SEHEMU YA 109
Ana ndiye aliyemuamsha mama yake baada ya kumkuta anakoroma sebleni,
"Mama, mama imekuwaje tena?"
Rose aliamka ila alikuwa akishangaa shangaa tu, mara wale mapacha nao walikuja na kumuamsha Sara maana waliona mama yao akiamshwa na Ana. Walimuuliza dada yao kuwa kapatwa na nini hadi kalala sebleni, hakukumbuka kwa wakati huo, wakamsogelea na mama yao ila mama yao akawaambia wamuache na alitaka kwenda chumbani kwake ila aongozane na Ana, basi akaondoka na Ana na kuwaacha wale wengine pale sebleni.
Walibaki wakiendelea kumuuliza tu Sara kuwa ni kitu gani ila bado Sara hakuweza kuwajibu kwani hakuwa na jibu la imekuwaje kwa wakati huo, akili yake ilikuwa kama imesizi hivi kwa kiasi fulani, basi kaka zake wakamshauri kuwa akajiandae ili waondoke pamoja, nae Sara akainuka ili akafanye hivyo alivyoshauriwa na kaka zake.
alipofungua mlango wa chumbani kwake alishtuka sana kwani alimkuta Salome akiwa kitandani kwake amejilaza,
"Kheeee Salome!"
"Ndio ni mimi, mbona umeshtuka sana?"
"Sikutegemea kukukuta chumbani kwangu, umeingiaje bila ruhusa yangu!"
"Na wewe kwako kunataka ruhusa? kwani mama yenu kabla ya kufanya yote aliyoyafanya aliomba ruhusa?"
Ndio hapa Sara akajikuta akikumbuka mambo ya usiku na kujikuta akiuliza kwa makini,
"Ni kweli mama yangu alitaka kuzini na mlinzi?"
"Nadhani itakuwa vyema kama ukimuuliza mwenyewe"
Sara hakuendelea tena kuuliza chochote bali alitoka na moja kwa moja akaenda chumbani kwa mamake, na kugonga mlango ila alimkuta mama yake ndio alikuwa anatoka na Ana,
"Kheeee mama unaenda wapi?"
"Ndio salamu hiyo?"
"Hapana mama, shikamoo"
"Sina haja, Ana twende mwanangu"
Wakatoka na kumuacha Sara akiwa palepale mlangoni, ila alijaribu kuwafata nyuma ambapo aliwashuhudia tu wakiondoka bila hata kuwaaga wale mapacha waliokuwepo pale sebleni. Sara aliwasogelea kaka zake, ila na wao wakamshangaa kuwa hajajiandaa toka muda ule,
"Vipi bado hujajiandaa tu!"
"Jamani, si muda huu huu jamani!"
"Muda huu huu! Tumekusubiri hapa karibia lisaa limoja, unasema muda huu huu, kwakweli tunaondoka Sara"
"Jamani acheni masikhara, lisaa limoja limepita saa ngapi wakati ni muda huu huu!"
"Utatukuta ukija"
Na wao wakatoka na kuondoka kwahiyo wakamuacha Sara pale sebleni.
Muda kidogo Salome alitoka na kumwambia Sara,
"Ulitaka kuniacha peke yangu, hapana leo utashinda na mimi hapa"
Sara alimuangalia Salome na kuona kama mtu anayefanya mambo ya ajabu kwenye nyumba yao, ila hakumuuliza chochote zaidi ya kwenda chumbani kwake ili ajiandae na atoke hivyo hivyo.
Basi Sara akajiandaa na alipomaliza alitoka sebleni ilia toke nje na aondoke zake ila pale sebleni alikuwepo Salome ambaye alimwambia Sara,
“Si nimekwambia leo tunabaki wote!”
“Tunabaki wote kivipi? Mimi nina safari zangu bhana”
“Usiwe mbishi Sara, leo tunabaki wote humu ndani. Mimi leo siendi popote na wewe leo huendi popote. Tunabaki wote”
“Na wewe Salome aaah usinibabaishe bhana”
Sara akafungua mlango na kutoka nje, ila gafla akajikuta yupo chumbani kwake,
“Jamani si nimefungua mlango wa kutoka nje, iweje nimerudi tena chumbani?”
Hakuelewa aliona kamavile ni mchezo wa kuigiza, akatoka mule chumbani kwake na kwenda tena sebleni ambako alimkuta Salome amekaa kama kawaida na kuwaza kuwa mwanzoni laba ilikuwa ni mawazo yake ila si kweli kuwa alifungua mlango na kutoka nje, basi akajikuta akimuuliza Salome,
“Hivi tumeongea mimi na wewe muda si mrefu?”
“Ndio tumeongea, kwanini umeuliza?”
“Ulinikataza kutoka nje na ukasema tutabaki wote leo?”
“Ndio, leo tutabaki wote. Mimi siendi popote na wewe utabaki hapa na mimi”
Sara akamuangalia Salome bila ya kummaliza, kisha akaenda tena kufungua mlango wa nje na kujikuta yupo chumbani kwake tena. Akili yake sasa ikaanza kuchanganyikiwa kwani aliona kamavile ni mazingaombwe kabisa ukizingatia mambo hayo yalikuwa ni ya ajabu sana kwake, alijiuliza kuwa ule mchezo anafanyiwa na nani, kama ni Salome basi Salome ni mtu wa aina gani mwenye uwezo wa kukurudisha chumbani wakati ulikuwa ukitoka nje? Alifanya hivyo kama mara tano, na mar azote alijikuta akirudi chumbani. Uoga ukamshika na kuamua kukaa chini pale chumbani, akachukua simu yake na kumpigia mama yake.
“Mama, nipo ndani nataka kutoka ila nashindwa, eti kila nikitoka najikuta nimerudishwa chumbani”
“Mbona sikuelewi Sara, hebu nieleweshe”
“Sijui nikueleze vipi ila kutoka ndani ya nyumba siwezi”
Sara aliamua kama kumuelekeza mama yake kwenye simu ila bado ilikuwa ngumu kwa Rose kumuelewa mwanae, ikabidi Sara akate tu simu ya mama yake na kujibaza kwenye kitanda chake.