Simulizi: Jini Katikati ya Shule

SEHEMU YA 06.

Sasa Masalu akachanganyikiwa, ilikuwa ni afadhali achanganywe na mke wake ambaye alimzoea na kulala naye chumba kimoja kila siku lakini si mwanamke kama Aisha. Alimpenda sana na alimuhitaji katika maisha yake.
Alipagawa, alitulia pale ofisini kwake lakini hakuona kama alitulia kama ipasavyo. Alifanya ujinga sana, hakutakiwa kumzingua mwanamke kama Aisha ambaye alikubaliana naye kwa kila kitu, yaani kwa ujinga wake tu mwisho wa siku likawa kama hilo la kutokea.
Alijifikiria sana kichwani mwake, akaona kazi hazifanyiki kama inavyotakiwa hivyo aliona ni jambo jema kama angerudi nyumbani kwake kupumzika. Akaaga na kuondoka.
Kila mtu alimshangaa, ilikuwa ni lazima kuwa hivyo kwa kuwa hakuonekana kueleweka hata kidogo. Alibadilika haraka sana tangu alipotoka huko Mbezi, kwa wakubwa wakahisi huko alikutana na jambo ambalo lilimfanya kuwa kwenye hali kama hiyo.
Hawakujua ni mwanamke ndiye aliyemfanya kuwa hivyo, hawakujua ni mapenzi ndiyo yaliyokuwa yakimpeleka kwa kasi kiasi hicho. Njiani alipokuwa akitembea kwa miguu kichwa chake hakikuacha kumfikiria Aisha, huyo mwanamke alikuwa namba moja moyoni mwake na hata kama angeulizwa kati ya Grace na Aisha alikuwa akimpenda nani, basi mwanamke huyo alikuwa namba moja.
Alitembea kwa mwendo wa taratibu kuelekea nyumbani. Alipofika maeneo yale ya shule sasa akaanza kumkumbuka zaidi Aisha. Alikutana naye hapo mara ya kwanza, alimfahamia hapo, alimruhusu kumshika mapaja yake laini na kumuongezea hamu ya kufanya naye mapenzi.
Leo alikuwa akirudi nyumbani huku akiwa amemuudhi mwanamke huyo, alimkasirisha kupita kawaida. Hapo shule hakutaka kuvuka, akatulia, kulikuwa na kelele za wanafunzi waliokuwa darasani wakisoma lakini hakutaka kujali sana, ulikuwa ni wakati wa kumfikiria mpenzi wake na ilikuwa ni lazima kufanya hivyo.
“Hivi mbona nilizingua?” alijiuliza.
“Ila nilifanya ujinga sana,” akajijibu.
Alitulia hapo kwa dakika kama kumi hivi, muda huo alikuwa akijaribu kumpigia simu Aisha na kwa bahati mbaya kwake haikuwa ikipatikana. Hilo likamchanganya sana, alimpigia zaidi ya mara thelathini na saba kote huko aliambulia ziro.
Akaamua kusimama na kuondoka mahali hapo kuelekea nyumbani kwake. Safari yake nzima ilitawaliwa na mawazo makubwa ya Aisha, alijilaumu kwa ujinga alioufanya ambao sasa ulionekana kumuharibia kumkosa mwanamke huyo, na mbaya zaidi akaonekana kuwa Mswahili.
Hakuchukua muda mrefu akafika nyumbani kwake. Ilikuwa ni mapema tu, akamsikia mkewe akiongea na mtu ndani ya nyumba hiyo, hakuwa peke yake, bila shaka alipata mgeni ambaye alikuwa akizungumza naye. Akavua viatu na kuingia ndani.
Alipofika sebuleni tu, macho yake yakagongana na mkewe aliyeonyesha tabasamu lakini alipomwangalia mgeni aliyekuwa humo, akashtuka sana baada ya kumuona Aisha.
Ndiyo!
Alikuwa Aisha!
Aisha yuleyule wa shuleni!
Yuleyule aliyemzingua miadi ya kuonana naye.
Sasa mapigo yake ya moyo yakaanza kwenda kasi, hakuamini alichokuwa akikiangalia mbele yake. Alikuwa na hofu, mwili wake ukaanza kutetemeka kwa hofu na kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Maswali kibao yakaanza kumiminika kichwani mwake.
Huyo Aisha alikuwa anafanya nini hapo?
Alijuanaje na mkewe?
Walikuwa marafiki kwa kipindi gani?
Sasa akatamani aulize maswali hayo yote.
Angeulizaje?
Aisha mwenyewe hakuwa na habari, ndiyo kwanza alikuwa akitoa tabasamu pana, na kubwa zaidi mwanamke huyo wala hakuonyesha kushtuka, ndiyo kwanza akasimama na kumsalimia.
“Habari yako shemeji!” alimsalimia Aisha. Sasa Masalu akawa na kitete.
“Salama! Karibu!”
Sasa mkewe akaanza kuwatambulisha. Hilo likafanyika, walikuwa wakijuana lakini kwa sababu mkewe alikuwa hapo sasa ikawabidi wazuge kama hawakuwa wakifahamiana hata kidogo na wakati siku hiyo tu walitaka kulala pamoja.
“Huyu rafiki yangu anaitwa Aisha!” alisema mkewe huku akimwangalia mumewe.
“Oh! Nimefurahi sana kumfahamu! Karibu sana,” alisema Masalu huku naye akijitahidi kutoa tabasamu, ila lile tabasamu ambalo halikutoka kabisa moyoni mwake.
“Basi mi nipo ndani!” alisema Masalu na kuelekea chumbani.
Humo, kwanza akajilaza kitandani, alichoka. Akili yake haikuwa sawa hata kidogo, alijiuliza huyo Aisha alikuwa akifanya nini chumbani hapo, halafu mbona mkewe hakuwahi kumwambia kama alikuwa na rafiki anayeitwa Aisha? Halafu akakumbuka kitu, siku ile mwanamke huyo alipokuwa ndani, mkewe aliporudi aliondoka kwa kupitia mlango wa nyuma, kwa nini hakubaki ndani?
Akaamua kupotezea japokuwa hakupata majibu ya maswali hayo. Huku akiwa humo chumbani mara simu yake ikaanza kuita, akaichukua na kuangalia, jina lilikuwa la Aisha, akashtuka, ila ikambidi apokee.
“We Aisha unataka nini kunipigia simu na wakati unajua mke wangu uo naye hapo?” aliuliza Masalu huku akionekana kushtuka.
“Nipo na mkeo? Unajitoa akili kwa sababu umenikosea sanaeeeee?” aliuliza mwanamke huyo.
“Aisha bhana!”
“Kwanza kwa nini umenifanyia hivi leo?”
“Najua nimekukosea. Ila tutaongea ukiondoka hapa nyumbani!”
“Nyumbani wapi? Hivi unajua nipo wapi?”
“Wewe si upo hapa nyumbani, nimekuacha sebuleni!”
“Masalu bwana! Yaani unanishangaza sana. Sasa mimi nije kwako kufanya nini? Mkeo mimi namfahamu kwani?’ aliuliza mwanamke huyo kwenye simu.
“Hebu subiri!”
“Sawa. Utanipigia nikusomee kesi zangu,” alisema mwanamke huyo na kukata simu.
Sasa hapo Masalu akashusha pumzi kwa nguvu, tena ile nzito kabisa. Maneno aliyozungumza huyo Aisha yalimchanganya mno, alimwambia hakuwa yeye, sasa yule sebuleni alikuwa nani? Alipoingia alimuona, halafu akamsalimia, tena alikuwa na uhakika alikuwa yeye, na jina lake aliitwa Aisha, sasa kama hakuwa Aisha, alikuwa nani?
Kwanza walifanana.
Sauti zao.
Sura.
Yaani kila kitu mpaka tabasamu.
Halafu eti anaambiwa siyo yeye! Akaona kama masihara.
Akatoka chumbani na kuelekea sebuleni, akateka kwenda kumuona kwa mara ya pili lakini alikuwa na uhakika aliyemuona alikuwa yuleyule Aisha. Alipofika sebuleni na kumwangalia. Hapo sasa akachanganyikiwa.
Hakuwa Aisha bwana!
Alimshangaa mgeni mpaka mgeni mwenyewe akajishtukia, maana haikuwa kwa kushangawa kule.
“Mimi nishakuwa mzee! Natoka kidogo! Hivi uliniambia mgeni anaitwa nani vile?” aliuliza Masalu huku akimwangalia mkewe, sasa akalazimisha tabasamu pana usoni mwake.
“Mwajuma!”
“Oh! Aya shemeji Mwajuma mimi natoka,” alisema Masalu na hakutaka kubaki mahali hapo, huyo akaondoka zake.
Mwajuma na Aisha! Mbona yalikuwa majina tofauti kabisa. Yaani aambiwe Mwajuma halafu yeye ahisi Aisha, hakika kwake ni kama kitu hicho hakikumuingia akilini mwake kabisa.
Sasa hapo kajifikiria ni wapi alitakiwa kwenda, kazini kwake ama wapi? Huku akiwa njiani kuelekea asipopajua akaona meseji ikiingia, kuifungua tu, mtumaji alikuwa Aisha.
‘Nipo huku karibu na uwanja wa mpira wa miguu, njoo huku’
Aliisoma meseji hiyo vizuri kabisa. Sasa akagundua Aisha alikuwa maeneo hayohayo ya karibu.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 06.

Sasa Masalu akachanganyikiwa, ilikuwa ni afadhali achanganywe na mke wake ambaye alimzoea na kulala naye chumba kimoja kila siku lakini si mwanamke kama Aisha. Alimpenda sana na alimuhitaji katika maisha yake.
Alipagawa, alitulia pale ofisini kwake lakini hakuona kama alitulia kama ipasavyo. Alifanya ujinga sana, hakutakiwa kumzingua mwanamke kama Aisha ambaye alikubaliana naye kwa kila kitu, yaani kwa ujinga wake tu mwisho wa siku likawa kama hilo la kutokea.
Alijifikiria sana kichwani mwake, akaona kazi hazifanyiki kama inavyotakiwa hivyo aliona ni jambo jema kama angerudi nyumbani kwake kupumzika. Akaaga na kuondoka.
Kila mtu alimshangaa, ilikuwa ni lazima kuwa hivyo kwa kuwa hakuonekana kueleweka hata kidogo. Alibadilika haraka sana tangu alipotoka huko Mbezi, kwa wakubwa wakahisi huko alikutana na jambo ambalo lilimfanya kuwa kwenye hali kama hiyo.
Hawakujua ni mwanamke ndiye aliyemfanya kuwa hivyo, hawakujua ni mapenzi ndiyo yaliyokuwa yakimpeleka kwa kasi kiasi hicho. Njiani alipokuwa akitembea kwa miguu kichwa chake hakikuacha kumfikiria Aisha, huyo mwanamke alikuwa namba moja moyoni mwake na hata kama angeulizwa kati ya Grace na Aisha alikuwa akimpenda nani, basi mwanamke huyo alikuwa namba moja.
Alitembea kwa mwendo wa taratibu kuelekea nyumbani. Alipofika maeneo yale ya shule sasa akaanza kumkumbuka zaidi Aisha. Alikutana naye hapo mara ya kwanza, alimfahamia hapo, alimruhusu kumshika mapaja yake laini na kumuongezea hamu ya kufanya naye mapenzi.
Leo alikuwa akirudi nyumbani huku akiwa amemuudhi mwanamke huyo, alimkasirisha kupita kawaida. Hapo shule hakutaka kuvuka, akatulia, kulikuwa na kelele za wanafunzi waliokuwa darasani wakisoma lakini hakutaka kujali sana, ulikuwa ni wakati wa kumfikiria mpenzi wake na ilikuwa ni lazima kufanya hivyo.
“Hivi mbona nilizingua?” alijiuliza.
“Ila nilifanya ujinga sana,” akajijibu.
Alitulia hapo kwa dakika kama kumi hivi, muda huo alikuwa akijaribu kumpigia simu Aisha na kwa bahati mbaya kwake haikuwa ikipatikana. Hilo likamchanganya sana, alimpigia zaidi ya mara thelathini na saba kote huko aliambulia ziro.
Akaamua kusimama na kuondoka mahali hapo kuelekea nyumbani kwake. Safari yake nzima ilitawaliwa na mawazo makubwa ya Aisha, alijilaumu kwa ujinga alioufanya ambao sasa ulionekana kumuharibia kumkosa mwanamke huyo, na mbaya zaidi akaonekana kuwa Mswahili.
Hakuchukua muda mrefu akafika nyumbani kwake. Ilikuwa ni mapema tu, akamsikia mkewe akiongea na mtu ndani ya nyumba hiyo, hakuwa peke yake, bila shaka alipata mgeni ambaye alikuwa akizungumza naye. Akavua viatu na kuingia ndani.
Alipofika sebuleni tu, macho yake yakagongana na mkewe aliyeonyesha tabasamu lakini alipomwangalia mgeni aliyekuwa humo, akashtuka sana baada ya kumuona Aisha.
Ndiyo!
Alikuwa Aisha!
Aisha yuleyule wa shuleni!
Yuleyule aliyemzingua miadi ya kuonana naye.
Sasa mapigo yake ya moyo yakaanza kwenda kasi, hakuamini alichokuwa akikiangalia mbele yake. Alikuwa na hofu, mwili wake ukaanza kutetemeka kwa hofu na kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Maswali kibao yakaanza kumiminika kichwani mwake.
Huyo Aisha alikuwa anafanya nini hapo?
Alijuanaje na mkewe?
Walikuwa marafiki kwa kipindi gani?
Sasa akatamani aulize maswali hayo yote.
Angeulizaje?
Aisha mwenyewe hakuwa na habari, ndiyo kwanza alikuwa akitoa tabasamu pana, na kubwa zaidi mwanamke huyo wala hakuonyesha kushtuka, ndiyo kwanza akasimama na kumsalimia.
“Habari yako shemeji!” alimsalimia Aisha. Sasa Masalu akawa na kitete.
“Salama! Karibu!”
Sasa mkewe akaanza kuwatambulisha. Hilo likafanyika, walikuwa wakijuana lakini kwa sababu mkewe alikuwa hapo sasa ikawabidi wazuge kama hawakuwa wakifahamiana hata kidogo na wakati siku hiyo tu walitaka kulala pamoja.
“Huyu rafiki yangu anaitwa Aisha!” alisema mkewe huku akimwangalia mumewe.
“Oh! Nimefurahi sana kumfahamu! Karibu sana,” alisema Masalu huku naye akijitahidi kutoa tabasamu, ila lile tabasamu ambalo halikutoka kabisa moyoni mwake.
“Basi mi nipo ndani!” alisema Masalu na kuelekea chumbani.
Humo, kwanza akajilaza kitandani, alichoka. Akili yake haikuwa sawa hata kidogo, alijiuliza huyo Aisha alikuwa akifanya nini chumbani hapo, halafu mbona mkewe hakuwahi kumwambia kama alikuwa na rafiki anayeitwa Aisha? Halafu akakumbuka kitu, siku ile mwanamke huyo alipokuwa ndani, mkewe aliporudi aliondoka kwa kupitia mlango wa nyuma, kwa nini hakubaki ndani?
Akaamua kupotezea japokuwa hakupata majibu ya maswali hayo. Huku akiwa humo chumbani mara simu yake ikaanza kuita, akaichukua na kuangalia, jina lilikuwa la Aisha, akashtuka, ila ikambidi apokee.
“We Aisha unataka nini kunipigia simu na wakati unajua mke wangu uo naye hapo?” aliuliza Masalu huku akionekana kushtuka.
“Nipo na mkeo? Unajitoa akili kwa sababu umenikosea sanaeeeee?” aliuliza mwanamke huyo.
“Aisha bhana!”
“Kwanza kwa nini umenifanyia hivi leo?”
“Najua nimekukosea. Ila tutaongea ukiondoka hapa nyumbani!”
“Nyumbani wapi? Hivi unajua nipo wapi?”
“Wewe si upo hapa nyumbani, nimekuacha sebuleni!”
“Masalu bwana! Yaani unanishangaza sana. Sasa mimi nije kwako kufanya nini? Mkeo mimi namfahamu kwani?’ aliuliza mwanamke huyo kwenye simu.
“Hebu subiri!”
“Sawa. Utanipigia nikusomee kesi zangu,” alisema mwanamke huyo na kukata simu.
Sasa hapo Masalu akashusha pumzi kwa nguvu, tena ile nzito kabisa. Maneno aliyozungumza huyo Aisha yalimchanganya mno, alimwambia hakuwa yeye, sasa yule sebuleni alikuwa nani? Alipoingia alimuona, halafu akamsalimia, tena alikuwa na uhakika alikuwa yeye, na jina lake aliitwa Aisha, sasa kama hakuwa Aisha, alikuwa nani?
Kwanza walifanana.
Sauti zao.
Sura.
Yaani kila kitu mpaka tabasamu.
Halafu eti anaambiwa siyo yeye! Akaona kama masihara.
Akatoka chumbani na kuelekea sebuleni, akateka kwenda kumuona kwa mara ya pili lakini alikuwa na uhakika aliyemuona alikuwa yuleyule Aisha. Alipofika sebuleni na kumwangalia. Hapo sasa akachanganyikiwa.
Hakuwa Aisha bwana!
Alimshangaa mgeni mpaka mgeni mwenyewe akajishtukia, maana haikuwa kwa kushangawa kule.
“Mimi nishakuwa mzee! Natoka kidogo! Hivi uliniambia mgeni anaitwa nani vile?” aliuliza Masalu huku akimwangalia mkewe, sasa akalazimisha tabasamu pana usoni mwake.
“Mwajuma!”
“Oh! Aya shemeji Mwajuma mimi natoka,” alisema Masalu na hakutaka kubaki mahali hapo, huyo akaondoka zake.
Mwajuma na Aisha! Mbona yalikuwa majina tofauti kabisa. Yaani aambiwe Mwajuma halafu yeye ahisi Aisha, hakika kwake ni kama kitu hicho hakikumuingia akilini mwake kabisa.
Sasa hapo kajifikiria ni wapi alitakiwa kwenda, kazini kwake ama wapi? Huku akiwa njiani kuelekea asipopajua akaona meseji ikiingia, kuifungua tu, mtumaji alikuwa Aisha.
‘Nipo huku karibu na uwanja wa mpira wa miguu, njoo huku’
Aliisoma meseji hiyo vizuri kabisa. Sasa akagundua Aisha alikuwa maeneo hayohayo ya karibu.

Je, nini kitaendelea?
Nyingine
 
SEHEMU YA 07.

Haraka sana Masalu hakutaka kupoteza hata dakika moja, akaanza kuelekea huko alipoambiwa na Aisha. Moyo wake ulikuwa na hofu tele, alijikuta tu akianza kumuogopa msichana huyo kwa kile alichokuwa amemfanyia, kiliendelea kubaki moyoni mwake.
Alitembea mpaka alipofika mahali alipoambiwa, akamuona Aisha akiwa pembeni ya duka moja dogo kulipokuwa na kibenchi, alikuwa peke yake, kulikuwa na wanaume kwa pembeni lakini kila mmoja aliogopa kumfuata pale alipokuwa kutokana na uzuri wake.
“Kwanza nisamehe!” alisema Masalu baada ya kumfikia, tena aliyasema hayo hata kabla ya salamu.
Sasa Aisha akajifanya kukasirika, alitaka kumuonyesha mwanaume huyo kwamba kulikuwa na mambo hakutakiwa kuyafanya, yeye kama msichana alikuwa na mambo mengi ya kufanya, aliamua kuyaacha hayo yote ilimradi tu aende akaonane naye lakini mwisho wa siku akamzingua.
“Ila sijapenda,” alisema Aisha.
“Ndiyo maana nikakuomba msamaha! Sikutakiwa kukukasirisha mwanamke mzuri kama wewe. Moyo wangu uliniuma sana kama nimefiwa na mama yangu,” alisema Masalu.
“Ila nyie wanaume bwana! Siku tukizinguaga sisi, mnajifanya kutumaindi sana. Kwanza ilikuwaje mpaka ukanirusha?” aliuliza Aisha.
“Yaani acha tu! Nilijikuta tu nipo Mbezi!”
“Mbezi kwa nani?”
“Kwa wakwe! Nikaja kushtuka baadaye sana! Halafu nilishangaa sana, sikwenda huko Mbezi, sasa ilikuwaje nikawa huko?” aliuliza.
“Sasa unaniuliza mimi?”
“Mauzauza tu! Kwanza tunafanyaje?”
“Nakusikiliza wewe!”
“Ukinisikiliza mimi, naweza kukwambia hata sasa hivi freshi tu! Mimi muda wote mambo yapo poa,” alimwambia.
“Ila kwanza acha niende nyumbani nikaoge, halafu baadaye tutaonana!” alisema Aisha.
“Wapi sasa?”
“Unataka nipange mimi? Hujiamini?”
“Najiamini! Ila leo haki ya Mungu sitozingua!”
“Una uhakika?”
“Kabisa yaani!”
“Saa ngapi unataka tuonane?”
“Saa moja usiku!”
“Na mkeo utamuagaje?”
“Nitajua mbele kwa mbele,” alimwambia.
Wakakubaliana muda huo waonane Manzese Midizini kulipokuwa na gesti nyingi, ilikuwa ni lazima wakutane huko na kuanza kufanya mambo yao.
Kwa Masalu hakuona kama kulikuwa na tatizo lolote lile, kwa jioni ya siku hiyo aliamua kujipanga vilivyo mpaka kulala na Aisha. Alijilaumu kwa kumzingua asubuhi, alijiambia kwamba kwa siku hiyo hakutaka kumzingua hata kidogo.
Sasa akaondoka huku akiwa ameridhika, tena hata uso wake ulionyesha kabisa mtu aliyekuwa na matumaini na furaha nyingi tu. Hakutaka kukaa huko sana, alichokifanya ni kurudi nyumbani. Kwa nini alifanya hivyo?
Sababu kubwa ni kuwa karibu na mke wake. Kama angekuwa karibu naye kuanzia muda huo mpaka usiku na kutoka, ingekuwa rahisi sana kwake kuruhusiwa bila shaka kuliko kukaa sehemu tu mbali na nyumbani halafu ghafla tu ampigie simu na kumwambia amekwenda mahali na atachelewa kurudi, kwake hakuona kama ingekuwa vizuri.
Siku hiyo alikaa na kumpetipeti mkewe, alikuwa na furaha tele na aliamini angeruhusiwa kwa moyo mmoja kwenda huko kuonana na Aisha. Msichana huyo aliendelea kumsisitiza kwenye meseji kwamba hakutakiwa kumzingua siku hiyo, waonane na kufanya mapenzi kama walivyokubaliana.
“Yaani hakuna kuzingua! Saa moja tu nipo ndani ya nyumba,” alisema Masalu.
“Sasa ukinizingua, tusijuane kabisaaaa!”
“Hilo haliwezi kutokea!”
Wakaendelea kuandikiana meseji mpaka majira ya saa kumi na mbili na robo ambapo mkewe akamwambia alikuwa akitoka na angerudi muda si mrefu. Masalu wala hakuwa na wasiwasi, hakutaka kutoka kwa kuwa lisingekuwa jambo zuri kama angeiacha nyumba peke yake, kwa kuwa mkewe alisema angerudi, basi angesubiri.
Dakika zilikimbia tu, ilipofika majira ya saa kumi na mbili na nusu, sasa akaona haiwezekani, ilikuwa ni lazima ajiandae kuondoka kwani bila hivyo, basi ingetokea kama ilivyotokea asubuhi yake.
Akaenda bafuni kuona, ile anamaliza tu akasikia mlango unagongwa. Alihisi ni mkewe ila akajiambia lilikuwa suala lisilowezekana kwa mwanamke huyo kugonga mlango, kwa kuwa haukuwa umefungwa, angeingia moja kwa moja.
Akaufuata na kuufungua.
Macho yake yakatua kwa watu ambao hakuwatarajia kabisa. Walikuwa wakwe zake, walifika nyumbani hapo kwa lengo la kuwatembelea. Alikasirika, akaonyesha tabasamu na kuwakaribisha ndani lakini hakuwa na furaha hata kidogo.
Sasa akajiuliza ni kwa namna gani angeweza kuondoka mahali hapo na kuwaacha wazazi hao nyumbani? Lilikuwa ni suala lisilowezekana hata kidogo.
Kama kulikuwa na kipindi ambacho Masalu hakuwahi kutamani ugeni basi kilikuwa kipindi hicho. Mkewe aliondoka, alikwenda wapi? Hakumwambia ila alisema angerudi muda si mrefuHuo muda mrefu haukufika, sasa alishindwa hata kwenda kuonana na Aisha kwa sababu yao.
Akakaa kwenye kiti, hakutulia, mara alisimama na kuelekea chumbani, mara arudi na kukaa hapo sebuleni. Yaani kwa kumwangalia tu alionyesha kuvurugwa.
“Grace yupo wapi?” aliuliza baba yake Aisha huku akimwangalia Masalu.
“Alitoka! Ila anakuja sasa hivi, acha nimpigie simu kwanza,” alijibu na kuchukua simu yake.
Akaanza kumpigia mkewe, simu ilikuwa inaita tu lakini haikuwa ikipatikana. Alikasirika, ilikuwa ni bora angepokea na kumwambia aende nyumbani mara moja kwa kuwa wazazi wake waliwatembelea, ubaya hakuwa akipokea simu.
“Grace! Grace!” aliita kwa sauti ya chini huku akiwa na hasira mno.
Macho yake hayakutoka kwenye saa yake, mara kwa mara alikuwa akiangalia huku akionekana kukasirika kupita kawaida. Muda haukumsubiri hata kidogo, ulizidi kwenda mbele
Wakwe zake hawakuwa na habari hata kidogo, hawakujua kama uwepo wao mahali pale ulimchanganya sana Masalu! Kuna wakati alitamani kuwatoroka na kuondoka zake lakini alishindwa kufanya hivyo.
Akawa anajiongelesha tu lakini moyoni mwake alikuwa na hamu ya kuondoka nyumbani hapo. Muda ulisogea mpaka ilipofika majira ya saa moja na dakika kumi, sasa hapo akaona kabisa na siku hiyo angeshindwa kuonana na Aisha.
“Nifanyeje?” alijiuliza, alionekana kukata tamaa.
Hata kumpigia simu na kuzungumza naye aliogopa, yaani alimuogopa zaidi ya mkewe, Grace, kuna wakati alitamani sana kama angemuoa mwanamke huyo lakini alishindwa kufanya hivyo.
Ilipofika majira ya saa moja na dakika ishirini ndipo Grace akarudi nyumbani hapo. Alisuka, alionekana kabisa alikwenda kwa msusi, alipowaona wazazi wake tu, akafurahi sana, akawasalimia.
“Natoka mara moja,” alisema Masalu.
Hakutaka kupoteza muda wake, ilikuwa ni lazima kuondoka mahali hapo. Alijua angeshindwa kuonana naye lakini kidogo angekuwa amejaribu kufanya hivyo na si kukaa tu nyumbani bila kufanya lolote lile.
“Naomba usinitafute tena! Na namba yangu futa,” alisema mwanamke huyo na kukata simu.
Moyo wa Masalu ukanyong’onyea sana, hakuamini alichokisikia, sasa akapagawa na kitu pekee kilichokuja kichwani mwake kilikuwa ni kuondoka na kuelekea kule alipokuwa akiishi Aisha, ilikuwa ni lazima amuombe msamaha kwa kile kilichotokea.
Akaondoka na kuelekea Mburahati alipokuwa akiishi. Alikwenda mpaka pale aliposhuka na bodaboda na kuanza kuifuata njia ileile kama alivyokuwa ameelekezwa na Aisha, cha ajabu hakupakumbuka nyumbani hapo.
Alijikuta akizunguka huku na kule, alipita njia zote alizokuwa akizifahamu lakini hakubahatika kuiona nyumba ile. Sasa akajiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea? Alizifuata njia zilezile lakini nyumba ile hakuiona. Akaona haiwezekani, akaamua kumsimamisha mwanaume mmoja na kumuuliza.
Alichomjibu ndicho kilichomvuruga sana. Eti tangu akae mtaani hapo hakuwa ameiona nyumba hiyo aliyokuwa akiizungumzia mahali hapo. Ilikuwaje? Iweje asiijue na wakati ilikuwa mtaani hapo?
“Bro! Mi nimezaliwa hapa Mburahati! Nimekulia hapa na nimesomea hapo shule, sijawahi kuiona nyumba unayoizungumzia!” alisema jamaa aliyekuwa akiulizwa.
“Sikiliza bro! Mi nilikuja huku, nikaonana na huyo manzi kwenye hiyo nyumba!”
“Sasa ipo wapi? Hujui hata njia ya kufika huko?”
“Najua! Ila sijui ipo wapi! Daah! Ila ilikuwa njia hii hii! Yaani nilipofika hapa, ndipo nimesahau ipo wapi!” alimjibu.
“Huku ukienda mbele unatokea makaburini, ukiyavuka unakwenda Kigogo, sasa wewe unazungumzia wapi?” aliuliza.
Masalu alijitahidi kujielezea lakini hakuwa na jibu lolote lile, kiukweli hakukumbuka hata kidogo kuhusu nyumba hiyo. Moyo wake ulimuuma sana lakini kwa kuwa ilikuwa ni usiku, akaamua kuondoka na kujiahidi kwamba ni lazima kesho yake mapema tu angerudi na kuanza kupatafuta, alijiambia inawezekana ilikuwa ni usiku ndiyo maana alishindwa kupakumbuka.
“Basi poa!” alimwambia na kuondoka, akaendelea kumtafuta Aisha kwenye simu lakini hakupatikana.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane kesho.
 
SEHEMU YA 08.

Asubuhi na mapema Masalu akaamka na kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuijaribu simu ya Aisha kama kawaida yake. Alitaka kujua kama alikuwa akipatikana ama la. Alimpigia na kumpigia lakini msichana huyo hakuwa akipatikana.
Kichwa chake kikauma, moyo wake ukamuuma mno, hakuamini kama kweli angemkosa msichana huyo mara baada ya kumzingua mara mbili. Alijijua hakuwa na kosa lolote lile, ni kweli alimzingua lakini alifanya hivyo si kwa kukusudia, bali kulikuwa na jambo fulani ndilo lililomfanya kuwa hivyo.
Sasa mawazo yakaongezeka, alichokifanya ni kuondoka nyumbani kwake na kuanza kuelekea Mburahati. Alikumbuka kwamba siku iliyopita alikwenda huko, cha ajabu kabisa, eti hakupakumbuka mahali alipokuwa akiishi Aisha na wakati alikwenda naye na ndani akaingia.
Alichukua bodaboda ambayo ilimpeleka mpaka huko. Alipofika, akateremka na kuanza kuelekea kwenye njia ileile aliyopita siku ile. Kwa siku hiyo aliikumbuka vilivyo kwa kuwa ilikuwa ni asubuhi, akawaza inawezekana jana hakupakumbuka kwa kuwa ilikuwa ni usiku.
Alitembea, alikata vichochoro na hatimaye kukutana na nyumba hiyo. Uso wake ukajawa na tabasamu pana, akakenua na kuanza kuufuata mlango kwa lengo la kugonga hodi. Alipoufikia, akaanza kugonga.
Sauti ya msichana ikasikika kutoka ndani. Aliifahamu sauti hiyo, ilikuwa ni ya Aisha, akajawa na tabasamu pana kwamba sasa ulifika muda wa kuzungumza na msichana huyo na kumuomba msamaha kwa yote yaliyokuwa yametokea.
Mara akatokea na macho yake kutua kwa Aisha! Ni kweli alikuwa yeye! Alipendeza, japokuwa ilikuwa ni asubuhi lakini uzuri wake haukujificha hata kidogo, tabasamu lake likamfanya kuvutia mno.
“Karibu sana!” alimkaribisha msichana huyo.
Masalu akaingia ndani. Alimwangalia Aisha, aliendelea kumpenda, tena siku hiyo alimpenda zaidi na zaidi, wakaelekea sebuleni na kukaa kwenye kochi. Aisha akatoka hapo na kwenda kumchukua soseji kwenye friji ambazo alikuwa ameziandaa kwa lengo la kunywa nazo chai, akampa Masalu. Akaanza kuzila.
Aisha hakuongea kitu chochote kile, alikaa kwenye kochi na kuanza kumwangalia Masalu aliyekuwa bize akila. Kwa kumwangalia tu aligundua mwanaume huyo alikuwa na furaha tele kumkuta mahali hapo, alikuwa na kesi naye na ilikuwa ni lazima azungumze naye.
“Naomba unisamehe mama!” alisema Masalu kwa adabu zote.
“Unajua kosa lako nini?”
“Ndiyo! Kosa langu ni kukuzingua kwa mara mbili ila naomba nikwambie jambo moja,” alisema Masalu.
“Jambo gani?”
“Sikukusudia kukukosea!”
“Hilo wala sio kosa hata kidogo! Dharura hutokea,” alisema Aisha huku akiwa pale kwenye kochi na miguu yake ikiwa kwa juu.
“Najua!”
“Kwa hiyo kosa lako umelijua ama hujalijua?”
“Nilijua ni hilo, kama si hilo, hebu niambie unalotaka kuniambia!” alisema Masalu.
“Kosa lako ni kuokotaokota hovyo wanawake na wakati una mke,” alisema msichana huyo huku akimwangalia Masalu aliyekuwa bize akila soseji.
Masalu akashtuka kidogo kusikia hivyo, ni kitu ambacho hakutegemea kukisikia kutoka kwa mtu kama Aisha, mtu ambaye aliwasiliana naye sana mpaka wakakubaliana kuonana loji na kufanya mapenzi, sasa alikuwa akizungumza maneno gani?
“Ni kwa sababu ninakupenda!” alisema Masalu.
“Kampende mkeo! Si kule kanisani ulisema utampenda maisha yako yote, imekuwaje tena baba?” aliuliza Aisha huku akitoka kicheko cha chini.
“Hebu tuachane na masuala ya mke wangu kwanza!” alisema Masalu, alionekana kummaindi kidogo.
“Sawa. Nakuja!” alisema msichana huyo na kuondoka kuelekea chumbani.
*
Watu walisimama pembeni ya makaburi wakimwangalia mwanaume mmoja aliyekaa kwenye kaburi moja na kula majani. Hawakujua mwanaume huyo alikuwa nani na alikuwa akifanya nini mahali hapo. Kila mmoja alikuwa akisema lake, kuna wengine walisema alikuwa kichaa lakini wengine wakasema alikuwa na akili timamu.
Sasa wakaanza kubishana. Kwa jinsi mwanaume huyo alivyovaa, ilikuwa ni vigumu kukubaliana kwamba alikuwa kichaa, alipendeza, alionekana kuwa mwanaume nadhifu sana, sasa swali likawa moja tu, kwa nini alikuwa akila majani?
Huyo hakuwa mwanaume wa kwanza kuwa kwenye kaburi hilo, kulikuwa na watu wengi, hasa wanaume waliokuwa wakifika mahali hapo na kukaa juu ya kaburi hilo. Kuna wengine walikuwa wakifika na kula mchanga, wengine udongo, huyo wa siku hiyo alifika hapo na kuanza kula majani.
Watu walikusanyika, walikuwa ni zaidi ya ishirini, kila mmoja alikuwa akimwangalia, wale waliokuwa wakiendelea na mambo yao, sasa wakaacha na kusimama wima na macho yao yakiwa kule makaburini. Huyo mwanaume aliwashangaza.
“Huyu kama mwanaume wa tano hivi kuja hapa makaburini na kukaa pale,” alisema kijana mmoja, alikuwa fundi viatu aliyekuwa na kibanda chake pembeni ya makaburi.
“Acha utani!”
“Kweli tena! Kuna mmoja alikuja wiki iliyopita, alikaa palepale kwenye lile kaburi na kuanza kula mchanga. Aisee nilimshangaa sana. Sasa leo amekuja mwingine,” alijibu fundi huyo.
“Kwa hiyo huyu si wa kwanza?”
“Ndiyo! Halafu jamaa alikuja juzi hapahapa, akaenda kukaa kwenye lilelile kaburi!”
“Ama la ndugu yake?”
“Hamna! Lile kaburi la demu fulani hivi anaitwa Aisha! Alikuwa anaishi mtaa wa nyuma hapo!”
“Sasa kwa nini watu wanakwenda kwenye kaburi lile?”
“Hata najua basi kaka!”
Mwanaume huyo alishangaza mno, watu waliokuwa na simu zao, wakazitoa na kuanza kumpiga picha, kwao ilionekana kama kituko fulani hivi, mtu kwenda makaburini na kuanza kula majani, hakika iliwashangaza.
Baada ya watu kujaa na kufikia hamsini, hatimaye mwanaume mmoja akajitolea na kwenda kumshtua mwanaume huyo, alihitaji kwanza kujua kama alikuwa kichaa ama la! Akaanza kupiga kelele huku akimsogelea, baada ya kumfikia, akamshika begani.
Mwanaume huyo alikuwa Masalu.
Masalu akashtuka baada ya kuguswa begani. Alimwangalia mwanaume aliyemgusa, alimshangaa, hakumfahamu na hakujua alikuwa akifanya nini mahali hapo.
Aliangalia vizuri alipokuwa.
Tobaaaa!
Hakukuwa ndani ya nyumba ya akina Aisha, alikuwa juu ya kaburi moja akiwa amekaa, alishangaa mno, hakujua alifikaje mahali hapo. Ilikuwaje mpaka kuwa makaburini?
Akasimama na kuanza kuangalia huku na kule. Kulikuwa na idadi kubwa ya watu, wote hao walikuwa wakimshangaa, alishangawa kwa kuwa alikaa makaburini, mkononi mwake alikuwa na majani.
Hapo ndipo alipogundua hakuwa akila soseji bali majani. Akayatupa chini.
“Bro! Imekuwaje tena?” aliuliza mwanaume huyo.
Masalu hakujibu lolote lile, bado alipigwa na bumbuwazi kwa kile kilichtokea, alishangaa, alijiuliza ni kwa namna gani alifika hapo makaburini, hakuwa na jibu lolote lile.
“Imekuwaje umekaa makaburini na kula majani?” aliuliza jamaa huyo.
“Nimefikaje makaburini?”
“Tukuulize wewe!”
“Hapana! Nilikuwa kwa akina Aisha!”
“Aisha ndiye nani?”
“Aisha.....” alisema Masalu, aliyageuza macho yake na kuangalia kaburi lile, liliandikwa Aisha Majidi, yaani huyo Aisha alizikwa hapo.
Akashtuka mno! Hakuamini alichokuwa akikiona mbele yake, ni kama alikuwa amechanganyikiwa na jamaa huyo akagundua, kwanza akamtoa humo makaburini na kumpeleka pembeni, alijua alichanganyikiwa.
Wanaume wengine watatu wakamsogelea na kumjulia hali. Hawakumjua lakini kwa maelezo ya fundi viatu alisema hiyo ilikuwa ni mara ya pili kwake kumuona jamaa huyo, walitaka kujua kilichokuwa kimetokea.
Kwa kuwa hakujua lolote lile, akawa hana jinsi, ikabidi aanze kuelezea kuhusu huyo Aisha, jinsi alivyokutana naye, walivyojenga urafiki na mpaka kuanza kwenda nyumbani hapo, kumbe alipelekwa kaburini.
“Aisee! Pole sana!”
Huku akiwa haelewi kilichokuwa kikiendelea, mwanamke mmoja akatokea hapo na kuuliza kilichotokea, akaambiwa, alichokisema ni kwamba mama Aisha alitakiwa kuonana na mwanaume huyo aliyekwenda hapo makaburini, angeongea naye na kumpa dawa ambayo ingemfanya kutokusumbuliwa tena na marehemu Aisha.
Kila mtu ambaye alikwenda hapo makaburini, ilikuwa ni lazima kupelekwa nyumbani kwa mwanamke huyo na kupewa dawa. Aisha alifariki zamani sana, tangu mwaka 1999 na walichokuwa wakikutana nacho watu hao hakuwa Aisha bali jini.
Kwa nini alikuwa hivyo?
Kwa nini hakuwaua?
Siri zote alikuwanazo mwanamke huyo. Hivyo Masalu akachukuliwa na kupelekwa nyumbani kwa akina Aisha huku akiwa bado hajakaa sawa kichwani mwake. Alikuwa na mawenge fulani hivi.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 09.

Hawakuchukua muda mrefu kufika nyumbani kwa akina Aisha. Mama’ake Aisha alipomuona Masalu tu akajua alikuwa ndiye mwanaume aliyekutwa makaburini, juu ya kaburi la marehemu binti yake. Alipomwangalia tu, kwa jinsi alivyokuwa, alikuwa tofauti na wenzake.
Akawakaribisha na kuingia ndani. Umati wa watu uliokuwa ukiwafuatilia ulibaki nje. Kila mtu alitaka kufahamu kilichokuwa kimetokea, ilikuwaje huyo mwanaume akae pale makaburini na kula majani? Halafu hakuwa peke yake, kulikuwa na wanaume ambao waliwahi kukutwa palepale makaburini kama yeye.
Masalu akakaa kwenye kochi, macho yake yalikuwa yakiangalia huku na kule. Nyumba aliyokuwa ndani yake muda huo ilikuwa ileile ambayo aliambiwa na Aisha ndipo alipokuwa akiishi.
Alishangaa sana.
Aliangalia kila kitu ndani ya nyumba hiyo, hakika ilikuwa ni ileile. Moyo wake ukawa na shauku ya kutaka kufahamu ni kitu gani kilitokea kwani kwa kila kitu kilimchanganya moyoni mwake, hata suala la kwenda kazini kwake hakutaka mpaka pale ambapo angejua ukweli wa kilichokuwa kimetokea.
Mama Aisha akaingia chumbani kwake na kuwaacha wageni wake sebuleni, baada ya dakika kama mbili hivi, akarudi huku akiwa na albamu iliyokuwa na picha kadhaa na kuanza kumuonyesha Masalu.
“Aisha!” alijikuta akijisemea baada ya kuiona picha ya msichana mmoja mrembo ambaye alisimama mbele ya maua. Alimfahamu mtu huyo, alikuwa Aisha wake.
“Huyo ndiye Aisha,” alisema mama yake.
“Nilimuona!”
“Uliyemuona si Aisha huyu! Hukumuona mtu, ulimuona jini,” alisema mwanamke huyo.
“Inawezekana vipi?”
“Kwani ilikuwaje?”
Hapo sasa Masalu akapata nafasi ya kuanza kusimulia kila kitu kilichokuwa kimetokea tangu siku ya kwanza alipoonana na msichana huyo na kuzungumza naye, kumpenda na hatimaye siku moja kwenda nyumbani kwake.
Kila alichokuwa akikisimulia, halafu aliposema hakujua kama alikuwa jini, kila mmoja alishangaa! Lilikuwa jambo lisilowezekana mauzauza hayo yote yamtokee halafu hata asiwe na wasiwasi, yaani asigundue kama kulikuwa na kitu.
“Nini kilimtokea Aisha?” aliuliza Masalu baada ya kuona kila mtu mule ndani akimshangaa kwa kutokugundua kama msichana huyo alikuwa jini.
“Aisha alifariki dunia mwaka 1999 mwezi wa saba kwa kugongwa na gari hapo Manzese,” alisema mama yake na kuendelea:
“Baada ya hapo mjomba wake akasema twende tukamzike kijijini kama mila zetu zinavyosema, ila baba yake akakataa kufanya hivyo, hivyo tukamzika kwenye makaburi ya hapahapa Mburahati!” alisimulia mwanamke huyo.
Kila mmoja alikuwa kimya akimsikiliza, walihitaji kujua nini hasa kilichotokea mpaka Aisha kuwatokea watu na kuwapeleka makaburini.
“Ikawaje baada ya hapo?” aliuliza mwanaume mmoja, Masalu alikuwa kimya tu, yaani bado akili yake haikuwa sawa.
“Sasa ndiyo nahisi hili jini likaanza kuwatokea watu. Kuna wanaume kadhaa waliokuwa wakitokewa na mwisho wa siku kupelekwa makaburini na kuanza kula michanga. Kwa kweli ninashangaa sana, nadhani ni kwa sababu ya kukataliwa mwili wake kuzikwa Tanga, hivyo kuna mauzauza huwa yanatokea,” alisema mwanamke huyo.
Alisimulia mambo mengi. Kila mtu aliyekuwa akisikiliza mahali hapo alishangaa. Kazi kubwa iliyokuwa ikifanywa na jini la Aisha ni kutisha watu tu, hakuwa akiwaua ama kuwapelekea matatizo yoyote yale, kazi yake ilikuwa ni kuwasumbua tu, kuwapelekesha na kuwapa mauzauza.
“Hebu subiri kwanza! Kwa maana hiyo huyu si mtu wa kwanza?” aliuliza jamaa mmoja.
“Ndiyo! Nililisema hilo kabla!”
“Ninachotaka kufahamu ni kitu kimoja mama! Kama huyu si wa kwanza, inamaana pia hatokuwa wa mwisho. Na mtu akiwa ametokewa hivi, nini kifanyike ili asitokewe?” aliuliza jamaa huyo.
“Subiri!”
Mwanamke huyo akainuka na kuelekea chumbani. Wageni wake wakabaki sebuleni, muda wote huo Masalu alikuwa kimya, ni kama alikuwa akifikiria yale yaliyokuwa yametokea, yalimtisha na kumuogopesha sana. Alikuwa na mkewe, akaingiwa na tamaa na kutaka kuwa na mwanamke mwingine, mwisho wa siku matokeo yake yakawa mabaya kama ilivyokuwa.
Mwanamke huyo hakuchukua dakika nyingi akarudi akiwa na unga fulani hivi na maji, akampa Masalu na kumwambia anywe, akafanya hivyo na kumsomea dua ndogo na baada ya hapo akamwambia kila kitu kingekuwa shwari kabisa, Aisha asingemtokea tena.
“Mama! Ninaogopa!” alisema Masali huku akimwangalia mama yake Aisha.
“Usiogope!”
“Mimi wa kula majani makaburini kweli?”
“Pole sana! Hutokea hayo! Usimtamani kila mwanamke mzuri unayekutana naye mtaani,” alisema mama Aisha na baaa ya hapo wageni hao wakaondoka mahali hapo.
Masalu akasindikizwa mpaka nyumbani kwake. Grace alipomuona mumewe akija na watu huku akionekana kama kutokuwa sawa akawa na hofu, akahisi kulikuwa na jambo baya lilimtokea, akawapokea na kumwangalia vizuri Masalu.
Ni kweli hakuwa sawa.
Akawauliza kilichotokea, akajibiwa kwamba ni matatizo tu ya kawaida, walimkuta akiwa amelala njiani, inaonekana alikuwa akiumwa. Hivyo akapelekwa chumbani na kutulia kitandani.
Hakuzungumza kitu chochote kile na kwa sababu watu wale walimwambia mkewe alikuwa mgonjwa, naye akaigiza hivyohivyo kiugonjwaugonjwa na kulala huku moyoni mwake akijiapiza kwamba mpaka atakapokufa hatochukua tena mwanamke njiani kama alivyofanya kwa Aisha.
Kutokana na hofu nzito aliyokuwanayo moyoni, hakutaka kurudia kupitia njia ile ya makaburini, akaamua kubadilisha na kupita barabarani.
Masalu akabadilika kabisa. Kila siku alikuwa akimfikiria Aisha, alimuogopa mwanamke huyo, japokuwa alikuwa akimpenda kipindi cha nyuma lakini hakutaka kuonana naye tena kwenye maisha yake.
Akabadilika!
Akaachana na mambo ya wanawake.
Akatulia na mkewe mpaka leo hii.

MWISHO.
 
Masalu bhana, nimemaliza
SEHEMU YA 09.

Hawakuchukua muda mrefu kufika nyumbani kwa akina Aisha. Mama’ake Aisha alipomuona Masalu tu akajua alikuwa ndiye mwanaume aliyekutwa makaburini, juu ya kaburi la marehemu binti yake. Alipomwangalia tu, kwa jinsi alivyokuwa, alikuwa tofauti na wenzake.
Akawakaribisha na kuingia ndani. Umati wa watu uliokuwa ukiwafuatilia ulibaki nje. Kila mtu alitaka kufahamu kilichokuwa kimetokea, ilikuwaje huyo mwanaume akae pale makaburini na kula majani? Halafu hakuwa peke yake, kulikuwa na wanaume ambao waliwahi kukutwa palepale makaburini kama yeye.
Masalu akakaa kwenye kochi, macho yake yalikuwa yakiangalia huku na kule. Nyumba aliyokuwa ndani yake muda huo ilikuwa ileile ambayo aliambiwa na Aisha ndipo alipokuwa akiishi.
Alishangaa sana.
Aliangalia kila kitu ndani ya nyumba hiyo, hakika ilikuwa ni ileile. Moyo wake ukawa na shauku ya kutaka kufahamu ni kitu gani kilitokea kwani kwa kila kitu kilimchanganya moyoni mwake, hata suala la kwenda kazini kwake hakutaka mpaka pale ambapo angejua ukweli wa kilichokuwa kimetokea.
Mama Aisha akaingia chumbani kwake na kuwaacha wageni wake sebuleni, baada ya dakika kama mbili hivi, akarudi huku akiwa na albamu iliyokuwa na picha kadhaa na kuanza kumuonyesha Masalu.
“Aisha!” alijikuta akijisemea baada ya kuiona picha ya msichana mmoja mrembo ambaye alisimama mbele ya maua. Alimfahamu mtu huyo, alikuwa Aisha wake.
“Huyo ndiye Aisha,” alisema mama yake.
“Nilimuona!”
“Uliyemuona si Aisha huyu! Hukumuona mtu, ulimuona jini,” alisema mwanamke huyo.
“Inawezekana vipi?”
“Kwani ilikuwaje?”
Hapo sasa Masalu akapata nafasi ya kuanza kusimulia kila kitu kilichokuwa kimetokea tangu siku ya kwanza alipoonana na msichana huyo na kuzungumza naye, kumpenda na hatimaye siku moja kwenda nyumbani kwake.
Kila alichokuwa akikisimulia, halafu aliposema hakujua kama alikuwa jini, kila mmoja alishangaa! Lilikuwa jambo lisilowezekana mauzauza hayo yote yamtokee halafu hata asiwe na wasiwasi, yaani asigundue kama kulikuwa na kitu.
“Nini kilimtokea Aisha?” aliuliza Masalu baada ya kuona kila mtu mule ndani akimshangaa kwa kutokugundua kama msichana huyo alikuwa jini.
“Aisha alifariki dunia mwaka 1999 mwezi wa saba kwa kugongwa na gari hapo Manzese,” alisema mama yake na kuendelea:
“Baada ya hapo mjomba wake akasema twende tukamzike kijijini kama mila zetu zinavyosema, ila baba yake akakataa kufanya hivyo, hivyo tukamzika kwenye makaburi ya hapahapa Mburahati!” alisimulia mwanamke huyo.
Kila mmoja alikuwa kimya akimsikiliza, walihitaji kujua nini hasa kilichotokea mpaka Aisha kuwatokea watu na kuwapeleka makaburini.
“Ikawaje baada ya hapo?” aliuliza mwanaume mmoja, Masalu alikuwa kimya tu, yaani bado akili yake haikuwa sawa.
“Sasa ndiyo nahisi hili jini likaanza kuwatokea watu. Kuna wanaume kadhaa waliokuwa wakitokewa na mwisho wa siku kupelekwa makaburini na kuanza kula michanga. Kwa kweli ninashangaa sana, nadhani ni kwa sababu ya kukataliwa mwili wake kuzikwa Tanga, hivyo kuna mauzauza huwa yanatokea,” alisema mwanamke huyo.
Alisimulia mambo mengi. Kila mtu aliyekuwa akisikiliza mahali hapo alishangaa. Kazi kubwa iliyokuwa ikifanywa na jini la Aisha ni kutisha watu tu, hakuwa akiwaua ama kuwapelekea matatizo yoyote yale, kazi yake ilikuwa ni kuwasumbua tu, kuwapelekesha na kuwapa mauzauza.
“Hebu subiri kwanza! Kwa maana hiyo huyu si mtu wa kwanza?” aliuliza jamaa mmoja.
“Ndiyo! Nililisema hilo kabla!”
“Ninachotaka kufahamu ni kitu kimoja mama! Kama huyu si wa kwanza, inamaana pia hatokuwa wa mwisho. Na mtu akiwa ametokewa hivi, nini kifanyike ili asitokewe?” aliuliza jamaa huyo.
“Subiri!”
Mwanamke huyo akainuka na kuelekea chumbani. Wageni wake wakabaki sebuleni, muda wote huo Masalu alikuwa kimya, ni kama alikuwa akifikiria yale yaliyokuwa yametokea, yalimtisha na kumuogopesha sana. Alikuwa na mkewe, akaingiwa na tamaa na kutaka kuwa na mwanamke mwingine, mwisho wa siku matokeo yake yakawa mabaya kama ilivyokuwa.
Mwanamke huyo hakuchukua dakika nyingi akarudi akiwa na unga fulani hivi na maji, akampa Masalu na kumwambia anywe, akafanya hivyo na kumsomea dua ndogo na baada ya hapo akamwambia kila kitu kingekuwa shwari kabisa, Aisha asingemtokea tena.
“Mama! Ninaogopa!” alisema Masali huku akimwangalia mama yake Aisha.
“Usiogope!”
“Mimi wa kula majani makaburini kweli?”
“Pole sana! Hutokea hayo! Usimtamani kila mwanamke mzuri unayekutana naye mtaani,” alisema mama Aisha na baaa ya hapo wageni hao wakaondoka mahali hapo.
Masalu akasindikizwa mpaka nyumbani kwake. Grace alipomuona mumewe akija na watu huku akionekana kama kutokuwa sawa akawa na hofu, akahisi kulikuwa na jambo baya lilimtokea, akawapokea na kumwangalia vizuri Masalu.
Ni kweli hakuwa sawa.
Akawauliza kilichotokea, akajibiwa kwamba ni matatizo tu ya kawaida, walimkuta akiwa amelala njiani, inaonekana alikuwa akiumwa. Hivyo akapelekwa chumbani na kutulia kitandani.
Hakuzungumza kitu chochote kile na kwa sababu watu wale walimwambia mkewe alikuwa mgonjwa, naye akaigiza hivyohivyo kiugonjwaugonjwa na kulala huku moyoni mwake akijiapiza kwamba mpaka atakapokufa hatochukua tena mwanamke njiani kama alivyofanya kwa Aisha.
Kutokana na hofu nzito aliyokuwanayo moyoni, hakutaka kurudia kupitia njia ile ya makaburini, akaamua kubadilisha na kupita barabarani.
Masalu akabadilika kabisa. Kila siku alikuwa akimfikiria Aisha, alimuogopa mwanamke huyo, japokuwa alikuwa akimpenda kipindi cha nyuma lakini hakutaka kuonana naye tena kwenye maisha yake.
Akabadilika!
Akaachana na mambo ya wanawake.
Akatulia na mkewe mpaka leo hii.

MWISHO.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom