Simu za mikononi katika Mahusiano | Mwenendo wa Walezi/Wazazi kwenye familia

Simu ni moja ya kifaa cha msingi katika maisha yetu ya kila siku, ndiyo inatuunganisha kirahisi pale tunapokuwa hatupo katika uwepo wa wale tunaotakiwa kuwasiliana nao. Zaidi ya kuweza kuendesha maisha yetu kijamii na kikazi, simu ina uwezo wa kuboresha mahusiano kama ambavyo ina uwezo mkubwa wa kudhoofisha mahusiano hayohayo kutegemeana na matumizi yake.

Makala hii ni ya kwanza katika mlolongo wa makala nilizoandaa ikizingatia matumizi ya simu katika kujenga au kubomoa mahusiano ya mtumiaji kwa watu waliomzunguka katika jamii, iwe ni wenza, wapenzi, ndugu, jamaa, marafiki, wafanyakazi, n.k

Leo nitajikita kwa wazazi/walezi majumbani dhidi ya matumizi ya simu na mwenendo wao kwa familia haswa watoto hadi kupelekea tabia na taratibu zao nyingi kuendeshwa na simu za mkononi wanazomiliki aidha kwa kutambua ama kutotambua. Napenda nitumie fursa hii kutathmini yale nitakayowasilisha, tutoe maoni yanayolenga kuboresha.

Uimara na ukaribu wa wanafamilia unategemea kwa kiasi kikubwa namna ambavyo familia hiyo inahusiana. Kuhusiana vizuri huambatana na matendo ya upendo, heshima na mawasiliano. Hata hivyo, kwa dunia ya leo imekuwa ni Changamoto kuweza kuhusiana vema majumbani, simu ikiwa moja ya sababu kubwa ya upungufu huo. Swali la msingi la kujiuliza, wewe kama Mzazi/Mlezi matumizi yako ya simu yanajenga au kudhoofisha/kubomoa?

Kuweza kufahamu kwa urahisi nafasi zetu katika matumizi ya simu, ni muhimu kuangalia, makosa ambayo wazazi/walezi huyafanya na simu.

Baadhi ya Makosa ambayo wazazi/walezi huyafanya na simu.

1. Kuipa simu umiliki wa akili na msingi wa maamuzi awapo nyumbani
Hili limekuwa suala la kawaida sana kwa wazazi/walezi wengi mara wafikapo nyumbani. Wanashinda kwenye shughuli siku nzima mbali na nyumbani, lakini bado wakifika nyumbani wanakuwa ‘busy’ na simu haswa kwenye ku-chati, kutembelea mitandao ya kijamii na kufuatilia masuala mbalimbali ya kiulimwengu kupitia kiganja na hivyo kupuuzia kabisa mwenza/mpenzi pamoja na watoto. Kiasi kwamba kuna wakati anaona kero hata pale mtoto anapokuwa anahitaji umakini (attention) yake kwake. Mbaya zaidi ni kwa zile familia ambazo wazazi/walezi wote wawili wametekwa na simu, hivyo watoto huleana wenyewe zaidi au na dada wa kazi (ikitokea naye hajatekwa na simu).​

2. Kutumia simu wakati wa mlo (meals)
Wakati wa mlo ni moja la wakati wa msingi wa familia kujamiiana, kufahamu nini kinaendelea katika maisha ya wanao/wanafamilia na ni wakati mzuri pia wa ku re-connect haswa kwa wazazi ambao siku zote wapo makazini na uwepo wao nyumbani kuwa mfinyu. Pamoja na kuwa mzazi hawekewi masharti ya jinsi ya kulea mtoto wake, na kipi cha kufanya ama kutofanya - kitendo cha mzazi kutumia simu akiwa na familia yake wakati wa mlo ni moja ya njia ya wazi inayoonesha kuwa, wale unaowasiliana nao kwenye simu au kile unachokifanya kuwa muhimu zaidi ya kuwapa ‘full-attention’ familia yako kwa ile nafasi ndogo unayobahatika kuwa nao. Heshima ni ya pande zote mbili, mkubwa anapaswa kumuheshimu mtoto kama vile ambavyo watoto wanatarajiwa kuwaheshimu wakubwa zao. Njia rahisi ya kumuonesha heshima mtoto hata mwenza/mpenzi ni kumsikiliza na kumpa usikivu, kujali kile kinachomgusa katika maisha yake ya kila siku na pia kuelewa kile anachokutana nacho kila siku bila kujalisha unaweza kutatua au hutoweza.​

3. Kuwapatia watoto simu kwa ajili ya kuchezea
Katika hoja hii tunajikita kwenye yeye kutumia simu ‘yako’ kama kifaa cha kuchezea (siku nyingine nitagusia umri sahihi unaoshauriwa mtoto kuwa na simu). Kuna tofauti ya mtoto kumiliki simu akiwa kanunuliwa na mzazi, na mzazi kumpatia mtoto simu awe anachezea. Kumpa mtoto simu achezee ni njia mojawapo rahisi ya kumridhisha mtoto kiasi kwamba atatulia hapo bila usumbufu wowote ule. Mzazi gani hataki apumzike mtoto asimkere au kumsumbua ? Ni wengi. Bahati mbaya, ni wazazi wachache ambao wanafahamu namna ya kuweka/kubadilisha matumizi ya vifaa hivyo ili viwe kwenye mfumo wa matumizi ya mtoto (kid mode). Na mbaya zaidi, wazazi wengi huitumia kama kumtuliza mtoto wakifuata njia rahisi na badala ya ile ndefu ya kuweza kumkatalia mwanae kwa kumwelewesha kuwa si wakati wote ni wa kuchezea simu na hivyo kujenga mtoto ambaye anaona anastahili kila kitu kilichopo machoni pake bila kujali simu hiyo ni ya mgeni ama lah.​

Athari

1. Kutojenga nidhamu ndani ya familia. Watoto wanakua katika mazingira ya kuonyweshwa kutokuwepo na umuhimu na haja ya muda wa familia na thamani yake. Na pia mtoto kuona ni sawa kudharau ‘ignore’ watu pale ambapo umakini wake unahitajika.

2. Kama mzazi/mlezi unakuwa unapitwa kwa kiasi kikubwa na yale yanayojiri katika maisha ya watoto haswa kama ni wadogo. Watoto wanapenda kusililizwa, kuheshimiwa na kuthaminiwa. Kuna changamoto ya mapenzi yanayopaswa kuelekezwa kwa mzazi yakatolewa kwa mtu ambaye anaweza kuwa si salama kwa mwanao.

3. Kukosekana kwa nyakati za msingi za kifamilia ambazo hujenga kumbukumbu za msingi kwa mtoto. Kama vile kukaa na kula pamoja, kusali sala ya usiku pamoja, kukaa na kufurahia kitu kwa pamoja.

4. Wazazi/Walezi kutofahamu yale yanayojiri kila siku katika maisha ya watoto wao. Inaweza kuonekana ni sawa, ila watoto nao wana changamoto zao wanazozipitia kila siku ambazo zinahitaji umakini na ukaribu wa wazazi na walezi patika kuwajenga kuwa vijana wazuri katika maisha yao. Wengine hupatwa na unyanyasaji wa kijinsia, na mtoto hutakiwa kujengewa kujiamini na kumuamini mzazi ili kueleza tatizo analokutana nalo, wakati mwingine hata ndani ya familia.

Ushauri

Tumekuwa wazazi na walezi ambao tupo Katika wakati ambao teknolojia imekuwa kubwa kuliko wakati wowote ule hapa duniani. Ni muhimu sana kuwa karibu sana na watoto wetu, na kuhakikisha hizi simu hazitufanyi mazezeta kiasi kwamba tunasahau majukumu na nafasi zetu pale tunapokuwa majumbani na familia zetu.

Kwa wale ambao kazi zinachukua maisha yako kwa kiasi kikubwa, wanaweza pia kujenga tabia ya kuwa na simu mbili. Simu ya kazi na simu ya nyumbani. Pale unapokuwa umefika nyumbani unazima kabisa simu na kutumia vema muda huo kwa ajili ya nyumbani ili kupunguza usumbufu. Nidhamu hutokana na kujiwekea misingi ya matumizi mazuri ya simu ambayo kwa namna yoyote ile hayataingiliana na nafasi yako kama mzazi/mlezi nyumbani.

Ni muhimu pia kwa familia kujiwekea taratibu za kuhakikisha simu haziruhusiwi kwenye baadhi ya nyakati za ‘family time’ ili kujenga mazingira ya kuwa karibu na kuzingatia wale walio mbele yako na si wanaopatikana kwenye simu.

Nimewasilisha hayo kwa uchache, una maoni, mawazo, ushauri au marekebisho? Tafadhali usisite kuchangia.

Karibuni katika kufahamishana zaidi,
Mitandao ya kijamii hasa hasa ndio imewafanya watu kuwa watumwa wa simu zao, ni wakati sasa wa kuweka kwenye mitaala kuhusu matumizi chanya ya simu na mitandao ya kijamii. Jamii inaangamia, tatizo linazidi kuwa kubwa kila kukicha. Leo hii mtu hahitaji kuzungumza lolote na mtu wanayesafiri naye pamoja kisa ameweka earphones yupo instagram na kwenye magroup ya whatsap.
 
kabla hatujawa na hizi simu za mikononi, Muda wetu tunaoutumia leo kwenye simu ,hapo kabla tuliutumia kufanya nini? na hicho tulichofanya kilikuwa cha manufaa au hasara pia. Hivi ni kweli tu nazitumia simu kwa mawasiliano tu au kuna vitu vingine tunafanya kwenye simu hizi? Je tunaweza kuacha na kurudi Enzi zile simu ya mezani, unaipokea au kupiga ukiwepo nyumbani tu? Je ni kweli simu za mezani zilitucheleweshea maendeleo na hizi mobile zimetuongezea maendeleo?
 
Wazazi wengi ni wahanga wa hili kwa watoto. Ni muhimu wazazi tuweke misingi ya kutumika simu kabla ya kumkabidhi mtoto wako simu kuliko ukamkabidhi ndiyo mkaanza mawasiliano ya vipi anakosea kuitumia. Ni vema pia kama mzazi/mlezi kutathmini matumizi yaka ya simu maana unakuwa unajenga msingi wa wao wataitumia vipi.

Kwenye hili sasa, badala ya kusubiri akiwa anakula kumkanya, tafuta muda na omega nae ni vipi yeye kutumda simu wakati wa Chakula si sahihi na kwamba hupendezwi na ungeomba ajitahidi kujirekebisha hilo. Inaweza ika work out.

kwa kweli the use of social media has shaped us for worse. mwanangu hata wakati wa chakula ana simu nimegomba, nimeshauri against this behaviour mpaka naona mpaka mdomo wangu utakuwa mrefu kama wa bata.
 
Mkuu,

Hii ni moja ya bandido nimependa sana Katixa hii mada. Imejaa mafunzo mengi ambayo natamani kila atakayeweza asome na kujifunza kitu hapo.

Unajua, shiva ya incidences kama hizi, siku zote huwa tunafikiria kwamba am too smart or alert or keen na haiwezi kutoka kwetu ila kwa wengine. Ndivyo ambavyo watu hujikuta wahanga. No one is too special aspite ajali unapotumia simu huku unaendesha gari. Ni hatari sana maana umakini unakuwa umepungua. Ndiyo maana hata kama unaendesha gari ikatokea umepata habari ambayo ni dharula huwa inashauriwa hata uegeshe gari pembeni ili uongee kwanza. Habari zinging za dharula tofauti kabisa na maongezi ya kawaida ama ya salamu katika simu.

Thanks for sharing.

MADA HII NI NZURI SANA. Matatizo ya kutumia simu vibaya ni mengi sana. Mimi binafsi nimeshuhudia mara mbili mtu anagonga gari la mwenzake kwa sababu ya simu. Mmoja alikuwa anaandika message huku anaendesha. Akagonga gari la mbele yake lilipofika kwenye mataa akashindwa kushika breki kwa wakati. Mwingine alikuwa anasikiliza simu. Ghafla akashindwa kuendesha sawasawa akasababisha ajali. Nadhani alipata habari mbaya alipokuwa anasikiliza simu wakati wanaendesha. Wenzetu kwenye nchi zilizoendelea wanaelewa athari mbaya za kuendesha gari wakati unazungumza na simu na ndio maana wanaweka adhabu kali sana kwa mtu anayekamatwa akiendesha gari huku anazungumza na simu.

Watu wengi tu wanatembea barabarani wakiandika ujumbe kwenye simu, na baadhi wanapata ajali. Vijana wengi wanavaa headphones na kusikilizia muziki kwenye simu - wanaharibu masikio yao bila kujua. Wengine wanashindwa kusikia honi za vyombo vya moto vinavyopita walipo na wanagongwa.

Jambo baya kuliko yote ni hili la vijana wengi sana kuwa wanaangalia picha chafu kwenye simu (pornography). Hakuna jambo baya katika maisha ya sasa kama hili. Ukishaanza kuangalia picha chafu, unajikuta 'umetekwa ufahamu' na ni vigumu sana kuacha. Hili ni jambo lenye madhara makubwa sana kwenye jamii. Ni kama matumizi ya madawa ya kulevya. Hizi ngono kinyume na maumbile ambazo zimejitokeza kwa wingi ndani ya jamii yetu kwa sasa, kwa sehemu kubwa zimetokana na kuangalia picha chafu ambazo nyingi ni za video za matendo hayo.

Kisaikolojia picha hizi ni mbaya sana. Zinamhamasisha mtazamaji kwenda kufanya ngono (au kujichua, jambo ambalo ni baya sana maana likizoeleka mno, mwanaume anakuja kukosa nguvu za kiume, na mwanamke anakuja kukosa hisia wakati akiwa na mumewe kwenye tendo la ndoa). Pili zinampa mtazamaji tamaa ya kufanya ngono kwa staili na kwa muda mrefu kama anavyoona kwenye picha kumbe zile picha nyingi zimefanyiwa 'editing' yaani sio za uhalisia. Na waigizaji wengi kwenye picha hizo wanatumia madawa ya kulevya ili 'kuondoa aibu' Mke anayeangalia picha hiyo akienda kukutana na mumewe akiona 'mambo' ni tofauti na aliyoona kwenye picha hizo anaanza kuona kama mumewe 'hajui wajibu wake' sawasawa. Binti ambaye hajaolewa akija kuoelewa naye anakuwa na mawazo hayo hayo. YOTE HAYO NI MATATIZO YA 'SIMU JANJA' (android phones). Yapo mengine meengi kama ambayo mtoa mada ameanza kuyaeleza, na naamini wachangiaji wataongezea hapa.
 
Ni mada nzuri.
simu imekuwa ni janga na si baraka tena.
1. Imeingiza familia nyingi kwenye matatizo.
2. wanafunzi kuto zingatia masomo.
3. wafanyakazi kutokuwa makini na kutilia maanani kazi wanazofanya.
4. watu wengi kuzitumia kusambaza habari zisizo za kweli.
5. zimetumika kuangalia picha chafu kwa watu wa rika zote.
6. inaathiri macho na masikio ya vijana wengi, kwani muda mwingi hutumia kutazama au kusikiliza simu.
7. Imetufanya watumwa, kila dakika LAZIMA tuiguse. hatuwezi kuiacha nyumbani asubuhi na kuikuta jioni.
n.k.
Tunahitaji hekima kutoka juu ili kutatua hili.

Umenikumbusha mbali sana Lucas philipo
 
Back
Top Bottom