SEHEMU YA THEMANINI NA TATU
Siku zilikatika huku maisha kwenye familia ya mzee Mgaya yakiwa poa kabisa, uhusiano Kati ya mama Kulwa na Samson ulizidi kwenda vizuri hasa baada ya Samson kuonesha mabadiliko fulani kinidhamu.
Siku moja wakati wanakaribia kufunga shule mara baada ya kuwa wamemaliza mitihani yao, wanafunzi wote shule nzima walikuwa makundi makundi wakifanya shughuli za usafi kuizunguka shule yao, huku kundi la Samson likiwa nyuma kabisa wakipiga stori tu bila kuwa kwenye majukumu na wenzao.
Zena alikuja mahali walipo kina Samson huku akiwa mbali kidogo akamwita Sam kwa ishara ya kufumba na kufumbua kiganja.
Oyaaaa Sam, mbona huyu demu kama anakuita wewe?
Halafuuu dah kweli wagombanao ndiyo wapatanao, nenda basi kaka , zali Hilo huenda ukaishi naye kwenye likizo hii. aliongea mwanafunzi mwenzie huku Samson akizugazuga kama hajaitwa yeye vile. Lakini hakuwa na namna alizunguka na Zena na kujificha kwenye miti ya maua marefu ambapo hakukuwa na watu kupitapita.
Vipi tena unataka kunichoresha, wewe unaona jinsi walimu wanavyoniandama hapa shuleni yaani muda wote wananitafutia vijisababu tu ili watimize azma yao, aliweka kituo Sam.
Hapana Sam bila shaka una hofu juu ya hilo, lakini Kuna kosa mwanafunzi wa kiume kusimama na mwanafunzi wa kike? mbona darasani tunakaa mchanganyiko?
Halafu nikwambie kitu Sam, huku ulikonileta ndiko tunaweza kufanya watu wahisi vibaya nikwambie .
alishauri Zena.
Sema nini unahitaji achana na Mambo mengine. Samson alimtaka Zena aweke wazi shida yake.
Zena hakuwa na la maana Kwa Samson zaidi ya kujing'atang'ata tu na kucheka hata pasipochekesha,
Samson likizo ndiyo hii nadhani Mimi na wewe kuonana ni hadi mwezi wa kwanza, so nitakumisi sana kwenye kipindi ambacho hatutaonana, yaani sijui itakuwaje dah. aliongea Zena huku akiinamia chini kwa aibu.
(Huyu Sina mazoea naye kivile Sasa huku kunimiss kunakujaje?
halafu tofauti na siku niliyojaribu kufanya naye mambo fulani, na tangu hapo sijawahi kuongea naye chochote na alikuwa kimya sana,
Halafu leo anadai atanimiss kwani Mimi mpenzi wake?
Haya ndiyo mambo yanayotokeaga na kuniweka matatizoni, lengo ashike ujauzito halafu nianze kukonda kwa mawazo,
Tena Sasahivi mama yupo vizuri huenda taratibu za uhamisho zikaanza, so nikivuruga si nitawakatisha tamaa ndugu wanaonipa msaada) Samson alijiwazia.
Vipi Sam unawaza nini mbona hunijibu? basi Mimi naondoka Sam naona mtu mwenyewe hueleweki. alilaumu Zena.
Samson kama kawaida yake alikuwa nusu nusu ashikilie msimamo wake au amkubalie Zena kuwa kipindi cha likizo watakuwa wanatembeleana licha ya Zena kukaa mbali kidogo, au amkatalie kuwa hataki mazoea,
Samson alikuwa njiapanda.
Kumuacha msichana mbichi kama Zena kwa kuogopa familia ya mzee Mgaya, Samson aliona kama ni uoga uliopitiliza na anapaswa kupata Division zero kwenye hiyo hali akamshika Zena kwa nguvu huku tayari bastola ya Samson ikiwa tayari kuua muda wowote.
Niachie, unanishika nini, mtoto wa kiume hunijibu unalambalamba tu midomo unataka nikueleweje niache niende bwaaana. Zena alilalamika.
Samson aliangalia kulia na kushoto hakuona mtu huku ile miti ya maua ikitengeneza giza fulani , akaona ni sehemu sahihi ya kumalizana na Zena, si kajileta mwenyewe? Lakini ile anataka kumvua nguo mtoto wa watu, kengele ilisikika ikiashiria wanafunzi wote wanatakiwa waende mistarini, hivyo zoezi la Sam likakwamia pale pale.
************************************
Mume wangu huyu mtoto hali yake inaendelea vizuri, lakini nataka nimpunguzie majukumu, hapa anahitajika dada wa kazi mwingine, Rahma atapumzika na Mimi mwezi huu wa kumi na mbili nitakuwa busy sana si unajua tena lazima tukimbizane na biashara na hapa napokwambia mzigo wangu umeshafika nilioagiza nje. Hivyo ni kipindi nitakuwa bize sana.
aliweka kituo mama Kulwa.
(Mzee Mgaya akacheka kidogo)
Sasa mke wangu masuala ya kuleta mgeni mpya sijui mfanyakazi mwingine sidhani kama yananihusu sana ila kila la kheri na namkaribisha huyo mtu japokuwa sijamuona naamini umezingatia vigezo maana wale wakukaa siku kadhaa na kutoroka huwa ni mtihani mke wangu. alijibu mzee Mgaya.
Siku inayofuata mama Kulwa alirudi jioni akiwa na mdada ambaye ni mtu mzima pengine alitakiwa awe kwenye ndoa yake, lakini ndiyo hivyo alikuwa housemaid mpya kwenye familia ya Mzee Mgaya.
Mwanamke mwenye sura nzuri na mwenye shepu yake huku urefu wake ukimpagawisha na kumshangaza Samson, aliingia jikoni huku Sam akishangaa tu.
Duh kweli mwanamke hana ugeni kwenye nyumba ya mtu hajataka hata kusubiri, hajataka kupumzikaaaa..... alijiuliza Samson ikabidi amfuate.
Habari za saizi Dada, alisalimia Samson.
Nzuri tu hujambo, alijibu yule dada.
Samahani naitwa Samson ni mwanafamilia wa hapa, mwenzangu unaitwa nani? aliuliza.
Yule dada alimwangalia Samson kwa muda kisha akatabasamu,
Achana na jina langu kwanza , ila naomba uniletee fagio na kitambaa naona vitu vimekaa ovyo . alijibu yule dada Kisha Samson akaleta vinavyohitajika na kwenda zake sebuleni maana aligundua yule dada hataki mazoea na yeye.
Wewe Samson hebu sogea hapa kwanza, Mzee Mgaya alimuita Sam Kisha kwa sauti ya chini akwambia kuwa katika kipindi kile awe makini kwani dada yake Glory huko aliko kazini kwake mipango imepamba moto akiteleza mipango ya uhamisho wake hivyo awe makini asije akaleta maudhi yeyote na kuwafanya watu wakarudi nyuma.
Sasa mke wangu mbona mmemleta dada ambaye umri wake ni mkubwa sana vipi imekuwaje tena hawa wanakuwaga wasumbufu kwenye maslahi maisha yenyewe unayaona atataka shida zake zote amalizie hapa mwisho wa siku ugomvi usiokuwa wa lazima utatokea.
aliweka kituo mzee Mgaya.
Ni kweli nimefanya hivyo kwasababu mbili, kwanza ni mtu mzima anaweza kumuhudumia Rahma kwa usahihi, na pili tuna mtoto mtukutu humu ndani hivyo itakuwa ngumu yeye kumrubuni huyu mtu mzima. Kuhusu maslahi tumeshakubaliana. Hivyo ondoa shaka mume wangu.
alifafanua mama Kulwa.
Samson alitoka nje na kumuona yule dada alivyobusy na kazi utasema ana muda mrefu kumbe ndiyo kwanza kafika siku ile, alijikuta anavutiwa sana na umbo la yule mwanamke
Itaendelea.........................