Simu ya mke au mme

LADY H

Member
Joined
Nov 26, 2011
Posts
57
Reaction score
18
Wadau naombeni mnisaidie, hivi ni sahihi kwa mwanaume/mwanamke kupekua cm ya mke/mume, girlfriend/boyfriend, mchumba wake? :sleepy:
 
Kwa usalama wa afya yako na ulinzi wa watoto na vyombo vya thamani,,, usipekue simu yake.
Kwa wapenzi waaminifu, pekua simu yake maana ni fahari ya zawadi waliokosa wengi.
 
na ikitokea umekutana na kitu ambacho kimekuudhi lkn ukimwambia yeye anachukulia poa na bado wewe unampenda?
 
mke na mme hakuna shida. Shida kwa wachumba na mahawala. Mimi si moja ya matatizo yangu lilinipa shida miaka 10 iliyopita ila sasa hapana.
 
Wadau naombeni mnisaidie, hivi ni sahihi kwa mwanaume/mwanamke kupekua cm ya mke/mume, girlfriend/boyfriend, mchumba wake? :sleepy:

Si sahihi. Kwani twaweza kukutana na mambo yanayoweza kukumaliza kwa presha. Me sikushauri kupekua kabisa.
 
Kwa usalama wa afya yako na ulinzi wa watoto na vyombo vya thamani,,, usipekue simu yake.
Kwa wapenzi waaminifu, pekua simu yake maana ni fahari ya zawadi waliokosa wengi.

Umemaliza
 
mpenzi pekua coz mnaweza kuachana kama utakuta anachepuka ila mume usipekue coz utakaa kwenye ndoa ukiwa na machungu moyoni
 
Wadau naombeni mnisaidie, hivi ni sahihi kwa mwanaume/mwanamke kupekua cm ya mke/mume, girlfriend/boyfriend, mchumba wake? :sleepy:

Kwa mume na mke usahihi upo kabisa kwa ndoa yenye amani na upendo hakuna wasiwasi....



Ila kwa wachumba inategemea na misingi ya penzi leo na malengo yenu ya baadaye...


Kwa boyfrend na girlfriend siyo sahihi maana bado mapema sana lakin sio mbaya kama wataaminiana...
 
Mimi naona Ni fahari kubwa na Ni kitu cha kujivunia kupekua cm ya mkw wangu na yeye yuko huru kuangalia yangu. Kwa nini ujifiche huko Ni kukosa uaminifu na mapendo kwa familiar yako
 
sina mtu ambae anaweza kunioa mpaka sasa juu ya hili swala

HIVI TUNASHEAR MAJIMAJI YA MWILINI IWE SIMU????
 
'Kupekua'.... Hapana! Whether wanandoa au vinginevyo. Usijitengenezee matatizo yasiyo na lazima... Tumia simu yake kama kawaida,ikitokea umekuta msg ya ajabu then uta-deal nae...ila isiwe unashika simu yake daily kwaajili ya kupekua. Not good,trust me#
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…