Simuamini tena mke wangu!


kwani ni ngapi nyie hutuma bila kushirikisha wake zenu... Nimeipenda sana hii.
 
Yeye anajua matumizi ya pesa yako yote? na je unahonga sh ngapi kwa mwezi? na inaonyesha umehonga sana mwezi huu ndo maana umekosa karo ya mtoto. wewe kuhonga unaona sahihi ila yeye kutumia ndg zake ni kosa? kwani majukumu ya baba nini? kama ulikuwa huwezi kuhudumia familia si ungeacha kuoa. Nawaza tu kwa sauti
 
Sijamhonga malaya yeyote ww mis wa kinyaru!
 
Duh,majanga,uyo lazima kuna mtu anadate nae uko aliko.Ukitaka kumjua mwanamke mwenye mahusiano nje ya ndoa hiyo ni dalili mojawapo coz huwa hawawezi kujificha.Nakushauri usichukue uamuzi mgumu kwa sasa ila nakuachia assignment ya kumchunguza kama ana mtu au lah achilia mbali kuwapa pesa ndugu zake.Tafuta tu kijana yeyote huko alipo na mkabidhi picha ya mkeo kwa ajili ya kumfuatilia,utapata jibu.Yameshawahi kunikuta maswaibu kama yako na nikatumia mbinu ninayokupa nilipata jibu.
 

Ndugu yangu wanawake ni janga la taifa!
 
Kama unafikiri mke ni ndugu yako pata matatizo,jaribu kujipanga mwenyewe,mambo ya Biashara hata wewe waweza fanya.
 

yeye kamwaga mboga nawe jipange umwage ugali tingisha kibert kama miez6 hiv mwambie cna pesa huyo kid kama vp akae home uone kama hata mlipiaa...
 
it is sad, lakini hakikisha unamsomesha mtoto kwa kulipa ww directly shuleni kwake. kama unaeweza usiache kumtumia wife kiasi kidogo cha pesa za matumizi. wewe usiwe wa kwanza kufanya uamuzi wa kuachana. kama hataridhika na hatua utakazochukuwa atabwaga manyanga na wewe utakuwa salama.
 
Umeoa au mmeoana??? Ndio maana wanatuchukulia poa wanawake. Duh!!!
 

Pole sana kaka, ila kuna kitu cha kujifunza hapa. Ni kweli kama ni wazazi/wanandoa ni vyema mambo mengi mkayafanya kwa kushirikiana ila tujaribu kwenye uwezekano, kutopekua simu za wenziwetu. Kama mwenziwako ni MTU wa msaada kwako atafanya hivyo bila kusumbuana wala kulazimishana. Endelea kumsoma mwenzi wako, inawezekana ukaweza kumuelewa zaidi na kwenda nae sawa
 
Mfanye mkeo akuamini...
Ndoa yako ina tatizo zaidi ya ada ya mtoto. .. hamuaminiani.
Wewe una kazi nae ana kazi... lazima umueleweshe kwa nini hauko vizuri kiuchumi!!!
Naona kila dalili kuwa mkeo alishapoteza imani na wewe kitambo. ..
Unless uje na stori nzima juu ya uhusiano wako na mkeo juu ya ndoa, itakuwa miujiza kukupa ushauri wa kueleweka hapa...
 

Sidhani kama ni sahihi kuwa na misimamo mikali kiasi hiki. Familia ni ya watu wawili na mojawapo ya kiungo cha UPENDO na MAFANIKIO ni kushirikiana na kusaidiana kwa HALI na MALI...
 

Kukata tamaa au kuzira sio sifa nzuri ya baba wa familia. Kwa kuwa mkeo ni binadamu na sio malaika, mapungufu yake ni changamoto za kawaida kwako ambazo ulitakiwa uzitarajie...
Wanaume wengine woote unaowaona miaka na miaka kwenye familia wamepitia au wanapitia changamoto sawa au kubwa kuliko hiyo. Kuna watu wanapambana na changamoto kubwa mara 100 ya hiyo uliyo nayo na wanashinda.
Mkeo ni binadamu kama wewe... anakosea na kujifunza. Kama unataka kumfundisha katika hili, muonyeshe WEMA na kujali. Lakini ukimuonyesha kiburi, hasira, na kisasi basi ujue hicho ndicho atakachojifunza juu ya kupambana na changamoto za maisha...
 
Usikwepe majukumu fight usomeshe. Mwanaume siyo kuvaa suruali.

Pia haujui pesa zilizotumwa ni za nini hivyo usilalame
 

mnapokuwa mwili mmoja ni kawaida kusaidiana majukumu,suala la ubini wa mtoto sio issue,huyo mwanamke mwenzangu ni mbinafsi tu au ana lake moyoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…