Simulizi: Basi la shetani

Simulizi: Basi la shetani

the_legend

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2019
Posts
1,612
Reaction score
7,110
Basi la shetani: SEHEMU YA-01

Ulikua usiku wa kiza kinene katika jiji la Dar es salam, kutokana na uchache wa magari barabarani basi yale machache yaliendeshwa kwa kasi.
“Tumuache hapa hapa”
“Jomba angalia hapa wanajeshi wakitunasa, tutatafuta samaki nchi kavu”
“Hakuna kukamatwa tutafanya kazi kwa sekunde”
“Haina tabu basi achia mafuta kidogo”
“Sikilizeni vijana, mnaona pale kwenye yale matuta, gari itapunguza mwendo na hapo mtamtupa kupitia mlango wa kushoto, hakikisheni umakini unazingatiwa”.
Yalikua mazungumzo ndani ya gari aina ya Toyota Land cruiser, gari hiyo ilikua inatembea kwa kasi ndani ikiwa imembeba mwanamke mmoja aliyefungwa mikono na miguu kisha kuzibwa mdomo kwa gundi, macho yake yalikua mekundu kwa kutoa machozi, alikua akisali na kutupatupa mikono huku na huko lakini hakuonewa huruma hata kidogo, mipango iliyokua ikifanyika ya kumtupa barabarani alikua akiisikia lakini hakuwa na namna ya kujiokoa.
Gari ilianza kupunguza mwendo, hapo mwanamke huyo alizidi kujitahid angalau kuongea ili awaambie viajna waliotaka kumtupa basi wasimtupe kwa kishindo lakini hakuweza kutoa neno lolote.
Lilikua eneo hatari kwa kufanyia tukio lolote la kihalifu kwani kama ingetokea wanajeshi kukukuta katika eneo hilo maisha yako yangeweza kuwa hatarini ,
“Mwache hapo hapo karibu na geti” iikua sauti ya kiongozi wa kikundi hicho aliyeitwa Ribeto, na baada ya kutamka maneno hayo mwanamke huyo alitupwa mita chache kutoka lango kuu lakuingilia kambi kuu kuu ya jeshi Lugalo, baada ya hapo gari iliongeza mwendo mara tano zaidi ya ilivyokua mwanzo.
Baada ya mwanamke huyo kutupwa alibingirika na kutumbukia katika bonde dogo lililokua pembeni ya barabara , licha ya mwili wake kufungwa kwa kamba ulitoa harufu kali ya muozo, harufu hiyo ilipelekea mbwa kusogelea eneo hilo na kuzama shimoni, alijitahidi kurusha mikono lakini bado mbwa walizidi kumzingira wakidhani ni mzoga wa kitu,
“Mungu naamini utanisaidia na nitatoka nikiwa hai, naomba tuma malaika mlinzi wako aje kuniokoa mahali hapa” mwanamke huyo alijisemea moyoni, huku akiendelea kuwakemea kwa vitendo mbwa waliotaka kumvamia ndani ya bonde hilo.
Mbwa wenye mafunzo maalumu, walihisi hali ya hewa kuwa tofauti na ilivyozoeleka, haraka walianza kubweka, huku wakizunguka ovyo. Wanajeshi waliokua zamu ya kulinda usiku walichukua tahadhari, kila mmoja alikaa katika nafasi yake huku baadhi ya mbwa kuachiwa na moja kwa moja walitoka haraka hadi katika lango kuu, walisogea kidogo na kuzama ndani ya shimo.
Mwanamke alizidiwa na hofu baada ya kusikia vishindo vya mbwa wakubwa wakija huku wakibweka kwa nguvu, mbwa koko mwaliokua pembeni walikimbia,
“Mungu naomba unisamehe dhambi zangu na unipokee katika ufalme wa mbinguni” mwanamke huyo alikata tamaa na kujikuta anatulia baada ya mbwa mwenye ukubwa wa ndama kumdondokea kifuani, mbwa huyo alimnusanusa na ndipo mbwa huyo aliruka juu na haraka akarudi hadi alipo askari kiongozi na kumpa taarifa ya kuwa mtu aliyepo ndani ya shimo ana bomu la mkono.
Taarifa kutoka kwa mbwa huyo ilisababisha hali ya taharuki ndani ya kambi, hawakujua lengo la mtu huyo na hawakujua kama kuna wengine ambao wamewazunguka, haraka taarifa ilitumwa kwa mkuu wamajeshi kuhusu tukio hilo, huku mbwa mwingine akitumwa akiwa amefungwa kamera lengo likiwa kurudi na picha za mtu huyo na jinsi alivyojipanga.
Wanajeshi wote walipatwa na mshtuko, kuona ni mwanamke aliyefungwa mikono na miguuu huku bomu likifungwa mkononii ili atakapofunguliwa bomu lilipuke.
Bila kuchelewa wanajeshi maalumu wenye uzoefu wa kutegua mabomu waliitwa na kuenda kumtoa mwanamke huyo hapo bondeni,
“Wewe ni nani ?”
“naitwa Winny naomba msiniue”
“Umekujaje hapa?”
“Nimetupwa na watu ambao hata siwajui”
“Kwa nini umefungwa hivi kwani wewe ni mhalifu na kwa nini utupwe hapa”
“Japo sikumbuki vyote ila watu walionitupa hapa walikua na lengo la kuniua, hapa naomba mniokoe kuna bomu limetegwa hapa na pindi hii mikono yangu itakapofungulia basi litalipuka, naombeni niko chini ya miguu yenu niokoeni”.
Yalikua majibizano baina ya mwanajeshi mkuu wa zamu ya kulinda usiku na mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina Winny baada ya kufikishwa katika hospitali ya kijeshi ya Lugalo na kuondolewa gundi iliyomziba mdomo.
Winny alitetemeka kwa hofu, huku akizidi kuumia mkono kutokana na maumivu ya kamba iliyokua imekaza mikono yake, alianza kupewa matibabu ya haraka ikiwemo kuongezewa maji na chakula bomu likiwa mkononi na kutibiwa katika chumba cha pekee.
***
FIFTEEN YEARS AGO (miaka kumi na tano iliyopita)
Zilikua zimepita siku kumi na tano tangu Winny ahitimu elimu yake ya msingi akiwa na miaka kumi na nne, licha ya umri wake kuwa mdogo umbo lake liliwapagawisha wanaume, sura yake ilikua ya kung’aa alikua mweupe na mwembamba wa wastani. Makazi yao yalikua mitaa ya Survey karibu na chuo cha Ardhi, ili kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza alilazimika kujiunga na masomo ya kabla (Pre-form one) baba yake aliitwa Mazengo alihakikisha mwanaye anapata elimu iliyo bora akawa anahudhuria masomo katika kituo kilichofunguliwa karibu na soko la Mwenge, hivyo hakuona sababu ya kupanda usafiri kutokana na ukaribu uliokuwepo kutoka nyumbani hadi shuleni.
“Hi baby girl your so beautiful (mambo binti wewe ni mzuri sana)”, ilikua sauti nzito iliyotokea ndani ya gari dogo aina ya Toyota Mark II, alikua mwanaume mweusi na mnene kiasi, baada ya sauti hiyo kumfikia Winny alilazimika kugeuka na kumuona aliyetamka maneno hayo, Winny alipogeuka alikutana na tabasamu zito kutoka kwa mwanaume huyo na haraka mwanaume huyo alimuita kwa mkono , Winny aligeuka na kurudi,
“Mambo mrembo”,
“Powa shkamoo baba”
“Nawewe shikamoo mama”
“Hahaha marahaba baba”
“Unafika wapi nikusogeze”
“Wala usijali mimi naenda shule nakaribia kufika asante”
“Naomba nitafute kwa mawasiliano haya”.
Maongezi kati ya Winny na mwanaume hayo yalikatishwa na taa za barabani kuwaka kijani kuashiria kupita, lakini Winny alipokea kadi ya biashara (Busness Card) yenye nambari za simu.
Moyo wa Winny ulidunda kwa kasi kwani katika maisha yake yote hajawahi kukutana na mwanaume asiyemjua na atokee kumzoea hadi kuongea nae tena barabarani.
“Dr. Martin” ndilo jina lililokua katika kadi ya biashara ambayo alipokea Winny, aliificha mfukoni na kuongeza mwendo kwa lengo la kufika na kumuomba rafiki yake simu ili aweze kumpigia Dr Martin,
“Shoga leo nimepata na mimi wakwangu naona hapo nitapiga pesa kama wewe” lilikua neno la kwanza la Winny kabla ya salamu huku akipeana mkono na rafiki yake waliyekutana katika masomo ya Pre-form one,
“Sasa ulikua unazubaa nini wewe mtoto wa kike Mungu akupe nini, hapo utapiga hela tena daktari huyu wa Muhimbili, hapa utapiga hela shosti angu”, baada ya maongezi hayo waliingia darasani na masomo yakaanza.
Winny alikaa kiti cha nyuma mwisho, kichwa chake kikitawaliwa na mawazo juu ya mwanaume aliyeonekana kuwa na hela, alivuta picha ya maisha yatakavyokuwa pale atakapoanza kumiliki simu za kisasa pamoja na kutolewa out za mara kwa mara, maneno ya wazazi wake yalimtoka kabisa, hakujali utu wake zaidi aliwaza ni kwa jinsi gani ataweza kuwa sawa na wasichana wenzake aliowaona wakimiliki simu na vitu vya bei gali kwa kutumia uzuri ambao hata yeye alikua nao.
***
Dr.Martin alikua akiishi na virusi vya UKIMWI kwa mda mrefu, aliishi kwa kukomoa wanawake, hakutaka kufa peke yake, kwani wakati anatoa mawasiliano kwa Winny alikua akielekea Sinza katika hotel ya Lantana, akienda kukutana na mwanamke mwingine aliyekua akimsubiria chumbani.
“Mpenzi umechelewa sana, au umepitia kwa mwanamke mwingine jamani”,
“No (hapana) mpenzi foleni kidogo imenibana”
“Twende zetu basi dear, nilikua nakusubiri kwa hamu”.
Maongezi kati ya Dr.Martin na mwanamke mwingine aitwaye Dorice, waliingia chumbani kwa ajili ya kuenda kula raha,
“Mpenzi tutumie kinga basi” sauti ya kubembeleza kutoka kwa Dorice ilisikika,
“Dah jamani, kwani huniamini, au unaogopa mimba?” Dr.Martin alimuuliza taratibu
“Naogopa mimba kwa sababu sijajipanga kuzaa kwa sasa”, Dorice alijibu ingawa ukweli ni kwamba alikua akihofia kupata UKIMWI ila ujasiri wa kumwambia mtu anayekupa hela kuwa naogop UKIMWI ukawa haupo,
“Ukipata mimba mimi nitalea usijali, kwanza nakuoa kabisa” Dr. martin aliongea kwa sauti ya chini iliyopenya sikioni mwa Dorice. Dr.Martin hakuwa tayari kutumia kinga kwa mwanamke yeyote ili lengo lake litimie la kufa na wengi.
Huku wakiendelea kufanya mapenzi simu ya Martin iliita, na kwa kutumia mkono wa kushoto aliikamata na kupokea,
“Halo, mimi umenipa Busness Card asubuhi, nimetumia simu ya rafiki yangu maana mimi sina simu”
“Ahaa sasa kama huna simu basi subiri hapo hapo kwa rafiki yako namtumia hela ukanunue simu alafu unitafute na namba zako”
“Sawa asante sana”.
Yalikua maneno machache lakini yalimfanya Winny aamini kweli amepata mwanaume wa ukweli,
“Haaa! shosti unapewa simu hata hujatumika, usimuache huyo atakua amekupenda kweli”

“Ila shosti nikipata mimba baba ataniua”
“Wee thubutu kwani kondomu zimeisha dukani, yaani ukienda kwa mwanaume hakikisha unakua na kondomu zako maana hawa wanaume some time hawana maana, wanaweza kukumbia hana kondomu sasa kumkomesha unatoa zako”,
“Kweli shogaa hapo umenena”, maongezi yao yalikatika baada ya ujumbe wa fedha kuingia katika simu, haraka walikimbia duka la simu hapo hapo mwenge na kununua simu ndogo. Baada ya dakika tano Dr.Martin alipiga simu na kuongea na Winny,
“Winny tumia tu hiyo, tukionana nakupa simu kubwa, tuwasiliana hata kwa WhatsApp”,
“Waoooo, asante basi ngoja nisajili laini nitakutafuta”.

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-02

Kwa mara moja mawasiliano yalianza , Winny alianza kuwasiliana na Martin kwa uoga lakini kama mwanaume Martin aliendelea kumwondoa Winny hofu taratibu,
“Lakini shoga sio kwamba huyu mwanaume anataka tu kunichezea?” Ni swali ambalo Winny alimuuliza rafiki yake wa karibu ambaye ndiye alikua anazidi kumshawishi aweze kujiingiza katika mambo hayo ili aweze kujiingizia kipato,
“Sikiliza Winny, nikwambie ukweli hapa usitarajie huyo mwanaume kuwa atakuoa hapana, hata kama anakuambia anakuoa basi hapo anakudanganya tu, wewe cha kufanya ni kupiga tu pesa, kwanza kuolewa kitu gani bhana, wewe huoni ndoa zinavyowatesa watu, huu ni wakati wako wa kula pesa, wewe mwenyewe huoni umri wako ni mdogo?”
“Sawa Kemmy ila sasa huyu mwanaume anavyonisumbua tuonane, vipi niende tu hatanifanyia lolote? Maana amesema anataka nitoke nae tukatembee ili aweze kunipa na simu kama hiyo yako”
“Kwa kweli, Winny hapo jiandae tu mwanaume akikuita kwa staili hiyo kuna mawili, akuache au akulale, hivyo jiandae tu ili kama akikikutaka uwe tayari kumpa ili pia naye apate hamasa ya kuzidi kukupa pesa zaidi”,
“Dah! Hapo ni mtihani Kemmy unajua mimi sijawahi kabisa, sitaumia kweli na mkaka mwenyewe alivyo mkubwa, hataniua, naskia mara ya kwanza mtu anaumia sana”,
“Ahh wapi hakuna kuumia kivile wala hakuna mwanaume mkubwa mbele ya mwanamke, tena heri wewe unaanza mkubwa hivi, mimi nilianza nikiwa nasoma darasa la tano na nilikua natembea na mwalimu wangu wa hesabu ili anizidishie alama, siunajua mimi sijui hesabu, sasa hapo ndiye aliyeniingiza katika ulimwengu wa mapenzi nakumbuka nilikua na miaka kumi na mbili tu lakini mbona nilihimili na leo hii hadi naweza lala na wanaume wakubwa kuliko baba yangu.
“Dah nitajikaza basi jumamosi ijayo nitajitahidi nikamuone, ila sasa best nisaidie kitu kimoja,mimi hata sijui namna ya kumkamata mwanaume kisawasawa, sijui utanipaje ujanja, ili nihakikishe nampagawisha ipasavyo”
“Ahaa hapo usijali kabisa nitakusaidia utaweza sasa kesho inabidi tuondoke wote tuende kwangu mchana nikakufundishe kwa vitendo kabisa”,
“Powa Kemmy, mwalimu huyo” Maongezi kati ya Winny na Kemmy yalikatika baada ya mwalimu kuingia darasani na kuendelea na kipindi.
Kichwa cha Winny kilikua nje kabisa ya masomo yaliyokua yakitolewa mahali pale, alipiga picha ya wiki mbili zijazo alijiona mwanamke anayenza kupata fedha, alijiona na simu kubwa mkononi, alijiona akiwa Kariakoo katika maduka ya wahindi akinunua nguo za thamani pamoja na mapambo ya aina mbalimbali, alijikuta akipuuzia kauli za wazazi wake kuhusu kujitunza na kusoma kwa bidii kwa ajili ya maisha yake ya baadae.
***
Dr. Martin bado aliendelea na tabia ya kuwalaghai mabinti, alitumia kiasi kikubwa cha pesa, ili aweze kulala na mabinti wadogo ili kuhakikisha anakufa na watu wengi, kutokana na kufanya mapezi karibia kila siku alikua akitumia vidonge vya kusisimua mwili vijulikanavyo kama Viagra, alihakikisha kila baada ya siku mbili anakutana na mwanamke, alikula vyakula vyenye afya pamoja na vidonge vya ARV ili kupunguza makali ya virusi na kuendelea kupata afya iliyomfanya kutogundulika kwa macho, mvuto wake wa sura pamoja na nguvu ya pesa aliyotumia kwa wanawake ilimfanya kuzidi kuwapata kwa wingi.
***
Ilikua siku ya alhamisi mchana, siku mbili kabla ya Winny kwenda kuonana na Dr Martin, siku hiyo Winny hakuhudhuria masomo kabisa kwani alikua katika mafunzo ya kumpagawisha mwanaume, rafiki yake Kemmy alikua akimsubiri nyumbani kwao baada ya wazazi wake kuenda kazini.
“Karibu shosti”Kemmy alimkaribisha Winny nyumbani na moja kwa moja walielekea chumbani,
“Shosti kwanza hapo kwenye chupi umekosea, kwa mwanaume inabidi uende na chupi nyeupe au ya pinki, ili uonekane msafi na kuvutia zaidi, hii nyeusi leo iwe mwisho wa kuivaa, lilikua neno la kwanza kutoka kwa Kemmy alipomvua Winny nguo kwa ajili ya kumfundisha,
“Haa, best sasa huoni mwenziio ningeenda kuaibika? Haya twende kazi mama”Winny alijibu huku akitabasamu kwa aibu kwani alikua akivua ngio mbele ya rafiki yake,
“Winny wewe mzuri eti, maziwa yako yenyewe yatammaliza jamaa, yamechongoka vizuri sana, alafu weupe wako ndio kabisa sumu kwa wanaume weusi kwani hupenda sana wanawake weupe hivyo hapo tayari umeshashinda katika muoenekano”,Kemmy alikua akitoa somo kwa makini zaidi,
“Sasa kwa mfano ndio naingia chumbani kwa mwanaume nitaanzaje”, Winny aliuliza swali na bila kuchelewa alijibiwa kwa matendo kwani Kemmy alimfuata na kumfundisha jinsi ya kumkiss mtu,
“Kwanza unamsogelelea hivi unamshika kifuani kama ni mrefu sana unamhimiza ajilaze kitandani ili uweze kumbusu vizuri, unaanza kwa kumbusu katika paji la uso, hapo atakuheshimu sana kwani wanawake wengi hawana tabia ya kumbusu mwanaume katika paji la uso, kisha utashuka na kumbusu mdomoni na hapo utamlambalamba lips zake, huku ukipenyeza ulimi wako mdomoni kwake taratibu mkono mmoja utakua unamapapasa tumboni taratibu, hapo utamuona akiguna tu taratibu, sasa hapo ukitaka busu liwe tamu kabisa, kuwa kama unapenyeza mate kidogo hakikisha yanamuingia mdomoni, utaona akitaka kuyapata zaidi na hapo zidisha utundu, panua mdomo wako hakikisha anaukamata ulimia wako na kuunyonya kisawasawa, hapo atapata msisimko wa ajabu, kisha penyeza na kuuzungusha kinywani mwake na mkono mmoja upenyeze ndani ya suruali, mchezee sehemu zake kwa ustadi kama hivi”, Kemmy alikua akimuelekeza Winny kwa matendo, pale chumbani palikua padogo kwani Winny alijikuta akipatwa na hisia za ajabu,
“ Hebu nifanyie kisl kitu”Winny aliongea kwa sauti ndogo huku akimvuta Kemmy aliyekua amejilaza kifuani mwake, bila kutarajia walijikuta wakisagana pale chumbani,
“Siku ingizii chochote ili huyo mwanaume akukute bikra pia Winny usijali sana maana kawaida ya mwanaume wa kawaida anatumia tu dakika 15 hutaumia tena maana uume wake unalala na wewe utapumzika kidogo”,Kemmy alimjibu Winny baada ya kutaka kuingiziwa angalau tango pamoja na kumtoa hofu kuhusu mwanaume kumwingilia kwa mda mrefu lakini hakujua kama Martin hutumia dwa ambazo humfanya awe na nguvu ya kufanya mapenzi kwa dakika zaidi ya hamsini bila kupumzika.
Mda ambao masomo ya kina Winny huisha, Winny alitoka huku akiitamani sana siku ya jumamosi ifike ili akaanze rasmi kuutumia mwili wake kwa ajili ya kujipatia kipato.
***
“Mwanangu vipi masomo ya sekondari unayaonaje?” Mama Winny alimuuliza mwanae aliporejea nyumani lakini lilikua swali la mtego baada ya kumuona Winny akiwa katika hali tofauti na aliyomzoea,
“Wala mama sio magumu wala marahisi kivile ila najitahidi mama”, Winny alijibu huku akiinamisha kichwa chini kwa aibu ya mambo aliyokua ametoka kuyafanya na rafiki yake,
“Sawa mwanangu, pambana sana siunamuona baba yako anavyopambana ili wewe usome kwa amani, naomba usimwangushe baaba yako sawa mwanangu mzuri?” mama Winny alimaliza kwa kumkaribisha mwanaye ndani, Winny aliingia moja kwa moja hadi ndani na kubadili nguo,
“Mfyuuuu, ungepambana wewe ungekua hata sahivi ni mwalimu wa msingi, acha mwanamke nile maisha”, Winny alijisemea kimoyomoyo huku akivua nguo na kujingalia katika kioo jinsi mwili wake ulivyoumbika.
***
Jumamosi asubuhi na mapema Winny alijiandaa na shule kama kawaida,
“Mama naomba basi nikiwahi kutoka shule niende hata Karikoo na rafiki yangu nikayape macho furaha” Winny alimuomba mama yake ruhusa lakini kutokana na mama kumpenda mwanaye basi alimruhusu,
“Sawa mwanangu, ila uwe makini na uwahi kurudi nyumbani kabla baba hajarudi”, alijibu mama Winny,
“Asante mama nitawahi”, Winny alitamka huku akiondoka na mkoba wake uliobeba madaftari pamoja na nguo za kubadilisha. Alifanya mawasiliano na rafiki yake na haraka alielekea hadi nyumbani kwake ili aweze kubadili nguo.
“Nipo makumbusho sasa siunajua sitaki kuonekana kabisa”, Winny alimtumia Martin ujumbe mfupi,
“Sawa hebu nakutumia hela kwenye simu utolee hapo kituoni ukodi bajaji ikulete hadi hoteli moja hapa Kinondoni, inayoitwa Butterfly,”Martin alijibu kiha baada ya dakika tano tayari elfu thelathini iliingia katika simu ya Winny,
“Mambo si ndio haya sasa”, alijisemea Winny huku akimuonesha Kemmy ujumbe huo wa pesa,
“Sawa mama nenda kapambane ila unikumbuke mimi mwalimu wako”, Kemmy aliongea huku akicheka
“Sawa mama nenda basi wewe shule na huu mkoba wangu tutawasiliana nikitoka huku niendako” Winny aliongea huku akimkabidhi Kemmy mkoba wenye madaftari pamoja na nguo alizotoka nazo nyumbani,
“Okey, all the best ( sawa kila la kheri ) hizo kondom uhakikishe unatumia”, maongezi yaliishia hapo na Winny aliiita bajabi na kupanda na kumwelekeza dereva sehemu ambayo alitaka kufika huku Kemmy akirudi shule.
“Ukifika Kinondoni studio uniambie” Ulikua ujumbe mfupi ulioingia katika simu ya Winny ukitoka kwa Martin kusudi la ujumbe huo lilikua ni Martin kuweza kujua mda kamili wa kumeza vidonge vya kusisimua mwili ili viweze kukaa ndani ya mwili nusu saa kusudi kufanya kazi vizuri, ndani ya chumba alikua na chupa ya Saint Anna,
“Kweli pesa ni kila kitu”, alijisema Martin huku akimeza kidonge kimoja baada ya Winny kumpa taarifa ya kufika Kinondoni studio,
“Okey mamii karibu sana nakusubiri kwa hamu” Martin alijibu ujumbe huo huku akinywa Wine yake taratibu,.

je nini kitatokea??

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA 03

Moja kwa Moja Kemmy alirudi masomoni huku kichwa chake kikimuwaza Winny,
“Leo ataonja joto la jiwe, anafikiri kupendeza hapa mjini ni kitu cha mchezo lazima mwanamke uteseka, uchane msamba miguu iunde nyuzi 180” alijisemea Kemmy wakati masomo yakiendelea.
***
katika hali ya kushtukiza, bajaji ambayo Winny alipanda ilipata ajali mita hamsini kutoka ilipo Geust ya Buterfly, ajali hiyo ilisababishwa na lori lililopoteza mwelekeo na kutaka kuigonga bajaji, hapo ndipo dereva bajaji alifanya juhudi kukwepa lori hilo na kuingia mtaroni, Winny alipoteza fahamu kutokana na mshtuko lakini hakupata jeraha lolote na pia dereva alitoka mzima kabisa.
Hapakua na mda wa kupoteza, Winny alibebwa kwa haraka hadi hospital ya Mwananyamala,
“Huyu dada alikua anaenda wapi ?” dereva bajaji aliulizwa swali ambalo hakujua alijibu vipi,
“Sijajua alikua anaeda wapi ila alikua anawasialiana na mtu kwenye simu, hivyo mimi nilikua naelekezwa tu kuwa kunja kushoto mara ingia kulia hadi hapa tulipopata ajali sikujua lengo lake lilikua kuenda wapi” dereva bajaji aliongea uongo wa kumlinda Winny kwani alitumia uzoefu wa kazi yake ya kulinda mteja asijulikane kama alikua anaenda kutoa mapenzi.
***
Kemmy akiwa darasani aliskia simu yake ikiita kwa mtetemeko ndani ya mkoba,
“Atakua tu Winny huyu” alijisemea huku akipenyeza mkono ndani ya pochi na kuchungulia kwa mbali, alishangaa kuona namba ya Dr.Martin
“Kuna nini tena?” alijiuliza kimoyomoyo huku akitoka nje kwa kisingizio cha kwenda kujisaidia, aliingia chooni na kuitoa simu mfukoni na kuanza kuongea na Martin,
“Abee shem wangu wa ukweli” sauti nyepesi ilipenya masikioni kwa Dr.Martin
“Naam shem, unaendeleaje” Martin ane aliitikia
“Naendelea vizuri shem wangu, nambie”, Kemmy aliongea kwa sauti ya kulegea sauti iliyomfanya Martin azidi kupagawa na hisia kupanda zaidi kutokana na dawa alizotumia kisha Winny kutotokea,
“Naendelea vizuri kabisa lakini wifi yako nimepanga nae kitu lakini kaniruka, kuna mahali nimemuambia anione lakini hadi sasa hivi namsubiri hajafika na hata simu yake haipatikani , sijui kwa nini kaamua kunifanyia hivi, naomba kama uko nayeye hapo nisaidie kumwambia aje tafadhali, nitampa chochote atakachohitaji” Martin aliongea kwa kwa sauti ya kutetemeka, dawa alizotumia zilimfanya ashindwe kutulia kitandani, alijizungusha zungusha ovyo,
“Haa! Shem mbona wifi yangu anakupeda hivyo hawezi kukufanyia ubaya, kweli yule ananiambia amekupenda kupita maelezo, na ukweli nikuambie asubuhi hii nimeachana na ameniambia anakuja mahali mlipoambiana mkutane, na mimi nikafikiri ameshafika sahivi” Kemmy aliongea kwa mshangao mkubwa, hakuamini maneno ya Martin kuhusu Winny,
“Kweli hajafika na simu yake haipatikani, sasa ya nini nikudanganye shem” Martin aliziidi kutoa msisitizo.
“Kwa hiyo itakuaje shem”, Kemmy alizidi kutoa sauti ya kulegea na kuzidi kumchanganya Martin
“Shem, najua wewe ni mwanamke na unaelewa mambo ya hisia pale unapopanga na mtu, kukutana kimwili alafu uwe umeshafika eneo la tukio na mwenzako asitokee, najua inauma, sasa naomba nionane na wewe kama hutojali”, Martin aliongea maneno ambayo yalimchanganya Kemmy,
“Jamani shem mimi naogopa maana wifi angu akijua ataumi sana” Kemmy aliongea lakini moyoni akiifurahia nafasi hiyo,
“Hawezi kujua maana tunakutana kwa siri nayeye hata sitaki kumsikia tena”Martin alizidi kuongea na Kemmy na hatimaye Kemmy alikubali kuenda hadi katika chumba alichokodi ili waweze kukutana,
“Hapa mdipo Winny amepoteza mume namchukua moja kwa moja huyu” alijisemea Kemmy akiwa njiani kwani shule alisingizia kuwa na tatizo la ghafla nyumbani.
***
CHUO KIKUU DAR ES SALAM (UDSM)
Kulikua na kijana mmoja anayeitwa Edson, hakika alikua kijana mwerevu na aliaminika na kila mtu pale chuoni na hiyo ilitokana na kuwa na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo, alikua akisomea sheria mwaka wa pili , licha ya kuwa anasoma kila siku alikua akiwaza ni kwa jinsi gani ataweza kuwa tajiri tena bilionare namba moja Tanzania,
“Hivi navyosomea hii sheria itaniwezesha kuwa tajiri namba moja Tanzania kwa miaka ijayo?” lilikua swali lake la mara kwa mara, kila siku alibuni mbinu ya kutafuta hela, alijaribu biashara mbalimbali lakini nyingi zilishindikana na baada ya mda mrefu aliweza kubuni mbinu ambayo aliamini ndiyo itakua mwisho wa matatizo yake.
Baada ya kufanya uchungzui wa kutosha basi alitafuta vijana kumi na saba, pamoja nayeye kisha wakafanya kikao cha siri.Kilikua kikao ambacho kiliwapa wote motisha wa wakuwa mabilionare wa miaka ijayo kikubwa kilichozingatiwa ni usiri wa hali ya juu, kila mtu aliapa kutomwambia mtu wa nje kitu kilichokua kikiendelea. Lengo la Edson kusisitiza suala la usiri hakuna aliyelitambua hata mmoja, hivyo walipanga siku ya kikao huku Edson akiwa kiongozi na kuupa huo mpango wao jina EDSON PROJECT.
“Wazee naomba hii kitu kiwe siri kubwa nataka niwafundishe namna ya kuwa matajiri, naomba hii siri isifike hata kwa mtu mmoja nje ya hapa tutakachokiongea kwenye kikao nataka kionekane kwa vitendo yaani watu watuone tukiendesha magari hapa chuoni na tuwe na biashara nyingi hapa mjini hivyo hakuna hata kuwaambia mademu hapa ni kimya kimya” Edson aliongea kwa msisitizo huku wakiahidiana kuitunza siri hiyo,
“Kesho basi nitawawekea wazi mpango mzima, lazima tupige hela”, aliongea Edson,
“Sawa mkurugenzi tunakuaminia kwa mipango” wote walijibu na kuagana kila mmoja akiwa na hamu ya kujua mpango wa kesho.
***
Winny alishtuka baada ya dakika kumi na tano na kujikuta yupo wodini,
“Hapa ni wapi ?” aliuliza Winny
“Hapa ni hospitali ya Mwananyamala, ulipata mshtuko kidogo ukapoteza fahamu, sijui unakumbuka ulipokua umetoka na ulipokua unaenda?” aliongea daktari aliyekua pembeni yake, alikua kijana wa kiume,
“Mungu wangu! Kaka angu nakuomba tu nitoe hapa haraka na iwe siri mama yangu akijua nilipo ataniuwa, niliaga naenda shule sasa hapa siri itafichuka, naomba tu nitoe bila taarifa kuvuja”, Winny alijikuta akiongea kila kitu mbele ya yule daktari,
“Utanipa nini kama nikikufanyia hayo?” daktari huyo alimuuliza Winny swali la mtego,
“Chochote utakachohitaji nitakupa mradi kwangu wasijue,andika namba yangu ya simu wewe nitoe hapa alafu tuwasiliane” Winny aliongea kisha wakafanya utaratibu wa kubadilishana namba za simu, hapo daktari alimtoa Winny kimya kimya bila uongozi wa hospitali hiyo kujua, Winny aliangalia ndani ya mkoba wake na kutoa simu yake,
“Kumbe hadi ilizima” alijisemea Winny huku akiiwasha simu yake, na mtu wa kwanza kumtafuta ni Kemmy ali aweze kumuuliza kilichotokea, alipiga simu ya Kemmy kwa mara tatu bila kupokelewa,
“Atakua darasani ama wapi mbona hapokei simu, ngoja niende moja kwa moja kule Buterfly nakumbuka alinambia yupo chumba namba 104” alijisemea Winny huku akiita bodaboda ambayo ndiyo ingemfikisha kwa haraka.
***
Dr.Martin hakuamini macho wala mwili wake pale Kemmy alipoingia chumbani,
“Oooh, Shem nataka nikupe vitu adimu ambavyo hujawahi kuvipata”, Kemmy alimwambia Martin wakati akimsogelea kitandani,
“Usiniite shem bhana niite mpenzi, ila ukiwa na wifi yako ndio uniite shem”, alijibu Martin huku akiendelea kuuficha uume wake uliosimama imara ndani ya suruali yake, aliamini kama Kemmy angeona ukubwa wake angeogopa lakini alishangaa kumuona mtoto huyo akifanya vitu ambavyo hakuwahi kukutana navyo, hakika ilikua siku ya kwanza kwa Martin kufanyiwa vitu alivyofanyiwa na Kemmy , vilikua vitu adimu ambavyo mwanaume yeyote atakayevipata basi ni ngumu kumsahau mwanamke huyo,
“Kama ningekua nna mke leo talaka ingemhusu”, Martin alijikuta akisema kwa sauti, aliamini Kemmy ndiye mwanamke pekee anayejua mapenzi dunia nzima, waliendelea kuchezeana kitandani, Kemmy alijituma kisawasawa kitandani hapo kabla ya kuanza tendo kabisa.
***
Winny alishuka kwenye bodaboda na haraka alipiga hatua kwa haraka hadi alipouona mlango wa chumba namba 104, moyo ulimdunda kwa kasi,
“Ngoja kwanza nimpigie simu” alijisemea Winny huku akitoa simu yake katika mkoba ili aweze kumpigia Dr. Martin,
“Dah! hata hapokei ila ngoja nigonge tu maana alinambia nikija niingie tu moja kwa moja” alijisema Winny huku akisogea karibu zaidi mlangoni.
***
“Dear it’s time now (mpendwa huu ni muda sasa wa kunifaidi)” aliongea Kemmy baada ya kuona yupo sawa kwa ajili ya tendo kamili lakini ghafla wote walishtuka mlango kugongwa,
“ngo, ngo, ngo”, Mlango uligongwa kwa kishindo,
“Nini tena mpenzi” Martin aliongea sauti ya chini huku akishangaa,
“Nikuulize wewe”, alijibu Kemmy huku akijitoa kifuani kwa Martin.
Mlango ulizidi kugongwa mfululizo na Martin alisimama kuelekea mlangoni huku akinyata lengo lake likiwa ni kusogeza pazia na kuangalia anayegonga ni nani..

Je nini kitatokea ? Endelea kufuatilia

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-04

“Oooh my God (Oooh Mungu wangu) ni Winny” yalikua maneno ya Martin baada ya kupenyeza jicho katika dirisha, maneno hayo yaliichanganya akili ya Kemmy,
“So what (kwahiyo ?)” Kemmy aliuliza huku akiwa anavaa nguo haraka haraka, , hakutaka rafiki ake wa karibu aone akimgeuka,
“Usijali ngoja nitumie akili za kiume” Martin aliongea huku akiifuata simu yake na kumtumia Winny ujumbe mfupi,
“Mpenzi nimekusubiri kwa mda hujafika sasa nimetoka kidogo na nitarudi baaada ya nusu saa, kwa hiyo tafadhali nenda kanisubiri hoteli ya pembeni hapo nikija nitakutafuta ila uwahi kuja, nakupenda mpenzi”, yalikua maneno machache na Winny alipomaliza kuyasoma alishtuka kuona ujumbe wa fedha, hakuamini macho yake kwa kile kilichokua kikiendelea,
“Yaani huyu ndiye mwanaume, hata hajalala na mimi ananipa pesa kiasi hiki ? asante Mungu kwa yote haya”, alijisema Winny huku akielekea Hotel iliyokua mita hamsini kutoka eneo hilo, na baada ya hapo Martin na Winny walipata nafasi ya kuendelea kufanya mapenzi, Kemmy, hakuwahi kukutana na mwanaume kama Martin, alihimili mapenzi kwa mda mrefu bila kuchoka, Kemmy alikua akiguna kwa raha alizokua akipata, huku nayeye Martin akipata raha ya kipekee ambayo hakuwahi kuipata tangu aanze kujihusisha na mapenzi.
Baada ya dakika 45 Kemmy alikua amechubuka uke wake damu ilikua ikimtoka kwa mbali lakini bado Martin aliendelea na mchezo, Kemmy alijikaza kwani alimini atapewa kiasi kikubwa cha pesa.
“Kwa huyu inatosha ngoja sasa nimuite mwenzake” alijisemea Martin kimoyomoyo kwani hakuwa tayari kulikosa pia penzi la Winny.
“Hakika nimefurahia sana mchezo wako, sasa nataka kumuita wifi yako nachokuomba ni kuwa msiri, nakupa hizi dola 200 zitakusaidia” aliongea Martin huku akimkabidhi Kemmy dola mia mbili ambazo ni zaidii ya laki nne za kitanzania, ilikua mara ya kwanza Kemmy kulala na mwanaume na kukabidhiwa kiasi kikubwa kama hicho,
“Jamani nashukuru sana, ila umeonaje mziki wangu?” Kemmy aliongea kwa mahaba huku akimkumbatia Martin,
“Hakika wewe ni mtamu na fundi hasa, natamani niwe nakutafuta kila napokukumbuka”, alijibu Martin huku akitabasamu,
“Wewe tu ukiamua nitafute ila siri yetu maana rafiki angu huyu ana mdomo balaa, tufanye kwa siri asijue chochote”, Kemmy alijibu na kumpa Martin uhuru wa kumtafuta mda wowote atakapomhitaji.Hawakupoteza mda waliingia bafuni na kuoga huku bado Martin akiwa na hamu ya tendo kwani dawa alizotumia bado zilimsisimua mwili ipasavyo,
“Huyu Winny hapa atalia kama mtoto mdogo”Kemmy alijisemea baada ya kuangalia maumbile ya Martin yalivyosimama imara.
***
Dakika kumi baada ya Kemmy kuondoka tayari Winny nae alikua chumbani pale, aliingiwa na hofu lakini alijikaza, alianza kufanya yale ambayo alifundishwa na Kemmy, alijitumja ipasavyo kumpagawisha Martin, na kwa kuwa Martin alikua ameshapunguzwa nguvu kidogo basi Winny hakupata wakati mgumu sana, lakini kila alipoingiza mkono wake na kumpapasa Martin katika sehemu za siri alishtuka kwa kuona ana maumbile makubwa,
“Ah nitayashinda tu haya”, Winny alkijipa moyo na mara moja Martin aligundua Winny kua hajawahi kulala na mwanaume, hapo alianza kumwondoa wasiwasi huku akimlaza chali, alimshikilia mikono yale ipasavyo na kumtanua miguu,
“Hapa nataka nipeleke moto mmoja tu, nifumue kila kitu” Martin alijisemea kimoyomoyo huku akimchezea Winny juu juu, Winny alikua akipata raha isiyo na kifani lakini alishtukia kupata maumivu ya hali ya juu huku damu ikimtoka, alipiga kelele lakini Martin aliwahi na kumziba mdomo, alijitahidi kumsukuma lakini alizidiwa nguvu,, hakuwa na lakufanya alijikaza kisabuni na kumuacha Martin afanye analolijua.
“Ina maana nazaa au” alijiuliza Winny baada ya kuona maumivu anayopata ni kama vile anavyosimuliwa mtu anavyozaa mtoto.
Baada ya dakika arobaini na tano, ndipo Martin alimwachia Wiinny, huku damu ikiwa imetapakaa mwilini,
“Mpenzi hata siwezi kutembea”, Winny alisema huku akijikaza kwani hata kusimama ilikua tatizo, hakuweza kubana miguu kama kawaida,
“Jikaze tu utazoea”aliongea Martin huku akimpeleka bafuni na wakaoga.
Kwa shida Winny alijifuta vizuri na kuvaa nguo,
“nikupe zawadi gani mpenzi” Martin alimuuliza Winny baada ya kumaliza kujipaka mafuta,
“Nipe zawadi yoyote unayoona inanifaa wewe”, Winny alijibu kwa tabasamu,
“Basi chukua hii”, Martin aliongea huku akimkabidhi bahasha ndogo, ndani ilivimba lakini Winny alishindwa kuvumilia, aliifungua ndani na kuangali zawadi iliyokua ndani, alifiurahi kukutana na simu nzuri aina ya Iphone inayotengenezwa na kampuni ya Apple, hakika alifurahi sana ,
“Chukua na hii pesa ya vocha” Martin alizidi kumpagawisha Winny baada ya kumkabidhi kiasi cha shilingi dola mia tatu, ambazo ni zaidi ya laki sita za kitanzania,
“Mungu anipe nini ?” Winny alitamka kwa sauti huku akimkumbatia Martin.
Baada ya kuagana kila mtu alitawanyika, Winny alipiga simu ya Kemmy na mara moja wakapanga wakutanane nyumbani kwa Kemmy.
“Shogaa, Mungu anipe nini?” liliku neno la kwanza kutoka mdomoni kwa Winny baada ya kuonana na Kemmy,
“Kulikoni shosti na wewe basi jikaze hiyo miguu unaitanua kama bata, watakushtukia home” Kemmy nae alijibu huku akitabasamu
“Yaani hapa ndio nimejikaza hadi mwisho”, Winny alijibu huku wakiingia ndani,Kemmy hakuonesha dalili yoyote ya kitu alichofanya na Martin wakati Winny akielezea kila kitu kilichotokea na vitu alivyopewa,
“Sasa shosti hapo usifanye kosa, yaani mshikilie na umlinde kama mboni ya jicho”. Waliongea mengi na mwishoni waliagana huku Winny akimkabidhi Kemmy dola mia moja kama shukrani ya kumfundisha.
***
Winny alifika nyumbani akiwa na hali ya uchovu, mama yake hakua na imani kuwa mwanaye ametoka sehemu salama, aliangalia mwendo wake alioingia nao nyumbani alihisi kuna kitu kimetokea ila hakuuliza chochote,
“Mama leo naumwa kidogo kichwa”Winny alimdanganya mama yake
“Usijali mwanangu ni mizunguko ya mjini ndiyo imechangia, kunywa maji mengi tu” mama Winny alijibu huku akiangali chini kwa aibu kwani alijua mwanaye tayari ameshaaza kukutana na wanaume,
“Nikimwambia baba yake atauwawa bure huyu acha nimtunzie hii siri”, mama Winny alijisemea moyoni.
***
Edson na kikundi chake walitumiana ujumbe wa kukutana katika chumba kimoja, walianza kikao huku mzungumzaji mkuu akiwa ni Edson, na suala lenyewe lilikua kuhusu mchezo wa bahati nasibu, aliwashauri wenzake wajiunge pamoja ili waweze kushinda michezo hiyo ya bahati nasibu katika kubashiri matokeo ya mpira wa miguu iliyoshika kasi hasa kwa vijana wa wakiume,
“Jamani hii EDSON PROJECT ina nia ya kushinda michezo ya JACKPOT ili tuiweze kupata fedha nyingi zaidi, hivyo basi tukiwa watu kumi na saba tutakua tunachangia kila mmoja shilingi mia mia na kila mmoja anachambua timu moja na baaye tunaziunagnisha pamoja na tunalipia kwa kutumia namba yangu kama kiongozi wenu ili tukishinda basi tugawane pesa, hebu fikirieni tukishinda million mita tano kila mmoja atapata zaidi ya million 40 je hazitatosha kabisa ili na sisi tuendelee kucheza zaidi ?” Edson aliongea mengi ambayo wenzake waliyafurahia na walijiona wakiwa matajiri,
“Kweli umoja ni nguvu utengano niudhaifu” alijisema mwanafunzi mmoja huku akiamini kama kila mmoja akichambua timu moja na kuibashiri basi ni rahisi zaidi kuliko mtu mmoja kuchambua michezo kumi na saba. Wote walikubaliana na kuifanya ile kuwa siri, Edson alizidi kuwaisistiza kuhusu kuitunza siri hiyo na ili wengine wasiige basi wote walikubali kuifanya iwe siri lakini bado hawakujua lengo la Edson kusisitiza swala la kutunza siri.Haraka kila mmoja alipewa timu yake ambayo ni ya siku ijayo, kila mmoja aliichunguza timu yake, aliangalia michezo ya timu husika iliyokwishachezwa, aliangali idadi ya michezo iliyowahi kushinda na hadi waliangalia kikosi kitakachocheza, waliingia katika mtandao wa Google na kuisoma timu husika, kila mmoja alijitahidi kuchambua timu yake, hakuna aliyekumbuka kusoma tena kwa siku hiyo , wazo la Edson liliwapa motisha wa kuwa matajiri ghafla tena kwa mtaji wa shilingi mia moja..

je nini kitaendelea

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-05

Hadi kufikia miezi miwili tayari Winny alikua ashazoea kufanya mapenzi hadi mara tano kwa wiki, tabia yake nyumbani ilibadilika sana, hakuwaheshimu tena wazazi kama zamani licha ya matokeo ya kujiunga na kidato cha kwanza kutoka hakuonesha utayari wa kujiunga na shule tena, kwa wiki alikua na uhakika wa kujiingizia zaidi ya laki tano kutoka kwa wanaume tofauti tofauti waliomtaka kimapenzi.
Kemmy pia alibadilika tabia, hadi nyumbani alihama na kuishi katika chumba alichopangishiwa na mwanaume maeneo ya Sinza Afrikasana.
Mama na baba Winny hawakuamini kilichokua kikiendelea,
“Ni kweli huyu mtoto wetu wa pekee amepotea hivi hivi, tukiwa tunaona? Ila yote haya nilikuambia mama Winny, unamdekeza mtoto, alikua anakuletea hela unapokea tu hujui anakozitoa, uliona anamilikiua simu za kisasa hukuuliza kwa kuwa alikua anakupa kitu kidogo, ona sasa hataki shule na hata ameanza kutuaibisha kwa kurudi nyumbani akiwa amelewa”, baba Winny aliongea huku machozi yakimtoka,
“Baba Winny usiseme tena hivyo acha kunihukumu mimi, kumbuka huyu mtoto ilitupasa sisi wote tumkuze katika maadili mema, na sio tu kumuonya bali kumfundisha, ni ngumu sana kumuambia mtoto wa kike kuwa ngono ni mbaya wakati akikaa na wenzake wanamwelezea jinsi ngono ilivyotamu, hivyo ilipaswa kumwelewesha uchungu ulio ndani ya utamu wa mapenzi,”Mama Winny alijibu huku akimfuta mumewe machozi,
“Sasa ona hadi saa sita hii usiku bado mtoto hajarudi, ni aibu kumsubiri binti wa miaka kumi na nne hadi usiku huu wa manane” baba Winny aliongea kwa hasira lakini kabla hawajaendelea mlango ulibishwa,
“Muuuuuuuuuumy” ilikua sauti ya Winny,
“Abeeee mwanangu” mama Winny alijibu kwa sauti ya huruma kwani alijua ni dhahiri mwanaye kwa mda huo alikua mlevi,
“Rudi huko huko pumbavu wewe”, baba yake alifoka lakini tayari mama alikua ashaufungua mlango na Winny kuingia, alikua akipepesuka, viatu alishikilia na mikono na moja kwa kwa moja alipita hadi chumbani, na kujitupa kitandani, ilikua kazi ya mama yake kumshushia chandarua na hadi wakati mwimgine alimywesha maji, waliamini mtoto wao amelogwa.
***
Martin bado aliendelea kutembea na Winny pamoja na Kemmy bila wote kujuana, Winny alijisifu kwa Kemmy jinsi ambavyo Martin anavyompa kiasi kikubwa cha pesa kila wanapokutana, Kemmy alihakikisha anatunza siri ya kutoka na Martin kama walivyopanga kwani hakuna kitu alichohitaji akakosa.
Siku moja moja Kemmy na Winny walikua wakifanya mazoezi ya kuwateka wanaume, walikua wanaangalia mikanda ya ngono kisha kujaribu pamoja kama sehemu ya majaribio, yote hayo waliyafanya ili kuzidi kuwa tofauti kwa mwanaume yeyote ambaye wangekutana naye,
“Hivi Winny huyo Martin kweli ni daktari au vipi maana kama ni daktari mbona hatujawahi kumuona akienda kazini, na kila siku anakua na pesa, itakua ana kazi nyingine ama”, lilikua swali gumu kwa Winny,
“Ah mwenzako mimi sihitaji kujua kazi gani anafanya ilimradi Napata pesa mimi” alijibu Winny kwa mkato.
***
EDSON PROJECT ikiongozwa na Edson mwenyewe bado iliendelea na utabiri wake, hawakukata tamaa licha ya kukaa zaidi ya miezi miwili na nusu bila kushinda, kila siku waliongea ufanisi katika kutabiri,
“Michezo ya mwisho wa wiki hii ni milaini kidogo hapo tujikaze masela” alisema Edson baada ya kukagua michezo ambayo ingechezwa mwisho wa wiki, na kama ilivyo kawaida ya wanaume kutunza siri hadi wakati huo hakuna hata mmoja aliyetoa siri hiyo kwa mtu mwingine.
***
Ili Winny kuepuka kero za nyumbani basi aliamua kuondoka nyumbani na kuenda kupanga nyumba jirani na Kemmy, suala la kujilipia kodi lilikua dogo, kila siku vijana wa chuo jijini Dar es salaam walipishana mlangoni kwa Winny, alijiremba kiasi kwamba kila mwanaume aliyemuona lazima angemtaka, machoni hakuonekana kama anajiuza na kila mwanaume aliyekua naye basi mwanaume huyo aliamini amepata binti mdogo wa malengo yake,
“ Hakika kama ameweza kunikubali basi huyu ananipenda kweli sitamuacha” yalikua maneno ya kila mwanaume aliyakutana na Winny, na hayo maneno yalitokana na jinsi Winny alivyowaigizia upendo wa kweli.
***
Edson na wenzake walikua katika chumba kimoja, wote wakiwa na simu zao walikua wakifuatilia matokeo ya michezo waliyotabiri kupitia LIVE SCORE,
“Bado hii timu moja tu inayochezwa saa tano usiku” alisema Edson, wote walikua wakishangilia, waligongeshana mikono huku kila mmoja akimsifu Edson kwa ubunifu wake, walipiga magoti na kumuomba Mungu ili matokeo ya timu ambayo ilisubiriwa yawe kama walivyotabiri,
“Wazee hii million mia sita ni yetu” hakuna aliyelala wote walikaa macho hadi pale mchezo ulipoanza, hakika mchezo ulianza kwa kasi ya ajabu, timu waliyoitabiria kushinda ilikua ikishambuliwa vilivyo,walianza kupoteza matumaini,
“Yaani huyu anakoswa koswa hivi ataweza kushinda kweli”Lilikua neno la Edson baaada ya timu kwenda mapumziko zikiwa sare ya kutofungana,
“Boss ungetuletea hata pombe tuondoe stress”, alisema mmojawapo wa vijana hao na hapo hapo Edson alitoka na kurudi na chupa tano kubwa za K-vant, kila mmoja alimiminiwa na wakaanza kunywa taratibu.
Moyo wa Edson ulijawa na furaha kwani aliamini mipango yake itatimia kirahisi hasa baada ya kuona wenzake wanatumia pombe huku yeye akidai kushikilia chupa yake mkononi,
“ Hii ni yangu mwenyewe hadi niimalize” alijisemea Edson lakini ukweli ni kuwa ndani ya chupa yake kulijazwa maji lakini yeye aliigiza kulewa, lakini wenzake wakilewa kweli.
hadi kufika dakika ya themanini zikiwa zimesalia dakika kumi mpira uishe bado timu zote zilikua sare, hasira ziliwazidi na kuzidi kunywa pombe kwa kasi, wale waliokua wepesi wa kulewa basi walikua tayari washaishiwa hadi nguvu za kukaa, walijilaza chini.
Dakika ya tisini, kama bahati timu iliyokua ikishambulia ilifungwa goli, lililowafanya washangilie kwa nguvu, waliuona utajiri na macho, hakika walikua na nguvu waligonga vifua kuashiria ushindi huo,refa aliongeza dakika tano, kitendo hicho kiliwaudhi kwani waliamini dakika tano ni nyingi sana katika mpira.Kimya na huzuni kilitawala baada ya timu pinzani kuzawazisha , tena zikiwa zimabki kama sekunde kumi mpira umalizike, hadi Edson alidondokwa na machzoi, wenzake wote walimalizia pombe yote kwa hasira, lakin bila kutarajia goli lilikataliwa na refa, hivyo likafutwa na mpira ukawa umeisha, walishangilia lakini pombe ilizidi kuwakamata na hatimaye wote wakaishiwa nguvu,Edson alisubiri wote wapitiwe na usingizi ili aweze kukamilisha mpango wa kumilikia pesa zote mwenyewe, hivyo alichofanya ni kuingiza mkono mfukoni na kutoa kibahasha, alikiangalia na kutikisa kichwa kutoka chini kwenda juu kuashiria ameweza kitu fulani.....

Je nini kitaendelea? Endelea kufuatilia

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI : SEHEMU YA-06

Asubuhi na mapema siku ya jumatatu katika jiji la Dar es salaam kulikucha na hali ya hewa nzuri iliyompendeza kila mtu, shughuli ziliendelea kama kawaida. Katika chuo kikuuu cha Dar es salaam masomo yaliendelea kama kawaida, haikuwa lazima kwa wanafunzi kuhudhuria kipindi kitendo ambacho hakikuwashangaza wengine juu ya kutowepo kwa wanachuo kumi na sita.
***
FIVE HOURS AGO (masaa matano kabla)
Ulikua usiku wa manane, furaha ilitawala uso wa Edson alipohakikisha wenzake wamelala wote kutokana na kunywa pombe kupita kiasi basi hapo alizidi kuwaongezea pombe alifanya hivyo kwa kumkalisha mtu na kumnywesha pombe kwa kumlazimishia tena safari hii akichanganya na dawa za kulevya aina ya Heroen, alifanya hivyo ili kuaminisha watu kuwa kifo cha hao vijana kilitokna na kuzidiwa na pombe, alihakikisha wote wamepata dozi ya kutosha kisha alikua akimsimamisha mmoja mmoja na kumtikisa tikisa ili kuzidi kuyapa maini shida, alifanya hivyo mmoja baada ya mwingine hakutaka wapate jeraha lolote , na kila alipomaliza kumtikisa basi alimlaza chini na kwa macho yake alishuhudia kila mmoja akitapika damu na pombe nyingi, damu zilikua zikitoka masikioni, mdomoni na puani, harufu kali ya pombe ilianza kutapakaa chumbani pale,baada ya kukamilisha mauaji hayo alitoka kimya kimya huku akihakikisha haonekani na mtu, alitembea kwa kunyata hadi chumbani kwake, na kuacha miili kumi na sita ikiwa chumba kimoja.
***
Winny kama kawaida alikua mtu wa kutoka asubuhi na kuanza mizunguko mitaaa ya Sinza, hiyo ndio ilikua mitaa iliyotawala kwa kuwa na starehe nyingi, kumbi za starehe zilikua nyingi, hivyo walikua wakienda katika kumbi maarufu na kuagiza Pombe laini aina ya Savanna, walikaa pamoja huku wakiamini lazima atajitokeza mwanaume ambaye atahitaji kukaa nae ambao wao humwita jina la kizungu (SPONSER) kwa maana ya mfadhili.
“Huyo anakuja” aliongea Kemmy baada ya kumuona kijana mmoja akija huku mkononi akiwa ameshikilia ufunguo wa gari,
“Habari zenu warembo?” aliongea kijana huyo huku akiachia tabasamu,
“Salama tu kaka” walijibu wote kama vile wameambizana,
“Naweza kujumuika na nyie?”, aliongea kijana huyo hukua akiwa bado amesimama,
“Wewe tu karibu”, Winny alijibu na mara moja kijana huyo alivuta kiti na kuketi.
Waliendelea kunywa huku kijana huyo akiaanza kuwaagizia pombe na chakula, walikaa zaidi ya masaa matatu, kilichowashangaza Winny na Kemmy hawakuelewa kwa nini kijana huyo hakua anakunywa kabisa pombe zaidi ya maji aliyokua ameagiza na hata hakua ameyafungua, yeye alikua anaongea tu na hadi alikua ameshajitambulisha kuwa anaitwa Paul.
“Lakini nimependezwa na huyu hapa zaidi vipi naweza kupata kampani yako peke yako”, Paul aliongea huku akimwangalia Winny usoni,
“It’s okey (ni sawa)”” alijibu Winny na mara moja walinyanyuka na kumuacha Kemmy mahali pale, Winny aligeuka na kumpungia Kemmy mkono huku nae Kemmy akimpungia.
walielekea sehemu ya maegesho ambako kulikua na gari aina ya BMW X6, gari hiyo haikua ngeni machoni mwa Winny,
“Mbona kama hii gari niliwahi kuipakia, hii itakua ya Martin”,alijisema kimoyomoyo , huku akiwa anafungua mlango,
“Kaka samahani hii gari sijui naifananisha”,
“Unaifananisha na ipi ?”,
“Ya kaka mmoja anayeitwa Martin”
“Martin?”
“Yeah Martin”
“Labda tu yanafanana maana hili gari ni langu kabisa”.
Maongezi hayo yalimfanya Winny kumkariri zaidi kijana huyo sura,
Paul aliingiwa na wasiwasi juu ya maongezi ya binti huyo lakini hakuweza kumuuliza maswali mengi kwani ilikua ukweli ni gari la Martin na aliendesha kama mmojawapo ya wafanyakazi wake waliotumika kusambaza dawa za kulevya jijini Dar es salam.
Dakika tano baaaye walikua nje ya nyumba ya wageni iitwayo LION LODGE maeneo ya KIjitonyama, haraka walichukua chumba na kuingia kwa ajili ya mapumziko.
***
Hadi kufika jioni wanafunzi kumi na sita wa chuo kikuu hawakua wameonekana na hapo marafiki zao wa karibu waliamua kumtembelea mmoja baada ya mwingine chumbani, katika hali isiyo ya kawaida walihisi harufu kali kutoka mojawapo ya chumba, cha mwanachuo ambaye hakuonekana kwa siku hiyo,
“Nini tena, mbona harufu kali sana inatoka humu ndani?” aliuliza kijana mmmoja huku akijaribu kufungua mlango uliionekana kufungwa kwa ufunguo,
Edson pia alikua mmoja wa waliokua katika harakati za kushangaa tukio hilo
“Mlango inabidi uvunjwe” alisema Edson huku akijaribu kutafuta upenyo wa kuchungulia ndani.
***
Ukweli wa Martin alikua akifanya biashara haramu ya madawa ya kulevya , alifanya safari nyingi katika mataifa ya China,Thailand, Pakistan, na nchi za Ulaya, alikua na utajiri mkubwa ndani na nje ya Tanzania, alifanya biashara hiyo kwa siri kubwa, alihimiza vijana wengi wenye pesa kujiingiza katika biashara hiyo ambayo aliwaaminisha kujiingizia kiasi kikubwa cha pesa pasipo kutumia nguvu, katika mitaa ya Ilala, Magomeni,Buguruni na Mwananyamala kulisambaa idadi kubwa ya walioathirika na madawa ya kulevya yaliyokua yakisambazwa na Martin.
Maranyingi alikua anatoa madawa hayo kutoka Pakistan ambapo ndiko yalikua yakizaliswa kwa wingi na kuyapeleka hadi nchini China ambako kulikua na idadi kubwa ya watumiaji, ili kuzidi kuifanya biashara hiyo bila kukamatwa aliwatumia sana wafanyakazi wa ndege,marubani, na watu maarufu kama wanasiasa na waimbaji waliokua wakisafiri nchi mbalimbali duniani.
“Pesa sio tatizo, kikubwa mzigo unifikie hapa Lantana Hotel leo saa tano usiku” ilikua sauti ya Martin akiwa amepumzika katika hotel ya Lantana , alikua akiongea na rubani wa ndege ya shirika la Qatar iliyokua inatoka China kuja Tanzania, siku hiyo alikua akisubiri zaidi ya kilo hamsini za Heroen, alipanga kuzisambaza nchini Zambia na Afrika Kusini,
“Sawa ondoa shaka kila kitu kitaenda sawa” rubani huyo aliongea na simu ikakatwa.
Hapo hapo Martin alinyanyua simu na kumpigia Kemmy,
“Uko wapi mrembo nahitaji tupumzike wote hadi kesho, nataka safari hii nikununulie nyumba yako huko Msasani pamoja na gari”, Martin aliongea maneno yaliyomchanganya Kemmy,
“Nipo hapa, Vatican,” alijibu Kemmy huku mapigo ya moyo yakiongezeka,
“Okey nakuitia Uber ikulete hapa Lantana hotel nipo room namba A123,”
“ Okey sweaty” Kemmy aliongea kwa mahaba ya hali ya juu kwani aliamini kama Martin atafurahishwa na mchezo wa siku hiyo basi anaweza kupewa nyumba na gari kama alivyoahidiwa.
Haraka aliingzia mkono ndani ya mkoba wake na kutoa baadahi ya mafuta na kuanza kujipaka alijiangalia katika kioo na kuhakikisha yupo vizuri,
‘Siku huyu shosti angu atajua kuwa namuibia bwana lazima ataniua” alijisemea Kemmy huku akifungua mlango wa gari tayari kuelekea Lantana Hotel.
***
Serikali ya China, ilikua imehisi mzigo wa Madawa ya kulevya kupakiwa ndani ya ndege na hivyo kukaanzishwa uchunguzi wa haraka katika sanduku ililobeba nguo picha zilitumwa katika makao makuu ya jeshi la polisi nchini Tanzania na kikosi cha kupambana na madawa ya kulevya kikawa tayari kupambana na mlanguaji huyo,
“Hapa inabidi tulifuatilie hadi kwa mhusika mkuu, leo nataka hii biashara ife, yaani huyu ndiye atakuwa wa kwanza kuenda kunyongwa nchini China”, yalikua maneno ya kiongozi wa oparesheni hiyo, alitamka kwa hasira kwani alipoona vijana walivyoharibikiwa na madawa hayo alizidi kupandwa na hasira juu ya wale wanaofanya biashara hizo.
***
“Mlango usivunjwe kwanza tuwaite polisi” Edson aliwasihi wenzake kutovunja mlango wa chumba kilichokua kikihisiwa kuwa na watu waliokufa kwani harufu iliytotokea ndani ilikua sio ya kawaida.
Hivyo wakati polisi wakisubiri mzigo wa madawa ya kulevya uliokua unaingizwa Tanzani basi walipokea taarifa nyingine ya kuenda kuvunja mlango ili kijulikane kilicho ndani.

Je nini kitatokea ?? Endelea kufuatilia

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA -07

Askari wakiandamana na waandishi wahabari kutoka vituo mbalimbali vya habari waliwasili katika mojawapo ya vyumba vilivyotumika na wanachuo wa mlimani, moja kwa moja walielekea katika chumba kilichotakiwa kuchunguzwa.
Baada ya dakika tano taarifa mbaya ilisambaa kwa haraka, miili ya wanachuo kumi na sita ilikutwa ndani ya chumba hicho, gari la kukubebea wagonjwa (AMBULANCE) liliwasili eneo hilo kwa haraka na moja kwa moja safari ya kuipelekea miili hiyo katika hospital ya taifa Muhimbili ilianza. Hali ya majonzi ilitanda chuoni hapo huku taarifa ikizidi kusambazwa kwa mitandao ya kijamii, hadi kuwafikia robo tatu ya watanzania pamoja na nchi za jirani kama Kenya na Uganda, kila aliyepata taarifa hiyo alishikwa na huzuni, wazazi wa marehemu walisikitika sana,
“Mbona mwanangu mimi najua haonji pombe kabisa” alijisemea mama mmoja ambaye mwanaye alikua mmojawapo wa marehemu baada ya uchunguzi wa daktari kutoka Muhimbili kuthibitisha kuwa wanafunzi hao wamekufa kutokana na kutumia pombe nyingi wakijichanganyia na madawa ya kulevya aina ya Heroen pia chumba walichokutwa kilibeba ushahidi tosha wa pombe walizokua wakitumia.Moja ka moja miili yao ikahifadhiwa mochwari ili kuanze kufanyika mipango ya mazishi.
***
Edson alitawaliwa nna uso wa furaha kuona kazi yake imeenda vizuri, alijiona akiwa tajiri, kila mda alikua akikagua account yake kama kiasi cha shilingi million mia nane kimeengia kutoka katika kampuni ya Russia, ambayo ndio ilikua kampuni namba moja duniani kwa kulipa vizuri pasipo usumbufu.
“Nikiipata hii pesa kitu cha kwanza naangalia biashara ambayo inalipa kwa haraka mimi lengo langu nataka kuwa tajiri namba moja Tanzania na baadaye hata duniani nataka kuwakomesha wanawake waliowahi kunikataa pia nataka niwe na hadhi ya kutokataliwa na mwanamke yeyote”, yalikua maneno ya Edson mara kwa mara.
***
Ndege ye Qatar 762 kutoka China ilitua katika uwanja wa Julias Kambarage mwendo wa saa kumi na mbili jioni, mzigo wa Martin ulikua wa kwanza kushuka kwa ridhaa ya rubani, na moja kwa moja aliyestahili kuutoa mahali hapo hadi katika hotel ya Lantana alikua tayari, na gari aina ya Carry new model nyeusi, bila kuchelewa mzigo ulipakiwa katika but na dereva kuingia ndani, Askari wawili walikua wakifkuzia gari bila dereva wa gari kujua.
“Umefika wapi”
“Ndio nipo Tabata”
“Ok kaa makini, hakikisha hakuna matatizo yoyote yatakayotokea”
“Sawa mkuu”.
Yalikua mazungumzo kati ya Martin na dereva aliyekua anamletea mzigo wake aliyeitwa Dullah, Dullah aliendesha gari taratibu hasa baada ya kuona kuna gari inamfuata nyuma, hivyo alifanya vile ili kuona kama gari hilo litampita lakini alishangaa kila alipopunguza mwendo na gari ya nyuma ilipunguza mwendo, hapo alilichunguza vizuri kupitia Side Mirrow hapo akaliona lina nembo ya L kumaanisha anayeendesha bado hajawa imara barabarani,
“Itakua wmanafunzi huyu”, alijisemea kimoyomoyo na kuondoa wasiawasi.
Baada ya Dakika kumi na tano, Dullah alikua anaegesha gari katika hotel ya Lantana, alifungua buti na kutoka begi kubwa na kuanza kuliburuza kuelekea chumba alicho Martin,
“Fungua mlango”
“Uko wazi wewe ukija ingia japo nipo na mwanamke, wewe ingia uache hilo bgi kuna begi lignine lipo hapa utalichukua”
Yalikua maongezi kati ya Martin na Dullah, maongezi hayo yaliisha baada ya mlango wa chumba alichokua Martin na kusukumwa, hata sekunde kumi hazikuisha, mlango ulisukumwa na askari wawili waliingia,
“Mko chini ya ulinzi”, sauti hiyo iliandamana na kunyooshewa bastola usoni, Dullah na Martin waligeukiana na kushangaa kitendo kile, Kemmy kwa woga alijifunika haraka na kuvaa nguo za ndani akiwa ndani ya shuka, aliingiwa na hofu kupita kiasi.
“What’s wrong (nini shida)?” aliuliza Martin kwa sauti ya kijasiri,
“Tunaomba kukagua mzigo wenu” alijibu askari mmoja huku akiinama na kutaka kufungua begi lakini Martin alizuia na kuuliza,
“Kwani mnahisi ni nini hadi mnikague?”
“Tumepata taarifa zako kuwa wewe ndiye unaharibu vijana wa hapa Afrika kwa kuwaauzia madawa ya kulevya, na kuna mzigo umeingia hapa mda sio mrefu umetoka China, sasa leo ndio mwisho wa kufanya hii biashara maana utaenda kunyongwa”,
“Okey sasa begi hilo hapo kagueni” Martin aliongea huku akinyooshea mkono bagi ambalo lilikua na pesa, kwani lenye madawa tayari lilikua limeshafichwa mvunguni, Askari alifungua zipu ya begi hakuamini macho yake kile alichokutana nacho, alishtuka sana kuona pesa nyingi kiasi kile, tangu amezaliwa hakuwahi kukaa karibu na pesa nyingi kiasi kile labda pale alipokua akiingia bank,
“Kuna begi lingine” alisema askari mwingine huku akiinamna na kuchungulia mvunguni, na kwa bahati mbaya walifanikiwa kuliona begi lililokua limesheheni dawa za kulevya, walinyanyua simu haraka na kuwapigia polisi wa kichina waliokua wakiwatafuta wahalifu hao kwa miaka mingi.Hapo Martin, Dullah na Kemmy walifungwa pingu na kubaki chumbani hapo ili maskari zaidi waweze kuwasili na waandishi wa habari ili waje kupiga picha kila kitu chumbani pale.
***
Ili kuweza kupigana na maisha, baba Winny alilazimika kutoka kila siku ili kujitafutia chakula chake na mkewe ambaye kwa wakati huo mkewe alikua na ugonjwa wa saratani ya koo, ugonjwa huo ulikua unamtesa sana, mumewe Mazengo, ndio alikua kila kitu japo wakati mwingine alizidiwa hadi kulazimika kuomba msaada msikitini na katika mashirika ya kidini, Winny pia aliwapa wakati mgumu sana pale walipomfikiria maisha anayoishi, waliamini atakuja akuteseka baadaye lakini hawakuwa na jinsi ya kumuokoa kwani hadi nyumbani alikua ameshatoweka. Hivyo jioni ya siku ya Jumatatu alikua akitoka katika makutano ya barabara ya Shekilango,alikua akitembea na miguu hadi Mliman City ili aweze kuhifadhi naulli pale alipokua amekosa kazi kwa siku hiyo, alitembea huku akiwa anaimba nyimbo za kumtukuza Mungu pamoja na kusali rozali, alikimbia na kutembea na kanuni yake ilikua ni usafi, alionekana nadhifu mda wote.
“Mungu atanisaidia kesho nitapata”, alijisemea akiwa maeneo ya Sinza, wakati huo giza lilikua limeanza kuingia, hivyo alitembea haraka haraka huku akihema. Alitamani kufika nyumbani mapema ili kumpa mkewe dawa pamoja na chakula, kwani alimwacha kitandani asubuhi kutokana hali yake ya ugonjwa.
“Mungu akulinde mke wangu, najua uko salama na malaika wanazidi kukupa nguvu na uwezo, mumeo nipo njiani ninakuja kukulisha dawa, naomba nisubiri”, Mazengo alijisemea kimoyomoyo akiamini mkewe anamsikia kupitia roho mtakatifu.
***
“Wazee haya ni mambo ya kuelewana tu” Martin aliongea kwa kujiamini baada ya kuona jinsi askari wale walivyokua wakiangalia pesa zile kwenye begi kwa jicho la tamaa,
“Hakuna ujanja siku yako imefika mwisho” walijibu askari mmoja. Waliongea kwa dakika kumi na bila kutarajia askari wale walikua wapole baada ya kuahidiwa kupewa Bilion moja za kitanzania, ilikua pesa nyingi ambayo hawakuwahi kuishika katika maisha yao,
“Sasa tushapiga simu kuwa kuna nmtu amekamatwa, je hapa tufanyeje?” Askari mmoja aliuliza,
“Wewe hilo ni jambo dogo, tafuteni mtu yoyote hapa tumpe kesi”, alijibu Martin na mara moja Martin alipiga simu na kuamuru kijana wake mmoja aingie barabarani na kuja na mtu wa kupakaziwa kesi,
“Sawa mkuu nakuletea sasa hivi”, Lilikua jibu la Paul ambaye alikua akifanya mapenzi na Winny,
“Mpenzi nisubiri hapa hapa nakuja” baada ya kuongea maneno hayo Paul alivaa nguo haraka na kuingia barabarani alikanyaga mafuta hadi Mliman City,
“Samahani baba”, Ilikua sauti ya Paul ikimuita baba mmoja aliyekua anavuka barabara, na alimuita baada ya kumuona kama amechanganyikiwa kwakua alikua akiongea mwenyewe,
“Bila samahani kijana”, alijibu baba huyo huku akiizidi kusogelea mlango, “
“Kuna kazi nataka ukanisaidie kidogo, nikulipe hata hela ya kula” aliongea Paul huku akitabasamu,
“Oooh Asante Mungu, kazi ya mda gani”,aliuliza baba huyo kwani alikumbuka nyumbani kuna mgonjwa anayestahili kupewa dawa usiku,
“Kama nusu saa hivi” , Paul alijibu na bila kubisha baba huyo aliingia ndani ya gari na gari ikaanza safari kuelekea hotel ya Lantana,
“Mimi kweli Mungu ameniuona dakika za mwisho nimetoka Shekilango hadi hapa nakuja kupata riziki karibu na nyumbani, asante Mungu”, alijisemea baba huyo ambaye ni Mazengo baba wa Winny. Alipata furaha lakin hakujua ndio anaelekea katika kifo, na mbaya zaidi atamuacha mke wake akiwa mgonjwa..

Je nini kitatokea ?

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA -08

Baada ya dakika kumi tayari Mazengo alikua ndani ya chumba katika hotel ya Lantana, aliingiwa na hofu baada ya kuwaona askari polisi waliokua eneo lile,
“Kazi gani mwanangu” aliuliza Mazengo baada ya kutoona kazi aliyoitiwa, hakujibiwa kitu zaidi ya kushuhudia askari mmoja akitoa pingu na kumvalisha mikononi,
“Mbona sielewi kitu ndugu zangu, kuna nini ?” aliuliza Mazengo lakini hakujibiwa kitu zaidi ya kupigwa kofi lililomfanya aanguke kitndani,
“Kila siku madawa ya kulevya yanakatazwa lakini wewe unajifanya mjanja wa kuharibu vijana wawatu huku mtaani sasa cha moto utakiona”, yalikua maneno ya askari polisi, maneno hayo yalimfanya mazengo kuangua kilio kilichokatizwa na kikundi cha askari walioingia chumbani hapo wakiandamana na waandishi wa habari, picha zilipigwa huku Mazengo akiwa bado haamini kilichokua kikiendelea, hakuruhusiwa kuongea chochote, alitolewa mahali pale na kupakizwa ndani ya gari la polisi tayari kuelekea katika mahakama ya Kisutu huku begi lililosheheni madawa ya kulevya likiambatanishwa.
Martin na Kemmy waliondoka na maeneo yale, Martin aliwatumia pesa za kutengeneza mashahidi wa uwongo, chumba cha haraka kilijazwa madawa ya kulevya pamoja na majirani wa uwongo kutafutwa.
“Hakikisheni mnakua makini kwa haya mambo, nyie semeni huyu mtu nyumba yake ni hii na ni jirani yenu, mtafuteni balozi na mwenyekiti wa mtaa mpeni fungu naye aweze kumuweka katika orodha ya wananchi wake”Yalikua maneno ya Paul huku akiwakabidhi mashahidi pesa waliotafutwa kwa ajili ya kushuhudia uwongo, mikanda ya video ilitengenzwa haraka na wataalamu wa kuhariri video huko nchini China zikimuonesha Mazengo akipanda ndege mara kwa mara kwenye majiji kama Shanghai, Beijing, Hong kong, picha hizo zilizidi kuaminisha kuwa Mazengo ni mlanguzi mkubwa wa madawa ya kulevya.
Martin alifurahia sana kila hatua ambayo ilifanyika kuhakikisha hataingia hatiani, huku Mazengo akizidi kulia peke yake mahabusu.
“Jamani nioneeni huruma mke wangu anaumwa sana tokea asubuhi ya leo hajala wala hakuna wakumuuguza naombeni mnisaidiie mimi sio muuzaji wa madawa ya kulevya, Mungu naomba uwape macho ya kutazama hawa watu wako, angalia naamini mke wangu anateseka huko aliko, eh baba wa mbinguni fanya njia pasipo na njia” Mazengo alilalamika bila msaada wowote, giza nene lilimzunguka, alipiga magoti na kusali usiku, maumivu aliyoyapata kwa kuumwa na chawa na mende havikumtisha, aliomba Mungu pakuche salama na aliamini ukweli utabainika kuwa yeye hahusiki kwenye madawa ya kulevya.
***
Baada ya Paul kuhakikisha kuwa mashahidi wa uwongo wamekamilika alitoka moja ka moja na kuelekea katika chumba alichomkodishia Winny, alimkuta Winny akiwa na furaha,
“Ulienda wapi mda wote mpenzi” aliuliza Winny huku akimrukia na kumkumbatia kwa furha,
“Nilienda kufanya ishu ya kuingiza hela dear siunajua tena mwanaume kutafuta?” Paul alijibu kwa tabasamu huku naye akiizungusha mikono yake kiunoni mwa Winny, waliendelea na mambo yao hadi ilipofika saa tano na nusu ya usiku wote wakalala. Winny hakujua chochote kilichokua kikiendelea kwa baba yake.
***
Mama Winny alizidiwa sana, mwili ulipata joto, hakuwa na nguvu za kuongea, alijikuta akijizungusha kitandani kwa shida, mbu walimshambulia sana hakuweza kushusha chandarua,
“Mume wangu kaenda wapi? Hata kama amekosa kazi lazima angerudi mapema”, alijisema mama Winny moyoni, kitanda kililoa kwa jasho lililomtiririka mwilini, hakuna jirani aliyehangaika nao kwa sababu hawakuwa na pesa,
“Mungu nisaidie” alijisemea mama Winny huku akipanga kubingirika kitandani hadi adondoke kisha aweze kuyafuata maji yaliyokua karibu na mlango, kuishiwa nguvu huko kulitokana na , njaa kali iliyozidi kumfanya aumwe kichwa kupita kiasi.
***
Kemmy hili tukio naomba liwe siri yako, naamini wewe ni mtu mzima na ninaamini umenilewa nilichosema” alitamka Martin wakati akiagana na Kemmy,
“Niamini, sitaivujisha siri hii”, Kemmy alijibu kwa tabasamu huku akipokea kiasi cha dolar elfu moja,
“Hii itakusaidia kipindi hiki mimi nina safari kidogo na ninasafiri na Winny, hivyo iwe siri yako pia”,Martin alimaliza kuongea na kumshusha Kemmy aweze kuenda nyumbani. Martin alipanga kutoroka usiku huo huo hadi katika jiji la Lusaka nchini Zambia, aweze kukaa huko hadi atakapohakikisha Mazengo anabeba msalaba wake wote,
“Hadi nihakikishe amenyongwa ili nirudi hapa Tanzania”, alijisemea maneno hayo na moja kwa moja aliinua simu yake na kumpigia Winny, alipiga zaidi ya mara tano bila kupokelewa, Winny alikua katika usingizi mzito kutokana na uchovu alioupata kwa kushinda mchaha kutwa akicheza na Paul kitandani,
“Shenzi huyu mtoto, mbona hapokei simu” alijisemea Martin huku akijaribu kupiga mara ya mwisho, na kwa bahati nzuri ilipokelewa,
“Hello baby”
“Mpenzi uko wapi, nataka kutoka na wewe”,
“Jamani mpenzi mbona usiku sana lakini”
“Najua ni usiku ndio lakini nakuhitaji, nimepata safari ya kwenda nje ya nchi nataka kampani yako, au hutaki kutembea”
“Ohoo sawa honey nipitie basi nyumbani baada ya nusu saa nitakua nimeshajiandaa”,
“Sawa fanya haraka”, maongezi yaliishia hapo na mara moja Winny alimkurupua Paul,
“Baby amka baba ananipigia simu”, Winny aliongea huku akishuka kitandani na bila kupoteza mda Paul alitii wito wa Winny, alitoka naye haraka huku Winny akisisitiza gari kuongezwa mwendo,
“Asante mpenzi nashukuru kwa penzi lako tamu” Paul aliongea huku akitoa dola mia tano na kumkabidhi,
“Asante pia kwa zawadi”, Winny akliongea huku akipiga hatua kuelekea getini, alifungua mlango na kuingia ndani. Alijipaka manukato mazuri pamoja na kupanga nguo zake katika mkoba wake tayari akimsubiri Martin.
Dakika mumi na tano tayari Martin alikua akipiga honi nje ya geti la chumba alichompangisha Winny, haikua ngumu kwa Winny kutambua mlio wa honi ya gari ya Martin hivyo bila kupoteza mda alitoka na moja kwa moja akaingia ndani ya gari na safari ikaanza, Winny hakujua ni nchi gani wanayoenda na wangekaa kwa mda gani hakutaka kujua hilo zaidi alitaka kusafiri tu nje ya nchi.
Bila kuongea lolote safari ilianza, Gari aina ya Jeep, iliikamata vyema barabara ya Morogoro, kuanzia zaa sita usiku alifika katika mbuga ya Mikumi saa kumi na moja asubuhi maafisa wa usalama barabarani walitulizwa kwa kiasi kikubwa cha pesa ili waweze kuachia njia kiurahisi. Baada ya kuwasili katika Mbuga ya Mikumi Martin alihonga kiasi kikubwa cha pesa na kuweza kupata msaada wa kupelekwa hadi mpakani mwa Zambia na Tanzania, katika boda ya Tunduma, Martin alijulikana na askari wa mipakani hivyo baada ya kuonesha visa yake alipita moja kaa moja,na kukodi taxi iliyomfikisha katika mji wa Isoka, ambako alikodi chumba ambacho angepumzika kwa siku mbili.
Winny alifurahia sana maisha aliyokua anapitia, aliamini kuwa na mwanaume mwenye hela unaweza kutembea dunia nzima na kuheshimika kama malkia,
“Hivi wanawake wanaokua na wanaume wasio na hela hujiskiaje?”Winny alijiuliza swali hilo moyoni huku akiwahurumia sana,
“Nataka tukae hapa kwa siku mbili, ili tuweze kusafiri tena”, Martin alimwambia Winny,
“Sawa usijali mpenzi, popote nikiwa na wewe ninakaa kwa amani, kwa sababu wewe ni mwanaume wa kweli unayejua mwanamke anachohitaji”, Winny aliongea huku akimpapasa Martin nywele za kifauni.
***
Mazengo alifurahi sana aliposkia kishindo cha kufunguliwa kwa mlango wa mahabusu, alishuhudia askari polisi wawili wakiingia huku wakiwa wameshikilia bunduki aina ya SMG 606 inayoweza kubeba risasi 40,
“Naombeni mniweke huru mimi sina hatia”, aliongea kwa uchungu huku akijiangusha chini lakini alkishtuka kupigwa na kitako cha bunduki kichwani kitendo kilichofanya atokwe na damu, alibebwa moja kwa moja hadi nje ambako alipakizwa ndani ya gari,
“Hapa ni safari ya kuenda kukagua nyumbani kwako”, ilikua sauti ya askari aliyeonekana kuwa na hasira kuliko wote, kitendo cha kusikia hivyo kilimpa Mazengo furaha ya ajabu, alijikuta akitabasamu, kwani aliamini kwa asilimia zote kuwa nyumbani kwake hapakua na hata chembe ya madawa ya kulevya.
“Kwangu sio upande wa huko ni huku”, Mazengo aliongea kwa sauti ya juu huku akinyooshea mkono upande wa nyumbani kwake baada ya kuona gari ya polisi ikishika barabara ya kuelekea Mbagala,
“Tulia sisi ndio tunajua kwako”, askari mmoja aliongea huku akimkanyaga Mazengo kichwani, huku akipigwa ngumi ya mdomo na askari mwingine.
“Basi sawa”, alijisemea moyoni huku akiamini labda wanatumia njia nyingine, hakujua kama anapelekwa sehemu iliyosheheni madawa ya kulevya na hadi kuna watu waliohongwa pesa ili waweze kushuhudia uongo, yeye alizidi kujipa imani kuwa atakua salama mda sio mrefu baada ya kuenda aliamini watakapoona mazingira ya nyumbani kwake na mkewe basi hata majirani zake wangemtetea.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-09.

Ilikua asubuhi ya furaha sana kwa Edson baada ya kutembelea account yake nakukuta kitita cha million mia nane, hakuyaamini macho yake hadi alipoenda katika tawi la kutolea pesa la Backlays na kujitolea laki mbili,
“Asante Mungu, kwaheri umasikini” alijisemea Edson huku akiondoka taratibu eneo la bank. Chuoni kulitawaliwa na hali ya majonzi, wanachuo waliopoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha walikua njiani ili kuja kuagwa na wanachuo kabla ya kila mmoja kuchukuliwa na familia yao kwa ajili ya maziko, bendera ya chuo ilipepea nusu mlingoti kuashiria majonzi.
***
“Mbona mnanipeleka mahali ambako sio nyumbani kwangu au mnaniteka?” Mazengo alizidi kulalamika, gari iliikamata barabara ya mbagala na baada ya mda walikunja na kuingia Mtongani, baada ya dakika tano waliegesha gari nje ya nyumba ambapo baada ya gari kupiga honi geti ilifunguliwa na gari ya polisi iliingia, waandishi wa habari waliamrishwa kubaki nje hadi watakapoitwa,
“Karibu boss, kuna nini?” ilikua sauti kutoka kwa mlinzi aliyefungua geti huku akimshika Mazengo kichwani,
“Nani boss wako?”, Mazengo aliuliza kwa mshangao,
“Si wewe, au nakosea kukuita boss wangu wakati wewe ndiye umeniajiri hapa” aliongea mlinzi huyo kitendo ambacho kilizidi kumshangaza Mazengo, moja kwa moja alijua ameuziwa kesi na alijua dhahiri hatatoka salama, mwenyekiti wa mtaa wa Mtongani aliitwa na kweli alithibitisha kuwa Mazengo ni mkazi wa eneo lake na hapo ndio kwake,
“Kwani naota au ninaigiza filamu?” alijiuliza Mazengo, na baada ya hapo waaandishi wa habari waliitwa na kuingia ndani, upekuzi ulifanyika na hapo ndipo walikuta madawa ya kulevya aina mbali mbali yakiwa yamefichwa darini.
“Nakuachia yote Mungu wangu unitetee, najua hawa wanatumia nguvu ya pesa naomba uoneshe ukweli”Mazengo alitamka maneno hayo kisha akafunga kuongea, hakujibu swali lolote aliloulizwa, zaidi alitikisa kichwa kutoka chini kwenda juu kuashiria kukubali kila alichoulizwa.
Taarifa zilitumwa kwa serikali ya China na moja kwa moja serikali ya China ilimuomba mtuhumiwa huyo kusafirishwa hadi nchini China mara moja, na bila kupoteza wakati mipango ya safari ilifanyika, chini ya ulinzi mkali Mazengo alisafirishwa hadi nchini China, kichwa chake kiliwaza hali ya mkewe ambaye hakujua kama atakua mzima hadi wakati huo, aliamini kama ilivyo kawaida pale unapohusika na biashara ya madawa ya kulevya nchini China hukumu yake ni kifo, hivyo naye alijua dhahiri kifo ndicho kilichobaki mbele yake,
“Mwanangu Winny uko wapi hata ukae na mama yako,? ona mimi naenda kufa bila kukuaga, bila kumuaga mke wangu, sijui nani atamhudumia mke wangu, Mungu nakuomba mrudishe mwanangu Winny akamlee mama yake”, alijisemea Mazengo akiwa chini ya ulinzi mkali nje kidogo ya uwanja wa wa ndege wa kimataifa jijini Beijing, machozi hayakumkauka hasa alipopakiwa katika ndege maalumu za washtakiwa wa makosa makubwa tayari kupelekwa katika jiji la Hong Kong, ambapo kulikua na jumba ambalo liliitwa JUMBA LA KUSEMA UKWELI jumba hilo liliitwa hivyo kwa sababu ya kilichokua kikifanyika ndani, hapo palikua sehemu maalumu kwa watuhumiwa wanaogoma kusema ukweli, hivyo mahali hapo kulikua na mateso ambayo ni vigumu binadamu wa kawaida kuyavumilia, kila aliyeingizwa mahali pale aliseme kila kitu.
“Hapo utakapopelekwa uhakikishe unasema ukweli wote maana utateswa sana, na kuliko wakutese kiasi hicho bora useme tu watu unaofanya nao hii biashara kwa hapa China”, yalikua maneno kutoka kwa askari mmoja wa kitanzania, alkiyekua anaandamana na Mazengo kutoka Tanzania, maneno hayo yalizidi kumliza Mazengo,
“Sasa niseme ukweli gani?” mimi mmeniuzia kesi, na nimemuachia Mungu anihukumu kama nyie mtaniuwa niuweni tu”, Mazengo alitamka kwa hasira.
***
Martin na Winny waliendelea kujirusha ndani ya nyumba waliyokodi katika mji wa Isoka, kupitia simu ya mkononi Martin alifuatilia taarifa zote zilizokua zikiendelea lakini hakujua kama mwanaume aliyepewa kesi yake ndiye baba yake Winny, pia nae Winny hakujua chochote kilichokua kikiendelea, zaidi ya kutawaliwa na furaha, alijiona mbarikiwa mbele za Mungu, aliishi maisha ambayo hakuwahi kuyawaza,
“Nilifikiri watoto wa marais ndio hufurahia maisha kumbe msichana yeyote akiamua kuutumia uzuri wake vizuri anaishi kilaini hivi?” Winny alijisemea akiwa bafuni kujiandaa kwa safari ya mji mkuu wa Zambia,Lusaka.
***
Mama Winny, alizidi kuchanganyikiwa japo alianza kupata nafuu, baada ya kusaidiwa na wasamaria wema, taaarifa ya kukamatwa kwa mumewe ilimchanganya, hakuamini taarifa kutoka kituo cha polisi,
“Mnaposema mmeenda kwake mmekagua mmekuta kumejaa madawa, ni wapi mbona mimi sikuwaona mkija hapa nyumbani?” lilikua swali kutoka kwa mke wa Mazengo aliyejulikana kwa jina Lusia,
“Mama kuwa mpole mumeo ana nyumba huko Mbagala, na ni uhakika ni ya mumeo labda alikuficha wewe usijue mipango yake”, mmojawapo ya askari aliyekua amehongwa pesa alimjibu Lusia,
“Kweli mume wangu awe na nyumba nisijue, je kama anafanya biashara yenye hela nyingi kama mnavyodai siangenipeleka kutibiwa?mume wangu hawezi kuniacha nife akisema hana pesa wakati anazo, naamini mnataka kumuua mume wangu ili na mimi nife kwa ugoinjwa ila Mungu anawaona kwa haya mnayofanya”Lusia alishindwa kuongea zaidi , machozi yalibubujika kwa kasi, hakuamini kama mume wake yupo katika mateso na mda sio mrefu ataweza kunyongwa,
“Mume wangu, unakufa utaniacha na nani nimekuzoea mume wangu usife huko uliko fanya urudi salama”, aliongea Lusia huku akiipa shingo yake iliyovimba mazoezi.
***
Majira ya saa mbili kamili usiku saa za China, Mazengo alikua ndani ya JUMBA LA KUSEMA UKWELI, alitetemeka kwa hofu sura ngumu za askari wa China zilimfanya akate tamaa ya kukaa dunaini hata kwa dakika kumi, aliketishwa katika kiti maamulu ambacho ukishakaa kinajifunga kiasi cha kushindwa hata kugeuka, baada ya hapo kiti hicho kilisogezwa kwa kutumia mitambo ya tarakilishi, na kujikuta ndani ya chumba kisicho na mtu, chumba hicho kilifungwa screen kubwa ukutani, bila kutarajia alijiona katika screen akikatiza katika mitaa ya Shaghai, alijiona akiwa katika vikao na watu mbali mbali, alijiona akihesabu hela pamoja na kukagua madawa ya kulevya, hakuamini macho yake kwa kile alichokua akishuhudia,
“Je hicho unachoona ni kweli au uwongo “ sauti ilisikika kutoka katika spika,
“Sijui” alitamka Mazengo bila kuelewa anayeongea yupo wapi,
“Sasa tunataka utuambie kila kitu, ili tuuwe kabisa hii biashara hapa China, taja wafanya biashara wote unaoshirikiana nao hapa China”, Mazengo hakuwa na lakusema kwani hakujua chochote, baada ya dakika moja akiwa kimya alishuhudia magurudumu ya kiti alichokalia yakizunguka na moja kwa moja kilikamata njia ya kuelekea chumba kingine,
“Utasema yote ukifika hapo unapopelekwa”sauti hiyo ilimshtua Mazengo, alijua ni dhahiri wakati wa kuteswa umefika.
***
Vijana wawili waliofunika nyuso zao kwa vitambaa walikua wakivunja vitasa, nyumbani kwa Mazengo, walifanya kila kitu kimya kimya kusudi Lusia waliyeamini yupo ndani asisikie kitu, dakika tano tayari walikua wameshavunja kitasa cha mlango wa kuingia sebuleni, huku wakiwa na mapanga mkononi, walianza kuvunja kitasa cha mlango wa kuingia chumbani,
“Hapa ni mwendo wa SK SM (Silence killing, Silence Moving) Kuuwa kimya kimya na kutembea kimya kimya, lengo la watu hao ni kupoteza ushahidi na malalamiko kutoka kwa mke wa Mazengo kwani Martin aliamuru vijana wake wachunguze alipo mke wa Mazengo na auwawe mara moja.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-10

Shughuli za kuiaga miili ya wanachuo walioaga dunia zilimalizika na kila familia iliyopatwa na msiba ikaweza kuchukua marehemu wao na kuanza safari ya kuenda kumhifadhi.
Edson alibaki na furaha kubwa moyoni kuona lengo lake limetimia kirahisi, kila mda aliweza kutembelea katika tawi la bank na kukagua salio lake. Hakuna mwanafunzi mwenzake aliyejua kitu kilichokua kikiendelea.
***
THREE HOURS BEFORE (masaa matatu kabla),
ilikua ni mwendo wa saa moja kamili jioni, Lusia akiwa kitandani amejilaza, aliona dalili za kuzidiwa usiku,
“Kichwa kinaniuma na usiku kinaweza kunizidi kama jana acha nijikongoje hadi kwa mama Mainda” alijisemea Lusia na taratibu alitembea hadi nyumba ya jirani na kuingia moja kwa moja hadi ndani kwa mama Mainda,
“Hodi mama Mainda”
“Karibu mama Winny”
“Nishakaribia mwenzako, nimesema nije kukutembelea nimeshazoea kukaa na mume wangu sasa niko mwenyewe na huyu binti yangu ndio kanitoroka kabisa, na mimi naumwa mama Mainda sijui nikuelezeje shoga angu”, aliongea Lusia huku akihema
“Utapona mama Winny mwamini Mungu tu, vipi nikupe mume wangu akakupe kampani kwa leo”, aliongea mama Mainda huku akimalizia kwa utani uliowafanya wote wacheke hasa baada ya mume wa mama Mainda kuongea kwa sauti kubwa kutoka chumbani,
“Kweli itakua vizuri nikienda kumpa mgonjwa kampani, ili usiku nimhudumie vizuri” maneno hayo yalimfanya mama Mainda aongee kwa sauti zaidi,
“Weeeeeeeee thubutu, endelea kulala mme wangu acha mimi nipige umbea kidogo hapa nakuja”,
“Usijali mke wangu” alijibu baba Mainda na kumuacha mkewe aendelee kuongea na rafiki yake wa siku nyingi, Lusia alimweleza rafki yake kila kitu kilichokua kikiendelea, alimueleza kuhusu askari waliokuja kumtembelea nyumbani,
“Mama Winny, usikate tama haya ni maisha na yatapita kikubwa uvumilivu tu na maombi, sasa nakushauri lala hapa hapa kwangu maana sio vizuri uende nyumbnani ukalale mwenyewe na unaumwa”
“Usijali mama Mainda sitalala hapa kwako bhana mara usiku nisikie mauno yako na mumeo”
“Acha zako mama Winny lala hapa, ngoja nikupakulie ule”
“Sawa shoga lakini inabidi Mainda aende akaniletee dawa zangu pale mezani” Lusia alitamka na mara moja mama Mainda hakuona sababu ya kumwamsha mwanaye aliyekua amepumzika, hivyo aliamua kutoka mwenyewe huku mkononi akishikilia simu yake aliyoitumia mara nyingi kama kurunzi, alichukua funguo na moja kwa moja akatoka huku akirudishia mlango.
***
Vijana wawili waliendelea kuvunja milango nyumbani kwa Lusia walifanikiwa kuvunja mlango wa kuingia chumbani, lakini walishikwa na hasira kwa kutokuta mtu chumbani hapo,
“Shit ! yupo wapi huyu kenge”, aliongea kijana mmoja huku akishikilia panga lake vizuri,
“Tulia tulia” mwenzake aliongea kwa sauti ya chini baada ya kusikia vishindo vya mtu anayetembea, haraka walijificha mvunguni wakiamini atakua Lusia,
“Akiingia ndani hakuna kuzubaa, upite na hiyo shingo haraka”, Jambazi mmoja alimnong’oneza mwenzake.
Mama Mainda apatwa na wasiwasi baada ya kukuta milango iko wazi huku kimya kikitawala nyumba ile,
“Ina maana Winny kaja kaingia? Sidhani katoa wapi funguo ?” alingia sebuleni huku akiwa na wasiwasi kua huenda Winny karudi,
“Winny”, mama Mainda aliita lakini hali ikawa ile ile ukimya, hapo aliinua simu na kumpigia mumewe,
“mbona huku kuko wa___” kabla hajamalizia sentensi hiyo alishtukia vijana wawili waliofunika nyuso zao kutokea, alitetemeka kwa hofu hadi simu ikadondoka chini, aliinama ili aweze kuiokota lakini alishtukia panga likipenya kiunoni, lilikua panga lenye makali kiasi cha kuutengenisha mwili wa mama Mainda,
“Msiniue jamani” Lilikua neno la mwisho alilotamka mama Mainda huku akitokwa na damu mdomoni, puani na katika masikio, kwa kutumia macho yake aliona kiuno chake kikiambatana na mapaja pamoja na miguu kikichezacheza sakafuni, aliona kama ndoto inayoendelea kwani alitamani kukiuliza kiuno chake kinaenda wapi lakini hakuweza kufanya hivyo kwani aligeuza macho na kuaga dunia.
***
Baba Mainda hakuelewa kitu alichokua akiskia kwenye simu, ila aliamini kuna hali ya hatari iliyokua ikiendelea,
“Kwani mama Mainda kaenda wapi?” lilikua swali la kwanza alilomuuliza Lusia aliyekua sebuleni,
“Kaenda kwangu kunichukulia dawa zangu leo nataka kupumzika hapa” Lusia alijibu lakini baba Mainda alionekana kama ana mshtuko, haraka alichukua fimbo yake anayoitumia kama silaha kwa ajili ya kupambana na hali ndogondogo za hatari kama kuuwa nyoka ndani na mara nyingine aliiweka kwa ajili ya kumnyoosha mkewe pale alipokua anenda kinyume na taratibu za nyumbani,
“Kwani kuna nini Baba Mainda” Lusia aliongea huku akijaribu kumzuia baba huyo,
“Subiri itakua kuna tatizo, nenda kajifungie chumbani kwa Mainda” baada ya hapo haraka alitoka kasi akielekea kwa Mazengo ili kuenda kuona mkewe kapatwa na mkasa gani.
***
Martin na Winny walitua katika jiji la Lusaka majira ya jioni, hali ya ubaridi ilitawala katika jiji hilo, hali ya hewa iliwaruhusu kuikamata barabara ya Chakeluka , gari aina ya Toyota Mark X iliikamata barabara sawasawa, dereva aliyewaendesha alikua akimeza mate wakati wote wa safari kwa vitendo vilivyokua vikifanywa na Martin na Winny, ilikua safari ya kuelekea Chita Lodge, ilikua hotel ya kitalii, jijini Lusaka, haraka waliingia chumbani na kupata chakula cha jioni kisha wakaingia bafuni. Waliogeshana kwa mahaba, Winny alizidi kujiona wa kipekee duniani, Martin alimuogesha kwa mahaba, walikumbatiana kusudi kupambana na ubaridi wa maji waliyokua wakiyatumia .
Winny hakujua yaliyoendelea kwa wazazi wake, simu yake haikua na uwezo wa kupigiwa wala kupiga kwani Martin alimzuia kuwa hewani huko Zambia ili waweze kufurahia vizuri,pia Martin hakujua kama Mazengo ndio baba yake Winny.
“Mpenzi nafurahia kuwa na wewe” Winny aliongea huku akipakwa mafuta na Martin, alijiona msichana wa kipekee kupendwa na mwanaume mwenye hela kiasi kile.
Baada ya kuandaana kwa ajili ya kufanya mapenzi basi walianza kufurahia miili yao.
***
Baba Mainda alipigwa na butwaa baada ya kukutana wanaume wawili, waliokua wamefunika nyuso zao, walimshika na kumpa vitisho ya kumuua,
“Huyu mama yupo wapi la sivyo tunakuuwa kama mkeo” Yalikua maneno yaliyotoka kwa mmojawapo ya vijana hao, huku baba Mainda akiona kama ni ndoto ambayo angezinduka mda wowote, hakuamini kama mwili wa mkewe ndio umetengenishwa sakafuni huku damu nyingi ikitapakaa,
“Mama yupi?” aliuliza baba Mainda kwa hofu,
“Huyu mama wa hapa nyumbani” aliongea kijana huyo huku akitekenya kwa mdomo wa bastola shingoni, mwili wa baba Mainda ulisisimka kwa uwoga alikiona kifo kwa macho,
“Sijui”alijibu huku akiangalia chini, kwa kusema neno sijui alishtuka kidole gumba chake kikiwa ardhini, baada ya kukatwa na mkasi, alihisi maumivu yasiyo na mfano, alitamani ardhi ipasuke azame lakini sio kwa maumivu aliyopata, waliendelea kumtesa ili aweze kusema mahali alipo mama huyo kwani waliamini lazima atajua kila kitu baba Mainda, alishindwa kuvumilia zaidi hasa baada ya kuminywa korodani ka kutumia plaizi akaamua kuongozana na vijana hao ili aweze kuenda kumtoa Lusia ndani kwake
“Mungu nakuomba angalau wakamuache mwanangu Mainda akiwa hai, maana nina imani Lusia na mimi tutakufa” alijisemea kimoyomoyo huku wakiendelea kupiga hatua.
***
Mazengo aliingizwa katika chumba kidogo, alikutana na mtu aliyefunika uso, mtu huyo alimsogelea na kuchuchumaa mbele yake, aliifungua zipu ya suruali na kuutoa uume wa mazengo, Mazengo hakujua kitu ambacho kilikua kikifuata baada ya hapo, lakini sauti iliyorekodiwa ilisikika kupitia spika
“Taja mtandao wako wote unaoshirikiana nao katia hii biashara” sauti hiyo ilimpa Mazengo wakati mgumu hakujua cha kuelezea, akawa anatikisa kichwa kutoka kushoto kwenda kulia kuashiria haelewi chochote, kwa macho yake alishuhudia kijiti chembembe kikipenya katikati ya uume wake katika mrija wa uretha, alilia kwa uchungu kwa naumivu aliyopata.

INAENDELEA

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA-11

Mapigo ya moyo ya baba Mainda yalidunda kwa kasi ya mara 120 kwa dakika, mwili wake uliishiwa nguvu, picha ya mkewe ilimjia kichwani, alimini katika mkosi alijua mda sio mrefu atakua marehemu,
“Shida yetu ukishatuonesha huyu mama wa huku nyumbani tunakuacha”maneno hayo yalipennya masikioni kwa baba Mainda ingawa hakuyaamini,
“Hivi majambazi wanaweza kukuacha mzima baada ya kuwaonesha mtu wakumuua ?” alijiuliza moyoni baba Mainda lakini jibu lililomjia kichwani ni HAPANA,
“Acha nife mwenyewe maana wakifika kwangu lazima watamuua huyu mama na mwanangu, hapa yanipasa nife kiume, Mungu pokea roho yangu” baba Mainda alijisemea na mara ,moja alianza kuzozana na wale vijana, kutokana na hali ile wale vijana walijua dhahiri kelele zikisikika basi nao watakua hatarini hivyo waliamua kumkata shingo na kumuacha njiani.
“Mpango umeharibika tukajipange upya” walisema vijana hao na kutokomea gizani huku wakiacha mwili wa baba Mainda ukiwa umetenganishwa na kichwa.
Kutokana na hali baba Mainda aliyoondoka nayo nyumbani kwake basi mama Winny alishindwa kuvumilia na kujikuta anaenda chumbani kwa Mainda na kumuamsha,
“Mainda amka kuna hali ya hatari” aliongea mama Winny huku akimgusagusa Mainda baada ya dakika mbili Mainda alikua anajifunga kanga yake vizuri, kwani kwa umri aliokua nao akiwa anasoma kidato cha pili basi alikua ashajua kulala na kanga pekee, hawakutaka kupoteza mda walitoka kwa lengo la kumfuata baba na mama yake, walipokaribia kufika kwa mama Winny hawakuamini macho yao,
“Baba usife baba, amka, amka baba” Mainda aligaragara ardhini, mwili wa baba yake ulikua ukitupatupa mikono huku akiona kichwa kikiwa pembeni yake,
Mama Winny ndiye hakuamini macho yake, walipiga kelele kuamsha majirani, na ndipo palijaa watu,
“Mama yangu yupo wapi?” Mainda aliiuliza akiwa bado haamini kinachoendelea,
“Mama ndiye aliyekua wa kwanza kuja kwangu hebu tukamuangalie kama yupo ndani” alijibu mama Winny huku kikundi cha watu kikiongozana kwenda kwa mama Winny, hali ya Mainda ilizidi kuwa mbaya, alidondoka chini baada ya kumuona mama yake amekufa pia, taarifa ilifika katika kituo cha polisi haraka na baada ya dakika kumi, tayari miili ya marehemu ilikua ikisafirishwa kwenda katika hospitali ya taifa Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi,
Matukio yote hayo Martin alikua akipata taarifa, alizidi kusisitiza askari aliowahonga pesa waweze kumuua mke wa Mazengo,
“Sawa mzee tutamuua kirahisi maana lazima tumuweke ndani kutokana na kwamba kuna mtu aliuwawa akiwa ndani kwake hivyo tunahakikisha tukimuweka ndani kwa ajili ya uchunguzi basi tutamuulia hukuhuku” lilikua jibu kutoka kwa kiongozi wa askari wasaliti.
***
Mazengo alikua katika mateso makali, alijuta kuzaliwa, hakuwahi kuwaza katika amaisha yake angeweza kuteswa kiasi hicho,
“Mungu naamini wewe ndiye umeyaruhusu yote haya yatokee, naamini una sababu yako, lakini naomba nilindie mke wangu japo sina imani kama nitakuja kukutana nae katika maisha yangu, naomba Mungu baba wa mbinguni mtazame mke wangu na huko mwanangu aliko mpiganie arudi katika njia zako Amina”, Mazengo alifanya maombi hayo mara kwa mara, askari aliyejifunika uso aliendelea kumtesa alipakwa pilipili machoni, macho yalibadilika rangi na kuwa mekundu, aliwekewa moto nje ya kucha kisha moto ukapenya taratibu dani ya nyama, kilio alicholia hakikufika popote.
***
Martin akiwa anaendelea kujirusha jijini Lusaka alifanya mawasiliano na askari wa kichina na kutoa pendekezo la Mazengo kuuwawa kwa kunyongwa, baada ya askari wasaliti wa kichina kulipeleka pendekezo hilo kwa uongozi mkuu wa kupambana na kesi za madawa ya kulevya basi uongozi mzima uliridhika na hatua hiyo. Siku ya kuuwawa ilitangazwa pamoja na kubuni namna nyingine ya kuuwa pasipo kunyonga, walitaka kuuwa kwa kuchoma moto, hivyo Mazengo aliipokea taarifa hiyo na haraka akaanza kutubu dhambi zake ili aweze kupokelewa mbinguni,
“Kweli mimi nitakufa, ama kweli dunia tambara bovu, nimeamini raha ya pekee ipo mbinguni”, alijisemea Mazengo baaada ya kuingizwa katika chumba chake kilicho na ulinzi mkali tayari kusubiria siku ya kuchomwa moto ifike.
***
Kemmy aliendelea kuuza mwili, alimkumbuka sana rafiki yake Winny, alimamini siku akirudi basi utajiri wake utaongezeka maradufu, wanaume walizidi kumgombania, umbo lake lilizidi kuvutia hasa baada ya kuanza kutumia dawa za kuongea makalio na kusimamisha maziwa, wanaume walimwita FIGURE 8 (umbo namba nane) kwani akikua mpana kifuani, mwembamba tumboni na mpana makalio, hivyo alitengeneza umbo la namba nane.
***
Edson bado aliendelea kuwaza biashara ambayo ingemuingizia faida kwa kiasi kikbwa, alizidi kuwa mvumilivu ili huzuni ya wanafunzi izidi kupungua, alifikiria biashara nyingi ambazo alitamani kuzifanya lakini iliyomkaa zaidi kichwani ni baishara haramu ya madawa ya kulevya, aliamini siku zote biashara haramu ndiyo ingemuingizia pesa kwa haraka.
“Cha kufanya inabidi nitafute mtu mwenye uzoefu na hii bishara ili anioneshe njia za kupitia”, alijisemea moyoni.
***
Marehemu baba na mama Mainda walizikwa baada ya siku tano, huku mama Winny akipelekwa katika matibabu hospital ya Muhimbili ili aweze kutibiwa na baadaye aweze kukaa mahabusu kwa ajili ya uchunguzi wa kifo cha baba na mama Mainda.
Mainda aliachwa yatima, alimlaumu sana mama Winny kwani aliamini yeye ndiye chanzo cha matatizo yote,
“Lakini huyu mama Winny amekua rafiki na wazazi wangu tangu nikiwa mdogo hivyo sina budi kumpenda” alijisema Mainda ikiwa ni wiki mbili zimepita.
***
Ili kuwa fundisho kwa watu wote waliokuwa wanafanya biashara ya madawa ya kulevya nchini China basi serikali kupitia kitengo maalumu kilichoundwa kuthibiti na kupambana na uhalifu huo kilitangaza siku ambayo dunia nzima ingeona moja kwa moja tukio la kuchomwa moto kwa mhalifu sugu ambaye alikamatwa,Picha ya Mazengo ilisambaa katika mitandao ya kijamii, watu wote walisubiria kuona siku ya kuuwawa kwa mhalifu huyo, vituo mbalimbali televisheni vilitarajia kuonesha tukio hilo mwanzo hadi mwisho.
“Hapa ndani una siku kumi na tano za kuomba Mungu akupokee salama”Lilikua neno la mwisho kabla ya kuletewa biblia ili aweze kujikumbusha neno la Mungu, alisoma baadhi ya vitabu muhimu, aliungama dhambi zake, alitumia mda mwingi kuombea familia yake ambayo aliamini ataiacha katika mateso, mkewe aliyekua anasumbuliwa na saratani alizidi kumpa huzuni.
“Mungu kwa nini unaruhusu haya yatokee?” alijiuliza mama Winny baada ya kuona picha ya mumewe ikisambaa katika mitandao ya kijamii pamoja na siku ya kuuwawa kwake,
“Mume wangu kama utakufa kweli basi naamini tutakutana mbinguni”, alijisemea mama Winny kisha akajifunika na kuendelea kulia peke yake.
Siku zilibaki tano kabla ya Mazengo kuchomwa moto, shimo lenye urefu wa zaidi ya mita mia lilichimbwa mfano wa tanuru, shimo hilo lilichimbwa maalumu ka ajili ya kuchomea miili ya watu watakaobainika kujihusisha na biashara yoyote ya mihadarati,pia shimo hilo lilichimbwa eneo la tume ya kuthibiti biashara hiyo pembeni ya shimo hilo kulikua na makaa ya mawe, makaa ya mawe yalikua na uwezo wa kuwaka mara tano zaidi ya mkaa wa kawaida.
Siku ya tukio ilifika, Mazengo alitamani mda usiende lakini haikukuwa hivyo, saa iliyokua ukutani ilisogea kwa kasi kuliko kawaida, alikiona kifo kikimsogelea, yalibaki masaa dakika, na hatimaye sekunde, huku akiwa amekata tama alishtuka mlango kufunguliwa , waliingia wanaume watatu, walimsukuma katika kiti alichofungiwa hadi eneo la nje kabisa, ambapo kulikua na waandishi wa habari waliokua wanachukua tukio hilo, vituo vya habari karibia nchi zote zilikua zikirusha tukio hilo moja kwa moja.
***
Macho ya Winny yalikwama kwenye screen kubwa ukutani katika chumba alichokua na mpenzi wake,
“Whaaaaaaaaaaaaaaaaaat (nini?)” aliongea Winny kwa sauti huku akitokwa na machozi,
“Nini zaidi mpenzi, mbona unashtuka ?” Martin aliongea huku akimvuta Winny akae kitandani kwani alikua akisogea karibu na televisheni ukutani apate kuona vizuri,
“Baba yangu kabisa huyu” aliongea Winny huku akirusha rusha mikono,
“Hapana umemfananisha sio baba yako, huyo ni mfanyabiashara wa madawa ya kulevya amekamatwa huko China, sasa anauwawa,”Martin aliongea kwa upole lakini Winny alizidi kulalama, alilia kwa sauti kitu ambacho kilimpa Martin wasiwasi wa kutokea kwa wahudumu,
“Nakwambia ukweli huyu ni baba yangu, wala siwezi kuwa nimemfananisha, namjua vizuri baba yangu, mpenzi baba yangu atakufa na ninajua hafanyi biashara hiyo” alizidi kulalamika Winny.
Mazengo alipewa dakika kumi na tano kuongea maneno ya mwisho pamoja na kuaga watu wote wanaomuangalia, aliinama kwa dakika chache kisha akainua uso na kuanza kuongea,
“Kwanza nimshukuru Mungu kwa yote mema aliyofanya kwangu, natumai hapa wakati wangu wa kufa umefika, naenda kulala usingizi wa milele, usingizi usio na mihangaiko najua hata kama nikisema sikufanya kosa hamtaniamini lakini nawasamehe wote walinisababishia mambo haya, mke wangu mama Winny kama upo hai na unanitazama mimi mumeo nakuaga, mwanangu Winny popote ulipo kama unanitazama tambua nakupenda sana mwanangu tukio hili lisikupe hofu, nakuomba kua na moyo wa kijasiri tutakutana mbinguni mwanangu, mama Winny mke wangu nakupenda sana katika shughuli zako popote ulipo mtangulize Mungu, kuwa na moyo wa kusamehe na kusahau, kama unanitazama basi usiwe na hasira juu ya haya yanayoendelea, sahau na samehe mke wangu kipenzi ukae salama” Mazengo alimaliza kusema maneno hayo yaliyomfanya mkewe aliyekua anaangalia tukio hilo katika televisheni ya wodini ambayo waandishi wa habari hawakuruhusiwa kuingia ndani, Winny alizidi kuchanganyikiwa Martin alijitahidi kumbembeleza bila mafanikio hatimaye alifungua begi lake na kutoa gundi yenye uwezo wa kumziba mtu mdomo na asitoe sauti yoyote, Martin aliiviringisha mdomoni mwa Winny kisha kumfunga miguuu na mikono,macho ya Winny yalishuhudia baba yake akiwekwa ndani ya mfuko sulphate , kichwa kikibaki nje.
Moja kwa moja walimbeba hadi katika shimo ambalo liliandaliwa kwa ajili ya kumtumbukiza kisha wamchome, pembeni ya shimo hilo makaa ya mawe yalikua yakipata moyo taratibu, baada ya dakika tano kila kitu kwa mujibu wa sheria kilikamilika na kiongozi alianza kuhesabu moja hadi tatu ili aweze kurushwa shimoni….

Je nini kilitokea, endelea kufuatilia

the Legend☆
 
BASI LA SHETANI: SEHEMU YA -07

Askari wakiandamana na waandishi wahabari kutoka vituo mbalimbali vya habari waliwasili katika mojawapo ya vyumba vilivyotumika na wanachuo wa mlimani, moja kwa moja walielekea katika chumba kilichotakiwa kuchunguzwa.
Baada ya dakika tano taarifa mbaya ilisambaa kwa haraka, miili ya wanachuo kumi na sita ilikutwa ndani ya chumba hicho, gari la kukubebea wagonjwa (AMBULANCE) liliwasili eneo hilo kwa haraka na moja kwa moja safari ya kuipelekea miili hiyo katika hospital ya taifa Muhimbili ilianza. Hali ya majonzi ilitanda chuoni hapo huku taarifa ikizidi kusambazwa kwa mitandao ya kijamii, hadi kuwafikia robo tatu ya watanzania pamoja na nchi za jirani kama Kenya na Uganda, kila aliyepata taarifa hiyo alishikwa na huzuni, wazazi wa marehemu walisikitika sana,
“Mbona mwanangu mimi najua haonji pombe kabisa” alijisemea mama mmoja ambaye mwanaye alikua mmojawapo wa marehemu baada ya uchunguzi wa daktari kutoka Muhimbili kuthibitisha kuwa wanafunzi hao wamekufa kutokana na kutumia pombe nyingi wakijichanganyia na madawa ya kulevya aina ya Heroen pia chumba walichokutwa kilibeba ushahidi tosha wa pombe walizokua wakitumia.Moja ka moja miili yao ikahifadhiwa mochwari ili kuanze kufanyika mipango ya mazishi.
***
Edson alitawaliwa nna uso wa furaha kuona kazi yake imeenda vizuri, alijiona akiwa tajiri, kila mda alikua akikagua account yake kama kiasi cha shilingi million mia nane kimeengia kutoka katika kampuni ya Russia, ambayo ndio ilikua kampuni namba moja duniani kwa kulipa vizuri pasipo usumbufu.
“Nikiipata hii pesa kitu cha kwanza naangalia biashara ambayo inalipa kwa haraka mimi lengo langu nataka kuwa tajiri namba moja Tanzania na baadaye hata duniani nataka kuwakomesha wanawake waliowahi kunikataa pia nataka niwe na hadhi ya kutokataliwa na mwanamke yeyote”, yalikua maneno ya Edson mara kwa mara.
***
Ndege ye Qatar 762 kutoka China ilitua katika uwanja wa Julias Kambarage mwendo wa saa kumi na mbili jioni, mzigo wa Martin ulikua wa kwanza kushuka kwa ridhaa ya rubani, na moja kwa moja aliyestahili kuutoa mahali hapo hadi katika hotel ya Lantana alikua tayari, na gari aina ya Carry new model nyeusi, bila kuchelewa mzigo ulipakiwa katika but na dereva kuingia ndani, Askari wawili walikua wakifkuzia gari bila dereva wa gari kujua.
“Umefika wapi”
“Ndio nipo Tabata”
“Ok kaa makini, hakikisha hakuna matatizo yoyote yatakayotokea”
“Sawa mkuu”.
Yalikua mazungumzo kati ya Martin na dereva aliyekua anamletea mzigo wake aliyeitwa Dullah, Dullah aliendesha gari taratibu hasa baada ya kuona kuna gari inamfuata nyuma, hivyo alifanya vile ili kuona kama gari hilo litampita lakini alishangaa kila alipopunguza mwendo na gari ya nyuma ilipunguza mwendo, hapo alilichunguza vizuri kupitia Side Mirrow hapo akaliona lina nembo ya L kumaanisha anayeendesha bado hajawa imara barabarani,
“Itakua wmanafunzi huyu”, alijisemea kimoyomoyo na kuondoa wasiawasi.
Baada ya Dakika kumi na tano, Dullah alikua anaegesha gari katika hotel ya Lantana, alifungua buti na kutoka begi kubwa na kuanza kuliburuza kuelekea chumba alicho Martin,
“Fungua mlango”
“Uko wazi wewe ukija ingia japo nipo na mwanamke, wewe ingia uache hilo bgi kuna begi lignine lipo hapa utalichukua”
Yalikua maongezi kati ya Martin na Dullah, maongezi hayo yaliisha baada ya mlango wa chumba alichokua Martin na kusukumwa, hata sekunde kumi hazikuisha, mlango ulisukumwa na askari wawili waliingia,
“Mko chini ya ulinzi”, sauti hiyo iliandamana na kunyooshewa bastola usoni, Dullah na Martin waligeukiana na kushangaa kitendo kile, Kemmy kwa woga alijifunika haraka na kuvaa nguo za ndani akiwa ndani ya shuka, aliingiwa na hofu kupita kiasi.
“What’s wrong (nini shida)?” aliuliza Martin kwa sauti ya kijasiri,
“Tunaomba kukagua mzigo wenu” alijibu askari mmoja huku akiinama na kutaka kufungua begi lakini Martin alizuia na kuuliza,
“Kwani mnahisi ni nini hadi mnikague?”
“Tumepata taarifa zako kuwa wewe ndiye unaharibu vijana wa hapa Afrika kwa kuwaauzia madawa ya kulevya, na kuna mzigo umeingia hapa mda sio mrefu umetoka China, sasa leo ndio mwisho wa kufanya hii biashara maana utaenda kunyongwa”,
“Okey sasa begi hilo hapo kagueni” Martin aliongea huku akinyooshea mkono bagi ambalo lilikua na pesa, kwani lenye madawa tayari lilikua limeshafichwa mvunguni, Askari alifungua zipu ya begi hakuamini macho yake kile alichokutana nacho, alishtuka sana kuona pesa nyingi kiasi kile, tangu amezaliwa hakuwahi kukaa karibu na pesa nyingi kiasi kile labda pale alipokua akiingia bank,
“Kuna begi lingine” alisema askari mwingine huku akiinamna na kuchungulia mvunguni, na kwa bahati mbaya walifanikiwa kuliona begi lililokua limesheheni dawa za kulevya, walinyanyua simu haraka na kuwapigia polisi wa kichina waliokua wakiwatafuta wahalifu hao kwa miaka mingi.Hapo Martin, Dullah na Kemmy walifungwa pingu na kubaki chumbani hapo ili maskari zaidi waweze kuwasili na waandishi wa habari ili waje kupiga picha kila kitu chumbani pale.
***
Ili kuweza kupigana na maisha, baba Winny alilazimika kutoka kila siku ili kujitafutia chakula chake na mkewe ambaye kwa wakati huo mkewe alikua na ugonjwa wa saratani ya koo, ugonjwa huo ulikua unamtesa sana, mumewe Mazengo, ndio alikua kila kitu japo wakati mwingine alizidiwa hadi kulazimika kuomba msaada msikitini na katika mashirika ya kidini, Winny pia aliwapa wakati mgumu sana pale walipomfikiria maisha anayoishi, waliamini atakuja akuteseka baadaye lakini hawakuwa na jinsi ya kumuokoa kwani hadi nyumbani alikua ameshatoweka. Hivyo jioni ya siku ya Jumatatu alikua akitoka katika makutano ya barabara ya Shekilango,alikua akitembea na miguu hadi Mliman City ili aweze kuhifadhi naulli pale alipokua amekosa kazi kwa siku hiyo, alitembea huku akiwa anaimba nyimbo za kumtukuza Mungu pamoja na kusali rozali, alikimbia na kutembea na kanuni yake ilikua ni usafi, alionekana nadhifu mda wote.
“Mungu atanisaidia kesho nitapata”, alijisemea akiwa maeneo ya Sinza, wakati huo giza lilikua limeanza kuingia, hivyo alitembea haraka haraka huku akihema. Alitamani kufika nyumbani mapema ili kumpa mkewe dawa pamoja na chakula, kwani alimwacha kitandani asubuhi kutokana hali yake ya ugonjwa.
“Mungu akulinde mke wangu, najua uko salama na malaika wanazidi kukupa nguvu na uwezo, mumeo nipo njiani ninakuja kukulisha dawa, naomba nisubiri”, Mazengo alijisemea kimoyomoyo akiamini mkewe anamsikia kupitia roho mtakatifu.
***
“Wazee haya ni mambo ya kuelewana tu” Martin aliongea kwa kujiamini baada ya kuona jinsi askari wale walivyokua wakiangalia pesa zile kwenye begi kwa jicho la tamaa,
“Hakuna ujanja siku yako imefika mwisho” walijibu askari mmoja. Waliongea kwa dakika kumi na bila kutarajia askari wale walikua wapole baada ya kuahidiwa kupewa Bilion moja za kitanzania, ilikua pesa nyingi ambayo hawakuwahi kuishika katika maisha yao,
“Sasa tushapiga simu kuwa kuna nmtu amekamatwa, je hapa tufanyeje?” Askari mmoja aliuliza,
“Wewe hilo ni jambo dogo, tafuteni mtu yoyote hapa tumpe kesi”, alijibu Martin na mara moja Martin alipiga simu na kuamuru kijana wake mmoja aingie barabarani na kuja na mtu wa kupakaziwa kesi,
“Sawa mkuu nakuletea sasa hivi”, Lilikua jibu la Paul ambaye alikua akifanya mapenzi na Winny,
“Mpenzi nisubiri hapa hapa nakuja” baada ya kuongea maneno hayo Paul alivaa nguo haraka na kuingia barabarani alikanyaga mafuta hadi Mliman City,
“Samahani baba”, Ilikua sauti ya Paul ikimuita baba mmoja aliyekua anavuka barabara, na alimuita baada ya kumuona kama amechanganyikiwa kwakua alikua akiongea mwenyewe,
“Bila samahani kijana”, alijibu baba huyo huku akiizidi kusogelea mlango, “
“Kuna kazi nataka ukanisaidie kidogo, nikulipe hata hela ya kula” aliongea Paul huku akitabasamu,
“Oooh Asante Mungu, kazi ya mda gani”,aliuliza baba huyo kwani alikumbuka nyumbani kuna mgonjwa anayestahili kupewa dawa usiku,
“Kama nusu saa hivi” , Paul alijibu na bila kubisha baba huyo aliingia ndani ya gari na gari ikaanza safari kuelekea hotel ya Lantana,
“Mimi kweli Mungu ameniuona dakika za mwisho nimetoka Shekilango hadi hapa nakuja kupata riziki karibu na nyumbani, asante Mungu”, alijisemea baba huyo ambaye ni Mazengo baba wa Winny. Alipata furaha lakin hakujua ndio anaelekea katika kifo, na mbaya zaidi atamuacha mke wake akiwa mgonjwa..

Je nini kitatokea ?

the Legend☆
Dah huruma kwa baba winny
 
The legend asante Ila ungetupa kidogo kidogo jamani episode nyingi hizo
Hahahaa, nimeona nitupie za kutosha ili hata ratiba nyingine zikinibana tayari mzigo upo wa kutosha kwa wadau. Kuna mda mambo yanakua mengi, mda mchache

the Legend☆
 
Asante sana the legend. Hadithi inasikitisha mno.kuna story kidogo imefanana na hii hadithi. Kuna msichana mmoja alikuwa anaishi na mjomba wake. Mjomba alimchukua akawa ana msomesha. Huyo binti kufika form 2 akapata bwana. Alimpagawisha huyo bwana na usichana wake alitolewa na huyo jamaa. Mjomba akasema akachoka maana sometimes anarudi kwao amelewa. Binti akaona anabanwa. Huyo jamaa alikuwa mkubwa kwake na ana mke akampangishia nyumba sehemu yule binti akaona hayo ndio maisha. Siku ya siku yule jamaa alikuwa gafla. Binti maisha yakamgeukia mjomba hakumsamehe na ukimwi aliambukizwa na yule jamaa. Sasa hivi ana maisha magumu ajabu. Mambo mengine ya maisha yanafunza
 
Asante sana the legend. Hadithi inasikitisha mno.kuna story kidogo imefanana na hii hadithi. Kuna msichana mmoja alikuwa anaishi na mjomba wake. Mjomba alimchukua akawa ana msomesha. Huyo binti kufika form 2 akapata bwana. Alimpagawisha huyo bwana na usichana wake alitolewa na huyo jamaa. Mjomba akasema akachoka maana sometimes anarudi kwao amelewa. Binti akaona anabanwa. Huyo jamaa alikuwa mkubwa kwake na ana mke akampangishia nyumba sehemu yule binti akaona hayo ndio maisha. Siku ya siku yule jamaa alikuwa gafla. Binti maisha yakamgeukia mjomba hakumsamehe na ukimwi aliambukizwa na yule jamaa. Sasa hivi ana maisha magumu ajabu. Mambo mengine ya maisha yanafunza
Tuko pamoja mkuu. Simulizi kama hizi zinafundisha kitu

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom