Nyamemba
JF-Expert Member
- Nov 3, 2011
- 845
- 447
Chama cha Mapinduzi kama ilivyo desturi yake kinaendelea na chaguzi zake na mara hii ni ndani ya jumuiya zake za wazazi,wanawake na jumuiya muhimu ya vijana UVCCM.
Leo nitajikita ndani ya jumuiya ya vijana UVCCM Taifa na hasa kwa huyu Simon Mathias Kipala. Huyu kwa mnaokumbuka vizuri amewahi kuwa Rais wa serikali ya wanafunzi pale Mlimani (UDSM) maarufu kama DARUSO, pia amewahi kuwa mwenyekiti wa shirikisho la vyuo vikuu yaani TAHLISO.
Mathias Kipala kama anavyojulikana na wengi amekuwa kwa Muda fulani mtumishi wa chama makao makuu na katibu msaidizi Ukerewe.
Kutokana na sifa hizo na nyingine kadhaa anastahili na nadiriki kusema ndiye miongoni mwao mwenye uzoefu, ushawishi, nia,uadilifu na uwezo wa kuirudishia jumuiya hii makali iliyokuwa nayo huko nyuma, akiwa amebobea kwenye sayansi ya siasa na utawala anao uwezo huo wa kuiongoza jumuiya hii kikamilifu na tena kwa kasi ya mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Mh Dkt Magufuli ili kuleta maana na matendo ya mageuzi chanya ndani ya CCM na serikali kwa kuisimamia kikamilifu serikali ambayo imepewa ridhaa ya kuongoza Tanzania kwa kutimiza kikamilifu ahadi ilizoahidi kipindi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.
Mara kadhaa Mh Rais amenukuliwa akiishangaa jumuiya hii kujitenga mbali na majukumu na wajibu wake na hasa kuandaa vijana ambao ndio wenye jukumu la uongozi kwa falsafa yake (Mh Magufuli).
UVCCM MPYA inamhitaji sana Kipala ili kuelekea 2019/2020 chama kiwe imara zaidi kushiriki na kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu tukiwa wamoja, wenye ari na mbinu bora zaidi.
Ni matumaini yangu kuwa kwa haya machache niliyoyabainisha hapa wapigakura wote mtakapokutana Dodoma mtamchagua kiongozi huyu shupavu, imara, mcha Mungu, mwadilifu ili aende kuiongoza UVCCM MPYA katika kutekeleza majukumu yake ya msingi kikamilifu.
UVCCM MPYA inamhitaji Simon Mathias Kipala na hakika ndiye chaguo letu na kamwe tusikubali maneno ya hujuma Kwani watani zetu hawapendi safu imara maana wameuona moto wetu kwenye uchaguzi mdogo, hivyo tuendelee kupeleka majonzi Kwao tena kwa mbinu za kisasa zaidi na ari zaidi.
M Jr
Leo nitajikita ndani ya jumuiya ya vijana UVCCM Taifa na hasa kwa huyu Simon Mathias Kipala. Huyu kwa mnaokumbuka vizuri amewahi kuwa Rais wa serikali ya wanafunzi pale Mlimani (UDSM) maarufu kama DARUSO, pia amewahi kuwa mwenyekiti wa shirikisho la vyuo vikuu yaani TAHLISO.
Mathias Kipala kama anavyojulikana na wengi amekuwa kwa Muda fulani mtumishi wa chama makao makuu na katibu msaidizi Ukerewe.
Kutokana na sifa hizo na nyingine kadhaa anastahili na nadiriki kusema ndiye miongoni mwao mwenye uzoefu, ushawishi, nia,uadilifu na uwezo wa kuirudishia jumuiya hii makali iliyokuwa nayo huko nyuma, akiwa amebobea kwenye sayansi ya siasa na utawala anao uwezo huo wa kuiongoza jumuiya hii kikamilifu na tena kwa kasi ya mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Mh Dkt Magufuli ili kuleta maana na matendo ya mageuzi chanya ndani ya CCM na serikali kwa kuisimamia kikamilifu serikali ambayo imepewa ridhaa ya kuongoza Tanzania kwa kutimiza kikamilifu ahadi ilizoahidi kipindi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.
Mara kadhaa Mh Rais amenukuliwa akiishangaa jumuiya hii kujitenga mbali na majukumu na wajibu wake na hasa kuandaa vijana ambao ndio wenye jukumu la uongozi kwa falsafa yake (Mh Magufuli).
UVCCM MPYA inamhitaji sana Kipala ili kuelekea 2019/2020 chama kiwe imara zaidi kushiriki na kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu tukiwa wamoja, wenye ari na mbinu bora zaidi.
Ni matumaini yangu kuwa kwa haya machache niliyoyabainisha hapa wapigakura wote mtakapokutana Dodoma mtamchagua kiongozi huyu shupavu, imara, mcha Mungu, mwadilifu ili aende kuiongoza UVCCM MPYA katika kutekeleza majukumu yake ya msingi kikamilifu.
UVCCM MPYA inamhitaji Simon Mathias Kipala na hakika ndiye chaguo letu na kamwe tusikubali maneno ya hujuma Kwani watani zetu hawapendi safu imara maana wameuona moto wetu kwenye uchaguzi mdogo, hivyo tuendelee kupeleka majonzi Kwao tena kwa mbinu za kisasa zaidi na ari zaidi.
M Jr