Simulizi: Mke Wangu Juliana

Simulizi: Mke Wangu Juliana

Sehemu ya 108

Christina alikuwa akipambana kivyakevyake, ilikuwa ni lazima mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikihitaji, kuwa na John na kumfanya mwanaume wake.

Kipindi hicho alikuwa bize sana lakini baada ya kuambiwa na Amanda kulikuwa na mwanaume mwenye pesa aliyekuwa naye akaamua kurudi na kuwa naye karibu kama ilivyokuwa chuoni.

Kila siku walikuwa wakionana na kuzungumza mambo mengi, alichokuwa akikihitaji ni namba ya mwanaume huyo tu. Alijua jina lake aliitwa John, japokuwa kulikuwa na John wengi lakini aliamini baada ya kuliona jina hilo na namba angejua tu ndiye mwenyewe.

Kama walikuwa wapenzi basi John huyo ndiye aliyekuwa akiongoza kupigiwa ama kupiga hivyo ilikuwa rahisi sana kuipata namba hiyo.
Siku moja wakiwa chumbani kwa Amanda na msichana huyo kuitwa na mama yake ndiyo ilikuwa siku ambayo aliichukua simu yake na kuichukua namba hiyo.

Haikuwa kazi kutoa loki ya simu hiyo, aliijua kwa kuwa walikuwa karibu, akaiandika namba hiyo na kuisevu kwa jina jingine kabisa na sasa kazi ikabaki kwake, kuhakikisha anafanikiwa kulichukua penzi la mwanaume huyo.

Alivumilia, hakutaka kuingia kwa pupa, aliamini tu kwamba baada ya kukaa na Amanda kwa kipindi fulani angejua mengi kuhusu John.

Na hilo ndilo lililotokea, bila msichana huyo kujua akamwambia kuhusu ofisi yake ilipokuwa na mambo mengine.

Hiyo ndiyo nafasi ambayo msichana huyo alihitaji kuitumia, hakutaka kufanya jambo jingine zaidi ya kumfuata John huko Posta alipokuwa akifanya kazi.

Hakuwa akijuana naye, aliamini baada ya kuonekana mbele ya macho yake angekuwa mtu mpya na kama angekuwa kama wanaume wengine inawezekana mwanaume huyo angeusha ndoano yake na kuhitaji penzi lake.
Siku hiyo alivalia vilivyo, akaamua kuelekea huko. Kwa kuwa alikuwa na kiwowowo cha kishkaji, akavalia kisketi cha kubana kilichoishia juu ya magoti, blauzi na viatu virefu kidogo.

Kila alipokuwa akipita, alivutia, alionekana kama msichana fulani aliyekuwa na pigo za hatari mno. Wanaume wote waliokuwa wakipishana naye walikuwa wakiangalia nyuma kuangalia kijungu chake.
 
Sehemu ya 108

Christina alikuwa akipambana kivyakevyake, ilikuwa ni lazima mwisho wa siku afanikiwe kwa kile alichokuwa akikihitaji, kuwa na John na kumfanya mwanaume wake.

Kipindi hicho alikuwa bize sana lakini baada ya kuambiwa na Amanda kulikuwa na mwanaume mwenye pesa aliyekuwa naye akaamua kurudi na kuwa naye karibu kama ilivyokuwa chuoni.

Kila siku walikuwa wakionana na kuzungumza mambo mengi, alichokuwa akikihitaji ni namba ya mwanaume huyo tu. Alijua jina lake aliitwa John, japokuwa kulikuwa na John wengi lakini aliamini baada ya kuliona jina hilo na namba angejua tu ndiye mwenyewe.

Kama walikuwa wapenzi basi John huyo ndiye aliyekuwa akiongoza kupigiwa ama kupiga hivyo ilikuwa rahisi sana kuipata namba hiyo.
Siku moja wakiwa chumbani kwa Amanda na msichana huyo kuitwa na mama yake ndiyo ilikuwa siku ambayo aliichukua simu yake na kuichukua namba hiyo.

Haikuwa kazi kutoa loki ya simu hiyo, aliijua kwa kuwa walikuwa karibu, akaiandika namba hiyo na kuisevu kwa jina jingine kabisa na sasa kazi ikabaki kwake, kuhakikisha anafanikiwa kulichukua penzi la mwanaume huyo.

Alivumilia, hakutaka kuingia kwa pupa, aliamini tu kwamba baada ya kukaa na Amanda kwa kipindi fulani angejua mengi kuhusu John.

Na hilo ndilo lililotokea, bila msichana huyo kujua akamwambia kuhusu ofisi yake ilipokuwa na mambo mengine.

Hiyo ndiyo nafasi ambayo msichana huyo alihitaji kuitumia, hakutaka kufanya jambo jingine zaidi ya kumfuata John huko Posta alipokuwa akifanya kazi.

Hakuwa akijuana naye, aliamini baada ya kuonekana mbele ya macho yake angekuwa mtu mpya na kama angekuwa kama wanaume wengine inawezekana mwanaume huyo angeusha ndoano yake na kuhitaji penzi lake.
Siku hiyo alivalia vilivyo, akaamua kuelekea huko. Kwa kuwa alikuwa na kiwowowo cha kishkaji, akavalia kisketi cha kubana kilichoishia juu ya magoti, blauzi na viatu virefu kidogo.

Kila alipokuwa akipita, alivutia, alionekana kama msichana fulani aliyekuwa na pigo za hatari mno. Wanaume wote waliokuwa wakipishana naye walikuwa wakiangalia nyuma kuangalia kijungu chake.
Unatafutwa kule!
 
Sehemu ya 109

Hilo likampa uhakika wa kumpata John, kama kulikuwa na wanaume wengi waliokuwa wakigeuka na kumwangalia basi alikuwa na uhakika wa kumpata pasipo tatizo lolote lile.

Alipofika nje ya jengo la ofisi ya John, kwanza akampigia simu Amanda, alihitaji kujua alikuwa mahali gani, hakutaka kugundulika, alizungumza naye na kumwambia aliagizwa na mama yake kwenda Mbezi Beach.
“Oh! Basi sawa kipenzi changu,” alisema Christina.

“Ulikuwa unahitaji nini my sweatie?”
“Nijue kama upo nyumbani nije! Basi tutaonana baadaye bestie!” “Sawa love! Baadaye!” alisema Amanda na kukata simu.
Christina akashusha pumzi ndefu na kuingia ndani. Alikuwa hajiamini hata kidogo.

Hapo getini akamuulizia John, akaambiwa yupo na hata alipoangalia pembeni, Range nyeupe ilikuwa imepaki, aliamini alikuwepo kwa kuwa ni gari hilohilo ndilo aliloambiwa na Amanda alikuwa akilimiliki.

Akapelekwa mpaka mapokezi, alipofika hapo akaomba kuonana naye kwani kulikuwa na kitu muhimu alihitaji kuzungumza naye, kilikuwa cha kiofisi zaidi.

Haraka sana sekretari akapiga simu kwa bosi wake, John akapokea na alipoambiwa hivyo, akamruhusu msichana huyo aingie ndani.

Akainuka na kupelekwa huko. Alipoufikia mlango, akashusha pumzi ndefu na kuingia ndani. Mlango ulipofunguliwa na sekretari, akashusha pumzi ndefu, mwanaume mzuri wa sura alikuwa nyuma ya meza iliyokuwa na iMac na mafaili kadhaa.

Kwa jinsi alivyokuwa akionekana, alivyovalia Christina alishindwa kuamini kama kulikuwa na mwanaume mzuri namna hiyo, aliaminishwa wanaume waliokuwa na sura za hivyo walikufa kwenye Vita vya Pili vya Dunia mwaka 1945 lakini cha ajabu leo alikuwa amekutana naye.
“Mungu wangu mbona natetemeka hivi?”

alijiuliza huku akimwangalia John ambaye akasimama, akamkaribisha na kumpa mkono.
Walipogusana tu, akahisi kama mwili wake ukipigwa shoti ya umeme, kijasho chembamba kikaanza kumtoka na wakati humo ofisini kulikuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikipuliza mfululizo.

“Karibu sana!” alisema John huku akimwangalia kwa tabasamu pana, hakujua kama lile tabasamu tayari jamaa alidata naye au ilikuwa kawaida yake kuwaonyesha wageni waliokuwa wakija ofisini mule.
 
Sehemu ya 110

“Nashukuru!” aliitikia kwa sauti nyembamba, nyororo ambayo aliamini hakuwahi kuitumia kwa mwanaume yeyote yule.

John alimwangalia msichana mrembo aliyekuwa mbele yake, ni kweli alipendeza na kuvutia, kila alipomwangalia na kujaribu kuweka kasoro zake, hakuona, alionekana kukamilika kwa asilimia mia moja.

Kama mwanaume akaingiwa na tamaa za kumtaka Christina lakini alipoikumbuka sura ya mpenzi wake, Amanda, ghafla tamaa hiyo ikamtoka.

Alimkaribisha kwa mbwembwe na msichana huyo kumwambia alikuwa na biashara alitaka kuifanya na kitu muhimu ambacho kilimpeleka hapo ni kutafuta network ya watu ambao walikuwa na uwezo wa kumsaidia na kumfanya kufika mbali.

Alijielezea kwa ustadi mkubwa kabisa kiasi kwamba John hakugundua kama msichana huyo alikuwa na mipango yake mingine. Kama mfanyabiashara akaanza kumwambia jinsi ya kukabiliana na changamoto zilizokuwa mbele yake, kama kweli alihitaji kufanya biashara basi lingekuwa jambo zuri sana kutafuta network kubwa kama alivyotaka.
“Ila hujaniambia ni biashara gani!” alisema John.

“Nataka nifungue biashara ya juisi, ila niwe nawapelekea watu mwenyewe ofisini kwao,” alisema John.

“Sijaona kama ni tatizo! Ninakuahidi kukusaidia kutafuta wateja, mimi nitakuwa namba moja, namba mbili watakuwa wafanyakazi wangu,” alisema John.

Hilo lilimpa furaha Christina, aliamini kabisa hakugundulika na John aliongea kwa roho nzuri kama kumsaidia kutoka hapo alipokuwa.
Walizungumza mambo mengi, kama saa moja na hatimaye msichana huyo kuondoka zake.

Aliridhika na John, ni kweli alikuwa na sura nzuri, pesa, na alipomwambia alikuwa na wafanyakazi wake akachanganyikiwa zaidi, akagundua kweli mwanaume huyo alikuwa na pesa za kutosha.

Hakutaka kumuonyesha Amanda kitu chochote kile, ilikuwa ni siri kubwa ambayo ilikuwa moyoni mwake siku zote. Walikuwa wakikutana, walizungumza kwa furaha pasipo kujua kwamba tayari mpenzi wake alianza mawasiliano ya kawaida na rafiki yake huyo.
 
Sehemu ya 111.

Christina alihitaji kuwa na John, hakutaka kutumia nguvu kubwa sana, alimuingia kama mtu aliyetaka kufanya biashara ya kuuza juisi katika ofisi mbalimbali, ili kuonyesha kwamba kweli alikuwa na lengo hilo, akaanza kutengeneza juisi hizo na kuzipeleka huko, akaongezewa na watu wengine na hatimaye kuanza kuingiza pesa.

Alichogundua ni kwamba kweli kukutana na watu waliofanikiwa inaweza kukufanya kufanikiwa kama ilivyoanza kuonekana kwake, kwa kipindi cha wiki moja tu, alitumia kiasi cha shilingi elfu hamsini tu lakini akaingiza zaidi ya laki tano.

Biashara ya juisi ilikuwa ndogo lakini aliuza kwa watu wengi. Hakuangalia kuhusu mafanikio hayo, hakuridhika nayo hata kidogo, lengo lake kubwa lilikuwa ni kumpata huyo John kwa kuamini angeingiza pesa nyingi kuliko kwenye biashara zake.

John hakuacha kuwasiliana naye, aliyaona mabadiliko kwa msichana huyo, alikuwa akifanikiwa taratibu na kila walipokuwa wakizungumza kwenye simu, alimtia moyo kwamba alitakiwa kupambana usiku na mchana.

“Christina! Biashara huwa zinaanza hivi! Cha msingi endelea kutafuta network ya watu wengine, nitaendelea kukupigania. Napenda sana kumuona msichana akipambana kama wewe,” alisema John.

“Nashukuru sana!”
“Usijali! Karibu!”
Christina alivumilia sana lakini baada ya mwezi mmoja akapiga moyo konde, hakutaka kuona akiendelea kuteseka kisa mapenzi, kama kweli alimpenda John basi ilikuwa ni lazima amwambie ukweli.

Alitaka kufanya mambo hayo kwa kuanza ishara ndogo tu, kuanza kumtumia emoj za makopa na mambo mengine. Kwa John alishangaa lakini hakutaka kuonyesha dhahiri juu ya mshangao wake, alimchukulia Christina kama msichana fulani aliyekuwa na uhuru wa kupenda, ila kwake, hakuwa radhi kumwambia kitu chochote cha mapenzi.

Baada ya wiki nyingine kukatika ndipo msichana huyo alipoanza kumwambia ukweli juu ya jinsi alivyokuwa akijisikia. Alimueleza kwa makini kila kitu kwenye simu.

John hakushangaa, alilitegemea hilo kwani hata wakati mwingine alipokuwa akizungumza naye na kuchati, msichana huyo alimuonyesha ishara fulani ambazo kwa mtu mzima kama yeye, alizielewa kabisa.
 
Sehemu ya 112

Alichomwambia ni kwamba alichelewa, tayari alikuwa na msichana wake, aliyekuwa akimpenda na kisingekuwa kitu kizuri kama angeanza kumsaliti na wakati hakuwahi kufanyiwa kitu kama hicho.

Hapo, Christina alitamani kumwambia kuhusu huyo Amanda kwamba alikuwa na mwanaume mwingine na yeye alipendwa kwa ajili ya pesa zake tu.

Kila alipotaka kusema hivyo, akasita, halikuonekana kuwa jambo zuri, yaani alitakiwa kutumia nguvu zake, kumpata mwanaume huyo pasipo kumtaja Amanda kwenye ishu yoyote ile.
“Najua John kwamba una mwanamke mwingine,” alisema Christina.

“Umejuaje?”
“Mwanaume mzuri kama wewe huwezi kukosa mwanamke,” alijibu.
“Ndiyo hivyo! Sitoweza kuwa na wewe! Samahani!”

“Lakini John! Hivi huoni jinsi ninavyokupenda?”
“Naona, unajitahidi lakini mpenzi wangu Amanda ananipenda hata zaidi ya unavyonipenda, huwezi kujua hilo tu!” alisema John.

Alipolisikia jina la Amanda moyo wake ukamchoma mno. Alikuwa akimchukia msichana huyo kwa kuwa tu alikuwa na mwanaume aliyekuwa na pesa, alihisi kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake.

Hakuacha kumwambia maneno ya kimapenzi, kila siku alitumia muda wake mwingi kumpigia simu na kumtongoza kumnunulia zawadi na vitu vingine kuonyesha alivyokuwa akimpenda lakini mwanaume huyo hakutaka kuelewa.

Siku zilikatika! Hatimaye mambo yote aliyokuwa akiyafanya yakamchosha, hivyo John akaamua kumualika kwenye chakula cha usiku, siku hiyo alipanga kumuonyesha sapraizi, awepo pamoja na mpenzi wake ili Christina aone tu sababu zilizomfanya kumkataa kila alipokuwa akimwambia kuhusu mapenzi.

“Leo una ratiba gani mpenzi?” aliuliza John, alikuwa akizungumza na Amanda.
“Nitakuwepo nyumbani!”
“Naomba tuonane, nataka kula chakula cha usiku na wewe...” alisema John.

“Wapi mpenzi?”
“Kilimanjaro hotel!”
“Sawa!”
Zilipita siku nyingi kidogo hawakuwa wamepata chakula cha usiku pamoja. Siku hiyo ambayo aliambiwa walitakiwa kula chakula cha usiku pamoja alipanga kwenda kulala kwa Martin.

Hakujua ni wapi alitakiwa kuchagua. Alikaa kwa kujifikiria ndipo akaamua kwenda kula chakula cha usiku na John lakini endapo angemwambia suala la kulala naye, akatae kwa kisingizo cha mama yake kuumwa, ili tu apate muda wa kwenda kulala na Martin.
 
Sehemu ya 113

Siku hiyo ilimfanya kuwa na furaha kama siku nyingine, alitamani kumpigia simu Christina na kumwambia lakini akauona moyo wake ukiwa mzito kufanya hivyo, hakutaka kujali sana, akaacha na hivyo kujiandaa kwa ajili ya usiku wa siku hiyo.

Kwa John, alichokifanya ni kumpigia simu Christina na kumwambia kuhusu chakula cha usiku ambacho alitamani sana kula naye siku hiyo.

Kwa msichana huyo ilikuwa kama ndoto, hakuamini kama kweli John angempa nafasi hiyo adhimu, hiyo ilionyesha kwamba alikubaliana naye, ila alitaka kuitumia nafasi hiyo kumuonyesha ni kwa namna gani alikuwa akimpenda.

“Can I ask you something?” (naweza kukuuliza kitu?) aliuliza Christina.
“Just go on...” (uliza tu)
“Is it a date?” (ni mtoko wa kimapenzi?) aliuliza.

“No! Just outing,” (hapana! Ni mtoko tu) alijibu John.
Japokuwa mwanaume huyo alimwambia hivyo lakini akajipa moyo kwamba ulikuwa ni mtoko wa kimapenzi ila hakutaka kumwambia ukweli tu.

Alichokifanya ni kumpigia simu Amanda na kumwambia alikutana na mwanaume ambaye alimpenda na siku hiyo alipanga kutoka naye mtoko wa kimapenzi.

Hakumwambia kuhusu hoteli, alimpa taarifa ya chakula cha usiku tu ili hata kama kuna siku ingetokea msichana huyo akajua kilichokuwa kikiendelea basi aseme kwamba hakujua kama huyo alikuwa mpenzi wake.

“Mungu akubariki! Sasa ndiyo utulie shoga yangu...” alisema Amanda kwa utani.
“Nitatulia tu! Si kama wewe, mara Martin, mara John!” alisema Christina.

“Yaani wewe acha tu! Yaani kama leo nimepata mtihani! John na Martin wote wanataka nikalale nao usiku wa leo!” alisema msichana huyo.

“Kwa huyo ukaamua nini?”
“Nitakutana na John mara moja ila kulala nitalala kwa Martin,” alisema.
“Safi sana! Wa kwanza ni wa kwanza tu,” alisema Christina huku akicheka na kukata simu.

John alikuwa akijiandaa, ilipofika majira ya saa moja, akampigia simu Christina na kumwambia ajiandae kwani angempitia baada ya kutoka kazini.
|
|

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom