fleha
Senior Member
- Oct 9, 2014
- 111
- 103
MNYAMA NDANI YANGU!
SEHEMU YA KWANZA
Na Nira Saire
Ilikuwa ni siku ya Alhamis majira ya saa nne za asubuhi nikiwa darasani nikisoma na wanafunzi wenzangu, mara hali yangu kiafya ikaanza kubadilika! Ikawa nahisi maumivu ya kichwa yakinianza polepole huku yakiambatana na kizunguzungu!. Nikaamua kulaza kichwa changu kwenye meza ya kusomea iliyokuwa mbele yangu ili kuweza kujisikilizia, nikiamini kuwa maumivu yale yangepita lakini hali ilikuwa tofauti na matarajio yangu,kwani maumivu yalizidi mara dufu hadi nikaanza kujihisi kuchanganyikiwa!. Akili ikanituma kuelekea kwenye vyoo vya shule ili niweze kupata maji ambayo niliamini kama ningeyatia kichwani basi yangeweza kunisaidia kupata unafuu, wakati huu rafiki yangu Majoba alikuwa amegundua kuwa sikuwa sawa hivyo akanifuata nilipokuwa natoka nje ya darasa lile huku akiniuliza nilikuwa na tatizo gani, sikuweza hata kumjibu, mimi niliendelea kukazana kuelekea maeneo ya vyoo naye akaendelea kunifuata kwa kasi akizidi kunisemesha, hata sikuweza kumsikia tena alikuwa anasema nini na wala sikuweza kujua nini kiliendelea kwani nilipoteza fahamu!......
Fahamu zilipokuja kunirudia nilijikuta katika mazingira ambayo yalikuwa ni mageni sana kwangu, lilikuwa ni eneo ambalo lilikuwa na miti mingi sana na kwa haraka haraka sikukumbuka kama nilishawahi kuwepo kwenye eneo lile abla, wakati huo fahamu ziliendelea kunirudia taratibu nikaanza kukumbuka safari yangu ya kutoka darasani na kuelekea eneo la vyoo vya shule, lakini kila nilipojaribu kukumbuka nini kilifuata nilibaki kuishia gizani. “unajisikiaje?” ilisikika sauti ikizungumza kutoka nyuma yangu, nilishtushwa sana na sauti ile kwa maana sikutegemea kama kuliuwa na mtu pale! Nikageuka na kumtizama mtu yule ambaye alikuwa ni mzee, “shikamoo” nikajikuta nimemsalimia, nikiwa bado nipo katika hali ya wasiwasi, mzee yule akaoesha tabasamu ambalo bila shaka lilidhamiria kunitoa wasiwasi kisha akaitikia “Marahaba Musa, maumivu ya kichwa yameisha?” Nikazidi kushangazwa baada ya kuona kuwa mzee yule alikuwa akinifahamu,kwani kwangu ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona! “ndio, lakini bado nahisi kizungu” nilijibu. Mzee yule akanipa kikombe ambacho kilikuwa na kimiminika ambacho kwa muonekano wa rangi yake kilitokana na kusagwa majani fulani,”kunywa hii dawa itakupa nguvu” alisema mzee yule wakati akinikabidhi, nami nikaipokea dawa ile na kuinywa kidogo kabla sijasitisha haraka baada ya kugundua kuwa ilikuwa chungu mno! “jitahidi uimalize yote hiyo dawa” alisema mzee yule kisha akaongeza “wala usijisikilizie, kunywa yote haraka kama maji” Sijui kwanini nilikuwa namsikiliza mzee yule ambaye sikuwa nikimjua lakini nilijikuta nikitii maelekezo yake na kuimaliza ile dawa mara moja, mwili wangu ulisisimka sana wakati nikisikilizia uchungu wa ule dawa lakini msisimko ule ukaondoka na kizunguzungu kilichokuwa kimeniandama kwa muda mrefu. “inabidi nikurudishe maana sasa utakuwa unatafutwa” alisema yule mzee! “Usithubutu kumuelezea mtu yeyote juu ya jambo hili, ninajua una maswali mengi ila kesho tutaongea vizuri na utaelewa kila kitu, alinielezea mzee yule kisha akanishika kwenye paji la uso na kunisukuma kwanguvu, nikaangukia mgongo nikiwa nimekaa pale chini, nikapoteza tena fahamu!
“Musa... Musa....we Musa” Fahamu zilikuwa zikinirudia huku nikisikia sauti ya mtu ikiniita kwa mbali kama vile nilikuwa naota, mtu yule alikuwa akiendelea kuita huku akinitikisa, nilipopata kujielewa zivuri niligundua mtu yule alikuwa ni mmoja wa walimu wangu, mwalimu Mdharuba ambaye alikuwa akinifundisha somo la hisabati, nilipojaribu kutizama huku na huko nikagundua kuwa nilikuwa katika eneo la mashamba ya shule nikiwa nimezungukwa na watu wengi sana miongoni mwao wakiwemo walimu, wanafunzi pamoja na skari polisi. Mwalimu Mdharuba akanisaidia kunyanyuka pale chini na tukaanza kutembea kuelekea wenye ofisi za waalimu, moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya mkuu wa shule ambapo kundi kubwa la watu lilibaki nje huko ndani nikaingia mimi pamoja na walimu wawili na askari polisi wawili, humo ndani tukamkuta mkuu wa shule na maongezi yakaanza! Watu wote waliokuwemo mule ndani walitaka kujua nini kilikuwa kimetokea, hivyo wakawa wananiulza maswali ambayo mengi sikuwa na uwezo wa kuyajibu. Lakini katika maswali yao yale nkagundua kuwa rafiki yangu Majoba hakuwa salama kwani walikuwa wakitaka kujua alishambuliwa na nini, hilo pia lilikuwa swali gumu sana kwangu kwani mara ya mwisho mimi kumuona Majoba alikuwa salama tu! Hivyo nikajibu kuwa sikuwa najua chochote kuhusu Majoba “lakini kwa maelezo ya wanafunzi wenzenu inasemekana wewe na Majoba mlitoka darasani pamoja, je mlienda wapi baada ya kutoka darasani?” aliuliza mmoja wa maasakari. “tulitoka tukaelekea chooni” hilo ndilo jibu pekee ambalo niliweza kulitoa. “enhee, nini kikatokea huko chooni?” aliendelea kuuliza yule askari! “kwakweli sikumbuki, nimekuja kujikuta tu mkiniamsha kule kweye mashamba” nilijibu huku nikiruka sehemu ya makutano yangu na yule mzee katika pori ambalo sikuwa nikilijua!. Labda tumpeleke eneo la tukio, anaweza kuona mazingira akakumbuka nini kilitokea, alishauri askari yule mwingine ambaye alikuwa msikilizaji zaidi kwenye maongezi yale, wazo wale likapita bila kupingwa na safari ya kuelekea eneo la vyoo vya shule ikaanza!.. tulipofika eneo ambalo fahamu yangu ilipotelea nilishangaa kuona eneo lile likiwa limetapakaa damu, damu ile ilikuwa nyingi sana kiasi cha kunitia hofu juu ya usalama wa Majoba ambaye tayari nilikuwa najua alikuwa ameshambuliwa ingawa sikujua alikuwa ameshambuliwa na nani..........
Usikose sehemu ya pili!
Nipate kupita:
+255653686008
nirasaire@gmail.com
facebook.com/nira.saire
@nira_saire(instagram)
SEHEMU YA KWANZA
Na Nira Saire
Ilikuwa ni siku ya Alhamis majira ya saa nne za asubuhi nikiwa darasani nikisoma na wanafunzi wenzangu, mara hali yangu kiafya ikaanza kubadilika! Ikawa nahisi maumivu ya kichwa yakinianza polepole huku yakiambatana na kizunguzungu!. Nikaamua kulaza kichwa changu kwenye meza ya kusomea iliyokuwa mbele yangu ili kuweza kujisikilizia, nikiamini kuwa maumivu yale yangepita lakini hali ilikuwa tofauti na matarajio yangu,kwani maumivu yalizidi mara dufu hadi nikaanza kujihisi kuchanganyikiwa!. Akili ikanituma kuelekea kwenye vyoo vya shule ili niweze kupata maji ambayo niliamini kama ningeyatia kichwani basi yangeweza kunisaidia kupata unafuu, wakati huu rafiki yangu Majoba alikuwa amegundua kuwa sikuwa sawa hivyo akanifuata nilipokuwa natoka nje ya darasa lile huku akiniuliza nilikuwa na tatizo gani, sikuweza hata kumjibu, mimi niliendelea kukazana kuelekea maeneo ya vyoo naye akaendelea kunifuata kwa kasi akizidi kunisemesha, hata sikuweza kumsikia tena alikuwa anasema nini na wala sikuweza kujua nini kiliendelea kwani nilipoteza fahamu!......
Fahamu zilipokuja kunirudia nilijikuta katika mazingira ambayo yalikuwa ni mageni sana kwangu, lilikuwa ni eneo ambalo lilikuwa na miti mingi sana na kwa haraka haraka sikukumbuka kama nilishawahi kuwepo kwenye eneo lile abla, wakati huo fahamu ziliendelea kunirudia taratibu nikaanza kukumbuka safari yangu ya kutoka darasani na kuelekea eneo la vyoo vya shule, lakini kila nilipojaribu kukumbuka nini kilifuata nilibaki kuishia gizani. “unajisikiaje?” ilisikika sauti ikizungumza kutoka nyuma yangu, nilishtushwa sana na sauti ile kwa maana sikutegemea kama kuliuwa na mtu pale! Nikageuka na kumtizama mtu yule ambaye alikuwa ni mzee, “shikamoo” nikajikuta nimemsalimia, nikiwa bado nipo katika hali ya wasiwasi, mzee yule akaoesha tabasamu ambalo bila shaka lilidhamiria kunitoa wasiwasi kisha akaitikia “Marahaba Musa, maumivu ya kichwa yameisha?” Nikazidi kushangazwa baada ya kuona kuwa mzee yule alikuwa akinifahamu,kwani kwangu ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona! “ndio, lakini bado nahisi kizungu” nilijibu. Mzee yule akanipa kikombe ambacho kilikuwa na kimiminika ambacho kwa muonekano wa rangi yake kilitokana na kusagwa majani fulani,”kunywa hii dawa itakupa nguvu” alisema mzee yule wakati akinikabidhi, nami nikaipokea dawa ile na kuinywa kidogo kabla sijasitisha haraka baada ya kugundua kuwa ilikuwa chungu mno! “jitahidi uimalize yote hiyo dawa” alisema mzee yule kisha akaongeza “wala usijisikilizie, kunywa yote haraka kama maji” Sijui kwanini nilikuwa namsikiliza mzee yule ambaye sikuwa nikimjua lakini nilijikuta nikitii maelekezo yake na kuimaliza ile dawa mara moja, mwili wangu ulisisimka sana wakati nikisikilizia uchungu wa ule dawa lakini msisimko ule ukaondoka na kizunguzungu kilichokuwa kimeniandama kwa muda mrefu. “inabidi nikurudishe maana sasa utakuwa unatafutwa” alisema yule mzee! “Usithubutu kumuelezea mtu yeyote juu ya jambo hili, ninajua una maswali mengi ila kesho tutaongea vizuri na utaelewa kila kitu, alinielezea mzee yule kisha akanishika kwenye paji la uso na kunisukuma kwanguvu, nikaangukia mgongo nikiwa nimekaa pale chini, nikapoteza tena fahamu!
“Musa... Musa....we Musa” Fahamu zilikuwa zikinirudia huku nikisikia sauti ya mtu ikiniita kwa mbali kama vile nilikuwa naota, mtu yule alikuwa akiendelea kuita huku akinitikisa, nilipopata kujielewa zivuri niligundua mtu yule alikuwa ni mmoja wa walimu wangu, mwalimu Mdharuba ambaye alikuwa akinifundisha somo la hisabati, nilipojaribu kutizama huku na huko nikagundua kuwa nilikuwa katika eneo la mashamba ya shule nikiwa nimezungukwa na watu wengi sana miongoni mwao wakiwemo walimu, wanafunzi pamoja na skari polisi. Mwalimu Mdharuba akanisaidia kunyanyuka pale chini na tukaanza kutembea kuelekea wenye ofisi za waalimu, moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya mkuu wa shule ambapo kundi kubwa la watu lilibaki nje huko ndani nikaingia mimi pamoja na walimu wawili na askari polisi wawili, humo ndani tukamkuta mkuu wa shule na maongezi yakaanza! Watu wote waliokuwemo mule ndani walitaka kujua nini kilikuwa kimetokea, hivyo wakawa wananiulza maswali ambayo mengi sikuwa na uwezo wa kuyajibu. Lakini katika maswali yao yale nkagundua kuwa rafiki yangu Majoba hakuwa salama kwani walikuwa wakitaka kujua alishambuliwa na nini, hilo pia lilikuwa swali gumu sana kwangu kwani mara ya mwisho mimi kumuona Majoba alikuwa salama tu! Hivyo nikajibu kuwa sikuwa najua chochote kuhusu Majoba “lakini kwa maelezo ya wanafunzi wenzenu inasemekana wewe na Majoba mlitoka darasani pamoja, je mlienda wapi baada ya kutoka darasani?” aliuliza mmoja wa maasakari. “tulitoka tukaelekea chooni” hilo ndilo jibu pekee ambalo niliweza kulitoa. “enhee, nini kikatokea huko chooni?” aliendelea kuuliza yule askari! “kwakweli sikumbuki, nimekuja kujikuta tu mkiniamsha kule kweye mashamba” nilijibu huku nikiruka sehemu ya makutano yangu na yule mzee katika pori ambalo sikuwa nikilijua!. Labda tumpeleke eneo la tukio, anaweza kuona mazingira akakumbuka nini kilitokea, alishauri askari yule mwingine ambaye alikuwa msikilizaji zaidi kwenye maongezi yale, wazo wale likapita bila kupingwa na safari ya kuelekea eneo la vyoo vya shule ikaanza!.. tulipofika eneo ambalo fahamu yangu ilipotelea nilishangaa kuona eneo lile likiwa limetapakaa damu, damu ile ilikuwa nyingi sana kiasi cha kunitia hofu juu ya usalama wa Majoba ambaye tayari nilikuwa najua alikuwa ameshambuliwa ingawa sikujua alikuwa ameshambuliwa na nani..........
Usikose sehemu ya pili!
Nipate kupita:
+255653686008
nirasaire@gmail.com
facebook.com/nira.saire
@nira_saire(instagram)