Simulizi: Harakati za maisha

SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

Nilirudi ofisini kwangu nikaendelea na mishe zangu huku akili fulani ikinijia , kiufupi sikuwa mtulivu,

Shabani bwana, Sasa imekuwaje anataka kuuza chombo ya wife wake tena kibabe, hizi ndoa hizi MUNGU atusaidie sana.
Ila hii gari nauza ugomvi wao Mimi haunihusu , kwanza ngoja nimpigie yule mwalimu siku nyingi ananisumbua magari ya taasisi yetu yatauzwa lini ili naye aweze kupata usafiri Sasa ngoja nimpe hii.
Nikampigia simu........

Hello Madam, naitwa Daniel ni yule uliniagiza nikufanyie mpango wa gari ,na nimeshapata,ipo ni nzuri haijatembea kabisa na bei ni rafiki.
Niliongea kwa mbwembwe huku nikiona pale ningepata hela nijuavyo wanawake wengi wakihitaji kitu huwa hawarudi nyuma na huwa si wabishi kwenye kupatana bei kama sisi wanaume.

Mmmh mwanangu,kwanza pole sana mimi nilishapata gari siku si nyingi.halafu pia ile Cruiser uliyomuuzia mume wangu, kipindi kile ilimsumbua sana tena mno si tukashangaa gari gani haipandi milima,muinuko kidogo tu inashindwa!! Kiufupi mwanangu ulivyokuwa unasifia chombo na kilivyo ni tofauti,ilibidi tuingie gharama zingine kufanya overall Engine na gharama zingine kama Pump na vitu vingine vingi .kiufupi Mr alikunyamazia tu lakini alichukia.
alijibu kisha tukaagana huku nikiona aibu fulani hivi

Niliendelea kuwasaka watu nikiwapigiapigia lakini hakuna hata mmoja niliyefanikiwa kumuweka kwenye ramani.

Niliacha mtumbwi wangu pale ofisini ,nikapanda chombo kipya,lengo nikaweke kwenye gereji iliyopo karibu na nyumbani kwangu halafu nitafute wateja taratibu,maana maeneo ya mjini majamaa wengi wangeingia tamaa ili tuanze kuwa na chain ndefu kwenye mgawanyo wa mshiko.
Huyoooo mpaka nyumbani kwangu.

Mke wangu licha ya kuona usafiri mpya ,hakuuliza chochote wala kushughulika na mimi.
Huwa ni mtu wa kuuliza haswa ukiwa na kitu ambacho si chetu lakini siku hiyo akawa kimya nilishangaa sana.

Nikiwa pale nje napekuapekua simu ili nione kama kuna mtu ataweza kuwa na utayari kwa ajili ya lile gari lakini nilichemka.

Baada ya muda kidogo,kuna watu wawili walikuja pale home,
Nawafahamu ni wasumbufu , hawajui kukataliwa ni kama hawakuwa na akili nzuri kwa mtazamo wangu

Vipi wazee ,
Usiku huu mnakuja kwenye majumba ya watu,hampigi simu ,hamtoi taarifa vipi, huu ni muda mtu anahitaji kupumzika baada ya shughuli za kutwa nzima eenh ,hebu jirekebisheni basi nyinyi ni watu wazima hakuna haja ya kusemana kama watoto.

Eeh mna shida gani,hebu tuingie ndani kwanza,niliongea huku nikiwa nishawachoka.

Sasa bro kwanza tusamehe upo sahihi kwa ulichoongea ,na tukiri wazi tumekosea.ila tumekuja kukuomba msaada wa Jersey kwaajili ya timu yetu ambayo ni kama yako eeeh.
Kifupi tumejichanga pale mtaani tumepata kukidhi vitu kadhaa laini tulitaka utusaidie suala la jezi tu .
aliweka kituo yule jamaa.

Ndugu zangu kwanza napenda niwaweke wazi tu kuwa mimi sina hela kama mnavyofikiria pengine muonekano wangu huwafanya watu wadhani nina kitu mimi ni kama nyinyi tu,tunaishi kiujanja ujanja.
Majukumu ni mengi nashindwa hadi kutimiza baadhi ya vitu.

Halafuuu mnamkumbuka yule mzee Mhindi mswahili mwenye Land Rover?niliuliza

Si yule alikuwa anasimama pale uwanjani ukawa unaongea naye mara nyingi huku akionesha anapenda mpira? waliuliza na wao.

Yes ni yule yule ,
Yule mzee ana hela sana tena mkiongea naye kwa adabu na utulivu atawaelewa.ni shabiki mwenzangu wa Arsenal ya Uingereza,yaani timu yetu licha ya kufanya vibaya kwa misimu kadhaa lakini tutakufa nayo.
Ila kwa suala la pesa nipo vibaya nisiwadanganye.niliweka kituo.

Aaaaaah bro muogope Mungu Brevis ina maganda kabisa hii halafu unasema upo vibaya ,na umeikata lini hii ? Aliuliza yule jamaa mwingine.

Huwezi amini hii siyo yangu kuna jamaa kanipa inasukumwa hii,watu wanataka kufanya mambo mengine tena.niliongea huku tukiizunguka .

Ok sawa kuna demu anataka gari ya mkononi kama hii tena alisema anataka chombo isiwe na matatizo,hii ingemfaa sana hii.

Ana hela ?mimi wanawake wengi nawajua wanalialia sana kwenye biashara wanatakaga kuonewa huruma kila eneo.nilitahadharisha.

Demu yupo vizuri,
tena kama vipi tukupe namba zake muongee wenyewe kwa muda wenu .
Sisi hatutaki shilingi mia yako,ila tunakuombea ufanikishe ili utununulie Jersey tu basi.waliongea huku tukipeana tano na kucheka kisha wakaondoka.

Kwani mume wangu hawa siku zote huwa wanafuata nini hapa? Aliuliza mke wangu.

Si wale watu wa michezo,yaani ni wasumbufu kama nini ,mtu hata ukatae jambo hawajui.nilijibu.

Siku nyingine muwe mnaongelea mambo yenu sehemu nyingine, siyo hapa ,nyumba inakuwa na makelele kama wodi ya watoto,watu mnacheeeka mnagonga mikono hamjui kama ni kero kwa wengine.
Mambo yenu sitaki ndani mwangu leo iwe mara ya kwanza na ya mwisho.aliweka kituo.

Nisamehe mke wangu wala usijali hata hivyo niliwaambia na mimi kwanini waje bila kupiga simu,nilijibu.

Na hiyo gari ni ya nani?
Aliuliza.

Ni ya mshikaji wangu fulani nimeazima yangu imeharibika nimeiacha ofisini .nilidanganya.

Babaaaa wewe una matatizo kama nini,na nimewasikia vizuri kuwa unauza hilo gari sasa kuwa na tahadhari na hiki chombo sitaki kilale
Hapa,na sijui kwanini huwa hukomi tu ,mtu una matatizo chungu mzima lakini bado hujifunzi,huwazi.
akionesha kuchukia.

Sasa usiku huu mimi chombo nitapeleka wapi usiku huu ,subiri asubuhi mimi naondoka nayo wala usijali.nilijibu kisha mambo mengine yakaendelea.

Asubuhi na mapema nilipokea simu kutoka kwa Lewis akinitaarifu jambo.

Shalom mtumishi ,kwanza namshukuru Mungu kwa kutupa kibali tena cha kuongea kwa mara nyingine hakika atukuzwe Mungu.aliongea Lewis ambaye ni mchungaji.

Eeeh kaka nipe taarifa kwanza maana simu yako ni muhimu nilikuwa naisubiri.niliongea kwa sauti ya chini.

Ndugu yetu siku ya leo ataletwa tena mahakamani kwa mujibu wa kanuni sheria akitokea gerezani,
Kwa hiyo sisi ndiyo tunajiandaa kwenda huko muda si mrefu.hivyo tulitaka kujua kama utaungana na sisi kwakuwa ulionesha nia ya kutaka kuwa karibu na sisi . aliweka kituo akinisikiliza.

Hapana mimi huko sitakuja ila nitakuwezesha chochote kitu kwakuwa kwasasa najua mambo yenu mengi yamesimama hayaendi .niliongea huku nikifanya kama nilivyoahidi huku nikingoja feed back kutoka kwa Pastor Lewis.

Nikiwa ofisini nilipiga namba fulani ambayo nilipewa na jamaa zangu ,simu ikapokelewa.

Nani mwenzangu,sauti upande wa pili ilisikika.

Nilijitambulisha huku nikisema shida yangu .

Samahani wewe ni dalali?
aliuliza yule dada ambaye sikuwa nimemuona.

Mimi siyo dalali na hizo siyo kazi zangu,bali kuna jamaa yangu kakwama na hayupo hapa yupo mbali hivyo kaniambia nimsaidie kutafuta wateja nilijibu

Ok ok safi,nataka gari ya maana iwe nzima ,sitaki chombo kiwe kinasumbua kila mara tutagombana ujue na kama una nafasi leo leo nakuja nione.aliongea huku nikigundua anaonekana mchangamfu sana.

Wewe ukiiona tu naamini utaipenda
Iko vizuri sana.nilijibu huku nikigonga meza nikitambua maisha lazima yaendelee.

Niliwahi kutoka huku tukiwasiliana na yule dada kila mara ili tukutane aone chombo kisha tufanye biashara.

Saa kumi na moja nilikuwa kwenye gereji tulivu isiyokuwa na makelele sehemu ambapo napaamini huku nikimngoja yule mgeni wangu

Nilishangaa akija na watu watatu wengine yeye wanne, wanawake wenzie wawili na mwanaume mmoja kutoka na mavazi yake nilijua huyu ni fundi maana alikuwa anatoka kwenye kampuni fulani ya motors . tulisalimiana huku akionekana si haba pesa ndogo ndogo hazimpigi chenga maana kuanzia mkoba ,nguo zake viatu na Cheni ndogo ya silver aliyovaa shingoni ilikuwa si haba unaweza kupata kiwanja pembeni ya mji huku Uwepo wa Convoy ya watu sikupenda mimi nilijua anakuja mwenyewe.

Naitwa Neema jina nililopewa na wazazi wangu, ila hapa mjini naitwa
Grace , maana ni ileile usijali kaka yangu . Dada alikuwa muongeaji kupita maelezo

Sasa kaka Daniiii hii gari ni mpya mimi nitaiweza kweli? Mimi nilitaka ile very cheap niwe na afford bei lakini hiiiiii no no no no.aliongea kwa kujishauwa yule dada

Lakini wale mashoga zake walidai anisikilize huenda tutaelewana ,kisha baada ya kumtajia bei ndipo alipopata nguvu ya kuizunguka kuiangalia vizuri huku nikifungua milango kwa mbwembwe ili awe na imani na amani nayo

Mmmmmh whaaat, ni kweli au macho yanguuuuu,mbona kama hii gari naifahamu,hii si gari ya mama Moo hii,yes ni yenyewe bwaanah, ni wiki moja imepita alinikuta maeneo ya kiluvya akanipa lift.alishtuka yule dada akiongea kwa kubana pua huku mimi nikishangaa .

Mama Moo ni nani wewe dada,
Hii gari kanipa mshikaji wangu anaitwa Shabani na yupo Mkoa Sasa hivi kaniambia nimuuzie.
Niliongea kwa kujiamini .

Sasa Shabani si ndiye mume wa mama Moo . Kisha akawageukia
Wale wenzie , jamani
Ile habari ya ugomvi wa shoga yangu aliyenyang'anywa gari na mumewe juzi niliyowaambia Sasa gari ni hii ,

Shabani anafanya biashara ya mazao yaani nafaka zote, Sasa kwakuwa anakuwa ofisini kwake kwahiyo show nzima huwa anasimamia mkewe,Sasa baada ya mke kununua gari Shabani alishtuka ndipo alipoichungulia account na kukuta Haina kitu na mwanamke kajenga nyumba kuuuuubwa wapi huko sijui ,na pia akajizawadia na gari

hii gari wala si ya muda mrefu mimi ndiye nilimshauri anunue baada ya kuwa kakamilisha ujenzi wa nyumba yake aliyojenga bila mumewe kujua.

Kumbe ndiyo maana shoga yangu Leo mnyooonge , kwenda polisi anashindwa ,gari hajui ilipo na Shabani kaenda Mkoa kufuata mazao safari kaenda mwenyewe, Sasa shoga yangu yupo katikati. Hajui afanyaje.

Weeeee tuondoke jamani hii gari ya moto , kaka Mimi biashara nimeshindwa kama ni hii gari tafuta mteja mwingine. Aliongea yule dada huku wakigonga mikono na mashoga zake wakiingia kwenye gari la kampuni aliyotoka yule fundi wakaishia huku nikishika tama nisijue Cha kufanya.

Jifunze,
Elimika.
Burudika.

Itaendelea......................
Dani,Dani!!
Sijui km utachomoka hapo.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

Nilirudi ofisini kwangu nikaendelea na mishe zangu huku akili fulani ikinijia , kiufupi sikuwa mtulivu,

Shabani bwana, Sasa imekuwaje anataka kuuza chombo ya wife wake tena kibabe, hizi ndoa hizi MUNGU atusaidie sana.
Ila hii gari nauza ugomvi wao Mimi haunihusu , kwanza ngoja nimpigie yule mwalimu siku nyingi ananisumbua magari ya taasisi yetu yatauzwa lini ili naye aweze kupata usafiri Sasa ngoja nimpe hii.
Nikampigia simu........

Hello Madam, naitwa Daniel ni yule uliniagiza nikufanyie mpango wa gari ,na nimeshapata,ipo ni nzuri haijatembea kabisa na bei ni rafiki.
Niliongea kwa mbwembwe huku nikiona pale ningepata hela nijuavyo wanawake wengi wakihitaji kitu huwa hawarudi nyuma na huwa si wabishi kwenye kupatana bei kama sisi wanaume.

Mmmh mwanangu,kwanza pole sana mimi nilishapata gari siku si nyingi.halafu pia ile Cruiser uliyomuuzia mume wangu, kipindi kile ilimsumbua sana tena mno si tukashangaa gari gani haipandi milima,muinuko kidogo tu inashindwa!! Kiufupi mwanangu ulivyokuwa unasifia chombo na kilivyo ni tofauti,ilibidi tuingie gharama zingine kufanya overall Engine na gharama zingine kama Pump na vitu vingine vingi .kiufupi Mr alikunyamazia tu lakini alichukia.
alijibu kisha tukaagana huku nikiona aibu fulani hivi

Niliendelea kuwasaka watu nikiwapigiapigia lakini hakuna hata mmoja niliyefanikiwa kumuweka kwenye ramani.

Niliacha mtumbwi wangu pale ofisini ,nikapanda chombo kipya,lengo nikaweke kwenye gereji iliyopo karibu na nyumbani kwangu halafu nitafute wateja taratibu,maana maeneo ya mjini majamaa wengi wangeingia tamaa ili tuanze kuwa na chain ndefu kwenye mgawanyo wa mshiko.
Huyoooo mpaka nyumbani kwangu.

Mke wangu licha ya kuona usafiri mpya ,hakuuliza chochote wala kushughulika na mimi.
Huwa ni mtu wa kuuliza haswa ukiwa na kitu ambacho si chetu lakini siku hiyo akawa kimya nilishangaa sana.

Nikiwa pale nje napekuapekua simu ili nione kama kuna mtu ataweza kuwa na utayari kwa ajili ya lile gari lakini nilichemka.

Baada ya muda kidogo,kuna watu wawili walikuja pale home,
Nawafahamu ni wasumbufu , hawajui kukataliwa ni kama hawakuwa na akili nzuri kwa mtazamo wangu

Vipi wazee ,
Usiku huu mnakuja kwenye majumba ya watu,hampigi simu ,hamtoi taarifa vipi, huu ni muda mtu anahitaji kupumzika baada ya shughuli za kutwa nzima eenh ,hebu jirekebisheni basi nyinyi ni watu wazima hakuna haja ya kusemana kama watoto.

Eeh mna shida gani,hebu tuingie ndani kwanza,niliongea huku nikiwa nishawachoka.

Sasa bro kwanza tusamehe upo sahihi kwa ulichoongea ,na tukiri wazi tumekosea.ila tumekuja kukuomba msaada wa Jersey kwaajili ya timu yetu ambayo ni kama yako eeeh.
Kifupi tumejichanga pale mtaani tumepata kukidhi vitu kadhaa laini tulitaka utusaidie suala la jezi tu .
aliweka kituo yule jamaa.

Ndugu zangu kwanza napenda niwaweke wazi tu kuwa mimi sina hela kama mnavyofikiria pengine muonekano wangu huwafanya watu wadhani nina kitu mimi ni kama nyinyi tu,tunaishi kiujanja ujanja.
Majukumu ni mengi nashindwa hadi kutimiza baadhi ya vitu.

Halafuuu mnamkumbuka yule mzee Mhindi mswahili mwenye Land Rover?niliuliza

Si yule alikuwa anasimama pale uwanjani ukawa unaongea naye mara nyingi huku akionesha anapenda mpira? waliuliza na wao.

Yes ni yule yule ,
Yule mzee ana hela sana tena mkiongea naye kwa adabu na utulivu atawaelewa.ni shabiki mwenzangu wa Arsenal ya Uingereza,yaani timu yetu licha ya kufanya vibaya kwa misimu kadhaa lakini tutakufa nayo.
Ila kwa suala la pesa nipo vibaya nisiwadanganye.niliweka kituo.

Aaaaaah bro muogope Mungu Brevis ina maganda kabisa hii halafu unasema upo vibaya ,na umeikata lini hii ? Aliuliza yule jamaa mwingine.

Huwezi amini hii siyo yangu kuna jamaa kanipa inasukumwa hii,watu wanataka kufanya mambo mengine tena.niliongea huku tukiizunguka .

Ok sawa kuna demu anataka gari ya mkononi kama hii tena alisema anataka chombo isiwe na matatizo,hii ingemfaa sana hii.

Ana hela ?mimi wanawake wengi nawajua wanalialia sana kwenye biashara wanatakaga kuonewa huruma kila eneo.nilitahadharisha.

Demu yupo vizuri,
tena kama vipi tukupe namba zake muongee wenyewe kwa muda wenu .
Sisi hatutaki shilingi mia yako,ila tunakuombea ufanikishe ili utununulie Jersey tu basi.waliongea huku tukipeana tano na kucheka kisha wakaondoka.

Kwani mume wangu hawa siku zote huwa wanafuata nini hapa? Aliuliza mke wangu.

Si wale watu wa michezo,yaani ni wasumbufu kama nini ,mtu hata ukatae jambo hawajui.nilijibu.

Siku nyingine muwe mnaongelea mambo yenu sehemu nyingine, siyo hapa ,nyumba inakuwa na makelele kama wodi ya watoto,watu mnacheeeka mnagonga mikono hamjui kama ni kero kwa wengine.
Mambo yenu sitaki ndani mwangu leo iwe mara ya kwanza na ya mwisho.aliweka kituo.

Nisamehe mke wangu wala usijali hata hivyo niliwaambia na mimi kwanini waje bila kupiga simu,nilijibu.

Na hiyo gari ni ya nani?
Aliuliza.

Ni ya mshikaji wangu fulani nimeazima yangu imeharibika nimeiacha ofisini .nilidanganya.

Babaaaa wewe una matatizo kama nini,na nimewasikia vizuri kuwa unauza hilo gari sasa kuwa na tahadhari na hiki chombo sitaki kilale
Hapa,na sijui kwanini huwa hukomi tu ,mtu una matatizo chungu mzima lakini bado hujifunzi,huwazi.
akionesha kuchukia.

Sasa usiku huu mimi chombo nitapeleka wapi usiku huu ,subiri asubuhi mimi naondoka nayo wala usijali.nilijibu kisha mambo mengine yakaendelea.

Asubuhi na mapema nilipokea simu kutoka kwa Lewis akinitaarifu jambo.

Shalom mtumishi ,kwanza namshukuru Mungu kwa kutupa kibali tena cha kuongea kwa mara nyingine hakika atukuzwe Mungu.aliongea Lewis ambaye ni mchungaji.

Eeeh kaka nipe taarifa kwanza maana simu yako ni muhimu nilikuwa naisubiri.niliongea kwa sauti ya chini.

Ndugu yetu siku ya leo ataletwa tena mahakamani kwa mujibu wa kanuni sheria akitokea gerezani,
Kwa hiyo sisi ndiyo tunajiandaa kwenda huko muda si mrefu.hivyo tulitaka kujua kama utaungana na sisi kwakuwa ulionesha nia ya kutaka kuwa karibu na sisi . aliweka kituo akinisikiliza.

Hapana mimi huko sitakuja ila nitakuwezesha chochote kitu kwakuwa kwasasa najua mambo yenu mengi yamesimama hayaendi .niliongea huku nikifanya kama nilivyoahidi huku nikingoja feed back kutoka kwa Pastor Lewis.

Nikiwa ofisini nilipiga namba fulani ambayo nilipewa na jamaa zangu ,simu ikapokelewa.

Nani mwenzangu,sauti upande wa pili ilisikika.

Nilijitambulisha huku nikisema shida yangu .

Samahani wewe ni dalali?
aliuliza yule dada ambaye sikuwa nimemuona.

Mimi siyo dalali na hizo siyo kazi zangu,bali kuna jamaa yangu kakwama na hayupo hapa yupo mbali hivyo kaniambia nimsaidie kutafuta wateja nilijibu

Ok ok safi,nataka gari ya maana iwe nzima ,sitaki chombo kiwe kinasumbua kila mara tutagombana ujue na kama una nafasi leo leo nakuja nione.aliongea huku nikigundua anaonekana mchangamfu sana.

Wewe ukiiona tu naamini utaipenda
Iko vizuri sana.nilijibu huku nikigonga meza nikitambua maisha lazima yaendelee.

Niliwahi kutoka huku tukiwasiliana na yule dada kila mara ili tukutane aone chombo kisha tufanye biashara.

Saa kumi na moja nilikuwa kwenye gereji tulivu isiyokuwa na makelele sehemu ambapo napaamini huku nikimngoja yule mgeni wangu

Nilishangaa akija na watu watatu wengine yeye wanne, wanawake wenzie wawili na mwanaume mmoja kutoka na mavazi yake nilijua huyu ni fundi maana alikuwa anatoka kwenye kampuni fulani ya motors . tulisalimiana huku akionekana si haba pesa ndogo ndogo hazimpigi chenga maana kuanzia mkoba ,nguo zake viatu na Cheni ndogo ya silver aliyovaa shingoni ilikuwa si haba unaweza kupata kiwanja pembeni ya mji huku Uwepo wa Convoy ya watu sikupenda mimi nilijua anakuja mwenyewe.

Naitwa Neema jina nililopewa na wazazi wangu, ila hapa mjini naitwa
Grace , maana ni ileile usijali kaka yangu . Dada alikuwa muongeaji kupita maelezo

Sasa kaka Daniiii hii gari ni mpya mimi nitaiweza kweli? Mimi nilitaka ile very cheap niwe na afford bei lakini hiiiiii no no no no.aliongea kwa kujishauwa yule dada

Lakini wale mashoga zake walidai anisikilize huenda tutaelewana ,kisha baada ya kumtajia bei ndipo alipopata nguvu ya kuizunguka kuiangalia vizuri huku nikifungua milango kwa mbwembwe ili awe na imani na amani nayo

Mmmmmh whaaat, ni kweli au macho yanguuuuu,mbona kama hii gari naifahamu,hii si gari ya mama Moo hii,yes ni yenyewe bwaanah, ni wiki moja imepita alinikuta maeneo ya kiluvya akanipa lift.alishtuka yule dada akiongea kwa kubana pua huku mimi nikishangaa .

Mama Moo ni nani wewe dada,
Hii gari kanipa mshikaji wangu anaitwa Shabani na yupo Mkoa Sasa hivi kaniambia nimuuzie.
Niliongea kwa kujiamini .

Sasa Shabani si ndiye mume wa mama Moo . Kisha akawageukia
Wale wenzie , jamani
Ile habari ya ugomvi wa shoga yangu aliyenyang'anywa gari na mumewe juzi niliyowaambia Sasa gari ni hii ,

Shabani anafanya biashara ya mazao yaani nafaka zote, Sasa kwakuwa anakuwa ofisini kwake kwahiyo show nzima huwa anasimamia mkewe,Sasa baada ya mke kununua gari Shabani alishtuka ndipo alipoichungulia account na kukuta Haina kitu na mwanamke kajenga nyumba kuuuuubwa wapi huko sijui ,na pia akajizawadia na gari

hii gari wala si ya muda mrefu mimi ndiye nilimshauri anunue baada ya kuwa kakamilisha ujenzi wa nyumba yake aliyojenga bila mumewe kujua.

Kumbe ndiyo maana shoga yangu Leo mnyooonge , kwenda polisi anashindwa ,gari hajui ilipo na Shabani kaenda Mkoa kufuata mazao safari kaenda mwenyewe, Sasa shoga yangu yupo katikati. Hajui afanyaje.

Weeeee tuondoke jamani hii gari ya moto , kaka Mimi biashara nimeshindwa kama ni hii gari tafuta mteja mwingine. Aliongea yule dada huku wakigonga mikono na mashoga zake wakiingia kwenye gari la kampuni aliyotoka yule fundi wakaishia huku nikishika tama nisijue Cha kufanya.

Jifunze,
Elimika.
Burudika.

Itaendelea......................
Ngoja apeleke umbea ujaziwe nzi.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

Nilirudi ofisini kwangu nikaendelea na mishe zangu huku akili fulani ikinijia , kiufupi sikuwa mtulivu,

Shabani bwana, Sasa imekuwaje anataka kuuza chombo ya wife wake tena kibabe, hizi ndoa hizi MUNGU atusaidie sana.
Ila hii gari nauza ugomvi wao Mimi haunihusu , kwanza ngoja nimpigie yule mwalimu siku nyingi ananisumbua magari ya taasisi yetu yatauzwa lini ili naye aweze kupata usafiri Sasa ngoja nimpe hii.
Nikampigia simu........

Hello Madam, naitwa Daniel ni yule uliniagiza nikufanyie mpango wa gari ,na nimeshapata,ipo ni nzuri haijatembea kabisa na bei ni rafiki.
Niliongea kwa mbwembwe huku nikiona pale ningepata hela nijuavyo wanawake wengi wakihitaji kitu huwa hawarudi nyuma na huwa si wabishi kwenye kupatana bei kama sisi wanaume.

Mmmh mwanangu,kwanza pole sana mimi nilishapata gari siku si nyingi.halafu pia ile Cruiser uliyomuuzia mume wangu, kipindi kile ilimsumbua sana tena mno si tukashangaa gari gani haipandi milima,muinuko kidogo tu inashindwa!! Kiufupi mwanangu ulivyokuwa unasifia chombo na kilivyo ni tofauti,ilibidi tuingie gharama zingine kufanya overall Engine na gharama zingine kama Pump na vitu vingine vingi .kiufupi Mr alikunyamazia tu lakini alichukia.
alijibu kisha tukaagana huku nikiona aibu fulani hivi

Niliendelea kuwasaka watu nikiwapigiapigia lakini hakuna hata mmoja niliyefanikiwa kumuweka kwenye ramani.

Niliacha mtumbwi wangu pale ofisini ,nikapanda chombo kipya,lengo nikaweke kwenye gereji iliyopo karibu na nyumbani kwangu halafu nitafute wateja taratibu,maana maeneo ya mjini majamaa wengi wangeingia tamaa ili tuanze kuwa na chain ndefu kwenye mgawanyo wa mshiko.
Huyoooo mpaka nyumbani kwangu.

Mke wangu licha ya kuona usafiri mpya ,hakuuliza chochote wala kushughulika na mimi.
Huwa ni mtu wa kuuliza haswa ukiwa na kitu ambacho si chetu lakini siku hiyo akawa kimya nilishangaa sana.

Nikiwa pale nje napekuapekua simu ili nione kama kuna mtu ataweza kuwa na utayari kwa ajili ya lile gari lakini nilichemka.

Baada ya muda kidogo,kuna watu wawili walikuja pale home,
Nawafahamu ni wasumbufu , hawajui kukataliwa ni kama hawakuwa na akili nzuri kwa mtazamo wangu

Vipi wazee ,
Usiku huu mnakuja kwenye majumba ya watu,hampigi simu ,hamtoi taarifa vipi, huu ni muda mtu anahitaji kupumzika baada ya shughuli za kutwa nzima eenh ,hebu jirekebisheni basi nyinyi ni watu wazima hakuna haja ya kusemana kama watoto.

Eeh mna shida gani,hebu tuingie ndani kwanza,niliongea huku nikiwa nishawachoka.

Sasa bro kwanza tusamehe upo sahihi kwa ulichoongea ,na tukiri wazi tumekosea.ila tumekuja kukuomba msaada wa Jersey kwaajili ya timu yetu ambayo ni kama yako eeeh.
Kifupi tumejichanga pale mtaani tumepata kukidhi vitu kadhaa laini tulitaka utusaidie suala la jezi tu .
aliweka kituo yule jamaa.

Ndugu zangu kwanza napenda niwaweke wazi tu kuwa mimi sina hela kama mnavyofikiria pengine muonekano wangu huwafanya watu wadhani nina kitu mimi ni kama nyinyi tu,tunaishi kiujanja ujanja.
Majukumu ni mengi nashindwa hadi kutimiza baadhi ya vitu.

Halafuuu mnamkumbuka yule mzee Mhindi mswahili mwenye Land Rover?niliuliza

Si yule alikuwa anasimama pale uwanjani ukawa unaongea naye mara nyingi huku akionesha anapenda mpira? waliuliza na wao.

Yes ni yule yule ,
Yule mzee ana hela sana tena mkiongea naye kwa adabu na utulivu atawaelewa.ni shabiki mwenzangu wa Arsenal ya Uingereza,yaani timu yetu licha ya kufanya vibaya kwa misimu kadhaa lakini tutakufa nayo.
Ila kwa suala la pesa nipo vibaya nisiwadanganye.niliweka kituo.

Aaaaaah bro muogope Mungu Brevis ina maganda kabisa hii halafu unasema upo vibaya ,na umeikata lini hii ? Aliuliza yule jamaa mwingine.

Huwezi amini hii siyo yangu kuna jamaa kanipa inasukumwa hii,watu wanataka kufanya mambo mengine tena.niliongea huku tukiizunguka .

Ok sawa kuna demu anataka gari ya mkononi kama hii tena alisema anataka chombo isiwe na matatizo,hii ingemfaa sana hii.

Ana hela ?mimi wanawake wengi nawajua wanalialia sana kwenye biashara wanatakaga kuonewa huruma kila eneo.nilitahadharisha.

Demu yupo vizuri,
tena kama vipi tukupe namba zake muongee wenyewe kwa muda wenu .
Sisi hatutaki shilingi mia yako,ila tunakuombea ufanikishe ili utununulie Jersey tu basi.waliongea huku tukipeana tano na kucheka kisha wakaondoka.

Kwani mume wangu hawa siku zote huwa wanafuata nini hapa? Aliuliza mke wangu.

Si wale watu wa michezo,yaani ni wasumbufu kama nini ,mtu hata ukatae jambo hawajui.nilijibu.

Siku nyingine muwe mnaongelea mambo yenu sehemu nyingine, siyo hapa ,nyumba inakuwa na makelele kama wodi ya watoto,watu mnacheeeka mnagonga mikono hamjui kama ni kero kwa wengine.
Mambo yenu sitaki ndani mwangu leo iwe mara ya kwanza na ya mwisho.aliweka kituo.

Nisamehe mke wangu wala usijali hata hivyo niliwaambia na mimi kwanini waje bila kupiga simu,nilijibu.

Na hiyo gari ni ya nani?
Aliuliza.

Ni ya mshikaji wangu fulani nimeazima yangu imeharibika nimeiacha ofisini .nilidanganya.

Babaaaa wewe una matatizo kama nini,na nimewasikia vizuri kuwa unauza hilo gari sasa kuwa na tahadhari na hiki chombo sitaki kilale
Hapa,na sijui kwanini huwa hukomi tu ,mtu una matatizo chungu mzima lakini bado hujifunzi,huwazi.
akionesha kuchukia.

Sasa usiku huu mimi chombo nitapeleka wapi usiku huu ,subiri asubuhi mimi naondoka nayo wala usijali.nilijibu kisha mambo mengine yakaendelea.

Asubuhi na mapema nilipokea simu kutoka kwa Lewis akinitaarifu jambo.

Shalom mtumishi ,kwanza namshukuru Mungu kwa kutupa kibali tena cha kuongea kwa mara nyingine hakika atukuzwe Mungu.aliongea Lewis ambaye ni mchungaji.

Eeeh kaka nipe taarifa kwanza maana simu yako ni muhimu nilikuwa naisubiri.niliongea kwa sauti ya chini.

Ndugu yetu siku ya leo ataletwa tena mahakamani kwa mujibu wa kanuni sheria akitokea gerezani,
Kwa hiyo sisi ndiyo tunajiandaa kwenda huko muda si mrefu.hivyo tulitaka kujua kama utaungana na sisi kwakuwa ulionesha nia ya kutaka kuwa karibu na sisi . aliweka kituo akinisikiliza.

Hapana mimi huko sitakuja ila nitakuwezesha chochote kitu kwakuwa kwasasa najua mambo yenu mengi yamesimama hayaendi .niliongea huku nikifanya kama nilivyoahidi huku nikingoja feed back kutoka kwa Pastor Lewis.

Nikiwa ofisini nilipiga namba fulani ambayo nilipewa na jamaa zangu ,simu ikapokelewa.

Nani mwenzangu,sauti upande wa pili ilisikika.

Nilijitambulisha huku nikisema shida yangu .

Samahani wewe ni dalali?
aliuliza yule dada ambaye sikuwa nimemuona.

Mimi siyo dalali na hizo siyo kazi zangu,bali kuna jamaa yangu kakwama na hayupo hapa yupo mbali hivyo kaniambia nimsaidie kutafuta wateja nilijibu

Ok ok safi,nataka gari ya maana iwe nzima ,sitaki chombo kiwe kinasumbua kila mara tutagombana ujue na kama una nafasi leo leo nakuja nione.aliongea huku nikigundua anaonekana mchangamfu sana.

Wewe ukiiona tu naamini utaipenda
Iko vizuri sana.nilijibu huku nikigonga meza nikitambua maisha lazima yaendelee.

Niliwahi kutoka huku tukiwasiliana na yule dada kila mara ili tukutane aone chombo kisha tufanye biashara.

Saa kumi na moja nilikuwa kwenye gereji tulivu isiyokuwa na makelele sehemu ambapo napaamini huku nikimngoja yule mgeni wangu

Nilishangaa akija na watu watatu wengine yeye wanne, wanawake wenzie wawili na mwanaume mmoja kutoka na mavazi yake nilijua huyu ni fundi maana alikuwa anatoka kwenye kampuni fulani ya motors . tulisalimiana huku akionekana si haba pesa ndogo ndogo hazimpigi chenga maana kuanzia mkoba ,nguo zake viatu na Cheni ndogo ya silver aliyovaa shingoni ilikuwa si haba unaweza kupata kiwanja pembeni ya mji huku Uwepo wa Convoy ya watu sikupenda mimi nilijua anakuja mwenyewe.

Naitwa Neema jina nililopewa na wazazi wangu, ila hapa mjini naitwa
Grace , maana ni ileile usijali kaka yangu . Dada alikuwa muongeaji kupita maelezo

Sasa kaka Daniiii hii gari ni mpya mimi nitaiweza kweli? Mimi nilitaka ile very cheap niwe na afford bei lakini hiiiiii no no no no.aliongea kwa kujishauwa yule dada

Lakini wale mashoga zake walidai anisikilize huenda tutaelewana ,kisha baada ya kumtajia bei ndipo alipopata nguvu ya kuizunguka kuiangalia vizuri huku nikifungua milango kwa mbwembwe ili awe na imani na amani nayo

Mmmmmh whaaat, ni kweli au macho yanguuuuu,mbona kama hii gari naifahamu,hii si gari ya mama Moo hii,yes ni yenyewe bwaanah, ni wiki moja imepita alinikuta maeneo ya kiluvya akanipa lift.alishtuka yule dada akiongea kwa kubana pua huku mimi nikishangaa .

Mama Moo ni nani wewe dada,
Hii gari kanipa mshikaji wangu anaitwa Shabani na yupo Mkoa Sasa hivi kaniambia nimuuzie.
Niliongea kwa kujiamini .

Sasa Shabani si ndiye mume wa mama Moo . Kisha akawageukia
Wale wenzie , jamani
Ile habari ya ugomvi wa shoga yangu aliyenyang'anywa gari na mumewe juzi niliyowaambia Sasa gari ni hii ,

Shabani anafanya biashara ya mazao yaani nafaka zote, Sasa kwakuwa anakuwa ofisini kwake kwahiyo show nzima huwa anasimamia mkewe,Sasa baada ya mke kununua gari Shabani alishtuka ndipo alipoichungulia account na kukuta Haina kitu na mwanamke kajenga nyumba kuuuuubwa wapi huko sijui ,na pia akajizawadia na gari

hii gari wala si ya muda mrefu mimi ndiye nilimshauri anunue baada ya kuwa kakamilisha ujenzi wa nyumba yake aliyojenga bila mumewe kujua.

Kumbe ndiyo maana shoga yangu Leo mnyooonge , kwenda polisi anashindwa ,gari hajui ilipo na Shabani kaenda Mkoa kufuata mazao safari kaenda mwenyewe, Sasa shoga yangu yupo katikati. Hajui afanyaje.

Weeeee tuondoke jamani hii gari ya moto , kaka Mimi biashara nimeshindwa kama ni hii gari tafuta mteja mwingine. Aliongea yule dada huku wakigonga mikono na mashoga zake wakiingia kwenye gari la kampuni aliyotoka yule fundi wakaishia huku nikishika tama nisijue Cha kufanya.

Jifunze,
Elimika.
Burudika.

Itaendelea......................
Mzee wa Majanga 7 kila siku janga jipya
 
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

Nilirudi ofisini kwangu nikaendelea na mishe zangu huku akili fulani ikinijia , kiufupi sikuwa mtulivu,

Shabani bwana, Sasa imekuwaje anataka kuuza chombo ya wife wake tena kibabe, hizi ndoa hizi MUNGU atusaidie sana.
Ila hii gari nauza ugomvi wao Mimi haunihusu , kwanza ngoja nimpigie yule mwalimu siku nyingi ananisumbua magari ya taasisi yetu yatauzwa lini ili naye aweze kupata usafiri Sasa ngoja nimpe hii.
Nikampigia simu........

Hello Madam, naitwa Daniel ni yule uliniagiza nikufanyie mpango wa gari ,na nimeshapata,ipo ni nzuri haijatembea kabisa na bei ni rafiki.
Niliongea kwa mbwembwe huku nikiona pale ningepata hela nijuavyo wanawake wengi wakihitaji kitu huwa hawarudi nyuma na huwa si wabishi kwenye kupatana bei kama sisi wanaume.

Mmmh mwanangu,kwanza pole sana mimi nilishapata gari siku si nyingi.halafu pia ile Cruiser uliyomuuzia mume wangu, kipindi kile ilimsumbua sana tena mno si tukashangaa gari gani haipandi milima,muinuko kidogo tu inashindwa!! Kiufupi mwanangu ulivyokuwa unasifia chombo na kilivyo ni tofauti,ilibidi tuingie gharama zingine kufanya overall Engine na gharama zingine kama Pump na vitu vingine vingi .kiufupi Mr alikunyamazia tu lakini alichukia.
alijibu kisha tukaagana huku nikiona aibu fulani hivi

Niliendelea kuwasaka watu nikiwapigiapigia lakini hakuna hata mmoja niliyefanikiwa kumuweka kwenye ramani.

Niliacha mtumbwi wangu pale ofisini ,nikapanda chombo kipya,lengo nikaweke kwenye gereji iliyopo karibu na nyumbani kwangu halafu nitafute wateja taratibu,maana maeneo ya mjini majamaa wengi wangeingia tamaa ili tuanze kuwa na chain ndefu kwenye mgawanyo wa mshiko.
Huyoooo mpaka nyumbani kwangu.

Mke wangu licha ya kuona usafiri mpya ,hakuuliza chochote wala kushughulika na mimi.
Huwa ni mtu wa kuuliza haswa ukiwa na kitu ambacho si chetu lakini siku hiyo akawa kimya nilishangaa sana.

Nikiwa pale nje napekuapekua simu ili nione kama kuna mtu ataweza kuwa na utayari kwa ajili ya lile gari lakini nilichemka.

Baada ya muda kidogo,kuna watu wawili walikuja pale home,
Nawafahamu ni wasumbufu , hawajui kukataliwa ni kama hawakuwa na akili nzuri kwa mtazamo wangu

Vipi wazee ,
Usiku huu mnakuja kwenye majumba ya watu,hampigi simu ,hamtoi taarifa vipi, huu ni muda mtu anahitaji kupumzika baada ya shughuli za kutwa nzima eenh ,hebu jirekebisheni basi nyinyi ni watu wazima hakuna haja ya kusemana kama watoto.

Eeh mna shida gani,hebu tuingie ndani kwanza,niliongea huku nikiwa nishawachoka.

Sasa bro kwanza tusamehe upo sahihi kwa ulichoongea ,na tukiri wazi tumekosea.ila tumekuja kukuomba msaada wa Jersey kwaajili ya timu yetu ambayo ni kama yako eeeh.
Kifupi tumejichanga pale mtaani tumepata kukidhi vitu kadhaa laini tulitaka utusaidie suala la jezi tu .
aliweka kituo yule jamaa.

Ndugu zangu kwanza napenda niwaweke wazi tu kuwa mimi sina hela kama mnavyofikiria pengine muonekano wangu huwafanya watu wadhani nina kitu mimi ni kama nyinyi tu,tunaishi kiujanja ujanja.
Majukumu ni mengi nashindwa hadi kutimiza baadhi ya vitu.

Halafuuu mnamkumbuka yule mzee Mhindi mswahili mwenye Land Rover?niliuliza

Si yule alikuwa anasimama pale uwanjani ukawa unaongea naye mara nyingi huku akionesha anapenda mpira? waliuliza na wao.

Yes ni yule yule ,
Yule mzee ana hela sana tena mkiongea naye kwa adabu na utulivu atawaelewa.ni shabiki mwenzangu wa Arsenal ya Uingereza,yaani timu yetu licha ya kufanya vibaya kwa misimu kadhaa lakini tutakufa nayo.
Ila kwa suala la pesa nipo vibaya nisiwadanganye.niliweka kituo.

Aaaaaah bro muogope Mungu Brevis ina maganda kabisa hii halafu unasema upo vibaya ,na umeikata lini hii ? Aliuliza yule jamaa mwingine.

Huwezi amini hii siyo yangu kuna jamaa kanipa inasukumwa hii,watu wanataka kufanya mambo mengine tena.niliongea huku tukiizunguka .

Ok sawa kuna demu anataka gari ya mkononi kama hii tena alisema anataka chombo isiwe na matatizo,hii ingemfaa sana hii.

Ana hela ?mimi wanawake wengi nawajua wanalialia sana kwenye biashara wanatakaga kuonewa huruma kila eneo.nilitahadharisha.

Demu yupo vizuri,
tena kama vipi tukupe namba zake muongee wenyewe kwa muda wenu .
Sisi hatutaki shilingi mia yako,ila tunakuombea ufanikishe ili utununulie Jersey tu basi.waliongea huku tukipeana tano na kucheka kisha wakaondoka.

Kwani mume wangu hawa siku zote huwa wanafuata nini hapa? Aliuliza mke wangu.

Si wale watu wa michezo,yaani ni wasumbufu kama nini ,mtu hata ukatae jambo hawajui.nilijibu.

Siku nyingine muwe mnaongelea mambo yenu sehemu nyingine, siyo hapa ,nyumba inakuwa na makelele kama wodi ya watoto,watu mnacheeeka mnagonga mikono hamjui kama ni kero kwa wengine.
Mambo yenu sitaki ndani mwangu leo iwe mara ya kwanza na ya mwisho.aliweka kituo.

Nisamehe mke wangu wala usijali hata hivyo niliwaambia na mimi kwanini waje bila kupiga simu,nilijibu.

Na hiyo gari ni ya nani?
Aliuliza.

Ni ya mshikaji wangu fulani nimeazima yangu imeharibika nimeiacha ofisini .nilidanganya.

Babaaaa wewe una matatizo kama nini,na nimewasikia vizuri kuwa unauza hilo gari sasa kuwa na tahadhari na hiki chombo sitaki kilale
Hapa,na sijui kwanini huwa hukomi tu ,mtu una matatizo chungu mzima lakini bado hujifunzi,huwazi.
akionesha kuchukia.

Sasa usiku huu mimi chombo nitapeleka wapi usiku huu ,subiri asubuhi mimi naondoka nayo wala usijali.nilijibu kisha mambo mengine yakaendelea.

Asubuhi na mapema nilipokea simu kutoka kwa Lewis akinitaarifu jambo.

Shalom mtumishi ,kwanza namshukuru Mungu kwa kutupa kibali tena cha kuongea kwa mara nyingine hakika atukuzwe Mungu.aliongea Lewis ambaye ni mchungaji.

Eeeh kaka nipe taarifa kwanza maana simu yako ni muhimu nilikuwa naisubiri.niliongea kwa sauti ya chini.

Ndugu yetu siku ya leo ataletwa tena mahakamani kwa mujibu wa kanuni sheria akitokea gerezani,
Kwa hiyo sisi ndiyo tunajiandaa kwenda huko muda si mrefu.hivyo tulitaka kujua kama utaungana na sisi kwakuwa ulionesha nia ya kutaka kuwa karibu na sisi . aliweka kituo akinisikiliza.

Hapana mimi huko sitakuja ila nitakuwezesha chochote kitu kwakuwa kwasasa najua mambo yenu mengi yamesimama hayaendi .niliongea huku nikifanya kama nilivyoahidi huku nikingoja feed back kutoka kwa Pastor Lewis.

Nikiwa ofisini nilipiga namba fulani ambayo nilipewa na jamaa zangu ,simu ikapokelewa.

Nani mwenzangu,sauti upande wa pili ilisikika.

Nilijitambulisha huku nikisema shida yangu .

Samahani wewe ni dalali?
aliuliza yule dada ambaye sikuwa nimemuona.

Mimi siyo dalali na hizo siyo kazi zangu,bali kuna jamaa yangu kakwama na hayupo hapa yupo mbali hivyo kaniambia nimsaidie kutafuta wateja nilijibu

Ok ok safi,nataka gari ya maana iwe nzima ,sitaki chombo kiwe kinasumbua kila mara tutagombana ujue na kama una nafasi leo leo nakuja nione.aliongea huku nikigundua anaonekana mchangamfu sana.

Wewe ukiiona tu naamini utaipenda
Iko vizuri sana.nilijibu huku nikigonga meza nikitambua maisha lazima yaendelee.

Niliwahi kutoka huku tukiwasiliana na yule dada kila mara ili tukutane aone chombo kisha tufanye biashara.

Saa kumi na moja nilikuwa kwenye gereji tulivu isiyokuwa na makelele sehemu ambapo napaamini huku nikimngoja yule mgeni wangu

Nilishangaa akija na watu watatu wengine yeye wanne, wanawake wenzie wawili na mwanaume mmoja kutoka na mavazi yake nilijua huyu ni fundi maana alikuwa anatoka kwenye kampuni fulani ya motors . tulisalimiana huku akionekana si haba pesa ndogo ndogo hazimpigi chenga maana kuanzia mkoba ,nguo zake viatu na Cheni ndogo ya silver aliyovaa shingoni ilikuwa si haba unaweza kupata kiwanja pembeni ya mji huku Uwepo wa Convoy ya watu sikupenda mimi nilijua anakuja mwenyewe.

Naitwa Neema jina nililopewa na wazazi wangu, ila hapa mjini naitwa
Grace , maana ni ileile usijali kaka yangu . Dada alikuwa muongeaji kupita maelezo

Sasa kaka Daniiii hii gari ni mpya mimi nitaiweza kweli? Mimi nilitaka ile very cheap niwe na afford bei lakini hiiiiii no no no no.aliongea kwa kujishauwa yule dada

Lakini wale mashoga zake walidai anisikilize huenda tutaelewana ,kisha baada ya kumtajia bei ndipo alipopata nguvu ya kuizunguka kuiangalia vizuri huku nikifungua milango kwa mbwembwe ili awe na imani na amani nayo

Mmmmmh whaaat, ni kweli au macho yanguuuuu,mbona kama hii gari naifahamu,hii si gari ya mama Moo hii,yes ni yenyewe bwaanah, ni wiki moja imepita alinikuta maeneo ya kiluvya akanipa lift.alishtuka yule dada akiongea kwa kubana pua huku mimi nikishangaa .

Mama Moo ni nani wewe dada,
Hii gari kanipa mshikaji wangu anaitwa Shabani na yupo Mkoa Sasa hivi kaniambia nimuuzie.
Niliongea kwa kujiamini .

Sasa Shabani si ndiye mume wa mama Moo . Kisha akawageukia
Wale wenzie , jamani
Ile habari ya ugomvi wa shoga yangu aliyenyang'anywa gari na mumewe juzi niliyowaambia Sasa gari ni hii ,

Shabani anafanya biashara ya mazao yaani nafaka zote, Sasa kwakuwa anakuwa ofisini kwake kwahiyo show nzima huwa anasimamia mkewe,Sasa baada ya mke kununua gari Shabani alishtuka ndipo alipoichungulia account na kukuta Haina kitu na mwanamke kajenga nyumba kuuuuubwa wapi huko sijui ,na pia akajizawadia na gari

hii gari wala si ya muda mrefu mimi ndiye nilimshauri anunue baada ya kuwa kakamilisha ujenzi wa nyumba yake aliyojenga bila mumewe kujua.

Kumbe ndiyo maana shoga yangu Leo mnyooonge , kwenda polisi anashindwa ,gari hajui ilipo na Shabani kaenda Mkoa kufuata mazao safari kaenda mwenyewe, Sasa shoga yangu yupo katikati. Hajui afanyaje.

Weeeee tuondoke jamani hii gari ya moto , kaka Mimi biashara nimeshindwa kama ni hii gari tafuta mteja mwingine. Aliongea yule dada huku wakigonga mikono na mashoga zake wakiingia kwenye gari la kampuni aliyotoka yule fundi wakaishia huku nikishika tama nisijue Cha kufanya.

Jifunze,
Elimika.
Burudika.

Itaendelea......................
Jack Daniel umetuacha na alosto, njoo utupe vituuuuz!
 
SEHEMU YA AROBAINI

Nilimpigia simu Shabani ili nimweleze changamoto kuhusu chombo chake huku nikipanga nimchane ukweli juu ya biashara ambayo alitaka kuniweka kwenye wakati mgumu, lakini licha ya kumtafuta mara kadhaa simu haikupokelewa.

Niliingalia ile gari mara mbili mbili huku nikicheka peke yangu namna watu wanavyoishi yaani mke kanyang'anywa chombo hivihivi dah ni hatari sana.nilijisemea moyoni.

Mida fulani usiku nikiwa bado nipo nje nikihakikisha usalama, simu iliita huku mpigaji akiwa ni Shabani,

Ee bro naona huniombei mema hata kidogo, unataka kuniingiza kwenye matatizo yako wewe na mkeo ni dhahiri mkeo ataniona kama ni sehemu ya mtu mfitini kwenye ndoa yake, inakuwaje kunipa niuze chombo chenye matatizo?
Niliuliza.

Daniii hujaacha tu mambo yako, yaani umri huu wetu sisi Mimi na wewe tunawezaje kufanya mambo ya hovyo? Mimi hapa nimeona missed calls zako nikaona labda unataka kunipa taarifa nzuri maana nimekuja huku mashambani mazao ni mengi halafu pesa inakaribia kukata hivyo nategemea sana senti utakayopata tukisukuma chombo kumbe bado tu mwanangu,
Kwani wife kaja kukudisturb?
aliuliza.

Hapana, shem hajaja.
Isipokuwa katika tafuta tafuta ya wateja nilimpata dada fulani ambaye alikuja mahali nilipoweka chombo, lakini , gari kaijua na kudai hatoinunua na pia anaonesha ana ukaribu na anafahamiana na mkeo, Sasa huoni unanitafutia lawama watu tuje kuchukiana bila sababu, Mimi naona njoo uuze mwenyewe, peleka hata yards za minada huko ila binafsi Mimi nimeshindwa kaka.
Niliongea kwa sauti ya kumaanisha .

Dah yaani Dani Wala sikujua kama upo hivyo, halafu usichojua ni kwamba hata kama mke wangu akijua gari ipo na wewe hawezi kukusumbua kwa lolote, kwasababu mimi sijaiba wala kuchukua kwa nguvu bali tulikubaliana baada ya kumwambia tu kuwa achague moja , niuze gari au nimpe talaka.
Akachagua niuze gari haswa baada ya kukiri makosa ambayo aliyafanya. Kwahiyo Dani kuwa huru hakuna mtu yeyote atakusumbua. aliongea huku akinitoa wasiwasi.

Pamoja na kunishawishi sana lakini sikuwa tayari kufanya biashara ile kwani niliona itaniletea matatizo baadaye.

Kesho mida ya mchana nikiwa natafuta lunch, nilipokea simu kutoka kwa Lewis, ni yule mchungaji mtoto wa dada yake na Jastini,

Niambie ndugu, naona kimya kidogo nipe habari. nilikuwa makini kumsikiliza.

Kaka, mambo yamekuwa magumu , ni kwamba uncle wangu Jastini amehukumiwa kifungo cha miaka kumi, ni baada ya jamhuri kumtia hatiani kwa kosa la kufanya biashara isiyokuwa na vibali huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria na hata yeye alikiri mbele ya mahakama.na tulipata wasaa wa kuongea naye na tulimueleza namna ulivyompigania , na hata yeye alifurahi kusikia hukumuacha ila ndiyo hivyo, alipangalo MUNGU mwanadamu mwenye mwili wa nyama hawezi kupangua.
aliweka kituo Lewis huku sauti yake ikiwa ya chini na yenye mkwaruzo akionesha amesikitika sana.

Dah poleni sana jamani , Mimi naamini Kila jambo hutokea kwasababu zake, tunapaswa kumshukuru Mungu kwa kila jambo . Niliweka kituo huku Lewis akikata simu.

Aiseee kweli haya maisha tutafute taratibu kama utani yaani jamaa kapigwa nyundo hizo zote , kwa maana hiyo Nigga, Mwamba, na , stronger Jax ni Prisoner?
Asalaaaaleeeeh , Dani napaswa kuwa makini pengine naweza kuwa nafuatia kwenye hili sakata, njia pekee ni kurudi kwa yule mganga maana huenda natafutwa sijijui tu. Niliwaza Kisha nikapiga vijiko viwili tu vya Chakula nikakiacha kama kilivyo huku hata gari la Shabani nikiona kama ni mipango ya shetani kuhakikisha naishia pabaya kama ilivyo kwa Jastini.
Nikawa narudi ofisini taratibu nikiwa mwenye mawazo kiasi kwani siku yangu iliharibika.

Nikiwa bize na mambo yangu, alikuja mtu akaniambia boss ananiita ofisini kwake. Nikainuka haraka nikipandisha ngazi kuelekea ilipo ofisi yake na kukutana na wenzangu wawili ambao wote tuna taaluma zinazofanana.

Niliwasalimia Kisha nikakaa huku nikiwa makini kuhakikisha nasikia point kwa point.

Jamani Mimi nimewaiteni nyinyi ndugu zangu au wafanyakazi wenzangu,

Dani unashangaa Nini ,(huku nikijichekesha) kwani Mimi ni mkurugenzi hapa, Mimi ni Mfanyakazi kama wewe hivyo tunatenganishwa na madaraja tuu.
aliongea kirafiki boss wetu huku siku hiyo nikishangaa namna alivyo mpole maana ni mwenye mikwara mno haswa ukizingatia akikukataa yeye tu basi taasisi nzima imekukataa.

Jamani kumekuwa na changamoto kwenye urekebishaji wa mashine mpya haswa vifaa vinavyotoka bara la Asia, nikamaanisha India, Japan, China na kwingineko.
Maopareta wanalalamika vifaa vinatengenezwa lakini siku mbili tu vinaharibika nini tatizo.

Aliuliza huku akituangalia kwa zamu huku akiandika vitu kwa notebook yake.

Lakini Kila mmoja alikuwa kimya sana huku Mimi tumbo likiunguruma kwa mbali sikujua wenzangu japo sura zao zilionesha nao hawakuwa sawa.

Sasa wiki ijayo Kila mmoja ataenda
Sehemu ninapopajua Mimi, nataka kujua uwezo wenu, lazima tufanyiane interview tena maana mambo hayaendi, mfumo wetu wa taifa unaamini sana katika vyeti kuliko utaalamu , kazi zinasimama kwa kujikuta tumejaza watu weeeengi wasio na ujuzi.
Mmependeza sana na suti zenu lakini nataka niakisi uwezo kama kweli mnaijua Hydraulic vizuri , siyo kupiga pasi nguo na kuja kuperuzi ofisini. Sasa nawapa siku tano mkapumzike nyumbani Kisha mtarudi tuje tupange ratiba zenu.
Aliweka kituo huku Kila mtu akiwa kimya

Tuliteremka Kisha wote tukasimama na kuangaliana kwa sekunde kadhaa pale kwenye korido bila kuongea Kisha Kila moja akielekea ofisini kwake.

Nilikuwa na hofu na mawazo mapya kabisa , sikuwaza kuhusu Jax,
Sikuwaza kuhusu gari la Shabani, Bali niliwaza kuhusu hatima ya kazi yangu , kazi iliyobeba mustakabali wa maisha yangu na familia yangu.
Huku nikiona kabisa boss alituita watu watatu lakini ni kama alinilenga
Mimi maana kazi nilizofanya kwa mara ya mwisho dizaini kama nilichemka hivi.

Jioni nilitoka nje nikawasha ngalawa
Yangu na kuingia highway huku nikiwa very stressed hata simu kadhaa za baadhi ya watu sikuwa na nguvu ya kuzipokea.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Itaendelea....................
 
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA

Ilikuwa ni siku ya kwanza Kati ya zile siku tano tulizopewa na boss ili tujiandae na kazi ambayo tutapewa nikiwa hata sijaijua.

Lakini nikapanga lazima zile siku tano nizitumie kutatua mambo yangu yote ikiwemo kuhakikisha narudi kwa mtaalamu nikajiself defence.

Nilimuaga mke wangu kuwa Kuna mahali naenda kikazi ,sikumwambia kuwa naenda kwa mganga najua asingekubali japo hangekuwa na uwezo wa kunizuia.

Kwahiyo mume wangu safari hii unaenda na usafiri binafsi , hii safari mbona kama nakuwa na mashaka nayo hivi, maana unaweza Kuta mpo wawili kwenye ndoa bila kujua, pengine safari hii ni kwa mwanamke mwenzangu Mimi sijui tu.
aliongea kwa utani wife.

Mimi mwanamke wa nini tena wewe mwenyewe nina mpango wa kukuacha, tulitaniana kisha nikakamata njia ya kuelekea kwa mtaalamu wa kipindi kilichopita.

Mida ya saa kumi na moja jioni nilikuwa nishafika kwenye Kijiji kile huku nikishangaa watu walivyozidi kuongezeka watu walikuwa wengi mno kiasi cha kujikuta tupo foleni , mtu ambaye nilimkuta kwa mara nyingine alikuwa ni jamaa mmoja aliyekuwa anauguza mtoto wake mwenye ukichaa.

Kaka vipi naona umerudi kwa mara nyingine vipi habari za huko mjini, ni mwezi wa pili Sasa tangu ulipotuacha hapa ndugu .vipi familia haijambo lakini.
aliongea yule jamaa huku nikigundua hata mwili kapungua tofauti na nilivyomzoea.


Tunashukuru MUNGU familia iko poa sijui nyinyi hapa na vipi kijana wetu anaendeleaje. Niliuliza.

Wewe acha tu kaka ,
Nahisi Mungu hasikii kilio changu, naona ni dhahiri hata Mimi nitakufa tu huu ni mwezi wa tano Niko hapa Kuna muda kijana anaonesha ana nafuu lakini ndani ya siku chache anakatisha tamaa hii inaniuma sana.

Pengine ndiyo maana wanaume tunakufa mapema ni kwakuwa kwenye vifua vyetu tumebeba mengi ambayo huwezi kumsimulia yeyote huku tukiugua kimya kimya.
Kwanza mtoto wangu aliugua mara tu baada ya kuhitimu chuo kikuu huku tukiwa na mpango wa kumtafutia kazi.lakini ile miezi michache akiwa nyumbani tulibaini mabadiliko ya tabia yake , kwani alikuwa anajiamini kupita kiasi huku akikosa adabu kwa baadhi ya watu.

Kila mtu alijua kijana yupo na makundi ya ajabu ya wavuta bangi lakini kadri siku zinavyokwenda ndipo tuligundua kuwa tayari amekuwa mgonjwa , huyu hapa ni mganga wa nne, lakini natamani kutoka niende kujaribu kwa mtaalamu mwingine tatizo pesa imekata kaka na baadhi ya ndugu wa mke wangu wanadai Mimi nilimroga mtoto wangu ili biashara zangu ziende.
aliongea kwa uchungu sana.

Kwani wewe bro una kazi gani, maana hata kipindi kile hatukufahamiana vizuri.
Niliuliza.

Mimi ni mfanyabiashara niliacha kazi ya upolisi miaka miwili tu tangu niajiriwe, nikajikuta nashawishika na biashara zaidi,nikianza na biashara za vyakula vya mifugo.
Huku nikiwa mshauri wa masuala ya ufugaji pia japo sikuwa mtaalamu sana lakini nilijenga jina na biashara ikawa kubwa zaidi.

Nina zaidi ya miaka 20 kwenye hii biashara lakini tayari mpaka muda huu Mimi ni masikini, kwasababu robo tatu ya pesa yangu imeishia kwa huyu mtoto, nilianza na hospital za Tanzania Kisha India lakini wapi , tukarudi Tanzania na kuamua kutafuta wataalamu Hawa ambao mpaka Sasa sioni dalili ya matumaini.
Jamaa aliongea kwa hisia kali sana.

Pole sana cha muhimu usimkufuru Mungu, unapaswa tu kushukuru kwa Kila hali kudra za mwenyezi MUNGU hazipo karibu.
nilimwambia huku nikigundua uso wake umebadilika.

Wewe acha tu kaka hata shemeji yako, kaamua kuondoka ni baada ya ndugu zake kumlisha maneno kuwa Mimi ndiye namsumbua mtoto wake, hivyo kwasasa nipo mwenyewe huku nikitupiwa lawama ambazo hata sikuwahi kufikiria. Safari hii alilia kabisa huku nikigundua huenda mambo yake anayo muda mrefu na hakuwa na wa kumwambia.

Kesho asubuhi foleni yangu ilifika
Nikaeleza shida yangu ,kisha nikaambiwa shida yangu ndogo tu natakiwa nipate kondoo dume,ambaye hajaota pembe bado.kisha nitarudi.

Niliulizia majirani wakaniambia kuna msukuma ana kondoo wengi sana,yupo kilomita saba tu toka tulipo ,huku wakiniambia nijipange maana tangu agundue kuwa kondoo ni dili basi bei imechangamka.sikujali kuhusu hilo nilichotaka nipate kondoo tu.

Nilifanikiwa,naam nilimpata kondoo saizi niliyoambiwa ,nikamtia kamba,na kumtia nyuma ya Isuzu yangu na kurudi kwa mtaalamu au fundi kama wengi walivyomuita.
Na sijui kama uganga nao ni taaluma.

Baada ya hapo tuliingia ndani ya kilinge huku kondoo akiwa kafungwa kwenye mti fulani ambako kulikuwa na kondoo wengine wanne huku nikijua huenda sipo peke ninayetaka kusafisha nyota.

Mganga akaanza ufafanuzi wake......
Kuna dawa nitakutengenezea wewe si unataka heshima?
aliuliza.

Nikatikisa kichwa kuashiria ndilo hitaji langu kuu.

Eeeh sasa hao watu wako tutawainamisha vichwa vyao viwe chini,watakuonea aibu kukutazama,
Kila watakalopanga kukufanyia vibaya watajikuta wanaghairi na kuinamisha vichwa vyao kama kondoo mdogo,ambaye hata akichinjwa hutoa sauti ndogo sana licha ya maumivu anayopata.

Kazi tutaifanyia hapo msituni nyakati za usiku,ila kuna wenzio wamekutangulia kwa hiyo itabidi uvumilie mpaka kesho kutwa, usiku wa leo ni zamu ya wengine.
Usijali tatizo lako dogo sana,si hautaki usumbufu?
Basi tulia hakuna atakayekupandishia sauti wote watajikuta sauti ndogo vichwa chini.

Sikuwa na jinsi nilikubali kuvumilia huku nikirudi kule kwa wenzangu kupiga stori.

Sema nini msomaji wangu,iko hivi

Maisha yana siri kubwa kati ya nguvu ya Mungu na ushirikina,
Mungu hutambua udhaifu wetu mapema.

Waweza fanikiwa ukijua ni nguvu ya mganga kumbe ni huruma za Mungu yaani unamuasi lakini Mungu hamtupi mja wake.

Nini kitaendelea sehemu ijayo ina majibu.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Loading.................
 
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA

Ilikuwa ni siku ya kwanza Kati ya zile siku tano tulizopewa na boss ili tujiandae na kazi ambayo tutapewa nikiwa hata sijaijua.

Lakini nikapanga lazima zile siku tano nizitumie kutatua mambo yangu yote ikiwemo kuhakikisha narudi kwa mtaalamu nikajiself defence.

Nilimuaga mke wangu kuwa Kuna mahali naenda kikazi ,sikumwambia kuwa naenda kwa mganga najua asingekubali japo hangekuwa na uwezo wa kunizuia.

Kwahiyo mume wangu safari hii unaenda na usafiri binafsi , hii safari mbona kama nakuwa na mashaka nayo hivi, maana unaweza Kuta mpo wawili kwenye ndoa bila kujua, pengine safari hii ni kwa mwanamke mwenzangu Mimi sijui tu.
aliongea kwa utani wife.

Mimi mwanamke wa nini tena wewe mwenyewe nina mpango wa kukuacha, tulitaniana kisha nikakamata njia ya kuelekea kwa mtaalamu wa kipindi kilichopita.

Mida ya saa kumi na moja jioni nilikuwa nishafika kwenye Kijiji kile huku nikishangaa watu walivyozidi kuongezeka watu walikuwa wengi mno kiasi cha kujikuta tupo foleni , mtu ambaye nilimkuta kwa mara nyingine alikuwa ni jamaa mmoja aliyekuwa anauguza mtoto wake mwenye ukichaa.

Kaka vipi naona umerudi kwa mara nyingine vipi habari za huko mjini, ni mwezi wa pili Sasa tangu ulipotuacha hapa ndugu .vipi familia haijambo lakini.
aliongea yule jamaa huku nikigundua hata mwili kapungua tofauti na nilivyomzoea.


Tunashukuru MUNGU familia iko poa sijui nyinyi hapa na vipi kijana wetu anaendeleaje. Niliuliza.

Wewe acha tu kaka ,
Nahisi Mungu hasikii kilio changu, naona ni dhahiri hata Mimi nitakufa tu huu ni mwezi wa tano Niko hapa Kuna muda kijana anaonesha ana nafuu lakini ndani ya siku chache anakatisha tamaa hii inaniuma sana.

Pengine ndiyo maana wanaume tunakufa mapema ni kwakuwa kwenye vifua vyetu tumebeba mengi ambayo huwezi kumsimulia yeyote huku tukiugua kimya kimya.
Kwanza mtoto wangu aliugua mara tu baada ya kuhitimu chuo kikuu huku tukiwa na mpango wa kumtafutia kazi.lakini ile miezi michache akiwa nyumbani tulibaini mabadiliko ya tabia yake , kwani alikuwa anajiamini kupita kiasi huku akikosa adabu kwa baadhi ya watu.

Kila mtu alijua kijana yupo na makundi ya ajabu ya wavuta bangi lakini kadri siku zinavyokwenda ndipo tuligundua kuwa tayari amekuwa mgonjwa , huyu hapa ni mganga wa nne, lakini natamani kutoka niende kujaribu kwa mtaalamu mwingine tatizo pesa imekata kaka na baadhi ya ndugu wa mke wangu wanadai Mimi nilimroga mtoto wangu ili biashara zangu ziende.
aliongea kwa uchungu sana.

Kwani wewe bro una kazi gani, maana hata kipindi kile hatukufahamiana vizuri.
Niliuliza.

Mimi ni mfanyabiashara niliacha kazi ya upolisi miaka miwili tu tangu niajiriwe, nikajikuta nashawishika na biashara zaidi,nikianza na biashara za vyakula vya mifugo.
Huku nikiwa mshauri wa masuala ya ufugaji pia japo sikuwa mtaalamu sana lakini nilijenga jina na biashara ikawa kubwa zaidi.

Nina zaidi ya miaka 20 kwenye hii biashara lakini tayari mpaka muda huu Mimi ni masikini, kwasababu robo tatu ya pesa yangu imeishia kwa huyu mtoto, nilianza na hospital za Tanzania Kisha India lakini wapi , tukarudi Tanzania na kuamua kutafuta wataalamu Hawa ambao mpaka Sasa sioni dalili ya matumaini.
Jamaa aliongea kwa hisia kali sana.

Pole sana cha muhimu usimkufuru Mungu, unapaswa tu kushukuru kwa Kila hali kudra za mwenyezi MUNGU hazipo karibu.
nilimwambia huku nikigundua uso wake umebadilika.

Wewe acha tu kaka hata shemeji yako, kaamua kuondoka ni baada ya ndugu zake kumlisha maneno kuwa Mimi ndiye namsumbua mtoto wake, hivyo kwasasa nipo mwenyewe huku nikitupiwa lawama ambazo hata sikuwahi kufikiria. Safari hii alilia kabisa huku nikigundua huenda mambo yake anayo muda mrefu na hakuwa na wa kumwambia.

Kesho asubuhi foleni yangu ilifika
Nikaeleza shida yangu ,kisha nikaambiwa shida yangu ndogo tu natakiwa nipate kondoo dume,ambaye hajaota pembe bado.kisha nitarudi.

Niliulizia majirani wakaniambia kuna msukuma ana kondoo wengi sana,yupo kilomita saba tu toka tulipo ,huku wakiniambia nijipange maana tangu agundue kuwa kondoo ni dili basi bei imechangamka.sikujali kuhusu hilo nilichotaka nipate kondoo tu.

Nilifanikiwa,naam nilimpata kondoo saizi niliyoambiwa ,nikamtia kamba,na kumtia nyuma ya Isuzu yangu na kurudi kwa mtaalamu au fundi kama wengi walivyomuita.
Na sijui kama uganga nao ni taaluma.

Baada ya hapo tuliingia ndani ya kilinge huku kondoo akiwa kafungwa kwenye mti fulani ambako kulikuwa na kondoo wengine wanne huku nikijua huenda sipo peke ninayetaka kusafisha nyota.

Mganga akaanza ufafanuzi wake......
Kuna dawa nitakutengenezea wewe si unataka heshima?
aliuliza.

Nikatikisa kichwa kuashiria ndilo hitaji langu kuu.

Eeeh sasa hao watu wako tutawainamisha vichwa vyao viwe chini,watakuonea aibu kukutazama,
Kila watakalopanga kukufanyia vibaya watajikuta wanaghairi na kuinamisha vichwa vyao kama kondoo mdogo,ambaye hata akichinjwa hutoa sauti ndogo sana licha ya maumivu anayopata.

Kazi tutaifanyia hapo msituni nyakati za usiku,ila kuna wenzio wamekutangulia kwa hiyo itabidi uvumilie mpaka kesho kutwa, usiku wa leo ni zamu ya wengine.
Usijali tatizo lako dogo sana,si hautaki usumbufu?
Basi tulia hakuna atakayekupandishia sauti wote watajikuta sauti ndogo vichwa chini.

Sikuwa na jinsi nilikubali kuvumilia huku nikirudi kule kwa wenzangu kupiga stori.

Sema nini msomaji wangu,iko hivi

Maisha yana siri kubwa kati ya nguvu ya Mungu na ushirikina,
Mungu hutambua udhaifu wetu mapema.

Waweza fanikiwa ukijua ni nguvu ya mganga kumbe ni huruma za Mungu yaani unamuasi lakini Mungu hamtupi mja wake.

Nini kitaendelea sehemu ijayo ina majibu.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Loading.................
Asante JD nyingine lini 😋😋
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom