OS ni kifupi cha operating system. Na OS ni mkusanyiko wa softwares nyingi ambazo zinamanage hardwares na kutengeneza mazingira ya softwares nyingine kufanya kazi.
Kuna OS nyingi kuanzia za computer mpaka za simu lakini nitataja mashuhuri. Kwa upande wa computer kuba Windows OS (windows 95,98,2000,XP,Vista,7 na sasa 8 n.k), Linux, Lion X (Macntosh), Ubuntu, Web OS n.k. Zote hizo ni OS za computer.
Kwa simu pia kuna Android, BBerry OS, iphone OS (IOS), Jolla, Maemo, symbian etc.
swali lako ulitaka jua android ni nini na ios ni nini?
Android OS ya simu inamilikiwa na google na iko huru kutumiwa na mtu yoyote ndio maana iko katika brand nyingi za simu. Google anaiacha itumiwe na makampuni ya simu mengi kama ambavyo microsoft anatengeneza windows kwa computers wakati yeye hatengenezi computer so inaweza tumiwa kwa Hp, dell, n.k.
IOS ni Iphone OS developed by apple kwa ajili ya simu za iphone ambapo baadaye ilianza tumiwa pia kwenye products zao nyingine kama ipad, na ipod touch. IOS haitumiwi na brand nyingine zaidi ya brand za apple wanatengeneza simu, ipad, na tablet zao zikiwa na os zao kama amavyo blackberry wanavyotengeneza simu zikiwa na OS yao na hawaruhusu wengine kuitumia.
Hope nimejitahidi eleza.