumza na mwenzake, gari likakata kushoto kuifuata barabara ya Bagamoyo na kwenda kwa kasi ile ile. Kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni kabisa siku hiyo, hivyo alikuwa na uwezo wa kuendesha kwa kasi aliyoipenda.
Nilijitahidi kukaa kimya, lakini tulipofika Mapinga, nilishindwa kuvumilia. Nikaamua kufungua kinywa changu na kuanzisha mazungumzo.
“Mbona umenyamaza muda wote? Bado una hasira Tyra?” Niliongea kwa sauti ya taratibu kabisa.
“Tutaongea Bagamoyo!”
“Ok!”
Ni kama Tyra alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mimi maana tukio la Monalisa lilimchanganya sana kichwa chake. Ni kweli hakufungua tena kinywa chake kuongea na mimi hadi tulipoingia Bagamoyo katika Hoteli ya Paradise, tukashuka na kwenda kukaa kwenye moja ya meza zilizokuwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi.
Punde mhudumu alifika kutusikiliza, tukaagiza vinywaji na vyakula. Muda mfupi baadaye alituletea vinywaji kisha akatuambia kwamba vyakula vilikuwa vikitayarishwa jikoni na vingeletwa mezani baada ya dakika thelathini na tano.
Tukaanza kunywa pamoja lakini usoni Tyra alionekana kama anatunga sheria. Uso wake ulionesha kuwa ana mambo mengi sana yanayomchanganya.
“Ndiyo umefanya nini Phillip?”
“Kwa nini? Kivipi?”
“Hujui ulichokifanya?”
“Niambie basi!”
“Sikutegemea kama uliniita ili uniumize. Kwa nini unanitesa kiasi hicho?”
“Unajua mpaka sasa hivi sijakuelewa Tyra, bila shaka unazungumza kuhusu Monalisa.”
“Ndiyo huyo huyo Monalisa wako ambaye nilikwambia mchana kwamba chuo kizima kinajua uhusiano wenu ukakataa, sasa nimeshuhudia kwa macho yangu.”
“Tyra kwani sitakiwi kuwa na marafiki?”
“Simaanishi hivyo lakini kwa nini unautesa moyo wangu kwa kiwango hicho?”
“Inabidi uwe muwazi zaidi ya hapo!”
“BABY I LOVE YOU SO MUCH I HAVE ALWAYS SHOWED YOU VARIOUS SIGNS AND DONE MANY THINGS TO SHOW YOU MY LOVE. DO YOU WANT TO TELL ME THAT YOU DO NOT SEE THEM? WHY DO YOU WANT TO TORTURE ME IN THIS WAY? PLEASE, I ASK YOU TO OPEN YOUR HEART FOR ME. I LOVE YOU PHILLIP!” (Mpenzi nakupenda sana, kila mara nimekuwa nikikuonesha ishara kadhaa za mapenzi yangu kwako. Unataka kuniambia huzioni? Kwa nini unataka kunitesa kiasi hiki? Tafadhali naomba uufungue moyo wako unikaribishe. Nakupenda Phillip!) Tyra alitamka maneno haya akionesha hisia kali za mapenzi.
Nilisisimka mwili, aliongea maneno mazito ambayo yalinichoma. Kwa hakika nilimwonea huruma, nikatamani kuwa naye lakini tatizo lilikuwa ni Zamaradi. Kwa mbali nilianza kuhisi harufu ya manukato ya Zamaradi wangu. Woga uliongezeka baada ya kugundua kwamba tulikuwa tumekaa ufukweni mwa bahari, eneo ambalo ndani yake ndiyo makazi ya Zamaradi.
HAKIKA Tyra alikuwa akinieleza maneno mazito sana, siwezi kumlaumu maana zilikuwa ni hisia kutoka ndani ya moyo wake. Alikuwa na haki ya msingi ya kueleza kila alichojisikia moyoni mwake.
Nilitegemea kusikia maneno hayo, maana siku zote niligundua kwamba Tyra alikuwa akinipenda sana. Si yeye peke yake bali wanawake wengi kila wanaponitazama walivutiwa na mimi. Haikuwa kosa lake bali moyo wake.
Ni kweli hata mimi nilimpenda sana, hilo napenda nikiri mbele yenu, lakini nisingeweza kuwa na mwanamke mwingine tofauti na Zamaradi. Natamani sana jambo hilo litokee lakini niliogopa kutokana na maneno ya Zamaradi aliyokuwa akijiapiza mara kwa mara anaponitokea usiku.
Ukimya wangu ukamfanya Tyra apate wasiwasi, alitamani kusikia sauti yangu nikisema chochote kuhusu ombi lake. Akayatuliza macho yake usoni mwangu, nami pia. Hata hivyo, sikuwa na jibu la kumpa.
“Phillip!” Tyra aliita kwa sauti ya taratibu sana.
“Nakusikia.”
“Nasubiri jibu lako.”
“Samahani, hatuwezi kubaki kuwa marafiki?”
“Hapana, acha utani wako bwana. Kumbuka hizi ni hisia za ndani ya moyo wangu. Naomba usizidhihaki, nipokee tafadhali. Nakupenda!”
“Najua lakini kwa nionavyo mimi, tunapendeza tukibaki hivi tulivyo kuliko kuanza uhusiano mwingine mpya!”
“Hapana sikia kilio changu, mimi nakupenda.”
“Najua hata mimi nakupenda tena nakupenda zaidi ya unavyonipenda, lakini kwa sababu ya mapenzi hayo ndiyo maana sitaki tuanzishe kitu kingine tofauti.”
“Mbona sikuelewi?”
“Hautanielewa kirahisi lakini unachotakiwa kufahamu ni kwamba ni hatari sana mimi kuwa na uhusiano na wewe. Tafadhali naomba uelewe.”
“Mbona sikuelewi? Unanichanganya kabisa!”
Kufikia hapo nikazidi kuchanganyikiwa maana Tyra alikuwa king’ang’anizi kweli kweli. Akanisogelea nilipokuwa nimekaa kisha akanikalia, hapo woga ukanizidi, nikamwona kabisa Zamaradi akija mbele yangu, kitu ambacho sikutaka kabisa kitokee.
Kwa mara nyingine nikaanza kumchukia tena Zamaradi, ni kweli alikuwa mwanamke mzuri lakini alininyima uhuru wa kufanya mambo yangu. Mbaya zaidi hatokei katika hali ya kawaida, ananinyanyasa na kuninyima uhuru.
Lakini sikutaka matatizo na Zamaradi, hivyo nikamsukuma Tyra aliyeanguka pembeni. Akaanza kulia kwa uchungu huku akilaumu kitendo nilichomfanyia.
“Kwa nini unanifanyia hivi, kwa sababu nimekupenda?”
“Hapana napenda sana maisha yako, utapata matatizo, usitake kuwa na mimi. Tafadhali niondoe kichwani mwako, nifanye kama rafiki tu,” nikamwambia kwa uchungu moyoni.
Maneno hayo ni kama hayakumwingia kabisa Tyra ambaye aliinuka pale chini na kunifuata kisha kunikumbatia kwa nguvu akiuleta mdomo wake kinywani mwangu, nilijua kilichotaka kutokea, sikuwa tayari.
Nikamsukuma kwa nguvu, akaanguka pembeni. Nikatumia nafasi hiyo kukimbia. Nilipofanya hivyo alinikimbiza kwa nyuma huku akiita jina langu lakini sikugeuka. Hakuweza kunikimbiza umbali mrefu nikafanikiwa kutoka nje ya geti la Hoteli ya Paradise kisha nikasimamisha pikipiki iliyonipeleka hadi kituo cha mabasi.
Hapo nikapanda basi linaloelekea Mwenge, Dar es Salaam. Moyoni nilikuwa na maumivu makali. Sikutaka kumuumiza kiasi kile Tyra lakini sikuwa na jinsi ya kufanya. Ilikuwa ni lazima niondoke maana maisha yake na yangu yalikuwa muhimu sana.
Nilimfahamu vyema Zamaradi, siku zote huwa na hasira sana juu yangu, nilijua kama ningeendelea kuwa na Tyra katika hali ile, lazima angemdhuru. Lakini pia nilisubiri adhabu yangu usiku ambapo nilitegemea lazima angenijia.
Nikiwa kituoni nilifanikiwa kupanda basi lililonifikisha mpaka Mwenge ambapo nilipanda daladala inayoelekea chuo. Niliposhuka katika kituo cha Utawala, macho yangu yaligongana na Monalisa aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Cresta. Akapiga honi kisha akafinya mkono kuashiria kuniita.
“Nakuja!” nilisema nikivuka upande wa pili.
“Ingia kwenye gari tafadhali,” alisema Monalisa kwa mtindo wa kuamrisha.
Nami nikaingia. Hakusema neno lolote zaidi ya kuwasha gari kisha akakata kulia akiifuata barabara ya chuo kuelekea kwenye geti la kwenda Ubungo.
“Vipi usharudi Bagamoyo?” aliuliza Monalisa akinitizama usoni.
“Ndiyo!” Nikamjibu kwa kifupi.
“Ok! Naona uliamua kuniacha sababu ya Tyra, lakini ni vile tu hujajua ni kiasi gani nakupenda. Ungenipa nafasi hiyo ningekuonyesha mapenzi motomoto.”
Hakujua ni kiasi gani maneno yake yalinichoma maana nilimkimbia Tyra huko Bagamoyo kutokana na mambo kama aliyoniambia. Nilimshangaa lakini pia nilimwonea huruma.
“Hatuwezi kubadilisha stori?”
“Tunaweza, naona unachukia sana tukizungumza kuhusu huyo mwanamke wako.”
“Halafu tunaelekea wapi?”
“Hapa Mlimani City, hutaki kukaa na mimi japo tupate maji ya matunda?”
“Ok!”
Monalisa akaendelea kuendesha gari hadi Mlimani City ambapo tulitafuta sehemu tukakaa na kuanza kula na kunywa. Tuliongea mambo mengi sana, kitu kilichonifurahisha zaidi ni kwamba Monalisa alinielewa maana hakuzungumza tena mambo ya mapenzi.
Tukaendelea kunywa kwa furaha hadi usiku sana. Monalisa akaniambia tuondoke, mimi nilikuwa nimeshika boksi lenye juisi na Monalisa alikuwa na boksi lenye mvinyo mweupe. Tulipoingia kwenye gari nikaanza kuhisi kuchangamka ghafla, ni hali ambayo sikuielewa, maana ilifikia mahali Monalisa alikuwa akinibusu nami nikamrudishia. Baada ya hapo sikukumbuka kitu chochote.
***
Utulivu ule ulinishitusha kidogo, lakini joto la mwanamke akiwa pembani yangu lilinizidishia woga, nilipofungua macho yangu na kujiangalia vizuri nikagundua kwamba nilikuwa mtupu na Monalisa.
Haikunichukua muda mrefu kugundua kwamba nilikuwa nimefanya mapenzi na Monalisa tena pembeni mwa barabara, ndani ya gari. Nikashituka sana.
“Umenifanya nini Monalisa?”
“Usiogope kwani hujui tulichokifanya? Naomba unisamehe lakini sikuwa na njia nyingine yoyote ya kukufanya uelewe kwamba nakupenda.”
“Utapata matatizo, nakuonea huruma sana, hatupaswi kufanya hivi.”
“I DON’T CARE PROVIDED I LOVE YOU, I’M READY FOR ANY EVENTUALITY!” (Sijali, maadam nakupenda nipo tayari kwa lolote.) Monalisa aliniambia akionesha kujiamini sana.
Nilimuonea huruma, maana hakujua kama kuna Zamaradi, mwanamke wa ndotoni mwangu ambaye ni hatari sana.