Simulizi: Harakati za Jason Sizya

safari buzwagi.JPG

30

“Ndiyo, ni mrembo kwelikweli na asiye na hatia, kwa hiyo usijaribu kutaka kuchezea hisia zake,” aliongea katika namna ya kunionya kisha akainamia tena kiti cha mbele yake na kufumba macho.

Alionekana kuwaza mbali. Kisha kama aliyekumbuka jambo, alifumbua macho yake lakini akiwa bado ameinamia kile kiti cha mbele yake na kunitahadharisha. “Tena, kuwa mwangalifu sana na wasichana warembo kama huyo, wakati mwingine ni nyoka wenye sumu kali.”

Sikusema neno, niliyapeleka macho yangu kuangalia nje, nikaona tukiupita uwanja wa mpira wa Samora (Samora Stadium) huku basi tulilopanda likizidi kuchukua kasi. Dereva wa basi alionekana kuwa mzoefu sana wa barabara hiyo tuliyopita kutokana na jinsi alivyokuwa anaendesha kwa mbwembwe huku akiwa makini barabarani akiwakwepa waendesha baiskeli, pikipiki na mikokoteni waliokuwa wakipita kandokando ya ile barabara.

Basi lilipofika katika mzunguko wa barabara za Tabora, Shinyanga, Bukene na ile ya Singida tuliyotokea, liliupita ule mzunguko na kuifuata barabara ya Bukene iliyokuwa inapitia Itobo. Hapo nikageuka tena kumtupia jicho yule mrembo wa shani, na wakati huohuo na yeye alikuwa anainua uso wake toka kwenye simu yake na kunitazama.

Alipogundua kuwa nilikuwa natazama upande wake akaachia tabasamu kabambe huku myumbo wa lile basi tulilopanda ukimpotezea umakini. Hata hivyo nilizuga nikajifanya sikuwa namtazama yeye.

Jambo moja lililonitatiza zaidi ni kwamba kila mara alipohisi kuwa nilikuwa namtazama alikuwa anaachia tabasamu, sikujua ni kwa nini, hata hivyo nilijipa subira huku nikiamini kuwa huo ulikuwa mwanzo mzuri wa kujenga daraja la urafiki baina yetu, urafiki ambao hatimaye ungetupeleka kwenye ulimwengu wa mahaba mazito.

Dereva wa basi la Makenga alionekana kuijua vizuri barabara ile, sasa alikuwa akipanga na kupangua gia wakati basi lile lilipokuwa likikatisha kwenye ofisi za Halmashauri na ofisi zingine, kisha tulianza kukatisha katikati ya makazi ya viongozi na watu wenye ukwasi. Baada ya dakika kadhaa tulikuwa tunashusha mteremko fulani kwenye kilima nje kidogo ya ule Mji wa Nzega katika eneo ambalo kulikuwa na majengo ya idara ya ujenzi.

Dereva alionekana kuifurahia sana kazi yake kwani alikuwa anaendesha kwa mbwembwe huku akiwa makini zaidi kuyakwepa mawe madogo madogo na makorongo yaliyosababishwa na mvua katika ile barabara. Niligeuza shingo yangu kutazama nje kupitia kwenye kioo cha dirisha na hapo nikagundua kuwa mwendo wetu ulikuwa wa kasi mno.

Hali hiyo iliifanya ile taswira ya kile kilima jirani na majengo idara ya ujenzi na hata nyumba za makazi ya watu katika Mji wa Nzega kutoweka taratibu katika upeo wa macho yangu kadiri lile gari lilivyokuwa linachanja mbuga.

Niliyatembeza tena macho yangu kuwatazama abiria wengine waliokuwa wameketi kwa utulivu mle ndani ya basi la Makenga na hapo nikagundua kuwa wengi walionekana kuzama katika tafakari, huwenda walikuwa wanawaza juu ya ile safari na wengine walipitiwa na usingizi kutokana na uchovu au njaa.

Muda mfupi baadaye tulikuwa tumeuacha Mji wa Nzega nyuma yetu katika mwendo wa masafa marefu na hatimaye tukatokomea kabisa mbali na mji ule huku tukikatisha katikati ya mashamba, vichaka na miti mirefu na mifupi ya porini. Kimya kiliendelea kutawala ndani ya basi la Makenga na sauti pekee iliyokuwa inasikika mle ndani ilikuwa ni ya muungurumo wa injini kukuu ya basi na mnuko wa harufu nyepesi ya dizeli.

Safari ikiwa inaendelea niligeuza tena shingo yangu kiaina kumtazama yule mrembo wa shani na hapo nikamwona akiwa amekiegemeza kichwa chake kwa nyuma kwenye kiti alichokalia huku akionekana kuanza kupitiwa na usingizi.

Japokuwa hata mimi nilikuwa na uchovu mwingi lakini kamwe sikuuruhusu usingizi unichukue kwa kuzingatia kuwa hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kusafiri katika barabara hiyo ya Itobo, hivyo nilikuwa mgeni kabisa wa barabara ile na mazingira yake. Kawaida yangu ilikuwa kwamba, kama sehemu niliyokuwa naenda ilikuwa ngeni kwangu sikupenda kusinzia kwa sababu nilitaka kuyakariri maeneo na vituo ili siku nyingine nisipate taabu ya kuuliza.

Nilipomuona yule mrembo wa shani amepitiwa usingizi nilihisi kumhurumia sana kwa hali ile ya uchovu aliyokuwa nayo, hata hivyo sikuwa na namna yoyote ya kumsaidia. Hisia fulani hivi za mahaba ndani yangu zilizidi kunitesa na kunifanya nihisi kuwa na hali isiyokuwa ya kawaida, hasa kitendo cha kukaa mbali na yule mrembo wa shani.

Ingekuwa ni amri yangu ningemwambia Eddy akakae kule kwenye kiti cha nyuma ili yule mrembo wa shani aje kukaa karibu yangu nimkumbatie.

Niligeuza tena shingo yangu kumtazama yule mrembo wa shani na kumwona akiwa ametopea kwenye usingizi. Nilishusha pumzi za ndani kwa ndani na kujiegemeza kwenye kiti changu, na mara nikaanza kuwaza jinsi ambavyo maisha mapya katika Mji wa Kahama yangekuwa baada ya kupata kazi katika mgodi wa dhahabu wa Buzwagi.

Kabla sijazama kwenye mawazo yale nikashtushwa na kupungua ghafla kwa mwendo wa lile basi letu. Haraka nikainua kichwa changu na kuangalia huku na kule na hapo macho yangu yakatua kwa askari mmoja wa usalama barabarani aliyekuwa anaibuka kutoka nyuma ya roli moja la mafuta aina ya Isuzu lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara ile.

Yule askari wa usalama barabarani alisimama katikati ya barabara, umbali mfupi mbele yetu akiwa ameshika kitu fulani mfano wa tochi au kamera.

Kitendo cha mwendo wa lile gari letu kupungua ghafla kiliwafanya abiria wengine, akiwemo Eddy, washtuke kutoka usingizini na kuangalia kule mbele. Basi letu liliposogea karibu zaidi nikawaona askari wengine wawili wa usalama barabarani wakiibuka na kusimama kando ya barabara huku wakilitazama lile basi la Makenga kwa umakini na uchu mkubwa wa kupata ‘kitu kidogo’.

Nilipochunguza vizuri nikagundua kuwa yule askari wa usalama barabarani aliyekuwa wa kwanza kujitokeza alikuwa ameshika kamera maalumu ya kuchunguza mwendo kasi wa magari na sasa alikuwa amesimama katikati ya barabara mbele yetu huku akimwonesha dereva wa gari letu ishara ya mkono kumtaka aegeshe gari lake kando ya barabara.

Niliwaona wale askari wengine wawili waliokuwa wamesimama kando ya barabara ile, mmoja alikuwa ameshika mkononi mashine ndogo ya kielektroniki ya kutolea risiti za papo kwa papo baada ya malipo na mwingine alikuwa ameshika bunduki aina ya SMG.

Nilimtazama dereva wetu kwa umakini huku nikijaribu kumchunguza kuona kama alikuwa na wasiwasi wowote juu ya lile tukio la kusimamishwa kwetu na wale askari wa usalama barabarani lakini sikuona wasiwasi wowote usoni kwake na badala yake nikamwona akikazana kupangua gia za lile basi huku akipunguza mwendo taratibu.

Hatimaye basi liliwapita taratibu wale askari wa usalama barabarani na kwenda kusimama mbele kidogo, umbali wa takriban mita therathini kutoka pale walipokuwa wamesimama askari wa usalama barabarani, kisha yule dereva wa basi letu aligeuza shingo yake kumtazama kondakta wake na kumpa ishara ambayo niliielewa vyema, ilikuwa ni kumtaka ampe fedha kwa ajili ya kuwapa wale askari wa usalama barabarani.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

31

Yule kondakta wa basi alitoa noti moja ya shilingi elfu mbili na kunyoosha mkono wake kumpa dereva wake, na hapo yule dereva aliibana vizuri ile noti kwenye kadi ya gari kwa vidole vyake na kufungua mlango wa gari. Alishuka na taratibu akaanza kupiga hatua zake kurudi nyuma akiwafuata wale askari wa usalama barabarani.

Niligeuza shingo yangu kutazama vizuri kule nyuma kwenye lile roli la mafuta lililoegeshwa barabarani nikagundua kuwa mbele yake kulikuwa na magari mengine mawili madogo yaliyokuwa yamesimama kando ya barabara na yalikuwa yanapekuliwa na askari wengine wa usalama barabarani.

Gari mojawapo lilikuwa ni aina ya NOAH na jingine lilikuwa Toyota Pick up lililokuwa limesheheni magunia, sikujua yalikuwa yamehifadhi nini. Niliitazama saa yangu ya mkononi na kugundua kuwa ilikuwa imeshatimu saa 8:10 mchana, maana yake ni kwamba tulikuwa tumetumia dakika 30 toka stendi ya mabasi ya Sagara mjini Nzega hadi hapo.

Kilipita kitambo kifupi cha maongezi kati ya yule dereva wa basi la Makenga na askari wa usalama barabarani aliyekuwa ameshika kamera mkononi, na wakati huo wote mimi nilikuwa nawalaani kimoyomoyo wale askari wa usalama barabarani kwa kutuchelewesha.

Kisha nikamwona yule dereva wetu akiangalia huku na kule na kunyoosha mkono wake kumpa yule askari ile kadi ya gari ikiwa na noti ya shilingi elfu mbili ndani. Yule askari mwenye kamera aliipokea ile kadi na kujifanya akisoma maandishi yaliyokuwa yameandikwa kisha akaitoa ile noti haraka na kuitia mfukoni na kisha akamrudishia dereva ile kadi ya gari.

Nilimtupia jicho yule mrembo wa shani nikamwona akiitupia jicho saa yake ya mkononi na kusonya kwa hasira, hapo nikajua kuwa hata yeye alikuwa amekerwa na kile kitendo cha wale askari wa usalama barabarani kuendelea kutuweka hapo.

Mara nikamwona yule askari wa usalama mwenye kamera aliyepokea fedha kutoka kwa dereva wetu akipiga hatua zake taratibu kulisogelea gari letu. Muda huo lile roli la mafuta na yale magari mengine mawili yalianza kuondoka taratibu kutoka eneo lile baada ya madereva wake kumalizana na wale askari wa usalama barabarani.

Na wakati huo huo gari jingine aina ya Fuso lilisimamishwa na askari mmoja wa usalama barabarani baada ya kulipungia mkono na kumtaka dereva aliegeshe gari lake kando ya barabara.

Yule askari wa usalama barabarani mwenye kamera alilifikia lile gari letu na hapo akaelekea upande wa mbele wa lile gari huku akitukata jicho la hadhari watu wote tuliokuwamo ndani ya basi. Alionekana kama aliyekuwa anakagua magurudumu ya lile gari kisha alielekea mbele kwenye kioo cha mbele na kukagua karatasi ya bima kabla ya kuja hadi kwenye mlango wa abiria na kuingia ndani, na hapo abiria wote tukamtazama kwa shauku wakati yeye akituangalia kidogo mmoja baada ya mwingine kwa udadisi.

“Habari zenu jamani?” yule askari wa usalama barabarani ambaye alikuwa na alama mbili za “V” chini ya bega lake la kulia alitusalimia huku akiendelea kutusaili kwa macho.

“Nzuri, afande!” karibia abiria wote tulimwitikia kwa pamoja.

“Poleni na safari…” yule askari wa usalama barabarani alisema na kisha akauliza kabla hata hatujajibu huku akitutazama kwa umakini. “Vipi, dereva wenu anaendeshaje gari?”

“Dereva yupo makini sana, na anaendesha vizuri tu,” abiria mmoja mwanamume wa makamo aliyekuwa ameketi kwenye kiti kilichokuwa nyuma ya kiti cha dereva alijibu haraka.

Kisha kitambo kifupi cha ukimya kikapita wakati yule askari wa usalama barabarani akitutazama kwa umakini kama aliyekuwa anatafuta neno la kuongea, kabla hajageuka kumtazama yule dereva ambaye muda wote alikuwa mkimya huku akimtazama askari wa usalama barabarani kwa utulivu.

Kisha yule askari wa usalama barabarani akashusha pumzi na kuanza kutoa somo fupi kwetu abiria kuhusu sheria za usalama barabarani na madhara ya mwendo kasi. Ilimchukua takriban dakika tano na mwisho alituomba kutuma ujumbe mfupi wa maneno au hata kupiga simu kwa kamanda wa kikosi cha usalama barabarani wa Wilaya ya Nzega au Kahama endapo dereva wetu angeonekana kukiuka sheria za usalama barabarani.

Tulimkubalia huku tukimhakikishia kushirikiana na Jeshi la Polisi, na hapo yule askari wa usalama barabarani akaminya midomo yake na kubetua kichwa huku akishuka kutoka kwenye lile gari na kisha alimwashiria dereva wetu aondoe gari.

Dereva aliketi kwenye kiti chake na kuwasha injini ya gari kisha akaingia barabarani huku akijitahidi, kwa kila hali, kuonesha tabasamu mbele ya wale askari wa usalama barabarani wakati akiondoka eneo lile.

Baada ya mwendo fulani tulimaliza kushuka mteremko kisha mbele kidogo tukaanza kuvuka mashamba na makazi ya watu katika eneo ambalo baadaye niliambiwa panaitwa Ipilili, dereva aliongeza tena mwendo na kulivuka lile lori la mafuta lililokuwa mbele yetu.

Mwendo wetu haukuwa wa kitoto kwani hatukuchukua muda, kwa mbali nilianza kuziona nyumba kadhaa kuukuu ingawa baadhi ya nyumba hizo zilikuwa za kisasa za matofali ya kuchoma na juu zilikuwa zimeezekwa kwa bati.

Kwa kupitia maongezi ya abiria wawili waliokuwa wameketi kwenye viti vya mbele yetu niliweza kutambua kuwa kile kijiji kiliitwa Busasi. Baada ya muda tulikifikia kile kijiji na kuanza kukatisha katikati ya mashamba na makazi machache ya watu katika barabara ile. Wakati huo miale mikali ya jua la saa nane na ushee mchana ilikuwa inapenya kwenye vioo vya madirisha ya lile gari na kutuama mle ndani huku ikileta joto lililotuchangamsha.

Safari ikiwa inaendelea basi tulilopanda lilianza kushuka mteremko mwingine mfupi na kulifikia daraja dogo la kalavati ambalo mara baada ya kulivuka tulianza kupanda kilima kidogo, hapo nikageuza tena shingo yangu kumtazama yule mrembo wa shani.

Nilimwona akiwa ameketi kwa utulivu akichezea simu yake, hivyo nami nikaamua kuchukua kitabu changu cha masimulizi ya kusisimua kinachoitwa “Rosa Mistika”. Kitabu hiki kiliandikwa na mmoja wa magwiji wa uandishi wa fasihi nchini, Profesa Euphrase Kezilahabi.

Ilikuwa kawaida yangu kila nilipokuwa nasafiri ilikuwa lazima nichukue kitabu kwa ajili ya kusoma nikiwa safarini au pale nilipokuwa nimejipumzisha. Nilikuwa mpenzi wa kusoma vitabu na hadi muda huo nilikuwa nimeshasoma vitabu vingi sana kadri Mungu alivyonijalia nafasi kwani niliamini kusoma vitabu kuliongeza maarifa.

Niliamini mtu unaweza kuongeza maarifa kwa kusafiri maeneo mbalimbali na kukutana na watu wengine wenye mtazamo, mawazo, uzoefu tofauti na wake. Lakini pia niliamini unaweza kuongeza maarifa kwa kusoma vitabu; kwani kwa kusoma vitabu unajikuta ukisafiri sehemu mbalimbali duniani huku ukiwa umekaa tu kwenye kiti chako na kitabu chako mkononi, ukisoma na kujipatia ujuzi, uzoefu na mawazo ya watu mbalimbali kutoka kila kona ya dunia.

Kwenye vitabu pekee ndiyo mahali nilipoweza kukutana na watu waliokwisha kufa, nikawasikia mawazo yao.

Rosa Mistika au waridi lenye fumbo; ni riwaya inayoyachora maisha ya msichana Rosa Mistika, maisha yaliyojaa mikasa ambayo kila nilipoisoma riwaya hiyo nilijikuta kama niliyekuwa naangalia sinema fulani ya kusikitisha na kusisimua mno. Ni riwaya iliyoyachora maisha na wasifu wa Rosa, kifungua mimba cha familia ya Zakaria na Regina kati ya wasichana watano na mvulana mmoja.

Kwa kiasi kikubwa, masimulizi ya Rosa yamejikita katika kueleza maisha ya mhusika, Rosa, tangu akiwa mtoto mpaka kifo chake na maisha baada ya kifo chake. Ni riwaya inayojenga taswira fika ya maisha na malezi ya mtoto wa kike na changamoto anazozipata katika jamii kutokana na malezi yenyewe, tamaduni, umasikini na mateso ya kifamilia. Na pia inaangazia kutawishwa kwa watoto wa kike na athari zake.

Wakati nikisoma riwaya hiyo nilisikitishwa sana na maisha ya Rosa kwa jinsi yalivyobeba fumbo kubwa; wapo waliomwita malaya, mzinzi mkuu, mvunja nyumba za watu; na wapo wengine waliomwona kama msichana mwenye nafsi isiyo na hatia. Kwa kweli alikuwa msichana aliyezingwa na kutekwa nyara na shinikizo hasi za mazingira, yakamghilibu bila ya kujitambua. Lakini walikuwepo wachache wenye malezi makali ambao waliamua kumwita asherati!

Rosa akiwa mtoto mdogo alionekana msichana mrembo na mwenye aibu, mrefu kiasi, mnyenyekevu na mkakamavu. Akakua chini ya malezi ya baba yake aliyekuwa na mtazamo hasi juu ya wanawake.

Zakaria akiwa kama mwalimu aliyeachishwa kazi kwa sababu ya ulevi, alimtesa mama yake Rosa kwa kumpiga na kutomjali pamoja na familia yake kwa sababu tu alimzalia watoto wa kike wengi. Mama huyo tangu aolewe hakuwa na raha: alikuwa anasumbuliwa na kuteswa na mumewe kwa kosa lisilo lake. Katika kijiji chote cha Namagondo hapakuwa na mwanamke aliyekuwa akipigwa karibia kila juma kama mama huyo.

Kiukweli nilikwisha isoma riwaya ya Rosa Mistika mara mbili lakini sikuchoka kuisoma, ilikuwa riwaya inayosisimua tangu mwanzo hadi mwisho…

Wakati nikiendelea kusoma masimulizi hayo mara nikahisi lile basi letu likipunguza tena mwendo na kutufanya abiria wote kushtuka kwa mara nyingine na kuangalia mbele. Kupitia kioo cha mbele cha lile gari niliweza kuona nyumba nyingi zikiwa zimejengwa kwa mfuatano na kulikuwa na mitaa, na hapo nikajua kuwa tulikuwa tunaingia katika mji fulani mdogo.

Niliwauliza wale abiria waliokuwa wameketi viti vya mbele yetu na jibu nililopata ni kwamba pale ndiyo Itobo, eneo ambalo kulikuwa na makutano ya barabara za Bukene iliyokuwa inanyoosha moja kwa moja, ya kuelekea Kahama iliyokuwa inakunja upande wa kulia. Pia kulikuwa na barabara nyingine ndogo iliyoingia upande wa kushoto ya kuelekea kijiji cha Bulunde/ Kalitu.

Wakati huo lile basi lilikuwa linakatisha katikati ya makazi ya watu katika mji ule mdogo wa Itobo, na tulipoyakuta yale makutano ya barabara na lile basi lilipinda kuingia upande wa kulia na kuifuata barabara ya kuelekea Kahama. Hapo likasimama kwenye stendi ndogo ya mabasi ya Itobo.

* * *

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

32

Taharuki!


Saa 8:20 mchana…

KATIKA stendi ndogo ya mabasi ya Itobo kulikuwa na watu wawili tu waliokuwa wamesimama; mwanamume na mwanamke. Yule mwanamume alikuwa kijana wa rika langu na alikuwa amevaa suruali nyeusi ya kitambaa cha kadeti na shati la pundamilia la mikono mirefu. Alikuwa na ndevu nyingi zilizozunguka kidevu chake na alikuwa amezinyoa kwa mtindo maarufu wa “O”, raba nyeupe miguuni na alivaa miwani ya macho.

Kisha macho yangu yalihama kutoka kwa yule mwanamume na kuhamia kwa mwanadada aliyekuwa amesimama pembeni yake akiwa amemuegemea kwa mahaba. Na hapo nilijikuta nikipatwa na mshtuko mkubwa.

Yule msichana alikuwa na umbo kubwa lililovutia mno lenye kiuno chembamba mfano wa mdudu dondola, umbo lake lilikuwa mfano wa namba 8, ni kama vile nilikuwa naangalia fungu la nyanya mbili zilizopangwa kiustadi, nyanya kubwa ikiwa chini na ndogo imewekwa juu yake. Hata hivyo, hicho si kitu kilichonipa mshtuko. Alikuwa anafanana sana na Zakia.

Nilihisi kama vile nilikuwa namtazama Zakia, nilihisi kabisa kuwa kama si yeye basi huyo alikuwa pacha wake! Na kwa mwonekano wa haraka tu alionekana kuwa hakuwa amezidi miaka ishirini na mbili. Ni umri ule ule wa Zakia! Ilikuwa ajabu sana! Na hapo nikahisi kijasho jepesi kikianza kutiririka mgongoni kwangu.

Msichana yule alikuwa mrefu wa wastani na mweupe kwa rangi, ni kama aliyokuwa Zakia. Alikuwa na mashavu mfano wa chungwa, nywele zake nyingi zilikuwa zimesukwa kwa ustadi mkubwa. Uso wake ulikuwa wa mviringo na macho yake yalikuwa makubwa kidogo yenye kung’ara kama nuru. Na alivaa gauni zuri la kitenge lililoshonwa na kudariziwa vizuri kwa nyuzi za dhahabu na kuushika mwili wake huku likilichora vema umbo lake maridhawa alilotunukiwa na muumba.

Muda huo alikuwa amesimama pembeni ya yule mwanamume akiwa ameegemeza kichwa chake kwenye bega la mwanamume huyo, na mkononi alishika begi dogo la mgongoni. Sikuhitaji kuambiwa kuwa wale wawili walikuwa ni wapenzi walioshibana au wanandoa kwa jinsi walivyoonekana.

“Oh… another Zakia!” niliwaza huku nikimtazama yule mwanadada kwa umakini.

Lile basi lilipokuwa limesimama, yule mwanamume aligeuka na kumkumbatia yule mwanadada mwenye umbo namba nane, wakakumbatiana kwa kitambo huku yule mwanamume akionekana kunong’ona jambo kwenye sikio la yule mwanadada na muda huo macho ya abiria wote ndani ya gari letu yalikuwa yakiwatazama kwa umakini.

Kitendo cha wale wenzi kukumbatiana kilinifanya nihisi donge fulani la wivu lianze kunikaba kooni na kupenya ndani ya moyo wangu huku wivu huo ukitishia kuurarua moyo wangu. Wivu huo haukuwa na maana kwamba nilikuwa nampenda yule mwanadada bali ulitokana na tamaa ya ngono, tamaa ya kutaka kujua kama mfanano wake na Zakia ulikuwa ni kwa kila kitu hadi ndani au yeye uzuri wake ulikuwa ni wa nje tu.

“Vipi, mmeoana hivi karibuni nini?” utingo wa basi letu ambaye muda huo alikuwa ananing’inia mlangoni aliwauliza kwa utani wale wapenzi huku akitabasamu.

“Huu ni mwaka wa kumi na mbili na tuna watoto kumi,” yule mwanamume alimjibu yule utingo wa basi letu kwa jeuri huku akionekana dhahiri kuchukizwa na swali lake na hivyo kuwafanya abiria ndani ya basi kuguna.

“Samahani kaka, sikudhamira kukukasirisha,” alisema yule utingo wa basi kwa upole. Alionekana muungawa sana.

“Nami pia sikudhamiria kukukwaza,” yule mwanamume alijibu huku akimkazia macho yule utingo.

Wakati huo yule mwanadada aliyekuwa anafanana na Zakia alikuwa ameinamisha uso wake chini kwa aibu na walikuwa wameachiana, kisha yule mwanadada alipanda ndani ya lile basi na kumpungia mkono yule mwanamume aliyebaki pale chini.

Dereva wa basi hakusubiri tena, aliliondoa gari huku tukimwacha yule mwanamume pale chini akiendelea kupunga mkono wake huku macho yake yakionesha kutoamini kama alikuwa anaachwa. Mbele kidogo nikashuhudia njia panda nyingine, barabara moja ikielekea kushoto na nyingine upande wa kulia. Tukaifuata barabara iliyoelekea kushoto tukiiacha ile nyingine ndogo ambayo baadaye nilifahamishwa kuwa ilielekea eneo lililoitwa Chamipula.

Niliyaondoa macho yangu kuangalia kule nje na sasa yakamlaki yule mwanadada ambaye alikuwa anasogea taratibu hadi eneo la viti vya katikati, pembeni yangu. Aliponisogelea tu pua zangu zikalakiwa na harufu nzuri ya manukato ambayo sikuyajua jina lake lakini yalikuwa manukato yenye kuhamasisha ngono. Alinisalimia na mara moja akayakwepesha macho yake baada ya kugundua kuwa nilikuwa namwangalia usoni kwa makini. Nilishtuka sana, maana hata sauti yake ilikuwa sawa na sauti ya Zakia!

Macho yangu yalianza kazi ya kumkagua tangu miguu iliyosimamia vidole hadi kwenye mikono yake iliyokuwa inasokomeza begi kwenye eneo maalumu la juu la kuwekea mizigo. Alipomaliza kuuweka vizuri mzigo wake alisimama akajiegemeza kwenye kiti nilichokalia, na kama aliyeshtukia kitu, aligeuza shingo yake, akaniangalia kwa umakini.

“Habari yako mrembo?” nilijikuta namsalimia tena ili niisike tu sauti yake.

“Jamani kaka yangu, si tumesalimiana?” yule mwanadada aliniuliza huku akiniangalia kwa mshangao huku akiachia tabasamu.

Nilizidi kuchanganyikiwa kwa sababu sauti yake ilishabihiana sana na sauti ya Zakia, na hata tabasamu lake lilikuwa kama la Zakia, ni kama nilikuwa namwona Zakia akiwa amesimama mbele yangu.

“Basi nitakuwa nimechanganyikiwa!” nilisema huku nikiminya midomo yangu kwa pozi la kimahaba.

“Kipi kimekuchanganya, kaka yangu?” yule mwanadada aliniuliza kwa sauti ya upole huku mshangao ukiwa bado haujamtoka.

“Baada ya kukuona!” nilisema kwa sauti tulivu.

Eddy alinitupia jicho kali lakini niliyakwepa macho yake nikijifanya kama sijamwona. Yule mwanadada alimtupia Eddy jicho mara moja kisha akayahamishia macho yake kwangu.

“Sasa nini kimekuchanganya baada ya kuniona?” yule mwanadada akazidi kunisaili.

“Umefanana sana na msichana mmoja alikuwa mchumba wangu lakini akaolewa na mwanamume mwingine…” nilisema kwa sauti ya kulalamika.

“Ooh! Pole sana,” alisema huku akiniangalia kwa huruma.

“Ahsante… yaani mmefanana sana kwa sura, rangi, umbo hadi sauti,” nilisema huku nikimtupia jicho la wizi Eddy, nikamwona akijiegemeza kwenye kiti chake na kufunga macho.

“Labda ndiye mimi!” yule mwanadada alisema kwa utani huku akiona aibu.

Nilichogundua ni kuwa macho yake yalijaa aibu na alikuwa hawezi kumtazama mwanamume usoni kwa sekunde tano mfululizo bila kukwepesha macho yake na kuangalia kando kwa jinsi alivyojaa haiba ya aibu.

“Inawezekana, au pengine ni pacha wake,” nilisema huku nikiendelea kumtazama usoni kwa tabasamu. Nilitaka aendelee kuongea ili nizidi kuisikia sauti yake.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

33

“Kama ni mapacha basi labda wa nje…” alinijibu huku akitabasamu kisha akaongeza huku akionekana kuvutiwa na maneno yangu. “Kwa hiyo baada ya kuolewa na mwanamume mwingine hukutafuta msichana mwingine?”

“Sijabahatika kumpata mwingine mwenye sifa kama zake. Ungekuwa hujawahiwa pengine ungechukua nafasi yake maana mnaendana sana,” nilimwambia yule mwanadada katika namna ya kumtania ingawa moyoni nilikuwa namaanisha na nilipania kuanzisha uhusiano wa kimapenzi.

“Mmh, ya kweli hayo? Wasichana wazuri waliojaa kila mahali utasemaje huoni mwenye sifa labda kama hutaki! Nina hakika wapo wasichana maelfu ambao wangependa waolewe na wewe,” yule msichana alisema huku akitabasamu kwa aibu.

“Kweli?” niliuliza kama punguani.

“Kweli. Unaonekana una kila kitu ambacho mwanamume yeyote angependa kuwa nacho na msichana yeyote angependa kuwa nawe! Wewe ni mtanashati, nadhifu na unaonekana umesoma vizuri… sina uhakika lakini nadhani pia unazo dola za kutosha!” yule mwanadada alisema na kubetua midomo yake. Nikacheka kidogo.

“Inawezekana ni kweli ninavyo vyote hivyo, isipokuwa sina msichana wa kunipenda!” nilisema kwa sauti ya kulalamika lakini iliyojaa mahaba.

“Nina uhakika hao pia wapo, ni kuwa tu hamjakutana!” yule mwanadada alisisitiza.

“Sawa, niombee kwa Mungu nimpate msichana mwenye sifa kama zako!” nilimchombeza.

“Usijali, naamini Mungu atakupa msichana atakayekupenda sana!” yule mwanadada alisema na kushusha pumzi.

“Amen, na awe kama wewe kwa kila hali!” nilizidi kuchombeza.

“Mmh!” yule mwanadada aliguna huku akitabasamu kwa aibu.

“Mbona unaguna?” nilimuuliza huku nikimtazama kwa umakini usoni.

“Hapana, asiwe kama mimi kwa sababu mimi tayari ninaye mtu tunayependana bali huyo awe mpenzi wako, mke wako na akupende nawe umpende…” yule mwanadada alisisitiza.

“Amina!” nilijibu huku nikikunjia mikono yangu kifuani kama niliyekuwa nasali.

Muda huo basi la Makenga lilikuwa linazidi kuchanja mbuga na tulikuwa tumeuacha mbali ule mji mdogo wa Itobo na kutokomea mbele zaidi huku tukikatisha katikati ya mashamba na vichaka vichache vilivyoonekana kando ya barabara.

“Lakini kwa nini mchumba wako alikubali kurubuniwa na mwanamume mwingine na akakuacha?” yule mwanadada aliniuliza kwa shauku.

“Dah, we acha tu. Ni historia ndefu sana na sidhani kama atanitoka moyoni mwangu mpaka nakufa. Ndiyo maana nilipokuona nikashtuka sana na kujikuta nikichanganyikiwa,” nilisema kwa uchungu.

“Ooh! Pole sana,” Zakia alisema huku akinitazama kwa huzuni.

“Asante,” nilijibu huku nashusha pumzi.

Sasa nilihisi mwili wangu ukichemka kwa tamaa, hasa nilipozikumbuka kashkash za Zakia katika uwanja wa huba, nilipanga nimuulize yule mwanadada kama alikuwa anamfahamu Zakia, kabla sijauliza yule kondakta wa lile basi akiwa na mkoba wa fedha na kitabu cha tiketi alifika na kusimama mbele ya yule mwanadada na kunyoosha mkono wake kudai nauli huku akitengeneza tabasamu jepesi usoni kwake.

Yule mwanadada alifungua pochi yake ndogo aliyokuwa ameishika mkononi na kutoa noti ya shilingi 5,000 kutoka kwenye ile pochi kisha akanyoosha mkono wake kumpa yule kondakta wa basi huku akionekana kuyakwepa macho yake makali yaliyokuwa yanamtazama kwa makini. Na hapo nikashuhudia macho ya yule kondakta wa basi yakijikita zaidi kwenye kulitazama umbo la yule mwanadada. Pasipo kuambiwa na mtu yeyote nikajua kuwa jamaa alikuwa amebabaishwa sana na uzuri wa yule mwanadada.

Yule mwanadada aliendelea kunyoosha mkono wake kwa kondakta wa basi huku akiwa ameangalia kando kuyakwepa macho yake lakini yule kondakta alionekana kusahau wajibu wake na kuendelea kumtazama kwa kitambo huku akionekana kuvutiwa mno na umbo la yule mwanadada. Kitendo kile kilimfanya yule mwanadada kutopendezwa na tabia ile ya kutazamwa, alimsisitiza yule kondakta achukue ile fedha ya nauli.

Yule kondakta alijishtukia na kugeuza shingo yake kunitazama kwa aibu huku akizuga na kuipokea ile noti kisha aliandika tiketi, hata hivyo aliendelea kumtupia jicho la wizi yule mwanadada, jicho lililoonesha matamanio makubwa ya kimwili. Na hapo nikajua kuwa yule kondakta alikuwa mkware kama mimi.

Wakati yule kondakta wa basi akiondoka simu ya yule mwanadada, aina ya Samsung Galaxy S8 ikaanza kuita. Aliitazama kwa umakini na kunitupia jicho la wizi lililojaa aibu na alipoona bado namtazama akayakwepesha haraka macho yake na kuangalia kando huku akiipokea ile simu, kisha akaanza kuzungumza kwa sauti ya chini sana akiwa hataki niyasikie maneno. Ilikuwa ni sauti ya kimahaba, sauti ya kubembeleza.

Muda huo nilikumbuka kugeuza shingo yangu taratibu kumtazama yule mrembo wa shani aliyekuwa ameketi kule kwenye viti vya nyuma. Nikamwona akiitazama saa yake ya mkononi kwa umakini, na nilichokishuhudia kutoka usoni kwake ilikuwa ni hali ya kupoteza utulivu na kwa namna nyingine nilimwona ni kama aliyekuwa amezama kwenye fikra fulani.

Kisha niliyarudisha macho yangu kumtazama yule mwanadada mwenye umbo la kuvutia la namba nane aliyekuwa amesimama kando yangu, alikuwa bado anazungumza na mtu kwenye simu, na kwa namna akivyokuwa anazungumza nilihisi kuwa huyo mtu upande wa pili wa simu alikuwa ni yule mwenzi wake. Baada ya dakika kadhaa za mazungumzo alimaliza na kukata simu, na hapo nikakohoa kidogo.

“Vipi, umpendaye anasemaje?” nilimuuliza swali la uchokozi, akanitupia jicho la wizi huku akajifanya hajanisikia na kubaki kimya. Kisha aligeuka haraka upande mwingine huku akinipa mgongo hali iliyoonesha kuwa hakutaka kunipa nafasi ya kuendelea kumsaili.

Sikutaka kuendelea kumsemesha baada ya kuonesha kunikwepa na badala yake kwa dakika kadhaa nilianza kumchunguza na kugundua kuwa alikwisha nishtukia dhamira yangu, kwani alikuwa anageuza shingo yake mara kwa mara kunitazama kwa jicho la wizi katika namna ambayo kwa kweli sikuweza kuielewa.

Nilimbonyeza kidogo Eddy kwenye paja lake na kumwonesha kwa ishara kwa yule mwanadada. Kama kawaida yake, Eddy alimtupia jicho yule mwanadada mara moja tu na hakuonesha tashwishwi yoyote usoni kwake kisha akanitazama kwa mshangao.

“Nimeyasikia yote uliyokuwa unamwongopea, naomba usipende kucheza na hisia za wanawake,” Eddy aliniambia kwa sauti tulivu ya chini lakini iliyoonya.

“Najua hupendi, lakini wakati mwingine inakuwa vigumu sana kujizuia,” nilisema huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani na kumtupia jicho yule mwanadada.

Wakati huo alikuwa ameinamia simu akitazama picha na kuperuzi taarifa kwenye mitandao. Wakati akiendelea kuperuzi kuna wakati alikuwa anacheka, anatoa mguno au anashangaa!

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

34

“Natamani na mimi nicheke na kushangaa,” nilimsemesha yule mwanadada kwa nia ya kutaka kuanzisha tena mazungumzo baada ya kushindwa kuvumilia.

Yule mwanadada alinigeukia na kunitazama mara moja tu bila kusema neno, kisha akayaondosha macho yake kwangu na kuyarudisha kwenye simu yake. Kitendo kile kikanifanya nianze kujilaumu kwa kuwa nilianza kuonekana kuwa najipendekeza sana na pengine ndiyo maana aliamua kunidharau.

Am sorry kama nimeanza kuwa msumbufu kwako,” nilimwambia yule mwanadada na kujiegemeza kwenye kiti changu kisha nikakikumbuka kile kitabu cha Rosa Mistika nilichokuwa nasoma kabla ya ujio wake. Yule mwanadada hakunijibu bali alinitupia jicho la wizi huku akiachia tabasamu la aibu.

Lile basi la Makenga lilikuwa linaenda mwendo wa kasi na dereva alionekana kuwa makini sana akionesha kuizoea vizuri ile barabara ya changarawe. Nilikumbuka kuwa kabla gari halijasimama pale Itobo nilikuwa nasoma riwaya ya Rosa Mistika na hivyo nikafungua kurasa mbili tatu za kile kitabu nikitafuta sehemu nilipokuwa nimeishia kisha nikajaribu kusoma aya mbili tu na kukifunga tena baada ya kugundua kuwa nilikuwa sielewi chochote, kwa kuwa akili yangu haikuwa pale kwenye kitabu.

Sasa ilionekana kuwa uwepo wa yule mwanadada mwenye umbo la namba nane karibu yangu ulikuwa umeifanya akili yangu isitulie kabisa. Muda huo nilijikuta naanza kufikiria jinsi ya kuendeleza mazungumzo kati yangu na mwanadada yule ili tufahamiane zaidi, na ikiwezekana tuwe pamoja jioni ya siku hiyo baada ya kufika katika mji wa Kahama.

Mwendo wa basi letu ulikuwa siyo wa kubabaisha, mara tulikifikia kijiji kimoja ambacho sikufahamu kiliitwaje, nilipoangalia vizuri nililiona jengo moja kubwa na zuri la kanisa lililokuwa takriban mita 100 toka pale barabarani, nikaamua kumuuliza yule mwanadada mwenye umbo la namba nane kuhusu jina la kile kijiji.

“Panaitwa Lububu,” yule mwanadada alinijibu kwa mkato bila hata kunitazama kwani macho yake yalikuwa bado yapo kwenye kioo cha simu yake aliyoshika mkononi.

Pale katika stendi ndogo ya mabasi ya Kijiji cha Lububu kulikuwa na kikundi cha watu zaidi ya kumi, wanawake kwa wanaume na watoto, waliokuwa wamesimama chini ya mti mkubwa kando ya barabara wakisubiria usafiri. Basi la Makenga lilisimama na hapo niliwashuhudia wale watu wakikumbatiana na kuagana kisha abiria wawili tu, wote wanawake, walipanda na wale wengine walibaki pale chini wakipunga mikono yao.

Basi liliondoka huku wale wanawake waliopanda garini wakiendelea kuwapungia mikono wale waliobakia pale stendi ya Lububu, na muda mfupi baadaye gari likaanza kuyaacha makazi ya watu katika kijiji kile. Baada ya mwendo wa takriban dakika tano tayari tulikuwa tumekiacha nyuma kile kijiji na hapo dereva akaongeza kasi na gari likawa linakwenda kwa mwendo wa kupaa huku tukianza kuingia katikati ya vichaka na miti mirefu katika pori dogo.

Barabara ile ilikuwa inakatisha katikati ya vichaka vile na kwa mbali niliweza kuona mashamba na nyumba moja moja zikiwa mbalimbali sana, na hapo basi letu likaanza kushuka bonde dogo kwa mwendo wa kasi huku likijitahidi kukata upepo na kutokomea mbele zaidi. Hakuna aliyekuwa anaongea wakati huo na hivyo ndani ya gari kulitawaliwa na kiasi kikubwa cha ukimya wa namna yake. Hata hivyo, safari bado ilikuwa inaendelea.

Niligeuza tena shingo yangu kuangalia nyuma, na kwa kupitia kioo cha nyuma cha madirisha niliweza kuona wingu kubwa la vumbi nyuma yetu likitimka kutokana na ule mwendo wa kasi wa lile gari.

Wakati safari ikiendelea nilikata shauri la kuanzisha tena mazungumzo ya kirafiki na yule mwanadada mwenye umbo la namba nane, lakini nilipomtazama kwa umakini usoni sikuona tashwishwi yoyote ya urafiki baina yetu katika uso wake kwani alionekana kuzama kwenye lindi la mawazo.

Muda huo tulikuwa tunaanza kushuka mteremko fulani mrefu na mbele yetu kulikuwa na kona kali iliyokuwa inapinda kuingia upande wa kushoto, mara nikahisi tena kuwa mwendo wa gari letu ukipungua kwa ghafla huku gari likianza kuyumba. Hisia mbaya zilinijia akilini na haraka nikainua kichwa changu na kuyapeleka macho yangu kule mbele yetu kuangalia kulikuwa na nini.

Nilipotazama vizuri kule mbele niligundua kuwa kulikuwa na kundi kubwa la ng’ombe waliokuwa wanakatisha barabara kutoka upande mmoja wa barabara na kuelekea upande wa pili na kijana mdogo aliyekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 14 na 16, mchungaji wa ng’ombe, alionekana kushtuka sana baada ya kuliona basi la Makenga likija katika uelekeo wake kwa mwendo wa kasi, na hivyo alikuwa anahangaika kuwaswaga wale ng’ombe haraka haraka akijaribu kushindana na kasi ya lile basi.

Nilimshuhudia dereva wa basi letu akijitahidi kupangua gia huku akipunguza mwendo na kulifanya gari kuyumba huku na kule wakati akijaribu kuwakwepa wale ng’ombe waliokuwa wanakimbia ovyo barabarani. Kitendo kile cha gari kuyumba huku na kule kilimfanya yule mwanadada mwenye umbo la namba nane aliyekuwa amezama kwenye lindi la mawazo kushtuka na kuanza kuyumba kama aliyekuwa na mapepo.

Nilimshuhudia akijitahidi kujishikilia vyema kwenye bomba lililokuwa linapita juu katikati ya uchochoro wa basi uliotenganisha viti vya upande mmoja na mwingine lakini hakuweza, hivyo akaanguka kama mzigo akiangukia juu ya mapaja yangu.

Kwa kuwa nilikuwa nimemshuhudia tangu alipoanza kuyumba, hivyo hakuwa amenishtukiza, kwa maana nyingine nilikwisha jiandaa kwa tukio la kumdaka na aliponikalia tu nikazungusha haraka mikono yangu kumkumbatia. Akawa amenikalia juu ya mapaja yangu kitendo kilichonifanya nijisikie faraja sana kukaliwa mapajani na yule mwanadada.

“Pole sana, mrembo!” nilinong’ona sikioni kwake kwa sauti tulivu huku nikiachia tabasamu la kirafiki.

Yule mwanadada mwenye umbo la namba nane hakunijibu bali alionekana kuzuga na kuyafumba macho yake akijaribu kupambana na aibu ya kiutu uzima huku akiwa bado ameketi juu ya mapaja yangu.

I hope hujaumia!” niliongea huku nikizidi kumsaili kwa macho katika namna ya kutengeneza mazingira ya kutufanya kuwa karibu zaidi. Mwanzo yule mwanadada hakunijibu badala yake alijiinamia kwa aibu, kisha akajiinua taratibu kutoka kwenye mapaja yangu huku akiendelea kutabasamu kwa aibu.

“Usijali kaka yangu, wala sijaumia,” hatimaye alinijibu huku akiendelea kuyakwepa macho yangu. Hata hivyo, harufu nzuri ya manukato aliyojipulizia ikazidi kuzipa uhai pua zangu wakati akiinuka kutoka pale kwenye mapaja yangu.

Eddy alinitazama kwa umakini akataka kucheka kisha akayahamisha macho yake kumtazama yule mwanadada mwenye umbo la namba nane na kutabasamu huku akiachia mguno uliomfanya yule mwanadada ageuke kumtazama huku akiachia tabasamu la aibu.

Muda wote dereva wa lile gari alikuwa akiwakwepa wale ng’ombe walioonekana kuwa wengi huku gari likiwa bado linaserereka, kisha nikamwona akimkosakosa yule kijana mdogo aliyekuwa anajitahidi kuwaswaga ng’ombe wa mwisho.

Utingo wa gari letu ambaye muda wote alikuwa ananing’inia mlangoni alimpigia kelele ya kumlaani yule kijana mchungaji wa mifugo. Baada ya kuwavuka wale ng’ombe gari letu halikwenda mbali sana mara kishindo kikubwa kilichoambatana na mtikisiko wa gari kikasikika na kutushtua abiria wote tuliokuwemo ndani ya lile gari.

Baadhi ya mizigo ilidondoka kutoka kwenye sehemu maalumu ya juu ya kuwekea mizigo na kuwaponda abiria vichwani huku hali ile ikizua taharuki. Nilishuhudia abiria wengi hususan wanawake, akiwemo yule mwanadada mwenye umbo la namba nane wakipiga yowe kubwa la hofu kutokana na tukio lile.

Yule mwanadada alijikunyata kwa hofu huku akiyatoa macho yake na wakati huo huo alinitupia jicho, na macho yetu yalipokutana niliweza kuiona hofu kubwa iliyokuwa imejengeka usoni kwake. Nilimshika mkono wake taratibu huku macho yangu yakimweleza nini alichopaswa kufanya muda ule. Nilikuwa nimedhamiria kumketisha juu ya mapaja yangu, kwa madai kuwa huo ndiyo ulikuwa usalama wake.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

35

Tukiwa katika hali ile akili yangu ikarudishwa mle ndani ya basi baada ya lile gari kuyumba tena na kuonekana likilala upande wa kushoto huku dereva wetu akizidi kung’ang’ana na usukani katika kujaribu kulidhibiti basi lisitoke nje ya barabara na kuingia kwenye korongo kubwa lililokuwa pembeni kabisa ya barabara.

Nilijikuta namsifu sana yule dereva kwani alionekana kuwa makini zaidi ingawa niligundua kuwa damu ilikuwa inamchemka mwilini kwa hofu. Kwa hali hiyo akawa anapangua gia huku akizidi kuudhibiti usukani na wakati huohuo akipunguza mwendo taratibu na hivyo kulifanya lile gari liyumbeyumbe barabara nzima.

Muda huo huo nilimwona utingo wa lile gari akiruka na kutua chini haraka huku akiwa makini zaidi kutazama huku na kule kujaribu kubaini nini lilikuwa tatizo la lile gari. Hatimaye dereva alifanikiwa kudhibiti ajali, kwani lile gari lilikwenda kugota kwenye ukingo wa barabara huku injini yake ikiendelea kuunguruma.

Nikiwa nimeupisha utulivu akilini mwangu, mitupo ya mapigo ya moyo wangu ilikuwa imeongezeka kasi mara dufu huku nywele zangu zikiwa zimenisimama kwa tahadhari.

“Gurudumu la mbele limepasuka!” yule utingo wa basi alisema kwa sauti huku akiwa analitazama gurudumu la mbele upande ule wa kushoto. Na hapo nikaona abiria wakitulia kidogo, ingawa walikuwa bado wamejawa na hofu. Niliitazama saa yangu na kuona kuwa ilikuwa imetimia saa 8:55 mchana.

Abiria wote tulianza kushuka kutoka ndani ya lile basi la Makenga huku wengi wakimlaani yule kijana mdogo aliyekuwa anaswaga mifugo ambaye muda huo alikuwa anazidi kutokomea porini na mifugo yake, kuwa ndiye aliyesababisha gurudumu lipasuke. Baada ya kushuka pale chini abiria wakaanza kuzagaa kwenye eneo hilo huku kila mmoja akiwa bado hajatokwa na hofu.

Sisi wanaume tulielekea upande wa mashariki wa ile barabara na kufungua zipu zetu za suruali ili ‘kuchimba dawa’ kwenye vichaka vifupi vilivyokuwa peupe, na wanawake walielekea upande mwingine wa barabara kwenye vichaka vilivyojificha.

Baada ya kuchimba dawa nilirudi haraka pale kwenye gari nikitaka kujua hatma ya safari yetu, na wakati nilipokuwa nasogea pale nilimsikia dereva wa lile gari ambaye muda huo alikuwa ameinama akilitazama lile gurudumu lililopasuka, akiongea na kondakta wake. “Fanyeni fanya fasta basi ili tusiuweke.”

Yule kondakta wa basi aliingia ndani ya basi haraka na kuinua siti ya mbele akaonekana kupekuapekua hapa na pale kisha alifanikiwa kupata jeki ndogo ya gari, halafu aliinama kwenye sanduku dogo jeupe la chuma lenye vifaa vya matengenezo ya dharura ya lile gari, juu ya sanduku lile la chuma kulikuwa na maandishi mekundu yaliyosomeka vizuri; “Tools Box”.

Alilifungua lile sanduku na kutoa spana kadhaa muhimu na muda mfupi uliofuata alikuwa mbele nje ya lile gari upande ule wa kushoto akitia jeki na kulifungua lile gurudumu lililopasuka.

“Oya, na wewe leta fasta gurudumu la akiba tufunge tuondoke. Leo sitaki kabisa tufike Kahama usiku,” yule dereva alimwambia utingo wa lile basi kwa msisitizo baada ya kumwona kondakta akimalizia kulifungua lile gurudumu lililopasuka.

Kazi ya kulifungua lile gurudumu ilikuwa imefanywa na yule kondakta kwa wepesi wa hali ya juu na ndani ya muda mfupi tu akawa amefanikiwa kulitoa na kulikokota haraka hadi kule nyuma ya gari kwenye buti la gari ambako yule utingo alikuwa amesimama akijaribu kufungua haraka haraka mlango wa buti kwa kutumia chuma fulani.

Mara nikawaona wote wawili, yule kondakta na utingo wa gari wakisimama na kujishika kiuno huku wakiwa wamepigwa na butwaa, mdomo wa kondakta ulikuwa wazi kwa mshangao. Nilimwona akifikiria kidogo kisha akakimbilia kule mbele kwa dereva aliyekuwa bado amesimama pale pale akiwa ameinamisha kichwa chake. Muda huo alionekana kuwa mbali kimawazo.

“Dah, gurudumu la akiba halimo!” yule kondakta alisema kwa mshangao huku akimtazama dereva wake kwa wasiwasi.

Asalallee! Si tumesahau kulipitia pale kwa Suma mziba pancha!” yule dereva wa basi alimaka kwa mshangao huku akishika kiuno chake katika namna ya kukata tamaa. Kisha kilipita kitambo kifupi cha ukimya huku wakitazamana kwa namna ya kukosa majibu.

Niliwatazama kwa umakini na hapo nikajikuta nikianza kupoteza matumaini kabisa ya kufika mapema mjini Kahama. Niliitazama saa yangu na kugundua kuwa ilikuwa imeshatimu saa 9:15 alasiri. Muda huo abiria wengine walikuwa wameanza kujikusanya makundi makundi wakijadiliana hili na lile.

Niligeuka kumtazama Eddy nikamwona akiwa amesimama ng’ambo ya pili ya barabara, muda huo alikuwa anapangusa vumbi kwenye viatu vyake kwa kutumia kipande cha sponji. Kisha macho yangu yalianza kumtafuta mmoja wa wale wadada warembo. Mara nikamwona yule mwanadada mwenye umbo la namba nane aliyekuwa anafanana na Zakia akiwa amesimama kando kabisa, peke yake, huku akiongea na simu, na muda wote alikuwa analitazama lile gari huku akiwa amekata tamaa.

Sikutaka kulaza damu, nilianza kupiga hatua zangu haraka kumfuata yule mwanadada nikiwa na lengo moja tu la kujaribu bahati yangu, nilikuwa nimepania kweli kweli kumpata mrembo wa kuniliwaza nikifika Kahama japo kwa kipindi kifupi ambacho ningekuwa katika mji huo wa Kahama.

Niliiona kuwa ile ndiyo ilikuwa fursa yangu ya pekee ya kuongea naye, nikaongeza mwendo na hatimaye miguu yangu ikawa myepesi ghafla na hivyo kujikuta nikimsogelea huku nikiitoa ile miwani ya jua niliyoivaa huku uso wangu ukianza kutengeneza tabasamu la kirafiki. Wakati namkaribia nikamwona akimaliza kuongea na simu na kugeuka kuangalia upande ule niliokuwa natokea.

“Habari za mida mrembo wangu?” niliwahi kumsalimia yule mwanadada mwenye umbo la namba nane kabla hajafanya lolote, na muda huo nilikuwa naining’iniza miwani yangu sehemu ya kifuani yenye upenyo katikati ya vishikizo viwili vya shati langu.

Yule mwanadada aliniangalia kwa umakini kidogo kama aliyekuwa ananifananisha kabla ya kulegeza uso wake na kuachia tabasamu.

“Ah, salama tu Mr Handsome Man,” hatimaye yule mwanadada aliitikia salamu yangu huku akinitazama kwa utulivu.

“Naitwa Jason Sizya,” nilijitambulisha kwa kujiamini huku nikinyoosha mkono wangu kwake, uso wangu ulikuwa umepambwa na tabasamu la kirafiki.

Kwa hakika tabasamu langu lilifanikiwa kuziteka hisia za yule mwanadada kwani nilimwona akipumbazika kidogo na utanashati wangu. Aliniangalia kwa umakini zaidi machoni katika namna ya kunisaili, na hapo nikaliona tabasamu lake maridhawa la aibu likichomoza usoni kwake na kuufanya mtima wangu usuuzike.

“Nafurahi kulifahamu jina lako,” yule mwanadada alisema huku akinyoosha mkono wake laini na kuukutanisha na wa kwangu, kisha akanipiga swali la papo kwa papo, “Halafu ulisema unataka kucheka na kushangaa?”

Swali lile lilinishtua kidogo kwani sikuwa nimekumbuka kuwa tulipokuwa ndani ya gari nilimwambia kuwa natamani na mimi nicheke na kushangaa nilipomwona akiperuzi kwenye simu yake na wakati fulani akionekana kucheka na kushangaa.

“Ah, hapana nilikuwa natania tu!” nilisema huku nikiachia kicheko hafifu cha kirafiki.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

36

“Oh, kumbe! Lakini sidhani kama mimi na wewe ni watani!” yule mwanadada alisema kwa utani huku naye akiangua kicheko hafifu. Muda huu alionesha kuchangamka zaidi.

Katika maisha yangu sikupenda kabisa kuona mrembo yeyote akinipita pasipo kumchombeza maneno mawili matatu ya mahaba. Kwangu lilikuwa kosa kubwa sana kumwacha mrembo kama yule aondoke bila kutupia maneno matamu.

“Lakini kuna utani na u-ta-ni,” nilisema huku nikicheka kidogo. “Enhe sijui unaelekea wapi mrembo wangu?” nilimuuliza yule mwanadada huku nikimtazama kwa tabasamu.

“Naelekea Kahama mjini!” yule mwanadada alinijibu huku akishusha pumzi zake taratibu na kunitazama moja kwa moja machoni katika namna ya kuuliza. “Bila shaka na wewe unaelekea Kahama mjini?”

“Ndiyo, tunaenda Kahama mjini, nipo na kaka yangu yule kule,” nilisema huku nikigeuza shingo yangu kumwonesha yule mrembo kule alikokuwa amesimama Eddy. “Lakini ni mara yetu ya kwanza kwenda Kahama.”

Yule mwanadada aligeuza shingo yake kumtazama Eddy kwa kitambo kidogo, kwa utulivu, huku uso wake ukishindwa kuonesha tashwishwi yoyote na hatimaye akaniuliza tena. “Mnakwenda Kahama kwa shughuli gani?”

“Tunakwenda kikazi. Vipi wewe unakwenda kwa shughuli gani huko Kahama?” niliongea kwa sauti tulivu na papo hapo nikamtupia swali.

“Mimi nakwenda nyumbani, nimezaliwa na kukulia Kahama, na huko ndiyo ninakoishi hadi sasa,” yule mwanadada alijibu kwa utulivu huku akinitazama katika namna ya kuonesha kufurahishwa na maongezi.

“Na pale Itobo tulipokukuta ni kwa nani?” nilimuuliza yule mwanadada kwa namna ya kutaka kuufahamu undani wake.

Swali langu lilimfanya ayakwepeshe macho yake na kuangalia kando ili yasikutane na macho yangu, alitulia kidogo huku akinikata jicho la kiaina, na namna ya utazamaji wake ilinifanya nihisi kuwa alikuwa anatafuta jibu la uongo.

Wakati huohuo niligeuza shingo yangu kutazama kule kwenye gari na kumwona utingo wa basi akichukuwa mtalimbo, yaani chuma fulani kirefu chenye umbo bapa na kuanza kukita juu ya ringi la lile gurudumu lililopasuka huku akilizunguka, na baada ya muda mfupi akawa anatembea juu yake akilizunguka kisha akaligeuza na kutembea tena juu yake.

Baada ya kutembea kwa muda juu ya gurudumu akachukua mtalimbo na kuuingiza katikati ya mpira wa gurudumu na ringi, akaukandamiza chini ule mpira dhidi ya ringi, kwa mguu. Kisha akaingiza mtalimbo wa pili karibu na pale ulipokuwa umechomekwa ule mtalimbo wa kwanza na kisha akauchomoa ule wa kwanza kwa nguvu, kitendo kile kilisababisha sehemu ya mpira wa ndani wa lile gurudumu (tube) kutoka nje ya ringi, kisha akaingiza tena mtalimbo. Niliachana na yule utingo na kumgeukia tena yule mwanadada aliyefanana na Zakia huku macho yangu yakimsaili.

“Hujaniambia bado, pale Itobo tulipokukuta ni kwa nani?” nililirudia tena swali langu huku nikizidi kumkazia macho.

“Kwa mchumba wangu! Kwani hukumwona pale stendi alipokuwa amenisindikiza?” hatimaye yule mwanadada alisema baada ya kusita kidogo.

“Oh, kumbe yule handsome boy aliyekusindikiza pale stendi ndiye mumeo mtarajiwa?” nilimuuliza yule mwanadada nikiwa natabasamu ingawa moyo wangu ulionekana kukosa utulivu kidogo.

“Mmh, mbona yule si handsome boy kama wewe, ni wa kawaida tu!” yule mrembo alisema huku akicheka kidogo.

Na hapo nikapata nafasi nzuri ya kuyaona meno yake meupe yaliyopangika vizuri katika kinywa chake huku yakiachia uwazi mdogo kwa mbele (mwanya) na kumfanya aonekane mrembo zaidi.

“Lakini huyo si ndo mtarajiwa?” nilimuuliza huku nikiwa nimeyatuliza macho yangu kwenye uso wake.

“Ndo huyo huyo, au unadhani kuna mwingine zaidi yake?” yule mwanadada alisema kwa sauti laini katika namna ya kujidai huku akiangua kicheko hafifu. “Mungu akipenda, mwakani tutakuwa mume na mke.”

“Hongera sana,” nilimwambia yule mwanadada na kuangua kicheko hafifu kisichokuwa na maana yeyote kisha nikaongeza, “Sasa mbona amekuacha uondoke peke yako, haogopi kuibiwa na wanaume wakware?”

“Aogope nini wakati ananiamini na mimi nampenda yeye tu! Ingekuwa kuibiwa angeshaibiwa siku nyingi sana,” yule mwanadada alisema kwa sauti tulivu.

“Safi sana. sasa kama unaishi Kahama na huku Itobo ulikuja kwa ishu gani, au ndiyo ulimkumbuka mzee?” nilimuuliza yule mwanadada huku nikitabasamu.

“Nilikuja kumjulia hali, alikuwa anaumwa. Au kuna kosa?” yule mwanadada alisema kwa namna ambayo sikuelewa alikuwa anamaanisha nini na muda huo alikuwa ananitazama kwa udadisi zaidi.

“Wala hakuna kosa kwenda kumsalimia mchumba wako hata kama haumwi, ila nimeguswa tu kuuliza. Kwani kuna ubaya?” nami nilimuuliza katika namna ya kujitetea.

“Hakuna ubaya wowote! Una haki kabisa kuuliza,” yule mrembo alijibu kisha kikazuka kimya cha kitambo kifupi, kabla ya yule mrembo kuvunja ukimya. “Karibu nyumbani kwetu Kahama.”

“Natamani sana nikaribie ila naogopa nisije nikakuponza…” nilisema katika hali ya kutaka kuujua mtazamo wake kisha nikaongeza kabla hajasema chochote. “Kwani unaishi sehemu gani hapo Kahama?”

“Wasiwasi wako tu…” yule mrembo alisema huku akiachia tabasamu kisha akaendelea. “Naishi maeneo ya Uwanja wa Taifa karibu na kituo cha kushushia mizigo ya malori. Umewahi kuusikia uwanja wa taifa?” aliniuliza huku akinikazia macho.

“Nimeshausikia mara kadhaa kwa kuwa huwa nafuatilia soka,” nilijibu huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Basi unakaribishwa sana,” yule mwanadada aliniambia kwa msisitizo huku sasa akinitazama usoni pasipo kuyakwepesha macho yake.

“Nitajitahidi sana nifike huko kabla sijaondoka kurudi kwetu, lakini sijui kama tutaweza kukutana tena!” nilisema kwa huzuni huku nikimtazama yule mwanadada kwa umakini.

“Kwa nini tusikutane? Kama ni mpango wa Mungu tutakutana tu!” yule mwanadada alisema na kuongeza, “Kwani ninyi mtafikia sehemu gani hapo Kahama, au utaniambia pia hujui mnafikia wapi kwa kuwa hamjawahi kufika!”

“Eneo hasa sijui linaitwaje ila mwenyeji wetu ametuelekeza kuwa tukishuka tuchukue teksi hadi Sambo Picnic Centre, huko ndiko anapoishi. Sijui unapafahamu?” nilimuuliza yule mwanadada huku nikimtazama kwa utulivu katika namna ya kuzidi kutengeneza urafiki, tabasamu likiwa limeshindwa kwenda likizo usoni kwangu.

“Sambo Picnic Centre!” yule mwanadada aliuliza kwa mshangao mkubwa huku akinitazama kwa namna ambayo sikupata tafsiri yake haraka, hata hivyo niliweza kugundua kuwa alikuwa ananitazama kwa namna ambayo alishaanza kunihusudu.

“Ndiyo… kwani unapafahamu?” nilimsaili.

“Napafahamu, tena sana tu. Kwani huyo mwenyeji wenu anaitwa nani?” yule mwanadada aliniuliza kwa pupa, na hapo nikapata mshawasha wa kutaka kujua kwa nini alikuwa ameshangaa sana nilipomtajia jina la Sambo Picnic Centre.

“Anaitwa Swedi Mabushi. Sijui unamfahamu?” nilimuuliza tena huku nikiyatuliza macho yangu usoni kwake nikiwa na hamu kubwa ya kutaka kujua jibu lake.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

37

“Swedi!” yule mwanadada alilitamka jina hilo kwa mshangao. “Hata yeye namfahamu, tena sana tu!” aliongea kwa sauti ya kujiamini na kuzidi kuniacha na mshangao, lakini kabla sijauliza aliongeza, “Swedi ni shemeji yangu, amemuoa dada yangu mkubwa. Na anapoishi siyo mbali kutoka nyumbani kwetu!” yule mwanadada aliniambia na kunifanya nishangae mno.

“Duh! Bahati iliyoje!” niliwaza huku nikiuona ukaribu wetu ukizidi kusogezwa karibu zaidi.

“Hata hiyo Sambo Picnic Centre ni ya baba yetu, na mke wa Swedi ndiye anayeisimamia,” yule mwanadada aliniambia na hapo nikagundua kwa nini alishangaa nilipotaja jina hilo.

“Oh, kumbe!” nilisema huku moyoni nikifurahi sana kwa kuwa niliamini kuwa ingekuwa rahisi kumpata na asingeweza kuokoka kwenye mtego wangu, nilianza kujihesabia kuwa mshindi na kwamba nilikuwa nimepata mtu wa kuniliwaza katika muda ambao ningekuwepo Kahama.

“Ndiyo, nyumbani kwetu ni mtaa wa pili tu kutoka hapo Sambo. Naona sasa huna kisingizio, utamwambia Swedi akulete nyumbani uje ututembelee,” yule mwanadada aliniambia huku uso wake ukiwa umepambwa na furaha.

Na hapo alikuwa amenifanya kuyafurahia sana maongezi yake huku nikijipongeza kwa kutolaza damu kwani nilikuwa nimepata mwenyeji halisi ambaye angeweza kunionesha mji niwapo katika mji huo wa Kahama, mji wenye pilika pilika kwa sababu ya kuzungukwa na migodi ya dhahabu.

“Kwani ni safari ya saa ngapi kwa basi kutokea hapa tulipo hadi kufika Kahama?” nilimuuliza yule mwanadada, na baada ya kufikiria kidogo alinijibu.

“Sina uhakika ni mwendo wa saa ngapi kutokea hapa, nadhani ni kama saa moja na nusu hivi,” alisema huku akiilamba midomo yake iliyoanza kukauka kisha akaachia tabasamu.

“Vipi kuhusu hali ya usalama katika Mji wa Kahama?” nilimuuliza swali jingine yule mwanadada, na swali langu likamfanya atabasamu kidogo huku akitazama kando.

“Hali ni shwari kabisa. Kwa nini umeuliza?” alisema huku akikunja sura yake kama mtu aliyekuwa anafikiria jambo fulani lisilo la kawaida.

“Napenda tu kujua kwani hii miji inayozungukwa na migodi huwa ina pilika pilika nyingi na vurugu na hapa na pale,” nilisema huku nikizidi kumchombeza.

“Kwa kweli tunaishukuru sana serikali yetu imejitahidi kudumisha usalama ingawa ni kweli kumewahi kuripotiwa vitendo vichache vya kiharamia,” alisema huku akiilamba tena midomo yake.

Kisha kikatokea kitambo kifupi cha ukimya kila mmoja wetu akizama katika mawazo.

“Tumeongea mengi sana lakini hadi sasa hujaniambia unaitwa nani, mrembo? Maana wote tunaelekea Kahama, sehemu moja, eneo moja na safari yetu bado ni ndefu sana,” nilivunja ukimya nikiongea kwa sauti tulivu huku nikimtazama kwa umakini usoni.

“Mimi?” yule mrembo aliniuliza kwa kuzuga huku akifahamu fika kuwa swali langu lilikuwa linamlenga yeye. Kisha kama aliyejishtukia aliachia tabasamu maridhawa lililochomoza usoni mwake na kukaribia kunitia wazimu. “Naitwa Amanda Gwambasa, na wewe je?”

“Duh, mara hii umeshasahau jina langu?” nilisema huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Aah, ulisema unaitwa nani vile! Sii-zya… yes, Jason Sizya, eh?” yule mrembo aliuliza huku akionesha kusita kidogo kabla hajangua kicheko hafifu na kuongeza, “Kwani wewe ni Mnyamwezi?”

“Ndiyo, kwani sifanani na Wanyamwezi?” nilimuuliza kwa utani huku nikijitazama.

“Unafanana nao sana kwa kila kitu kuanzia utanashati, kimo na hata umbile. Ila sizungumzii hawa Wanyamwezi wa Tabora, namaanisha wale wa Unyamwezini akina P Diddy, Jay Z na wengineo,” yule mwanadada alisema kwa utani huku akiangua tena kicheko.

Nami nilicheka kicheko hafifu bila kusema neno kisha baada ya hapo yakafuata maongezi ya kawaida ya kufahamiana zaidi. Ni katika wakati huo Amanda alinieleza mambo mbalimbali kuhusu maisha yake, uhusiano wake na mwanamume aliyemchumbia na kuuhusu mji wa Kahama na jinsi alivyoufahamu, jambo ambalo lilionekana kunisaidia zaidi kuuelewa mji huo. Mambo mengi aliyoniambia kuhusu Kahama sikuwahi kuyasikia wala kuyafahamu.

Hata hivyo, kama kawaida yangu, na mimi sikuacha maongezi yale yaelemee upande mmoja tu bali nilikuwa natia vionjo vya hapa na pale vilivyomfanya Amanda ajikute akicheka mara kwa mara.

Mara nikamwona Eddy akinifanyia ishara ya kuniita, nilimuaga Amanda na kuelekea sehemu alipokuwa amesimama Eddy, wakati huo alikuwa anawatazama dereva wa lile basi na utingo wake kwa umakini huku akionekana kuwaza mbali.

“Ni nini kinachoendelea kwenye hili basi, ujue hadi sasa hivi sielewi?” Eddy alinidaka kwa swali kabla hata sijamfikia.

Niligeuza shingo yangu kuangalia kule walikokuwa utingo, dereva na kondakta wa lile basi, nikawaona wakiwa wamesimama kama waliokata tamaa huku wakijadiliana jambo.

“Hata mimi sielewi, naona kizungumkuti tu!” nilimjibu Eddy huku nikiwa nimeanza kukata tamaa.

“Njaa itatuua. Kama vipi tukatafute chochote kijijini,” Eddy alinisihi huku akirekebisha tai yake.

“Ngoja nikawaulize kwanza ili tujue itachukua muda gani kuziba pancha maana inavyoonekana hawana hata gurudumu la akiba,” nilimwambia Eddy na kuondoka haraka kuelekea kule alikokuwepo dereva na wenzake.

Wakati naelekea kule nikamwona yule utingo wa basi akijaribu kujaza upepo kwenye mpira wa ndani (tube) wa lile gurudumu kwa pampu ya kukanyaga na mguu. Wakati huo huo kondakta wa basi alikuwa ameshika kipande kidogo cha mpira wa ndani na dawa ya kuzibia matundu kwenye mpira, aina ya Patex.

Niliposogea karibu zaidi nikashuhudia upepo ndani ya ule mpira wa ndani ukiwa unaingia na kutoka kupitia matundu tofauti makubwa na madogo na ule mpira haukuonekana kujaa upepo. Utingo akawa anauvingirisha na kuangalia kwa makini huku sikio lake likiwa makini kusikiliza sehemu zilizokuwa zinatoa upepo. Alizungusha mara kadhaa na kutingisha kichwa huku akiwaangalia dereva na kondakta wa lile basi.

“Hata sijui tutafanyaje, naona kuna matundu mengine ambayo ni vigumu kuyaona hadi tupate maji!” yule utingo alisema kwa masikitiko.

Wote watatu walitoka pale barabarani kila mtu na uelekeo wake wakitafuta tafuta ardhini. Baada ya muda dereva aliwaita wenzake ambao walimfuata haraka na kumkuta akiwa amesimama kando ya kidimbwi cha maji.

Yule utingo akajaza tena upepo kwenye ule mpira wa ndani na kuanza kuuzungusha kwenye kile kidimbwi cha maji, na hapo mtokoto wa matundu kadhaa makubwa kwa madogo yaliyokuwa yanatoa upepo ukajitokeza kwenye yale maji. Utingo akainua uso wake kuwatazama wenzake akiwa amekata tamaa.
“Dah, dawa tuliyonayo haiwezi kutosha kuziba matundu yote. Hapa hatuna ujanja itabidi tufungue gurudumu moja la nyuma tulifunge mbele ili safari iendelee,” yule utingo alionekana kushauri huku sura yake ikiwa imepambwa na huzuni.

“Duh, hatuwezi kufungua gurudumu lolote nyuma maana hayo pia hayaaminiki, tukifanya hivyo tunaweza kusababisha taharuki nyingine,” yule dereva wa lile basi alionekana kupingana na wazo la utingo wake.

“Nadhani tutafute utaratibu mwingine wa kufanya…” alisema yule dereva huku akishusha pumzi.

Hata hivyo, nilijikuta nikianza kujiuliza maswali, walipanga kutafuta utaratibu upi maana sikuona kama tungeweza kuondoka pale porini pasipo kupata gurudumu jingine! Sasa huo ulikuwa mtihani mwingine mkubwa kwangu!

* * *

Endelea kuufuatilia mkasa huu wa kusisimua...
 
safari buzwagi.JPG

38

Pumbazo la Moyo


Saa 9:50 alasiri…

NILIKUWA bado nimesimama hapo kwa kitambo pasipo kusogea hata inchi moja kana kwamba nilikuwa nimepigiliwa misumali miguuni, niliposhtuka nikaitazama saa yangu ya mkononi na kujikuta nikipoteza kabisa matumaini ya kufika Kahama kwa siku hiyo, kisha niliyahamisha macho yangu toka kwenye saa na kuwatazama utingo na dereva wake walivyokuwa na nyuso za kukata tamaa, na hapo nikajikuta nikikata tamaa.

Japokuwa njaa ilikuwa inalikoroga tumbo langu lakini akili yangu haikufikiria kutafuta namna gani tungepata chakula kama ambavyo kaka Eddy alikuwa ameshauri, bali akili yangu ilikuwa inamfikiria zaidi Amanda.

Mawazo ya jinsi ambavyo ningemsomesha hadi aelewe somo na kuwa nami pindi tukifika Kahama yalianza kuchukua nafasi kubwa akilini mwangu, na muda huo nilianza kujiwa na picha ya kupendeza ikinionesha nipo na Amanda kitandani tukiwa tumezama kwenye ulimwengu wa huba.

Niliyazungusha macho yangu taratibu kuwatazama abiria waliokuwa wamezagaa eneo lote na wengine wakilizunguka lile basi la Makenga, nikagundua kuwa wengi wa abiria hao walikuwa wamechoka sana na nyuso zao zilionesha kukata tamaa. Wengi walikuwa wameketi kiuchovu chini ya vivuli vya miti kandokando ya barabara.

Nilipotaka kuondoka mara nikahisi kulikuwa na mtu nyuma yangu akijongea kwa tahadhari mahali nilipokuwa nimesimama, na kabla sijageuka kuangalia nyuma yangu mtu huyo aliniwahi na kunifunga macho yangu kwa mikono yake laini.

Mawazo yangu yalishindwa kabisa kumbaini mtu huyo ingawa harufu nzuri ya marashi aliyokuwa amejinyunyizia na ulaini wa mikono yake vilitosha kabisa kunijulisha kuwa alikuwa msichana, tena si msichana wa kawaida bali alikuwa mrembo haswa!

Nilijikuta nasisimkwa mwili wangu na kupata wazo kuwa huwenda alikuwa Amanda lakini nilijikuta nalifuta wazo hilo haraka kwa kuwa harufu ya marashi aliyojipulizia Amanda ilikuwa tofauti kabisa na manukato ya mtu huyo aliyekuwa amesimama nyuma yangu akiniziba macho yangu kwa mikono yake. Nikatweta!

“Anaweza kuna nani tena?” nilijiuliza moyoni huku nikiipeleka mikono yangu nyuma na kuipapasa mikono yake lakini katika namna ya kujaribu kumbaini, sikuweza kupata jibu. Nikachanganyikiwa!

Niliposhusha mikono yangu na yule mtu akaitoa mikono yake toka usoni kwangu huku akiangua kicheko hafifu. Niligeuka haraka kutazama nyuma yangu huku mapigo ya moyo wangu yakienda kasi mara dufu, na nilichokiona sikuweza kuamini macho yangu! Kwa nukta kadhaa moyo wangu uliyasahahu mapigo yake. Na yalipoanza nilivuta pumzi ndefu kisha nikazishusha taratibu.

Macho yangu yalikuwa yametia nanga kwenye umbo zuri la msichana mzuri na mrembo. Alikuwa ni yule mrembo wa shani aliyekuwa amevalia suruali ya jump suit ya rangi ya maruni na alikaa kule kwenye viti vya nyuma. Nilimtazama kwa umakini nikijaribu kuhisi kuwa huwenda alikuwa amenifananisha.

Nilipomtazama kwa umakini zaidi sikuona kama alikuwa amekosea kwani muda huo alikuwa ananitazama kwa uchangamfu mkubwa mno lakini akiwa makini kuliko hata simba jike anayewinda.

Nilianza kuhisi msisimko wa ajabu ukinitambaa mwilini mwangu na nywele zangu zilisimama. Midomo yangu ilinikauka ghafla na mapigo ya moyo wangu yalizidi kukimbia. Nikashusha pumzi za ndani kwa ndani kama bata dume huku nikishindwa kuficha mduwao wangu… sikujua niseme nini kwani ndege niliyepanga kumnasa alikuwa amejileta mwenyewe tunduni, bila hata kutumia chambo.

Niliendelea kumtazama kwa umakini vile alivyokuwa amesimama mbele yangu nikahisi kama nipo ndotoni. Hata hivyo, milango yangu ya fahamu ilikuwa makini zaidi kuniletea habari huku nikijaribu kuishirikisha akili yangu kikamilifu.

“Yaani wewe, ndiyo nini kunichunia!” yule mrembo wa shani aliongea kwa huzuni huku akiniangalia usoni kwa utulivu kisha aliachia tabasamu laini kabla ya tabasamu lake halijageuka kuwa kicheko cha kirafiki. “Au ulidhani kunivalia hiyo miwani yako mikubwa myeusi basi nisingekutambua!”

Sauti yake laini ilipenya vyema masikioni mwangu na kuzidi kuzivuruga hisia zangu kwa kiwango ambacho kilinifanya nihisi kuanza kukosa uvumilivu. Kama tungekuwa wawili tu katika sehemu ya faragha huenda ningeshamkumbatia na kuanza kumporomoshea mabusu mfululizo.

Hakika sikuwahi kumwona mrembo wa shani kama yule akiwa amesimama mbele yangu huku akiniangalia namna ile. Niliyapeleka macho yangu kuutazama mkufu wa dhahabu aliokuwa ameuvaa shingoni kwake na kidani chake kilikuwa kimezama kwenye uchochoro katikati ya matiti yake, na hapo taswira ya matiti yake mazuri ikazidi kuzivuruga hisia zangu.

Nilijikuta nakikodolea macho ya uchu kifua chake kilichokuwa kimebeba matiti yenye ukubwa wa wastani yaliyokuwa na chuchu zilizochongoka mbele na zilizokuwa na hasira ya kutaka kutoboa blauzi yake aliyovaa.

“Mbona unanitazama hivyo au umefadhaika baada ya kuniona?” yule mrembo wa shani aliniuliza tena huku akiendelea kunitazama usoni kwa udadisi zaidi.

“Wala sijafadhaika… isipokuwa…” nilianza kuongea katika namna ya kujitetea ila alinikata kauli.

“Isipokuwa nini?” yule mrembo wa shani aliuliza kwa hamaki kidogo huku akiyatuliza macho yake moja kwa moja machoni kwangu, akanitazama kwa umakini.

“Isipokuwa najaribu kukumbuka nilikuona wapi! Sura yako ni ngeni kidogo machoni kwangu,” nilisema kwa sauti ya chini huku nikianza kukosa ujasiri.

Na hapo nilimwona yule mrembo wa shani akishangaa sana na kunitazama kama vile alikuwa ameona kiumbe kigeni cha kushangaza (alliens) toka sayari ya mbali, kisha alikunja sura yake kwa hasira.

“Kwa hiyo hunikumbuki, Jason?” yule mrembo wa shani aliniuliza kwa sauti iliyoonesha hasira za wazi.

Nilipatwa na mshangao zaidi na kwa sekunde chache nilibaki kama sanamu nikiwa sijui niseme nini. Sikuweza kabisa kumjibu swali lake bali nilikuwa kimya nikimtazama kwa umakini.

Nilianza kujiuliza alikuwa amelijuaje jina langu? Kuna mawazo yalinijia haraka haraka kichwani kwangu kwamba huenda alikuwa mmoja wa wasichana wengi niliowahi kubanjuka nao mara moja tu na kuachana nao (hit and run) kwa kuwa mara nyingi sikuwa na mwanamke maalumu kwa kuogopa mambo ya kuoneana wivu. Hata hivyo akili yangu iligoma kabisa kukubali maana msichana huyo alikuwa mzuri mno na nisingeweza kufanya hivyo!

Kisha nilijiuliza, kama yeye si mmoja wa wasichana niliotoka nao basi alikuwa nani kwenye maisha yangu? Je, nilikutana naye wapi? Na mbona sikuwa namkumbuka? Kila nilipomtazama kwa umakini nilihisi kuwa sura yake ilikuwa inakuja halafu inapotea, na hapo nikazidi kuchanganyikiwa! Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nilijikuta nakosa kabisa ujasiri wa kusimama mbele ya msichana.

Yule msichana alionekana kama aliyekumbuka jambo na kuingiza mkono wake ndani ya blauzi yake kwenye kifua na mkono ulitoka na mkufu aliokuwa ameuvaa shingoni, ulikuwa mkufu mzuri sana wa dhahabu halisi, alinionesha kidani cha ule mkufu kilichokuwa na herufi “J”.

“Unaukumbuka huu mkufu?” yule mrembo wa shani aliniuliza huku akinitazama kwa umakini usoni.

Niliutazama ule mkufu kwa umakini kisha nikakiangalia kile kidani chenye herufi “J” huku nikifikiria kidogo lakini sikuweza kukumbuka chochote kuhusiana na ule mkufu, nikatingisha kichwa changu kukataa. Yule mrembo akaonekana kushangaa zaidi.

“Hivi inawezekanaje ukanisashau kiasi hiki, Jason! Au labda sikuwa mtu muhimu kwako?” yule mrembo alilalamika kwa huzuni huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani. “Pengine inawezekana sikuwa kitu kwako ndiyo maana ukaamua kutupa jongoo na mti wake!”

“Nimetupaje jongoo na mti wake!” nilijiuliza moyoni huku nikijihisi huenda nilikuwa nimeanza kuchanganyikiwa!

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

39

Sikuwa na shaka kabisa kuwa yule mrembo wa shani alikuwa ananifahamu vyema na pengine tulikuwa watu wenye ukaribu mno ndiyo maana aliweza kulitaja jina langu pasipo shaka yoyote. Lakini kwa nini sikuweza kumkumbuka! Niliwaza sana moyoni mwangu lakini sikuweza kupata jibu. Nikabaki kumkodolea macho.

“Mbona hivyo!” yule mrembo wa shani alizidi kunisaili na mara akaonekana kusita kidogo. “Kwani una tatizo gani, Jason? Hukutarajia kukutana na mimi leo? Au unaogopa nitakuharibia mambo yako?” yule mrembo aliuliza tena maswali mfululizo huku akinisaili kwa macho yake kuanzia unyayoni hadi utosini.

“Sina tatizo lolote na wala sina mambo ambayo naogopa utaniharibia… ila najaribu kujiuliza umelijuaje jina langu?” nilimwambia yule mrembo wa shani kwa sauti tulivu, hata hivyo nilihisi kuwa sauti yangu ilikuwa inanisaliti kwa kukosa ujasiri.

“Siwezi kuwa nimekufananisha. Your name is Jason Sizya, right?” (Jina lako ni Jason Sizya, sawa?) yule mrembo aliniuliza tena baada ya kukubaliana na uchunguzi wake kwangu.

Yeah, I’m Jason Sizya, but…” (Ndiyo, mimi ni Jason Sizya, lakini…) nilijibu lakini nikajikuta nasita kidogo huku nikiyahamisha macho yangu na kuangalia kando ili kuyakwepa macho yake makali yaliyokuwa yananiangalia kwa umakini.

“…labda unaweza kunikumbusha sijui tulionana wapi mara ya mwisho?” nilimuuliza baada ya kitambo kifupi.

It can’t be like this!” (Haiwezi kuwa kama hivi!) yule mrembo wa shani alisema huku akitingisha kichwa chake kwa huzuni.

“Yaani hadi sasa bado umeamua kuendelea kuumiza moyo wangu!” aliongeza huku akiendelea kunitazama kwa macho makali yaliyowaka kwa hasira, kisha nikamwona kama aliyekuwa anajishauri jambo, na kabla sijajua nifanye nini nikamwona akigeuka na kuanza kuondoka toka eneo lile.

Sikutaka kumwacha aondoke hivi hivi pasipo kunifumbulia lile fumbo, haraka nikaudaka mkono wake wa kulia na kumvutia kifuani kwangu. Alisimama na kunitazama moja kwa moja machoni. Macho yake yaliendelea kuwaka kwa hasira. Tulibaki tumetazamana kama majogoo waliotaka kupigana.

“Samahani sana…” nilisema kwa sauti ya chini yenye kusihi.

“Samahani kwa lipi! Wala hujanikosea chochote,” yule mrembo wa shani alinikata kauli huku akishindwa kuficha hasira yake.

“Samahani kwa yote yaliyotokea kati yetu… ila unaweza kuacha…” nilisema.

“Kuacha nini?” alinidaka juu kwa juu kabla hata sijamalizia sentensi yangu huku akiendelea kunitazama kwa hasira, macho yake yalijaa ghadhabu na alikuwa ananitazama moja kwa moja machoni pasipo kupepesa macho yake.

“Jason, hatuwezi kuendelea na mwendo huu! Kwa nini umeamua kuchezea hisia zangu?” yule mrembo aliongeza hata kabla sijajieleza, safari hii aliongea kwa utulivu mkubwa na sauti yake ilikuwa ya upole kiasi.

“Naomba unisamehe na tusahau yote yaliyotokea kati yetu, please…” nilimwambia kwa sauti ya kusihi huku nikiachia tabasamu maalumu la kumlainisha na muda wote nilikuwa namwangalia machoni nikijaribu kuyasoma mawazo yake.

Hata hivyo, maswali lukuki yalizidi kunizonga kichwani kwangu, nilijiuliza, je, alikuwa nani? Tulikutana wapi na alilijuaje jina langu wakati mimi sikumkumbuka hata kidogo? Mara nikajiwa na mawazo mengine ya kuwa huenda alikuwa mmoja wa matapeli waliokuwa wanatumia mazingaombwe kujifanya wanakujua ili waweze kukuibia.

Lakini nilijipa moyo kuwa kama angekuwa tapeli basi kwangu angeambulia patupu kwani sikuwa mjinga wa kiasi hicho. Kila nilivyojaribu kuwaza ndivyo nilivyojikuta nazidi kuchanganyikiwa.

Anyway, tuyaache yote… naomba unikumbushe basi tulionana wapi maana nahisi akili yangu imeanza kuchoka au pengine naanza kuzeeka!” nilimsihi yule mrembo wa shani nikiwa bado nimeushika mkono wake na macho yangu nimeyatuliza usoni kwake.

Yule mrembo alinitazama kwa umakini kwa kitambo kirefu kisha akaachia kicheko hafifu. Hata hivyo niligundua kuwa hakikuwa kicheko cha furaha bali kilibeba uchungu. Nilimwona anatingisha kichwa chake taratibu kisha alibetua midomo yake na kunyanyua mabega yake juu na kuyashusha.

Are you serious?” (Unamaanisha?) aliniuliza huku akionekana kutoamini kile nilichokuwa nakiulizia.

Yes, I do,” (Ndiyo, namaanisha) nilimjibu na kupitisha ulimi kwenye midomo yangu iliyoanza kukauka kuilamba.

Okay! Nitakwambia lakini lazima niseme ukweli kuwa umenivunja moyo sana… laiti ingekuwa ni mtu mwingine wala nisingejali sana lakini si wewe, Jason! Hivi inawezekanaje ukanisahau haraka namna hii?” yule mrembo wa shani alilalamika kwa sauti yake laini lakini yenye utulivu na kubeba huzuni na hasira kwa wakati mmoja.

Sikusema neno bali nilibaki kimya nikimtazama usoni kwa umakini.

“Labda niseme hivi…” yule mrembo wa shani alianza kusema na kusita kidogo, akameza funda la mate kutowesha koo lake lililokauka. “najua umesoma Mzumbe,” alisema huku akiwa bado amenitulizia macho yake usoni.

“Ni kweli!” nilimjibu huku nikiwa makini kusikiliza kile alichotaka kuniambia.

“Unakumbuka wakati unaingia kidato cha sita kulikuwa na wiki ya michezo na mashindano mbalimbali yaliyozishirikisha shule zote za sekondari za Manispaa ya Morogoro na zile za pembezoni, mashindano hayo yalifanyikia shuleni kwenu Mzumbe…” yule mrembo alieleza.

Nilijaribu kuongeza umakini wa kumsikiliza huku nikiishirikisha akili yangu kikamilifu katika kuniletea picha ya kuaminika ya kile alichotaka kuniambia.

“Wanafunzi wa shule zote walihudhuria na katika michezo yote pia wanafunzi mbalimbali walionesha vipaji vyao… kati yao wapo walioshangiliwa sana na wapo waliofanya vibaya wakazomewa. Nakumbuka siku ya tatu ya mashindano kulikuwa na shindano la kumtafuta mrembo kwa shule zote, majaji walikuwa walimu wa michezo pamoja na baadhi ya wanafunzi…” yule mrembo alinyamaza tena na kuilamba midomo yake huku akiendelea kuyatuliza macho yake usoni kwangu kuona kama nilikuwa napata picha ya kile alichokuwa anakieleza.

Nilijaribu kuvuta kumbukumbu zangu za wakati huo wa shule ili kukumbuka kuhusu tukio lile la michezo lakini bado nilikuwa sipati picha sawasawa.

“Siku hiyo ukumbi ulijaa, warembo waliochanganyika vidato mbalimbali wakawa wanapita mmoja mmoja. Kulikuwa na msichana mmoja wa kidato cha tatu kutoka Sekondari ya Kilakala baada ya kupita tu jukwaani, ulikuwa umekaa siti za mbele kabisa ulinyanyuka kwa furaha na kupiga makofi baada ya kumwona na kusababisha ukumbi mzima kulipuka kwa shwangwe. Nakukumbuka vyema kwa sababu ulikuwa mwanafunzi maarufu sana, si Mzumbe tu bali hata kwenye shule nyingine kutokana na uwezo wako darasani na uwezo katika kucheza basketball, soka na hata maigizo…”

Maelezo ya yule mrembo yalianza kujenga picha fulani ya tukio lile kichwani kwangu, kwa mbali nilianza kukumbuka jambo ingawa bado sikuweza kuelewa alitaka kunikumbusha nini kupitia yale mashindano ya warembo. Kama aliyekuwa anayasoma mawazo yangu nilimwona akiachia tabasamu laini, vishimo vidogo mashavuni mwake vikajitokeza na kuzivuruga kidogo hisia zangu. Nikiwa katika kutafakari, sauti yake ikanizindua kutoka katika mawazo yangu.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

40

“Kisha warembo walijipanga mbele ya majaji na kuulizwa maswali kwa Kiingereza, mmoja baada ya mwingine… warembo wote walijibu kwa kadiri ya uelewa wao lakini ilipofika zamu ya yule msichana kutoka Kilakala ukumbi mzima, wakiongozwa na wewe ukanyanyuka na kushangilia sana. na muda wote wakati yule msichana anavalishwa taji baada ya kushinda na kukabidhiwa zawadi na mgeni rasmi, wewe ulikuwa unashangilia sana… sijui unakumbuka?” yule mrembo wa shani alinitupia swali huku tabasamu lake usoni likichanua.

“Endelea nakusikiliza kwa makini, au umemaliza?” nilimuuliza huku picha kamili ya tukio lile ikiwa bado haijanijia akilini kwangu, shida yangu kubwa ilikuwa kwamba nilikuwa mtu wa matukio mengi mno kiasi cha kushindwa kuyakumbuka yote.

“Sijamaliza bado, nilitaka tu kujua kama unakumbuka,” yule mrembo wa shani alisema, macho yake yaliendelea kunitazama moja kwa moja machoni.

“Nakumbuka kwa mbali, si unajua imeshapita miaka mingi na mambo mengi sana yametokea hapa katikati,” nilimjibu huku nikiwa nashusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Basi ilipofika muda wa kucheza muziki MC alimwomba yule mshindi wa urembo amchague mvulana wa kufungua naye muziki, wanafunzi wote walikaa kimya kusikilizia ni mvulana gani angepata bahati ya kuitwa mbele ya ukumbi huo… yule msichana hakuhangaika kutazama huku na kule bali macho yake yalielekea moja kwa moja kwako, alinyoosha kidole chake kukuchagua…” yule mrembo alisema.

“Alinichagua mimi?” nilidakia kuuliza swali lile kama punguani.

Yeah! Alikuchagua wewe. Na wakati mnacheza ulianza kumsifia huku ukiibinya mikono yake kwa mahaba, huyo mrembo alijihisi faraja ya aina yake moyoni kusifiwa na kijana handsome kama wewe uliyekuwa unagombewa na wasichana wengi. Muda wote mlikuwa mnatazamana kwa umakini, na kwa dakika tano tu mlizocheza pamoja ilitosha kuwajulisha kuwa kila mmoja alikuwa amevutiwa na mwenzake… kila mmoja alikiona kitu fulani kwenye macho ya mwenzake…” yule mrembo alisema na kuachia kicheko.

“Basi yule msichana ni…” alisema lakini nikamkata kauli kabla hata hajamaliza kuongea.

Oh my God! Ray the MP!” nilisema kwa mshangao mkubwa huku nikiwa siyaamini macho yangu.

Kwa sekunde kadhaa akili yangu ilishindwa kufanya kazi sawa sawa huku nikianza kujishangaa! Nilijishangaa kweli kweli maana iliwezekanaje nikamsahau mtu muhimu sana kama huyo! Dah! Sasa sura yake ilijaa machoni kwangu. Niliweza kumkumbuka vyema na nilikumbuka kila kitu tulichowahi kufanya pamoja. Alikuwa anaitwa Rehema Mpogolo.

Nilimtumbulia macho yaliyojaa mshangao mkubwa huku nikishindwa kujizuia, nikamvutia kifuani kwangu na kumkumbatia kwa nguvu.

“Dah, nisamehe sana Rehema… ama kweli milima haikutani!” nilisema nikiwa nimemkumbatia. Kisha nikaongeza, “Kwa nini hukunieleza moja kwa moja na badala yake ukaanza kuzunguka!”

Rehema hakujibu, alibaki kimya akinitazama usoni, hata hivyo sura yake haikuonesha tashwishwi yoyote.

“Nina haki ya kukusahau maana umezidi kuwa mrembo haswa, ni zaidi ya vile nilivyokufahamu…” nilijaribu kumchombeza lakini akanikatisha.

“Acha unafiki… kumbuka mimi bado yule yule Rehema uliyemwongopea na kisha ukamwacha kwenye mataa,” Rehema aliniambia kwa sauti iliyojaa huzuni huku akijaribu kujitoa toka kwenye mikono yangu lakini nikazidi kumkumbatia kwa nguvu zote.

Japo nilizidi kumkumbatia lakini nilishindwa kupingana na kauli yake. Nilikuwa mnafiki kwa kuwa sikupaswa kumsahau mtu kama Rehema.

Na nikiwa bado nimemkumbatia nilihisi joto la aina yake likitambaa mwilini mwangu, matiti yake laini yenye ukubwa wa wastani yaliyochongoka yalikuwa yananichoma kifuani kwangu na kuniletea joto la mahaba, na wakati huohuo kumbukumbu za mahaba yetu zilianza kunijia akilini.

Sasa niliweza kukumbuka vyema tukio lile la michezo pale shuleni na baada ya hapo… ilinichukua takriban miezi sita kumfukuzia Rehema bila mafanikio ingawa kila tulipokutana nilikuwa namweleza jinsi nilivyokuwa nateketea ndani kwa ndani kutokana na moto wa mapenzi yake.

Japo mara nyingi nilikuwa namwongopea lakini sikuweza kukana kuwa umbo matata la Rehema na sauti yake nyororo viliuteka vibaya moyo wangu pasipo kujua na kunifanya nijihisi kuwa nilikuwa mateka wa nafsi mbele yake.

Kuna wakati nilianza kujishangaa. Na wala haikuaminika kabisa! Kwa Jason, kijana mtanashati ambaye warembo wa kila aina walipigana vikumbo na wengine waligombana kwa ajili yangu, kijana ambaye sikuwa na msichana maalumu iliwezekanaje Rehema akawa ananisumbua kiasi kile! Hapana, haiaminiki!

Kuna wakati nilikuwa nikijiuliza, alikuwa na nini huyu Rehema hadi kunifanya kuteketea ndani kwa ndani kwa moto wa mapenzi yake? Lakini kila nilipojiuliza jibu lilikuwa rahisi sana. Rehema alikuwa ana kila kitu ambacho wasichana wengine wengi walikikosa. Kila kitu!

Kuna siku tulikutana, siku hiyo alikuwa amevaa blauzi nyepesi iliyonifanya kukiona vizuri kidani chenye herufi “R” kilichokuwa kikining’inia kwenye mkufu wa silver aliouvaa shingoni. Na hapo nikapata wazo la kumfanyia ‘surprise’ lakini sikumwambia chochote kwa wakati huo bali nilizidi kumbana nikitaka aniambie kwa nini alikuwa ananikwepa na hakuwa tayari kushirki ngono na mimi.

“Naomba nikuulize Jason… ni kweli unanipenda?” Rehema aliniuliza huku akicheka kwa chini chini.

“Ndiyo nakupenda… nimetokea kukupenda sana,” nilimjibu nikiwa sielewi alikuwa amekusudia nini kwa kuniuliza swali kama lile, maana siku zote nilikuwa nahangaika sana kumfukuzia.

“Haiwezekani bwana,” Rehema alisema huku akibetua mabega yake.

“Haiwezekani? Kwa nini isiwezekane? Au sina hadhi ya kuwa pamoja nawe?” nilimuuliza huku nikimkazia macho.

“Hadhi unayo, tena una hadhi kubwa sana ila sidhani kama unanipenda bali utakuwa umenitamani tu. Yaani unataka kulala nami tu ili kuongeza idadi ya wasichana uliolala nao,” Rehema aliniambia kwa sauti tulivu.

“Hapana. Kitu gani kimekufanya kusema hivyo?” nilimuuliza huku nikiendelea kuyatuliza macho yangu kwenye uso wake.

“Mbona unajulikana! Kila unavyoona wasichana wazuri basi unapagawa na kutaka kulala nao,” Rehema aliniambia huku akiachia tabasamu.

“Watu wananizushia tu wala hakuna ukweli wowote. Sijakutamani,” nilijitetea.

“Mimi najua kuwa umenitamani tu,” Rehema alisisitiza.

“Sidhani kama umeshaingia kwenye moyo wangu ukakiona hicho unachokisema. Amini usiamini, nimetokea kukupenda kuliko unavyoweza kudhani,” nilimwambia huku nikishusha pumzi. Rehema aliniangalia kwa umakini na kutingisha kichwa chake taratibu.

“Unajua Rehema, kusema kweli unautesa sana moyo wangu kila siku hasa pale unapokataa hata kusikiliza kilio changu,” sasa niliamua kutupa karata muhimu ili kumnasa.

“Nasikia hayo maneno huwa unamwambia kila msichana mrembo unayekutana naye. Na hicho kilio umeshawalilia wangapi?” Rehema aliniuliza huku akinipandisha na kunishusha.

“Najua na wewe umeshalishwa maneno mengi ya kutungwa juu yangu, najua sifa yangu imekuwa mbaya kutokana na tabia za vijana wanaohofia utanashati wangu kuwa nitawachukua wasichana wao ndiyo maana wameamua kunipakazia. Pia mazoea na wasichana imekuwa nongwa kwa kuwa nina damu ya kupatana na watoto wa kike,” nilimwambia Rehema katika namna ya kujitetea.

“Kwa hiyo sasa unatakaje hasa?” Rehema aliniuliza huku akinikazia macho.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

41

“Nadhani unajua hasa ni nini ninakitaka kwako!” nilimjibu huku nikimtulizia macho yangu usoni kwake.

“Najua, si unataka kile kitu ambacho umekuwa ukikitaka kwa kila msichana mrembo unayekutana naye?” Rehema alisema na kunikata maini.

"Aah, ni nani mwingine niliyemtaka?” niliuliza kwa kujikausha lakini dhamiri yangu ilinisuta.

“Wengi tu, wala sihitaji kuanza kutaja majina yao hapa,” Rehema alisema kwa sauti tulivu.

“Si kweli, watu wanataka kunipakazia tu,” nilizidi kujitetea lakini Rehema akacheka.

“Tena kwa kukuonesha kuwa nakupenda sana nitakununulia mkufu mzuri wa dhahabu halisi wenye kidani chenye herufi ya jina langu, nikuvalishe shingoni kwako ili kila ukiutazama ukumbuke jinsi gani nilivyo wa muhimu kwako. Na uache kuvaa mikufu yako ya chuma chakavu,” nilimwambia huku nikiukodolea macho mkufu wake.

Rehema alishtuka na kunipiga kofi dogo kwenye bega langu na sote tukacheka kisha aliniangalia kwa umakini kwa kitambo fulani.

“Nitashukuru kama ni kweli,” Rehema alisema kwa sauti tulivu na kisha aliongeza, “lakini kama kweli unanipenda basi endelea kuwa na subira tu ipo siku utakuja kula vinono vyangu hadi ukinai.”

Maneno hayo aliyaongea huku akionekana wazi kusimamia alichopanga. Alionekana kuwa hakuwa tayari kuyumbishwa japo alisisitiza kuwa alikuwa ananipenda sana.

Kwa kuwa nilikuwa mkware kwa vidosho niliyejaliwa maneno matamu na nilijua kuyasuka maneno yangu, hivyo muda mwingi nilijaribu kumchombeza kwa maneno matamu ya kumlaghai ili aingie kwenye kumi na nane zangu na kukubali kubadili uamuzi wake.

Hata hivyo, hali iliendelea kuwa ileile kwa miezi takriban sita ya kumfukuzia hadi akaingia kidato cha nne, Rehema alijitahidi sana kunikwepa na hakukuwa na hata siku moja tuliyowahi kukutana kwenye uwanja wa huba. Rehema alikuwa mjanja sana na hakutaka kunipa nafasi ya kubaki tukiwa wawili tu faragha.

Baada ya usumbufu mkubwa hatimaye nilikuja kugundua kuwa alikuwa bado hajamjua mwanamume na aliogopa sana kuingia kwenye ulimwengu wa huba kwa kukurupuka. Kwa hakika kumshawishi Rehema ilikuwa kazi ngumu. Tena ngumu kweli kweli! Pengine ingekuwa rahisi zaidi kwa bubu kuongea au kiwete kutembea kuliko kumshawishi Rehema akubaliane nami. Huo ulikuwa msimamo thabiti usio na mfano!

Nikakumbuka Jumapili moja baada ya kutoka kanisani nilimwomba Rehema twende katika mgahawa wa kisasa maarufu kwa jina la Wazawa Pub uliopo eneo la Misufini mjini Morogoro, tulikubaliana kwenda kupata chakula na kuongea mambo yanayotuhusu. Alikubali.

Nilipanga kuwa siku hiyo iwe ya kuukata mzizi wa fitina na nilikusudia jambo moja tu, akubaliane nami au biashara iishie hapo na tusijuane tena. Kama mbwai, mbwai. Niliwahi kufika hapo Wazawa Pub na Rehema alinikuta nikimsubiri, tulisalimiana kisha aliketi kwenye kiti kwa utulivu huku akinitazama kwa umakini. Siku hiyo nilikuwa nimetulia isivyo kawaida.

“Umeniagizia chakula?” Rehema aliniuliza baada ya kuketi.

“Ningejuaje unapenda chakula gani?” nilimjibu kwa sauti iliyoonesha hasira ya dhahiri iliyokuwa moyoni mwangu. Sikupenda kuendelea kuonekana bwege.

Rehema alitulia kwa muda, akanitazama kwa umakini sana na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. Kisha alinyoosha mikono yake na kuivuta ya kwangu niliyokuwa nimeiegemeza juu ya meza.

“Naomba niangalie machoni,” Rehema aliniambia kwa sauti tulivu. Nikamwangalia.

“Nakupenda sana Jason, na ninajua malengo yetu yalivyo. Amini usiamini, kama utalazimisha unachotaka kitokee nakuhakikishia tutauvunja uhusiano wetu wenyewe…” Rehema alisema kwa utulivu huku akinitulizia macho yake usoni kwangu.

“Ni bora uhusiano uvunjike maana sioni faida yake, siwezi kuendelea kufanywa fala, kula wale wengine halafu shombo nipakazwe mimi!” nilisema kwa hasira na kuitoa mikono yangu kwenye mikono ya Rehema.

“Kwa nini unasema hivyo? Siwezi kulala na mwanamume mwingine zaidi yako, wewe amini kuwa muda ukifika utafaidi,” Rehema alisema kwa sauti ya upole.

“Nitaamini vipi kuwa huna mwanamume mwingine? Ona… kama kweli unanipenda basi nipe hata siku moja tu kisha nitakubali kusubiri kwa muda wowote utakaotaka!” nilimwambia Rehema huku donge la hasira likiwa limenikaba kooni.

Rehema aliinamisha kichwa chake chini kwa kitambo kirefu akionekana kuwa njia panda ya kuamua endapo akubaliane na matakwa yangu au ndiyo uwe mwisho wa uhusiano wetu. Kisha aliinua uso wake kunitazama.

“Naomba nikwambie ukweli Jason, sijawahi kukutana na mwanamume yeyote tangu kuzaliwa kwangu… ni kweli nimetokea kukupenda sana lakini pamoja na ushawishi wako bado sikuamini kabisa hasa kwa tabia yako ya kubadilisha wanawake kama nguo,” Rehema aliniambia huku akinitazama usoni.

Mwili ulinisisimka baada ya kusikia kuwa hakuwa amekutana na mwanamume yeyote kimwili, kwa maana hiyo ningekuwa mwanamume wake wa kwanza.

“Kwa hiyo unanitaka nifanye nini ili uniamini?” nilimuuliza kwa sauti tulivu ingawa mapigo ya moyo wangu yalikuwa yanaenda kasi. Rehema alifikiria kidogo kisha alishusha pumzi.

“Nipo tayari kukupa unachotaka…” Rehema aliniambia huku akionekana kufikiria jambo.

“Kweli?” niliuliza kwa pupa kama punguani.

“Ndiyo. Lakini kwa masharti…” Rehema alisema huku akionekana kuwaza mbali.

“Kama?” nilimuuliza huku donge la hasira likianza kuyeyuka taratibu kooni kwangu.

“Nataka ukapime HIV,” Rehema aliongea huku akinitazama machoni kujaribu kuyasoma mawazo yangu.

“Ha! Nipime HIV ili iweje?” nilimuuliza huku nikiwa nimeshtushwa sana na kauli yake.

“Nikiyaona majibu ndiyo nikuamini,” Rehema alisema huku akionekana kusimamia msimamo wake.

“Inamaana nikikuletea cheti cha majibu ndiyo utaniamini na kukubali?” niliuliza kwa shauku.

“Ndiyo maana yake!” Rehema alijibu kwa msisitizo.

Kauli yake ilinifanya nifikirie kuachana na wazo la kutoka naye kimapenzi lakini baada ya kukumbuka kwamba lengo langu lilikuwa ni ngono tu nikajikuta napata wazo. Nilimkubalia na tulipoagana kila mmoja akishika hamsini zake nikaanza kutafuta namna ya kufanya. Nilimfuata rafiki yangu Selemani Abeid ambaye tulikuwa tunasoma darasa moja pale Mzumbe, nikamweleza kuhusu sharti nililopewa na Rehema, akaahidi kunisaidia.

Baba yake Selemani alikuwa daktari mkuu wa Mkoa wa Morogoro jambo lililomfanya Selemani afahamiane na madaktari wengi, si wa hospitali ya mkoa tu bali hata wa hospitali binafsi, hivyo aliniunganisha kwa daktari mmoja kijana asiye muadilifu, ambaye baada ya kumpatia kitu kidogo aliniandikia cheti kuonesha kuwa hali yangu kiafya ilikuwa njema.

Siku mbili baadaye nikiwa na karatasi ya majibu, ilikuwa majira ya alasiri nilipotoroka toka Mzumbe nikachukua pikipiki na kwenda hadi shule ya Kilakala kuonana na Rehema. Nilipompata nilimpatia ile bahasha iliyokuwa na cheti cha majibu. Rehema alishangaa sana kuona kuwa niliweza kutoroka shuleni na kwenda pale kumpa bahasha ambayo hakujua ilikuwa ya nini ndani!

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

42

“Ya nini?” aliniuliza kwa mshangao huku akiitumbulia macho.

“Umesahau tuliongea nini?” nilimuuliza huku nikimtulizia macho. Rehema alifikiria kidogo kabla hajakumbuka na kuachia tabasamu.

“Ha! Inamaana ulienda kweli kupima?” Rehema aliuliza huku akizidi kushangaa.

“Nataka kukuonesha kuwa huwa nasimamia maneno yangu,” nilimwambia kwa kujiamini huku nikitabasamu. Rehema alinitazama kwa umakini kwa kitambo fulani akiwa haamini.

Okay, majibu yanasemaje?” hatimaye aliniuliza akiwa bado amenitulizia macho yake usoni kwangu.

“Nenda kayasome mwenyewe na Jumamosi utanipa jibu zuri,” nilimwambia na kuondoka haraka, nikachukua pikipiki iliyonirudisha Mzumbe huku nikimwacha bado anashangaa.

Mwisho wa wiki, ilikuwa Jumamosi baada ya kazi za usafi pale shuleni niliondoka moja kwa moja hadi Kilakala nikamtafuta Rehema huku uso wangu ukiwa na tabasamu pana. Lakini alikuwa na uso wenye mashaka.

Siku ile Rehema alivaa blauzi nyepesi ya rangi ya bluu iliyoyaficha vyema matiti yake madogo na alivaa mkufu wake ulionasa vyema kwenye shingo yake ndefu na kupotelea katikati ya matiti yake. Chini alivaa suruali nyeupe ya dengrizi.

“Kuna tatizo?” nilimuuliza kwa wasiwasi.

“Kwa nini umenidanganya kwa kughushi cheti ili uonekane mzima? Kwa nini unataka kuniua?” Rehema alilalamika huku macho yake yakilengwa lengwa na machozi.

Nilishtuka sana, nikajiuliza ni nani aliyemweleza kuwa nilikuwa nimeghushi majibu! Mawazo ya haraka haraka yalipita kichwani kwangu na katika kuwaza nilihisi kuwa huenda zilikuwa hisia zake tu na wala hakuna yeyote aliyemwambia. Hata hivyo, sikutaka kuonesha mshtuko wangu.

“Kwa nini nikuuwe mpenzi wangu? Nafikiri baada ya Mungu ni mimi ninayeyajali maisha yako, na kama huniamini basi tuongozane mguu kwa mguu popote unapopataka nikapime ili uniamini,” nilimwambia Rehema huku nikionekana kujiamini zaidi ingawa ukweli nilikuwa tofauti moyoni.

“Upo tayari twende hata sasa hivi?” Rehema aliniuliza akiwa amenikazia macho. Kauli yake ilikuwa kama kisu chenye moto kwenye siagi katika moyo wangu. Nikakosa jibu la kumpa.

“Jason, ninalazimika kufanya hivi kwa kuwa tunahitaji kuwa waangalifu, tuna mipango mingi sana mbele yetu kuhusu maisha yetu. Kama kweli unanipenda tutoke sasa hivi twende tukapime, wote wawili, ili tuwe na uhakika na afya zetu kisha tuendelee na mambo mengine,” Rehema alisisitiza. Nilimtazama machoni nikaona kuwa alikuwa hatanii.

“Nipo tayari. Twende!” nilisema huku nikijiuliza moyoni vipi endapo angetaka tuongozane muda huo. Lakini nikajipa moyo huku nikijikuta namkubalia kwa sharti kuwa endapo majibu yangu yangekuwa safi angenipa penzi siku hiyo hiyo.

Moyoni nilikuwa na mawazo mengi sana. Nilijaribu kuyafikiria maisha yangu, sikuwa mtu wa kutosheka na msichana mmoja na wala sikupenda kutumia kinga wakati wa kujamiiana. Pia niliwaza nini kingetokea endapo majibu yangu yasingekuwa safi? Ni kweli Rehema alionesha kunipenda lakini hakuwa tayari kuingia kwenye mtego kirahisi kama nilivyodhani. Muda wote nilikuwa na wasiwasi mwingi sana moyoni mwangu.

Hata hivyo sikutaka kuonesha wasiwasi, tulitoka kwa miguu hadi kwenye kituo cha teksi na nilikuwa natembea bila wasiwasi kabisa. Sikutaka kuonekana kama nilikuwa nafikiria jambo lolote baya kichwani. Nilijitahidi kuwa katika hali ya kawaida kabisa.

Tulipopata usafiri tukamtaka dereva atupeleke hadi katika Kituo cha Afya cha Uluguru kilichopo Mtaa wa Karume katikati ya mji wa Morogoro. Tulipofika Uluguru tulipokewa na dada mmoja mrembo, mhudumu wa mapokezi katika hospitali hiyo.

“Ahsante, tunahitaji huduma ya ushauri na kupima,” Rehema alimweleza yule dada baada ya kutukaribisha.

Yule dada alituelekeza chumba tulichopaswa kuingia, tukaongozana kuelekea chumba hicho cha mshauri, na kwa namna tulivyoelekezwa, haikuwa vigumu kufika.

Tulipoingia tukapokelewa na mshauri mmoja aliyekuwa amekaa kwenye kiti cha kiofisi, akatukaribisha na tabasamu mwanana. Alijitambulisha kwetu kuwa aliitwa Daktari Chambo, nasi tulijitambulisha na baada ya hapo alituuliza kilichotupeleka hapo, tukamweleza kusudio letu la kwenda pale. Kisha zilifuata nasaha huku akitutoa hofu.

Hata hivyo, hofu kuu ilikuwa bado imenivaa moyoni ingawa kila nikimtazama Rehema sikumwona kuwa na hofu yoyote. Muda wote aliniangalia kwa tabasamu. Ingawa ni kweli nilikuwa tayari kwa vipimo lakini kwa ndani sikujiamini kabisa.

“Wacha nipime tu, ni vizuri kujijua afya yangu hata kama si kwa ajili ya Rehema. Nafikiri ni sahihi kupima,” niliwaza huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Daktari Chambo alichukua vifaa, haikuwa kazi kubwa, maana alitumia kifaa kidogo na kwa urahisi. Alitutoboa wote wawili vidole, kisha akachukua damu na kuweka kwenye kipimo ambacho majibu yake hutoka haraka na wanaopimwa wakiwa hapo hapo.

Zoezi lilipokamilika, Daktari Chambo alituangalia kwa kitambo kirefu huku akionekana kujishauri. Kwa mara ya kwanza nikamwona Rehema akinitazama kwa wasiwasi sana. Sikujua kama wasiwasi huo ulikuwa ni juu yangu au hata yeye alikuwa na wasiwasi na afya yake? Muda huo nilikuwa natokwa na jasho jingi.

“Majibu yenu yapo tayari, naweza kuwapa sasa?” Daktari Chambo alituuliza huku akitutazama kwa zamu.

“Tupo tayari kabisa, tupo tayari,” Rehema alisema huku akinitupia jicho kwa wasiwasi.

“Kama tulivyokubaliana, naomba iwe vilevile. Majibu yote ni majibu, kwa hiyo naomba muyapokee kama yalivyo, sawa jamani?” Daktari Chambo alituambia huku akitutazama kwa zamu.

“Hakuna shida, dokta…” nilisema kwa sauti ya kitetemeshi kutokana na kutojiamini.

“Majibu yaliyopatikana kwenye damu zenu wote wawili yanaonesha kuwa…” Daktari Chambo alisema akasita kidogo na kuyatupia jicho tena yale majibu. “Hamna maambukizi… mko negative. Hongereni sana kwa hilo.”

Tulipatwa na furaha isiyo kifani, Rehema alinikumbatia kwa furaha na siku ile ile baada ya kutoka pale kituo cha afya nilimpeleka kwenye getto la rafiki yangu, Jotham Msimbe, aliyekuwa anaishi eneo la Misufini. Tulipoingia ndani Rehema alisimama mlangoni na hakuonekana kuwa na wazo la kutaka kukaa.

“Ingia basi mbona umeganda tu hapo mlangoni?” nilimuuliza Rehema aliyeonekana hakuwa na dalili ya kutaka kukaa.

“Sitaki kukaa sana hapa, nina assignment shuleni,” Rehema aliniambia na kuinua mkono wake wa kushoto kuitazama saa yake ndogo ya kike aliyokuwa amevaa mkononi. Muda ule ilikuwa imetimia saa 9:15 alasiri.

Nilimtazama kwa macho yaliyojaa ubembe wa huba. Niliona kama alitaka kunichezea akili yangu. Muda huo nilikuwa nahisi moyo wangu ukienda mbio kama saa mbovu na nilikuwa namtazama Rehema kwa uchu kama vile fisi ameona mzoga.

Kiukweli Rehema alikuwa mbichi kabisa. Alikuwa msichana mrembo kuliko hata neno lenyewe. Kwa namna alivyokuwa ananiangalia alionekana dhahiri hakuwa na mpango wa kubadili uamuzi wake. Ni kama alipanga kuondoka muda ule ule.

Nikakumbuka jambo na sikutaka kuipoteza nafasi ile, nikamsogelea na kumshika mikono yake. “Funga macho yako.”

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

43

What!” Rehema aliniuliza kwa sauti yenye kitetemeshi.

“Funga macho, please trust me,” nilimsihi huku nikimtazama machoni.

“Jason, unataka kunifanya nini!” Rehema aliniuliza huku akionesha kuwa na wasiwasi.

Come on! Funga macho yako,” nilisisitiza.

Rehema aliniangalia moja kwa moja machoni kama aliyekuwa anajaribu kuyasoma mawazo yangu kisha akayafumba macho yake. Niliingiza mkono wangu kwenye mfuko wa suruali yangu na kutoa kimkebe kidogo kilichokuwa na mkufu mzuri wa dhahabu wenye kidani chenye herufi “J” nilionunua, nikazunguka nyuma yake na kuufungua mkufu aliouvaa na kisha nikaufunga vizuri mkufu niliokuja nao shingoni kwake.

Rehema alifumbua macho yake na kustaajabu sana alipouona mkufu wa dhahabu uliokuwa unang’aa na kutiririka kifuani kwake.

Oh my Gosh!” Rehema alisema kwa mshangao mkubwa na bila kutarajia akanirukia na kunikumbatia kwa furaha.

“Umeupenda eh?” nilimuuliza huku nikimtazama machoni kwa tabasamu.

Of course, nimeupenda sana. Halafu hii ni dhahabu halisi” Rehema alisema huku akikitazama kwa umakini kile kidani chenye herufi “J” na kukibusu.

“Nimefanya kama nilivyokuahidi,” nilisema kisha nikaanza kumbusu. Kama aliyezinduka, Rehema aliniachia na kugeuza kichwa chake akijaribu kuiepuka midomo yangu.

Oh, come on, Jason!” Rehema alilalama kwa sauti yenye kitetemeshi huku akiachia kicheko hafifu.

Sikutaka kumsikiliza hivyo nilizidi kumvutia kifuani kwangu. Rehema alijigandamiza kwenye mwili wangu na kutulia huku akihema kwa nguvu. Kisha nilimsukumia juu ya kitanda, akaanguka kama mzigo na kutulia huku akinitazama kwa wasiwasi.

Muda huo huo nililiendea dirisha na kulishusha pazia kisha nikageuka kumtazama bila ya kusema neno lolote. Nilimwona ametulia nikaanza kufungua vifungo vya shati langu na kulivua kisha nikalitupia kando na kujitupa kitandani, nikamshika na kugandisha midomo yangu kwenye midomo yake huku nikihisi kijasho chembamba kikinitoka mwilini.

Nilimwona Rehema akiyafumba macho yake na kukunja uso wake kama aliyekuwa anahisi kizunguzungu na hapo akaanza kutokwa na jasho kupita kiasi. Mikono yangu ikaanza kuvinjari mwilini mwake na hapo nikashuhudia pumzi zikimpaa!

Sikutaka kupoteza muda, nilikamata shingo yake vizuri nikakiinua kidogo kichwa chake kisha nikawa nakunywa sharubati ya mlenda taratibu huku namtazama machoni, alikuwa ameyafumba macho yake na kutulia tuli pasipo kuleta purukushani za aina yoyote, ni kama vile alikuwa amepoteza fahamu.

Kuona hivyo sikulaza damu nilimvua nguo zake kisha nikaipa mikono yangu wasaa wa kuzidi kutalii sehemu mbalimbali za mwili wake ulioumbika vizuri kwa uzuri kabisa bila chenga, nilianzia maeneo ya kifuani, nilikuwa nazinyonya chuchu zake ngumu zilizosimama na kuchongoka kwa kuzungusha ncha ya ulimi wangu kwa ustadi wa hali ya juu, alianza kuweweseka kwa weweseko la kimahaba.

Wakati huo mikono yangu ilikuwa kazini kutomasa hapa na pale katika sehemu mbalimbali za mwili wake na mara nikamsikia akianza kutokwa na milio ya ajabu ajabu, nilipomtazama machoni nilimwona akirembua muda wote. Nilitumia dakika nyingi kujivinjari katika mwili wake kwa ustadi wa hali ya juu mpaka pale uvumilivu ulipomshinda, akaanza kulalamika kwa sauti ya kimahaba iliyogubikwa na shauku ya kufanya tendo lenyewe.

Kuona hivyo nilizidisha ufundi na hapo Rehema alizidi kulalamika kwa sauti iliyoashiria kuwa yupo tayari kwa kwa mtanange. Sikutaka kukurupuka kuingia kwa pupa mchezoni kwa wakati ule, nilipanga kuwa mpole ili nikiamua kula tofaa basi nilile kwa kulifaidi utamu wote mpaka ndani. Macho yangu yalikuwa yakimtazama usoni, alionekana kulegea kila kiungo na alizidi kutoa miguno iliyonipandisha mizuka, nikatamani nivue nguo na kuzama golini lakini nilijikaza.

Sikuwa na haraka, nilitaka nimtese kwanza kutokana na kunisumbua kwa miezi sita, nilipanga kutumia ufundi na ustadi wa wangu wote ili hata nikizama golini nimfunge mabao ambayo yangemfanya asinisahau katika maisha yake yote.

“Ooooooohhhhh! Jamani Jason, ni nini lakini hivyooo!” Rehema alilalamika huku akinikandamiza kkwenye mwili wake.

Kisha nilianza kuisikia mihemo na miguno ya ajabu ambayo kiukweli ilizidi kuniweka katika wakati mgumu, mtalimbo wangu ulikuwa umesimama na mishipa ya damu ilitutumuka kiasi cha kunifanya nianze kuyahisi maumivu lakini baharia ndiyo kwanza nilikuwa makini kuzama chumvini kwa ufundi, alikuwa hoi bin taabani kwa wakati huo.

Alishindwa kuvumilia, aliamka na kunisukuma, nikaangukia chali kisha akaja juu yangu na kuanza kuzitoa nguo zangu haraka haraka kama mtu aliyepandwa na wazimu, hakujali ule usumbufu aliokuwa anaupata wa kuvua nguo zangu. ila alipokutana na mtalimbo uliofura kwa hasira, akasita na kutoa macho ya mshangao.

Nilijua kilichomfanya kusita kwa sababu alikuwa mgeni wa mambo hayo, nikamlaza chali taratibu. Sikutaka kuzama haraka dimbani bali niliutumia mtalimbo wangu kuusugua kwenye kitumbua chake upande wa juu kushuka chini kisha nikawa kama vile napapigapiga huku nizidi kupasugua.

Rehema alilalamika sana huku akitoa miguno na kujaribu kupambana na mimi kutaka kuuingiza mtalimbo katika lango lake. Nilikataa kufanya hivyo kwa makusudi ili niendelee kumtesa. Rehema alinyamaza na kunitazama usoni.

Nami nilimtazama na sikutaka kuyakwepesha macho yangu, tulitazama kwa sekunde chache tu nikamwona akiyakwepesha macho yake kwa aibu, kisha aliyaficha macho yake kwa kutumia viganja vyake huku machozi ya furaha yakimtoka.

Nikaona kuwa mateso yalikuwa yanamtosha na hapo nikaamua kuingia kwenye lango kuu la ikulu, nilipoanza kuuzamisha tu mtalimbo wangu nikamwona akikunja sura yake na kutoa ukelele mdogo wa maumivu huku akiuma meno yake. Baada ya hapo kilichoendelea kilitufanya kuihama kabisa sayari hii na tukahamia katika sayari nyingine ya mbali, sayari ya huba.

Muda mfupi baadaye tulisitisha safari yetu ya huba, si kwamba kila mmoja wetu alikuwa amemkifu mwenziwe. La hasha! Isipokuwa usichana wa Rehema ulikuwa umepotea na mwili wake wote ulikuwa unatetemeka.

Katika ukware wangu wote Rehema ndiye alikuwa msichana wangu wa kwanza niliyekutana naye, ambaye kizinda chake kilikuwa bado hakijavunjwa, yaani bikra. Na hivyo kwa mara ya kwanza kabisa nilikuwa nimefanikiwa kumwonesha msichana wa kwanza ulimwengu mpya. Hata hivyo Rehema alionekana kuufahamu ulimwengu huo kwa kuusoma kwenye vitabu na pengine kuangalia filamu lakini kiuhalisia hakuwahi kusafiri katika ulimwengu huo.

Pamoja na hayo bado Rehema alikuwa binti mwenye busu za kusisimua sana na aliniachia maswali kibao kichwani kwangu nikijiuliza aliyajulia wapi mambo yale!

Ingawa alikuwa mgeni katika ulimwengu wa huba lakini alikuwa wa aina ya pekee kabisa, licha ya uzuri wake pia alikuwa na utundu wa kuzaliwa nao na mwenye majibu yote ya maswali yahusuyo mapenzi. Na kama kungefanyika mashindano ya utundu na ufundi kwenye ulimwengu wa huba, nina imani pia wasichana wengine, licha ya uzoefu wao kwenye ulimwengu wa huba lakini wasingefua dafu kwa Rehema…

_______

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

44

“Jason!” sauti nyororo ya Rehema ilipenya vyema masikioni kwangu na kunizindua kutoka kwenye lindi mawazo. Nilimtazama, nikamwona akiwa ananiangalia usoni kwa utulivu.

“Unawaza nini?” Rehema alinitupia swali huku akinikazia macho.

“Ah, kuna mambo tu nilikuwa nayafikiria!” nilimwambia huku nikiutazama tena ule mkufu wa dhahabu shingoni kwake kisha nikaachia tabasamu la aibu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Rehema aliyapeleka macho yake kuuangalia ule mkufu aliokuwa ameuvaa shingoni kwake na kuugusa.

“Tangu siku uliponivalisha mkufu huu sijawahi kuuacha, kila nilipokuwa nauangalia nilikuwa nahisi kama upo nami, hii maana yake ni kwamba bado hujanitoka moyoni,” Rehema aliniambia kwa sauti nyororo huku akiachia tabasamu kabambe.

Nilitabasamu tu pasipo kusema neno na akilini kwangu niliona jambo lile kama riwaya fulani ya mapenzi au mchezo wa kuigiza. Sikuamini kama mtu angeweza kukaa na mkufu kwa miaka yote hiyo eti kwa sababu aliyempa mkufu huo bado yupo moyoni mwake! Ilikuwa vigumu kuamini…

“Samahani Jason, unaoneakana umo ndani ya mawazo mengi mno, natamani ningejua unawaza nini ili nami kama nitaweza, nikusaidie kuwaza,” sauti ya Rehema ilinizindua, nikamtazama na kushusha pumzi.

“Wala sina mawazo yoyote…” nilimwambia. “Ila nahisi kama nimo ndotoni na pindi nikiamka nitajikuta nikiwa peke yangu bila wewe.”

Rehema alinitazama kwa umakini kwa kitambo fulani na kuachia tena tabasamu.

“Lakini nahitaji kujua ukweli, na tafadhali naomba usiniongopee. Niambie tu hata kama utaniumiza,” Rehema aliniambia huku akiendelea kunitazama usoni kwa umakini.

“Unataka kujua nini?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakiwa yanakwenda mbio, lakini nilijitahidi kuwa makini katika maneno yangu. Muda huohuo nikamwona Eddy akipita karibu yetu huku akitutupia jicho la wizi na kuelekea kule walikokuwa wamesimama dereva wa basi na wenzake.

“Bila shaka tayari umeshaoa, namaanisha una mke na watoto!” Rehema aliongea jambo lililonifanya nitabasamu kidogo huku nikigeuza shingo yangu kuwaangalia watu waliokuwa wamezagaa eneo lile na wengine walikuwa wanatuangalia kwa umakini.

“Bado sijaoa… namaanisha sina mke, sina mchumba na wala sina mtoto,” niliongea kwa utulivu huku nikiendelea kutabasamu.

“Hujaoa, huna mchumba na wala huna mtoto! Unasubiri nini? Yaani kijana mtanashati kama wewe bado hujaoa hadi sasa?” Rehema aliuliza kwa mshangao huku akionesha kutoamini.

“Kwani msichana mzuri sana na mrembo, tena wa shani kama wewe tayari umeshaolewa?” nami nilimtupia swali na kumfanya aachie tabasamu.

“Ningeolewaje wakati nilikuwa bado nasoma! Na chuo chenyewe nimemaliza hivi karibuni tu,” Rehema aliniambia kwa sauti tulivu ya kujiamini.

“Lakini naamini tayari una mchumba, uongo?” nilimuuliza tena na hapo nikamwona akisita kidogo na kuinamisha uso wake chini, akafikiria jambo kwa kitambo kidogo. Kikapita kitambo kifupi cha ukimya na mara akainua uso wake kunitazama huku akilazimisha tabasamu.

Yeah, nina mchumba,” Rehema aliongea kwa utulivu huku akiminyaminya vidole vya mikono yake.

“Hongera! Lakini hapa upo peke yako, mchumba wako yupo wapi?” nilimuuliza Rehema huku nimekunja uso wangu, maana sikutegemea kupata jibu kama hilo lililoonekana kuurarua moyo wangu.

“Yupo South Africa anamalizia shahada yake ya pili ya International and Development Economics,” Rehema aliniambia huku akiyakwepa macho yangu na kutazama chini.

“Kwa hiyo mtaoana mara tu atakaporejea nchini?” nilimuuliza tena lakini wakati huo nikijitahidi kuliondoa donge la wivu lililokuwa limenikaba kooni.

“Sidhani kama hilo litatokea,” Rehema alisema kwa sauti tulivu iliyojaa huzuni na kunifanya nipigwe na butwaa.

“Kwa nini lisitokee! Kuna tatizo lolote kati yenu?” niliuliza huku nikihisi kuwepo jambo lisilo la kawaida.

“Hakuna tatizo lolote isipokuwa sina uhakika kama nampenda. Kwa kweli moyo wangu bado upo kwako…” Rehema aliniambia kwa sauti tulivu huku akiipitisha mikono yake nyuma ya shingo yangu na kufanya chuchu za matiti yake kukitekenya kifua changu. Hakujali macho ya watu yaliyokuwa yanatutazama kwa mshangao.

Na hapo nikajikuta nikiwa na wakati mgumu sana wa kupambana na joto kali la mwili wake ingawa lilinifanya nijisikie faraja ya aina yake.

“Hata hivyo, kuna kitu bado kinanitia wasiwasi mkubwa,” Rehema aliongea kwa utulivu huku akiitoa mikono yake kutoka shingoni kwangu.

“Kitu gani?” nilimuuliza kwa shauku huku nikishtushwa na kauli yake.

I’m just curious… na naomba uwe mkweli. Inawezekanaje hadi leo bado hujaoa na huna mchumba!” kauli ya Rehema ikanifanya nizidi kutabasamu.

Trust me. Sina sababu ya kukuongopea… by the way, nadhani huu ndiyo muda wangu sasa wa kuoa,” nilisema huku nikiendelea kutabasamu.

Rehema hakusema kitu kwa nukta kadhaa bali alinitazama kwa umakini kama ambaye hakuwa amenisikia. Alionekana kuwaza mbali. Nilimtazama machoni nikajaribu kuyasoma mawazo yake lakini sikuweza kujua alikuwa anawaza nini. Kitambo kifupi cha ukimya kilipita huku Rehema akinitazama kwa macho ya wizi. Kwa mtazamo huo nilishindwa kabisa kuelewa, na uzoefu wangu kwa wasichana warembo wa aina yake ukaniacha njia panda.

“Naamini sasa furaha yangu inaweza kurudi tena,” hatimaye Rehema alisema kwa sauti ya chini na kushusha pumzi, sauti yake iliendelea kuwa tulivu.

“Kwani ilikwenda wapi?” nilimuuliza kiuchokozi.

“Uliondoka nayo…” aliniambia na kuminya midomo yake mizuri yenye maki kisha akaongeza. “Kwa kweli nilishindwa kukutoa akilini mwangu jambo lililonifanya nishindwe kuingia katika uhusiano na mwanamume mwingine.”

“Lakini si una mchumba? Au yeye si mwanamume?” nilimuuliza Rehema kwa mshangao.

“Ni mwanamume, lakini…” Rehema alinijibu lakini nikamdaka kabla hajamalizia.

“Lakini nini? Kwani kuwa na mchumba si kuwa na uhusiano?” nilimuuliza huku nikimkazia macho.

Rehema alitaka kusema jambo lakini akasita, mdomo wake ulikuwa unataka kusema jambo lakini akili yake haikuonekana kufanya kazi kwa muda. Nilibaki kimya nikiangalia kila hatua aliyokuwa akiipitia.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

45

“Naomba unielewe, Jason… tangu uliponiingiza kwenye ulimwengu wa huba na baadaye ukaniacha kwenye mataa niliwachukia wanaume wote na sikutaka kuwa na uhusiano na mwanamume yeyote kwa kuogopa kuumizwahadi mwaka jana nilipokuja kukutana na huyo bwana nilipokwenda kumtembelea dada yangu mkubwa, Dk. Camila. Akanitongoza lakini nilimwambia ni mapema mno kukubali, nahitaji kumaliza kwanza masomo yangu ndipo nifikirie kuhusu suala la uhusiano… hakuwa na neno, alikubali kunisubiri nimalize kwanza chuo kwa kuwa hata yeye anasoma. Ni hivyo tu,” Rehema alisema kwa sauti ya chini yenye kuonesha mashaka na kisha akailamba midomo yake iliyokauka.

Nilibaki kimya huku nikimtazama usoni kwa umakini, hata hivyo sikuiona yakini kwenye macho yake. Nikamhurumia sana nikijiuliza, aliwezaje kumpenda mtu kama mimi ambaye sikuwa na mapenzi ya dhati na neno mapenzi au ndoa kwangu lilikuwa sawa na msamiati wa Kichina!

“Umesema umemaliza chuo lini?” nilimuuliza kwa shauku.

“Nime-graduate mwaka huu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na nilikuwa nachukua social science,” Rehema alijibu huku akinitazama machoni.

Ooh! Congratulation.” Nilisena huku nikinyoosha mkono wangu kumpa. “Na huku unaeleka wapi?”

“Ahsante… huku nakwenda Kahama kwa dada Camila. Ni Daktari wa Mifugo wa Wilaya ya Kahama,” Rehema alisema.

Okay!” nilijibu huku nikibetua kichwa changu.

“Sasa naomba uniambie ukweli, Jason… kwani nilikukosea nini kikubwa hadi ukaamua kukata mawasiliano? How could you do this to me?” Rehema aliniuliza maswali mfululizo. Nilipomtazama machoni nikayaona macho yake yakianza kulengwalengwa na machozi, sikujua kama yalikuwa machozi ya furaha au ya huzuni.

“Kwa nini tusiachane na mambo yaliyopita na tuzungumzie mustakabali wetu?” nilimwambia Rehema huku nikipeleka vidole vyangu kufuta machozi yaliyokuwa yanamlengalenga machoni.

“Si rahisi kihivyo kama unavyodhani. Unajua hasa ni kiasi gani nilikupenda na kujitoa kwa ajili yako lakini ukaamua kuumiza moyo wangu! Si hivyo tu, leo pia umenidhihirishia kuwa kumbe ulishanitupa kwenye kapu la sahau!” Rehema alisema na kisha akageuza shingo yake kutazama kule alikokuwa amesimama Amanda, halafu akayarudisha tena macho yake usoni kwangu.

Nami niligeuza shingo yangu na kumwona Amanda akiwa amesimama chini ya kivuli cha mti, alikuwa peke yake na alikuwa anatuangalia kwa umakini, macho yake yalikuwa makini kufuatilia kila hatua tuliyokuwa tunaipitia.

By the way, yule ni nani?” Rehema aliniuliza huku akionekana kudhibiti donge la wivu lililomkaba kooni mwake. Nikagundua kuwa Rehema alikuwa bado ana wivu mkubwa juu yangu.

“Yupi?” nilimuuliza huku nikijifanya sielewi alichokuwa anamaanisha.

“Yule msichana pale uliyekuwa unaongea naye muda mfupi uliopita huku mkipambwa na tabasamu na vicheko muda wote. Ni nani kwako?” Rehema aliniuliza tena huku akinionesha kwa kichwa kule alikokuwa amesimama Amanda.

Dah! Ni kweli Rehema aliendelea kuwa yule yule ‘Ray the MP’ kama tulivyozoea kumwita! Alikuwa msichana mwenye sifa zote nzuri lakini alikuwa mtata sana ilipotokea msichana yeyote akaingilia anga zake kwa kutaka kuwa karibu na mimi.

Nikakumbuka mgogoro mkubwa uliwahi kuibuka kati yetu wakati naelekea kufanya mtihani wangu wa kidato cha sita, tuliingia katika mgogoro mkubwa uliotia doa sugu uhusiano wetu. Mgogoro huo ulisababisha kukatika kwa mawasiliano baina yetu. Tangu wakati huo ni takriban miaka sita na ushee ndiyo tukakutana tena siku hii tukiwa safarini kuelekea Kahama.

Niliikumbuka vyema siku hiyo aliponikuta nikiwa sehemu ya faragha na msichana Minaeli Mshana, rafiki yake wa karibu waliyesoma darasa moja katika Shule ya Kilakala, na kwa mkao tuliokuwa tumekaa, Rehema aligundua kuwa kulikuwa na jambo lisilo la kawaida kati yetu. Mbaya zaidi tulipomwona tulishtuka sana na kumfanya aziamini moja kwa moja hisia zake, akamtuhumu Minaeli kuwa mwizi wa penzi lake.

Wee! Siku hiyo nilijuta! Rehema aliumia sana akijiona amesalitiwa kabisa, alilia kwa uchungu na hata nilipojaribu kumwelewesha kuwa hisia zake zilikuwa kinyume na ukweli bado hakunielewa kabisa. Ukazuka ugomvi mkubwa baina yake na Minaeli, ugomvi ulioishia katika kuvunja urafiki wao na kutupiana vijembe na kejeli huku chuki isiyo kifani ikipamba moto. Nilipojaribu kuingilia kati kwa lengo la kutafuta suluhu, Rehema hakunielewa kabisa.

Ni mimi ndiye nilikuwa chanzo cha mawasiliano baina yetu kuvurugika, kiasi cha kufikia hatua ya kukatika kabisa kwa mwezi mzima. Ni wakati huo nilipoanza mitihani ya kumaliza kidato cha sita, na Rehema akiwa ameingia kidato cha nne. Tulipomaliza tu mitihani nikaondoka kurudi nyumbani Tabora pasipo kumuaga Rehema. Huo ndiyo ulikuwa mwisho wa uhusiano wetu na hatukuonana tena.

Sasa tulikuwa tumekutana tena tukiwa safarini na bado Rehema alionesha kunipenda sana ingawa hakujua nilikuwa naishi maisha gani kipindi chote tangu tulipoachana, na alionesha kuendelea kunionea wivu hata aliponiona nikiongea na Amanda…

“Mbona hutaki kujibu, yule mwanamke ni nani wako?” Rehema alinizindua toka kwenye mawazo yangu kwa swali lake huku akinitazama kwa umakini.

“Oh, jamani Ray, hivi bado tu hujaacha wivu wako! She is nothing,” nilisema huku nikigeuza shingo yangu kumwangalia Amanda ambaye muda huo alikuwa anaongea na simu lakini macho yake yakiwa kwetu.

“Hivi unajua ni kiasi gani umeniumiza, Jason?” Rehema aliniuliza huku akinitazama machoni kwa umakini, “Una uhakika hakuna kinachoendelea kati yako na yule dada?”

You don’t trust me, right?” nilimuuliza Rehema huku nafsi yangu ikinisuta kisha nikageuza shingo yangu kumwangalia Eddy aliyekuwa anapita karibu yetu na kunifanyia ishara kuwa nimfuate. Rehema pia alimwona Eddy kisha akayarudisha macho yake kwangu.

“Yule ni kaka yako?” Rehema aliniuliza huku akiyahamishia macho yake kwa Eddy.

“Ndiyo, kaka yangu mkubwa. Kwani vipi!” nilimuuliza kwa shauku.

“Mnafanana sana, japo yeye anaonekana ni mtu rahimu, mkweli na mstaarabu sana tofauti na wewe,” Rehema alisema huku akinitazama machoni kwa umakini. Sikusema kitu, nilibaki kimya nikimtazama kwa tabasamu.

“Sasa ngoja kwanza nikamsikilize kwanza brother then nitakuja tuongee vizuri,” nilimwambia Rehema kisha nikambusu kwenye paji la uso wake.

Okay! Nakusubiri kwa hamu uje ujibu maswali yangu,” Rehema alisema kwa sauti tulivu.

Nilimwacha nikaanza kupiga hatua zangu haraka kumfuata Eddy. Wakati natembea nilijua kabisa kuwa macho ya Rehema yalikuwa nyuma yangu yakinisindikiza.

“Kweli milima haikutani! Yule msichana tulipotezana kitambo na sikujua kama ningeweza kukutana naye tena. Ni msichana niliyempenda sana!” nilimwambia Eddy mara tu nilipomfikia.

Eddy alinitazama kwa umakini na kuangua kicheko kikali cha kejeli. “Una uhakika kuwa ulimpenda sana?” aliniuliza huku akiendelea kucheka.

“Inamaana huniamini au vipi! Amini kuwa sijawahi kupenda msichana kama nilivyompenda Rehema. Lakini naona unacheka kwa dharau,” nilimwambia Eddy huku nikiwa nimekerwa kidogo.

“Ni kwa sababu hujawahi kupenda kabisa. Kazi yako ni kuchezea hisia za wasichana na kuwaacha kwenye mataa!” Eddy alisema kwa msisitizo. “Nani atakuamini kwa tabia yako ya kuwabadili kama nguo na wala hujawahi kuamini kuwa duniani kuna mapenzi ya kweli. Au naongopa?” aliniuliza huku akinikazia macho.

“Lakini si kwa Rehema…” nilijikakamua kusema lakini Eddy akanizuia kwa ishara ya mkono.

“Hakuna cha lakini, Jason. Mimi ni kaka yako nakufahamu vizuri sana kuliko mtu yeyote…” Eddy alisema huku akigeuza shingo yake kumwangalia Rehema. “Kama kweli ulikuwa unampenda sana usingeshindwa kumkumbuka ulipomwona akipanda ndani ya basi!” aliongea neno lililonifanya nishikwe na kigugumizi.

“Ni msichana mzuri sana na asiye na hatia. Ni kama Belinda tu… nakuomba kuwa mkweli kwake na usijaribu kuchezea hisia zake.” Eddy alisema huku akiwa bado anamwangalia Rehema.

Nilitaka kusema neno lakini hatia ikanikaba kooni. Kwa kweli kukumbushwa kifo cha Belinda lilikuwa jambo lililoniumiza mno kihisia. Japokuwa katika maisha yangu niliamini kuwa kiumbe aliyeitwa mwanamke alikuwepo duniani kwa ajili ya kumfurahisha na kumburudisha mwanamume tu, ila kifo cha Belinda kiliniumiza.

“Tafadhali, kuwa mwangalifu sana unapolitaja jina hilo mbele yangu. Belinda amekwenda na ninatakiwa kumsahau…” nilimwonya Eddy huku nikiwa nimemkazia macho.

“Lakini huo ndiyo ukweli. Lazima nikwambie ukweli ili…” Eddy alisema lakini nikamkatisha kwa hasira.

“Nimesema sitaki kulisikia jina la Belinda kwenye maongezi yetu yoyote. Please, brother!” niliongea kwa hasira huku nikishusha pumzi ndefu.

Eddy alinitazama kwa umakini usoni bila kusema neno kisha alionekana kukubaliana nami. “Ok, tuachane na hayo… vipi kuhusu chakula maana naona kama vile mwenzangu huhisi njaa kwani muda wote unaongea na warembo tu! Nimekwambia muda mrefu tukatafute chakula lakini huonekani kujali!” Eddy aliniambia huku akinitazama usoni kwa makini.

“Hatuwezi kuachwa na gari?” nilimuuliza Eddy kwa wasiwasi, lakini ukweli wasiwasi wangu haukuwa kuachwa na basi bali akili yangu ilikuwa kwa Rehema.

“Nimeongea na dereva, amesema uwezekano wa kuondoka saa hizi haupo. Wanamsubiri mtu mmoja atoke Nzega mjini awaletee gurudumu jingine, na hiyo itachukua zaidi ya saa kufika hapa na kulifunga,” Eddy alisema na kuanza kuondoka, akashika njia iliyokuwa ikiingia vichakani.

Nilijikuta nikiwa njia panda, sikujua nimfuate Eddy au nikaongee na Rehema! Katika hatua hiyo niligeuza shingo yangu kumwangalia Rehema, macho yetu yalipokutana nikamfanyia ishara ya kwamba ningerudi kwake baada ya muda mfupi na hapo nikaanza kupiga hatua zangu taratibu kuelekea ile njia iliyokatiza vichakani nikimfuata Eddy.

* * *

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

46

Binti Afrika.


Saa 10:20 jioni…

NILIJIKUTA naenda umbali wa zaidi ya mita 100 ya bila kumwona Eddy, nilikuwa katikati ya vichaka vidogovidogo, na nilipotaka kumwita Eddy mara nikaiona njia nyembamba ikiingia upande wangu wa kulia, ilionekana ni njia iliyokuwa ikipitiwa na watu pamoja na mifugo mara kwa mara.

Kwa sekunde kadhaa nilisimama hapo nikiitazama ile njia kwa umakini huku nikifanya tathmini dhidi ya mazingira yale, na kwa kufanya vile hisia zangu zilinitanabaisha kuwa njia hiyo ilikuwa inaelekea kwenye makazi ya watu ambayo hayakuwa mbali sana kutoka eneo lile nililokuwa nimesimama.

Nilipoyatega kwa umakini masikio yangu kusikilizia nilihisi kuzisikia sauti za watoto wakicheza na hata sauti za wanyama wa kufugwa, kwa mbali zikihanikiza.

Hatimaye nikaanza kutembea haraka nikiifuata ile njia kwa kuamini kuwa ingenifikisha alikokuwepo Eddy kwani sikuwa na shaka yoyote kuwa alikuwa ameifuata njia ile. Pamoja na kuongeza mwendo lakini sikuona dalili zozote za uwepo wa Eddy katika eneo lile jambo lililoanza kunishangaza sana.

Lilikuwa ni eneo lenye vichaka vidogovidogo na mbele kidogo niliona mashamba ya mahindi na mihogo iliyokuwa imestawi barabara. Nikajiambia kuwa kama nisingekuwa makini basi ningeweza kupotelea vichakani, nikaanza kumwita Eddy kwa sauti kubwa lakini yenye wasiwasi, huku nikizidi kusonga mbele.

Niliita na kuita lakini eneo lile lilikuwa kimya kabisa! Ni sauti za ndege warukao ndizo zilizosikika. Nikahisi kuwa labda Eddy alikuwa ametokomea mbali zaidi na kwa maana hiyo nilikuwa napoteza muda wangu bure kuita.

Mwishowe nilisimama nikiwa nimeanza kukata tamaa na kutaka kurudi kule nilikotokea, lakini kabla sijafikia uamuzi wa kurudi kule barabarani nikasikia sauti ya Eddy akiniita kwa sauti iliyokuwa na tahadhari zote. Niligeuka haraka kutazama kule ambako nilihisi sauti hiyo ilikuwa inatokea na nikaona shamba la mihogo iliyokuwa imestawi hasa. Sauti ilikuwa inatokea ndani ya shamba hilo, sikujiuliza mara mbili nikaanza kupiga hatua zangu kuzama ndani ya shamba la mihogo.

Eddy hakuwa ndani sana, nilimkuta akiwa amekaa kwenye tuta la mihogo huku akimenya kipande cha muhogo kwa meno yake na kukitafuna, kando yake kulikuwa na shina la muhogo lililofukuliwa.

Nilisimama nikalitazama lile shina la muhogo lililokuwa kando ya Eddy kwa umakini kisha bila ya kujiuliza mara mbili nikatoa kisu changu kidogo cha kukunja nilichopenda kutembea nacho mfukoni, nikakikunjua. Nilipokuwa nainama ili kuukwanyua muhogo, nikasikia sauti nyororo ya mwanamke ikiongea kutoka nyuma yangu.

“Kwa hiyo huo ndiyo ustaarabu wa mjini kula vitu vya watu wengine pasipo hata ruhusa!” ilikuwa sauti laini iliyonifanya niinuke haraka na kugeuka haraka kutazama upande ilikotokea ile sauti.

Na hapo macho yangu yakaangukia kwenye umbo lililovutia sana la msichana wa kijijini. Alikuwa binti wa Kiafrika haswa mwenye uzuri wa asili usiohitaji mapambo mengine. Alikuwa amevaa dela la bluu lenye maua mekundu na juu ya dela hilo alijifunga mtandio kiunoni, na kichwani alikuwa amebeba ndoo ya maji.

Kwa mwonekano tu alionekana ni msichana ambaye hakuwa amezidi miaka 21, alikuwa mrefu wa wastani na maji ya kunde. Rangi yake ya ngozi ilikuwa na mng’aro wa aina yake na ilipendeza sana, na wala hakuhitaji kabisa vikorombwezo vya aina yoyote ile kuinakshi ngozi yake.

Macho yake yalikuwa makubwa na legevu lakini yalikuwa aina ya yale macho yanayoita kwa mng’aro sadifu, yakiambatana na kope nyingi nyeusi ambazo ziliachia nafasi kwa nyusi ili zipate kujidai. Alikuwa na nywele nyingi nyeusi za kibantu zisizotiwa dawa na alikuwa amezisuka kwa aina fulani ya msuko ambao sikujua uliitwaje, na hivyo kumfanya aonekane ni binti halisi wa Afrika.

Kwa ujumla hakuwa msichana wa kumtizama mara moja tu ukamwacha, alikuwa na umbo fulani hivi “amazing” ambalo lisingeshindwa kuikondesha akaunti ya mwanaume yeyote rijali (hata kwa wale mabahili) bila ya taabu yoyote.

Mimi na Eddy tulitazamana tukiwa hatuna la kusema kwani ni kweli tulikuwa tumevamia shamba la mihogo la watu na kuanza kula pasipo ruhusa ya wenye shamba. Hata hivyo, yule msichana baada ya kusema maneno yale hakuonekana kutujali, alitupita na kuendelea na safari yake kana kwamba hakuwa ametuona.

Alipokuwa anatembea maji kwenye ndoo yalikuwa yanamdondokea mgongoni na kuchuruzika hadi kwenye makalio yake makubwa na miguuni.

“Dah, type zangu hizo! Huyu ndiye binti Afrika!” nilijikuta nawaza huku nikiwa nimevutiwa mno na umbo lake. Sikujiuliza mara mbili nikaanza kupiga hatua zangu haraka kumfuata.

“Subiri basi, bibie… ni kweli tumekosea lakini hata kutosimama na kuwasikiliza wakosaji wanaotaka kuomba msamaha nalo pia ni kosa,” nilimwambia yule msichana ambaye ningependa kumwita Binti Afrika, hata hivyo hakusimama wala kugeuka.

Kuona hivyo niliamua kuongeza mwendo wangu kumfuata huku Eddy akiwa ananitazama kwa mshangao ingawa hakuinuka wala kutoka pale kwenye tuta la mihogo alipokuwa ameketi. Niligeuza shingo yangu kumwangalia nikamwona akiendelea kutafuna muhogo taratibu.

Nilimfikia yule msichana aliyekuwa anatembea taratibu na kwa madaha, wakati alipokuwa anaifikia kona moja karibu na kichaka. Nikamshika mkono wake wa kushoto na kumfanya asimame na kunitazama usoni kwa umakini.

“Najua tumefanya kosa, lakini kwa nini hutaki kunipa nafasi ya kunisikiliza?” nilimuuliza yule msichana huku nikisimama mbele yake katika namna ya kumzuia asiondoke.

Yule msichana alinitazama kwa tabasamu pasipo kusema neno na wala hakuwa akipepesa macho yake. Na hapo nikapata nafasi ya kuuona vizuri uzuri wake.

“Dah, sijui mwanamume gani anamfuja mtoto mzuri kama huyu huku kijijini?” nilijiuliza moyoni baada ya kumtazama vizuri usoni na kuyaona macho yake meupe makubwa na legevu yakinitazama usoni kwa namna ya pekee huku tabasamu lake likichanua kuashiria urafiki.

Japokuwa alikuwa amevaa dela tu la kawaida na kujifunga mtandio lakini bado uzuri wake uliweza kuonekana waziwazi, kwa hakika alikuwa binti halisi wa Kiafrika mwenye uzuri halisi usiohitaji vipodozi vya aina yoyote ili kumpendezesha, na pia hakuhitaji mafuta mazuri au manukato kumfanya anukie vizuri kwani hata angejipaka grisi bado angevutia tu.

“Haya, unasemaje?” yule msichana aliniuliza kwa sauti tulivu na hivyo kunifanya, kwa sekunde kadhaa, nikose neno la kuongea kutokana na kupumbazika na uzuri wake ulioendana na sauti yake nyororo.

Alipoona nimezubaa aligeuza shingo yake kuangalia huku na kule kama aliyekuwa anatafuta kitu fulani kisha akayarudisha macho yake kwenye uso wangu. Muda wote nilikuwa namtazama kwa tabasamu, na hapo tukabaki tukitazamana kwa kitambo kifupi huku ukimya ukitawala kati yetu.

“Tusalimiane kwanza mrembo… hujambo?” nilimsalimia kwa sauti ya chini baada ya kitambo kile kifupi cha ukimya huku nikiendelea kutabasamu.

“Sijambo,” yule msichana alinijibu kwa mkato huku akionesha haya. Kisha aliyaondosha macho yake haraka toka kwenye uso wangu akionekana kushindwa kunitazama usoni kisha akajitoa kwenye mkono wangu na kuanza kupiga hatua taratibu kuondoka.

Niligundua kuwa alikuwa msichana mwenye haya na hivyo nikamfuata tena na kumshika mkono, sasa sikutaka kulemba bali nilianza kumchombeza kwa maneno matamu niliyoamini yangemfanya anisikilize.

“Unajua kwa msichana mzuri kama wewe si vizuri kuwa hivyo, hata Mungu hapendi ujue…” nilimwambia kwa sauti tulivu ya chini huku nikimtazama usoni.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

47

“Kwani nikoje?” yule msichana aliniuliza huku akinitupia jicho la wizi na kisha akatazama chini.

“Nimeshakiri kosa letu lakini mbona hutaki hata kusema kama umetusamehe? Namna hiyo si nzuri mrembo…” nilisema kwa kuchombeza.

“Niliwasamehe tangu nilipogundua kuwa ninyi ni wageni hapa kijijini. Kwani ninyi ni akina nani na mnatokea wapi?” yule msichana aliniuliza huku akinitazama kwa umakini kisha akageuza shingo yake kumwangalia Eddy ambaye muda huo alikuwa amesimama kando ya ile njia akitutazama kwa umakini.

Umbali wa kutoka alipokuwa amesimama Eddy hadi sehemu tuliyokuwepo mimi na yule msichana ilikuwa ni takriban mita 60 tu.

“Sisi ni wasafiri tunaelekea Kahama ila bahati mbaya basi letu limepata pancha na tupo hapa kijijini kwenu tangu saa nane. Tuna njaa ya kufa mtu na hatujui tutapata wapi chakula,” nilimwambia yule msichana kwa sauti tulivu lakini ya kutia huruma.

“Mko na basi gani, Makenga Trans?” yule msichana aliniuliza huku akinitazama kwa umakini kutaka uthibitisho wangu. Nilibetua kichwa changu kukubali.

“Pancha ya ngapi tangu mtoke Nzega?” aliniuliza tena akionesha kutoshangazwa na tukio lile. Nikashangazwa sana na swali lake.

“Ya kwanza, gurudumu la mbele limepasuka wakati tukilikwepa kundi la ng’ombe,” nilijibu huku mshangao wangu ukiwa bado haujanitoka.

“Hata hivyo mna bahati sana. Makenga Trans inajulikana kwa pancha,” yule msichana aliniambia huku akishusha pumzi.

“Wala hatuna bahati maana hadi sasa hatujui tutaondoka saa ngapi kuelekea Kahama kwa sababu hata gurudumu la akiba hawana,” nilimwambia yule msichana huku nikiitupia jicho saa yangu ya mkononi. Yule msichana akaonekana kusikitika.

“Itabidi mvumilie tu maana hakuna namna ya kufanya, Makenga Trans na Kadwisha Bus Service ndiyo mabasi pekee yaliyobaki katika barabara hii, magari mengine yote yanapitia Tinde! Basi la Kadwisha huwa linaondoka Nzega asubuhi na kurudi alasiri,” alisema huku akinitazama kwa huzuni.

“Dah! Sasa sijui itakuwaje!” nilijikuta nasema huku nikiwa nimeanza kukata tamaa.

“Vumilieni tu,” alisema kisha akaniuliza huku akinitazama kwa umakini usoni “Kwa hiyo shida yenu ni chakula?”

Niliitikia kwa kubetua kichwa.

“Basi nisubirini nipeleke maji, narudi sasa hivi na chakula,” alisema kisha akaanza kuondoka haraka toka eneo lile.

“Unatuletea chakula gani?” nilimuuliza kwa pupa.

“Wewe subiri… naamini utakipenda sana,” aliniambia huku akizidi kupiga hatua.

Wakati anatembea akili yangu ilijikuta inazidi kupumbazika na mtikisiko maridhawa wa mzigo wa makalio yake. Nilikitazama kiuno chake chembamba kilivyokuwa kinajinyonga nyoga alipokuwa anatembea na mara nikahisi msisimko wa aina yake kwenye mwili wangu huku sehemu ya mbele ya suruali yangu ikianza kututumka.

“Natumaini atarudi kweli! Ngoja nivute subira maana namhitaji zaidi yeye kuliko hata chakula chake,” niliwaza huku nikiendelea kumsindikiza kwa macho yaliyojaa matamanio.

Ndani ya kichwa changu kulikuwa na sauti fulani iliyokuwa inanishawishi, “akija anguka naye, wala usifanye makosa.”

Niliendelea kumsindikiza kwa macho ya utulivu hadi pale alipotokomea kabisa kwenye macho yangu na kupotelea kwenye vichaka huku nikijihisi faraja ya kipekee moyoni mwangu kisha mawazo yangu yalihamia kwenye tafakuri nyingine. Ni hapo nilipomkumbuka Eddy aliyekuwa bado amesimama akinitazama kwa umakini, niligeuka na kumkonyeza huku nikianza kupiga hatua za haraka kumfuata.

“Tuvute subira kidogo, yule msichana anatuletea chakula,” nilimwambia Eddy mara tu nilipomfikia kisha nikazama kwenye shamba la mihogo na kuchukua kipande cha muhogo na kukimenya kisha nikawa nakitafuna taratibu. Eddy aliendelea kunitazama kwa umakini, kuna wakati alitaka kusema neno lakini akaonekana kusita.

“Mbona kama unataka kusema jambo lakini unasita?” nilimuuliza huku nikimwangalia kwa udadisi.

“Hata sijui nisemeje, lakini nahisi kinachokuweka hapa wala si hicho chakula bali mawazo yako yapo kwenye ngono tu, unataka kucheza na hisia za huyo binti,” Eddy alisema kwa sauti iliyoashiria huzuni.

“Wala si kweli, au kwa sababu wewe umeshiba mihogo!” nilimwambia Eddy kwa kumlaumu.

“Nakujua Jason na huwezi kunidanganya… labda niambie unaamini kweli huyo binti kuwa ataleta chakula?” Eddy aliniuliza huku anageuza shingo yake kuangalia kule alikoelekea yule msichana.

“Hata sijui lakini namwamini tu!” nilimjibu kwa wasiwasi kidogo.

“Sasa kama hujui unajipaje matumaini kiasi hicho?” eddy aliniuliza kwa mshangao.

“Sijui kwa kweli, lakini bado namwamini!” nilisema kwa sauti ya chini huku nikishusha pumzi.

Eddy aliachia tabasamu huku akitingisha kichwa chake taratibu. Nilimtazama kwa umakini na kumwona akigeuza shingo yake kuangalia kule barabarani kwenye basi huku akijaribu kusikilizia kwa umakini. Nikahisi kuwa alikuwa anapima wapi penye uzito kati ya kurudi kwenye basi au asubiri mlo tulioahidiwa!

“Sawa, ngoja nikachungulie na huku kwenye basi ili tusije tukaachwa kwa sababu ya kusubiri chakula,” Eddy alisema huku anaondoka haraka kuelekea kule barabarani na kuniacha peke yangu.

Nilipoachwa peke yangu nilianza kuwakumbuka Rehema na Amanda niliokuwa nimewaacha kule barabarani. Kwa jinsi nilivyokuwa na ugwadu nilitamani kuwamiliki wote wawili na hata ikibidi nibanjuke nao kwenye ulimwengu wa huba katika kitanda kimoja na kwa usiku mmoja. Sikujua sana kwa upande wa Amanda ila Rehema alikuwa mtata, asingekubali kuchanganywa.

Na hapo nikakumbuka siku moja nilipomgonganisha Rehema na msichana mwingine aliyeitwa Kinoge baada ya kuzuka ghafla eneo nililokuwa nimeketi na Rehema.

Ilikuwa siku ya Jumapili nilipompeleka Rehema pale Wazawa Pub, sehemu iliyotulia sana kwa starehe katika eneo la Misufini mjini Morogoro. Huo ulikuwa ni mwendelezo wa kula bata na warembo wakati nasoma Mzumbe. Wakati tukisubiri kuhudumiwa mara nikasikia sauti ya msichana ikinisemesha kwa hasira kutokea nyuma yangu.

“Yaani wewe mwanaume hujatulia kabisa! Hakya Mungu siku ukifa makahaba wote mjini wataomboleza kifo chako kwa kujifunga khanga nyeusi, na tena watazivalia mapajani yaani nusu mlingoti!” nilimsikia msichana huyo akiongea maneno ya shombo lakini sikujua kama alikuwa ananiambia mimi.

Niligeuka haraka kutazama kule ilikotokea sauti hiyo na kumwona Kinoge, msichana wa Kiluguru aliyekuwa anaishi kwenye makazi ya wanakijiji yaliyokuwa yanazunguka eneo la shuleni kwetu Mzumbe. Kinoge alikuwa mweupe, hakuwa mrefu wala mfupi na alikuwa na umbo kubwa kidogo lakini lililovutia. Alikuwa na mashavu mfano wa chungwa na siku hiyo alivaa gauni zuri la kitenge lililoushika vyema mwili wake. Nilibaki kumkodolea macho pasipo kusema neno lolote.

“Kwa hiyo juzi ulifurahi sana kunichomesha mahindi, si ndiyo? Yaani mimi nakusubiria pale getto kumbe wewe umeondoka na yule malaya wa Kisambaa!” Kinoge alibwata huku akinikazia macho. Alikuwa ameshika chupa ya bia na alikuwa anaja pale tulipoketi. Sikujua alitokea wapi!

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

48

Pamoja na kumwekea ‘uso wa mbuzi’ lakini aliendelea kuhororoja maneno mengi ya shombo huku akiwafanya watu wote walioketi eneo lile waache mambo yao na kumtazama kwa mshangao, na kubwa zaidi walitaka kujua ni nani aliyekuwa akiambiwa maneno yale.

“Kwa hiyo unajiona wewe ndiyo kidume sana hapa mjini, si ndiyo?” Kinoge aliendelea kubwata huku akiwa amesimama mbele yangu akinitazama kwa hasira. Sikumjibu. Nilibaki kimya nikimtazama kwa dharau kana kwamba alikuwa mwendawazimu asiyejitambua huku nikijifanya simfahamu kabisa.

“Si naongea na wewe, hendisam’boi!” Kinoge alisema huku akinishika bega.

Nilipandwa na hasira lakini sikutaka kuonesha chochote kwani moyo wangu uliingiwa na fadhaa na sikupenda kugeuka sinema katika eneo lile lenye watu wastaarabu. Nilijitahidi kuzuia hasira zangu huku nikimtazama Rehema kwa namna ya kujifanya nashangaa kwamba simfahamu Kinoge. Mwanzoni Rehema alinitazama huku akijitahidi kuwa mtulivu.

“Samahani aunt, kwani wewe ni nani maana naona unafika hapa na kuanza kutukana tu bila hata salamu?” Rehema alimuuliza Kinoge huku akimtazama kwa mshangao.

“We mwanamke koma! Unataka ujue mimi ni nani ili iweje?” Kinoge alimjibu Rehema kwa hasira.

Rehema akanikata jicho kali akionesha kutaka kujua kilichokuwa kikiendelea pale. “Jason, kwani nini kinaendelea hapa?” aliniuliza huku kanikazia macho.

“Achana na huyu mwanamke mlevi, naona ana stress na kupigwa kibuti na bwana yake kwa hiyo anatafuta pa kuangukia,” nilimjibu Rehema lakini hakuonekana kuridhika.

“Lakini…” Rehema alitaka kuongea lakini alikatishwa na Kinoge aliyeanza kubwata.

“Kwa hiyo wewe sungura-tope unataka kunijua mimi, ili iweje? Wewe si kahaba tu kama hao makahaba wengine! Kwanza sijui Jason kakuokota wapi kinyago kama wewe?” Kinoge alibwata huku akiyumbayumba kilevi na kumshika bega Rehema.

Kitendo kile hakikuwa cha kuvumiliwa hata kidogo, Rehema aliuputa mkono wa Kingoge huku akiinuka kwa hasira, na hapo nikajua sasa kumekucha na kama ni ngoma basi imepata mpigaji. Sikuona tena sababu ya kuendelea kuwa kimya au kumvumilia Kinoge. Nilinyanyuka haraka nikamtuliza Rehema na kumkalisha kwenye kiti kisha nilimkabili Kinoge huku namnyooshea kidole kwa hasira. Midomo yangu ilikuwa inatetemeka kwa ghadhabu.

“Naomba usiletee pombe na bangi zako hapa. Umesikia we malaya? Iwe mara ya kwanza na ya mwisho kumtamkia maneno hayo mpenzi wangu na ukithubutu siku nyingine kumdharau mbele yangu naapa nitavunja shingo yako!” nilimwambia Kinoge kwa hasira huku nikimtazama kwa macho makali.

Kinoge alitaka kusema neno lakini nilimkatisha kwa hasira. “Na kama umetumwa kamwambie aliyekutuma kuwa hujanikuta!” nilimwambia kwa hasira huku nikiwa tayari kumchapa makofi endapo angejaribu kufungua tena mdomo wake na kutoa lugha isiyo ya staha.

Nikamwona akinywea kama kifaranga kilichonyeshewa na mvua huku akinitumbulia macho yaliyojawa na hofu kubwa. Siku zote Kinoge alikuwa ‘ananichukulia poa sana’ na hakuwahi kuniona nikiwa nimekasirika namna ile. Alianza kurudi nyuma taratibu huku akinitumbulia macho ya hofu.

“Poa wewe si mjanja! Tutaona mimi na wewe nani mzawa na nani wa kuja, mimi ndo Kinoge,” alisema huku anaondoka na kutembea kwa mwendo wa kujitingisha huku akiufanya mzigo wa makalio yake kule nyuma kutingishika na kuwaacha watu wote waliokuwa wanamtazama wakiwa hoi…

______

“Naona mtu wako huyo anarudi!” sauti ya Eddy ilinizindua kutoka kwenye mawazo yangu. Sikujua alikuwa amerudi muda gani toka kule barabarani.

Niligeuza shingo yangu kuangalia kule alikokuwa akiangalia Eddy, nikamwona yule msichana aliyeahidi kutuletea chakula akija kwa hatua za haraka pale tulipokuwa tumesimama. Mkononi alikuwa amebeba ndoo na lile tabasamu lake la kirafiki lilikuwa halikauki usoni kwake.

Alitupofikia akasimama na kutoa mfuko mweusi wa plastiki uliokuwa ndani ya ile ndoo, akanyoosha mkono wake wa kulia kunipa ule mfuko kwa unyenyekevu huku akipiga goti moja chini. Kitendo cha kunipigia goti kikanifanya nikione vizuri kifua chake kilichobeba matiti madogo mfano wa embe dodo changa.

Na hapo nikahisi msisimko usio wa kawaida ukinitambaa mwilini wangu huku mapigo ya moyo wangu yakibadili mwendo wake na kwenda mbio isivyo kawaida! Nilishindwa kuupokea ule mfuko na kubaki nikikikodolea macho kifua chake kwa matamanio. Yule msichana alinishtukia, akaachia tabasamu la aibu huku akiinuka haraka na kutazama kando kwa aibu.

Eddy aligundua kuwa akili yangu haikuwa kwenye ule mfuko wenye chakula bali ilizama kutazama kifua cha yule msichana na muda huo nilikuwa natokwa na udenda wa uchu wa mapenzi.

Haraka Eddy aliupokea ule mfuko na kuufungua bila kuchelewa. Nikaona akitoa bakuli kubwa la plastiki lenye mfuniko na kulifungua, lilikuwa na viazi vilivyochemshwa, karanga za kuchemshwa na mapande ya nyama ya mbuzi iliyokaangwa. Pia kulikuwa na chupa kubwa ya plastiki yenye ujazo wa lita moja na nusu ikiwa imejazwa maziwa na kulikuwa na vikombe viwili vidogo vya plastiki.

“Mnaweza kuondoka navyo tu wala hakuna shida,” yule msichana alisema huku akianza kuzitupa hatua zake taratibu kuelekea kisimani. Nilishindwa kuvumilia kwa wema wake, nikapiga hatua zangu haraka kumfuata na kumshika mkono wake.

“Ahsante sana mrembo, hakika nakosa maneno mazuri ya kukushukuru!” nilimwambia huku nikiung’ang’ania mkono wake.

“Wala usijali kaka, hata siku mkiwa mnarudi pia mnakaribishwa,” yule msichana alisema bila kunitazama machoni huku akijaribu kujitoa kutoka kwenye mkono wangu bila mafanikio.

“Jason, twende kwenye gari tusije tukaachwa,” nilimsikia Eddy akiniambia huku akianza kuondoka kwa mwendo wa taratibu toka eneo lile.

Hata hivyo, sikuweza kuuachia mkono wa yule msichana kwani pepo wa ngono alikwisha nipanda kichwani. Niligeuza shingo yangu kumtazama Eddy nikamwona anachukua pande moja la nyama na kuanza kulitafuna huku akitembea.

Kitendo cha kumtazama Eddy kikamfanya yule msichana afanikiwe kujitoa kwenye mkono wangu na kuanza kuondoka haraka lakini sikumpa nafasi, nilimfuata haraka hadi karibu na kichaka kimoja kikubwa kisha nikamshika tena mkono wake huku nikimzuia.

Alisimama na kuniangalia machoni kisha akashusha pumzi za ndani kwa ndani. “Nenda mwenzako anakuacha.”

“Ujue hadi sasa hujaniambia unaitwa nani mrembo! Maana umekuwa mwema sana kwetu!” nilimwambia yule msichana. Akanitazama kwa tabasamu lake la aibu.

“Naitwa Kabula,” alisema huku akiangalia kando.

Itaendelea...
 
safari buzwagi.JPG

49

“Una jina zuri sana la Kiafrika, kama la mama yangu…” nilisema huku nikiachia tabasamu la aina yake lililoonekana kumroga haswa. “Kwa kweli leo nimefurahi sana kukutana na wewe.”

“Kweli?” Kabula aliniuliza kama mtoto mdogo.

“Unadhani ni mwanamume gani asingefurahia kukutana na mrembo kama wewe? Au ni mwanamume gani asingetamani kutaka kumkumbatia msichana mzuri kama wewe? Hakika siku ya leo nitaikumbuka katika maisha yangu,” nilimwambia huku nikiupapasa mkono wake.

“Nashukuru kusikia hivyo lakini kwangu haitakuwa hivyo,” Kabula alisema huku akiinamisha uso wake kuangalia chini kwa aibu.

“Kwa nini?” nilimuuliza kwa shauku ya kutaka kusikia upande wake alijihisi vipi juu yangu.

“Tayari nimeshaolewa,” Kabula alisema huku akinitazama kwa jicho la wizi.

“Kwani ndoa yako itaingiliaje furaha yetu saa hii, au kwani huyo mumeo yupo hapa?” nilimuuliza Kabula huku nikimkazia macho.

“Hapa hayupo lakini pengine yupo sehemu anatuangalia, unajua sijawahi kuwa na mwanaume mwingine zaidi yake kabla na hata baada ya kuolewa,” Kabula alisema na kuufanya mwili wangu uzidi kusisimkwa kutokana na kiu ya penzi lake.

“Hiyo si kitu, elewa kuwa kila jambo huja kwa kusudi lake, na hii kwetu ndiyo nafasi nzuri. Huwezi kujua huenda kukutana kwetu ndiyo ikawa mwanzo wa bahati na kufanikiwa kwako,” nilimwambia Kabula huku nikiupeleka mkono wangu kwenye shingo yake na kuanza kumpapasa. Nikamwona akiyafumba macho yake taratibu kuusikilizia mpapaso wangu.

“Ningetamani sana iwe hivyo lakini miye si mhuni, ni mke wa mtu ninayejiheshimu. Yaweza ikawa si vibaya kufanya mapenzi na mwanaume mwingine iwapo mume wangu hayupo lakini nisingependa kumdharau kiasi hiki!” Kabula alisema huku akionekana kupumua kwa shida.

Wakati akiyasema hayo alikuwa ananitazama kwa macho ya kiwiziwizi, macho yake yalikuwa yamelegea zaidi kama aliyekuwa amekula kungu. Sura yake ilionekana wazi kunisubiri nifanye kitu na mwonekano wake haukuonekana kumaanisha kile alichokuwa anakiongea muda huo. Alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kuanza kuondoka taratibu.

Niligundua kuwa alikuwa tayari ‘amekolea’ ingawa haikuwa rahisi kwake kukubali moja kwa moja, hivyo nikamfuata tena na kumshika mkono kisha nikaanza kumwongoza kuelekea kwenye shamba la mihogo iliyostawi sana kiasi cha kutengeneza vichaka. Hakuleta pingamizi lolote kwani alionekana kutojiweza na uso wake aliuinamisha chini kwa aibu.

Niligeuza shingo yangu kumtazama Eddy nikamwona kwa mbali akiishia vichakani huku akigeuka na kunifanyia ishara kuwa niachane na yule msichana na tuondoke zetu. Hakujua kuwa hatua niliyokuwa nimeifikia ilikuwa ikinihakiniza kusongesha majeshi mbele tu na nisingeweza tena kuikatili nafsi yangu. Tayari nilishapandwa na wazimu wa mapenzi.

Tulizama ndani ya lile shamba la mihogo, tukasimama katikati ya mihogo iliyotuficha na kubakisha sehemu ndogo ya juu hususan vichwa tu, kisha nikapitisha mikono yangu kumshika kiunoni bila ruhusa yake, hata hivyo nikashukuru kuwa sikukutana na upinzani wowote. Kabula akainua uso wake na kunitazama moja kwa moja machoni kisha tabasamu maridhawa likachomoza usoni mwake.

“Basi fanya haraka tusije tukakutwa, mwenzio naogopa,” Kabula aliniambia kwa sauti tulivu yenye mtetemo wa mapenzi huku akiipitisha mikono yake nyuma ya shingo yangu na kuzifanya chuchu za matiti yake kukitekenya kifua changu. Nikahisi kizunguzungu na mapigo yangu ya moyo yakienda mbio zaidi.

Kabula alioneka kuwa na kiu kikali cha mapenzi na sikutaka kuamini kuwa mume wake hakuwa anamtosheleza, au pengine hisia zetu ziliendana kwa kiwango cha juu kabisa kwa wapenzi.

Kama mtu aliyepandwa na wazimu hakutaka kupoteza muda, alinivuta karibu yake na kunimwagia mabusu mfululizo yaliyonichanganya, nikaanza kuhisi pumzi zangu zikinipaa na kuanza kuhema kwa nguvu kama mtu aliyekosa hewa safi ya oksijeni.

Kisha akaanza kufungua mkanda wa suruali yangu na baadaye akafungua zipu na mara suruali hiyo ikaanguka chini huku nikibakiwa na boksa tu. Kisha alipeleka mkono wake kwenye mtalimbo wangu na kuanza kupapasa juu ya boksa taratibu huku akinifanyia manjonjo yaliyozidi kunipagawisha.

Sikuwa na ujasiri wa kupingana na hisia zangu, hivyo nami nikaupenyeza mkono wangu taratibu hadi ndani ya mtandio wake kisha nikaupitisha hadi ndani ya dela alilovaa na baadaye ukapenya kwenye nguo ya ndani na hapo nikaanza kuyatomasa makalio yake laini yaliyoshiba minofu.

Kabula akashtuka kidogo na kuachia mguno hafifu wakati mkono wangu mwingine ulipokuwa unazitomasa taratibu chuchu zake zilizosimama. Muda huohuo nikamshuhudia akiivuta taratibu boksa yangu, akaishusha hadi magotini na kuupeleka mkono wake ikulu na kuanza kunichua taratibu kitendo kilichonifanya nianze kuhema ovyo utadhani bata mzinga. Sikuwa najiweza tena, hivyo akanisukuma nami nikaanguka chini kwenye nyasi laini.

Kutahamaki akawa amevuta mtandio wake na kuutupa chini kisha haraka sana akapandisha juu dela lake na kuja juu yangu. Muda mfupi uliofuata tukajikuta tukiwa tumehamia kwenye dunia ya maraha, dunia ya huba huku kila mmoja wetu akiwa amepandwa na wazimu wa mapenzi.

Kabula alikuwa msichana mtundu sana aliyeimudu vyema kazi ile kiasi cha kunishangaza. Nilijiuliza iliwezekanaje msichana wa kijijini asiye mhuni kama alivyodai lakini akaonekana kulimudu gwaride kiasi kile na kunipigisha kwata kwa kiwango kile!

Pamoja na ufundi wangu wote wa kucheza kwata lakini sikuweza kufua dafu kwa Kabula, alikuwa amenidhibiti kwa kila idara. Mimi nipo chini na yeye alikuwa juu yangu huku nikiishuhudia mijongeo yake ambayo sikujua kama ni ya haraka au taratibu alipokuwa akipanda juu na kushuka chini huku akizungusha kiuno chake kilichojaa shanga za rangi tofauti.

Kabula alikuwa amezitendea vyema hisia zangu, raha niliyokuwa naipata muda huo ilinifanya nisiweze hata kumtazama usoni na ningeweza kumwahidi chochote kama angeniomba. Wakati nikiwa mbioni kuvunja dafu mara nikashangaa kumwona Kabula akisitisha ghafla lile gwaride huku akiwa na uso uliojawa na hofu, alitulia kabisa kama aliyekuwa anajaribu kusikiliza kitu.

Kabla sijajua nini kilikuwa kinaendelea nikamwona anakurupuka kutoka pale chini na kusimama wima huku uso wake ukijawa na hofu kubwa. Jasho lilikuwa linamtiririka utadhani alikuwa amemwagiwa ndoo nzima ya maji na wakati huohuo macho yake aliyatoa utadhani alikuwa amemwona ziraili mtoa roho akimsogelea.

Nikataka kumuuliza lakini nikahisi kulikuwa na kishindo cha mtu au watu wakija katika eneo lile. Sikutaka kusubiri niliinuka haraka huku nikivuta juu boksa yangu kuvaa na wakati huohuo nikijitahidi kuipandisha suruali yangu, kisha nikageuka kuangalia kule ambako nilihisi sauti ya kishindo ilikuwa inatokea.

Macho yangu yakakutana na macho ya Eddy aliyesimama ghafla huku akitutazama kwa mshangao usioelezeka. Eddy alikuwa anahema kwa nguvu huku akionekana mwenye wasiwasi, mkononi alikuwa bado ameshika ule mfuko mweusi wa plastiki wenye chakula tuliopewa na Kabula.

“Vipi basi limeondoka?” nilimuuliza Eddy huku akili yangu ikiniambia kuwa tumeshaachwa na basi.

“Tuondoke haraka, kuna wanakijiji wanakuja huku wameshika mapanga na marungu,” Eddy aliniambia huku akigeuza shingo yake kuangalia kando kwa hofu, kisha akaanza kutimua mbio kuondoka eneo lile.

Sikusubiri tena, nilifunga haraka zipu ya suruali yangu na kuanza kuondoka haraka eneo lile huku nikijitahidi kufunga mkanda. Wakati huo Kabula alikuwa amejifunga mtandio wake na kuchukua ndoo yake kisha akaondoka haraka toka eneo lile.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom