Simulizi: Kazi ya mzungu

Simulizi: Kazi ya mzungu

Mogambi

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2012
Posts
213
Reaction score
357
Kazi ya Mzungu

1

DAVID NGOCHO SAMSON

Miaka miwili iliyokuwa imepita, Masuke aliamua kuondoka kijijini kwao Malonje na kuingia jijini kutafuta maisha kama ilivyo kuwa desturi ya vijana wengi. Alifika jijini Dar es salaam na kufikia kwa dada ake Maimuna ambako kwa miezi miwili alokaa kwake alikuwa akifanya kazi ya kulisha ng’ombe wa tajiri Soud wa Masouud, kabla ya kuamua kuyatafuta maisha huko Zanzibar, kufuatia fununu alizosikia kwa rafikize kuwa huko maisha yalikuwa na uafadhali. Kazi kidogo kipato cha juu! Dada yake alipojaribu kumshauri aangalie kwanza hapo jijini, yeye alikuwa ameshaamua la kuamua. Hakusikiliza na alisisitiza maisha ni kutafuta. Ujira wake kwa bwana Soudi ulimwezesha kuabiri boti ya Azam na kuingia Zanzibar tayari kwa maisha. Hakubahatika kuonana na rafikize waliotangulia huko. Mawasiliano yalikatika walipoondoka Dar na hilo halikumtia wasiwasi bali aliamini wangekutana huko.

Alifikia nyumba ya kulala wageni nje kidogo ya feri ya Zanzibar. Usiku huo akautumia kutafakari. Alijiuliza ni nini angefanya. Alfajiri ya kesho yake, Masuke alijiamsha na kuanza harakati za kuzunguka kuufahamu mji aliofikia. Katika mizunguko hiyo ndipo alipopata wazo la nini cha kufanya. Angeweza kusukuma mkokoteni wenye mizigo ya abiria kwa ujira mdogo mdogo ambao kwa kutwa nzima ungemudu kumpa hela ya kujikimu. Wakati akitafakari hayo, alimuona ustadhi mmoja mwenye kuvalia kanzu na barakshia kama ilivyo kawaida ya wazanzibar wengi. Masuke alimsogelea na kumsabahi

‘Asalam aleikum sheikh!' Masuke alitoa salam

‘Aleikum msalam! Wa bara weye!’ Alijibu ustadhi na kuuliza kwa lafudhi yake ya kizenji, Ilikuwa dhahiri kuwa sheikh yule alitanabahi kuwa Masu alikuwa mtu wa bara, na sio bara TU,bara huko nyikani na sio Pwani.

‘Naam sheikh na kazi yangu kubeba mizigo kwa ujira kidogo tu!’ Masu alilazimu kujinadi. Biashara matangazo ati.

Ustadhi alimtazama na bila shaka akaona imani.

‘Mizigo yenyewe mizito utaiweza weye?’

‘Naam sheikh, hii indo kazi yangu!’ Alizungumza kwa kujiamini.

‘Sawa, kwa mizigo hii utanitaka nikupe pesa ngapi?’

‘Mia tano tu itanifaa sheikh wangu!’

‘Haya basi, nipelekee hii kwenye ofisi hiyo ya Azam!’

Ni kama hakuamini bahati aliyokuwa nayo. Tayari ndoto zake alihisi zingetimia hapa. Kufikia magharibi, masuke alikuwa kamudu kujipatia buku nane. Hakutarajia. Sasa aliporejea pale guest alipofikia. Masuke alikuwa na wazo moja tu. Kesho angeamkia kazi yake mpya na saa za adhuhuri angezunguka kutafuta chumba cha kupanga maeneo ya jirani. Uzuri alikuwa na akiba kiasi ambacho angemudu kulipia chumba walau kwa mwezi mmoja. Akiba aliyomudu kukusanya alipomfanyia kazi bwana Soud wa Masoud kule jijini Dar.

**

Bwana Steve Curl alikuwa katinga suti yake mpya iliyomkaa vema, machoni alipachika miwani ya jua, nywele zake akiwa kazilaza kwa mafungu, na kutengeneza kijibarabara kidogo kwenye kichwa chake chenye nywele fupi nyeusi. Mkononi alikuwa na smartphone yake, na alionekana kutazama saa yake ya mkononi ya gharama kuonesha alikuwa anajaribu kupimana kasi na muda. Mwendo wake pia ulithibitisha kuwa, bwana huyo ama alikuwa anawahi ndege au basi kuna zito lilomtia mota miguuni hata aonekane kuvuja jasho kwa haraka alokuwa nayo. Aliikatiza mitaa ya mji mkongwe kwa haraka akielekea kwenye hotel aliyokuwa amefikia. Boda boda wala hawakuonekana mitaani, labda hicho ndicho kilichomfanya mzungu huyo kutoka marekani avuje jasho asubuhi hii ya saa kumi na mbili kwa kutumia usafiri nafuu, miguu yake.

Masuke alikuwa keshaamka mapema. Sasa na yeye alikuwa kwenye harakati za kuwahi kivukoni, huko huenda angepata kazi ya kumbebea mtu kitu ili apate kitu kidogo kama ujira wake. Alishaanza kuzoea kutengeneza hela ya kutosha tu hasa alipowahi alfajiri. Kwa kazi yake hii ambayo alijipachika, alijikuta akipata kuzoeleka hasa kutokana na lafudhi yake, waliyoipa jina wenyeji, ‘lafudhi ya kibara.’ Asubuhi hii aliamka akiwa na tabasamu. Jana ilikuwa njema, ikimfanya ahisi leo itakuwa bora zaidi.

Kwenye kichochoro hapo mji mkongwe, Masuke akamuona mzungu akihangaika na mabegi. Akachanua tabasamu murua, hii ndio kazi yake. Ila sasa, akajikuta lile tabasamu likiyeyuka ghafla. Nini? Akakumbuka wakati wenzake wanajifunza alfabeti na kiingereza, yeye alikuwa kwenye mabanda ya kubeti akitengeneza hela na kuliwa hela. Mwisho wa siku, hakuna cha maana alichopata. Anaanzaje sasa kumuomba hiyo kazi huyu mzungu aliyekuwa mbele yake? ‘Ah, kwani nini! Nitaongea Kiswahili changu cha bara, asiponielewa potelea mbali, hata yeye alipokuja nchi za wenyewe alipaswa kujua lugha yao pia’ hivo ndivyo alivyowaza, huku akiongeza kasi kumfuata Yule mzungu. Tabasamu mwanana kabisa likiambaa ambaa kwenye midomo yake. Alishajua siri, siri ya kufanikiwa kwenye kazi yake, ilikuwa ni tabasamu lake. Hakuna aliyeliona akagoma kutoa kazi. Hiyo ilikuwa siri yake kuu.

‘Halo mzungu, unaweza kuongea Kiswahili? Mimi kazi yangu ni kubebea watu mizigo na kuwafikishia wanapotaka kwa pesa kidogo sana. Naweza kukusaidia, naona hiyo mizigo yako inakuelemea bosi wangu.’ Masuke alitamka huku akiliachia lile tabasamu lake.

‘Sawa, sawa. Ni shilingi ngapi?’ bwana Steve Curl alitamka maneno hayo mithili ya mtoto mdogo anayejifunza kusoma. Neno moja moja kwa tuo.

‘Oh, mefurahi sana unazungumza Kiswahili. Pesa itategemea ni wapi unapoenda.’

‘Nazungumza kidogo sana. Nataka kufika kwa taksi!’ Curl aliongea kwa ishara ya kuonesha kwa vidole vyake kwamba Kiswahili chake kilikuwa kiduchu sana.

‘Hapo bosi utanipa elfu mbili tu!’

‘Elfu mbili, hiyo ni kidogo sana. Nitakupa elfu tano’ Curl alizungumza tena kwa mtindo wake ule wa kusoma. Lakini ikaonekana kama kutangaza dau hilo kubwa ingemsaidia kuwahi alikokuwa anaenda, kwa vile kuzungumza na mswahili kulionekana kunamchelewesha. Hivyo alitumia vitendo zaidi kumhamasisha Masuke abebe haraka na wawahi huko walikokuwa wanaenda. Masuke alielewa, fasta sana akabeba mabegi yake, akanyanyuka kwa mwendo wa haraka, kumwahisha mteja wake.

Hakutaka kuongea, nadhani aliona kabisa kwamba huyo bwana wa kizungu, alikuwa na haraka isiyohitaji soga za kupoteza muda. Alipomfikisha, na kuiweka mizigo kwenye taksi, Masuke akatoa tabasamu lake akipokea buku tano yake, halafu akatamka;

‘Ukirudi, ukiwa na kazi yoyote, mimi nipo tayari kufanya kwa ujira mdogo’

‘Uko tayari, kazi yoyote? Sawa sawa, mimi natafuta wewe nikirudi. Naitwa nani wewe?’

‘Niite Masu, ukinitafuta, tumia ‘M’bara’ watu wanafahamu M’bara zaidi kuliko Masu!’

‘Mubara, mubara!’ Steve alitamka jina hilo huku akiliandika kwenye shajara yake ndogo.

‘Asante sana, hii itakusaidia pia’ Steve aliongea huku akimuongezea shilingi elfu kumi. Akazama kwenye gari, taksi ile ikaondolewa kwa mwendo wa kasi. Steve alikuwa anawahi sehemu bila shaka.

‘Yyess, ah leo zari leo. Hesabu ya siku nimeshaingiza kwa kazi ya kwanza tu? Mungu mkubwa wallah! Naamini leo naweza kulaza hata hamsini. Leo, ah Asante Mungu.’ Masu alimaarufu M’bara, alijiongelesha huku akipanga mipango lukuki kichwani mwake. Alianza kuona mpango wake wa kumiliki guta unaelekea kuwa kweli. Alishaulizia dukani, akaambiwa laki moja na nusu angeweza kujipatia guta la kutengenezwa na mafundi welding, lenye tairi za baiskeli. Na sasa kwa muda mfupi aliokuwa amefanya kazi tayari alikuwa keshajiwekea akiba ya elfu themanini, ukiongezea na hii, hii aliyojipatia alfajiri hii, basi alikuwa na shilingi elfu tisini na tano akiba. M’bara akadhamiria siku hiyo ajitume angalau aingize kama elfu kumi na tano nyingine.

Akajiendea zake akiimba wimbo wa hip hop wa msanii wa Kenya Jua kali, mwoto sana! Si kama aliimba kweli, basi ni ile tu kusema alipenda mdundo na hivyo alijiwekea maneno anayojua mwenyewe kwa rhythm ya wimbo ule. Safari na mdundo.

Aliingia kivukoni saa kumi na mbili unusu hivi, harakati zilikuwa zinaendelea. Leo alichelewa kwa nusu saa hivi, hata hivyo haikuwa bure, ilikuwa nusu saa sawa na siku nzima ya kazi. Tabasamu lake lilichanua vema.

‘We M’bara, kuja hapa, nataka ubebe mizigo hii uipeleke kwa duka yangu. Fanya haraka.’ Babu G, ilikuwa jina la duka lake, mhindi aliyekuwa na duka la kuuza vifaa vya ujenzi. Mara nyingi mizigo yake ilifikia hapa kabla ya kwenda dukani, maana muhindi huyu kama walivyo wafanyabiashara wengine pia, alikuwa hapa kaweka stoo. Na kuna wakati alificha mali humo na kuwaambia wateja imeadimika halafu tena angewaambia kuna kidogo amepata lakini gharama ikiwa imepanda. Hivyo ndivyo alivyojipangia bei na kutengeneza faida maradufu. Hapa, kulikuwa na mzigo wa saruji. Mifuko hamsini. Yote ilikuwa imepata wateja na kilichofanyika ni kuipeleka dukani wateja wachukue mali yao.

Kawaida Masu alipopata tenda kama hizi basi alilazimika kukodi maguta au torori kwa mkinga aliyekuwa ashakuwa mzanzibar bwana Faustine Kyando. Hadi lugha na mavazi yake sasa yalikuwa ya kizanzibar kabisa. Usingemtambua. Huyu alijua kutumia fursa. Kama ilivyokuwa kwa Masu, Kyando naye aliingia Zanzibar kama mtu aliyepotea njia. Kutahamaki akakuta wazanzibar ni watu wa kupenda sana maisha hadi ikawa si kuyapenda tena bali kuyaendekeza. Hawakuwa na muda wa kufanya kazi hizi ndogo ndogo, kwao kazi za kuvuja jasho zilikuwa na wafuasi wachache sana. Na hata hao, walizifanya watimize kusudi, walipolikamilisha usingewaona tena.

Kwake, Kyando hiyo ilikuwa ni fursa. Aliitumia vema akajikuta anafungua duka kubwa na kuwekeza pia kwenye vifaa vya welding. Akajitengenezea bidhaa na kuuza. Akatengeneza pia mikokoteni na maguta kwa ajili ya kukodisha. Akawatonya marafikize waje, walipokuja wakawa wanaitumia mikokoteni na maguta kufanya zile kazi alizoanza nazo. Yeye akawa ashinda dukani na kupokea hesabu ya kukodisha mikokoteni yake jioni.

Masu alikuta huo utaratibu ukiwa umeshawekwa mahali pake. Alijihimu haraka na kumfuata rafiki yake Paulo, ambaye sasa alijiita Bakari. Wakachukukua mkokoteni mmoja walioupa jina ‘moto faya’. Kazi ikaanza. Tabasamu mwanana likienea usoni mwake. Alijipangia hesabu ya siku kuwa kumi na tano, lakini hapa walipewa mifuko hamsini. Mfuko mmoja kawaida walibeba kwa shilingi mia tano. Elfu ishirini na tano. Bakari angeambulia elfu tano tu na yeye angetia kibindoni shilingi elfu ishirini. Huo ndio utaratibu waliojiwekea. Kama aliona ndogo basi angetafutwa mwingine. Bahati nzuri, haikuwa siku njema kwa Bakari, alikuwa majalala mbaya. Alihitaji hela kama alivyohitaji oksijeni. Kwake elfu tano ilikuwa kubwa sana. Naye alikubali kwa tabasamu akimshukuru nduguye huyu kwa kumpa mchongo.

Siku yake ilikuwa njema, na sasa aliamini marafiki waliomwambia Zanzibar kunazo fursa.

Fuatilia episode 2 Kesho

DAVID NGOCHO SAMSON

Facebook: David Samson

FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 2


Kazi ya mhindi babu G ilikuwa ngumu Sana, mfuko wa saruji wa ratili hamsini (50), kutoka hapo stoo Hadi dukani mwendo wa kilometa Kama mbili (2) hivi Ilikuwa inachosha, lakini SI kwa M'bara Masu! Alikwishazoea kazi hizi, hata Ilikuwa Kama asipozifanya hujisikia hovyo tuu kutwa nzima.


Masu na Bakari walichangamka, kazi iishe haraka, waone ustaarabu mwingine mahali pengine. Mkokoteni wao 'motofaya' uliweza kupakia mifuko mitano kwa mzunguko mmoja, hivyo ingewachukua mizunguko kumi kumaliza kazi ya babu G.


Wanaume kazini. Jasho na kivumbi. Mwanaume hasifiwi kula, mwanaume anasifiwa kazi. Vijana hao wawili waliusukuma mkokoteni huku wakiimba kufuatisha ngoma ya Juma Nature na wanaume TMK, 'shiibe shibe, haina bei! Shibe shibe, haina bei', kazi ikawa Ni Mwendo mdundo. Kufikia saa nne hivi za asubuhi, Masu na Bakari wakawa wamemaliza kazi. Miili ikiwa imeloweka kwa jasho. Harufu za kiume zikikerehesha waliopishana nao.


'Masuu' ilikuwa sauti laini ya mtoto wa kike Mwamvita, binti wa mzee Abuubakr!. Mwamvita na Masu wanafahamiana, vile Masu hupooza njaa yake hapo mgahawani kwa mama Mwamvita. Ashaweka uteja hapo, hata asipoonekana, yeye huwekewa msosi pembeni maana hajapata kukosa hata siku moja.


'Bee malkia' hivyo ndivyo Masu humuitikia Mwamvita, na Mwamvita hufurahi Sana! Kwa Masu Ni utani, lakini lo! Hajui tu vile Mwamvita anamzimia.


'Leo nitakuandalia chakula kitamu Sana. Ushawahi kula biriani wewe?. Wabara mshazoea kula magimbi na viazi vitamu, mkipiga hatua mwala wali bokoboko! Hivo Ulisema watokea bara wapi?'


'Wewe mwanamke maneno mingi mingi Sana veve, Mimi mutu ya India veve!' Masu aliongea, na hivyo ndivyo anavyomroga mtoto wa watu, utani utani, na vichekesho vyake, humvunja mbavu binti Abuu na kumfanya awe Teja kwake. Asipomuona Masu, Mwamvita hukaa siku nzima akimtarajia na Hali hiyo humfanya apoteze umakini. Na kitu kingine, Mwamvita hupenda Sana kuinusa harufu ya jasho la Masu!


Mwamvita Ana umri wa miaka 17, Ni mwanafunzi katika skuli ya Maji kupwa, Yupo kidato Cha nne. Mara nyingi mgahawani, huwapo jioni baada ya kutoka skuli. Hakosi hapo, maana shurti amtie Masu machoni, alinuse na jasho lake la kutwa nzima. Hapo moyo wake huwa buhudaani sana.


Masu hajawahi kumuwazia mapenzi binti huyo. Kwanza, kwa sababu Ni mwanafunzi, pili kwa kuwa kazi zake hizi alishajiwekea miiko, ili kufikia malengo. Hivyo utani utani wake, hajawahi kudhani unachukuliwa siriazi. Hata anapomwita mama Mwamvita 'mamkwe', hajui vile anampa shida mama huyo, maana mama Mwamvita alishaziona dalili za huba za bintiye kwa kijana huyo, na anajua kijana huyo Hana habari.


'Mbona leo uko hapa muda huu Malkia? Unatakiwa uwe skuli usije pata shida nazopata mumeo. Kunuka jasho kwa kubeba mizigo kutwa nzima, wewe unapenda?'


'Nilitaka nikuandalie biriani, ukija lunch uupate utamu wa pishi la mkeo, nimefanya vibaya?'


'Shule Kwanza mama, mapenzi jioniii!'


'Unanipenda Masu?' Mwamvita akauliza kwa deko, akiutupia mgongoni ukosi wa hijabu yake!


'Aah Malkia? Swali gani Hilo? Hujui Kama nakupenda mdogo wangu?'


'Mdogo wako? Mi sitaki. Mimi si mdogo wako, Mimi mkeo!' Mwamvita alimaanisha, alipoyatamka maneno hayo, aibu aliziweka pembeni kwa muda, akamtazama Masu machoni barabara!


'Wewe msomi bwana, soma uolewe na waziri, mimi msukuma mkokoteni nitakupa Nini mrembo ka wewe, Wacha niwe nakuita mdogo wangu tu!'


'Nakupenda Masu, usiniambie hivyo buana. Wallah nakupenda!' Mwamvita alizungumza kwa hisia, hata ikampambazukia Masu kuwa, utani wake ulikuwa umeleta balaa! Hakulitarajia hili.


'Sawa Malkia, nakupenda unajua, ila sikuwa nimefikia kiwango hicho. Kwa hiyo, hebu nipe muda kucheki nipo kiwango gani.?'


'Unanipenda Masu, Unataka ukajidanganye eti hunipendi. Mimi sitaki bwana, utakapokuja kwenye biriani mchana, nitakuwa nakusubiri hapa, tupange mipango ya familia!'


'Hahaha Malkia umejua kunizingua leo!' Masu akaongea huku akipanga hiyo baadae amkwepe mtoto wa Shule. Habari za miaka 30 jela hakutaka kuzisikia.! Masu alikunywa chai chapati, akaondoka huku akimuonesha tabasamu adhimu Mwamvita. Mwamvita akafurahia Sana.


***

Masu alirejea ghetto, ajipumzishe Kidogo halafu aingie Tena barabarani kuona uwezekano wa kubutua mchongo mwingine ambao ungetokeza.

Alipofika gheto tu, akamkuta Jamaa mwingine waliyefanya kazi hizi za kubeba mizigo, kakaa juu ya jabali upenuni mwa gheto lake.


'Ohoo! M'bara huyo! Nsha...kusubiri Sa...sana hapa we bwa..bwana, umekua a..adimu ka chozi la sa..samaki?!' Yusufu ndio jina la mgeni huyo. Aliongea hayo huku akitoa tabasamu. Na vile Yusufu Ana kigugumizi, Basi Ilikuwa tafrani kubwa kukamilisha kauli zake.


'Ah Yusuf mtu wangu, we chenga Sana ujue, kupata ile efu kumi ukapotelea kwa Hamida, najua imeisha Sasa, enhee, nambie mtu wangu, fureshi?'


'Hahaha, Ha...hamida wa...wapi, nliku..wa Daslam bwana. Ndo nimerejea. A..asa, Ku...kuna ishu mu..himu mekuja na..nayo. Hafu si..siku..jua wewe a..aluwatani shehe?'


'Das'salam au chumbageni? Acha urongo mapema yote hii. Sema Kama unatafuta dili, we Yusufu mi nakumanya sana, unapenda Sana hizi..' Masu aliongea akimuoneshea kwa vidole kifuani kwake, kumaanisha matiti, huku akipuuza kauli ya Yusuf ya kuwa na Jambo muhimu.


Yusuf Kama alivyotuhumiwa na Masu, Ni Kweli alikuwa Ni mtu wa totoz, yaani alikuwa radhi asile Cha mchana na chajio inapobidi, ahonge msichana wa kulala naye. Ilikuwa Kama Ni ugonjwa. Ajabu kuwa, Pamoja na kutibiwa Mara kadhaa magonjwa ya zinaa, Yusuf hakukoma. Masu na Bakari walishamkalisha kitako Mara kadhaa kumuasa juu ya tabia hiyo, lakini, Mara zote aliporudia makosa, alikuwa mwepesi kumsingizia shetani. Ikafika mahali, Masu na Bakari wakamkubali tu kuwa alikuwa mraibu, mraibu wa wanawake! Na labda kwa vile Ni muhali Sana kuachana na uraibu, wakakubali TU kuwa, huyo mwenzao alikwisha kuwa Teja!


'Ushagazoea fiksi, Nina ishu mujarabu Sana! Ishu ya hela mwanangu. Karibuni tutastaafu hii kazi ya punda.!' Yusuf aliyasema hayo kwa kigugumizi chake.


'Enhee, nambie kijana wa ku-kaya, mgosii. Leo umeniletea dili badala ya kutafuta dili? Mambo yamechenji!'


'Usishangae, Mimi Ni mtu na koneksheni zake. Unamfahamu yule Mzungu wa safari?'


'Mzungu wa safari?'


'Eee, wale wamarekani wanaomiliki ile hotel kwa weupe tu hapo kisiwani! Anaitwa Steve, buana!'


'Mie sio mwenyeji Sana maeneo Haya babu!'


'Yule alokupa 15,000/= kubeba mizigo yake!'


'Ahaa, kumbe aitwa Steve?'


'Naam, yule bwana anadili kwa ajili yetu!'


'Enhee!'


'Sasa ndo wavuta makini, masikio yamekusimama ka sungura, kusikia Ni Mzungu alokupa fedha?'


'Utaeleza ama utaanza mipasho?' Masu akambwatukia Yusuf.



Tukutane tena kwa sehemu inayofuatia.

David Ngocho Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 3
DAVID NGOCHO SAMSON

#Tulipoishia#.

'Usishangae, Mimi Ni mtu na koneksheni zake. Unamfahamu yule Mzungu wa safari?'

'Mzungu wa safari?'

'Eee, wale wamarekani wanaomiliki ile hotel kwa weupe tu hapo kisiwani! Anaitwa Steve, buana!'

'Mie sio mwenyeji Sana maeneo Haya babu!'

'Yule alokupa 15,000/= kubeba mizigo yake!'

'Ahaa, kumbe aitwa Steve?'

'Naam, yule bwana anadili kwa ajili yetu!'

'Enhee!'

'Sasa ndo wavuta makini, masikio yamekusimama ka sungura, kusikia Ni Mzungu alokupa fedha?'

'Utaeleza ama utaanza mipasho?' Masu akambwatukia Yusuf.

KAZI YA MZUNGU 3

'Tulia basi'

'Ah, Yusuf ee, acha u****' Masu, subra ilionekana kukosekana. Kwa kazi zao hizi, kutoa matusi hovyo hovyo ilikuwa kawaida na hawakuchukulia siriazi.

'Ok, iko hivi, yule bwana ataka watu wa kumbebea mizigo. Kuitoa Zanzibar na kuiingiza Zanzibar! Tofauti na hi tunayobeba, ya Mzungu haitoi jasho na mshiko wake si Kidogo pia.' Yusuf alimweleza.

'Enhee, lini hiyo?'

'Sio lini, Ni kazi ya kuajiriwa, sema Ni kazi fulani tutakuwa tunalipwa dollars kibao Mwisho wa mwezi.'

'Dollars kibao ndio Kiasi gani? Hebu nyoosha maelezo mgosi, watu wa mwambao nyie mna kiswahili mrefu Sana!'

'Maelezo zaidi utayapata kwa bosi mwenyewe. Halafu, dah! Jamaa kanisisitiza sana.'

'We ulifahamiana naye vipi kwani?'

'Ah wapi, mi nilikutana naye, nikashangaa naitwa na ngozi nyeupe, nikageuka nyuma kuona Kama Kuna Mzungu nyuma yangu, haha nilikuwa mwenyewe, ikabidi nijongee jirani yake. Nikasikia; 'Habari yako bwana, Mimi nauliza kuhusu Mubara, wewe fahamu yeye? Yeye nabeba zigo!', Nilivyosikia 'Mubara' na 'zigo' nikakumbuka ile story yako, nikajua Ni wewe watafutwa.'

'Enhee!'

'Nikamuuliza, 'unamtaka wa Nini? Mimi pia nabeba mizigo!', Akasema Kuna ahadi mliweka, kuwa akirudi utamfanyia kazi. Alipomaliza kauli hiyo, kabla sijamjibu, akaniuliza; 'wewe pia nataka kazi siyo?' nikaona hapa zali, nikakubali fasta. 'Unataka nikubebee mzigo bosi? Nikamuuliza! Akajibu, No... Not today', akimaanisha SI leo, akasema Ni kazi ina mshahara mzuri na safari za hapa na pale.'

'Anhaa! Aisee Mzungu Mzungu tu, hawanaga mizunguko, akiahidi anatimiza. Hivi unafahamu nlishaga sahau habari zake kabisa? Lakini, cheki ameurudi na kunitafuta kweli. Halafu Yusuf, kwani Hawa wazungu unafahamu hapa Zenj wana ishu gani?'

'Ntafahamia wapi M'bara? Mi nachojua, wanaomiliki hotel ya kitalii kwa ajili ya watu wenye ngozi nyeupe TU!'

'Wee, albino pekee?'

'Haha, Mimi sijasema albino, nimemaanisha wazungu. Hotel yao inabagua rangi man.'

'Ah, isijekuwa wabongo ndo wanajibagua, maana mihoteli ya kisasa ya watalii, inatoza dollars TU, mshiko mrefu, sa mbongo gani ataacha kwenda penye urahisi akatapanye fedha zake nyingi kwa siku moja TU? Nina uhakika, weusi ndio wanakwamishwa na kukosa fedha, enzi hizi, haiwezekani kuwa na ubaguzi wa rangi.!'

'Labda, Mie nasikiaga, pale ukienda mweusi ka Mimi unatimuliwa.'

'Mh, dah, enewei, itajulikana TU. Kwa hiyo huo mchongo umekaaje Sasa!'

'Hilo sio swali babu, Ni wewe TU, muda wowote ukiwa tayari, Mie nakupeleka kwake.'

'Poa poa, mi naona Kesho tukaicheki hiyo kazi.'
Nitakupitia asubuhi mapema, uwe tayari saa moja basi.'

'Poa aisee.'

'Sasa, Mie najikataa hivi!'

'Haina noma Yusuf, iwe Heri, Kesho tujaaliwe uzima!'

Wakaagana, Yusuf huyoo, akasepa zake, Masu akazama ndani kujilaza walau anyooshe mgongo.

***
Ilikuwa ajiegeshe TU kunyoosha mgongo, usingizi ukamvaa bila hiyana. Akashituka saa kumi jioni, baada ya kusikia mlango wa gheto lake unagongwa mfululizo. Akajinyanyua kivivu na kuufuata mlango, akaufungua, ndani akazama Mwamvita bila kusubiri 'karibu ndani'. Masu alishangaa TU, mtu keshazama ndani. Wasi wasi ukamkumba ghafla. Mtoto wa skuli ghetoni mwake? Hi Ilikuwa hatari.

'Nilikusubiria Sana mchana, hukutokea. Nimeamua nikuletee mwenyewe!' Mwamvita alitamka huku akilitua kapu lake kwenye meza ndogo mle chumbani. Taratibu akaanza kutoa vilivyomo ndani. Hotpot kubwa ilibeba biriani, hotpot ndogo ilikuwa na mboga, nyama roast, mboga za majani Kiasi, na tufaa mbili. Soda ya koka kola, aliyopendekea zaidi. Muda wote huo, Masu alikuwa kaganda TU akimtazama binti huyo mrembo kwa Hali ya mfadhaiko. Heri Basi ingekuwa fadhaiko lile la awali. Fadhaiko hili liliupeleka moyo wake puta. Likaifunga akili yake isifanye kazi, likautia mwili wake joto. Macho yake yakakodoka kwa huba, yakawa yanapanda na kushuka kufuatisha mtikisiko wa mwili maridhawa wa Mwamvita. Mwamvita ima kwa kukusudia au kwa majaliwa, akampa mateso yaso chuki M'bara wa watu.

'Na mbona hukuja lunch mpenzi? Ndio umetoka kuamka, unaumwa Masu jamani?' Mwamvita akahoji kwa hamaniko, makini yake ikisadifu simanzi. Akamsogelea Masu na kumpima joto la homa kwa mgongo wa kiganja Cha mkono wake wa kuume, kwenye paji la uso. Masu akasismkwa kwa kitendo hicho. Hata akashindwa aseme Nini isipokuwa kumkumbatia Mwamvita. Mwamvita akatabasamu, furaha yake ikidhihirika wazi. Harufu ya Masu ilipopenya pua zake, Mwamvita akajihisi raha ya pekee. Akajitahidi kwa ujanja, akajinasua kwenye kumbato la Masu.

'Karibu chakula mpenzi, nawa ule tafadhali!' Mwamvita akazungumza, sauti yake tamu, ikasikika Kama sauti laini tamu ya malaika watukufu. Masu akatii na kufanya alichoagizwa.

Akala chakula Cha Mwamvita, akilishwa ka mtoto, akakubali kudekezwa. Hali yao ikibadilika kadri muda ulivyozidi kusogea. Masu akaridhia yote, akaridhia kuvunja miiko yake. Ilidhihiri udhaifu wa mwili, akili ikafunikwa isitafakari Cha ziada. Wakaruhusu miili yao kugusana, wakayaamsha yaliyojificha.

David Ngocho Samson
2020
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 4
David Ngocho Samson
0629077792

#Tulipoishia
Akala chakula Cha Mwamvita, akilishwa ka mtoto, akakubali kudekezwa. Hali yao ikibadilika kadri muda ulivyozidi kusogea. Masu akaridhia yote, akaridhia kuvunja miiko yake. Ilidhihiri udhaifu wa mwili, akili ikafunikwa isitafakari Cha ziada. Wakaruhusu miili yao kugusana, wakayaamsha yaliyojificha.

KAZI YA MZUNGU 4

Masu alishituka saa 10 za alfajiri. Lo! Asalale! Akakumbana na mwili wa malkia pembeni yake!. Akatabasamu kwa furaha, akaunyoosha mkono wake wa kuume, akaifikia redio yake ndogo na kuifungulia. Akakutana na sauti ya mtangazaji ikimtaarifu Ni saa kumi kamili za alfajiri. Alfajiri? Haikumwingia akilini. Ina maana alilala na mwanafunzi usiku wote? Hofu ikamwingia na kuutikisa uhimilivu wake.

Kumbukumbu ya usiku uliopita ikamrejelea vema, hakukumbuka Ni saa ngapi alipopitiwa na usingizi. Kitu kingine pia kikagutua akili yake. Mwamvita aliingia Kama mvamizi. Hakukumbuka Nini hasa kilichomkwamisha kusimamia misimamo yake. Ikampambazukia kuwa walishiriki tendo Mara kadhaa Tena bila kizuizi. Je! Kama kamtia mimba mwanafunzi?

Masu akaamua kumuamsha Mwamvita, 'amka Malkia, amka!', akamtikisa taratibu, Mwamvita akaamka akipendezea pozi la kupiga miayo na kujinyoosha. Masu akasema moyoni, 'hakika wewe Ni Malkia, unanivutia kwa kila kitu, ona mwayo wako unavyonivutia, na huto tudimpo twako, we mtoto umeniweza!'

'Masu, Ni saa ngapi?' Mwamvita akauliza kwa hamaki. Masu akarejea kutoka huko alikotopea kwa hisia na fikra.

'Ni saa kumi alfajiri!' Masu akatamka akiwaza kwa sikitiko!

'Woii! mzee Abuu ataniua, mamaa!' Mwamvita akalalamika.

'Nipeleke nyumbani Masu, niwahishe nyumbani. Mzee akiamka saa kumi na nusu lazima ataniulizia, ili kunikumbushia swala ya alfajiri saa kumi na moja.' wakati anayaongea hayo, Mwamvita alikuwa anavaa nguo kwa haraka Sana. Ikamlazimu Masu kuamka na kuvaa pia.

Walipokwisha kuvaa, haoo, mdogo mdogo wakaanza kuikatiza mitaa ya Mwembe makumbi kuelekea nyumbani kwa mzee Abuubakr barabara ya tatu tokea hapo alipoishi Masu. Ikawa Ni Mwendo wa nusu kukimbia nusu kutembea.

Katika Kona ya kuingia nyumbani kwa mzee Abuubakr, wakamshuhudia mzee huyo akipiga mswaki upenuni. Wakalazimika kurejea nyuma Kidogo na kuingia nyumbani kwa mzee huyo kwa kupitia uwani kabla hajawaona. Ilibidi kufanya uninja ili kuingia ndani ya fensi. Masu akainamisha mgongo, Mwamvita akaukwea na kukamata mgongo wa ukuta, Masu akajinyanyua na kumuinua juu, mtoto wa kike akarukia ndani. Kishindo Kidogo kikisikika. Masu akalazimika kutoka hapo, nduki.

***
'Oyaa M'baraa, leo wapi mtu mzima?'

'Ah, leo hakusomeki mwanangu!'

'Vipi, aisee mbona umedoro Sana?'

'Dah! Mwanangu! Zenj kunanishinda muda SI mrefu! Jana nimejikuta nikivunja miiko yangu. Nimetembea na mwanamke bila hata Kinga!'

'Ah!, faza Masu kaanguka kwenye uzinzi? Hahaha! Da! Hii hatari Sana. Ila mwanangu, hayo Ni Mambo ya kawaida Sana, we Ni mwanaume bana, utakaaje bila demu? Cha msingi, Tulia na huyo Sasa, usiongeze mwingine ukawa Kama Yusuf!'

'Dah, acha Bakari, Heri ingekuwa hivyo, binti mwenyewe mwanafunzi mwanangu!'

'Mwanafunzi kitu gani man, kwani umefumaniwa?'

'Acha kunijaza ujinga Bakari! We hujui kuwa na mwanafunzi Ni hatari ya mvua thelathini?'

'Ah, ila Kweli aisee, mwanetu Muddy tushasahau habari zake. Walisema amebaka mwanafunzi ilhali demu ndio alimfuata ghetto!'

'Dah, unanitisha ujue, maana dogo alinifuata mwenyewe na nikajikuta Mambo SI Mambo, hofu yangu Ni Kama dogo hajadaka Kweli? Na mzee wake mwenyewe ni swala tano, mtoto wa shehe!'

'Loh, mwanangu, jipange aisee. Kama vipi Rudi jijini kwa wajanja, usikilizie Kwanza kabla ya kibendi kutokeza, kinapojitokeza wakikusaka uwe mbali, wapooze hasira zao. Halafu, wakati huu, jipange kusilimu aisee maana huyo lazima utamuoa Kama ameshiba mimba!'

'Dah, nipo njia panda. Mtoto mwenyewe nimemkubali Sana aisee. Wacha nisikilizie Kwanza! Kama akinambia Mambo yameharibika ndio nitalala mbele'

'Yeah hata Hilo nalo Ni wazo zuri! Lakini ikikubalika, SI mnaichomoa TU, Yupo dokta Mgambo, yule M'bara mwenzio ndiyo michongo yake, we wekeza vijisenti TU kwa Sasa, Enhee mpango umekaaje?'

'Kuna ishu nafuatilia, ikiwa fresh, nitakujulisha. Ila inahusiana na yule Mzungu niliyowasimulia siku zile. Anadai Kuna kazi ya kuajiriwa! Hivi nataka niende huko mida ya saa moja. Alimtuma Yusuf kunipasha habari!'

'Dah, siwezi kuunga tela?'

'Ah, we sikilizia Kwanza, nikifika huko nitakupigia pande! Akiingia kingi, nitakujulisha, wewe Tena mwanangu mwenyewe nakuachaje Sasa?'

'Poa poa mtu wangu, fanya hivyo! Naona inabidi sasa nende zangu kwa Kyando pale, nicheki Kama kunaweza kuwa na dili.'

'Haina noma, baadaye Basi.'

Saa moja asubuhi, Masu na Yusuf walikuwa kiguu na njia kwenda kwa Mzungu Steve Curl. Walivalia poa siku hiyo, fulana na jinsi za bluu ziliwatoa, wakapendeza Kweli kweli. Mdogo mdogo wakaambaa na barabara ya Malawi kutokea Stone town, wakakutania Gulioni na Dereva wa Steve Curl. Kijana wa kihindi, anayaongea kiswahili kwa ufasaha. Gari likachoma mafuta na kuondoka Gulioni, likipandisha na Malawi road, kuelekea kaskazini mashariki,Hadi walipokutana na Barabara ya Nungwi. Waliifuatisha hiyo Hadi kwenye ufuo wa Nungwi. Mbele yao wakashuhudia hotel ya kitalii yenye kila sifa ya usasa. Kwa M'bara, hii Ilikuwa Mara ya kwanza kuona mazingira ya hoteli hiyo ya kisasa kwa ukaribu na kutalii kwa ndani,kila Kona na mandhari zake maridadi. Bwawa kubwa la kuogelea, vyumba vya kulala vyenye hadhi ya kifalme. Utulivu na usafi ulozingatia weredi wa kimataifa kwenye uga wa kitalii..

Kwa muda wote waliozunguka eneo la hotel hiyo, wakiwa na mwenyeji wao Khassam, Hilo ndiyo jina la Dereva aliyewafuata, hawakuweza kuona mtu mwenye ngozi nyeusi Kama wao. Masu akakumbuka ile simulizi ya Yusuf kuwa hotel hiyo Ilikuwa kwa ajili ya wazungu pekee. Alielekea kuamini Hilo Hadi pale Yusuf alipovunja ukimya na kumuuliza Khassam kwa Nini mtu mweusi hakuonekana. Khassam akamtazama kwa mshangao na kutamka.

'Si kwa ubaya, lakini nadhani watu weusi Ni stingy(bahili) Sana, hawawezi kulipia milioni 2 kwa chumba kwa usiku mmoja TU. Hapa Kama uonavyo, Ni wazungu pekee, na hata hao, unaona wengi Ni vibabu ambavyo hapa wanakuja kutumia pensheni zao baada ya kustaafu. Na wengine Ni wale matajiri wenye kumiliki vyanzo imara vya kipato na biashara huko Kwao. Na kingine, hapa hawaji watoto, Ni watu wazima pekee!' Khassam aliongea na kujibu maswali yaliyokuwa yafuate bila shaka. Na kuthibitisha Hilo, kabla Masu hajafunua mdomo wake kuuliza, Khassam aliongea.

'Nachojua Ni kwamba, huo Ni utaratibu wa hoteli hii. Sijui kwa Nini waamue kuwa Ni eneo kwa ajili ya watu wazima pekee.' Maelezo hayo, yakawa Ni Kama yamelenga kumnyamazisha Masu asiulize swali lake. Swali ambalo tayari Khassam alilijibu.

'Mnaonaje Haya mazingira?' Khassam akauliza.

'Dah! Nadhani walokole wa huko bara ndanindani wakifika hapa, haki ya Mungu watajua wameingia mbinguni. Maana zile nyimbo zao kuwa mbinguni Kuna barabara za almasi, majumba ya kifalme yenye kungara kwa dhahabu, taa maridadi na mazingira tulivu!, Hapa Ni zaidi ya wanavyodhania.' Masu alizungumza na kuchokoza vicheko kwa wenzake.

'Kama hivyo ndivyo, Basi ndugu M'bara, sisi tunayo bahati ya kufika mbinguni kabla yao haha!' Yusuf aliongezea. Wakacheka Tena.

'Na Kweli, mnayo Bahati Sana. Kwa maana tangu nianze kufanya kazi hapa, huu mwaka wa kumi Sasa, na sijawahi kuona ngozi nyeusi kwenye eneo hili. Bahati yenu Ni kubwa sana.' Khassam alizungumza, wakiwa wanaketi kwenye sofa katika moja ya maeneo yenye mandhari nzuri, kwa nje bahari ya Hindi ikionekana mubashara kwa uzuri usio kifani na kwa nyuma yao, bwawa la kuogelea likikolea bluu bahari yenye mvuto unaovutia.

'Steve atakuwa hapa anytime soon (muda wowote kuanzia Sasa, haichukui muda mrefu). Mtakula nini niwaagizie?'

'Ah, da! Braza, tuchagulie mwenyewe. Na vipi, twalipa wenyewe'? Yusuf akauliza na kuongezea,
'Kama tunalipia wenyewe, kwa Kweli Mimi Sina njaa!'.

'Msihofu, kila kitu Steve analipia. Bei za hapa nyinyi hamziwezi wazee, nyie furahieni fursa hii adimu.'

Khassam akawaagizia wali samaki. Wakala na kushiba na walipokwisha kunawa, wakiwa wanashushia na juisi ya ukwaju, wakamuona Mzungu akitokeza.

David Samson
2020

Ukiipenda, like, comment na share na wengine!
FB_IMG_1582973075137.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 5

#Tulipoishia"

'Ah, da! Braza, tuchagulie mwenyewe. Na vipi, twalipa wenyewe'? Yusuf akauliza na kuongezea,
'Kama tunalipia wenyewe, kwa Kweli Mimi Sina njaa!'.

'Msihofu, kila kitu Steve analipia. Bei za hapa nyinyi hamziwezi wazee, nyie furahieni fursa hii adimu.'

Khassam akawaagizia wali samaki. Wakala na kushiba na walipokwisha kunawa, wakiwa wanashushia na juisi ya ukwaju, wakamuona Mzungu akitokeza.

KAZI YA MZUNGU 5.

'Oh, furaha Sana kuona wewe mubara! Na leo uko pendeza Sana. Sasa tutaenda mahali kwa mazungumuzo. Yeye wawili, nafuata Mimi!' Steve alizungumza huku akiwaashiria kufuatana naye. Kiswahili chake kikionekana kuboreka Kiasi. Kwa Sasa alitamka maneno Kama anavyosoma mtoto wa darasa la tatu.

Waliongozana na Steve na kutoka nje ya jengo la hotel ile ya kisasa kwenye eneo kubwa la wazi miliki ya hotel hii. Ilikuwa na eneo kubwa la wazi lenye misitu ya mikoko. Huko wakaona ubunifu mkubwa uliotengenezwa kwa ajili ya kuwapa burudani wageni waliofika mahali hapo. Bembea imara ziliwekwa humo msituni, kwa umbali wa kukadiria ili kwamba, isitokeze usumbufu kwa watumiaji bembea wengine. Sasa, Ilikuwa dhahiri kwa Nini watoto chini ya miaka 17 hawakuruhusiwa. Hotel hii Ilikuwa maalumu kwa wapendanao. Hasa wale waliotoka kuoana wakataka faragha kwa ajili ya fungate lao. Na labda pia kwa wale wazee waliokuwa wanazeeka Pamoja.

Walilibaini Hilo maana waliweza kuona wazee hao, na kwenye bembea zile, walionekana pia watu wawili wawili wa jinsia tofauti wakifurahia huba!

Uzuri wa hili eneo la hotel, lilikuwa limeinuka, na kufanya kuwepo mwonekano Bora kabisa wa bahari chini yao. Na hapa walipokuwa, kulitoa mandhari nzuri Sana ya kuiona hotel ile ya kisasa na mazingira yake tulivu, lakini pia, ilitoa fursa kuliona jua linapozama baharini saa za jioni.

Walijitenga mbali na watu wale waliokuwa wakifurahia bembea, wakaketi chini ya mti mkubwa uliopandwa, ukitengeneza kivuli mujarabu kuwakinga na jua.

Hapo, wakavuta makini zao kupokea maelekezo ya kazi yao mpya.

'Ok, mubara welcome, and you Mr Yusuf. Hii kazi Ilikuwa kwa ajili ya mubara, na Ni kusema wewe Yusuf uliamua kutumia fursa ya Mimi kukuulizia, kulazimisha upate kazi pia. Najua mubara Yuko tayari, alinambia mwenyewe atafanya kazi yoyote ile. Je wewe, Yusuf uko tayari kwa kazi yoyote ile??'

Yusuf akataka kutafakari Kwanza, lakini akahisi kusita kwake kungetumika kumtoa kwenye fursa, maana Kama Steve alivyosema, ilionekana yeye alikuwa hahitajiki ila alilazimisha. Akajibu haraka haraka bila kusita.
'Ndiyo'

'Ok, Kama hivyo ndivyo, nataka nipate Kiapo chenu Cha utii. Kazi hii Ni kazi inahitaji ujasiri, na ukakamavu, na Kama Unadhani kufanya kazi ya ujasiri na ukakamavu, Tena inayohitaji usiri mkubwa Ni shida, Basi Sasa Ni muda mwafaka wa kujiondoa. Kama unakubali, maana yake Ni kwamba, huwezi kurudi nyuma kamwe. Ukikubali utakuwa unalipwa pesa nzuri Sana. Mnaonaje kulipwa elfu sitini kwa siku?' Steve aliongea na kuuliza.

Masu na Yusuf macho yakawatoka kodo! Akilini mwao mchakato wa hisabati ulikuwa unaendelea. Sio kanuni za Pythagoras wala Newton wabobezi wa mahesabu. Lah, Ni zile hesabu maarufu za magazijuto. Wakagawanya, wakazidisha, wakajumlisha na kutoa. Wakapata Sawa Sawa na 'NDIYO' yenye herufi kubwa. Wangeachaje sitini kwa siku, ilhali kazi yao ya awali Ilikuwa ya maguvu, na walipojitahidi Sana na Mungu kuwaangazia Nuru za uso wake, walifanikisha elfu ishirini TU!

'Tuko tayari.' wakatamka Kama waimba ngonjera, kwa kupokezana.

'Vema, kwa kusaini hapa kwenye hii dokumenti mtakuwa mmekubali masharti ya kazi na kula Kiapo Cha utii. Pia mtakuwa mmesaini mkataba wa malipo ya shilingi elfu sitini kwa siku!' vijana hao kusikia elfu sitini kwa siku, kukawapumbaza, wakang'ang'aniana kalamu, kila mmoja akitaka kuwa wa Kwanza kusaini. Maelezo ya mkataba yaliyoandikwa kwa lugha ya malkia wa uingereza hawakujali kuyasoma. Waliridhika na Maelezo ya Steve Curl.

Walipokwisha kusaini, kila mmoja akiandika majina yake matatu na kuweka dole gumba, waliongozana na Steve Curl kuingia kwenye eneo lililokuwa na fensi ndefu ya ukuta mle mle kwenye pori, likiwa na maandishi mlangoni, ' WAHUSIKA TU'. Steve aliingiza namba fulani fulani kwenye kifaa kilichofanania na meta ya luku yake, hivyo ndivyo Masu alivyodhania. Baada ya zoezi Hilo, kwenye mlango ule, kulikuwa na kitu Kama katobo hivi, Steve alisogeza jicho lake jirani na tobo like, ikawa Ni Kama anapiga chabo kinachoendelea mle ndani, Mara, Masu na Yusuf wakasikia sauti ya mwanamke ikitamka maneno, 'welcome Steve' mlango ule ukaachama kwa uwazi. Nafasi ikajitokeza na wao wakazama ndani. Walipokwisha kuingia ndani, mlango ule ukajifunga Tena. Kwa M'bara Masu, hii Ilikuwa kitu mpya! Mlango unaozama ukutani unapofunguka!!

Fensi ile ndefu, kumbe ndani Ilikuwa Ni eneo kubwa Sana lenye ofisi chache, na magodauni mengi ya kuhifadhi bidhaa na Mali kadhaa ya hoteli bila shaka,lakini walichogundua baadaye Ni kuwa, chini ya ardhi kulikuwa na vyumba ndani ya eneo hili lililolindwa kwa mitambo ya kisasa na makamera ya cctv. Huko chini, kulikuwa na Mambo mengi ajabu. Kama SI kwa kuingizwa kule na Steve, Wasingejua kuwa, huko kulifanyika anasa za kila namna.

Waliteremka kwa lifti, wakashuhudia ukumbi mkubwa unaowaka Waka taa za rangi tofauti. Huko walijazana wazungu na waafrika pia. Vinywaji mikononi, wengine sigara, na hata waliotumia dawa za kulevya za unga unga wakizisokomeza kwenye pua zao. SI hivyo TU, wapo walioonekana wakipapasana miili hadharani bila aibu. Lakini ilivyodhihiri machoni mwao, wengi wa waafrika waliokuwamo humu, walikuwa Ni wasichana warembo wa miaka kumi na mbili Hadi ishirini hivi!

Wote hao, wakionekana kuwepo pale kwa ajili ya kuwaburudisha wazungu wale. Muziki ulikuwa unasikika kwenye ma-spika makubwa ya kisasa. Muziki uliochujika Vema na kuburudisha masikio. Ilikuwa club moja ya kisasa. Ajabu, muziki huo, haukusika walipotoka pale ukumbini na kutokeza kwenye korido ndefu iliyokuwa na ngazi za kupanda juu. Kukiwa na taa zenye mwanga hafifu wa njano kuwaongoza. Walitokezea nje kwenye pango. Isingekuwa rahisi mtu kudhani kuwa Hilo pango liliongoza njia ya kuingia kwenye jumba la starehe na anasa ardhini. Kwa nje lilitisha, nyasi kibao zilijiotea hapo, na Kuna namna Masu alishuhudia bonge la joka likiishilia kule walikotokea. Hata hivyo, akapotezea kwa kuhisi Ni fikara zake TU.

Baada ya kutokeza huku kulikoonekana kuwa porini, waliuona ukuta ule uliozunguka zile godauni kwa nyuma yao.

'Huku Ni eneo la mazoezi, mtajifunza kutumia silaha mbalimbali kushambulia na kwa ajili ya kujilinda pia!' Steve alizungumza na kuuondoa ukimya uliokuwa umetawala safari yao.

Masu akatabasamu, hofu akaiondoa moyoni, Nuru ya matumaini ikamrejea.
'Kumbe kazi yenyewe Ni ulinzi!' akawaza. Kwake hii Ilikuwa Ni kazi rahisi yenye mshahara mnono. Akakumbuka maneno ya awali ya Mzungu Steve, kuwa Ni kazi inahitaji ujasiri na ukakamavu. Masu akatabasamu Tena, safari hii akionesha furaha yake wazi wazi.

Mbele yao, akatokeza mwanaume mwenye mwili uliojengeka Vema. Kijasho chembamba kikinatia kwenye ngozi yake. Alikuwa kifua wazi. Huyu hakuwa Mzungu, labda mchanganyiko wa mkorea na Mzungu, maana sura Ilikuwa ya kikorea, lakini mwili wa kimarekani. Alikuwa mrefu wa kimo, kifua kipana, mwili wa kati kiwastani, au tuseme, SI mpana SI mwembamba!

'Master Park Hye, kutana na 'mubara' Pamoja na Yusuf, wanafunzi wako wapya!
Mubara, Yusuf, mwalimu wenu, master Park Hye!'. Ni vile jina M'bara alipewa na watu, lakini Kuna wakati alitamani kumrekebisha Steve utamkwaji wake, akaazimu kupotezea. Hatukuwa na madhara.

Masu akamsogelea master na kumpa mkono.

'Naitwa Masuke Masu...!' Masu alikuwa anaongea Kama anayelia. Mkono wake ulipokutana na wa master, Masu alihisi kubanwa na chuma! Maumivu makali yakampenya ngozi ya mkonowe na kuipeleka taarifa ya maumivu kwenye ubongo.

'Karibu' Park Hye akajibu akiwa bado ameshikilia mkono wa Masu. Uchozi ukamdondoka Masu, huku akifanya jitihada za kujinasua. Alionekana kujinyonga nyonga kwa maumivu!

Yusuf alishuhudia kilochomtokea mwenzie, akajaribu kutafuta namna ya kuuepuka mkono chuma wa master. Yeye akajifanya salamu yake badala ya handshake, anatoa salute. Ah wapi! Mkono chuma wa master ulimkamata barabara, tofauti na Masu aliyedondosha chozi na kugugumia maumivu, Yusuf alitoa kilio Cha mtoto mdogo!

'Mamaaa!'

'Hapa panaitwa kwa master. Kuna vitu kadhaa tutavi-master mkiwa hapa. Nitawapatia ratiba na mtatakiwa kuifuata kikamilifu' Master aliwaeleza, wakati huo, Steve alikuwa hatua kadhaa kurejea kule walikotokea.

2020
David Ngocho Samson
0629077792
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 6
David Ngocho Samson

#Ilipoishia#

'Hapa panaitwa kwa master. Kuna vitu kadhaa tutavi-master mkiwa hapa. Nitawapatia ratiba na mtatakiwa kuifuata kikamilifu' Master aliwaeleza, wakati huo Steve alikuwa hatua kadhaa kurejea kule walikotokea.

KAZI YA MZUNGU 6

Kama walidhani kazi hii mpya ingekuwa na urahisi wowote, walikosea kudhani hivyo! Waliamka alfajiri ya saa kumi usiku, wakaingia uwanjani. Baada ya hapo, saa moja kamili walipata kifungua kinywa kwa dakika kumi na tano. Saa moja na robo waliingia darasani kujifunza lugha mbili muhimu. Kiingereza na Kifaransa. Zoezi Hilo lingefanyika Hadi saa sita za mchana. Kulikuwa na walimu wa kuwafundisha kusoma, wa kuongea, na wa kuwaonesha kwa vitendo tamaduni za wenye hizo lugha mbili. Walipomaliza Hilo, walikula. Wakaruhusiwa kupumzika kwa masaa mawili, wakarejea Tena darasani kujifunza computer na masuala ya kiteknolojia. Jioni saa kumi walirejea uwanjani kwenye mazoezi ya kijeshi.

Walianza na mazoezi Kidogo Kidogo ya mwili, yakaongezeka kadri siku zilivyosogea. Baadaye wakaanza drill za kijeshi kwenye upande wa mazoezi ya viungo, kutembea na mizigo mizito, kujongea Kama nyoka, miruko ya aina mbalimbali. Miili yao ikabadilika. Umakini wao ukaongezeka. Wakatengeneza mlango wa sita wa fahamu! Uwezo wa kuona bila kufumbua macho, kuhisi hatari kabla haijatokea, kusikia sauti ya kimya! Mwishoni walijifunza matumizi ya silaha, kila aina ya silaha! Hotel hii, Ilikuwa Sawa na nchi inayojitegemea kiulinzi. Hivyo ndivyo walivyodhania. Walimudu kuzitumia silaha na hata kutengeneza zingine. Mabomu madogo madogo waliweza kuyatengeneza kwa kutumia vifaa mbalimbali, na raw materials muhimu kwa kazi hizo.

Miezi tano Sasa Ilikuwa imekatika tangu waingie hotelini. Kama ungewaona, Masu na Yusuf, hakika usingewatambua. Walibadilika! Walikuwa tofauti. Waliongea kiingereza na Kifaransa Kama vile walizaliwa huko. Miili yao, ilionekana kubadilika Sana. Zaidi mno, walionekana Ni watu wenye fedha zao, maofisa wa idara nyeti labda.

Walipopewa likizo ya mwezi mmoja kabla ya kurejea kazini kuanza rasmi kazi yao, Wazo la Masu lilikuwa kwa Mwamvita pekee! Hivyo, aliliendesha gari dogo aina ya ist, Mali ya Steve, ambalo aliamua kumzawadia kwa kufuzu Vema zile harakati, na moja kwa moja akakamata break mgahawani kwa mama Mwamvita. Akaitafuta Kona yake mle mgahawani, meza aliyokua kajizoeza kutumia miezi kadhaa hapo awali, akaketi. Alivalia miwani myeusi na suti Kali ya bluu. Mkononi alikuwa na smart watch (saa ya mkononi ya kijanja)ambayo ilimpa taarifa kadhaa muhimu Kama vile Hali ya joto Ni kiwango gani, Kama simu yake iliita, lakini pia ilimpa taarifa juu ya chumba alichoishi kule porini chini ya ardhi,na kumtaarifu Nini kiliendelea akiwa hayupo. Picha za video zilionekana kwenye kioo Cha saa hiyo, mubashara kabisa. Aliketi hapo akisubiri muhudumu amfuate.

Mara akaja muhudumu, Masu akatoa macho yake kwenye saa yake hiyo na kuyainua amtazame huyo mhudumu. Akautaliii mwili wa muhudumu kwa macho yake, kuanzia miguuni na kupandisha juu huku akitabasamu. Aliifahamu miguu ya Malkia wake Mwamvita. Bila shaka akijiambia Sasa Mwamvita atakuwa keshamaliza kidato Cha nne, na Kama Kuna lolote, itakuwa Ni kusubiri matokeo ya kujiunga kidato Cha tano. Akawaza vile atapata wasaa mzuri wa kutumia na malkia wake kwa mwezi huu mmoja.

Masu akaendelea kuutalii mwili huo kwa pozi, akayatua macho juu Kidogo ya nyonga ya Malkia huyo. Mshituko ukamkamata ghafla. Uvimbe wa kitambi, ama la! Basi mimba. Macho yake yakataka majibu. Akakutana na uso wa malkia wake, macho yake yakamtazama usoni. Kulikosekana lile tabasamu adhimu, tabasamu ambalo lilimfanya Mwamvita avutie na kupendezea. Alionekana kupungua pia. Mawazo! Alionekana kujawa mawazo na wasiwasi.

'Karibu mgeni, nikuhudumie Nini tafadhali?' Mwamvita akazungumza huku akilazimisha tabasamu!
Ha! Mwamvita hajanitambua? Masu akashangaa. Akaamua kuivua miwani.

'Kama kawaida yangu, ila Kama biriani ipo basi utakuwa umenitendea haki zaidi Malkia!' Masu akatamka kwa ile sauti yake ya utani! Akawa Sasa anaiwazia mimba ya Malkia, akijiuliza Kama yeye ndiye baba au la!

Mwamvita aliposikia hivyo akashituka. 'Sauti Kama Masu, Hadi macho na sura zao zafanana. Lakini hawezi kuwa Masu. Duniani wawili wawili.' akajiwazia huku akijaribu kupotezea hisia kuwa huyu alikuwa Masu wake. Lakini kitu fulani hakikuwa Sawa. Ni Masu pekee aliyemwita malkia, huyu kaanzaje, kwamba Ni Bahati TU? Hata! Kuna kitu hakikuwa Sawa. Labda Ni Kaka yake, na Masu kamsimulia habari zangu na yeye! Masu aliyemjua, alipewa habari za kuaminika kuwa alitekwa na watu wasiojulikana, na tangu hapo hakuwahi kuonekana kokote kule Zanzibar. Alikwisha muombolezea machozi yakakauka. Vipi Sasa hili litokee! Kama hiyo haitoshi, huyu alikuwa mtu wa familia Bora! Suti Kali, gari, mwonekano wa kifedha!

'Kawaida yako Ni ipi, samahani, Ni kwa sababu ndiyo Mara ya kwanza nakuhudumia!' Mwamvita aliuliza, huku akidhamiria kufuta kabisa kumbukumbu ya Masu iliyokuwa imefufuliwa.

'Ok, bila samahani. Nikuombe tafadhali uketi hapo!' Masu alimweleza Mwamvita na kumuoneshea kiti kilichokuwa mkabala naye. Mwamvita akaketi huku akijiuliza, 'wanawezaje kufanana sauti hivyo?'

'Dah, Hadi Sasa siamini kabisa Malkia wangu unaweza kuwa umenisahau kabisa Kiasi hiki. Miezi mitano TU na umeniondoa kabisa akilini mwako?. Nisamehe Sana mpenzi, naweza kuwaza TU, kwa ujauzito huo na Mimi kutoonekana itakuwa ilikutia simanzi kubwa…..' hakumalizia, Mwamvita alinyanyuka na kumsogelea Masu, akamshika mashavu, akaipapasa shingo yake, akanusa shati lake kwa pua zake, akakutana na harufu nzuri ya marashi, bila shaka marashi ya ghali pia. Akaikosa ile harufu nzuri ya jasho la Masu. Hakuelewa. Akatamka

'Masu!?'

'Naam, Ni Mimi Malkia, Ni Mimi Masu wako!' Masu akamvuta Mwamvita na kumkumbatia! Mwamvita alikuwa analia. Machozi yake yakatotesha shati lake. Masu akatoa kitambaa Safi cheupe mfukoni mwake. Akamfuta machozi. Dakika moja na ushei ikakatika wakiwa kimya, wamekumbatiana.

Mwamvita alipoona Vema akatamka.

'Niliambiwa ulitekwa na wasiojulikana! Lakini nikuonavyo, hukutekwa. Kuna siku niliota umekuja, ukanambia umetuandalia sehemu Mimi na mwanao tukaishi.! Mbona hukuniaga? Ulinifanya nikuomboleze. Kumbe uko hai Masu!' machozi yakamdondoka.

'Nipo hai, Nani huyo alokudanganya nimetekwa?'

'Masu hapa mtaani kila mtu anajua umetoweka baada ya kutekwa na wasiojulikana!'

'Dah, ila binadamu wana habari nyingi. Malkia, Mimi sikutekwa. Kuna dili nilipata, nilipoenda kwenye interview, nikafuzu na sikupewa nafasi ya kurudi, tukawa tumepelekwa nje ya nchi kwa ajili ya kazi. Sikuwa na namba ya simu ya hapa kwenu, ningekupigia simu walau nikujulishe kilichojiri, lakini ndio hivyo Tena, mawasiliano yalikatika!' Masu alidanganya, alizingatia maelekezo ya bosi wake kuwa, habari za kule walikokuwa, hazikutakiwa kutoka.

'Kwa hiyo Sasa umerudi?'

'Kwa likizo ya mwezi mmoja TU!'

'Utaondoka Tena?'

'Ndiyo Malkia….'

'Bora usingekuja. Nilishaanza kuzoea hali. Kuja kwako na uondoke Ni Kama umeamua kufumua kovu la kidonda kilichopona na kutengeneza donda kubwa jipya!' Mwamvita alizungumza akitoa machozi.

'Mbona wasema hivyo Malkia?'

'Baba ananilazimisha kuolewa Kama bi mdogo wa babu mmoja, Mzee Kisiki, Mie sitaki Masu, hii mimba niliyobeba, Ni matokeo ya mahaba yetu ya siku ile. Wakinilazimisha Sana nitakufa Masu!' Mwamvita akazungumza kwa huzuni kuu machozi yakitiririka.

'Kwa Nini, mbona mzee Abuubakr Ni ulamaa mzuri, nwanazuoni wa dini, vipi akufanyie hivi.?'

'Kwa sababu kupata' mimba nyumbani nimemfedhehesha Sana, anavyosema yeye!'

'Hata Kama, bado haimpi haki ya kukulazimisha uolewe na kibabu. Ila usijali. Wewe na mtoto wetu hamtalazimishwa kuishi na huyo kibabu! Nataka nikupeleke kwa dada yangu Dar, huko utakaa kwa furaha, nitakuwa nakutumia fedha kwa ajili ya matumizi yako yote. Au nikupangie Nyumba kabisa huko? Ah, nitakupangia Nyumba Dar, ila kwa Sasa, utakaa kwa dada Hadi utakapojifungua. Ukishajifungua, Kuna mdogo wangu yupo kijijini atakuja kuishi na wewe kwenye hiyo Nyumba nitakayokupangia, anaitwa Maureen. Unaonaje Hilo Wazo?' Mwamvita Kidogo amrukie Masu kwa furaha, lakini mgahawani akawa ameingia mteja.

'Asante Sana Masu, nilikuambia, Unanipenda, huwezi kujidanganya eti hunipendi! I love you Masu' Mwamvita akatamka huku akiondoka akamhudumie mteja alioingia.!

2020
David Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 7

#Ilipoishia
'Asante Sana Masu, nilikuambia, Unanipenda, huwezi kujidanganya eti hunipendi! I love you Masu' Mwamvita akatamka huku akiondoka akamhudumie mteja alioingia.!

KAZI YA MZUNGU 7

Mwamvita akaondoka, Masu akawa anamwangalia. Akabaini Mwendo wa Malkia ulikuwa tofauti na alipokuja kumhudumia. Alionekana kuchangamka zaidi.

Aliporejea, kutoka kumhudumia mteja, Mwamvita alikuwa tofauti, huyu ndio Mwamvita aliyemfahamu. Malkia. Tabasamu mwanana!

Jioni ya siku hiyo Masu na Mwamvita walikuwa Pamoja wakizungumzia mpango wao wa kutoroshana. Walipofikia mwafaka, wakakubaliana mawasiliano yafanyike ili kuweka mazingira ya pa kufikia kueleweka.

Siku hiyo, Mwamvita hakulala kwa Masu, na hata hivyo SI Kama Masu alikuwa bado mpangaji pale Mwembe makumbi, hivyo hata hapa walikokuwa wamekutania Ilikuwa TU Lodge, mtaa mwingine mbali na Mwembe makumbi.

Kufikia saa tano hivi, Masu alimrejesha Mwamvita nyumbani. Safari hii hawakutumia njia ya kuuruka ukuta. Walimtumia ujumbe dada wa kazi, akafungua geti Mwamvita akaingia ndani'.

***
Masu aliingia jijini mnamo saa tano alfajiri. Akapanda daladalai kuelekea Tandika. Dada yake Maimuna alikuwa Ni mchuuuzi wa mboga na matunda kwenye soko la Tandika. Ilikuwa kitambo tangu aonane na dadake, Toka alipoondoka kwenda Zanzibar. Mawasiliano yao hayakudumu Sana hasa baada ya simu ya dadake kufungiwa na TCRA, na alipofanikiwa kusajili namba mpya, hakuwa na namba ya Masu. Hiyo ndiyo sababu iliyopelekea afunge safari kwenda jijini ili kufanya mkakati wa kumhifadhi Mwamvita hapo.

Alitokeza gengeni kwa dada yake akiwa kavaa kizungu, suti nyeusi, miwani machoni, shingoni alininginiza tai nyekundu maridadi kabisa. Mfukoni alikuwa na senti za kutosha. Senti zilizomwezesha Masu kumbebea dadake na wapwa zake zawadi za kutosha Toka Zanzibar, na zingine akiwa amezichukulia hapo hapo jijini.

Ilikuwa furaha, kuku walichinjwa, mchele ukapembuliwa kuondoa chuya, mchele wa gredi. Vinywaji vikaletwa, Ilikuwa sherehe. Walipokwisha kushiba, simulizi zikaanza, maswali kede kede. Ulikuwa wapi, unafanya Nini? Mbona umebadilika. Anko siku hizi Una hela? Anko ulikuwa Ulaya? Anko unaongea kizungu? Yote hayo akayajibu kiufasaha kabisa. Akiwa makini kutotoa Siri za kule kwa Mzungu.

Akawaeleza kwamba bado Yuko Zanzibar na anafanya kazi kwenye shirika kubwa la kitalii Kama mwongozaji wa watali. Mwishoni, anapata faragha na dada yake na kumweleza mpango wake. Dada yake Maimuna, akamweleza Hana shida na hili, isipokuwa maamuzi ya Mwisho yalikuwa kwa shemejie Bwana Jumanne Mgunda.

'Bwana shemeji, Hilo ndilo Jambo nataka unifadhili, akishakujifungua, nitampangishia Nyumba na ataishi hapo akifanya biashara nitakayomfungulia. Tafadhali Sana bwa'shemeji!' Masu alimrai shemejie

'Bwana shemeji unachoniomba Ni kitu kigumu Sana. Huyo Ni mtoto wa wenyewe, akapata tatizo, sie tutafanya Nini? Mimi ningekushauri uwatake radhi hao wakwezo, umtolee mahari awe mkeo! Shida gani hata umfiche binti wa wenyewe, ilhali unao uwezo wa kumuoa?, mbona ufanye hivyo bwa'shemu!?!' Bwana Mgunda alijihami. Labda kwa uzoefu na umri wake, alijua hili lilikuwa suala la kitoto, ambalo hakutaka kulishiriki.

'Nakuelewa Vema usemacho bwa'shemeji, shida Ni kazi nayofanya, hainitaki kuwa na mke!'

'Kazi ya kuongoza watalii haikutaki uwe na mke? Bwana shemeji, una hakika kazi yako Ni uongazaji watalii Zanzibar?' Mgunda aliongea, akitilia mashaka kauli za Masu.

Ni Kweli hakupaswa kuwa na mke, kazi yake hii, kwa mujibu wa maelekezo ya master Park Hye, kuwa na mke, au familia, lilikuwa Ni kosa kubwa Sana. Bila ufafanuzi wa ziada, masta alionesha kuwa Ni rahisi familia kutekwa na kusababisha mhusika kutoa Siri. Ilikuwa bado kuchakatwa na ubongo wa Masu Kama kazi ya ulinzi Ilikuwa na Siri nyingi vile. Hoja ya shemejie, Ilikuja kumpa changamoto. Ingawa alipewa onyo juu ya familia, Masu alikuwa radhi kuifanya Siri, lakini SI kumkana Mwamvita, Tena akiwa tayari kumletea mtoto? Atafanya lolote kumlinda Mwamvita na mtoto wao ajaye.

Kwa Nini walisisitizwa kuwa na Siri? Mbona Siri zenyewe hawakuzifahamu bado? Siri pekee waliyojua Ni kutoeleza kile walichofundishwa na mahali walikojifunzia. Je kulikuwa na umuhimu wa kuendelea kuficha hata nduguze?

'Asijue baba Wala mama, asijue mpenzi au nduguyo. Siku atakayojua mtu Siri hizi ndiyo siku utakuwa umetangaza kiama chako.' maneno ya master yakajirudia kichwani mwake. Maneno ambayo yalifuatana na kunyweshwa kinywaji kichungu kupata' kuonjwa na ulimi wake. Ikiaminika kuwa kinywaji hicho Ni Kama jini lililowekwa kuilinda Siri. Siri gani na kwa Nini Siri?

Kumbukumbu hiyo ikamuonesha hatari iliyokuwepo mbele yake. Hakutaka kuendelea na mazungumzo zaidi. Hakutaka kupoteza kazi kabla hajaianza kazi.

'Nimekuelewa bwana shemeji. Wacha nione Nini Cha kufanya.' Masu akaongea huku akisimama. Kichwani mwake alitafakari safari ya kijijini Malonje.

***
Baada ya mazungumzo ya Masu na shemejie kutozaa matunda aliyotarajia, alimpigia simu Mwamvita na kumjulisha kilichojiri, hata hivyo hakumweleza ukweli kwamba, sababu ya ombi lao kukataliwa lilikuwa na uzito wa kutosha. Sababu ambayo Kama angemjulisha, Mwamvita angekaa upande wa shemeji. Akamwahidi Hilo halitakuwa kikwazo Cha yeye kumhudumia na kumtoa kwenye zahma ya kuozeshwa kwa babu Kisiki.

Kesho ya siku hiyo, Masu akapanda Basi kutoka Dar kwenda Morogoro, hapo Tena angetafuta usafiri wa kumfikisha kijijini Malonje. Mbali na hitaji la kumchukua Maureen ili aishi na Mwamvita, Masu aliwamisi familia yake. Miaka Ilikuwa imepita akiwa hajamuona mamake kipenzi bi Lusia Masuke. Alimmisi kuliko wengine wote.

Alfajiri Sana, Masu alijihimu na kuamka mapema, alipanda gari la Msango Exp lililofanya safari zake kutoka Moro mjini kwenda vijijini, kikiwemo Kijiji Chao Malonje. Kikawaida gari hizi hazikuwa Basi, zilikuwa Ni zile gari maalum za kubeba mizigo, canter na fuso. Hili alilopanda lilikuwa Ni fuso. Kutokana na haiba yake kubadilika, maana hakuwa Masu wa miezi kadhaa nyuma, aliamua kutumia haiba mpya kupata huduma ya kiwango Cha hadhi yake. SI kwa ubaya, na Wala SI kwamba maskini akipata sijui Nini kulia mbwata, hataa! Ukweli Ni kuwa hakuna anayeoga akarudi kugalagala kwenye tope. Masu alipewa siti kwa Dereva. Leo, alivalia suruali ya kadet ya kaki, iliyomkaa Vema, juu akaningiza fulana yake form six maridadi, iliyokuwa ndani ya jaketi saizi yake. Miaka ya nyuma, Masu alikuwa na kawaida ya kuvaa ovasaizi. Siyo kwa kupenda lakini, uwezo wake ulimudu hayo maovasaizi aliyojichagulia kwenye mitumba iliyoletwa na mnada kijijini Malonje. Muda wake wa kuyavaa ulikwisha pita na Sasa ulihifadhiwa Vema kwenye kasiki la kumbukumbu, Kama hatua muhimu ya maisha yake.

Mvua kubwa ilinyesha na kufanya safari kuwa na mushikeli, hata hivyo baada ya vikwazo vya hapa na pale, Kama vile utelezi, kukwama, na hata pancha, Masu aliwasili kijijini Malonje. Aliposhuka, alikodi baiskeli impandishe nyumbani, kitongoji Cha mlimani. Hali ya hewa Ilikuwa njema. Kijani kibichi kila Kona. Maharage, mahindi, miti ya matunda, Malonje ilivutia Sana. Alipofika TU nyumbani, mbwa wao akawa wa kwanza kumlaki, akitikisa mkia kwa furaha na kumrukia rukia. Hali hiyo ya mbwa ndio iliwafanya mama yake na mdogo wake waliokuwa bize wakipepeta ngano, wabaini ujio wake. Na hata hivyo, walionekana kusita sita kuamini Ni yeye. Alikuwa amebadilika Sana.

'Kakaa!' Maureen aliita kwa mshangao!

'Hujambo mdogo wangu?' kusikia hivyo Maureen akamkimbilia na kumrukia, akamkumbatia Kaka yake kwa nguvu, Kidogo waanguke. Mama naye akajinyanyua chini kwa furaha, akamsogelea huku akiimba nyimbo za lugha yao, nyimbo za kumkaribisha mwanae nyumbani. Wakakumbatiana wote watatu kwa furaha.

Akakaribishwa nyumbani, wakatoa kiti Cha mbao Cha kukunjwa, kikakunjuliwa, Masu akaketi akinesanesa kifalme. Ilionekana Kama Masu huyu waliyekuwa wanamuona Ni Masu tofauti na waliyemzoea. Ingawa ucheshi wake ulidumu naye, lakini hadhi yake Ilikuwa tofauti. Wakawa wanamwangalia kwa kuibia. Walimtamani. Maisha aliyoishi huko alikotoka walitamani wayaone. Wayaishi. Maureen, alikwisha amua kichwani, atamganda Hadi akubali kwenda naye. Kama Masu, Masu ambaye kuoga Ni Hadi anyeshewe zamani zile ametakata hivi, huko alikotoka ndiko kwa kuishi.

Haikuchukua muda kabla majirani kujua kuwa Masu karejea kijijini. Tetesi zilisema kijana huyo kawa mzuri kupindukia. Wote walitaka wamuone. Mama Saba yeye hakusubiri kumuona, alichotaka Ni mwanae Marietta kupata nusura ya kuolewa na kijana huyo, aliyekuwa gumzo kijijini masaa machache TU baada ya kurejea. Mwendesha baskeli alikuwa mpiga mbiu makini bila shaka.

'Marietta, we Marietta!!' mama Saba aliita kwa sauti. Marietta aliyekuwa jikoni akiosha vyombo, akaisikia sauti ya mamaye.
'Bee mama' akaitika huku akitoka kwenda kumsikiliza mama yake.
'Njoo mwanangu, njoo nikwambie!' mama Saba akaongea. Marietta akafanya hima kumfikia mama yake.
'Umeahamaliza kuosha vyombo mama?' mama Saba alimuuliza mwanae.
'Ndio namalizia mama'
'Anhaa, Sasa hivyo vyombo achana navyo. Cha kufanya, nenda kaoge uvae upendeze. Tutaenda kwa mzee Masuke. Yule kijana wake Masu nimeambiwa karudi. Nijuavyo Mimi, wakishaenda mjini, ukisikia wamerudi wakiwa tofauti na walivyoenda, wengi wanakuwa wamefuata jiko. Fanya hima upendeze na ujipendekeze kwa Masu mapema, kabla hajaona wengine. Mwanangu ulivyo mrembo, wewe ndio unastahili kwenda mjini. Jiandae mama ee!' mama Saba alimpasha Marietta. Marietta aibu ikamshika. Ingawa uhusiano wake na mama yake ulikuwa wa kirafiki mno, hili la Leo kuambiwa na mamake, lilimtia fadhaa Kidogo. Lakini, Marietta alimfahamu Vema Masu, walisoma na mdogo wake Maureen. Haikuwahi kuwa bayana kwenye ufahamu wake, lakini huenda alimpenda mvulana huyo. Kama sivyo, mbona alimuogopa bila sababu?. Mbona alipokutana naye alikosa kujiamini? Kwa Nini sauti ilimkauka kila alipotaka kumsabahi au aliposabahiwa naye? Mbona alimuonea aibu? Bado hakuwa na jibu. Na hapo, alikuwa anamtafakari Masu yule wa zamani. Hajamuona huyu Masu mpya!

2020
David Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 8
Imeandikwa na David Samson Ngocho

#Tulipoishia
'Anhaa, Sasa hivyo vyombo achana navyo. Cha kufanya, nenda kaoge, uvae, upendeze. Tutaenda kwa mzee Masuke. Yule kijana wake Masu nimeambiwa karudi. Nijuavyo Mimi, wakishaenda mjini, ukisikia wamerudi wakiwa tofauti na walivyoenda, wengi wanakuwa wamefuata jiko. Fanya hima upendeze na ujipendekeze kwa Masu mapema, kabla hajaona wengine. Mwanangu ulivyo mrembo, wewe ndio unastahili kwenda mjini. Jiandae mama ee!' mama Saba alimpasha Marietta.

Marietta aibu ikamshika. Ingawa uhusiano wake na mama yake ulikuwa wa kirafiki mno, hili la Leo kuambiwa na mamake, lilimtia fadhaa Kidogo. Lakini, Marietta alimfahamu Vema Masu, walisoma na mdogo wake Maureen. Haikuwahi kuwa bayana kwenye ufahamu wake, lakini huenda alimpenda mvulana huyo. Kama sivyo, mbona alimuogopa bila sababu?. Mbona alipokutana naye alikosa kujiamini? Kwa Nini sauti ilimkauka kila alipotaka kumsabahi au aliposabahiwa naye? Mbona alimuonea aibu? Bado hakuwa na jibu. Na hapo, alikuwa anamtafakari Masu yule wa zamani. Hajamuona huyu Masu mpya!

KAZI YA MZUNGU 8.

Kidogo Kidogo, familia ya mzee Masuke ilianza kupokea wageni. Mmoja, wawili, watatu, kadri muda ulivyosonga mbele, watu wakaongezeka. Hatimaye mikeka ikakunjuliwa na kutandazwa nje. Haikuwa Tena Siri, kwa mzee Masuke kulikuwa sherehe ya kumkaribisha Masu kutokea jijini Dar.

Huko mitaani watu walialikana, wakaungana wawili ama watatu wakaelekea nyumbani kwa mzee Masuke.

'Unaambiwa kijana Ana hela SI Kidogo. Ameamua kuchinja ng'ombe wa kutosha kulisha Malonje na vitongoji vyake!' alisikika kijana mmoja akipasha wenzie habari njema za sherehe.
Lo! Heri Masu angelijua taarifa zilizoonea kijijini. Ajabu, WAHUSIKA wa sherehe wenyewe hawakujua wana sherehe!

Kutanabahi, muziki ukashushwa kwenye baiskeli, mitambo ikaunganishwa, muziki ukasikika. Alouleta muziki ndio kabisa akawashitua wale ambao hawakupata taarifa awali kujua kwa mzee Masuke neema imeshuka.

'Braza Kama utataka tukeshe utachangia elfu ishirini tu.' Dj alinongona sikioni kwa Masu.

'Kukesha kwa ajili ya Nini?' Masu akahoji.
'Ah Braza, kwani Una mpango wa kuzima muziki muda gani? Dj Yusto akauliza.
'Sina mpango wowote, muziki umekuja nao utauzima utakapoona vema.!'
'Hadi saa sita usiku, kawaida tunatoza elfu tano TU, na inakuwa burudani ya uhakika braza.'
'Sasa.,. Kwani aliokualika hapa nani? Sikia Dj, hapa hapana taarifa yoyote ya sherehe.,mie nikajua mmefurahi TU kuniona mmeamua kunikaribisha kistaarabu!?' Masu alizungumza na kuongezea
'Tangu lini mmeanza utaratibu wa kuvamia Nyumba za watu na kuwatoza fedha za muziki?'
'Bro Mimi nimefuatwa, nikaambiwa hapa Pana sherehe ya ukaribisho, hivyo muziki unahitajika, wakanambia pesa nalipwa hapa hapa, Sasa nashangaa Tena unachosema!' Dj Yusto akalalamika.
'Ila, Haina noma bro, naondoka na muziki wangu.'
Masu aligeuka nyuma, akaona jinsi mama yake na wakina mama wengine walivyokuwa wamefurahi wakicheza ngoma ya kikabila iliosikika kwa ubora kutoka kwenye spika za Dj Yusto huku waliifuatisha maneno ya wimbo.
'Nikuombe TU uchangie hata buku nikalipe nishati. Sola na betri nimelazimika kukodi maana zangu zinatumika baa kwangu.' Dj Yusto akarai.
'No, we gonga muziki Hadi watakapochoka!' Masu akaongea huku akiwatazama mama zake.

Hakutarajia hili. Lakini kwa vile kijijini vitu si ghali Sana, Masu akajikuta akiridhia sherehe iendelee. Tayari ng'ombe mnono alikuwa keshachinjwa bila hata yeye kutaarifiwa, mwenye ng'ombe alikuwa katulia anasubiri kulipwa fedha zake.

Giza lilishaanza kuingia Masu alipomuona mzee wake 'Masuke mwana wa Miganda'. Hivyo ndivyo alivyojiita. Masuke Miganda Kama wazee wengi kijijini Malonje, alikuwa na familia za mitaala. Kwa maana ya wake wawili na zaidi. Habari za kijana wake Masu kurudi kijijini na kufanya sherehe kubwa, alizipata kilabuni alipokuwa anakunywa ngano na wazee wenzake. Mpashaji wa habari alisisitiza kuwa kila mwenye nafasi alikaribishwa huko nyumbani kwa mama Masu. Masuke wa Miganda kusikia hivyo akasimama kwa ufahari na kutangaza,
'Pombe yote iliyopo hapa, ibebwe ipelekwe nyumbani. Wazee wenzangu, leo tutakunywa pombe kwa hisani ya kijana wangu, Haya twendeni nyumbani.' Wazee wenzake wakasimama na kuambatana na Masuke wa Miganda.

Masu akashuhudia kundi la wazee nane walioambatana na mzee wake. Akafurahi. Ingawa Masuke wa Miganda alikuwa chapombe, alimudu kutengeneza mahusiano chanya na wanae. Aliwasomesha, alifurahia muda Pamoja nao na kuwapa mawaidha Haya na Yale kuwajenga. Hakuwa bahili alipokuwa na hela. Na, Kama Kuna kitu kimoja alichokijua mzee Masuke wa Miganda, Basi Ilikuwa Ni furaha na matumizi ya fedha.

Pamoja na ugumu wa maisha ya kijijini, kwa mzee Masuke hakukosekana chakula. Na ilipopatikana fedha, kwa mzee Masuke Ilikuwa sherehe. Ndio maana Masu aliporejea akiwa kapendeza na kutakata, watu wakajua itakuwa sherehe tu. Wakatangaza sherehe.

Masu alimfuata baba yake na kumsalimia kwa heshima Pamoja na wazee wenzake alioambatana nao.
'Ah kijana wangu umenifurahisha Sana. Ona wazee wako Hawa wanavyofurahi Ni kwa sababu yako. Na ashukuriwe Mungu kwa kukufikisha salama.'
'Asante Sana baba.'
'Masuke wa Miganda umejua kutengeneza urithi na hata wajionea vile utakavyoenziwa siku ukiwafuata baba zako. Kijana anapita kwenye njia zako kabisa. Hapa kijijini kila mtu anajua nyumbani kwa Masuke Ni nyumbani kwa sherehe!' alidakia mzee. Albano na kumsifia Masu. Wazee wengine wote wakacheka wakitikisa vichwa vyao kuafiki kauli za mzee Albano.
'Asanteni kwa maneno mazuri wazee wangu na karibuni Sana. Vipi mwajionaje na Hali?' Masu akahoji.
'Salama kijana, furaha TU.' alijibu mzee Kisoka kwa niaba ya wengine wote.
'Asante Sana kijana wetu Masu kwa kuona umuhimu wa kutualika kwenye sherehe yako hii ya kumtambulisha mchumba wako. Hizi zimekuwa habari njema Sana maana umri nao unaruhusu Sasa. Hilo Ni Jambo jema Sana!' alizungumza mzee Rashid. Wazee wenzake wakaafiki kwa kutikisa vichwa vyao.

Masu alizidi kachanganyikiwa na habari zilizokua zinaendelea hapa. Yalikuwa yanaibuka mapya kila baada ya muda, uchovu wa safari ukaisha bila hiyana. Akalazimika kukabiliana na Haya yaliyokuwa yanatokea. Akataka akanushe lakini akaona SI busara. Akajisemea moyoni;
'Nitamwita baba pembeni, nimkanushie habari hii wasijekuamini Ni sherehe ya utambulisho wa mchumba.'
Busara hiyo hiyo ikamweleza ampe muda kwanza angalau awakaribishe wageni wake ndiyo afanye mpango huo wa ukanushaji habari.

Akatoka hapo, akaongee na mama yake kuhusu Hilo suala pia. Ile anageuka akakumbana uso kwa uso na Marietta. Ilikuwa Kidogo TU wavaane.
'Oh, samahani Sana, sikukuona!' Masu akatamka.
'Asantee!' Marietta akaitoa sauti yake tamu huku akitawaliwa na aibu zake, akawa anatafuna TU ukucha wa kidole chake. Marietta alijua kujipamba wee, jioni hii na Giza lake kwa mbali, yeye aling'ara kwa uzuri. Kwa sekunde kadhaa, Masu alipotezwa. Akazama kwenye wingu la fikra ghafla. Nadhani alijiuliza Kuna msichana mrembo kijijini hapa Kama huyu. Akili yake iligoma kumuachia aondoke zake.

'Waitwa Nani ewe mrembo?' Masu akatamka kwa huba.
'Masu jamani, umeenda mjini ndio umetusahau hata sisi tuliosoma Shule moja?' Marietta akajitia moyo wa ushujaa, ule woga akajitahidi kuuondoa, japokuwa Ni Kweli moyoni kulikuwa na kitetemeshi kwa mbali, lakini alibaini SI Kama enzi zile. Masu alikuwa handsome. Hakuwa yule Masu wa zamani. Marietta akakiri moyoni kuwa alimpenda kijana huyo. Akajishangaa vile leo alivyomudu kusimama na hata sauti yake kutoka bila hofu Kama zamani. Bila shaka safari yake ya Dar, Ilikuwa na mengi ya faida. Moja ikiwa Ni kumuondolea hofu, lakini pia ilimfunza kuvaa kisasa, na Hilo lilimpa kujiamini zaidi. Ndiyo, hata aliporudi kijijini Toka Dar, Marietta alikuwa habari mpya. Wanaume walimfuata fuata na yeye aliwakatalia, aliamini heshima ya mwanamke si kukimbizana na wanaume. Lakini, daa! Maisha Ni nyoso Sana. Ukikaa kizembe yanakutia kidole jichoni. Hakuwa na pesa za kudumisha usistaduu kijijini. Alipotafakari, akagundua hakutaka kuwa mwanakijiji aliyekuwa hapo awali kabla ya kwenda jijini. Akaona kudumisha usistaduu sharti awe na pesa. Angezipataje? Marietta akaweka mpango.

Mpango wake ulimhakikishia anapata fedha za kununulia viwalo na vipodozi. Walimu wa Shule ya msingi Malonje, walitoa hizo fedha, walimu wa kiume vijana na hata wale wenye wake zao. Na Wala walimu hao, hawakujua kuwa, Marietta alikuwa wao wote, wote Saba. Kila mmoja akifanya kuwa Ni Siri. Kisa Nini? Marietta alikuwa binti mdogo, na hakuna mwalimu Kati yao alitaka ifahamike anatoka na mtoto huyo. Marietta Sawa na Mwamvita, alikuwa na miaka 17 tu. Ni mama yake pekee aliyeona binti huyo anafaa kuolewa. Na Sasa akawa anampambanisha na Masu. Umaskini mbaya nyie!

'Wee, Unataka kunambia wewe tumesoma wote pale Malonje Shule ya msingi?'
'Ndio bwana. Mimi nilikuwa darasa moja na Maureen. Sema Kuna kipindi nilienda Dar kwa dada ndio nikamalizia darasa la Saba, niliporudi wewe ulikuwa ushaondoka. Naitwa Marietta'
'Marietta mtoto wa mzee Thomas?'
'Ndio'
'Waoo! Dah tungekutana sehemu tofauti nisingekubali kabisa kuwa wewe unatokea Malonje. Mtoto unapendeza, unawaka Kama Malaika. Unawazidi hata waliopo Dar.'
'Asante' Marietta alijua kutumia sauti yake kuamsha hisia. Alipotamka Asante, Kuna vile alimvutia zaidi Masu, na kwa kutambua Hilo akajitia kuondoka. Ah wapi? Masu akamkamata mkono.
'Usiondoke Marii! Tunahitaji kuongea.' akatamka, mara, simu yake ya mkononi ikaita. Akavaa earphones masikioni ili kuipokea simu.
'Samahani kidogo.' akamweleza Marietta. Akaipokea simu.
'Hello!'
'Masu' Ilikuwa sauti ya Malkia wake Mwamvita. Sauti hii iliambatana na kilio Cha kwikwi. Kulikoni? Akajiuliza.
Akajisogeza mbali na Marietta.
'Kulikoni Malkia, mbona walia mpenzi? ee Kuna Nini mamii?'
'Masu wanapanga kunifungisha ndoa ya mkeka kwa hila, nimepata habari kutoka kwa watu wa jirani na familia ya mzee Kisiki, sijui nifanyeje Masu!'
Masu akili ikachanganyikiwa. Katika kutapatapa akamwambia 'subiri hapo dakika moja!'
Akaonekana kuzunguka hapa na pale Kama anayetafuta majibu. Akapiga simu Tena.
'Malkia, nakutumia pesa mpesa, Tumia Kama nauli uende Dar, Kuna mtu atakupokea.'
Alipomaliza mazungumzo hayo, hakukumbuka Tena Kama kulikuwa na Marietta akimngojea. Masu akatoka hapo kwenda chumbani kwake. Huko akapata utulivu wa kutafakari nani wa kumpokea Mwamvita. Dada yake, Maimuna. Akampigia simu na kumjulisha akampokee wifi yake. Hakumpa nafasi ya kuhoji.
'Ukishampokea mweke Lodge jirani na hapo kwako!' alitoa agizo akakata simu. Akafanya muamala na Sasa akapata ahueni nafsini mwake. Hapo tena, ndipo kumbukumbu ya Marietta ilipomrejea. Akatoka nduki kumfuata. Hakumuona.

Dj Masu alikuwa kafunga mitambo yake Vema. Nyumbani kwa mzee Masuke wa Miganda kuling'aa kwa taa za Sola na harakati za kufurahi, kula na kunywa ziliendelea Kama kawaida. Mara, kwenye spika kukasikika sauti aliyoifahamu Vema. Sauti ya mzee Masuke wa Miganda.

'Mh... ah!' Mzee alianza kwa kusafisha koromeo ili sauti itoke vema, halafu akafanya kupuliza kwenye spika kujaribu ufanisi wa maiki.

'Ah, karibuni Sana wanamalonje nyumbani hapa tusherehekee ujio wa kijana wetu Masu. Nimeambiwa sherehe hii inahusika pia na utambulisho wa mchumba wake, Marietta binti wa mzee Thomas.' mzee Masuke akavuta pumzi kabla ya kuendelea. Akaachia mwanya kwa akina mama kushangilia kwa vigelegele na nderemo zikiwemo na mbija kutoka kwa vijana.

Tangazo Hilo likapokelewa kwa mshituko na Masu, lakini kwa mama yake Hali Ilikuwa tofauti kabisa. Alizimia baada ya kusikia tangazo Hilo.

Kwa upande wa pili, mzee Thomas mwenyewe ambaye pia alikuwa kwenye sherehe hii, alionekana akisukumana na watu wampishe njia, akielekea alipokuwa Masuke wa Miganda. Alionekana kujawa na Shari isiyo na kipimo. Labda, hili lilikuwa tangazo ambalo lilitolewa bila maelewano ya familia zilizohusika na hivyo mzee Thomas akaona anadhalilishwa. Labda! Ila kilichoanza Kama furaha kilikuwa kinaenda kubaya.

2020
David Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 9
David NGOCHO Samson

#Tulipoishia

Tangazo Hilo likapokelewa kwa mshituko na Masu, lakini kwa mama yake Hali Ilikuwa tofauti kabisa. Alizimia baada ya kusikia tangazo Hilo.

Kwa upande wa pili, mzee Thomas mwenyewe ambaye pia alikuwa kwenye sherehe hii, alionekana akisukumana na watu wampishe njia, akielekea alipokuwa Masuke wa Miganda. Alionekana kujawa na Shari isiyo na kipimo. Labda, hili lilikuwa tangazo ambalo lilitolewa bila maelewano ya familia zilizohusika na hivyo mzee Thomas akaona anadhalilishwa. Labda! Ila kilichoanza Kama furaha kilikuwa kinaenda kubaya.

KAZI YA MZUNGU 9

Mzee Albano alimuona mzee Thomas alipokuwa anamfuata mzee Masuke akiwa kaghafirika anafuka Shari. Akaona kinachoenda kutokeza Ni aibu, akanyanyuka haraka na kuwafuata wazee wenzake kabla hawajachafua heshima ya wazee kwenye kadamnasi ile. Akaukaza Mwendo na kumfikia mzee Thomas na kuudaka mkono wake uliokuwa unarusha ngumi kwa mzee Masuke. Akaingilia Kati kile kilichoonekana kutaka kutokeza balaa.

Akawachukua wazee wale na kuingia nao ndani. Akiwatuliza hasa hasa mzee Thomas aliyeonekana kufura kwa hasira Kali. Mzee Masuke alipigwa na butwaa! Hakuamini hiki kilichokuwa kinaendelea hapa. Kumbukumbu yake ilimwambia hili suala lilikuwa na baraka za mzee Thomas, vipi Sasa ageuke mbogo? Hakuelewa.

Kitu Kama dakika kumi hivi kabla ya mzee Masuke kupanda jukwaani na kushika kipaza sauti, alikuwa amefanya mazungumzo na mkewe mzee Thomas, mama Saba. Mama Saba alikuwa anampa taarifa kuwa watoto wao, Marietta na Masu walimpasha habari kuwa wao wanapendana. Akataka kujua Kama mzee Masuke alikuwa na taarifa hiyo. Kwa mzee Masuke lilikuwa geni. Akamweleza kwamba alikuwa bado kupata' nafasi ya kuzungumza na mwanae. Lakini pia akamuuliza Hilo suala mzee mwenzie, mzee Thomas alilichukua vipi. Mama Saba akamwambia 'hana pingamizi' Yuko tayari kabisa endapo yeye mzee Masuke angeridhia. Masuke wa Miganda, labda kwa vile alikuwa keshachangamka kwa ile ngano aliyokunywa, hakuona haja ya kupoteza fursa. Vipaza sauti vipo, Nani mwenye maamuzi Kama SI yeye? Mama Masu atapata taarifa baadaye, na kilichompa kujiamini zaidi Ni ile habari kuwa kijana wake mwenyewe alikuwa karidhia. Akataka amfanyie hamaniko la furaha. Amshangaze kwa kutangaza habari njema.

'Wazee wenzangu, aibu gani hii mnataka kufanya hapa, mbele ya jamii nzima, mnataka kuonesha Nini wazee?!' mzee Albano alizungumza kwa hisia.

'Huyu Bwana Ni mpuuzi Sana huyu. Na ningemuonesha kazi leo!. Anaanzaje kumtangaza binti yangu hadharani kwa suala Kama hili? Anajipatia mamlaka ya kumtangaza binti yangu bila hata kuwasiliana na Mimi? Upuuzi gani huu.? Mwanangu nimemlea katika maadili,Leo huyu Bwana anajifanya yeye ndiye mwenye maamuzi ya kumuozesha kijana wake? Ndo utaratibu gani huo.?' mzee Thomas alikuwa na hasira Kweli Kweli!

Masuke wa Miganda aliinamisha kichwa chini kwa Soni. Maneno ya mzee Thomas yakamwingia na kumsuta. Akajutia kukurupuka kwake. Ama Kweli shibe mwana malevya!

'Ya Kweli Haya mzee Masuke? Kwamba hata bila kuwasiliana na mzee mwenzio wewe umeona fahari kujichukulia maamuzi? Umesahau tamaduni na Mila zetu?' mzee Albano Sasa alizungumza kwa jaziba. Kama Kweli mzee Masuke alifanya hayo bila kuwasiliana na mwenzake, alikuwa amemkosea Sana mzee Thomas.

'Wazee wenzangu nikiri kwamba nimeteleza. Na kuteleza kwangu kumetokana na mazoea mabovu. Nilisahau kwamba Mila zetu zinatutaka sisi wanaume ndio tufanye maamuzi. Nikajikuta nimempa sikio langu mama Saba, ah nimekuwa dhalili kwa kusahau ya wahenga!. Mkeo, amenihakikishia mlikubaliana, na Mimi ndio mlikuwa mwataka kusikia nasemaje, Kumbe Ilikuwa tamanio tu la mama Saba vijana wetu waoane? Ah, mzee Thomas Nisamehe Sana ndugu yangu. Tuliangalie suala hili kwa jicho lingine tafadhali. Bado tunaweza kuzungumza na kuwapa baraka vijana wetu Kama wamependana wakaanzishe familia zao.' Masuke wa Miganda alionesha uungwana.

'Umemsikia mzee mwenzio, Kumbe naye kauingia mkenge tu. Hebu yamalizeni Haya kiungwana wazee wenzangu.' mzee Albano alitoa Rai.

'Wanawake, wanawake. Mama Saba Mara ngapi nimuonye kuingilia majukumu ya wanaume? La! Shida hii. Lakini hata hivyo, mzee Masuke, Mimi na wewe hatuwezi kuoleana kabisa. Wewe na Mimi mwiko kabisa kuoleana.' mzee Thomas alizungumza huku akijaribu kutafuta kigezo Cha kuweka kikwazo kwa wao kuoleana. Hakikuwepo. Siri ya siku nyingi Ilikuwa ifichuke kama angesema Sababu..

'Kwa Nini iwe mwiko, Mimi na wewe hatuna udugu wowote, mbona iwe mwiko kijana wangu kumuoa binti yako?' Masuke wa Miganda akatahamaki. Hayakumwelea Haya! Mara, mlangoni akasimama mzee Kisoka na kutamka maneno yaliyoahirisha kikao kile Cha usuluhishi.

'Wazee wenzangu, Kuna shida Kidogo imetokezea. Mama Masu Yu nusu kaputi hivi navyoongea. Hebu tuone namna gani tunasaidia Kidogo.' Wazee wakanyanyuka na kumfuata mwenzao. Lo! Kizaazaa!

'Mama Masu kimempata Nini? Hajawahi kuzimia Leo anazimia, shida Nini hasa?' Masuke wa Miganda alijiuliza bila kupata' majawabu.

Sherehe Ilikuwa imeingia dosari. Kila mmoja alionekana kuhaha na kushangazwa na matukio yaliyokuwa yanageuka geuka. Minong'ono ikasikika, watu wakiongea hili na lile. Kuna waliosema, Kuna uwezekano mtu mbaya kaona wivu kamtupia jini kuharibu sherehe. Lakini wapo walioenda mbali na kutoa kauli za tuhuma nzito dhidi ya Masu
.
'Wewe Unadhani huu utajiri Masu kautoa wapi? Fikiria, ametoka hapa juzijuzi tu, Leo anarejea akiwa tajiri, Tena hakai hata siku moja, anaweka sherehe kubwa Kiasi hiki! Hamjiulizi tu? Huyu atakuwa kapata pesa za manyoka. Mtanambia Kama hajamtoa kafara mama yake. Hawa wakishaenda mjini tu, kazi yao Ni kujiunga Freemason. Haipiti mwaka unasikia mtu wa karibu kaaga dunia.' alisikika mama mmoja akisimulia kikundi Cha wanawake.

'Wee, ndiyo maana anavaa bonge la Pete kidoleni. Ah kwa Kweli pesa za majoka mie aku sizitaki!' msichana mmoja alidakia akishika kiuno chake na kukitikisa kwa nyodo.

'Hebu huko, hivi nyie kazi yenu kuongea ya wenzenu tu.! Watu wazima hamfanyi kazi, kazi kuzusha maneno tu. Kuna mwenye uhakika na msemacho hapa? Na mkishamchafulia jina nyie mwafaidikani?' Ilikuwa sauti ya Marietta akiwazodoa wazushi. Moyoni alijaa tele Masu, hakutaka kusikia habari za kumchafulia sifa mahabuba wake.

***
Masu alipopata taarifa ya mama yake kuzimia tu, haraka haraka, alikodi baiskeli ili kumuwahisha dispensari.
Akajikuta anajutia uamuzi wake wa kutowaambia wazee, juu ya habari za mchumba, kwamba hazikuwa za Kweli. Akadhani kuwa tangazo lile lilisababisha hayo madhila.

Alikokota baskeli akisaidiwa na Kaka yake, kwa mke wa kwanza wa mzee Masuke wa Miganda, aliyejulikana kwa jina Miganda. Ilikuwa Kama utaratibu wa kikabila wazazi kuwapa watoto majina ya ndugu zao waliokwisha kutangulia mbele za haki.

Miganda alisukuma baiskeli, huku Masu akimshikilia mama yake kumpa balansi. Maureen na dada zake, na wakeze Masuke wa Miganda, kwa Pamoja walionekana kuhuzunika Sana na walionesha ushirikiano mkubwa. Tukio hili liliwaweka wakeze Masuke wa Miganda Pamoja Kama familia.

Kwa mbali, Masuke wa Miganda na wazee wenzake walikuwa wanajongea kuwafuata wale waliokuwa na baiskeli. Kimya kilitawala Kati yao.

SI mzee Masuke tu aliokuwa na wasiwasi juu ya mkewe. Yeye alikuwa hajui Nini kimempata mkewe, lakini mzee Thomas alihisi lile la tangazo la awali ndio sababu. Alijua mshituko alioupata mama Masu, utakuwa ulipelekea Hali hiyo. Kwa sababu hata yeye, Ni kujikaza kiume tu kulikosababisha asidondoke chini. Mzee Thomas alikuwa na Jambo lililomfanya awe mwenye huzuni zaidi. Walikuwa wanamalizia kamtremko, jirani na kwa mzee Albano, hatua chache kutoka nyumbani kwa daktari wa kijiji bwana Mgode. Mama Masu akapiga chafya! Akafunua macho Kama atokaye usingizini.

'Ameamka, ameamka!' Masu akajikuta anaimba kwa furaha na kumkumbatia mama yake. Kumbato lake likamnyima hewa mama yake. Ilimlazimu Miganda kumtandika ngumi ili kumpa taarifa ya janga alilokuwa asababishe. Masuke akashituka, akajitoa kwa mama yake, mama akapata nafasi ya kupumua.

'Pole mama!' Masuke na Miganda wakatamka kwa Pamoja.
'Kimenipata Nini. Mbona mmenibeba kwa baiskeli utadhani mgonjwa?' mama Masu alihoji.
'Usijali utakuwa Sawa tu. Ni mshituko ulikupata halafu ukazimia'
Taratibu kumbukumbu zikarejea.
'Naona Niko Sawa, tungerejea tu nyumbani.!' akatamka kwa huzuni. Kuna kitu kilimtia hofu moyoni, au kilikusudia kumnyong'onyesha kabisa. Kwa muda wote huo walipokuwa wakizungumza, walikuwa Sasa wamesimama.

Mzee Masuke na wenzake waliwafikia mama Masu na wanawe. Wote wakionekana kushusha pumzi za 'Oh afadhali, Asante Mungu'. Kila mmoja alikuwa anasema pole, pole. Mzee Masuke akapata taarifa ya mkewe kutaka warudi nyumbani. Hakuiafiki.

'Kwanza tumuone daktari Mgode, akufanyie vipimo, aangalie shida Ni Nini na ikibidi atuambie chanzo Cha shida hiyo ndio Sasa turejee nyumbani.' akahitimisha. Safari ya kwa daktari Mgode ikaendelea.

***
Mwamvita aliamka alfajiri mapema kwa ajili ya sala. Akamwandalia baba yake chai na vitafunwa. Baadaye saa moja hivi, alikuwa na mpango wa kuondoka nyumbani. Akili yake ilitawaliwa na habari ya kutoroka tu, kwani habari ya kuolewa na mwanaume makamo ya babake haikumwingia akilini.

Alimweka Sawa dada wa kazi. Kawaida walitumia huduma ya dobi Nyumba ya tatu Toka pale. Kazi ambayo ilifanywa na Husna, dada wa kazi, kubeba lundo la nguo chafu na kwenda kuziosha kwenye mashine hapo kwa dobi Juma. Kwenye mzigo wa nguo zile chafu, nguo na begi lake vilitangulizwa mbele. Mwamvita angezipitia na kuanza safari ya kuelekea feri ili kuabiri boti kwa safari ya kuingia jijini Dar. Lakini shida ikawa kujulikana. Nani hakumfahamu Mwamvita mtaani Kwao. Mtoto wa shekhe Abuubakr? Akamuwaza Masu, vile angekuwepo amsaidie kuibeba, ili asiulizwe 'aenda wapi Tena', au kuambiwa, ah 'Wenda bara?'. Wazo Hilo likampatia njia. Akachukua simu yake, akatafuta jina, Bakari, akaliona,akampigia!

'Halo' simu ikapokelewa, na sauti ya Bakari ikasikika. Aliifahamu Vema sauti hiyo. Sauti iliyowahi kumpasua moyo kwa taarifa ya majonzi, ilipomtaarifu kuhusu kutekwa kwa Masu. Ni kipindi hicho walipobadilishana namba ili kutaarifiana habari za Masu Kama angepatikana.

'Shem wangu najua nimekuangusha! Kusema Kweli bado sijapata fununu wapi alikopotelea Masu…' Bakari hakumalizia Maelezo yake. Mwamvita akadandia mazungumzo yake.
'Shemu Nina shida, nahitaji msaada wako tafadhali. Kuna mzigo wa kubeba, waweza kuja?'
'Naja Shem, wapi upo?'
'Njoo kwa Juma dobi'
'Nipo njiani'

Tangu Masu alipomweleza habari za Mzungu, kwamba kulikuwa mchongo, Bakari hakupata kusikia Tena habari yoyote kutoka kwa Masu au Yusuf. Wiki zikakatika, juhudi za kuwapata rafikize hao hazikuzaa matunda. Kutokana na wimbi la watu kupotea, kutekwa na hata kutoweka lililokuwa limeikumba nchi, Bakari, alipoulizwa juu ya Masu na Mwamvita, akajikuta ametengeneza sababu rahisi kueleweka, 'Masu alitekwa na wasiojulikana!'. Hata hivyo, Bakari alihisi M'bara atakuwa aliamua kurejea Kwao kuuepuka msala wa kutia mimba mwanafunzi.

Dakika tano zilimwezesha Bakari kumfikia Mwamvita. Walikutania kwa dobi Juma. Wakaongea mawili matatu, kusabahiana na kujuliana Hali. Kisha mdogo mdogo wakaanza kutoka, Bakari akiusukuma mkokoteni wao 'motofaya'. Hawakujua hawajui.

Zile habari za mipango ya kuozeshwa kwa mzee Kisiki, hazikuwa utani. Mwamvita alikuwa mwali. Alitakiwa kukaa ndani wakati mipango ikiendelea. Mzee wake sheikh Abuubakr, hakutaka kufedheheshwa kwa Mara ya pili. Aliweka ulinzi kwa bintiye bila Mwamvita kuwa na taarifa.

Habari ya Mwamvita kukutana na Bakari ilimfikia mzee Abuubakr. Aliyempasha hakumweleza utofauti Kati ya Masu na Bakari. Hivyo sheikh Abuubakr, alijihimu kuondoka dukani kwake na kuelekea kituo Cha polisi kutoa taarifa na kupata' Askari wa kumkamata mhalifu, kijana aliyetia mimba bintiye mwanafunzi.

Hawakujua kilichokuwa kinawapata muda mfupi ujao. Ilikuwa ghafla tu, Askari alitokeza mbele yao na kuwaweka chini ya ulinzi. Bakari na Mwamvita hawakuamini kilichotokea. Walikumbwa na fadhaiko. Hawakujua Nini Cha kufanya. Bakari alichukuliwa kupekekwa polisi Asijue kosa. Sheikh Abuubakr alikuwa mbogo, amefura kwa hasira.
'Afande, huyu anayetia mimba wanafunzi, afungwe kwa mujibu wa sheria, tutashirikiana kukamilisha ushahidi.' Sheikh Abuubakr alitamka, tamko ambalo Sasa lilimwamsha Bakari juu ya balaa lililomkumba. Hakuwa na kosa, wema wake ulikuwa unamponza. Akajaribu kutaka majibu, akamkazia macho Mwamvita, 'kulikoni?', macho yake yaliuliza, Mwamvita hakuwa na jibu.
'Nakuapia sikulijua hili Bakari.' Mwamvita akajibu huku chozi likimdondoka,wakati huo sheikh Abuubakr alikuwa anamvuta mkono bintiye kuondoka kituoni.

2020
David Ngocho Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 10

MTUNZI: DAVID SAMSON NGOCHO

#TULIPOISHIA
Hawakujua kilichokuwa kinawapata muda mfupi ujao. Ilikuwa ghafla tu, Askari alitokeza mbele yao na kuwaweka chini ya ulinzi. Bakari na Mwamvita hawakuamini kilichotokea. Walikumbwa na fadhaiko. Hawakujua Nini Cha kufanya. Bakari alichukuliwa kupekekwa polisi Asijue kosa. Sheikh Abuubakr alikuwa mbogo, amefura kwa hasira.
'Afande, huyu anayetia mimba wanafunzi, afungwe kwa mujibu wa sheria, tutashirikiana kukamilisha ushahidi.' Sheikh Abuubakr alitamka, tamko ambalo Sasa lilimwamsha Bakari juu ya balaa lililomkumba. Hakuwa na kosa, wema wake ulikuwa unamponza. Akajaribu kutaka majibu, akamkazia macho Mwamvita, 'kulikoni?', macho yake yaliuliza, Mwamvita hakuwa na jibu.
'Nakuapia sikulijua hili Bakari.' Mwamvita akajibu huku chozi likimdondoka,wakati huo sheikh Abuubakr alikuwa anamvuta mkono bintiye kuondoka kituoni.

KAZI YA MZUNGU 10
(Zamani za ujana wa wazazie Masu)

Kwa kawaida Mnada wa bidhaa mbalimbali ulifanyika kijijini Malonje siku ya jumamosi. Janice alikuwa mrembo, lakini hakuruhusu ulimbwende huo umfanye tegemezi. Alikuwa mchakarikaji Kweli Kweli. Mjasiriamali. Mwanamke mchakarikaji. Ijumaa hii Ilikuwa Ni miongoni mwa ijumaa kadha zilizompeka mjini Morogoro kujichagulia mabelo ya nguo za watoto na wanaume, kwa ajili ya kuyapeleka mnadani huko Malonje. Soko lilikuwa zuri, hasa miezi ya tano, sita, Saba Hadi nane. Ni kipindi ambacho wanakijiji wachapakazi wa Malonje walikuwa wanavuna mazao yao. Pesa zilikuwepo za kutosha mifukoni mwao, hata wakawepo waliowehuka kwa wingi wake, kiasi kwamba ungekaa kizembe, Basi wangeweza hata kukuzaba makofi, na kwa kiburi, wangekuzaba Tena halafu uulizwe Unataka kulipwa sh'ngapi!

Janice, kwa wastani kipindi Cha miezi hiyo aliuza Sana, Tena kwa Bei iliyomrudishia mtaji, na faida Mara mbili au tatu, ukitoa fedha ya nauli, chakula na malazi. Alikuwa na uhakika wa kuuza zaidi pia kwa sababu, ukiachana na lugha yake ya mvuto kwa wateja, yeye mwenyewe alikuwa na mvuto hasa kwa wanaume. Hao walikuwa wateja wake wakubwa. Wengi waliamini kwa kuwa wateja waaminifu kwa Janice kungewapa ngekewa ya kukubalika kirahisi siku za usoni. Wakaendelea kuishi kwa Imani, huku Janice akitengeneza faida maradufu.

Janice hakuwahi kumkatalia mwanaume yeyote kijijini pale aliyejitokeza kumtongoza, ila vigezo alivyowapa hao watongozaji, ndivyo vilivyowakwamisha kumpata. Na Mara nyingi Janice alijua kuwafanya hao kuwa waaminifu kwenye uteja wao wakitarajia siku moja watafikia vigezo vyake. Kwa njia hiyo, Janice hakuwa na adui, Bali alijitengenezea marafiki wengi miongoni mwao hao wanaume. Lakini pia, kwa wale majasiri waliopendelea kuonesha umwamba wao, wengi walitoka kimaisha baada ya kuingia kwenye ligi ya kumuwania Janice.

'Ah Janice, mtoto mzuri. Nakuahidi vigezo vyako nitavifika tu, siwezi kukukosa asilani. Nambie, u Hali gani mrembo?' Ilikuwa sauti ya Masuke wa Miganda.
'Niko poa Masuke, Leo nimekuletea bidhaa adimu Sana. Mahsusi kwa ajili yako. Tena usimwambie mtu. Hebu shika hii kwanza, halafu nambie waionaje? Hayo ndo mapigo ya vijana sasa.' Janice alizungumza huku akimkabidhi suruali ya jinsi la bluu. Ilikuwa nzuri, na Masuke alivutiwa nalo Sana.
'Janice unajua kunishika pabaya we mtoto, utaja nifilisi ujue, wakati ndio kwanza nachipukia kwenye utajiri wangu. Hii unaitoaje?'
'Elfu kumi TU, Na hapo Ni kwa sababu wewe Ni mshikaji wangu. Kawaida naziuza hizi kwa shilingi ishirini na tano.' Janice aliongea kwa sauti ya chini akimnong'oneza Masuke wengine wasisikie.
Masuke alizama mfukoni mwa suruali yake na kuibuka na shilingi elfu tano. Akamshikisha kwa kificho na kumnong'oneza Janice.
'Sina ziada na suruali hii Ni mahsusi kwa ajili yangu, naanzaje kuiacha Sasa?. Asante kwa hii zawadi!'
Janice alikuwa mjanja, lakini alikiri Masuke alikuwa mjanja zaidi yake.

Kwa miaka miwili, Masuke na Janice walionana mnadani kila ulipokuwapo Mnada kijijini pale. Wakati huo Janice alikuwa anatokea mjini Morogoro ingawa alikuwa mwenyeji wa kijiji jirani na Malonje. Mazoea yakawafanya marafiki walioshibana. Utani wa Masuke, ulikuwa kitu kingine kilichomfanya Janice kuvutiwa naye. Hata ilitokea kwamba Masuke alitoweka ghafla kijijini. Hakuna aliyejua alipopotelea kijana huyo. Janice akahisi Kuna kitu hakikuwa sawa. Alijihisi upeke na upweke! Alimkosa na kumkosa huko kukalinyausha tabasamu lake. Akawa hutabasamu tu kimazoea, lisiwe Ni tabasamu halisi lililompa furaha ya Kweli. Alimpenda kijana huyo!

Miezi kadhaa mbele, karibia mwaka baada ya kutoweka kijijini, Masuke alirejea kijijini. Akakutana na kisanga. Uamuzi ulifanyika Kwao. Familia yake haikujua Kijana wao alipopotelea, na kwa tamaduni za wanamalonje, mtoto wa kiume, sharti kuwa na familia. Awe kazaliwa mlemavu, awe na mtindio wa ubongo, haikujalisha. Mwanamke aliozwa kwenye familia ya kijana huyo, ili tu, kuendeleza kizazi kwa jina la ndugu yao ambaye angekuwa na mojawapo ya sababu hizo. Uchizi, ulemavu, kifo kabla ya kuoa, kupotea iwe vitani au kupotelea mbali na jamii hiyo. Jina la mtu huyo lingeenziwa tu. Ndugu wa mhusika, walihusika kuzaa na mwanamke aliyeozwa ndugu yao, majina ya watoto wangeitwa kwa jina la ndugu yao huyo alokumbwa na hayo madhila tajwa.

Aliporejea akakutana na habari za mke. Alikuwa na mke. Wakamkabidhi. Akampokea. Maisha yakaendelea. Lakini, yeye alikuwa bado hajaridhika Hadi atimize ahadi yake. Ahadi ya kumpata Janice.

Jumamosi iliyofuata, Masuke akaenda mnadani. Akamuona Janice akiwa kwenye jukwaa lake la kunadi mavazi. Akafurahi kumuona. Akiwa mbali, furaha ya kumuona ikimkereketa moyoni, akashindwa kuizuia furaha hiyo. Akaita kwa sauti kubwa jina la Janice. Janice alipomuona Masuke wa Miganda, furaha ikamwingia. Akaweka nguo chini, akatoka mbio kumlaki Masuke. Wakakumbatiana kwa furaha kila mmoja akionesha alivyokuwa amem-miss mwenzie.

'Nimekidhi vigezo, nimekamilisha ahadi. Je Janice, binti wa mzee Petero, utakubali nikuoe?' Masuke wa Miganda akahoji, walikuwa wameingia kwenye banda la Janice, alimohifadhi bidhaa zake. Mabelo ya mitumba. Juu ya Belo moja akaweka kijifuko Kidogo, kilichoshonwa Kama hirizi, ndani kilikuwa na madini aina ya almasi. Punje moja yenye ujazo wa karati mbili ushei hivi. Kumbukumbu ikapita kichwani mwake Janice. Akakumbuka vigezo alivyompa Masuke wa Miganda,
'Kunioa Mimi gharama Sana Masuke, ukiweza vigezo, hata Sasa, leo hii unanioa Mimi binti wa Petero.' ndivyo alivyoanza kumbabaisha.

'Vigezo gani mpenzi?' Masuke akauliza kwa upole.

'Nilitee Almas yenye ujazo wa karats 1 angalau.'

'Mh, Kama hunipendi ungesema, kwa Nini unipe mtihani unaojua nitafeli?'

'Kama wanipenda hutafeli.' Janice aliongea kwa msisitizo, akamwangalia kwa namna iliyoonesha kumsuta kijana wa watu.

'Kwa uwezo wa mola mtukufu, nitaileta almasi. Utakuwa wangu.' mazungumzo hayo yakapita kwa Kasi akilini mwake Janice alipoyakumbuka.

Masuke wa Miganda hakujua tu. Janice Petero, alikwishampa nafasi hata kabla ya hizo almasi. Kilichodhihiri wazi, Ni Kweli kwamba kuja kwa almasi kulimfanya awe mwanaume kamili kwa Janice. Hatimaye Masuke wa Miganda na Janice binti Petero, wakaoana. Hakuona shida kuwa mke wa pili!, Alimpenda Masuke.

Mwaka mmoja ukapita, Janice na Masuke hawakujaaliwa mtoto. Mke wa kwanza, tayari alikwisha jifungua mtoto wa kiume. Waliyempa jina, Miganda. Jina la marehemu babu yake Masuke.

Almasi ile, Janice aliihifadhi. Ikafika kipindi akaona heri waiuze, wabadili maisha, labda ingemsaidia Janice kuwa na maisha yenye heshima. Alitafuta heshima kwa sababu, tayari maneno maneno yalianza kuwa mengi kutoka kwa watu wa Malonje, wakihoji kwa Nini hakumzalia Masuke watoto. Wajuaji wa Mambo wakayafichua Yale waliyojifanya kuyajua, ili kujenga hoja zenye mashiko. Wakadai, huko mjini alikokuwa anafuata mitumba ya kuuza,( maana Sasa alikuwa na duka kubwa kijijini Malonje), basi kulimharibu, kwa sababu huko wanawake walikuwa sawa na wanaume. Walitumia dawa za kuzuia mimba ili washindane kibiashara na wanaume. Wakahitimisha kwa kumtuhumu Janice kuwa alikuwa kwenye kundi la wazuia mimba. Hali hiyo aliipuuza mwanzoni, lakini moyo umeumbwa kwa nyama laini, Ni mwepesi kuhisi furaha, lakini Ni mwepesi zaidi kuhisi maumivu. Alianza kuhisi maumivu, akapoteza uchangamfu. Hapo ndio alipata Wazo la kuiuza almasi aliyozawadiwa na Masuke wa Miganda.

Janice akamshirikisha Masuke Wazo lake. Masuke wa Miganda akamwambia ruksa kufanyia chochote hiyo almasi maana alimletea yeye na Ilikuwa yake. Akamkubalia kuiuza ili wafungue duka kubwa mjini Morogoro. Alitaka atoke kijijini, ajiepushe na maneno ya waja!

Alipata habari soko la almasi yake lipo jijini Dar es salaam. Akafunga safari kwenda huko. Mjini Morogoro, akapanda Basi la Abood, kiti Cha jirani yake kilikuwa wazi. Wakati gari linaondoka, mwenye kiti akatokea, hakuwa mwingine, alikuwa mmoja Kati ya wateja wake waaminifu. Thomas Mogetango. Alifahamika zaidi kwa jina la Thomas Waa. Jina la pili halikufahamika Sana.

'Waa! Cheki nayekaa naye leo?' Thomas akachombeza.
'Thomas mzee wa waa!' Janice akatamka kwa bashasha.
'Waenda wapi Janice, na wapi umemuacha mumeo?'
'Nilikuwa nikuulize swali Hilo hilo, umemwachia Nani mkeo?'
'Ah, Kuna kazi nimeitiwa na rafiki zangu. Nataka nikaicheki.' Thomas Waa Kama alivyojulikana zaidi, kutokana na kupenda kutumia mshangao wa 'waa!' alikuwa Ni fundi ujenzi. Rafiki zake walikuwa wamepata dili la kujenga Nyumba ya daktari huko Mbande jijini Dar. Hivyo, Thomas Waa alikuwa njiani kufuata ajira hiyo ya muda.
'Oh, hongera bwana, hongera Sana'
'Asante Sana Janice, tunaomba Heri tu kwa Mungu. Enhee, Kama kawaida yako, Mambo ya biashara siyo?'
'Ndiyo Toma, sema hii ndiyo Safari yangu ya kwanza kwenda jijini.'
'Oh, na Mimi nikajua wewe Ni mwenyeji!'
'Hataa, Sina uwenyeji wowote na Hilo jiji!'
'Sawa, enhe nambie, ukanipa vigezo wakati navikamilisha nikasikia umeolewa na Masuke. SI ungenambia ukweli TU jamani?' Thomas akaituoa lawama yake. Hata Sasa, Thomas alionekana bado anamhusudu Sana Janice.
'Ooh! Pole. Ulifanikisha lakini?'
'Ndio, na kusema Kweli ndio màana sikulaumu kabisa. Nilichelewa mwenyewe, lakini nashukuru bidii ya kutafuta kigezo chako ilinipa badiliko kubwa, ndio maana unaona hatua nilizopiga. Bila shaka unakubaliana nami kuwa Mimi ndiyo mjanja pekee kijijini mwenye kumiliki jengo la maana, ramani ya ulaya, paa la msauzi. Bila wewe kunipa ile changamoto, bado ningekuwa naishi kwenye kile kibanda changu Cha awali. Najivunia hatua hizo, ila bado nakosa furaha kamili. Nakukosa wewe mrembo.'
'Eboh! We mwanaume wewe, huna aibu? Mie mke wa mtu. Shemeji yako Sasa!' Janice alizungumza akiigiza ukali, lakini ikawa Ni kituko ambacho waliishia kukicheka wote. Mazungumzo yakanogea wawili hao. Walipowasili jijini, Janice na Thomas wakajikuta kwenye Nyumba moja ya kulala wageni. Roho iradhi lakini mwili Ni dhaifu. Udhaifu wao ukawazidi nguvu. Siku hiyo ikawaweka Pamoja kwa huba. Kesho yake, wakaagana huku wakiapizana kuwa hiyo ingekuwa Mara ya kwanza na ya Mwisho ili kulinda heshima ya ndoa zao.

Walipokutana Tena kijijini,Ilikuwa Ni miezi miwili tokea walipokutana kimwili jijini Dar. Janice alikuwa Ni mjamzito.

***
Ukweli kwamba Masu alikuwa kijana wa Masuke wa Miganda ulikuwa uongo ulioishi kuaminiwa kuwa Ni Kweli. Ukweli huo ukilindwa na Siri iliyobebwa kwa dhati na mioyo ya watu wawili. Janice mama mzazi wa Masu na Thomas baba mzazi wa Masu. Tangazo la Masuke wa Miganda, lilikuja Kama tetemeko lililotishia kuing'oa Siri hiyo katika msingi wake imara. Moyo. Moyo wa Janice, ulizima kwa sekunde. Ukatikiswa Kidogo ung'olewa. Asingeruhusu mtu na dada yake kuoana. Laana kubwa hiyo! Lakini pia asingeruhusu Siri hiyo kuwekwa wazi.

Aliporejelewa na fahamu zake, mama Masu aliapa moyoni kupinga mahusiano Kati ya Masu na dadake Marietta. Potelea mbali kuchukiwa na mwanae. Alipanga kutishia kuacha radhi Kama Masu angeshupaza shingo yake.

Daktari Mgode baada ya kumpima mama Masu alimwandikia dawa za kutuliza maumivu, ingawa hakukuwa na ulazima huo. Lakini, watu wa Malonje usipowapa dawa, hawakubali kuwa u daktari makini. Mgode aliwaeleza kuwa Ni mshituko wa kawaida ambao ulitokana na kusikia taarifa ambayo hakupendezewa nayo.

Wakarejea nyumbani. Ilikuwa yapata saa sita za usiku. Mbalamwezi ikiuangaza ulimwengu kwa mwanga wake akisi. Masu akawalipa wadeni wake. Dj Yusto, mwenye ng'ombe mnono. Muuza mchele, muuza nyanya na vitunguu, kila aliyeorodhesha Deni akalipwa. Jumla zikatumika laki nne na ushei. Mfukoni akabakiwa na Kiasi Kama elfu themanini hivi. Akaazimu kukikimbia Kijiji.

Kesho yake, Masu akapata muda wa faragha na mamake Janice.

'Hizi habari kwamba unamuoa binti wa mzee Thomas, Zina ukweli gani?' Janice akamhoji Masu.
'Kwa Kweli sijui hata zilianzaje, labda mzee anaweza kuwa na majibu na hili swali mama!' Janice roho ikadunda kwa tumaini jema.
'Wewe umezipokeaje?'
'Dah nilishituka Sana mama, Kama Ni sapraizi, Basi haikuwa njema hata Kidogo!'
'Kwa Nini wasema hivyo?'
'Nilidhani ingekuwa Bora kushirikishana kabla ya kuliweka mbele za kadamnasi. Huwezi jua, unawezakuta binti Ana mchumba tayari, fikiria huyo mchumbaake anamchukuliaje Sasa? Na huyo binti je? Haikuwa nzuri kwa Kweli. Na… na kusema Kweli mama, Mimi tayari Nina mchumba tayari, muda usiozidi miezi mine hivi mtaitwa babu na Bibi!'
Habari hiyo, japo kuwa haikuwa imezingatia Mila na desturi zao, ilimpa faraja mama Masu na kumrejeshea tabasamu lake halisi.
'Alulululuuu!' mama Masu akapiga vigelegele.
'Anaitwa Mwamvita, mzanzibar, wazazi wake Ni chotara wa kishrazi na kitumbatu.'
'Mie nakutakia Heri mwanangu, yote ya Mungu, kwa vile yameshakuwa hivyo, hatuwezi kubadili matokeo. Ila mwanangu, nakuasa baba, asilani asilani usijekufikiria mahusiano na Marietta. Tafadhali Sana unisikie mwanangu. Hilo tu ndilo nakuomba. Uwe Masu wangu anisikilizaye, nakutakie mema mwanangu. Nakukanya kwa Heri kabisa.' mama Masu akasisitiza.
'Nimekusikia mama.'
'Asante mwanangu, nakuamini. Nachukua kauli yako Kama Kiapo!'
'Ninakuahidi, nitakaa mbali naye. Pia nitumie muda huu kukujulisha kuwa Kesho nitakuwa safarini kurejea Zanzibar. Nahitajika kibaruani keshokutwa.'

Masu hakutaka kubishana au kujua kiundani, kwa Nini alikuwa anakatazwa mahusiano na Marietta. Hata hivyo, kwa kazi yake, asingemudu kuwa na wake wawili. Huyo mmoja tu alilazimika kufanya Siri uwepo wake. Kumbukumbu ya maelekezo ya master Park Hye Ilikuwa Moto bado akilini mwake.

'Oh jamani, na Mimi nikidhani tunao muda mwingi wa kuwa nawe?' mama Masu akalalama.
'Ningependa iwe hivyo, lakini kazi, kazi zenyewe za wazungu, hawapendi kupoteza muda kabisa.'
'Ah, sawa mwanangu, nashukuru kwa zawadi na kutukumbuka mwanangu. Ubarikwe Sana mwanangu. Iwe Heri unapoenda kuanza kazi yako. Ukafanikiwe mwanangu.'
'Asante Sana mama. Nanyi pia mbarikiwe. Lakini, ninalo ombi pia. Kwa Hali aliyonayo mkwe wenu, anahitaji usaidizi kwa karibu Sana. Nilitaka nimuibe Maureen akamsaidie kipindi hiki Cha kuelekea kujifingua.'
'Hapana, mlete nyumbani hapa, mamako mkubwa Ni mkunga, akiwa hapa atakuwa Salama. Mie Sina Imani na Mambo ya mjini. Siku hizi kila mzazi anayejifungulia hospitalini utasikia operesheni. Mbona huku Wala si lazima hizo operesheni? We mlete tu nyumbani. Maureen nenda naye ili arudi naye. Na lini Sasa sisi tutakutana na wazazi wake?.!'
'Ngoja kwanza ajifungue, halafu tutapanga tu.'
'Vipi lakini, wazazi wake wako radhi na uhusiano wenu?'
'Hilo ndilo suala gumu Kidogo. Hawanijui bado na hivyo sijui Kama wataridhia au la! Nisingeweza kujitambulisha, ningekamatwa kwa sababu alikuwa mwanafunzi bado, kidato Cha nne. Ila alifanikiwa kufanya mtihani bila kushitukiwa.'
'Mhh!' mama Masu akaguna huku akionekana kutafakari kwa kina.

2020
David Ngocho Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 11

MTUNZI: DAVID NGOCHO SAMSON

#TULIPOISHIA
'Vipi lakini, wazazi wake wako radhi na uhusiano wenu?'
'Hilo ndilo suala gumu Kidogo. Hawanijui bado na hivyo sijui Kama wataridhia au la! Nisingeweza kujitambulisha, ningekamatwa kwa sababu alikuwa mwanafunzi bado, kidato Cha nne. Ila.. alifanikiwa kufanya mtihani bila kushitukiwa.'
'Mhh!' mama Masu akaguna huku akionekana kutafakari kwa kina.

KAZI YA MZUNGU 11

Simu ya Masu iliita wakati tu alipomaliza mazungumzo na mama yake. Ilikuwa namba ngeni. Akaipokea na kutega simu sikioni.
'Hallow' akazungumza.
'Masu jamani, wamemweka ndani Bakari. Wanadhani yeye Ni wewe!' sauti ya Mwamvita ilijaa kitetemeshi.
'Taratibu Basi mpenzi, nieleze taratibu Malkia, Bakari kazua Nini Tena huko jamani. Na Mimi nikidhani muda huu utakuwa Dar?'
'Nilikuwa natoroka asubuhi na Bakari alinibebea bag la nguo kwenye mkokoteni. Sikutaka nionekane nasafiri, ili kupoteza nyayo. Sijui baba alijuaje, alikuja na polisi wakamkamata Bakari wakimdhania ndio mhusika wa mimba yangu na alijaribu kunitorosha. Hivi navyoongea, Yupo kituo Cha polisi ….. nimekwama mpenzi.' habari hiyo haikuwa njema. Ilivuruga mipango kabisa, na mbaya zaidi ilimweka Masu kwenye hatari ya jela. Adhabu ya kutia mimba mwanafunzi Ilikuwa sawa na adhabu ya ubakaji. Alihitaji kutuliza akili yake ili kujua Nini angefanya kujinasua. Lakini, Hilo halikuwa changamoto pekee, msela wake Bakari alikuwa ndani akisotea starehe yake aliyofanya kipindi hicho, akiwa Hana hatia! Alitakiwa kumtoa ndani kwa namna yoyote ile.

'Ok, nisikilize Malkia. Wewe Tulia, na jaribu kuangalia Nani anakuchunga na kufuatilia nyendo zako. Kwa Sasa, ninalazimika kuamini kwamba Kuna mtu kawekwa na baba mkwe ili kuchunguza nyendo zako. Hivyo ndivyo walivyofanikisha kumkamata Bakari. Hii namba Ni ya Nani?'
'Ni ya rafiki yangu Radhia.'
'Namba yako vipi?'
'Baba kaninyang'anya!'
'Anhaa, Unadhani Radhia anaweza kutunza Siri akitakiwa kufanya hivyo?'
'Kwa Kweli Sina hakika, Ni mtu wa maneno mengi!'
'Basi usimjulishe Kama unawasiliana na Mimi. Tumia namna nyingine kuwasiliana nami.'
'Kwa Sasa anajua mpenzi. Nilimweleza nataka kuwasiliana nawe!'
'Anhaa! Ok, mwambie asimweleze mtu kuwa tumewasiliana. Mimi nitaingia huko muda wowote, na tutayamaliza Haya. Mpango wetu tutaukamilisha Kama tulivyopanga. Kama kabla sijakufikia watakuwa wanajaribu kulazimisha ndoa na Babu Kisiki, jitahidi ukaripoti kwa sheha au jaribu hata kutoroka lakini usikubali wakuozeshe tafadhali. Nakuja kukuchukua Malkia'
'Asante mpenzi, nakutegemea! naa.. Masu!'
'Naam Malkia'
'I love you so much!'
'I love you as much!

***
Alitaka alale, lakini kwa habari hiyo, usiku usingelalika. Hakuwa tayari kupoteza hata sekunde, wakati mpenzi wake Mwamvita, alikuwa kwenye hatari ya kuozeshwa. Asingeruhusu Hilo litokee kwa maana, Kama lingetokea, jamii isingemwelewa Kama angefanya juhudi za kumchukua kutoka kwa babu Kisiki. Jamii ingemhukumu kwa kosa baya kabisa la kuchukua mke wa mtu. Kosa ambalo jamii isingesita kumhukumu bila kupepesa macho.

Masu akawaeleza wazazi kuwa angeondoka usiku huo. Kwa Nini? Waliuliza. Kulikuwa na dharura kazini. Akadanganya.

Alisota barabarani kusubiri gari ambalo lingekuwa linaenda mjini Morogoro. Masaa mawili alikuwa Kakaa kwenye upenu wa duka la nguo la mama yake. Pamoja naye, alikuwepo Kaka yake Miganda na vijana wengine kadhaa Rika lao wakisogoa, wakati akisubiri gari, na ndugu zake hao wakipoteza muda, siku ipite. Ajira Ilikuwa changamoto. Hicho ndio kitu kilichomchosha akaamua kwenda Dar Mara ya kwanza. Hakuona maana ya kuamka, ukae upenuni ukipiga soga, ulitazame jua likichomoza na ulishuhudie likizama ukiwa hujaingiza shilingi. Na shida ya kijijini, ukishalima, huna Cha kufanya Bali kusubiri muda wa palizi, kuweka mbolea unasubiri Tena muda wa kuvuna. Muda mwingi unamkuta kijana Hana kazi. Matokeo yake wengi walitokea kuwa walevi wa pombe, wakinywa mataputapu. Kama hiyo haikutosha walikuwa na muda mwingi wa kujaribu aina nyingine za ulevi, bangi, mirungi, ugoro na gongo. Hayo yote kwa Masu hayakuwa na maana. Hakutaka hata kujaribu. Alikwisha ona madhara yake, kwa Nini ajaribu sumu kwa kuonja? Vijana walizeeka kuliko baba zao, hawakuwa na nguvu za kuanzisha familia. Wizi mdogo mdogo ulishamiri. Wanakijiji hawakuhofia mwewe au vicheche dhidi ya kuku wao, waliwahofia vijana wao walevi. Wezi wa kuku.

Lorry la mageyo trans lilifika baada ya masaa mawili. Masu hakujali hadhi yake safari hii, alidandia gari Hilo na safari ya mjini ikaanza. Waliingia mjini Morogoro usiku wa saa tatu. Masu alitafuta Nyumba ya kulala wageni kupata' huduma ya bafu, alipokwisha kuoga, akaingia stendi, akabahatika kupata gari la mtu binafsi safari ya jijini ikaanza. Hakujali m-banano uliokuwemo ndani ya gari Hilo dogo aina ya probox, Wala hakuwa na namna ya kuikwepa harufu nzito, mbaya, iliyotokea kwenye moja ya vinywa vya wasafiri wenzie, isipokuwa kumlazimisha mtu huyo kunyamaza, maana Jamaa alijua kila soga za jijini, siasa, uchumi, mastaa wakubwa duniani na nchini. Ajabu hakujishitukia kwamba hakuna aliyempa makini yake, na kuwa kila mtu alionekana kukwepesha sura yake mbali naye.
'Oya broo, hebu tupumzishe Kidogo. Hili gari Ni dogo mno kwa kila mtu kuzungumza wakati kila mtu anajua alichokula jioni hii. Wengine tumetoka mbali, tunahitaji utulivu wa kutosha kupumzisha akili na miili yetu.' Masu alimfikishia ujumbe.
'Unataka kusemaje….' yule bwana alitaka kuanzisha zogo. Lakini hakufanikiwa,abiria wote waliunga mkono hoja ya Masu. Jamaa akatulia Kama kanyeshewa mvua ya mawe!

Waliingia jijini Mwendo wa saa Saba usiku. Masu akaelekea feri. Akatafuta boti za kukodi, akapata moja na safari ya Zanzibar ikawiva.

***
'Oyi M'bara!' Yusuf alipokea simu ya Masu. Alikuwa Yupo kwenye club moja ya usiku, akiwa kawekwa Kati na watoto wa kike, mmoja wa kiitaliano na mmoja wa kibongo. Walikuwa wanatumia vilevi vya gharama, maana Yusuf hakuwa mchoyo kwa jinsia ke, hasa akiwa na pesa.

'Nahitaji kampani yako kwenye misheni fulani muhimu. Uko wapi kwanza.?' Masu aliuliza.

'Nilipo Mimi we M'bara huwezi kutia miguu. Swali ni, lazima nihusike na hiyo misheni yako?' Yusuf aliongea kwa kigugumizi chake kilichokolezwa na kilevi Basi ikawa Kama burudani kwa wale warembo wake.

'Ni muhimu sana.' Masu akajibu.
'Swali kwako Sasa, uko wapi wewe, ndiyo la kujibiwa na siyo nilipo Mimi?' Yusuf alitamka kwa mbwembwe akilenga kuwakoga warembo wake aonekane Ni mtu mwenye maamuzi.

'Njoo forodhani!'
'Nakuja, jas giv mi e miniti!' Yusuf akachomekea kiingereza chake. Ingawa walikula kozi ya lugha zile mbili muhimu, Yusuf alikuwa na kauzito Kiasi kwenye kushika. Lakini haikuwa sawa na bure, alijua Cha kuweza kusikia na kusikika kwa kiwango kikubwa tu.

Walipokutana, Masu alimweleza msala uliokuwa mbele yao. Akamtaka Yusuf ampe Wazo Nini Cha kufanya. Labda kwa sababu ya ulevi, Yusuf akapendekeza wavamie kituo Cha polisi wakamuokoe rafiki yao, halafu wakodi boti imkimbize Mwamvita mafichoni, Dar.

'Unataka wanitoe busha Nini? Mbona mpango wako Ni Kama nguvu za Giza?. Hivi wewe unajua Hilo Ni kosa kubwa Kiasi gani? Uvamie kituo Cha polisi? SI sawa na ugaidi huo? Halafu kuwa siriazi Mara moja moja Yusuf.!' Masu akawaka. Kwa Yusuf, alikuwa na hamu kubwa ya kuweka mafunzo aliyopata kwa master Hye kwenye uwanja mapambano.

'Haya Sasa wewe sema Una mpango upi, haya, haraka, nakusikiliza!' Yusuf akakoroma.
'Nataka tumtie kashkash sheikh Abuubakr, iwe njia ya kumnasua mwanetu Beka, na kuondoka na Mwamvita!'

'Huna nidhamu wewe, wabara hamnaga Miko kwenye Mila zenu, nini?. Unataka kumfanya Nini baba mkwe wako?' Yusuf akuliza kwa dhihaka akitokwa na kicheko Cha nguvu.
'Una ujinga mwingi Sana Yusuf, maana hukomi kutoa pumba wewe mtu. Hebu nisikilize kwa makini. Tunahitaji cash, kitu kama em moja hivi. Tukishaipata hiyo, tutaenda nayo kwa sheikh Abuubakr. Tunamwekea hizo fedha zote mezani. Tunampa ilani. 'Kesho mzee, tunatarajia kusikia Beka ametoka ndani. Hiyo hapo milioni moja. Ifikapo saa kumi jioni, tunataka tusikie Bakari ameachiwa huru. Kwa Nini tunataka aachiwe? Kwa sababu, siye muhusika wa mimba ya binti yako.' unaliona vipi Hilo Wazo Yusuf?' Masu akamsaili rafiki yake Yusuf.
'Naona ukosefu mkubwa wa nidhamu kwa baba mkwe wako. Huwezi kumfanyia hivyo. Hata hivyo, Nakubaliana na mpango wako. Ila Swali la msingi Ni, tunaipata wapi hiyo million ya kumpa mkweo, M'bara?'
'Kuna yule mjinga mmoja amekuwa anatapeli fedha wafanyakazi wa serikali. Anajifanya anawakopesha halafu anachukua kadi zao za kutolea hela. Unampata?'
'Wapo wengi siku hizi.'
'Yeah, ila Kuna mmoja aliyesababishia kifo cha mzee Konokwe, alimpiga nusu ya mafao yake, mzee akapata stroke kwa mshituko, maana wanasema mzee yule alikuwa na mpango wa kufungua kampuni ya usafirishaji abiria akistaafu. Kumbe Jamaa walikuwa washatega, zilipotoka TU, wakatoka pasu kwa pasu. Mzee hakuamini, wakamkuta anatoka udenda'
'What? Hivyo ndivyo ilivyokuwa?'
'Eee!'
'Unajua hii mifumo ya kulipa pensheni wazee Ni shida kwa Kweli. Mtu keshasota miaka yote ya ujana na Hadi uzee wake akitegemea mshahara kiduchu, wakati Hana uwezo wa kusimamia mipango mipya anakutana na fedha ambazo hakuwahi kushika, lazima awehuke TU. Wengi hufa kwa sababu ya pesa hizo.'
'Ndiyo, kwa hiyo yule mjinga anazo hela za kutufanikishia huu mchongo. Tumvamie usiku huu huu, ili Kesho tumtoe mwanetu.'
'Haina noma, ila ninapendekeza maboresho namna ya kumweka sawa sheikh Abuubakr!'
'Enhee!'
'Hakuna haja ya kumvamia na kumpa hizo fedha. Yule ndo keshakuwa baba mkwe wako, lazima uoneshe heshima kwake. Njia Bora Ni kumtumia hizo fedha zikiwa na ujumbe wetu. Ujumbe wetu ndio unapaswa kuwa na ultimatum. Nina uhakika haitafika saa sita za mchana, tutapata habari mwana keshatoka.'
'Ah kudadeki wallah! Skuli Ni skuli tu. Leo hii siamini kabisa Yusuf wewe unaweza kuwa na mipango makini namna hii. Bonge la idea mtu wangu. Tusilaze damu Sasa. Mida ya wanga hii, tuingie kazini kabla hakujakucha!'
'Unayo idea yoyote ya ramani ya kuingilia nyumbani kwa huyo mjinga? Kama Ana walinzi? Au anamiliki Cha Moto? Wanaishi watu wangapi hapo nyumbani kwake?'
'Hayo ndio Mambo ya msingi Sasa. Nimekuwa naliwazia suala Hilo safari yangu yote. Kuna njia ya kurahisisha misheni yetu.'

2020
David Samson Ngocho

Usikose episode ijayo
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 12
David Samson Ngocho

#Tulipoishia
'Ah kudadeki wallah! Skuli Ni skuli tu. Leo hii siamini kabisa Yusuf wewe unaweza kuwa na mipango makini namna hii. Bonge la idea mtu wangu. Tusilaze damu Sasa. Mida ya wanga hii, tuingie kazini kabla hakujakuchwa!'
'Unayo idea yoyote ya ramani ya kuingilia nyumbani kwa huyo mjinga? Kama Ana walinzi? Au anamiliki Cha Moto? Wanaishi watu wangapi hapo nyumbani kwake?'
'Hayo ndio Mambo ya msingi Sasa. Nimekuwa naliwazia suala Hilo safari yangu yote. Kuna njia ya kurahisisha misheni yetu.'

KAZI YA MZUNGU 12

'Nipo makini bro, nakusikiliza,leta hizo Intel (taarifa)!'
'Iko hivi, Jamaa Ana walinzi wawili wenye mafunzo ya Mgambo. Bastola atakuwa nayo, lakini si kisheria. SI unajua hio biashara yake sio halali kwa sababu Hana vibali ingawa nimeskia Yupo kwenye ufuatiliaji wa kuhalalisha. Nyumbani Yuko na mke na watoto wa kike watatu, mmoja akiwa Yaya. Jengo lake Ni la kisasa, ameweka CCTV camera kila Kona, hivyo tunahitaji kwenda kininja. Tutaficha sura zetu, na tukishamaliza misheni tunaondoka na footage za CCTV. Nimekadiria kwamba, misheni yetu itatuchukua dakika kumi na tano Hadi ishirini hivi kukamilika.'

'Walinzi tutadili nao vipi?'
'Swali la msingi. Kwanza, hatuna mpango wa kuchukua uhai wa mtu. Kwa hiyo, tutawazimisha TU kwa muda wakati tukifanya shughuli yetu. Tukishaingia ndani tunawalaza usingizi wa nusu kaputi familia nzima isipokuwa huyo mjinga. Huyo mjinga akishatupatia fedha na yeye tunamzimisha kwa pigo tunasepa zetu baada ya kuondoka na footage.'
'Sawa. Ila huyo tapeli kwa Nini tusimvunje wallau kidole?' Yusuf akahoji akiweka sura ya kauzu.
'Hahaha, Kama unaona Hilo litakupa faraja, we mvunje tu, yeye keshavunja wangapi? Vunja mbaba!'

Baada ya kukubaliana na kuweka mipango yao sawa, Masu na Yusuf walitinga mavazi kwa ajili ya kazi. Damu zao zilichemka kwa hamu ya kufanya aksheni. Hawakuwa na bunduki, na waliamini wangeweza kutumia za wenyeji wao Kama ingelazimu.

Nyumba aliyoishi Nzinyangwa, mkopeshaji maarufu wa fedha za riba kubwa, kinyume Cha sheria, Ilikuwa imezungushiwa ukuta mrefu wenye nyaya za umeme juu yake. Namna pekee ya kuingia ilikuwa kwa kupitia getini. Ukiwa usiku wa saa Tisa, walihitaji kutumia akili Sana kuzama ndani ya jengo Hilo lenye ulinzi mkali.
Ndio maana Walivaa magwanda ya polisi.

Kwa muda, Masu alikuwa keshafanya upelelezi wake na kugundua Nzinyangwa alivyoshirikisha baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi kwenye utapeli wake, akiwatumia kuwaweka ndani wadeni wake walioshindwa kulipa riba zake, ili kishinikiza familia zao kuchangishana kulipa hizo fedha. Utaratibu wao wa kufuata malipo yao kwa nzinyangwa wakiwa doria usiku aliufahamu pia.

Walipofika getini, walibonyeza switch ya kengele. Mlinzi aliyekuwepo Zamu getini akachungulia kwenye dirisha dogo la kioo. Akaona sura ya afande. Afande Masu akaonesha kitambulisho chake fasta na kukirejesha mfukoni haraka.
'Tunahitaji kuonana na Nzinyangwa. Fungua geti.' akatamka kwa sauti iliyojaa mamlaka. Kuna namna Askari wanaamrisha heshima kwa Walinzi. Nadhani kwa vile Walinzi wengi wana ndoto za kuwa maaskari wakikuwa wakubwa!

Haikuwa Mara ya kwanza kwa mlinzi kupata' ugeni aina hiyo. Kwa kazi ya bosi wake, hii ilitokea Mara kwa Mara, na kawaida polisi hai walishikishwa fungu la fedha wakasepa zao. Leo, mlinzi hakuwa na taarifa ya ujio wao na hakuachiwa fungu kuwapa wanapokuja. Akalazimika kufungua geti. Hilo likawa kosa kubwa kwa upande wa mlinzi.

Jamaa walivyoingia tu! Mlinzi akajikuta anapaa juu. Alipotua chini, tayari alikuwa nusu kaputi. Master Park Hye angetabasamu Kama angeona jinsi vijana wake walivyokuwa wameiva!
Kishindo alichotua nacho mlinzi huyo kikamwamsha mwenzake aliyekuwa amejilaza kwenye mkeka kwenye kile chumba Cha Walinzi. Akakurupuka kwa wenge, akamuona Masu akinyata kuelekea kwenye mlango wa jumba la Nzinyangwa. Akatoka kwa kunyata vile vile. Alipokaa kwenye nafasi ya kumudu shambulizi, akarusha rungu lake kwa mkono wake wa kushoto, isingekuwa ile hisia ya sita aliyofunzwa na master Park Hye, Masu angekuwa marehemu. Alichezwa machale akaikwepa Kidogo, akasikia mvumo wake ukipita sikioni mwake kwa Kasi. Mlinzi yule Sasa alikuwa anamfuata kwa Kasi ya ajabu.

Huyo, akairusha ngumi yake iliyokuwa na ujazo wa kilo kadhaa, lakini Masu aliiona, akaidaka ngumi ile na kumvuta mlinzi upande wake, mlinzi akavutika na kukosa balansi, hapo hapo Masu akanyanyua guu lake la kushoto na kumchota mlinzi tumboni, mlinzi akapaa juu, aliporudi chini, Masu akampa bapa la kono lake maeneo fulani nyuma ya sikio, mlinzi akalala usingizi.

Mlinzi wa tatu alikuwa amelala fofofo kwenye godoro kwenye Nyumba ya walinzi, hata hivyo walibaini baadaye kuwa huyu hakuwa mlinzi Bali raia TU asiye na ujuzi wowote wa ulinzi. Labda ndugu wa mmoja wa Walinzi, ambaye waliamua kumpa hifadhi hapo ofisini Kwao. Yusuf alimnyatia raia yule, akampa pigo la kininja akaendelea kulala unono.

Walinzi walikuwa na funguo nyingi Sana. Masu na Yusuf wakahisi Kuna funguo ya kuingilia ndani ya jengo la Nzinyangwa. Wakazijaribisha haukuwepo wa kufungua mlango wa mbele. Wakati Yusuf anaendelea na Hilo zoezi, Masu alikumbuka kwamba SI Kawaida wabongo kutumia mlango huo. Hata Kuna baadhi ya familia funguo wa mlango wa mbele haujulikani ulipo kabisa kwa jinsi usivyotumika, aliamua kuzunguka kwa nyuma. Mlango wa nyuma kuingilia jikoni ulikuwa umerudishiwa TU. Akafanya kuusukuma kwa tahadhari. Hapo jikoni akamuona binti wa kazi, alikuwa kalala chini kwenye mkeka, kajifunika kanga. Mbu wakimgeuza pipa la pombe, walikuwa wanamnyonya damu binti wa watu maana hakuwa na chandarua Cha kumlinda dhidi ya wadudu hao hatari wanaoongoza kwa kuua watu kusini mwa jangwa la Sahara.

Masu akabonyezabonyeza saa yake ya mkononi, smart watch na kuandika maandishi 'back door'. Yusuf akahisi mtetemo wa saa yake mkononi akaitazama na kusoma maneno Yale. Back door. Akazunguka kule.

Masu alimfuata yule binti pale chini, akamfunika mdomo huku akimwamsha.
'Kimya!' akanong'ona. Dada wa kazi mkojo ukamtoka. Alikuwa anatetemeka vibaya Sana. 'Chumba Cha bosi Ni kipi?'
Binti akaonesha kwa kidole Cha shahada.
'Sina shida na wewe lakini ukileta ujuaji, nakulipua. Kaa kimya.' Masu akamtishia binti wakati akimfunga kwa kanga yake mwenyewe mikononi kwa nyuma pamoja na miguu, akamtia tambara mdomoni. Akafungua mlango walimolala watoto wa Nzinyangwa, akapuliza dawa ya usingizi na kufunga.

Wakati akienda kwa Mwendo wa kunyata, ili aingie chumba Cha Nzinyangwa, akashuhudia mlango ukivutwa kwa Kasi ya ajabu Sana. Hakutarajia hili.
'Chwaa!' Masu akachezea mjeledi, akawewesuka na kupiga magoti chini. Alipojaribu kujinyanyua, akakumbana na mdomo wa bastola. Nzinyangwa alikuwa na mwili mkubwa. Jitu. Ligoliati kabisa. Jamaa huyo, alipomuona Masu Ni mtu mwenye mwili mdogo, akajua atamuweza. Akamdharau. Akamshushia mjeledi wa pili mgongoni. Masu maumivu yakaupenya mwili wake. Akayumba kushoto. Mjeledi wa tatu ulikuwa unamfuata, akaruka Kama ngedere kwa namna ambayo Nzinyangwa hakutarajia, akawa ameikamata koromeo yake mkono mmoja na mkono mwingine ukadaka bastola. Nzinyangwa akawa anapigania pumzi yake. Masu akamtandika na kitako Cha bastola na kumsukumia ukutani, haraka Sana akamtegua miguu, Nzinyangwa akanguka chini Kama zigo.

Masu akasikia sauti toka chumbani, mkewe Nzinyangwa alikuwa anaongea kwenye simu. Akamwacha Nzinyangwa aliyekuwa anagugumia kwa maumivu, akazama chumbani alipokuwa mkewe Nzinyangwa, Akamrukia mwanamke huyo na kuidaka simu, akaiweka sikioni.

'Sijakuelewa unasemaa..!' mtu wa upande wa pili wa simu alikuwa anahoji. Ilikuwa sauti ya kike.
Masu akampa simu yule mwanamke ikiwa loudspeaker, 'malizia mazungumzo yako' akimwashiria kwa vitendo huku akimwonyesha bastola. Alijua inamaanisha Nini.
'Nimesema ile hela ya vikoba Ni Kesho!' mwanamke akatamka. Masu akatikisa kichwa kukubaliana na akili aliyotumia mwanamke huyo kupoteza lengo la awali la kupiga simu ile.

'Jamani, ndiyo unanipigia usiku huu mama Shani? Sisi ni majirani umeshindwa kungoja kukuche unambie?'
'Ee nawe, saa Tisa mwanamke bado umelala. Haya Basi endelea kulala!' akakata simu.

Yusuf alipoingia mlango wa uani, alikuta binti wa kazi kalazwa chini, akapita kwenye korido na mbele akamuona mtu akigalagala, akamsogelea kwa tahadhari. Alikuwa mtu wao. Akajua Masu keshamaliza kazi. Alijidanganya, Kumbe Nzinyangwa alikuwa kazuga TU, alinyanyuka haraka Sana, akamtwika Yusuf konde moja hatari, Yusuf akayumba na kugonga ukuta. Akapasuka Kidogo, damu zikavuja Kidogo. Hali hiyo ikamtia hasira Yusuf.

Nzinyangwa alikuwa anamfuata kwa pigo lingine, Yusuf akawa amemuona, kwa wepesi akageuka na kutupa teke lililompata Vema adui yangu kwenye mvungu wa kiuno chake, Nzinyangwa akatoa ukelele akizikumbatia Mali zake na kuketi chini. Maumivu makali yakasambaa kutoka hapo hadi tumboni mwake. Mara, Masu akatoka chumbani akiwa amemtanguliza mkewe Nzinyangwa mbele.
'Enhee!' Yusuf akauliza, akiwa mguu mmoja kaikanyaga shingo ngumu ya Nzinyangwa.
'Ukileta ubishi, nakumaliza' Yusuf akatamka akimkazia macho Nzinyangwa.
'Hawataki kueleza zilipo fedha. Nataka tuwaue pamoja na watoto wao. Tunaanza na watoto kwanza. Watu wanna roho mbaya Sana Hawa. Umeona binti wa kazi anapolala? Na wanajiita matajiri.'
'Fedha ziko wapi?' ule mjeledi wa bwana Nzinyangwa Sasa ulikuwa mkononi mwa Masu. Aliunyanyua halafu akaushusha mgongoni kwa bwana Nzinyangwa kwa hasira za kulipiza.
Chwaa!
Nzinyangwa akatoa kelele za maumivu. Alikuwa Hana ujanja, bastola yake mwenyewe ilikuwa inatishia uhai wake.
'Mfunge mikono' Masu akamuamrisha Yusuf.
Yusuf akachomoa kamba kwenye gwanda lake. Akamfunga mikono Nzinyangwa. Masu akaushusha Tena mjeledi mgongoni kwa Nzinyangwa.
'Nawapa pesa, tafadhali msiue wanangu.' Nzinyangwa akawarai.
'Simama utuoneshe zilipo'. Yusuf alikuwa kamshika mkono binti mdogo wa Nzinyangwa.
Nzinyangwa akaongoza njia kwenda chumbani.
'Dah na unafaidi Sana we mjinga, Una mwanamke bomba Sana!' Yusuf alizungumza.
Mkewe Nzinyangwa akajua leo Ni leo alikuwa bubu ghafla akitetemeka kwa hofu.

Chumbani kwa Nzinyangwa kulikuwa kasiki. Kasiki la chuma. Akawaonesha funguo la kasiki hiyo. Masu akalifungua kasiki. Mlikuwa na fedha nyingi Sana.
'Zipo Kiasi gani jumla?!' Masu akauliza wakati huo akizipakua na kuzihifadhi kwenye mfuko waliokuja nao kwa kusudi Hilo.
'Mia mbili' Nzinyangwa akatamka.
'Milioni Mia mbili! Tunachukua Mia tunakuachia Mia.' Masu akatamka.
'Tunakomba zote, mwachie hamsini tu' Yusuf akabwata. Wakazichukua zote, na halafu wakapunguza hamsini. Walipomaliza zoezi Hilo. Wakawalaza kitandani, wakapuliza dawa ya usingizi wakatokomea zao na footage ya CCTV. Hawakuacha ushahidi. Master Park Hye aliwafunza vyema. Walikuwa wametumia dakika 25

***
Walipokwisha kuondoka nyumbani kwa Nzinyangwa, walipanda pikipiki la Yusuf waliokuwa wametumia awali Hadi alikoishi Yusuf. Alikuwa SI Yusuf yule, huyu aliishi kwenye Nyumba nzuri, Nyumba yenye kiwango, self contained. Wakahesabu zile fedha wakagawana pasu kwa pasu. Walikuwa mamilionea. Milioni sabini na tano za utajiri.

Wakakubaliana kutoa milioni tano kila mmoja kwa ajili ya kumpa kianzio msela wao. Beka. Walikuwa na uhakika anaachiwa mchana wa siku hiyo. Ilikuwa yapata saa kumi Sasa. Uchovu wa safari na aksheni iliyomtwika mijeledi miwili yenye ujazo, Masu alikuwa kachoka mbaya. Aliposema anajiegesha kwenye sofa, usingizi mzito ulimvaa akiwa ndani ya mavazi Yale ya 'misheni.'

Alipoamka usingizini, ilikuwa saa nne za asubuhi. Akamkurupua Yusuf ambaye alikuwa anakoroma kwa sauti kubwa.
'Oya! Kushakucha mzee baba, amka tukamilishe misheni.'
Yusuf akaamka akionekana kuchoka. Pombe za usiku zilimpa hangover ya hatari.
Walioga Kisha wakaweka mpango wao mbashara.
Waliamka mamilionea. Wakashukuru kukutana na Steve Curl. Huu ulikuwa mwanzo mzuri, na bado walikuwa hawajaanza kazi ya Mzungu.

***

Sheikh Abuubakr, alikuwa dukani akichezea tasbih yake! Akaingia mtoto mdogo wa miaka takribani nane. Alimfahamu mtoto huyo.
'Wa jina huyoo, wamekuagiza Nini? Tambi?' Sheikh Abuubakr alimchangamkia Abuubakr mtoto.
'Kuna dada amenipa hi bahasha nikuletee.'
'Dada? Dada gani Abuu?'
'Mi simfahamu, ndio nimemuona leo! Na keshaondoka, alikuja na gari'
'Haya, asante swahiba!'
'Haya, Mie naenda'
'Mung'unya hizo ukienda' akampatia pipi tatu.

Sheikh Abuubakr akafungua bahasha na kutoa vilivyomo,
'Astaghfirullah!' sheikh Abuubakr akatamka huku akirudi nyuma kwa kihoro. Yalikuwa manoti ya shilingi elfu kumi. Jumla milioni moja.
Ndani ya bahasha hiyo pia kulikuwa na ujumbe.

'Sheikh Abuubakr,
Pesa hiyo Ni yako. Tunakutaka amani. Kijana unayekusudia kumfunga jela SI mhusika wa mimba ya binti yako. Kwa sadaka hiyo, tunakuomba umwachie huru. Yeye hajui lolote kuhusu suala Hilo. Ni ungwana TU Kama utaona vema kumuomba msamaha kwa kumweka ndani pasipo hatia. Mwanao ndiye anamfahamu mhusika wa mimba yake, hukuona busara kumuuliza Hilo? Tunakutaka uwiwe kutenda haki. Kama kufika saa Tisa atakuwa bado hajaachiwa, utakuwa umetangaza Vita na sisi. Ukiona vema kuripoti ujumbe wetu kwa polisi, Ni uamuzi wako. Tunatumaini busara itakuongoza vema.
Wapenda haki.'

Alipomaliza kusoma ujumbe huo, sheikh Abuubakr alikuwa anatetemeka mikono. Akafanya hima, akafunga duka na kuelekea polisi. Njiani akawa anawaza kuwashirikisha polisi kuhusu fedha na ujumbe ule. Akawa yuasita Sana kufanya hivyo. Ingemsaidia Nini kuingia vitani na watu asowajua? Akaona heri kufuata Rai ya 'wapenda haki'. Hata bintiye pia alikuwa kamlaumu Sana kumweka ndani kijana yule. Lakini hasira Ilikuwa imempofusha asione Kama alikuwa anatenda kosa bila kujua.

'Naama Sheikh Abuubakr, karibu Sana sheikh.' Askari wa Zamu alimkaribisha mzee Abuubakr.
'Asante Sana afande, vipi, mwaendeleaje hapa?'
Hapa Ni heri sheikh wangu, Munyazi Mungu atutendea heri TU, tuwazima wa afya sheikh!'
'Hilo la kheri Sana. Sasa bwana Askari, Mimi nimekuja hapa kwa ajili ya ile kesi ya Jana.!'
'Naam!, Yule mbakaji tupo naye, na kusema ukweli Ni mgumu Sana huyo kijana, hata baada ya mateso mengi, amegoma kukiri Ni mhusika wa ile mimba. Mgumu Sana sheikh'
'Oh!' sheikh Abuubakr akatoa sauti, akahisi Kama Kuna maumivu yaliupenya moyo wake.
'Tumemkosea Sana kijana wa watu Afande, nimekuja kubaini tulifanya makosa. Huyo kijana Kumbe Kazi yake kubebea TU watu mizigo yao. Sasa nilivyokuta binti yangu kachukua mizigo anatoroka, nikajua huyu yuamtorosha Kumbe yeye alikuwa TU kapewa kibarua Cha kubeba Asijue aa Wala be! Tumemkosea Sana huyo kijana.'
'La! Haula! Mimi nikasema kijana mgumu Kweli kukiri makosa, Kumbe alikuwa aonesha uadilifu?. La la la! Kwa Kweli Tumemkosea Sana.'
'Naam afande, hivyo mie naomba tumwachilie huru kijana huyu.'
'Hilo la kheri sheikh wangu, SI vema kuendelea kumweka hapa shughuli zake zikiendelea kulala. Ila hapo utachangia shilingi elfu hamsini TU, kufidia usumbufu uliojitokeza kwa jeshi la polisi'
'Hamna tabu, wacha tulimalize hili.' sheikh Abuubakr akatamka akijua wazi ile Ilikuwa hongo. Lakini yeye hakuona Hilo, alijua baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi kwa hongo Ni chuma kwa sumaku, na hapa alikuwa anakimbizana na muda! Wapenda haki walimpa muda mahsusi kutekeleza Rai yao.

2020
David Ngocho Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
KAZI YA MZUNGU 10

MTUNZI: DAVID SAMSON NGOCHO

#TULIPOISHIA
Hawakujua kilichokuwa kinawapata muda mfupi ujao. Ilikuwa ghafla tu, Askari alitokeza mbele yao na kuwaweka chini ya ulinzi. Bakari na Mwamvita hawakuamini kilichotokea. Walikumbwa na fadhaiko. Hawakujua Nini Cha kufanya. Bakari alichukuliwa kupekekwa polisi Asijue kosa. Sheikh Abuubakr alikuwa mbogo, amefura kwa hasira.
'Afande, huyu anayetia mimba wanafunzi, afungwe kwa mujibu wa sheria, tutashirikiana kukamilisha ushahidi.' Sheikh Abuubakr alitamka, tamko ambalo Sasa lilimwamsha Bakari juu ya balaa lililomkumba. Hakuwa na kosa, wema wake ulikuwa unamponza. Akajaribu kutaka majibu, akamkazia macho Mwamvita, 'kulikoni?', macho yake yaliuliza, Mwamvita hakuwa na jibu.
'Nakuapia sikulijua hili Bakari.' Mwamvita akajibu huku chozi likimdondoka,wakati huo sheikh Abuubakr alikuwa anamvuta mkono bintiye kuondoka kituoni.

KAZI YA MZUNGU 10
(Zamani za ujana wa wazazie Masu)

Kwa kawaida Mnada wa bidhaa mbalimbali ulifanyika kijijini Malonje siku ya jumamosi. Janice alikuwa mrembo, lakini hakuruhusu ulimbwende huo umfanye tegemezi. Alikuwa mchakarikaji Kweli Kweli. Mjasiriamali. Mwanamke mchakarikaji. Ijumaa hii Ilikuwa Ni miongoni mwa ijumaa kadha zilizompeka mjini Morogoro kujichagulia mabelo ya nguo za watoto na wanaume, kwa ajili ya kuyapeleka mnadani huko Malonje. Soko lilikuwa zuri, hasa miezi ya tano, sita, Saba Hadi nane. Ni kipindi ambacho wanakijiji wachapakazi wa Malonje walikuwa wanavuna mazao yao. Pesa zilikuwepo za kutosha mifukoni mwao, hata wakawepo waliowehuka kwa wingi wake, kiasi kwamba ungekaa kizembe, Basi wangeweza hata kukuzaba makofi, na kwa kiburi, wangekuzaba Tena halafu uulizwe Unataka kulipwa sh'ngapi!

Janice, kwa wastani kipindi Cha miezi hiyo aliuza Sana, Tena kwa Bei iliyomrudishia mtaji, na faida Mara mbili au tatu, ukitoa fedha ya nauli, chakula na malazi. Alikuwa na uhakika wa kuuza zaidi pia kwa sababu, ukiachana na lugha yake ya mvuto kwa wateja, yeye mwenyewe alikuwa na mvuto hasa kwa wanaume. Hao walikuwa wateja wake wakubwa. Wengi waliamini kwa kuwa wateja waaminifu kwa Janice kungewapa ngekewa ya kukubalika kirahisi siku za usoni. Wakaendelea kuishi kwa Imani, huku Janice akitengeneza faida maradufu.

Janice hakuwahi kumkatalia mwanaume yeyote kijijini pale aliyejitokeza kumtongoza, ila vigezo alivyowapa hao watongozaji, ndivyo vilivyowakwamisha kumpata. Na Mara nyingi Janice alijua kuwafanya hao kuwa waaminifu kwenye uteja wao wakitarajia siku moja watafikia vigezo vyake. Kwa njia hiyo, Janice hakuwa na adui, Bali alijitengenezea marafiki wengi miongoni mwao hao wanaume. Lakini pia, kwa wale majasiri waliopendelea kuonesha umwamba wao, wengi walitoka kimaisha baada ya kuingia kwenye ligi ya kumuwania Janice.

'Ah Janice, mtoto mzuri. Nakuahidi vigezo vyako nitavifika tu, siwezi kukukosa asilani. Nambie, u Hali gani mrembo?' Ilikuwa sauti ya Masuke wa Miganda.
'Niko poa Masuke, Leo nimekuletea bidhaa adimu Sana. Mahsusi kwa ajili yako. Tena usimwambie mtu. Hebu shika hii kwanza, halafu nambie waionaje? Hayo ndo mapigo ya vijana sasa.' Janice alizungumza huku akimkabidhi suruali ya jinsi la bluu. Ilikuwa nzuri, na Masuke alivutiwa nalo Sana.
'Janice unajua kunishika pabaya we mtoto, utaja nifilisi ujue, wakati ndio kwanza nachipukia kwenye utajiri wangu. Hii unaitoaje?'
'Elfu kumi TU, Na hapo Ni kwa sababu wewe Ni mshikaji wangu. Kawaida naziuza hizi kwa shilingi ishirini na tano.' Janice aliongea kwa sauti ya chini akimnong'oneza Masuke wengine wasisikie.
Masuke alizama mfukoni mwa suruali yake na kuibuka na shilingi elfu tano. Akamshikisha kwa kificho na kumnong'oneza Janice.
'Sina ziada na suruali hii Ni mahsusi kwa ajili yangu, naanzaje kuiacha Sasa?. Asante kwa hii zawadi!'
Janice alikuwa mjanja, lakini alikiri Masuke alikuwa mjanja zaidi yake.

Kwa miaka miwili, Masuke na Janice walionana mnadani kila ulipokuwapo Mnada kijijini pale. Wakati huo Janice alikuwa anatokea mjini Morogoro ingawa alikuwa mwenyeji wa kijiji jirani na Malonje. Mazoea yakawafanya marafiki walioshibana. Utani wa Masuke, ulikuwa kitu kingine kilichomfanya Janice kuvutiwa naye. Hata ilitokea kwamba Masuke alitoweka ghafla kijijini. Hakuna aliyejua alipopotelea kijana huyo. Janice akahisi Kuna kitu hakikuwa sawa. Alijihisi upeke na upweke! Alimkosa na kumkosa huko kukalinyausha tabasamu lake. Akawa hutabasamu tu kimazoea, lisiwe Ni tabasamu halisi lililompa furaha ya Kweli. Alimpenda kijana huyo!

Miezi kadhaa mbele, karibia mwaka baada ya kutoweka kijijini, Masuke alirejea kijijini. Akakutana na kisanga. Uamuzi ulifanyika Kwao. Familia yake haikujua Kijana wao alipopotelea, na kwa tamaduni za wanamalonje, mtoto wa kiume, sharti kuwa na familia. Awe kazaliwa mlemavu, awe na mtindio wa ubongo, haikujalisha. Mwanamke aliozwa kwenye familia ya kijana huyo, ili tu, kuendeleza kizazi kwa jina la ndugu yao ambaye angekuwa na mojawapo ya sababu hizo. Uchizi, ulemavu, kifo kabla ya kuoa, kupotea iwe vitani au kupotelea mbali na jamii hiyo. Jina la mtu huyo lingeenziwa tu. Ndugu wa mhusika, walihusika kuzaa na mwanamke aliyeozwa ndugu yao, majina ya watoto wangeitwa kwa jina la ndugu yao huyo alokumbwa na hayo madhila tajwa.

Aliporejea akakutana na habari za mke. Alikuwa na mke. Wakamkabidhi. Akampokea. Maisha yakaendelea. Lakini, yeye alikuwa bado hajaridhika Hadi atimize ahadi yake. Ahadi ya kumpata Janice.

Jumamosi iliyofuata, Masuke akaenda mnadani. Akamuona Janice akiwa kwenye jukwaa lake la kunadi mavazi. Akafurahi kumuona. Akiwa mbali, furaha ya kumuona ikimkereketa moyoni, akashindwa kuizuia furaha hiyo. Akaita kwa sauti kubwa jina la Janice. Janice alipomuona Masuke wa Miganda, furaha ikamwingia. Akaweka nguo chini, akatoka mbio kumlaki Masuke. Wakakumbatiana kwa furaha kila mmoja akionesha alivyokuwa amem-miss mwenzie.

'Nimekidhi vigezo, nimekamilisha ahadi. Je Janice, binti wa mzee Petero, utakubali nikuoe?' Masuke wa Miganda akahoji, walikuwa wameingia kwenye banda la Janice, alimohifadhi bidhaa zake. Mabelo ya mitumba. Juu ya Belo moja akaweka kijifuko Kidogo, kilichoshonwa Kama hirizi, ndani kilikuwa na madini aina ya almasi. Punje moja yenye ujazo wa karati mbili ushei hivi. Kumbukumbu ikapita kichwani mwake Janice. Akakumbuka vigezo alivyompa Masuke wa Miganda,
'Kunioa Mimi gharama Sana Masuke, ukiweza vigezo, hata Sasa, leo hii unanioa Mimi binti wa Petero.' ndivyo alivyoanza kumbabaisha.

'Vigezo gani mpenzi?' Masuke akauliza kwa upole.

'Nilitee Almas yenye ujazo wa karats 1 angalau.'

'Mh, Kama hunipendi ungesema, kwa Nini unipe mtihani unaojua nitafeli?'

'Kama wanipenda hutafeli.' Janice aliongea kwa msisitizo, akamwangalia kwa namna iliyoonesha kumsuta kijana wa watu.

'Kwa uwezo wa mola mtukufu, nitaileta almasi. Utakuwa wangu.' mazungumzo hayo yakapita kwa Kasi akilini mwake Janice alipoyakumbuka.

Masuke wa Miganda hakujua tu. Janice Petero, alikwishampa nafasi hata kabla ya hizo almasi. Kilichodhihiri wazi, Ni Kweli kwamba kuja kwa almasi kulimfanya awe mwanaume kamili kwa Janice. Hatimaye Masuke wa Miganda na Janice binti Petero, wakaoana. Hakuona shida kuwa mke wa pili!, Alimpenda Masuke.

Mwaka mmoja ukapita, Janice na Masuke hawakujaaliwa mtoto. Mke wa kwanza, tayari alikwisha jifungua mtoto wa kiume. Waliyempa jina, Miganda. Jina la marehemu babu yake Masuke.

Almasi ile, Janice aliihifadhi. Ikafika kipindi akaona heri waiuze, wabadili maisha, labda ingemsaidia Janice kuwa na maisha yenye heshima. Alitafuta heshima kwa sababu, tayari maneno maneno yalianza kuwa mengi kutoka kwa watu wa Malonje, wakihoji kwa Nini hakumzalia Masuke watoto. Wajuaji wa Mambo wakayafichua Yale waliyojifanya kuyajua, ili kujenga hoja zenye mashiko. Wakadai, huko mjini alikokuwa anafuata mitumba ya kuuza,( maana Sasa alikuwa na duka kubwa kijijini Malonje), basi kulimharibu, kwa sababu huko wanawake walikuwa sawa na wanaume. Walitumia dawa za kuzuia mimba ili washindane kibiashara na wanaume. Wakahitimisha kwa kumtuhumu Janice kuwa alikuwa kwenye kundi la wazuia mimba. Hali hiyo aliipuuza mwanzoni, lakini moyo umeumbwa kwa nyama laini, Ni mwepesi kuhisi furaha, lakini Ni mwepesi zaidi kuhisi maumivu. Alianza kuhisi maumivu, akapoteza uchangamfu. Hapo ndio alipata Wazo la kuiuza almasi aliyozawadiwa na Masuke wa Miganda.

Janice akamshirikisha Masuke Wazo lake. Masuke wa Miganda akamwambia ruksa kufanyia chochote hiyo almasi maana alimletea yeye na Ilikuwa yake. Akamkubalia kuiuza ili wafungue duka kubwa mjini Morogoro. Alitaka atoke kijijini, ajiepushe na maneno ya waja!

Alipata habari soko la almasi yake lipo jijini Dar es salaam. Akafunga safari kwenda huko. Mjini Morogoro, akapanda Basi la Abood, kiti Cha jirani yake kilikuwa wazi. Wakati gari linaondoka, mwenye kiti akatokea, hakuwa mwingine, alikuwa mmoja Kati ya wateja wake waaminifu. Thomas Mogetango. Alifahamika zaidi kwa jina la Thomas Waa. Jina la pili halikufahamika Sana.

'Waa! Cheki nayekaa naye leo?' Thomas akachombeza.
'Thomas mzee wa waa!' Janice akatamka kwa bashasha.
'Waenda wapi Janice, na wapi umemuacha mumeo?'
'Nilikuwa nikuulize swali Hilo hilo, umemwachia Nani mkeo?'
'Ah, Kuna kazi nimeitiwa na rafiki zangu. Nataka nikaicheki.' Thomas Waa Kama alivyojulikana zaidi, kutokana na kupenda kutumia mshangao wa 'waa!' alikuwa Ni fundi ujenzi. Rafiki zake walikuwa wamepata dili la kujenga Nyumba ya daktari huko Mbande jijini Dar. Hivyo, Thomas Waa alikuwa njiani kufuata ajira hiyo ya muda.
'Oh, hongera bwana, hongera Sana'
'Asante Sana Janice, tunaomba Heri tu kwa Mungu. Enhee, Kama kawaida yako, Mambo ya biashara siyo?'
'Ndiyo Toma, sema hii ndiyo Safari yangu ya kwanza kwenda jijini.'
'Oh, na Mimi nikajua wewe Ni mwenyeji!'
'Hataa, Sina uwenyeji wowote na Hilo jiji!'
'Sawa, enhe nambie, ukanipa vigezo wakati navikamilisha nikasikia umeolewa na Masuke. SI ungenambia ukweli TU jamani?' Thomas akaituoa lawama yake. Hata Sasa, Thomas alionekana bado anamhusudu Sana Janice.
'Ooh! Pole. Ulifanikisha lakini?'
'Ndio, na kusema Kweli ndio màana sikulaumu kabisa. Nilichelewa mwenyewe, lakini nashukuru bidii ya kutafuta kigezo chako ilinipa badiliko kubwa, ndio maana unaona hatua nilizopiga. Bila shaka unakubaliana nami kuwa Mimi ndiyo mjanja pekee kijijini mwenye kumiliki jengo la maana, ramani ya ulaya, paa la msauzi. Bila wewe kunipa ile changamoto, bado ningekuwa naishi kwenye kile kibanda changu Cha awali. Najivunia hatua hizo, ila bado nakosa furaha kamili. Nakukosa wewe mrembo.'
'Eboh! We mwanaume wewe, huna aibu? Mie mke wa mtu. Shemeji yako Sasa!' Janice alizungumza akiigiza ukali, lakini ikawa Ni kituko ambacho waliishia kukicheka wote. Mazungumzo yakanogea wawili hao. Walipowasili jijini, Janice na Thomas wakajikuta kwenye Nyumba moja ya kulala wageni. Roho iradhi lakini mwili Ni dhaifu. Udhaifu wao ukawazidi nguvu. Siku hiyo ikawaweka Pamoja kwa huba. Kesho yake, wakaagana huku wakiapizana kuwa hiyo ingekuwa Mara ya kwanza na ya Mwisho ili kulinda heshima ya ndoa zao.

Walipokutana Tena kijijini,Ilikuwa Ni miezi miwili tokea walipokutana kimwili jijini Dar. Janice alikuwa Ni mjamzito.

***
Ukweli kwamba Masu alikuwa kijana wa Masuke wa Miganda ulikuwa uongo ulioishi kuaminiwa kuwa Ni Kweli. Ukweli huo ukilindwa na Siri iliyobebwa kwa dhati na mioyo ya watu wawili. Janice mama mzazi wa Masu na Thomas baba mzazi wa Masu. Tangazo la Masuke wa Miganda, lilikuja Kama tetemeko lililotishia kuing'oa Siri hiyo katika msingi wake imara. Moyo. Moyo wa Janice, ulizima kwa sekunde. Ukatikiswa Kidogo ung'olewa. Asingeruhusu mtu na dada yake kuoana. Laana kubwa hiyo! Lakini pia asingeruhusu Siri hiyo kuwekwa wazi.

Aliporejelewa na fahamu zake, mama Masu aliapa moyoni kupinga mahusiano Kati ya Masu na dadake Marietta. Potelea mbali kuchukiwa na mwanae. Alipanga kutishia kuacha radhi Kama Masu angeshupaza shingo yake.

Daktari Mgode baada ya kumpima mama Masu alimwandikia dawa za kutuliza maumivu, ingawa hakukuwa na ulazima huo. Lakini, watu wa Malonje usipowapa dawa, hawakubali kuwa u daktari makini. Mgode aliwaeleza kuwa Ni mshituko wa kawaida ambao ulitokana na kusikia taarifa ambayo hakupendezewa nayo.

Wakarejea nyumbani. Ilikuwa yapata saa sita za usiku. Mbalamwezi ikiuangaza ulimwengu kwa mwanga wake akisi. Masu akawalipa wadeni wake. Dj Yusto, mwenye ng'ombe mnono. Muuza mchele, muuza nyanya na vitunguu, kila aliyeorodhesha Deni akalipwa. Jumla zikatumika laki nne na ushei. Mfukoni akabakiwa na Kiasi Kama elfu themanini hivi. Akaazimu kukikimbia Kijiji.

Kesho yake, Masu akapata muda wa faragha na mamake Janice.

'Hizi habari kwamba unamuoa binti wa mzee Thomas, Zina ukweli gani?' Janice akamhoji Masu.
'Kwa Kweli sijui hata zilianzaje, labda mzee anaweza kuwa na majibu na hili swali mama!' Janice roho ikadunda kwa tumaini jema.
'Wewe umezipokeaje?'
'Dah nilishituka Sana mama, Kama Ni sapraizi, Basi haikuwa njema hata Kidogo!'
'Kwa Nini wasema hivyo?'
'Nilidhani ingekuwa Bora kushirikishana kabla ya kuliweka mbele za kadamnasi. Huwezi jua, unawezakuta binti Ana mchumba tayari, fikiria huyo mchumbaake anamchukuliaje Sasa? Na huyo binti je? Haikuwa nzuri kwa Kweli. Na… na kusema Kweli mama, Mimi tayari Nina mchumba tayari, muda usiozidi miezi mine hivi mtaitwa babu na Bibi!'
Habari hiyo, japo kuwa haikuwa imezingatia Mila na desturi zao, ilimpa faraja mama Masu na kumrejeshea tabasamu lake halisi.
'Alulululuuu!' mama Masu akapiga vigelegele.
'Anaitwa Mwamvita, mzanzibar, wazazi wake Ni chotara wa kishrazi na kitumbatu.'
'Mie nakutakia Heri mwanangu, yote ya Mungu, kwa vile yameshakuwa hivyo, hatuwezi kubadili matokeo. Ila mwanangu, nakuasa baba, asilani asilani usijekufikiria mahusiano na Marietta. Tafadhali Sana unisikie mwanangu. Hilo tu ndilo nakuomba. Uwe Masu wangu anisikilizaye, nakutakie mema mwanangu. Nakukanya kwa Heri kabisa.' mama Masu akasisitiza.
'Nimekusikia mama.'
'Asante mwanangu, nakuamini. Nachukua kauli yako Kama Kiapo!'
'Ninakuahidi, nitakaa mbali naye. Pia nitumie muda huu kukujulisha kuwa Kesho nitakuwa safarini kurejea Zanzibar. Nahitajika kibaruani keshokutwa.'

Masu hakutaka kubishana au kujua kiundani, kwa Nini alikuwa anakatazwa mahusiano na Marietta. Hata hivyo, kwa kazi yake, asingemudu kuwa na wake wawili. Huyo mmoja tu alilazimika kufanya Siri uwepo wake. Kumbukumbu ya maelekezo ya master Park Hye Ilikuwa Moto bado akilini mwake.

'Oh jamani, na Mimi nikidhani tunao muda mwingi wa kuwa nawe?' mama Masu akalalama.
'Ningependa iwe hivyo, lakini kazi, kazi zenyewe za wazungu, hawapendi kupoteza muda kabisa.'
'Ah, sawa mwanangu, nashukuru kwa zawadi na kutukumbuka mwanangu. Ubarikwe Sana mwanangu. Iwe Heri unapoenda kuanza kazi yako. Ukafanikiwe mwanangu.'
'Asante Sana mama. Nanyi pia mbarikiwe. Lakini, ninalo ombi pia. Kwa Hali aliyonayo mkwe wenu, anahitaji usaidizi kwa karibu Sana. Nilitaka nimuibe Maureen akamsaidie kipindi hiki Cha kuelekea kujifingua.'
'Hapana, mlete nyumbani hapa, mamako mkubwa Ni mkunga, akiwa hapa atakuwa Salama. Mie Sina Imani na Mambo ya mjini. Siku hizi kila mzazi anayejifungulia hospitalini utasikia operesheni. Mbona huku Wala si lazima hizo operesheni? We mlete tu nyumbani. Maureen nenda naye ili arudi naye. Na lini Sasa sisi tutakutana na wazazi wake?.!'
'Ngoja kwanza ajifungue, halafu tutapanga tu.'
'Vipi lakini, wazazi wake wako radhi na uhusiano wenu?'
'Hilo ndilo suala gumu Kidogo. Hawanijui bado na hivyo sijui Kama wataridhia au la! Nisingeweza kujitambulisha, ningekamatwa kwa sababu alikuwa mwanafunzi bado, kidato Cha nne. Ila alifanikiwa kufanya mtihani bila kushitukiwa.'
'Mhh!' mama Masu akaguna huku akionekana kutafakari kwa kina.

2020
David Ngocho SamsonView attachment 1448055

Sent using Jamii Forums mobile app
UniTag ukiendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom